MAPEPO NI NINI?

MAPEPO NI NINI?

Mapepo ni nini?


Mapepo ni Malaika walioasi zamani ambao hawakuilinda enzi yao mbinguni. (Yuda 1:6)

Na shetani mwenyewe akiwa kama pepo mkuu.

Sasa walipoasi ndipo wakatupwa duniani, na hiyo ilikuwa  kabla hata ya mwanadamu kuumbwa. Wote walikuwa wameshatupwa huku duniani wakisubiria hukumu yao ya mwisho.

Lakini mwanadamu alipoumbwa, na shetani akafanikiwa kumdanganya pale Edeni ndipo yeye na mapepo yake yote wakapata uhali wa mambo mengi ulimwenguni,

Haya mapepo yakaanza kuwaingia watu jambo ambalo lilikuwa haliwezekani hata kidogo, yakashikilia mambo mengi, na kufanikiwa kuharibu, kwa ufupi yalikuwa na uwezo wa kujiamulia kufanya chochote,  yakiongozwa na kiongozi wao mkuu shetani

Mpaka ilipofikia kipindi cha Yesu Kristo kuja duniani, hapo ndipo yalinyang’anywa sehemu kubwa ya mamlaka waliyokuwa nayo, waliyoyaiba kwa Adamu, Yesu ndio akayachukua yakawa ya kwake.

Ufunuo 1:17 “…………Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu”.

Hivyo mapepo yaliyopo duniani leo hii hayana nguvu tena juu ya mtu ikiwa tu, atakuwa ndani ya Kristo basi..Kwasababu yeye ndio aliyepewa mamlaka yote ya mbinguni na duniani kwa sasa (Mathayo 28:28)..

Zamani shetani alikuwa na uwezo hata, wa kuwaendea hata wafu na kuzungumza nao, utaona hilo katika kipindi cha Samweli jinsi Yule mwanamke mchawi alivyompandisha Samweli juu kuzungumza na Mfalme Sauli. Lakini sasahivi wafu wote wanamilikiwa na Yesu Kristo, kiasi kwamba ukifa leo, shetani hawezi kukufikia huko ulipo kwa namna yoyote ile.

Mapepo ni nini

Hivyo fahamu tu, ikiwa upo nje ya Kristo, kwa namna moja au nyingine, mapepo yatakusumbua tu, na lengo lao si lingine zaidi ya kukuua na kukupeleka kuzimu.. Ili kufahamu ubaya wa mapepo, fungua hapa usome >> Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Hivyo usijidanganye na kusema mimi siwezi kuwa na mapepo kisa tu hayajawahi kulipuka ndani yangu..Ndugu fahamu kuwa si mapepo yote ni ya kulipuka kama unavyodhani..

  • Mengine ni ya magonjwa.(Luka 13:11)
  • Mengine ni ya mateso/mkandamizo wa nafsi, mpaka kupelekea kujiua. Mf. Ndio Yule alimwingia Yuda ikampelekea kwenda kutenda dhambi na kujinyonga.
  • Mengine ni ya utambuzi: (Matendo 16:16)
  • Mengine ni mapepo bubu na kiziwi;(Marko 9:25)
  • Mengine ni ya kukudanganya.(1Wafalme 22:22) N.k.

Hivyo ikiwa wewe upo nje, kwa namna moja au nyingine ipo roho ya ibilisi imejishikamanisha  na wewe hata pasipo wewe kujijua. Njia pekee ya kuyaondoa ndani yako ni kumpa tu YESU KRISTO maisha yako. Ukishamwamini na ukatubu na ukabatizwa, basi maroho hayo yanaondoka ndani yako..Na wakati huo huo ROHO MTAKATIFU anaingia ndani yako. Hapo ndipo utakapojua tofauti yako ya wewe ni jana.

Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Naamini mpaka hapo umeshafahamu kwa ufupi mapepo ni nini.

Usisahau kuwa hizi ni siku za mwisho, Na Yesu yupo mlangoni kurudi, na shetani naye analijua hilo vizuri, hivyo utendaji wake kazi sasa sio kama ule wa zamani, mapepo/majini yanatenda kazi kwa nguvu kuliko pale mwanzo. Hivyo nawe pia unaposikia habari za wokovu usikawie kawie kwasababu, shetani naye yupo karibu yako kuindoa hii mbegu iliyopandwa ndani yako.

Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu’.

Shalom.

Mada Nyinginezo:

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Kuna Malaika wangapi?

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

JIHADHARI NA UPOTEVU ULIOACHIWA SASA.

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

UHARIBIFU WA MTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments