Shalom. Karibu tujifunze Neno la Mungu, maadamu ule mwisho unakaribia..
Kila siku tunapaswa tukumbuke kuwa wokovu ni tunu ya thamani ambayo tunapaswa tuishikilie kwa gharama zozote, wokovu kuupata ni rahisi sana, lakini kuushikilia mpaka mwisho si kitu kirahisi, kwasababu kuna ufalme mwingine (wa giza) hapa duniani ambao upo mahususi kwa kazi hiyo moja tu ya kuhakikisha watu wanaupoteza wokovu hata kama walikuwa wameshaupata.
Na ndio hapa wahubiri tunapaswa tusisitize kwa watu, Kwasababu ndivyo walivyofanya hata na mitume (baba zetu wa imani), ukiangalia utaona mafundisho yao yote yalikuwa ni ya kutilia msisitizo suala la kuishindiania imani, wakatuambia TUISHINDANIE imani ambayo tumekabidhiwa sisi watakatifu mara moja tu.
Yuda 1:3 “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu”.
Sio kwamba walikuwa hawaoni fursa za kibiashara zilizokuwa zimewazunguka mitaani mwao, walikuwa wanaziona, pengine hata zaidi ya sisi, lakini hawakuona sababu ya kutuandikia kwenye hichi kitabu kinachoitwa biblia, kwasababu walijua vita hasaa vipo wapi, mapambano hasa ya mwanadamu duniani yapo wapi..
Tukumbuke kuwa tukibadilishwa maisha yetu, na kufanywa kuwa viumbe vipya, mambo hayatabakia kuwa vilevile kama yalivyokuwa mwanzoni.. Shetani ni lazima aamke na kuanza kuuwinda wokovu wako kwa gharama zozote zile.. atakuchukia kwa ukomo wa chuzi pale tu atakapokuona unaanza kupiga hatua katika wokovu wako, na sio katika mafanikio ya biashara yako, shida yake kubwa ni Imani yako.
Na katika kipindi ambacho unapaswa ujiandae kukutana naye uso kwa uso basi ni wakati ambapo umeanza maisha mapya ya wokovu.
Lakini kama usipoliweka hilo akilini, ukaambiwa ukiokoka basi, wewe ni wa mbinguni moja kwa moja, njoo sasa tukufundishe mambo mengine ya kidunia..Nataka nikuambie maisha yako ya rohoni yapo hatarini sana kugeuka.(Ndio maana kuna kundi kubwa la wakristo waliorudi nyuma leo hii).
Kwasababu shetani ni lazima atahakikisha analeta mambo mawili kwako, la kwanza ni DHIKI, na la pili ni UDHIA.
Mathayo 13:20 “Naye aliyepandwa penye miamba, huyo ndiye alisikiaye lile neno, akalipokea mara kwa furaha;
21 lakini hana mizizi ndani yake, bali hudumu kwa muda; ikitukia dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa”.
Dhiki, ni mateso unayoyapata kutokana na kile ulichokiamini; Na udhia ni maudhi utakayoyapata kutoka kwa watu, kwa kile unachokiamini, huu ndio wakati ambapo pengine hata ndugu/familia hawatakuelewa au watakutenga, ni wakati ambapo pengine utajikuta unapingwa na viongozi wako wa dini, au wanakupiga na kukufunga kisa tu umemfuata Yesu, au umekuwa na msimamo Fulani wa Neno la Mungu, ni wakati ambapo mambo yako yanaweza yasiende sawa, utapitia kuvunjwa moyo mara kadhaa, lakini Mungu atakuwa pamoja na wewe, kumbuka yote hayo yanasababishwa na shetani, ili tu kukutikisha urudi ulipotoka. Yanatokea kwa ruhusa maalumu kutoka kwa Mungu.
Lakini ni ya muda tu, hayawezi kudumu milele, Mungu hawezi kuruhusu yadumu milele. Kuna kipindi kitafika yataisha. Lakini ni wachache sana wanaoweza kuvumilia hata hicho kipindi kiishe..
Na hapa ndipo watu wengi wanaporudi nyuma. Na kuuacha wokovu. Kwasababu hawakujiandaa kwa huo wakati.
Kumbuka kuwa tutaufikia mwisho mzuri wa imani, kwa kuishindania kwa gharama zozote na kwa kuvumilia..hilo tu.
Luka 8:15 “Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda kwa kuvumilia”.
Bwana atusaidie tuweze kuyashinda hayo yote.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kamsa ni nini?
Kamsa ni Ukelele wa habari ya moto au vita (kwa lugha ya kiingereza-Battle cries)
Vifungu hivyo vinaeleza Neno hilo;
Wimbo 3:8 “Wote wameshika upanga, Wamehitimu kupigana; Kila mtu anao upanga wake pajani Kwa hofu ya KAMSA ZA USIKU”.
Sefania 1:15 “Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,
16 Siku ya tarumbeta NA YA KAMSA, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.
17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.
18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha”.
Unaona? Ile siku kuu ya Bwana imefananishwa na ya kama kelele za vita..ambazo huwa zinatokea ghafla..Mfano tu wa Wana wa Israeli walivyozizunguka zile kuta za Yeriko kwa muda wa siku 7 na siku hiyo hiyo ya saba, wakapiga kelele kubwa sana (Kamsa) kuashiria kuwa vita vimeanza..
Na baada ya kilele kutoka, zile kuta za Yeriko zilizama chini saa ile ile, na biblia inatuambia mioyo ya watu wa Yeriko ikayeyuka (Yoshua 5:1) wakaishiwa nguvu kabisa.
Yoshua 6:20 “Basi watu wakapiga kelele, na makuhani wakazipiga tarumbeta; hata ikawa, hapo watu waliposikia sauti ya tarumbeta hao watu wakapiga kelele kwa sauti kuu sana, na ule ukuta wa mji ukaanguka nchi kabisa, hata watu wakapanda juu, wakaingia katika mji, kila mtu akiendelea kukabili mbele; wakautwaa huo mji.
21 Basi wakaangamiza kabisa vitu vyote vilivyokuwa ndani ya mji, wanaume na wanawake, watoto na wazee, na ng’ombe, na kondoo, na punda, kwa makali ya upanga”.
Ndivyo itakavyokuwa katika siku ule ya Mwisho Kristo atakapotokea mawinguni na malaika zake watakatifu.. Tarumbeta na Kamsa italia kutoka mbinguni, kuashiria kuwa mwisho wa kila mwenyewe dhambi umefika..
Siku hiyo kila jicho litamwona, na mataifa yote wataomboleza kwa kilio kisichoweza kuelezeka, lakini hiyo haitasaidia, waovu wote watakuwa kama mizoga juu ya dunia nzima. Ndugu tusitamani tuwepo katika hicho kipindi kibaya sana.
Soma Ufunuo sura ya 19 na 20 yote uone jinsi waovu watakavyoangamizwa na Bwana mwenyewe siku hiyo ikifika.
Swali ni Je! Na wewe unataka uwepo huo wakati? Mimi sitaki, Kumbuka mpaka hayo yote yatokee unyakuo utakuwa umeshapita. Watakaoshuhudia hayo ni wale wote ambao hawakwenda katika unyakuo, watakaopokea chapa ya mnyama.
Ili kufahamu kwa marefu juu ya kalenda ya matukio yote ya siku za mwisho, angalia vichwa vya masomo mengine chini.
Hivyo tubu dhambi zako kama bado wewe ni mwenye dhambi, hizi ni siku za mwisho kweli kweli , siku za Kamsa za Mungu mwenyezi.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
SIKU YA HASIRA YA BWANA.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Juya maana yake ni jarife, au wavu wa kuvulia samaki.
Habari hiyo inapatikana kwenye vifungu hivi vya maandiko;
Habakuki 1:13 “Wewe uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu, wewe usiyeweza kutazama ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya, hapo mtu mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye;
14 na kufanya wanadamu kuwa kama samaki wa baharini, kama vitu vitambaavyo, ambavyo havina mtawala?
15 Yeye huwatoa wote kwa ndoana yake, huwakamata katika wavu wake, na kuwakusanya katika JUYA lake; ndiyo sababu afurahi na kupendezwa.
16 Kwa sababu hiyo huutolea wavu wake sadaka, na kulifukizia uvumba JUYA lake; kwa sababu kwa vitu vile fungu lake limenona, na chakula chake kimekuwa tele.
17 Je! Atawatoa walio katika wavu wake, asiache kuwaua watu wa mataifa daima”?
Na katika agano jipya Bwana Yesu aliutumia pia mfano wa Juya la mvuvi kufananisha na jinsi mwisho wa dunia utakavyokuwa.
Mathayo 13:47 “Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;
48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa.
49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,
50 na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.
Hapo katika mfano wa Yesu tunaona walivuliwa samaki wa aina zote na kupelekwa nje kabisa ya pwani, ikiashiria kuwa wanadamu wote watavunwa ile siku ya mwisho, wawe ni watakatifu wawe ni waovu wote watavunwa, maana yake ni kuwa kila mmoja wetu atahusika, tutatolewa kwenye huu ulimwengu wa sasa, na hapo ndipo walio wema wataenda mbinguni kwa Mungu na wale walio waovu watatupwa katika ziwa la moto.
Na kibaya zaidi siku zenyewe ndio hizi tuishizo. Wakati wowote paraparanda italia, na mwisho utafika, Je bado upo vuguvugu, bado unautumaini ulimwenguni usiodumu milele?.
Kama wewe ni mwenyewe dhambi na unataka leo Yesu ayaokoe maisha yako. Ili ikitokea hata mwisho umefika leo, uwekwe kapuni mwa Bwana, basi uamuzi huo ni mzuri sana. Kumbuka biblia inasema saa ya wokovu ni sasa, Na wakati uliokubalika ni huu.
Kama ni hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na Mungu akubariki >>>> SALA YA TOBA
Tazama pia maneno mengine ya biblia chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.
UMEFUMBULIWA MACHO YAKO YA KIROHO?
UNYAKUO.
https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/
Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?
Luka 17:26 “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.
27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.
28 Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;
29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote”.
Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe.
Unabii huo ulitolewa na Bwana wetu Yesu mwenyewe kupitia kinywa chake, haukutolewa kwa kutumia kinywa cha Mtume Paulo, au Yohana, au Petro au hata Luka mwenyewe aliyekiandika hichi kitabu, bali ni Bwana mwenyewe ndiye aliyeutoa…akilelezea jinsi ujio wake unavyofananishwa.
Katika unabii huo aliufananisha na siku za Nuhu pamoja na za Lutu. Sasa pamoja na mengi aliyoyafananisha kwamba watu watakuwa wakioa na kuolewa (ndoa za jinsia moja), watu watakuwa wakila na kunywa (karamu za ulafi pamoja na ulevi)kama nyakati za Nuhu, pia katika siku za ujio wake watu watakuwa wakiuza na kununua (biashara haramu na za magendo) kama ilivyokuwa nyakati za Lutu
Lakini pamoja na hayo yote ambayo mengi ya hayo yameshatimia..kuna vipengele viwili ningependa tuvione katika mistari hiyo, ambavyo ukiisoma kwa haraka haraka ni rahisi kuvipita tu. Na vipengele hivyo ni 1) KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU na 2) KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA LUTU
Katika vipengele hivyo hakusema “kama zilivyokuwa siku za gharika, au kama zilivyokuwa siku za maangamizi ya moto ya Sodoma na Gomora”..Bali utaona anatumia siku za Nuhu na siku za Lutu…
Sasa Nuhu na Lutu walikuwa ni watumishi wa Mungu.. Kwasababu walionywa na Mungu juu ya maangamizi yanayokuja mbeleni na pia wakapewa nafasi ya kwenda kuwahubiria wengine.
Lutu kabla ya kutolewa Sodoma, alihubiriwa na wale malaika wawili mambo yatakayokwenda kutokea kipindi kifupi mbele na akapewa nafasi ya kwenda kuwahubiria wakwe zake, na ndugu zake pia, ikiwemo mke wake, wanawe wawili na ndugu zake.. Waliokubali ni mke wake pamoja na wanawe wawili, wengine walimwona kama kikaragosi tu kinacholeta habari za mababu.
Mwanzo 19:12 “Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa;
13 maana tutapaharibu sisi mahali hapa, kwa kuwa kilio chake kimezidi mbele za Bwana; naye Bwana ametupeleka tupaharibu.
14 Lutu akatoka akasema na wakweze, waliowaposa binti zake, akasema, Ondokeni mtoke katika mahali hapa kwa sababu Bwana atauharibu mji huu. Lakini akawa kama achezaye machoni pa wakweze”
Vivyo hivyo Nuhu kabla ya kuingia safinani alihubiriwa na Mungu juu ya hukumu itakayokwenda kutokea kipindi kifupi mbele, na pia akapewa nafasi ya kwenda kuwahubiria ndugu zake, lakini waliokubali kuambatana naye ni mke wake na wanawe watatu, pamoja na wake za wanawe, jumla watu 8 tu..wengine wote walimwona kama fundi mbao aliyerukwa na akili.
Hivyo utaona hapa Bwana Yesu anazitaja kama siku ni ZAO.. Na anazifananisha na siku za ujio wake.. Maana yake ni kwamba siku za ujio wake, atawanyanyua watumishi wake mfano wa Nuhu na Lutu kuonya ulimwengu juu ya hukumu ijayo.
Ndugu..hukumu ipo!.. Wakina Nuhu wapo wengi leo, katika kila Taifa na mkoa..(Watumishi wote wanaouonya ulimwengu juu ya siku za mwisho ni wakina Nuhu na Lutu), na hizi ndizo siku zao… “zinaitwa Siku za Hao watumishi” na sio “siku za kuangamizwa dunia”..Lutu alionekana anacheza mbele za wakwe zake.
Kibaya zaidi ni kwamba, watu wengi watakaokuwa wanasikia habari hizo wataoana kama wanacheza tu nao pia, wanapiga ngonjera, wamekosa kazi ya kufanya,.Lakini mwisho utakapowakuta kwa ghafla ndipo watakajuta majuto yasiyoelezeka…
Ukiona unasikia habari za mwisho wa dunia kwa nguvu, jua ndio injili ya kumalizia hiyo, baada ya hapo ni hukumu. Hizi ni siku za mwisho, siku za Watumishi wa Mungu..Na zitaisha!
Je umempokea Kristo? Kwa kutubu na kubatizwa?.. kama bado unasubiri nini?.. Yesu yu karibu kurudi, hivi karibuni hutasikia tena ukiombwa uingie ndani ya safina, hutasikia tena sauti ya Roho Mtakatifu ikikushawishi kutubu..kutakuwa na ukimya nje na ndani, mlango wa Neema utakuwa umeshafungwa, kitakachobakia ni hukumu..
Watu wa kipindi cha Nuhu walisubiri Mungu azungumze nao pengine kwa kutumia jua ndipo waamini, hivyo wakaishia kumdharau Nuhu, vivyo hivyo wa kipindi cha Lutu. Wakati huu ambao watu wanaidharau injili ya kurudi kwa Kristo, hatupaswi kufanana na wao hata kidogo.
Hivyo ndugu mpokee Kristo leo kama hujafanya hivyo, kisha nenda katafute ubatizo sahihi wa maji mengi (Yohana 3:23) na kwa Jina la YESU, ambalo ndio jina la Baba, mwana na Roho Mtakatifu (Matendo 2:38, Mathayo 28:19), na kuanzia wakati huo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukuongoza na kukutia katika kweli yote ya maandiko.. Na utaiepuka hukumu ambayo ipo karibuni kuujilia ulimwengu wote.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.
SIKU ZA MWISHO WA DUNIA.
Naomba kujua watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?
KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.
JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.
Daawa ni madai, au mashitaka, malalamiko, au hukumu.
Kwamfano pale mwenzako anapokukosea, au amekudhulumu, au amekutukana au amekufanyia jambo baya, na unataka kwenda kumshitaki , sasa hilo shitaka au madai ndio kwa jina lingine linaitwa Daawa.
1Wakorintho 6:1 “Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu?
2 Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo?
3 Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya”?
Unaona, biblia inatushauri sisi kama watakatifu tukiwa na daawa/shitaka juu ya ndugu zetu wa kikristo, hatupaswi kuyapeleka kwa watu wasioamini watusaidie kuamua, badala yake tunapaswa tuyawasilishe mbele ya kanisa, sisi kwa sisi wenyewe tuyaamue, Kwasababu Mungu mwenyewe ametupa jukumu hilo la kuhukumu mambo ya mwili kwa haki, kwasababu hata huko tutakapokwenda tutawahukumu malaika pia biblia inatuambia ..Hivyo basi, hakuna sababu ya kupelekana mahakamani, ili watu waioamini watusaidie kutoa hukumu, wakati sisi wenyewe tupo na tunayo hukumu ya haki zaidi ya wale wengine kule. Hivyo daawa zetu zote, zinapaswa ziamuliwe na kanisa.
Mistari mingine inayoeleza juu ya Neno hili, ni kama ifuatayo:
Ayubu 31:13 “Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;
14 Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?
15 Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni”?
Kumbukumbu 16:19 “Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza daawa ya wenye haki”.
Kumbukumbuku 17:8 “Ikiwa limezuka neno lililo zito kukupita wewe, katika maamuzi kati ya damu na damu, na kati ya daawa na daawa, na kati ya pigo na pigo, nayo yashindaniwa katika malango yako; ndipo nawe uondoke, ukwee uende mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako”;
Mengine ni hii: (2Samweli 15, Ayubu 5:8, 23:4,29:16,35:14)
Hiyo ndio tafsiri ya Neno hilo, pia angalia tafsiri ya maneno mengine chini..
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?
Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?
MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)
TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
Beramu ni nini?
Beramu ni jina lingine la neno BENDERA. Hivyo mahali popote kwenye biblia unapolisoma neno hili basi fahamu kuwa linamaanisha bendera.
Hesabu 1:52 “Na wana wa Israeli watazipanga hema zao, kila mtu katika marago yake mwenyewe, kila mtu hapo ilipo beramu yake mwenyewe, kama majeshi yao yalivyo”.,
Vipo vifungu vingi katika biblia, vinavyolitaja neno hili hatuwezi kuvihorodhesha hapa vyote, kwahiyo kama unahitaji kuvijua baadhi yao, basi soma kitabu cha Hesabu sura ile ya pili yote utakutana na Neno hili sehemu kadha wa kadha.
Lakini beramu/bendera sikuzote inasimama badala ya nini?
Tunafahamu kuwa kila bendera tunayoiona mahali fulani imesimamishwa, aidha kwenye mji, au chama, au jamii n.k. huwa ina maana yake.
Nyingine zimebeba historia ya jamii husika/taifa, nyingine zimebeba tunu, nyingine zinaeleza tabia ya nchi, au vitu vya asili vya nchi n.k.
Hivyo hata rohoni napo, kila mmoja wetu kwa namna moja au nyingi ni lazima atakuwa ameshikilia bendera mojawapo inayomwakilisha yeye.
Na ndio maana leo hii ukienda kwenye mabalozi yote, ni lazima uone bendera ya nchi yake inayoiwakilisha imesimamishwa pale. Hiyo ni kukutambulisha kuwa umefika katika makao ya muda ya nchi ile.
Hivyo mambo yote yahusuyo nchi hiyo huko ugegenini utasaidiwa ukifika pale, huduma zote utapewa sawasawa tu na kama ungekuwa katika nchi yako.
Vivyo hivyo na hapa duniani, kila mmoja wetu ni balozi wa mahali Fulani. Na tunatambuliwa kwa beramu/bendera zetu rohoni.
Ikiwa wewe ni mwenye dhambi, moja kwa moja unapeperusha bendera ya kuzimu, kwa matendo yako maovu, ambayo asili yake ni kuzimu na mkuu wake ni ibilisi.
Lakini kama wewe ni mtakatifu, nawe pia ni lazima upeperushe bendera ya ufalme wa mbinguni kwa matendo yako, ambayo ni lazima yawe ya kumpendeza Mungu, na pili uwe unaihubiri injili(kuwashuhudia wengine habari njema).
Kama hayo mawili huyafanyiki ndani yako na unasema umeokoka, hakuna beramu/bendera yoyote unayoipeperusha ya ufalme wa mbinguni duniani.
Hivyo jitathimini maisha yako ni beramu gani unaipeperusha, katika hichi kipindi kifupi tuliobakiwa nacho hapa duniani. Je, ni ya mbinguni au kuzimu?
Lakini ikiwa leo hii unasema mimi na dhambi basi, nataka Yesu anibadilishe maisha yangu kuanzia leo , nataka anifanye kiumbe kipya nianze na mimi kuipeperusha beramu ya Yesu maishani mwangu. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, ambao utaufurahia maisha yako yote. Bwana anasema:
Na uzuri ni kuwa yeye mwenyewe anasema “yeye ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe” (Yohana 6:37)..
Hivyo kama upo tayari na umemaanisha kufanya hivyo leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/
Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?
Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)
Mahuru ndio nini?
UNYAKUO.
Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
SWALI: Yakobo aliposhindana na Malaika alishikwa uvungu wa paja akateguka…Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?
Mwanzo 32:24 “Yakobo akakaa peke yake; na mtu mmoja akashindana naye mweleka hata alfajiri.
25 Naye alipoona ya kuwa hamshindi, alimgusa panapo uvungu wa paja lake; ukateguka uvungu wa paja la Yakobo alipokuwa akishindana naye.
26 Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.
27 Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo.
28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda”.
Jibu: Uvungu wa paja, ni eneo la juu ya paja ambapo mfupa wa paja umekutana na ule wa kiuno. Kama tunavyosoma hapo Yakobo baada ya kushindana na Yule malaika kwa masaa mengi sana usiku kucha bila kuwa na dalili yoyote ya kumwacha, tunaona biblia inatuambia Yule malaika, alimtengua uvungu wa paja lake.
Kumbuka kutegua/kutengua ni tofauti na kuvunja,..Kitu kikivunjwa maana yake ni kinaharibiwa, kinahitaji kuunganishwa, lakini kikitenguka maana yake ni kinahama eneo lililopo kwa muda tu.. Hivyo kwa namna ya kawaida mwanadamu maeneo yote ambayo mifupa miwili inakutana huwa ni rahisi kutenguka, husani pale anapoanguka sehemu ndefu, au kubanwa au kuvutwa kwa nguvu mahali penye maongeo, kwa mfano goti, au viwiko vya mikono au miguu, vidole, bega au kwenye paja.. Na huwa inaambatana na maumivu makali sana, ambayo maumivu yake yanafanana tu ya yale ya kuvunjika, wakati mwingine yanamfanya mtu asindwe kabisa kutembea kama sio kuchechemea, na mpaka yaishe inaweza kuchukua wiki mbili mpaka tatu au Zaidi.
Sasa Yakobo yeye, alitenguliwa kwenye huu mfupa mkubwa wa paja, ambao ndio mkubwa na maumivu yake ndio makali kushinda yote.
Lakini kwanini Mungu afanye vile, Ni jambo gani tunajifunza hapo?
Baraka za Mungu ni za kuzipigania, na sio hilo tu, bali pia zinaambatana na maumivu.. Ukitaka Mungu akubariki kubali kukutana na mapigano na maumivu fulani, Jina la Israeli halikuja hivi hivi, lilikuwa ni la jasho na maumivu. Vivyo hivyo na sisi, tusikubali kuambiwa njoo, ubarikiwe, na huku, hatutaki kusikia gharama za kubarikiwa, ambazo ni kuishi maisha ya kubarikiwa.
Maisha ya kubarikiwa ni kama haya:
Bwana Yesu alisema Mathayo 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.
Lakini kama ulichonacho unajilimbikizia wewe tu mwenyewe, Na hapo hapo bado unataka nawe pia ubarikiwe, hilo jambo halipo!. Ipo mifano mingi sana..Ikiwa humtolei Mungu, tena kile kinachokugharimu kabisa, mpaka unaona maumivu rohoni, ni ngumu kubarikiwa na Mungu.
Si wakati wote unahitaji kuomba ili Mungu akuone, unahitaji kufanya zaidi..Pale ulipo unaanza, Mtume Yohana alimwambia Gayo, maneno haya 1Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”.
Utajiuliza huyu Gayo ni nani, kwanini hakumwandikia kila mtu waraka ule wa mafanikio, bali Gayo tu peke yake, Hivyo ukitaka kujua ni kwanini alimwandikia yeye na si wengine, nenda kasome sura ile yote ujue ni mambo mangapi alijitoa kwa Mungu katika kuwahudumia watakatifu na kuwakaribisha wageni wale waliokuwa wanasafiri kuipeleka injili na kuwapatia mahitaji yao, mpaka sifa zake zikavuma katika kanisa lote.. Hapo ndipo Mtume Yohana kwa uongozo wa Roho Mtakatifu akaongozwa kumwandikia maneno yale ya baraka.
Lakini hiyo ilikuwa ni mashindano na maumivu makali ya kuinyima nafsi yake.
Vivyo hivyo na sisi, tukumbuke kuwa Baraka za Mungu zitaambatana na kutenguliwa miguu yetu..Kama tupo tayari kwa hayo basi tuingie mapambano, Na tunaingia mapambanoni, sio kwa maneno bali kwa matendo.
Bwana atubariki sote, katika safari yetu ya imani.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/ushirikina-na-madhara-yake/
Jabari maana yake ni mtu hodari, asiyeogopa, shujaa.
Isaya 49:24 “Je! Aliye hodari aweza kunyang’anywa mateka yake, au jeshi lao waliofungwa halali wataokoka?
25 Naam, Bwana asema hivi, Hata jeshi la wafungwa wake aliye hodari watapokonywa mikononi mwake, na mateka yake aliye JABARI wataokoka; kwa maana nitateta na yeye atetaye nawe, nami nitawaletea wana wako wokovu”.
Unaona, Jabari ni mtu shujaa lakini kibiblia kuna majabari wa aina mbili,
Zaburi 52:1Kwa nini kujisifia uovu, EWE JABARI? Wema wa Mungu upo sikuzote.
2 Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila
3 Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.
4 Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.
5 Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung’oa katika nchi ya walio hai.
6 Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka; 7 Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. ALIUTUMAINIA WINGI WA MALI ZAKE, NA KUJIFANYA HODARI KWA MADHARA YAKE.
8 Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.
9 Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako.
Waebrania 11:33 “ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba,
34 walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, WALIKUWA HODARI KATIKA VITA, walikimbiza majeshi ya wageni.
35 Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;
36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;
37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya;
38 (watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi.
39 Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi;
40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi”.
Swali ni Je! Wewe ni Jabari katika nini?
Jibu unalo, lakini ikiwa upo katika ouvu, au mambo ya kidunia, basi Yesu anaweza kukufanya kuwa Jabari lake teule ikiwa tu leo utampokea..Ukipomkea atakusamehe dhambi zako zote, atakufanya kuwa mwana wake,atakuondolea laana zote, atakupa Roho wake Mtakatifu bure, atakupa amani, na kikubwa zaidi atakupa na uzima wa milele .
Unasubiri Nini? Tangu ulipoanza kuitumikia dunia imekupa nini? Hivyo usikawie, ikiwa umedhamiria kwa moyo wako wote, kumkaribisha Yesu katika maisha yako, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Sasa Ikiwa ufuata maaelekezo hayo hapo juu, basi kuanzia sasa wewe ni JABARI la Bwana Yesu. Na utamwona atakavyoanza kutembea na wewe kukutengeneza..
Bwana akubariki.
1Wakorintho 16:13 “Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari”.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?
Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?
NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Baradhuli ni nani/ ni nini kama lilivyotumika kwenye biblia?
Kibiblia Baradhuli ni mtu asiyefaa, mpumbavu sana, aliyevuka mipaka
Ipo mistari kadha wa kadha inayoeleza tabia za watu wabaradhuli. Kwa mfano:
Wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji angali wanajua kabisa wanachokifanya ni kinyuma na mapenzi ya Mungu, wanaofanya uchawi, wanaofanya matambiko n.k. Hao ni mabaradhuli kibiblia.
Kumbukumbuku 13:12 Ukisikia yasemwa habari ya miji yako mmojawapo, akupayo Bwana, Mungu wako, ukae humo, ukiambiwa,
13 Kumetoka katikati yako MABARADHULI kadha wa kadha, wamewapotoa wenyeji wa mji wao, wakisema, Twendeni tukaabudu miungu mingine msiyoijua;
14 ndipo nawe uulize na kutafuta, ukiuliza kwa bidii; nawe angalia, ikiwa kweli, na jambo lile halina shaka, kwamba machukizo mfano wa haya yafanyika katikati yako;
15 hakika yako uwapige wenyeji wa mji ule kwa makali ya upanga, kwa kuwaangamiza kabisa, pamoja na vitu vyote vilivyomo, na wanyama walio humo, kwa makali ya upanga.
Ukisoma kitabu cha Waamuzi utaona Gideoni alikuwa na watoto sabini na wawili, lakini baada ya Gideoni kufa, mtoto wake mmoja aliingiwa na tamaa kutawala sehemu ya Gideoni hivyo akaamua kuwaua ndugu zake wote waliosalia ili yeye afanywe muamuzi badala yake, Ndipo biblia inatuambia alikwenda kuwaajiri watu Mabaradhuli ili kutekeleza adhma yake hiyo ya uuaji,..Hao watu wakashirikiana naye kuwaua ndugu zake wote siku moja juu ya jiwe. (Waamuzi 9:1-5).
Ukisoma tena kitabu cha Waamuzi 19 utamwona Yule mlawi ambaye alikuwa na suria wake, aliyekwenda kufanya ukahaba, kitendo ambacho kilimpelekea amrudishe nyumbani kwa baba yake, hivyo akakaa kule kwa muda wa miezi 4, ndipo baadaye akaghahiri akaamua amfuate surua wake amrudishe kwake, sasa alipokuwa njiani mji mmoja wa ugenini, alikaribishwa na mzee mmoja wa mji ule. Lakini usiku mambo yalibadilika kwani wale watu wa mji ule wa Benyamini, waliizingira nyumba wakataka wapewe hao wageni walale nao..Kama tunavyoijua habari Yule mlawi akaona ni heri amtoe suria wake wamfanye waliyotaka kumfanya..Wakafanya hivyo mpaka asubuhi baadaye Yule Suria akafa..
Waamuzi 19:22 “Hapo walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, tazama, watu wa mji huo, watu MABARADHULI wakaizingira hiyo nyumba pande zote, wakagonga mlango; wakasema na huyo mwenye nyumba, huyo mzee, na kumwambia, Mlete nje mtu yule aliyefika nyumbani kwako, ili tupate kumjua”.
Soma sura yote ya 19,20 na 21, upate picha kamili, na nini kiliendelea baada ya pale..
Watu wanaoshikamana na viongozi waasi, au waliokosa heshima katika jamii.
2Nyakati 13:7, Waamuzi 11:3.
Je mpaka sasa mabaradhuli wapo?
Unapaswa ujiulize je! tabia mojawapo ya hizo unazo?
Kumbuka kuwa waovu wote, sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Ikiwa wewe ni muuaji, wewe ni baradhuli, ikiwa wewe ni mchawi(unakwenda kwa waganga) wewe ni baradhuli, n.k.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Lakini tumaini lipo kwa Yesu tu peke yake. Yeye peke yake ndiye anayeweza kuyageuza maisha yako na kukusaheme kabisa kabisa. Na kukufanya kuwa mwana wake.
Je! unahitaji kuokoka leo?
Unahitaji Yesu ayabadilishe maisha yako leo?
Unahitaji kupokea Roho Mtakatifu?
Biblia inasema..
Isaya 1:18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.
19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi”;
Kama ndivyo basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Bwana akubariki.
Mada Nyinginezo:
MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?
Arabuni maana yake ni nini?
LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
Areopago ni nini?
Areopago ni baraza kuu la Waathene au mahali walipokutanika wakuu wa Athene. Kwa ajili ya kuzungumza mambo mbalimbali ya muhimu,kama vile kusikiliza kesi zinazohusiana na mauaji au dini, au kutoa hukumu, au kuchambua mambo mengine yenye uzito katika jamii.
Eneo hili lilikuwa upande wa kaskazini magharibi mwa mji wa Athene,Ukigiriki, na lilijengwa ya juu ya mwamba mkubwa.
Baraza hili, lilifanana na lile baraza la wayahudi ambalo, wazee pamoja na kuhani mkuu walikuwa wanakutanika kutoa mashahuri juu ya kesi za kidini, kama vile ilivyokuwa wakati wa Bwana Yesu (Mathayo 26:57-68)
Sasa Mtume Paulo alipofika katika mji huu na kuanza kuhubiri, tunaona baada ya habari zake kusikika sana katikati ya jamii ya waethene, walimkamata na kumpeka mbele ya baraza hili kuu (Areopago) ili kumsikiliza vizuri juu ya imani yake.
Tusome:
Matendo 17:16 “Paulo alipokuwa akiwangojea huko Athene na kuona jinsi mji ule ulivyojaa sanamu, roho yake ilichukizwa sana ndani yake.
17 Basi katika sinagogi akahojiana na Wayahudi na waliomcha Mungu, na wale waliokutana naye sokoni kila siku.
18 Na baadhi ya Waepikureo na Wastoiko, wenye ujuzi, wakakutana naye. Wengine wakasema, Mpuzi huyu anataka kusema nini? Wengine walisema, Anaonekana kuwa mtangaza habari za miungu migeni, kwa maana alikuwa akihubiri habari za Yesu na ufufuo.
19 Wakamshika, wakamchukua AREOPAGO, wakisema, Je! Twaweza kujua maana ya elimu hii mpya unayoinena?
20 Kwa maana unaleta mambo mageni masikioni mwetu, tutapenda kujua, basi, maana ya mambo haya.
21 Kwa maana Waathene na wageni waliokaa huko walikuwa hawana nafasi kwa neno lo lote ila kutoa habari na kusikiliza habari za jambo jipya.
22 Paulo akasimama katikati ya AREOPAGO, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini.
23 Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua……
32 Basi waliposikia habari za ufufuo wa wafu wengine walifanya dhihaka; wengine wakasema, Tutakusikiliza tena katika habari hiyo.
33 Basi hivi Paulo akaondoka akawaacha.
34 Baadhi ya watu wakashikamana naye, wakaamini; katika hao alikuwamo Dionisio, MWAREOPAGO, na mwanamke mmoja jina lake Damari, na watu wengine pamoja na hao”.
Kama tunavyoona wapo miongoni mwa hao wakuu wa baraza wapo waliodhihaki, na wapo walioamini kama vile huyo Dionisio mwareopago.
Ndio, Hata sasa katika agano jipya ma-areopago yapo mengi, Bwana Yesu alishayazungumzia na kuonya kuwa watakatifu watakutana nayo katika safari zao za Imani, na katika kuhubiri injili.. Lakini Bwana Yesu alitupa kanuni ya kusimamia, akasema hivi;
Mathayo 10:17 “Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;
18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.
19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.
20 Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.
Hivyo, kama umeokoka,au unahubiri injili na ukajikuta umewekwa katikati ya viongozi wa dini, hupaswi kuogopa Areopago lolote..Kwasababu Bwana ameahidi kuwa na wewe.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
KWA MUNGU ASIYEJULIKANA.
SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.
JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.
Israeli ipo bara gani?
Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?