Behewa ni nini?

 Behewa ni nini?

Behewa kwa jina lingine ni UA, ni eneo la wazi lililokuwa limezungushiwa fensi mbele ya Hema ya kukutania , kwa ajili ya makuhani kutoa sadaka za kuteketezwa, na kufanya shughuli za kikuhani tazama picha juu..

Lakini  baadaye Hekalu lilipokuja kutengenezwa na Sulemani pale Yerusalemu, eneo la behewa/Ua lilizungushiwa ukuta, na pakawa na behewa kuu mbili, 1) ya ndani 2) na ya nje, ili ya ndani ikabakia kuwa ya makuhani tu, kufanya mambo ya upatanisho na sadaka za kuteketezwa, Na ile ya nje ikabakia kuwa ya Wayahudi  wote kukutanika kuabudu..Tazama picha chini..

hekalu la sulemani

Lakini pia behewa, kwenye biblia haikumaanisha tu ni lazima iwe mbele ya hema ya kukutania au mbele ya Hekalu la Mungu, biblia inayonyesha pia, zilikuwa pia kwenye majumba ya kifalme na ya kikuhani.

1Wafalme 7:1 “Naye Sulemani alikuwa katika kuijenga nyumba yake mwenyewe miaka kumi na mitatu, akaimaliza nyumba yake yote….11 Na juu kulikuwa na mawe ya thamani, mawe ya kuchongwa, sawasawa na cheo, na mierezi.

12 Na behewa kubwa pande zote ilikuwa na safu tatu za mawe ya kuchongwa, na safu moja ya mihimili ya mierezi; mfano wa behewa ya ndani ya nyumba ya Bwana, na ukumbi wa nyumba”.

Mathayo 16:3 “Wakati ule wakuu wa makuhani, na wazee wa watu, wakakusanyika katika behewa ya Kuhani Mkuu, jina lake Kayafa”;

Lakini pia katika kitabu cha ufunuo tunasoma, kuwa wakati wa mwisho, behewa/ua iliyo nje ya hekalu ambalo litakuja kujengwa na Wayahudi pale Yerusalemu siku za mwisho, litamilikiwa na watu wa mataifa kwa muda wa miezi 42..

Ufunuo 11:1 “Nikapewa mwanzi kama fimbo; na mmoja akaniambia, Inuka, ukalipime hekalu la Mungu, na madhabahu, na hao wasujuduo humo.

2 Na behewa iliyo nje ya hekalu uiache nje wala usiipime, kwa maana Mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili”.

Ili kufahamu habari kamili, sababu na maana yake rohoni ya mambo hayo fungua vichwa vingine vya masomo tulivyovirodhesha chini.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye namba hizi: +255789001312/ +255693036618

  Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo

Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Wakoko Samuel
Wakoko Samuel
1 year ago

Amen. God bless you abundantly as you continue to bless us with the teachings

Peace Damian
Peace Damian
1 year ago

Amen sana…Mungu awabariki kwa mafundisho haya Yenye nguvu..

Anonymous
Anonymous
1 year ago

Amen sana …Mungu awabariki kwa mafundisho haya yenye Nguvu