Category Archive Home

 MAVUNO NI MENGI

Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.


Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Karibu tujikumbushe baadhi ya mambo muhimu katika safari ya Imani.

Tukiwa kama wakristo ni wajibu wetu kuifanya kazi ya Mungu, kulingana na karama tulizopewa. Faida ya kuifanya kazi ya Mungu ni kubwa kuliko kutoifanya kabisa. Kwa jinsi tunavyozidi kuukaribia ule mwisho wa dunia, kazi ya Mungu inazidi kurahisishwa Zaidi lakini inazidi kuongezeka kiwango.

Kwamfano mtu anaweza kupewa alime shamba lenye kichaka la hekari mbili, aanze kwa kuondoa nyasi na miti yote na kisha alilime kwa jembe la mkono, na baada ya hapo apande mbegu, na mwingine anaweza kupewa kazi ya kuvuna hekari 10.

Sasa huyo wa kwanza amepewa kazi ngumu lakini kwa hekari chache..lakini huyo wa mwisho amepewa kazi nyepesi tu! Ya kuvuna lakini hekari nyingi. Na ndio hivyo hivyo siku hizi za mwisho, kazi ya Mungu si ngumu kwasababu haihusishi  kulima, kupanda wala kumwagilia…bali inahusisha tu kuvuna!…Lakini hiyo haitoshi…mashamba ya mavuno ni mengi sana, hivyo inaifanya kazi iwe kubwa sana..

Bwana Yesu alisema…

Yohana 4:35  “  Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, INUENI MACHO YENU MYATAZAME MASHAMBA, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.

36  Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja.

37  Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine.

38  Mimi naliwatuma MYAVUNE YALE MSIYOYATAABIKIA; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao”

Anaendelea kwa kusema…

Mathayo 9:36  “Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.

37  Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, MAVUNO NI MENGI, LAKINI WATENDA KAZI NI WACHACHE.

38  Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake”.

Ndugu katika Kristo, zama hizi sio zama za kanisa la kwanza ambalo utakwenda mahali ambapo utakuta watu ambao hawajawahi kumsikia kabisa Yesu..(hao watu wapo ila ni wachache sana) asilimia kubwa ya watu tayari wameshawahi kumsikia Yesu mahali Fulani, wawe nii wakristo au wasio waKristo, tayari wameshawahi kumsikia Yesu..fanya utafiti mwenyewe, mfuate mtu yeyote muulize Je! Unamfahamu Yesu..utasikia jibu atakalokuambia..Hiyo ni kwasababu tayari wengine walishapanda na kutia maji, tayari yanao msingi Fulani ndani ya Maisha yao…kazi iliyobaki ni mavuno tu!.

Na kazi ya mavuno sio ngumu! Ni nyepesi sana isipokuwa ni kubwa sana!..Kwahiyo tunategemewa kufanya kazi sana kuliko watu wa kanisa la kwanza. Wengi wameshamjua Kristo tayari, lakini bado wapo mashambani (ulimwenguni) kazi inayohitajika ni  kuwatoa mashambani na kuwaingiza ghalani mwa Bwana, wakibaki huko mashambani wapo ngedere, wapo wezi kuiba, wapo ndege, wapo wadudu wanaoharibu mazao n.k..

Lakini wakiwekwa ghalani kwa Bwana watakuwa salama..mbali na wadudu na Wanyama, na  wezi…watakuwa wamefichwa mbali na kuhifadhiwa na kila aina ya uharibifu.

Ghalani mwa Bwana ni wapi?

Mtu aliyemtii Kristo na kuamua kuacha uovu na kumgeukia Yeye kikamilifu na kubatizwa, katika ulimwengu wa roho anakuwa tayari kashaingia ghalani mwa Mungu, kafichwa na Mungu…ataonekana kwa macho lakini katika roho hataonekana, uhai wake unakuwa umefichwa kama biblia inavyosema katika..

Wakolosai 3:3 “ Kwa maana mlikufa, NA UHAI WENU UMEFICHWA PAMOJA NA KRISTO KATIKA MUNGU. 4 Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu”.

Hivyo Ghala la Mungu linaanzia hapa hapa duniani!..Wokovu unaanzia hapa hapa duniani. Kama upotevu unaanzia hapa hapa duniani, na wokovu ni hivyo hivyo…Huwezi kumwona mtu ambaye anafanya uovu wa kupitiliza na kusema bado hajapotea kwamba atapotea akishakufa hapana!..katika uovu wake tayari kashapotea, labda ageuke tu! Lakini pale alipo tayari kashapotea!…hali kadhalika huwezi kusema mtu mwenye haki bado hajaokoka..na kwamba ataokoka akifika kule…huo ni uongo wa shetani…katika haki yake tayari kashaokoka!!

Wokovu unaanzia hapa hapa duniani…GHALA LA MUNGU LINAANZIA HAPA HAPA ULIMWENGUNI…Mavuno yanaingizwa ghalani hapa hapa ulimwenguni…mbingu ni mwendelezo wa ghala, ambalo tayari limeshaanzia kazi zake duniani.

Kwahiyo ni wajibu wetu kuitenda kazi ya Mungu…Tayari wameshamsikia Yesu akitajwa katika Maisha yao, pengine tangu utoto wao? Wamebakia tu kuwa wakristo-jina, wakristo wa-kidini tu lakini Yesu hayupo ndani ya mioyo yao….hivyo hatua iliyobaki ni kuwaeleza kwa maarifa yote umuhimu wa Yesu katika Maisha tofauti na walivyosikia huko nyuma. Jinsi Yesu anavyoweza kuwabadilisha watu mioyo.

Lakini likumbuke pia hili neno la Bwana “Mavuno ni mengi ila watenda kazi ni wachache”. Maana yake kazi bado ni kubwa sana…na hivyo ni wa kujitoa sisi na pia kumwomba Bwana anyanyue watenda kazi wengi duniani kote. Kipengele hicho cha maombi ni muhimu sana katika Maisha na kinapuuziwa na wengi…lakini ni kipengele cha muhimu sana cha kuomba Bwana apeleke watenda kazi. Na sisi pia kila mmoja wetu akisimama katika nafasi yake.

Bwana atusaidie na kutushika mkono, na Zaidi sana atubariki wote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

KAMA MHUBIRI NI WOKOVU UPI UNAUPELEKA KWA WATU?

UTAFIKA WAKATI WA WEWE KUACHWA NYIKANI.

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

BWANA WA MAJESHI.

Kwanini Mungu aitwe Bwana wa majeshi? Je! Ni kweli anayo majeshi au ni cheo tu amependa kujivika?

Watu wengi hatufahamu kuwa Mungu anayo majeshi yake…Ni kweli hili jina limekaa sana ulimini mwetu, lakini bado hatufahamu vizuri ni kiwango gani Mungu anajiita Bwana wa majeshi..Naamini siku tukilifahamu hilo vema basi tutaishi maisha yasiyo na woga na wasiwasi hata kidogo hapa ulimwenguni.

Kumbuka hajiiti Mungu wa “Jeshi” kana kwamba ni moja hapana bali anajiita Mungu wa “Majeshi” ikiwa na maana ni mengi.

Ni majeshi ambayo yaanzia mbinguni mpaka duniani. Na kama tunavyojua sikuzote majeshi kazi yake, kulinda usalama, kutunza amani, na kuupigania ufalme, kinyume na maadui zao.

Mungu alijitambulisha kama Bwana wa Majeshi, sio kwamba alitaka  sisi tumwogope, Hapana, bali alitaka sisi tujue nguvu aliyonayo katika kutupigania watu wake dhiki maadui zao (Shetani na mapepo yake). Embu Jaribu kutengeneza picha Mungu angejiita tu  majina haya, ingekuwaje?

  • Bwana wa Amani(Jehova-Shalom), au
  • Bwana mpaji wetu, (Yehova-yire), Au
  • Bwana atuponyaje(Yehova-Rafa), Au
  • Bwana atuonaye (Yehova-Shama) N.K.

Unadhani hiyo ingetosha tu?..Kwamfano tungekuwa tunapitia katika vita vikali tumezungukwa na maadui wa mwilini na rohoni, kilichobaki ni kufa na kupona, unadhani Bwana mpaji wetu(Yehova yire), tungemuhitaji wakati huo? Wakati unaona unakaribia kuchinjwa Je, utamwambia Mungu nipatie mali?..Jibu la, kinyume chake atamuita Bwana kwa nguvu  zote asimame mwenyewe akupiganie na kuwasambaratisha  maadui zako ili upone.

Hapo ndipo jina la BWANA WA MAJESHI linapoitwa (Yehova-Saboati)

Ilifika wakati Daudi alikuwa anakwenda kupigana na adui yake mkubwa Goliathi, moyoni alijua kabisa mtu kama huyu wa vita, haiwezekani kumshinda, Lakini alipogundua kuwa yupo Bwana wa Majeshi Mungu wa vita,karibu naye ndipo aliposimama kwa ujasiri na kwenda kupigana naye..tusome..

1Samweli 17:43 “Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.

44 Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni.

45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe KWA JINA LA BWANA WA MAJESHI, MUNGU WA MAJESHI ya Israeli uliowatukana.

46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.

47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu”.

Unaona hapo Daudi alimuita Bwana wa Majeshi, aje kumsaidia..

Ndugu fahamu kuwa, Unapokuwa mkristo, hupaswi kuwa woga wa kitu chochote, Inasikitisha kuona ni mkristo wa muda mrefu halafu bado anaogopa wachawi na washirikina, pamoja na mapepo na majini.

Shetani mwenyewe anawashaangaa, anapoona watu wa Bwana wa majeshi kama sisi, nasi tunamwogopa yeye..

Kuna wakati Elisha alikuwa anatembea na mtumishi wake Gehazi, wakafika mahali wakajikuta wamezungukwa na majeshi mengi ya maadui zao, yule mtumishi akawa anatetemeka na kuogopa sana..Lakini Elisha hakuogopa kwasababu alijua majeshi ya Mungu wa Israeli aliyo nayo ni mengi kuliko ya wale wengine..Bwana wa majeshi ndio nguvu yake.. Ndipo Elisha akamwomba Mungu amfungue macho alione hilo.

2Wafalme 6:17 “Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.

18 Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha.

19 Elisha akawaambia, Njia hii siyo, na mji huu sio, nifuateni mimi, nami nitawapeleka kwa mtu yule mnayemtafuta. Akawapeleka Samaria”.

Hivyo hata wewe ukiwa unapitia mahali ambapo, unaona vita vikali vipo mbele ya basi mwite Bwana wa Majeshi atakusaidia,..

Lakini ikiwa wewe bado upo nje ya wokovu, nataka nikuambie hata umwite vipi Mungu katika vita vyako hawezi kukusikia wala kukusaidia, kwasababu wewe sio wa ufalme wake. Wachawi watakutesa, mapepo yatakutesa, ibilisi atakutesa,.. Lakini ukitaka leo awe upande wako, basi ni sharti kwanza umpokee YESU KRISTO katika moyo wako. Akusemehe dhambi zako, ndipo pale utakapoliita jina la Bwana wa majeshi atakusikia na kukusaidia.

Ikiwa upo tayari Kumpa YESU leo  maisha yako basi bofya hapa, kwa Sala ya toba >>> SALA YA TOBA.

Pia yapo mafundisho mengi unahitaji kujua juu ya majeshi ya mbinguni(malaika) wanavyofanya kazi na sisi(tuliookoka), hivyo nakusihi fungua na masomo mengine hapa chini, ufahamu zaidi juu ya ulimwengu wa roho wa malaika wa Bwana na utendaji kazi wao.

Zaburi 24: 10 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Bwana wa majeshi, Yeye ndiye Mfalme wa utukufu.

Mungu akubariki.

Mada Nyinginezo:

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MASERAFI NI NANI?

Yapo makundi tofauti tofauti ya Malaika wa Mbinguni.  Wapo Maserafi ambao ndio tutakaowazungumzia leo, wapo Makerubi (ambao ndani yake ndio alikuwa shetani), wapo wenye uhai wanne, wapo wazee ishirini na nne.. na wapo Malaika wa vita ambao ndani yake ndio  wakina Mikaeli na wenzake.

Na katikati ya hayo makundi, yamegawanyika vipengele vingi!..wapo malaika wenye mbawa na wasio na mbawa, wapo wenye maumbo kama ya wanadamu lakini pia wapo wenye maumbo kama ya wanyama na ndege.

Kwa ufafanuzi kuhusu makundi hayo ya Malaika,  mwisho kabisa wa somo hili utaona LINK za masomo hayo, zifungue ili uweze kuzisoma.

Sasa Maserafi ni kundi la Malaika ambao kazi yao ni kumsifu na kumtukuza Mungu mbinguni, Wamekizunguka kiti cha enzi kwa maelfu yao, wakimsifu Mungu usiku na mchana. Maserafi wana mabawa sita kila mmoja. Mawili yanakifunika kichwa kufunua kuwa KUFUNUA MAMLAKA YA MUNGU, NA UTAWALA WA KIMUNGU. Kwamba Mungu ndiye kichwa cha mambo yote. Na pia wanafunika kichwa kwasababu wanaona hata hawastahili kumtazama Mungu, wala Mungu kuwatazama wao kwajinsi yeye Mungu alivyo mtakatifu sana.

Na pia hawaishii tu! Kufunika kichwa..bali wanafunika pia Miguu, kufunua jambo kufunua kuwa hawastahili hata Mungu aliye mtakatifu kuona miguu yao.

Na mabawa mawili yaliyosalia ni kwaajili ya kuruka (yaani kupaa).

Kundi hili la malaika tunaona limetajwa katika Kitabu cha Isaya.

Isaya 1: 1 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.

2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.

 3 Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi, dunia yote imejaa utukufu wake”.

Bwana aliwaumba malaika hawa kwa lengo hilo la kumsifu yeye na kuufunua utakatifu wake kwa viumbe vyake vyote…ndio maana katika sifa zao wanaanza na neno.. “Mtakatifu mtakatifu”.  

Na malaika hawa (maserafi) wanatufundisha na sisi jinsi ya kumsifu Mungu..Kwamba tuwapo mbele zake tujisitiri!..

Hebu tujifunze kitu hapa!..sio malaika wote wanaofunika vichwa mbele za Mungu…lakini kundi hili linafanya hivyo? kwanini?…Huoni pia katika kanisa kuna kundi la watu ambao ni lazima lifunike vichwa liwapo ibadani?..na sio tu kufunika kichwa bali hata kujisitiri mwili mzima ikiwemo na miguu.

1Wakorintho 11:5 “Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa”

Na ukiendelea kusoma mistari hiyo utaona suala la wanawake kufunika vichwa ibadani limehusishwa na “Malaika”..kasome 1Wakorintho 11:10.

Kwahiyo pia si vyema mwanamke kuingia kanisani bila kufunika kichwa wala kujisitiri mwili..Utakuta mwanamke anaingia ibadani kichwani kaweka wigi, chini kavaa kimini au suruali. Jiulize hapo unakwenda kumwabudu Mungu gani?..Maserafi wasio na dhambi wanajisitiri wewe uliye na dhambi inakupasaje?

Mwisho, Kumbuka Malaika yoyote yule sio wa kuabudiwa!..wala hatupaswi kuweka picha au sanamu ya malaika yoyote yule na kuisujudia, ni Mungu pekee ndiye anayestahili kuabudiwa na kusujudiwa.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MAKERUBI NI NINI?

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

Kuna Malaika wangapi?

Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?

Malaika wa maji ni yupi na Je kuna aina ngapi za malaika?

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

Mjumbe asiyekuwa na ujumbe:

Ukisoma katika biblia utakumbuka habari ile ya Daudi na mwanawe Absalomu, jinsi walivyoingia katika mapambano makali,.mpaka kuepelekea vita vizito kupiganwa kule msituni..Kama wengi wetu tunavyofahamu, katika vita vile Daudi hakuwepo bali alimtuma amiri jeshi wake mkuu aliyeitwa Yoabu, kupigana nao. Lakini kabla ya kuanza vita Daudi alimwagiza Yoabu, kuwa ahakikishe kijana hawamuui bali wanamleta mikononi mwake akiwa mzima.

Lakini Yoabu alipomkamata Absalomu, alimuua, na kisha akamtupa kwenye shimo refu sana. Na Israeli walipoona kiongozi wao Absalomu amekufa, vita vikaishia pale pale, watu wote wakatawanyika na kwenda makwao.

Sasa kilichokuwa kimebakia, ni kumpelekea Daudi taarifa za vita, Lakini ni nani wa kumpelekea Daudi Habari ya kifo cha mwanawe. Hapo ndipo wakatokea wajumbe wawili mmoja aliitwa, Ahimaasi, mwana wa Sadoki na mwingine, alikuwa ni mkushi.

Sasa huyu Ahimaasi, akamwomba Yoabu, akimbie ampelekee ujumbe Mfalme Daudi kuhusu vita, lakini Yoabu alimwambia, kwasasa wewe huwezi kupeleka ujumbe, na sababu ya kutopeleka ujumbe ni kwasababu zile sio Habari njema apelekazo..

Ndipo Yoabu akamwita kijana mwingine mkushi akamtuma badala yake akamwambia nenda ukamwambie mfalme uliyoyaona..

2Samweli 18:21 “Ndipo Yoabu akamwambia Mkushi mmoja, Nenda ukamwambie mfalme hayo uliyoyaona. Na huyo Mkushi akajiinamisha mbele ya Yoabu, akaenda zake mbio.”

Ndipo huyu mkushi akatii akaondoka mbio mara moja..Lakini yule Ahimaasi, alipoona mwenzake katumwa halafu yeye bado kabaki, akaendelea kumsisitiza Yoabu na yeye aende..Tusome.

2Samweli 18:22 “Ndipo Ahimaasi, mwana wa Sadoki, akamwambia Yoabu mara ya pili, Haidhuru, tafadhali nipe ruhusa, nipige mbio na mimi nyuma ya huyo Mkushi. Naye Yoabu akasema, Mbona wewe unataka kupiga mbio, mwanangu, kwa maana hutapata kitu kwa habari hizo unazopeleka?

23 Akasema, Haidhuru, nitapiga mbio. Akamwambia, Haya, piga mbio. Ndipo Ahimaasi akapiga mbio, akishika njia ya uwandani, akampita yule Mkushi”.

Hivyo wote wawili wakaanza safari, lakini tofauti ya mjumbe wa kwanza na yule wa pili ni kuwa yule mkushi, alikuwa na ujumbe wa kupeleka kwa yale aliyoyaona vitani jinsi Absalomu alivyouliwa, lakini yule mwingine hakuona chochote, alisikia tu..

Sasa biblia inatuambia yule wa pili alipiga mbio Zaidi ya yule wa kwanza na kufika kwa mfalme, (hatujui alipiga short-cut au vipi), lakini alifikia wa kwanza kuliko yule mwingine.

Akafika mpaka malangoni mwa mfalme, akaulizwa, umeleta ujumbe gani? Akasema, Mungu ashukuruwe kwa kuwa maadui zako wametawanyishwa.

Lakini Daudi alipomuuliza Habari za kijana? … sikiliza majibu yake.

2Samweli 18:29 “Mfalme akauliza, Je! Yule kijana, Absalomu, yu salama? Ahimaasi akajibu, Yoabu aliponituma mimi mtumishi wa mfalme, mimi mtumishi wako, NALIONA KISHINDO KIKUBWA, LAKINI SIKUJUA SABABU YAKE”.

Daudi aliposikia hivyo akamwambia simama pembeni, akamngojea yule mwingine afike.. Ndipo alipofika yule mwingine na kuulizwa..naye akajibu, “wote wainukao ili kukudhuru, na wawe kama alivyo yule kijana”(akimaanisha kuwa Absalomu Amekufa).

Ndipo Daudi aliposikia vile alienda kulia sana, akimwombolezea mwanawe..

NI NINI BWANA ANATAKA TUJIFUNZE?.

Kama haujafikiria, kuwa mhubiri, au mchungaji, au nabii au mwinjilisti au mtume, au mjumbe yoyote wa Mungu, kwa njia yoyote ile,iwe katika uimbaji, au uandishi n.k. ni vizuri kwanza ukafahamu na kuuelewa vizuri ni ujumbe gani unakabidhiwa kuupeleka..

Ujumbe/ Agizo kuu tulilopewa na Bwana Yesu kwa mtu yeyote anayetaka kuifanya kazi ya Mungu ni hili..

Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi;..”

Sasa jiulize, Je, katika kujibidiisha kwako kuwahubiria watu, Je! Lengo lako ni kuwafanya watu kuwa wanafunzi wa Kristo?, Je! Ni kuwafundisha kuyashika yale yote Yesu aliyotuamuru au mambo ya kidunia tu?..

Wengine wakiulizwa kwanini auhubiri injili kama ile ya mitume injjili kamilifu na ya utakatifu, watakwambia, mimi sikuitwa kuhubiri injili hiyo! Mimi nimeitwa kuwa mfariji tu!! ..Nataka nikuambie ndugu hapo ni sawa na unakimbia bure bila ujumbe wowote kama yule Ahimaasi. Kumbuka hapo kwenye Mathayo 28, agizo hilo lilipewa kwa watu wote kiujumla, hapo Bwana alikuwa hazungumzi na Petro peke yake, au Mathayo peke yake, au Filipo…alikuwa anazungumza na wote waliokuwepo pale Pamoja na sisi wote tunaosoma.

Ikiwa mafundisho yako, hayalengi kuwavuta watu wa Kristo, kinyume chake, ni kuwahubiria tu jinsi ya kufanikiwa hapa duniani..Basi ujue wewe ni mjumbe usiyekuwa na ujumbe.. Na kazi yako haina faida yoyote, haijalishi utakuwa unawakusanya maelfu ya watu kiasi gani kukusikiliza, au wanakusifia kiasi gani.

Ujumbe tuliopewa ni mmoja tu, nao ni kuwafanya “mataifa yote kuwa wanafunzi wake”. Na unamfanyaje mtu kuwa mwanafunzi, Bwana Yesu alishasema katika Luka 14:27

Hivyo chochote tukihubiricho hakipaswi kwenda mbali na kiini hicho cha agizo..Hata kama tutahubiri hayo mengine lakini kiini hicho kionekane, na hiyo ni kwa faida yetu wenyewe ili kazi yetu isiwe bure mbele za Mungu.

Bwana akabariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

SADAKA YA MALIMBUKO.

KUOTA UNACHEZA MPIRA.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

WAKATI WA KRISTO KUSIMAMA,UMEKARIBIA SANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NGUVU YA SADAKA.

Ijue nguvu ya sadaka.


Kuna nguvu ya kipekee  iliyo ndani ya sadaka ambayo watu wengi hawaifahamu.

Mungu anaweza kweli akawa ni Rafiki yako mkubwa sana, anaweza kweli akawa anazungumza na wewe, na ukaisikia sauti yake, ikikwambia nimekusikia mwanangu na nitakupa kitu Fulani..Lakini ukashangaa kitu hicho hujakipata japokuwa alikuahidia kabisa atakuwa na wewe..

Hiyo ni kutokana na kuwa ulichomwomba Mungu, hukukiambatanisha na sadaka..Leo hii nitakuonyesha mfano wa watu wa namna hiyo katika biblia ambao walimwomba Mungu sana Na Mungu akawasikia na kuwaahidia kuwa anatakuwa nao, lakini majibu yalikuja tofauti na walivyokitarajia mpaka walipogundua kuwa tatizo ni nini?….

Bwana atusaidie tuifahamu Nguvu ya Sadaka.

Hiyo ni Habari ya wana wa Israeli siku ile walipotaka kwenda kupigana na ndugu zao Benyamini kutokana na wao kuwa na tabia ya kuutamia uovu wa wazinifu, bila kuwashaadhibu. Hivyo vita vikapangwa dhiki yao na waisraeli wengine wote waliosalia, Sasa Israeli wote walimwomba Mungu aende nao ili wakawapige Benyamini, mara ya kwanza, Mungu akawajibu akawaambia nitakuwa Pamoja nanyi, nanyi mtashinda, Lakini walipokwenda walipigwa mapigo makubwa sana..

Wakamrudia Mungu wakamuuliza tena, Je utakwenda Pamoja nasi mara hii nyingine?, Mungu akawaambia ndio nitakuwa Pamoja nanyi, lakini walipoenda kapigwa, tena wakafa watu wengi kweli.

Wakamrudia tena Mungu kwa mara ya tatu, lakini safari hii hawakumrudia mikono mitupu, walimrudia kwa kufunga, na kwa sadaka nyingi sana, jambo ambalo hapo Mwanzo hawakulifanya..Kisha wakamuuliza Mungu tena Je! Utakwenda Pamoja na sisi, ndipo Mungu akawaambia, Hakika nitakwenda Pamoja na nyie..

Na kweli walipokwenda waliwapiga Wabenyamini wengi sana, wakatoka na ushindi mnono (Waamuzi 20:22-29)..Hapo ndipo walipojua nguvu ya sadaka ipo wapi!

Kwa marefu ya Habari hiyo na fundisho lake fungua  hapa usome. >>> UMUHIMU WA SADAKA.

Hata wewe, inawezekana unamtii Mungu sana, unajibidiisha sana katika kumwomba kwa bidii, lakini kwenye suala la kumtolea Mungu, hulizingatii sana, unaona kama halina umuhimu kwa mkristo, ni pengine kwasababu hukujua nguvu ya sadaka…

Ndugu Ijue nguvu ya sadaka..

Umekuwa ukimwomba Mungu akupe kitu Fulani, na muda mrefu umepita..Leo hii fahamu kanuni za kupokea kutoka kwa Mungu. Kumbuka Mungu hana shida na fedha zako..Kwasababu vyote ni mali yake, alishasema hivyo (Hagai 2:8) , lakini anataka kuona mtu anayemwomba anao moyo wa kujali..Hicho tu..

Pale unapomtolea kinono, ndipo unapougusa moyo wake Zaidi na kuona sababu ya kwanini wewe akujibu haraka kuliko yule mwingine asiyemjali?. Fedha unazomtolea Mungu, zinakwenda katika kuwabariki wengine pia rohoni,

Hivyo unapomwomba Mungu akupe, au akutendee jambo lolote, hakikisha kwa uwezo ulio nao, ambatanisha sadaka yako tena iliyo  NONO ya hicho unachomwombea… Usiombe tu Mungu nipe, gari, nipe nyumba, nipe hiki, nipe kile halafu huna mpango wa wewe pia kumtolea Mungu, nataka nikuambie, ukiwa na tabia hiyo  majibu yako yatakuwa ni ya kuchelewa sana.

Hivyo anza leo, kujifunza kuambatanisha sadaka ya kila unachomwomba Mungu, kwa jinsi Mungu alivyokujalia…

Ijue nguvu ya sadaka..

Na kumbuka pia sadaka hiyo haipaswi kupelekwa sehemu nyingine yoyote Zaidi ya madhabahuni pa Mungu.. Haipaswi kupelekwa kwa watoto yatima, au watu wasiojiweza, au kwa mtu mwingine yoyote hapana..Inapaswa ifikishwe madhabahuni pa Mung utu! yaani Kanisani kwako.

Hivyo zingatia vigezo hivyo, Na hakika utaona matokeo chanya, katika maombi yako.

Hiyo ndiyo nguvu ya sadaka.

Bwana akubariki.

Soma masomo mengine chini…

Mada Nyinginezo:

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

NGUVU YA MSAMAHA

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTAFIKA WAKATI WA WEWE KUACHWA NYIKANI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia leo tena.

Vipo vipindi tofauti tofauti ambavyo kila mkristo atavipitia…maana biblia inasema katika..

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; ….

4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”.

Hata uwe unampendeza Mungu kiasi gani/ hata uwe mkamilifu mbele za Mungu kiasi gani..ni lazima utapitia vipindi vya kulia tu katika Maisha yako!..ni kweli asilimia kubwa ya Maisha yako itatawaliwa na furaha na amani..lakini ni lazima utapitia tu vipindi tofauti tofauti vya kulia na vya huzuni.

Sasa katika Imani pia vipo vipindi ambavyo utamwona Mungu sanaaa..na vipindi ambavyo hutamwona (utaona kuna ukimya Fulani maishani mwako)!…Sio kwamba atakuwa amekuacha kabisa! Au hakufuatilii wala kukusaidia…Hapana atakuwa yupo anakuona na kukujua lakini atakuwa kama amejiepusha na wewe”. Bwana Yesu kuna kipindi alisema “Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha”…hivyo huo wakati wa kuachwa upo!…Wengi hawalijui hili, ndio maana wanapopitia kipindi Fulani cha Maisha wanarudi nyuma na kuuacha wokovu…

Sasa leo tutajifunza hicho kipindi ni kipi lakini kabla ya kuendelea mbele zaidi hebu usome mfano huu taratibu sana, kisha tutaendelea…

Luka 15:3  “Akawaambia mfano huu, akisema, 

4  Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda NYIKANI, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone? 

5  Naye akiisha kumwona, HUMWEKA MABEGANI PAKE AKIFURAHI. 

6  Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea. 

7  Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu”.

Mfano huo unaonyesha ni jinsi gani..Bwana anaweza akawaacha kondoo 99 nyikani na kwenda kumtafuta kondoo mmoja aliyepotea. Umewahi kujiuliza kwanini awaache wale kondoo 99, na kwanini asiende nao?..na kwanini awaache NYIKANI na si kwenye zizi, mahali palipo salama?…

Maana yake ni kwamba anawaacha peke yao sehemu ya wazi isiyo na uzio, ambayo inaonekana ni sehemu hatari, lakini ni salama….Sehemu ambayo Wanyama wakali wanapita, sehemu ambayo inaogopesha!…na mbaya zaidi wanaachwa peke yao…Na lengo la Bwana kuwaacha ni ili akatafute kondoo wengine..

Sasa hao kondoo walioachwa nyikani pengine ni wewe unayepitia ukame sasa, humwoni Bwana kama ulivyomwona wakati umeokoka. Sasa ufanye nini katika hiyo nyika yenye utata?

Kumbuka hapo ni nyikani, mahali pasipo na uzio.. hivyo sio wakati wa kuzunguka zunguka huko na kule…kaa hapo hapo ulipo ndio mahali salama!…hapo hapo mahali Bwana alipokuacha!..(maana yake ni kwamba anaelewa kabisa mahali alipokuacha  utakuwa salama mpaka atakaporudi) tulia hapo hapo hata kama ukitazama kushoto humwoni Bwana, ukitazama kulia umwoni Bwana kama ilivyokuwa hapo kwanza…wewe tambua kuwa hapo ulipo upo sehemu salama..lishike Neno lake lile lile na Imani!…

Haupo ndani ya uzio, ikiwa na maana kuwa  vishawishi vya kukuvuta utoke kwenye mstari wa wokovu, utaviona, usianze kuzurula…wala kuhama hama…tulia hapo hapo….Hali kadhalika pembeni unaweza kuona dalili ya kudhurika na wanyama wanaopita kule, na unaweza kuona kama vile hakuna ulinzi, usiogope! Kaa hapo hapo ndio sehemu salama (aliyekuacha hapo sio mjinga)….Hivyo tumia muda wako kujifunza Neno na kuwaimarisha wengine na kuwalinda wasitoke kwenye hifadhi ya Mungu..kwa kuwafundisha wokovu na kuwafariji mpaka wakati wa Bwana kurudi.

Kumbuka tena kuna wakati Fulani Kristo alikuweka mabegani alipokupata…lakini si wakati wote utakuwa mabegani mwake…wakati ukiwa mabegani mwake ulikuwa unamwona kwenye ndoto kila siku, ulikuwa unauhisi uwepo wake kila mahali, ulipomwomba kitu ulikipata papo kwa hapo…(wakati huo ulikuwa mabegani mwake, mbingu ilifurahia kukupata) lakini hautakuwa hivyo siku zote…utafika wakati utashushwa mabegani na wewe utakwenda kuungana na wenzako nyikani na Bwana atakwenda kutafuta kondoo wengine waliopotea.

Kama ni leo umempa Kristo Maisha yako, basi uwe tayari kwa hicho kipindi kuja mbele yako. Jifunze kumwelewa sana Bwana wakati huu wa sasa, ambao unamwona sana… kwasababu wakati wa ukame utafika!..kama hutamwelewa sana wakati huu, wakati wa kuachwa nyikani utaikimbia na kuiacha nyika.

Na hapo ndipo watu wengi walipopotelea. Imani ni ya kuilinda sana.

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

JUMA LA 70 LA DANIELI

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

Ukisoma kitabu cha Warumi sura ya 9, ya 10, na ya 11..utaona mambo mazito sana mtume Paulo aliyokuwa akiyazungumza juu ya ndugu zake wayahudi. Akieleza jinsi neema ya Mungu ilivyoondolewa kwao, kiasi kwamba hata wangehubiriwa vipi injili wasingeweza kuipokea.

Chukua muda kwa wakati wako, pitia sura hizo kwa utulivu sana, ukisoma juu juu hutaona chochote, lakini ukisoma kwa utulivu huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, nakuambia hutaichezea hata kidogo hii neema tuliyopewa sisi watu wa mataifa.

Mtume Paulo alipewa kulijua hilo mpaka akawa anasema, anayo huzuni nyingi, na maumivu yasiyokoma moyoni mwake kwa ajili ya ndugu zake (yaani wayahudi), maumivu ya kila siku, akijua kuwa wokovu umeondolewa kwao..

Kiasi kwamba alitamani hata kama ingewezekana yeye  mwenyewe aupoteze wokovu wake, atengwe na Kristo ili kusudi kwamba ndugu zake wote wapone, basi angefanya hivyo..soma..

Warumi 9:1  “Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,

2  ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.

 3  Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe NIHARIMISHWE NA KUTENGWA NA KRISTO kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili”;

Kauli hiyo si rahisi kuizungumza, lakini kwa huruma ya watu wengine, na huzuni unayoisikia moyoni mwako inakulazimu uitamke, si kwamba unatamani iwe hivyo, lakini kama ingewezekana.. Ni sawa leo umuone mtoto wako mchanga, kapata ajali halafu kakatika mikono, halafu anatapata tapa pale chini kwa maumivu,akilia, ni wazi kuwa utatamani ungeyapitia wewe yale maumivu yake..Kuliko kumuona anaendelea kuteseka katika ile hali.

Ndivyo ilivyokuwa kwa mtume Paulo, alitamani kama ingekuwa inawezekana yeye kuharamishwa, (kufanywa kuwa mwana-haramu,atengwe na Kristo) kusudi kwamba ndugu zake wayahudi waiamini Injili waokolewe.. Lakini ilikuwa haiwezekani.

Ndugu kama hufahamu wakati ule wa kanisa la kwanza ni wayahudi wachache sana, waliiamini Injili, japokuwa ilikuwa ni mamilioni waliokuwa wanaisikia, na ndio maana ukisoma mbele kidogo mtume Paulo anasema.

Warumi 9.27  “..Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa”

Waliokolewa wachache sana, mpaka akasema, kama Mungu asingewaachia mabaki basi wangefananishwa na Sodoma na Gomora,(yaani akiwa na maana asingeokoka myahudi hata mmoja wakati wao)..

Na hiyo yote ilikuwa ni kwasababu waliikataa neema ya wokovu iliyoletwa na Yesu Kristo, alipokuwa duniani, na kuendelea na njia zao za kumtafuta Mungu, huku wamemweka Kristo pembeni. Ikapelekea mlango wa neema kufungwa juu yao. Na ndio maana utaona haijalishi walikuwa na bidii kiasi gani kwa Mungu lakini hawakuweza kuuona mlango wa neema hata kidogo kwasababu tu walimkataa Kristo (kasome Luka 13:34-35). Mtume Paulo alisema hivyo katika ile sura ya 10

Warumi 10:1  “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.

2  Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa”.

Hilo jambo linaendelea mpaka sasa, takribani miaka 2000 imepita, lakini  bado mlango wa neema haujafunuliwa kwao. Na hiyo yote ni ili mimi na wewe (watu wa mataifa), tuipokee neema.

Lakini mwisho kabisa mtume Paulo alipewa siri na Mungu, na siri hiyo aliiweka wazi akataka sisi nasi tuijue (yaani mimi na wewe), kwamba utafika wakati ambao Mungu atawarehemu tena..Na kikisha fika hicho kipindi basi sisi tufahamu Habari yote ndio imeishia hapo, kama mtu yeyote wa mataifa atakuwa hajaingia ndani ya Kristo, ndio basi tena..Soma

Warumi 11:25  “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26  Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.

Jiulize wayahudi kwa miaka 2000 wanautafuta uso wa Mungu lakini hawaupati, unadhani siku hiyo neema ikiondolewa kwetu, sisi tutaipatia wapi? Na dalili zote zinaonyesha wakati wao upo karibuni sana…Tayari taifa hili lilishachipuka tangu mwaka 1948, unadhani ni nini kinachosubiriwa hawa watu Mungu asiwageukie? Usiku na mchana wapo pale kwenye “ukuta wa maombolezo wa Nehemia” wanamlilia Mungu awaokoe (hayo yalikuwa ni majonzi ya mtume Paulo)..Lakini Bwana anakawia kidogo kwa ajili yangu mimi na wewe.

Moja ya hizi siku, Mungu atakisikia kilio chao,.mlango wa neema utafunguliwa kwao, na kwetu utafungwa,. Huo ndio ule wakati wa mwenye nyumba kusimama na kuufunga mlango, na watu watakuwa wakisimama nje na kugonga wafunguliwe lakini Bwana atawaambia siwajui mtokako.(Luka 13:25-28)…Duniani kutakuwa na kilio na kusaga meno.

Hivyo tunaposikia maneno haya, tujitathimini Je! Ni kweli bado tupo ndani ya Kristo? Au tupo vuguvugu. Kama wewe unaisikia injili na bado unasua sua basi uingie sasa kwa nia yote acha kusitasita kwenye mawazo mawili muda unazidi kwenda, kwasababu siku hizi ni za mwisho. Lango hili likishafungwa, halitafunguliwa kamwe.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

MADHARA YA KUTOA MIMBA.

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ulokole ni nini? Na kwanini wakristo waliookoka wanaitwa walokole?

Ulokole/ Walokole wametoka wapi?


JIBU: Kabla ya kwenda kujua maana ya ulokole, ni muhimu kujua kwanza maana ya neno ‘kanisa’..Tafsiri ya kwanza ya kanisa sio “jengo” bali ni “mkusanyiko wa watu waliomwamini Yesu”..Kwahiyo popote palipo na mkusanyiko wa watu waliomwamini Yesu, tayari hilo ni kanisa hata kama hakuna jengo. Soma mistari ifuatayo itakusaidia Matendo 2:47,1Wakorintho 1:2,14:5,14:23,15:9,16:19 n.k

Na kanisa la Kristo ni moja tu duniani kote ambalo linajulikana kama Bibi-arusi wa Kristo…Hilo ndio linajumuisha wakristo wote waliomwamini Yesu na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake (kumbuka hapa hatuzungumzii madhehebu), bali kanisa la Kristo moja ambalo pia sio jengo, bali watu wote duniani waliomwamini Yesu. Na watu hawa ambao ndio kanisa la Kristo, ndio watakaokuja kunyakuliwa siku ya parapanda katika tukio lijulikanalo kama UNYAKUO WA KANISA. Unaitwa unyakuo wa kanisa na si makanisa…kwasababu kanisa la Kristo ni moja tu.

Lakini sasa Kanisa la Kristo ni kweli ni moja lakini lina washirika wengi, na haliwezi lote kukusanyika pamoja na kwa wakati mmoja kufanya ibada, au kumwabudu Mungu, kama ni hivyo basi halina budi kuwepo na makusanyiko tofauti madogo madogo katika kila eneo ili kukamilisha kusudi lile lile la kukusanyika pamoja…Ndio hapo wakristo waliopo Mkoa wa kilimanjaro watakusanyika kivyao, na waliopo Morogoro watakusanyika kivyao huko waliko, n.k..

Lakini kumbuka Imani ni moja, na Kristo ni yule yule anayeabudiwa kote, utendaji kazi unaweza ukawa unatofautiana kulingana na kanisa na kanisa, lakini Imani ni sharti iwe ile ile moja, Bwana mmoja, Roho Mmoja, Ubatizo mmoja sawasawa na (Waefeso 4:3-7), tofauti na hapo hilo ni jambo lingine.

Sasa katika mkoa huo huo wa Morogoro pia sio wakristo wote wapo Morogoro mjini, kuna wengine wapo vijiji vya ndani huko…hao nao hawana budi wakusanyike huko walipo, hakuna sababu ya kusafiri mpaka mjini….na huko vijijini pia kuna uwezekano wa watu wasiwe karibu karibu…hivyo tena yatazaliwa makundi mengine madogo madogo mengi kulingana na mahali, hata inaweza kufikia kanisa likawa na watu watano..lakini yote yenye imani moja. Umbali ndio unaosababisha yajigawanye hivyo.

Sasa haya makanisa mengi madogo madogo ambayo yanakuwa katika eneo husika kwa kiingereza yanajulikana kama LOCAL CHURCHES, (Yaani kanisa la eneo husika aidha mtaa, au kijiji).

Na makanisa haya zamani, kutokana na uchache wa watu yaliyonayo na maeneo yalipo mengi yaliishia kudharaulika… na asilimia kubwa ya washirika wake ni maskini…kwasababu wengi wanaoishi vijijini au katika miji midogo midogo si matajiri kulinganishwa na wale wanaoishi mijini. Hivyo walidharaulika lakini kama biblia inavyosema kuwa..

Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao”

Hivyo hao waliodharaulika na kujulikana kama “Local churches”… ndio waliokuwa wa kiroho zaidi..Ishara nyingi na miujiza mingi ilifuatana na haya makanisa madogo madogo, kuliko hayo makubwa, …ndio watu waliokuwa na bidii zaidi ya kumtafuta Mungu, na ndio waliokuwa wanamheshimu zaidi Mungu.

Sasa kutokana na makanisa hayo madogo madogo kufahamika kama local churches…na washirika wao ndio wakajulikana kama “local people”..na kwa lugha yetu hii wakatafsiriwa kama (wa-locally) au WALOKOLE.

Hivyo kama mtu utaitwa mshamba kwa sababu unamwamini Yesu na kuzishika amri zake basi hiyo ni THAWABU. Kuliko kama utaitwa mwenye Elimu na wa-kisasa na huku umemwacha Kristo.

Ufunuo 3:17 “Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona”

Usijisifie ukubwa wa kanisa unaloabudu, wala wingi wa watu wa kanisani kwenu…Jisifie Yesu uliye naye maishani mwako hata kama upo kanisa la watu watano..jitathmini je! unazishika amri zake hapo ulipo?, je! unaishi kulingana na neno lake? Kiasi kwamba hata parapanda ikilia utakwenda naye!..Je hapa nilipo nanufaika roho yangu kiasi gani?..kama sinufaiki rohoni ni heri nikatafute wenzangu wenye Imani ya kweli hata kama ni wachache, ninusuru roho yangu..kuliko kuendelea kwenye umati wa watu wengi na kuipoteza nafsi yangu…

Ni heri nijulikane mlokole lakini naenda mbinguni kuliko kukubalika na kila mtu, mwisho wa siku naishia kwenda jehanamu. Na kama pia hapo ulipo penye watu wachache huoni dalili ya kuurithi uzima wa milele ni heri ukaenda kutafuta penye watu wengi ambao wanakwenda mbinguni..Lakini siku zote kumbuka mlango ni mwembamba na njia ile imesonga na ni wachache wanayoiona…na mlango ni mpana wa njia iendayo upotevuni na wengi wanauendea.

Bwana akubariki na Bwana atusaidie.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?

MIHURI SABA

Wafilisti ni watu gani.

YEREMIA

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MANENO ALIYOWEZA KUTAMKA YESU TU PEKE YAKE.

Yapo maneno ambayo huwezi kuzungumza, isipokuwa kwanza unaelewa vizuri ni nini unazungumza vinginevyo unaweza kujiweka kwenye kitanzi mwenyewe na kuingia matatizoni..

Kuna wakati Bwana aliwaambia wale watu wanaoshindana naye maneno haya…

“Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi..”? (Yohana 8:46)

Maneno haya si mepesi kabisa, Kumbuka juu kidogo tu kwenye sura hiyo hiyo swali la namna hii hii aliwauliza wale watu waliomfumania yule mwanamke katika uzinzi, lakini majibu yake ni kuwa sio tu kutomtupia yule mwanamke mawe, bali pia waliona aibu kuendelea kubaki maeneo yale, kwa mtihani huo mgumu waliopewa.

Yohana 8:7 “Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.

8 Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.

9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao;

akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati”.

Unaona? Lakini hapa na yeye pia anajiweka katika hicho kitanzi na kuwauliza watu.. Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi?

Jaribu kujiweka wewe katika hiyo nafasi ukiwa kama kijana wa miaka 33 ambaye tayari umeshapitia mambo mengi katika maisha, halafu unasimama katikati ya umati wa watu wanaoshindana na wewe, unawauliza ni nani kati yenu anayenishuhudia kuwa nina dhambi?

Je! Wewe unaweza kusema hayo maneno?(Mimi siwezi)..Ndugu zako wote wamesimama karibu nawe , marafiki zako wote uliowahi kuishi nao na kusoma nao, wote pia wamesimama karibu hapo, majirani zako nao wapo, wafanyakazi wenzako wanasimama hapo vilevile halafu unawauliza wote “Kati yenu ninyi ni nani anayenishuhudia kuwa nina dhambi”..

Ni nani alishawahi kuniona au kusikia nimemsengenya mtu, ni nani nilishawahi kumdanganya au alishawahi kunisikia nadanganya, ni wapi nilishawahi kutamani, ni wapi nilishawahi kumvunjia mtu heshima, au kumwonea wivu, au kumwekea kinyongo, au kuonyesha unafki, kumfokea, kumtukana? ..Kama yupo hapa asimame, au ajitokeze, asimeme wewe siku fulani nilikuona ukikwepa kodi kwenye ile biashara yenu ya useremala…

Lakini wote waliosimama pale, hakuonekana hata mmoja aliyekuwa na la kumshitaki Yesu..sio jambo rahisi kama tunavyofikiri,

Na ndio maana mahali pengine biblia inasema..

1Petro 2:22 “Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.”

Ni Yesu peke yake, katika ulimwengu mzima, katika vizazi vyote, ambaye tangu amezaliwa mpaka anakufa, hakuwahi kutenda dhambi hata moja, japokuwa alipitia majaribu mazito ya dhambi kuliko hata sisi.

Ndugu yangu Kwa YESU pekee mimi nimetia nanga! Sijui kwako?, kwasababu hakuna mwingine kama yeye, huyu pekee ndio wa kumtumainia, ni huyu pekee ndio wa kumtegemea kutusaidia kushinda huu ulimwengu kama yeye alivyoshinda, ni huyu huyu pekee ndio atakayetuokoa tukimwamini. Mimi na wewe tukimfanya kuwa rafiki wa maisha yetu, jambo la kwanza na la ajabu ni kuwa anatusamehe dhambi zetu zote, halafu anatuhesabia haki bure pasipo matendo yetu kwa neema, kiasi kwamba mbele za Mungu tunaonekana kuwa tumestahili haki yote.

Kisha baada ya hapo anamtuma Roho wake Mtakatifu ndani yetu. Ambaye kazi yake ni kutupa sisi nguvu ya kuishinda dhambi kama yeye alivyoishinda, na kutuongoza katika kuijua kweli yote.

Hivyo kama bado hujaokoka, saa ya wokovu ni sasa, fanya haraka mkaribishe Yesu maishani mwako. Kama umezichoka dhambi kweli, kama hutaki nafsi yako ipotee, basi mkimbilie Yesu haraka maadamu muda upo, Lakini tukikataa kuyasikia maneno yake basi yeye naye atatuacha, na kutuona tu kama sio watu tuliochaguliwa na Baba yake soma..

8:46 “Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi? Nami nikisema kweli, mbona ninyi hamnisadiki?

47 Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu”.

Natumaini wewe leo utayasikia maneno yake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

RABI, UNAKAA WAPI?

NENO HILI NI GUMU,NI NANI AWEZAYE KULISIKIA?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

KUMBUKA, VIVUKO VYA YORDANI VINAKUNGOJA MBELENI.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

AHADI ZA MUNGU.

Ahadi za Mungu ni za kweli kabisa,.. Lakini tatizo kubwa linalotukabili  sisi wanadamu ni kutokujua njia Mungu anazozitumia kutimiza ahadi zake.

Na hiyo inawafanya watu wengi waishie kukata tamaa pale anapoona mbona ahadi za Mungu zimechelewa, pengine nimemkosea Mungu, au Hanisikii..

Fahamu kuwa wakati wa Mungu kutimiza ahadi zake, sio lazima uwe ule wakati ulioupanga wewe Tena mara nyingi huwa anauchagua ule wakati ambao haufahau, wakati ambao mambo yote yanaokana yameharibika, mipango imevurugika, umeshachelewa, hapo ndipo Mungu anasimama ili kutimiza ahadi zake kwako.

  • Utamwona Ibrahimu, alipokuwa na miaka 75 Mungu alimwambia nitakupa mwana, na nitakufanya kuwa taifa kubwa.. Jaribu kufiria katika uzee ule, ungedhani labda, baada ya mwaka mmoja tu, ndio Mungu angemtimizia ahadi yake, ili viungo vya uzazi visife kabisa..Lakini tunaona Mungu aliendelea kusubiri, hadi miaka karibia 25 mbeleni, akiwa sasa na umri karibia na miaka 100 ndio Mungu anamtembelea na kumpa mtoto.

Na hakupewa tu mtoto basi, bali na mwili wake pia ulirudishwa na kuwa kama wa kijana, yeye pamoja na mke wake Sara.

Lakini Ibrahimu katika kipindi chote hicho hapo katikati hakumkosea Mungu imani na ndio maana akaitwa baba wa Imani, tunasoma hilo katika..

Warumi 4:18 “Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ili apate kuwa baba wa mataifa mengi, kama ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.

19 Yeye asiyekuwa dhaifu wa imani, alifikiri hali ya mwili wake uliokuwa umekwisha kufa, (akiwa amekwisha kupata umri wa kama miaka mia), na hali ya kufa ya tumbo lake Sara.

20 Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu;

21 huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.

22 Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki”.  

  • Unaona? Vivyo hivyo Yusufu naye , tayari alishapewa neon la ahadi katika ndoto, kuwa upo wakati atakuzwa kiasi kwamba mpaka ndugu zake watakuja kumwinamia. Lakini hilo halikutimia kwa wakati ule ule alioonyeshwa, kinyume chake akiwa na umri wa miaka 17 aliuzwa na ndugu zake, akawa mtumwa kule Misri mpaka anafikia miaka 30 ndio hizo ndoto zinakuja kutimia.

Na hazikutimia akiwa nyumbani mwa Potifa hapana, bali zilitimia akiwa gerezani, mahali ambapo hapana tumaini lolote, la kuishi. Kwa kipindi karibu cha miaka 2 akiwa kule gerezani, siku moja isiyokuwa na jina Mungu alimtembelea na kumwinua, akatoka na kufanywa kuwa Waziri mkuu na makamu wa Raisi wa taifa kubwa lililokuwa lina nguvu kuliko yote ulimwenguni wakati ule (Misri).

Hivyo zipo ahadi za Mungu nyingi katika biblia ambazo tukianza kuzichambua hapa moja baada ya nyingine hatuwezi kumaliza zote..

Ahadi za Mungu kwa mkristo:

Hiyo ni kutupa tu hamasa mimi na wewe ambao pengine umesubiria ahadi za Mungu kwa muda mrefu sasa na bado hujaona matokeo yoyote. Unachopaswa kufanya ni kusubiri ndugu yangu, huku ukiendelea kumtumikia Mungu kwa moyo ule ule wa kwanza.

Unaweza ukawa ni mtumishi wa Mungu, na umejaribu kuacha kila kitu ili tu uifanye kazi yake..Nataka nikuambie endelea hivyo hivyo, upo wakati utafika ile hadi yake ya kuwa UTAPATA MARA MIA, itatimia juu yako, haijalishi ni miaka miwili tokea sasa, au 5 au 10 au 20, lakini fahamu kuwa ukiendelea kung’ang’ania njia yako bila kuiacha, utavuna ulichopanda.

Mungu atakulipa tu, mema, ukiwa hapa hapa duniani, na vyote ulivyovipoteza utarejeshewa vyote mara mia. (Marko 10:28-30) Hivyo endelea kumtumikia MUNGU.

Vilevile Bwana aliposema, usisimbukie maisha ule nini, unywe nini, avae nini, bali utafute kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine utazidishiwa. Basi fahamu kuwa ukijikita kuutafuta kwanza uso wa Mungu, na kutaka kumjua yeye, ni ahadi yake kuwa  hatakuacha ufe njaa, bali atahakikisha kuwa anakuhudumia ili uendelee kuishi,..Kwasababu unautafuta ufalme wake..Hiyo ni kweli kabisa hawezi kudanganya.. Ahadi za Mungu ni thabiti.

Vivyo hivyo na ahadi nyingine yoyote aliyowahi kukuahidia , endelea tu kuingoja, wakati wake utafika tu,. Kikubwa usiuache wokovu wako na utakatifu wako kama wewe umeokoka.

Lakini kama hujaokoka, basi hakuna ahadi yoyote ya Mungu inayoweza kutimia juu yako. Hivyo unachopaswa kufanya ni kumpa Kristo maisha yako ili ayaokoe, kwani hizi ni siku za  mwisho na Unyakuo upo karibu,..Moja ya hizi siku mabadiliko makubwa sana yatatokea duniani. Na dhiki kuu itaanza, hivyo mgeukie muumba wako kabla ya hizo za hatari hazijakufikia kwa ghafla.

Bwana akubariki.

Ahadi za Mungu ni Yakini.

Mada Nyinginezo:

KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

UNYAKUO.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post