Ushirikina na madhara yake, rohoni ni yapi?
Ushirikina ni kitendo cha kwenda kutafuta msaada wa kiroho au wa kimwili katika mamlaka ya giza. Nikisema mamlaka ya giza namaanisha kwa shetani na mapepo na majini yake yote yanayofanya kazi kupitia watu wanaoitwa waganga au wachawi.
Sasa unapoumwa, halafu badala ya kwenda kuwa Mungu upate msaada, wewe unakimbilia kwa waganga wa kienyeji ili upate msaada ya kiganga, hapo moja kwa moja tayari umeshashirikiana na mashetani katika ulimwengu wa roho.
Au unapopitia matatizo Fulani aidha ya kifamilia, au ya kikazi, au unahaja ya jambo Fulani pengine masomo, au ndoa, au cheo, halafu wewe moja kwa moja unakimbilia kwa mganga akusaidie kutatua tatizo lako, ujue kuwa tayari umeshaingizwa katika mtandao wa Mashetani.
Jambo ambalo wengi hawajui ni kuwa, walau kwa mtu wa kawaida yeyote, kunakuwa na ka-ulinzi Fulani kutoka kwa Mungu, ambacho anazaliwa nacho hicho kanamfanya shetani asiweze kujiamulia tu jambo lolote atakalo juu ya huyo mtu, vinginevyo ungekuwa shetani kashawamaliza watu wote duniani, kwa kuwaua, Ndio ni kweli ataweza baadhi lakini sio yote. Sasa pale mtu anapokwenda kwa shetani mwenyewe kumwomba msaada, maana yake ni kuwa anasaini naye mkataba rasmi kuwa kuanzia sasa, huy mtu ni wangu na naweza kufanya jambo lolote juu yake.
Haya ndio madhara ya moja kwa moja ya ushirikina.
Angalia vizuri utaona asilimia kubwa ya watu wanaoudhuria kwa waganga wanakuwa wanasumbuliwa na nguvu za giza, au wengine wanapata ulemavu Fulani ambao hapo kabla hawakuwa nao, au ugonjwa Fulani, ambao hauponi, hiyo yote ni kutokana na mtu kujishughulisha na ushirikina.
Kutokana na kuwa tayari umeshajihalalisha kwa shetani, basi shetani kazi yake kubwa iliyobakiwa nayo kwako ni kukuua,..Kwasababu ndio dhumuni lake hapa duniani, kuua biblia inasema hivyo…
Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake”.
Hata kama kitaonekana kukuletea matokeo mazuri kiasi gani mwanzoni, kumbuka hiyo ni gia tu ya shetani kukuvuta kwake, ili usimwache, lakini katika kipindi cha muda mrefu, hakitakufikisha popote, kama ulikuwa umekwenda kutafuta mali, hizo mali zitapotea tu baada ya kipindi Fulani, kama ulikuwa umekwenda kutafuta kazi, hiyo kama unaweza usiipate, na hata ukiipata haitadumu, utakuwa ni mtu ambaye anafanya jambo lakini baada ya muda mrefu haoni faida ya jambo hilo, au haoni maendeleo yoyote. Na mwisho wa siku unajikuta ni heri usingeenda.
Mithali 11:21 “Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu; Bali wazao wa wenye haki wataokoka”.
Ayubu 21:13 “Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula”.
Kumbuka pale unapokwenda kwa waganga, ni unaonyesha kuwa humuhitaji Roho Mtakatifu kukusaidia, na kazi ya Roho Mtakatifu ni kuwavuta watu kwa Mungu, na kuwapa macho ya rohoni, Hivyo unapojihusisha na ushirikina na uchawi, ni kuwa unapoteza huo uwezo, na matokeo yake unakufa kiroho.. Hapo ndipo unaanza kufanya hata yale mambo ambayo mwanadamu wa kawaida hawezi kufanya,..Hayo unaweza usiyaone leo, lakini kwa jinsi siku zitakavyozidi kwenda mabadiliko hayo utayaona, kwasababu nguvu za giza wakati huo zitakuwa zinakutawala.
2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.
Washirikina wote, wachawi wote, biblia inasema sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Ukifa leo na upo katika hali hiyo , basi ni moto wa milele unakuongoja.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Sasa kwanini hayo yote yakukute?
Lakini Habari njema ni kuwa, hata kama umeingia huko, bado unayo nafasi ya kutengenezwa upya. Na anayeweza kufanya hivyo, si mwingine zaidi ya YESU KRISTO tu peke yake..Huyo ndiye aliyetiwa mafuta na Mungu, ili kuwatoa watu katika vifungo vya giza, mwingine yeyote hawezi….
Isaya 61:1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.
Hivyo kama ulishaingia humo, au bado hujaingia, lakini Kristo bado hayupo ndani yako, basi leo hii fanya uamuzi huo, wa kumkaribisha ndani yako ayaokoe maisha yako moja kwa moja, haijalishi wewe ni muislamu, Yesu anawaokoa wote, wanaomkimbilia yeye kwa moyo wa dhati.
Akikuweka huru, amekuweka huru kweli kweli, haachi hata alama ya uovu ndani yako, akikusamehe amekusamehe kweli kweli, kana kwamba hukuwahi kumkosea, kwa lolote. Atakufungua kutoka katika malango hayo ya mauti ya ibilisi yaliyokufunga, na kukuletea katika ufalme wa wana wa Mungu. Roho Mtakatifu akiingia ndani yako, hakuna pepo lolote litakaloweza kukaa ndani yako, Ukimkaribisha leo hii atakufanya huru, na kuna amani itaingia ndani mwako, ambayo utashangaa imetoka wapi..Huyo ndio Yesu mwokozi.
Hivyo kama upo tayari leo hii kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuacha, na kusema kuanzia sasa namfuata Yesu, sitaki ushirikina, sitaki dhambi, Namfanya Yesu kuwa kiongozi wa maisha yangu basi uamuzi huo ni mzuri na wa busara, basi, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala fupi ya Toba..>>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ubarikiwe sana.
Mada Nyinginezo:
NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?
EPUKA MUHURI WA SHETANI
JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.
JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUTOKA NJE YA MWILI WAKE?.
MAONO YA NABII AMOSI.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Isaya 24:3 “Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo.
4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.
5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele.
6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.
Nabii Isaya alipotabiri juu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo na bikira (Isaya 7:14), miaka 700 kabla ya Masihi kuja duniani, wapo watu pengine walioona kuwa hizo ni hadithi tu za kufikirikika… Alipotabiri tena juu ya mateso yake yatakayoompata (Isaya 53), nazo pia zikaonekana pengine ni habari tu, lakini wakati ulipofika, hayo yote kutimia kwa ufasaha wote, ndipo wakajua kuwa Neno la Mungu huwa halipiti.
Isaya huyo huyo aliyetabiri ujio wa Kristo kwa uvuvio wa Roho, ni huyu huyu alioonyeshwa pia hatma ya huu ulimwengu utakavyokuja kuwa siku za mwisho, na habari zake kaziandika sehemu nyingi sana kwenye kitabu hicho chenye sura 66, alionyeshwa jinsi hii dunia itakavyokwenda kuwa utupu, na kuharibiwa kabisa, jinsi jua litakavyotiwa giza, jinsi watu watakavyoadimika kama dhahabu duniani, na kibaya zaidi alionyeshwa fedha ya mtu wakati huo haitafanya kazi yoyote, umaarufu wa mtu utakuwa hauna maana, biashara za mtu zitakuwa ni kama takatakata, elimu ya mtu haitafanya kazi..tajiri na maskini wote watakuwa wakiomboleza sawa.
Na nyakati zenyewe ndio hizi tunazoishi mimi na wewe, kila mtu analijua hilo, hata ukimuuliza mtoto mdogo atakuambia, hizi ni nyakati za mwisho, watu wengi wanaposikia maneno haya wanapuuzia wakidhani hichi ni kama kile kipindi cha mitume..Ndugu hichi sio kipindi cha mitume.. Fuatilia mambo yanayoendelea duniani hata kupitia mitandao ndipo utakapojua kuwa tunaishi nyakati nyingine.
Bwana Yesu alisema hivi..
“Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;
33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.
34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia” (Mathayo 24:32).
Sasa kama wewe ni msomaji wa Biblia utajua kuwa Mtini unafananishwa na Taifa la Israeli (Yeremia 24), na wakati ule Israeli ilikuwa bado haijachipua (yaani haijawa taifa), ilipitia miaka zaidi ya 2,500 tangu wachukuliwe utumwani Babiloni, na ulipofika mwaka 1948, Israeli ikachipuka tena na kuwa taifa kwa mara ya kwanza,..Na tunajua kabisa agenda ya Mungu ya wokovu itamalizia tena na Israeli pale Yerusalemu.
Hivyo tangu huo wakati Bwana alisema kizazi hiko, (yaani kilichoshuhudia Israeli kuchupuka tena), hakitapita mpaka hayo yote, kutimia,..Mambo yote aliyoyazungumzia katika Mathayo 24, hadi kurudi kwa pili kwake,..Na kizazi huwa hakizidigi miaka 120, sasa piga hesabu hapo, tunaishi katika wakati gani.. (Hatujui siku wala saa lakini tunayajua majira).
Sikuzote, kiwango chako cha maarifa kuhusu Mungu, ndio kinachoelezea maisha ya kiroho unayoishi sasa hivi, kama jicho lako bado halioni kuwa tunaishi katika majira ya unyakuo, na kwamba huu ndio ule wakati ambapo watu watadhanishia mbona ni amani, na salama, na kumbe ule uharibifu unakuja kwa ghafla (1Wathesalonike 5:3)..Kama ilivyokuja Corona kwa ghafulani pasipo ulimwengu kujiandaa…Ndicho kitakachoitokea dunia kipindi sio kirefu.
Sijui kama hilo unalijua ndugu yangu, kanisa hili linaitwa Laodikia, (Sio dhehebu linaloitwa Laodikia! Hapana!..Bali ni hali ya kanisa kwa ujumla inayofananishwa na Kanisa la Laodikia la Nyakati za kwanza, kasome Ufunuo 3:14), na ndio kanisa la mwisho la 7, na hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hili, niambie ni dalili ipi ambayo haijatimia Yesu aliyoirodhesha kwenye Mathayo 24.
Internet imeweza kurahisisha mambo, siku hizi haihitaji mtu aende tena kwenye mikutano ya Injili asikie mahubiri, pale pale alipo hata kama ni kijijini akiwa chumbani mwake Injili inamfikia, utasema Injili haijahubiriwa dunia nzima leo?..
Shetani anataka watu waendelee kufikiria hivyo hivyo, kwamba bado sana, anataka watu waangalie upepo wa dunia unavyokwenda, lakini wasiangalie biblia inasema nini kuhusu siku hizi. Usipokuwa mvivu kusoma biblia ndipo utakapojua ni kwa jinsi gani tunaishi katika nyakati za hatari kushinda zote ambazo zilishawahi kupita katika historia.
Hivyo huu ni wakati wa kuamka usingizini..
Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza”.
Kama bado hujaokoka, au umeokoka lakini bado mguu mmoja nje mwingine ndani, Embu anza, kuyaangalia upya maisha yako ya rohoni ndugu, Je! Yesu amekuokoa kweli kweli? Kama sio, basi huu ndio wakati, na sio kesho, unachopaswa kufanya ni kuamua kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha na kutozifanya tena, na kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 3:38,8:16 na 10:48 Upate ondoleo la dhambi zako.(Maagizo hayo ni muhimu sana!). Na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.
Na kuanzia hapo, anza kuishi maisha ya kama mtu unayemngojea Bwana Yesu kwasababu nyakati hizi, sio za kubembeelezewa wokovu tena, ni kubutuka haraka na kuishindania Imani.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME
Watapigana nawe lakini hawatakushinda maana yake ni nini?
Yeremia 1:18 “Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma, na kuta za shaba, juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii.
19 Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe”.
Haya ni maneno ambayo alipewa Yeremia baada ya kuitwa na Mungu katika huduma. Lakini kwa hofu ya labda atakapokwenda kuwaeleza watu juu ya hukumu za Mungu, watakasirika na kumletea madhara ya ghafla labda watampiga mawe, hapo ndipo hapo Mungu akamuhakikishia kuwa ni kweli watakuja kupigana na yeye, lakini hawatamshinda, kwasababu yeye yupo pamoja naye.
Hata sasa adui hawezi kuja kupigana na mtu kama huna huduma ya Mungu mkononi mwake, mstari huu unapendwa kutamkwa na watu wengi kirahisi rahisi hata watu ambao wapo katika dhambi, wanajidanganya wakisema..
watashindana lakini hawatakushinda
Huo ni uongo, shetani hashindani na watu waovu,hata mara moja, kwasababu tayari alishawashinda siku nyingi. Hivyo ukijiona unapitia vita visivyokuwa na maana angali wewe ni mwenye dhambi ujue hayo sio mapambano.
Lakini ili Neno hili liwe na nguvu ndani yako, ni sharti kwanza, uokoke, umkabidhi Yesu maisha yako kweli kweli, kisha uwe na kazi ya kufanya katika injili yake, ndipo hapo hata shetani akinyanyuka na majeshi yake yote kutaka kukuangusha wewe ni sawa na kazi bure, kwasababu Mungu yupo pamoja na wewe daima.
Wakati huo hata ulimwengu mzima uungane vipi kutaka kukupindua usisonge mbele, watakuwa ni kama wanapoteza Muda kwasababu Mungu yupo upande wako.
Hivyo kama upo tayari leo kuokoka, ili maneno haya yawe na nguvu kwako, basi uamuzi huo ni wa busara, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Shalom.
Mada Nyinginezo
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.
Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu
KWANINI TUNAOMBA KWA JINA LA YESU?
NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI.
YEREMIA
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe!.
Karibu tujifunze Biblia.
Ndege tunazozipanda zinazoruka angani, hazijaundwa na mtu mmoja, kuna jopo kubwa sana la watu wamechangia maarifa katika kuiunda ile.. Utaona aliyegundua injini ya ndege ni mwingine, aliyegundua mfumo wa hewa ndani ya ndege ni mwingine, aliyebuni umbile na mwonekano wa ndege ni mwingine, aliyegundua sayansi ya kuifanya iruke ni mwingine, aliyegundua mfumo wa umeme ndani ya ndege ni mwingine, aliyegundua Mafuta ya ndege ni mwingine, aliyegundua kona ya ndege ni mwingine, aliyebuni matairi ya ndege ni mwingine n.k.
Sasa hao wote kila mmoja akiandika kitabu chake kidogo cha maelezo kuhusu mchango wake huo na vitabu hivyo vikakusanywa Pamoja bila shaka tunaweza kujikuta tuna kitabu kimoja kikubwa kama Biblia au hata Zaidi ya biblia, kilichojaa elimu kuhusu ndege. Maana yake ni kwamba mtu atakayejifunza hicho na kukielewa anaweza naye pia kutengeneza ndege yake.
Hivyo basi kama ilikuwa ni mpango wa Mungu kwamba wanadamu siku moja waruke angani, waende mbali sana kule juu Zaidi ya Tai..kumbe mpango wake haukuwa wa kumpa mtu mmoja maarifa hayo, bali aligawanya ujuzi huo kwa watu tofauti tofauti wanaojulikana kama wanasayansi..ambao katika hao kila mmoja alipochangia ujuzi wake na uvumbuzi wake ndipo kitkapoumbwa kitu kinachoitwa Ndege.
Kama ulikuwa ni mpango wa Mungu siku moja tusafiri kutoka bara moja hadi lingine kwa muda mfupi kwa kutumia ndege, na tena kama ulikuwa ni mpango wa Mungu siku moja turuke mbali sana Zaidi ya mawingi hata kuufikia mwezi kwa kutumia roketi…Basi pia upo mpango mwingine wa Mungu ulio mkubwa Zaidi ya huo, ambao utatufanya tupae Zaidi ya mawingu na mwezi na Zaidi ya nyota… Na huo si mwingine Zaidi ya ule wa kutupeleka mbinguni yeye alipo.
Na kama vile maarifa ya uvumbuzi wa kifaa kinachoitwa ndege au roketi, yalivyogawanyika katikati ya watu tofauti tofauti, vivyo hivyo maarifa ya kwenda mbinguni wamefunuliwa Mitume na Manabii mbalimbali wa kwenye biblia…Wakina Yeremia, Danieli, Musa, Ezekieli,…Wakina Petro, Paulo, Yohana n.k Hao kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu kila mmoja kaandika siri za ufalme wa Mbinguni kwa jinsi alivyojaliwa…ambazo sisi kama wakristo, tunajifunza leo katika kitabu kinachoitwa biblia, na kama tukifuzu kukielewa vyema basi tunaweza kupaa juu Zaidi ya yale mawingu. Tunaweza kutengeneza roketi na kuingia ndani yake na kuruka Zaidi ya yale mawingu, na ndege yetu hiyo au Roketi ni YESU KRISTO.
Yesu ndiye NJIA, KWELI na UZIMA…Mtu hawezi kufika kwa Baba mbinguni isipokuwa kwa Njia yake yeye (Soma Yohana 14:6).
Teknolojia inahubiri injili, ukiona wakati tunaoishi inawezekana kusafiri hewani, basi jua kuna safari kubwa kuliko zote inakaribia. Lakini hayo yote hayaji pasipo maarifa.
Ndugu dada/kaka usiache kusomana kujifunza kamwe biblia, Hakuna sehemu yoyote utaweza kupata maarifa ya kumjua Yesu nje ya biblia. Usiposoma biblia kwa kujifunza utachukuliwa na kila aina ya upepo wa uongo.
Usipende kusubiria tu kufundishwa biblia, Jifunze kuisoma mwenyewe!.. Hata mwanafunzi anayefanikiwa masomoni ni yule kwanza anayependa kujisomea mwenyewe…Na anapokutana na maswali magumu ndipo anapokwenda kuuliza kwa mwalimu wake!..Lakini mwanafunzi anayependa kufundishwa tu! Na wala hana muda wa kujisomea yeye mwenyewe..kamwe hawezi kufanya vizuri..Na ndivyo hivyo hata sisi, Mungu anataka tuisome biblia wenyewe!.
Kumbuka pia hajayarekodi maneno yake kwa njia ya Audio, kayaweka kwenye kitabu…Ukiona kitu kimewekwa kwenye kitabu maana yake anayekisoma anahitaji kuketi chini mahali pasipo na usumbufu, akiwa na kalamu yake na daftari..Biblia hatuisomi kama gazeti, tunajifunza na ndivyo Roho Mtakatifu anataka tuwe hivyo ili aweze kutufunulia siri zake..
Je unataka kwenda mbinguni?..Mimi nataka sijui wewe?..kama wewe nawe unataka basi Ni lazima tuifahamu biblia sana.
Bwana akubariki
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.
ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.
MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.
USIRUHUSU MUNGU AWEKE UADUI KATI YAKO NA WATU WAKO.
Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?
WAMWENDEA YESU KWA KUSAFIWA lyrics (Are you washed in the Blood?)
Wimbo huu uliandikwa na ndugu mmoja aliyeitwa Elisha Hoffman mwaka 1878, huko Ohio Marekani. Baada ya kuhitimu katika chuo cha biblia alisimikwa na kuwa mchungaji na kutumika kwa miaka mingi katika huduma hiyo, katika maisha yake yote ya huduma alifanikiwa kuandika nyimbo za kikristo zaidi ya 2000. Na huu “Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,
” Ulikuwa ni mmojawapo.
Wimbo huu umechukia maudhui yake kutoka katika sehemu nyingi za biblia ikiwemo;
Ufunuo 7:14 “Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe. Akaniambia, Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo”.
Wamwendea Yesu kwa kusafiwa.
****
Wamwendea Yesu kwa kusafiwa, |
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo? |
Je, neema yake umemwagiwa? |
Umeoshwa kwa damu ya kondoo? |
Kuoshwa, kwa damu, |
Itutakasayo ya kondoo; |
Ziwe safi nguo nyeupe mno; |
Umeoshwa kwa damu ya kondoo? |
Wamwandama daima Mkombozi, |
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo? |
Yako kwa Msulubiwa makazi, |
Umeoshwa kwa damu ya kondoo? |
Kuoshwa, kwa damu, |
Itutakasayo ya kondoo; |
Ziwe safi nguo nyeupe mno; |
Umeoshwa kwa damu ya kondoo? |
Atakapokuja Bwana-arusi, |
Uwe safi kwa damu ya kondoo! |
Yafae kwenda mbinguni mavazi, |
Yafuliwe kwa damu ya kondoo. |
Kuoshwa, kwa damu, |
Itutakasayo ya kondoo; |
Ziwe safi nguo nyeupe mno; |
Umeoshwa kwa damu ya kondoo? |
Yatupwe yalipo na takataka, |
Na uoshwe kwa damu ya kondoo, |
Huoni kijito chatiririka, |
Na uoshwe kwa damu ya kondoo? |
Kuoshwa, kwa damu, |
Itutakasayo ya kondoo; |
Ziwe safi nguo nyeupe mno; |
Umeoshwa kwa damu ya kondoo? |
****
Je na wewe uimbapo wimbo huu, maisha yako kweli yameshwa kwa damu ya mwana-kondoo (Yesu Kristo), Je unajua kuwa hukumu haikwepeki kwako ikiwa bado upon je ya Kristo. Hivyo kama hujatubu ni heri ufanye hivyo sasa, Bwana akusafishe uwe safi.
Shalom.
Tazama historia ya tenzi nyingine chini.
Mada Nyinginezo:
NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics
YESU KWETU NI RAFIKI
USINIPITE MWOKOZI Lyrics
UNYAKUO.
EPUKA MUHURI WA SHETANI
Kuota upo makaburini kuna maanisha nini kibiblia?
Makaburini sikuzote ni mahali wanapolazwa wafu, ikiwa unaota ndoto hii mara kwa mara upo makaburini ni ishara kuwa hali yako ya rohoni ni mfu. Upo mfano mmoja katika biblia wa mtu ambaye makao yake yalikuwa ni makaburini tu maisha yake yote haondoki pale.. Na biblia inatoa sababu kwamba ni nguvu za giza za mapepo zilikuwa zimemfunga..Na mapepo yale yalikuwa hayana lengo lingine zaidi ya kumuua..
Utasema umejuaje hilo? Tumejua hilo pale tulipoona baada ya kukemewa na Yesu, yalimpotoka na kuwaingia wale nguruwe, na moja kwa moja yale mapepo yakawakimbiza wale nguruwe kwenye maji kuwaangamiza..Hiyo yote ni kuonyesha kuwa lengo lao lilikuwa kuua tu na si kingine..Embu tusome kidogo..
Marko 5 :1-15
“1 Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.
2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;
3 makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo;
4 kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda.
5 Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe.
6 Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia;
7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese.
8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu.
9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi.
10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.
11 Na hapo milimani palikuwa na kundi kubwa la nguruwe, wakilisha.
12 Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao.
13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; nalo kundi lote likatelemka kwa kasi gengeni, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini.
14 Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea.
15 Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mwenye pepo, ameketi, amevaa nguo, ana akili zake, naye ndiye aliyekuwa na lile jeshi; wakaogopa”.
Unaona, Vivyo hivyo ikiwa unaota upo makaburini ni ishara kuwa hali yako ya kiroho ni mbaya sana, Lakini habari njema ni kuwa YESU Yule Yule wa zamani ndio huyo huyo wa leo.
Siwezi jua maisha yako upo katika hali gani sasahivi kiroho, pengine upo katika vifungo vya dhambi, au vyovyote vile, lakini Nataka nikuambie ni Yesu pekee tu, ndiye anayeweza kukupa raha maishani mwako, haijalishi wewe ni muislamu au nani, ni Yesu peke yake ndio anayeweza kukupa tumaini la maisha mema, ya hapa duniani na mbinguni.
Yeye (Bwana Yesu) mwenyewe alisema..
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”;
Unachopaswa kufanya ikiwa unahitaji kumkaribisha Yesu leo maishani mwako, akutengeneze upya, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako, Kumbuka sio hilo tu, yapo na mengine usiyoyajua wewe, Yesu anataka kuyarekebisha katika maisha yako, ni wewe tu kuufungua moyo wako,. Hivyo kama upo tayari leo kutubu, dhambi zako kwa kumaanisha kabisa, na kusema kuanzia leo nitamfuata Yesu, basi ni uhakika kuwa leo leo, atakuja ndani yako na kukuokoa, na utaanza kuona mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yako ya rohoni na mwilini..
Ikiwa upo tayari sasa kufanya hivyo basi, na kuanza safari mpya ya wokovu, basi fungua hapa, kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo
BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.
Bawabu (kwa kiingereza -Doorkeeper/Porter) ni nani katika biblia?
Bawabu maana yake ni msimamzi wa mlangoni, anayefunga na kufungua, na anayeruhusu na kutoruhusu mtu au vitu kuingia, Hawa wanakuwa hususani katika mageti ya kuingilia miji mikubwa na kwenye majumba ya kifalme na mahekalu,
2Samweli 18:26 Kisha huyo mlinzi akaona mtu mwingine anapiga mbio; mlinzi akamwita bawabu, akasema, Angalia, mtu mwingine anakuja mbio peke yake. Mfalme akasema, Huyu naye analeta habari.
Soma pia 2Wafalme 7:10,11
1Nyakati 9:23 “Basi watu hao na wana wao walikuwa na usimamizi wa malango ya nyumba ya Bwana, yaani, nyumba ya maskani, kwa zamu….
27 Nao wakalala kandokando nyumbani mwa Mungu, kwa kuwa ulinzi wake ulikuwa juu yao, nayo ilikuwa kazi yao kuyafungua malango asubuhi baada ya asubuhi.”.
Kazi hii ni kazi iliyokuwa inaonekana kama nyonge kuliko kazi zote kwenye utumishi wa Majumbani au kwenye ulinzi, hata sasa ndivyo zinavyoonekana..
Lakini Daudi alisema..
Zaburi 84:10 “Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu”.
Daudi alitumia kazi yenye cheo cha chini kabisa, katika jumba kubwa akasema kama na kwa Mungu ipo hivyo, basi angependelea walau apate hata kazi hiyo ndogo tu, maadamu ni ya Mungu, kuliko kupata cheo kikubwa na kibali katika mambo ya kidunia.
Akasema tena siku moja nyuani kwa Bwana ni bora kuliko siku elfu penginepo..
Alijua faida ya kazi ya Mungu, hata kama ni ndogo kiasi gani, alijua akipoteza siku moja kuitenda kazi ya Mungu ni sawa zaidi ya siku elfu kujisumbua na shughuli nyingine za kidunia..Firikia siku elfu ni karibia na miaka 3, Hivyo miaka 3 yako wewe kwenye masumbufu yako ni siku moja kwa mtu anayedeki choo cha kanisa.
Hivyo na wewe jiulize kazi yako ni nini kwenye nyumba ya Mungu? Mchango wako wa kusambaza kazi ya Mungu ni ipi? Nguvu zako za kifedha unazimalizia wapi ndugug? Au kwako kazi ya Mungu haina faida yoyote..
Daudi anasema ni heri “Ni heri niwe bawabu nyumbani mwa Mungu..”
Shalom.
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara katika email yako au Whatsapp yako basi tutumie ujumbe kwenye namba hii :+255 789001312
Mada Nyinginezo:
Bwana alimaanisha nini kusema JIKANE mwenyewe?(Mathayo 6:24)
JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?
Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?
Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?
MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.
Behewa kwa jina lingine ni UA, ni eneo la wazi lililokuwa limezungushiwa fensi mbele ya Hema ya kukutania , kwa ajili ya makuhani kutoa sadaka za kuteketezwa, na kufanya shughuli za kikuhani tazama picha juu..
Lakini baadaye Hekalu lilipokuja kutengenezwa na Sulemani pale Yerusalemu, eneo la behewa/Ua lilizungushiwa ukuta, na pakawa na behewa kuu mbili, 1) ya ndani 2) na ya nje, ili ya ndani ikabakia kuwa ya makuhani tu, kufanya mambo ya upatanisho na sadaka za kuteketezwa, Na ile ya nje ikabakia kuwa ya Wayahudi wote kukutanika kuabudu..Tazama picha chini..
Lakini pia behewa, kwenye biblia haikumaanisha tu ni lazima iwe mbele ya hema ya kukutania au mbele ya Hekalu la Mungu, biblia inayonyesha pia, zilikuwa pia kwenye majumba ya kifalme na ya kikuhani.
1Wafalme 7:1 “Naye Sulemani alikuwa katika kuijenga nyumba yake mwenyewe miaka kumi na mitatu, akaimaliza nyumba yake yote….11 Na juu kulikuwa na mawe ya thamani, mawe ya kuchongwa, sawasawa na cheo, na mierezi.
12 Na behewa kubwa pande zote ilikuwa na safu tatu za mawe ya kuchongwa, na safu moja ya mihimili ya mierezi; mfano wa behewa ya ndani ya nyumba ya Bwana, na ukumbi wa nyumba”.
Mathayo 16:3 “Wakati ule wakuu wa makuhani, na wazee wa watu, wakakusanyika katika behewa ya Kuhani Mkuu, jina lake Kayafa”;
Lakini pia katika kitabu cha ufunuo tunasoma, kuwa wakati wa mwisho, behewa/ua iliyo nje ya hekalu ambalo litakuja kujengwa na Wayahudi pale Yerusalemu siku za mwisho, litamilikiwa na watu wa mataifa kwa muda wa miezi 42..
Ufunuo 11:1 “Nikapewa mwanzi kama fimbo; na mmoja akaniambia, Inuka, ukalipime hekalu la Mungu, na madhabahu, na hao wasujuduo humo.
2 Na behewa iliyo nje ya hekalu uiache nje wala usiipime, kwa maana Mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili”.
Ili kufahamu habari kamili, sababu na maana yake rohoni ya mambo hayo fungua vichwa vingine vya masomo tulivyovirodhesha chini.
Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye namba hizi: +255789001312/ +255693036618
Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo
Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?
NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA
Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?
Kuna wakati ulifika Nabii Nahumu alifunuliwa juu ya hatma ya mji mmoja ulioitwa Ninawi, Mji huu ndio uliokuwa mji mkuu waTaifa la Ashuru, ulikuwa mji wa kwanza kwa ukubwa kuliko mji yote iliyokuwa ulimwengu kwa wakati ule. Baadaye ndio ikaja kutokea miji mwingine ulioitwa Babeli ..Sasa katika mambo aliyoongozwa Nabii Nahumu kuandika ni pamoja na uvumilivu wa hasira ya Mungu, pamoja na ukali wa hasira ya Mungu. Maneno hayo utayaona mwanzoni kabisa mwa kitabu cha Nahumu..
Nahumu 1:1 “Ufunuo juu ya Ninawi. Kitabu cha maono aliyoyaona Nahumu….
2 Bwana ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; Bwana hujilipiza kisasi, NAYE NI MWINGI WA HASIRA; Bwana hujilipiza kisasi juu ya adui zake, huwawekea adui zake akiba ya hasira.
3 BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, ana uweza mwingi….”
Unaona, sasa unaweza ukajiuliza ni kwanini Mungu azungumze maneno hayo mawili kwa wakati mmoja?
Utakumbuka kuwa mji huu wa Ninawi ndio ule mji ambao Nabii Yona alitumwa kwenda kuwahubiria juu ya dhambi zao kwamba watubu..Kama tunavyoijua ile habari, watu wale walisikia injili ya Yona, na walipotubu Mungu aliwarehemu japokuwa walikuwa sio wakamilifu ipasavyo.. hiyo ilimfanya mpaka Yona amkasirikie Mungu kwanini hajawaangamiza wale watu waovu..Ndipo Mungu akamwambia Yona maneno yafuatayo;
Yona 4:11 “na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi ya mia na ishirini elfu, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufugwa wengi sana?”
Unaona huruma za Mungu jinsi zilivyokuwa nyingi?.. Japokuwa walikuwa ni waabudu miungu, wapagani, lakini Mungu aliwahurumia tu pale walipotubu dhambi zao na kugeuka…Lakini tunavyozidi kusoma biblia tunaona, mambo hayakuwa hivyo siku zote ulifika wakati mji huo wa Ninawi ulirudia mambo yale yale ya kale, uovu ukaendelea kama ulivyokuwa pale mwanzo kipindi Yona anatumwa, wakasahau kuwa walinusurika kuwa jivu mfano wa Sodoma na Gomora.
Matokeo yake ndio tunakuja kuona Nabii Nahumu akitokea na kutoa unabii juu ya mwisho wa Taifa hilo..Pengine wakati Nahumu anatoa unabii huu waliona kama ni utani tu, kwamba watatubu tu kama kipindi kile cha Yona?..Wakawa wanasema tunajua Mungu siku zote si mwepesi wa hasira, Mungu ni wa rehema, anaghahiri mabaya..Hata hivyo hawezi kuliangamiza Taifa kubwa kama hili duniani (Ashuru) na mji wetu huu Ninawi ulio msaada wa mataifa mengi ulimwenguni.
Ndivyo walivyodhania, wakapumbazwa, wakajisahau kabisa, tena na jinsi walivyoona wamefanikiwa kuwachukua wayahudi utumwani, (yale makabila 10), ndio wakadhani kuwa Mungu amewapendelea..
Lakini Nabii Nahumu akatoa unabii juu ya mji huo..akisema.
Nahumu 3:7 “Hata itakuwa, wote wakutazamao watakukimbia, wakisema, Ninawi umeharibika; ni nani atakayeuhurumia? Nikutafutie wapi wafariji”?
Hayo maneno aliyoyasema nabii Nahumu yalikuja kutimia kama yalivyo, ni kwa vile tu, biblia haiwezi kuandika kila kitu, na kila historia, kama ingekuwa ni hivyo vitabu visingetosha duniani vya biblia. Lakini historia ipo wazi kabisa inaonyesha, ulipofika mwaka wa 612 KK, Wababiloni pamoja na wamedi waliunganisha nguvu, na kuizunguka Ninawi mji mkuu wa Ashuru, na kuuteka na kuungamiza, na hapo ndipo ikawa mwisho wa Taifa linaloitwa ashuru na mji wa Ninawi mpaka leo hii tunavyozungumza ni miaka zaidi ya 2,500, ni vipande vya mawe tu vimesimama pale kaskazini mwa Iraq. Na taifa la Babeli ndipo lilipopatia nguvu hapo, ambalo nalo baadaye lilikuja kuangamizwa hivyo hivyo.
Nahumu 3:19 “Jeraha yako haipunguziki; jeraha yako ni nzito sana; wote wasikiao habari zako wapiga makofi juu yako; kwa maana ni nani ambaye uovu wako haukupita juu yake daima”?
Biblia inasema Ninawi ni mji uliokuwa umekaa pasipo kufiri, upo upo tu, ukidhani wenyewe ndio wenyewe, ulipokuwa unashinda vita vingi, na unafanikiwa kuchukua mateka mataifa mengi, lakini siku yao ilipofika, yalikuwa ni majuto yasiyoelezeka..
Sefania 2:13 “Naye atanyosha mkono wake juu ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza Ashuru; naye ataufanya Ninawi kuwa ukiwa, kuwa mahali pakavu kama jangwa…..
15 HUU NDIO MJI ULE WA FURAHA, ULIOKAA PASIPO KUFIKIRI, ULIOSEMA MOYONI MWAKE, MIMI NIKO, Wala hapana mwingine ila mimi. Jinsi ulivyokuwa ukiwa, Mahali pa kulala pa wanyama wa bara! Kila mtu apitaye atazomea, Na kutikisa mkono wake”.
Ezekieli 32:22 “Ashuru yuko huko, na watu wake wote jamii; makaburi yake yamzunguka; wote pia wameuawa, wameanguka kwa upanga”
Ni nini Bwana anataka tujue?
Hiyo ni kuonyesha kuwa japokuwa Mungu si mwepesi wa Hasira, lakini hasira yake inapofika kilele basi ni MWINGI WA HASIRA..yaani haipoi kwa haraka, inadumu milele kama sio kwa kipindi kirefu sana..
Na ndio maana leo hii watu wengi wanaposoma yale mapigo yaliyoandikwa kwenye kitabu cha ufunuo wanaona kama hayafikirikiki kwa akili za kibinadamu, ni kweli unaweza kudhani hivyo lakini ndugu yale mapigo unavyoyaona pale ndivyo yatakavyokuwa.. Ziwa la moto unavyolisikia ndivyo lilivyo. Ukienda kule, hutatamani hata adui yako afike huko kwa mateso yaliyo kule yasiyoelezeka.. “Mungu si mwepesi wa hasira, lakini ni mwingi wa hasira”
Kama leo unalikataa Neno lake, na unaona hakuna chochote kinachotokea au kitakachoweza kutokea juu yako, pengine Mungu amekuambia utubu mara nyingi, lakini unafanya hivyo leo, kesho unarudia mambo yale yale ya kidunia.. Upo wakati utafananishwa na Ninawi..Utakatwa na kupotea moja kwa moja, wakati huo ukifika hata uombeje, hata ulieje, hakuna rehema tena juu yako.
Mambo haya sio uongo!..yaliwatokea watu wa Ninawi kama yalivyo..kasome katika Historia baada ya kukataa maonyo, na pia yaliwatokea wana wa Israeli vile vile kwa kukataa maonyo, na hata kusababisha Mungu kukataa kuwasamehe. Soma mistari ifuatayo utathibitisha..
2Nyakati 36: 15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake”.
Mathayo 3:10 “Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.
Kama hujampokea Yesu, fanya hivyo sasa..
Bwana akubariki.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Ni vizuri kufahamu kwanza maana ya uwanda, Uwanda ni sehemu iliyowazi iliyonyooka. Hivyo uwanda wa Dura ni sawa na kusema eneo la Dura lililo wazi.
Eneo hilo lilikuwepo Babeli na ndilo Nebukadneza mfalme alilichagua kuwa sehemu ya sanamu yake ya dhahabu aliyoitengeneza kwa ajili ya watu wa ulimwengu mzima kuisujudia. Eneo hilo la uwanda wa dura lilikuwa zuri kwa sanamu kuonekana vizuri na watu wengi kukusanyika.
Danieli 3:1 “Nebukadreza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita; akaisimamisha katika uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli.
2 Ndipo Nebukadreza akatuma watu kuwakusanya maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, ili wahudhurie wakati wa kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha”.
Je! unafahamu ile sanamu inafunua nini siku hizi za mwisho?
Je! unajua chapa ya mnyama ndio itakuja kwa namna hiyo? Ili kufahamu hayo kwa upana fungua vichwa vya masomo tulivyoviorodhesha chini.
Mada Nyinginezo:
DANIELI: Mlango wa 3
UFUNUO: Mlango wa 13
CHUKIZO LA UHARIBIFU
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?