JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Fahamu jinsi ya kusoma biblia.


Awali ya yote ninakupongeza kwa nia yako kutamani kujua jinsi ya kusoma biblia. Hapo mwanzoni kabla sijamjua vizuri Mungu, kati ya  vitabu ambavyo nilikuwa ninaona ni vigumu kuvielewa, basi kimojawapo kilikuwa ni BIBLIA.

Lakini siku, na miaka ilivyozidi kwenda niligundua kuwa sio, nataka nikuambie hakuna kitabu kilicho kirahisi kama Biblia. Kwanini ninakuambia hivyo?.. Kwasababu ni kitabu kinachoweza kusomwa na watu wa makundi yote.  Mzee anaweza kukisoma, kijana anaweza kukisoma, asiye na elimu anaweza kukisoma mwenye PH.D anaweza kukisoma..Na wote wakafaidika na kilichoandikwa mule. Vilevile hakina ngazi yoyote ya awali kukipitia ndio uelewe kama vilivyo vitabu vingine. Leo hii ukihitaji kusoma kitabu cha Fizikia, itakugharimu kwanza upitie elimu za chini uwe na msingi, vinginevyo hutaweza kukielewa..Lakini biblia haina misingi hiyo.

Tena na cha kushangaza Zaidi ni kwamba, biblia imetoa nafasi ya kueleweka na watu wasio na elimu kuliko wenye hekima na ujuzi..(Luka 10:21)

Jinsi ya kusoma biblia.

Mambo ya kuzingatia kabla hujaanza kusoma biblia.

  • Kwanza: Omba Kabla hujaanza kusoma Habari yoyote, hata kama unaifahamu, mshirikishe kwanza Roho Mtakatifu, na mwombe msaada akusaidie kuyaelewa maandiko. Siri moja ya maandiko ni kuwa Habari ile ile inaweza ikawa na mafunuo mengi sana..Hivyo usipokuwa mnyenyekevu na kujiona kwamba Habari Fulani unaijua, nakuambia utabakia kuwa hivyo hivyo. Lakini ukimwomba kwanza Roho Mtakatifu akufunulie, maandiko basi utashangaa mambo mengi sana ambayo hukuwahi hata kuyafikiria.
  • Pili: Hakikisha upo katika utulivu wa kutosha. Mahali palipo na machafuko siku zote hata akili haiwezi kukaa katika utulivu wa kuzingatia kile kinachosomwa, na hivyo Roho Mtakatifu anakosa wigo wa kukufunulia, yale anayotaka kukufunulia. Hivyo kama upo kwenye makelele basi, subiri uwe katika utulivu, tenga muda wako, hususani usiku ni muda mzuri Zaidi.
  • Tatu: Tafakari Neno, Kumbuka Neno la Mungu halisomwi kama gazeti tu, Chukua muda mrefu kuyatafari maandiko Zaidi ya kuyasoma, ikiwa na maana mtu yule anayeitafakari sura moja vizuri, ni Zaidi na mtu yule atakayesoma kitabu kizima bila kutafakari chochote kilichoandikwa. Roho Mtakatifu anazungumza kwa kasi sana, pale mtu anapojibiisha kuitafakari Habari husika.
  • Nne: Endelea kutumia muda mwingi, katika kutafakari hilo Neno, kwa jinsi unavyokaa sana katika uwepo huo ndivyo unavyompa Roho Mtakatifu wigo wa kukufunulia maandiko katika uelewa mzuri zaidi. Mpaka dakika ya mwisho unamaliza, unatoka na kitu ambacho hapo kabla hukuwahi kukijua, tena moyo wako ukiwa na amani ya kutosha.
  • Tano: Kuwa na daftari na kalamu. Hiyo itakusaidia kuandika kile Mungu anachokufundisha, kwa kumbukumbu la baada usije ukasahau, Kumbuka mwanafunzi mzuri ni yule anaandika chini kile mwalimu wake anachomfundisha, kila anapomfundisha. Hivyo na wewe hakikisha unakuwa na daftari lako.

Hivyo ukizingatia hizo hatua, utakuwa umeshajua jinsi ya kusoma biblia. Pia kumbuka, kwenye suala la kitabu kipi uanzane nacho, au kipi usianzane nacho, hilo halina umuhimu sana, unaweza kuanza na kitabu chochote kile na  huko huko Roho Mtakatifu mwenyewe atakufunulia mambo ya ajabu, Na kukufikisha pale anapotaka ufike kwa siku hiyo, kwasababu hiyo ndio kazi yake aliikusudia juu yetu.

Yohana 16:13  “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”.

Jinsi ya kusoma biblia.

Pia Kujifunza biblia ni Pamoja na kusikiliza na mafundisho mengine ya Neno la Mungu yanayohubiriwa.. Yale yanakuwa kama TUTION kwako. Hivyo hapa pia yapo mafundisho mengi ya kukusaidia kuielewa biblia, kwenye website hii yapo mafundisho Zaidi ya 1000 ya mada mbalimbali, na Maswali na Majibu mengi sana, ambayo ukiyasoma naamini utapiga hatua kubwa sana katika kuielewa biblia..Hivyo kama upo tayari bofya hapa uende moja kwa moja katika orodha hiyo….>> MAFUNDISHO

                                                                                >> MASWALI NA MAJIBU

Bwana akubariki sana.

Jinsi ya kusoma biblia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au tutumie ujumbe kwa namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mihimili mikuu (4) ya mkristo katika safari yake ya wokovu.

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTAFIKA WAKATI WA WEWE KUACHWA NYIKANI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia leo tena.

Vipo vipindi tofauti tofauti ambavyo kila mkristo atavipitia…maana biblia inasema katika..

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; ….

4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”.

Hata uwe unampendeza Mungu kiasi gani/ hata uwe mkamilifu mbele za Mungu kiasi gani..ni lazima utapitia vipindi vya kulia tu katika Maisha yako!..ni kweli asilimia kubwa ya Maisha yako itatawaliwa na furaha na amani..lakini ni lazima utapitia tu vipindi tofauti tofauti vya kulia na vya huzuni.

Sasa katika Imani pia vipo vipindi ambavyo utamwona Mungu sanaaa..na vipindi ambavyo hutamwona (utaona kuna ukimya Fulani maishani mwako)!…Sio kwamba atakuwa amekuacha kabisa! Au hakufuatilii wala kukusaidia…Hapana atakuwa yupo anakuona na kukujua lakini atakuwa kama amejiepusha na wewe”. Bwana Yesu kuna kipindi alisema “Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha”…hivyo huo wakati wa kuachwa upo!…Wengi hawalijui hili, ndio maana wanapopitia kipindi Fulani cha Maisha wanarudi nyuma na kuuacha wokovu…

Sasa leo tutajifunza hicho kipindi ni kipi lakini kabla ya kuendelea mbele zaidi hebu usome mfano huu taratibu sana, kisha tutaendelea…

Luka 15:3  “Akawaambia mfano huu, akisema, 

4  Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda NYIKANI, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone? 

5  Naye akiisha kumwona, HUMWEKA MABEGANI PAKE AKIFURAHI. 

6  Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea. 

7  Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu”.

Mfano huo unaonyesha ni jinsi gani..Bwana anaweza akawaacha kondoo 99 nyikani na kwenda kumtafuta kondoo mmoja aliyepotea. Umewahi kujiuliza kwanini awaache wale kondoo 99, na kwanini asiende nao?..na kwanini awaache NYIKANI na si kwenye zizi, mahali palipo salama?…

Maana yake ni kwamba anawaacha peke yao sehemu ya wazi isiyo na uzio, ambayo inaonekana ni sehemu hatari, lakini ni salama….Sehemu ambayo Wanyama wakali wanapita, sehemu ambayo inaogopesha!…na mbaya zaidi wanaachwa peke yao…Na lengo la Bwana kuwaacha ni ili akatafute kondoo wengine..

Sasa hao kondoo walioachwa nyikani pengine ni wewe unayepitia ukame sasa, humwoni Bwana kama ulivyomwona wakati umeokoka. Sasa ufanye nini katika hiyo nyika yenye utata?

Kumbuka hapo ni nyikani, mahali pasipo na uzio.. hivyo sio wakati wa kuzunguka zunguka huko na kule…kaa hapo hapo ulipo ndio mahali salama!…hapo hapo mahali Bwana alipokuacha!..(maana yake ni kwamba anaelewa kabisa mahali alipokuacha  utakuwa salama mpaka atakaporudi) tulia hapo hapo hata kama ukitazama kushoto humwoni Bwana, ukitazama kulia umwoni Bwana kama ilivyokuwa hapo kwanza…wewe tambua kuwa hapo ulipo upo sehemu salama..lishike Neno lake lile lile na Imani!…

Haupo ndani ya uzio, ikiwa na maana kuwa  vishawishi vya kukuvuta utoke kwenye mstari wa wokovu, utaviona, usianze kuzurula…wala kuhama hama…tulia hapo hapo….Hali kadhalika pembeni unaweza kuona dalili ya kudhurika na wanyama wanaopita kule, na unaweza kuona kama vile hakuna ulinzi, usiogope! Kaa hapo hapo ndio sehemu salama (aliyekuacha hapo sio mjinga)….Hivyo tumia muda wako kujifunza Neno na kuwaimarisha wengine na kuwalinda wasitoke kwenye hifadhi ya Mungu..kwa kuwafundisha wokovu na kuwafariji mpaka wakati wa Bwana kurudi.

Kumbuka tena kuna wakati Fulani Kristo alikuweka mabegani alipokupata…lakini si wakati wote utakuwa mabegani mwake…wakati ukiwa mabegani mwake ulikuwa unamwona kwenye ndoto kila siku, ulikuwa unauhisi uwepo wake kila mahali, ulipomwomba kitu ulikipata papo kwa hapo…(wakati huo ulikuwa mabegani mwake, mbingu ilifurahia kukupata) lakini hautakuwa hivyo siku zote…utafika wakati utashushwa mabegani na wewe utakwenda kuungana na wenzako nyikani na Bwana atakwenda kutafuta kondoo wengine waliopotea.

Kama ni leo umempa Kristo Maisha yako, basi uwe tayari kwa hicho kipindi kuja mbele yako. Jifunze kumwelewa sana Bwana wakati huu wa sasa, ambao unamwona sana… kwasababu wakati wa ukame utafika!..kama hutamwelewa sana wakati huu, wakati wa kuachwa nyikani utaikimbia na kuiacha nyika.

Na hapo ndipo watu wengi walipopotelea. Imani ni ya kuilinda sana.

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MHUBIRI.

Kitabu cha mhubiri kiliandikwa na mfalme Sulemani.

Kitabu hichi kinaeleza, jumla ya mambo yote, na mwisho kinatoa ushauri ni nini mwanadamu anapaswa achague.

Ikiwa wewe ni mmojawapo wa  wanaojiuliza nini maana ya maisha, ni nini ufanye ili upate mwisho mwema mwenye mafanikio, basi nakushauri ukipitie kitabu hichi cha mhubiri kwa utulivu, Kwasababu Mungu alikiandika mahususi kwa ajili ya watu wenye maswali kama ya kwako.

Kwa ufupi (Mhubiri)Sulemani anajaribu kueleza jinsi alivyoanza safari yake yake ya kutafuta kitu kitakachompa raha maishani, kitu kitakachotatua matatizo yake moja kwa moja, Hivyo akaanza kujaribu kufanya kwa bidii jambo moja hadi  lingine ili aone kama linaweza kumletea jawabu la maisha yake.,

  • Alijaribu kufanya biashara nyingi sana kuliko watu wote waliomtangulia duniani lakini hakupata kile alichokuwa anakitafuta..
  • Alijaribu starehe na anasa zote unaozijua wewe, lakini katika hivyo vyote bado hakupata jumla ya maisha.(Mhubiri 2:1)
  • Akajaribu kwa kujijengea makasri ya kifahari lakini bado hakuipata hiyo jumla ya maisha (Mhubiri 2:4)
  • Alijiongezea elimu kuliko watu wote ulimwenguni, alikuwa na elimu juu ya miti yote, na karibu viumbe vyote duniani lakini katika elimu yake, na hekima yake bado hakupata jumla ya mambo yote.(Mhubiri 1:13)

Mpaka mwisho wa siku akakata tamaa, akaona kila kitu ni sawa na ubatili tu, na kujilisha (kufuata) Upepo. Japokuwa alijusumbua kupata kila kitu roho yake inapenda,  lakini bado kile alichokuwa anakitazamia hakukipata.

Na ndipo mwisho wa siku  akagundua jumla ya mambo yote ambayo  mwanadamu anapaswa kuyafanya chini ya jua nayo si nyingine zaidi ya KUMCHA BWANA, NA KUZISHIKA AMRI ZAKE.

Hivyo mimi na wewe hatupaswi, kuanza tena, kufanya utafiti, wa kitu kitakachotupa jawabu la maisha duniani,..Sulemani alishatusaidia, ukisema leo hii wewe mwenyewe ngoja uanze, kwa akili zako na nguvu zako, kutafuta maana ya maisha, nakawambia utazunguka kote na utarudi pale pale Sulemani alipoishia. Na wakati huo utakuwa umeshachelewa.

Unasema, ngoja nitafute elimu sana, hiyo ndio itanipa raha, Mungu hawezi kunipa raha,..Ni kweli utaisumbukia na kuipata, na kufanikiwa lakini mwisho wa siku utakuja kugundua mbona bado kuna shimo ndani yako? Ile raha ambayo uliitazamia mbona hujaipata?

Unasema, ngoja nitafute mali, nijiwekee miradi, mingi, kwasababu hiyo itanipa raha.. Nataka nikuambie yupo aliyefanya kazi kubwa zaidi yako aliyeitwa Mhubiri Sulemani, lakini hilo mwisho wa siku halikumpa jawabu alilokuwa analitarajia.

Vivyo hivyo na wewe kama unataraji utapata raha, sehemu yoyote, aidha kwa waganga, au kwa wanadamu, na huku umemwacha Mungu nyuma, ukweli ni kwamba mwisho wa siku utakuja kugundua uliacha kitu cha thamani sana nyuma yako.

Sasa mwishoni kabisa mwa kitabu hicho cha mhubiri, maneno hayo ya Mhubiri Sulemani ndio tunayapata,

Anasema..

Mhubiri 12:13 “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya”.

Unaona, anasema, mche Bwana, uzishike amri zake. Hivyo ikiwa bado angali unao muda ndugu yangu, mimi na wewe tumtafute Mungu, kwasababu huyo ndio atakayetupa furaha yote ya maisha yetu..

Na ndio maana mhubiri juu kidogo  alisema..

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo 2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

3 Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema; Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha; Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba; Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;

4 Na milango kufungwa katika njia kuu; Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo; Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege; Nao binti za kuimba watapunguzwa;

5 Naam, wataogopa kilichoinuka Na vitisho vitakuwapo njiani; Na mlozi utachanua maua; Na panzi atakuwa ni mzigo mzito; Na pilipili hoho itapasuka; Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele, Nao waombolezao wazunguka njiani.

6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani;

7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.

8 Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!”.

Ubarikiwe.

Kwa ziada ya masomo kuhusu kitabu cha Mhubiri, Fungua masomo haya;

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

UBATILI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

habari za ziada.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAPEPO NI NINI?

Mapepo ni nini?


Mapepo ni Malaika walioasi zamani ambao hawakuilinda enzi yao mbinguni. (Yuda 1:6)

Na shetani mwenyewe akiwa kama pepo mkuu.

Sasa walipoasi ndipo wakatupwa duniani, na hiyo ilikuwa  kabla hata ya mwanadamu kuumbwa. Wote walikuwa wameshatupwa huku duniani wakisubiria hukumu yao ya mwisho.

Lakini mwanadamu alipoumbwa, na shetani akafanikiwa kumdanganya pale Edeni ndipo yeye na mapepo yake yote wakapata uhali wa mambo mengi ulimwenguni,

Haya mapepo yakaanza kuwaingia watu jambo ambalo lilikuwa haliwezekani hata kidogo, yakashikilia mambo mengi, na kufanikiwa kuharibu, kwa ufupi yalikuwa na uwezo wa kujiamulia kufanya chochote,  yakiongozwa na kiongozi wao mkuu shetani

Mpaka ilipofikia kipindi cha Yesu Kristo kuja duniani, hapo ndipo yalinyang’anywa sehemu kubwa ya mamlaka waliyokuwa nayo, waliyoyaiba kwa Adamu, Yesu ndio akayachukua yakawa ya kwake.

Ufunuo 1:17 “…………Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu”.

Hivyo mapepo yaliyopo duniani leo hii hayana nguvu tena juu ya mtu ikiwa tu, atakuwa ndani ya Kristo basi..Kwasababu yeye ndio aliyepewa mamlaka yote ya mbinguni na duniani kwa sasa (Mathayo 28:28)..

Zamani shetani alikuwa na uwezo hata, wa kuwaendea hata wafu na kuzungumza nao, utaona hilo katika kipindi cha Samweli jinsi Yule mwanamke mchawi alivyompandisha Samweli juu kuzungumza na Mfalme Sauli. Lakini sasahivi wafu wote wanamilikiwa na Yesu Kristo, kiasi kwamba ukifa leo, shetani hawezi kukufikia huko ulipo kwa namna yoyote ile.

Mapepo ni nini

Hivyo fahamu tu, ikiwa upo nje ya Kristo, kwa namna moja au nyingine, mapepo yatakusumbua tu, na lengo lao si lingine zaidi ya kukuua na kukupeleka kuzimu.. Ili kufahamu ubaya wa mapepo, fungua hapa usome >> Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Hivyo usijidanganye na kusema mimi siwezi kuwa na mapepo kisa tu hayajawahi kulipuka ndani yangu..Ndugu fahamu kuwa si mapepo yote ni ya kulipuka kama unavyodhani..

  • Mengine ni ya magonjwa.(Luka 13:11)
  • Mengine ni ya mateso/mkandamizo wa nafsi, mpaka kupelekea kujiua. Mf. Ndio Yule alimwingia Yuda ikampelekea kwenda kutenda dhambi na kujinyonga.
  • Mengine ni ya utambuzi: (Matendo 16:16)
  • Mengine ni mapepo bubu na kiziwi;(Marko 9:25)
  • Mengine ni ya kukudanganya.(1Wafalme 22:22) N.k.

Hivyo ikiwa wewe upo nje, kwa namna moja au nyingine ipo roho ya ibilisi imejishikamanisha  na wewe hata pasipo wewe kujijua. Njia pekee ya kuyaondoa ndani yako ni kumpa tu YESU KRISTO maisha yako. Ukishamwamini na ukatubu na ukabatizwa, basi maroho hayo yanaondoka ndani yako..Na wakati huo huo ROHO MTAKATIFU anaingia ndani yako. Hapo ndipo utakapojua tofauti yako ya wewe ni jana.

Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Naamini mpaka hapo umeshafahamu kwa ufupi mapepo ni nini.

Usisahau kuwa hizi ni siku za mwisho, Na Yesu yupo mlangoni kurudi, na shetani naye analijua hilo vizuri, hivyo utendaji wake kazi sasa sio kama ule wa zamani, mapepo/majini yanatenda kazi kwa nguvu kuliko pale mwanzo. Hivyo nawe pia unaposikia habari za wokovu usikawie kawie kwasababu, shetani naye yupo karibu yako kuindoa hii mbegu iliyopandwa ndani yako.

Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu’.

Shalom.

Mada Nyinginezo:

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Kuna Malaika wangapi?

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

JIHADHARI NA UPOTEVU ULIOACHIWA SASA.

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

UHARIBIFU WA MTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA.

Ndio kwa kupigwa kwake sisi tumepona!!

Tunao ujasiri wote wa kusema hivyo, kwasababu kuacha kwake enzi na mamlaka mbinguni, kisha kuja kuishi maisha ya taabu na mateso hapa duniani, kuanzia kuzaliwa katika zizi la ng’ombe, Kisha kuishi maisha ya umaskini tangu utoto wake hadi utu uzima,(japokuwa alikuwa ni tajiri)

1Wakorintho 8:9 “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”.

Hakuwa hata na mahali pa kulaza kichwa chake, hata mbweha na ndege walimshinda, hiyo yote ni kwa ajili yangu mimi.

alijaribiwa zaidi yetu sisi, bila kutenda dhambi yoyote, alifunga na kukesha kwa kuomba kwa ajili yangu, na kama hiyo haitoshi, ilimgharimu kuingia matesoni ateswe na ibilisi, atemewe mate, apigwe mijeledi, agongelewe misumari, adhihakiwe, achomwe mkuki, halafu mimi nisiponywe roho yangu hilo litakuwa ni jambo lisiloingia akilini.

Kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

Ni haki yako wewe na mimi kuupokea uponyaji wa roho zetu kwanza, na hiyo inakuja kwanza kwa kutubu dhambi zetu , kwa kudhamiria kutubu kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu na tama zake, kisha ndio anakuja ndani yetu na kutuokoa na  kufanya makao na sisi. Na baada ya hapo atatuponya na miili yetu pia, kwasababu Kwa kupigwa kwake sisi tumepona, roho zetu na miili yetu pia.

Hivyo kabla sijakwenda kukuombe tatizo lako, Ni vema kwanza ukamkaribisha Bwana Yesu katika maisha yako. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu wako. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako(sawasawa na Matendo 2:38).

Sasa ikiwa wewe Ni mgonjwa, Kumbuka Bwana Yesu haponyi tu roho, anaponya pia miili yetu..mimi ninayekuandikia huu ujumbe ni shahidi alishaniponya mara nyingi, kwa kufuatisha maombi kama haya ninayokuombea vilevile atakuponya na wewe leo. Kwasababu Yesu ni yeye Yule.

Unachopaswa kufanya hapo ulipo..Weka mkono mahali unapoumwa, kisha.

Sema maneno haya kwa sauti.

EWE UGONJWA (UTAJE UGONJWA UNAO KUSUMBUA), MIMI NI MILKI HALALI YA MKUU WA UZIMA YESU KRISTO. NAKUAMURU KWA JINA LA YESU ONDOKA NDANI YANGU KUANZIA HUU WAKATI NA MILELE, KWA KUPIGA KWAKE SISI TUMEPONA. HAKUPIGWA BURE, HAKUDHARAULIWA BURE, HAKUTESWA BURE..BALI HIYO YOTE ILIKUWA NI MIMI NIUPOKEE UPONYAJI KAMILI WA ROHO YANGU NA MWILI WANGU. HIVYO ONDOKA NDANI YANGU SASA KWA JINA LA YESU KRISTO.

EE BWANA YESU, MWOKOZI WANGU, INGIA SASA NDANI YA MWILI WANGU, UNIRUDISHIE AFYA ULIYONIAHIDIA.

ASANTE KWA UPENDO WAKO.

JINA LAKO LIBARIKIWE DAIMA.

AMEN.

Sasa ikiwa  umefuatisha maombi hayo mafupi, basi kuwa na uhakika kuwa Kristo ameshakuponya tayari, ikiwa ulikuwa huwezi kufanya jambo Fulani anza kulifanya, ikiwa ni ugonjwa wa kwenye damu, nenda kapime, ikiwa ni wa viungo vyovyote vile Kristo ameshakuponya.

Hivyo usiache kwenda kushuhudia na kumpa yeye utukufu.

Bwana akubariki sana.

“Ndio Kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Mada Nyinginezo:

YESU MPONYAJI.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

RABI, UNAKAA WAPI?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

 

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

Ukisoma kitabu cha Warumi sura ya 9, ya 10, na ya 11..utaona mambo mazito sana mtume Paulo aliyokuwa akiyazungumza juu ya ndugu zake wayahudi. Akieleza jinsi neema ya Mungu ilivyoondolewa kwao, kiasi kwamba hata wangehubiriwa vipi injili wasingeweza kuipokea.

Chukua muda kwa wakati wako, pitia sura hizo kwa utulivu sana, ukisoma juu juu hutaona chochote, lakini ukisoma kwa utulivu huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, nakuambia hutaichezea hata kidogo hii neema tuliyopewa sisi watu wa mataifa.

Mtume Paulo alipewa kulijua hilo mpaka akawa anasema, anayo huzuni nyingi, na maumivu yasiyokoma moyoni mwake kwa ajili ya ndugu zake (yaani wayahudi), maumivu ya kila siku, akijua kuwa wokovu umeondolewa kwao..

Kiasi kwamba alitamani hata kama ingewezekana yeye  mwenyewe aupoteze wokovu wake, atengwe na Kristo ili kusudi kwamba ndugu zake wote wapone, basi angefanya hivyo..soma..

Warumi 9:1  “Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,

2  ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.

 3  Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe NIHARIMISHWE NA KUTENGWA NA KRISTO kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili”;

Kauli hiyo si rahisi kuizungumza, lakini kwa huruma ya watu wengine, na huzuni unayoisikia moyoni mwako inakulazimu uitamke, si kwamba unatamani iwe hivyo, lakini kama ingewezekana.. Ni sawa leo umuone mtoto wako mchanga, kapata ajali halafu kakatika mikono, halafu anatapata tapa pale chini kwa maumivu,akilia, ni wazi kuwa utatamani ungeyapitia wewe yale maumivu yake..Kuliko kumuona anaendelea kuteseka katika ile hali.

Ndivyo ilivyokuwa kwa mtume Paulo, alitamani kama ingekuwa inawezekana yeye kuharamishwa, (kufanywa kuwa mwana-haramu,atengwe na Kristo) kusudi kwamba ndugu zake wayahudi waiamini Injili waokolewe.. Lakini ilikuwa haiwezekani.

Ndugu kama hufahamu wakati ule wa kanisa la kwanza ni wayahudi wachache sana, waliiamini Injili, japokuwa ilikuwa ni mamilioni waliokuwa wanaisikia, na ndio maana ukisoma mbele kidogo mtume Paulo anasema.

Warumi 9.27  “..Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa”

Waliokolewa wachache sana, mpaka akasema, kama Mungu asingewaachia mabaki basi wangefananishwa na Sodoma na Gomora,(yaani akiwa na maana asingeokoka myahudi hata mmoja wakati wao)..

Na hiyo yote ilikuwa ni kwasababu waliikataa neema ya wokovu iliyoletwa na Yesu Kristo, alipokuwa duniani, na kuendelea na njia zao za kumtafuta Mungu, huku wamemweka Kristo pembeni. Ikapelekea mlango wa neema kufungwa juu yao. Na ndio maana utaona haijalishi walikuwa na bidii kiasi gani kwa Mungu lakini hawakuweza kuuona mlango wa neema hata kidogo kwasababu tu walimkataa Kristo (kasome Luka 13:34-35). Mtume Paulo alisema hivyo katika ile sura ya 10

Warumi 10:1  “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.

2  Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa”.

Hilo jambo linaendelea mpaka sasa, takribani miaka 2000 imepita, lakini  bado mlango wa neema haujafunuliwa kwao. Na hiyo yote ni ili mimi na wewe (watu wa mataifa), tuipokee neema.

Lakini mwisho kabisa mtume Paulo alipewa siri na Mungu, na siri hiyo aliiweka wazi akataka sisi nasi tuijue (yaani mimi na wewe), kwamba utafika wakati ambao Mungu atawarehemu tena..Na kikisha fika hicho kipindi basi sisi tufahamu Habari yote ndio imeishia hapo, kama mtu yeyote wa mataifa atakuwa hajaingia ndani ya Kristo, ndio basi tena..Soma

Warumi 11:25  “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26  Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.

Jiulize wayahudi kwa miaka 2000 wanautafuta uso wa Mungu lakini hawaupati, unadhani siku hiyo neema ikiondolewa kwetu, sisi tutaipatia wapi? Na dalili zote zinaonyesha wakati wao upo karibuni sana…Tayari taifa hili lilishachipuka tangu mwaka 1948, unadhani ni nini kinachosubiriwa hawa watu Mungu asiwageukie? Usiku na mchana wapo pale kwenye “ukuta wa maombolezo wa Nehemia” wanamlilia Mungu awaokoe (hayo yalikuwa ni majonzi ya mtume Paulo)..Lakini Bwana anakawia kidogo kwa ajili yangu mimi na wewe.

Moja ya hizi siku, Mungu atakisikia kilio chao,.mlango wa neema utafunguliwa kwao, na kwetu utafungwa,. Huo ndio ule wakati wa mwenye nyumba kusimama na kuufunga mlango, na watu watakuwa wakisimama nje na kugonga wafunguliwe lakini Bwana atawaambia siwajui mtokako.(Luka 13:25-28)…Duniani kutakuwa na kilio na kusaga meno.

Hivyo tunaposikia maneno haya, tujitathimini Je! Ni kweli bado tupo ndani ya Kristo? Au tupo vuguvugu. Kama wewe unaisikia injili na bado unasua sua basi uingie sasa kwa nia yote acha kusitasita kwenye mawazo mawili muda unazidi kwenda, kwasababu siku hizi ni za mwisho. Lango hili likishafungwa, halitafunguliwa kamwe.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

MADHARA YA KUTOA MIMBA.

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MSAMARIA MWEMA.

Msamaria mwema ni mtu wa nanma gani?


Ni kauli ambayo tunaisikia katika jamii yetu mara kwa mara. Na hiyo inatokea pale mtu mfano amekumbana na matatizo au shida Fulani halafu akakutana na mtu asiyemfahamu kisha akamsaidia kutatua tatizo hilo. Sasa mtu kama huyo baadaye akija kuulizwa ilikuwaje ukafanikiwa au ukafanikisha kitu kile katika yale mazingira? ..Ndio hapo utamsikia anasema nilikutana na msamaria mwema akanisaidia…

Lakini baadhi ya watu hawajui chanzo cha msamaria mwema ni nini?..

Habari yake tunaipata kutoka katika biblia, tusome,

Luka 10:25  “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?

26  Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?

27  Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.

28  Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.

29  Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?

30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

31  Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.

32  Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.

33  Lakini, MSAMARIA MMOJA katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34  akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.

35  Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.

36  Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?

37  Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.

Ni yapi tunajifunza katika Habari ya msamaria mwema?

  • Ili na wewe ufanyike msamaria mema, ni sharti uwe moyo wa huruma.
  • Ni sharti, uwe mwepesi kumsaidia mtu, ambaye hata haonyeshi dalili ya kuomba msaada kwako, lakini unajua kabisa yupo katika hali ya kuhitaji msaada.
  • Upo tayari kutoa hata mali zako, au vitu vyako vya thamani kwa ajili ya kumsaidia tu mtu

Sasa ukizingatia hayo, Basi mbele za Mungu utakuwa umekidhi vigezo vya kumpenda jirani yako kama nafsi yako.. Hapo utakuwa umeshida amri ya pili iliyo kuu kuliko zote, kama yule msamaria mwema.

Kumbuka  tendo hilo lina thawabu kubwa sana mbele za Mungu.

Hivyo ni wajibu wetu sote, kulikumbuka hilo wakati wote tunapoishi humu duniani, ili na sisi Mungu atuhurumie siku ile tuurithi uzima wa milele..

Mada Nyinginezo:

JIRANI YANGU NI NANI?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

ADAM NA EVA.

Adam na eva akina nani?


Hawa ni wazazi wetu wa kwanza.

Biblia inasema

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. 

28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”.

Lakini kama tunavyojua waliasi, na ndio hapo ikawa chanzo cha matatizo ambayo ndio mpaka leo mimi na wewe yanatuathiri.

Hawa alidanganywa na nyoka kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, Kumbuka “alidanganywa” wala hakushawishiwa, hii ikiwa na maana kuwa hakujua kuwa kitendo anachokwenda kukifanya kingekwenda kuleta madhara yoyote kwa mtu kwa udanganyifu alioambiwa na nyoka, kwasababu alidanganywa kuwa hatakufa, bali kinyume chake atafumbuliwa macho, atakuwa kama Mungu, akijua mema na mabaya.

1Timotheo 2:13 “Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye. 14 Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa”.

Lakini siku ile alipojaribu kujitetea kwa kumrushia nyoka mpira, hilo halikusaidia yeye kutoshiriki adhabu.

Vivyo hivyo na sasa, Udanganyifu mwingi umetokea leo hii duniani.. Lakini ni wajibu wako wewe kuujua ukweli na kuushika, kwasababu siku ile hautakuwa na la kujitetea na kusema, mimi mbona sikujua hili, au mimi mbona niliambiwa vinginevyo na watu wanaojiita watumishi wa Mungu.

Kumbuka si watu wote wanaojiita watumishi wa Mungu ni watumishi kweli wa Mungu,, Mtumishi wa Mungu ni lazima akufundishe kweli ya biblia, na kukuongozwa kwa Kristo na sio kwenye mambo ya ulimwengu huu.

Tusidanganywe kama Adam na Eva.

Ndio maana wakati huu wa machafuko mengi ya rohoni, ni vizuri ukawa na Kristo moyoni mwako, na kujifunza Neno la Mungu kwa bidii, ili likae ndani yako ibilisi asikushinde. Kwasababu kama Neno la Mungu halipo ndani yako kwa wingi, kamwe huwezi kuzishinda njama za mwovu,

Utakumbuka kilichomtokea Bwana Yesu kule jangwani, shetani alipomjia na maandiko na yeye alimjibu kimaandiko. Sasa huyo ni mwokozi wa ulimwengu yamemkuta. Itakuwaje mimi na wewe?

Tung’ang’anie NENO LA MUNGU. Maana hilo ndio silaha yetu nyakati hizi za mwisho dhidi ya mwovu shetani, ili tusiwe kama Adam na Eva.

Mada Nyinginezo:

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

VUKA UJE MAKEDONIA UTUSAIDIE.

https://wingulamashahidi.org/2018/07/17/uzao-wa-nyoka/

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAFIRAJI KWENYE BIBLIA.

Je! biblia inasema nini juu ya wafiraji?


Ufiraji ni Neno  linalojumisha kitecho chochote cha kumwingilia mwanadamu mwanzako  kimapenzi kinyuma na maumbile.

  • Uwe unamwingilia mwanaume mwenzako (Ulawiti na ushoga),
  •  Au uwe Unamwingilia  mwanamke, hajialishi  ni mkeo, hicho tayari ni kitendo cha ufiraji.

Na ni dhambi biblia imesema hivyo na kwamba watu wote wanaofanya vitendo kama hivyo hawawezi kuurithi uzima wa milele.

1Wakoritho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala WAFIRAJI, WALA WALAWITI,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Watu wengi wanajidanganya na kudhani kuwa wakiwaingilia wake zao, maadamu tayari wapo nao katika ndoa, sio dhambi..Ndugu usidanganyike, tendo lolote la kumwingilia mtu mwingine kinyume na maumbile haijalishi ni rafiki, au jirani, au kahaba, au mke, hiyo tayari ni ufiraji.

Vinjari yetu, na chaguzi mbalimbali ili kukidhi kila ladha na bajeti, http://swisswatch.is/ replica watches inapatikana kwa kununua mtandaoni.

Na wafiraji wote watahukumiwa.

Kilichosababisha Sodoma na Gomora viangamizwe, kilikuwa ni kitendo hichi cha ufiraji,

Yuda 1:7 “Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
8 Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu”.

Hivyo kama wewe ni mmojawapo tubu haraka sana, kwa kuacha kitendo hicho. Mgeukie Yesu Kristo ayaokoe maisha yako. Ikimbie hukumu ya Mungu. Ziwa la moto lipo kweli.

Jiepushe na utazamaji wa picha na video chafu za ngono zinazozagaa mitandaoni, watu wengi wanaingiliwa na hizi roho kwa kuzitazama tu. Utakuta hapo mwanzo, hakuwa hivyo lakini siku alipooanza kuzitazama tu, anaona kama, shinikizo fulani la nguvu linatoka ndani kumuhimiza kufanya hivyo.

Kama na wewe ni mmoja wapo basi, nakushauri, kaa mbali sana na mambo hayo, shetani anafahamu kuwa wakati wake ni mfupi aliobakiwa nao. Hivyo itazame sana mienendo yako.

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ulokole ni nini? Na kwanini wakristo waliookoka wanaitwa walokole?

Ulokole/ Walokole wametoka wapi?


JIBU: Kabla ya kwenda kujua maana ya ulokole, ni muhimu kujua kwanza maana ya neno ‘kanisa’..Tafsiri ya kwanza ya kanisa sio “jengo” bali ni “mkusanyiko wa watu waliomwamini Yesu”..Kwahiyo popote palipo na mkusanyiko wa watu waliomwamini Yesu, tayari hilo ni kanisa hata kama hakuna jengo. Soma mistari ifuatayo itakusaidia Matendo 2:47,1Wakorintho 1:2,14:5,14:23,15:9,16:19 n.k

Na kanisa la Kristo ni moja tu duniani kote ambalo linajulikana kama Bibi-arusi wa Kristo…Hilo ndio linajumuisha wakristo wote waliomwamini Yesu na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake (kumbuka hapa hatuzungumzii madhehebu), bali kanisa la Kristo moja ambalo pia sio jengo, bali watu wote duniani waliomwamini Yesu. Na watu hawa ambao ndio kanisa la Kristo, ndio watakaokuja kunyakuliwa siku ya parapanda katika tukio lijulikanalo kama UNYAKUO WA KANISA. Unaitwa unyakuo wa kanisa na si makanisa…kwasababu kanisa la Kristo ni moja tu.

Lakini sasa Kanisa la Kristo ni kweli ni moja lakini lina washirika wengi, na haliwezi lote kukusanyika pamoja na kwa wakati mmoja kufanya ibada, au kumwabudu Mungu, kama ni hivyo basi halina budi kuwepo na makusanyiko tofauti madogo madogo katika kila eneo ili kukamilisha kusudi lile lile la kukusanyika pamoja…Ndio hapo wakristo waliopo Mkoa wa kilimanjaro watakusanyika kivyao, na waliopo Morogoro watakusanyika kivyao huko waliko, n.k..

Lakini kumbuka Imani ni moja, na Kristo ni yule yule anayeabudiwa kote, utendaji kazi unaweza ukawa unatofautiana kulingana na kanisa na kanisa, lakini Imani ni sharti iwe ile ile moja, Bwana mmoja, Roho Mmoja, Ubatizo mmoja sawasawa na (Waefeso 4:3-7), tofauti na hapo hilo ni jambo lingine.

Sasa katika mkoa huo huo wa Morogoro pia sio wakristo wote wapo Morogoro mjini, kuna wengine wapo vijiji vya ndani huko…hao nao hawana budi wakusanyike huko walipo, hakuna sababu ya kusafiri mpaka mjini….na huko vijijini pia kuna uwezekano wa watu wasiwe karibu karibu…hivyo tena yatazaliwa makundi mengine madogo madogo mengi kulingana na mahali, hata inaweza kufikia kanisa likawa na watu watano..lakini yote yenye imani moja. Umbali ndio unaosababisha yajigawanye hivyo.

Sasa haya makanisa mengi madogo madogo ambayo yanakuwa katika eneo husika kwa kiingereza yanajulikana kama LOCAL CHURCHES, (Yaani kanisa la eneo husika aidha mtaa, au kijiji).

Na makanisa haya zamani, kutokana na uchache wa watu yaliyonayo na maeneo yalipo mengi yaliishia kudharaulika… na asilimia kubwa ya washirika wake ni maskini…kwasababu wengi wanaoishi vijijini au katika miji midogo midogo si matajiri kulinganishwa na wale wanaoishi mijini. Hivyo walidharaulika lakini kama biblia inavyosema kuwa..

Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao”

Hivyo hao waliodharaulika na kujulikana kama “Local churches”… ndio waliokuwa wa kiroho zaidi..Ishara nyingi na miujiza mingi ilifuatana na haya makanisa madogo madogo, kuliko hayo makubwa, …ndio watu waliokuwa na bidii zaidi ya kumtafuta Mungu, na ndio waliokuwa wanamheshimu zaidi Mungu.

Sasa kutokana na makanisa hayo madogo madogo kufahamika kama local churches…na washirika wao ndio wakajulikana kama “local people”..na kwa lugha yetu hii wakatafsiriwa kama (wa-locally) au WALOKOLE.

Hivyo kama mtu utaitwa mshamba kwa sababu unamwamini Yesu na kuzishika amri zake basi hiyo ni THAWABU. Kuliko kama utaitwa mwenye Elimu na wa-kisasa na huku umemwacha Kristo.

Ufunuo 3:17 “Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona”

Usijisifie ukubwa wa kanisa unaloabudu, wala wingi wa watu wa kanisani kwenu…Jisifie Yesu uliye naye maishani mwako hata kama upo kanisa la watu watano..jitathmini je! unazishika amri zake hapo ulipo?, je! unaishi kulingana na neno lake? Kiasi kwamba hata parapanda ikilia utakwenda naye!..Je hapa nilipo nanufaika roho yangu kiasi gani?..kama sinufaiki rohoni ni heri nikatafute wenzangu wenye Imani ya kweli hata kama ni wachache, ninusuru roho yangu..kuliko kuendelea kwenye umati wa watu wengi na kuipoteza nafsi yangu…

Ni heri nijulikane mlokole lakini naenda mbinguni kuliko kukubalika na kila mtu, mwisho wa siku naishia kwenda jehanamu. Na kama pia hapo ulipo penye watu wachache huoni dalili ya kuurithi uzima wa milele ni heri ukaenda kutafuta penye watu wengi ambao wanakwenda mbinguni..Lakini siku zote kumbuka mlango ni mwembamba na njia ile imesonga na ni wachache wanayoiona…na mlango ni mpana wa njia iendayo upotevuni na wengi wanauendea.

Bwana akubariki na Bwana atusaidie.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?

MIHURI SABA

Wafilisti ni watu gani.

YEREMIA

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post