Title September 2020

How long did it take for Noah to build an ark?

How long did it take for Noah to build an ark?


The Bible does not specify how long it took for the Noah to build an Ark. Some say it was 120 years old, according to Genesis 6:3,

” And the LORD said, My spirit shall not always strive with man, for that he also is flesh: yet his days shall be an hundred and twenty years. “

However his argument can still don’t  make sense. But the Bible also says that Noah begat his sons when he was 500 years old, (Genesis 5:32).And it says he entered the ark at the age of 600 years old, thus making a difference of 100 years , that gap between he probably used to build the ark, but also this argument has a few limitations.

In short, the Bible does not say how long it was built, so it is probably something that is not very important for us to know.

The important thing to know is that, If the first world was flooded with water for the wickedness of mankind, then this second world in which you and I live will also be flooded in the same way because of human evil. Yes it wont be flood by water since God had promised that will never happen again, but the same God promised that the world we are living now will be destroyed by fire.

2 Peter 3:6-7kjv

Whereby the world that then was, being overflowed with water, perished:

But the heavens and the earth, which are now, by the same word are kept in store, reserved unto fire against the day of judgment and perdition of ungodly men.

Sin such as adultery, corruption, hatred, intrigue, drunkenness, homosexuality, blasphemy, lust, abortion, theft and all others are what drowned the first world in the water. And that is what will drown the world we now live in.

Are you saved?

Other articles:

Who is Azazel/ scapegoat we read in Leviticus 16:8?

Is masturbation a sin?

Is it sin to charge interest (unsury)?

WHAT IS LOVE, HOW MANY KINDS OF LOVE ARE THERE?

WHAT IS LOVE, HOW MANY KINDS OF LOVE ARE THERE?

IS IT TRUE, WATER BAPTISM IS NO LONGER NEEDED?

Home:

Print this post

How many children did Ibrahim have?

How many children did Ibrahim have?


Ibrahim had total number of eight(8) children according to the bible, And all were men.

The first son was Ishmael, who was born to a concubine of his wife Sarah, named Hagar (Genesis 16: 1-4).

Second son, was Isaac (The son of promise), who was born 14  years later after the birth of Ishmael.

Genesis 21:1-2 kjv

21 And the Lord visited Sarah as he had said, and the Lord did unto Sarah as he had spoken.

For Sarah conceived, and bare Abraham a son in his old age, at the set time of which God had spoken to him.

When Sarah died, Abraham took another wife, whose name was Keturah. (Genesis 25: 1-2)

This Keturah is the one who When Sarah died, Abraham took another wife, whose name was Keturah. (Genesis 25: 1-2)

This Keturah is the one who was born to Abraham with 6 other sons. To make the total number of Abraham’s children 8,

However the Bible does not say that he had daughters..

Genesis 25:1-2kjv

1 Then again Abraham took a wife, and her name was Keturah.

And she bare him Zimran, and Jokshan, and Medan, and Midian, and Ishbak, and Shuah.

Of Abraham’s descendants, only Isaac was the heir. Other sons were given only gifts, but Isaac was given all, gifts as well as inheritance, because he was the son of the Promised One from God.

Genesis 25:5kjv

And Abraham gave all that he had unto Isaac.

In the same way, we can all become God’s people, created by God, but not all of us are God’s promised children in the likeness of Isaac. The sons of promise are those who have been born again (ie being saved). And these are the ones God has prepared  everything to them, both rewards/gifts and inheritance of the kingdom of heaven.

So you and I should strive to be the sure we all children of promise..

Godbless.

Other Articles:

Did Paul truly worship the angel who he was walking with?

What was the thorn in Paul’s flesh?

HE IS BEING MADE SO MUCH BETTER THAN THE ANGELS

Where did cain get his wife from?

ARE YOU SAVED?

Home:

Print this post

What does mote and beam mean? (Matthew 7:3 )

What does mote and beam mean? (Matthew 7:3 )


A beam is a very large piece of wood, it can be a log, or a pillar, or any wide plank.

But a mote is a very tiny piece of wood, like a sand, even the dust of wood that is very hard to see is still a mote/speck.

Now the Lord Jesus gave that parable, to emphasize what He wanted to say, that is, in a normal situation, if you can’t see the pillar of wood standing in front of your eyes blocking you from seeing everything ahead, how will you be able to see the wooden dust in your partner’s eye?

See, without doubt, that is hypocrisy.

In the same way, before we judge people, let us examine our lives first. what they do, are we not doing them? Before you point finger to someone who is gossiping, be sure first those things are not in you? If not then it is better to keep quiet, because the verses above say, with what measure ye mete, it shall be measured to you again.

Matthew 7:1-5

7 Judge not, that ye be not judged.

For with what judgment ye judge, ye shall be judged: and with what measure ye mete, it shall be measured to you again.

And why beholdest thou the mote that is in thy brother’s eye, but considerest not the beam that is in thine own eye?

Or how wilt thou say to thy brother, Let me pull out the mote out of thine eye; and, behold, a beam is in thine own eye?

Thou hypocrite, first cast out the beam out of thine own eye; and then shalt thou see clearly to cast out the mote out of thy brother’s eye.

May the Lord help us all to overcome that.

Other articles:

Are all sins equal? and have the same punishment?

What was the thorn in Paul’s flesh?

What was the thorn in Paul’s flesh?

What is the difference between a dream and a Vision?

What is the difference between a dream and a Vision?

Is it a sin to get a tattoo?

Home:

Print this post

Who is Azazel/ scapegoat we read in Leviticus 16:8?

Who is Azazel/ scapegoat?


The word Azazel/scapegoat is mentioned only once in the bible, we read it in the book of Leviticus chapter 16.

Azazel was not a man or a priest but a goat set apart for the atonement of the sins of the children of Israel, was not slaughtered for sin like any other goat but was taken alive to the wilderness and abandoned there. such kind of goat is known by that name.

These instructions was given to the children of Israel by God, to be held  on the great day of Atonement only once a year, on the 10th day of the seventh month of the Jewish calendar, when the High Priest went to atone for the sins of all the Jews

On that day no one was allowed to work, but to dwell in his house, tormenting himself with his own sins.

Now in this day the High Priest is first responsible for making atonement first for himself and for his people ( his households), and then he goes to make atonement for the sins of others, otherwise he will die.

After he has finished to make an atonement for his sins now he is ready to make atonement for the children of Israel, here he was commanded to take two goats from the congregation for a sin offering and one ram for a burnt offering (Leviticus 16:5), after which the high priest stood before the tabernacle and voted between the two goats.

Leviticus 16:7 KJV

And he shall take the two goats, and present them before the Lord at the door of the tabernacle of the congregation.

When he has finished, one is taken for the burnt offering for the sins of all the people, then his blood was sprinkled in the tent of meeting and the altar, and the second one is not killed but rather the high priest puts both his hands on the horns of the goat (who is called Azazel) and then the priest confesses all the sins of children of Israel which they have committed against God, before the goat that stood before them, after which the goat is delivered to one man  and then taken to the desert far away from the dwelling of the people and get abandoned there. Then due to that act the iniquity of Israel is covered.

Leviticus 16:21-22 KJV

21 And Aaron shall lay both his hands upon the head of the live goat, and confess over him all the iniquities of the children of Israel, and all their transgressions in all their sins, putting them upon the head of the goat, and shall send him away by the hand of a fit man into the wilderness:

22 And the goat shall bear upon him all their iniquities unto a land not inhabited: and he shall let go the goat in the wilderness.

It is a complete picture we see in the New Testament, Christ as our Azazel took our sins and all our accusations, was crucified outside the city, was counted as Nothing for us. And through him our sins are blotted out, unlike the goat who in the coming year should be given another… How happy you are to be redeemed by Christ,. If you have been forgiven of your sins, you have been forgiven indeed.

Hallelujah.

Other articles:

HE IS BEING MADE SO MUCH BETTER THAN THE ANGELS

Who is Jeshurun  in the bible?

What is the difference between a dream and a Vision?

Who is the Holy Spirit?

FOR I KNOW THE THOUGHTS THAT I THINK TOWARD YOU.

Home.

Print this post

NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!

Shalom, nakukaribisha tuyatafakari Pamoja maneno ya uzima.

Katika hichi kipindi cha mwisho, kuna mwitikio mmoja tu, ambao utamtambulisha bibi-arusi wa kweli wa Kristo ni nani..

Kumbuka bibi-arusi ni tofauti na Suria, Sulemani alikuwa na Masuria 700 lakini wake au (bibia-arusi) walikuwa ni 300 tu. Tofauti ya mke na suria ni kuwa mke anauhalali wa vyote ikiwemo urithi na mali, lakini suria yeye anaweza kupewa vyote lakini sio urithi au jina..Jambo hilo utaliona kwa Ibrahimu, ambaye mbali na Isaka alikuwa pia na watoto wengine 7, lakini wao walipewa zawadi tu, mashamba, majumba n.k..Lakini Isaka peke yake ndiye aliyepewa vyote, zawadi pamoja na urithi na jina,..Na ndio maana mpaka leo, tunamtambua Isaka, na sio wale wengine..Hiyo ni kwasababu walikuwa ni wana wa Masuria na sio wana wa mke halali kama ilivyokuwa kwa Sara. (Kasome Mwanzo 25:5-6)

Ndivyo hivyo hata wakati huu wa mwisho, haya makundi mawili yapo, hivyo usifurahie tu, Mungu kukubariki, usifurahie tu Mungu kukupa hiki au kile..furahia pale unapokuwa na uhakika kuwa wewe ni mrithi wa ahadi za milele za Mungu baada ya Maisha haya..

Kwasababu Masuria sikuzote ni wengi kushinda wake.

Sasa tukirudi katika kitabu cha ufunuo, utaona sehemu nyingi, Bwana Yesu alianza kulitamka  hili Neno “tazama, naja upesi”;.. Utasoma..

Ufunuo 22:7 “Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki….

12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Hiyo ni kuonyesha kuwa wakati wake wa kurudi duniani umekaribia sana..

Lakini ukishuka chini kidogo utaona, wanaorodheshwa wawili walioitikia mwito huo, nao ni Roho Mtakatifu na bibi-arusi.

22:17 “NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.

Ni kwasababu gani bibi-arusi alikuwa na ujasiri wa kuitikia mwito huo “Njo Bwana Yesu”? Ni kwasababu, alijua urithi wake halisi upo karibu, ni kwasababu alikuwa na ajasiri wa Imani yake, kwa Yule Roho Mtakatifu aliye ndani yake.

Na ndio maana hata Mtume Yohana, aliposikia Bwana akiyarudia maneno hayo tena chini kidogo, naye pia aliitikia kwa ujasiri mkubwa na kusema amina na uje Bwana Yesu..

Ufunuo 22:20 “Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu”.

Maneno haya bibi-arusi tu peke yake aliyejazwa Roho Mtakatifu ndio atakayekuwa na ujasiri wa kuyasema wakati huu wa mwisho..

Swali la kujiuliza ni je! mimi na wewe tunaweza kuyasema maneno hayo? kumbuka Jibu halipo katika vinywa vyetu bali katika mioyo yetu. Kama hatuna ujasiri huo basi sisi sio bibi-arusi, haijalishi tutasema tumeokoka kiasi gani, sisi tutakuwa ni Masuria tu. Na siku ya unyakuo itakapofikia tutabaki hapa dunia, hatutanyakuliwa Pamoja na bibiarusi wa kweli.

Masuria kwa jina lingine ndio wale wanawali wapumbavu ambao walichukua taa zao, lakini hawakuwa na mafuta ya ziada katika vyombo vyao, Na Bwana arusi alipokuja walikutwa hawana mafuta ya kutosha (Mathayo 25)

Kwahiyo ndugu tusifurahie tu, kusema sisi ni wakristo, bali tufurahie kusema sisi ni bibi-arusi, tuliojazwa Roho Mtakatifu.. Kumbuka lile neno la Bwana “Waitwao ni wengi, ila wateule ni wachache”

Kama tulishaokoka, lakini bado tulikuwa tunaishi maisha ya uvuguvugu, basi  huu ni muda wetu sasa, kuzitengeneza taa zetu katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho.

Na Mungu atatujalia tufikie mwisho mwema kwa neema zake.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIEPUSHE NA UNAJISI.

Jina La Bwana wetu Yesu libarikiwe. Karibu tuyatafakari maandiko tena siku ya leo.

Kuna mtafaruku mkubwa sana katika ukristo kuhusu vyakula, wapo wanaoamini kuwa vipo vyakula najisi na wapo wanaoamini kuwa vyakula vyote ni halali kuliwa. Na hivyo kusababisha mashindano yasiyoisha.

Kama tukiyasoma maandiko tutaona kuwa vyakula haviwezi kumtia mtu unajisi. Ingawa hatuwezi kusema kwamba vyote vinafaa, hapana si vyote..huwezi kula mbao, au chuma, au sumu au pombe na kusema vinafaa…hapana hivyo havifai kwasababu vinauharibu mwili badala ya kuujenga.

1Wakorintho 10:23 “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.

Kwahiyo kama umehakiki hicho ulacho hakina madhara katika mwili wako, basi kula! Si dhambi..lakini kama umehakiki kwamba kina madhara basi usile. Na pia kama unawasiwasi na mashaka kwamba hicho ulacho kinaweza kuwa na madhara basi usile kabisa. Kwasababu hata usipokula hutendi dhambi!!

Warumi 14:22 “ Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.

23 Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi”.

Sasa leo hatutaingia sana kujifunza juu ya vyakula, kama utahitaji somo juu ya hilo, basi utatujuza inbox..Lakini tutajifunza namna ya kuepukana na unajisi, kwa kupitia maandiko yafuatayo ambayo ni maarufu sana.

Tusome…

Marko 7:5 “Basi wale Mafarisayo na waandishi wakamwuliza, Mbona wanafunzi wako hawaendi kwa kuyafuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi?……………………………..

14 Akawaita makutano tena, akawaambia, Nisikieni nyote na kufahamu.

15 Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu.

16 Mtu akiwa na masikio ya kusikilia, na asikie.]”

Sasa maneno haya Bwana wetu Yesu aliwaambia makutano, ambao pengine idadi yao ilikuwa ni mamia au maelfu, na ndani ya mkutano huo walikuwepo pia wanafunzi wake wale 12, Na kwa Pamoja wakasikia maneno hayo…kwamba hakuna kimwingiacho mtu kimtiacho unajisi bali kimtokacho..sasa baada ya maneno hayo kama umefuatilia kwa makini Bwana hakuendelea kuongea zaidi. Hivyo kila mmoja akatoka na tafsiri yake kichwani…naamini wengi walifiki kwamba ni kimwingiacho mtu ni chakula na kimtokacho ni matapishi au kinyesi na mkojo..na kwamba hivyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi..Lakini ule mkutano wote ulitawanyika ukidhani umemwelewa Bwana vizuri kumbe hawakumwelewa hata kidogo..

Baadaye ndipo wanafunzi wake wakahisi kuna kitu hawakukielewa na hivyo wakaamua kumfuata wakiwa peke yao kumwomba awafafanulie zaidi..

Tusome..

“17 Hata alipoingia nyumbani, ameuacha mkutano, wanafunzi wake wakamwuliza habari za ule mfano. 18 Akawaambia, Hivi hata ninyi hamna akili? Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia unajisi;

19 kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni tu; kisha chatoka kwenda chooni? Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote.

20 Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.

21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,

22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.

23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”.

Umeona hapo?. Wanafunzi wamepata ufafanuzi vizuri, lakini makutano hawakupata!..Makutano wameondoka wakidhani unajisi ni majasho, matapishi, haja kubwa na haja ndogo…Kumbe sivyo!. Vitu najisi ni vile vinavyotoka moyoni na si mwilini…

Unapopita barabarani na kwa bahati mbaya ukasikia matusi yakitukanwa… yale yanaingia moyoni mwako, na kwenda kwenye hazina ya kumbukumbu zako, (hapo hakuna unajisi)..lakini unapopitia hali ya kuudhiwa siku za mbeleni na kwenda kuifungua ile hazina na kisha kuyatumia yale matusi uliyoyasikia huko nyuma na kumtukana mwingine hapo ndipo unapokuwa najisi.

Unapoona mauaji yamefanyika ambayo sio wewe umeyafanya kwamfano mauaji ya utoaji mimba..Jambo lile linakwenda kwenye hazina ya moyo wako, hapo hujawa najisi, lakini siku moja ukapata ujauzito na ukaenda kuutoa au mwingine akapata ujauzito na ukamshauri akaitoe, hapo tayari umekuwa najisi. Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo.

Na mtu najisi mbele za Mungu ni mtu mchafu..Katika agano la kale mtu najisi alikuwa haruhusiwi hata kuingia katika kusanyiko la Mungu, anatengwa mpaka atakaposafishika…Na hata sasa bado unajisi upo!..Ukiwa mlevi tayari umejitia unajisi, ukiwa mwasherati, mzinzi, muuaji, mtukanaji, mlawiti, mtazamaji picha za tupu, msengenyaji n.k tayari wewe ni najisi mbele za Mungu, hustahili kuwepo katika kundi la Mungu, haijalishi umeshakuwa mkristo kwa miaka mingapi, bado ni najisi mbele za Mungu, kwamba unahitaji kutubu..Na kujitenga na hayo mambo.

Tito 1:15 “Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia. Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai”.

Kama hujaokoka! Kristo anakupenda na alikufa kwa ajili yetu..Wokovu unapatikana bure leo, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kupiga magoti binafsi, na kutubu mbele zake kwa dhati kabisa..Kama umemaanisha kweli pale utakaposema tu Amen, basi tayari ameshakusikia na kukusamehe..na utaona amani ya ajabu imeingia moyoni mwako, baada ya hapo nenda katafute ubatizo sahihi wa kimaandiko, ambao ni ule wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo, ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (Mathayo 28:19, Matendo 2:38)..Kwa kuyatii maagizo hayo machache na mepesi utakuwa utakuwa umeihakikishia mbingu kuwa kweli umeanza umegeuka na hivyo Mungu atakuheshimu zaidi. Na utakaso halisi wa Kristo utakuja ndani yako.

Bwana akubariki.

Kama umeokoka usisahau kuliombea Kanisa Pamoja na wakristo wote na watumishi wa Mungu kila siku..

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hazama ni nini katika biblia?(Ezekieli 16:12, Kutoka 24:47)

Hazama ni nini?


Hazama ni pete ya puani.

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

Mwanzo 24:47, Kutoka 35:22,

Na pia ukisoma Ezekieli sura ya 16 yote utaona jinsi Mungu anavyolilinganisha taifa la Israeli na msichana ambaye alipozaliwa tu alitelekezwa porini na wazazi wake akiwa hata hajakatwa kitovu chake. Na Bwana alipokuwa anapita (hapa akijifananisha na mwanaume fulani), alimwona na kumuhurumia, akamchukua na kwenda kumtunza, akamkuza,  akafanya naye maagano kuwa atakuwa wake, akamkuza vizuri sana, akawa mrembo sana, akamvisha mavazi mazuri, na kumpamba kwa kila aina ya mapambo ikiwemo hazama na vikuku, lakini baadaye alipokuja kuwa mtu mzima alikengeuka na kuanza kuzini na wanaume wengi, na kuwa kahaba wa kipindukia, ..

Ezekieli 16:11 “Nikakupamba kwa mapambo pia, nikatia vikuku mikononi mwako, na mkufu shingoni mwako.

12 NIKATIA HAZAMA PUANI MWAKO, na pete masikioni mwako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.

13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha; na mavazi yako yalikuwa ya kitani safi, na hariri, na kazi ya taraza; ulikula unga mzuri, na asali, na mafuta; nawe ulikuwa mzuri mno, ukafanikiwa hata kufikilia hali ya kifalme.

14 Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kwa sababu ya uzuri wako; kwa maana ulikuwa mkamilifu, kwa sababu ya utukufu wangu niliokutia, asema Bwana MUNGU”.

Lakini sasa mfano huo haumaanishi kuwa wanawake wa ki-kristo wanaruhusiwa kujipamba hapana, kumbuka huo ni mfano tu ambao Mungu aliutoa kuonyesha ni jinsi gani Israeli taifa lake alilolipamba rohoni kwa utukufu wake, tangu zamani, baadaye likaja kukengeuka kuabudu miungu mingine tofauti nay eye.

Biblia inasema..

1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.

3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu”.

Umeona, mwanamke wa kikristo hapaswi kuweka hazama, au vikuku, au lipstick, au wanja, au mikufu, au hereni mwilini mwake, badala yake mapambo haya anapaswa ayahamishie rohoni, kwa matendo mema. Ndivyo biblia inavyoagiza.

Kwahiyo kama wewe ulikuwa unaweza hazama au vipini puani mwako, ni vyema ukaacha. Ishi sasa maisha ya kama wanawake wacha Mungu walivyoyaishi. Mapambo yasikusababishe uikose mbingu.

Shalom.

Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MASERAFI NI NANI?

Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.

Katika biblia shetani amepewa majina tofauti tofauti na hiyo ni kutokana na aina ya kazi anazozifanya hapa duniani, kwamfano biblia inapomwita shetani/ibilisi ni kwasababu ni mpinzani na mshitaki wa roho zetu kwa Mungu ndio tafsiri ya jina hilo,.

Vilevile sehemu nyingine inapomwita Joka (Ufunuo 12), ni kwasababu ni mwongo kama alivyokuwa nyoka, na anameza roho za watu kama majoka yafanyavyo kumeza wanyama,..

Bado sehemu nyingine inamwita, mkuu wa ulimwengu huu, (Yohana 12:31,2Wakorintho 4:4), kwasababu mambo yote yaliyotukuka ulimwenguni sasa yanashikiliwa na yeye, yeye ndiye kiongozi wa hayo ..

Pia inamwita mfalme wa uweza wa anga (Waefeso 2:2) kwasababu nguvu zote za giza katika ulimwengu wa roho anazishikilia yeye, baba wa mapepo na wachawi duniani.

Vilevile sehemu nyingine inamwita mjaribu (Mathayo 4:3,1Wathesalonike 3:5), kwasababu, yeye ndio chanzo cha majaribu yote kwa mkristo..Na ndio maana Bwana Yesu alituambia kesheni mwombe msije ingia majaribuni..Kwasababu tusipoomba huyu atapata nafasi kubwa ya kutuletea majaribu ili kutuangusha.

Lakini zaidi ya yote biblia inatuonyesha kuwa atakuja kuwa na jina lingine, lijulikanalo kama Abadoni au Apolioni,.. Tafsiri ya jina hili ni MHARIBIFU…Ikiwa na maana atakuja kuwa na kazi ya kufanya uharibifu tu.

Kama leo hii unamwona shetani ni mharibifu, basi bado haujajua vizuri uharibifu wake upoje.

Tukisoma kitabu cha ufunuo, kama tunavyojua mara baada ya unyakuo wa kanisa kupita, kutafuata matukio ambayo hayaelezeki kwa namna ya kawaida. Tukiachana na yale mapigo ya vile vitasa 7 na ile siku ya Bwana mwenyewe ambayo jua hili litaondolewa, kutatangulia kwanza mapigo ya baragumu 7,..Sasa hatuwezi kuyachambua yote hapa, ikiwa utahitaji somo lake utuambia inbox tukutumie..

Lakini leo tutatazama, baragumu la tano, ambalo ndio kiini cha somo letu la Leo. Baragumu hilo litakapopigwa, biblia inatuambia, Shimo la kuzimu litafunguliwa na humo watatoka nzige wabaya sana..tusome;

Ufunuo 9:1 “Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu.

2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni.

3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi.

4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao.

5 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama kuumwa na nge, aumapo mwanadamu.

6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia.

7 Na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita, na juu ya vichwa vyao kama taji, mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu.

8 Nao walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.

9 Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani.

10 Nao wana mikia kama ya nge, na miiba; na nguvu yao ya kuwadhuru wanadamu miezi mitano ilikuwa katika mikia yao.

11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni ABADONI, na kwa Kiyunani analo jina lake APOLIONI.

Sasa hapa biblia imetumia tu lugha ya mfano ili upate halisi ya jinsi mambo yatakavyokuwa.. Hapo anasema wakatoka nzige..Sasa hao sio nzige halisi bali hayo ni Mapepo (maroho) ambayo kwasasa yapo kifunguni..Kumbuka si idadi yote ya mapepo yafayanyayo kazi sasa, yapo mengine mengine yapo kifungoni, biblia inasema hivyo katika kitabu cha Yuda.

Sasa mapepo hayo Yamefananishwa na wale Nzige waharibifu wa mazao, na ulimwengu umefananishwa na shamba lenye mazao (Mathayo 13:38) Na kama unavyojua nzige wakipita mahali kwenye mazao ya kijani, kitendo cha masaa machache tu, hilo shamba linageuka na kuwa vijiti tu.. Ni tishio kubwa sana duniani hata sasa, fuatilia tu habari ya nzige wa jangwani walipopita Afrika Mashariki kipindi cha hivi karibu uone uharibifu wao ulivyokuwa tishio.

Sasa tunajuaje kama haya ni mapepo na si nzige halisi, ni kwasababu hayajapewa kudhuru nchi, bali wanadamu ambao hawana muhuri wa Mungu duniani. Kazi hiyo huwa inafanywa na shetani mwenyewe na malaika zake, Soma Ufunuo 7 utaona hao ambao watakuwa wameitiwa muhuri ni wakina nani. Lakini kama ikitokea unyakuo leo hii umekupita, ujue kuwa mambo hayo yatakukuta tu..

Mapepo haya yatakayoachiliwa kutoka kuzimu na moja kwa moja yatapokea oda kutoka kwa kiongozi wao mkuu shetani/Apolioni/Abadoni, kwa lengo la KUWAHARIBU wanadamu tu. Kama jinsi atakavyojulikana kwa jina hilo.

Mapepo haya yatawaingia watu, bila kizuizi chochote, mengine yatawafanya watu kuwa vichaa, na kuwatesa tu kama yalivyomtesa Yule bwana aliyekutana na Yesu kule makaburini, mengine yatawafanya watu wawe wakatili kupita kiasi, kuchukiana kitaongezeka mara nyingi zaidi, kugombana, kuumizana, na kuuana n.k. mengine yatawafanya watu wapate ajali lakini si za kuwaua, bali za kuwaumiza tu vibaya..

Mengine yatawaletea watu magonjwa yasiyo ya kawaida lakini hakuna kifo, kama vile wakati wa Ayubu, siku hiyo kama hukwenda kwenye unyakuo utakaa kwenye majivu ya kila namna kujipoza lakini wapi, utatamani kufa lakini kifo kitakukimbia, yaani kwa ufupi duniani kutakuwa na watu ambao si watu, maroho hayo yatafanya uharibifu usio kuwa wakawaida.

Mioyo ya wanadamu itaharibiwa kwa kiwango cha juu sana, na kama vile yanavyofananishwa na nzige maana yake ni kuwa mpaka hicho kipindi chao kiishe, watu watakuwa kama makapi tu, wamechoka sana..

Huo wakati ndugu yangu, si wa kuwepo, ukisikia hizi ni siku za mwisho, usidhani unyakuo ukishapita mambo yatakuwa kama unavyoyaona leo.. Ni Roho Mtakatifu ndani ya kanisa lake ndiye anayezuia hayo mambo kwasasa. Lakini kuna wakati utafika, ataondolewa, na akiondolewa anaondoka na kanisa lake takatifu (Ndio unyakuo wenyewe).Kitakachosalia duniani ni vilio tu na kusaga meno (Mathayo 25:30).

2Wathesalonike 2:5 “Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?

6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; LAKINI YUKO AZUIAYE SASA, HATA ATAKAPOONDOLEWA”.

Swali la kujiuliza, Je! Bado tunaudharau wokovu wa Yesu?.

Je! Bado tunaishi maisha ya kutokujali, mpaka haya mambo yote yatukute? Kama ndivyo ni heri tuyakabidhi maisha yetu kwa Bwana leo, ayaokoe. Vilevile tukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na Kwa jina la YESU KRISTO tupate ondoleo la dhambi zetu. Bwana wetu ni mwingi wa huruma, anatuonya mbele kabla ya mambo hayajatokea kwa ghafla. Hivyo mpokee Kristo leo na atakufanya kiumbe kipya, ulimwengu unapita na mambo yake yote, lakini Kristo na Neno lake wanadumu milele. Na yeye anatuambia itatufaidia nini kuupata ulimwengu mzima na kupata hasara za nafsi zetu?

Bwana atusaidie, Bwana atubariki sote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

UFUNUO: Mlango wa 10.

Nini maana ya maneno haya ya Bwana? “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mavu ni nini katika biblia?(Kutoka 23:28, Kumb 7:20)

 Mavu ni nini?


 Mavu ni wadudu jamii ya nyuki, kwa jina maarufu ni NYIGU. Maumbile yao ni makubwa zaidi ya nyuki wa kawaida, Na mauvimu yao ni kama tu yale ya nyuki..

Wametajwa mara kadha wa kadha katika biblia, na hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowaelezea;

Kutoka 23:27 “Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao.

28 NAMI NITAPELEKA MAVU MBELE YAKO, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako.

29 Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja; nchi isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua”.

Kumbukumbu 7:19 “uyakumbuke hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako; ndivyo atakavyowafanya Bwana, Mungu wako, mataifa yote unaowaogopa.

20 Tena Bwana, Mungu wako, ATAMPELEKA MAVU KATI YAO, hata hao watakaosalia, hao wajifichao, waangamie mbele zako.

21 Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho”.

 

Yoshua 24:11 “Nanyi mliuvuka Yordani, mkafika Yeriko; nao watu wa Yeriko wakapigana nanyi, Mwamori, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhiti, na Mgirgashi, na Mhivi, na Myebusi; nami nikawatia mikononi mwenu.

12 NIKATUMA MAVU MBELE YENU, waliowafukuza mbele yenu hao wafalme wawili wa Waamori, si kwa upanga wako, wala kwa upinde wako”.


 Katika mistari hiyo tunaona Mungu alivyowatumia wadudu hawa mavu kama silaha ya kuwafukuza maadui wa Israeli. Kufunua kuwa wapo mavu wa rohoni, ambao Mungu huwa anawatuma kuwafukuza maadui wa watakatifu duniani sasa.

Na mavu wenyewe ni malaika wa Bwana, na maadui wa watakatifu ni majeshi ya mapepo.. Mtakatifu yeyote rohoni huwa analindwa na kundi la malaika wa Bwana, hivyo shetani na mapepoo yake hawezi kumgusa kwa namna yoyote.

Lakini ikiwa mtu yupo nje ya Kristo, ibilisi ni lazima awe na mamlaka juu ya mwili wako. Na mapepo pia ni lazima yatajiamulia kufanya chochote yapendacho ndani yako, kwasababu hawapo mavu wa kukulinda wewe.

Kama hujaokoka na unahitaji kuokoka leo, basi fungua hapa kwa ajili ya sala ya Toba, >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Kumbuka Ni kwa Yesu tu unaweza kuwa salama pengine pote unapotea.

Bwana akubariki.

Tazama na tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Neno beramu lina maana gani katika biblia?

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Pomboo ni nini?


Pomboo ni aina ya samaki jamii ya nyangumi anayeishi baharini, Anajulikana kwa jina maarufu la DOLPHIN, Ni samaki anayezaa, pia ananyonyesha, lakini zaidi ya yote anasifa ya kuwa mnyama mwenye akili nyingi kuliko wote ulimwenguni baada ya mwanadamu. Na kuwa na tabia ya uokozi. Tazama picha juu.

Samaki huyu ni rahisi kufundishika, na ni rahisi kuishi na wanadamu.

Katika biblia pomboo(Dolphin) ametajwa sehemu nyingi, hususani katika matumizi ya ngozi yake, ambayo ilitumika katika kutekengeza hema ya kukutania, pamoja na vitu vingine vitengenezwayo kwa ngozi, kama vile viatu vya thamani.

Hivi ni baadhi ya vifungu katika biblia vinavyomtaja Pomboo.

Kutoka 25:3 “Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii; dhahabu, na fedha, na shaba,

4 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na nguo za kitani safi, na singa za mbuzi;

5 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na NGOZI ZA POMBOO, na miti ya mshita,

6 na mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka, na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri”;

 

Kutoka 26:14 “Nawe fanya kifuniko cha ile hema, cha ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake KIFUNIKO CHA NGOZI ZA POMBOO.

15 Nawe fanya hizo mbao za maskani za mti wa mshita, zenye kusimama”.

 

Kutoka 35:5 “Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba;

6 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani nzuri, na singa za mbuzi;

7 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na NGOZI ZA POMBOO, na mbao za mshita”;

 

Ezekieli 16:9 “Kisha nikakuosha kwa maji; naam, nalikuosha kabisa damu yako, nikakupaka mafuta;

10 nikakuvika nguo ya taraza, nikakupa VIATU VYA NGOZI YA POMBOO, nikakufunga nguo ya kitani safi kiunoni mwako, nikakufunika kwa Hariri”.

Mistari mingine ni kama hii;

(Kutoka 35:23, 36:19, 39:34, Hesabu 4:6,8,10,11,12,)

Ni kwanini Mungu aliruhusu hema ya kukutania ifunikwe na ngozi ya samaki hodari (pomboo)?

Kumbuka, wana wa Israeli, waliwashinda maadui zao kabisa kabisa, kwa njia ya habari tu,.pale walipojaribu kuvuka kama wao waligharikishwa,.Hivyo ni kama samaki hodari Mungu aliwavusha baharini pasipo wao kuzama..

Hiyo ni kuwakumbuksha kuwa kila watakapokusanyika mbele ya Hema, na kuitazama hiyo hema iliyofunikwa kwa ngozi ya pomboo, wakumbuke wema wa Mungu aliowafanyia wakati wanaivuka bahari ambayo kwa namna ya kawaida haiwezekani mwanadamu yeyote kuivuka isipokuwa samaki tu peke yake..

Hivyo wamtukuze yeye, na kumpa shukrani zote peke yake.

Bwana akubariki.

Tazama maana maneno mengine ya biblia chini;

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

Kamsa ni nini kwenye biblia? (Sefania 1:16, Wimbo 3:8)

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MPINGA-KRISTO

Rudi Nyumbani:

Print this post