NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

Ni salama rohoni mwangu lyrics- It is well with my soul.


Nyimbo hii ilitungwa na mwanasheria mmoja mkristo aliyeitwa Horatio Spafford, alitunga wimbo huu kutokana na mambo mazito aliyoyapitia katika maisha yake, Matatizo yake yalianza kwa kufiwa na mtoto wake wa pekee wa kiume aliyekuwa na miaka minne, hiyo ilikuwa ni mwaka 1870

Muda mfupi baadaye (mwaka 1871) moto mkubwa uliozuka huko Chicago Marekani mjini kwake, ukaharibu mali zake nyingi ukizingatia alikuwa ni mwanasheria aliyekuwa amefanikiwa sana. Hilo likafuatana na biashara zake pia kuporomoka kutokana na anguko la uchumi lililotokea mwaka 1873, Hivyo ikambidi apange safari ya kwenda Ulaya pamoja na familia yake, Lakini aliahirisha safari kwa ajili ya kuweka mambo yake ya vibiashara vizuri yaliyokuwa yameathiriwa na moto, hivyo ikambidi msafirishe kwanz mkewe na mabinti zake wanne,akiahidi kuwa atawafuta baadaye.

Lakini Meli ilipokuwa inakatisha bahari ya atlantiki, ilizama ghafla kwa kugongana na meli nyingine na mabinti zake wote wanne wakafariki kwenye ajali hiyo akasalimika mke wake tu, akiwa kule Marekani alipokea ujumbe wa telegrafu kutoka kwa mke wake unaosema “Nimepona peke yangu” ndipo Spafford akaondoka kumfuata mkewe, na huko huko akauandika wimbo huu..

https://www.high-endrolex.com/15

Baadaye vina vingine vya mashairi viliongezwa ndipo ukazaliwa wimbo huu, Ni salama Rohoni Mwangu.

****

Nionapo amani kama shwari,

Ama nionapo shida;

Kwa mambo yote umenijulisha,

Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,

Rohoni, Rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

Ingawa Shetani atanitesa,

Nitajipa moyo kwani;

Kristo ameona unyonge wangu,

Amekufa kwa roho yangu.

Salama, Salama,

Rohoni, Rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

Dhambi zangu zote, wala si nusu,

Zimewekwa Msalabani;

Wala sichukui laana yake,

Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,

Rohoni, Rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

Ee Bwana himiza siku ya kuja,

Panda itakapolia;

Utakaposhuka sitaogopa,

Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,

Rohoni, Rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

****

Hata sisi Je! Tunapopitia shida na magumu tunazo nguvu za kusema ni salama rohoni mwangu?, Tunapopitia njaa, tunapopitia misiba, tunapopitia matatizo mazito Je! Bado Tunaweza kumwambia shetani ni Salama rohoni mwangu? Kama ilivyokuwa kwa Ayubu?

Siku zote kumbuka hili Neno..

Mithali 24: 10 Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache.

Hivyo jipe moyo songa mbele ikiwa wewe ni mkristo, Kwasababu mwisho wa Mungu sikuzote ni mzuri, kama ilivyokuwa kwa Yusufu, kama ilivyokuwa kwa Ayubu, na ndivyo itakavyokuwa na kwako.

Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma”.

Shalom.

Tazama chini historia ya nyimbo nyingine za Tenzi:

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Kwa maombezi/ubatizo/ Kumpokea Yesu. Wasiliana nasi kwa namba hizi; +255789001312/+255693036618

Mada Nyinginezo:

MWAMBA WENYE IMARA

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

TENZI ZA ROHONI

YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.

YESU AKALIA KWA SAUTI KUU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?

SWALI: Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, Je! Ina maana hakuwa na wana wengine au hana wana wengine zaidi yake?


JIBU: Tusome..

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Hivyo ndivyo inavyotafsiriwa na watu wengi na madhehebu mengi ya dini..Lakini sivyo inavyomaanisha hapo, Mungu kumwita Yesu mwanawe pekee, haimaanishi, hajawahi kuwa na wana wengine,(ambao ndio sisi), bali alimaanisha Yesu ni mwana-wake-wa-kipekee tofauti na sisi wengine aliyebakiwa naye, mwenye mahusiano ya kitofauti na wengine, mwana wa maagano ndio maana akimwita Kristo  mwanawe pekee.

Ili kulithibitisha jambo hilo embu tutazame baadhi ya vifungu vya maandiko vinavyoelezea habari inayofanana na hiyo, Na hiyo si nyingine zaidi ya ile ya Ibrahimu na mwanawe Isaka..tusome.

Mwanzo 22:2 “Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia”.

Soma tena..

Mwanzo 22:12 “Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee”.

Soma tena…

Waebrania 11:17 “Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee”;

Unaona ukisoma mistari hiyo yote, unaweza kudhani Isaka ndio aliyekuwa mwana  tu wa Ibrahimu hakuwa na wengine, lakini tunajua kuwa kabla ya Isaka alikuwepo Ishmaeli. Na baada ya Isaka walikuja wengine wengi (Mwanzo 25:1-4).

Lakini ni kwanini Mungu amwite Isaka kama mwana pekee wa Ibrahimu, ni kwasababu alikuwa mwana wa maagano, mwana wa ahadi, tofauti na wale wengine,…Isaka alifananishwa na Kristo

Hivyo Kristo Bwana wetu ndio mwana pekee wa Mungu, ambaye ameshikilia maagano yetu yote, kwa kupitia yeye, Mungu ametupenda tena, kwa kupitia yeye sisi tumebarikiwa, na kwa kupitia yeye, tunapata uzima wa milele, na tumaini la ufufuo baada ya kifo.  Hivyo tukimwamini na kumpokea tunaingia katika huo mnyororo wa Pendo la Mungu.

“Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye”. Kama hujampokea huu ni wakati wako sasa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

  Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABİSA lyrics ~Swahili  (How Great Thou Art).


Toleo la kwanza kabisa la Wimbo huu liliandikwa na mtu mmoja raia wa Sweden, aliyeitwa Carl Boberg wimbo huu aliuandika mnamo mwaka 1885 baada ya kuvutiwa na mazingira aliyopishana nayo alipokuwa akitoka Kanisani yeye na marafiki zake. Anasema muda wa mchana walipokuwa njia hali ya hewa iliwabadilikia ghafla, wakaona wingu la tufani likitokea kwa mbali, na mara hiyo hiyo kukaanza kumulika mianga mingi kama ya radi angani, upepo mzuri ukaanza kuvuma juu ya mashamba yaliyokuwa pembeni, Na kisha manyunyu ya mvua matulivu  yakaanza kudondoka juu yao, na baada ya muda kidogo, wingu lile la tufani likapotea, muda huo huo ukatokea upinde mzuri wa mvua angani..

Na alipofika nyumbani na kufungua madirisha atazame nje, aliona ufukwe ya mji wake kama vile kioo, akatazama upande wa pili akasikia ndege wazuri wakitoa milio yao na kwa mbali kegele za kanisa zikilia, Hapo ndipo wimbo huu ulipomjia kichwani kuutunga na kuuandika.

****

Bwana Mungu nashangaa kabisa,

Nikifikiri jinsi ulivyo,

Nyota, ngurumo, vitu vyote pia,

Viumbavyo kwa uwezo wako.

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu,

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu.

Nikitembea pote duniani,

Ndege huimba nawasikia,

Milima hupendeza macho sana,

Upepo nao nafurahia.

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu,

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu.

Nikikumbuka vile wewe Mungu,

Ulivyompeleka mwanao,

Afe azichukue dhambi zetu,

Kuyatambua ni vigumu mno.

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu,

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu.

Yesu Mwokozi atakaporudi,

Kunichukua kwenda mbinguni,

Nitaimba sifa zako milele,

Wote wajue jinsi ulivyo.

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu,

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu.

*****

Tujiulize na sisi tunao utaratibu kwa kukaa chini na kuushangaa utukufu wa Mungu na kumtukuza?..Au kila kitu tunaona ni kawaida tu..Kumbuka Sifa kamili kama hizi mbele za Mungu ni bora kuliko dua na sala tunazompelekea kila siku.

Mungu anataka kuona, na sisi tukiufurahia uumbaji wake, kwa kumwimbia.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia kwa  email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

MWAMBA WENYE IMARA

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

POPOBAWA NI KWELI YUPO?

Karibu tuongeze maarifa ya rohoni. Yapo maswali machache ya kujiuliza ambayo yanaendelea katika jamii yetu..maswali hayo ni je! popobawa ni nani? Na je popobawa ni kweli yupo?..

Popobawa kulingana na waathirika wanasema ni viumbe (majini)..yanayowatokea watu usiku na kuwaingilia watu kinyume na maumbile pasipo hiari yao. Viumbe hao wanaonekana wakati wa usiku tu!..na vinawaingilia watu wa jinsia zote, wakiume na wakike pamoja na watoto wadogo.

Sasa kabla ya kujua hawa viumbe (popobawa ni nani)?..Hebu kwanza tujifunze historia ya uumbaji kulingana na biblia.

Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye IBILISI NA SHETANI, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye”.

Biblia inasema hapo huyo joka aliyetupwa chini ni shetani/ ibilisi, na hakutupwa peke yake, bali alitupwa pamoja na Malaika zake… Sasa hapo kwenye hilo neno “pamoja na malaika zake” ndio kiini cha somo hili.

Kama tunavyojua katika vita Yule kiongozi wa juu..hana tabia zinazofanana na wanajeshi wake asilimia mia…Ni wazi kuwa kila mwanajeshi anatabia yake na kazi yake maalumu..wapo wanajeshi waangani, wapo wa nchi kavu, wapo wa majini..Na katikati ya hao wanajeshi wapo wakatili sana, na wapo wenye roho ya wastani, na pia wapo wenye tabia mbaya na wapo wenye tabia za wastani…Na wanapopigwa basi wote wanakuwa wameshindwa na wanaonekana waasi…kwasababu wanashirikiana kwa kila kitu.

Kadhalika na malaika wa shetani ni hivyo hivyo, hawa malaika wa shetani baada ya kuasi na kushindwa vita mbinguni waligeuka na kuwa mapepo…sasa sio wote wanatabia zinazofanana..wapo walio wabaya sana, na wapo walio wa wastani..lakini wote ni wabaya tu!..kwasababu wanafanya kazi katika upande wa giza!..lakini wanatofautiana viwango…Na pia wanatofautiana vitu wanavyovipenda..yapo mapepo yanayopenda mazingira ya ulevi, yapo yanayopendelea mazingira ya uuaji na ukatili, yapo yanayopendelea mazingira ya uzinzi na uasherati, yapo yanayopendelea mazingira ya wizi n.k…Kama vile jinsi watu walivyo na tabia tofauti tofauti na haya mapepo ni hivyo hivyo.

Sasa pepo linaloitwa na watu “POPOBAWA” lipo katika hilo kundi la mapepo yanayofanya kazi katika mazingira ya UZINZI na UASHERATI. Kwa ufupi ni mapepo ya “uzinzi”…Lipo kundi moja na hayo mengine wanayoyaita “majini mahaba”..Yote yanafanya kazi moja ambayo ni “kupalilia dhambi ya uasherati duniani”.

Na Mapepo hayo (popobawa na mengineyo) yanaweza kuwatokea watu kwenye ndoto! Au  kwa wazi kabisa..Lakini huwa ni nadra sana kutokea kwa wazi, mara nyingi yanawajia watu kwenye ndoto. Kwahiyo hiyo popobawa ni kweli yupo?; Jibu ni ndio yupo!…anaweza kujulikana kwa majina tofauti tofauti kulingana na mahani na mahali…na pia anaweza kuonekana kwa maumbo tofauti tofauti, sio lazima aonekane na mabawa ya popo kama, anavyoshuhudiwa na watu….Ni mapepo yaliyoasi pamoja na shetani mbinguni, hivyo yanaweza kuchukua umbo lolote lile.

Sasa ni kwanini haya maroho (popobawa) yanawatokea watu na kuwafanya hayo yanayofanya?

Jibu ni rahisi sana..ni kutokana na hali za kiroho za watu!.

Mtu yeyote aliye nje ya Kristo ambaye hajaokoka anakuwa ni mlango uliofunguliwa wa kuingiliwa na roho yoyote ya mapepo…Na mapepo hayo yanayomwingilia yanaweza kumfanya chochote yanachokitaka kwa jinsi tabia zao zilivyo…kama ni pepo la uzinzi basi likimwingia litamfanya kuwa mzinzi, na hata linaweza kumtokea na kumwingilia..kama ni pepo la uuaji ni hivyo hivyo.

Hakuna mtu yoyote ambaye ameokoka kikamilifu na akasumbuliwa na hizi roho, hakuna! Kwasababu biblia inasema..Mtu aliye ndani ya Kristo “uhai wake unakuwa umefichwa” (Wakolosai 3:3).

Sasa ni namna gani unaweza kujidhibiti na hizi roho za popobawa na nyinginezo?

Kuna uongo uliozagaa kwamba unaweza kuzidhibiti kwa kuchoma ubani au udi, au kutojiangalia kwenye kioo, au kulala huku umevaa nguo, au kukesha usiku, au kulala na mfupa wa nguruwe!. Ndugu usidanganyike hakuna njia hata mojawapo ya hizo inayowafukuza au kuzidhibiti hizo roho. Dawa ni moja tu!..Ingia ndani ya Yesu UHAI WAKO UFICHWE. (Mwisho wa somo hili nitakufundisha jinsi ya kuingia ndani ya Yesu)!. Ukitumia  njia nyingine ndio utayaita zaidi badala ya kuyafukuza.

Pili utafanyaje kama tayari umetembelewa na hizi roho(popobawa) na bado zinakusumbua katika mwili na hata katika ndoto?.

Usiende kutafuta msaada kwa waganga wa kienyeji, wala usiende kutangaza…upo usemi kuwa ukienda kutangaza ndio zitaacha..nataka nikuambie tu hazitaacha!..badala yake ndio zitazidi, pengine utaona unafuu kwa kipindi Fulani lakini bado zipo ndani yako na zitaendelea kukutesa. Suluhisho pekee ni YESU KRISTO.

Sasa utaingiaje ndani Yesu Kristo! Ili usalimike na hayo mapepo?(popobawa na mengine) pamoja na kuurithi uzima wa milele.

Hapo ulipo piga magoti peke yako!..Sali sala hii kwa imani…Sema..

 “Bwana Yesu nakuja mbele zako leo, mimi ni mwenye dhambi, naomba nisamehe dhambi zangu zote, nami nawasamehe wale wote walionikosea…naomba nioshe kwa damu yako iliyomwagika pale msalabani…kuanzia leo nakupokea wewe maishani  mwangu.. Nisaidie nisiishi tena katika dhambi,  naomba uniponye na roho zote za adui kuanzia leo, roho zote za uasherati, na nyingine zote zinazoninyemelea, zisinifuate tena… katika Jina lako tukufu, jina la Yesu. Amen”

Baada ya kusali sala hii kwa imani, amini kwamba tayari Bwana Yesu kashaingia ndani yako…kuanzia sasa utaanza kuona kuna amani Fulani inaingia ndani yako..Na yale maroho ambayo leo umeyakana kwa kinywa chako tayari hayana mamlaka tena juu yako, wewe ni mshindi…Hivyo usiishi tena katika dhambi, wala usijiuhusishe na mazingira yoyote ambayo maroho hayo yanayapenda…mazingira kama kwenye disko, mazingira ya kutazama picha za ngono mitandaoni..na mengineyo..Kuanzia sasa tafuta kanisa lolote la kiroho lililo karibu nawe..Nenda huko kuanzia leo..Bwana atazungumza na wewe huko huko kupitia watu utakaowakuta huko. Pia anza kusoma kitabu cha Mathayo ili roho yako ianze kujengeka na kukua.

Bwana akubariki sana.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

CHA KUTUMAINI SINA, Swahili Lyrics. (My hope is built on nothing less)


Tenzi hii iliandikwa na mchungaji wa kanisa la kipatisti, aliyeitwa Edward Mote, raia wa nchi ya uingereza, mnamo mwaka 1834, Edward Mote alifanikiwa pia kuandika tenzi nyingine nyingi Zaidi ya 100, lakini iliyopata umaarufu mkubwa ni hii ijulikanayo kama “Cha Kutumaini sina”.

Tenzi hii aliibuni akirejea ule mfano alioutoa Bwana Yesu wa mjenzi mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba imara, Na yule mpumbavu ambaye aliijenga nyumba yake https://www.high-endrolex.com/2juu ya mchanga (Mathayo 7:24-27), Na kuonyesha ni jinsi gani mtu anapaswa aishi kwa kwa kumtegemea Kristo aliye mwamba salama, na ulio imara.

1Wakorintho 10:4  “wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo”

Na ndio hapo akaundika wimbo huu;

Cha kutumaini sina
Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha
Dhambi zangu kuziosha;

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba; ni salama
Ndiye mwamba ni salama

 

Njia yangu iwe ndefu
Yeye hunipa wokovu;
Mawimbi yakinipiga
Nguvu zake ndiyo nanga.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba; ni salama
Ndiye mwamba ni salama

Damu yake na sadaka
Nategemea daima,
Yote chini yakiisha,
Mwokozi atanitosha.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba; ni salama
Ndiye mwamba ni salama

Nikiitwa hukumuni,
Rohoni nina amani;
Nikivikwa haki yake
Sina hofu mbele zake.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba; ni salama
Ndiye mwamba ni salama

*****

Amen hata mimi na wewe, tukiwa ndani ya Kristo, tupo salama wakati wote, lakini tukimkosa yeye ndani yetu, basi hata kuimba kwetu ni bure, tutakuwa tu sawa na yule mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga..

Hivyo ukiwa unahitaji kuokoka ili Yesu leo awe kweli Mwamba ulio salama, basi fungua hapa kwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAMBA WENYE IMARA

MWAMBA WETU.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/2-swali-kwanini-mtu-atoe-pepo-aombee-wagonjwa-wapone-asikie-sauti-ya-mungu-ikimwambia-hiki-na-kile-kuhusu-watu-na-yeye-mwenyewe-kufunua-siri-za-mioyo-yao-aone-maono-na-kutembea-na-malaika-katika/

Rudi Nyumbani:

Print this post

WEWE NI BWANA UNIPONYAYE.

SALA FUPI YA UPONYAJI!

Zaburi 107:17 “Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao, Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa.
18 Nafsi zao zachukia kila namna ya chakula, Wameyakaribia malango ya mauti.
19 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao”.

(Uimbe wimbo huu uliotungwa na Don Moen, kufuatia Zaburi hiyo)

Mimi ni Mungu nikuponyaye,
Mimi ni Bwana mponyaji wako,
Hulituma Neno langu,
Na kukuponya magonjwa yako,
Mimi ni Bwana mponyaji wako.

Wewe ni Mungu,
Uniponyaye,
Wewe ni Bwana Mponyaji wangu,
Hulituma Neno lako,
Na kuniponya magonjwa yangu,
Wewe ni Bwana mponyaji wangu.

Urudie kwa kadri uwezavyo pale Upitiapo misiba, magonjwa na shida..mwambie “Mungu” wewe ni Bwana uniponyaye,.. wewe ni Bwana uniponyaye..wewe ni Bwana mponyaji. Na nguvu uponyaji utashuka juu yako, na kukuponya na magonjwa uliyonayo  au misiba unayopitia.

“Amen”


Mada Nyinginezo:

UPONYAJI WA YESU.

KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA.

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

UFALME WAKO UJE.

JIFUNZE KUJITOA KWA MUNGU NA KUWA MKARIBISHAJI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?

Shalom karibu tujifunze biblia.

Mojawapo wa uhuru Mungu aliompa mwanadamu ni kuoa/kuolewa…Mtu yeyote anayeoa/kuolewa sawasawa na maagizo ya Mungu (yaani ndoa ya mume mmoja na mke mmoja) basi anabarikiwa.

Mathayo 19:4 “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?”.

Lakini Pamoja na hayo sio lazima pia kuoa au kuolewa kwa sababu maalumu.

Kwamfano biblia inasema katika..

1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. YEYE ASIYEOA hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.

34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. YEYE ASIYEOLEWA HUJISHUGHULISHA NA MAMBO YA BWANA, APATE KUWA MTAKATIFU MWILI NA ROHO. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe”.

Hivyo sababu kuu ya mtu kujizuia kuoa au kuolewa ni ili apate nafasi kubwa ya kujishughulisha na kazi ya Mungu.. Ni kweli Mume au Mke ni msaidizi mzuri pia katika kazi ya Mungu lakini…kuwa kumtumikia Mungu binafsi pia ni vizuri Zaidi.. Kwasababu ukiwa na mke/mume kuna mambo ya kidunia ambayo hautayakwepa…kwamfano vitakuwepo vipindi vya kutunza Watoto, vitakuwepo vipindi vya kutafuta sana vya kidunia ili kuitunza familia na mke au mume. Vitakuwepo vipindi vya kukaa pamoja faragha!..

Huwezi kusema unasafiri miezi 5 mbali na mke/mume wako umeenda kufanya huduma…ni lazima kwa sehemu Fulani utamkwaza tu mwenzako! au utakuwa hujamtendea haki. Na biblia inasema ukishaoa/ukishaolewa..mwili wako ni mali ya mwenzako, huna amri juu ya mwili wako(kasome 1Wakorintho 7:3-5)..Sasa hayo ndio baadhi ya mapungufu katika kuoa/kuolewa.

Lakini usipooa au usipoolewa…utakuwa huru Zaidi..unaweza kufunga safari muda wowote unaotaka kuifanya kazi ya Mungu, unaweza kufunga siku nyingi bila usumbufu, unaweza kwenda kusali mlimani kipindi kirefu au kuhubiri bila kukumbuka una jukumu Fulani umeliacha nyumbani …kadhalika, hutapata usumbufu wa Watoto wanahitaji hiki, wanahitaji kile.. kadhalika hutaishi kwa matakwa ya mtu Fulani, bali kwa kile Mungu anachokuongoza kila mara. Jambo ambalo lina faida katika ufalme wa mbinguni mara dufu kuliko hilo lingine.

Wa kwanza kabisa ambaye tunaona hakuoa na huduma yake iliikuwa na matokeo makubwa sana ni Bwana wetu Yesu. Mwingine ni Paulo ambaye ndiye aliyeandika mistari hiyo hapo juu kwa uwezo wa roho..Paulo hakuwa miongoni mwa Mitume 12 wa Bwana Yesu, lakini alifanya kazi kubwa kuliko hata mitume wa Yesu (kasome1Wakorintho 15:10), na wengine ni Yohana Mbatizaji na Eliya Mtishbi.

Lakini hilo sio lazima na wala sio amri, kwamba kila mtu ni lazima asiolewe/asioe. Ni jinsi mtu aonavyo yeye kwamba anaweza kujizuia au la!…Wapo wanaoweza kujizuia na wapo wasioweza!…Biblia inasema kama huwezi kujizuia ni afadhali uoe/uolewe kuliko kuwakwa na tamaa.

1Wakorintho 7:8 “Lakini nawaambia wale WASIOOA BADO, na wajane, Ni heri wakae kama mimi nilivyo. LAKINI IKIWA HAWAWEZI KUJIZUIA, NA WAOE; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa”……

 

1Wakorintho 7:1 “Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke. 2 Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe”.

Bwana akubariki.

Kumbuka kama unaishi na mwanamke/mwanaume ambaye hamjafunga ndoa..basi mnaishi katika uzinzi!..haijalishi mmeishi miaka mingapi Pamoja, au mmezaa Watoto wangapi..Mnapaswa mkatubu na kufunga ndoa takatifu, mbele ya kanisa la Kristo, ndipo mbarikiwe (na ndoa sio sherehe na matarumbeta)..mmeshaishi miaka yote hiyo, sherehe ya nini tena?..hatua mliyopo ni ya kutubu tu, na kwenda mbele ya kanisa kufungishwa ndoa mbele ya mashahidi na kurudi nyumbani kuendelea na maisha basi haihitaji maandalizi kana kwamba ndio mmketana kwa mara ya kwanza!. Lakini msipofanya hivyo mkifa leo mtahukumiwa, hiyo ni kulingana na maandiko.

Na mwisho kama hujaolewa na unatafuta wa kukuoa..Ni vizuri ukamtafuta kwanza Mwokozi. Kwasababu ukifa leo bila mwokozi utapotea milele, na Zaidi ya yote mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa, hayo mambo yataishia humu humu duniani..miili tutakayopewa tukifika kule haina hisia za kimwili. Huko tutaishi na Kristo milele. Hivyo Wokovu ni muhimu na wa kwanza katika Maisha, hayo mengine ndio yafuate.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana alimaanisha nini kusema JIKANE mwenyewe?(Mathayo 6:24)

 MAVUNO NI MENGI

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

KUOTA UNASAFIRI.

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KITABU CHA UCHAWI.

Kabla ya kutafuta kitabu cha uchawi ni vizuri kufahamu kwanza Uchawi asili yake ni wapi.

Wapo watu wengi mitandaoni, wengine ni wachawi kweli, na wengine ni matapeli, wameandika vitabu wanakuambia ununue, na katika vitabu hivyo, wanaorodhesha njia mbalimbali za kutatua matatizo yako, au njia za kuwapiga maadui zao.. Lakini kabla hujafikiria kuungana nao ndugu yangu, ni vizuri kwanza ukafahamu uchawi asili yake ni wapi?

Uchawi ni kitendo cha kwenda kutafuta msaada kutoka katika mamlaka mengine tofuati na yale ya Mungu  ili kutimiziwa malengo Fulani, ya mwilini au rohoni. Na kama tunavyofahamu hakuna mamlaka mengine yaliyo tofauti na Mungu zaidi ya yale ya shetani.

Kwamfano, unapokuwa na uhitaji labda wa mke, na unaona kwa akili zako huwezi kumpata mwanamke umtakaye, hapo inakugharimu kutafuta msaada kutoka katika mamlaka nyingine..

Ndio hapo yanazuka mambo mawili, aidha uende kwa Mungu, au uende kwa shetani, ukienda kwa shetani utapata maagizo Fulani, yanatoka katika kitabu cha kichawi walichonacho, Vivyo hivyo ukienda kwa Mungu utapokea maagizo kutokana na kitabu kitakatifu cha Mungu kiitwacho BIBLIA.

Lakini jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa, shetani hana lengo lolote zuri  na mwanadamu zaidi ya kumwangamiza, atakupa kwa lengo la kukuangamiza mwisho wa siku, na ukishakufa ni moja kwa moja unakwenda katika moto wa milele..

Zipo shuhuda nyingi za watu waliokwenda kwa waganga, kutafuta msaada wa shetani, lakini mwisho wake wameishia pabaya sana.. Na kibaya zaidi ulimwengu huu wa sasa, watu wengi wanakimbilia humo hawajui kuwa lile ni shimo kubwa sana la mauti..Ambalo ukiingia kutoka huko ni kugumu sana.

Usihatarishe maisha yako, kwa mambo ambayo hayakupeleki popote, Usije ukasema haujaambiwa, kukutana na ujumbe huu ni makusudi kabisa Mungu anakuonya, ikiwa wewe ni mmojawapo unayetafuta kujui kitabu cha uchawi, hizi ni siku za mwisho, biblia inasema hivi..

1Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;”

Unaona, biblia inasema wengi watajitenga na Imani na kusikiliza mafundisho ya mashetani,..Kumbuka Uchawi wa kwanza kabisa ulifanywa na Shetani pale Edeni, Ukitaka kujua uchawi wenyewe ni upi na madhara gani yalitokea baada ya pale..fungua hapa usome..>>>> JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Na ndio maana hata katika Israeli Mungu alipiga kabisa marufu watu wanaofanya uchawi, kwasababu alijua madhara yake kwao.

Kumbukumbu 18:9 “Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.
10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,
11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.
12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.
13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako”.

Hivyo ndugu, usifirie kutafuta eti hicho kinachoitwa kitabu cha uchawi, Ni heri utubu dhambi zako leo umgeukie YESU KRISTO, haijalishi wewe utakuwa ni muislamu, au mhindu, vyovyote vile, ukimpa Yesu maisha yako leo atakuokoa na kukupa uzima wa milele. Na atakupa pia vile vitu ambavyo ulikuwa na haja navyo kwa wakati wake.

Hivyo kama upo tayari leo kufanya hivyo, na unahitaji kuyakabidhi maisha yako kwake, basi fungua hapa kwa ajili ya sala ya Toba na Mungu akubariki..>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Pia unaweza pia kufungua na masomo mengine hapa chini ujifunze, naamini yatakutoa sehemu moja hadi nyingine kiroho.

Mada Nyinginezo:

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIAMA KINATISHA.

Ikiwa leo hii Unyakuo utapita, na wewe ukabaki, basi fahamu dunia itakuwa na miaka 7 tu mbele yako kabla haijaisha, yaani kama leo ni mwaka 2020, basi haitapita mwaka 2027, kabla ya kila kitu unachokiona leo hii kuwa jivu.. Miaka hiyo saba imepatikana kutoka katika ule Unabii wa Danieli wa yale majuma 70, (Danieli 9:24) ambapo mpaka sasa limebakia juma moja tu, lenye miaka 7 kuanza.

Sasa katika hicho kipindi cha miaka 7 dunia haitakuwa tu umestarehe ikisubiria mwisho ufike hapana.. Kutaanza kuwa na mabadiliko ya haraka na ya ghafla sana duniani, jambo ambalo litawashitusha wengi, hapo ndipo ule unabii wa Bwana Yesu unaosema siku hiyo itawajilia kwa ghafla utakapotimia (Luka 21:34-35), kama tu unavyoona huu ugonjwa wa Corona ulivyoijilia hii duniani kwa ghafla bila taarifa, ndivyo itakavyokuwa hicho kipindi.

Miaka hii 7 inajulikana kama miaka ya dhiki, na imegawanyika katika vipengele vikuu viwili, Kipengele cha kwanza, ni cha miaka 3 na nusu, ya kwanza, na cha pili ni miaka 3 na nusu ya mwisho.

Sasa katika hiyo miaka mitatu na nusu ya kwanza, kitakuwa ni kipindi cha mpinga-kristo, kujiimarisha, na kuingia agano na watu(mataifa mengi),Danieli 9:27, ikiwemo taifa la Israeli,.na wakati wa watu kupokea chapa. Lakini wakati huo huo Wale manabii wawili (Mashahidi 2), tunaowasoma katika ufunuo 11, watasimama kuihubiria Israeli, kwa muda huo wa miaka mitatu na nusu ya kwanza,.Injili yao haitakuwa ya maneno matupu tu, bali itafuatana na mapigo kadha wa kadha mwishoni mwishoni karibia na kumaliza ushuhuda wao, soma Ufunuo 11, mapigo hayo yatakuwa ni makali na ya kutesa kiasi kwamba siku mpinga-Kristo atakapowaua, dunia nzima itafurahia tukio hilo na kuepelekeana zawadi wao kwa wao.

Sasa hiyo miaka 3 na nusu ya mwanzo itakapokwisha, Mpinga-Kristo atakuwa ameshapata nguvu za kutosha, wakati huo, ndio atanyanyuka sasa, kuleta dhiki kuu juu ya wale wote ambao hawatakuwa na chapa/Utambulisho wake (666).. Hapa hatanusurika mwanadamu yeyote ulimwenguni aliyeikwepa chapa hiyo, kutakuwa na mawili aidha upokee chapa, au ufe.. Na kifo sio cha kupigwa risasi au kunyongwa…Ni heri ingekuwa hivyo!…lakini kifo watakachokufa wale walioikataa chapa kitakuwa ni cha kuteswa mda mrefu sana…Watu watateswa hata kwa mwaka mmoja au miwili bila kuruhusiwa wafe…Ni mateso ya kuwekwa kwenye kambi maalumu za mateso..yale ya kale ambayo unatolewa macho, unavuliwa nguo, wakati wa baridi..halafu unafanyishwa kazi ngumu, huku unapewa mlo mmoja kwa wiki,(na mlo wenyewe ni supu tu) na huku unachapwa na viboko, yatakuwa ni mateso madogo sana…Watu watatamani wafe huko lakini hawatakufa..watateseka katika hiyo hali hata kwa miaka miwili ndio uje wafe!…

Bwana Yesu alisema dhiki hiyo ambayo itakuja kutokea haijawahi kutokea tangu dunia iumbwe na wala haitakaa itokee tena baada ya hapo.. Kiasi kwamba watakaowezi kuyastahimili hayo watakuwa ni watu wachache sana, wengine wote wataipokea chapa ya mnyama. Na jambo hilo litaendelea kwa muda wote wa miaka mitatu na nusu ya mwisho.

Hapo katika kutakuwa ni mapigo mengine mengi sana, mapigo ya baragumu saba yataendelea..na mapigo ya vitasa saba vya Mungu nayo pia yatafuata, mwishoni mwa miaka mitatu na nusu, kwa urefu wa somo hili fungua hapa >> SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!..hatuwezi kueleza yote hapa sehemu moja.

Sasa mwisho kabisa ya dhiki hizo kupita, unaweza kudhani, mambo ndio yamekwisha?, Wale waliopokea chapa, basi wamepona,? Hapana, ndugu kinyume chake huo ndio mwanzo wa ukurusa mwingine ujulikanao kama SIKU YA BWANA.

Hii siku ya Bwana, itakuwa ni kipindi cha siku 30 nyingine juu ya ile miaka saba kupita…Watu watadhani kuipokea chapa ndio kupona, lakini ni sawa na mtu aliyemkimbia Simba akakutana na dubu biblia inasema hivyo..ni heri wangekufa kwenye dhiki kuu ya mpinga-Kristo.

Amosi 5:18 “Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru.

19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma”.

Hichi kipindi watakaokuwepo duniani hawataamini macho yao, watashikwa na butwaa la ajabu, kwasababu, watashuhudia hii dunia ikigeuzwa na kuwa kama mojawapo ya sayari Fulani huko angani isiyokaliwa na watu, Kwasababu hili jua tunaloliona litazimwa lote, (kutakuwa na giza kubwa) mwezi utakuwa mwekundu kama damu, nyota zote zitaondoka huko mbinguni kutakuwa na giza tororo ambalo halijawahi kutokea duniani…

Amosi 5:20” Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga”.

Lengo la siku hiyo ya Bwana, ni kuifanya dunia kuwa ukiwa kama tulivyoikuta siku ile ya uumbaji..Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. NAYO NCHI ILIKUWA UKIWA, TENA UTUPU, NA GIZA lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji”

Hivyo dunia itafanywa ukiwa tena..

Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ILI IIFANYE NCHI KUWA UKIWA, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.

11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;

12 nitafanya wanadamu kuadimika kuliko dhahabu safi, na watu kuliko dhahabu ya Ofiri”.

Siku hii itaambatana na tetemeko kubwa la Ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu dunia iumbwe, visiwa vitahama,..

Ufunuo 16:18 “Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo.

19 Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake.

20 Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.

21 Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno”.

Unaona, tutakayokuwa yanaendelea kwenye hii dunia wakati huo?? Ndugu kuna vifungu vingi sana vya kuandika hapa,vinavyoilezea hii siku ya kuogofya ya Bwana, lakini hatuwezi kuviorodhesha vyote, kwa muda wako pitia vifungu hivi (Yoeli 1:15, Yoeli 2:1, 2:11, Yoeli 3:14),

Sasa baada ya hayo kupita, Ndipo Kristo atatokea mawinguni, Na kila jicho litamwona, naye atawaua waliosalia na majeshi yao, na kumaliza kila kitu, wale waovu waliosalia (Mathayo 24:29-30, Ufunuo 19:11-21)..

Na baada ya hapo kutakuwa ni siku nyingine 45, juu ya zile siku 30, ambapo ndani ya siku hizo, wafu watafufuliwa watawale pamoja na yeye, pamoja na ile hukumu ya mataifa ya kuwatenga kondoo na mbuzi, na katika kipindi hicho hicho Kristo ataitengeneza tena hii dunia upya, Nayo itakuwa nzuri zaidi ya Edeni, nasi tutawala naye kwa kipindi kingine cha amani cha miaka 1000, wakati huo hakuna mwovu yoyote, ayatakayenusuruka..

Sasa hapa tumefupisha tu, unaweza kudhani kama hizi ni hadithi tu, au mambo hayo bado sana, yatachukua mamia ya miaka huko mbeleni, Lakini fahamu kuwa hivyo ndivyo shetani anavyotaka ujue ili siku ile ikujie kwa ghafla..Lakini maandiko yanakuambia hivi..

Sefania 1:14 “Hiyo siku ya Bwana iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya Bwana; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko!

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,

16 Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.

17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.

18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha”.

Tusiwe na mengi ya kusema, ila ombi langu ni kuwa kama hujampa Kristo maisha yako, basi fanya uamuzi huu haraka, Kumbuka anakupenda sana, anakujali sana, anakuthamini, na anatamani sana uyarithi aliyokwenda kukuandalia miaka 2000 iliyopita kule juu mbinguni..Kwa muda wote huo! Ni lazima ni mambo mengi na mazuri aliyotuandalia….Wokovu wake ni bure, tena unapatikana sehemu yoyote, bila malipo. Fanya hivyo naye atajifunua kwako. (kiama kinatisha!)

Bwana akubariki, Bwana atubariki sote.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

Kabla ya kufahamu ubatizo ni nini…Hebu jiulize mtu katokea na akakuuliza “kuzamisha maana yake ni nini?”..utamjibuje?…Bila shaka utamwelezea kwa kina kwamba ni kitendo cha kukitosa kitu chote kwenye kimiminika Fulani au kitu Fulani, pasipo kubakisha sehemu ambayo ipo wazi. Meli iliyopata ajali na kushuka chini ya bahari, tunasema meli hiyo imezama baharini. Mtu anayechimba shimo la taka akachimba chini sana na kuzitupa humo na kuzifukia, hapo ni sawa na kusema kazizamisha/kazizika.

Sasa mpaka hapo tutakuwa tumeshajua maana ya neno “KUZAMA au KUZAMISHA”..Sasa ukilichukua neno hilo “kuzamisha”  ukalitafsiri kwa lugha ya kigiriki linakuwa ni BAPTIZO…Ni sawa uchukue Neno la kiswahili “kanisa” na kulitafsiri kwa kiingereza na kuwa “CHURCH”…Vivyo hivyo Neno “kuzamishwa” likitafsiriwa kwa kigiriki linakuwa ni Baptizo..neno hilo hilo likipelekwa kwa lugha ya kiingereza linakuwa ni “IMMERSION”..na linaweza kutafsiriwa kwa lugha mbali mbali..

Kwahiyo mtu anayesema “leo naenda chachi”..ni sawasawa na mtu aliyesema “leo naenda kanisani”…neno “chachi” sio Kiswahili, na wala sio kiingereza fasaha lakini utakuwa umemwelewa amemaanisha nini kusema hivyo.

Vivyo hivyo mtu akikuambia “leo nime batizwa kwenye maji” utakuwa umemwelewa kwamba amemaanisha leo kazamishwa kwenye maji…kwa lengo Fulani.. (katumia tu msemo wa kigiriki lakini utakuwa umeshamwelewa).

Kwahiyo mpaka hapo utajua kuwa hakuna mtu atakayekuambia kwamba kabatizwa kwenye maji halafu awe “amenyunyuziwa”…Mtu aliyenyunyuziwa hajabatizwa!…kwasababu kubatizwa sio kunyunyuziwa bali kuzamishwa kabisa. (mpaka hapo tutakuwa tumeshaelewa ubatizo ni nini)

TUKIRUDI KATIKA IMANI YA KIKRISTO.

Katika imani ya kikristo, yapo mambo ambayo yanafanyika kama ishara lakini yanafunua kitu kikubwa sana katika roho. Kwamfano utaona Bwana Yesu alitoa maagizo ya kushiriki meza ya Bwana, ambapo wakristo wakutanikapo wanakula mkate pamoja na divai. Hivyo ni vyakula vya kimwili lakini vinapolika kwa maagizo hayo ya Bwana Yesu vinakuwa vinafunua vitu vingine katika roho. Kwamba ni sawa na tunainywa damu ya Yesu na Mwili wake katika ulimwengu wa roho. Na alisema mtu asiyefanya hivyo basi hana uzima ndani yake. (maana yake hana ushirika na Yesu).

Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu”.

Umeona ni agizo dogo tu, la kula chakula cha kimwili, lakini lina maana kubwa sana katika roho, sio la kulipuuza wala la kulifanya isivyopaswa…Na hapo hajasema tuonje!..bali tuule..

Kadhalika Bwana Yesu alitoa maagizo mengine yanayofanana na hayo ya watu kuzamishwa katika maji kwa jina lake (au kirahisi kubatizwa), ambapo alisema kwa kufanya hivyo katika mwili..kunafunua jambo kubwa sana katika roho, ambalo jambo lenyewe ni “kufa na kufufuka pamoja naye”

Wakolosai 2:12 “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu”.

Umeona na hapo?..maana yake usipobatizwa (yaani kuzamishwa katika maji)..basi katika roho bado hujafa wala kufufuka pamoja naye…wewe bado si wake!. Vile vile kama hujazamishwa na badala yake umenyunyuziwa hapo bado hujabatizwa, unapaswa ukabatizwe tena katika maji mengi.. kwasababu ndio tafsiri ya neno ubatizo.

Sasa yapo maswali machache machache ya kujiuliza?

Je ina maana kama mtu hajabatizwa katika maji mengi na badala yake katika kunyunyiziwa hawezi kwenda mbinguni?..Na kama hawezi vipi Yule mwizi aliyesulibiwa na Bwana pale msalabani..mbona yeye aliokolewa na wala hakubatizwa?..mbona wakina Musa hawakubatizwa?…mbona wakina Eliya hawakubatizwa?…Majibu ya maswali haya yote utayapata hapa >> Mtu akifa bila kubatizwa atakwenda mbinguni?

Hivyo ndugu mpendwa kamwe usiudharau “ubatizo”..kama bado hujaelewa kwa undani ubatizo ni nini, na umuhimu wa ubatizo tafadhali rudia kusoma tena taratibu na nakuomba chukua muda mwingi…katafute kuuliza huko na huko na pia piga magoti peke yako mwulize Roho Mtakatifu, halafu kasome biblia yako atakupa majibu.

Na ubatizo sahihi ni wa Jina la Yesu kulingana na mistari hii; Matendo 2:38, 8:16,10:48 na 19:5. Jina la Yesu ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kufahamu haya zaidi fungua masomo mwisho kabisa mwa somo hili (sehemu ya chini)..yanaelezea kwa kina masuala ya ubatizo.

Bwana akubariki.

Kama hujampokea Yesu saa ya wokovu ni sasa. Kristo yupo mlangoni kurudi kuwachukua wateule wake..hivyo ingia leo ndani ya neema hii, kabla mlango wa neema haujafungwa. Yesu anakupe


nda na anataka kukupa raha nafsini mwako leo kama utamkubali…sawasawa na neno lake hili..

Mathayo 11: 28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:

BIBLIA TAKATIFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post