SWALI: Je! Kusoma biblia kwenye simu ukiwa kanisani, au sehemu yoyote ile ni dhambi? au kutumia Tablet madhabahuni, pia hilo nalo ni dhambi?
JIBU: Ili tupate jibu sahihi la swali hili, hebu tulihamishe na kumwuliza Mwalimu wa shuleni, Je! Ni vizuri yeye kuwafundisha wanafunzi wake kwa kutumia kitabu au tablet au simu?…Au je ni vizuri wanafunzi wake kumfuatilia anachofundisha kwa kutumia simu zao au tablets zao na si vitabu?.
Kwa Mwalimu yoyote ambaye anajua wajibu wake kamwe hataweza kuruhusu mwanafunzi wake aingie na simu pindi anapofundisha, haijalishi hiyo simu itakuwa na material gani anayoyahitaji yeye..wala yeye mwenyewe hawezi kuwafundisha wanafunzi wake kwa kutumia simu. Ataruhusu wanafunzi wake watumie hizo tablet zao, au simu zao, au ipad au computer baada ya kutoka kwenye masomo au endapo somo analotaka kuwafundisha wanafunzi wake linahusiana sana na hizo simu, au computer, au tablets..Lakini katika hali ya kawaida hawezi kamwe kuruhusu simu darasani kwake. Na lengo la kufanya hivyo sio kwamba simu ni mbaya, hapana!..bali ni kwasababu simu zina vitu vingi ambavyo ni rahisi kumtoa mwanafunzi katika umakini wa darasani, kwasababu wakati mwalimu anafundisha mara meseji imeingia, mara simu imeita, mara imezima chaji ghafla, mara imeganda ghafla n.k..
Tofauti na kitabu, Kitabu hakina muingiliano wa vitu vingi ambavyo vinaweza kuhamisha usikivu na umakini wa mtu. Hawezi mtu kusoma kitabu ghafla kikazima chaji, au kikaleta jumbe nyingi nyingi n.k. Ndio maana mpaka leo kusoma kwa kutumia kitabu imebaki kuwa njia bora na ya umakini kwa wanafunzi.
Na kanisani ni hivyo hivyo, Kanisani ni zaidi ya mashule na madarasa ya kidunia. Mtu anayeingia pale anakwenda kujifunza au kufundisha Elimu ya Mbinguni, ambayo ni kubwa kuliko elimu zote, hivyo umakini mkubwa sana unahitajika kwa anayekwenda kufundisha na anayekwenda kujifunza. Hivyo biblia iliyoandikwa kwenye kitabu Ndio njia bora na itabakia kuwa hivyo mpaka mwisho. Mtu anayefundisha kwa kutumia simu au anayeingia kanisani na simu iliyowashwa, bado hajajua anakwenda kumtafuta nani, na wala hajajua thamani ya Neno la Mungu.
Sasa sio kwamba matumizi ya biblia ya kwenye simu na Tablet na Computer ni mabaya! La si mabaya ni mazuri katika eneo husika, lakini si kanisani..Unaweza kuwa kwenye gari unasafiri umbali mfupi kwenye basi na ukatamani kusoma biblia na huna, hapo unaweza kutumia biblia kwenye simu yako, hali kadhalika unaweza ukawa upo kazini au barabarani na ukakutana na mtu ukamshuhudia na mahali hapo huna biblia ya kuweza kunukuu maandiko, hapo unaweza kutumia biblia ya kwenye simu yako au Tablet yako au ipad yako, kushuhudia au kujikumbusha maandiko. Lakini kanisani ni darasani, na si darasa la kidunia bali la kimbinguni, hivyo panahitajika Kitabu cha uzima kinachoitwa BIBLIA TAKATIFU.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Shalom, Jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima.
Kama wewe umeokoka, na kwa kitambo sasa upo katika wokovu, nataka nikuambie katika wakati unapaswa uwe nao makini sana basi ni huu, kwasababu neema uliyokuwa nayo kipindi cha mwanzoni ulichookoka, sio sawa na uliyonayo sasa..
Kulikuwa na wakati Bwana Yesu aliwaambia watu wote ikiwemo wanafunzi wake maneno haya….
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Maneno ya kukaribisha, maneno ya kufariji, maneno ya kutia moyo. Huu ni wakati ambao chochote walichokitaka kwa Bwana walikipita..
Lakini mambo hayakuendelea hivyo hivyo milele..Kuna wakati alianza kuwafundisha wanafunzi wake na makutano kwa namna nyingine, na baadhi yao kukwazika kwa maneno yake, utaona hakuwaambia tena, njoni, nifuateni, nitawafanya kuwa wavuvi wa watu, hakuwaita tena Boarnege, hakuwaambia tena nyie ni waisraeli kweli kweli msio na waa, kana kwamba anataka kuwavuta..bali aliwaambia “Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka”?..
Unajua mpaka mtu anakuuliza hivyo ni kiashirio kuwa yupo tayari kwa uamuzi wowote utakaoutoa, ..Kama unataka kwenda ni sawa nenda tu,kama unataka kubaki baki, hakuna kupembelezwa, wala kupewa maneno ya faraja tena..kama unakwenda nenda wala sitakuulizia wala kukutafuta..Lakini Petro kuona hilo alijibu haraka sana..
Yohana 6:67 “Basi Yesu akawaambia wale Thenashara, Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka?
68 Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele”.
Huo wakati hata wewe na mimi tutaupitia tu..Si muda wote katika ukristo wako Yesu atakuambia Tubu, au njoo kwangu, si kila wakati atakuonya juu ya madhara ya dhambi.. Kuna wakati ile neema uliyokuwa nayo mwanzo hutaisikia tena ndani yako..Kwasababu Kristo anakuhesabia kuwa umeshafahamu yakupasayo kutenda..
Hivyo, atakapokuona upo nusu nusu, mguu mmoja nje, mwingine ndani, upo ndani ya wokovu lakini mambo ya kidunia bado unayatamani, miezi inaenda, miezi inarudi upo vilevile.. Nataka nikuambie sauti ya Kristo utakayoisikia ndani yako ni hii NA WEWE UNATAKA KUONDOKA? Unataka kurudi nyuma?
Hatakwambia kwa mdomo, lakini atakuambia kwa vitendo. Kipindi hicho, Roho mtakatifu hatakuwepo pembeni yako tena kukushuhudia chochote, au kuugua ndani yako kukuvuta upande wake, kama ilivyokuwa kule mwanzo, ambapo ulipokuwa unaona dhambi unaogopa, hapo utakuwa ni wewe na maamuzi wako binafsi, kuchagua Mungu au dunia..Kristo atakuwa amesimama pembeni anasubiria uamue moja.
Ukichagua dunia, wala hutaona badiliko lolote ndani, unaweza ukafikiri kama vile Mungu hakuoni, utaendelea na hali hiyo hiyo, mpaka siku ile utakapojikuta kuzimu.
Hivyo mimi na wewe tusifikie hicho kipindi ndugu yangu, hata kama Mungu hakupi kile unachokitaka leo hii, hata kama unaona maneno yake ni magumu, hupaswi kufikiria kurudi nyuma au kufikiria mambo ya ulimwenguni, kumbuka walioitwa ni wengi, lakini wateule ni wachache, wanafunzi wa Yesu walikuwa ni wengi sana, lakini waliovumilia mpaka mwisho walikuwa ni 11 tu, na wengine wachache sana mfano wa Mathiya.
Jiulize ni nini kilichokuvuta kwa Yesu zamani, mpaka ukaamua kuokoka, na leo hii ni nini kinachokufanya utake kurudi nyuma? Neema ya kukuvuta haipo tena..Kwako Neno linalobakia kutoka kwa Yesu ni hili; Je! Na wewe unataka kuondoka?
Waebrania 6:4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,
5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri”.
Hivyo tusonge mbele katika Imani, mitume walivumilia mpaka mwisho, lakini sasa sote tunatamani kuwa kama hao, Lakini wale wengine hata mmoja husikii habari yake baada ya pale.. Hivyo na sisi tukivumilia mpaka mwisho kwa Kristo, tutazirithi Baraka tulizoahidiwa na Mungu tangu zamani.
Taji la uzima limewekwa mbele yetu. Na siku ile tutaketi naye katika kiti chake cha enzi kama alivyotuahidia sisi wakristo wa kanisa hili la Laodikia(Ufunuo 3:21).
Bwana atusaidie, Bwana atutie nguvu sote.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Kristo hakuitwa Imanueli badala yake akaitwa Yesu?
JE! KUNA UCHAWI KATIKA KUTENDA WEMA?
YESU AKALIA KWA SAUTI KUU.
KWANINI LEO HII KUNA KUNDI KUBWA LA WAKRISTO WALIORUDI NYUMA?
UNYAKUO.
NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!
Hakuna asiyejua kuwa Mzazi mwenye hekima anapokaribia kumaliza siku zake, huwa anawaita wanawe kuwapa wosia mfupi wa maisha pamoja na kuwabariki. Na Mzazi mwenye upendo ni yule anayewaambia wanawe au wajukuu wake ukweli wa maisha, na anayewapa tahadhari na anayewapa faraja na tumaini.. Na zaidi sana anapokaribia kumaliza siku zake huwa anawaambia wanawe siri ambazo walikuwa hawazijui.
Ndivyo alivyofanya pia Bwana wetu Yesu Kristo, kabla ya kuondoka kwake..Aliwaita wanafunzi wake na kuwapa wosia na kuwaonya mambo watakayokutana nayo baada ya yeye kuondoka. Alitumia masaa kadhaa kuzungumza nao mambo kadha wa kadha.
Na wosia wake huo umegawanyika katika vipengele vitano:
KİPENGELE CHA KWANZA: Ambacho ndiyo ile sura ya 13 yote, utaona Bwana anawaonya wanafunzi wake juu ya unyenyekevu, utaona anawafundisha kwa vitendo namna ya kunyenyekeana, (kwa kuonyesha kielelezo yeye mwenyewe, kwa kuchukua maji na kuosha miguu yao) na akawaambia atakayetaka kuwa mkubwa kuliko wote sharti awe mdogo kuliko wote. Na kama yeye wanayemwita Bwana ameshika miguu yao wao, inawapasaje wao?..Hawana budi kunyenyekeana sana na kujishusha baada ya Bwana kuondoka.
KİPENGELE CHA PİLİ: Ambacho ni sura ya 14 yote utaona Bwana anawapa faraja wanafunzi wake, kwamba wasiogope wala wasifadhaike atakapowaacha…kwani anakwenda kuwaandalia makao. Na anawaambia hatawaacha yatima, bali atawaletea msaidizi ambaye ndiye Roho Mtakatifu, na furaha yao itarudia tena. Nao watajiona kama vile hawajaachwa.
KİPENGELE CHA TATU: Ambacho ni ile sura ya 15 yote, Utaona Bwana anawaonya na kuwakumbusha kuwa wazae matunda baada ya kuondoka kwake, na kuwakumbusha kupendana..
KİPENGELE CHA NNE: Ambacho ndiyo ile sura ya 16 yote, Utaona Bwana anawaonya kuhusu mambo yatakayokwenda kuwatokea baada ya yeye kuondoka, akawaambia, dhiki watakazopitia na mateso, lakini wasiogope kwasababu yeye atakuwa pamoja nao.
Yohana 16: 1 “Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa.
2 Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada.
3 Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.
4 Lakini nimewaambia hayo, ili makusudi saa ile itakapokuja myakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia. Sikuwaambia hayo tangu mwanzo, kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi”.
KİPENGELE CHA TANO NA CHA MWİSHO: Ambacho ndiyo ile sura ya 17, ni kipengele cha Yesu mwenyewe kuhitimisha kwa kuwaombea wanafunzi wake.
Sasa hata baba anapotoa wosia kwa wanawe kabla ya kufariki kwake, Mwishoni huwa anapowaombea baraka na heri, hawezi kuwaombea watu wa mtaani, au watu wa kazini kwake, ni lazima atawaombea na kuwabariki wale aliowausia pamoja na watoto wao, kwasababu ndio urithi wake.
Ndicho Bwana alichokifanya hapa, katika kipengele hichi baada ya kuwaambia mambo yatakayowatokea na majukumu yao, baada ya kuondoka kwake ndipo anawaombea..
Na anawaombea nini?
Jibu tunalipata mbele kidogo..(Zingatia hivyo vipengele vilivyoanishwa kwa herufi kubwa)
Yohana 17: 9 “Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;
10 na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao.
11 Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, KWA JİNA LAKO ULİLONİPA UWALİNDE HAWA, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo.
12 Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
13 Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.
14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
15 Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; BALİ UWALİNDE NA YULE MWOVU.
16 Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
17 UWATAKASE KWA İLE KWELİ; NENO LAKO NDİYO KWELİ.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni.
19 Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli.
20 WALA Sİ HAO TU NİNAOWAOMBEA; LAKİNİ NA WALE WATAKAONİAMİNİ KWA SABABU YA NENO LAO.
21 WOTE WAWE NA UMOJA; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.
24 BABA, HAO ULİONİPA NATAKA WAWE PAMOJA NAMİ PO POTE NİLİPO, WAPATE NA KUUTAZAMA UTUKUFU WANGU ULİONİPA; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.
25 Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma.
26 Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao”
Wosia huu unatuhusu sisi pia, kama tumefanyika kuwa wanafunzi wa Kristo hatuna budi kupendana, kunyenyekeana, kuwa na umoja na kuifanya kazi yake. Tukizingatia huo wosia basi tutafanikiwa sana katika huu ulimwengu.
Vile vile maombi hayo si ya mitume peke yao..bali ni ya kwetu pia.. kwasababu hapo kwenye mstari wa 20 anasema “WALA Sİ HAO TU NİNAOWAOMBEA; LAKİNİ NA WALE WATAKAONİAMİNİ KWA SABABU YA NENO LAO.”
Bwana alishatuombea miaka 2000 iliyopita na ameshatubariki na kutupa utukufu..Ni haki yetu kudai utukufu wetu na baraka zetu, na hatuzidai kwa maneno, bali kwa kuyafanya mapenzi yake, tunapofanya mapenzi yake katika ulimwengu wa roho ni haki yetu kupata baraka na heri na afya.
Bwana atubariki tuzidi kuwa na umoja na kupendana na kunyenyekeana…Na zaidi sana tuifanye kazi yake..Na mwisho tuzipokee baraka zake alizotubariki miaka 2,000 iliyopita.
Maran tha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Tunamtumikia Mungu kwa karama tulizopewa, na karama ndizo zinazozaa Huduma..Na Karama za Roho Mtakatifu zimefananishwa na viungo katika miili yetu. Maana yake tukijifunza kwa kina jinsi viungo vya miili yetu vinavyofanya kazi basi tutakuwa tumeelewa vyema pia jinsi karama za Roho zinavyotenda kazi.
Warumi 12:4 “Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja.
5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake”
Tabia moja ya kipekee ya viungo vya mwili ni kwamba kila kiungo kipo kwaajili ya kuvisaidia viungo vingine…Kwamfano Miguu utaona ipo kwa kazi ya kuubeba mwili, haipo kwa kazi ya kujibeba yenyewe..Mikono ni hivyo hivyo, ipo kwa kazi ya kuhudumia mwili sehemu mbalimbali kama kupeleka chakula mdomoni, kuosha mwili, kuchana nywele n.k..
Vile vile macho yapo si kwaajili ya kujiangalia yenyewe, bali kwaajili ya kutazama mambo yanayoendelea katika mwili na nje ya mwili na hivyo kupeleka taarifa kwenye ubongo. Masikio hayapo kwaajili ya kujisikia yenyewe, wala ngozi haipo kwaajili ya kujifunika yenyewe, bali kuufunika mwili na viungo vya ndani.
Moyo haudundi kujifurahisha, au kujipa burudani, bali unafanya vile kuhakikisha unasukuma damu katika viungo vyote vya mwili. Na viungo vingine vyote ni hivyo hivyo, vipo kwaajili ya kusaidia viungo vyenzake.
Na karama za rohoni zinatenda kazi kwa namna hiyo hiyo. Ukiona mahali hakuna kusaidiana basi hapo kuna kasoro, Roho wa Mungu hayupo hapo, lakini mahali ambapo Roho Mtakatifu yupo ni lazima viungo vyote visaidiane.
Ukiona ndani yako huna msaada wowote katika mwili wa Kristo, au huhitaji msaada wowote basi huo ni uthibitisho kwamba wewe ni kiungo kilichokufa na tena kimezikwa.. Kwasababua hata mkono uliokufa haufanyi chochote, na kama umekufa muda mrefu basi maana yake ni kwamba umeshaoza na kilichobakia ni mifupa tu..
Vivyo hivyo kama huna msaada wowote katika Mwili wa Kristo wewe ni mifupa katika roho, na usifurahie kuwa katika hiyo hali, ni afadhali ukafufuka leo!.
Utasema mimi siijui karama yangu! Hivyo nasubiri Mungu anifunulie kwanza.
Ndugu hakuna kitu kinakuja kwa kukaa tu na kukisubiri…Wengi wanakaa tu wakisubiri Mungu awafunulie karama zao, (Wengine wanafanya hivyo kwasababu hawajui na wengine ni wavivu). Nataka nikuambie mtu wa Mungu kama ulikuwa unakaa kusubiri kwasababu hujui basi nataka nikuambie usiendelee kusubiri kwasababu utakaa sana, na wala hutaona chochote…kila siku utabaki ukikisia tu labda ni hii, au ile.. utabaki ukihuzunika unapoona wengine wanafanya kazi ya Mungu na wewe hufanyi chochote..Hivyo usibaki kusubiri!. (Kasome hichi kisa 2Wafalme 7:1-15 )
Kuifahamu karama yako hakuji kwa namna hiyo (ya kusubiri), kunakuja kwa wewe kujiingiza kwenye kazi yoyote au huduma yoyote ya Mungu ambayo inaona inafunguka mbele yako, na huko huko utaona kuna mahali umefit vizuri!..utaona kuna mahali unafanya vizuri na kwa furaha zaidi ya wengine na tena unafanya kwa ubora na pasipo kusukumwa..Utaona Mungu anaanza kukufungulia milango na kukupa akili na uwezo wa kutumika katika hilo eneo siku baada ya siku. Ukiona umefikia hiyo hatua, basi hapo huenda ndio mahali huduma yako ilipo, usianze kunia Makuu na kutamani makubwa, anza na hicho hicho chako kwasababu ni muhimu sana katika Mwili wa Kristo kwaajili ya kuwahudumia watu wake, na siku zinavyozidi kwenda Kristo atazidi kukistawisha.
Usisubiri maono wala kuoteshwa ndoto wala kutokewa na Bwana au malaika!..Je siku ulipokwenda kutafuta kazi ulisubiri maono au ndoto?. Vivyo hivyo katika kuifanya kazi ya Mungu hatuenendi kwa kuona bali kwa IMANI. (2Wakorintho 5:7).
Sasa utaanzaje safari ya kuilelekea huduma yako Mungu aliyoikusudia?
Kwanza kabisa, jichanganye na watakatifu mahali unapoabudu na mahali unapoishi, au popote pale unapoweza kukutana nao (Usijitenge wala usijione bora).. Shiriki nao katika kazi wanazozifanya za kanisa au za kihuduma, popote pale ambapo unaona unaweza kuchangia mawazo yako, au ujuzi wako, au chochote kile, wewe changia!. Utaona pale ulipochangia pengine mawazo yako yamekuwa bora mara nyingi kuliko ya wengine, au pale ulipotumia ujuzi wako au elimu yako pameleta matokeo makubwa sana, na hivyo pakafanya uwepo wako uwe wa muhimu sana..n.k
Kwamfano unaweza kuingia kwenye kundi, katikati huko ukasikia kuna mtu fulani alipatwa na matatizo haya na yale hivyo sasahivi yupo katika masononeko makubwa, wameenda watu kumfariji lakini wapi!..na hata kashafikia hatua ya kukata tamaa na kurudi nyuma, sasa wewe kama karama yako ni faraja, utaona kuna kitu kitakuchoma ndani..na kujisikia huruma mara mbili zaidi ya wenzako, na kutafuta kwenda kumsaidia yule mtu, na utashangaa umemrudisha na amerudia katika hali yake, na watu wote wanashangaa umewezaje! ..ukishaanza kuona hizo hali za kuweza kufanya kitu ambacho ni kigumu kwa wengine kukifanya lakini wewe umeweza tena kwa ufasaha!, basi huo ni uthibitisho kuwa haupo mbali na huduma yako. Ukifikia hiyo hatua utaona Bwana ataanza kukusafishia njia zaidi ya kuliendea kusudi alilokuitia utaona hekima inazidi kuongezeka juu yako siku baada ya siku, na utaona majukumu ya wewe kuifanya hiyo kazi ya Mungu yanazidi kuongezeka, utaona mzigo unazidi kuongezeka ndani yako..Na mwisho wa siku Mungu ataweka ndani yako UZIO.
Uzio ni hali fulani ambayo inawatokea watumishi wa Mungu, ambao ikipita siku au masaa hawajafanya kazi ya Mungu, wanasikia hali moja mbaya sana, hata kufikia KUUMWA! au kuishiwa nguvu za Mwili. Ndio kama ile hali ya Bwana aliyosema katika Yohana 4:34 “Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake”.
Kazi ya Mungu inakuwa kama ni chakula kwao!. Hivyo hiyo hali ni kama ishara ya kumsaidia mtu wa Mungu asitoke nje ya mstari. Hivyo ikitokea amemaliza siku moja au mbili hajatumika kabisa katika kazi yake hiyo, hali ya mwili wake inaanza kumbadilikia na hivyo inamfanya siku zote aifanye kazi ya Mungu kama vile ni chakula chake.
Sasa kumbuka kama tulivyotangulia kusema..Karama na huduma ni kwaajili ya masaidiano na si kwaajili ya kujisaidia mwenyewe.. Kwahiyo ukiona umeingia kwenye huduma fulani katikati ya watakatifu na moyo wako unaelekea kupata pesa, au kupata umaarufu wako binafsi na si wa Kristo, au kupata jina au cheo, au umaarufu..basi jua hiyo ni roho nyingine ya Adui ipo ndani yako, ambayo shetani kakupandikizia, na lengo la roho hiyo ni kwenda kuliharibu kundi la Mungu
Lakini ukiona ni kwenda kusaidia watakatifu na watu wengine, basi zidi kufanya mbele ya safari Bwana atakufungulia milango zaidi.
Ndugu kama ulikuwa unasubiria maono ndipo uanze kuifanya kazi ya Mungu, leo umejua…usisubiri, jiunganishe na wanaofanya kazi za Mungu na huko huko Bwana atakusafishia njia..Lakini pia kabla ya kwenda huko kama hujaokoka! Ni vyema ukafanya hivyo leo, kwasababu huwezi kwenda kufanya kazi ya mtu ambaye hampatani. Hivyo ni lazima umkubali ndipo ukafanya kazi zake, hivyo mpokee leo Kristo moyoni mwako, na kisha katafute kubatizwa na Roho Mtakatifu atakuongoza katika njia unayoiendea.
Tafuta kwa bidii kuifanya kazi ya Mungu, na Mungu atakuheshimu.
Bwana akubariki!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Ni wajibu wa kila mkristo kutambua kuwa kuna vita vikubwa sana katika kuyafanya mapenzi ya Mungu, na mapenzi ya Mungu ni Neno la Mungu..Mtu anapolisoma Neno la Mungu na kulielewa na kulifanya au kulitenda kama lilivyoandikwa, hapo anakuwa anafanya mapenzi ya Mungu.
Leo tutakwenda kutazama kipengele kimoja cha Neno la Mungu ambacho huwa shetani anakiua kwa watu wengi. shetani huwa hapendi watu walishike Neno la Mungu, kwasababu Neno la Mungu ndio ufunguo wa mafanikio yote.
Kwamfano Neno la Mungu linasema tuwe watu wa kuomba (Wakosai 4:2, Wafilipi 4:6, Yakobo 5:16, Yuda 1:20) na pia kuomba/kusali ndio ngao pekee ya kujilinda na majaribu ya yule Adui Marko 14:38. Hivyo mtu anayeomba, kamwe shetani hawezi kumshinda kwa majaribu..Na njia mojawapo shetani anayoitumia kuangusha watu ni kwa njia ya majaribu.
Utauliza majaribu kwa namna gani?
Unapopanga kwenda kanisani halafu linatokea jambo la kukukwamisha, hilo tayari ni jaribu, unapopanga kwenda kutenda wema lakini kinatokea kitu cha kuvuruga huo mpango hilo tayari ni jaribu..Sasa majaribu kama hayo yanaweza kuepukika kama ukiwa mtu wa kuomba.
Ukiwa mtu wa kuomba utaona kila unalolipanga linakwenda kama ulivyolipanga…Ulipanga jumapili uende kanisani, unaona siku hiyo inafika hakuna vikwazo vyovyote vinavyojitokeza kuanzia asubuhi mpaka jioni, umepanga uende ukahubiri unaona ratiba zinakwenda kama ulivyopanga n.k.
Sasa turudi kwenye somo letu, lenye kichwa kinachosema je! Kuna uchawi katika kutenda mema?
Ndugu hakuna uchawi wowote katika kutenda wema/mema. Shetani amekuwa akiwatishia watu wengi kuwa ukifanya kitu fulani kwa mtu fulani unaweza kujikuta unalogwa!. Hivyo ni vitisho vya shetani kuwazuia watu wasibarikiwe. Kwasababu anajua funguo mojawapo ya kubarikiwa ni kuwa mtoaji..Bwana wetu Yesu alitufundisha hiyo siri ambayo tulikuwa hatuijui alisema..
Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.
Sasa shetani hataki tufanikiwe! Anachotaka tuendelee kuwa jinsi tulivyo..Na ili kuhakikisha hilo linafanikiwa anakimbilia kuligeuza hili neno la Bwana wetu Yesu, linalosema wapeni watu vitu nanyi mtapewa…yeye (shetani) analigeuza na kusema (usimpe mtu usiyemjua kitu usimpe nguo zako, atazipeleka kwa mganga na mwisho wa siku utajikuta wewe ndio unakuwa maskini, atakwambia usisaidie watu barabarani wengine ni wachawi, chuma ulete, utajikuta nyota yako inahamishwa).
Hayo ndiyo mahubiri ya shetani, ya kuwazuia watu wasibarikiwe. Na kwasababu inakuja na vitisho vikali, watu wengi inawaogopesha na hivyo inawafanya wasidhubutu kusaidia saidia hovyo!!. Nimewahi kuona filamu fulani inaonyesha mtu kapita barabarani akakutana na mtu anaomba msaada, na katika kuomba kwake akamsaidia kwa kumpa fedha, ghafla yale matatizo ya yule mtu yakahamia kwake huyo aliyetoa msaada.
Ndugu usidanganyike na injili hiyo ya kuzimu!..(kumbuka kulishika Neno la Mungu ni vita!)..lazima upambane hiyo vita na uishinde..na huishindi kwa maneno tu! Bali kwa kulijua Neno la Mungu vizuri, vinginevyo ni rahisi kwenda na maji..kwasababu shetani anavitisho vya kutosha kuhakikisha hulitendi neno la Mungu. Kila jambo kwako atakuundia picha ya kulogwa tu.
Hivyo ni uongo kwamba ukifanya wema utalogwa, au utafungua mlango kwa shetani kuyadhuru maisha yako…Huo ni uongo
Sasa unaweza kuuliza hata kama “yule fulani namjua ni mchawi, au anaamini ushirikina, au ni mganga wa kienyeji” akija kuniomba fedha au chochote kile nimpe??..je hatanidhuru?..Jibu ni ndio mpe..hutapatikana na madhara yoyote badala yake ndio utabarikiwa…hata kama ni mchawi kaja kukuomba na umeona ni kweli anahitaji msaada mpe usifikiri mara mbili mbili…kwasababu hakuna uchawi katika kutenda mema!..
Mithali 25:21 “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; 22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu”..
Utasema hilo ni agano la kale, vipi katika agano jipya? Kasome Warumi 12:20.
Sasa hapo anasema “Adui yako” na si rafiki yako, maana yake ni kwamba “yule mtu ambaye unaona anaweza kukuletea madhara”.. Huyo ndiye msaidie kwa kumpa chakula au chochote kile, kwasababu hakuna chochote kitakachokupata wewe cha kukuletea madhara unapomsaidia, badala yake hicho ulichompa ndio kitakuwa chachu ya kumponya yeye, na Mungu atakubariki wewe kwa kufanya hivyo.
Ndugu kuna vita kali katika kulishika Neno, tena si ndogo…Hilo Neno la Bwana Yesu kulisoma ni rahisi, lakini ukilileta katika maisha halisi linavita vingi, limejaa vitisho vya shetani ndani yake, limewafanya hata watu wakiona mtu kalala barabarani, kaishiwa nguvu wampite tu! Bila kutoa msaada wowote..wakihofia kwamba endapo wakimsaidia ndio nyota zao zitakwenda hivyo..kumbe kwa kumpita yule ndio wanazipita baraka zao hivyo hivyo.(kasome Luka 10:32-36).
Na kuna mahubiri siku hizi yanayofundisha kinyume cha hilo Neno zuri la Bwana wetu Yesu Kristo, “neno lililojaa upendo wa ajabu”…lakini wanahubiri na kulitukuza neno la Adui shetani lililojaa chuki na vitisho!. Tangu lini Mungu aliye na upendo akamkataza mwanadamu wake kuwa na upendo?.
Unataka kupata fursa? Unataka kupata vitu? Unataka kubarikiwa?..Njia ni hiyo (wapeni watu vitu nanyi mtapewa), na sio tu fedha, au chakula.. bali hata faraja..wafariji wanaohitaji kufarijiwa nawe pia siku ya kupata mashaka na masononeko, Bwana atamtuma mtu wa kukufariji, watie moyo wanaohitaji kutiwa moyo ili itakapofika siku ambayo utakuwa umekaribia kukata tamaa, uwe na deni kwa Mungu wako la wewe kufarijiwa pia n.k n.K.
Mathayo 5:42 “Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.
43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”
Bwana akubariki, na Bwana atubariki wote.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
JIEPUSHE NA UNAJISI.
NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!
KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.
UPONYAJI WA ASILI
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Shalom, nakukaribisha tuyatafakari Pamoja maneno ya uzima.
Katika hichi kipindi cha mwisho, kuna mwitikio mmoja tu, ambao utamtambulisha bibi-arusi wa kweli wa Kristo ni nani..
Kumbuka bibi-arusi ni tofauti na Suria, Sulemani alikuwa na Masuria 700 lakini wake au (bibia-arusi) walikuwa ni 300 tu. Tofauti ya mke na suria ni kuwa mke anauhalali wa vyote ikiwemo urithi na mali, lakini suria yeye anaweza kupewa vyote lakini sio urithi au jina..Jambo hilo utaliona kwa Ibrahimu, ambaye mbali na Isaka alikuwa pia na watoto wengine 7, lakini wao walipewa zawadi tu, mashamba, majumba n.k..Lakini Isaka peke yake ndiye aliyepewa vyote, zawadi pamoja na urithi na jina,..Na ndio maana mpaka leo, tunamtambua Isaka, na sio wale wengine..Hiyo ni kwasababu walikuwa ni wana wa Masuria na sio wana wa mke halali kama ilivyokuwa kwa Sara. (Kasome Mwanzo 25:5-6)
Ndivyo hivyo hata wakati huu wa mwisho, haya makundi mawili yapo, hivyo usifurahie tu, Mungu kukubariki, usifurahie tu Mungu kukupa hiki au kile..furahia pale unapokuwa na uhakika kuwa wewe ni mrithi wa ahadi za milele za Mungu baada ya Maisha haya..
Kwasababu Masuria sikuzote ni wengi kushinda wake.
Sasa tukirudi katika kitabu cha ufunuo, utaona sehemu nyingi, Bwana Yesu alianza kulitamka hili Neno “tazama, naja upesi”;.. Utasoma..
Ufunuo 22:7 “Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki….
12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.
Hiyo ni kuonyesha kuwa wakati wake wa kurudi duniani umekaribia sana..
Lakini ukishuka chini kidogo utaona, wanaorodheshwa wawili walioitikia mwito huo, nao ni Roho Mtakatifu na bibi-arusi.
22:17 “NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.
Ni kwasababu gani bibi-arusi alikuwa na ujasiri wa kuitikia mwito huo “Njo Bwana Yesu”? Ni kwasababu, alijua urithi wake halisi upo karibu, ni kwasababu alikuwa na ajasiri wa Imani yake, kwa Yule Roho Mtakatifu aliye ndani yake.
Na ndio maana hata Mtume Yohana, aliposikia Bwana akiyarudia maneno hayo tena chini kidogo, naye pia aliitikia kwa ujasiri mkubwa na kusema amina na uje Bwana Yesu..
Ufunuo 22:20 “Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu”.
Maneno haya bibi-arusi tu peke yake aliyejazwa Roho Mtakatifu ndio atakayekuwa na ujasiri wa kuyasema wakati huu wa mwisho..
Swali la kujiuliza ni je! mimi na wewe tunaweza kuyasema maneno hayo? kumbuka Jibu halipo katika vinywa vyetu bali katika mioyo yetu. Kama hatuna ujasiri huo basi sisi sio bibi-arusi, haijalishi tutasema tumeokoka kiasi gani, sisi tutakuwa ni Masuria tu. Na siku ya unyakuo itakapofikia tutabaki hapa dunia, hatutanyakuliwa Pamoja na bibiarusi wa kweli.
Masuria kwa jina lingine ndio wale wanawali wapumbavu ambao walichukua taa zao, lakini hawakuwa na mafuta ya ziada katika vyombo vyao, Na Bwana arusi alipokuja walikutwa hawana mafuta ya kutosha (Mathayo 25)
Kwahiyo ndugu tusifurahie tu, kusema sisi ni wakristo, bali tufurahie kusema sisi ni bibi-arusi, tuliojazwa Roho Mtakatifu.. Kumbuka lile neno la Bwana “Waitwao ni wengi, ila wateule ni wachache”
Kama tulishaokoka, lakini bado tulikuwa tunaishi maisha ya uvuguvugu, basi huu ni muda wetu sasa, kuzitengeneza taa zetu katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho.
Na Mungu atatujalia tufikie mwisho mwema kwa neema zake.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Jina La Bwana wetu Yesu libarikiwe. Karibu tuyatafakari maandiko tena siku ya leo.
Kuna mtafaruku mkubwa sana katika ukristo kuhusu vyakula, wapo wanaoamini kuwa vipo vyakula najisi na wapo wanaoamini kuwa vyakula vyote ni halali kuliwa. Na hivyo kusababisha mashindano yasiyoisha.
Kama tukiyasoma maandiko tutaona kuwa vyakula haviwezi kumtia mtu unajisi. Ingawa hatuwezi kusema kwamba vyote vinafaa, hapana si vyote..huwezi kula mbao, au chuma, au sumu au pombe na kusema vinafaa…hapana hivyo havifai kwasababu vinauharibu mwili badala ya kuujenga.
1Wakorintho 10:23 “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.
Kwahiyo kama umehakiki hicho ulacho hakina madhara katika mwili wako, basi kula! Si dhambi..lakini kama umehakiki kwamba kina madhara basi usile. Na pia kama unawasiwasi na mashaka kwamba hicho ulacho kinaweza kuwa na madhara basi usile kabisa. Kwasababu hata usipokula hutendi dhambi!!
Warumi 14:22 “ Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.
23 Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi”.
Sasa leo hatutaingia sana kujifunza juu ya vyakula, kama utahitaji somo juu ya hilo, basi utatujuza inbox..Lakini tutajifunza namna ya kuepukana na unajisi, kwa kupitia maandiko yafuatayo ambayo ni maarufu sana.
Tusome…
Marko 7:5 “Basi wale Mafarisayo na waandishi wakamwuliza, Mbona wanafunzi wako hawaendi kwa kuyafuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi?……………………………..
14 Akawaita makutano tena, akawaambia, Nisikieni nyote na kufahamu.
15 Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu.
16 Mtu akiwa na masikio ya kusikilia, na asikie.]”
Sasa maneno haya Bwana wetu Yesu aliwaambia makutano, ambao pengine idadi yao ilikuwa ni mamia au maelfu, na ndani ya mkutano huo walikuwepo pia wanafunzi wake wale 12, Na kwa Pamoja wakasikia maneno hayo…kwamba hakuna kimwingiacho mtu kimtiacho unajisi bali kimtokacho..sasa baada ya maneno hayo kama umefuatilia kwa makini Bwana hakuendelea kuongea zaidi. Hivyo kila mmoja akatoka na tafsiri yake kichwani…naamini wengi walifiki kwamba ni kimwingiacho mtu ni chakula na kimtokacho ni matapishi au kinyesi na mkojo..na kwamba hivyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi..Lakini ule mkutano wote ulitawanyika ukidhani umemwelewa Bwana vizuri kumbe hawakumwelewa hata kidogo..
Baadaye ndipo wanafunzi wake wakahisi kuna kitu hawakukielewa na hivyo wakaamua kumfuata wakiwa peke yao kumwomba awafafanulie zaidi..
Tusome..
“17 Hata alipoingia nyumbani, ameuacha mkutano, wanafunzi wake wakamwuliza habari za ule mfano. 18 Akawaambia, Hivi hata ninyi hamna akili? Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia unajisi;
19 kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni tu; kisha chatoka kwenda chooni? Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote.
20 Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.
21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,
22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.
23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”.
Umeona hapo?. Wanafunzi wamepata ufafanuzi vizuri, lakini makutano hawakupata!..Makutano wameondoka wakidhani unajisi ni majasho, matapishi, haja kubwa na haja ndogo…Kumbe sivyo!. Vitu najisi ni vile vinavyotoka moyoni na si mwilini…
Unapopita barabarani na kwa bahati mbaya ukasikia matusi yakitukanwa… yale yanaingia moyoni mwako, na kwenda kwenye hazina ya kumbukumbu zako, (hapo hakuna unajisi)..lakini unapopitia hali ya kuudhiwa siku za mbeleni na kwenda kuifungua ile hazina na kisha kuyatumia yale matusi uliyoyasikia huko nyuma na kumtukana mwingine hapo ndipo unapokuwa najisi.
Unapoona mauaji yamefanyika ambayo sio wewe umeyafanya kwamfano mauaji ya utoaji mimba..Jambo lile linakwenda kwenye hazina ya moyo wako, hapo hujawa najisi, lakini siku moja ukapata ujauzito na ukaenda kuutoa au mwingine akapata ujauzito na ukamshauri akaitoe, hapo tayari umekuwa najisi. Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo.
Na mtu najisi mbele za Mungu ni mtu mchafu..Katika agano la kale mtu najisi alikuwa haruhusiwi hata kuingia katika kusanyiko la Mungu, anatengwa mpaka atakaposafishika…Na hata sasa bado unajisi upo!..Ukiwa mlevi tayari umejitia unajisi, ukiwa mwasherati, mzinzi, muuaji, mtukanaji, mlawiti, mtazamaji picha za tupu, msengenyaji n.k tayari wewe ni najisi mbele za Mungu, hustahili kuwepo katika kundi la Mungu, haijalishi umeshakuwa mkristo kwa miaka mingapi, bado ni najisi mbele za Mungu, kwamba unahitaji kutubu..Na kujitenga na hayo mambo.
Tito 1:15 “Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia. Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai”.
Kama hujaokoka! Kristo anakupenda na alikufa kwa ajili yetu..Wokovu unapatikana bure leo, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kupiga magoti binafsi, na kutubu mbele zake kwa dhati kabisa..Kama umemaanisha kweli pale utakaposema tu Amen, basi tayari ameshakusikia na kukusamehe..na utaona amani ya ajabu imeingia moyoni mwako, baada ya hapo nenda katafute ubatizo sahihi wa kimaandiko, ambao ni ule wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo, ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (Mathayo 28:19, Matendo 2:38)..Kwa kuyatii maagizo hayo machache na mepesi utakuwa utakuwa umeihakikishia mbingu kuwa kweli umeanza umegeuka na hivyo Mungu atakuheshimu zaidi. Na utakaso halisi wa Kristo utakuja ndani yako.
Bwana akubariki.
Kama umeokoka usisahau kuliombea Kanisa Pamoja na wakristo wote na watumishi wa Mungu kila siku..
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?
LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.
KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.
MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.
Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)
JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.
Hazama ni nini?
Hazama ni pete ya puani.
Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;
Mwanzo 24:47, Kutoka 35:22,
Na pia ukisoma Ezekieli sura ya 16 yote utaona jinsi Mungu anavyolilinganisha taifa la Israeli na msichana ambaye alipozaliwa tu alitelekezwa porini na wazazi wake akiwa hata hajakatwa kitovu chake. Na Bwana alipokuwa anapita (hapa akijifananisha na mwanaume fulani), alimwona na kumuhurumia, akamchukua na kwenda kumtunza, akamkuza, akafanya naye maagano kuwa atakuwa wake, akamkuza vizuri sana, akawa mrembo sana, akamvisha mavazi mazuri, na kumpamba kwa kila aina ya mapambo ikiwemo hazama na vikuku, lakini baadaye alipokuja kuwa mtu mzima alikengeuka na kuanza kuzini na wanaume wengi, na kuwa kahaba wa kipindukia, ..
Ezekieli 16:11 “Nikakupamba kwa mapambo pia, nikatia vikuku mikononi mwako, na mkufu shingoni mwako.
12 NIKATIA HAZAMA PUANI MWAKO, na pete masikioni mwako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha; na mavazi yako yalikuwa ya kitani safi, na hariri, na kazi ya taraza; ulikula unga mzuri, na asali, na mafuta; nawe ulikuwa mzuri mno, ukafanikiwa hata kufikilia hali ya kifalme.
14 Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kwa sababu ya uzuri wako; kwa maana ulikuwa mkamilifu, kwa sababu ya utukufu wangu niliokutia, asema Bwana MUNGU”.
Lakini sasa mfano huo haumaanishi kuwa wanawake wa ki-kristo wanaruhusiwa kujipamba hapana, kumbuka huo ni mfano tu ambao Mungu aliutoa kuonyesha ni jinsi gani Israeli taifa lake alilolipamba rohoni kwa utukufu wake, tangu zamani, baadaye likaja kukengeuka kuabudu miungu mingine tofauti nay eye.
Biblia inasema..
1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.
3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu”.
Umeona, mwanamke wa kikristo hapaswi kuweka hazama, au vikuku, au lipstick, au wanja, au mikufu, au hereni mwilini mwake, badala yake mapambo haya anapaswa ayahamishie rohoni, kwa matendo mema. Ndivyo biblia inavyoagiza.
Kwahiyo kama wewe ulikuwa unaweza hazama au vipini puani mwako, ni vyema ukaacha. Ishi sasa maisha ya kama wanawake wacha Mungu walivyoyaishi. Mapambo yasikusababishe uikose mbingu.
Shalom.
Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
MASERAFI NI NANI?
Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?
Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)
Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.
Katika biblia shetani amepewa majina tofauti tofauti na hiyo ni kutokana na aina ya kazi anazozifanya hapa duniani, kwamfano biblia inapomwita shetani/ibilisi ni kwasababu ni mpinzani na mshitaki wa roho zetu kwa Mungu ndio tafsiri ya jina hilo,.
Vilevile sehemu nyingine inapomwita Joka (Ufunuo 12), ni kwasababu ni mwongo kama alivyokuwa nyoka, na anameza roho za watu kama majoka yafanyavyo kumeza wanyama,..
Bado sehemu nyingine inamwita, mkuu wa ulimwengu huu, (Yohana 12:31,2Wakorintho 4:4), kwasababu mambo yote yaliyotukuka ulimwenguni sasa yanashikiliwa na yeye, yeye ndiye kiongozi wa hayo ..
Pia inamwita mfalme wa uweza wa anga (Waefeso 2:2) kwasababu nguvu zote za giza katika ulimwengu wa roho anazishikilia yeye, baba wa mapepo na wachawi duniani.
Vilevile sehemu nyingine inamwita mjaribu (Mathayo 4:3,1Wathesalonike 3:5), kwasababu, yeye ndio chanzo cha majaribu yote kwa mkristo..Na ndio maana Bwana Yesu alituambia kesheni mwombe msije ingia majaribuni..Kwasababu tusipoomba huyu atapata nafasi kubwa ya kutuletea majaribu ili kutuangusha.
Lakini zaidi ya yote biblia inatuonyesha kuwa atakuja kuwa na jina lingine, lijulikanalo kama Abadoni au Apolioni,.. Tafsiri ya jina hili ni MHARIBIFU…Ikiwa na maana atakuja kuwa na kazi ya kufanya uharibifu tu.
Kama leo hii unamwona shetani ni mharibifu, basi bado haujajua vizuri uharibifu wake upoje.
Tukisoma kitabu cha ufunuo, kama tunavyojua mara baada ya unyakuo wa kanisa kupita, kutafuata matukio ambayo hayaelezeki kwa namna ya kawaida. Tukiachana na yale mapigo ya vile vitasa 7 na ile siku ya Bwana mwenyewe ambayo jua hili litaondolewa, kutatangulia kwanza mapigo ya baragumu 7,..Sasa hatuwezi kuyachambua yote hapa, ikiwa utahitaji somo lake utuambia inbox tukutumie..
Lakini leo tutatazama, baragumu la tano, ambalo ndio kiini cha somo letu la Leo. Baragumu hilo litakapopigwa, biblia inatuambia, Shimo la kuzimu litafunguliwa na humo watatoka nzige wabaya sana..tusome;
Ufunuo 9:1 “Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu.
2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni.
3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi.
4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao.
5 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama kuumwa na nge, aumapo mwanadamu.
6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia.
7 Na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita, na juu ya vichwa vyao kama taji, mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu.
8 Nao walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
9 Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani.
10 Nao wana mikia kama ya nge, na miiba; na nguvu yao ya kuwadhuru wanadamu miezi mitano ilikuwa katika mikia yao.
11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni ABADONI, na kwa Kiyunani analo jina lake APOLIONI.
Sasa hapa biblia imetumia tu lugha ya mfano ili upate halisi ya jinsi mambo yatakavyokuwa.. Hapo anasema wakatoka nzige..Sasa hao sio nzige halisi bali hayo ni Mapepo (maroho) ambayo kwasasa yapo kifunguni..Kumbuka si idadi yote ya mapepo yafayanyayo kazi sasa, yapo mengine mengine yapo kifungoni, biblia inasema hivyo katika kitabu cha Yuda.
Sasa mapepo hayo Yamefananishwa na wale Nzige waharibifu wa mazao, na ulimwengu umefananishwa na shamba lenye mazao (Mathayo 13:38) Na kama unavyojua nzige wakipita mahali kwenye mazao ya kijani, kitendo cha masaa machache tu, hilo shamba linageuka na kuwa vijiti tu.. Ni tishio kubwa sana duniani hata sasa, fuatilia tu habari ya nzige wa jangwani walipopita Afrika Mashariki kipindi cha hivi karibu uone uharibifu wao ulivyokuwa tishio.
Sasa tunajuaje kama haya ni mapepo na si nzige halisi, ni kwasababu hayajapewa kudhuru nchi, bali wanadamu ambao hawana muhuri wa Mungu duniani. Kazi hiyo huwa inafanywa na shetani mwenyewe na malaika zake, Soma Ufunuo 7 utaona hao ambao watakuwa wameitiwa muhuri ni wakina nani. Lakini kama ikitokea unyakuo leo hii umekupita, ujue kuwa mambo hayo yatakukuta tu..
Mapepo haya yatakayoachiliwa kutoka kuzimu na moja kwa moja yatapokea oda kutoka kwa kiongozi wao mkuu shetani/Apolioni/Abadoni, kwa lengo la KUWAHARIBU wanadamu tu. Kama jinsi atakavyojulikana kwa jina hilo.
Mapepo haya yatawaingia watu, bila kizuizi chochote, mengine yatawafanya watu kuwa vichaa, na kuwatesa tu kama yalivyomtesa Yule bwana aliyekutana na Yesu kule makaburini, mengine yatawafanya watu wawe wakatili kupita kiasi, kuchukiana kitaongezeka mara nyingi zaidi, kugombana, kuumizana, na kuuana n.k. mengine yatawafanya watu wapate ajali lakini si za kuwaua, bali za kuwaumiza tu vibaya..
Mengine yatawaletea watu magonjwa yasiyo ya kawaida lakini hakuna kifo, kama vile wakati wa Ayubu, siku hiyo kama hukwenda kwenye unyakuo utakaa kwenye majivu ya kila namna kujipoza lakini wapi, utatamani kufa lakini kifo kitakukimbia, yaani kwa ufupi duniani kutakuwa na watu ambao si watu, maroho hayo yatafanya uharibifu usio kuwa wakawaida.
Mioyo ya wanadamu itaharibiwa kwa kiwango cha juu sana, na kama vile yanavyofananishwa na nzige maana yake ni kuwa mpaka hicho kipindi chao kiishe, watu watakuwa kama makapi tu, wamechoka sana..
Huo wakati ndugu yangu, si wa kuwepo, ukisikia hizi ni siku za mwisho, usidhani unyakuo ukishapita mambo yatakuwa kama unavyoyaona leo.. Ni Roho Mtakatifu ndani ya kanisa lake ndiye anayezuia hayo mambo kwasasa. Lakini kuna wakati utafika, ataondolewa, na akiondolewa anaondoka na kanisa lake takatifu (Ndio unyakuo wenyewe).Kitakachosalia duniani ni vilio tu na kusaga meno (Mathayo 25:30).
2Wathesalonike 2:5 “Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?
6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; LAKINI YUKO AZUIAYE SASA, HATA ATAKAPOONDOLEWA”.
Swali la kujiuliza, Je! Bado tunaudharau wokovu wa Yesu?.
Je! Bado tunaishi maisha ya kutokujali, mpaka haya mambo yote yatukute? Kama ndivyo ni heri tuyakabidhi maisha yetu kwa Bwana leo, ayaokoe. Vilevile tukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na Kwa jina la YESU KRISTO tupate ondoleo la dhambi zetu. Bwana wetu ni mwingi wa huruma, anatuonya mbele kabla ya mambo hayajatokea kwa ghafla. Hivyo mpokee Kristo leo na atakufanya kiumbe kipya, ulimwengu unapita na mambo yake yote, lakini Kristo na Neno lake wanadumu milele. Na yeye anatuambia itatufaidia nini kuupata ulimwengu mzima na kupata hasara za nafsi zetu?
Bwana atusaidie, Bwana atubariki sote.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Mavu ni nini?
Mavu ni wadudu jamii ya nyuki, kwa jina maarufu ni NYIGU. Maumbile yao ni makubwa zaidi ya nyuki wa kawaida, Na mauvimu yao ni kama tu yale ya nyuki..
Wametajwa mara kadha wa kadha katika biblia, na hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowaelezea;
Kutoka 23:27 “Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao.
28 NAMI NITAPELEKA MAVU MBELE YAKO, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako.
29 Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja; nchi isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua”.
Kumbukumbu 7:19 “uyakumbuke hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako; ndivyo atakavyowafanya Bwana, Mungu wako, mataifa yote unaowaogopa.
20 Tena Bwana, Mungu wako, ATAMPELEKA MAVU KATI YAO, hata hao watakaosalia, hao wajifichao, waangamie mbele zako.
21 Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho”.
Yoshua 24:11 “Nanyi mliuvuka Yordani, mkafika Yeriko; nao watu wa Yeriko wakapigana nanyi, Mwamori, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhiti, na Mgirgashi, na Mhivi, na Myebusi; nami nikawatia mikononi mwenu.
12 NIKATUMA MAVU MBELE YENU, waliowafukuza mbele yenu hao wafalme wawili wa Waamori, si kwa upanga wako, wala kwa upinde wako”.
Katika mistari hiyo tunaona Mungu alivyowatumia wadudu hawa mavu kama silaha ya kuwafukuza maadui wa Israeli. Kufunua kuwa wapo mavu wa rohoni, ambao Mungu huwa anawatuma kuwafukuza maadui wa watakatifu duniani sasa.
Na mavu wenyewe ni malaika wa Bwana, na maadui wa watakatifu ni majeshi ya mapepo.. Mtakatifu yeyote rohoni huwa analindwa na kundi la malaika wa Bwana, hivyo shetani na mapepoo yake hawezi kumgusa kwa namna yoyote.
Lakini ikiwa mtu yupo nje ya Kristo, ibilisi ni lazima awe na mamlaka juu ya mwili wako. Na mapepo pia ni lazima yatajiamulia kufanya chochote yapendacho ndani yako, kwasababu hawapo mavu wa kukulinda wewe.
Kama hujaokoka na unahitaji kuokoka leo, basi fungua hapa kwa ajili ya sala ya Toba, >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Kumbuka Ni kwa Yesu tu unaweza kuwa salama pengine pote unapotea.
Bwana akubariki.
Tazama na tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Neno beramu lina maana gani katika biblia?
Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)
MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU