Huruma ni nguzo muhimu sana ambayo tunapaswa tuwe nayo sisi tuliompokea Kristo maishani mwetu.
Ni kwanini tuwe na huruma? Ni kwasababu Baba yetu naye ni mtu mwenye huruma.
Luka 6:36 “Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma”.
Lakini wengi wetu bado hatujafahamu vema huruma hasaa ni nini. Kuna tofauti kati ya huruma na Rehema(wafilipi 2:1). Rehema ni neno pana linalomaanisha kusamehe au kusaidia hata kama mtu huyo hastahili kupewa fadhili hizo, lakini huruma ni kitendo cha kuonyesha kusamehe/kusaidia/kujali kwa mtu ambaye anaonekana anahitaji msaada huo hata kama hatosema,au kuonyesha.
Kwa mfano mwanajeshi vitani anapomkamata adui yake (ambaye ni mwanajeshi kama yeye). Na ikatokea adui huyo akajisalimisha kwa magoti akiomba asiuliwe,..Na yule mwanajeshi akamsaheme, kwa kuomba kule, basi hapo kaonyesha kitendo cha huruma.
Lakini ikitokea, Yule adui amekamatwa lakini bado analeta ubishi, bado ni mkaidi, anataka kuleta madhara, na wakati huo huo Yule mwanajeshi bado akayahifadhi tu maisha yake..Hiyo sio huruma bali ni rehema.
Mfano mwingine wa rehema ni pale raisi anapowaachilia wafungwa, sio kwamba wale watu walimwomba watoke, au wamejirekebisha kwa tabia zao mbaya, au ni wema sana hapana bali ni pengine raisi anatimiza tu wajibu wake wa kisheria kama raisi, wa kusamehe wafungwa kila muhula kwake.
Mfano mwingine wa huruma ni pale Baba anapomtimizia mtoto wake mahitaji yake ya chakula au mavazi,huwezi kusema anaonyesha kitendo cha rehema, hapana, bali huruma, kwasababu anajua sikuzote mtoto ni dhaifu, hana uwezo wa kujiamulia mambo yake mwenyewe.
Hivyo rehemu na huruma vyote vinahitajika sana kwetu. Lakini leo tutajikita sana katika upande wa huruma, na tayari tumeshapata msingi wa maana halisi ya huruma, kwamba huwa unaenda moja kwa moja kwenye kundi la watu wanaoonyesha kuhitaji msaada fulani. Basi biblia inatufundisha sisi kama wakristo, tuonyeshe huruma zetu, kwa makundi kama hayo; kwasababu Baba yetu wa mbinguni naye anaonyesha huruma zake kwetu sisi tunapomlilia, usiku na mchana.
Kibiblia ni makundi gani tunapaswa tuyaonyeshee huruma zetu?
1) HURUMA KWA WENYE MAGONJWA.
Utaona katika maandiko Bwana Yesu aliwaponya wagonjwa wengi sana kwasababu aliwahurumia, hakuwaacha tu waende zao,bali alijitahidi kuchukuliana nao, na kuwaponya.
Marko 1:40 “Akaja kwake mtu mwenye ukoma, akamsihi na kumpigia magoti, na kumwambia, Ukitaka, waweza kunitakasa.
41 NAYE AKAMHURUMIA, akanyosha mkono wake, akamgusa, akamwambia, Nataka, takasika.
42 Na mara ukoma wake ukamtoka, akatakasika.
Unaona? nasi vivyo hivyo, tunapoona wengine wanataseka na magonjwa, wanaumwa, hatupaswi kuwaacha hivi hivi, tuwe nao karibu tuwaombee, tujiweke na sisi katika nafasi zao, Jiulize je! Kama na wewe ungekuwa unaumwa kansa, au kisukari, au ukimwi kama Yule, halafu unaona watu hawakujali hata kukuombea, utajisikiaje?.
Tazama tena kisa hiki kingine..
Luka 7:12 “Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye.
13 Bwana alipomwona ALIMWONEA HURUMA, akamwambia, Usilie.
14 Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka”.
2) HURUMA KWA WENYE UHITAJI.
Kuna wakati jirani yako atakuwa amepungukiwa na kitu fulani aidha mboga kidogo, au sabuni, au pesa kidogo za matumizi, na pengine hilo lipo ndani ya uwezo wako, hupaswi kumuacha tu hivi hivi, bali uonyeshe huruma zako, kwasababu hivyo ndivyo Mungu anataka..
1Yohana 3:17 “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia HURUMA ZAKE, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?
18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli”.
3) HURUMA KWA WALIOKUMBWA NA MATATIZO:
Kuna muda ambao, mtu fulani atahitaji msaada wa haraka kutoka kwako, labda mgonjwa wake kazidiwa anaomba msaada wako,wa kumfikisha hospitali, na wewe pekee ndio upo hapo wa kuweza kumsaidia, wakati kama huo, usijione kuwa upo buzy sana, au unawahi ibadani, zingatia kumsaidia kwanza, kwasababu biblia inatufundisha hivyo kwa ule mfano wa msamaria mwema;
Luka 10:30 “Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona ALIMHURUMIA,
34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza”.
4) HURUMA KWA WAKRISTO WALIORUDI NYUMA:
Hapa ni mahali pengine ambapo tunapaswa kupazingatia sana. Kuna wakati ndugu mwenzako katika imani anaweza kurudi nyuma, pengine akauacha wokovu kabisa, lakini akawa anatamani kurudi tena kwa Mungu, wewe kama mkristo, ni lazima uonyeshe huruma zako kwa mtu kama huyo kumsaidia, tutalisoma hilo katika ule mfano wa mwana mpotevu, utaona baada ya kuasi nyumbani na maisha kuwa magumu huko alipokwenda alizingatia kurudi nyumbani. Na aliporudi alimwambia baba yake maneno haya; Lakini utasoma babaye hakumfukuza bali alimuhurumia.
Luka 15:19 “sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.
20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, AKAMWONEA HURUMA, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena.
22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;
23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;
24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia”.
Vivyo hivyo na sisi tuwahurumie wale ambao wanarudi kwa moyo wa dhati kwa Mungu.
5) HURUMA KATIKATI YA WAAMINIO.
Vilevile sisi kama waaminio, tuliokoka, kanisa la Kristo, ni lazima tujue kuwa kila kiungo kinamuhitaji mwenzake, unapoona kiungo kimoja kimeumia, au kimefadhaika huna budi kukitibu, unapoona kimepungukiwa huna budi kukijali, kinapokukosea huna budi kikisamehe. Ndivyo Bwana anavyotaka.
Waefeso 4:32 “tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi”.
Bwana atusaidie tuyazingatie hayo, ili na sisi tufanane na Baba yetu wa mbinguni, ambaye anatuhurumia kila wakati.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo litukuzwe daima, karibu katika kuyatafakari maandiko.
Katika biblia tunasoma Kisa cha mabinti wa tano wa mtu mmoja, wa kabila la Manase, waliokuwa mashujaa katika Imani, hata kuibadilisha taratibu ambazo zilikuwepo.
Zamani wakati wana wa Israeli wanatoka Misri, kuelekea Kaanani. Mungu alimpa Musa maagizo ya kuigawanya hiyo nchi watakayoiendea.. Kwamba kila kabila, lipate sehemu ya ardhi katika hiyo nchi ya kaanani wanayoiendea. Lile kabila lenye watu wengi, basi litapewa sehemu kubwa ya ardhi, na lile lenye watu wachache basi litapewa sehemu ndogo ya ardhi. Na kabila la Yuda ndio kabila lililokuwa na watu wengi kuliko kabila zote za Israeli, na kabila la Manase ndilo lililokuwa dogo kuliko yote (yaani lenye watu wachache).
Hivyo wakati wa kugawa urithi, walikuwa wanaangaliwa wale wazee wa ukoo ambao ndio vichwa vya ukoo, wanaomcha Mungu, hao ndio wanaopewa labda tuchukue mfano, hekari elfu moja, na hao ndipo wanagawa hizo ekari elfu kwa watoto wao wa kiume, kufuatia kila familia iliyopo chini yao. Hivyo mwisho wa siku kila familia ilikuwa inapata urithi wa ardhi katika hiyo nchi ya Kaanani waliyokuwa wanaiendea.
Lakini sasa katika hilo kabila lenye watu wachache kuliko kabila zote, yaani kabila la Manase, kulikuwepo na mtu mmoja ambaye alikuwa mashuhuri katika kumcha Bwana, ambaye naye pia alihesabiwa kama kichwa, ambaye aliandikiwa urithi katika hiyo nchi waliyokuwa wanaiendea.. Mtu huyo aliitwa SELOFEHADI.
Lakini kwa bahati mbaya mtu huyo alikufa kabla ya kuzaa mtoto wa kiume ambaye angerithi sehemu ya urithi huo, akawa anao mabinti tu!. Hivyo kutokana na jambo hilo, wana wa Israeli wakalitoa jina lake miongoni mwa watakaopata sehemu ya ardhi katika hiyo nchi ya ahadi wanayoiendea..Kwasababu wanawake hawawezi kupewa urithi!..
Lakini tunasoma jambo moja la kipekee lililotokea..kwa mabinti wa huyo Selofehadi, hatujui Baba yao aliwafundisha nini, lakini tunasoma kwamba walifanya jambo la kipekee kugeuza sheria na taratibu za Israeli kwa IMANI. Kwani walipoona tu! Baba yao amekufa na sehemu yake ya urithi imeondolewa, hawakuridhika, wakasema watamwendea Musa na kudai haki ya baba yao.. Kwamba sehemu ya urithi wa baba yao wapewe wao!.. jambo ambalo ni kinyume na utaratibu, kwani wanawake hawana ruhusa ya kurithi mali..Lakini wanawake hawa watano wa familia moja!, walishindana mpaka wakapata haki yao hiyo.
Hebu tusome kidogo..
Hesabu 27:1 “Wakati huo wakakaribia hao binti za Selofehadi, mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, wa jamaa za Manase mwana wa Yusufu; na majina ya hao binti za Selofehadi ni haya; Mala, na Noa, na Hogla, na Milka, na Tirsa.
2 Nao wakasimama mbele ya Musa, na mbele ya Eleazari kuhani, na mbele ya wakuu, na mkutano wote, mlangoni pa hema ya kukutania, wakasema,
3 Babaetu alikufa nyikani, naye hakuwamo katika mkutano wa hao waliojikutanisha kinyume cha Bwana katika mkutano wa Kora; lakini akafa katika dhambi zake mwenyewe; naye alikuwa hana wana wa kiume.
4 Kwa nini basi jina la babaetu kufutwa katika jamaa zake kwa sababu alikuwa hana mwana wa kiume? Tupe sisi urithi pamoja na ndugu zake babaetu.
5 Basi Musa akaleta neno lao mbele ya Bwana
6 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
7 HAO BINTI ZA SELOFEHADI WANANENA LILILO HAKI; KWELI UTAWAPA MILKI YA URITHI PAMOJA NA NDUGU ZA BABA YAO; NAWE UTAWAPA URITHI WA BABA YAO.
8 Kisha utanena na wana wa Israeli, na kuwaambia, MTU AKIFA, NAYE HANA MWANA WA KIUME, NDIPO UTAMPA BINTI YAKE URITHI WAKE.
9 Tena ikiwa hana binti, mtawapa nduguze urithi wake.
10 Na ikiwa hana ndugu, mtawapa ndugu za babaye huo urithi wake.
11 Tena ikiwa babaye hana ndugu, utampa huyo aliye karibu naye katika jamaa zake huo urithi wake, naye atakuwa nao; na neno hili litakuwa ni amri ya hukumu kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Musa”.
Kabla ya hapo hakukuwa na sheria kwamba mtu akifa, kama hana mtoto wa kiume urithi wake uende kwa mabinti wake, lakini Mabinti hawa watano, WALILIFUNGUA HILO KWA IMANI. Laiti wangeendelea hivyo, labda mpaka leo Israeli, mabinti wasingekuwa wanapata urithi wowote. Lakini kwa Imani ya hawa mabinti watano wa mtu mmoja ambao majina yao yalitajwa kama MALA, NOA, HOGLA, MILKA, na TIRSA, waliweza kubadili majira kwa Imani..na kuwafanya mabinti wengine wote wa Israeli wafurahi.
Mwanamke au binti, unayesoma haya…kabla ya kwenda kujifunza kwa akina Eliya, na Elisha, na Paulo walio wanaume, hebu jifunze kwanza kwa wanawake hawa!, jinsi gani walivyopata urithi wao!, hawakwenda kwa waganga!..wala hawakwenda kwenye vikundi vya kijamii, wala hawakuanzisha mgomo!, wala vurugu.. bali walikimbilia kwa Musa, aliye mtumishi wa Mungu pekee wakati huo, huku wakiwa na hoja zilizo shiba, ambaye huyo Musa alilipeleka hoja zao kwa Baba wa mbinguni, na Baba wa mbinguni akatoa majibu..
Lakini sasa aliyesimama kama Musa, ni Bwana Yesu, huyo ndiye wa kukimbilia ili kudai urithi wako..Ukienda na hoja zenye nguvu mbele zake, utapata haki yako.. Na hoja zenye nguvu tunazipata katika Neno la Mungu..
Isaya 41:21 “Haya, leteni maneno yenu, asema Bwana; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo”.
Isaya 43: 26 “Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, UPATE KUPEWA HAKI YAKO”
Jambo lingine la kujifunza juu ya mabinti hawa watano ni UMOJA!. Hakutoka binti mmoja na kumfuata Musa.. hoja yake isingekuwa na nguvu.. Lakini walipojiunga mabinti wote watano na kuwa kitu kimoja..Ndipo hoja yao ilipokuwa na nguvu. Ni vile vile hata sasa, ili Hoja zetu ziwe na nguvu mbele za Mungu, ni lazima tuungane watu wa familia moja, ambao imani yetu ni moja, Baba yetu ni mmoja, na ndipo tukamsogelee.. Tukienda kwa umoja kama huo, basi nirahisi sana kupokea majibu kuliko kwenda mmoja mmoja..
Mathayo 18:19 “Tena nawaambia, ya kwamba WAWILI WENU WATAKAPOPATANA duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni”.
Umeona hapo, anasema “wawili wenu”.. maana yake ni zaidi ya mmoja.. watakapopatana… maana yake kinachotangulia ni kupatana na kukubaliana… na baada ya kupatana, wakiliomba hilo jambo watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
Bwana atusaidie tuwe na imani kama ya mabinti wa Selofehadi pamoja na Umoja, ili tuweze kufungua milango iliyofungwa mbele yetu.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Je! Israeli wote wataokolewa siku ya mwisho kulingana na Warumi 11:26?
Kikawaida tumezoea kujifunza mambo mema kutoka kwa maaskari, kwamfano pindi tunapoyaona majeshi ya polisi katika magwaride yao, jinsi yalivyo na utaratibu mzuri, huwa tunavutiwa nayo.. tunapoyaona yakiwa katika mafunzo ya kukamata wahalifu, tunavutiwa nayo.. na hata wakati mwingine kuitamani kazi ya uaskari..
Lakini kamwe huwa hatuvutiwi na tabia za mwizi!, na wala hatutamani kuwa wezi. Kwasababu mwizi, anakuja kwa lengo la kuchukia kitu ambacho ni cha mwingine, pasipo taarifa!..jambo ambalo linaudhi sana na lisilokubalika.
Lakini Neno la Mungu linasema “Bwana Yesu atakuja kama mwivi” na “si kama askari”
Na kama tunavyojua mwizi lengo lake ni kuiba vile vya thamani na si kingine!. Hivyo Bwana Yesu anakuja duniani kuiba vile vilivyo vya thamani na kuviacha vile visivyo vya thamani..
Ulimwengu huu unafananishwa na NYUMBA.. ambamo ndani yake kuna watu wema na waovu. Na mkuu wa huu ulimwengu ni shetani, na malaika zake..
Kama vile mwizi ajavyo usiku, haji kuiba vitu vibaya bali vile vizuri vyenye thamani, ndivyo Bwana Yesu atakavyokuja kuiba watu wake (wale walio watakatifu na wenye thamani machoni pake) na kwenda nao mbinguni.
Kufumba na kufumbua, ufalme wa giza utashangaa baadhi ya watu hawapo tena duniani, wale ambao walidhani wapo chini yao, wale ambao walidhani siku moja watawatumia kwa shughuli zao za giza.. watashangaa wametoweka duniani, siku hiyo hata shetani haijui.. ghafla atashangaa tu watu baadhi hawapo!
Luka 17:34 “Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
35 Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
36 Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa”
Je! Hiyo sio tabia ya mwizi??.. hebu jiulize unakaa na mwanao ndani, mmelala asubuhi unakuta hayupo na milango imefungwa kwa ndani vile vile, umekaa na mume wako ghafla unashagaa katoweka..upo kazini na mtu Fulani ambaye unamjua ni mtu anayejishughulisha sana na masuala ya wokovu, ghafla unashangaa hayupo!!!
Ndugu yupo Mwivi anayeutazama sasa ulimwengu kutoka juu!.. Anatazama vile vilivyo vya thamani!.. anapanga mipango!.. na mipango imeshakamilika kitambo sana, atakuja saa tusiyodhani.. kufumba na kufumbua wale tuliokuwa tunawajua wanampendeza Mungu, watanyakuliwa.. na mkuu wa ulimwengu huu (atakasirika) kwasababu vile vilivyo vya thamani vimeondoka!, kama vile mtu anavyoamka asubuhi na kukuta vitu vyake vya thamani vimeibwa, atajikuta anavichukia hata vile vilivyoachwa na hata kuviharibu kwa hasira.
Ndicho kitakachotokea baada ya unyakuo, wakati watakatifu wapo mbinguni, wale walioachwa watakutana na ghadhabu ya mpinga kristo, katika dhiki kuu.
Je wewe ni chombo cha thamani?..
Kumbuka vyombo vya thamani ni wale wote waliomwamini Yesu, na kutubu dhambi zao, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu na kupokea Roho Mtakatifu.. Hao ndio biblia inawaita watakatifu.
Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.
Na hao ndio waliopo sasa katika shabaha ya Bwana, (yaani kuja kuwatwaa na kwenda nao mbinguni). Lakini wengine watakaosalia wakati wa kurudi Bwana, biblia inasema watapitia dhiki kuu, pamoja na mapigo ya siku ya Bwana.
Je wewe ni chombo cha thamani ulimwengu?.. au kisicho cha thamani?
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana na mwokozi wetu, Mkuu wa uzima, Mfalme wa wafalme, Yesu Kristo libarikiwe.
Hajawahi kutokea duniani Mtu wa muhimu, na wa Baraka kama Yesu. Leo tutaangalia kwa sehemu, ni jinsi gani ni wa muhimu kwetu.
Je unajua kwa undani ni kwanini maandiko yanasema, Bwana Yesu alipigwa kwaajili yetu?
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”
Sio kwamba Mungu alikuwa anataka kutuhukumu ndio akaona amtafute mwanae aje kufa kwa ajili yetu Hapana! Ni kwamba tayari Mungu alikuwa ameshatuhukumu, adhabu ilikuwa imeshapitishwa.. ilikuwa ipo njiani kutufikia, na ndipo Bwana Yesu akaingilia kati kufa kwaajili yetu.
Ni sawa na mtu ambaye tayari amesharusha jiwe kumlenga mwingine, na lile jiwe wakati lipo njiani kumfikia mlengwa, anatokea mwingine kukubali kupigwa kwa niaba ya Yule aliyekusudiwa kupigwa jiwe hilo. Ndicho Bwana Yesu alichokuja kukifanya.. Hakuja kuifuta hukumu, bali alikuja kuichukua ile hukumu na kuwa yake.. ndio maana ilikuwa hana budi afe!..
Hivyo Kile kifo hakikuwa cha kwake, hakukusudiwa yeye, kilikuwa ni chetu tulikusudiwa sisi, ile aibu haikuwa ya kwake ilikuwa ni yetu!… Yale maumivu hakukusudiwa yeye, tulikusudiwa sisi, kifo cha mateso hakukusudiwa yeye, tulikusudiwa sisi.. Maana yake ni kwamba endapo, Mwokozi Yesu asingetokea.. ni kipindi kifupi sana mbele yetu kilikuwa kimebaki.. ghadhabu ya Mungu ingetumaliza wote, tungekufa kikatili na kwa aibu kama watu wa gharika, na sodoma na ghomora, tungesikitika, na kulia, na kuhuzunika, na kuteseka kwa maumivu, na hatimaye kufa na kuishia katika lile ziwa la moto.
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
6 Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote”.
Kumbuka hapo maandiko yanaposema “Ameyachukua masikitiko yetu”.. haimaanishi magonjwa yetu, wala shida zetu, wala huzuni tulizo nazo sasa, wala masikitiko tuliyonayo… La! Haimaanishi hivyo, (ingawa si kosa kutafsiri hivyo), lakini maana yake ya awali kabisa sio hiyo bali inamaanisha zile huzuni ambazo tungezipata baada ya sisi kupigwa na Bwana, na yale masikitiko ambayo tungeyapata baada ya kuipata ile adhabu ya Mungu.. yeye ndiyo kayachukua hayo.. yeye ndio atahuzunika badala yetu baada ya kupigwa na Mungu, yeye ndiye atasikitika katika kuadhibiwa kule.. hiyo ndio maana ya kubeba masikitiko yetu..
Ndio maana kuna mahali Bwana Yesu alisema “nina huzuni nyingi kiasi cha kufa, Marko 14:34”
Umeona umuhimu wa Yesu kwetu?… Je unamthamini Bwana?.. bado tu hujaona umuhimu wa Yesu maishani mwako?
Kumbuka ghadhabu ya Mungu bado ipo, tena ina nguvu mara dufu kwa wale wote wanaoidharau kazi ya msalaba..
Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”
Umempokea Yesu?.. Kama bado unasubiri nini?.. kumbuka mlango wa neema hautakuwa wazi milele.. ingia leo ndani ya safina, kwa kutubu dhambi zako zote, ukimaanisha kuziacha na ubatizwe ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu Kristo, na upokee kipawa cha Roho Mtakatifu.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.
Kuna mahali Bwana wetu Yesu alisema maneno haya..
Ufunuo 16:15 “ (Tazama, naja kama mwivi. HERI AKESHAYE, NA KUYATUNZA MAVAZI YAKE, ASIENDE UCHI HATA WATU WAKAIONE AIBU YAKE.)”
Umewahi kujiuliza ni kwanini, Bwana aseme heri akeshaye “na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi”?.
Katika hali ya kawaida mtu hawezi kutoka mahali na kwenda uchi labda awe na matatizo ya akili, lakini kwa mtu mwenye akili timamu, haiwezekani kutoka nje akiwa uchi na kutembea hivyo barabarani na watu kumwona..
Lakini Bwana alivyosema hayo, alikuwa na maana!. Kwamba inawezekana pia mtu kutoka nje akiwa uchi, na watu kuiona aibu yake. Endapo atakuwa yupo katika mazingira Fulani.. Hebu tusome kisa kimoja kwenye biblia kisha tuendelee mbele.
Marko 14:48 “Yesu akajibu, akawaambia, Je! Ni kama juu ya mnyang’anyi mmetoka wenye panga na marungu, kunitwaa mimi?
49 Kila siku nalikuwa mbele yenu hekaluni nikifundisha, msinikamate; lakini haya yamekuwa ili maandiko yapate kutimia.
50 ndipo wakamwacha, wakakimbia wote.
51 NA KIJANA MMOJA ALIMFUATA, AMEJITANDA MWILI WAKE NGUO YA KITANI; WAKAMKAMATA;
52 NAYE AKAIACHA ILE NGUO YA KITANI, AKAKIMBIA YU UCHI”.
Umeona mazingira kama hayo?.. Kijana alikuwa ni moja wa wanafunzi wa Yesu!, Lakini alipoona hali imekuwa tete!!.. Anakwenda kufa na Bwana!.. na ameshakamatwa, lile vazi lake zuri la KITANI, aliliacha!, pale na kumkimbia Bwana, akakimbia uchi!.. na watu wakaiona aibu yake.
Jambo hilo hilo linaendelea katika roho leo hii.. Tunapoamua kuwa wanafunzi wa Yesu, tunakuwa tunavikwa na Bwana VAZI ZURI LA KITANI, Ambalo vazi hilo tafsiri yake ni “utakatifu”..tunalithibitisha hilo katika…
Ufunuo 19:8 “Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni MATENDO YA HAKI YA WATAKATIFU”.
Hivyo tunapoamua kumfuata Bwana, na kuwa wanafunzi wake ni lazima tujikane nafsi tubebe misalaba yetu, pamoja na mavazi yetu mazuri ya kitani. Tuwe tayari kufa tukiwa na Bwana. Lakini kama hatumtaki Bwana tufahamu kuwa hatuwezi kumkimbia bado tukiwa na yale yale mavazi yetu ya kitani(matendo ya haki).. ni lazima tuache mavazi yetu pale ndipo tukimbie uchi!, na watu wataiona aibu yetu.
Je! na wewe leo umeyaacha mavazi yako nyuma, na kukimbia uchi! Kwasababu tu umepitia mtikisiko kidogo kwenye imani yako??, kwasababu umetengwa na wazazi?, kwasababu umechukiwa na ndugu?, kwasababu boss wako hataki wewe usali, hivyo na wewe umeamua kumwachia Bwana mavazi yako(yaani matendo yako ya haki) na kukimbia uchi (kurudia machafu ya ulimwengu)??.. Kumbuka tena Bwana anasema maneno haya…
Ufunuo 16:15 “(Tazama, naja kama mwivi. HERI AKESHAYE, NA KUYATUNZA MAVAZI YAKE, ASIENDE UCHI HATA WATU WAKAIONE AIBU YAKE.)”
Je unayatunza mavazi yako?.. Usimwachie Bwana mavazi yako na kukimbia uchi kwasababu ya majaribu.. Kabla ya kuamua kumfuata Bwana Yesu, kumbuka kujikana nafsi, ujue kuwa kuna majaribu utakutana nayo mbeleni, ambayo yanaweza hata kuhatarisha maisha yako, katika hayo hupaswi kuyavua mavazi yako, ili kuusalimisha mwili wako.
Marko 8:35 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha”.
Bwana atusaidie, na kutubariki.
ANAKUJA KAMA MWIVI!.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kati ya watoto ambao Daudi aliwapenda sana na wakati huo huo wakamsumbua sana, ni Absalomu. Absalomu alikuwa ni kijana mzuri wa umbo, na vilevile alikuwa ni kijana aliyetumia mbinu za kipekee sana katika kutimiza malengo yake.
Absalomu, alileta taharuki kuu mbili Israeli, Taharuki ya kwanza, ni ile ya kumuua ndugu yake, aliyeitwa Amnoni, mwana wa mfalme, na ya pili ni ile ya jaribio lake la kuupindua ufalme wa Baba yake (Daudi).
Kama wewe ni msomaji wa biblia, kitabu cha 2Samweli sura ile ya 13-19, utakutana na habari hizo, utakumbuka kuwa huyu Absalomu alikuwa ni dada yake wa tumbo moja aliyeitwa Tamari, lakini ikatokea siku moja ndugu yake wa mama mwingine aliyeitwa Amnoni, akamtamani, na mwisho wa siku akamwingilia kwa nguvu, bila kufuata utaratibu, hivyo akamletea aibu kubwa binti Yule, pamoja na ndugu yake. Sasa huyu Absalomu, ambaye ni kaka wa mama mmoja na Tamari, alipopata habari akaudhika sana kwa kitendo kile, akamchukia Amnoni kupindukia.
Lakini tabia moja ya Absalomu,ilikuwa si ya kuchukua maamuzi ya muda huo huo, na ndio maana utasoma, hakuzungumza naye neno lolote lile liwe la heri au la shari, bali alitulia kimya tu. Sio kwamba moyoni alikuwa hawaki.
2Samweli 13:22 “Ila Absalomu hakusema na Amnoni wala kwa heri wala kwa shari; kwa maana Absalomu alimchukia Amnoni kwa kumtenza nguvu umbu lake Tamari”.
Akaanza chini chini kupanga mipango yake, ambayo ilikuja kutimia MIAKA MIWILI MBELE. Na mipango hiyo ilikuwa ni ya kumwangamiza ndugu yake.
Ukisoma utaona alianza kazi ya ukataji manyoya, na alipofanikiwa baada ya miaka miwili mizima akamwalika baba yake na ndugu zake waje washereheke pamoja naye, hivyo akatumia sasa fursa ile kumwomba baba yake yule ndugu yake aliyembaka dada yake, awepo, akakubali, na alipoenda, akamvizia saa amelewa, akatuma watumishi wake wamuue. Lengo lake likawa limetimia hapo hapo. Amnoni akafa. Kirahisi hivyo. Unaweza kujiuliza ni kwanini, Absalomu hakuchukua hatua za haraka tangu mwanzoni? Jibu ni kuwa ipo tabia ambayo Mungu anataka tujifunze kwa mtu huyu, jinsi alivyokuwa mtu wa mikakati.
Baadaye, baba yake alipopata taarifa akataka kumuua, lakini Absalomu akakimbilia taifa lingine akakaa huku muda wa miaka mitatu mizima.Sasa, kwa muda wako fuatilia kisa hicho katika biblia, lakini nataka tuone jinsi tabia yake ile ile ya uvumilivu na malengo ilivyomletea mafanikio mengine makubwa mbeleni.
Ukisoma biblia utaona, ulifika wakati akarudi Israeli, na kwenda kuonana na baba yake, Lakii akiwa kama mgeni alidhamiria ndani ya moyo kuwa mfalme wa Israeli. Kama ilivyo kawaida yake alijua njia pekee sio kuanza kukurupuka na kuleta mapinduzi kwa haraka hapana, hatafanikiwa bali, alijua uvumilivu na bidii, ni nguzo muhimu sana za kutimiza malengo yake.
Hivyo akaanza mikakati yake, biblia inatuambia, akawa anaamka kila siku asubuhi sana na mapema, labda saa 10 alfajiri, anakwenda kusimama, karibu la lango la kuelekea kwa mfalme, ili kukutana na watu wenye shida zao,ambao wanahitaji kutatuliwa. Alipokutana nao, kila mmoja kabla ya kufika kwa mfalme alimbusu, akajinyenyekeza kwake, akamsikiliza shida zake, akamjibu kwa upole, ikawa kila mtu aliyetoka pale alimpenda sana, na mwisho akawa anawaambia, maneno ya uongo, kuwa hakuna mtu anayewajili, kama wakimfanya yeye kuwa mfalme awatafanyia mema mengi..
2Samweli 15:1 “Ikawa baada ya hayo, Absalomu akajiwekea tayari gari na farasi, na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
2 Tena Absalomu huondoka asubuhi na mapema, na kusimama kando ya njia ya lango; kisha ikawa, mtu ye yote aliyekuwa na neno, lililokuwa halina budi kufika kwa mfalme ili kuhukumiwa, Absalomu humwita mtu huyo kwake, na kumwuliza, Wewe u mtu wa mji gani? Naye akasema, Mtumwa wako ni mtu wa kabila fulani ya Israeli.
3 Naye Absalomu humwambia, Tazama, maneno yako ni mema yenye haki; lakini hapana mtu aliyeagizwa na mfalme kukusikiliza.
4 Tena Absalomu husema, Laiti mimi ningewekwa kuwa mwamuzi katika nchi hii, ili kila mtu mwenye neno au daawa aje kwangu, nimpatie haki yake!
5 Tena ikawa hapo alipokaribia mtu ye yote kumsujudia, hunyosha mkono wake, na kumshika, na kumbusu.
6 Hivyo ndivyo Absalomu alivyowatendea Israeli wote, waliomwendea mfalme ili wapate hukumu; na hivyo Absalomu akawadanganya watu wa Israeli.
7 Hata ikawa mwisho wa miaka minne, Absalomu akamwambia mfalme Tafadhali uniache niende nikaondoe nadhiri yangu, niliyomwekea Bwana huko Hebroni”.
Aliendelea hivyo kwa muda wa MIAKA MINEE (4), Mfululizo, akiamka asubuhi, kwa ajili ya kukutana na shida zao hao watu.. Ndipo watu wote, wakamtambua, wakampenda sana, kwa unyenyekevu wake, na kujali kwake, wakamsikiliza hata kwa uongo wake, Absalomu akafanikiwa kujikusanyia wimbi kubwa la watu waliompenda..akapata nguvu, huku baba yake hajui chochote.
Ndipo siku ya siku ilipofika, ghafla, Daudi akasikia mtoto wake Absalomu, amekusanya majeshi ya watu, yanataka kuja kumpindua. Daudi kuona vile ikampasa akimbilie msituni kuokoa maisha yake. Na kama sio Bwana alikuwa upande wake, ule ufalme ulikuwa ni wa Absalomu. Kwasababu watu wengi sana waliandamana naye. Na vita vilivyopiganwa Israeli kipindi hicho vilikuwa ni vikubwa sana, hatuna nafasi ya kueleza habari yote, lakini kwa muda wako soma kwenye biblia utajionea.
Mpaka wakati ambapo Absalomu anakufa, Mfalme Daudi alikuwa ameshapata somo kubwa sana.
Ni nini tunajifunza?
Kumbuka hadithi zote tunazozisoma katika agano lake, zimebeba funzo kubwa kwetu, haijalishi ni za mtu mwovu au mwema. Leo sisi kama watoto wa Mungu, tumekuwa watu wa kutazamia mapinduzi ya wakati huo huo. Tunataka yote tunayoyatazamia yatokee ndani ya usiku mmoja. Kumbe hiyo siyo kanuni, ili tuteke, wakati mwingine tunahitaji uvumilivu na bidii. Itakupasa uhubiri injili kila siku kwa muda wa miaka kadhaa, bila kuona chochote, ndipo baadaye sana uanze kuvuna matunda ya kusumbuka kwako.
Itakugharimu ufanye mazoezi mengi sana ya kuimba, utunge nyimbo nyingi tu, ndipo baada ya kipindi fulani pengine miaka kadhaa, Bwana ndio azifanye nyimbo zako kuwa Baraka kwa watu wengi. Kama unataka karama ya uponyaji itende kazi ndani yako, itakugharimu uwe mvumilivu wa kuchukuliana na matatizo ya watu wengi, kuwaombea kwa bidii, hata kama hutaona lolote katika siku za kwanza kwanza, itakubidi uendelee hivyo hivyo, hata kwa miaka kadhaa pengine, lakini mwisho wake Bwana atakujalia kipawa hicho kwa viwango vingine. Uvumilivu na bidii, inapaswa iwe sehemu ya maisha yetu.
Absalomu, hakuwa mtu wa papo kwa papo, lakini uvumilivu wake na mikakati yake ilimsaidia sana baadaye, kuitikisa Israeli. Hivyo usikate tamaa, unapoona chochote unachomfanyia Mungu sasa, hakizai kama vile unavyotazamia.. Kamwe usife moyo, kinyume chake ongeza bidii. Na wakati utafika utaona matunda ya taabu zako.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.
Katika uvuvi, upo uvuvi wa kutumia ndoano, na pia upo uvuvi wa kutumia nyavu.
Uvuvi wa kutumia ndoano ni uvuvi ambao unahusisha kukamata samaki mmoja mmoja, Hivyo unachukua muda mrefu kidogo na pia una matokeo madogo. Na katikauvuvi huu ni vitu viwili tu vinahusika katika kukamata samaki, navyo ni Ndoano yenyewe, pamojana Chambo!.
Na chambo inayotumika ni kipande kidogo cha mnofu ambacho kitamvutia samaki, hivyo kila samaki anaponaswa basi mvuvi hana budi kuweka chambo nyingine kwaajili ya samaki mwingine. Huu ni uvuvi mzuri lakini unamatokeo madogo na unachukua muda mrefu..
Lakini upo uvuvi mwingine usiotumia chambo ya mnofu lakini una matokeo makubwa. Na huo simwingine Zaidi ya uvuvi wa nyavu! naTaa.
Uvuvi huu mara nyingi unafanyika usiku, ambapo wavuvi wanakwenda kwenye bahari kuu na kisha kuwasha TAA ZAO zenye mwanga mkali. Na wanapoziwasha basi wale samaki wanavutiwa naule mwanga na hivyo kusogelea chombo na hatimaye kunaswa katika zile nyavu. Na matokeo yake ni makubwa sana, samaki wanapatikana wengi na kwa muda mfupi.
Hii inatufundisha nini, CHAMBO YA MWANGA ni bora kuliko CHAMBO YA MNOFU. Na sisi tunaohubiri Bwana Yesu katufananisha na wavuvi. Na ulimwenguni bahari. Na kama vile wavuvi wanavyokwenda kuvua usiku, kadhalika na sisi tunakwenda kuvua watu katika ulimwengu wenye giza nene. (Ulimwengu uliopotea, watu waliozama katikagiza la ulimwengu, ambao shetani kawapofusha macho wasione).
Lakini chambo yetu sisi si minofu ya nyama..Hiyohaitakuwa na matokeo yoyote katikati ya giza nene la bahari kuu. Chambo tunayohitaji ni TAA ZINAZONG’AA SANA.
Mathayo 5:4 “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.
15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.
16 VIVYO HIVYO NURU YENU NA IANGAZE MBELE YA WATU, WAPATE KUYAONA MATENDO YENU MEMA, WAMTUKUZE BABA YENU ALIYE MBINGUNI”.
Kama vile Taa za wavuvi zinavyovutia samaki wengi wakati wa usiku, kadhalika na sisi MATENDO YETU (ambayo ndio mianga kwa ulimwengu), hayo ndio yanayohubiri sana na yanayo wavuta wengi kwa Kristo kuliko, miujiza tutakayoifanya, au lugha tutakazoongea, au karama zetu au kingine chochote kile.
Kumbuka siku zote chambo iliyo bora ni TAA ZETU ZINAZOWAKA (Ambayo ndio matendo yetu), kwa jinsi taa zetu zinavyozidi kung’aa ndivyo mianga yetu inapoonekana mbali na kuvutia samakiwengi Zaidi..lakini taa zetu zikiwa hafifu, hakuna samaki yeyote tutakayemvuta kwa nyavu zetu.
Wafilipi 2:15 “mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, walaudanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa KAMA MIANGA katika ulimwengu”.
Je Nuru yako inaangaza katikati ya huu ulimwengu wa giza??
Bwana atusaidie na kutubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Walawi 19:14 “Usimlaani kiziwi, wala usitie kwazo mbele ya kipofu, bali umche Mungu wako; Mimi ndimi Bwana”.
Vifungu hivyo vinatuonyesha, tabia ya watu ambao wanatumia udhaifu wa watu wengine kuwaletea madhara au matatizo zaidi badala ya kuwasaidia.
Kibinadamu ukikutana na kipofu njiani, na anataka asaidiwe kuvuka barabara, bila shaka utamwonea huruma na kwenda kumshika mkono umvushe, huwezi kwenda kumvizia wakati gari linapita ndio umsogeze barabarani agongwe afe, afe huo sio utu.
Lakini cha ajabu ni kwamba hao watu wapo. Kwa mfano utakuta mtu anataka kununua bidhaa fulani, lakini kwa bahati mbaya mteja huyo hajui sana ubora wa bidhaa hizo, labda tuseme simu. Sasa muuzaji badala atumie busara kumwelekeza bidhaa bora, kinyume chake anatumia fursa ile, kwenda kumletea feki, na kumuuzia kwa bei ile ile ya orijino, kisa tu haijui orijino ipoje. Na mwisho wa siku mnunuzi anaitumie siku mbili tatu, imeharibika, anaitupa, anakuwa amepata hasara. Sasa huo ndio ukwazo Bwana anaouzungumzia hapo mtu anaomwekea kipofu.
Hilo jambo linamkasirisha sana Mungu, Na kwa bahati mbaya wafanyabiashara wengi sana wanayo tabia hii. Ni tabia ya shetani, ambayo alikuwa nayo tangu zamani, Utakumbuka pale Edeni alipoona Hawa ni kipofu, hajui mema na mabaya, akatumia udhaifu huo kumdanganya, badala ya kumwelekeza kuyashika maagizo ya Mungu, na mwisho wake ukawa ni Hawa kutumbukia shimoni. Sasa wapo baadhi ya wanadamu waliokosa UTU namna hii, wanatumia udhaifu wa watu wengine kujitafutia faida zao.
Au utakuta ni mama ntilie, anaona akipika chakula bora hapati faida ya kutosha, anachowaza ni kwenda kutia hamira kwenye ubwabwa wake, ili uvimbe awauzie wateja wengi zaidi, kwasababu anajua wateja wanapenda chakula kingi, Na amekuwa akifanya hivyo kwa muda mrefu, Hiyo yote ni kisa tu haonekani kwa wateja, wakati mwingine anapikia na mafuta ya trasfoma.. Hiyo ni dhambi inayomchukiza sana Mungu.
Walawi 19:14 “Usimlaani kiziwi, wala usitie kwazo mbele ya kipofu, bali umche Mungu wako; Mimi ndimi Bwana”.
Mwingine ni mtumishi wa Mungu, anakutana na mtu mwenye matatizo fulani, pengine ya kiafya, au ya kifamilia, au ya kiroho sasa yeye badala amuhudumie kama mtumishi wa Bwana,anatumia nafasi hiyo ya udhaifu wake, kumtisha, na kumpa shuhuda za uongo, lengo tu ni atumie fursa hiyo kuchukua pesa zake. Watu kama hawa nimeshakutana nao sana. Huko ndio kutia kwazo mbele ya kipofu, na kumlaani kiziwi.
Tunapaswa tuwe kama Ayubu, ambaye alisema..
Ayubu 29:15 “Nalikuwa macho kwa kipofu, Nalikuwa miguu kwa aliyechechemea”.
Tuwasaidie wale ambao wanahitaji msaada, vilevile tuwaongoze mahali sahihi wale ambao wanahitaji kusaidiwa. Tumche Bwana wetu, Tupate siku nyingi na za heri za kuishi katika dunia yake.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.
Shalom, Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya Bwana wetu.
Katika mambo ya uvuvi, zipo kanuni za uvuvi za kufuatwa, wengi wetu tunadhani, kazi ya mvuvi ni ya kwenda tu kutupa nyavu baharini, kukusanya samaki, kisha kuwatoa nje, halafu basi analala, anaamka tena kesho na nyavu yake hiyo hiyo, anakwenda kuitupa habarini na kuvua samaki wengine tena.. Ndugu Kama umekuwa ukifikiria hivyo basi umekosea.. Vinginevyo kazi ya uvuvi ingekuwa ni rahisi sana.
Kwa kawaida, wavuvi ni sharti, kila wamalizapo uvuvi mmoja, wazioshe nyavu zao kama sio kuzitengeneza, Kwasababu wanapokwenda kuvua sio tu samaki peke yake wanajinasa kwenye nyavu, bali pia kunakuwa na takataka nyingine nyingi zinakwama kwenye neti, sana sana magugu ya baharini, masalia ya magamba ya viumbe , na matope, kiasi kwamba nyavu zile zikiachwa, siku kadhaa bila kuoshwa, vinavundisha nyavu.
Na si hilo tu, kunakuwa na samaki waliokufa, katikati ya neti, nao pia wakaachwa kipindi kifupi sana wanaozesha , na hiyo inapelekea kukaribisha panya kula neti, na kuifanya iwe dhaifu sana, hususani kwenye kamba zake,
Na bado wanasema, ili samaki wawezi kukamatwa kiwepesi, ni sharti ni yenyewe iwe kama vile haionekani itupwapo habarini ,lakini kama inauchafu mwingi, wanasema samaki wakiona, wanaogopa na kukimbia.
Pia nyavu hiyo hiyo inapaswa itengenezwe/au ifanyiwe ukarabati, kwasababu wakati mwingine, kunakuwa ni miamba yenye ncha kali chini inayochana nyavu, au samaki wenye miiba mikali ambao wakipita mara moja tu katikati wanachana nyavu. Hivyo kama mvuvi kila unapoliza kuvua ni sharti ukague neti yako kama inamatundu uizibe.
Hivyo suala la kusafisha na kukarabiti neti ni lazima kwa mvuvi yeyote kila anapomaliza kuvua, haijalishi siku hiyo amepata samaki au hajapata. Haijalishi atakuwa amechoka au hajachoka, Ni lazima aisafishe, kwasababu ni lazima tu itakuwa na uchafu.
Na ndio maana wakati ule Bwana Yesu alipokuwa anapita pwani aliwaona akina Petro, wametoka kuvua samaki, na hawajapata chochote usiku kucha, lakini kanuni ilikuwa ni lazima wazioshe nyavu zao, haijalishi walipata au hawakupata.
Luka 5:1 “Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,
2 akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, LAKINI WAVUVI WAMETOKA, WANAOSHA NYAVU zao.
3 Akaingia katika chombo kimoja, ndicho chake Simoni, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.
4 Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.
5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu”.
Umeona, sasa soma tena vifungu hivi, uone kuna wakati pia walizitengeneza nyavu zao, na sio kuosha tu peke yake.
Marko 1:19 “Akaendelea mbele kidogo, akamwona Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, nao pia walikuwa chomboni, WAKIZITENGENEZA NYAVU ZAO.
20 Mara akawaita, wakamwacha baba yao Zebedayo ndani ya chombo pamoja na watu wa mshahara, wakaenda, wakamfuata.
SASA MAMBO HAYO KATIKA ROHO YANAFUNUA NINI?
Sisi kama wahubiri, sisi kama watumishi wa Mungu tunaofanya kazi ya kuwavua watu kwa Kristo, huwa tunajisahau sana na kudhani kuwa kuhubiri tu kunatosha, Au kufundisha tu, au kushuhudia tu. Hatujui kuwa tunapaswa kila siku TUSAFISHE na kutengeneza NYAVU zetu, tunazozitumia kuvulia.
TUNATENGENEZAJE NYAVU ZETU?
Na tunazitengeneza kwa NENO LA MUNGU. Ikiwa na maana tunapaswa Neno la Mungu likae kwa wingi ndani yetu, tusome Neno, tujue misingi na kanuni za uvuvi Kristo anazozitaka, tujue ni nini tunapaswa tufundishe, na nini tusifundishe kwa wakati husika, ujumbe upi tutoe, na upi tusitoe kwa watu fulani. Vinginevyo tukipuuzia, tutajikuta samaki watapenya kwenye nyavu zetu, tukawakosa, kwasababu zina matundu matundu.
TUNAOSHAJE NYAVU ZETU?
Vile vile, Kuosha nyavu zetu. Ni kwa kujitakasa maisha yetu. Maana yake kuishi maisha yanayompendeza Mungu, maisha ya ushuhuda, maisha matakatifu. Ikiwa tuna ushuhuda mbaya katika mazingira yanayotuzunguka, na huku bado tunahubiri injili ni kuonyesha kuwa NYAVU zetu ni chafu. Hivyo Samaki watatukimbia wanapoona uchafu huo kwetu. Na ndio maana pale tunapovua hatuona matunda yoyote, kumbe ushuhuda wetu ndio unaowakimbiza mbali na sisi.
Hivyo ni wajibu wetu, sisi kama wahubiri kuzingatia hayo mambo mawili kila siku. Kwasababu wavuvi nao wanafanya hivyo kila siku. Nasi tuifuate kanuni hiyo rohoni. Na hakika tutamletea Kristo matunda mengi.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha sasa tuzidi kuyatafakari maneno matukufu ya Mungu wetu, Maadamu katujalia kuiona leo.
Kwanini leo hii imekuwa ngumu sana kuipeleka injili kwa watu walio nje, ili wamwamini Yesu Kristo (Tukisema walio nje, tunamaanisha watu wa kidunia, au watu walio katika dini nyingine), Tunaweza kusema Mungu anawajua walio wake, ni kweli, lakini hicho sio kisingizio, ipo sababu nyingine ambayo tumeikosa sisi kama kanisa na sababu yenyewe ni kukosa UMOJA.
Tukiupata huo kama kanisa basi hatutamia nguvu nyingi sana kuulezea ulimwengu uzuri wa Yesu, bali huo umoja wenyewe tu utauaminisha ulimwengu yeye ni nani.
Bwana Yesu alilizungumza hilo katika..
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Umeona, kumbe ulimwengu unaweza kumwamini Yesu, kuwa ndiye mwokozi wa ulimwengu, ikiwa tu tutajitengeneza sisi kwanza katika umoja. Lakini tunapaswa tujue si kila umoja, ni umoja sahihi unaotokana na Mungu..Hapo Bwana hazungumzii umoja wa kichama au umoja wa kidini, au umoja wa kimadhehebu, kama unaoendelea sasa hivi ulimwenguni.. bali umoja anaouzungumzia hapo ni umoja wa Roho,. Kwasababu haiwezekani watu wawili wanaamini vitu viwili tofauti, halafu wawe na umoja, huo sio umoja utakuwa ni umoja wa kimaslahi tu, lakini sio wa Roho.
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.
Umeona vifungu hivyo? Agizo mojawapo ni kwamba tuutambue ubatizo mmoja na sahihi ni upi, kisha wote tuwe nao, ambao ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5, kisha wote tumpokee Roho mmoja, ambaye ndiye Roho Mtakatifu, tuwe na Bwana mmoja ambaye ni YESU KRISTO jiwe kuu la pembeni, na sio mtume mwingine, au mtakatifu mwingine pembeni yake hapana,.. Na vilevile tuwe na Imani moja, ambayo mzizi wake na shina lake ni BIBLIA TAKATIFU na sio dini au dhehebu.
Tukizingatia hayo, kisha tukashirikiana na ulimwengu ukatuona, basi hatutatumia nguvu kubwa kuwaamishi Kristo kwao, kwani huo umoja wenyewe tu utawahubiria watu uzuri wa Kristo. Lakini tukizidi kuupoteza umoja huo, kila mtu na imani yake, dhehebu lake,. Ni ngumu sana kuugeuza ulimwengu. Hivyo ni wajibu wetu sisi, kama kanisa la Kristo tujipime, je! Umoja huu uliosahihi upo ndani yetu? Kama haupo, basi ipo kasoro. Tujitahidi sana tuunde kwa bidii zote, ili Bwana aaminiwe katikati ya mataifa, matunda mengi yaje kwake..
Hilo ni agizo la Bwana, na sio la mwanadamu.
“Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Shalom.
Maran atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo: