KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA.

KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA.

Ndio kwa kupigwa kwake sisi tumepona!!

Tunao ujasiri wote wa kusema hivyo, kwasababu kuacha kwake enzi na mamlaka mbinguni, kisha kuja kuishi maisha ya taabu na mateso hapa duniani, kuanzia kuzaliwa katika zizi la ng’ombe, Kisha kuishi maisha ya umaskini tangu utoto wake hadi utu uzima,(japokuwa alikuwa ni tajiri)

1Wakorintho 8:9 “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”.

Hakuwa hata na mahali pa kulaza kichwa chake, hata mbweha na ndege walimshinda, hiyo yote ni kwa ajili yangu mimi.

alijaribiwa zaidi yetu sisi, bila kutenda dhambi yoyote, alifunga na kukesha kwa kuomba kwa ajili yangu, na kama hiyo haitoshi, ilimgharimu kuingia matesoni ateswe na ibilisi, atemewe mate, apigwe mijeledi, agongelewe misumari, adhihakiwe, achomwe mkuki, halafu mimi nisiponywe roho yangu hilo litakuwa ni jambo lisiloingia akilini.

Kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

Ni haki yako wewe na mimi kuupokea uponyaji wa roho zetu kwanza, na hiyo inakuja kwanza kwa kutubu dhambi zetu , kwa kudhamiria kutubu kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu na tama zake, kisha ndio anakuja ndani yetu na kutuokoa na  kufanya makao na sisi. Na baada ya hapo atatuponya na miili yetu pia, kwasababu Kwa kupigwa kwake sisi tumepona, roho zetu na miili yetu pia.

Hivyo kabla sijakwenda kukuombe tatizo lako, Ni vema kwanza ukamkaribisha Bwana Yesu katika maisha yako. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu wako. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako(sawasawa na Matendo 2:38).

Sasa ikiwa wewe Ni mgonjwa, Kumbuka Bwana Yesu haponyi tu roho, anaponya pia miili yetu..mimi ninayekuandikia huu ujumbe ni shahidi alishaniponya mara nyingi, kwa kufuatisha maombi kama haya ninayokuombea vilevile atakuponya na wewe leo. Kwasababu Yesu ni yeye Yule.

Unachopaswa kufanya hapo ulipo..Weka mkono mahali unapoumwa, kisha.

Sema maneno haya kwa sauti.

EWE UGONJWA (UTAJE UGONJWA UNAO KUSUMBUA), MIMI NI MILKI HALALI YA MKUU WA UZIMA YESU KRISTO. NAKUAMURU KWA JINA LA YESU ONDOKA NDANI YANGU KUANZIA HUU WAKATI NA MILELE, KWA KUPIGA KWAKE SISI TUMEPONA. HAKUPIGWA BURE, HAKUDHARAULIWA BURE, HAKUTESWA BURE..BALI HIYO YOTE ILIKUWA NI MIMI NIUPOKEE UPONYAJI KAMILI WA ROHO YANGU NA MWILI WANGU. HIVYO ONDOKA NDANI YANGU SASA KWA JINA LA YESU KRISTO.

EE BWANA YESU, MWOKOZI WANGU, INGIA SASA NDANI YA MWILI WANGU, UNIRUDISHIE AFYA ULIYONIAHIDIA.

ASANTE KWA UPENDO WAKO.

JINA LAKO LIBARIKIWE DAIMA.

AMEN.

Sasa ikiwa  umefuatisha maombi hayo mafupi, basi kuwa na uhakika kuwa Kristo ameshakuponya tayari, ikiwa ulikuwa huwezi kufanya jambo Fulani anza kulifanya, ikiwa ni ugonjwa wa kwenye damu, nenda kapime, ikiwa ni wa viungo vyovyote vile Kristo ameshakuponya.

Hivyo usiache kwenda kushuhudia na kumpa yeye utukufu.

Bwana akubariki sana.

“Ndio Kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Mada Nyinginezo:

YESU MPONYAJI.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

RABI, UNAKAA WAPI?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

 

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments