Title July 2020

KWANINI HUNA HAJA YA KUANDIKIWA JUU YA NYAKATI NA MAJIRA?

1 Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya NYAKATI NA MAJIRA, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa SIKU YA BWANA yaja kama vile mwivi ajavyo usiku”.

Shalom.

Katika mistari hiyo miwili, yapo mambo mawili pia ninataka uyaone. Jambo la kwanza ni “Nyakati na Majira” na Jambo la pili ni “Siku ya Bwana”..Mtume Paulo ameitenganisha hiyo mistari miwili, kwasababu inazungumziwa vitu viwili tofauti,

Kwamfano tukianzana na huo mstari wa Kwanza, unazungumzia Nyakati na Majira ya kurudi kwake Bwana, lakini huo wa pili unazunguzia siku yenyewe ya Bwana itakavyokuwa..

Sasa mpaka mtu anaposema kwa habari ya nyakati na majira sina haja ya kuwaandikia..anamaanisha kuwa suala la majira na nyakati ambayo Kristo atarudi ni jambo ambalo kila mtu anajua, sio siri lipo wazi!, limeshaelezwa kila mahali, sio jambo jipya..na ndio maana hawezi kuandika tena kuwakumbusha watu..

Nataka nikuambie ndugu yangu ikiwa wewe ni mkristo na mpaka sasa bado hujui majira na nyakati za kurudi kwa Yesu duniani kulinyakuwa kanisa lake, basi ujue kuwa kuna tatizo kubwa sana katika Imani yako tena sana ambalo utanatakiwa ulichukulie ‘seriously”…

Biblia imetuweka wazi kabisa na kutuambia tukishaona majira Fulani au nyakati zimebadilika basi tujue ndani ya hicho kipindi siku yoyote Kristo anarudi..Ili kuelewa vizuri tafakari mfano huu,

Leo hii labda unatafuta Kazi mahali fulani, kwenye shirika Fulani la utafiti wa kilimo, halafu ukapata, ukaitwa kwenye interview, ukafanikiwa kupita, lakini wakakwambia kazi yetu rasmi itaanza kipindi cha msimu wa masika, hivyo tutakupigia simu wakati huo ukifika hakikisha tu unakuwa hewani wakati wote, ili tusikukose pindi kazi zitakapoanza. Lakini ukiangalia wewe leo hii upo mwezi wa 9 na umeshajua masika huwa inaanza kuanzia mwezi wa 2-5 mwakani..

Sasa kwa namna ya kawaida hichi kipindi cha katikati utakuwa kawaida tu, lakini itakapofika mwakani kuanzia mwezi huo wa 2 hadi wa 5, utakuwa makini sana, utakuwa karibu na simu yako kwasababu unajua wakati wowote, utapigiwa simu ukaanze kazi,.Unaona hapo! hujapewa tarehe lakini umepewa majira na Nyakati..inaweza ikawa mwezi wa pili mwanzoni, au wa tatu mwishoni, au wa nne katikati hujui..bali utajiweka tayari muda wowote..

Vivyo hivyo na sisi wakristo, tumepewa majira ya kurudi kwa Bwana Yesu, lakini hatujapewa siku, wala saa. Na majira yenyewe ndio haya tunayoyaishi sasa.. Ndugu katika wakati ambao tungepaswa tuwe makini sana na wokovu wetu basi ni katika majira haya.. Kwasababu Bwana Yesu alituambia, mtakapoanza kuona milipuko ya magonjwa yenye mfano wa Tauni yanaipiga dunia (Corona) Luka 21:11 basi mjue yupo mlangoni, mtakapoona matetemeko ya nchi, basi mjue mpo ndani ya wakati huo, mtakapoona wimbi la manabii wa uongo wengi wakizuka duniani, mtakapoona watu wanapenda anasa kuliko kumpenda Mungu, watu wanapenda fedha, basi mjue hayo ndio majira yenyewe.

Mtakapoona maasi yanayongezeka kwa kasi (ushoga na uuajji), upendo wa watu wengi kupoa, kutokea kwa wimbi kubwa la watu wenye kudhihaki wakisema mbona huyo Yesu haji, dunia ipo vilevile wakati wote,(2Petro 3:3) basi tujue tupo katika hayo majira kabisa…

Na ndio pale sasa tukirudi katika ule mstari wa Pili anasema..

2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa SIKU YA BWANA yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

Tukiwa katikati ya majira hayo, ghafula wakati wowote, muda wowote, Bwana atatokea kama mwizi ajavyo usiku.. Kwa bahati mbaya kwa upande wao watasema mbona duniani tupo salama na kuna amani, Hapo ndipo Unyakuo unapita kwa ghafla sana na kwa haraka..wafu wanafufuliwa, na watakatifu wachache sana wanatoweka duniani..

Wakati baadhi ya watu wakipigwa butwaa kufikiri ni nini kimetokea mbona watu wachache hatuwaoni duniani..(wengi watajua ni kawaida watu kupotea potea na kuja kupatikana baada ya siku/miaka kadhaa hivyo watapuuzia) hapo ndipo mpinga-kristo ataanza kufanya kazi..wakati huo dunia haitakuwa na zaidi ya miaka 7, usitamani wakati huo ukukute kwasababu kutakuwa ni vilio na kusaga meno kwa watakaobaki.

Embu jiulize, ni kitu gani kinakufanya uishi maisha ya kubahatisha-bahatisha wakati huu wa siku za mwisho? Neema tuliyonayo haitakuwa hivi sikuzote, upo wakati utatamani ungerudi siku moja nyuma utengeneze mambo yako lakini haitawezekana, wakati huo wenzako wakiwa wanakula karamu ya mwana kondoo mbinguni wewe utakuwa umebaki halafu kibaya zaidi uliujua ukweli lakini hukuukubali kwa wakati.

Ndugu tubu dhambi zako, mgeukie mkuu wa uzima YESU KRISTO, azifute dhambi zako..Achana na mambo ya ulimwengu hayakufikishi popote, wala hayakupi faida yoyote wewe mwenyewe unajua. Hivyo fanya uamuzi mwema wa kugeuka na kumfuata Yesu ili uwe na amani katika kipindi cha maisha yako ulichobakiwa nacho hapa duniani.

Ni matumaini yangu utafanya hivyo. Na Kristo awe pamoja na wewe, na pamoja na sisi sote.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

TAFUTA KUWA NA AMANI NA WATU WOTE.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.

Ni agizo la Mungu kwamba tuwe na amani na watu wote..Ukijiona una shari na mtu au watu basi kuna tatizo mahali…Sio kila jambo ni la kupambana nalo, na njia ya kupambana na moto ni kuuzima na si kujitosa ndani ya moto. Hivyo tunapoudhiwa si wakati wa sisi kulipiza kisasi, ni wakati wa kuyazima hayo maudhi, kwa hekima na upole.Na mara nyingi kitu kinachowasha moto katika miasha yetu ni ULIMI.

Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ULIMI NI MOTO; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”

Unaona hapo? Biblia inasema pia ukiweza kuuzuia ulimi wako hata SIKU YAKO ITAKUWA NJEMA…na ndivyo utakavyopata amani..

1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.

11 Na aache mabaya, atende mema; ATAFUTE AMANI, aifuate sana”

Hivyo mara zote tukijifunza kukaa kimya na kuwa wapole na wenye busara…basi ni lazima tu tutakuwa na amani na watu wote….Sisemi kwamba hautakuwa na watu wanaokuchukia kabisa,…hapana watu wanaokuchukia watakuwepo tu! lakini hawatakuwa na la kufanya kwako kwasababu muda wote watakuona ni mtu wa amani. Watatafuta maneno kwako lakini hawatayapata…hivyo mwisho wa siku wataachana na wewe, na kuendelea kufikiri mambo yao mengine.

Lakini ukiwa ni mtu wa kujibiza, kamwe vita kwako havitaisha..na hakuna siku utapata amani…kama mtu akikuudhi wewe nawe unajibu mashambulizi kwa kumrudishia maneno…nataka nikuambia hakuna siku utakuwa na amani, utakuwa ni mtu wa kugombana tu kila siku, na wa kukosa raha, na muda mwingine kuweka vinyongo tu…na pasipo kujua kuwa tatizo kubwa lipo upande wako.

Mithali 15:1 “Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu”.

Kila mahali jaribu kuwa mpole…hiyo ndiyo njia ya kupata Amani na watu wote…Na kuwa mpole sio “udhaifu”….Bwana wetu Yesu alikuwa ni mpole(Mathayo 11:28) na mtu mpole mara nyingi sio mtu wa kuzungumza sana, na sio mtu wa kuzungumza mambo ya wengine (msengenyaji).

Wafilipi 4:5 “Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu”.

Sisi kama wakristo tukiudhiwa kwa maneno sio lazima tujibu neno,.. ukiumizwa hupaswi na wewe kumuumiza..kila wakati tafuta namna ya kulitatua tatizo badala ya kulichochea…na kwa jinsi utakavyoonesha bidii ndivyo Mungu atakavyozidi kukupatanisha na wale ambao wanaonekana ni maadui zako wa kudumu..Na hivyo utazidi kuwa na amani.

Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.

Hivyo Bwana anavyotuambia tutafute kwa bidii (maana yake tufanye kila tuwezalo) tuwe na amani na kila mtu, kama vile tunavyofanya bidii kuutafuta utakatifu ambao hakuna atakayemwona Mungu asipokuwa nao.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

Mtu astahiliye hofu ni yupi?

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?

DANIELI: Mlango wa 9

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Kwanini biblia inasema mtu wa rohoni huyatambua yote?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MATENDO YETU YANAPIMWA KATIKA MIZANI.

Ukisoma katika biblia utakuta kuna mahali Bwana alikuwa anasema maneno haya…

1Wafalme 16: 25 “Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, akatenda maovu kuliko wote waliomtangulia”

1Wafalme 16: 30 “Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana kuliko wote waliomtangulia”.

Utaona hapo huyo Mfalme aliyeitwa Omri alifanya machukizo makubwa kuliko baba zake waliomtangulia…na anakuja kupata mtoto anayeitwa Ahabu na huyo mtoto anafanya naye mabaya kuliko yeye na wote waliomtangulia…Maana yake ni kwamba hali ya mtoto inakuwa ni mbaya kuliko ya mzazi, na ya mjukuu ni mbaya kuliko ya Baba na babu.

Sasa unaweza kujiuliza ni kwanini Bwana aweke hilo neno “ naye akafanya mabaya kuliko wote waliomtangulia”?..Jibu ni kwasababu matendo yetu yanapimwa yakilinganishwa na ya waliotutangulia..

Kama baba kaua mtu mmoja, na mtoto wake akaua wawili…basi maasi ya mtoto yamezidi yale ya Baba mara mbili…yaani kama yangewekwa katika mizani basi mzigo wa mtoto ni mkubwa kuliko wa Baba.

Kadhalika kama mtoto kafanya mema kuliko baba yake basi matendo yake kama yakiwekwa katika mizani yataonekana yamezidi ya Baba yake…na kama Baba yake amefanya mema kuliko yeye basi matendo ya Baba yake katika mizani ya kimbinguni ni mazito kuliko ya mtoto, na hivyo ya mtoto yataonekana yamepunguka…

Ndicho kilichomtokea Mfalme Belshaza wa Babeli…Mfalme huyu ijapokuwa alikuwa anayajua matendo ambayo Mungu wa Israeli alimfanyia Baba yake…lakini bado matendo yake yalikuwa maovu kuliko baba yake…Na mema yake yalionekana ni pungufu kuliko mema ya Baba yake katika mizani ya kimbinguni. Kwani Baba yake alimheshimu Mungu lakini yeye hakumweshimu na kwenda kuvichukua vyombo vitakatifu na kuvitumia kwa karamu zake za kiasherati.

Na Bwana akamwambia maneno haya..

Danieli 5:27 “TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka”.

Maana yake ni kwamba matendo mema aliyoyafanya baba yake yamezidi ya kwake…Bwana Mungu alitegemea matendo ambayo angeyafanya yazidi ya baba yake lakini kinyume chake yamepungua, na hivyo akamhukumu.

Biblia inasema….

2 Samweli 2:3 “Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo; Majivuno yasitoke vinywani mwenu; Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa maarifa, NA MATENDO HUPIMWA NA YEYE KWA MIZANI”.

Ndugu matendo yetu yanapimwa katika mizani kila siku yakilinganishwa na ya wengine kama sisi…kizazi chetu kinapimwa katika mizani kikilinganishwa na vizaza vilivyotangulia..

Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona”.

Mahali tunapoishi, tunapofanyia kazi tunapimwa…kila tunalolifanya linapimwa linalinganishwa na la wengine. Hata maisha tunayoishi sisi kama wakristo yanapimwa ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5:20 “Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”.

Unapovaa suruali binti wa Mungu ambaye umezaliwa katika mazingira ya kikristo, pengine hata baba yako ni mchungaji…na unasema unakwenda mbinguni…ukumbuke kuna mwingine kama wewe mwenye umri kama wa kwako mahali fulani ambaye ni mzuri kuliko wewe na mwenye umbo zuri kuliko lako lakini havai hizo suruali wala vimini, ingawa mazingira yote yanamruhusu kufanya hivyo…yeye ameshinda katika mazingira magumu ya vishawishi vingi lakini wewe umeshindwa katika mazingira marahisi..Jua upendo wako kwa Mungu unapimwa!.

Unaposhindwa kumtafuta Mungu kwa kazi yako unayofanya masaa 8 tu kwa siku, na kusema upo bize sana…kumbuka kuna mwingine aliye bize kuliko wewe mwenye kufanya kazi masaa 10 mahali pengine lakini hakosi ibada, wala hakosi muda wa kusali na kuomba na kusoma Neno…ingawa anachoka kulko wewe…Fahamu kuwa upendo wako unapimwa!

Hivyo ndugu huu ni wakati wa kujipima kabla ya kupimwa!…na kujitathimini upya…

Kumbuka siku zote, usilisahau hili Neno utembeapo, uishipo…matendo yako yanapimwa katika mizani.

Ayubu 31: 5 “Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;

6 (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WALA SIJIHUKUMU HATA NAFSI YANGU.

Kuna hatua unafika Mungu anahitaji umuangilie sana yeye kuliko kujiangalia nafsi yako ili uweze kusonga mbele katika kumtumikia. Lipo tatizo kubwa ambalo lilishawahi kunikumba mimi, siku za mwanzoni nilipookoka, na naamini linawakumbuka watu wengi hata sasa waliookoka, Jambo hilo mtume Paulo alishaliona na kulitolea ufumbuzi wake kwa ufunuo wa Roho..

Kuna wakati unafika, unaona kila jambo unaloweza kujaribu kulifanya unaona pengine linaweza likawa linamkosea Mungu, au kama umefanya dhambi fulani ukatubu, unaona kama vile Mungu hajakusamehe vizuri, au amekukakasirikia, na hiyo inakufanya ujilaumu muda mwingi, Unajihukumu na kuhitimisha kuwa Mungu hawezi kuwa na mimi tena, Mungu hawezi kunitumia, Mungu ananiona mimi ni mchafu sana, Nimeuhuzunisha moyo wake sana hivyo ameshakata tamaa na mimi..

Paulo alisema hivi..

1 Wakorintho 4:1 “ Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.

2 Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.

3 LAKINI, KWANGU MIMI, SI KITU KABISA NIHUKUMIWE NA NINYI, WALA KWA HUKUMU YA KIBINADAMU, WALA SIJIHUKUMU HATA NAFSI YANGU.

4 MAANA SIJUI SABABU YA KUJISHITAKI NAFSI YANGU, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana.

5 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu”.

Kama tunavyojua Paulo ni mtu ambaye mawazo yake yote yalielekea kwa Mungu sana, alikuwa anajitahidi kwa kadiri awezavyo kumpendeza Mungu lakini pengine katika Nyanja fulani za Maisha yake ya huduma alishawahi kufanya makosa kadha wa kadha, au alishawahi kushindwa kufanikisha hiki au kile kwa ajili ya Mungu, kiasi kwamba hata yeye mwenyewe au watu wengine wangemwona kama ameshindwa kabisa, lakini hapa anasema..

“Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu.

4 Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu”

Unaona madhaifu yake hayakuwa sababu ya yeye kujihukumu kuwa anafaa au hafai mbele za Mungu, japokuwa hilo halimthibitishii kuwa anafaa, lakini hakuruhusu ajihukumu kwasababu haoni sababu kwanini afanya vile, Pengine aliwaza Mungu hakuwahi kumwambia kuwa hampendi, Au Mungu hakuwahi kumuonyesha katika maono kuwa hamtaki tena? Kama sivyo, ni kwanini ajihukumu mwenyewe?

Hivyo Paulo aliamua kuendelea kuishi Maisha ya kumtegemea Kristo kuliko kuutegemea ukamilifu wake wote umsaidie katika huduma yake, na hiyo ilimfanya afike mbali, japokuwa alikutana na milima na mabonde,

Lakini kumbuka jambo kama hili halimuhusu mtu anayefanya dhambi za makusudi. Wewe kama mzinzi, Maisha yako yapo mbali na wokovu unafanya dhambi kwa makusudi, ndani yako hakuna hofu yoyote ya Mungu, ujue kuwa hata kama hutajihukumu, basi dhamira yako itakushuhudia ndani yako kuwa kuwa wewe ni mnafki na mwovu. Na utahukumiwa siku za mwisho…Na kumbuka mojawapo ya dhambi za makusudi kabisa, zisizo za madhaifu, ni dhambi ya uzinzi na uasherati. Mtu anayefanya uasherati baada ya kuokoka anafanya dhambi ya makusudi inayostahili hukumu. Hivyo kama unaifanya ndugu iache mara moja.

Lakini ikiwa upo ndani ya Kristo, na una kiu kweli ya kuzidi kumpendeza Mungu na unajitahidi kujizuia kwa kila kitu kiovu, basi kataa hukumu yoyote inayokuja ndani ya moyo wako inayokuambia wewe hufai, kataa mawazo yote yanayokuambia unachofanya kwa Mungu hakimpendezi hata kidogo, kataa hayo mawazo yanayokuambia Mungu hana mpango wa wewe, yakija yaulize mbona Mungu hajawahi kuniambia hilo jambo?. Endelea kumtumikia Mungu kwa karama aliyoiweka ndani yako..

Ikiwa ulifanya makosa Fulani madogo, basi rekekebisha makosa yako, kisha endelea kusonga mbele, mtazame Kristo, na yeye atakuwa na wewe siku baada ya siku, Vilevile usikubali hukumu kutoka kwa mtu yeyote ikutaabishe moyo,..yupo mtu anaweza kukuambia wewe bado hujaitwa na Mungu kwa kutazama maisha uliyokuwa unaishi huko nyuma?…na akakwambia Mungu hawezi kukutumia mtu kama wewe, muulize mbona Mungu hajawahi kunisemesha mambo kama hayo? Wengine wanaweza kukutamkia maneno ya laana hata kama yataonekana yana ukweli ndani yake lakini wewe yakatae matazame Kristo, endelea na safari…

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je mtu akifa anakuwa hana dhambi tena?

 Je ni kweli mtu akifa anakuwa hana dhambi tena kufuatia hili andiko Warumi 6:7 “kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.”


JIBU: Bwana Yesu alisema haya maneno mahali Fulani…

Yohana 8:21 “Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi MTAKUFA KATIKA DHAMBI yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja………

24 Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU”.

Bwana Yesu aliwaambia Waandishi na Mafarisayo maneno hayo..kuonyesha kuwa Kama mtu akikataa kutubu dhambi angali hai na kumwamini basi atakufa na hizo dhambi zake (maana yake hizo dhambi zake zitamfuata hata huko anakokwenda, na atahukumiwa kulingana na hizo).

Hilo utalithibitisha katika andiko hili..

1Timotheo 5:24 “Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata”.

Kwasababu hiyo basi mstari huo wa Warumi 6:7, haumaanishi kuwa mtu mwenye dhambi anapokufa basi anakuwa hana dhambi tena…bali unamaanisha kuwa mtu “yeye aliyekufa Pamoja na Kristo, amehesabiwa haki mbali na dhambi”…Maana yake mtu aliye ndani ya Kristo hakuna hukumu ya adhabu juu yake kwasababu anakuwa amevuka kutoka mautini kuingia uzimani, ingawa bado anaishi ulimwenguni.

Ndio maana ukianzia mstari wa 6 na kuendelea kidogo mpaka wa 8 utaelewa vizuri..anasema..

Warumi 6: 6 “mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena;

7 kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.

8 Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”

Hivyo andiko hilo linatuhusu sisi sote…Hatuna budi kufa Pamoja na Kristo, kila mmoja wetu kwa kumwamini yeye na kutubu dhambi na kufufuka Pamoja naye kwa njia ya ubatizo wa maji na wa Roho Mtakatifu.

Warumi 6:3 “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima”

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

TUMAINI NI NINI?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

PARAPANDA ITALIA.

Siku moja inapopita, ndivyo tunavyoikaribia ile siku kuu ya kwenda mbinguni, siku ile ya Parapanda kulia, ambapo watakatifu wote duniani wataisikia, hakika itasikiwa na wao tu, na sio kila mtu duniani kama wengi wetu tunavyodhani…Watu wenye dhambi wakati huo hawataisikia parapanda hiyo hata chembe..

Siku hiyo pengine itakuwa ni asubuhi kwa upande wetu, au jioni au  usiku wa manane ukiwa umelala.. Kama wewe ni mtakatifu utasikia sauti nzuri ya shangwe, ikiambatana na parapanda ya Mungu, na wale wafu waliokufa katika Kristo, wao nao pia wataisikia kutoka kule makaburini, na kufufuka na kuanza kutembea duniani, na wewe utawaona, halafu ghafla, tutaliona jeshi kubwa la malaika likitokea, likiambatana na Bwana, na wakati huo huo ghafla tutaona miili yetu ikibadilishwa kutoka katika miili hii ya unyonge ya mauti na kuwa miili ya utukufu, wakati hilo likuwa linaendelea katika kipindi kifupi sana cha kufumba na kufumbua tutajikuta mawinguni na Bwana YESU, huo ndio wakati tutaenda naye kule mbinguni kula naye ile karamu ya mwana kondoo aliyokwenda kutuandalia miaka 2000 iliyopita.

Unaweza kudhani jambo hilo ni bado sana, lakini nataka nikuambie mimi na wewe tunaishi katika yale majira ya kuja kwa Bwana mara ya pili. Dalili zote zinaonyesha, Angalia milipuko ya magonjwa mfano wa Tauni (Corona) yaliyotabiriwa na Bwana Yesu yakitokea ulimwenguni (Luka 21:11)..Hiyo ni dalili ya kwamba tupo ukingoni mwa wakati kuliko tunavyoweza kudhani, angalia tena kuchipuka kwa taifa la Israeli, yaani mtini, ndio kunathibitisha kabisa wakati wa majira ya mataifa(yaani mimi na wewe) upo ukingoni.

Jambo ambalo wakristo wengi hatufahamu, ni pale tunapodhani Mungu ana ile kauli ya “wengi wape”..Yaani, kwasababu ulimwengu huu uliojawa na uovu na waovu wengi Mungu hawezi kuuangamiza au kunyakua wale wachache walio waaminifu kwake..

Yesu alisema kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, na kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, jiulize, waliookoka katika siku za Nuhu walikuwa ni wangapi kama sio 7 tu katika ya mabilioni ya watu waliokuwa ulimwenguni, vilevile waliookoka katika siku za Lutu walikuwa wangapi kama sio watatu katika ya Malaki ya watu waliokuwa katika miji ile ya Sodoma na Gomora,

Ukitazama tena kwa ukaribu utaona aliye nyakuliwa alikuwa  ni mtu mmoja tu (HENOKO) kati ya watu wote waliokuwa wanaishi kipindi chote kabla ya gharika, kwasababu ni yeye tu peke yake ndiye aliyempendeza Mungu.

Vivyo hivyo katika wakati huu watakaonyakuliwa ni wale tu watakaompendeza Mungu, hao ndio peke yao watakaosikia Parapanda ya Mungu ikilia kutoka mawinguni, hata kama watakuwa ni watu 100 katika ulimwengu mzima, hao tu ndio watakoenda, wengine wote waliosalia hawatajua chochote, watashangaa tu mbona kundi dogo la watu wachache sana halipo duniani..

Wengine watadhani, wameibiwa tu, wengine watadhani wametoroka, n.k. Lakini ulimwengu hautaelewa chochote kwasababu litakuwa ni kundi dogo sana, kumbe hawajui wenzao siku nyingi tayari wapo mbinguni wakila karamu ya mwana kondoo, lakini huku chini kitakachokuwa kinaendelea ni dhiki kuu ya mpinga Kristo. Na baada ya hapo ni maangamizo.

1Wathesalonike 4:16  “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17  Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.

18  Basi, farijianeni kwa maneno hayo.”

Ndugu yangu jiulize, Yesu akirudi leo utakuwa katika upande upi? Na injili zote hizi ulizosikia utajitetea vipi siku ile kusema hujaambiwa? Ishara zote hizi za siku za mwisho utajitetea vipi siku ile mbele za Mungu? Mungu ni mwingi wa rehema lakini pia ana ghadhabu nyingi.

Ili kufahamu vizuri ni jinsi gani tunaishi katika siku za mwisho angalia MADA nyingine, mwisho kabisa wa somo hili, uone ni wakati gani huu tunaishi..

Kama hujaokoka, basi huu ndio wakati wako wa kuyatengeneza mambo yako na Kristo, ili kusudi kwamba hata ikitokea paraparanda italia leo usiku basi uwe na uhakika kuwa na wewe utakwenda kumlaki mawinguni. Unachopaswa kufanya ni kukusudia tu kumkaribisha Yesu maishani mwako, kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, na kuwa tayari kuyaanza Maisha mapya  ya wokovu.

Kama utamaanisha kufanya hivyo ni ahadi yake kuwa atakuja ndani yako na wewe kuanzia huo wakati utaanza kuona badiliko kubwa ndani yako, hivyo kama upo tayari kufanya hivyo sasa,

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tazama mada nyingine chini zinazoeleza Habari za kurudi kwa Kristo duniani..

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAONO YA NABII AMOSI.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

RAFIKI MWEMA.

Rafiki mwema ni nani?


Uzuri ni kwamba kila mmoja wetu alishawahi kuwa na rafiki au marafiki katika maisha yake.. Kama ulishawahi kuwa na marafiki wengi utagundua kuwa wengine walikuwa marafiki zako kwasababu mliendana tu tabia hivyo tu,, na  wengine walikuwa marafiki kutokana na maslahi Fulani au mazingira Fulani au fursa Fulani, labda shuleni,  au kwenye biashara au kazini, au katika mambo ya kiimani n.k…

Kati ya hao wapo ambao ni wa kudumu yaani mnaweza kupotezana hata kwa muda mrefu lakini urafiki wenu ukadumu palepale, au mazingira Fulani yakatokea aidha ya kutofautiana kipato lakini bado urafiki wenu ukaendelea kudumu,  na wapo ambao ni wa muda tu, kukitokea kutengana kidogo, au mazingira Fulani kubadilika basi urafiki huo unakufa hapo hapo..

Lakini kwa vyovyote vile katika makundi yote hayo swali ni je utawezaje kumtambua rafiki mwema?

Jibu ni rahisi rafiki mwema, ni Yule ambaye atauweza kuutoa uhai wake ili wewe upone. Kwamfano, rafiki  yako asikie wewe umelazwa figo zako zote mbili zimekufa upo hoi kitandani mahuti huti, ili uishi ni lazima figo zote mbili zipatikane kutoka kwa watu wengine ili upachikwe wewe uendelee kuishi, Halafu wakati huo huo anatokea rafiki yako, ambaye hana hata undugu na wewe, mlikutana tu mkaendana tabia, mkashirikiana pamoja..

Na sasa anakuambia rafiki yangu, mimi leo hii nimeamua kuzitoa figo zangu zote mbili, ili wewe upone, Unaweza ukajiuliza huyu mtu anawaza nini? Akitoa figo zake sisi yeye atakufa, na itakuwa hasara tu ile ile..Ukizingatia yeye bado anayo malengo yake mengi ya maisha, mimi ninafaida gani kwake? Pengine unamkatalia Lakini yeye bado anakusisitiza kuwa anakwenda kutoa figo zake zote mbili afe ili wewe upone.. Na kweli anakwenda kufanya hivyo. Anatolewa unapewa wewe na yeye muda huo huo anakufa.. Je! Mtu kama huyo si zaidi ya rafiki mwema kwako?

Ukweli ni kwamba Katika ulimwengu mzima hakuna mtu anayeweza kufanya hivyo..

Lakini habari njema ni kwamba yupo ambaye aliweza kufanya hivyo kwa ajili yangu na wewe ili tupone..Na mtu huyo si mwingine zaidi ya YESU, alisema mwenye hivi…

Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo”.

Upendo huu ni zaidi ya upendo wa ndugu, Ndugu yako hawezi kuifikia hatua hii, ya kufa ili wewe uokoke, lakini Kristo alikufa ili mimi na wewe tupate uzima wa milele..

Na ndio maana maandiko yanasema..

Mithali 18: 24 Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.

Sasa huyu rafiki aambatanaye kuliko ndugu, ndio YESU KRISTO mwenyewe..

Hivyo ukimkaribisha huyu maishani mwako, ni uhakika kuwa utakuwa salama, na hutakuwa na wasiwasi kwamba utapotea tena baada ya hapo, kwasababu yeye tayari alishalipa gharama za upotevu wako kabla hata hujazaliwa. Kwahiyo kama ukimfanya leo kuwa rafiki yako, basi atakuwa rafiki yako kweli kweli, na mema yote utayaona..

Lakini ule mtari wa 14 anasema..

“Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.”

Unaona?  Ili na wewe Yesu awe rafiki yako ni sharti utii anayokuamuru.. Kama ulikuwa ni mwenye dhambi unatubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, kisha unakwenda kubatizwa katika maji mengi kama alivyotupa  maagizo katika Mathayo 28:19, Na baada ya hapo atakutia muhuri kwa Roho wake Mtakatifu atayemwachilia ndani yako wakati huo huo. Na hapo ndipo utakuwa na uhakika kuwa sasa umeshafanyika kuwa rafiki yake.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

YESU MPONYAJI.

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

HATA NA BARNABA PIA AKACHUKULIWA NA UNAFIKI WAO!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE.

Wokovu huu ambao tumeupata bure, tusidhani yule aliyetugawia hakuingia gharama yoyote kuupata,..Halikuwa ni jambo la kukaa mbinguni tu na kusema niamnini mimi mtaokoka!..Hilo lisingewezekana kamwe, ili kuunda kitu kinachoitwa “wokovu” ilimpasa afuate kanuni Fulani..ilimpasa kwanza aache enzi na mamlaka yote mbinguni, awe hana kitu, kisha ashuke hapa duniani, aishi kama mwanadamu mwingine yoyote yule aliyezaliwa na mwanamke, aumwe wakati mwingine, audhiwe, apitie umaskini, kisha na yeye pia ajaribiwe na shetani, aonekane kama atashinda au la, ..Lakini kama tunavyosoma aliyashida yote kwa muda wa miaka 33 bila kutenda dhambi yoyote licha ya kupitia vipingamizi vyote vya kibinadamu..

Lakini sio hilo tu, ilimgharimu uhai pia, ili aweze sasa kukikamilisha hicho kitu kinachoitwa WOKOVU KWA MWANADAMU.. Ndio hapo akalazimika aende msalaba akapigwe afe, damu imwagike ili kusudi kwamba mimi na wewe tupokee huo wokovu kwa gharama alizoingia..

Lakini wengi wetu tunadhani mateso aliyoyapita yalikuwa ni ya kawaida tu, biblia inatuambia Bwana aliharibiwa uso wake, na mwili wake, Zaidi ya mwanadamu mwingine aliyewahi kuishi hapa duniani..

Soma..

Isaya 52:13 “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.

14 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE, NA UMBO LAKE ZAIDI YA WANADAMU),

15 ndivyo atakavyowasitusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu”.

Jaribu kuchua muda utafakari!, chukua muda utafakari hata dakika 15 au 20, fikiria huo uso uliwezekanikaje kuharibiwa Zaidi ya mtu yoyote hapa duniani, na mwili wake vivyo hivyo, ndipo utakapofahamu kuwa mapigo aliyopigwa Bwana hayakuwa ya mwanadamu wa kawaida, alikuwa kama nyama buchani, kile unachokifahamu kwenye filamu ni mfano mdogo wa jinsi Bwana alivyokuwa anaonekana, na hiyo yote ilimpasa apitie vinginevyo mimi na wewe tusingeupata wokovu..

biblia inasema..

“Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, NA KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA”.(Isaya 53:5)

Uso wake na mwili wake usingeharibiwa kwa mapigo mabaya kama yale ambayo mengine hata hayajaandikwa kwenye biblia, mimi na wewe leo hii tusingeufikia uponyaji wa roho zetu. Lakini jiulize wewe ndugu ambaye bado hujamwamini yeye licha ya kwamba umekusogezea wokovu huo bure mbele yako bila malipo yoyote..Jiulize, siku ya leo ukifa katika hali yako ya dhambi utawezaje kuokoka?

Kumbuka wokovu unapatikana bure, sasa bila gharama yoyote, usisubiri mpaka mlango wa neema ufungwe ndipo uje uutafute, hilo halitawezekana tena, wakati huo ukifika wewe utakuwa ni wa kusubiria tu kwenda jehanamu ya moto, lakini leo hii ukiyasalimisha Maisha yako kwake, licha tu ya kwamba unayo tiketi ya kwenda mbinguni, lakini pia ile damu yake ya thamani iliyomwagika pale msalabani wakati huo huo itaanza kukunenea mema juu ya Maisha yako angali ukiwa bado hapa duniani.

Hivyo tubu ndugu kama bado hujafanya hivyo..maadamu Bwana Yesu ni Rafiki yetu wa kweli, anayetupenda upeo.

Jina lake libarikiwe daima.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

YATAFUTE YALIYO JUU SIKU ZOTE.

Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

NI KITU GANI PETRO NA YOHANA WALIKIGUNDUA KABURINI?

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

NGUVU YA MSAMAHA

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

JIBU: Vipo vyeo vitatu maalumu ambavyo vilimtambulisha Bwana Yesu Kristo…1) Mwana wa Mungu 2) Mwana wa Adamu 3) Mwana wa Daudi. Vyeo hivi kila kimoja kina maana yake..

Sasa kabla ya kuendelea mbele zaidi…ni muhimu kufahamu kuwa cheo cha “Mwana” ni cheo cha “urithi”…Maana yake ni kwamba mfano ukiwa na mtoto wako mmoja wa pekee huyo atarithi kila ulicho nacho…ikiwemo enzi yako yote, mali zako pamoja na hata jina lako…

Sasa katika biblia..mahali popote ambapo Neno Mwana linaanza kwa herufi kubwa…hilo linamzungumzia mtu mmoja tu maalumu ambaye ni Yesu Kristo…lakini ukiona neno “mwana” limeanza kwa herufi ndogo kama hivyo, basi fahamu ni mtu mwingine tofauti na Yesu anayezungumziwa hapo.. Kwa mantiki hiyo basi “wana wa Mungu” wapo wengi lakini “Mwana wa Mungu ni mmoja tu”…mimi na wewe tuliompokea Yesu ni wana wa Mungu….kadhalika wana wa Daudi wapo wengi..lakini “Mwana wa Daudi” ni mmoja tu ambaye ni Yesu…Sulemani alikuwa pia ni ‘mwana wa Daudi’, Hezekia, Yosia, Manase wote hao walikuwa ni wana wa Daudi….Hali kadhalika pia “wana wa Adamu wapo wengi”…mimi ni mwana wa Adamu(au kwa kifupi Mwanadamu)..wewe ni mwana wa Adamu lakini “Mwana wa Adamu” yupo mmoja tu ambaye ni Yesu…ni kama vile miungu wapo wengi lakini Mungu ni mmoja tu!.

Sasa tukirudi kwenye shabaha yetu ya msingi, ambapo tumeona kuwa Neno ‘mwana’ linazungumzia ‘urithi’

Hivyo basi vyeo hivyo vitatu tunaweza kuviweka katika mnyumbuliko ufuatao…1)Mrithi wa Mungu 2) Mrithi wa Adamu na 3) Mrithi wa Daudi.

Sasa unaweza kujiuliza Kristo alirithi nini kutoka kwa hawa watatu?

  1. Mrithi wa Mungu.

Kama mtu ataitwa Mwana wa Mungu maana yake ni kwamba ni Mrithi wa enzi yote ya Mungu na Ukuu …na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo, ambaye alirithishwa vyote.

Waebrania 1:1 “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,

2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika MWANA, ALIYEMWEKA KUWA MRITHI WA YOTE, TENA KWA YEYE ALIUFANYA ULIMWENGU.

3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu”

Kwahiyo hiyo ndio sababu ya Kristo kujulikana kama MWANA WA MUNGU..Ni kwasababu amerithi milki zote za Mungu..

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.

  1. Mrithi wa Daudi.

Cheo cha pili ni cheo cha MWANA WA DAUDI/Mrithi wa Daudi..Sasa ili kujua ni kwanini Kristo aliitwa mwana wa Daudi ni vizuri kumjua kwanza Daudi alikuwa ni nani…(kwa maelezo marefu unaweza kututumia ujumbe inbox tutakutumia somo lake)…lakini kwa ufupi ni kwamba Daudi alikuwa ni mfalme pekee aliyepata Hekima ya kufikiria kumjengea Mungu nyumba ya kifalme katika wa Yerusalemu…na hivyo kumfanya Mungu kuuchagua ule mji kuwa makao makuu yake ya kifalme Duniani (yaani Yerusalemu).

Kama sio Daudi basi mpaka leo pengine Mungu asingekuwa na mji wake maalumu duniani kati ya miji ya Israeli…(Tusingelisikia hili neno Yerusalemu au Sayuni likirudiwa rudiwa katika maandiko, kwani ungekuwa mji kama miji mingine tu, wala ile Yerusalemu mpya kwenye ufunuo pengine ingeitwa kwa jina lingine)…

Lakini Daudi ndiye aliyefanya Yerusalemu ikawa mji wa kifalme wa mwokozi..na Mungu alimwahidi hatakosa mtu wa kukaa katika kiti cha kifalme kutoka katika uzao wake…na katika uzao wake huo yupo mmoja ambaye ni mkuu sana alitabiriwa kutokea huko na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO mwenyewe(kasome Mathayo 1:1-17) ambaye atakuwa mfalme juu ya Dunia nzima! Na ndiye atakayeijenga Yerusalemu mpya ile itakayoshuka kutoka mbinguni…na kukaa na watu wake. Na ndio maana Kristo ilimpasa aitwe mwana wa Daudi kufuatana na yale Daudi aliyoyafanya na kukabidhiwa.

  1. Urithi wa Adamu.

Na cheo cha Mwisho cha Yesu Kristo ni cheo cha MWANA WA ADAMU au Mwana wa mtu,…sasa kama tunavyomjua Adamu alikuwa ni mtu wa kwanza kuumbwa na kupewa Urithi wote na mamlaka yote duniani, kwamba atawale kila kitu, na kwamba viumbe vyote vitamwogopa!….lakini kama tunavyojua aliuuza na kuupoteza ule urithi wake aliopewa na Mungu kwa adui shetani…Hivyo ili urithi huo umrudie tena mwanadamu..basi hakuna budi aje kutokea Adamu mwingine wa pili, ambaye atakaribiana sana kufanana na Yule Adamu wa kwanza,…ambaye ataurithi ule urithi na enzi yote aliyopewa Adamu ya kwanza…

1Wakorintho 15:45 “Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha”.

Adamu wa pili atakuwa ni mwanamume kama Yule wa kwanza, naye atapewa mamlaka kama Yule wa Kwanza wa pale Edeni, na yeye ni lazima awe wa kwanza kuumbwa …na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo..ambaye ndiye limbuko letu rohoni na ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya duniani. Hiyo ndiyo sababu Yesu anaitwa Mwana wa Adamu…ni kwasababu amerithi mamlaka yote na enzi yote Yule Adamu wa kwanza aliyokuwa nayo (aliyopewa na Mungu)..

Mathayo 11:27 “Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia”.

Hivyo Yesu Kristo ndiye Mwanzo na Mwisho, Alfa na Omega…Ndiye mwanadamu kamili, ndiye aliye na mamlaka yote sasa, ndiye mwenye enzi ya kifalme, ndiye Mungu mwenyewe katika mwili. Na ndiye njia ya kufika mbinguni…Kama hujamwamini wala kumpokea…ni vyema ukafanya hivyo kwasababu hakuna njia nyingine yoyote unaweza kumfikia Mungu kama isipokuwa kwa kupitia yeye..

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO, WA KWANZA NA WA MWISHO.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.

Bwana atubariki. Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUTOMZUIA MTOTO WAKO NI DHAMBI.

Shalom, karibu tujifunze biblia…Kuna madhara makubwa sana ya kutombana mwanao..na kumruhusu tu kufanya lolote analojiamulia, kwa kuogopa kuwa atakuchukua…

Mtoto kamwe hawezi kukuchuku! unapomwonya au kumbana.…Hebu jiulize wewe wakati ukiwa mdogo, mzazi wako alipokuzuia au alipokubana ufifanye jambo Fulani je ulimchukia?…ni wazi kuwa hukumchukia zaidi uliona tu ni kama mzazi hakipendi kile kitu na si kwamba hakupendi wewe.

Vivyo hivyo na wewe unapombana mwanao asifanye vitu Fulani Fulani ambavyo unaona vina muelekeo mbaya wa kumletea madhara mwanao huko mbeleni, hufanyi dhambi…unapoona kuna tabia inaanza kukithiri ya kupenda kutazama Tv kwa muda mrefu, usiache kuithibiti hiyo tabia..Unapoona kuna tabia ya kuanza kuzurura zurura…mbane, si kila siku ni ya kwenda kucheza cheza na kutazama Tv, ni lazima ziwepo siku za kujifunza Neno nyumbani, watoto wana vichwa vizuri sana vya kushika mambo/kukariri…Kwahiyo katika hali walizopo ni lazima uwape mistari ya kuishika kichwani, hata kama hawaielewi sasa, lakini itakaa ndani yao kama akiba, watakapokuwa watu wazima itakuwa tayari ipo kichwani, hivyo watakapoanza kuitafakari watakuwa hawana kazi ya pili ya kuikariri tena…

 Na pia ni lazima ziwepo siku za kujisomea masomo ya shuleni wawapo nyumbani, ni lazima yawepo masaa ya kumfundisha mwanao kusaidia vijishuhuli vidogo vidogo..Hata kama hakuna shughuli yoyote ya kusaidia (labda nyumbani wapo wafanya kazi wa kutosha)…usikubali mwanao abweteke, mtengenezee kazi ya kufagia, kupika, kuosha vyombo, kupasi, kufua nguo, kufanya usafi n.k..Pia mtume mahali kama dukani n.k..Na pia unapoona kuna vijitabia vya kiburi na utundu vinaanza basi tumia kiboko kidogo kuvidhibiti…

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

sio dhambi na wala hatakuchukia….Usiusikilize uongo wa shetani moyoni mwako kwamba ukimrudi mwanao atakuchukia…Kamwe watoto hawana chuki, wala vinyongo…

Ukiona mtu anakinyongo na mtu Fulani kwa kitu alichofanyiwa utotoni…kiuhalisia kinyongo hicho kilimwingia baada ya yeye kuwa mkubwa na kukitafakari kile kitu kibaya alichofanyiwa…Lakini katika hali ile ya utoto aliyokuwepo hakuwa na ufahamu huo…Hivyo hata mtoto leo hii ukimwadhibu kwa kosa lolote lile hawezi kukuchukia badala yake atajifunza kutokukifanya kile kitu….na siku atakapokuwa mkubwa ndipo atakumbuka zile adhabu na atakapotafakari kwamba ulikuwa unamwadhibu au ulikuwa unambana kwa kwa faida yake mwenyewe ndipo atakapokupenda zaidi…atasema moyoni mwake kama mama/baba asingenizuia na ile tabia yangu sijui leo ningekuwa wapi..na hivyo atakupenda zaidi kuliko kukuchukia lakini tabia ya kutombana mwanao kwa kuogopwa kuchukiwa…nakuambia ukweli siku mtoto Yule atakapokuwa mtu mzima na kutafakari ni jinsi gani ulivyokuwa unamwangalia tu anapotukana, au anapofanya mambo yasiyofaa pasipo kumwambia chochote atakuchukia na kusema hukuwa unamjali.

Kumbuka Uzao wa Tumbo lako ni thawabu yako mwenyewe…Mtoto uliyepewa ukimtunza vyema ni kwa thawabu yako mwenyewe katika siku za baadaye…

Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, UZAO WA TUMBO NI THAWABU”.

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”.

Pia kama bado hujapata mtoto na umeolewa/umeoa….usiwe na hofu, mwamini Mungu, usijiangalie umri uliopo, hata kama ni miaka 50..wapo waliozaa wakiwa na miaka 90 sembuse wewe mwenye miaka 60?..Kwahiyo wakati wa Mungu ni bora kuliko wa wanadamu..zidi kujitenga na ulimwengu na kuishi maisha ya utakatifu na kumcha Mungu kama kawaida…hayo mengine mwachie Baba, huwa anafanya njia mahali pasipo kuwa na njia, na mahali pasipoonekana dalili….na huwa anarudishaga miaka iliyoliwa na parare kwa watoto wake..Hivyo muamini Mungu na mngojee. Na upatapo mtoto kumbuka siku zote kwamba kutombana kufanya mambo yasiyofaa ni kwa hasara yako mwenyewe na yake pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

USIPUNGUZE MAOMBI.

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani:

Print this post