Category Archive Home

WAMNGOJEAO BWANA WATAPATA NGUVU MPYA.

Wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya.


Ipo ahadi kubwa sana ambayo Mungu kaitoa kwa wale walioamua kuiacha dunia na kumfuata yeye kwa gharama zote. Na ahadi yenyewe ni “kupokea nguvu mpya kipindi baada ya kipindi”. Mungu anafahamu kabisa safari ya wokovu ni ngumu kama ilivyosafari nyingine yeyote ya haya maisha…kuna milima na mabonde, kuna kuchukiwa na kudharauliwa, kuna kuonekana umerukwa na akili na kutokuthaminiwa, kuna kutengwa na kuudhiwa, kuna kupungukiwa na kuvunjwa moyo, kuna msiba na dhiki n.k. vyote hivyo mtu yeyote aliyeamua kumfuata Kristo, kwa namna moja au nyingine atakumbana navyo…

Lakini utajiuliza pamoja na hali kama hizo ni kwanini bado watu waliookoka wengi ki-kweli kweli wanaweza kustahimili?..Ni rahisi mtu kwa kidunia kuvunjika moyo au kukatishwa tamaa na mambo kama hayo lakini kwa mkristo aliyedhamiria kumfuata Yesu, ndio kwanza anazidi kuwa karibu na Mungu wake..Hiyo yote ni kwasababu ipo nguvu inayoachiliwa ndani yake kipindi baada ya kipindi..

Biblia inasema..

Isaya 40:28 “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.

29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;

31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Kama sio neema hiyo, hakuna hata mmoja wetu angeweza kumwamini na kumtuamini Mungu asiyemwona sikuzote za maisha yake..Lakini kwasababu ipo nguvu anayoiachia ndani ya wale wanaomngojea wanajikuta tu wanazidi kumtafuta Mungu, safari yao ya wokovu wanaiona kama vile imeanza jana..

Hiyo ndio tofauti na mtu aliyeokoka na yule ambaye hajaokoka..Yule ambaye hajaokoka, anaweza akawa anajisumbua katika jambo Fulani, au katika shughuli yake,.. au katika elimu yake, lakini upo wakati atachoka, ataboreka, atazimia na kusema ngoja nipumzike kwanza, nitakuja kuendelea baadaye, lakini kwa mtu aliyejitwika msalaba wake na kumfuata Kristo, pale ambapo ataonekana anakaribia kuzimia hapo ndipo Mungu anapompa nguvu mpya, anapompa uwezo mpya.

Hufanya njia pale pasipo na Njia:

Pale ambapo watu watasema sasa huyu ndio basi, kwa hali hii, anayoipitia hamalizi huu mwaka atakuwa amesharudi tu huku kwenye dunia, lakini wanashangaa mwaka unapita, miaka inapita,.. ndio kwanza anazidi kumpenda na kumtafuta Mungu wake Zaidi ya hapo mwanzo..Kwasababu gani, Ni kwasababu Mungu anahakikisha anawapa nguvu mpya wale wao waliodhamiria kujitwika msalaba wao na kumfuata..kama maandiko yanavyosema:

watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Ukristo ni safari ya kuwezeshwa, ukiona mtu anasema nimeishiwa pumzi njiani siwezi kuendelea mbele nimezidiwa na tamaa za ulimwengu, fahamu kuwa mtu huyo tangu mwanzo alikuwa bado hajadhamiria kumfuata Kristo kwa moyo wake wote.. Kwasababu ni kitu ambacho hakiwezekani kuishiwa pumzi katikati angali kila wakati unawezeshwa, unapokea nguvu mpya, sasa huko kuishiwa pumzi kunatoka wapi?.

Leo hii unaweza ukajiuliza hivi kweli nikiokoka, nitaweza kuishi bila uzinzi kwa muda mrefu?, nitaweza kuacha kunywa pombe kwa kipindi kirefu,.. nitaweza kuvumilia kutovuta sigara kwa miaka 2 kweli, nikiamua kumfuata Kristo nitaweza kujizuia kutokuweka make-up maisha yangu yote, na kutokuvaa suruali,.. nitaweza kutokwenda Disko, nitaweza kutokufanya Musturbation…Nataka nikuambie kwa akili zako na nguvu zako chache hutaweza, lakini ukiamua kwa kudhamiria kweli kumfuata Kristo kwa moyo wako wote, ukasema leo hii naanza upya kupiga mwendo na Kristo, hilo jambo ni rahisi sana kulishinda kuliko unavyodhani..

Utapokea nguvu mpya:

Kabla hata hujakaribia kuishiwa pumzi Bwana atakuwa pembeni yako kukutia nguvu mpya..Kila siku itakuwa fresh kwako, wiki itapita, mwezi utapita, mwaka utapita, miaka itapita na bado ile hamu ya kufanya hayo mambo haipo ndani yako, ..Hiyo ni neema kubwa Mungu aliyowahaidia wale wote watakaomngojea…Hapo ndipo tunapouna wepesi wa wokovu, vinginevyo hakuna ambaye angeweza kuushinda huu ulimwengu, si mchungaji, si mwinjilisti..hakuna atakayeweza kuushinda ulimwengu.

Hata kama utapitia hali ambayo unaona kesho au kesho kutwa haifiki, lakini maadamu upo kwa Bwana, na unamtazama yeye, utaona tu jinsi atakavyokufanyia njia mahali ambapo hapana njia na wewe mwenyewe utajikuta unamwimbia, EBENEZA MWAMBA WANGU!..

Hata katika magonjwa, au dhiki, katikati yake atakufungulia mifereji ya faraja na uponyaji, nawe utasema ni heri Mungu nilichagua kukufuata maana ninauona mkono wako ukinizunguka!..Hali hiyo hiyo utaendelea nayo mpaka utakapomaliza mwendo wako hapa duniani kama unyakuo hautakukuta..hata Katika raha atakuwa na wewe pia kukuongezea raha Zaidi..

Je na kwa mwenye dhambi ni hivyo hivyo?

Lakini ikiwa upo mbali naye, na unasema kuishi maisha ya wokovu haiwezekani hapa duniani..Nataka nikuambie utajikuta unaendelea kusema hivyo mpaka unakufa na dhambi zako,..

Bwana Yesu aliwaambia mafarisayo katika Yohana 8:24 ‘Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu’.

Kuna madhara makubwa sana kufa katika dhambi…Ukifika kule mbele ya kiti cha hukumu wataletwa watu wa kizazi chako walioweza kukishinda hicho kinachokushinda wewe leo hii,..Nao wataulizwa ilikuaje kuaje nyie mliweza kuushinda uzinzi katika dunia iliyojaa vishawishi namna ile? na wakati hawa wengine wameshindwa?..Nao watajibu kwa ku-unukuu mstari huo;

Isaya 40:29-31

 ‘29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;

31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Hapo utakosa cha kujibu, ukijua kuwa kumbe na wewe ulikuwa na fursa kama hiyo lakini uliikataa.

Hivyo usisibiri upendeleo wa kipekee kama huo ukupite, acha kufikiria fikiria kwa juhudi zako utawezaje. Leo hii dhamiria kutubu dhambi zako zote, hapo ulipo tenga muda mchache ukiwa peke yako piga magoti, anza kumweleza Mungu mambo yako maovu yote uliyomtendea,… kisha mwambie Naomba msamaha,..Fanya hivyo kwa kumaanisha kabisa kutoka moyoni mwako kwasababu yupo hapo kukusikia, na yupo hapo kukusamehe dhambi zako zote..

Na Ile damu yake Yesu Kristo itakusafisha kabisa, na uthibitisho wake ni kuwa, baada ya Toba Amani ya ajabu na utulivu wa kipekee utaingia ndani yako, ukishaona hivyo, dhamiria sasa kuacha kufanya yale yote uliyokuwa unafanya nyuma yasiyompendeza Mungu, kwasababu Mungu kashakukaribia….kama ulikuwa ni mlevi kaa mbali na walevi na pombe, ulikuwa ni mzinzi kaa mbali na wazinzi na acha uzinzi, Na Mungu akishaona mwitikio wako, na kwamba umegeuka kivitendo sawasawa na toba yako, Sasa ile nguvu yake ya kukufanya uzidi kupiga mbio upae juu Zaidi kwa mbawa za tai, itaanza kuachiliwa ndani yako..Na kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndivyo utakavyojiona tamaa ya vile vitu ulivyokuwa unavifanya vinakufa ndani yako, na mwisho wa siku vitapotea kabisa..

Hatua inayofuata baada ya toba:

Hivyo ukishatubu bila kupoteza muda hakikisha unatafuta kanisa, ukabatizwe, katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38 ili kuukamilisha wokovu wako.

Kumbuka ubatizo sahihi ni muhimu sana..Vilevile anza kujumuika na wakristo wenzako, wale unaoona wamesimama kweli kweli na anza kusoma Neno kwa bidii na kusali..Yaliyosalia Roho Mtakatifu atakuongoza kuyatenda..jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Shalom.

Mada Nyinginezo:

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

MNGOJEE BWANA

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?

Je! Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?


JIBU: Tukisoma kitabu cha Ufunuo ni kweli tunamwona mnyama aliyetajwa mwenye vichwa saba na pembe kumi..Tofauti na idhaniwavyo na wengi kwamba zile pembe kumi zimejigawanya kwenye vichwa vyote 7..na kwamba kuna vichwa vingine labda vitakuwa vimepata pembe mbili mbili au zaidi…Lakini ukweli ni kwamba ni kichwa kimoja tu ndicho kilichokuwa na pembe zote 10..Hivyo vingine havikuwa na pembe yoyote.

Na kama ukitafakari kwa makini kwa msaada wa Roho utagundua kuwa vile vichwa saba ni Wanyama saba katika mwili mmoja na sio tu vichwa kama vichwa vilivyojiotea kwenye mwili mmoja…bali ni Wanyama saba tofauti wanaoshiriki mwili mmoja (yaani wana-share mwili mmoja)..

