Category Archive Home

Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?

Kiango ni kifaa maalumu cha kushikilia au kuning’inzia taa, tazama picha, kwa jina lingine kinaitwa kinara. Na nilazima kinyanyuke au kiwe sehemu ya juu kidogo, ili kuruhusu mwanga wa hicho kilicho juu yake (yaani taa) kuangaza mahali pote.

kiango

Na Pishi ni bakuli dogo, au kapu ndogo. Tazama picha,

Hivi ni vifungu ambavyo utaweza kukutana na maneno hayo;

Mathayo 5:15 “Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani”.

Marko 4:21 “Akawaambia, Mwaonaje? Taa huja ili kuwekwa chini ya pishi, au mvunguni? Si kuwekwa juu ya kiango”?

Luka 11:33 “Hakuna mtu awashaye taa na kuiweka mahali palipositirika, au chini ya pishi; bali huiweka juu ya kiango, ili waingiao wapate kuuona mwanga”.

Soma pia Luka 8:16

Hivyo mpaka hapo tunaweza kupata picha sasa Bwana Yesu alimaanisha nini kutoa mfano huo, kuwa tunapoamua kuokoka hatupaswi kuuficha wokovu wetu, kuuweka chini ya bakuli bali ni sharti tuungaze kwa watu wote, kwanza kwa matendo yetu na pia kwa kuwahubiria ili kusudi kwamba wavutwe na wao katika wokovu tulionao.

Na ndio maana pale kwenye Mathayo 5:15 akamalizia na kusema..

16 “Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Shalom.

Tazama maana nyingine ya maneno ya biblia chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

Bwana Yesu alimaanisha nini aliposema; Mafarisayo Hupanua HIRIZI zao, na kuongeza MATAMVUA yao?

GOGU NA MAGOGU, Katika biblia ni nani?

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Shalom, jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe milele.

Karibu tujifunze Neno lake.

Ukisoma kitabu cha Ufunuo sura ya 12, utaona habari kuu inayouzungumziwa pale ni kuhusu mapambano ambayo aliyafanya tangu akiwa  mbinguni, na anayoendelea kufanya hadi sasa.

Utaona mapambano hayo yamegawanyika katika vipengele vikuu vitatu. Cha kwanza vita ile aliyoifanya mbinguni akiwa na malaika zake, ambayo alishindwa, na matokeo yake akatupwa chini,

Kipengele cha pili utaona ni ile vita aliyoifanya na yule mwanamke aliyemzaa mtoto mwanaume, ambaye nchi ilimsaidia. Na mwanamke yule analiwakilisha Kanisa la Israeli  kwa ujumla. Wakati Bwana Yesu anazaliwa, utaona shetani kwa kupitia Herode alikuwa ameshaanza kuleta maafa Israeli, kwa kuwaaua wale watoto wote waliozaliwa wakati mmoja na Yesu, lengo likiwa ni kumwinda Yesu, afe, Lakini Mungu akamuhamisha Kristo akilimbilie Misri kwa muda, na hiyo ilikuwa ni kulinusuru taifa zima.

Na kipengele  cha tatu na cha mwisho ambayo ndio kiini cha somo letu la leo  Ni vita ambayo shetani aliita kwa uzao wake wote wa huyo mwanamke uliosalia. Yaani wote watakaofanana na Kristo, waisraeli wa rohoni, hao ndio anamalizia kufanya nao vita , na vita hiyo ni endelevu, ilianza  tangu kipindi kile Kristo anaondoka duniani, mpaka leo hii, na itaisha na unyakuo.

Lakini kuna jambo moja la kuona pale, shetani alipoanza kufanya vita na kanisa la Kristo, hakusimama mbinguni tena au nyuma yetu kuleta mafuriko, kama alivyofanya kwa yule mwanamke, hapana, bali biblia inatuambia alikwenda kusimama JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake AFANYE VITA JUU YA WAZAO WAKE WALIOSALIA, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI”.

Sasa mchanga wa bahari unawakilisha nini?

Hapo inaposema kwenye mchanga wa habari inamaanisha kwenye  ufukwe, yaani alikwenda kusimama ufukweni, mpakani, kati ya habari na nchi kavu. Hii ikiwa na maana vita vyake hasa vipo pale mpakani, kuhakikisha kinachotoka habarini hakiji nchi kavu. Na hata kama kikitokea kimevuka nchi kavu, basi hakitapita hivi hivi tu.

Sasa kibiblia habari au palipo na maji mengi inawakilisha ulimwengu,(Ufunuo 17:15) ..Na nchi kavu ni wokovuni..Bwana Yesu alimwambia Petro njo nami nitakufanya kuwa mvuvi wa watu. Yaani kuwatoa watu kutoka kwenye ulimwengu na kuwaleta katika Nuru ya wokovu,

Hii ikiwa na maana mtu yeyote ambaye hajaokoka, kwamba yupo baharini, hivyo akishaokoka, ni anakuwa anahamishwa kutoka kwenye maji na kuletwa nchi kavu.

Hivyo sasa tunamwona hapa shetani kasimama ufukweni, lengo lake likiwa ni kukipinga kile kinachotoka kule kuja nchi kavu. Kumpinga mtu Yule ambaye anataka kutoka kwenye dunia na kuja katika wokovu. Mtu yule nayetaka kuacha kuishi maisha yake machafu na kuja katika maisha mapya ya utakatifu. Hapo ndipo vita vya ibilisi vilipo haswaa.

Hapo ndipo utakapokutana na shetani, hakuna mahali pengine utamwona ibilisi kwa uwazi wote kama hapo. Ndio vita vyake vilipo. Hatahangaika na wewe ambaye sikuzote upo dhambini, wala hutamwona akikugasi, lakini siku ambapo unafanya uamuzi ndipo utakapomwona akitaka kukusumbua, kama vile alivyotaka kumwangamiza Kristo tu alipozaliwa duniani.

Lakini ni wajibu wetu kumshinda, na tunamshinda kwa damu ya mwanakondoo na kwa Neno la ushuhuda wetu sawasawa na

Ufunuo 12:11 “Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.

Hivyo kaa ukijua kuwa pale unapotaka kufanya badiliko la kweli la maisha hapo ndipo pa muhimu sana, na shetani analijua hilo na ndio maana anasimamia hapo, kwahiyo ni wajibu wako kumshinda, haijalishi ataleta vita vya aina gani, Kumbuka hizi ni siku za mwisho, na Bwana Yesu alisema, ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu ndio watakaouteka. Mathayo 11:12

Kwahiyo huna sababu ya kuanza kuogopa kudharauliwa, au kuchekwa, au kutengwa au kudhihakiwa kisa tu umeamua kuokoka au kuishi maisha ya wokovu. Jitwike msalaba wako umfuate Yesu, ili upokee taji la ushindi ufikapo kule.

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

JINSI  DHAMBI ILIVYO NA SHINIKIZO KUBWA SANA.

ROHO ANENA WAZIWAZI

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

JIFUNZE KUTOA KATIKA HAZINA YAKO VITU VIPYA NA VYA KALE.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI  DHAMBI ILIVYO NA SHINIKIZO KUBWA SANA.

Wakati mwingine kuna mambo unasoma kwenye biblia unaishia kuogopa sana, hususani pale unapoona mtu Mungu anafanya mambo ambayo hata mwenye dhambi si rahisi ayafanye. Kwamfano embu tuwaangalie hawa watu wawili, [Daudi na Yuda]. Hawa wote tunajua walikuwa ni watiwa mafuta wa Mungu, tukianzana na Daudi, tunajua alikuwa ni shujaa sana, na katika ushujaa wake, aliweza kuchagua mashujaa wake wengine 37 waaminifu ili kumsaidia katika vita, na kuipigania Israeli.

Lakini katikati ya mashujaa hao kulikuwa na mwingine ambaye alikuwa mwaminifu sana pengine hata Zaidi ya mashujaa wengine wote, na huyo aliitwa Uria. Uaminifu wake tunausoma jinsi ulivyokuwa.. hakuwa tayari kwenda kujiburudisha nafsi yake wakati kazi ya vita haijamalizika, na wenzake wapo bado mapambanoni, haijalishi kuwa ni mfalme ndiye aliyempa ruhusu ya kuondoka, hakuwa tayari kuondoka. 

2Samweli 11:8 “Daudi akamwambia Uria, Haya, shuka nyumbani kwako, ukanawe miguu yako. Basi Uria akatoka katika nyumba ya mfalme, na tunu ya vyakula ikamfuata, iliyotoka kwa mfalme.

9 Lakini Uria akalala mlangoni pa nyumba ya mfalme, pamoja na watumishi wote wa bwana wake, wala hakushuka nyumbani kwake.

10 Watu walipomwambia Daudi ya kwamba, Uria hakushuka nyumbani kwake, Daudi akamwambia Uria, Je! Hukutoka safarini? Mbona hukushuka nyumbani kwako?

11 Naye Uria akamwambia Daudi, Sanduku, na Israeli, na Yuda, wanakaa vibandani; na bwana wangu Yoabu, na watumishi wa bwana wangu, wamepiga kambi waziwazi uwandani; nami niende nyumbani kwangu, kula na kunywa, na kulala na mke wangu? Uishivyo, na kama roho yako iishivyo, mimi sitafanya jambo hili. 12 Basi Daudi akamwambia Uria, Ngoja hapa leo tena, na kesho nitakuacha kwenda zako. Basi Uria akakaa Yerusalemu siku ile, na siku ya pili yake.

13 Naye Daudi akamwalika, akala, akanywa mbele yake; naye akamlevya; hata wakati wa jioni akatoka kwenda kulala kitandani mwake pamoja na watumishi wa bwana wake, lakini hakushuka nyumbani kwake.”

Unaweza ukajiuliza, mtu kama huyu, labda ndio angependwa kipekee na Daudi, na kupewa zawadi nyingi kwa moyo wake huo wa uaminifu na Upendo, lakini kinyume chake Daudi ndio akampangia njama za kumwangamiza. Tena kumwangamiza katika huo huo uaminifu wake.. Na akafanikiwa,  akamuua kwenye vita, pale alipowaambia mashujaa wake wamwache mwenyewe auawe.

Huyo ndio Daudi mtiwa mafuta wa Bwana,  Lakini ni nini kilichompelekea afanye vile, hakufanya vile kwasababu alipenda, bali kwasababu ya shinikizo la dhambi lililokuwa nyuma yake. Na dhambi yenyewe ilianzia pale, alimuona mke wa Uria, akamtamani, kisha akamchukua alale naye, akadhani itaishia pale pale tu, hakujua kuwa madhara Zaidi yanaweza kuja, matokeo yake akapata mimba yule mwanamke, Na Daudi alipoona hivyo akataka kumbambikizia Uria mimba ambayo si yake ,  ili tu kusitiri aibu, ndio maana akampa likizo ya ghafla, ili akalale na mkewe, lakini Uria alikuwa mwaminifu hakukwenda kulala na mke wake, alibaki kambini, ndipo Daudi ikambidi abuni mbinu nyingine ya kusitiri uovu wake, ndipo akaamua kukiua kiungo chake kiteule, kisichokuwa na hatia yoyote. Hilo ndio shinikizo la dhambi.

Mwingine ni Yuda, huyu naye alianza dhambi kidogo kidogo tu, ya wizi, hakujua tamaa hiyo itampelekea kuisaliti damu isiyokuwa na hatia, akadhani  ni mambo rahisi rahisi tu, akaendelea kuwa mwizi, mpaka ikafikia hatua ile dhambi iliyokuwa ndani yake ikamshinikiza, kupata hela nyingi Zaidi na njia pekee ambayo ingempelekea kuipata ni kwa kumsaliti Bwana wake, Mtakatifu ili wale wakuu wa makuhani wampe Hela.

Sasa usidhani kwamba kumsaliti Bwana wake ambaye alijua anampenda upeo, na kumweshimu ilikuwa ni jambo analolifurahia sana, hapana, bali lile shinikizo la dhambi ndio lililompelekea kuchukua maamuzi ambayo yalimletea majuto ya milele.

Yuda alimsaliti Bwana wake, alimsaliti jemedari wake, alimsaliti mwokozi wake aliyependa, kwa dhambi ndogo tu ya kupenda fedha na wizi.

Huoni leo hii watu wanawatoa ndugu zao kafara kwa waganga wa kienyeji, unadhani hawawapendi ndugu zao, wanawapenda lakini lile shinikizo la dhambi ambalo lilianza zamani kama tamaa tu ya mali ndilo lililowafikisha mahali ambapo inawagharimu wafanye hivyo, wasipofanya ndio wamekwisha.

Huoni leo hii mabinti wengi, wanatoa mimba ovyo, kama vile si kitendo cha uuaji wanachokifanya. Usidhani hawawapendi watoto wao, lakini lile shinikizo la dhambi pengine la kukwepa aibu, kukwepa kutengwa, kukwepa kufukuzwa shule, kukwepa  majukumu, linawafanya watende vitendo hivyo vya kinyama kila kukicha.

Hata wewe leo hii usidhani huwezi kumuua mtu kwa kumpiga risasi, usidhani huwezi kufanya mambo ya ajabu kupindukia, usiseme hivyo kama ni mtendaji wa dhambi hizo ambazo unaziona za kawaida tu, unaweza kutenda tena na ukawa ni mnyama kuliko hata magaidi wenyewe, kama utaivumilia dhambi ndani yako, Haijalishi utajiita ni mtumishi wa Mungu.

Dhambi ni ya kuiogopa sana, usiseme yule ni mke wa mtu ngoja nikazini naye  leo tu basi, hakutakuwa na shida yoyote, usijaribu kufanya hivyo ndugu, usiseme ngoja niibe kile kidogo kwenye kampuni, hakitaniletea madhara yoyote, usifanye hivyo.. Dhambi inashinikizo kubwa sana, inakupeleka mahali ambapo huwezi kuchomoka mpaka ufanye kufuru mbaya sana. Laiti Daudi au Yuda angelijua tangu mwanzo kuwa watasababisha damu  zisizo na hatia  kumwagika wasingedhubutu kufanya mambo kama yale.

Lolote unaloliona ni dogo maadamu ni dhambi jiepushe nalo tu, kwa usalama wa maisha yako ya rohoni.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

Je mtu anayeua anabeba dhambi zote za yule aliyemuua?

USIINGIE MKATABA NA DHAMBI.

ROHO ANENA WAZIWAZI

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

ROHO ANENA WAZIWAZI

Shalom..Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Neno la Mungu linasema katika…

1 Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani”

Maana ya kunena waziwazi ni kwamba…“ananena pasipo maficho yoyote wala pasipo siri yoyote”..yapo mambo ambayo Roho Mtakatifu akiyanena yanahitaji ufunuo mpana kutoka kwake..kwamfano utaona katika kitabu cha ufunuo sehemu kadha wa kadha, anasema “yeye aliye na sikio na asikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”. Au kwa lugha rahisi ni sawa na kusema “yeye mwenye akili na aweze kuyajua haya yanayozungumzwa maana yake ni nini”..kwamaana inahitajika ufunuo kuyajua.

Kwamfano tunaweza kujifunza mfano mmoja, ambapo Roho hajanena waziwazi.

Ufunuo 2:26 “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu.

28 Nami nitampa ile nyota ya asubuhi.

29 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”

Hapo Roho kanena..lakini si wazi..kwasababu atakayesoma hajaambiwa nyota ya asubuhi hapo ni nini, wala hajaambiwa hao mataifa atakaowachunga ni wakina nani…maana yake mambo hayo yote yanahitaji ufunuo wa Roho kuyaelewa…hayajanenwa waziwazi..

Lakini katika hiyo 1Timotheo 4 biblia inasema Roho anena waziwazi..kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na Imani, wakisikiliza roho zidanganyazo….na mafundisho ya mashetani..

Hapo anasema wakizisikiliza roho zidanganyazo…na si wakizitazama au wakiziabudu..bali wakizisikiliza..maana yake hizo roho zinazungumza na zipo nyingi.

Sasa hizo zinazungumzaje?

Roho hizi zinazungumza kwa njia kuu mbili.

1. Katika nafsi ya mtu
2. Kupitia watumishi wa shetani, ambao wamevaa mavazi ya kondoo.

1. Katika nafsi ya mtu ni pale mtu anaposikia sauti au msukumo wa kwenda kufanya jambo lililo kinyume na mapenzi ya Mungu.. Kwamfano kama mtu atasikia sauti ikimwambia akatoe mimba, au akaue, au akaibe, akaabudu sanamu au akafanye uasherat, ukavae nguo za nusu uchi, ukapake lipatick, ukavae suruali kwa mwanamke, ukaende kwa waganga, ukaachane na mke wako/mume wako wa ndoa..n.k.kama akiisikiliza hiyo sauti na kwenda kufanya mojawapo ya hayo tayari atakuwa kasikiliza roho hiyo idanganyayo.

2. Vile vile kama atamsikia mtu au mhubiri akimshawishi kufanya mojawapo ya mambo hayo hapo juu tayari, na kwenda kufanya kama alivyosikia kutoka kwa huyo mtu au mhubiri, tayari atakuwa ameisikiliza roho hiyo na imeshamdanganya, aidha kwa kujua au kwa kutokujua..kupitia huyo mhubiri.

Hivyo Roho anatuambia waziwazi kuwa nyakati za mwisho ambazo ndizo hizi watu wengi sana watakuwa wanazisikiliza hizi roho..na si wachache bali ni wengi..Hivyo ni wajibu wetu kuwa macho,na kuwa makini sana ili tusiwe miongoni mwa hao “wengi”…ndio maana ametuambia waziwazi ili tujue hali halisi, na tuweze kujilinda.

Huu ni wakati wa kuzichunguza sana roho..niliwahi kukutana na mtu akaniambia ameokoka na anaamini sana sauti yoyote inayomjia ndani yake ni ya roho mtakatifu..Nikamuuliza anatumia nini kuipima hiyo sauti.. akasema anatumia hisia tu…hivyo hawezikudanganyika.
Ndugu hata uwe mhubiri mkubwa kiasi gani, hata uwe unanena kwa lugha, hata uwe unatabiri, au unaona maono, hata uwe kila siku unatembelewa na malaika..roho za yule adui yetu shetani hazichunguzwi kwa ujuzi au utaalamu au uzoefu fulani au kwa hisia..hapana!! bali zinachunguzwa kwa Neno la Mungu tu..

Maana yake ni kwamba hata kama nimeokoka sio kila sauti inayokuja ndani yangu ni ya kuiamini, bali ni lazima ipimwe na neno la Mungu..kama inakubaliana na Neno hiyo ni sauti kutoka kwa Mungu..lakini kama inapingana na Neno, haijalishi imekuja kwa nguvu kiasi gani, au umekuja na amani kiasi gani, au imekuja na hisia nzuri kiasi gani…hiyo si ya kuifuata ni sauti kutoka kwa yule adui. Biblia inasema..

2 Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru”.

Na neno la Mungu tunalijua kwa kusoma biblia kwa bidii sana…hiyo ndiyo silaha.
Kumbuka tena usisahau neno hili… Roho anena waziwazi, kuwa nyakati za mwisho wengi watajitenga na Imani, na kusikiliza roho zidanganyazo… ni maombi yangu kuwa mimi na wewe hatutakuwa miongoni mwa hao “wengi”.

Kama hujampokea Yesu mpaka sasa, kwasababu fulani fulani, unazozijua wewe, fahamu kuwa umeshasikiliza roho hizo na zimekudanganya…Hivyo fungua leo macho yako na mgeukie Kristo uanze upya, naye atakupokea na kukusaidia kwasababu anatamani wewe uwe na uzima kuliko wewe unavyotamani.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine


Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO YA MASHETANI

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

Rudi nyumbani

Print this post

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

Ulishawahi kujiuliza ni kwanini Roho Mtakatifu alicheleweshwa kushuka juu ya mitume ikawachukua muda mrefu  kidogo, Na hata baada ya Yesu kufufuka tunaona iliwapasa tena kungojea kwa muda wa siku 50? Ulishawahi kujiuliza ni kwanini? Sio kwamba walikuwa hawastahili kupokea Roho Mtakatifu tangu zamani, hapana lakini ndio tabia ya Roho Mtakatifu aliyojiwekea, na anafanya hivyo kwasababu zake maalumu.

Hawi mwepesi sana kushuka juu ya mtu kwa haraka kwasababu anajua akishashuka huwa hashuki kwa kipimo au nusunusu, au kuchunguza chunguza. Na ndio maana Bwana Yesu alisubiri kwanza, wanafunzi wake wakamilishwe katika madarasa yake, ili kusudi kwamba watakaposhukiwa na Roho kile kilicho ndani yao kitendeke kwa ufasaha ziadi kama kilivyokusudiwa.

Roho Mtakatifu anafananishwa na MVUA,  Na kama tunavyojua mvua sikuzote ikishuka huwa haichagui hapa kuna ngano au magugu, au mboga, au bangi, au mbigili kazi yake ni kwenda kustawisha tu, hiyo ndio kazi yake. Hivyo ni wajibu wa mwenye shamba kuhakikisha kitu alichokipanda shambani kwake ni chenye manufaa, ahakikishe shamba lake amelipalilia vya kutosha, kwamba hakuna mbegu za magugu chini ya ardhi,vinginevyo itakuwa ni kwa hasara yake mwenyewe pale mvua itakaponyesha na kustawisha magugu badala ya chakula.

Na ndivyo Roho Mtakatifu alivyo, anaposhuka juu ya mtu au kanisa, huwa anakuza au kukiwezesha kile ambacho kimeshapandwa ndani yake. Na ndio maana anaitwa msaidizi, Sasa Kama ulitubu dhambi zako, ukawa unaishi maisha matakatifu, ukawa unabidii katika kumtafuta Mungu, basi Roho akija juu yako, anaikuza hiyo mbegu iliyopo ndani yako, kuwezesha kumjua Mungu zaidi na kuishi hayo maisha kwa viwango vingine vya juu sana.

Na ndio hapo atakuongezea vipawa na karama ili kuhakikisha unafikia pale ambapo umepakusudia na Mungu ufike na hata zaidi. Lakini pale atakaposhuka juu yako, na bado haujajiweka tayari kwa Mungu, kinyume chake, ni mzinzi, au unayo mambo yako ya kidunia, na bado unasema ni  mkristo, atakuja kweli na akija hatakufanya uwe mtakatifu bali atakufanya uwe mwovu zaidi. Hapo ndipo wengi wetu hatujui. Tendo hili katika biblia sehemu nyingine imeitwa “nguvu ya upotevu” itokayo kwa Mungu.. Soma 2Wathesalonike 2:10-12

Utajiuliza ni wapi tena jambo  hilo tena utalipata katika biblia,  Embu vitafakari  hivi vifungu, hususa ni hivyo vilivyo katika herufi kubwa.

Waebrania 6.4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7 MAANA NCHI INAYOINYWA MVUA INAYOINYESHEA MARA KWA MARA, NA KUZAA MBOGA ZENYE MANUFAA KWA HAO AMBAO KWA AJILI YAO YALIMWA, HUSHIRIKI BARAKA ZITOKAZO KWA MUNGU;

8 BALI IKITOA MIIBA NA MAGUGU HUKATALIWA NA KUWA KARIBU NA LAANA; AMBAYO MWISHO WAKE NI KUTEKETEZWA”.

Embu jiulize upo katika kanisa muda mrefu, unasema umeokoka, unasali, unafanya ushirika, unaimba kwaya n.k. lakini bado una maisha ya dhambi ya siri  unayoyajua wewe.. Unatazamia nini pale Roho Mtakatifu atakaposhuka juu yako au juu ya kanisa, upaliliwe kitu gani?

Roho Mtakatifu anaposhuka ndani ya kanisa lake kulinyeshea mvua, halafu anakukuta, wewe ni gugu umepandwa ndani yake, ujue kuwa mvua hiyo itaistawisha gugu, lizidi kustawi zaidi ili siku ya kuteketezwa na kutupwa motoni likapate adhabu iliyokubwa zaidi. Ili kutimiza andiko hili;

Mathayo 13:24 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.

27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?

28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?

29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.

30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu”.

Kumbuka kilichomfanya mfalme Sauli ashukiwe na Roho mbaya kutoka kwa Mungu, ni tabia yake ya wivu na ile ya kudharau maagizo ya Mungu, hivyo ile Roho njema ya Mungu iliposhuka juu yake na kukutana na tabia yake mbaya, ndio ikamfanya awe mbaya, kutaka kumwangamiza Daudi. Lakini kama angekuwa ni mtiifu kwa Mungu na mwenye upendo, Roho ya Mungu ingekutana na tabia hiyo njema na kumfanya kuwa mfalme Hodari zaidi na mshupavu kama alivyokuwa hapo mwanzoni. Hiyo ndio sababu kwanini biblia ilikuwa inasema “Roho mbaya kutoka kwa Mungu” ilikuwa inamjia Sauli..Hizi ndio sababu.(1Samweli 16:14-23)

Hata sasa, tunapaswa tujiangalie sana mienendo yetu katika kanisa, wapo watu baada ya kukaa kanisani   ndio wamezidi kuwa wabaya zaidi, wanafanya mambo ambayo hata watu wa kidunia hawafanyi, kama ulikuwa hujui sababu ndio hii. Sasa usidhani mtu kama huyo alianza tu kuwa mbaya, hapana, bali alidharau maagizo ya Mungu, akawa anafanya mambo yasiyofaa kidogo kidogo hivyo hivyo, na mwisho wa siku akajikuta anayafanya kwa nguvu zaidi,..Hajui kuwa tayari kashapotea milele, Na biblia inasema mtu akishafikia hatua hiyo, hawezi kufanywa upya tena atubu, anasubiria kwenda tu katika ziwa la moto. Kwahiyo tujitathimini ni mbegu za aina gani zipo ndani yetu. Ili tuwe na amani pale Roho anaposhuka juu yetu, kutuwezesha zaidi.

Tukipanda mbegu njema katika utakatifu, Roho Mtakatifu atatufanya kuwa watakatifu zaidi, tukipanda katika imani,atatuongezea imani zaidi, tukipanda katika upendo vivyo hivyo, katika kulitafakari Neno lake, atatuongezea mafunuo mengi zaidi n.k. Huo ndio uzuri wa Roho Mtakatifu, ndio maana anaitwa msaidizi.

Yohana 16:13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Hivyo katika hili eneo tunapaswa tuwe makini sana, hata Bwana Yesu alituonya hivyo. Ni heri ukafanya mizaha katika mambo ya kidunia, lakini sio ndani ya kanisa la Kristo. Kwasababu huko ndani Roho Mtakatifu yupo kuwezesha watu, kwahiyo angalie zisije zikawa ndio dhambi zako zinawezeshwa huko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

AOGOPACHO MTU ASIYE HAKI NDICHO KITAKACHOMJILIA.

MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.

Rudi nyumbani

Print this post

MKESHA WA KUINGIA MWAKA MPYA KILA MWAKA NI WA KUUTHAMINI SANA.

Leo  tutaona kibiblia ni kwanini uuthamini mkesha wako wa kuingia mwaka mpya. Wengi wetu tunapuuzia, tunaona ni jambo la kawaida tu, na hivyo tunautumia msimu huu pengine kulala, au kwenda kufanya anasa, au kwenda kufanya part na ndugu au marafiki n.k.. Ni heri upange kwenda kusheherekea nao siku inayofuata kuliko siku ya mkesha wa kuukaribisha mwaka mpya.

Lipo jambo kubwa sana la kiroho katika usiku wa siku hiyo.

Ukisoma biblia utaona Mungu alipokuwa anawatoa wana wa Israeli Misri, siku hiyo  kwao ndio ilikuwa siku ya kwanza ya mwaka wao mpya.. Lakini utaona Mungu hakuwatoa mchana, au jioni, au alasiri bali aliwatoa usiku wa manane,  Sio kwamba mchana wasingeweza kusafiri, hapana, lakini siku ya kutengwa na maadui zako, na siku ya kuukaribisha mwaka mpya sikuzote ni lazima maandalizi yaanzie angali bado kuna giza nene.

Utasoma usiku ule kabla ya kuamkia tarehe moja, walimla yule pasaka(mwanakondoo), wakiwa wamevaa viatu vyao chini, kiashirio kuwa wapo mbali na vitanda vyao, na huku wamefunga mikanda yao viunoni, kuashirio kuwa wapo tayari kwa safari, kisha wamejifungia ndani wakimtafakari Mungu na kumwimbia, wakisubiria tu muda ufike wa kuondoka..

Kutoka 12: 11 “Tena mtamla hivi; mtakuwa mmefungwa viuno vyenu, mmevaa viatu vyenu miguuni, na fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka; ni pasaka ya Bwana.

12 MAANA NITAPITA KATI YA NCHI YA MISRI USIKU HUO, NAMI nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi Bwana”.

Kwasababu walifahamu wanaingia katika mwaka wao mpya wa kufanywa huru mbali na maadui zao. Sasa embu fikiria kama wangekuwa wamelala, halafu asubuhi ndio wanaamka watake kuondoka Misri, hali  ingekuwaje? Ni wazi wasingetoka kwa ushindi mnono kama walivyotarajia.

Vivyo hivyo na sisi, siku kama ya leo, ndio tunavuka kuingia mwaka mpya. Usiku ambao tunayaacha mambo ya mwaka huu, na kuyakaribisha mambo ya mwaka mwingine mpya, Hivyo kama tunataka  Mungu ampige adui yetu shetani kwelikweli, ili mwaka wetu mpya tunapouanza uwe wa kuwa huru, na wa Baraka nyingi na wa mafanikio, hatuna budi leo kukesha nyumbani mwake, katika kuomba, kumwabudu na kumfanyia ibada.

Yaani tarehe moja ya mwaka mpya isikukute upo kitandani, isikukute unaangalia MUVI, isikukute unacheza gemu, isikukute unazurura zurura mtaani, isikukute unapiga piga stori na marafiki zako n.k., bali ikukute nyumbani mwa Bwana unamshukuru na kumtukuza.

Hata kama upo katika nchi ambazo, ibada zimekatazwa makanisani, bado unayo nafasi ya kujifungia mwenyewe nyumbani na familia yako ukawa unaomba na kumshukuru Mungu, kama wana wa Israeli walivyofanya. Hakikisha kuwa mwaka wako mpya unaukaribisha ukiwa macho kwa Bwana.

Itakuwa ni ajabu sana, kama mwaka huu utashindwa kumshukuru Mungu kwa wema wake aliokutendea mwaka mzima..Wewe mwenyewe unajua mambo tuliyoyapitia mwaka huu jinsi yalivyokuwa mazito , lakini umepewa neema ya kuyavuka, ujue sio kwa nguvu zako,wala fedha zako, wala afya yako wala chochote ulicho nacho.

Hivyo utumie mkesha huu, vema kwasababu hakutakuwepo tena na mwingine kama huu, kwa miezi mingine 12 ijayo. Bwana akubariki

Pia wakumbushe na wengine, jambo hilo. Na shea kwa wengine.

Mwisho kabisa, nikutakie HERI YA MWAKA MPYA WENYE MAFANIKIO YOTE YA MWILINI NA ROHONI KATIKA JINA LA BWANA YESU KRISTO.

AMEN.

Mawasiliano/ Whatsapp: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NAKUTAKIA HERI YA MWAKA MPYA!

UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?

NJIA MUNGU ALIYOIWEKA KWA KILA JAMBO.

THAWABU ZA SIRI, ZA WATAKATIFU MBINGUNI.

Rudi nyumbani

Print this post

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Shalom, karibu tena tuyatafakari maneno ya Bwana wetu Yesu, biblia inasema manabii wengi na wenye hekima walitamani sana kusikia tunayoyasikia na kuyaona tunayoyaona lakini hawakupata neema hiyo, Lakini mimi na wewe tumepewa neema ya kuyasikia maneno ya Bwana wetu Yesu. Ni furaha iliyoje?

Yesu ambaye aliiumba dunia kwa Neno lake, leo hii inakaa na sisi kutufundisha hilo hilo Neno lake, unadhani ni rahisi sisi kuacha kuyatafakari maneno yake kwa kuyarudia rudia kila siku? Tutafanya hivyo kwa msaada wake.

Leo tuutafakari tena kwa pamoja mfano huu alioutoa. Unaweza ukawa umeusoma mara 100, lakini tuutafakari tena, Neno la Bwana huwa haliishi ubora.

Luka 15:3 “Akawaambia mfano huu, akisema,

4 Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone?

5 Naye akiisha kumwona, humweka mabegani pake akifurahi.

6 Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea.

7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu.

8 Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione?

9 Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea.

10 Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye”.

Katika maneno hayo, tunaweza kujifunza jambo moja, kwa hawa watu wawili, kwanza, furaha yao haijaja katika kukipata kitu kipya, bali ni katika kitu kile kile cha zamani walichokuwa nacho.  Lingekuwa ni jambo la heri kama wangekuwa wamezalisha kitu jipya na kwa hicho kikawapatia faida, hapo ndio tungesema furaha yao inamaana, lakini tunaona ni vilevile walivyokuwa navyo hapo mwanzo ndivyo wanavyovifurahia.

Furaha hii sio ya kawaida, bali ni furaha inayojificha ndani ya uthamani wa kitu. Inazuka pale kitu hicho kinapoathiriwa na kupata suluhisho.

Furaha ya namna hii inaweza kujengeka hata kwako, kwamfano unaweza ukawa na simu yako nzuri, lakini ghafla kibaka akapita mbele yako akakupokonya akakimbia nayo..Ni wazi kuwa hilo jambo litakuudhi sana kama sio kukuhuzunisha. Lakini baada ya wiki moja pengine wakati unafikiria labda kwenda kununua simu  nyingine, unashangaa unapigiwa simu na polisi, unaambiwa simu yako tumemshika nayo mtu mmoja mwizi alikuwa anakwenda kuiuza.. Hivyo njoo chukua simu yako.

Ni wazi kuwa taarifa hizo zitauchangamsha moyo wako, na kukufurahisha sana kana kwamba ni jambo fulani la maana sana umelipata, kumbe ni kitu kile kile. Furaha hii inakuja yenyewe tu ndani, haulazimishwi, unasema daah! Afadhali nimeipata simu yangu, asante Mungu. Tena ukikutana na Yule mtu aliyekusaidia utataka hata umpe chochote cha kumpongeza au kumfuta jasho kwa kukuhangaikia.

Sasa huzuni na  furaha ya namna hiyo, ndiyo Mbingu yote na malaika wa Mungu wanayoipitia kila siku, pale mwenye haki mmoja anapoicha imani, mbinguni wanahuzunika, na kukasirika, lakini pale mwenye dhambi aliyeiacha imani anapotubu , Malaika wanamshukuru Mungu,wanasema afadhali fulani kapatikana, siku yao huwa inakwenda vizuri sana, wanamshukuru Mungu sana kwa hilo. Hivyo na sisi tusichoke kuwahubiria wenye dhambi wamgeukie Mungu hata kama hapo mwanzo walikuwa wameokoka wakapotea, Unaweza kudhani wakitubu na kumgeukia Mungu,ndio basi, mbinguni wanalichukulia hilo jambo kawaida tu, fahamu kuwa huko mbinguni ni shangwe tu.

Biblia inatuonyesha hilo jambo huwa linawafurahisha na kuwachangamsha sana malaika. Wapo kondoo wa Mungu wengi sana leo hii wamepotea, wengine wamerudi nyuma, ule moto waliokuwa nao umezima,

Idadi ya wakristo walioacha imani ni kubwa kuliko idadi ya watu ambao hawakuijua imani kabisa kwasasa hivi..tafakari tu mpaka Yesu mwenyewe  anasema mwenye dhambi MMOJA TU, atubupo, hajataka wengi, bali mmoja tu, inaipa furaha mbingu. Itakuwaje wakitubu mia, au mia mbili au elfu, Hivyo kwa pamoja tusimame katika karama zetu, kuwarejesha wale waliopotea katika imani tena, na Bwana atusaidie.

Vilevile ikiwa na wewe unayeusoma ujumbe huu, hapo mwanzo ulikuwa kwa Mungu lakini sasa umeurudia ulimwengu, hapo Mwanzo ulikuwa moto lakini sasa umekuwa baridi tena, fahamu kuwa umemuhuzunisha Mungu sana kwa maamuzi yako hayo mabaya. Mungu anasikitika gharama alizoingia kukukomboa na leo hii unamwacha na kwenda kuunufaisha ulimwengu. Hilo jambo linamsikitisha kweli kweli ndugu, yangu pamoja na malaika wake.

Mungu anataka leo hii umrudie tena, ujumbe huu unakuhusu wewe, mwana mpotevu, leo mrudie muumba wako, hizi ni siku za mwisho, dunia hii haina muda mrefu mpaka iishe, na hata kama bado itakuwepo, wewe hauna garantii ya kuiona kesho.Au unayo? Vifo vinakujaga ghafla tu bila hodi, ziwa la moto halishibi watu, na kila sekunde maelfu ya watu wanashuka huko. Wanajuta kwa majuto ambayo hayaelezeki, mfano wake ni Yule tajiri wa Lazaro, habari yake unaifahamu.

Huko walipo sasahivi wanatamani wewe utii injili uokoke, ili usifike hizo sehemu za mateso walizopo. Dakika moja tu ya uhai uliyopewa, usiichee rafiki yangu, itathamini, shetani anaiwinda roho yako, kwa namna isiyo ya kawaida. Hivyo tubu mgeukie Kristo upokee ondoleo la dhambi. Na yeye mwenyewe atakutia muhuri kwa Roho wake mtakatifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI UNAPASWA UWE BIBI ARUSI NYAKATI HIZI ZA MAJERUHI?

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI UNAPASWA UWE BIBI ARUSI NYAKATI HIZI ZA MAJERUHI?

Shalom, biblia inasema..

Yohana 3:29 “Aliye naye bibi arusi ndiye bwana arusi;..”

Huu ni wakati wa kupigania kwa bidii kuwa bibi arusi wa Kristo kwelikweli, kwasababu kama ukifa leo hii na sio bibi-arusi au unyakuo umekukuta na bado hujafanyika kuwa bibi arusi ujue kuwa unyakuo hautakuhusu hata kidogo, haijalishi utasema mimi ni mkristo wa miaka mingi, hutakwenda popote. kumbuka si wakristo wote ni bibi-arusi, jambo ambalo wengi wetu hatulijui, Wakati huu wa mwisho maandiko yanatuonyesha wazi kuwa kutakuwa na makundi makuu mawili ya watu wanaojiita wakristo.

Na hao wamezungumziwa kwa marefu sana katika kile kitabu cha Mathayo 25, kama wanawali werevu na wapumbavu.  Hao kwa jina lingine ndio wanaojulikana kama bibi arusi na masuria. Suria ni mwanamke aliyetwaliwa tu na kuwekwa ndani, hana mkataba wala urithi wowote kwa mume wake, isipokuwa kupewa tu zawadi na kuondoka,  lakini bibi arusi yeye ni mke, ambaye si tu kupokea zawadi, na urithi, kutoka kwa mume wake, bali pia anakuwa na kitu kingine cha zaida, ambacho leo tutajifunza kwasababu ndio kiini cha somo letu la leo.

Na kitu chenyewe ni “Kufahamu ya sirini ya Bwana wake”. Kama vile tunavyojua mtu pekee anayeweza kumfahamu mtu ndani nje, ni mke wa mtu, au mume wa mtu. Kwasababu watu hawa walishaunganishwa na kuwa mwili mmoja, hivyo usishangae kuona mke au mume anajua mambo mengi ya mwenzi wake kuliko hata ndugu zake alioishi nao kwa miaka mingi tangu utotoni.

Ndivyo ilivyo katika wakati huu wa mwisho. Bwana Yesu analiandaa kundi lake dogo sana, ambalo linajulikana kama bibi-arusi, kumbuka hili sio suria, yaani sio watu tu wanaojiita ni wakristo lakini wanaishi maisha yao ya kidunia wanayoyajua wao, hapana bali ni kundi lingine kabisa. Ambalo tutaona tabia zake kidogo mbeleni.

Sasa Watu hawa ndio Kristo atakaowafunulia  baadhi ya siri ambazo si watu wote watazifahamu. Kwasababu  Biblia inatabiri wakati dunia inakwenda kukaribia kuisha, zipo siri ambazo Mungu alizihifadhi wala hakutaka ziandikwe kwa wazi kwenye biblia, siri hizo atakuja kuwafunulia watu wake.

Ufunuo 10:4 “Hata ngurumo saba zilipotoa sauti zao, nalikuwa tayari kuandika. Nami nalisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, YATIE MUHURI MANENO HAYO YALIYONENWA NA HIZO NGURUMO SABA, USIYAANDIKE”.

Kama tunavyosoma hapo, yapo maneno ambayo yalitiwa muhuri, lakini hayakuandikwa.. Yalisikiwa tangu zamani lakini hayakuandikwa. Unaweza ukajiuliza ni kwanini yasiandikwe kama tayari yalishasikiwa? Ni kwasababu sio kila jambo ni la kila mtu. Mengine ni ya siri, ya Kristo na bibi arusi wake tu.

Na siku hizo ambazo siri hizi zitakapomalizika kuachiliwa mioyoni mwa kundi hili dogo la watakatifu, ujue kuwa tayari mstari wa neema umeshavukwa, na makundi mawili yameshajinga.

Hivyo Wakati huu tunaoishi,ni wa kumaanisha sana ndugu yangu, kwasababu ukijidanganya mwenyewe umeokoka, na huku nyuma unafanya matendo yako maovu sirini, kwa kisingizio wewe ni mchungaji, au mwalimu, au mwana kwaya, au nabii n.k…ukweli ni kwamba unajidanganya tu mwenyewe, wala usipoteze  muda wako mwingi kujisiri sitiri. Kwasababu Kristo anawajua walio wake, anamjua bibi arusi wake wa kweli yupoje, tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Hana mzaha mzaha katika kuchagua.

Na tabia inayomtambulisha Bibi arusi wa kweli ni mataendo yake ya haki (yaani utakatifu). basi

Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; KWA MAANA KITANI NZURI HIYO NI MATENDO YA HAKI YA WATAKATIFU”.

Je! Na wewe utakatifu upo ndani yako?. Kama jibu ni hapana, basi anza kutengeneza taa yako sawasawa iwe na mafuta ya kutosha,. Kwasababu Bwana arusi wetu Kristo yupo mlangoni kuja kulinyakua kanisa lake. Na hakuna anayejua itakuwa ni lini, lakini kila dalili inatuonyesha ni hivi karibuni pengine ni leo usiku. Hivyo usiishi maisha ya kubahatisha. Maanisha kweli kumfauta Yesu.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Rudi nyumbani

Print this post

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

SWALI: Naomba kufahamu hichi “Chuo cha vita vya Bwana” kinachozungumziwa katika Hesabu 21:14  ni kipi?.


Hiki ni moja ya vitabu ambavyo vinatajwa katika biblia lakini leo hii havipo, vinginevyo ikiwemo kitabu cha Yashari,(2Samweli 1:18), Kitabu cha tarehe cha wafalme wa Yuda(1Wafalme 14:29), Kulikuwa pia na  kitabu cha tarehe ya Nathani nabii, halikadhalika kitabu cha tarehe ya Gadi mwonaji, Na kitabu cha tarehe cha Samweli mwonaji, (1Nyakati 29:29); Vitabu hivi vyote havipo kwenye biblia hadi hii leo, japokuwa vimezungumziwa.

Kama vile jina lake linavyojieleza kinadhaniwa kuwa ni kitabu kilichokuwa kinarekodi matukio yote ya vita ambavyo Bwana aliwapigania watu wake, na kuwaokoa kwa mkono mkuu.

Japo, habari zote za kitabu hicho hazijawa wazi hadi leo, ni mambo gani na gani yalizungatiwa kuandikwa ndani yake. Lakini enzi za agano la kale, kitabu hichi kilikuwa ni kitabu maarufu kati ya vitabu vya kihistoria vya kiyahudi.

Habari ya kitabu hichi utaipata sehemu moja tu katika biblia,

Hesabu 21:13 “Kutoka huko wakasafiri, wakapanga upande wa pili wa Arnoni, ulio jangwani, utokao katika mpaka wa Waamori; maana, Arnoni ndio mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.

14 Kwa hiyo imesemwa katika chuo cha Vita vya Bwana, Wahebu katika Sufa, Na bonde za Arnoni,”

Lakini ni kwanini Mungu hakukiruhusu kiwepo hadi leo?

Kama Biblia ingerekodi matendo yote makuu Mungu aliyowafanyia watu wake tangu kuumbwa kwa ulimwengu hadi sasa, vitabu vyote duniani visingetosha kwa habari zake. Kama tu habari za matukio ya Yesu aliyoyafanya hapa duniani biblia inasema vitabu havitoshi kuelezea itakuwaje yaanzie tangu agano la kale.

Hivyo habari hizo chache zilizoandikwa kwenye biblia, Mungu ameona walau zitamtosha kila mtu azisome na kumsaidia,. Sasa ikiwa tumerahisishiwa habari njema hizi njema, kwa bahari chache sana, halafu tutakataa kusoma, basi hapo tunaonyesha ni jinsi gani tulivyo wavivu.

Ni lazima ujiulize ni kwanini hadi wakati huu uliofikia hujawahi kuisoma biblia yote? Lakini wakati huo huo magazeti uliyoyasoma, pamoja na vitabu shuleni, na mtaani umemaliza hata kurasa milioni 5, lakini biblia hujamaliza. Jiulize tatizo ni nini? Au urahisishiwe nini tena ndio usome.?

Kusoma biblia ni kutia bidii kidogo tu, Paulo alimwambia Timotheo maneno haya;

1Timotheo 4:13 “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma…”

Hivyo jijengee utaratibu wa kusoma biblia kila siku.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

NGURUMO SABA

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

Wakati ule Mbingu inafungwa Israeli mvua isinyeshe miaka mitatu na nusu, tunaona Mungu alimwagiza Eliya aende akakae karibu na kijito cha Maji cha Kerithi, anywe maji ya mto ule, na pamoja na hayo, kunguru watatumwa kumletea chakula na nyama asubuhi na jioni.

Lakini tunasoma, upo wakati kijito kile kilikauka.. pengine yeye alidhani ataendelea kufaidika hivyo hivyo kwa muda wote mpaka Mungu atakapoileta tena mvua juu ya nchi, lakini haikuwa hivyo, Ni kweli yalikuwa ni maagizo ya Mungu yeye abaki pale, lakini Mungu hakukusudia abaki pale milele. Ingekuwa labda ni mimi wakati huo naona kijito ambacho Mungu alichoniagiza nikinywee kimekauka mawazo ya kuwa nimeashaachwa na Mungu yangeshaniingia.

Lakini baada ya tukio lile tunaona Mungu akampa maagizo mengine, ya kuelekea Sarepta akalishwe na mwanamke mjane, na sio tena kunguru.

1Wafalme 17: 2 “Neno la Bwana likamjia, kusema,

3 Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani.

4 Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; nami nimewaamuru kunguru wakulishe huko.

5 Basi akaenda akafanya kama alivyosema Bwana; kwa kuwa akaenda akakaa karibu na kijito cha Kerithi, kinachokabili Yordani.

6 Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito.

7 Ikawa, baada ya siku kupita, kile kijito kikakatika, kwa sababu mvua haikunyesha katika nchi.

8 Neno la Bwana likamjia, kusema,

9 Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama, nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe.

10 Basi, akaondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa.

Nachotaka tujifunze leo ni kuwa, ni tabia ya Mungu kutuvusha madarasa, si desturi yake sisi tuendelee katika darasa lile lile la ukristo kwa miaka yetu yote tuliyopo hapa duniani, ni lazima akikatishe kile kimoja, ili afungue mlango wa kutuletea kingine, na anafanya hivyo sio kutukomoa, bali ni kutukuza kiimani, tufikie utimilifu wa yeye anaoutaka kwetu.

Ikiwa wewe ni mkristo wa muda mrefu, utaelewa ninachokisema,ile  neema uliyokuwa unaipata kutoka kwa Mungu wakati unaokoka, sio neema ambayo unatembea nayo sasa hivi. Pengine siku za mwanzoni mwanzoni ulizookoka, ulihisi kama vile Mungu kakukumbatia kwa kila kitu, ni sawa na unalishwa na kunguru kama vile Eliya, lakini majira unafika unaona, kama neema hiyo imetoweka au imepungua kwako. Kile kijito kimekauka.

Sasa kama wewe ni mkristo ambaye umesimama, ukifikia katika hatua kama hiyo, usianze kufikiri kuwa Mungu amekuacha, kwasababu tu huoni yale mema uliyokuwa unayapata siku za mwanzoni. Badala yake fahamu kuwa, ni hatua nyingine Mungu anataka kukupigisha, ambayo hiyo itakufanya uwe imara zaidi kiimani kuliko ile uliyokuwa nayo hapo kabla.

Ukifikia hatua kama hiyo usikumbatie sana yale ya mwanzoni, kwasababu hata ukijaribu kuyaishi hutaweza tena, uvuli wake umeshapita, unachopaswa kufanya ni  kukaa katika utulivu mpya wa Mungu, omba, kisha pale Mungu anapokufungulia neema ya kuanzana napo, bila kukawia nenda napo..Wala usiogope, kwasababu Mungu atakuwa pamoja na wewe. Huku ukizingatia kuutunza tu utakatifu na Imani, viwango vyake vilevile vya kumcha Mungu.

Kwasababu ni Mungu Yule Yule aliyekuwa na wewe kukupigania, ndiye atakayekuwa na wewe, kukushindania katika darasa lingine jipya ambalo anakupeleka. Jambo unalopaswa kufanya ni wewe tu, kuongeza umakini wako kwa Mungu, na kutoruhusu kurudi nyuma kwa namna yoyote ile.

Kwamfano hapo nyuma ulikuwa katika mazingira tulivu sana ya kumtafakari Mungu, lakini unaona kama yamebadilika, mazingira mengine yamekuja, ambayo yanakulazimu kuwafundisha wengine zaidi, au kuwahubiria, ujue kuwa ni Mungu ndiye anayekuvusha darasa hilo, hawezi miaka yote, akufanye mtoto tu wa kulishwa, utafika wakati na wewe atakulazimisha uwalishe na wengine.

Pengine Mungu atakuhamisha hapo unapoishi na kukupelekea mahali pengine, Na kule unapata changamoto kidogo ya kukipata chakula cha kiroho, kama ilivyokuwa hapo mwanzoni, sasa  Unapoona hivyo, usifikiri kuwa Mungu amekuacha, bali ni wewe, kuishindania zaidi Imani, kutengeneza tena ratiba zako, Na Mungu atakufikisha mahali ambapo anataka ufike.

Hivyo ni jukumu letu kukumbuka kuwa tunapokuwa wakristo ni lazima Mungu atatupitisha  katika madarasa tofauti tofauti, atatuvikisha katika vipindi mbalimbali na katika madarasa hayo, tunapaswa tuwe wepesi wa kuyajua mapenzi yake ni nini, ili tuweze kuelewa ujumbe wa darasa hilo. Na faida yake ni kuwa yeye mwenyewe aliahidi kuwa hatatuacha, bali atakuwa pamoja nasi.

Eliya hakuachwa na Mungu alipoondolewa pale mtoni, na kupelekwa kwenye nyumba ya mjane, Baraka zile zile alizipata isipokuwa zilikuja tu katika maumbile tofauti. Huo ndio uzuri wa Mungu wetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wale mamajusi walikuwa ni wakina nani?

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

RAHABU.

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Rudi nyumbani

Print this post