Title 2020

Nini maana ya ‘Usimwekee mtu mikono kwa haraka’?

SWALI: Andiko hili lina maana gani?..1Timotheo 5: 22 “Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi”


JIBU: Maana ya awali ya mstari huo sio ile inayodhaniwa na wengi ya “Mtumishi wa Mungu, kumwekea mikono mtu mwenye tatizo fulani au ugonjwa fulani” na kumwombea…Hiyo sio maana ya msingi ya mstari huo…inaweza kuwa maana ya pili ya mstari huo …lakini maana ya msingi kabisa ya mstari huo ni “kuwekewa mikono kwa ajili ya utumishi”.

Huu ni waraka ambao Mtume Paulo alimwandikia Timotheo ambaye alikuwa ni mtumishi wa Mungu…Paulo alimfundisha madaraka ya kuitumishi kwa uongozo wa Roho Mtakatifu, ambayo unaweza kuyasoma yote katika wakara huo (yaani kuanzia sura ya kwanza hadi ya mwisho). Na mojawapo ya madaraka aliyompa ni madaraka ya kuwawekea mikono watumishi wapya, wale ambao tayari karama zao zimeshaanza kuonekana katika kanisa hivyo wapo tayari kuifanya kazi ya ki-utumishi katika mwili wa Kristo..kama jinsi yeye alivyowekewa..

1Timotheo 4:14 “Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa KUWEKEWA MIKONO YA WAZEE”

Kwahiyo hapa Timotheo naye anaagizwa wakati wa kuwawekea mikono watumishi wapya (mfano..maaskofu wapya, wachungaji wapya wa makanisa, waalimu, au manabii) asiwe na haraka!…bali achukue muda kumsoma mtu yule, tabia yake, mwenendo wake, je kama ni kweli kaitwa, ama ni kweli ana nia ya Kristo, kama ni kweli amekidhi vigezo vyote vya kimaandiko..Ndipo amtie mikono na kumbariki.

Kwasababu wale waliotiwa mikono ni kama wamehalalishwa kuwa wamestahili kulitumikia kundi la Mungu, na hivyo watu wengi ni rahisi kuwaamini, kwahivyo endapo akiwekewa mikono mtu ambaye si sahihi, ambaye hana nia ya Kristo, ni mtu wa kidunia tu, anawaza fedha au ukubwa tu…na kundi lote likimwamini, basi ni rahisi kuleta uharibifu mkubwa sana katika kanisa…Ndio maana hapo juu Mtume Paulo anamwagiza Timotheo na kumwambia “asiwe mwepesi kumwekea mtu mikono kwa haraka”, maana yake achukue muda kumchunguza..

Na hata sasa makanisani inapaswa iwe hivyo hivyo..Kabla ya mtu kuwekewa mikono kuwa mchungaji, au askofu, au shemasi, au nabii, au mwalimu ni lazima awe ameshajaribiwa na kuhakikiwa vya kutosha ili asije akaliharibu kundi, vigezo vya uaskofu vinapatikana katika hiyo hiyo 1Timotheo

1Timotheo 3:1 “Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.

2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;

3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;

4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;

5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)

6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi

7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.”.

Hiyo ndio maana ya awali ya KUMWEKEA MTU MIKONO, iliyomaanishwa katika mstari huo…Maana ya pili ndio ile inayojulikana na wengi, ambayo ni ya kumfahamu mtu kwanza kabla ya kumwekea mikono kumwombea..

Wengi hususani watumishi mtu anapokuja ana tatizo fulani, au ugonjwa fulani ni wepesi kumwekea tu mikono pasipo kumjua mtu huyo kwa undani..ili tu mtu aonekane ni mtumishi wa Mungu…pasipo kujua ni hatari kufanya hivyo…Kwasababu unaweza kujikuta unalaani kilichobarikiwa au una bariki kilicholaaniwa.

Kwamfano mtu unaweza kukuta anafanya kazi ya madawa ya kulevya, au ujambazi, au ya ukahaba au uzaji pombe..na yeye anakuja kwako kuomba kazi zake ziende vizuri (mtu kama huyo alishawahi kunifuata mimi)..na wewe pasipo kufikiri, kwasababu kaja tu kutafuta msaada kutoka kwako, unamwekea mikono na kumbariki katika jina la Bwana…(hapo umebariki kilicholaaniwa.).

Badala yake ungepaswa umhoji kwanza shughuli anayoifanya, na kama akikiri ni ya madawa ya kulevya basi, unamhubiria kwanza atubu na kumpa Kristo Maisha yake, na kutafuta kazi nyingine ndipo umeombee baraka kwa Mungu wako na ndipo huyo mtu abarikiwe..

Wengine ni makahaba na hawajui kama katika ukahaba wao wanamkosea Mungu (nimewahi kukutana na kahaba ambaye katika ukahaba wake aliniambia anamwamini Mungu, na huwa Mungu anamleteaga wateja, na huwa anaiombeaga biashara yake mara kwa mara ili iende vizuri)..baada ya kumhubiria sana ndipo alipoelewa kwamba alikuwa anafanya makosa pasipo kujijua…Sasa mwanamke kama huyu, anapokwenda kanisani au kwa mtumishi ambapo hataulizwa maisha yake ni rahisi watu kuibariki kazi iliyo laaniwa na Mungu..Hivyo ni kuwa makini sana.

Na pia tumeonywa hapo! Tusizishiriki dhambi za watu wengine, unapomwekea mtu mikono kwa pupa ni rahisi kuzishiriki dhambi za yule mtu, kadhalika unaposhirikiana na watu waovu katika kanisa ambao wanajua kabisa mambo wanayoyafanya ni kinyume na maandiko lakini bado wanaendelea kuyafanya huko ni sawa na kuzishiriki dhambi zao..

Bwana atusaidie tuwe wakamilifu mbele zake daima.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

HAKI HAIMWACHI KUISHI.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

Rudi Nyumbani:

Print this post

PALE UNAPOKUWA NA SABABU ZA KUMLAUMU MTU, UFANYE NINI?

Ni mara chache sana inatokea mtu anakosana na mwingine bila sababu yoyote, (Hiyo mara nyingi huwa inatokea kutokana na wivu), Lakini kutokuelewana kwingi au kuchukiana na watu, au kutokusameheana, au kukosana na watu mara nyingi huwa kunatokana na sababu Fulani..Kwamfano utakuta mtu amemdhulumu mwenzake, tukio hilo linamfanya yule aliyedhulumiwa amchukie yule mdhulumuji, au mtu amemuua ndugu yake, hilo linamfanya ndugu ya mfiwa amchukie yule muuaji..Au pengine amemtukana, au amemdhalilisha kwa namna moja au nyingine, au amemsengenya, au amempiga n.k…Hizo zote ni “sababu” zinazoweza kumfanya mtu asimpende yule mwingine..

Zinaweza zikawa ni sababu za msingi kabisa ambazo hata ukifa mbele za Mungu, unaoujasiri wa kumwambia Mungu ni kwanini ninamlaumu mtu yule, ni kwasababu alikuwa ni muuaji, ni fisadi, ni mchawi n.k.

Lakini Je biblia inatufundisha nini tunapojikuta katika mazingira kama hayo?

Inasema..

Wakolosai 3:12 “Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,

13 mkichukuliana, na kusameheana, MTU AKIWA NA SABABU YA KUMLAUMU MWENZAKE; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

14 Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.

15 Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani”.

Soma tena huo mstari wa 13 Unasema.. “Mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake”.. unaweza ukawa na sababu zote za msingi za kumlaumu mzazi wako kwanini hakukupeleka shule wakati ulikuwa na uwezo, unazo sababu za msingi za kuwalaumu viongozi wako, au waalimu wako kwanini hawakuwajibika kutimiza wajibu wao.. Lakini biblia inasema…Kama Bwana alivyotusamehe sisi, vivyo hivyo na sisi tuwasamehe wao.

Mtu mwingine anaweza kusema mtu Fulani nilimsaidia hiki na kile, lakini baadaye alipokuwa hana shida, alianza kunizungumzia maneno mabaya kwa watu wengine akiniita mimi mchawi.. Hivyo maisha yangu kamwe sitakaa nimpende yule mtu, Ni kweli unazosababu zote za kufanya hivyo, kwa hali ya kibinadamu sababu zote zipo za kumwekea kinyongo..Lakini Mungu anatuambia Pamoja na sababu zetu, tunapaswa tuwasamehe kama vile Bwana alivyotusamehe sisi.

Tukijua kuwa Mungu naye anazosababu za kutosha za kutuhukumu na sisi, kwa mambo yote maovu tunayomtendea kila siku, lakini anatusamehe tu bure, Matusi tuliyokuwa tunatukana yalimtosha kutuhukumu na kututupa kuzimu, dhambi tulizozifanya zinatosha kumpa Mungu sababu za kutushusha Jehanum.

Na ndio maana anatuambia tena mahali pengine..

Luka 6:37 “…. msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa”.

Unaona? Zipo faida nyingi za kusamehe(kuachilia), na faida mojawapo ambayo ni kubwa, ni kwamba utasikia mzigo mzito umedondoka moyoni mwako, na utaona amani ya ajabu imemwagika ndani yako.Lakini ukibakia na vinyongo, ujue kuwa Mungu naye atakuwekea kinyongo.

Hatuna budi kujifunza hili kila wakati, kwasababu maisha ya humu ulimwenguni yamejaa makwazo ya kila namna, kama hutakutana nalo leo, basi utakutana nalo kesho.. Hivyo na sisi tukiruhu makwazo yatawale mioyo yetu, kwa kutokuwasamehe wale ambao wanatuudhi, au kutukera kwa makusudi, tujue kuwa tuna dalili kubwa ya kutoiona mbingu.

Hivyo tujifunze kusamehe, na kuachilia hata kama tunazo sababu zote za kufanya hivyo.

Mwisho kabisa soma kisa hiki na Bwana akubariki.

Mathayo 18:23 “Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.

32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake”.

Bwana akabariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

NGUVU YA MSAMAHA

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

 

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 4

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIPUNGUZE MAOMBI.

Katika Maisha usijaribu kufanya kosa la kupunguza maombi…Ni heri ukapunguza muda wa kufanya mambo mengine ambayo unaona ni ya muhimu lakini usipunguze kuomba hata kidogo!..Kama tayari ulishaanza kuwa muombaji, halafu ukaanza kupunguza unamtengenezea adui nafasi ya kufanya uharibifu mkubwa sana katika maisha yako.

Kuna siri moja Bwana aliwaambia wanafunzi wake kuhusu maombi.. alisema “KESHENI, MWOMBE, MSIJE MKAINGIA MAJARIBUNI; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu (Mathayo 26:41)”

Hilo Neno “msije mkaingia majaribuni” ni neno kubwa sana…Hivi unajua ni kwanini Bwana alisema “hata nywele zetu zote za kichwani zimehesabiwa (Mathayo 10:30 )?”….Ni kwasababu kuna kiumbe kingine ambacho kinatutafuta sana hata kwa vitu vidogo…na hicho si kingine zaidi ya ibilisi….wengi hawajui kuwa shetani hata baada ya kufa maiti yako bado ina thamani kwake..sasa si zaidi nywele zako?, si Zaidi mate yako?, si Zaidi vidole vyako, si Zaidi mikono yako?..naam vyote hivyo anavihitaji sana…Ndio maana biblia inasema hapo, hata nywele zetu zote zimehesabiwa (maana yake zinalindwa zisipotee hata moja wala zisitumike na adui).

Shetani akikukosa kukuua na ajali siku hiyo, atatafuta hata ujikate na kisu tu wakati unaosha vyombo, akikosa kukutoboa jicho siku hiyo atatafuta hata uchubuke tu!..akikukosa kukupatia ugonjwa fulani wa mauti kama HIV, atafanya juu chini siku hiyo angalau upate tu mafua yatakayokusumbua, na akikukosa kwenye mafua pia hataridhika atatafuta njia hata uchomwe na mwiba barabarani! Ili uumie tu!,…hivyo vile vitu vidogo unavyovidharau ambavyo unahisi shetani hawezi kujishuhulisha navyo, yeye kwake bado anavyo nafasi navyo.

Lakini mtu ukiwa mwombaji kila siku…kabla ya kulala au wakati wa asubuhi, au mchana upatapo nafasi nzuri ya utulivu…unampa shetani wakati mgumu wa kupata  nafasi katika Maisha yako. Lakini usipokuwa mwombaji matukio ya ajabu ajabu yatajifululiza katika Maisha yako ambayo hutajua hata chanzo chake ni nini?…kama ni mfanyakazi unaweza kujikuta unagombana kazini tu au unagombezwa!, au unafika huko jambo lile ambalo ulikuwa umelipanga liende vizuri halijaenda vizuri, umeamka mzima jioni unarudi ni mgonjwa wa kupindukia..na mambo kama hayo (hayo ni majaribu ya kimaisha)…sasa majaribu ya kiimani ndio hayo unajikuta umeingia katika mazingira ya kuikana Imani au kuisaliti…

Unakumbuka dakika chache baada ya Bwana Yesu kumwambia Petro na wenzake waamke wasali ili wasije wakaingia majaribuni, walipopuuzia ni nini kilifuata?…masaa kama matatu baadaye kabla hata jogoo hajawika na hata kabla ya usingizi wao kuisha waliamshwa na kikosi cha watu wenye marungu na mapanga…na moja kwa moja baadhi ya wanafunzi wakakimbia mpaka mwingine alikimbia uchi wakamwacha Bwana peke yake (hiyo tayari ni kuikana imani)..Na sio hilo tu!…Petro naye kwa kujifanya shujaa kwamba anaweza kushinda majaribu bila nguvu ya maombi, alipomfuata Bwana kule alipopelekwa yeye naye akaikana Imani, (alimkana Bwana mara tatu kwamba hamjui).

Na sisi ni hivyo hivyo, usipokuwa mwombaji…asubuhi utaamka na ujumbe wa watu wanaokutaka uwape rushwa ili jambo lako Fulani lifanikiwe….Lakini kama ukiwa mwombaji, mambo hayo Mungu anakuepusha nayo!..utaona yule ambaye angepaswa akuombe rushwa, unashangaa hata hakuombi na bado anakupa haki yako ile ile…

Ukiona umepunguza kuomba jua tayari umeanza kurudi nyuma kiimani…hiyo ni dalili ya kwanza, dalili ya pili ni kupunguza kusoma neno.

Maombi yanafananishwa na lile tukio la Nabii Musa, aliponyoosha mikono yake juu wakati wa vita…alipoionyoosha juu wana wa Israeli kule vitani walikuwa wanapata nguvu ya kuwapiga maadui zao na kuwashinda…lakini alipoishusha nguvu ziliwaondokea wana wa Israeli na kuhamia kwa adui zao na kuwashinda wana wa Israeli..Na sisi ni hivyo hivyo nguvu za Mungu zinashinda juu ya Maisha yetu dhidi ya nguvu za Adui endapo tu na sisi kila siku/kila wakati tutakuwa tumeinyanyua mikono na mioyo yetu juu kuomba…Hizo ni faida chache tu za maombi zipo nyingi hatuwezi kuwa na muda wa kuzichambua zote hapa.

Hivyo usiache kuomba kabisa!..na kumbuka ndugu kuomba sio sala ile ya kuombea chakula!..au sio ile sala la “Baba yetu”…Hiyo haitoshi…kiwango cha chini kabisa biblia imetuambia angalau lisaa limoja kwa siku, ukienda masaa 3 au 4 ni vizuri Zaidi…na pia maombi sio kwenda kuombewa na mtumishi Fulani wa Mungu au ndugu yako!!..Maombi ni wewe kama wewe kusimama mwenyewe kuomba kwa bidii!.

Kumbuka tena, shetani anashida na nywele zako, ana shida na Maisha yako na anashida na viungo vyote katika mwili wako, na sio hata kwa njia ya uchawi au kwa kuwatumia wachawi…anayo idadi kubwa ya mapepo kuliko wachawi..hivyo kazi zake nyingi anatumia mapepo yake kuzifanya hata zaidi  ya wachawi….asilimia kubwa sana ya watu wanasumbuliwa na mapepo wakidhani ni wachawi!

Hivyo ng’oa nanga leo anza safari ya maombi ya kina kila siku!..kama umerudi nyuma rudia desturi yako kabla mambo hayajazidi kuwa mabaya.

Kama hujampa Bwana Maisha yako!..hizi ni siku za mwisho, Kristo anakaribia kurudi…hivyo geuka leo mkabidhi Maisha yako naye atakusamehe.

Bwana akubariki na Bwana atubariki sote.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



Mada Nyinginezo:

HISTORIA YA ISRAELI.

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

UCHAWI WA BALAAMU.

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

Ayubu 26:6 “Kaburi li wazi mbele yake, Uharibifu nao hauna kifuniko”.

Kama tunavyojua mashimo mengi yanayochimbwa huwa yanawekwa mifuniko juu, ili kusudi kwamba ikitokea mtu mgeni akapita kwa njia ile iwe ni mchana au usiku kwa bahati mbaya asitumbukie,

Lakini biblia inatumbia kaburi la mauti lipo wazi sikuzote, na uharibifu hauna kifuniko..

Uharibifu kwa jina lingine ni kuzimu.. Akimaanisha kuwa kuzimu haina mfuniko wowote, mfano ikitokea umepita katika njia hiyo kwa namna yoyote, basi kutelezea humo na kuzama ni mara moja..haijui huyu ni mgeni, au ni mwenyeji au ni mtoto. Ukizama umezama!.

Na ndio maana leo hii mtu akifa katika dhambi, moja kwa moja atajikuta ghafla tu yupo kuzimu, (Ayubu 21:13). atajiuliza amefikaje fikaje huko. Lakini ndio hivyo tayari ameshafika huko mahali ambapo hatatoka tena milele,.atakachokuwa anasema huko ni Laiti ningejua, laiti ningefahamu, nisingefanya hiki au kile..

Biblia inatuambia..

Isaya 5:14 “Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo”.

Unaona? Unashuka kwa ghafla sana, tusitamani tufike huko. Kila inapoitwa leo, tumwombe Mungu vilevile tujitahidi kukaa mbali na dhambi kwa kadiri tuwezavyo.

Watu wote wanaochukuliwa katika maono na kupelekwa kule, na kuonyeshwa sehemu tu ya mambo yanayoendelea humo, huwa hawatamani kuhadithia, kwasababu wote wanaowaona humo, ni vilio vya majuto tu, wanatamani wapewe dakika hata moja warudi watengeneze mambo yao lakini haiwezekani tena..

Ayubu 7:9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, NI VIVYO HUYO ASHUKAYE KUZIMUNI HATAZUKA TENA KABISA.

10 Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena”.

Utatamani urudi duniani siku hiyo itashindikana…Mfano tu wa Lazaro na yule Tajiri…Yule tajiri aliomba akawahubiriwe ndugu zake ili wasifike mahali pale alipo pa mateso lakini ilishindikana..Na Watu wanaoshuka huko ni wengi sana wasiohesabikia. Hivyo mimi na wewe tulio hai, tuikwepe dhambi…

Tusipende kufuata mikumbo ya watu, kisa wanakwenda Disko na sisi tuende, kisa wanavaa nguo za kikahaba na sisi tuvae, kisa wanafanya uasherati na sisi tufanye..kisa wanatumia pombe na sisi tutumie ..Kamwe usiwaige hao..Kwasababu wanaoshuka huko ni wengi sana, na kuzimu haijai watu..(Mithali 27:20, Mithali 30:16)

Kumbuka hizi ni zile siku zilizotabiriwa za maasi kuongezeka. Kwahiyo usishangae kuona wimbi kubwa la watu wanaofanya dhambi hadharani bila hofu.

Zaidi macho yetu yaelekee mbinguni, kwani unyakuo upo karibu, Au hata kama hautakukuta wakati wako, basi tufahamu kuwa kifo nacho hakipo mbali, Hivyo ni wajibu wetu kujiimarisha na kujithibitisha kwamba tupo katika mstari wa Imani.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 2

MADHARA YA KUTOA MIMBA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

2Timotheo 3:6 Inazungumzia watu wanaowachukua wanawake wajinga mateka, Je! Mstari huu una maana gani?


JIBU: Ukianzia kusoma tokea mstari wa kwanza utaona pale Paulo anamwonya Timotheo juu ya baadhi ya tabia za ajabu ambazo zitaanza kujitokeza katika siku za mwisho, alimwambia..

2Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari…”

Ukiendelea kusoma utaona akizihorodhesha tabia zenyewe zitakazozuka..anasema watatokea watu wanaopenda fedha, watu wenye kiburi,wasio safi, wanaopenda anasa kuliko kumpenda Mungu..n.k. Lakini ukushuka mpaka mstari wa tano anasema tabia nyingine kuwa, nyakati hizo kutaibuka pia wimbi la watu wenye mfano wa utauwa, lakini wakizikana nguvu zake, na hapa ndipo pa hatari zaidi..Tusome..

2Timotheo 3:5 “wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.

6 Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;

7 wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli”.

Unaona hapo?

Na wanawake pia wanahusishwa na watu hawa wanatajwa kuwa wao ndio waathirika wakubwa wa wimbi hilo la hao watu wanaojifanya kuwa ni watu wa Mungu(wenye mfano wa utauwa) lakini nyuma yake hawana Habari na Mungu hata kidogo (ni vyombo vya ibilisi dhahiri).

Hapa ndipo wewe kama mwanamke unapaswa ujichunge sana, tupo katika nyakati za hatari, kwasababu shetani tangu Edeni alikuwa anaufahamu mlango mwepesi wa kuuingilia ni mwanamke na si mwanaume (1Timotheo 2:14).. Leo hii utaona watu wa aina hii, hifadhi yao imekuwa wanawake wengi.., tena biblia inatumia neno

“Wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi na waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi ”.

Ikiwa na maana kuwa wanawake hawa suala la wokovu kwao halina maana sana,(ni wajinga katika roho) wanachotafuta ni mambo ya mwilini tu, wabarikiwe kazi zao, wapewe waume, wapate fedha, wapigiwe maadui zao, na huku waendelee na mavazi yao ya nusu uchi barabarani, waendelee kuwasengenya majirani zao, waendelee kuzini, waendelee kuishi kidunia..

Hawataki kujishughulisha na mambo ya rohoni,(hawaupendi utakatifu hata kidogo!) wakiona tu nabii yule ni mtanashati, anachekesha, ana magari, ana majumba, ana wafuasi wengi bila kujiuliza mara mbili kwasababu tu kashajiita ni mtu wa Mungu wanaingiwa na tamaa wanakwenda kujiunganisha naye.

Hayo yote, ni mambo yaliyotabiriwa kuwa yatatokea katika siku za mwisho, na tunayaona sasa.. Na kibaya Zaidi wanawakaribisha kwenye majumba yao, wewe angalia utaliona hilo, ni mara chache sana utawaona kwenye nyumba zenye mchanganyiko wa wanaume, muda wote utawaona wanazunguka kwenye nyumba za wanawake tu, na wakigundua mwanamke huyo kaolewa hawataenda kwake au kama wakienda wataenda wakati mumewe hayupo!…(Na wanawachukua mateka kimwili na kiroho)

hiyo yote ni ili maandiko yatimie, kwamba siku za mwisho watatokea watu wa namna hiyo.

Na ndio maana mtume Yohana alipomwandika wakara yule MAMA Mteule, mtakatifu kuwa alimwonya asiwakaribishe watu kama hawa ambao wanakuja kwake lakini hawaleti mafundisho ya Kristo..

2Yohana 1:10 “Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo [ya Kristo/utakatifu], msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.

11 Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu”.

Hivyo wewe kama mwanamke, iga mfano wa huyo “Mama mteule” Ipende kweli. Na sisi wote kwa Pamoja vivyo hivyo tu tutafute utakatifu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

YONA: Mlango wa 4

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

Dalili ya kwanza ya uchanga mkubwa wa kiroho ni hofu ya wachawi…Ukijiona unaogopa wachawi, au “uchawi” huo ni uthibitisho wa kwanza kabisa kwamba wewe ni mchanga kiroho, na Neno la Mungu bado halijakaa ndani yako, haijalishi upo madhabahuni unahubiri kwa miaka mingapi! Bado ni mchanga.. Mtu anayeogopa wachawi au anayewatukuza mno wachawi hana tofauti ni kima anayeogopa kinyago cha mtu shambani, kinachomtishia asile mazao…

Uchawi ni sehemu ndogo sana ya vita vya mkristo!..Idara kubwa ya shetani sio “vitunguli na vibuyu”..Hiyo ni idara ndogo sana ya shetani, ambayo hata pasipo kujijua Mungu tayari anakulinda nayo pasipo hata wewe kujijua. Sasa kama wewe ni msomaji wa biblia hebu nionyeshe mahali popote ambapo Bwana Yesu alizungumzia habari za wachawi/uchawi..au mahali popote alipokuwa anawafundisha wanafunzi wake aliwaonya wajihadhari na wachawi???…

Idara kubwa na kuu ya shetani ni roho ya mpinga-Kristo ambayo hiyo inakwenda kinyume na Kristo…Na hiyo inatenda kazi ndani ya kanisa, na inatumia watumishi wa uongo wanaojigeuza na kuwa kama watumishi wa Mungu! Na inakaribiana sana na roho ya kweli. Ndio hiyo hata Bwana alikuwa anapambana nayo,(ndio ile iliyokuwa inafanya kazi ndani ya mafarisayo na masadukayo) na ndio Bwana aliwaonya sana mitume wajihadhari na hao…

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali”.

Idara hiyo iliwasumbua sana mitume walipokuwa wanahubiri injili, mpaka wengine kuuawa, ilihusika kuwaua wakristo Zaidi ya milioni 80 duniani kote kikatili tangu kipindi cha kanisa la kwanza, inaua rohoni inaua pia mwilini, ndio hiyo hiyo inazungumziwa sehemu kubwa kwenye kitabu cha Ufunuo. Na ndio hiyo itakayokuja kufanya kazi katika kipindi cha dhiki kuu.

Sasa tukirudi kwenye mada..je! Mnyama paka kulia usiku juu ya bati ni uchawi?..

Jibu ni La!..sio uchawi…ukisikia paka analia usiku nje sio uchawi!!!….Paka wanaolia usiku ni kutokana na sababu za mazaliano..(sauti zile wanazitoa ili kuvutia mazaliano)..Paka wa aina yeyote Yule wakati wa mazaliano ni lazima atoe hizo sauti, awe ni paka wa kahaba, awe wa kanisa, au wa mtumishi wa Mungu…ni lazima ikifika kipindi cha mazaliano atoe hizo sauti, na anaweza kutoa wakati wa mchana au wakati wa usiku…na sauti hizo ni lazima zifanane na sauti za watoto wachanga!!…kama hatatoa sauti zinazofanana na za watoto wachanga basi kuna kasoro katika huyo paka!..paka asiye na kasoro yoyote ni lazima atoe hiyo sauti.

Sasa kwanini wanatoa hizo sauti zinazofanana na watoto wachanga???…Ndivyo Mungu alivyowaumba!..kama tu sauti wanazotoa kanga, au mbuzi au kuku wanapofikia wakati wa mazaliano au wakati wa kutaga!!. Na paka macho yake usiku ni lazima yang’ae yanapopigwa na mwanga…Na paka wana tabia zinazofanana na chui..ni wepesi kupenya mahali hata kama ni padogo sana..na wanapotembea si rahisi kusikika, na ni wepesi wa kutoroka mahali kwa haraka, kufumba na kufumbua unaweza usiwaone mahali walipopotelea…ndivyo walivyoumbwa!..(ili sisi tumtukuze Mungu, kwa uumbaji wake), na paka wote tabia zao ni kama za chui kupenda kutembea usiku na sehemu zilizoinuka!..

Kwahiyo ni kawaida kutembea juu ya mabati na ukuta wakati wa usiku, na hata kukimbizana!..na wanatabia pia za kuingia ndani kwa mtu hata kama hawajakaribishwa, hivyo kama hujafunga mlango anaweza kuingia mpaka ndani na hata kuzalia huko…na wanatabia ya kuwa ving’ang’anizi (utamfukuza atarudi tena, na utarudia hivyo mara kwa mara), ndivyo walivyoumbwa!!

Na sio dhambi kufuga paka! wa rangi yeyote Yule (awe mweusi, mweupe, kahawia au yeyote yule), kama ndani una panya wengi!..wanafaa kwa shughuli hizo za kuwadhibiti…au kwa fahari/(kwa kupenda tu) sio dhambi kuwafuga…tena ni vizuri zaidi kama una mapenzi nao!

Na bundi na popo ni hivyo hivyo…wameumbwa kipekee na Mungu (hawatembei mchana bali usiku na vyakula vyao vinapatikana huko huko gizani). Hawa si wanyama wa kufuga ndio maana unawaona wapo kivyao vyao..

Sasa wengi wasiokuwa na maarifa wanakuwa na hofu wanapowaona wanyama hawa wanaonyesha tabia zao hizo za kipekee walizopewa na Mungu, ambazo hazionekani kwa wanyama wengine!…na kuishia kusema ni wachawi wamewatembelea…wanaposikia paka usiku wanalia batini kama watoto wachanga, wanakosa usingizi na kuamini wachawi wamewatembelea!..wanapoona popo wametoka mitini jioni na kutanda angani, wanakosa amani..wanapoona bundi kasimama anamacho kama ya mtu, nguvu zinawaishia kabisa!!…wanajua sasa ni wachawi wanafanya kazi zao!!….kumbe ni kukosa tu maarifa!. Mwisho wa siku wanaishia kuwaua hao viumbe wakidhani ndio wamemshinda shetani!..

Na hiyo inamfanya mkristo kupoteza muda mwingi, hata wiki nzima,au mwezi mzima, au miaka na miaka kupambana katika sala dhidi ya wanyama hao(akiamini kuna uchawi ndani yao)…paka kaonekana kaingia ndani hapo hapo, maombi ya kufunga mwezi mzima yanaanza!..maji ya upako yatakwenda kutafutwa mitaa yote!, kila mtumishi ataitwa!..mwisho wa siku ni hofu hofu kila mahali…kila mtu unayekutana naye unahisi ni mchawi!, nimewahi kusikia watu wanasema na kuamini mende na mijusi, wanatumika kiuchawi!..hivyo ukiona mende ndani kwako ni wachawi kuna nguvu za giza hapo!

Usikose maarifa ndugu, wala usipoteze muda wako kwa vitu visivyokuwa na maana…Ukisikia paka wanalia batini usiku, kama wanakukera toka nje wafukuze! Wataondoka, na muda huo ombea mambo mengine ya muhimu kama, familia yako, kanisa na huduma yako kama unayo, ombea na wengine..usianze kushindana kukemea wanyama hao ambao wapo katika ulimwengu wao..Ukiona kelele za kuku usizozielewa hebu nenda kaulize kwanza uzijue tabia za viumbe hao kabla ya kuchukua maamuzi yasiyokuwa na maarifa!, kama sauti za fisi a zinakukera usiku basi hama nenda maeneo ya mjini hutazisikia kamwe..

Ni hofu tu ambazo shetani anawajengea watu waaamini kwamba yeye ni mkuu kuliko Mungu…ili wamwogope yeye zaidi ya Mungu. Wewe kama ni mkristo, unapaswa uwe na ujasiri na Imani yako useme “wachawi hawana kitu kwangu” Kama vile Bwana alivyosema “shetani hana kitu kwangu”..Kisha endelea kuishi Maisha yako ya kawaida.

Bwana akubariki!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

JE! TUNAPASWA KUUAMINI UNABII WA SYLVIA BROWNE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI.

Isaya 66:15 “Maana Bwana atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.

16 Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; nao watakaouawa na Bwana watakuwa wengi’.

Bwana Yesu atakaporudi mara ya pili, yaani siku ile mbingu zitakapofunguka na kila jicho kumwona hatarudi tena kwa upole kama alivyokuja hapo mwanzo, biblia inatuambia atakuja na jina jipya..Siku hiyo hataitwa tena YESU, Jina linalomaanisha mwokozi, hapana kwasababu hatakuja tena kuokoa, bali atakuja na jina jipya ambalo kwasasa bado halijafunuliwa..

Jina hilo litakuwa ni la kifalme, la kimamlaka, lenye uweza na ukuu mwingi sana..Watu watakamwona siku hiyo duniani hatawaamini kuwa huyu ndiye Yule tuliyekuwa tunamsikia habari zake, akihubiriwa na watu dhaifu…Kwasababu hatakuwa vile tena..

Siku hiyo wale watakaomwona, hakuna atakayesaliwa na nguvu hata kidogo, kwasababu wataingiwa na hofu kubwa, wataomboleza kusivyokuwa kwa kawaida, na ndio maana tunapaswa tusiichezee hii neema kabisa, kwasababu haitakuwa hivi siku zote.

Mtu mmoja nilikuwa ninamweleza habari za hukumu ya mwisho, na jinsi watu waovu watakavyoangamizwa, akaniambia ninamhukumu…Nikamuuliza nimekuhukumu wapi?..Akanipa lile andiko la Yule mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, ambaye Yesu aliwaambia wale watu waliomleta kwake, kuwa asiyekuwa na dhambi awe wa kwanza kumtupia Yule mawe…Nikamwambia ni kweli mimi sitakutupia mawe lakini Kristo siku ile atakutupia mawe wewe..na utakufa, kama usipotubu sasa.

Najua unaweza kuuliza ni wapi Kristo anaua..

Soma hapa..

Ufunuo 2:22 “Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake;

23 NAMI NITAWAUA WATOTO WAKE KWA MAUTI. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake”.

Hayo ni maneno yaliyotoka katika kinywa cha Kristo mwenyewe!. ATAWAUA WAOVU..Na kama vile yale maandiko pale juu yanavyotuambia..watakaouliwa hawatakuwa wachache bali ni wengi sana..

Ndugu, kikombe cha ghadhabu ya Mungu kinakaribia kujaa, (kama hujui vizuri kasome kitabu cha Ufunuo 16) Unyakuo ukishapita yatakayofuata si mambo mazuri!, ni mambo mabaya ambayo laiti ungeonyeshwa leo, usingetamana hata adui yako awepo hicho kipindi, Kwasababu siku atakaposhuka, jua litazimwa lote, na nyota na mwezi vitaondoshwa, duniani kutakuwa giza tororo, kutakuwa na tetemeko kubwa ambalo halijawahi kutokea tangu dunia iumbwe, na baada ya yeye kushuka wale ambao watakuwa bado hai atawaua mara moja..Hakuna huruma!.

Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 NA UPANGA MKALI HUTOKA KINYWANI MWAKE ILI AWAPIGE MATAIFA KWA HUO. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA Mabwana………..

20 Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;

21 na wale waliosalia waliuawa kwa upanga wake yeye aliyeketi juu ya yule farasi, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.”.

Bado tu unayapenda maisha ya dhambi? Bado tu unazidi kutazama pornografia, unafanya uasherati, unakula rushwa, unakwenda Disko, unaiba, unatembea na waume/wake za watu?…

Usilisahau hili Neno.. “WATAKAUAWA NA BWANA WATAKUWA NI WENGI”

Ni heri tumkimbilie yeye maadamu bado anaokoa sasa, Kabla Bwana hajaondoka Mtume Yohana alikuwa anaegemea kifuani kwake alikuwa anadeka kama mtoto karibu na Bwana, lakini Yohana huyo huyo anamwona Bwana Yesu Yule Yule kwenye maono Patmo kama miale ya moto, anatisha sana mpaka anaanguka chini ya miguu yake kwa hofu…Hivyo wakati wa neema ukiisha, Kristo hatakuwa Yule tunayemjua sasa…hivyo Bwana atusaidie neema hii tuithamini sana.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNATEMBEA JUU YA MAJI.

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

MALEZI YA MTOTO MCHANGA.

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

NI WAKATI WA KUJIPIMA, WEWE KAMA MTUMISHI WA MUNGU!

Rudi Nyumbani:

Print this post

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

SWALI: Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako, mafuta ya upako au chumvi katika kufanya maombezi?


JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa kinachomponya mtu ni damu ya Yesu Pekee. Na ndani ya damu ya Yesu ndio kuna Jina la Yesu…Hivyo jina la Yesu linapotajwa ni tangazo maalumu la damu ya Yesu katika utendaji kazi wake, hivyo kila ugonjwa au tatizo kwa jina la Yesu linaondoka na kupotea kabisa!.

Kwahiyo haipaswi kwa vyovyote vile kufikiri au kuamini kwamba kitu kingine zaidi ya damu ya Yesu kinaweza kumponya mtu au kinaweza kuondoa matatizo ya mtu au kumbariki. Kuamini hivyo hakuna tofauti na kuabudu sanamu.

Sasa pamoja na hayo, Mungu ameruhusu uponyaji wa damu ya Yesu wakati mwingine ufuatane na maagizo Fulani…Kwamfano daktari anaweza kutoa dawa kwa mgonjwa wa ngozi na kutolea maagizo kwamba akameze vidonge hivi na maji ya kutosha..au akampa vidonge vingine na kumwambia akavitie kwenye maji kisha aogee, afanye hivyo mara tatu kwa siku tatu na huo ugonjwa huo wa ngozi utamwisha..Au anaweza asimpe kidonge chochote na badala yake akamchoma sindano tu na bado ukapona vile vile…Ni kwajinsi tu yeye atakavyopenda kuchagua njia iliyobora.

Na Roho Mtakatifu ni hivyo hivyo…katika suala la kumponya mtu, mara nyingine anaweza kuambatanisha na maagizo Fulani…aidha mtu atumie mafuta, au udongo kwa jinsi Roho Mtakatifu atakavyopenda…kama alivyofanya Bwana katika Yohana 9:6 (alimwongoza atumie tope la mate yake), au anaweza akampa mtu maelekezo atumie unga kama Elisha alivyofanya katika 2Wafalme 4:41, au chumvi kama alivyofanya Elisha katika 2Wafalme 2:21 au kutumia leso kama alivyofanya Paulo katika Matendo 19:11-12..au chochote kile…Lakini ni kulingana na uongozo wa Roho Mtakatifu…Na sio kama mtindo!..kama inavyofanyika leo na wengi wanaofahamika kama watumishi wa Mungu.

Leo hii kila tatizo linatatuliwa na chumvi wanazoziita chumvi za upako, au mafuta …hata mtu akiugua tu, suluhisho ni mafuta ya upako! Au maji ya upako!..kila kitu ni mafuta ya Upako na ni kitendo endelevu na kinachojirudia kila siku…Sasa hilo sio agizo la Roho Mtakatifu…kwasababu Roho Mtakatifu hana mtindo Fulani/staili Fulani ya kumponya mtu.

Kwasababu hata Bwana Yesu sio kila mahali watu walipomjia mwenye matatizo Fulani alikuwa anatema mate chini na kutengeneza tope na kuwapaka na kufunguliwa shida zao!…utaona alifanya hivyo mara moja tu! Na tena kuna jambo alikuwa anafundisha, Na hakuna sehemu nyingine yoyote alirudia kufanya hivyo, kuonyesha kuwa nyakati zote alikuwa anasubiria maagizo ya Roho Mtakatifu, na hakufanya agizo Fulani la Roho Mtakatifu kuwa kama mtindo.

Na sio yeye tu! Hata Elisha hakuwa na staili/mtindo wake maalumu, wala hata Mtume Paulo ambaye nguo zake na Leso yake kuna wakati ilitumika hata kuondoa mapepo(Matendo 19:12)…utaona kuwa haikuwa hivyo kila mara, na wala Paulo hakugeuza kuwa kama mtindo..kwamba kila aliyekutana naye alimtupia leso ili afunguliwe!..hutaona akizituma nguo zake korintho au Galatia watu wakafunguliwe wala hakuwahi kuhubiri hayo mambo… sehemu kubwa sana alikuwa anatumia jina la Yesu…na alikuwa anamuhubiri Kristo na si mavazi yake wala leso zake. Na mitume wengine wote wa Bwana Yesu ni hivyo hivyo…tunamsoma Mtume Petro kuna wakati hadi kivuli chake kilikuwa kikimpitia mtu mwenye ugonjwa, Yule mgonjwa anafunguliwa! (kasome Matendo 5:15). Lakini hutaona mahali popote Petro akiitumia hiyo kama ndio staili yake/mtindo wa kuwafanya watu wafunguliwe…bali utaona mara karibia zote alikuwa anatumia Jina la Yesu tu!..

Matendo 3:3 “Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka.

4 Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi.

5 Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao.

6 Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. KWA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETI, SIMAMA UENDE.

7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.

8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu”.

Hapo Petro hakutumia “kivuli” chake!…Bali jina kuu la YESU KRISTO!.

Sasa utauliza mbona kuna watu wanayatumia maji ya upako, au mafuta ya upako kama mtindo wao na wanafunguliwa?

Wengi wanaofunguliwa ni wale ambao ni wachanga kiimani, ambao ndio kwanza wamemjua Kristo, au wameingia kwenye imani ya kikristo, Hivyo Bwana anaruhusu wapokee miujiza yao kwa njia yoyote ile..ili wazidi kumsogelea Mungu katika hivyo vipindi vya awali, lakini baada ya kipindi Fulani kupita wakaujua ukweli, au kusikia injili kwa muda mrefu na kushupaza shingo, zinabadilika kwao kuwa ibada za sanamu, na havitawapii chochote zaidi ya kuzidi kuwaweka mbali na Mungu, na hata wakati mwingine kuingiliwa na mapepo, na kupoteza hata vile walivyo navyo kwasababu ni ibada za sanamu…wanatanga huko na huko kutafuta na kununua maji ya upako, chumvi ya upako…Na kwasababu wengi wao hawapendi kuzidi kumjua Mungu wanadanganyika!

Na manabii wengi wa uongo wamezuka sasa, katika siku hizi za mwisho kama ilivyotabiriwa…Mungu ameachilia nguvu ya upotevu kwa wale wote wanaoukataa ukweli…Na nguvu hiyo ya upotevu kaiweka ndani ya manabii wa uongo…Na lengo la nguvu hiyo ni ili watu wote wanaoukataa ukweli wazidi kudanganyika!…ili tofauti ya magugu na ngano ionekane kwaajili ya mavuno.(Mavuno hayawezi kuja bila magugu na ngano kujitenga kisawasawa!..)

2Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

11 Kwa hiyo Mungu AWALETEA NGUVU YA UPOTEVU, wauamini uongo;

12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”.

Hivyo ni wakati wa kuwa makini sana na kuwa macho, na kujihadhari na roho zidanganyazo!…Kama hujapewa maagizo yoyote na Roho Mtakatifu basi usikurupuke kutumia maji,chumvi, udongo, au chochote kile ni hatari sana kwa roho yako!…Tumia Jina la Yesu tu pekee linatosha…

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 693036618/ 0789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

BIRIKA LA SILOAMU.

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

Mtu astahiliye hofu ni yupi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

DAKIKA MOJA TU, INAKUFANYA UMWAMINI SHETANI?

Luka 4:5 “ Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu KWA DAKIKA MOJA.

6 Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo”.

Hilo ni moja ya jaribu shetani alilomletea Bwana kule jangwani..

Lakini jiulize ni kwa nini iwe kwa dakika moja?, kwanini amwonyeshe ndani ya muda mfupi kiasi hicho, kwani alikuwa na haraka gani? Chukulia mfano mtu aje na kukwambia nataka kukuonyesha plani ya mji wetu na shughuli zote zinazofanyika ndani yake kwenye CD..Ni wazi kuwa hawezi kumaliza kukuonyesha kila kitu kwa dakika moja, itachukua dakika nyingi sana kama sio masaa, lakini tunaona hapa kwa ibilisi iliwezekana..

Alifanikiwa kumuonyesha Bwana milki zote za ulimwenguni kwa kitendo cha dakika moja..Ni kwanini afanye hivyo? Sio kwamba alikuwa hawezi kumwonyesha milki zote kidogo kidogo, huo uwezo alikuwa nao lakini sikuzote ni desturi yake, kutompa nafasi mtu ya kutafakari vizuri kazi zake..

Hakutaka Bwana atafakari nyuma ya milki zile kuna nini? Bali alikuwa anamwonyesha haraka haraka, ule upande mzuri tu wa fahari hizo, ili kusudi kwamba Bwana achukue maamuzi ya haraka haraka ya kumsujudia bila hata kutafakari vema, ili awe amemshinda. Hakumwonyesha Bwana wagonjwa waliolala hoi mahospitalini waliokuwa wanahitaji msaada, hakumwonyesha watu waliofungwa kwa kuonewa, au wanaotumikishwa na nguvu za giza, hakumwonyesha maskini wa roho, wala mayatima ambao wazazi wao waliuawa na huyo huyo shetani, hakumwonyesha uchawi uliokithiri katika hiyo miji n.k ..yeye alimwonyesha tu mali, na fahari..Lakini hakumweza Bwana kwasababu pale alikutana na Mkuu wa Uzima mwenyewe ambaye anajua vyema kuzipambanua roho!.

Hii ni mbinu ambayo shetani anaitumia hata sasa kuwaangusha wengi katika dhambi..kwamfano akitaka leo kummaliza mtu na dhambi ya uasherati, mara moja atamletea katika mawazo yake uzuri wa kufanya lile jambo..Lakini hatamruhusu kutafakari ni nini kipo nyuma yake, na yeye bila kutafakari vyema, moja kwa moja ataingia humo, kuitenda, hajui kuwa nyuma yake kuna hata hatari hata ya kifo hata kupata ukimwi, nyuma yake kuna mimba zisizotarajiwa, nyuma yake kuna kupata aibu, na kibaya Zaidi kuliko vyote ni kuwa nyuma yake kuna laana itokayo kwa Mungu..

Au mwingine shetani anamletea mawazo ya kuwa Tajiri kwa dakika moja, atamwambia njoo utapata utajiri wa haraka, bila kufikiri vema kuwa akienda kule, atakutana na waganga wa kienyeji waliolaaniwa, hajui kuwa nyuma yake kuna kutoa kafara, kuna uchawi, kuna kutumikishwa, na mwisho wake ni kifo, na baada ya hapo ni ziwa la moto..au anakutana na kazi ya wizi au utapeli, pasipo kutafakari nyuma yake kuna kifo, au kifungo, mtu anaingia huko…..Sasa yeye kwasababu kaonyeshwa pesa tu za haraka haraka ambazo hazihitaji kuzihangaikia sana, anaingia humo na kupotelea humo..

Mwingine, anakutana tu na kazi Fulani ya ghafla, halafu baada ya hapo anashurutishwa akaifanye, lakini yeye badala achukue muda kumwomba Mungu na kuichunguza kazi ile, moja kwa moja atakwenda kuingia nayo mkataba na kuifanya kisa tu imemuahidia mshahara mzuri, hajui kuwa kazi ile ililetwa na shetani, ili kuharibu utaratibu wake aliokuwa nao wa kusali, wa kumtumikia Mungu, na kibaya Zaidi anakuja kugundua kazi yenyewe inafanya shughuli za kipepo kama uuzaji pombe, au bidhaa haramu na mambo mengine ya ajabu.

Mwingine atakuwa anatembea madukani, ghafla anakutana na simu ya mtu imejiegesha mahali ambapo haionekani, na saa hiyo hiyo shetani anaanza kumletea mawazo ya dakika moja ya wizi, kumwonyesha faida za simu ile akienda kuuza atapata laki kadhaa, ndani ya dakika chache baadaye..kisha atanunua hiki na kile.. Na yeye bila kuruhusu fikra zake kuwaza mbali anakwenda kuiiba, bila kujua nyuma yake, kuna kupigwa na watu, kuna kuchomwa moto, kuna kufungwa, na kibaya Zaidi kuna laana ya Mungu, kwamba hata kama hatakufa pale siku ya mwisho atakwenda motoni..

Mithali 13:11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”.

Mwingine kamwona mwanamke na hapo hapo kamtamani, bila kupata muda mrefu wa kumchunguza tabia zake, yeye wazo la dakika moja tu, anaingia humo, na ndio hapo baadaye anakuja kugundua alikuwa ni mke wa mtu aliyemwacha mume wake, au kahaba tu, na ghafla matatizo ndani ya nyumba yanaanza. Vivyo hivyo na mwanamke naye, shetani atampitishia dakika moja mwanaume mwenye fedha, na yeye bila kujitafakarisha anaingia moja kwa moja, kumbe ndio kaenda kuharibu Maisha yake moja kwa moja.

Na sehemu nyingine nyingi za Maisha ni vivyo hivyo..Shetani huwa anawaletea watu mawazo ya chap-chap ..Ya dakika moja tu yanayovutia lakini nyuma yake yana miaka mingi ya majuto.

Ndugu, tusiwe wateja wa shetani..biblia inasema..

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, TAMAA YA MWILI, NA TAMAA YA MACHO, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”.

Zingatia hilo, ni moja kati ya majaribu makuu 3 ya ibilisi aliyoyaona yanawazomba watu wengi kwake, na ndio maana akamchagulia na Bwana, hivyo hatashindwa kutuletea na sisi (mimi na wewe), hivyo tuwe makini sana na mambo ya humu ulimwenguni

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

MTAIFAHAMU KWELI NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuungama ni nini?

SWALI: Kuungama maana yake ni nini?

JIBU: Maana ya kuungama ni “kukiri jambo kwa wazi” kukubali….Kwamfano mtu anayetubu kwa kuzikiri dhambi zake kwa wazi kwamba yeye ni mwenye dhambi mbele za Mungu, mtu huyo ni “ameungama dhambi zake”

1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Mathayo 3:5 Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;

6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao”.

Kadhalika kuikiri imani mbele za watu ni “kuiungama imani”..na kuukiri uongo ni kuungama uongo!

Bwana wetu Yesu Kristo alipopelekwa mbele ya Pontio Pilato, na Pilato alipomwuliza je wewe ndiwe Kristo?..Alikiri (aliungama) wazi kuwa yeye ndiye!

Luka 23:3 “Pilato akamwuliza, akisema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu akamwambia, Wewe wasema”…..

Neno “wewe wasema” maana yake ni “kama ulivyosema”..Kwahiyo Kristo alikiri kwa wazi pasipo hofu mbele ya Pilato kwamba yeye ndiye Kristo!..Hivyo aliungawama Imani yake kwa wazi.

1Timotheo 6:13 “Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, ALIYEYAUNGAMA MAUNGAMO MAZURI yale mbele ya Pontio Pilato,

14 kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo”

Kadhalika na sisi kama hatujatubu mbele za Mungu…tunapaswa tuziungame dhambi zetu kwanza, (maana yake tuzikiri kwa dhati kwamba sisi ni wenye dhambi, tusipokiri na kukubali kwamba sisi ni wakosaji mbele zake kamwe hatuwezi kupata msamaha kutoka kwake!)..kisha tumwombe Mungu rehema naye atatusamehe…Na tukiishaziungaa dhambi zetu na kuipokea Imani kwa kumwamini mwanawe mpendwa Yesu Kristo tunapaswa kila siku TUUNGAME MAUNGAMO YA IMANI YETU!…maana yake tuikiri Imani ya kikristo kila mahali tuendapo, na popote pale tusimamishwapo pasipo hofu wala kujali ni nani yupo mbele yetu!..kama Bwana wetu Yesu alivyoungama..

1Timotheo 6:12 “Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele ulioitiwa, UKAUNGAMA MAUNGAMO MAZURI MBELE YA MASHAHIDI WENGI”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

YONA: Mlango wa 4

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post