Title 2020

Biblia ina vitabu vingapi?

Je! Biblia ina vitabu vingapi?


Biblia takatifu ina jumla ya vitabu 66, kati ya hivyo 39 ni vya agano la kale, na 27 ni vya agano jipya.

Hii ni orodha ya vitabu vya agano la kale:

  1. Mwanzo
  2. Kutoka
  3. Mambo ya walawi
  4. Hesabu
  5. Kumbukumbu la Torati
  6. Yoshua
  7. Waamuzi
  8. Ruthu
  9. 1 Samweli
  10. 2 Samweli
  11. 1 Wafalme
  12. 2 Wafalme
  13. 1 Mambo ya Nyakati
  14. 2 Mambo ya Nyakati
  15. Ezra
  16. Nehemia
  17. Esta
  18. Ayubu
  19. Zaburi
  20. Mithali
  21. Mhubiri
  22. Wimbo ulio bora
  23. Isaya
  24. Yeremia
  25. Maombolezo
  26. Ezekieli
  27. Danieli
  28. Hosea
  29. Yoeli
  30. Amosi
  31. Obadia
  32. Yona
  33. Mika
  34. Nahumu
  35. Habakuki
  36. Sefania
  37. Hagai
  38. Zekaria
  39. Malaki

Ifuatayo ni orodha ya vitabu vya agano jipya:

  1. Mathayo
  2. Marko
  3. Luka
  4. Yohana
  5. Matendo
  6. Warumi
  7. 1 Wakorintho
  8. 2 Wakorintho
  9. Wagalatia
  10. Waefeso
  11. Wafilipi
  12. Wakolosai
  13. 1 Wathesalonike
  14. 2 Wathesalonike
  15. 1 Timotheo
  16. 2 Timotheo
  17. Tito
  18. Filemoni
  19. Waebrania
  20. Yakobo
  21. 1 Petro
  22. 2 Petro
  23. 1 Yohana
  24. 2 Yohana
  25. 3 Yohana
  26. Yuda
  27. Ufunuo

Zipo zinazosemekanakuwa ni biblia, ambazo zina vitabu 72 na nyingine zaidi. Na zinatumiwa na baadhi ya madhehebu ya kikristo kama vile Katoliki na Othrodoksi.  Vitabu hivyo vilivyoongezwa havijathibitishwa kuwa vimevuviwa na Roho Mtakatifu hivyo hatupaswi kuviamini.

Biblia tunayopaswa kuiamini ni ile yenye vitabu hivyo 66 vilivyoorodheshwa hapo juu.

Shalom.

Je! utapenda uwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp? kama ndivyo basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia ni nini?

Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wakaldayo ni watu gani?

Wakaldayo ni wenyeji wakongwe wa Mji wa Babeli. Mji wa Babeli ulikuwepo maeneo ya nchi ya Iraq kwasasa.

Hawa wakaldayo ndio waliowachukua mateka wana wa Israeli na kuwapeleka utumwani Babeli..

Yeremia 21:8 “Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.

9 Yeye atakayekaa katika mji huu atakufa kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni; bali yeye atakayetoka, na kujitia pamoja na Wakaldayo wanaowahusuru, yeye ataishi, na maisha yake yatakuwa nyara kwake.

10 Maana nimeweka uso wangu juu ya mji huu niuletee mabaya, wala nisiuletee mema, asema Bwana; utatiwa katika mkono wa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza”.

Ezra 5:12 “Lakini hapo baba zetu walipomkasirisha Mungu wa mbingu na nchi, hata akaghadhibika, akawatia katika mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Mkaldayo, naye ndiye aliyeiharibu nyumba hii, akawachukua watu mateka mpaka Babeli”

Pia Ibrahimu kabla ya kuhamia nchi ya Kaanani, alikuwa anaishi huko Uru ya Wakaldayo. Kwasababu Babeli tayari ilikuwepo miaka mingi kabla hata ya Taifa la Israeli kuwepo, ndipo ule Mnara wa Babeli ulipotengenezewa.

Mwanzo 11:31 “Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko”.

Hivyo popote biblia inapowataya Wakaldayo ina maanisha Wenyeji wa Babeli.

Je una habari kuwa Babeli iliyowachukua wana wa Israeli mateko kwa namna ya kimwili, ipo leo kwa namna ya kiroho?..Kama ulikuwa hujui basi kasome kitabu cha ufunuo mlango wa 17 na kuendelea.

Na Babeli hiyo ya rohoni inawachukua utumwa watu wengi leo pasipo wao kujua, na mwisho wa siku inawaua kiroho na kuwapeleka kuzimu. Na Babeli hii sasa inafanya kazi kwa nguvu katika dini na madhehebu, na Bwana ataihukumu katika siku za mwisho.

Ufunuo 14:8 “Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake”.

Kwa urefu kuhusu Babeli hii ya rohoni fungua hapa >> BABELI YA ROHONI

Je umeokoka?.  Kumbuka Kristo anarudi saa na wakati usiodhani?..Wakati unafikiri bado sana ndio wakati anaokuja..

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.

Kama hujampokea ni vizuri ikampokea sasa hivi, wala usisubiri hata dakika 5 mbele, kwasababu hujua yatakayojitokeza dakika mbili mbele. Hivyo hapo ulipo piga magoti, kisha tubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na Bwana wa huruma na Neema atakusamehe bure, na kukutakasa. Na baada ya hapo tafuta ubatizo sahihi, wa maji mengi na kwa jina la Yesu, na  tafuta kanisa la Kristo la kiroho, lililo karibu nawe,  jiunge hapo na wakristo wenzako ili ujengeke kiroho, na Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MNARA WA BABELI

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

JUKUMU LA MUHIMU LINALOKWEPWA NA WENGI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

SWALI: Wibari ni nani? Na kwanini wanatajwa kama moja wa viumbe wanne wenye akili nyingi?(Mithali 30:26)


JIBU: Wibari ni wanyama wadogo wanaokaribia kufanana na sungura, kwa jina lingine wanajulikana kama pimbi, au kwanga, au perere, tazama kwenye picha.

Wanyama hawa utawaona wakitajwa kwenye vifungu hivi katika biblia;

Walawi 11:4 “Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; ngamia, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu. 5 Na wibari, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu”.

Zaburi 104:18 “Milima mirefu ndiko waliko mbuzi wa mwitu, Na magenge ni kimbilio la wibari”.

Mithali 30:24 “Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana.

25 Chungu ni watu wasio na nguvu; Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.

26 Wibari ni watu dhaifu; Lakini hujifanyia nyumba katika miamba”.

Lakini ni kwanini wametajwa kama moja ya viumbe vinne vyenye akili nyingi duniani?

Ni kwasababu ya tabia yao, wanyama hawa ni waoga, hawali nyama, wala hawapo machachari sana ukilinganisha na wanyama wengine, hawawezi kukimbia sana, kwa ufupi ni viumbe dhaifu ambavyo ni rahisi kukamatwa na maadui zao, lakini katika udhaifu wao, wanajua ni wapi pa kujihifadhi nafsi zao, na si hapo pengine zaidi ya kwenye miamba.

Wibari wanatengeneza nyumba zao kwenye mapango ya miamba, mirefu, na migumu, kiasi kwamba adui zao ni ngumu kuwaona au kuwakamata, tofauti na wanyama wengine kama ngiri au sungura n.k ambao wao wanachimba mashimo ambayo hata adui zao wanaweza kuwafuatilia na kuyafukua na kuwakamata, au mvua ikija ikajaza mashimbo yao wakafa, au upepo mkubwa ukivuma unaweza kufukia mashimo yao kwa udongo utakaoporomoka au kuingia, hivyo hiyo inawafanya maisha yao kuwa hatarini sana japokuwa ni machachari au wana uwezo mkubwa wa kukimbia.

Lakini wibari kweli sio kama wanyama wengine, ni wadhaifu sana lakini wanafahamu ni wapi wanaweza kuwa salama.

Je na sisi, tutashindwa akili na wibari?

Usalama wetu upo wapi? Je tumeyajenga maisha yetu wetu wapi? Je, ni mashimoni au kwenye vichuguu, au kwenye miti au kwenye mwamba?. Tujue tu kuwa mwamba ni mmoja tu, naye ni YESU KRISTO peke yake. Ukiwa nje ya Kristo, fahamu kuwa maisha yako yapo katika hatari zote, haijalishi utajiona wewe ni mjanja kiasi gani, haijalishi utajiona ni hodari kiasi gani, haijalishi ni tajiri  kiasi gani, shetani atakumaliza tu..Huna safari ndefu..

Sikiliza maneno ya Yesu..

Mathayo 7:24 “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.

26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa”.

Kweli itakuwa ni ajabu sana tukishindwa akili na mnyama pimbi.

Shalom.

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=mJ0AkfAcM4I[/embedyt]

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mavu ni nini katika biblia?(Kutoka 23:28, Kumb 7:20)

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bustani ya Edeni ipo nchi gani?

Bustani ya Edeni ipo nchi gani kwa sasa duniani?


Mungu alipoiumba dunia, alichagua eneo moja, na kulifanya kuwa la kipekee na la kitofauti na maeneo mengine yote aliyoyaumba duniani. Eneo hilo akaliita Edeni. Edeni maana  yake ni eneo la furaha kuu, utulivu,paradiso ya Mungu.

Lakini hakuishia hapo tu bali ndani ya hiyo Edeni upande wa mashariki alitengeneza bustani nzuri sana,  ambayo inajulikana na wengi kama bustani ya Edeni. Bustani hii ndiyo  Mungu aliyomweka mwanadamu wa kwanza hapo aishi (yaani Adamu na uzao wake.)

Lakini kama tunavyosoma biblia, wazazi wetu wa kwanza walipoasi, walifukuzwa kutoka katika bustani ile, na kuanzia hapo, hakuna aliyejua makao halisi ya bustani ya Edeni yalikuwa wapi, vifunguu pekee vinavyotupa taswira ya eneo la bustani ya Edeni ni hivi;

Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya.

9 Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

10 Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne.

11 Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu;

12 na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham.

13 Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi.

14 Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati”.

Kama tunavyoona hapo, kulikuwa na mto uliokuwa unatoa maji kutoka bustanini na baadaye ukagawanyika katika vichwa vinne, na viwili kati ya hivyo (yaani Hidekeli na Frati) vinajulikana  mpaka sasa na vipo maeneo ya nchi ya Iraq, ili kusoma na kufahamu zaidi historia yao fungua hapa >>>> Mto frati na Hidekeli Na hiyo imewafanya masomi wengi wa biblia kudhania kuwa Edeni ilikuwa maeneo ya nchi ya Iraq au kando kando yake.

Lakini vile vingine viwili (yaani Pishoni na Gihoni) havijajulikana bado. Na iyo imewafanya wengine kudhani bustani ya Edeni ilikuwa nchi ya Uturuki ya sasa n.k.

Hivyo, hakuna uthibitisho wa moja kwa moja wa kudhania kuwa Edeni ilikuwa Iraq, au Uturuki au sehemu nyingine yoyote. Na hiyo ni kwasababu ya mabadiliko makubwa ya nchi yaliyokuwa yanatokea wakati wa gharika na  ule wakati wa kugawanyika kwa nchi (Mwanzo 10:25). Historia inaonyesha kuwa dunia ilibadilika mwonekano wake kwa sehemu kubwa sana.

Lakini ni wazi kuwa Edeni haikuwa pengine zaidi ya mashariki ya kati, na sio Afrika kama wanasayansi wanavyoamini, nami naamini ilikuwa katika nchi Kaanani (Yaani Israeli ya sasa).

Lakini ikiwa biblia haikutupa maelezo ya kutosha kuhusu jeografia ya bustani ya Edeni baada ya wazazi wetu wa kwanza kuasi, ni wazi kuwa hakuna umuhimu sana wa kujua bustani hiyo iko wapi kwasasa, kwasababu hayo yalishapita. Bali sasa Mungu ametutilia mkazo hasaa kutufahamisha juu ya Edeni yetu ya mbinguni inayokuja.

Yaani ile Yerusalemu mpya, mji mtakatifu ushukayo kutoka mbinguni kwa Mungu. Na Yerusalemu hiyo itashuka juu ya mbingu mpya na nchi mpya zitakazoumbwa kwa wakati huo baada ya utawala wa miaka elfu moja kuisha. Kama vile tu ilivyokuwa  Edeni ilivyoumbwa juu ya dunia ya wakati ule. Kufahamu zaidi juu ya utawala wa miaka 1000 fungua hapa >>>  UTAWALA WA MIAKA 1000.

Lakini kisichojulikana na wengi ni kuwa, si kila mtu atakayeruhusiwa kuingia ndani ya mji huo. Bali wale watakatifu tu watakaoshinda ulimwengu huu.

Tujiulize, Je! Mimi wewe tutakuwa miongoni mwa hao watakaouingia huo  mji mpya wa dhahabu yaani Yerusalemu ya Mbinguni, Edeni halisi ya Mungu? Je! Mambo ya ulimwengu huu bado yanatusonga, mpaka siku ile itukute ghafla tukaachwa?. Je! Unajua kuwa unyakuo upo karibu sana, na dalili zote za kurudi Kristo duniani zimeshatimia?

Ikiwa wewe bado hujaokoka na leo hii utapenda kumkabidhi Kristo maisha yako ayaokoe na akupe uweza wa kufanyika mtoto wake, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako ambao hautaujutia milele. Hivyo kama upo tayari, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

   Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?

Israeli ipo bara gani?

ORODHA YA WAFALME WA ISRAELI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi Nyumbani:

Print this post

Masheki ni nini?(Zaburi 105:22, Ayubu 29:10)

Masheki ni watu wenye hadhi ya juu sana, wenye jina kubwa na heshima katika jamii au taifa,

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi katika biblia;

Ayubu 29:9 “Wakuu wakanyamaa wasinene, Na kuweka mikono yao vinywani mwao;

10 Sauti yao masheki ilinyamaa, Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao”.

Zaburi 68:31 “Masheki watakuja kutoka Misri, Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara”.

Zaburi 83:11 “Uwafanye wakuu wao kama Orebu na Zeebu, Na masheki yao wote kama Zeba na Zalmuna”.

Zaburi 105:22 “Awafunge masheki wake kama apendavyo, Na kuwafundisha wazee wake hekima”.

Hata Kristo atakaporudi mara ya pili hapa duniani na kutawala kama BWANA WA MABWANA na MFALME WA WAFALME, Atakuwa na masheki wake chini yake. Watu ambao atawapa heshima kubwa kuwa makuhani wake na wafalme katika enzi yake yote duniani kote.

Na watu hao watakuwa si wengine zaidi ya watakatifu walioshinda zamani, na watakaoshinda sasa ulimwengu huu mbovu.

Hizi ni baadhi ya ahadi alizowaahidia watakaoshinda.

Ufunuo 2:26 “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu”.

Ufunuo 3:12 “Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya”.

Ufunuo 3:21 “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”.

Je! Mimi na wewe tupo miongoni mwa watakaoshinda? Kama bado, Je! Upo tayari kumpa Yesu maisha yako leo? Ikiwa jibu ni ndio basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> SALA YA TOBA

Bwana atutie nguvu.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Tazama maana ya maneno mengine ya biblia chini.

Na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 06930366018

Mada Nyinginezo:

Kicho ni nini? (Waefeso 5:21, 2Samweli 23:3)

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.

21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Kitabu cha Mithali na Mhubiri ni vitabu vilivyojaa mafunzo mengi ya maisha ya kawaida, tukiachilia mbali yale ya rohoni.  Vitabu hivi vimeandikwa na mtu mmoja ambaye ni Sulemani. Hivyo leo tutaangalia jambo moja la kujifunza kwenye maisha yetu ya kawaida sisi kama wakristo.

Kama tunavyosoma hapo katika mstari wa 21 na 22 inasema “usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa”… Sasa ni jambo la kawaida kwa kadiri tunavyoishi hapa duniani, kupitia katika hali tofauti tofauti, kuna wakati utapitia hali ya kuzungumziwa vibaya, kusengenywa, haijalishi utakuwa ni mwema, au umefanya mazuri kiasi gani, hilo haliepukiki, hata kama wewe ni mtakatifu vipi?.

Sasa biblia inatuambia, tunapokuwa katika mazingira kama hayo, tusitie moyoni kila kitu tunachokisikia, au kwa namna nyingine tuvipuuzie, haijalishi tulichoambiwa kinachoma  kiasi gani, hiyo ni kwa faida yetu wenyewe..

Lakini tatizo linakuja kwetu pale ambapo tunakisikia kidogo tu tumezungumziwa vibaya, na sisi hapo hapo tunaanza kutafuta, ni nani huyo kasema, ni nani kamwambia, na kama hiyo haitoshi tunaendelea kutafiti na yule aliyemwambia ni nani kamweleza, na yule aliyeelezwa katolea wapi taarifa hizo, na kwanini wamefanya hivyo, hivyo tunaendelea, mpaka unazalika mlolongo mrefu ambao hauna mwisho.

Sasa ukisoma mstari wa 22 utaona unatupa madhara ya kufanya hivyo na kutuambia ikiwa mtu ataendelea kutafuta tafuta hivyo, kuchunguza chunguza hivyo.., kutafuta mchawi ni nani,.mwisho wa siku atashangaa kusikia mambo ambayo asingetazamia kusikia kutoka kwa watu wake ambao hawategemei kabisa.. Ukisoma hapo anatumia mfano wa “mtumwa”, mtu ambaye ni mjakazi wake anayekuheshimu atasikia  anamtukana..

“21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana”.

Hivyo kabla hujaanza kuyafikiria mambo ya wanadamu, utakapoona habari fulani inakujia ya kusemwa vibaya, ikwepe, au ipuuzie kabisa kwa usalama wa moyo wako, kisha endelea na shughuli zako za kawaida, Watu wengi (hususani wakristo) wanaohangaika huku na huko kutafuta ni nani aliyewasengenya au Yule anazungumzia nini kuhusu mimi, mwisho wa siku wanakuwa na vinyongo na watu wote, wanakuwa na chuki zisizokuwa na sababu, wanapoteza hata imani na Mungu na kuanza kuishi maisha ya visasi, maisha ya kutokusamehe, na Maisha ya uchungu, hata maombi yao yanakuwa ni ya kuwalenga tu maadui zao,  mawazo yao ni kukomoa tu, nipate hiki nimfundishe yule adabu n.k. kisa tu alimsikia Fulani akimcheka.. Na pia kamwe hawawezi kuwa na maombi ya unyenyekevu mbele za Mungu, bali ya kunung’unika tu na kulalamika.

Na kumbe hajui yule mtu aliyemsengenya pengine hata hakuwa na chuki na yeye kwa kiwango hicho anachokifikiri yeye, alizungumza tu kama mwanadamu ambaye hawezi kuuzuia ulimi wake, na pengine alishatubu na akawa anamuombea, lakini yeye kwa kuwa alishasikia fulani alimzungumzia vibaya, hilo jambo ataendelea nalo moyoni mwake kwa miaka na miaka..Atasema kwanza yule nilishawahi kumsikia akinisema hivi au vile.

Hivyo kabla hatujamkasirikia fulani kwasababu ya kutuzungumzia vibaya, tunapaswa tujiulize je na sisi hapo nyuma hatujawahi kumsengenya mtu yeyote katika maisha yetu?. Kwasababu Ule mstari wa 22 unasema;

“21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Unaona? Imetumia neno “mara nyingi”. Pengine hata wewe ulishawahi kuzungumza maneno ambayo usingeweza kuyasema mbele ya huyo jirani yako, Lakini akija mbele yako humwekei vinyongo.

Hivyo na sisi pia tunapaswa tuachilie, tusiwe wapelelezi sana kwa yale tunayoyasikia kuhusu sisi, ukisikia mtu anakuambia fulani kakuzunguzia hivi au vile, usitake kujua zaidi ya hapo.. Kwasababu utajikuta una chuki na kila mtu, pengine hata mke wako, au dada yako, au mwanao, kwa sababu hiyo tu ya udadisi.

Tunapaswa tufahamu tu, kuzungumziwa vibaya au kusengenywa ni sehemu ya maisha yetu maadamu tupo hapa duniani. Hivyo hakuna haja ya kufuatilia fuatilia. Hiyo kazi tumwachie shetani, Sisi tutafute mambo msingi ya imani yetu. Na kamwe hutapata mtu mkamilifu asilimia mia moja hapa duniani, kama unayemtaka wewe, tukilielewa hilo tutaishi Maisha ya upendo na furaha sana.

Bwana atusaidie katika hilo kwenye safari yetu ya wokovu.

Je! Umeokoka? Je! Unajua kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Na kwamba hatutakuwa na muda mrefu sana Unyakuo utapita, na mwisho wa dunia utafika? umejiandaaje? Je! Bado upo vuguvugu? Ikiwa hujamkabidhi Yesu maisha yako ni heri ufanye hivyo sasa. Na wokovu unakuja kwa kutubu dhambi zako na kwa kubatizwa ipasavyo hivyo, zingatia hayo na uyakamilishe. Kwani hizi ni dakika za majeruhi. Bwana yupo mlangoni kurudi.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kicho ni nini? (Waefeso 5:21, 2Samweli 23:3)

Kicho ni hali ya hofu. Kwamfano pale biblia inaposema kicho cha Bwana, inamaanisha  hofu ya Bwana.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolitaja neno hilo katika biblia;

Matendo 9:31 “Basi kanisa likapata raha katika Uyahudi wote na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongezeka katika kicho cha Bwana, na faraja ya Roho Mtakatifu”.

Waefeso 5:20 “na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;

21 hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo”.

Waebrania 12:28 “Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho”;

Kumbukumbu 7:21 “Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho”.

Kumbukumbu 28:67, 2Samweli 23:3, Ayubu 15:4

Hivyo nasi pia tunapaswa tuwe na kicho cha Mungu ndani yetu, hicho ndicho kitakachotufanya tuishi maisha yampendazayo yeye hapa duniani, tukikosa hofu ya Mungu, hatutaona hata shida kuua, au kuiba, au kuzini, kwasababu hatumwogopi Mungu. Lakini ikiwa kicho chake kinakaa ndani yetu,tutaogopa kufanya mambo yasiyompendeza kwasababu tunajua Mungu wetu ni mkuu sana, anaweza kutenda lolote juu ya maisha yetu.

Yeremia 5:22 “Je! Hamniogopi mimi? Asema Bwana; hamtatetemeka mbele za uso wangu; mimi niliyeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari, kwa amri ya daima, isiweze kuupita? Mawimbi yake yajapoumuka-umuka, hayawezi kushinda nguvu; yajapovuma sana, hayawezi kuupita.

23 Lakini watu hawa wana moyo wa kuasi na ukaidi; wameasi, wamekwenda zao.

24 Wala hawasemi mioyoni mwao, Basi, na tumche Bwana, Mungu wetu, aletaye mvua, mvua ya mwaka, na mvua ya vuli, kwa wakati wake; na kutuwekea juma za mavuno zilizoamriwa”.

Bwana atusaidie kicho chake kiumbike ndani yetu.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Angalia maana ya maneno mengine ya biblia chini.

Na ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

Nyuni ni nini?(Mathayo 13:32, Sefania 2:14)

Kutabana ni nini? (Mika 5:12)

Baghala ni nini katika maandiko?(2Wafalme 5:16).

Njuga ni nini (Isaya 3:16, Zekaria 14:20)?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

SWALI: Marinda yanayozungumziwa kwenye Yeremia 13:26 ni kitu gani?

Jibu: Tuanze kusoma kuanzia juu kidogo..

Yeremia 13: 24 “Kwa sababu hiyo nitawatawanya, kama makapi yapitayo, kwa upepo wa jangwani.

25 Hiyo ndiyo kura yako, fungu lako ulilopimiwa na mimi, asema Bwana; KWA KUWA UMENİSAHAU, NA KUUTUMAİNİA UONGO.

26 Kwa ajili ya hayo, MİMİ NAMİ NİTAYAFUNUA MARİNDA YAKO MBELE YA USO WAKO, na aibu yako itaonekana.

27 Nimeona machukizo yako, naam, uzinifu wako, na ubembe wako, na uasherati wa ukahaba wako, juu ya milima katika mashamba. Ole wako, Ee Yerusalemu! Hutaki kutakaswa; mambo hayo yataendelea hata lini”.

Habari hiyo sio maonyo kwa wanawake, au wanaume wazinifu waliomwacha Mungu..La! Bali ni maonyo ya Taifa zima la Israeli lililomwacha Mungu..

Kama wewe ni mwanafunzi wa biblia itajua kuwa karibia mara zote, Mungu wa mbingu na nchi analifananisha kanisa lake na mwanamke, kadhalika alilifananisha Taifa lake la Israeli na mwanamke, Ndio maana utaona sehemu kadhaa anazungumza habari za binti Sayuni,..sasa binti Sayuni anayezungumziwa katika biblia sio binti fulani ambaye anaitwa Sayuni, au anayeishi mji unaoitwa Sayuni.. La!..bali binti Sayuni anayezungumziwa ni Taifa zima la Israeli. Yeremia 13:8-10. Kwa urefu kuhusu Binti Sayuni unaweza kufungua hapa >> SAYUNI

Sasa basi kama jamii ya watu wa Mungu, kwa ujumla inafananishwa na mwanamke, kibiblia jamii hiyo ikimwacha Mungu na kwenda kuifuata miungu mingine ya kigeni, mbele za Mungu jamii hiyo ya watu inaonekana kama inafanya ukahaba/inazini. Mbele za Mungu ni kama mwanamke anayezini..

Vifuatavyo ni baadhi ya vifungu vya biblia vinavyozungumzia habari ya Taifa la Israeli jinsi linavyofananishwa na Mwanamke, na jinsi linavyoonekana kama linazini pale linapomwacha Mungu…vifungu hivi unaweza kuvisoma binafsi.. (Kumbukumbu 31:16, Waamuzi 8:27, Isaya 23:17, Yeremia 3:1-7, 1Nyakati 5:24-26).

Kwahiyo tukirudi kwenye huo mstari unaozungumzia MARINDA.. Sasa marinda yanayozungumziwa hapo sio kitu kingine kinachoweza kudhaniwa, bali ni SKETI ZENYE MARINDA. Sketi za wanawake zamani na hata siku hizi zipo zinazotengenezewa na marinda.. Nguo za mabinti zote nyakati za zamani ni lazima zitengenezwe na marinda. Hivyo biblia inaposema hapo “ MIMI NAMI NITAYAFUNUA MARINDA YAKO MBELE YA USO WAKO”.. maana yake ni kwamba “Taifa hilo limemwacha Mungu na kwenda kuvua sketi zao na kufanya uasherati, kwa siri”… Basi Mungu atalifanya jambo hilo kwa wazi, atalivua nguo taifa hilo na aibu yake (au uchi wake) utaonekana.

Na kweli tunaona jambo hilo lilikuja kutimia kama lilivyo, pale wana wa Israeli walipomwacha Mungu na kukataa kutubu, na badala yake ikaenda kuabudu miungu migeni (yaani kufanya ukahaba)..Na baada ya kuonywa muda mrefu bila matunda yoyote, Mungu alilivua nguo taifa hilo kwa kulipeleka Babeli kwa aibu kubwa. (huko ndio kufunuliwa marinda).

Maombolezo 1:8 “Yerusalemu amefanya dhambi sana; Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote waliomheshimu wanamdharau, Kwa sababu wameuona uchi wake; Naam, yeye anaugua, Na kujigeuza aende nyuma.

9 Uchafu wake ulikuwa katika MARINDA YAKE; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, Bwana, teso langu; Maana huyo adui amejitukuza.

10 Huyo mtesi amenyosha mkono wake Juu ya matamaniko yake yote; Maana ameona ya kuwa makafiri wameingia Ndani ya patakatifu pake; Ambao kwa habari zao wewe uliamuru Wasiingie katika kusanyiko lako.

Sio hilo tu, yapo pia baadhi ya Miji kama Ninawi, nayo pia Mungu aliyaonya na kuyapa ujumbe kama huo huo wa wana wa Israeli, kwamba yatubie uchafu wao,  lakini hayakufanya hivyo, na siku ilipofika marinda yao, yalifunuliwa kwa aibu na Mungu mwenyewe kama Israeli walivyofunuliwa.

Nahumu 3: 4 “Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake.

5 Tazama, mimi ni juu yako, asema Bwana wa majeshi; NAMİ NİTAFUNUA MARİNDA YAKO MBELE YA USO WAKO; nami nitawaonyesha mataifa uchi wako, na falme aibu yako.

6 Nami nitatupa uchafu uchukizao juu yako, kukufanya uwe mchafu, nami nitakufanya kuwa kitu cha kutazamwa kwa dharau.

7 Hata itakuwa, wote wakutazamao watakukimbia, wakisema, Ninawi umeharibika; ni nani atakayeuhurumia? Nikutafutie wapi wafariji?”

Mungu hajabadilika ni yule yule jana, leo na hata milele..alilowatendea wana wa Israeli, na Ninawi, kwa kumwacha yeye ndicho anachokifanya kwa wale wote wanaomwacha yeye na kufuata miungu yao wanayoijua..

Biblia inasema Roho Mtakatifu anatutamani kiasi cha kutuonea wivu. Wivu anaotuonea ni wivu kama ule wa mtu na mke wake..Unaweza kujua ni wivu mbaya kiasi gani, maana yake ni kwamba tunapomkataa Roho Mtakatifu tunamtia Mungu wivu sana na hivyo tunajitafutia kupata aibu kubwa kama hiyo waliyoipata wana wa Israeli na Ninawi na kufunuliwa marinda yao..

1Wakorintho 10:21  “Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.

22  AU TWAMTIA BWANA WIVU? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?”

Kama hujampa Kristo maisha yako, fahamu kuwa unamtia Bwana wivu..ni wakati wako sasa wa kutubu na kusalimisha maisha yako kwake.. Kama upo tayari kutubu leo basi fuatisha sala hii kwa kufungua hapa >> SALA YA TOBA.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618


Mada Nyinginezo:

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

WAFIRAJI KWENYE BIBLIA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

SWALI: Biblia inajichanganya yenyewe katika Marko 5:1-6 na Mathayo 8:28-31?..Kwa maana tunaona ni habari moja lakini kila moja imezungumzwa tofauti na nyingine.


JIBU: Tusome

Marko 5:1  “Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.

2  Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;

3  makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo;

4  kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda.

5  Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe.

6  Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia;

7  akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese”

Lakini habari hiyo hiyo tunaisoma pia katika Mathayo inasema..

Mathayo 8:28  “Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile.

29  Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?

30  Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha.

31  Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe”.

Sasa swali la msingi la kujiuliza, ni kwanini habari zinatofautiana hapo?.

Ili kupata jibu la hili swali vizuri , hebu tutafakari mfano ufuatao.

Upo wewe na rafiki yako, mmeenda mahali labda kwenye interview ya kazi, mlipofika sehemu ya kazi, mkasimamishwa getini na mlinzi, ili mkaguliwe kabla ya kuingia ndani, na kwenye hiyo ofisi ndogo ya mlinzi ndani kulikuwa na mlinzi mwingine wa pili, alikuwa kasimama pembeni akitazama, ambaye ni kama msaidizi, hivyo baada ya kukaguliwa na huyu mlinzi wa kwanza hapo nje, mkaandikishwa majina yenu,  kisha mkaruhusiwa muingie ndani. Na mlipomaliza interview mlitoka getini mkasaini kisha mkaondoka.

Mlipofika majumbani kwenu mkaulizwa kila  mmoja mambo yaliendaje  huko?..Na ushuhuda wa kila mmoja ulikuwa kama ifuatavyo.

WEWE: Wewe ulianza kusimulia, kwamba baada ya kutoka nyumbani mlifikia salama hadi sehemu ya interview lakini mlipofika getini mlisimamaishwa mkakaguliwa na MLINZI, kisha mkaruhusiwa kuingia ndani, na kufanya interview salama na kutoka. (sasa zingatia hilo neno MLINZI {maana yake ni mmoja}).

RAFIKI YAKO: Ushuhuda wa rafiki yako, naye akasimulia akasema… “Tulipotoka hapa tulifika kweli eneo la kazi, lakini tulipofika pale hatukuingia moja kwa moja, kulikuwa na WALINZI, pale getini wakatukagua, kisha wakaturuhusu kuingia ndani, tukaenda kufanya interview salama na tukaondoka. (Zingatia hilo neno WALINZI, maana yake ni zaidi ya mmoja)”.

Sasa hao ni mashuhuda wawili wanaelezea tukio moja!..Je kwa shuhuda zao hizo walizotoa, ni kwamba wametoa ushuhuda wa uongo au wa kujichanganya?.. Maana wa kwanza kasema kakaguliwa na MLİNZİ MMOJA, wa pili kasema KAKAGULİWA NA WALİNZİ maana yake ni zaidi ya mmoja… Sasa yupi tumwamini hapo, na yupi tusimwamini?.

Umeona?..ukitafakari kwa makini utagundua kuwa sio kwamba wote ni waongo, isipokuwa kila mmoja kaelezea kile alichokiona chenye umuhimu zaidi kwake..Ndio maana huyu wa kwanza kaeleza kakaguliwa na mlinzi mmoja..jambo ambalo ni kweli kabisa!..Aliyemkagua ni mlinzi mmoja tu na sio wawili, yule wa pili alikuwa ndani pembeni akitazama.

Na rafiki yako naye alikuwa yupo sahihi kusema “tulikaguliwa na walinzi” kwasababu ni kweli pale kulikuwa na walinzi wawili, ambao kazi yao wote ni moja, na wote wanashirikiana. Hivyo naye pia hajatoa ushuhuda wa uongo, kazungumza ukweli.

Sasa kwa mfano huu, tutakuwa tumeanza kupata picha ni nini kilichokuwa kinaendelea hapo kwenye Mathayo na Marko.

Ni kwamba Ushuhuda wa Mathayo hauwezi kufanana na ushuhuda wa Marko wala hauwezi kufanana na ushuhuda wa Luka asilimia mia moja. Lazima kutakuwa na tofauti kidogo, vinginevyo kama utakuwa umefanana asilimia mia basi ni uthibitisho kuwa sio ushuhuda wa ukweli lazima kutakuwa na (ku-copy na ku-paste). Na pia kulikuwa hakuna haja ya kuwepo injili tofauti tofauti kwasababu zote zingekuwa zinaeleza kitu kimoja.

Hiyo ndio sababu utaona Marko anatoa ushuhuda wa mtu mmoja aliyetoka makaburini, na Luka anatoa ushuhuda wa watu wawili. Lakini kiuhalisia walikuwepo pale watu wawili waliotoka makaburini, isipokuwa ndiye aliyekuwa amepagawa zaidi na ndiye aliyekuja kumsujudia Yesu na kumsihi asimtese.

Na sio tukio hilo tu katika biblia, ambapo habari mbili zinaonekana zikishuhudiwa tofauti. Lipo tukio lingine wakati Petro anamsaliti Bwana, sehemu moja inasema “kabla jogoo hajawika mara mbili utanikana mara tatu” na katika kitabu kingine inasema tu “kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu”. Sababu ni hizo hizo tulizozitaja hapo juu.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tunaomba usibadilishe chochote katika ujumbe huu na mwingine wowote, na pia jihadhari na watumishi wa shetani ambao wanatumia masomo haya, kwa kusema kuwa wao ni waalimu wa huduma hii, na mwisho  wanaomba hela!, wanaochangia huduma hii ni wale wanaoguswa wenyewe kwa moyo wao kuchangia lakini sio kwa kuombwa fedha. Wingu la Mashahidi haijawahi kumpigia mtu simu na kumwomba hela. Ukiona mtu yeyote kashare au kushiriki masomo haya na mwisho akaweka namba zake za simu tofauti na hizi zetu +255789001312. Tunaomba umwonye aache kufanya hivyo au utujulishe kwa namba yetu hii hii +255789001312 / 0693036618

Maran atha

Na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

Jehanamu ni nini?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi Nyumbani:

Print this post