Title March 2020

MAFUNDISHO YA NDOA.

Mafundisho ya ndoa, na mahusiano.


Ikiwa wewe ndio kwanza unataka kuingia katika mahusiano Yapo mambo kadha wa kadha unahitaji kufahamu.

Jambo la kwanza:

ni lazima ujue njia sahihi ya kumpata mwenza wako, vilevile ujue wakati sahihi wa kumchagua huyo mwenza unayemtaka..

Hapa ndipo watu wengi wanapokosea, wakidhani ni yule tu anayevutia machoni huyo ndiye anayefaa, au ni ule wakati tu wanapojisikia kuoa au kuolewa ndio wanapopaswa waingie katika mahusiano. Ukitumia kanuni hiyo upo hatarini sana  kujutia huko mbeleni..Ni sharti kwanza utulize akili yako bila kuruhusu hisia zako kukuongoza..

Ili kufahamu kwa urefu njia sahihi ya kumpata Mwenza wa Maisha Bofya hapa >>NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

Jambo la Pili:

Unahitaji kufahamu Mambo ya kuepukana nayo wakati mpo katika mahusiano ya uchumba. Watu wengi wanadhani ukishamchumbia binti, basi tayari mpo huru kufanya naye tendo la ndoa wakati wowote..Usijaribu kufanya hivyo kwasababu yapo madhara mengi na makubwa ya ndani na ya nje,.Kwanza Licha ya kuwa unafanya uasherati, ambao hata ukifa utakwenda jehanum, Lakini pia unapoteza baraka zote ambazo Mungu alikuwa ameshakuandalia kwa ajili ya ndoa yako inayokuja.. yapo madhara mengine pia,

Ili kufahamu zaidi madhara hayo na jinsi ya kujiepusha nayo bofya hapa >>JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Jambo la Tatu:

Ili ndoa yako iwe ni ya heri na mafanikio, na yenye kupokea baraka kamili kutoka kwa Mungu, Ni lazima ndoa hiyo  iwe imefungishwa na Mungu mwenyewe..Nikisema Mungu namaanisha KANISANI.

Wapo watu wanaosema, mimi nimefunga ndoa yangu kimila, wengine wanasema tumefunga kiserikalini, N.k., Haijalishi hizo zote utaziita ni ndoa, Lakini hizo sio ndoa za kikristo zinazostahili baraka zote za Kristo.

Ili kufahamu faida na madhara ya kutokufungika ndoa kanisani bofya hapa >> NDOA NA HARUSI TAKATIFU.


Sasa ikiwa wewe tayari umeshaingia kwenye ndoa, na umekidhi hivyo vigezo vyote hapo juu.

Basi yapo pia mambo kadhaa unahitaji kujua. Nimekutana na watu wengi wenye matatizo katika ndoa zao. Husasani wanawake, wengine wameachwa na waume zao, wengine wametelekezwa, wengine wao ndio wanamatatizo n.k.k

lakini zipo siri ambazo bado hawajazijua za mafaniko ya ndoa zao ambazo biblia imeziweka wazi..

Kwamfano Ukimtazama Ruthu, yule hakuwa mwanamke wa Kiyahudi kama wengine tuonaowasoma kwenye biblia, lakini jiulize ni kwanini hadi leo hii unamsoma katika maandiko matakatifu,vilevile ni kwanini uzao wake ulibarikiwa kuliko hata uzao wa wanawake wengine waliokuwa wazao wa kiyahudi,? kiasi kwamba mpaka mfalme Daudi, alipitishwa  katika uzao wake,na sio tu wa Daudi bali pia wa Bwana wetu Yesu Kristo kwa kupitia Yusufu?..

Kama hujafahamu bado siri ni nini , leo nataka nikupe, siri ipo kwa MKWEWE, NAOMI..Hivyo Ili na wewe mwanamke ubarikiwe uzao wako, na uwe na jina kubwa basi siri yako ipo kwa wakwe zako, hilo haliepukiki..

Ili kufahamu Zaidi habari hizo bofya hapa..>>EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

Vilevile unahitaji kumfahamu mwanamke mwengine anayejulikana  kama ESTA.. Cha ajabu Esta na Ruthu ni wanawake wawili pekee ambao wanavitabu vyao maalumu vinavyojitegemea katika biblia nzima..Lakini cha kushangaza Zaidi ni kuwa wanawake wengi hawajua siri zilizo ndani ya wanawake hawa. Wanakimbilia kusoma habari za  wanaume, kama wakina Daudi, na Eliya, na Samweli, lakini wanaacha mafundisho ya msingi yanayowahusu kutoka habari za wanawake wenzao kama hawa..

Kama ulikuwa hujui Esta, mpaka amekuwa malkia ni kwasababu kulikuwa na mwanamke mwingine ambaye alikosa heshima kwa mume wake ambaye ni Mfalme, na hiyo yote ni kutokana na uzuri aliokuwa nao,..

Hivyo Baada ya mfalme kukiona kiburi chake ndipo akamtoa katika nafasi ya umalkia, na baadaye Esta akapata kibali cha kuchukua nafasi yake, ukisoma pale utaona Esta naye kilichomfanya awe malkia hakikuwa kigezo cha uzuri wake kama wengi wanavyodhani, au elimu yake, au umaarufu wake, hapana, bali kutoka kwa Hegai msimamizi wa mfalme…ambapo kuna  siri kubwa sana hapo unapaswa uifahamu pia wewe kama mwanamke..

kwa maelezo marefu bofya hapa>> ESTA: Mlango wa 1 & 2

Vivyo hivyo na wewe mwanamke, kudhani kuwa uzuri wako, au elimu yako, au fedha zako, ndio zinaweza kukufanya usimuheshimu mume wako, ukweli ni kwamba ndoa yako haitadumu, na atakayeilaani sio mume wako. Bali ni Mungu mwenyewe kwasababu umekosa kufuata kanuni za kimaandiko Mungu alizoziweka juu ya ndoa ya kikristo.

Waefeso 5:24  “Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo”

Vilevile, kama mwanamke unapaswa ujue nafasi yako katika familia, na katika kanisa la Kristo ni ipi…

Tumezoea kuona nyaraka nyingi zilizoandikwa na mitume zikielekezwa kwa makanisa au wanaume kama vile Timotheo, au Tito, au Filemoni, lakini Upo waraka mmoja mtume Yohana aliuandika kwa mama mmoja mteule..Ambao hata wewe mwanamke ukiujua ufunuo wake  utajifunza nafasi yako katika kanisa la Mungu na  uleaji wako wa Watoto.

Bofya hapa ili kufahamu zaidi >> MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

Vilevile na wewe  kama MWANAUME (Baba), ni lazima ufahamu nafasi yako pia katika Familia..

Jambo moja kwako ni hili  Bwana Yesu alisema..

Waefeso 5:25  “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;

26  ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;

27  apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

28  Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.

29  Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.

30  Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake.

31  Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.

32  Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa.

33  Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe”

Ukimpenda mke wako, utamuhudumia, kwa chakula, kwa malazi, na makazi, ukimpenda mke wako utamtunza kwa mavazi, ukimpenda mke wako utawapenda na ndugu zake..Ukimpenda mke wako, utawapenda na Watoto wake, na hivyo utawatimizia majukumu yote ya nyumbani..

Lakini ukikosa akili kama Nabali alivyokuwa, Unakuwa mlevi, hujali wageni, huwi mkarimu, humchi Mungu, wala hutimizii familia yako mahitaji yake, wewe ni pombe tu, Ujue kuwa Mungu atakuuwa mwenyewe kabla ya wakati wako kama alivyomuua Nabali, na Mke wako mwenye akili ataenda kuolewa na mtu mwingine mwenye akili zaidi yako wee na atakayemjali kuliko wewe..kama ilivyokuwa kwa Abigaili mke wa Nabali.. (Soma 1Samweli 25 )

Sasa kwanini hayo yote yakukute?

Hivyo wote wawili mkizingatia kanuni hizo kila mmoja katika nafasi yake, basi muwe na uhakika kuwa Bwana ataifanya ndoa yenu kuwa ya amani siku zote, yenye mafanikio, na yenye matunda kwa Mungu.

Lakini Mwisho kabisa..

Kila mmoja analojukumu lake binafsi la kumtafuta Bwana, na kumpenda Bwana kuliko kitu kingine chochote. Kwasababu Biblia inasema, wakati tuliobakiwa nao ni mfupi..

1Wakorintho 7:29  “Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana”

Hizi ni nyakati za mwisho ambazo, biblia inatushauri tujikite Zaidi katika kuutafuta ufalme wa Mbinguni, kwasababu unyakuo upo karibu. Hivyo japokuwa utakuwa katika ndoa lakini usijiingize sana, au kwa namna nyingine usizamishwe sana katika mambo ya kifamilia mpaka ukasahau kuwa kuna wokovu na Unyakuo..Kwasababu hata huyo uliye naye, Akifa leo anaweza kuwa wa mwingine..Na Zaidi ya yote kule juu mbinguni tuendapo hakutakuwa na kuoa au kuolewa, Hivyo masuala ya ndoa si masuala ya kuyapa kipaumbele sana ziadi ya yale ya ufalme wa mbinguni..Lakini yape kipaumbele Zaidi ya mambo mengine ya kidunia.

Bwana akubariki sana.


Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Mahusiano ya uchumba, ni tofuati na mahusiano ya kimapenzi. Yapo mahusiano ya uchumba ambayo mtu anakuwa nayo kwa mtu aliyemchumbia, hilo halina tatizo maadamu halihusanishwi na vitendo vyovyote vya zinaa. Watu hao wawili wanaweza wakakutana wakala pamoja, wakazungumza pamoja, wakafurahi pamoja, wakatembeleana nyumbani kwao, wakaweka mpingano pamoja..lakini si kulala, pamoja, au kukaribiana kimapenzi au kuonyesha dalili zozote za kukaribiana kihisia, ..

Lakini wapo watu wanaosema, huyu tayari kashakuwa mke wangu, hivyo hakuna shida, sasa nikifanya naye tendo la ndoa si tayari kashakuwa wangu nitamuoa tu?..

Lakini kabla hujafikiria kuwaza hivyo, embu jaribu kuwaza kwanza ni kwa nini lile tendo linaitwa Tendo la Ndoa?..Ulishawahi kujiuliza hivyo?.Linaitwa hivyo kwasababu ni tendo linalofanywa na wanandoa tu peke yao..Nje ya hapo haijalishi unampenda sana huyo mwenzako au unamalengo naye makubwa kiasi gani au kwamba atakuja kuwa mke wako baadaye au mume wako, haijalishi huo  tayari ni uasherati..Na waasherati wote Mungu atawahukumu.

Kama ingekuwa ni rahisi hivyo tu, hata mtu anayekutana na kahaba barabarani na kwenda kufanya naye uasherati basi na yeye angejitetea na kusema siku moja nitakuja kumuoa wacha nifanye nae kwanza..Unaona? Hilo jambo halimfanyi yeye kutokuwa muasherati…Tendo la ndoa linalofanywa kwa watu ambao sio wanandoa ni dhambi.

Waebrania 13.:4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.

Hivyo ikiwa wewe umempenda binti, na umeshamchumbia, ili ndoa yako ikubaliwe na Mungu..Subiri mpaka wakati Mungu atakapokuunganisha naye rasmi mbele ya Kanisa la Kristo. Na ni kwanini iwe ni katika kanisa la Kristo na si penginepo. Ni kwasababu Mungu unayetaka awaunganishe ndipo alipo. Wapo wengine wanafungishwa ndoa za kimila, au za kiserikali n.k…Unaweza kuziita ni ndoa lakini hizo zote Sio ndoa za kikristo..Ambazo zinaweza kupokea Baraka za Kristo mwenyewe.

Kwasababu kabla ndoa haijaitwa ndoa ni lazima kuwe na makubaliano na mapatano na maagano fulani, sasa kama ukifungishwa nje ya Kristo, hapo ndipo utakutana na nyingine zinaruhusu kuolewa au kuoa mke zaidi ya mmoja, nyingine zinaruhusu kuachana wakati wowote mnapochokana, nyingine ni lazima mtambike, n.k. mambo ambayo yanakinzana kabisa na mpango wa Kristo.

Hivyo ndugu/Dada,..Ndoa yako ikipitia hatua sahihi Kristo anazozihitaji. Basi ujue zipo Baraka tele za kindoa ambazo Mungu ataziachilia kwako na kwa uzao wako baadaye ikiwemo ndoa yenu kupokea ulinzi wa kiMungu tangu huo wakati. Lakini ukiwa na haraka na kuvuruga mipango, na kukimbilia kufanya jambo ambalo wakati wake haujafika, ujue kwa hakika kabisa Mungu hayupo na wewe, na hata ndoa yako hataibarikiwa…Na jaribu kuangalia utaona wengi wa wanaofanya hivyo, mwisho wa siku hawaoani, au wanazaa, na baadaye wanaachana, na watoto wanabakia kuwa na mazazi mmoja,.Hiyo yote ni matokeo ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa.

Hivyo ikiwa leo hii upo katika mahusiano ya kimapenzi(ngono) na mwenza wako, mpaka mmeshafikia hatua ya kuzaa, acha mara moja, mkatubu dhambi zenu wote wawili, kwa kumaanisha kabisa kisha muanze utaratibu wa kwenda kufungishwa ndoa yetu kanisani..Na hapo ndipo Bwana atakapowatazama na kuwaangazia rehema zake…Lakini vinginevyo ukiendelea kufanya hivyo ujue kuwa wewe ni mwasherati mbele za Mungu.

1Wakorintho 6:9  “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Fanya hivyo Na Bwana atakubariki.

Mada Nyinginezo:

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

CHAPA YA MNYAMA

 

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Kifo cha mtakatifu perpetua na felista kimebeba ujumbe gani kwetu?

Perpetua alizaliwa huko Tunis (Mji mkuu wa Tunisia) Afrika ya Kaskazini mwaka unaokadiriwa kuwa wa 182, alizaliwa katika familia ya kitajiri, yenye kuheshimika sana, baba yake alikuwa ni mpagani, lakini Perpetua aliupokea Ukristo na kuwa mfuasi kamili wa Kristo, japo historia haionyeshi ni kipindi gani aligeuzwa kuwa mkristo..Lakini ilifika wakati mfalme wa Kirumi aliyeitwa Septimius Severus…Alipiga marufuku ukristo katika majimbo ya Afrika kaskazini, kwamba mtu yoyote asijihusishe na imani yoyote ya kikristo au ya kiyahudi..Wakati huo Perpetua alikuwa anaishi na mume wake, pamoja na kijakazi wake aliyeitwa Felista, na katoto chake kachanga alichokuwa bado anakinyonyesha wakati huo ..

Sasa wakati agizo hilo linatolewa Perpetua alikuwa katika mafundisho ya kuelekea kubatizwa, lakini alibatizwa kabla ya kupelekwa gerezani..Ndipo baadaye yeye pamoja na wenzake wanne, wote walikamatwa na kupelekwa gerezani.

Baba yake kusikia vile, alikwenda moja kwa moja mpaka gerezani kumtazama binti yake ili kutafuta njia ya kumtoa, ndipo akamshauri Perpetua aukane ukristo, atoke gerezani aendelee na maisha yake ya kawaida..

Lakini Perpetua alimwambia Baba yake maneno haya.. “Baba unakiona hichi chungu hapa?”

Akasema ndio,

Je kinaweza kuitwa jina lingine tofauti na vile kilivyo?

Akasema, hapana!

Basi hata mimi siwezi kuitwa jina lingine tofuati na mimi nilivyo..Mkristo.

Ilipofika Siku ya pili Perpetua, alihamishwa gereza alilokuwepo na kupelekwa gereza lingine zuri zaidi ili aweze kumnyonyesha mtoto wake…Lakini baba yake hakukata tamaa alimfuata tena siku nyingine, lakini safari hii alikuja kwa kumbembeleza sana.

Akimwambia…Nihurumie mwanangu!, nihurumie mwanangu!, ikiwa ninastahili kweli kuitwa baba yako, ikiwa nimekupenda zaidi hata ya kaka zako, ikiwa nimekulea mpaka umefikia hatua hii ya heshima..basi nihurumie mimi baba yako..kubali kukataa tu wewe sio mkristo.

Akamdondokea, mpaka magotini akambusu mikono yake..akamwambia, mwanangu usiniache nikapata aibu kama hii katikati ya watu. Fikiri juu ya kaka zako, fikiri juu ya mama yako, fikiri juu ya shangazi zako, fikiri hata juu ya huyu mtoto wako mchanga ambaye hataweza kuishi pindi utakapokufa..Ghairi hayo maamuzi yako magumu!, uendelee na maisha yako ya kawaida.

Perpetua alizidi kuwa imara na msimamo yake akamtia moyo baba yake..Akaendelea kukaa kule kule gerezani.

Na Siku ya kuhojiwa ilipofika Perpetua na wenzake walipandishwa kizimbani mbele ya gavana, Na wenzake walipoulizwa kwanza juu ya msimamo wao walikiri kuwa wao ni wakristo, na wote wakakataa ibada za mfalme. Swali likageuzwa kwa Perpetua, naye akaulizwa na Gavana kuhusu msimamo wake.

Wakati huo baba yake alikuwa hapo karibu, amembeba mtoto wake yule, akamwambia, kubali ibada za mfalme, achana na hiyo imani yako, mwonee huruma mtoto wako.

Lakini Perpetua akasema mbele ya wote..Siwezi kufanya hivyo!!

Gavana akamuuliza, kwahiyo wewe ni mkristo.

Ndio! Perpetua alijibu..

Baba yake akaingilia kati akimlazimisha Pepertua aikane imani, lakini Hawakuwa na muda tena, wakamchukua yeye na wenzake wakawapeleka katika viwanja vya michezo (Arena) ili wauawe. Kufika kule kuliwa na wanyama wakali ambao tayari wameshaandaliwa, ambapo wanyama kama chui, dubu walikuwa wanaachiliwa kwa wanaume, na nyati kwa wanawake..wakamtupa Perpetua na yeye pamoja na wenzake, na kijakazi wake Felista ambaye kwa wakati huo alikuwa ni mjamzito naye..

Akaachiliwa nyati, akamchota Perpetua juu, wakati akiwa chini akaende kumsaidia kijakazi wake Felista, huku wote wamelowa damu..Wakaona haitaoshi wakawaleta kwa wauaji wa kirumi katika ma-arena hayo ili wauliwe kwa upanga..

Perpetua alikufa mwaka wa 203 akiwa bado mama mdogo mwenye umri wa miaka 22, hakuona ujana wake kuwa ni kitu kuliko Kristo, hakuona heshima yake ya kitajiri kuwa ni kitu kuliko Kristo, wala hakuhesabu kuikana imani kisa baba, au mama au mtoto wake.. Bali aliisimamia imani hadi dakika ya mwisho..

Biblia inatuambia..

Waebrania 11:35 “…..Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;

36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;

37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga;

Swali la kujiuliza kwetu sisi hususani kwako wewe mwanamke kutokana na mada hii:

Je unauthamini wokovu wako vipi?..Unasema umeokoka lakini kuacha kuvaa vimini na masuruali na manguo ya utupu, unaona ni vigumu, unajiona wewe ni kijana, Perpetua pengine alikuwa ni kijana Zaidi yako, tena aliyezaliwa katika nyumba ya kitukufu ya kitajiri pengine kuliko wewe, lakini hakuudosha utakatifu wake.

Kila tusomapo habari kama hizi tusiishie tu kuzisoma kama hadithi bali tufahamu kuwa..tunahimizwa na sisi pia tupige mbio kama hao, na kutupa kila mzigo wa dhambi unaotulemea na kutuzungika kwa upesi, kwasababu hawa ndio watakaotuhuku siku ile mbele za Bwana..kuwa walikuwa wazuri kushinda sisi lakini hawakuikana imani, walikuwa katika hatari kubwa kuliko sisi lakini hawakuupuuzia wokovu, walikuwa ni matajiri kuliko sisi lakini hawakusema utajiri wangu ni kizuizi nisikane nafsi..Walikuwa ni wajawazito, na wenye watoto wachanga, lakini hawakuthamini hicho zaidi ya wokovu wao..wewe na mimi tutajibu nini mbele za Bwana siku ile? Au tunafikiri watu hao walikuwa hawasikii maumivu, au walikuwa wana roho sana..hapana, ni walikana tu!..Biblia inasema hata Eliya hakuwa mtu wa ajabu sana, alikuwa ni mtu mwenye tabia sawa na sisi, lakini walijikana kwa gharama zote.

Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?

BONDE LA KUKATA MANENO.

Yeremia 33:3 (NIITE NAMI NITAKUITIKIA)

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUPATA MAONO YA MBINGUNI SIO KUFIKA MBINGUNI.

Kupata maono ya mbinguni sio kufika mbinguni…ndio mwanzo wa safari.

Bwana anatupenda, na wakati mwingine anawachukua baadhi ya watu (sio wote) ili kuwaonyesha mambo yaliyopo kule nyumbani, juu kwa baba yetu.

Anawapeleka kuwaonyesha mambo mazuri aliyowaandalia wanawe, anawaonyesha makazi yao ya kuduma yasiyoharibika na hazina zinazowangoja kule nga’mbo ikiwa watashinda..Anawaonyesha utajiri aliowaandalia na heshima na utukufu..anawaonyesha ni kwa jinsi gani mbingu inavyowatamani na ilivyojiandaa vya kutosha kuwalaki…na mambo mengine mengi ambayo hata hayaelezeki.

Ni mfano tu wa Wana wa Israeli baada ya kutolewa nchi ya Misri na kufikishwa kule jangwani..ambapo maili chache kabla kufika nchi ya Ahadi…Mungu aliwatuma wakaipeleleze nchi ya ile waliyoahidiwa, na aliruhusu waende watu wachache sana(yaani watu 12 tu) ndio walioteuliwa kwenda kuipeleleza…Na walifika kweli Kaanani na kuipeleleza walirudi kila mtu na jibu lake…lakini wote walikubaliana na jambo moja  kuwa nchi ile ilikuwa ni njema sana na imejaa unono na maziwa na asali, na baraka tele na kweli ni nchi yenye urithi mzuri usioelezeka.

Hesabu 13:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,

 2 Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.

3 Basi Musa akawatuma kutoka nyika ya Parani kama alivyoagizwa na Bwana; wote walikuwa ni watu walio vichwa vya wana wa Israeli……..

17 Musa akawapeleka ili waipeleleze nchi ya Kanaani, akawaambia, Pandeni sasa katika Negebu mkapande milimani,

18 mkaitazame nchi ni ya namna gani; na watu wanaokaa ndani yake, kwamba ni hodari au dhaifu, kwamba ni wachache au wengi;

 19 na nchi wanayoikaa kwamba ni njema au mbaya; kwamba wanakaa katika matuo au katika ngome;

 20 nayo nchi ni ya namna gani, kwamba ni nchi ya unono au ya njaa, kwamba ina msitu au sivyo. Iweni na moyo mkuu, mkayalete matunda ya nchi. Basi wakati ule ulikuwa wakati wa kuiva zabibu za kwanza.

21 Basi wakapanda wakaipeleleza nchi toka jangwa la Sini hata Rehobu, mpaka kuingia Hamathi.

22 Wakapanda katika Negebu, wakafika Hebroni; na Ahimani, na Sheshai, na Talmai, wana wa Anaki, walikuwako huko. Nao Hebroni ulijengwa miaka saba kabla ya Soani wa Misri.

 23 Wakafika bonde la Eshkoli, na huko wakakata tawi lenye kishada kimoja cha zabibu, wakalichukua kwa mti kati ya watu wawili; wakaleta makomamanga pia, na tini.

24 Bonde lile liliitwa bonde la Eshkoli kwa sababu ya hicho kishada walichokata huko wana wa Israeli.

25 Wakarejea baada ya kuipeleleza nchi, mwisho wa siku arobaini.

 26 Wakaenda wakafika kwa Musa, na kwa Haruni, na kwa mkutano wote wa wana wa Israeli, katika jangwa la Parani, huko Kadeshi; wakawaletea habari, wao na mkutano wote, wakawaonyesha matunda ya nchi.

27 Wakamwambia wakasema, TULIFIKA NCHI ILE ULIYOTUTUMA, NA HAKIKA YAKE, NI NCHI YENYE WINGI WA MAZIWA NA ASALI, NA HAYA NDIYO MATUNDA YAKE”.

Watu hawa ni kweli walifika katika ile nchi…lakini sio kwamba kwasababu wamefika basi ndio hawana haja ya kurudi tena kwa wenzao…Muda wa wao kufika kule ulikuwa bado…walikwenda tu kuonyeshwa nafasi zao kule…Lakini bado walikuwa hawajaiteka ile nchi, walipaswa warudi kwanza wakapange vita wapambane wayaondoshe yale majitu yaliyoshikilia urithi wao katika nchi ya Ahadi ambayo wameahidiwa, wakishawaangusha ndipo waimiliki…

Ndio maana Bwana Yesu alisema katika..

 Mathayo 11:12 “ Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”

Shetani sasa kashikilia nafasi zetu katika ulimwengu wa roho, tunapaswa tumwangushe chini kabla ya kufika nga’mbo, na vita tunapambana hapa hapa duniani…tutakapomwangusha chini ndipo tutazirithi baraka zetu….(na tunamwangusha chini kwa kuishi Maisha matakatifu na makamilifu ya Neno la Mungu, yanayompendeza yeye),….hatuna budi kupambana vita hapa…kusikia tu mbinguni ni kuzuri tumeandaliwa hiki na kile haimaanishi kwamba ndio tayari tumekwishafika…bado kuna vita vya kupambana kumwangusha shetani katika Maisha yetu..

Shetani hataki tuende mbinguni kabisa, hataki hata kidogo kwasababu anajua uzuri tutakaoukuta kule, … anapambana sana kuhakikisha hatufiki kule, kama alivyopambana na wana wa Israeli kuhakikisha hawafiki nchi ya Ahadi, au hata wakifika basi watafika wachache sana na kwa shida sana..Hebu tafakari katika ule umati wote waliotoka Misri Zaidi ya watu milioni 2 waliofanikiwa kuingia nchi ya Ahadi walikuwa ni watu wawili tu (2)! Na iliwachukua miaka 40 kuingia tu ile nchi ambayo ni maili chache tu, safari ya mwezi mmoja tu. Alikuwa ananyanyua kila aina ya vikwazo walipokuwa njiani..aliwatumia mpaka manabii wa uongo kuwaangusha wana wa Israeli walipokuwa njiani.

Na sisi ni hivyo hivyo…mbinguni hatuendi kwa miguu kama wana wa Israeli walivyokwenda Kaanani, kama tutaishi Maisha ya kutoujali wokovu kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokuwa, tutaangamizwa na hatutaurithi ufalme wa mbinguni, kama tukikubali maneno ya manabii wa uongo kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokubali kuyasikiliza maneno ya akina Kora na Balaamu basi na sisi hatutairithi nchi.

Kama hatutamheshimu Mungu kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokosa kumheshimu Mungu wakiwa safarini basi haijaishi tumeikaribia mbinguni  kiasi gani hatutairithi.. Kama tutakata tamaa na kutoamini kwamba tunaweza kufika mbinguni basi hatutafika kweli kama wale watu ambao baada ya kwenda kanaani kuipeleleza walileta ripoti za kuwaogopesha watu, na wote walikufa..

1Wakorintho 10:5  Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.

6 BASI MAMBO HAYO YALIKUWA MIFANO KWETU, KUSUDI SISI TUSIWE WATU WA KUTAMANI MABAYA, KAMA WALE NAO WALIVYOTAMANI.

7  Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.

8  Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.

9  Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

10  Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.

11  Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

12  Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Biblia inasema..

Ufunuo 21:7  “Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

8  Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”

Ufunuo 21:27  “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”

Mpe leo Yesu Maisha yako kama hujampa. Na pia jikane nafsi yako, jitwike na msalaba wako mfuate Yesu kama ulikuwa hujafanya hivyo..Safari yetu karibia inafika ukingoni, na shetani ndivyo anavyozidi kuongeza jitihada kuwapunguzia watu kasi ya kuingia uzimani..

Kumbuka mtume Paulo alichokisema, aliponyakuliwa kule juu na kuonyeshwa mambo ambayo hayatamkiki, Hiyo ni kuonyesha ni kwa jinsi yalivyo ya ajabu na ya kushangaza kiasi kwamba hata lugha haziwezi kuelezea, (2Wakorintho 12:4)..sasa unasubiri nini..Kimbilia kwa YESU ayaokoe maisha yako.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

RABI, UNAKAA WAPI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

TUNA WAJIBU WA KUOMBEA MAHALI TULIPO.

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.

HISTORIA YA ISRAELI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.

Livunjeni hekalu hili nami katika siku tatu nitalisimamisha..

Mara nyingine Bwana Yesu alipotaka kufikisha ujumbe Fulani, alikuwa anatumia mfano wa mahali husika ili kuchanganya mada mbili kwa wakati mmoja …Kwamfano utaona wakati ule mitume wa Bwana Yesu waliposahau kuchukua ile mkate ambayo ilibaki wakaanza kugombana wao kwa wao kwa kulaumiana kwanini hawakuibeba, …lakini Bwana Yesu alipowasikia, mabishanao yao alitumia mfano mwingine kuzungumza nao kana kwamba alikuwa hamaanisha hicho walichokuwa wanakibishania kwa wakati huo..

Marko 8:13 “Akawaacha, akapanda tena chomboni, akaenda zake hata ng’ambo.

14 Wakasahau kuchukua mikate, wala chomboni hawana ila mkate mmoja tu.

15 Akawaagiza, akasema, Angalieni, jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.

16 Wakabishana wao kwa wao, kwa kuwa hawana mikate.

17 Naye Yesu akatambua, akawaambia, Mbona mnabishana kwa sababu hamna mikate? Hamfahamu bado, wala hamjaelewa? Je! Mioyo yenu ni mizito?

18 Mna macho, hamwoni; mna masikio, hamsikii? Wala hamkumbuki?

19 Nilipoivunja ile mikate mitano na kuwapa wale elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vimejaa vipande? Wakamwambia, Kumi na viwili.

20 Na ile saba kuwapa wale elfu nne, mlichukua makanda mangapi yamejaa vipande? Wakamwambia, Saba.

21 Akawaambia, Hamjafahamu bado?”

Unaona hapo? Bwana Yesu alitumia mfano wa chachu, na kusema, jilindeni na chachu ya mafarisayo…Lakini mitume wakadhani anazungumzia chachu ya mikate ya mafarisayo, hiyo ikiwafanya wazidi kugombana zaidi ili apate kuwanasa vizuri,..Hapo ndipo Bwana akapata nafasi ya kuwakemea kwa kukosa kwao ufahamu, akawaambia hamjafahamu bado?, mimi sizungumzii habari za mikate, mmesahau ni mikate mingapi mlikusanya kama masalia wakati ule?, hamjafahamu bado, hamjaelewa, mioyo yenu ni mizito, hamna imani kwa Mungu bado kuwa hata sasa anaweza kuwafanyia muujiza kama ule ule wa mikate mengine mkala mkashiba, pasipo kuwa na chochote?…lakini bado mnamtilia shaka Mungu?…Mimi sizungumzii habari za mikate ninaachomaanisha ni jilindeni na mafundisho ya mafarisayo..

Sasa utaona hapo mitume walipata mafundisho mawili, la kwanza ni kutokana na kile walichokuwa wanakifiria juu ya tumbo, kuwa Mungu bado anaweza kuwahudumia hata kama kunaonekana hakuna mlango wa kupata chakula, na cha pili ni kuhusu mafundisho ya mafarisayo (ambayo yanafananishwa na chachu/hamira) ambayo kazi yake ni kuumua na kupindua uhalisia wa Neno la Mungu…Lakini waliupata ule ujumbe uliokuwa unawahusu kwa wakati wao.

Ndivyo hivyo hata wakati ule Bwana Yesu alipokwenda hekaluni, akaona jinsi watu walivyoweka tumaini lao lote katika lile hekalu, jinsi lilivyokuwa limepambwa kwa namna ya ajabu, jinsi lilivyokuwa kubwa, na kukarabatiwa kwa muda mrefu wa miaka 46 na Herode..jinsi watu wengi walivyokuwa wanatoa sadaka zao kwa ajili ya hekalu lile.. Lakini jicho la Bwana Yesu lilikuwa linaona mbali zaidi yao, lilikuwa linaona muda si mrefu hekalu lile halitakuwepo, litakuwa limebomolewa, mahali pale patakuwa pamechomwa moto, watu watauawa na kuchinjwa kama kuku..lakini wale watu hawakuliona hilo, walikuwa wanajisifia tu majengo yake, hawaoni wakati umekaribia mji huo waliokuwepo ambao wanaupenda utateketezwa kwa moto…

Ndipo sasa wakati Bwana akiwa pale hekaluni anavuruga vuruga bishara zao.. wayahudi wakamfuata na kumuuliza, Ni ishara gani utuonyeshayo, kwamba unafanya haya?

Yesu akawajibu…

Yohana 2:19 “…..Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha.

20 Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?

21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake.

22 Basi alipofufuka katika wafu, wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa alisema hivi, wakaliamini lile andiko na lile neno alilolinena Yesu”.

Unaona, Bwana Yesu alimaanisha kweli juu ya hekalu la mwili wake kuwa atakufa na siku ya tatu atafufuka, lakini pia alitaka wafikirie vile vile juu ya habari za kubomolewa kwa hekalu, ili awafundishe jambo..lakini wengi wao hawakuwa tayari kutaka kujua zaidi, wakamwona kama karukwa na akili..anazungumza ujinga.

Lakini baadaye wanafunzi wake wanyenyekevu waliliweka hilo akilini…wakaanza tena kumwonyesha majengo ya hekalu lile ambalo yeye alisema watu walibomoe,..jinsi lilivyojengwa vizuri kwa mawe ya thamani…

Mathayo 24:1 “Yesu akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya hekalu

2.Hamyaoni haya yote? Amin, nawaambieni, Halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa”.

Lakini wanafunzi walivyosikia vile, hawakuishia pale, walizidi kuendelea kutaka kujua hatma ya hayo mambo itakuwaje, wakamfuata sasa faraghani, wakiwa peke yao tu Bwana, ndipo wakamuuliza..mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja kwako? Na ya Mwisho wa dunia? Maswali matatu.

Hapo sasa ndipo Bwana Yesu akaanza kuwafunulia hatua kwa hatua, mambo yatakayotendeka kuanzia ule wakati, mpaka siku mji ule utakapozingirwa na majeshi, na hekalu kubomolewa, mpaka siku za mwisho..ambayo maneno haya hata sisi wa kizazi hiki tunayatumia kama dira ya kutambua majira ya kuja kwa Bwana Yesu..Soma Mathayo 24, Marko 13, na Luka 21. Utaona habari zote za siku za mwisho zitakavyokuwa.

Lakini mafunuo hayo yote yalitoka katika Neno moja tu la Kubomolewa kwa hekalu..Kama mtume wasingetaka kujua zaidi, basi habari za kuteketezwa kwa Yerusalemu na warumi mwaka 70W.K, ambapo watu waliuawa kikatili, wasingekaa wajue pia habari za manabii wa uongo, na kusimama kwa chukizo la uharibifu wasingekaa wajue..

Vivyo hivyo hata sasa, tukiwa tayari kutaka kujua zaidi juu ya maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo katika Neno lake, kwa kumaanisha kujifunza Neno lake na sio kusoma tu kama gazeti, ndipo tunapojijengea nafasi nzuri ya kupokea mafunuo zaidi yamuhusuyo yeye.

Lakini kama tutasoma biblia juu juu tu, na kusema aa hii haiwezekani, au tunasema kile Bwana alimaanisha vile sio hivi..Tutabakia, kuujua upande mmoja tu wa maandiko..Na kufanana na wale watu waliomsulubisha pale msalabani na kumdhihaki…walisikia tu upande mmoja (livunjeni hekalu hili)

Zaburi 25:14 “Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake”.

Hivyo Bwana atusaidie tuzidi kumjua Zaidi yeye, mpaka tutakapofikia ukamilifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! UMEFANYIKA KUWA MWANAFUNZI WA BWANA?

Kuna mambo machache ya muhimu sana ya kufahamu pindi tu unapoamua kumfuata Yesu(kuwa mwanafunzi wa Bwana)..Mambo haya ni ya muhimu sana, ingawa wengi hawayajui na hata wakiyasikia wanaziba masikio yao wasitake kuyasikia wala kuyapokea. Na mojawapo ya hayo ni “kujikana nafsi”. Kama unasema umemwamini Yesu na bado hujajikana nafsi bado unakuwa hujaokoka.

Tafsiri ya kumfuata Yesu ni kujikataa wewe mwenyewe, kuyakataa mapenzi yako…kwamba hapo kwanza ulikuwa unapenda hichi na sasa unalazimika kukiacha, hapo kwanza ulikuwa unapenda kunywa hichi au kile na sasa unaamua kukiacha…hapo kwanza ulikuwa unapenda kufanya hivi au vile na sasa unakatisha, unaacha kufanya hayo mambo.

Hatua hiyo ukiikimbia kamwe huwezi kuzalisha chochote katika Imani.

Hali kadhalika, sio tu kuyakana mapenzi yako binafsi, bali pia na mapenzi ya Baba yako, au mama yako, au mwana wako… Baba yako hataki uokoke hapo huna budi kuyakataa Mashauri yake na kufuata ushauri wa biblia, mama yako anataka muende kwa mganga hapo huna budi kuyakataa mawazo yake hayo na kufuata ya kibiblia. Mtoto wako anakufanya usimtafute tena Mungu kama hapo zamani, unampenda kiasi kwamba upo tayari kula rushwa ili tu umpatie fedha za kwendea kwenye michezo…upo tayari kuiba na kutapeli au kufanya chochote kinachomchukiza Mungu ili tu umpatie mwanao kitu Fulani kitakachompendeza.

Bwana Yesu alisema maneno haya…

Mathayo 10:37  “Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38  Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.

39  Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.

Usipojikana namna hiyo bado hujawa mkristo kabisa…Bwana amekukana, na wala huna ushirika wowote na wewe, haijalishi mchungaji wako atakufariji kiasi gani, haijalishi utafarijiwa na wapendwa kiasi gani, haijalishi utasoma mistari mingine ya biblia na kuona inakufariji kiasi gani, haijalishi utakuwa unahudhuria kanisani namna gani.…Lakini mbele za Kristo umekataliwa!.. Anasema mwenyewe hapo juu… “ukimpenda baba au mama au mwana kuliko yeye humstahili”..yaani maana yake haumfai. Anakwenda kumtafuta mwingine wewe haumfai.

Hutaki kuamua kuacha pombe, kuacha kuishi na mwanamke/ mwanamume ambaye hamjaona…yeye kakukataa, huna ushirika naye…unasema umeokoka lakini uasherati kwako ni kama chakula, haijalishi unalipa zaka, au unahudhuria ibada kiasi gani, au unaimba kwaya, au ni kiongozi wa maombi kiasi gani…Neno lake lipo pale pale… MTU ASIYECHUKUA MSALABA WAKE AKANIFUATA, HANISTAHILI.

Unasema umeokoka lakini unachati kwenye magroup ya ngono, magroup ya mizaha na matusi, unasema umeokoka bado unafanya mustarbation kwa siri, bado unavaa kama wanawake wanaojiuza. Hapo hujajikana nafsi..Hivyo HUMFAI!..kulingana na maneno yake mwenyewe. Hata sala zako hazisikilizi kwasababu wewe sio wake.. una mambo yako na yeye ana mambo yake…una mapenzi yako na yeye ana mapenzi yake…hamhusiani kwa lolote.. Yeye anatembea na kujidhihirisha kwa wale waliojikataa nafsi zao,.waliyoyakataa mapenzi yao na kuamua kuyafuata mapenzi yake yeye. Wengine wote walio nje na Neno lake hilo, kasema hawajui. Haijalishi ni mchungaji au muumini wa kawaida..kama hajajikana nafsi HAMFAHAMU.

Kama unaona aibu kuacha pombe, kama unaona aibu kumwambia ukweli huyo mwanamume/mwanamke unayeishi naye sasa kwamba umeokoka na hivyo Maisha ya dhambi huwezi kuishi tena…fahamu wewe na Bwana Yesu ni vitu viwili tofauti, kama unaona aibu kuacha kuvaa suruali na nguo zinazobana na na vimini kupaka make-up kwamba unaogopa/unaona aibu utaonekanaje mbele za wale waliozoea kukuona hivyo, au utaonekanaje mbele ya mume wako.. Kama unaogopa kufanya hivyo…tayari Kristo hayupo na wewe.

Luka 9:23 “Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

24  Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.

25  Kwa kuwa yamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, kama akijiangamiza, au kujipoteza mwenyewe?

26  KWA SABABU KILA ATAKAYENIONEA HAYA MIMI NA MANENO YANGU, MWANA WA ADAMU ATAMWONEA HAYA MTU HUYO, ATAKAPOKUJA KATIKA UTUKUFU WAKE NA WA BABA NA WA MALAIKA WATAKATIFU”

Kama ulikuwa hujajikana nafsi na ulikuwa unadhani unaye Yesu moyoni mwako..Tubu tena leo!..Na baada ya kutubu, GEUKA! Acha yale maovu uliyokuwa unayafanya pasipo kutazama kwamba utamkwaza mtu au utachukiwa na mtu, au utagombana na mtu…acha ulevi, acha rushwa, acha uasherati, acha kujichua, acha kampani za marafiki wabaya..Wengi wanasema wamejaribu kuacha kufanya uasherati na kujichua wameshindwa hivyo wanahitaji maombi…nataka nikuambie bado hujajikana nafsi! hakuna maombi yoyote ya kuondoa hiyo tabia ndani yako..ni wewe kuamua kuiacha!…mbona hulali na kuku anayekatiza hapo pembeni yako, au mbuzi au ndugu yako wa damu, au mzazi wako? Hata ile hamu tu haipo!..hapo umeombewa na nani mpaka ukaishinda hiyo hali?..Umeona? hivyo hata hayo mengine usitafute kuombewa..Ni kutoyaendekeza tu na kuyaacha kabisa.

Na baada ya kutubu, usifanye tena hayo, ndipo Roho Mtakatifu atakuongezea uwezo wa kuyashinda hayo. Bwana anakupenda sana.

Bwana akubariki sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.

NI KWANINI MUNGU HAONEKANI?

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini tofauti kati ya Husuda, faraka na uchafu?

SWALI: Husuda ni nini?, faraka ni nini? na uchafu ni nini katika biblia?


JIBU: Husuda limeonekana sehemu kadhaa katika biblia na maana yake ni “WIVU”  na mtu kuwa na HUSUDA/WIVU ni Dhambi…..Ifuatayo ni baadhi ya mistari iliyozungumzia husuda.

Wagalatia 5:21 “HUSUDA, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”

Na mwingine ni huu…

1Petro 2:1 “Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na HUSUDA na masingizio yote”

Na mingine ambayo unaweza kusoma kwa muda wako ni hii; Tito 3:3,Mathayo 27:18, Marko 15:10, Warumi 1:29, 1Wakorintho 3:3 n.k

Faraka ni nini?

Neno Faraka inatokana na neno mafarakano…Tafsiri yake inakaribiana na tafsiri ya neno matengano, na kuwa na faraka ni dhambi, Biblia imekataza wakristo kufarakana..na baadhi ya mistari kwenye biblia inayozungumzia “faraka” ni kama ifuatayo.

1Wakorintho 1:10 “Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu FARAKA, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja”

Na mwingine ni..

1Wakorintho 12:25 “ili kusiwe na FARAKA katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe”

Na mingine ambayo unaweza kuisoma kwa muda wako ni kama ifuatayo; 1Wakorintho 11:17 na Wagalatia 5:20.

Uchafu ni nini?

Uchafu kila kitu kinachomtia mtu unajisi…mfano uasherati, ulawiti, ufiraji, ulevi na mambo yanayofanana na hayo, vile vile wachafu wote hawataurithi ufalme wa mbinguni biblia inasema hivyo….Baadhi ya mistari katika biblia inayozungumzia uchafu ni kama ifuatayo.

2Wakorintho 7:1″Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”

Na mwingine ni huu..

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, UCHAFU, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Na mingine inayozungumzia uchafu ni Waefeso 4:19,Wakolosai 3:5, 1Wathesalonike 4:7 n.k

Je umeokoka?..Je una husuda? au una faraka au ni mchafu?..Biblia imesema watu wa namna hiyo hawawezi kuurithi uzimwa wa milele…Mpe Kristo leo maisha yako ayaokoe kama hujaokoka.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAJISAIDIA SEHEMU ZA WAZI.

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

WAKAMWACHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SALA YA TOBA

Sala ya Toba ni nini?..Je ni lazima kuongozwa sala ya Toba pale mtu unapoamini?

Jibu: Sala ya Toba ni sala, ambapo mtu mmoja aliyeamini anamwongoza mwingine ambaye ndio anaingia katika Imani..Mtu anayeingia katika Imani anakuwa anafuatiliza maneno yale kwa Imani na kumkiri Yesu kwa kinywa chake, kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yake na alikufa kwa ajili ya dhambi zake.

Sasa hakuna maagizo yoyote katika biblia yanayosema mtu baada ya kumwamini Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake..basi anahitaji kuongozwa sala ya toba. Hakuna andiko kama hilo,  Lakini lipo andiko moja tu linalosema..

Wagalatia 6:2 “Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo”

Maana yake ni kwamba..aliye dhaifu wa Imani hana budi kushikwa mkono na kusaidiwa kusimama na hatimaye kutembea mwenyewe…Kama vile mtoto mchanga anayejitahidi kusimama ili atembee…Mzazi huna budi kumshika mkono na kumnyanyua na kumsaidia atembee..

Vivyo hivyo katika safari ya Imani. Mtu anayetoka katika dhambi moja kwa moja na kumpokea Kristo ni sawa na kitoto kichanga kilichozaliwa…wengi wa hawa hata kusali tu hawajui, zaidi ya yote hata wakiomba wanahisi Mungu hawasikii…wanakuwa hawajamjua Mungu, wala hawaujui uweza wa Mungu vizuri. Hivyo unapowashika mkono na kuwasaidia kusali pamoja nao kwa mara ya kwanza…Imani zao ni rahisi kukua na kunyanyuka na kusonga mbele.

Lakini ukiwaachia kwamba waombe wenyewe katika siku za kwanza kwanza…ni rahisi shetani kuwaletea mawazo kwamba bado hawajaokoka wala kumpokea Yesu..Hivyo wataendelea siku chache na baada ya hapo ni rahisi  kurudi nyuma. Wapo wachache ambao wanaweza kujishika wenyewe hata kusimama na kukua kiroho bila hata kuongozwa sala hiyo.. lakini wengi wa wanaomwamini Bwana Yesu katika hatua za awali wanahitaji msaada mkubwa sana..Kwasababu ni watoto wadogo kabisa kiroho waliozaliwa.

Lakini baada ya kipindi fulani, wakishakuwa basi hawana haja ya kushikwa tena mkono bali wanapaswa wakawasaidie wengine walio dhaifu kama wao walivyokuwa.

Hivyo sala ya Toba inatokana na upendo wa mkristo kwa mtoto mpya aliyezaliwa kiimani, na sio dhambi kuwaongoza watu wala kuongozwa. Hivyo upendo hauna masharti..Bwana wetu Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kusali..si zaidi sisi kuwafundisha na kuwaongoza sala wale walio wachanga kiroho katika hatua za awali?

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA?.Mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

BUSTANI YA NEEMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAJISAIDIA SEHEMU ZA WAZI.

Kuota Unajisaidia sehemu za wazi. Maana yake ni nini?


Ndoto hii, imekuwa ikiotwa mara kadhaa wa kadha na watu wengi. Kwa mfano mtu mmoja alinisimulia ndoto yake, anasema katika ndoto alijikuta yupo stendi ya basi, na pale palikuwa na watu wengi sana, ghafla akaanza kujisaidia lakini yeye alikuwa anajitahidi kufanya vile asionekana..Na alipomaliza akidhani hajaonekana wakati akiwa anarudi nyumbani mtu mmoja ambaye alikuwa anamjua akamfuata akamwambia mbona nilikuona unajisaidia pale stendi?..Anasema kwa kweli aliposikia hivyo   alijisikia aibu sana.

Na ndivyo ilivyo ndoto za namna hii, ni lazima mwisho wa siku utajisikia aibu tu, wengine wanaota wamejinyea, mavi, wengine wakiwa shuleni, kazini, uwanjani n.k. ..kwasababu kitendo cha kujisaidia huwa sikuzote ni cha aibu na ndio maana kinafanyika kwa siri chooni.. Lakini ikiwa unajisaidia kwa wazi ni Mungu anakuonyesha ni jinsi gani, mambo yako machafu yatakavyokuja kuwa dhairi siku moja mbele za watu wengi..kama hutatubu dhambi zako au hutasimama imara leo hii kwa Mungu wako.

Inaweza isiwe sasa, lakini kumbuka siku ile ya hukumu inafika..ambapo mambo yote yaliyokuwa yanafanyika kwa siri yatawekwa wazi.

2Wakorintho 5:10  “Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya”

1Wakorintho 4:5  “Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye ATAYAMULIKISHA YALIYOSITIRIKA YA GIZA, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu”.

Unaona? Hivyo ikiwa hujatubu dhambi zako, maisha yako bado ni machafu, YESU KRISTO bado hajaingia ndani yako kukusafisha uwe hai..Ni heri ukaamua kufanya hivyo kabla nyakati hizo mbaya hazijafika..Huu ndio wakati wa wewe, kusema basi..Nahitaji kuanza upya na Kristo..Usiseme mimi ni muislamu, hata wewe Unapaswa umgeukie YESU Kristo kwasababu yeye ndio njia na kweli na Uzima ya kukufikisha wewe mbinguni.

Ukimkaribisha leo maishani mwako, atakupokea na kukufanya upya. Unaona ni hali gani ulijisikia ulipojiona unafanya kitendo cha aibu katikatika ya umati wa watu..Sasa embu fikiria siku ile ya hukumu, Maisha yako yataanza kutazamwa  na Mungu mbinguni, pamoja na majeshi ya malaika zake, pamoja na watakatifu wa Mungu mamilioni kwa mamilioni..wote wanakutazama siku ile ulivyokuwa unazini na mume au mke ambaye si wako, watakutazama ulivyokuwa unajisaga kisirisiri mwenyewe nyumbani mwako..watakutazama ulivyokuwa unafanya mustarbation kwa siri chumbani, watakutazama ulivyokuwa unaangalia picha za uchafu, lakini kwa nje unaonekana wewe ni mwema, watakutazama mimba ulizotoa japo ulikuwa unajulikana kama ni mwanamke mstaarabu, machoni pa watu watu..watakutazama ufiraji uliokuwa unaufanya kwa mkeo, japo kwa nje unaonekana mtu unayejiheshimu….Siku hiyo watakutazama..Ni itakuwa ni AIBU KUU, ambayo utatamani hata usingezaliwa.

Lakini hayo yote ya nini mpaka yakukute wakati Kristo bado anakupenda?..Njoo kwa YESU ayabadilishe maisha yako leo hii..biblia inasema..saa ya wokovu ni sasa..Umeshindwa kuacha pombe, lakini Ukimruhusu Yesu aingie maishani mwako, ataikata hiyo kiu ya pombe, itakwisha kabisa..Umeshindwa kuacha uzinzi lakini ukimfuata Yesu leo hii, atakusaidia na hiyo hali utaishinda..na mambo mengine yote maovu unayoyatenda saa hii, ukimkabisha Yesu maishani mwako atakugeuza..anachohitaji kwako ni moyo wa toba tu basi..Na kumaanisha kweli kweli wala sio kujaribu..

Hivyo ikiwa umemaanisha kufanya hivyo..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

KUOTA UPO UCHI.

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MTETEZI WAKO NI NANI?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.

Muonekano mpya wa yesu baada ya kufufuka, unabeba somo gani?


Bwana Yesu alipokuwa bado anaishi duniani, ilikuwa ni rahisi kumtambua, kwani kwa sura yake tu watu waliweza kumtambua kuwa huyu ndiye. Lakini mara baada ya kufufuka kwake, mambo yalikuwa tofauti kabisa, haikuwezekana kumtambua tena Bwana Yesu kwa sura yake..Ilihitaji kipimo kingine tofauti..

Hilo tunalithibitisha sehemu kadha wa kadha, wengine walipomwona walidhani ni mtunza bustani makaburini, wengine walidhani ni mpita njia tu, na wengine walidhani ni mzee Fulani tu anapunga upepo beach..Na kama wangekikosa hicho kipimo kingine ndani yao cha kumtambua Yesu basi wasingekaa wamjue daima haijalishi huko nyuma waliishi naye na kutembea naye na kulala naye muda mrefu kiasi gani..kamwe wasingemjua.

Kwamfano embu tumwangalie Mariamu Magdalene, yeye ile siku ya kwanza ya juma, siku Yesu aliyofufuka, ndio aliyekuwa wa kwanza kufika pale makaburini, lakini alipomkosa Bwana, akidhania kuwa ameibiwa, alikwenda kuwaambia mitume, nao walipokwenda hawakukuta mtu kaburini.. wakaamua kuondoka zao, Sasa wakati Mariamu akiwa pale kaburini analia, kulikuwa na mtu yupo pale muda mrefu tu, anazunguka zunguka, pengine wakina Petro walimwona wakadhani ni watu wale wasio na shughuli wanaozunguka makaburini, lakini Mariamu alipokaa pale muda kidogo akiwa analia, ndipo Huyu mtu ambaye alimwona kama mtunza bustani akamfuata na kumuuliza unatafuta nini?.

Mariam akasema: ikiwa ni wewe ndio umemuiba Bwana wangu niambie..Kumbe hakujua anayezungumza naye ni YESU mwenyewe..Ndipo Yesu akalitaja jina lake Mariamu!..Na alipolitaja tu, Hapo hapo Mariamu akaitambua sauti ile, ni ile sauti yake yenye uweza, sauti ile ile iliyomwita Lazaro atoke makaburini kipindi kile kule nyuma, sasa imemwingia na yeye mpaka kwenye vilindi vya moyo wake ikampa uhakika kuwa huyu ndiye BWANA….Haikujalisha sauti ilikuwa ni ya mtu mwingine,inayofanana na mtu wa taifa lingine, lakini uweza tu wa ile sauti ulimpa uhakika kwamba huyu ndiye Bwana..(Soma..Yohana 20:1-18).

Lakini kama Mariamu asingekuwa na ushuhuda huo huko nyuma, basi ingekuwa ni rahisi kumpoteza Yesu..

Vivyo hivyo wale watu wawili ambao walikuwa wanakwenda katika kile Kijiji cha Emau, nao pia walipokuwa wanatembea njiani, Yesu alikutana nao isipokuwa katika sura nyingine..Na akaanza kuzungumza nao habari za kutabiriwa kwake, kuja kwake, na kufufuka kwake..Wale watu waliposikia tu yale maneno, jinsi yalivyokuwa yenye nguvu kwa namna ile ile waliyokuwa wanamsikia Bwana akifundisha makutano akiwa bado hai, hawakumuacha aondoke hivi hivi, wakamkaribisha nyumbani kwao, ndipo baada tu ya kuumega mkate na kuwapa, wakafumbuliwa macho wakatambua kuwa alikuwa ni YESU. Na saa hiyo hiyo akatoweka mbele ya macho yao.(Luka 24:13-33)..Lakini kama wasingetilia maanani uweza uliokuwa unatoka ndani ya maneno yale..wasingekaa wamtambue Kristo.

Mwisho kabisa Petro na wenzake, walipokuwa wanakwenda kuvua samaki, baada ya kuhangaika usiku kucha hawajapata kitu..Asubuhi yake kwa mbali walimwona mtu kama mzee akiwa pwani, mwenye sura wasioijua, mtu yule akawauliza wanangu mmepata kitoweo, wakasema hapana Bwana, akawaambia, tupeni jarife upande wa pili, wakidhani ni mzee tu wa kawaida anawashauri, wajaribu bahati yako, ..Na walipotupa tu jarife, wakapata samaki wengine..Mwanafunzi mmoja alipoiona ile ishara, akatambua kuwa hii ni ishara ile ile aliyotufanyia Bwana kipindi kile akiwa hapa duniani..Ndipo Yule mwanafunzi akamwambia Petro aliyetupa maagizo haya ni Bwana Yesu..Petro kusikia hivyo muda huo huo akapiga makasia kumfuata Pwani..

Biblia inatuambia walipomwona Bwana japo aliwatokea katika sura nyingine tofuati kabisa..Lakini hakuna hata mmojawao aliyetaka uthibitisho kama yeye ni Bwana kweli au la, Wote walipata uhakika ule, kwa ule uweza wake mkuu , na yale maneno aliyokuwa anazungumza nao akiwa pale ufukweni..(Yohana 21:1-25)..Lakini kama wasingeyaona matendo makuu kama yale Bwana aliyowahi kuwafanyia huko nyuma, kamwe wasingejua hata kama yule ni YESU. Wangedhani ni mzee Fulani tu amewapa dili la kazi.

Hivyo ndivyo Kristo alivyochagua kujidhihirisha kwa watu baada ya kufufuka kwake..Mpaka ikawafanya hata wengine wamtilie shaka..Hao ndio wale ambao walioukosa ushuhuda wake ndani yao..ndio wale waliokuwa wanalitazama umbo la Yesu, lakini hawayatafakari matendo yake, na ishara zake.

Mathayo 28:16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu. 17 Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka”.

Sasa kwa mabadiliko hayo, mitume kuanzia huo wakati wakatoa akili zao kabisa katika kuitegemea sura ya YESU, kama kipimo cha kumtambua Kristo mpaka kuutegemea ushuhuda wa YESU Maishani mwao.

Hivyo sura ya Yesu ikawa haina umuhimu tena kwao..Na ndio maana utaona Mitume mahali popote hawakuwahi kujisifia umbile la Yesu au Sura yake, au sauti yake..Bali ule Ushuhuda wa YESU uliokuwa ndani yao, ndio uliowafanya wamjue na kumtambua Yesu.

Vivyo hivyo leo hii KRISTO yupo kila mahali, lakini kama umeukosa ule ushuhuda wake ndani yako, utamwona tu kama mtunza bustani, utamwona tu kama mpita njia, utamwona tu kama mzee Fulani..

Ndio maana kuna umuhimu sisi tunaojiita wakristo, kujifunza biblia sana..kwasababu wakati utafika Kristo atajidhihirisha kwako, lakini hutamtambua kwasababu huujui ule ushuhuda wake alipokuwa hapa duniani ulivyokuwa.

Kwamfano Injili ya Kristo inapohubiriwa kwako, na unaona kabisa imekuja kwa ukali, na uzito, na kwa nguvu, labda inakutaka wewe ufanye jambo Fulani.. Sasa kwa kuwa wewe huna ushuhuda wa Yesu ndani yako, unaokushuhudia hata katika maandiko kuwa kulikuwa na watu wawili wa Emau, ambao neno la Kristo liliwajia kwa uzito kama huo, wakachukua hatua ya kusikiliza mpaka mwisho..Wewe unapuuzia, Unadhani ni mlokole Fulani anahubiri, au mchungaji tu Fulani, au kijana tu Fulani anauhibiri..kumbe hujui unampuuzia Kristo mwenyewe.

Na wakati huo huo unakesha kuomba kwamba Bwana akutokee, unataka akutokee vipi? Unataka umwone kavaa mavazi meupe, mwenye nywele ndefu, ndio umtambue?. Hilo wazo na ufute. YESU ameshafufuka, haji kwetu kwa muonekano ule tena.

Huu ni wakati wa kumjua yeye kwa ushuhuda wake.Hapo ndipo tutakapomwona akitembea katika Maisha yetu kila siku. Na hiyo inakuja pale tu Neno la Kristo linapokaa kwa wingi ndani yetu.

Vingenevyo tutamtilia shaka tu sikuzote, hata akitokea kwa sura ipi, kama wale wengine walivyomtilia shaka kule Galilaya, na wewe utamtilia shaka hivyo hivyo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye boksi la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

TULICHUNGUZE UMBO LA YESU NA MWENENDO WAKE.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

Rudi Nyumbani:

Print this post