Ufunuo 17: 11 “Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu”.

Sasa hiyo imekaaje kaaje?..Inawezekana Wanyama Zaidi ya mmoja kushiriki mwili mmoja?..

Hiyo inawezekana asilimia 100..wapo ng’ombe mapacha wanaozaliwa wakiwa na mwili mmoja lakini vichwa viwili tofauti, kadhalika wapo nyoka wanaozaliwa hata watatu au wanne wakiwa na wanashea mwili mmoja…Na Zaidi ya yote wapo pia wanadamu ambao wanaozaliwa wakiwa wameungana…Kuna mapacha wanaoishi leo duniani ambao wameungana kila kitu isipokuwa kichwa tu…yaani ukikutana nao unaweza kusema umekutana na mtu mmoja mwenye vichwa viwili lakini kumbe ni watu wawili waliozaliwa wameungana wanaoshea mwili mmoja..Na watu hao walioungana kila mmoja anatafakari kivyake na ana malengo yake na mipango yake, na matamanio yake.

Na katika tukio hilo la Ufunuo ni vivyo hivyo..Biblia imemtaja mnyama huyo kuwa mwenye vichwa saba..Lakini kiuhalisia ni Wanyama saba tofauti wenye mwili mmoja…Na kila mnyama (yaani kichwa kina mambo yake)…Na pia ni mnyama mmoja tu kati ya hao wote mwenye pembe kumi (yaani ni kichwa kimoja tu chenye pembe hizo kumi).

Sasa hao Wanyama saba au vichwa saba ni nini?

Biblia inasema ni wafalme saba..

Ufunuo 17:9 “Hapo ndipo penye akili zenye hekima. Vile vichwa saba ni milima saba anayokalia mwanamke huyo

10 Navyo ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, na mmoja yupo, na mwingine hajaja bado. Naye atakapokuja imempasa kukaa muda mchache. ”.

Falme hizo kama zinavyojidhihirisha katika taifa la Mungu kwenye biblia ni MISRI, ASHURU, BABELI, UMEDI & UAJEMI, UYUNANI, RUMI YA KIPAGANI na RUMI YA KIDINI..Hizi ndizo falme hizo saba au Wanyama hao 7..Falme hizi ni Mataifa aliyotumia shetani kuutesa uzao wa Mungu kwa ujumla wake…

Mataifa Matano ya kwanza yaliwatesa wana wa Israeli peke yao, wakiwa Misri, na mengine baada ya kuchukuliwa tena mateka babeli..lakini haya mawili ya mwisho yaliwatesa wana wa Israeli pamoja na Kanisa la Kristo…Na hicho kichwa ndicho cha mwisho na ndiye mnyama wa 7 ambaye ni RUMI YA KIDINI,.. nacho ndicho chenye pembe zote saba.. mnyama huyu ndiye ambaye yupo sasa na anazidi kuongezeka nguvu siku baada ya siku,.atakapofikia kilele chake atazitumia pembe zake 10 ambayo ni mataifa yanayounda umoja wa ulaya (EU) kuhimiza ile chapa ya mnyama. Kwasasaba umoja huo una wanachama Zaidi ya 10..

Lakini unabii unaonyesha yatakuja kubakia 10 tu yenye nguvu kwenye umoja huo. Na Kwa pamoja yatashirikiana na mnyama huyo, (Rumi ya kidini Iliyopo chini ya kiongozi wa kanisa katoliki ,Papa) kuishawishi dunia kuendesha zoezi la kuwatia watu chapa. Kwa kipindi kifupi sana kisichozidi miaka mitatu na nusu, Chapa itakuwa imeshawafikia watu wote duniani…Watakaoikataa watakamatwa na kupelekwa kwenye kambi maalumu za mateso…

Wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita…Watakatifu wameondolewa duniani,.kuepushwa na ghadhabu ya Mungu na majaribu ya mpinga-kristo.

Ukali wa dhiki kuu.

Na huko katika magereza hayo ya mateso, watu watakitafuta kifo hawatakiona kama unabii unavyosema.. “kwasababu mtu anayekutesa siku zote hataki ufe haraka..lengo lake uteseke kwa muda mrefu”..Ndicho kitakachotokea siku hiyo..watu watateswa lakini hawatauawa kwa haraka (Yatakuwa ni mara 100 zaidi ya yale ya Hitler, ambayo alikuwa anawapiga watu kwa nyundo yenye uzani mdogo kichwani mara nyingi aangalie ni kwa kiwango gani watu wanasikia maumivu, na kiwango cha watu kustahimili vifo wanapouliwa taratibu..mtu huyo anapigwa nyundo hata saa 4 mpaka anazirai, na mwisho wa siku kufa..

Au wanamfanyia mtu operation bila ganzi huku anatazamwa uwezo wake wa kumudu maumivu, au wanawatia watu kwenye barafu kali wakiwa uchi kwa masaa kadhaa kila siku)…ndivyo atakavyofanya mpinga-kristo na ziadi wakati huo wa dhiki kuu, na mateso hayo yatadumu kwa muda mrefu sana kwenye kambi hizo..kwa miaka sio chini ya mitatu na nusu..baadaye ndipo watawaua..wakati wengine waliosalia huko nje wakiendelea kufurahia Maisha baada ya kuipokea chapa…Hivyo dhiki kuu haitawahusu watu wote, bali tu wale watakaoikataa chapa…

Dhiki ya mataifa.

Baada ya wale waliokataa chapa kufa wote…Itakuwa ni zamu ya wale walioikubali chapa kupitia dhiki na wao…Dhiki hiyo ni ghadhabu ya Mungu mwenyewe atakayoimwaga juu ya wale wote walioipokea chapa…Ghafla tu wakati wanaona dunia ni tamu mambo yataanza kubadilika…Bahari itakuwa damu, mito na chemchemu zote zikuwa damu, majipu na magonjwa ya ajabu yataanza kuwatokea, roho za mapepo wabaya zitaachiwa juu ya wanadamu, kutokuelewana kutaanza kutokea,vita vya wenyewe kwa wenyewe vitazuka, mvua ya mawe makubwa kama talanta zitaanza kushuka juu ya wanadamu,.. jua litashushwa chini kuwaunguza wanadamu kwa kipindi kirefu..na mwisho jua na mwezi na nyota vitatiwa giza, tetemeko kubwa duniani litatokea, kila visiwa kitapotea na kuzama kwenye bahari ya damu, na milima itafumuka..

Wanadamu wote walioipokea chapa watakufa kifo kibaya kuliko hata cha wale walioikataa chapa..na baada ya kifo hicho wote wataelekea jehanamu ya moto..Na kabla hawajamalizika wote kufa, wale wa mwisho mwisho kufa wachache sana ambao ni washirika wa vita vya Harmagedono ndani ya giza hilo kuu watamwona Kristo akija katika mawingu wataomboleza sana , lakini biblia inasema wataangamizwa kwa upanga utokao katika kinywa chake..

Biblia inasema

Mathayo 24:29 “Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;

30 ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi”

Je! Unatamani kuwepo kwenye dhiki kuu?.. mimi sitamani..Natumai hata na wewe pia hutamani, Lakini unafahamu kuwa huo wakati upo karibu sana yamkini mambo hayo yatatokea katika kizazi chetu? Je! umempa Kristo Maisha yako?..Una uhakika wa kwenda kwenye unyakuo?…au bado upo kwenye ulimwengu?..kama bado ni mwasherati endapo parapanda italia leo utabaki hapa kukutana na hayo yote tuliyoyasoma hapo juu..

Kama hujaokoka na unataka kuokoka, fanya hivyo sasahivi.. Hapo ulipo tubu..na mwambie Bwana unataka kufanyika kuwa kiumbe kipya..baada ya kutubu tafuta kanisa ushiriki na wengine wenye Imani moja na wewe.. Na baada ya hapo pia hakikisha unabatizwa katika ubatizo sahihi kama hujabatizwa…Ubatizo sahihi ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo..Na Roho Mtakatifu atakusaidia kufanya yaliyosalia katika Maisha yako, na kukuweka katika mstari wa wale watakaonyakuliwa na kuepushwa na hukumu ya Mungu ya milele.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 13

UFUNUO: Mlango wa 17

UFUNUO: Mlango wa 16.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je mama mjamzito anaruhusiwa kufunga?

Je mama mjamzito anaruhusiwa kufunga?..Na je watoto wadogo wanaruhusiwa kufunga na kusali? Na je inawezekana kufunga siku 40 bila kula?..

Kabla ya kufahamu kama mama mjamzito anaruhusiwa kufunga au la!..Hebu jiulize swali lifuatalo..{Je! Mtu katika hali ya kawaida anaruhusiwa kufunga siku 40 bila kula wala kunywa?..Au inawezekana mtu kufunga siku 40 bila kula wala kunywa na asife?}

Kama jibu ni ndio! basi Mjamzito naye anaweza kufunga.

Bwana Yesu alifunga siku 40 mchana na usiku bila kula wala kunya na hakufa…Na Mjaribu ibilisi alipomjia na kumwambia ageuze jiwe kuwa mkate..alimjibu na kumwambia imendikwa ..”mtu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila Neno litaokalo katika kinywa cha Mungu”

Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi.

2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.

3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.

4 Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu

Kama imewezekana mtu kuishi  siku 40 bila kula wala kunya na hajafa basi inawezekana mjamzito au mtu mwingine yeyote yule kufunga bila kupatikana na madhara yoyote isipokuwa tu afunge kwa Imani na si kwa kutimiza wajibu fulani, au kulazimishwa…

Nimewahi kukutana na kumthibitisha mtu binafsi ambaye amemaliza siku 40, bila kunywa wala kunywa na hawajafa…na wapo wengi tu wengine wanaokwenda mfungo hata wa wiki 2, 3 hadi 4..bila kula wala kunywa na wanaishi vizuri tu…Shetani anachowadanganya watu wengi siku hizi ni kwamba “jambo la kufunga siku 40 kama Bwana Yesu siku hizi halipo”…Huo ni uongo wa shetani..

Hivyo mwanamke mjamzito anaweza kufunga hata katika hiyo hali ya ujauzito na isimuathiri yeye wala mtoto..

Lakini afunge tu kwa Imani, na si kwa dini wala mazoea, wala kulazimishwa..kama atafunga kwa dini na mazoea au kwa kulazimishwa basi ni afadhali asifunge kwa maana atapata madhara…lakini akifunga kwa Imani, huku binafsi akijiweka katika imani, utakatifu na ukamilifu,.. anaweza kumaliza hata siku 40 na mtoto akazaliwa akiwa na afya yake kamili na baraka tele.

Na sio tu mama mjamzito anaruhusiwa kufunga bali hata watoto..Wengi hawawaruhusu watoto wao wafunge wakihofia kwamba watadhoofika..Huo pia ni uongo wa shetani..mtoto kama anasukumwa ndani yake kufunga, hapaswi kuzuiliwa kwasababu “Mtu  hataishi kwa mkate tu bali kwa kila Neno litokalo katika kinywa cha Mungu”…Na Neno lenyewe ndio hilo kwamba ” mambo mengine hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kusali”. Hivyo watoto wadogo wanaruhusiwa kufunga kama watu wazima.

Maran atha!


Mada Nyinginezo:

MSIJISUMBUE KWA NENO LOLOTE.

Je! taratibu za kufunga ndoa [yaani harusi] ni agizo la Mungu au ni mapokeo tu ya kibinadamu?

SIKU ILE NA SAA ILE.

Adamu alikuwa na watoto wangapi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

Je Vibwengo ni kweli vipo au ni hadithi za kutunga?.. Je namna ya kuvidhibiti vibwengo, mapepo na mashetani ni ipi? Na roho hizo za vibwengo zifanyaje kazi?

Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa kuna roho za malaika na roho za mashetani…Malaika walioasi ndio wanaojulikana kama mashetani leo…Na malaika hawa wanafanya kazi katika mamlaka ya giza…Yaani kazi yao ni kwenda kinyume na kila kazi ya Mungu…

Kadhalika malaika hao walioasi (yaani mashetani au kwa jina lingine Mapepo)..wapo wa aina nyingi na wenye tabia tofauti tofauti…Kama vile malaika walivyo wengi  na wenye tabia tofauti tofauti…kadhalika na mapepo nao ni hivyo hivyo…Katika biblia tunasoma kuna malaika wa maji..(Ufu.16:5)..kadhalika kuna malaika wanaohusika na nchi, bahari, pia wapo malaika wa kuleta habari kama Gabrieli, ..wapo malaika wa sifa kama maserafi na makerubi, wapo wa vita kama Mikaeli na wengine wengi.

Na katika upande wa pili wa malaika walioasi ni hivyo hivyo wana vipawa tofauti tofauti..yapo mapepo yanayohusika tu na maji, mengine moto, mengine yanahusika kusababisha majanga kama ajali,.. mengine kuleta magonjwa, mengine kuharibu nchi n.k..Lakini yote lengo lao kuu ni kupambana dhidi ya ufalme wa Nuru..

Sasa Vibwengo ni aina ya mashetani/mapepo yanayoangukia katika moja wapo ya hilo kundi…Vibwengo vina kazi ya kuwasumbua wale watu ambao hawajaokoka au hawajasimama vizuri kiimani..Na kwasababu ni roho za mapepo zile zile ambazo zinatenda kazi katika ufalme wa giza..hivyo lengo lao ni kuleta mauti ndani ya Mtu.

Na mtu anaweza kuishi na jamii hiyo ya mapepo aidha kwa kujua au kwa kutokujua…wakati mwingine mapepo hayo (vibwengo) vinaweza kujidhihirisha dhahiri kwa mtu..na mtu kuvishuhudia kabisa kwa macho…

Mara nyingi vinajidhihirisha kwa umbo la mtu mfupi sana aliyejaa..au aina fulani ya wanyama ambao wanaonekana kama watu..mfano wa maumbo yanayoonekana mara nyingi na vibwengo ni maumbo ya mfano wa nyani..Anaonekana mtu kama nyani lakini si nyani n.k…Na mapepo hayo yasipopatiwa  ufumbuzi mapema yanaweza kusababisha hata kifo cha kiroho na cha kimwili kwa mtu..au yanaweza kusababisha tatizo fulani lenye madhara makubwa…Hivyo si busara kuzipuuzia roho hizo chafu.

Mambo gani yanayokaribisha uwepo wa vibwengo?

Jambo la kwanza ni dhambi ndani ya maisha ya mtu..Mtu yeyote ambaye anaishi katika maisha ya dhambi anafungua mlango mpana sana  wa kusumbuliwa au kuingiliwa na roho zozote za mapepo..Mtu anayetenda dhambi ni kama mtu aliyewasha WIFI data kwenye simu yake ya mkononi.. kiasi kwamba simu yoyote iliyokaribu na yake inaweza kukamata mawimbi yatokayo katika hiyo simu yake…Kadhalika mapepo ni hivyo hivyo, mtu anayefanya dhambi ni kama amewasha WIFI katika ulimwengu wa roho,..kwamba hata mapepo yaliyokuwa yanatembea tembea huko na huko ni rahisi kupata habari za huyo mtu.. na kumwingia au kumletea madhara fulani.

Dhambi zifuatazo ndizo zinazoongoza kukaribisha uwepo wa vibwengo kwa mtu..na si tu vibwengo bali hata jamii nyingine zote za mapepo.

1) IBADA ZA SANAMU : Hii inahusisha aina zote za aubuduji sanamu, aidha za watu au za wanyama…unapoisujudia sanamu ya aina yoyote ile ni mlango mpana sana wa kuingiliwa na mapepo..au kuishi na vibwengo pamoja nawe…

2) UASHERATI : Dhambi hii inashika nafasi ya pili katika kukaribisha uwepo wa mapepo ndani ya mtu na hata kuvutia uwepo wa vibwengo..Asilimia kubwa ya watu wanaoona roho hizo za vibwengo lazima kwa namna moja au nyingine ni waasherati. wa kimwili.

3) USHIRIKINA/UCHAWI : Ushirikina ni hali ya kujihusisha husisha na masuala ya nguvu za giza,… kama kwenda kwa waganga au kwa watabiri wa nyota, au utambuzi…Mtu anayehudhuria kwa waganga huyo ni mshirikina hata kama sio mchawi kabisa…lakini kitendo tu cha kwenda kwa waganga kutafuta suluhisho fulani..huo tayari ni ushirikina..na ni mlango mpana sana unaoshika namba tatu kukusogeza karibu na uwepo wa roho za mapepo hususani vibwengo.

4) KUJIPAMBA:

Ikiwemo uvaaji wa wigi, kujitoboa mwilini na kujiweka vito kama hereni, mabangili, mikufu…pia upakaji wa wanja, upuliziaji wa marashi makali yasiyojulikana hata yametengenezewa wapi,..uchoraji wa hina na uchoraji tattoo..Mambo hayo  yanahusika sana katika kuvuta uwepo wa roho za vibwengo na jamii nyingine za mapepo…Ndio maana hata vibwengo vyenyewe vinakuwa kama vimepaka chokaa usoni, au vinatoa harufu ya marashi fulani yasiyojulikana..hiyo yote ni kuonesha vimekutana na mahali ambapo panastahili wao kuwepo..

5) UVAAJI MBAYA:

Mavazi yote yasiyopasa…kama suruali kwa wanawake, magauni kwa wanaume, mavazi ya nusu uchi kama vimini, vitop, nguo za kubana n.k…ni WIFI kwa mapepo….Hata roho hizo za vibwengo viwatokeapo watu zinakuwa kama zimevaa mavazi yasiyoeleweka, kiasi kwamba huwezi kukitambua kama ni jinsia ya kiume au ya kike…Sasa vinakuwa vinatafuta mahali panapowastahili…kwa watu wa jamii zao.

6) ULEVI, UVUTAJI SIGARA na ANASA: Disko ni makao ya mapepo, mtu anayeingia disko tayari anatoka na pepo pasipo hata yeye kujijua…Mapepo ndio makao yao huko, sehemu ambazo watu wapo akili nusu kutokana na ulevi…sehemu ambazo watu wanacheza cheza madansi na kucheka cheka na kuwa na mizaha…Ndio maana hata vibwengo vyenyewe viwatokeapo watu ni lazima viwe nusu-nusu kama vimelewa hivi…vinakuwa nusu vinaakili timamu nusu vitahira…vinachekacheka, mara vinacheza cheza, vinakuwa na mizaha mizaha…yote hiyo ni kwasababu ndiyo asili yao..Hivyo vinatafuta watu wenye asili kama yakwao vikae nao..na hao wapo bar, disko au kwenye vikundi vya kamari.

7) UTAZAMAJI WA PORNOGRAPHY: Pornograph ni picha za ngono..ambazo siku hizi zinatazamwa hata kupitia simu za mkononi…Ufahamu uliojaa zinaa ni lango kubwa la roho hizo…

Namna ya kuvidhibiti vibwengo na roho nyingine zozote za mapepo.

Suluhisho pekee la kuepukana na roho hizo za vibwengo ni kuokoka!…Kuokoka maana yake ni kutubu kwa kudhamiria na kumaanisha kabisa kuacha dhambi…unaacha dhambi zote ulizokuwa unazifanya hizo zilizoorodheshwa hapo juu na nyingine zote ambazo hazijaorodheshwa…Unatubu na kumwambia Bwana Yesu unahitaji wokovu na unamuhitaji yeye..si tu kwaajili ya kuepukana na vibwengo, bali kwasababu unahitaji kufanyika kuwa kiumbe kipya na kuwa mkamilifu kama Mungu alivyo.

Ukisha tubu hatua inayofuata ni kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kama ulikuwa hujabatizwa,.. na baada ya hapo Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yako atafanya mengine yote yaliyosalia.

Ukishaokoka namna hiyo! na kudhamiria kuacha dhambi…basi wewe mlango wa mapepo hautakuwepo ndani yako…Haiwezekani funza kuwepo ndani yako au kwenye mazingira yanayokuzunguka kama umefanya usafi kweli kweli…Dawa ya kuondoa funza ndani kwako ni kuwa msafi sio kuwaambia funza ondokeni kwangu…kadhalika dawa ya kuondoa mapepo na vibwengo karibu na wewe ni kuwa msafi.. (yaani kujiweka katika hali ya utakatifu), ambayo hiyo inakuja kwa kutubu dhambi na kuziacha..(yaani kuokoka) na sio kwenda kutafuta maombezi huku na huko…

Ikiwa umeshawahi kusumbuliwa na roho hizo za vibwengo..basi hiyo ndio dawa pekee tuliyopewa katika biblia takatifu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312 jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Wakatoliki wanaabudu sanamu?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

Kifo cha Reinhard Bonkey kinaacha ujumbe gani kwetu?


Mwinjilisti wa kimataifa Reinhard Bonkey, raia wa Ujerumani, aliyezaliwa tarehe 19 Aprili 1940.. Anaeleza jinsi alivyompa Kristo Maisha yake akiwa bado kijana mdogo mwenye umri wa miaka 9, baada ya kuhubiriwa na mama yake kuhusu habari za Yesu na dhambi zake.

Alidumu katika Imani mpaka kufika kwenda chuo cha biblia na Mara baada ya kumaliza chuo cha mafunzo ya biblia huko Wales na kusimikwa utumishi wa Uchungaji nchini kwake Ujerumani, ndipo alipoanza kuja Afrika, kwa ziara zake za umishionari na kuweka maskani yake rasmi  katika nchi ndogo ya Lesotho.

Ono la kumtumikia Mungu Afrika.

Akiwa huko Lesotho Reinhard Bonkey anasema kabla hajaanza kazi ya Uinjilisti katika bara la Afrika akiwa na mke wake, usiku mmoja aliota ndoto ambapo aliona bara la Afrika likioshwa kwa damu ya Yesu kuanzia kusini kwenda kaskazini, na kutoka magharibi kwenda mashariki. kwa siku ya kwanza anasema aliipuuzia ndoto hiyo akidhani kuwa labda usiku uliopitia alikula ndizi, lakini ndoto hiyo ikajirudia kwa siku nne mfululizo ndipo alipotambua kuwa ni Mungu ndiye alikuwa anasema naye.

Akaenda kuwaeleza viongozi wake juu ya jambo hilo na nia yake lakini walimkataza na kumwambia afanye kazi kama za wamishionari wengine, lakini sio hiyo ya kuzunguka kuhubiri injili..Lakini Bonkey aliondoka na kwenda kukaa hotelini kwa kipindi kumwomba Mungu ampe ruhusu ya kupata kibali kwa viongozi wake, kama ikiwa ni yeye kweli aliyemuita lakini wakati akiwa anaomba alisikia sauti ya Mungu ikimwambia..“USIPOIFANYA HII KAZI, NITACHAGUA MTU MWINGINE WA KUIFANYA”

Mwanzo ya uinjilisti:

Aliposikia hivyo alishituka kwa hofu, ndipo akamfuata mke wake, na kumweleza kuwa siku hiyo hiyo ataandika barua ya kuacha, kazi yake ya utumishi aliyowekwa na viongozi wake..Na ndipo akaanza safari ya kuhubiri injili katika miji mbalimbali bila kugeuka nyuma.

Kwa kuwa hakuwa na mtu wa kumuuliza jinsi kuandaa mikutano na jinsi ya kufundisha kwenye mikutano ya hadhara, alitumia uzoefu wake ule ule akijua kuwa Roho Mtakatifu atakuwa naye katika kila hatua, japo alipotoka hakufundishwa juu udhihirisho wa nguvu za Mungu, hivyo kila mahali alipokuwa akiandaa mikutano watu walikuwa wakimtazama tu,

Anasema siku moja nguvu za Mungu zilishuka katika mkutanao ule, na yule mtafsiri wake alidondoka chini kwa kuzidiwa na nguvu hizo, na huku akiwa analia alisikia sauti ikimwambia “NENO LANGU LITOKALO KINYWANI MWAKO, LINA NGUVU ILE ILE SAWA NA LINAVYOTOKA KATIKA KINYWA CHANGU”..

Imani ilivyoanza kutenda kazi:

Alivyosikia vile alishangaa, akapata msukumo mkubwa sana ndani yake, ndipo kwa ujasiri akasema “Vipofu wote walio katika huu mkutano wasimame, na leo hii kwa mara ya kwanza watakwenda kuuona uso wa Bonkey”..Alivyosema vile, ndani ya moyo wake alisikia sauti nyingine ikimwambia..Na ikiwa hatawataona utafanyaje…Lakini yeye alisema Ninalisema Neno la Mungu..Na alipotamka tu “KWA JINA LA YESU, MACHO YENU YAFUMBUKE!!” ..Alichosikia tu ni kelele za watu wakisema ninaona…wakirukaruka, na mara mda huo huo alimwona mtoto mdogo aliyekuwa amebebwa na mama yake, akipitishwa juu ya vichwa vya watu, na kurushwa mbele mpaka pale alipo na kujikuta mtoto yule yupo mikononi mwake..

Anasema mtoto huyo alikuwa na viungo vilivyokunjana mfano wa tambi…Lakini saa ile ile alipofika mikononi mwake, nguvu za Mungu zikaanza kumtetemesha mtoto yule, akamwachia akadondoka lakini hakutua vibaya bali alitua kwa miguu yake na kuanza kukimbia na kurukaruka. Na huo ndio ulikuwa mwanzo wa huduma yake iliyoambata na nguvu za Roho Mtakatifu.

Jinsi huduma ilivyokuwa:

Mwanzoni kabisa mwa huduma yake Alianza kwa kuitisha mikutano midogo midogo, japo anasema haikuwa na mwitikio mkubwa kwa siku za mwanzo, kwani mkutano ulio mkubwa sana uliweza kuhudhuriwa na watu mia nane tu (800). Lakini, baadaye alivyozidi kuhubiri idadi ya watu ilizidi kuongezeka kwa kasi, mpaka kufikia hatua kila mkutano anaouitisha haupungui watu laki moja na nusu (150,000). Na kwa jinsi ilivyozidi kuendelea alipoitisha tu mkutano mmoja katika mji mmoja, kuliweza kukusanyika watu Zaidi ya milioni moja na laki sita (1,600,000).

Zaidi ya watu milioni moja kwa siku walikuwa wanarekodiwa kumpa Kristo Maisha yao.

Na Tangu mwaka 1986, huduma ya Reinhard Bonkey inarekodi ya watu Zaidi ya milioni 77 waliokuja kwa Kristo. Hiyo ni Zaidi ya idadi ya watu waliopo katika la Tanzania.

Kifo cha Reinhard Bonkey:

Mnamo tarehe 7 Disemba 2019, safari ya mtumishi huyu mwaminifu wa Mungu ilifikia kikomo..Reinhard Bonkey, bila shaka watu kama hawa ndio wanaostahili waandikiwe kwenye makaburi yao maneno haya:

2Timotheo 4:7  “Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda”;

NI FUNZO GANI AMETUACHIA KATIKA UTUMISHI WA MUNGU?

Ukweli ni kwamba Huduma ya mtumishi huyu ilifanikiwa kwa jambo moja linaloitwa utiifu. Alitii pale alipoitwa bila kujali mahali atakapokwenda, na kazi atakayoifanya.. Enzi hizo hakukuwa na miundo mbinu mizuri kama iliyopo sasa, lakini alijitoa kwa hali na mali kwa ajili ya injli ya Kristo..

Waebrania 12:1  Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

2  tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.

Watu kama hawa, tutawezaje kwenda kupata thawabu moja na wao kama na sisi hatutapiga mbio kama za kwao?

Unasubiri nini usitubu dhambi zako?

Ikiwa bado upo nje ya Kristo, usisubiri kifo kikukute, tubu leo hii umpe Bwana Maisha yako, Akuokoe..Fanya hivyo kwa kumaanisha hapo ulipo kwa kupiga magoti na kumwambia Mungu, Nisamehe makosa yangu yote, na kuanzia leo ninakiri kukutumikia na kukufuata,. Nisafishe kwa damu ya mwanao mpendwa YESU KRISTO, nifanyike kuwa mwana wako kuanzia wakati huu.

Sasa ikiwa umefanya hivyo, kwa kumaanisha kutoka moyoni, unachopaswa kufanya ni kuithibitisha hiyo Imani yako kwa kuacha yale ambayo ulikuwa unayafanya nyuma, na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kimaandiko wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa jina la YESU KRISTO, sawasawa na Matendo 2:38 ili uukamilishe wokovu wako.

Na Kristo akishaona mwitikio wako atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, bure, ambaye huo ndio muhuri wa wokovu wako, atakayekaa nawe mpaka mwisho wa safari yako hapa duniani,..ikiwa unyakuo utakuwa haujapita. Fanya hivyo na Bwana akubariki sana.

Maran Atha!

Mbali na histori na Kifo cha Reinhard Bonkey, ungependa kupata habari za mashujaa wengine wa Imani?. Mtazame William Branham chini utajifunza mengi pia.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM

USHUHUDA WA RICKY:

MTETEZI WAKO NI NANI?

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NENO HILI NI GUMU,NI NANI AWEZAYE KULISIKIA?

NENO HILI NI GUMU, NI NANI AWEZAYE KULISIKIA?


Tuwe tayari pia kuyapokea maneno magumu kutoka kwa Kristo.

Si maneno yote aliyokuwa anayazungumza Bwana yalikuwa ni mepesi kuyapokea kwa namna ya kawaida,..

Kuna wakati aliwaambia wanafunzi wake,

Mathayo 10:37 “Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.

39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”

Jaribu kufikiria wakati huo, Kristo alikuwa bado hajasulibiwa, na wala hakukuwa na mtu yeyote aliyewahi kudhani kuwa siku moja atakwenda kutundikwa mtini uchi mfano wa wanyanganyi..Lakini tunaona hapa Kristo anawaambia wanafunzi wake juu ya kujitwika misalaba kana kwamba wanaelewa ni nini maana ya kujitwika msalaba na kumfuata yeye, au walishawahi kumwona yeye akijitwika msalaba wake…

Kwa namna ya kawaida, unaweza ukadhani ni rahisi kulipokea hilo neno,.. ni sawa na leo hii, umsikie raisi anasema mtu yeyote anayetaka nimfanye kuwa waziri ahakikishe kwanza anabeba bomu lake mkononi na kutembea nalo kila siku,.. na muda wowote awe tayari kujilipua…Unaweza kusema raisi anazungumza maneno gani haya..

Ndivyo ilivyokuwa kwa Kristo, misalaba ilikuwa ni kwa ajili ya watu waovu tena wale walioshindikana wenye kesi nzito za mauaji..sasa kusikia eti mtu mwema kama yeye anataja mambo ya misalaba ilikuwa ni kauli tata sana.

Kauli nyingine ya Bwana ni hii:

Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.

54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.

56 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake”

Fikiria tena leo hii mtu anakuambia uule mwili wake, na uinywe damu yake, si utamwona kama ni mchawi?.. Vivyo hivyo na maneno mengine mengi, kama lile alilosema yeye ni chakula kitokacho mbinguni, na bomoeni hekalu hili nitalijenga ndani ya siku tatu. N.k.

Maneno kama hayo ndiyo yaliyowafanya wengi wa wanafunzi wake wasifuatane naye tena..

Yohana 6:60 “Basi watu wengi miongoni mwa wanafunzi wake waliposikia, walisema, Neno hili ni gumu, ni nani awezaye kulisikia?

61 Naye Yesu akafahamu nafsini mwake ya kuwa wanafunzi wake wanalinung’unikia neno hilo, akawaambia, Je! Neno hili linawakwaza?

62 Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza?

63 Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima”.

Je! Na leo hii bado anatenda hivyo?

Hata leo hii Kristo anapowaita watu wamfuate sio kila jambo atalitolea sababu zake siku hiyo hiyo,…wewe unachopaswa kufanya ni kumtii tu na kumwamini maadamu ni mwanafunzi wake,… anapokuambia acha hiki, hata kama hukielewi vizuri leo wewe acha na umfuate, anapokuambia badilisha mavazi yako,tupa vimini, na mawigi, na malipstik na mahereni, usiwaze waze mara mbili anamaanisha nini,….wewe ni kipofu hivyo usijifanye unaona!.

Anapokuambia jitenge na marafiki wa aina hii usianze kuwaza dunia itanionaje, akikuambia acha hiyo kazi unayoifanya, usianze kuwaza Kesho nitakula nini,..Sababu zote hizo atakuja kukupa huko baadaye mbeleni kwa jinsi unavyozidi kutii…lakini kwasahivi mtii kwa kile atakachokuambia ufanye..

Mitume 12, walipoitwa waliambiwa neon moja tu! “NIFUATE”..wakaacha kila kitu hapo hapo na kumfuata, hawakupewa maelezo ya kutosha wanakwenda wapi…

walistahimili maneno magumu kama hayo, mpaka ukafikia wakati wa wao kuelewa sababu ya mambo yote, wengine walishindwa kuyapokea na ndio maana hawakufika Pentekoste, lakini mitume wale 11 wa Bwana na mwingine mmoja wa 12 aliyekuja kuongezeka walitii na ndio maana walifika Pentekoste. Na Mungu akawafanya kuwa nguzo za kanisa.

Sikuzote unapaswa ujue maneno ya Kristo Ni Roho tena ni uzima, hata kama huyaelewi kwasasa.. Ibrahimu aliambiwa akamtoe mwanawe kafara, lakini kwasababu alimwamini Mungu anayemtumikia, akahesabu kuwa Mungu anaweza kumfufua tena mwanae huko atakakokuwa hata kama atakuwa ameshaoza na kuwa udongo,..(Waebrania 11:18-19) hakujali kwamba kitendo anachokwenda kufanya ni kitendo cha kigaidi..lakini alitii, leo hii ndio tunaelewa Mungu alikuwa anafunua nini katika kumwambia afanye vile..Lakini badala ya kupoteza ilikuwa kinyume chake kupata..

Kubali kuipoteza nafsi yako leo kwa ajili ya Kristo, Ukifahamu kuwa siku moja utaipata. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

KARAMA YA MUNGU NI UZIMA WA MILELE.

SIKU ILE NA SAA ILE.

 

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?

Utaachaje kula kucha?..dawa ya kuacha kula kucha ni ipi?..Je ni kweli tatizo la kula kucha haisababishwi na mapepo?..Je mtu atahukumiwa kwa kosa la kula kucha?..Karibu tujifunze pamoja kwa kuongeza maarifa juu  ya mambo haya ili yaweze kutusaidia kuishi kwa amani na furaha..

Tatizo la kula kucha limekuwa limewakabili watu wengi..Na endapo ikitokea mtu anakula kucha mpaka ukubwani na anapojaribu kuacha inashindikana..basi ni rahisi kujihisi kuwa na kasoro fulani,.. Na wakati mwingine kujihisi kwamba kuna roho fulani inayomsukuma kufanya hivyo..na hivyo kumpotezea ujasiri.

Kula kucha ni kitendo ambacho mtu anakuwa katika hali fulani ya kiakili labda mawazo, au katika hali ya kutafakari kwa kina, au katika hali ya kuona aibu, au katika hali ya upweke sana, au furaha sana, au huzuni sana n.k inatofautiana kati ya mtu na mtu….ambapo mtu akiwa katika hali hiyo anajikuta vidole vimefika mdomoni pasipo hata kujijua..Na ufahamu unaporudi anajikuta tayari kashapunguza kiwango fulani cha kucha au nyama pembezoni mwa kucha. Atajaribu kuacha lakini kesho itajirudia hiyo hali…

Sasa swali ni je! ni kweli ni roho za mapepo ndio zinahusika na hiyo hali au ni Tabia tu ya mtu!.

Kwanza ni muhimu kufahamu utendaji kazi wa roho za mapepo…ndipo turudi kuamua kama ulaji kucha ni mapepo ndani ya mtu au la!..

Mapepo yanapomwingia mtu kazi ya kwanza yanayofanya ni kumfanya yule mtu awe mwovu…Mapepo yakiwa ndani ya mtu yanamfanya asipende kusoma Neno,..yanamfanya atamani kutenda dhambi, yanafanya kuwa mwasherati,..mtazamaji pornography, mtukanaji, mlawiti..yanamfanya avae vibaya (Nusu uchi)..Yanamfanya mtu anaposikia habari za injili anachukia..

Na mapepo yanampeleka mtu siku zote mbali na kweli ya Biblia…yanampeleka mtu mahali pasipo kuwa na MAJI YA UZIMA (Jangwani) Soma Luka 11:24..Na mahali ambapo watu wamekufa kiroho kama disko, bar, kwenye kamari, kwenye vikao vya usengenyaji, penye mikusanyiko ya watu wenye mizaa n.k sehemu hizo katika roho ni makaburini…Bar ni makaburi ya kiroho, disko ni makaburini,  kadhalika na madanguro na sehemu nyingine zote za kiulimwengu..

Marko 5:1 “Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.

2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;”

Kadhalika mapepo yakiwa ndani ya mtu yanaweza kumsababishia ugonjwa fulani au udhaifu fulani,..Udhaifu huo unaweza ukawa ulemavu wa viungo au ulemavu wa kiakili, au kiufahamu… kama wa kushindwa kujizuia kufanya kitu fulani.

Ulemavu wa kiufahamu inahusisha mtu kula vitu visivyoliwa, ufahamu wa huyo mtu unampeleka kula vitu ambavyo sio kawaida mwanadamu kuvila…kwamfano mtu utakuta anatamani kula chuma, mwingine anakula sindano, mwingine anakula glasi, mwingine makaratasi, mwingine nyama mbichi unakuta hajisikii kabisa hamu ya kula nyama iliyoiva…mwingine mchanga, n.k mara nyingi watu wa namna hii wanakuwa na roho fulani inayowasukuma wao kufanya hivyo hata kama hawajijui..na ndio roho hizo hizo zinazowasukuma watu kupata hamu ya kuvuta sigara, bangi na hata kunywa pombe…Hivyo suluhisho ni kufunguliwa…ambapo tutaona namna ya kufunguliwa na hizo roho mwishoni  mwa somo hili..

Sasa kuna matatizo mengine ambayo hayasababishwi na mapepo yoyote bali tabia au hali fulani ya kimaumbile..

Kwamfano wanawake wajawazito  kutamani kula udongo (ingawa sio wote) lakini wengi wao,..sisemi udongo gunia zima..hapana bali ile hamu ya kula kiwango kidogo cha udongo..hiyo haisababishwi na mapepo bali maumbile..Mwanamke akishajifungua hiyo hali inakwisha…

Kadhalika hali ya kuvutiwa kula udongo wakati mvua kunyesha…Harufu ile ya udongo  inawavutia maelfu ya watu na hata wakati mwingine watu wanafikia hatua ya kulamba kidogo udongo..Hiyo pia haisababishwi na mapepo bali maumbile ya miili yetu jinsi yalivyoumbwa.

Pia hali ya kupenda harufu ya petrol au mafuta ya taa na kutamani kuyala..Hiyo pia haisababishwi na mapepo bali maumbile..

Lakini mambo yote haya..ni kwa kiasi, yakizidi sana kufikia kumfanya mtu anywe lita za petroli au kula magunia kadhaa ya udongo hilo ni tatizo lingine ambalo linaweza kusababishwa na roho za mapepo..hivyo tendo la kiroho linahitajika haraka kuliondoa tatizo hilo.

Sasa tukirudi katika suala la kula kucha..

Asilimia kubwa ya watu wanaokula kucha ni tatizo la kiufahamu, ambalo chanzo chake sio mapepo…Wengi wanachukua tabia hiyo kutoka aidha kwa wazazi au ndugu zao au  marafiki pindi wanapokuwa wadogo na kuendelea nayo hivyo hivyo mpaka kufikia hatua ya kuwa sehemu ya maisha yao.

Tabia ya kula kucha haina tofauti sana na tabia ya kula kifuniko cha kalamu au kulamba lamba lips, au kung’ata ng’ata meno…Ni tabia ambazo mtu alipokuwa aidha mtoto au mtu mzima, alimwona mtu fulani akifanya na hivyo yeye naye akajikuta anaiga pasipo kujitambua na hivyo kuwa ni tabia yake..

Hivyo tatizo la kula kucha sio mapepo..Hautasimamishwa kwenye kiti cha hukumu kwa kosa la kula kucha…

Kumbuka; Tunapozungumzia kula kucha hatumaanishi kula vidole mpaka vitoke damu zitoke kama bomba, au kula nyama ya vidole mpaka vidole vichuruzike damu kabisa..hapana. Hali kama hiyo ikitokea basi kuna roho nyingine ya adui inahusika hapo…Lakini kama ni kwa kiwango cha kawaida kama cha watu wengine unaowafahamu hilo halisababishwi na mapepo..

Ifuatayo ni dawa ya kuacha kula kucha.

Utaachaje kula kucha? (Zingatia mambo makuu mawili yafuatayo).

KWANZA: Ni kumkabidhi Yesu maisha. Ukitaka kuondoa tabia yoyote katika maisha yako…Kwa nguvu zako huwezi, ni lazima uhitaji nguvu za ziada…Wewe mwenyewe umeona!..Umepambana sana lakini bado…Hiyo ni kuonesha kwamba sisi wanadamu kwa nguvu zetu hatuwezi kufanya lolote…Hivyo mkabidhi Yesu Kristo maisha yako ili kwamba akusafishe na kukufanya mtu kamili…Tubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, tubia uasherati kama ulikuwa mwasherati, rushwa, wizi, ulevi, uvutaji sigara, rushwa, ukahaba, anasa n.k..Na ukishaacha..Hakikisha unakwenda kutafuta ubatizo sahihi kama hujabatizwa..Ubatizo sahihi ni wa kuzama mwili wote kwenye maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo (kulingana na Matendo 2:38)…Na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukusaidia kufanya yale ambayo ulikuwa huwezi kufanya.

Usiokoke tu kwasababu unataka kuacha kula kucha..Hapana bali okoka kwasababu unahitaji kubadilishwa maisha yako na Bwana Yesu na unataka kuwa mkamilifu kama Mungu.

PILI: Baada ya kuokoka…

Mwambie Bwana Yesu katika sala..wala usifunge wala usiingie kwenye maombi ya mkesha…Mwambie tu..“Bwana kuanzia leo sitaki kula kucha nisaidie”..Basi hivyo tu!..Ukishafanya hivyo..Hatua inayofuata ni ya muhimu sana….NENDA KANUNUE NAIL-cutter au Nail-clipper..kama hufahamu nail cutter ni nini  Tazama picha chini..

Unapoacha kula kucha, kucha zako zitaanza kukua na hivyo usipozipunguza kwa kifaa maalumu ni rahisi kushawishika kurudia kuzipugnuza kwa meno..Hivyo ili kuonyesha imani yako ipo katika matendo kanunue kifaa hicho, au kingine chochote kile kitakachotumika kupunguza kucha zako zinapokua..Usiwe na hofu wakati mwingine unaweza ukajisahau na kufikisha vidole mdomoni…Lakini kabla hujaanza kuzitafuna Roho atakusaidia kukukumbusha..hivyo unapokumbushwa kubali kutii… na hiyo hali hatimaye itaisha kabisa…haijalishi umekaa nayo kwa miaka mingapi…Itaisha!..Zipo shuhuda za waliomaliza tatizo kwa msaada wa Mungu, na kwako pia litaisha kama utapenda liishe…Na hata kama tatizo lako linasababishwa na roho za fulani za mapepo basi hatua hizi mbili ni dawa tosha ya kuziondoa hizo roho ndani yako..Hauhitaji kuombewa..Wewe fuata hizo hatua hapo juu na tatizo lako litaisha.

Bwana akuabariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali share na wengine nao wanufaike.


Mada Nyinginezo:

Ubatizo wa moto ni upi?

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.

Usilete ujira wa kahaba, nyumbani kwa Mungu.


Shalom, Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Maandiko..

Kuna mambo ambayo unaweza kuyasema ukadhani hayapo kabisa kwenye biblia..Lakini yapo!…Na kuna mambo machache yanayopuuziwa na wengi..lakini ni ya kuzingatia sana tunapomkaribia Mungu..Kitu kimoja ambacho wengi hawajui ni kwamba Mungu wetu tunayemwabudu hachangamani na uchafu…Mtu yeyote Yule aliye mchafu awe mchungaji, au mwalimu, au mwinjisti, au nabii, au muumini wa kawaida..

Mungu hawezi kutembea naye akiwa katika hali ya uchafu, hastahili hata kushiriki meza ya Bwana wala kumtolea Mungu sadaka!!…wala maombi yake hayasikilizwi wala dua zake hazimfikii…Kwa ufupi mtu huyo tayari ameshafarakana na Mungu na ni Adui wa Mungu (Soma Isaya 59:1-5)..Na endapo akilazimisha kumfanyia Mungu ibada katika hali hiyo huku anajijua kuwa yeye ni mchafu na hataki kubadilika…Mtu huyo anajitafutia laana badala ya Baraka…

Asilimia kubwa ya wahubiri wanalijua hilo, isipokuwa hawapendi kuwaambia watu ukweli..kutokana na kwamba mapato yao kanisani yatashuka…watawezaje kumwambia kahaba asitoe kwanza sadaka zake mpaka atakapomgeukia Mungu kwa moyo wake wote kwanza, kwa kuacha uasherati wake??..Hawawezi kufanya hivyo kwasababu ndio ulaji wao upo hapo! akimwambia hivyo anaogopa atakasirika na hivyo kuondoka…Lakini matokeo ya kutokufanya hivyo ni kumtafutia laana Yule anayetoa sadaka hizo haramu mbele za Mungu…

Leo tutajifunza mistari kadhaa ihusuyo habari hizo..Ambapo tukishajifunza itatusaidia kudhamiria kuokoka kwanza kwa kumaanisha kuziacha dhambi ndipo tumkaribie Mungu.

Kwanza kabisa kama hujaokoka, na unajua kabisa unastahili kuokoka lakini hutaki na unaendelea kuwa vuguvugu..Bado unaendelea kufanya kazi yako ya kujiuza kisirisiri, bado unaendelea kula rushwa kisirisiri, unaendelea kutapeli kisirisiri..Na Jumapili unakwenda kanisani kuabudu na kutoa sadaka yako kwa Mungu..NATAKA NIKUAMBIE UNAFANYA DHAMBI!!..Inawezekana hujawahi kabisa kuhubiriwa hivi kanisani kwako..lakini leo hii sikia Neno la Mungu…Acha kabisa usimtolee Mungu, sadaka hizo kwasababu ni unamdharau..unajitafutia laana badala ya Baraka…

Biblia inasema…

Kumbukumbu 23: 18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Lengo la Mungu kutuagiza kumtolea, sio kwamba anashida ya Hela,.au anatafuta kuwatajirisha watumishi wake…hapana hilo sio lengo lake..Yeye ana njia zaidi ya milioni moja ya kuwalisha watumishi wake wa kweli, tofauti na hata hiyo ya madhabahuni…Lengo lake kuu ni kutuumbia sisi moyo wa utoaji ndani yetu kama yeye alivyo mtoaji..kwamba hata ikitokea yupo mtu mwenye uhitaji katokea mbele yetu tuwe na moyo wa kutoa sehemu ya vitu vyetu na muda wetu kumsaidia…jambo ambalo linampendeza na lituletealo Baraka kutoka kwake…

Anataka tuwe wakamilifu na watakatifu kama yeye alivyo…Lakini unapokwenda kanisani na lengo la kwamba Mungu anahitaji fedha kutoka kwako au unakwenda kumpa mchungaji fedha,..Na hivyo fedha yoyote tu itakayokuja mkononi mwako hata ya rushwa ni ruksa kuipeleka nyumbani kwa Mungu…Kanisa sio benki ya madanguro wala mafisadi kwamba mafedha yote haramu ndiyo yanakwenda kuhifadhiwa huko…..Ni kujitafutia laana badala ya Baraka.

Soma tena mstari huu..

Mhubiri 5: 1 “Jitunze mguu wako uendapo nyumbani kwa Mungu; Maana ni heri kukaribia ili usikie, Kuliko kutoa kafara ya wapumbavu; Ambao hawajui kuwa wafanya mabaya”.

Unaona!..Biblia inasema ni heri ungeenda tu kusikiliza kuliko kwenda na kutoka kafara za wapumbavu ambao hawajui kuwa wanafanya dhambi…Usitie mkono wako kushiriki shughuli zozote za kanisa kama unajijua huna mpango na Mungu…Unafanya dhambi na utajitafutia laana badala ya Baraka.. Kadhalika usishiriki meza ya Bwana kama hujaokoka kikweli kweli na kupokea Roho Mtakatifu,.Kama ni mzinzi na mwasherati..pengine hukuhubiriwa kanisani, kwasababu Mhubiri wako pengine aliogopa angekwambia ukweli kwamba unatenda dhambi ungekwazika na kuhama kanisa na yeye akakosa mapato..lakini leo lisikie Neno la Mungu usiisogelee madhabahu kama hujaamua kumgeukia Yesu Kristo kikweli kweli…Usiule mwili wa Kristo, wala damu yake isivyopaswa kwasababu utajitafutia laana badala ya Baraka…

Usilete ujira wa kahaba, nyumbani kwa Mungu.

Soma…

1Wakorintho 11:27 “Basi kila aulaye mkate huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa amejipatia hatia ya mwili na damu ya Bwana.

28 Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe.

29 Maana alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kutokuupambanua ule mwili.

30 Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala. Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu tusingehukumiwa”

Yuda hakujipambanua vizuri..akaenda kushiriki meza ya Bwana huku moyoni mwake kulikuwa na mawazo ya kumsaliti Bwana Yesu..kilichotokea ni shetani kumwingia saa hiyohiyo baada ya kupokea tonge na matokeo yake yaliishia ni kifo kasome Yohana 13:26-27 (Tonge linalozungumziwa hapo sio tonge la ugali bali mkate wa Bwana). Wakati wengine wamepokea Baraka kwa kushiriki ile meza ya Bwana, Yuda yeye kapokea laana kwa kushiriki kitendo hicho hicho…

Kadhalika Kabla ya kwenda kupokea ule mkate wala kupokea kile kikombe jiulize mara mbili mbili je!..umeokoka kweli kweli?..Kama hujaokoka na unakwenda kushiriki basi umeenda kujizolea laana badala ya Baraka.

Kadhalika kama Hujaamua kuacha dhambi na kugeuka na kukusudia kumfuata Yesu Kristo kwa moyo wako wote,..halafu unakwenda kubatizwa na huku moyoni mwako unajua kabisa hujaamua kuacha uasherati, ulevi au sigara au uchafu uliokuwa unaufanya..na hivyo ukaenda kuingia kwenye yale maji na kubatizwa nataka nikuambie utakuwa umekwenda kujitafutia laana badala ya Baraka..Kama hujaamua kumguekia Yesu kwa dhati..usiende kubatizwa kabisa..subiri mpaka wakati utakapoamua kama hiyo nafasi itakuwepo..

Usishiriki jambo lolote la kiimani kama hujaamua kweli kuwa upande wa Mungu.

Na mambo mengine yote hahusuyo madhabahu usiyafanye kama huna uhusiano wowote na Mungu…hata usimfuate Mtumishi wa Mungu kumwomba akutabirie wala kukuombea kama mwenyewe unajua moyoni huna mpango na msalaba..ni hatari kubwa sana kufanya hivyo nenda kasome kitabu cha (Ezekieli 14:3-4) na kilichomtokea mke wa mfalme Yeroboamu, uone ni nini kitamtokea mtu Yule ambaye kwa makusudi hana mpango na Mungu na bado anataka kwenda kuuliza kwa Mungu..

Usilete ujira wa kahaba, nyumbani kwa Mungu.

hata ya kuhubiri madhabahuni ni hatari,..kama hujatakaswa kwa Damu ya Yesu, usiisogelee kabisa madhabahu…

Kama ulikuwa unafanya hivyo na hujui kwamba ulikuwa unakosea..Ulikuwa hujui kwamba sadaka yako ya ukahaba ni machukizo mbele za Mungu..na sasa unataka kutubu na kujitakasa ili sadaka zako zikubaliwe mbele za Mungu..Mlango upo wazi leo..unachopaswa kufanya ni kudhamiria kwanza kuacha dhambi na kukiri kwamba ulikuwa mkosaji..kisha unatubu na kumwambia Bwana akusamehe na kukuosha tena kuwa mpya…

Ukifanya hivyo kwa kumaanisha kabisa kutoka moyoni, basi Bwana YESU atakuwa ameshakusamehe..Hivyo Baada ya hapo nenda kabatizwa kama hujabatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa Jina la Yesu, na kisha Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukutia muhuri kuwa wake milele..

Na mwisho ni kusudia kuishi maisha ya usafi na utakatifu kuanzia huo wakati na kuendelea kulingana na maagizo ya Mungu..Hapo sadaka zako zitampendeza Mungu, na sala zako kwake zitakuwa kama manukato mazuri mbele zake, Maombi yako yatasikiwa, dua zako zitasikilizwa, sifa zako zitampendeza Mungu, kwasababu upo chini ya damu ya Emanueli, YESU KRISTO..

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

Vifo vya mitume wa Yesu/ jinsi mitume walivyokufa.


Mtume pekee ambaye biblia inarekodi mauaji yake jinsi yalivyokuwa ni mtume Yakobo ndugu yake  mtume Yohana. Huyu biblia inasema katika Matendo 12:1-2, kuwa Mfalme Herode alimuua kwa Upanga, alikatwa kichwa. Lakini kwa habari ya mitume wengine waliosalia biblia haijarekodi jambo lolote kuhusu vifo vyao.

Hivyo ili kupata taarifa zihusuzo huduma zao na vifo vyao ilipasa watu warejee katika hadithi ambazo zinaamika ziliandikwa na watu ambao walikuwa karibu sana na mitume, au walioshuhudia vifo vyao. Japo habari hizo hatuwezi kuzithibitisha kuwa zina usahihi wa asilimia mia, lakini kwa sehemu kubwa zimethitishwa kuwa kweli, kulingana na kupatana kwa maneno ya mashuhuda.

Mathayo:

Mathayo alijeruhiwa vibaya na upanga alipokuwa anahubiri katika nchi ya Ethiopia kaskazini mwa Afrika. Na baadaye kukumbwa na mauti kutokana na pigo la jeraha hilo..

Mtume Yohana:

Wakati wa wimbi kubwa la dhiki za wakristo likishamiri huko  Rumi , walimkamata Mtume Yohana na kumzamisha katika karai la mafuta yaliyotokota ili afe, lakini aliokoka kimiujiza. Wakamchukua na kumpeleka  katika kisiwa cha Patmo, na huko ndipo alipoandika kitabu cha Ufunuo. Lakini baadaye aliachiwa huru na kurudi Asia ndogo ili kupeleka barua zile kwa yale makanisa saba huko Asia ndogo. Ambayo kwa leo inajulikana kama nchi ya Uturuki. Huyu ndiye mtume pekee aliyekufa kifo cha Amani katika uzee.

Mtume Petro:

Mtume Petro aliuawa huko Rumi, inasemekana, walimkamata na kusulibisha kichwa chini miguu juu, kutimiza unabii Bwana Yesu aliompa katika:

Yohana 21;17  Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.

18  Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka.

19  Akasema neno hilo kwa kuonyesha ni kwa mauti gani atakayomtukuza Mungu. Naye akiisha kusema hayo akamwambia, Nifuate.

Hivyo ndivyo vifo vya mitume wa Yesu vilivyokuwa.

Batholomayo au Nathanaeli:

Alikuwa ni mmishionari huko Asia, aliuliwa kwa kuchapwa na mijeli mikali mpaka kufa. Unaweza ukaona jinsi mitume walivyokufa kikatili.

Andrea:

Walimkamata na kumfunga katika msalaba uliolazwa kama alama ya “X”. Kisha wakamwacha akiwa amefungwa kwa muda mrefu ili kumwongezea mateso ya kufa kwake,  huko ukigiriki. Na Wale waliokuwa wakimfuata mfutua walisema walimsikia akisema maneno haya;

Nukuu: ”Kwa muda mrefu, nimekuwa nikiingojea kwa hamu saa hii, msalaba umekuwa wakfu sikuzote kwa mwili wa Kristo kutundikwa juu yake”.

Aliendelea kuhubiri injili mbele ya wale watesi wake akiwa pale msalabani kwa siku mbili, mpaka mauti ilipomkuta.

Thomaso:

Alipigwa mkuki  katika moja ya ziara zake za kuhubiri injili na kupanda makanisa kule India.

Filipo:

Aliuawa kwa kusulibiwa alipokuwa akiitaabikia Injili huko kaskazini mwa Asia ndogo,.Alikamatwa kwanza na kutupwa gerezani, kisha baadaye wakaja kumsulubisha. Mwaka 54 W.W

Thadeo/Yuda:

Aliuawa kwa kusulibiwa mwaka 72 W.W huko Eddessa.

Simoni, Zelote:

Alihubiri injili Mauritania, na baadaye Uingereza ambapo huko ndipo naye alipokuja kusulibiwa.

Mathia:

Huyu ndiyo yule mtume aliyechukua nafasi ya Yuda aliyemsaliti Yesu. Historia inarekodi alipigwa naye kwa mawe na mwishowe kukatwa kichwa.

Yuda Iskariote:

Huyu alijinyonga baada ya kupata maumivu makali ya kumsaliti Yesu kwa vile vipande 30 vya fedha.

Mtume Paulo:

Paulo ambaye hakuwa miongoni mwa wale mitume 12, Aliteswa na jemedari wa Kirumi Nero, na baadaye akaja kukatwa kichwa.

Mitume wengine kama vile, Luka alitundikwa juu ya mti wa mizeituni kutokana na msimamo wake na Imani yake thabiti kwa Kristo..N.k. wapo mitume wengine pia waliouwa kwa njia mbalimbali wameandikwa katika vitabu vya historia za wakristo ukipenda unaweza kusoma mwenyewe kitabu kinachoitwa FOXES BOOK OF MARTYRS.. Hivyo ndivyo vifo vya mitume wa yesu/ jinsi mitume walivyokufa.

Lakini tunajifunza Nini?

Biblia inasema;

Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”

Wingu kubwa la mashahidi linatuzunguka mimi na wewe. Watu waliokuwa tayari kufa lakini wasiiache Imani. Kwasababu walikuwa wanajua thawabu iliyowekwa mbele yao ni kubwa kiasi gani. Vilevile walikuwa anajua hukumu itakayowapata kama wakiikana Imani ni kubwa kiasi gani. 

Je! Sisi (mimi na wewe) tutawezaje kupona tusipouthamini wokovu mkuu namna hii?.

Ukiwa bado upo nje ya Kristo, kumbuka kuwa mlango wa neema hautakuwa wazi siku zote.  Tubu leo umgeukie muumba wako. Unachotakiwa kufanya Hapo ulipo chukua muda mchache piga magoti. Kisha anza  wewe mwenyewe mweleze Mungu makosa yako yote. Na kwamba unahitaji msamaha.  unahitaji msaada kutoka kwake kukusaidia kuushinda ulimwengu.

Hivyo Ikiwa utatubu kwa kumaanisha kutoka moyoni mwako. Basi ujue kuwa Mungu yupo hapo kukusikia. Na  atakusamehe dhambi zako zote. Na kukuosha kwa damu ya mwanawe YESU KRISTO. Na Amani ya ajabu itaufunika moyo wako kuanzia huo wakati.

Bila kupoteza muda. Nenda katafute kanisa la Kiroho.Ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi. Na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38. Na Mungu mwenyewe atakumwagia kipawa chake cha Roho Mtakatifu kukusaidia siku zote. Fanya hivyo sasa na Mungu atakusaidia.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/bwana-alimaanisha-nini-aliposema-mtu-akija-kwangu-naye-hamchukii-baba-yake-hawezi-kuwa-mwanafunzi-wangu/

UNYAKUO.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MTINI, WENYE MAJANI.

Mtini, wenye majani ni upi?

Jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Neno la Mungu, Na leo tutajifunza somo lenye kichwa kinachosema “MTINI, WENYE MAJANI”..Unaweza usielewe kichwa hichi kina maana gani lakini twende pamoja mpaka mwisho naamini lipo jambo kubwa utajifunza.

Tunaona siku moja kabla Bwana Yesu kwenda kukaa na wanafunzi wake katika mlima wa mizetuni ili kuwaeleza habari za siku za mwisho, kuna jambo la kustaajabisha kidogo alilifanya mbele ya macho yako kwa makusudi kabisa..Na alifanya hivyo ili kuja kuwafundisha somo Fulani kesho yake..Na jambo lenyewe ni lile la “kuulaani mtini”

Akiwa anatoka Bethani asubuhi ili aende Yerusalemu hekaluni kufundisha alikutana na mtini njiani,(Mtini ni mti unaotoa matunda ya Tini) Embu tusome alichokifanya:..

Marko 11:12 “Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.

13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.

14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia”.

Mtini ni nini.

Mtini ni mti unaozaa matunda yanayoitwa TINI. Mti huu unastawi sana maeneo ya mashariki ya kati.

Sasa ukisoma juu juu unaweza kuona kama vile Bwana Yesu alikuwa hajui kuwa ule sio wakati wa TINI,.. na ndio maana akaulaani ule mtini kimakosa alipokosa matunda juu yake..Lakini alilifahamu hilo vizuri tutakuja kuona ni kwa namna gani hapo mbeleni kwa jinsi tunavyozidi kusoma. Lakini Kinyume chake alifanya vile kwa makusudi ili kuja kuwafundisha wanafunzi wake somo.. ambalo sisi watu kizazi hichi cha siku za mwisho ndio tunalolielewa vizuri..

Tukirudi kwenye ile Mathayo 24 yote, Bwana Yesu sasa akiwa na mitume wake pale katika Mlima wa mizeituni alianza kwa kuwaeleza dalili kuu za siku za mwisho,.. kwamba kutatokea manabii wa uongo na makristo wa uongo, kutakuwa na vita na habari za matetesi ya vita,kutaongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa, kutasimama chukizo la uharibifu, upendo wa wengi utapoa, habari njema ya ufalme itahubiriwa katika mataifa yote n.k.

Na karibu na pale mwisho kabisa akawaambia maneno haya kwa kuwakumbusha kilichotokea nyuma:

Mathayo 24:32 “Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;

33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.

34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia.

35 Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

Sasa embu tafakari vizuri tena kwa ukaribu pale anaposema, “tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;”…Kumbe alijua mtini unapofikia hatua ya kuchipua, na matawi yake kuonekana basi wakati wake wa mavuno unakuwa upo karibu sana…Kumbe alilitambua hilo hata kwa ule mtini wa kwanza alioulaani, kwasababu ule ulikuwa katika hatua hiyo hiyo ya majani, lakini aliulaani usifikie hatua ya kufikia mavuno kwa haraka,, bali wa muda mrefu sana mbeleni alioufananisha na milele..

Inafunua nini?

Hii dunia ungekuta imeshakwisha tangu zamani za mitume, lakini Bwana YESU aliuvuta muda wa mavuno mbele ili zile dalili za mwisho wa dunia zisionekane kwa kipindi kile walichokuwa wanaishi…aliyakawiisha mavuno kwa mfano wa ule mtini alivyoukawiisha.

Kwasababu kumbuka MTINI huwa unapitia hatua kuu tatu,.. ya kwanza kupukutisha majani yake yote, ya pili ni kuchipua majani, na ya tatu ni kuzaa matunda…Sasa ile hatua ya kupukitisha, huwa unapukutisha majani yake kweli kweli na kuwa kama kijiti kikavu kilichonyauka… soma..

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi”.

Unaona hapo? Biblia inatoa picha jinsi nyota za mbinguni zitakavyoanguka katika siku za mwisho mfano wa mtini unavyopukutisha mapooza (majani makavu) yake.

Sasa kwasababu Bwana Yesu aliukawiisha wakati wa mavuno ndio tunaweza kuona tangu kipindi kile cha mitume hadi zaidi ya miaka elfu mbeleni,..hakukuwa na dalili za wazi zinazothibitisha kuwa mwisho upo karibu, kwa yale aliyoyazungumza katika Mathayo 24 kwamba manabii wa uongo watatokea, taifa kuondoka kwenda kupigana na taifa hayo hayakuwepo,… lakini tunaona kuanzia karne ya 20 yaani kuanzia mwaka 1900, mambo hayo yalianza kuonekana kwa kasi, vita kuu mbili za dunia zimepiganwa kwa mpigo ndani yah ii karne.., magonjwa ya kutisha ambayo hayakuwepo enzi za nyuma, yameonekana kwa kasi kuanzia karne ya 20, magonjwa ya ajabu yamezuka na bado yanaendelea kuzuka, kansa, ukimwi, ebola, zika, n.k…

Dalili zote zimetia:

Na dalili zile alizozingumzia pale zimeendelea kutimia kwa kasi, hadi sasa, mambo yote yameshatimia hususani katika hii karne ya 21 tuliyopo sasahivi.. karibu yote yameshatimia..

Hapo ndipo tunapojua sasa, wakati wa mavuno umeshafika..Ule mtini wa mwisho wa dunia umeshafikia hatua ya mavuno yake, matawi yake tunayaona…Wimbi kubwa la manabii wa uongo tunaloliona leo hii ungemweleza mtu wa mwaka wa 1980, angekushangaa na kusema hicho kitu hakiwezekani,.. lakini tazama hali ilivyo sasa, sodoma iliyopo sasa hivi duniani, ni zaidi ya ile ya Gomora..pornography mitandaoni, watu wanafanya uasherati na wanyama, simu za mikononi zimekuwa shimo refu la kuelekezea watu kuzimu n.k..Hii yote ni kutuonyesha kuwa Mtini umeshachipua..

Sasa Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake..mnyaonapo hayo CHANGAMKENI, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”..(Luka 21:28)

Unyakuo wakati wowote utapita. Wale waliookolewa wanapaswa wafurahie kwasababu siku yoyote tutakuwa utukufuni, Lakini wewe ambaye upo dhambini Je! Wewe ambaye unautazama ulimwengu utakuwa wapi?… Mkimbilie Kristo ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, acha kupoteza muda, ulimwengu haukujali kama unavyofikiria wewe…Tubu dhambi zako mgeukie Mungu, naye atakupokea, na kukupa Roho wake Makatifu bure,..Unasubiri nini?.

Fanya hivyo sasa hapo uliopo piga magoti utubu, na yeye anakusikia na yupo tayari kukusamehe bure bila gharama yoyote.., kisha baada ya hapo anza kutafuta ushirika na wakristo wenzako, tupa kila nguo mbaya yoyote uliyokuwa unavaa, vimini, suruali, ma-lipstik, acha matendo yote mabaya uliyokuwa unafanya..ili kumthibitishia Mungu kweli umeamua kutubu na kumgeukia yeye..Na yeye akishaona Imani yako na Nia yako kweli umeamua kugeuka…Hiyo tayari ni sababu tosha ya yeye kukupa Roho wake Mtakatifu… atakuvika uwezo wa ajabu ambao utakusaidia kuviondoa vile vilivyosalia..

Fanya hivyo na Bwana atakubariki..Kumbuka tena.. Tunaishi katika majira ya kuchipuka kwa mtini, hivyo mavuno yapo karibu ..

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Shalom.

Mada Nyinginezo:

USISIKILIZE DHIHAKA ZA SHETANI, ZITAKUKWAMISHA.

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

HATUTAACHA KUJIFUNZA NENO KILA INAPOITWA LEO.

YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.

Rudi Nyumbani:

Print this post