Habari za Balaamu tunazipata katika agano la kale kitabu cha Hesabu 22. Tunasoma kuwa wakati wana wa Israeli wakiwa jangwani katika safari yao ya kuelekea nchi ya ahadi walikutana na wana wa Moabu njiani, na walipotaka kukatiza katika nchi yao mfalme wao aliyeitwa Balaki aliwazuia. Na zaidi ya yote akaenda kumwajiri Balaamu nabii wa uongo ili awalaani wana wa Israeli (Kuwaloga) wasifanikiwe katika safari yao. Hivyo Bwana alimzuia Balaamu mara tatu asiwalaani, na kinyume chake akawabariki. Lakini haikuishia hapo Balaamu yule nabii wa uongo kwa kupenda fedha ya udhalimu, kutoka kwa mfalme Balaki alitafuta njia mbadala ya kuwakosesha wana wa Israeli. Ndipo akamshauri Balaki afanye karamu na kuwaalika wanaume wa Israeli ili wafanye uzinzi na wanawake wa kimoabu na kutoa sadaka kwa miungu yao, ili iwe ukwazo kwao kwa Mungu wa Israeli na Mungu awaadhibu. Hivyo njama yake kweli ilifanikiwa, na hasira ya Mungu ikawaka juu ya Israeli, nao wakaadhibiwa kuzungumzia suala hilo. Na ndipo wote wakafikia muafaka wa kuundwa Dini moja ya ulimwengu mzima (Kanisa Katoliki). Kumbuka tafsiri ya Neno Katoliki ni “ulimwengu wote” hivyo kanisa Katoliki maana yake ni “Kanisa la ulimwengu wote”.. Sasa kuanzia hapo ule ukristo ambao ulikuwa haujachanganyikana na mafundisho yoyote ya uongo, ukafa na kuzaliwa ukristo mpya bandia ambao umechukuliwa na desturi za kipagani za Rumi mfano wa kuabudu miungu mingi, na ndio hapo vitu kama ubatizo wa vichanga ukazaliwa, ubatizo wa kunyinyuziwa ukaundwa, ibada za sanamu,kusali rozari na za kuomba kwa watakatifu waliokufa zamani mambo ambayo huwezi kuyaona katika maandiko matakatifu au kufanywa na mitume wa zamani,pamoja na ibada za miungu mitatu, Ambazo utazikuta kwenye desturi za kirumi.