Mwandishi wa kitabu cha wimbo uliobora.

Mwandishi wa kitabu cha wimbo uliobora.

Aliyekiandika kitabu hiki ni Sulemani, mwana wa Daudi. Kufuatana na utambulisho wake mwanzoni kabisa mwa kitabu hichi.

Wimbo 1:1 Wimbo ulio bora, wa Sulemani

Mfalme Sulemani alijaliwa hekima na Mungu kuandika nyimbo nyingi sana Pamoja na Mifano mingi. Kama 1Wafalme 4:32 inavyosema aliandika Nyimbo elfu moja, na tano.

Sasa miongoni mwa hizo nyimbo, basi huu ulikuwa mmojawapo. Na ndio uliokuwa bora kuliko zote. Ndio maana umeitwa wimbo ulio bora.

Ni sawa na kusema Mfalme wa Wafalme, au Patakatifu pa Patakatifu. Ikiwa na maana kuna pazuri  kweli, lakini papo pazuri Zaidi ya kote, au kuna wafalme kweli lakini yupo aliyezidi wote. Ndivyo ilivyo katika vitabu vya Sulemani.

Hichi ndio kitabu ambacho, kimebeba hekima ya juu kuliko zote Sulemani alizojaliwa na Mungu kuziandika. Ni kitabu chenye maudhui ya kimahusiano kati ya mtu na mpenzi wake, ikifunua mahusiano yaliyopo kati yetu sisi na Kristo rohoni.

Kwa Maelezo mapana juu ya uchambuzi wa kitabu hichi bofya hapa >>> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Lakini pia kwa mafunzo mbalimbali yaliyomo ndani ya kitabu hichi, bofya masomo yafuatayo.>>

 Nini maana ya Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, (Wimbo 2:7)

USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO

NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

 

 

Print this post

About the author

Nuru ya Upendo administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments