Title 2020

USISUBIRI MPAKA MUNGU AKUAMBIE, NDIO UFANYE!

Unajua ni kwanini Daudi alipewa jina kuu na kubwa kuliko wafalme wote na watu wote waliomtangulia katika Israeli? Ni kwasababu kuna kipindi aliwaza, Mungu amenipa vyote, amenipa ufalme, amenipa uongozi bora juu ya Israeli yote, amenipa nyumba nzuri ya kukaa, lakini mbona ni mimi tu ananifanyia wema, na mimi simfanyii chochote?. Akatazama huku na kule, akaangalia ni wapi pamepunguka, akagundua kuwa Mungu hana maskani yoyote ya kukaa, akatazama akaona lile sanduku la agano la Mungu linakaa kwenye mapazia, katika giza nene (1Wafalme 8:12) kwenye vihema vilivyochoka na kuchakaa..

Akajiwazia tu moyoni akasema hii haiwezekani, nitamjengea Mungu nyumba ya kukaa..

Lakini biblia inatuambia usiku huo huo Neno la Mungu lilimfikia Nadhani nabii wa Mungu, kwa Daudi kumwambia kwamba Mungu anasema: Je nilishawahi kusema Neno lolote kwa mwamuzi yoyote wa Israeli juu ya kujengewa mimi nyumba? Nilishawahi kumdokeza Yoshua juu ya jambo hilo? Nilishawahi kumdokeza Gideoni kuhusu kunijengea nyumba, Au Samsoni, au Ehudi au Yeftha, au Samweli juu ya jambo hilo?

Kwa namna nyingine Bwana alikuwa anamaanisha kumwambia Daudi hivi..

Sikuwahi kuwauliza chochote, ili nisionekane kama nawalazimisha, bali niliwaacha wao wenyewe waligundue hilo, lakini hakuna hata mmoja aliyelijali jambo hilo isipokuwa wewe Daudi, Sasa Basi kwa kuwa umefikiria hivyo, kunipa heshima, kunitoa katika giza nene, kwenye vihema vibovu, mimi nami nitakupa jina kuu sana, na sehemu nzuri Zaidi.

2 SAMWELI: MLANGO 7

1 Ikawa, mfalme alipokuwa akikaa katika nyumba yake, hapo Bwana alipomstarehesha, asiudhiwe na adui zake waliomzunguka pande zote,

2 mfalme akamwambia Nathani, nabii, Angalia sasa, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi, bali sanduku la Mungu linakaa ndani ya mapazia.

3 Nathani akamwambia mfalme, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; maana Bwana yu pamoja nawe. 4 Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema,

5 Enenda, ukamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Je! Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake?

6 Kwa maana mimi sikukaa ndani ya nyumba, tangu siku ile niliyowatoa wana wa Israeli katika Misri, hata leo, lakini nimekaa katika hema na maskani.

7 Mahali mwote nilimokwenda na wana wa Israeli wote, je! Nimesema neno lo lote na mtu ye yote wa waamuzi wa Israeli, niliyemwagiza kuwalisha watu wangu Israeli, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mierezi?

8 Basi, sasa, mwambie mtumishi wangu, Daudi, maneno haya, Bwana wa majeshi asema hivi, Nalikutwaa katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo, ili uwe mkuu juu ya watu wangu, juu ya Israeli;

9 nami nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote mbele yako; NAMI NITAKUFANYIA JINA KUU, KAMA JINA LA WAKUU WALIOKO DUNIANI”.

Na tunaona Daudi alianza maandalizi yote ya ujenzi wa hekalu la Bwana, na mwanawe Sulemani akaja kulimalizia..

Sasa leo hii sisi ndio tunaojua vizuri ni jinsi gani Mungu amempa Daudi jina kuu kuliko wengine wote waliomtangulia.. (hata Bwana wetu Yesu katokea katika huo huo uzao wa Daudi katika mwili) Lakini hiyo yote ni kutokana na kwamba hakusubiri aambiwe ndipo afanye..

Hata leo hii, zipo kazi za Mungu nyingi sana zimepwaya, Na Mungu amekaa kimya anaangaalia, wala hasemi chochote, Ni kweli ataendelea kuwa na sisi kama Watoto wake, kama watumishi wake, atatutumia sisi kama manabii wake, mfano wa Samweli, Lakini kama hatutachunguza na kuchukua hatua ni wapi palipopunguka, tusitazamie kamwe kama Mungu siku moja atakuja kutuambia naomba unifanyie hiki au kile.

Vivyo hivyo ikiwa wewe umeokoka, na unajua kabisa ni jukumu lako kumtolea Mungu, kamwe usidhani ipo siku Mungu atakuuliza mbona hujanitolea, au mbona hujanifanyia hichi au kile….hilo jambo hawezi kufanya kabisa, wewe ndio unapaswa ulitambue hilo si yeye.

Unajua kabisa unapaswa ukaisambaze injili kwa wengine kwa karama Mungu aliyoiweka ndani yako, halafu unasubiria siku moja Mungu akutokee akwambie nenda kahubiri, hilo wazo lifute kabisa, ni rahisi kumwambia yule ambaye ndio kwanza anaingia kwenye wokovu lakini wewe ambaye umeshakaa miezi, na miaka, na huna ushuhuda wowote, unasubiri siku moja Mungu akuambie uipeleke Habari njema katika maono, hawezi kufanya, kwasababu anajua kabisa unajua jukumu lako, kwanini tena akuambie, si itakuwa kama anakulazimisha?..

Pale tunapochukua hatua ndipo hapo Mungu anatuongezea na hatua nyingine..(Usisubiri mpaka Mungu akuambie)

Hivyo siku ya leo ya tarehe hii na mwezi huu, biblia inatufundisha kuwa na jicho kama la Daudi, ili na sisi pia Bwana atupe jina lililo kuu huku na kule ng’ambo tutakapofika.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona?

JE MUSA ALIFIA WAPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu.

SWALI: Huu mstari una maana gani? Mhubiri 3:16-17 “Zaidi ya hayo,nikaona tena chini ya jua ya kwamba,Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu.17 Nikasema moyoni mwangu,Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki, kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi”.


JIBU: Hizi ni hekima zilizoandikwa na mfalme Sulemani ambae alimwomba Mungu ampe hekima badala ya Mali (Jambo la kwanza na la muhimu sana ambalo na sisi pia tunapaswa tuanze kumwomba Mungu)..

Hapo katika mstari huo anasema kwa hekima ya Roho “nikaona tena chini ya jua ya kwamba,Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu”….Zingatia hapo anaanza na neno “NIKAONA CHINI YA JUA!”..Maana yake sio mbinguni, bali ni duniani. Ikiwa na maana kuwa mbinguni mahali pa haki hapana udhalimu, vilevile Hukumu za mbinguni Mungu alipo hazina uovu,

Ayubu 34:12 “Naam, hakika, Mungu hatatenda mabaya, Wala Mwenyezi hatapotosha hukumu”.

Lakini kinyume chake hukumu za duniani (chini ya jua) ndizo zenye uovu, na haki za duniani ndio zina udhalimu…Kama Mhubiri anavyosema hapo juu.

Na hiyo ni kweli kabisa..je! huoni leo, hata mahakamani (mahali ambapo pangepaswa kutolewa hukumu ya haki)..wapo mahakimu wanaopotosha hukumu?..wanaopokea rushwa na kumnyima haki yule anayestahili haki, na kumpatia yule asiyestahili?..na wapo wengi wanaopewa kesi ambazo sio zao kwasababu tu ya rushwa..n.k

Kwahiyo ni kweli kabisa chini ya jua na si mbinguni…hukumu nyingi zinapotoshwa!..Mahali ambapo ni pa hukumu kuna uovu na mahali pa haki kuna udhalimu…mahali ambapo mtu anapaswa apate haki, ananyimwa haki yake.

Na ndio maana katika mstari wa mwisho kabisa amesema.. “Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki”. Maana yake ni kwamba Wale wanaosimamia haki duniani kama mahakimu watasimama katika kiti cha hukumu pia kutoa hesabu ya uhakimu wao, kadhalika na wasio haki(maana yake waovu wote) pia watasimama mbele ya kiti cha hukumu) siku ile ya mwisho, na kila mtu atahukumiwa kulingana na matendo yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/maana-ya-huu-mstari-ni-ipi-mithali-144-zizi-ni-safi-ambapo-hapana-ngombebali-nguvu-za-ngombe-zaleta-faida-nyingi/

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

BWANA AKAMWAMBIA SHETANI, BWANA NA AKUKEMEE EWE SHETANI;

Rudi Nyumbani:

Print this post

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

Na upepo wa kusi ulipoanza kuvuma kidogo, wakidhani ya kuwa wamepata waliyoazimu.


Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Si kila dalili nzuri inayoonekana mbele yetu, itatuletea mwisho mwema, Kama hatutakaa chini kutaka kutafuta mashauri ya Mungu, tuwe na uhakika kuwa kuna uwezekano mkubwa sana wa kupotea..Kama vile biblia inavyotuambia katika…

Mithali 14:12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”.

Tukiiangalia mfano ile safari ya Mtume Paulo kutoka Yerusalemu kwenda Rumi kama mfungwa, haikuwa safari ya kawaida, kama sio neema ya Mungu tu kuwa pamoja na Paulo basi asingenusurukia mtu yeyote kwenye ile safari waliyosafiri yeye pamoja na wafungwa wengine, pamoja na maasakari wote na manahodha wote..Lakini hiyo yote ilisababishwa na wengi wao kuyadharau mashauri ya Mungu na kuyafuata mawazo yao wenyewe na akili zao wenyewe zinavyowatuma.

Kwani walipofika kwenye kisiwa kimoja kinachoitwa bandari nzuri, walitulia pale kwa muda wakingoja hali iwe shwari kidogo kisha waanze safari tena, Lakini ghafla kukaanza kuvuma upepo mzuri sana unaovutia ujulikanao kama upepo wa Kusi , Upepo huu ukivuma basi manahodha huwa wanafurahi kwasababu ni upepo rafiki kwa kusafiria baharini, na zaidi ya yote unawafanya safari yao kuwa nyepesi Zaidi na isiyogharimu.. Lakini Mtume Paulo kwa kuonywa na Roho aliwaambia wasisafiri, kwani mbeleni alionyeshwa watakumbana na madhara makubwa ambayo sio tu ya kupoteza shehena na merikebu bali yatahatarisha pia na maisha yao… Jambo hilo Yule Akida wa askari wala hakulizingatia, kwani aliyasikiliza zaidi mashauri ya mabaharia ambao wao kila siku wapo vilindini wenye uzoefu wa mambo hayo, pengine akajisemea moyoni huyu mfungwa maskini anatueleza nini..

Lakini biblia inatuambia walipoondoka tu kwenye kisiwa kile, hawakufikia hata mbali ule upepo wa kusi uligeuka na kuwa upepo wa Tufani wa aina nyingine ujulikanao kama Eurakilo.

Matendo 27:13 “Na upepo wa kusi ulipoanza kuvuma kidogo, wakidhani ya kuwa wamepata waliyoazimu kupata, wakang’oa nanga, wakasafiri karibu na Krete pwani kwa pwani.

14 Baada ya muda mchache ukavuma upepo wa nguvu wa namna ya tufani, uitwao Eurakilo,

15 merikebu iliposhikwa, na kutoweza kushindana na upepo, tukaiacha tukachukuliwa”.

Tufani ya namna hii ikikukumba ukiwa katikati ya bahari basi kupona hapo ni jambo ambalo haliwezekani, tufani za namna hii huwa zinakwenda kuathiri mpaka makazi ya watu nchi kavu, sasa jiulize kwa wale waliokuwa baharini ilikuwaje?..Na ndio maana ukisoma pale utaona jinsi safari ile ilivyowagharimu sana maisha,baada ya merikebu kuvunjwa, Kama sio mwenye haki mmoja kuwepo kwenye ile meli asingepona mtu kabisa..

Hayo ni mambo ambayo tunapaswa tujifunze katika maisha, tunaweza tukawa tunauzoefu mwingi wa kimaisha, tunaweza tukawa na ujuzi Fulani wa mambo, lakini tusipokaa chini na kuyatafuta mapenzi ya Mungu katika maisha yetu, badala yake tukawa tunagemea akili zetu tu, ziamue kila jambo..tufahamu kuwa Eurakilo ipo mbele yetu..siku moja itatuangamiza tu.. Haijalishi hapo mwanzo zilishatusaidia mara ngapi, ipo siku tutanasika tu.

Tunaweza tukasema mbona jambo hili au shughuli hii, inauelekeo wa kunifikisha ninapotaka kufika? Ndugu je kabla hujaliendea ulishawahi kumshirikisha kwanza Mungu? Kama ni mapenzi yake au la?

Madhara ya kutomshirikisha Mungu njia zetu ni Mengi sana.. Na mojawapo ni ghafla tu tutajikuta tumepotea, tukiangalia kumbe ni mambo Fulani yalituponza mpaka tukafikia pale.

Hivyo maandiko haya matatu yakiwapo akilini mwetu, basi kuna uwezekano mkubwa wa kuufikia mwisho mwema..

  1. Mithali 14:12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”.

Na hili..

  1. Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako”.

Na la mwisho ni hili…

  1. Mithali 16:3 “Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika”.

Bwana atubariki na kutuongoza katika njia zetu katika Jina la Yesu Kristo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Maadamu tunaishi hapa duniani, kila siku tupo mapambanoni….Unapomwamini Yesu Kristo tu na kuamua kumfuata kwa moyo wote, kwa kitendo hicho tu tayari umeshatangaza vita na ufalme wa giza..Na vita hivyo huna budi kuvikabili mpaka siku unaondoka hapa duniani. Hakuna siku hivi vita vya imani vitaisha..utapitia hiki, utatulia kidogo ghafla kitanyanyuka kingine, lakini Bwana atakuwa upande wako kukupa ushindi. Lakini shetani huwa hakati tamaa kama sisi wanadamu…Kuanzia mwanzo wa safari yako mpaka mwisho utakuwa vitani tu!…kwahiyo jiandae kwa hilo…Kama alikupa shamba wakati ukiwa wake, leo umemsaliti atalidai shamba lake, kama alikupa heshima hiyo heshima atakunyang’anya na atawatumia watumishi wake.

Tunaweza kujifunza kwa ufupi kwa Bwana wetu Yesu, jinsi shetani alivyoanzana naye kwenye huduma yake na alivyomaliza naye. Inadhaniwa na wengi kuwa siku ile shetani alipomjaribu Bwana kule jangwani ndio ilikuwa mwisho wa majaribu.. Lakini nataka nikuambie sivyo!…Ndio ilikuwa ni mwanzo tu wa majaribu…ingekuwa ndio ilikuwa mwisho sidhani kama Bwana angesulubiwa…Hebu tusome.

Luka 4:12 “Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

13 Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha AKAENDA ZAKE KWA MUDA”.

Nataka uone hicho kipengele cha mwisho kinachosema “akaenda zake kwa muda!”…Maana yake ni kwamba atarudi tena baadaye!. Anakwenda kuandaa vita vingine vipya..hivyo kakubali kashindwa lakini hiyo haimpi sababu ya kukata tamaa…Na utaona aliporudi tena alirudi kwa nguvu nyingi akishindana na Bwana kupitia watu na wakuu…Aliwavaa mpaka viongozi wa dini wakubwa, na wakuu wa nchi kupambana na Yesu…Mpaka ilifikia wakati mfalme Herode anatafuta kumuua Bwana Yesu. Hebu jiweke kwenye nafasi kama hiyo,!..viongozi wa dini wanakupinga! Na bado mkuu wa nchi anatafuta kukuua?..Bila shaka hivyo ni vita vikali sana..

Na haikutosha hapo, kuonyesha jinsi gani shetani hakati tamaa…japokuwa alimshindwa, lakini bado hata wakati yupo pale msalabani anamjia tena na kumwambia maneno yale yale kama aliyomwambia kule jangwani… “ikiwa kweli wewe ni mwana wa Mungu jishushe msalabani!”…bado anaamini anaouwezo wa kumwangusha Bwana hata akiwa bado amebakisha dakika moja ya pumzi ya uhai wake…Mpaka sekunde ya mwisho Bwana yupo vitani.. Na ndio maana Bwana aliwaambia hivi wanafunzi..

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Sasa dhiki inayozungumziwa hapo ndio hayo majaribu…Na mfano wa dhiki hizo sio kuvunjiwa bar yako iliyokuwa inakupatia kipato, au kuibiwa fedha zako na mfanyakazi wako wa Bar!…au kupigwa baada ya kufumaniwa, au kuingizwa jela baada ya kushikwa unaiba!… Hapana hizo sio dhiki(sio vita vya imani) bali ni majibu ya dhambi zako!…Dhiki hasa ni zile unazozipitia baada ya wewe kuukataa ubaya!..mfano unafukuzwa kazi kwasababu umekataa kufanya uasherati, unasingiziwa kitu Fulani kwasababu umekataa kwenda katika njia zao, unachukiwa na kutengwa kwasababu umebadilisha njia zako na umeacha kuwa wa kidunia au kuabudu sanamu, au mizimu au kufanya matambiko…Mfano wa dhiki hizo ndio majaribu..

Kwasababu majaribu haya yataendelea mpaka mwisho wa maisha yetu!..biblia inatuonya TUVUMILIE! Na TUSTAHIMILI na pia tusiogope!…kwasababu Bwana atakuwa upande wetu kutusaidia tukijua kuwa lipo taji la uzima linatungojea huko mbeleni.

Yakobo 1:12 “Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea TAJI YA UZIMA, Bwana aliyowaahidia wampendao”.

Ufunuo 2:9 “Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.

10 USIOGOPE MAMBO YATAKAYOKUPATA; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa TAJI YA UZIMA”.

Bwana akubariki.

Kama hujaokoka, mlango wa neema upo wazi..lakini hautakuwa hivi siku zote…nyakati hizi muda unaenda kwa kasi sana…kufumba na kufumba dunia itaisha..na utaanza utawala mpya wa Bwana wetu Yesu Kristo..ambapo Huko atawalipa watakatifu wake kwa kadri ya Uvumilivu wao…Waliostahimili zaidi watapewa thawabu kubwa zaidi..Bwana atusaidie tufike huko.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE UNAMTHAMINI BWANA?

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

JE! KUBET NI DHAMBI?

Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BWANA AKAMWAMBIA SHETANI, BWANA NA AKUKEMEE EWE SHETANI;

Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Tunaweza kujiuliza maswali mengine ni kwanini mara nyingi malaika walipokuwa wakishindana na shetani, hawakutumia uweza wao wote kupambana naye,bali walimwachia Mungu aamue, japokuwa walikuwa na mamlaka na uwezo wa kufanya lolote juu yake..

Tunaweza kuona baadhi ya maeneo katika biblia, kwamfano kama lile tukio la Yoshua kuhani mkuu alipokuwa anahudumiwa na Yule malaika, na shetani naye akiwa pembezoni mwao kulipinga kusudi la Mungu..Utaona pale yule malaika hakutoa maneno ya kulaani , japokuwa ibilisi ni mlaaniwa sikuzote..bali alisema..

Zekaria 3:1 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye.

2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni”?

Unaona? Sehemu nyingine tena ni pale Mikaeli alipopewa jukumu la kuuhifadhi mwili wa Musa, lakini shetani akatokea ghafla ili kushindana naye lakini utaona hakudiriki, kumtamkia hukumu palepale, japokuwa tayari ibilisi ni mlaaniwa, badala yake alimkabidhi Mungu hukumu yote..

Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee’.

Kama hilo halitoshi, malaika watakatifu bado, wanapotuona tunafanya mambo yasiyompendeza Mungu, wanaporudisha ripoti mbinguni juu ya mienendo yetu duniani, wanapofika mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, hawatupelekei yale mashitaka mabaya kwa Mungu, wanajaribu kuyasitiri kwa kadiri wawezavyo, Uone jinsi wanavyoogopa hata kutoa neno la laana kwa kiumbe chochote cha Mungu kiwe ni kizuri au kibaya..

2Petro 2:11 “Wenye ushupavu, wenye kujikinai, hawatetemeki wakiyatukana matukufu; IJAPOKUWA MALAIKA AMBAO NI WAKUU ZAIDI KWA UWEZO NA NGUVU, HAWALETI MASHITAKA MABAYA JUU YAO MBELE ZA BWANA.

12 Lakini hao kama wanyama wasio na akili, ambao walizaliwa kama wanyama tu wa kukamatwa na kupotezwa, wakikufuru katika mambo wasiyoyajua, wataangamizwa katika maangamizo yao”

Hiyo ni kutufundisha na sisi pia tunavyopaswa tuchukuliane na maadui zetu mbele za MUNGU, Pale wanaposhindana na sisi, Je na sisi tushindane nao kwa kuwalaani au kuwalaumu?..Pale unaposikia umesengenywa kidogo je na wewe uende kuwaombea mabaya mbele za Mungu, wapigwe? Je! wewe ni mtu wa kupeleka mashitaka tu kila siku zote mbele za Mungu..Huna lingine..?

Wapigwe, waangushwe, warudishwe nyuma, wafedheheshwe, ni hayo tu ndio tunayoweza kumwambia Mungu kwenye maombi yetu ya kila siku?, Hatuna Muda wa kumuomba Mungu ufalme wake uje juu ya roho zetu kama Bwana alivyotufundisha, sisi ni kushindana na maadui zetu ?

Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.

10 Lakini watu hawa huyatukana mambo wasiyoyajua, na mambo wayatambuayo kwa asili wajiharibu kwayo kama wanyama wasio na akili.

11 Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya Kora”.

Kaka/Dada watu watakaokwenda kinyume na wewe watakuwepo tu daima kutupinga, lakini sisi tumwachie hayo Mungu ayashughulikie kama wafanyavyo malaika, tuendelee na kusudi lililotuleta hapa duniani la kumtafuta Mungu na hiyo ndio ishara nzuri ya unyenyekevu tunayopaswa tuige kwa malaika watakatifu dhidi ya maadui zetu (wanadamu).

Mithali 24:17 “Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM

Rudi Nyumbani:

Print this post

Usimwache mwanamke mchawi kuishi! Biblia ilimaanisha nini?

SWALI: Nina swali juu ya uchawi, Biblia iliposema kuwa usimwache mwanamke mchawi kuishi ilimaanisha nini?


JIBU: Katika agano la kale Mungu aliwapa wana wa Israeli hukumu…akawaambia wazishike hizo..na hukumu hizo ni kwa wale wote watakaokwenda kinyume na Torati…Kwamfano Torati ilikataza KUZINI..Mojawapo wa zile amri kumi ilikuwa ni USIZINI.

Hivyo mwanamke/mwanamume yeyote atakayeivunja hiyo sheria..adhabu yake ilikuwa ni KIFO!..Na walioitekeleza hiyo hukumu walikuwa ni hao hao wana wa Israeli kufuatia maagizo waliyopewa na Mungu mwenyewe…Kwamfano mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, adhabu yake ilikuwa ni kupigwa mawe mpaka kufa!..aliyekamatwa vilevile analala na mnyama adhabu yake ilikuwa ni kifo,

Hebu tusome baadhi ya hukumu hizo

Walawi 20:10 “Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa.

11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.

12 Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo uchafuko; damu yao itakuwa juu yao.”

Kutoka 22: 19 “Mtu awaye yote alalaye na mnyama sharti atauawa”.

Na sio hizo tu!…kulikuwa na sheria zilizokuwepo za kumuua ndugu yako wa damu endapo atakwenda kuabudu miungu mingine tofauti na Mungu wa Israeli. Na zaidi ya hayo Mungu alikataza shughuli zozote za kishirikina na kichawi katika Taifa takatifu la Israeli..

Kumbukumbu 18: 9 “Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.

10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,

11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, WALA MCHAWI, wala mtu awaombaye wafu.

12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.

13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako”.

Sasa yeyote Yule aliyekiuka amri hiyo Mungu aliyoitoa ya kutojihusisha na ushirikina na uchawi..hukumu yake ilikuwa ni kifo tu!..Ndio hapo Musa akaiandika hiyo hukumu katika..

Kutoka 22:18 “Usimwache mwanamke mchawi kuishi. 19 Mtu awaye yote alalaye na mnyama sharti atauawa”.

Maana yake mwanamke/mwanamume akikamatwa katika ushirikina ni kuuawa kwa aidha kupigwa kwa mawe au kwa vyovyote vile…(ilimradi afe tu)

Kwahiyo sheria ya kuwaua wachawi ilikuwepo kama tu sheria ya kumuua mwanamke aliyekamatwa katika uzinzi..

Lakini sasa katika agano jipya la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo..wanadamu hatujapewa tena mamlaka ya kuhukumu kutoka kwa Mungu, kama wana wa Israeli walivyopewa amri ya kuhukumu na Mungu mwenyewe. Hatuna tena hukumu ya jino kwa jino, jicho kwa jicho, mguu kwa mguu, Wakati huu wa sasa wa agano jipya, Hukumu yote amekabidhiwa Yesu Kristo.

Yohana 5:22 “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, BALI AMEMPA MWANA HUKUMU YOTE”

Umeona hapo? Mwana (yaani Yesu Kristo) Ndio kakabidhiwa hukumu yote sasa…na ndiye atakayewahukumu walio hai na walio kufa (Kasome 2Timotheo 4:1)…hakuna tena mtu yeyote mwenye mamlaka ya kumuua mwanamke aliyeshikwa katika uzinzi, wala kumuua mtu aliyekamatwa analala na mnyama wala kumuua mwanamke/mwanamume aliyekamatwa katika uchawi. Hukumu hizo Yesu Kristo ndio kakabidhiwa na Baba, na sasa ametupa neema….Ambapo tunamkosea Mungu lakini tuna nafasi ya kutubu kabla ya kuhukumiwa…

Maasi tunayoyafanya sasa tunastahili kuhukumiwa na Bwana Yesu papo kwa hapo!!…lakini tumependelewa na kupewa nafasi ya kukimbilia msalabani na kupata msamaha kabla ya hukumu ya mwisho!…Utafika wakati hii neema itaisha na huyu Yesu Kristo tunayemwona sasa anayeturehemu bure watu tusiostahili kurehemiwa, atafunga mlango wa Neema na atasimama kwenye kiti chake cha hukumu na atawahukumu wazinzi wote, wachawi wote na watenda dhambi wote kwa kuwatupa katika ziwa la moto..Lenye adhabu kali kuliko ya kupigwa kwa mawe.

Hivyo haturuhusiwi kwa namna yoyote kuwaua wezi kwa kuwapiga kwa mawe,wala kuwaua tuliowafumania katika uzinzi wala tuliowakamata katika uchawi, wala kulaani mtu yeyote yule..kwa kuutumia huo mstari wa “usimwache mwanamke mchawi kuishi”..Wasiolielewa Neno ndio wanaoutumia huo mstari kwa kukosa maarifa…lakini mimi na wewe tusikose hayo maarifa…Kwasababu hakuna astahiliye kuhukumu sasa isipokuwa Mwana wa Mungu pekee.

Jukumu letu ni sisi kuomba kwa bidii dhidi ya nguvu zote za giza, kwamba zisiwe na nguvu juu yetu, wala juu ya watu wetu na familia yetu, na vitu vyetu…na kumwomba Mungu awaokoe ndugu zetu waliozama katika nguvu za giza, ambao wanatumika na mamlaka ya giza aidha kwa kujua au kwa kutokujua, kwasababu nao pia ni watu kama sisi wanaohitaji wokovu, na sio kutafuta njama za kuwaua,au kuwaombea vifo ni kinyume na maandiko…

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

UTUKUFU NA HESHIMA.

Kwanini Bwana aliongea na Abramu baada ya kutengeana na Lutu?

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

HAKI HAIMWACHI KUISHI.

…Japokuwa ameokoka katika bahari,haki haimwachi kuishi…


Ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu, unapaswa ujue kuwa kuna wakati sio mambo yote yataenda vizuri kama unavyofikiri, Hilo ni vizuri ukaliewa kwasababu watu wengi wameishia njiani na kuona kama wokovu ni mgumu wakidhani kuwa ndio utaendaelea kuwa hivyo hivyo wakati wote.

Biblia ni kitabu ambacho kimeturahisishia kuielewa vizuri hii njia ya imani, kiasi kwamba yale ambayo tunaona kama sisi ndio wa kwanza kuyapitia, Kumbe tayari wengine walishayapitia zamani sana huko nyuma, na hivyo Habari zao zikaandikwa ili kututia moyo na kutupa nguvu sisi tuliotokea huku mwishoni.

Sasa tusipokuwa watafakariji wazuri wa maandiko namna hiyo, hapo ndipo shetani anapata njia rahisi ya kutuangusha katika hatua za awali kabisa za wokovu wetu.

Leo tutakiangazia kile kisa cha Mtume Paulo, baada ya kufungwa na kusafirishwa kupelekwa Rumi kutoka Yerusalemu, sasa Ili kuifanya Habari kuwa fupi, ni kwamba safari ile ilikuwa ni ya kufa na kupona, bahari iliwachafukia katikati ya vilindi, dhorubu kali iliwakumba, kaisi kwamba hawakuona jua wala nyota kwa siku nyingi..Yeye akiwa kama mmojawapo wa mfungwa, wakiwa wameishiwa chakula kutokana na kwamba shehena nyingi za hazina zilitupwa baharini ili kuifanya meli iwe nyepesi, sasa wakiwa katikati ya njaa kali ,anasema walifikia hatua wakakata tamaa ya kuokoka.. kwa jinsi hali ilivyokuwa mbaya, mpaka kuvunjikiwa meli yao, na kunusurika kibahati bahati kwa neema za Mungu..(Soma Habari hiyo yote katika Matendo 27&28).

Lakini walipofika kwenye kisiwa kimoja walichotulia, wakiwa wamepewa hifadhi kwa muda na wenyewe wa pale, wakati wa usiku wanaota moto, Paulo akiwa ameshika mzigo wa kuna, ghafla akatokea nyoka (jamii ya kifutu), akajifiringisha na kujikaza kwa nguvu mkononi mwake, Wenyeji kuona vile wakasema huyu ni lazima atakuwa Muuaji tu, japokuwa kanusurika kule baharini, lakini haki haimwachi aishi, ..Tusome..

Matendo 28:3 “Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni, na kuuweka motoni, nyoka akatoka kwa ajili ya ule moto akamzonga-zonga mkononi.

4 Wenyeji walipomwona yule nyoka akilewa-lewa mkononi, wakaambiana, Hakosi mtu huyu ni mwuaji; ambaye ijapokuwa ameokoka katika bahari haki haimwachi kuishi.”

Jaribu kutengeneza picha, jinsi Paulo alivyokuwa anaonekana mbele za watu wakati huo, kwasasa watu wanaweza kusema, Ana Nuksi huyu, ana mikosi, ni laana za wazazi wake zinamwandama, au za ukoo.. haiwezekani apitie shida tu yeye sikuzote..

Kwanini afilisike, kwanini nyumba yake iinguliwe na moto, kwanini aibiwe mali zake, kwanini afiwe na Watoto wake wote watatu kwa mpigo.. Kama Mungu yupo naye, si angemuepusha na mambo hayo yote? Mungu gani huyo.. Kwanini akose mahali pa kulala, n.k.n.k.

Maneno mengi sana yanaweza kuzuka, kwa njia hizo, Lakini Paulo alipoumwa na nyoka yule mwenye sumu kali, kwasababu nyoka wale wanakufanya uvimbe kwa haraka, na baadaye damu inaganda, na kisha kukutwa na kifo cha ghafla kama hutawahishiwa matibabu.. Lakini Paulo hakuhitaji matibabu yao, bali alimtupa motoni akatulia kimya..

Muda ukapita, masaa yakapita, siku ikapita wakaona mbona havimbi, mbona haonyeshi hata dalili ya kuumwa.. Ndipo zile shutma zao zikageuka kuwa kitu kingine.

Matendo 28:5 “Lakini yeye akamtukusia motoni asipate madhara.

6 Wao wakadhani ya kuwa atavimba au kuanguka chini kwa kufa ghafula; na wakiisha kumwangalia sana, na kuona kwamba halimpati dhara lo lote, wakageuka, wakasema kwamba yeye ni mungu”.

Jambo tunalopaswa tujifunze (Sisi kama watakatifu), ni kuwa si kila tatizo ni Mkosi, au laana, au mapigo wala matokeo ya uchawi..…

Hapana, mengine Mungu anayaruhusu tu, kwasababu lipo kusudi anataka kulipitisha nyuma yake.. Kama Paulo asingeumwa na nyoka , wasingemwamini pale alipokuwa anawahubiria Habari za Kristo na uponyaji wa kiungu. Lakini kwa tukio lile baada ya muda Mungu alitukuzwa.

Vivyo hivyo na sisi, tukijijua maadamu hatuna tatizo lolote na Mungu wetu, basi tutulie kimya tuiache mitazamo ya watu ipite, lakini wakati utafika watagundua kuwa haukuwa na nuksi, au mkosi, bali ulikuwa katika njia ya mafanikio yako rohoni.

Lakini ikiwa wewe ni mwenye dhambi, hilo ni jambo lingine. Hapo Mungu hausiki, ni vizuri ukampa Kristo Maisha yako, shetani hana urafiki na wewe, ukifa leo mwisho wako utakuwa ni kuzimu na ndicho anachokitafuta na kukifurahia..Biblia inasema..

1Petro 4:18 “Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?”

Jiulize utaonekania wapi siku ile? Kama leo hii hutampokea Kristo?

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

 

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

Mtu astahiliye hofu ni yupi?

KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

SWALI: Waebrania 1:7 “Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto”..Je Mungu anawageuza malaika zake kuwa mapepo?


JIBU: Ndio! Wale malaika walioasi mbinguni waligeuka na kuwa mapepo baada ya kutupwa duniani, ndio haya yanayowasumbua wanadamu leo. Lakini mstari huo hapo juu hauzungumzii roho za malaika walioasi(yaani mapepo)… bali unazungumzia juu ya upepo huu wa asili(yaani hewa iliyopo kwenye mwendo). Sasa sio kwamba Mungu anawageuza na kuwafanya upepo hapana bali anafananisha na upepo malaika wake. Ili kuelewa hilo Zaidi tusome mstari ambao umelizungumzia jambo hilo vizuri..ambao ndiko Mtume Paulo aliko linukuu..

Zaburi 104:1 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Umejivika heshima na adhama.

2 Umejivika nuru kama vazi; Umezitandika mbingu kama pazia;

3 Na kuziweka nguzo za orofa zake majini. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, Na kwenda juu ya mabawa ya upepo,

4 HUWAFANYA MALAIKA ZAKE KUWA PEPO, NA WATUMISHI WAKE KUWA MOTO WA MIALI

5 Uliiweka nchi juu ya misingi yake, Isitikisike milele”.

Katika mistari hiyo unaona Mungu anavifananisha vitu vya asili kama hifadhi yake..utaona anasema umejivika nuru kama vazi!..kiuhalisia Nuru haliwezi kuwa vazi…hali kadhalika anasema ameyafanya mawingu kuwa kama gari lake, vilevile mawingu hayawezi kuwa gari…lakini kwake yeye ni kama gari…na mbingu amezifananisha kama pazia, hizo zote ni lugha za picha tu..ni kama isemavyo kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa Taifa…kuonyesha kilimo ni kama vile mfupa uliopo nyuma ya mngongo wa mtu unaoufanya mwili uwe wima. Pasipo huo mwili hauwezi kusimama vivyo hivyo pasipo kilimo nchi haliwezi kuwepo!

Na hapa Mungu anawafananisha Malaika wake na upepo…Upepo ndio unayoyafanya mawingu yatembeee, kama vile ulivyo wa muhimu kwa merikebu baharini, bila upepo mawingu hayawezi kutembea, wala merikebu haziweki kutembea, wanasema Upepo ndio kitu chenye nguvu kuliko vitu vyote vya asili, hata majini hayakuti….na hapo tayari Mungu kashayafananisha mawingu na gari lake ambalo linakwenda juu ya upepo. Ikifunua kuwa malaika wana sehemu kubwa katika kulitimiza kusudi la Mungu na kulisogeza mbele kusudi lake.

Lakini ukisoma hiyo Waebrania utaona, Yesu Kristo ambaye ni Mwana wa Mungu, yeye hajafananishwa na upepo kama Malaika…Yeye amefananishwa na yule aketiye juu ya kiti cha enzi mwenyewe ndio maana anaitwa (chapa ya nafsi ya Mungu)..Alipopaa alikwenda kuketi katika mkono wa kuume wa Mungu Baba, hivyo ni mfano wa Baba, yeye naye mawingu yatakuwa ni Gari lake, na Malaika ni kama upepo wa kulisukuma gari lake..Ndio maana biblia inasema hapo “amefanyika bora kuliko malaika”…Haleluya!..

Na kwakuwa yeye kafanyika bora, na wale waliomwamini na watakaomwamini..watafanyika bora kama yeye..kwasababu yeye alipo ndipo na sisi tutakapokuwepo. Na hapo ndipo malaika wanatuhudumia (Waebrania 1:14)

Atukuzwe Mungu kwa kumtoa mwanawe kwaajili yetu.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

UCHAWI WA BALAAMU.

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

MTANGO WA YONA.

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mstari huu una maana gani? “Mathayo 23:39 Hamtaniona kamwe tangu sasa”

SWALI: Mathayo 23:39 “Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, AMEBARIKIWA AJAYE KWA JINA LA BWANA.”


JIBU: Ukisoma kuanzia juu utaona habari hiyo alikuwa anaizungumza Bwana Yesu alipokuwa anaingia Yerusalemu, Na kuona jinsi mji ule ulivyo mkataa, na kukataa wokovu tangu zamani za Manabii wa agano la kale hadi wakati wake, Na jinsi ulivyowaua wale wajumbe wote waliotumwa kwake,..Ndipo hapa sasa Yesu akautabiria kuwa atauacha katika hali ya ukiwa mpaka hapo watakapogeuka..

Embu tusome..

Mathayo 23:37 “Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!

38 Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.

39 Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana”.

Unaona, Na historia inaonyesha kweli, Wayahudi waliachwa na Mungu, tangu huo wakati hadi sasa ni miaka 2000 imeshapita, bado hajawarudiwa na mji wa Yerusalemu nao ulikuwa ni magofu tangu zamani, ni karne za juzi juzi tu ndio umeanza kujengwa tena na kukaliwa na watu.., lakini Bwana hakuishia tu pale, bali alisema, utaendelea kuwa hivyo hivyo katika hali ya ukiwa mpaka siku hiyo watakaposema tena Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana..Yaani ikiwa na maana watakapotubu na kumtambua Kristo kuwa ni yule masihi kweli..

Lakini ni kwanini aseme “hata mtakaposema, AMEBARIKIWA AJAYE KWA JINA LA BWANA.” Na si mpaka hapo mtakaposema mimi ni Masihi?

Utakumbuka tukio lililotendekea nyuma kidogo kabla hajafika Yerusalemu alikuwa anaimbiwa hayo maneno Hosana, Hosana Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana…

Na ndio maaana utaona Bwana akitumia maneno hayo hayo tena kuashiria kuwa mpaka siku wayahudi watakapompokea yeye kwa namna hiyo hiyo, ndipo wokovu utageuka kwao. Na dalili zote zimeshaanza kuonekana sasa, Israeli imeshakuwa taifa huru, wayahudi wanaanza kuyagundua makosa yao kidogo kidogo..Je! Unadhani ni kitu gani kitatokea muda mfupi baadaye.. Bila shaka watamgeukia na kutubu..Na biblia inasema siku watakapomgeukia uovu wao utaondolewa wote ndani ya siku moja..

Kama unabii inavyosema..

Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.

11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido.

12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;

13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.

14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.

Sasa tukishaona mambo hayo yanatokea, basi ujue kuwa Neema ya wokovu imeshaondoka kwetu, na Unyakuo tayari umeshapita.

Ni nyakati za mwisho tunazoishi, Je, bado na wewe upo vuguvugu? Unataka na wewe uachwe ukiwa kwa mfano wa Wayahudi walivyoachwa zamani kwa kutokutubu kwao? Wakati ambao utamtafuta Bwana hutamwona, utautafuta wokovu hutaupata?. Usitamani kabisa wakati huo ukukute hali bado upo dhambini, tubu, itii injili inapohubiriwa kwako kila siku,..UNYAKUO upo mlangoni.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MAOMBI YA VITA

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.

BUSTANI YA NEEMA.

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

Ujana ni wa thamani..hususani unapotumika vyema…Na kila mahali panaitaji vijana kwaajili ya nguvu kazi, nchi inahitaji vijana kwaajili ya nguvu kazi, shetani naye anawahitaji vijana zaidi kuliko wazee kwa ajili ya nguvu kazi zake…Hali kadhalika Roho Mtakatifu anawahitaji vijana pia.

Na takwimu zinaonyesha kuwa kipindi cha kati ya miaka 13-20 ndio kipindi ambacho watu wengi wanausikia wito wa ki-Mungu, 21-30 mara nyingi ni kipindi cha madarasa ya kiroho na 30-50 ni wakati wa kazi… Sasa ni wachache sana wanapata neema ya kuvutwa kwa Kristo wakiwa na miaka 40 au 50… Utakuwa umepewa neema kubwa sana kama utampokea Kristo katika umri huo Kwasababu ujana pia unathamani mbele za Mungu…

Sasa katika umri wa ujana…Ndio wakati wa kuwa na nguvu nyingi za kiroho..(hiyo ni neema ya kipekee ambayo Mungu anaiachia kwa vijana tu)..haiwahusu wazee.

1Yohana 2:14 “Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna NGUVU, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, NANYI MMEMSHINDA YULE MWOVU”.

Kama vile nguvu kazi ya Taifa ni vijana, vivyo hivyo Taifa la Mungu linajengwa na vijana watakatifu, kwasababu hao ndio wamepewa nguvu!..wazee hawana nguvu hizo..Kwahiyo UJANA ni wa kuuthamini sana.

Mtume Paulo mwishoni mwa huduma yake, alilijua hilo ndipo akatafuta vijana kadha wa kadha kwaajili ya kazi maalumu ya kuujenga ufalme wa Mbinguni…Baadhi yao walikuwa ni Timotheo na Tito. (walikuwepo wengi lakini hebu tuwatazame hawa wawili).

Hawa ni vijana ambao Mtume Paulo aliwaandaa..akawa anawatuma pia…walikuwa ni vijana tu! Labda miaka 20-25 hapo!..Lakini walikuwa wanaifanya kazi kubwa Sana! na kuleta uharibifu mkubwa kwenye ufalme wa giza…Mpaka Paulo ilimbidi kuwaandikia nyaraka zao binafsi, Timotheo alipewa jukumu kubwa sana la kuyasimamia makanisa yaliyopo Asia, na Tito naye hivyo hivyo, Huyu Tito Mtume Paulo alimpa jukumu kwa uwezo wa Roho wa kuteua maaskofu wa kanisa, ambao walikuwa ni wa umri mkubwa kuliko yeye…

Hebu jiulize ni kijana lakini ndiye anayesimamia makanisa yote na ndiye anayepewa jukumu la kuteua wazee na maaskofu wa makanisa…(kasome kitabu cha Tito chote utaona) na Timotheo naye ni hivyo hivyo, alikuwa ni kijana mdogo lakini alipewa majukumu kama hayo kasome 1Timotheo 3, na utaona kwa majukumu hayo Mtume Paulo alikuwa anawaasa pia wakaripie na kukemea na kuwaonya wazee kama wazazi.

Lakini lililo kubwa na muhimu pia Mtume Paulo alilowaasa hawa vijana ni kwamba MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO!..Hebu tusome kidogo

1Timotheo 4:12 “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi”.

Huyu ni Timotheo, hebu tumwangalie na Tito naye..

Tito 2:15 “Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote”.

Maana yake unapofika wakati wa injili, Hubiri injili usitazame uso wa mtu au kichwa cha mtu kina mvi kiasi gani….Sema kwa ujasiri kwamba WAZINZI WOTE WASIPOTUBU WATAKWENDA MOTONI !!!…usijiangalie wewe ni mdogo na wao ni wakubwa!!..kwamba watakudharau..Kile kitu ambacho Roho Mtakatifu amekiweka ndani yako kizungumze kwasababu ni Mungu ndiye aliyekuambia ufanye hivyo na sio wao!!… Na utaona wote unaowahubiria hata kama wana umri wa Baba yako wanakuja kwa Kristo..Kwasababu Injili ni Uweza wa Mungu uletao wokovu. Hivyo usiudharau ujana wako wala mtu yeyote asikudharau.

Ukidharauliwa na kuambiwa wewe hujui kitu..puuzia hayo maneno!..Lihubiri Neno kwasababu kuna nguvu nyingi za Mungu katika ujana kuliko walizonazo wazee.. Na shetani analijua hilo ndio maana hawapendi vijana na ndio anaowatafuta wengi awaangushe.

Lakini pia Mtume Paulo aliwaonya hawa vijana kwamba wazikimbie TAMAA ZA UJANANI! Katika utumishi wao.

1Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.

Maana yake ni kwamba ujanani kuna vishawishi vingi,na kuna tamaa nyingi…(sio kwamba ukishakuwa mtumishi wa Mungu kijana basi ndio hautakutana na vishawishi/tamaa)…Utakutana navyo lakini biblia imesemaje? TUZIKIMBIEEE…na sio TUZIOMBEEE…Hakuna maombi yeyote ya kuziepuka tamaa wala kuzishinda!…Hakuna maombi yoyote ya kuepukana na uasherati na ulevi na uzinzi!!..HAKUNA! wala usidanganywe na mtu yeyote hata anayejiita mtumishi! …suluhisho ni kuzikimbia…maana yake ni kwamba kama ulikuwa unamahusiano au unaona kuna dalili ya kuzama kwenye uasherati na mtu Fulani, unajiepusha naye! Sio unamwomba Mungu akuepushe naye! Ni wewe ndiye unayeanza kujiepusha naye..unakata mazoea naye.…kadhalika kama ni marafiki ndio waliokuwa wanakushawishi kwenda kuzini kwa mazungumzo yao au tabia zao..unajitenga nao…huko ndiko kuzikimbia tamaa….Yusufu alimkimbia mke wa Potifa hakumwombea!.

Picha za uchi na pornografia unazoziangalia kwenye simu ndizo zilizokuwa zinakupeleka kujichua na kufanya uasherati…hakuna maombi yeyote katika maandiko ya kuiondoa hiyo tabia!…Suluhisho ni wewe kuamua kuachana na hiyo tabia…kufuta hizo picha kwenye simu yako na kama bado inakushinda unajikuta unazifungua, badilisha hiyo simu yako ya smart unayoitumia na anza kutumia simu ya tochi!..Hilo tatizo utakuwa umelitatua moja kwa moja/umelikimbia….Biblia inasema kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate, ili usije ukapoteza roho yako yote..

Usisubiri ujana wako uharibiwe na ibilisi, umri ulionao ni wa thamani, kama hutastuka leo, utafika wakati utajuta sana kwanini hukumtumikia Mungu katika ujana wako. Zinduka usingizini.

Bwana akubariki, kijana!..

Kama hujampa Kristo maisha yako, basi tayari yapo mikononi mwa shetani hata kama utakuwa hujui…Kuwa nje ya Kristo tayari upo kinyume cha Kristo kwasababu hukusanyi pamoja na Kristo, Na hivyo unatapanya..(Mathayo 12:30). Hivyo geuka leo mpe maisha yako, ujana wako unathamani sana katika ufalme wake…Wengi watabadilika kupitia wewe endapo utakubali kumtii Kristo, na siku ile utapewa taji ya Uzima.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post