Title 2020

Nasaba ni nini kibiblia?(1Nyakati 9:1, Tito 3:9)

Nasaba ni nini kibiblia?


Ni mfululizo wa majina ya watu au watawala  katika ukoo mmoja, Kwamfano kitabu cha Mathayo sura ile ya kwanza kinaonyesha nasaba ya Bwana wetu Yesu Kristo (yaani ukoo wake tangu Ibrahimu mpaka kuzaliwa kwake), Na kile cha Luka sura ya tatu kuanzia mstari wa 23-38, kinaeleza ukoo wake tangu kuumbwa kwa Adamu, yaani huyu alimzaa huyu, na huyu akamzaa huyu,  hivyo hivyo mpaka vizazi vyote vipite hapo katikati. Hiyo ndio maana ya Nasaba.

Wana wa Israeli nao pia walihesabiwa kwa nasaba,

Na hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakutana na neno hilo;

1Nyakati 9:1 “Hivyo Israeli wote walihesabiwa kwa nasaba; na tazama, hizo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli; na Yuda wakachukuliwa mateka mpaka Babeli, kwa sababu ya makosa yao”.

1Nyakati 5:1 “Na wana wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli; (kwa maana ndiye aliyekuwa mzaliwa wa kwanza, lakini, kwa kuwa alikinajisi kitanda cha babaye, haki yake ya mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yusufu, mwana wa Israeli; tena nasaba isihesabiwe kwa kuifuata hiyo haki ya mzaliwa wa kwanza”.

Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana”.

1Timotheo 1:4 “wala wasiangalie hadithi na nasaba zisizo na ukomo, ziletazo maswali wala si madaraka ya Mungu yaliyo katika imani; basi ufanye hivyo”.

Soma pia,

1 Nyakati 5:7, 9:22 2Nyakati 12:15, 31:16,17,19, Ezra 2:62,8:2.

Hata sisi pia tunahesabiwa kwa nasaba rohoni, pale unapomletea mmoja kwa Kristo, mbinguni inarekodi kuwa huyo ni mwana wa wako uliyemzaa kwa Bwana, na Yule uliyemzaa akakomaa akaenda kumleta mwingine kwa Kristo, anaonekana kuwa yeye ndiye aliyemzaa, hivyo hivyo, lakini chanzo ni wewe.

Na hiyo inafanya jina lako liwe kubwa katika ufalme wa mbinguni, kulingana na Nasaba yako.

Je! Na sisi tunayo juhudu katika kumzalia Mungu matunda?. Kama hatuna tunapaswa tuanze ili tujijengee daraja zuri mbinguni.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Rangi ya kaharabu ni ipi kibiblia(Ezekieli 1:4,27,8:2)?

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

UCHAWI WA BALAAMU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MAONO YA NABII AMOSI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kabari ni nini kwenye biblia?(Yoshua 7:21,24)

Kabari ni nini?


Kabari ni ni kipande kikubwa cha kitu Fulani aidha mbao, chuma,  dhahabu, shaba n.k.. (donge)

Katika biblia tunaona wana wa Israeli walipoingia nchi ya ahadi na kuwepo maagizo kuwa vitu vyote vya thamani watakavyovikuta kule vitatolewa wakfu kwa Bwana(Yoshua 6:19), lakini tunaona walipofika kulikuwa na mtu mmoja aliyeitwa Akani, mwana wa Karmi, huyu alipofika tu aliyeingiwa na tamaa, pale alipoona vitu vya thamani, ikiwemo hizi kabari (vipande) vya dhahabu, hakuvithaminisha kwa Bwana, bali alikwenda kuvificha(Yoshua 7:11).

Akasababisha mpaka taifa zima la Israeli kupigwa na kufadhaishwa mbele ya maadui zao. Hiyo ikawafanya wapepeleze tatizo ni nini, ndipo walipogundua kuwa ni huyu Akani ameficha baadhi ya vitu vya thamani walivyovikuta kule, hivyo wakamkamata na kumuua.

Yoshua 7:21 “Nilipoona katika nyara joho nzuri ya Babeli, na shekeli mia mbili za fedha, na kabari YA DHAHABU, uzani wake shekeli hamsini, basi nalivitamani nikavitwaa; tazama, vimefichwa mchangani katikati ya hema yangu, na ile fedha chini yake…..

24 Kisha Yoshua, na Israeli wote pamoja naye, wakamtwaa Akani, mwana wa Zera, na ile fedha, na Lile joho, na ile KABARI YA DHAHABU, na wanawe, na binti zake, na ng’ombe zake, na punda zake, na kondoo zake, na hema yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta juu hata bonde la Akori”.

Hiyo inatufundisha nini? Inatufundisha kuwa tusiwe na tamaa ya mali ikiwa sisi ni watoto wa Mungu, kwani haitatugharimu maisha yetu tu, bali itagharimu kama sio kuathiri na maisha ya wengine pia. Na ndio maana biblia inasema,

1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.

Bwana atusaidie, tupende kujikusanyia  zaidi kabari za ufalme wa mbinguni kuliko hizi za hapa duniani..Kwani za hapa duniani ni za kitambo tu, lakini zile zinadumu milele.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

JIEPUSHE NA UNAJISI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

Kuna tofauti ya kumpa Mungu utukufu na kumshukuru Mungu. Mungu anapokufanyia jambo zuri, lakukupa faraja na furaha, na moyoni ukafurahi, ni kawaida ya kila mwanadamu mwenye moyo wa shukrani, huwa anakwenda kupiga magoti na kumshukuru Mungu wake kwa alilomtendea aualiyomtendea, na zaidi sana huwa anaambatanisha hata na sadaka yake ya shukrani.

Sasa hilo ni jambo moja ambalo linampendeza sana Mungu wetu, pale tunapomshukuru, lakini lipo lingine linalompendeza pia ambalo litatufungulia milango ya baraka mara mbili. Na jambo hilo si lingine zaidi ya KURUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

Kurudi kumpa Mungu utukufu, ni kitendo cha kurudi na kutangaza kwa wazi, yale yote Mungu aliyokufanyia.. Hivyo Mungu wako anakuwa anatukuzwa katikati ya watu.

Ni jambo linalodharaulika na wengi lakini ni la umuhimu sana. Kurudi kumpa Mungu utukufu…Je umeshawahi kurudi kumpa Mungu utukufu kwa jambo lolote jema alilokufanyia?

Hebu tusome hichi kisa maarufu kwenye biblia..

Luka 17:11 “Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria naGalilaya.

12 Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,

13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakiendawalitakasika.

15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, HUKU AKİMTUKUZA MUNGU KWA SAUTİ KUU;

16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

18 JE! HAWAKUONEKANA WALİORUDİ KUMPA MUNGU UTUKUFU İLA MGENİ HUYU?

19 Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa”

Waliponywa wote kumi lakini ni huyu mmoja tu ndiye Aliyepaza sauti yake, kwa sauti kuu, akitangaza jinsi alivyoponywa njia nzima, mpaka alipofika kwa Bwana Yesu..Pengine wale 9 walikwenda kutoa sadaka zao za shukrani tu!..Lakini hawakumtukuza Mungu, walakutangaza waliyofanyiwa kwa wazi, kwasababu zao wenyewe, labda waliona aibu, au waliogopa kutengwa, au kuonekana wa kikale…Lakini huyu hakujali hayo, alitangaza kwa watu lililomtokea kuanzia mwanzo hadi mwisho..

Na hivyo likawa ni jambo jema mbele za Mungu..

Je na wewe ulishawahi kurudi kumpa Mungu utukufu?… Bwana alipokuponya ugonjwa ambao ilikuwa ni ngumu kupona, je! Ulishawahi kusimama na kutangazia watu wawili au watatu mambo makuu Mungu aliyokufanyia?..au uliishia kuwatukuza madaktari tu! Kwamba walikupambania lakini hukuwahi kumtaja Mungu maneno yasiyozidi mawili?..Kama ndivyo basi badilika leo.

Je ulishawahi kumpa Mungu utukufu kwa huyo mtoto uliyempata ambaye ulihangaika miaka mingi bila kupata mtoto?..Ni kweli pengine ulitoa sadaka ya shukrani, hiyo ni vizuri…lakini bado haitoshi…Mungu wako anapaswa atukuzwe mbele za watu kwa hicho alichokufanyia.. Inapaswa watu wamwonapo mwanao aliyekupa Mungu, wamfikirie Mungu wako na si daktari wako wala jitihada zako.

Nyumba Mungu aliyokupa, mali alizokupa, afya aliyokupa, uzima anaokupa, cheo alichokupa, elimu aliyokujalia, nguvu alizokupa n.k…Je Mungu wako anatukuzwa katika huo? Au jitihada zako?..Watu wanapaswa wakitazama cheo chako wanakumbuka ushuhuda uliowasimulia wa jinsi Mungu alivyokuweka pale kimiujiza, na sio wanakumbuka jinsi ulivyopambana…Watu wanapokuona leo umesimama ni mzima, wanapaswa wakumbuke ushuhuda uliowaambia jinsi ulivyokuwa hatiani kupona na ukamwomba Mungu na Mungu akakufungulia mlango wa uponyaji… ili Mungu wako atukuzwe kwao.

Watu wanapokuona una hiki au kile..wanapaswa wautafakari uzuri wa Mungu wako, na utukufu wake, kwa utukufu uliomrudishia wakati unavipata hivyo…kila kitu wajue ni Mungu kakusaidia na si nguvu zako.

Na hatumpi Mungu wetu utukufu kwa yale aliyotutendea kwa kuwawekea watesi wetu CD za  mipasho!.. Kwasababu siku hizi zipo nyimbo za dini ambazo hazina tofauti na nyimbo za kidunia (Taarabu)..zimejaa maneno ya kiburi na ushindani. Kwamba Mungu kanitendea hichi ili maadui

zangu waone waumie moyo…Hapana! mpango wa Mungu sio maadui zetu waumie moyo na waone Mungu alichotufanyia halafu basi!. Mungu hatupiganii ili awachome watu mioyo, bali ili awageuze nia zao wamgeukie yeye.

Hivyo ukimpa Mungu utukufu mbele za watu, jinsi inavyopaswa, kwa kutangaza kwa kina ulipotoka na ulipo sasa, na jinsi gani Mungu alivyokuokoa, kwa neema…Wale wanaokusikiliza akili zao zitahama kutoka kushindana na wewe, na kuhamia kumtafakari Mungu wako, na hivyo nao pia wamtamtamani Mungu wako aliyekutendea mambo makuu namna hiyo. Na watakuuliza “nami nifanyaje Mungu anitendee kama alivyokutendea wewe”

Lakini ukianza kuwawekea mipasho, watakuchukia na hawatavutiwa na unachokiamini, hivyo utakuwa nawe pia unaifanya kazi ya ibilisi ya kuwapeleka watu mbali na Mungu, na moyoni ukidhani umemtukuza Mungu kwa nyimbo zako hizo za kiburi na majivuno kumbe ndio unaenda kinyume na mapenzi ya Mungu.

Hivyo Usiache kamwe kurudi kumpa Mungu utukufu kwa jambo lolote lile analokutendea, hata liwe dogo kiasi gani…Nenda kalitangaze kanisani, kalitangaze kwa rafiki zako, kalisimulie kwa ndugu, kalisimulie kwa yoyote yule ambaye utapata nafasi ya kumsimulia..hakikisha tu lengo lako ni Mungu atukuzwe na si wewe utukuzwe, au kujisifu.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Mavu ni nini katika biblia?(Kutoka 23:28, Kumb 7:20)

UTAWALA WA MIAKA 1000.

CHAPA YA MNYAMA

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hedaya ni nini katika biblia (Zaburi 68:29, Isaya 18:7)?

Hedaya ni nini?


Hedaya ni neno linalomaanisha zawadi. Ni zawadi inayotolewa kuonyesha shukrani,  au kuridhishwa kwa wema Fulani uliofanyiwa au  kwa uzuri wake.

Katika biblia Neno hilo tunaliona katika vifungu vifuatavyo;

Zaburi 68:28 “Ee Mungu, uziamuru nguvu zako; Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.

29 Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu Wafalme watakuletea hedaya”.

Zaburi 76:11 “Wekeni nadhiri, mkaziondoe Kwa Bwana, Mungu wenu. Wote wanaomzunguka wamletee hedaya, Yeye astahiliye kuogopwa”.

Isaya 18:7 “Wakati huo Bwana wa majeshi ataletewa hedaya na watu warefu, laini; Watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu, wakanyagao watu, Ambao mito inakata nchi yao; mpaka mahali pa jina la Bwana wa majeshi,mlima Sayuni”.

Hata sisi leo hii kila mmojawetu analojukumu la kumpelekea Mungu wetu hedaya,

Na tunampelekea kwa njia mbili:

Njia ya kwanza: ni kwa sifa za midomo yetu: Yaani kumsifu na kumwabudu, na kumpa shukrani kwa vinywa vyetu kwa wema wake wote anaotutuendea, na kwa ukuu wake wote alionao ulimwenguni kote.

Njia ya pili: Ni kwa Kumtolea sadaka: Unapotoa sadaka( yaani fedha, mali n.k.), ni unaonyesha shukrani kwa Mungu, kwa kile alichokufanyia, unaonyesha shukrani kwa neema aliyokupa ya uhai, na kila kitu.

Hivyo huo ni wajibu wa kila mmojawetu. Na hiyo ndio tafsiri ya Hedaya kibiblia.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama maana nyingine za maneno chini;

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

 

UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

TAFUTA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KWA HUDUMA MUNGU ALIYOIWEKA NDANI YAKO.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! MAWAZO YAKO UMEYAELEKEZA WAPI HAPA DUNIANI?

Yusufu alipochukuliwa Misri alikuja kuwa mtu mkuu, kama tunavyosoma katika biblia, lakini kilichomtofautisha yeye na ndugu zake mbele za Mungu, sio ule ukuu aliokuwa nao, wala sio kile cheo alichokipata, hapana, bali ni mahali ambapo moyo wake ulikuwepo pindi alipokuwa Misri, utaona japokuwa aliishi kule kwa miaka mingi sana, tangu akiwa kijana mdogo kabisa, lakini moyo wake wote ulikuwa katika nchi ya ahadi ya baba zake, na ndio maana utaona alipokaribia kufa aliwaambia wana wa Israeli, kuwa siku watakapopandishwa kutoka katika nchi ya Misri na Mungu, basi mifupa yake wasiiache kule, bali waibebe mpaka nchi ya kaanani.

Kutoka 13:19 “Musa akaichukua ile mifupa ya Yusufu pamoja naye; maana, alikuwa amewaapisha sana wana wa Israeli, akisema, Mungu hana budi atawajilia ninyi; nanyi mtaichukua mfupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi’.

Tofauti na wale watoto wengine 11 wa Yakobo, japokuwa walikaribishwa tu Misri, hawakuwepo kule maisha yao yote, lakini walipofika, waliishi kama ndio nyumbani kwao, mawazo ya kurudi Kaanani hayakuwepo, na ndio maana hata waliposikia habari za Yusufu kuondolewa mifupa yake, hilo halikuwawazisha nao waseme hivyo, kwasababu uzuri wa Misri ulishawaridhisha mioyo yao.

Utaona hiyo tabia Yusufu aliyokuwa nayo aliirithi kutoka kwa baba yake Yakobo, kwani alipokuwa Misri kwa kipindi kifupi, aliwaambia, atakapokufa wahakiishe hawamziki katika nchi ile, bali katika nchi ya Baba zake walizozikiwa (yaani Kaanani).

Mwanzo 49:29 “Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti;

30 katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia.

31 Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea”;

Unaona, hicho pia ndicho kilichomtofautisha Yakobo kwa Esau.. sikuzote, wana wa urithi, hawatazami ya hapa, bali wanatazama ya mbele, wanaishi kama wapitaji, na mazingira huwa hayawakwamishi hata kidogo kutokuwaza makao yao ya milele, utajiri hauwakwamishi, vyeo vyao vya muda, haviwafanyi wasahau makao yao halisi, hata hali ngumu za kimaisha haziwakwamishi wasiwaze kurejea nchini mwao siku moja.

Na ndicho utakiona pia kwa Danieli, japokuwa alichukuliwa utumwani Babeli, hadi akawa mtu mkuu katika nchi ile ya kipagani, Lakini kila siku (mara tatu kwa siku) alikuwa haachi kuomba dua juu ya Yerusalemu, madirisha yake yalikuwa yamefunguliwa kuelekea Yerusalemu ilipo, mbali sana, maelfu kwa maelfu ya kilometa, lakini aliiwaza kila wakati na kuiombea kana kwamba alikuwa Israeli. Tofauti na wayahudi wote waliochukuliwa utumwani Babeli kwa wakati ule.(Danieli 6:10)

Utamwona Nehemia naye, japokuwa alikuwa ni mnyweshaji wa Mfalme wa Umedi na Uajemi, lakini akili yake yote, na mawazo yake yote, yalikuwa Yerusalemu, akawa anaulizia habari za mji na hekalu linaendeleaje kila wakati, hadi siku moja aliposikia hali ya mji sio nzuri, kuta zake zimeharibiwa, alilia na kufunga na kuomboleza kwa muda mrefu (Nehemia 1)

Watu kama hao wanaonyesha ni kama kwa bahati mbaya tu walikuwepo katika nchi ya ugenini, wengine walitumainia kabla hawajafa wataiona Yerusalemu, lakini mpaka wanakufa hawakuiona, lakini mioyo yao ilikuwa huko.

Waebrania 11:13 “Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi, bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, na kukiri kwamba walikuwa wageni, na wasafiri juu ya nchi.

14 Maana hao wasemao maneno kama hayo waonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.

15 Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea.”.

Swali Na sisi ambao tunasema ni wapitaji hapa duniani (Kizazi cha watakao nyakuliwa) Je siku zote tunaishi maisha ya kuutafakari urithi wetu wa kimbinguni tuliowekewa, Je tunaitafakari hiyo Yerusalemu mpya ya kimbinguni? Au tunaishi tu hapa duniani kama tumefika?

Shughuli za ulimwengu zinatuzidi mpaka hatuyawazi tena mambo ya mbinguni? hatuwezi kusema tupo busy, zaidi ya Yusufu ambaye dunia nzima alikuwa anaihudumia kwa chakula, na isitoshe alikuwa ni waziri mkuu wa taifa kubwa ulimwenguni, lakini aliiwaza Yerusalemu kiasi cha kukataa kuzikwa kwenye nchi isiyo yake..Sisi hatuwezi kuwa bize zaidi ya Danieli na Nehemia ambao wao walikuwa ni wakuu katika nchi ya Babeli na Umedi, lakini walilia usiku na mchana juu ya Yerusalemu mji wao..wengine mpaka wakaenda kuukarabati.

Lakini sisi tunao mji ulio mkuu kuliko yao. Tunapoishi hapa duniani tukumbuke kuwa, biblia inasema, kule hakitaingia kilicho kinyonge, maana yake ni kuwa hawataingia wasiokuwa na mpango nao, hawataingia ambao hawaulizii habari zake sasa, watakaoingia kule ni wale tu waliostahili kuingia humo, Si kila mtu atauingia huo mji wa kimbinguni, haijalishi utasema leo umeokoka,

Hivyo tuanze sasa kuishi maisha ya kama watu waonaomngojea Bwana wao (Luka 12:36), kwasababu muda tuliobakiwa nao ni mchache sana, Siku ya ukombozi wetu imekaribia, Parapanda wakati wowote italia, kisha tutakwenda mbinguni kwenye karamu ya mwana-kondoo, na baada ya hapo utafuata utawala wa miaka 1000, wakati huo wote tutakuwa tukijiandaa kwa ajili ya mbingu mpya na nchi mpya na hiyoYerusalemu mpya ishukayo kutoka mbinguni.

2Petro 3:13 “Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake”.

Ufunuo 21:1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.

Tukose vyote, tupitwe na vyote, lakini tusikose mambo hayo ambayo biblia inasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

WAKATI WA KRISTO KUSIMAMA,UMEKARIBIA SANA.

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

JE! KUNA UCHAWI KATIKA KUTENDA WEMA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini tofauti kati ya Roho Mtakatifu na Roho Takatifu?

JIBU: Roho Mtakatifu na Roho Takatifu ni kitu kimoja, inategemea neno hilo limetumika wapi

Roho wa Mungu anapozungumza ndani yetu, au kutuongoza, au kutufundisha..anakuwa kama ni mtu yupo ndani yetu akifanya hizo kazi..anakuwa kama ni mtu mwingine mpole ndani yetu anazungumza nasi, anatufundisha, anatushauri, anatufariji, anatutia moyo, anatuongoza n.k..Hivyo hiyo tabia ya kuwa kama mtu wa pili ndani yetu, ndiyo inayofanya biblia sehemu zote iitaje Roho ya Mungu, kwa cheo cha uutu. (yaani Roho M-takatifu).

Hali kadhalika, linapokuja suala la tabia ya Roho ya Mungu, ni sahihi kabisa kusema Roho ya Mungu ni Roho Takatifu, ni Roho Nyenyekevu, ni Roho Tulivu, Ni roho Njema (Danieli 5:12) n.k Hapo hatujaivisha uutu lakini tumeielezea sifa yake.

Yapo madhehebu yanayofanya mambo haya yawe magumu kwa maneno hayo mawili, na hata mengine yamebadilisha biblia zao, kila mahali palipoandikwa kwenye biblia neno Roho Mtakatifu, yamebadilisha na kuweka Roho Takatifu..Hivyo kwao ni kosa kutumia neno Roho Mtakatifu mahali popote. Vile vile yapo mengine ni kosa kutumia neno Roho Takatifu. Pasipo kujua kwamba maneno yote mawili ni sahihi, inategemea ni wapi yametumika.

Kumbuka pia ni wajibu wa kila mmoja aliyeokoka kuwa na Roho Mtakatifu.

Mungu atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE WAJUA?

MAKEDONIA.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mungu anaposema yeye ndiye achunguzaye “viuno na mioyo” anamaanisha nini?

SWALI: Mungu anaposema yeye ndiye achunguzaye “viuno ya mioyo” anamaanisha nini, Je! hivyo viuno ni vipi? Kama tunavyovisoma katika vifungu vifuatavyo;

Yeremia 11:20 “Lakini, Ee Bwana wa majeshi, uhukumuye haki, ujaribuye viuno na moyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu”.

Yeremia 17: 10 “Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake”.

Yeremia 20: 12 “Lakini, Ee Bwana wa majeshi, wewe wawajaribu wenye haki, waona viuno na mioyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu”.

Zaburi 7: 9 “Ubaya wao wasio haki na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na viuno Ndiye Mungu aliye mwenye haki”.

Ufunuo 2:22 “Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake;

23 nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo.

Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake”.

Ukisoma pia Mithali 23:16 , na Ayubu 31:19 inazungumzia maneno hayo hayo;


JIBU: Mara nyingine biblia inapolitaja Neno viuno haimaanishi tu hivi viuno vya miili yetu tunavyovivalia mikanda, hapana, bali viuno sehemu nyingine linatumika kumaanisha NIA au WAZO, la mtu. Mungu kabla hajambariki mtu au kumuhukumu au kumsamehe huwa anatazama vitu hivyo viwili, cha kwanza ni Moyo na cha pili ni Nia.

Kwamfano, Mungu anaweza kumsamehe mtu dhambi zake bila hata ya kuzungumza maneno yoyote kwenye kinywa chake kuonyesha anaomba msamaha, Yaani ule moyo tu wa kujutia dhambi zake, moyo wa kuugua, moyo wa kusema kosa hili sitakaa nilirudie tena, siku baada ya siku anajutia makosa yake, na hataki kuyatazama wala kuyarudia tena, hiyo tayari ni toba inayozungumza sana mbele za Mungu kuliko sala za toba elfu mtu anazoongozwa kila siku na huku hana majuto na dhambi zake.

Jambo kama hilo utaliona kwa Yule mwanamke kahaba, aliyekwenda kumlilia Yesu, utaona hakuzunguza Neno lolote lakini Bwana Yesu alimwambia umesamehewa dhambi zako. (Luka 7:37-48)

Vilevile Mungu huwa anachunguza Nia, kwa mfano wengi wetu tunamuhukumu Yuda kama ndiye aliyempeleka Yesu msalabani, lakini ukisoma pale utaona Yuda hakuwa na Nia ya Bwana Yesu kufikishwa katika mateso na kusulibiwa na ndio maana akawaomba watakapomchukua wasimtendee dhara lolote (Marko 14:44), kwani yeye lengo lake lilikuwa ni kupata pesa tu..Lakini alipoona wale watu wamevuka mipaka, mpaka kwenda kumsulibisha alijuta kwa kulia sana, hadi ikamfanya aende kujinyonga, kwa madhara aliyosababisha, Hivyo Mungu anayechunguza Nia hatamuhukumu kwasababu alimpeleka Yesu msalabani bali atamuhukumu kwa kosa lingine la kutokuwa na moyo mkamilifu kwake kama ilivyokuwa kwa mitume wenzake.

Huo ni mfano tu,

Hivyo nasi tunapaswa tuwe makini sana, usiende kuzini ukamwambia Mungu nilipitiwa, yeye hashawishiwi kwa maneno , anachunguza moyo na Nia ya mwanadamu zaidi ya fikra zetu. Hivyo tusijidanganye tuna la kujitetea mbele zake, hata Siku ile ya Hukumu (Anachunguza viuno vyetu). Halikadhalika hata ukitenda tendo la haki, huna haja ya kumwambia Mungu, kumbuka hiki kumbuka kile, yeye anajua yote (Mhubiri 5:8).

Bwana atusaidie,

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Malaika wa maji ni yupi na Je kuna aina ngapi za malaika?

JINSI MUNGU ANAVYOIPIGA NA KUIPONYA AFRIKA.

BWANA WA MAJESHI.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)

Rudi Nyumbani:

Print this post

Maana yake nini “Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko”

SWALI: Huu mstari una maana gani? Amos 9:2 “Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko”


JIBU: Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, Ni muhimu kufahamu sio kila mahali panapozungumzia Neno mbinguni katika biblia panamaanisha “mbinguni kule Malaika watakatifu walipo” Hususani katika agano la kale. Neno mbinguni pia linaweza kutumika na wapagani kumaanisha mbingu yao, kadhalika mbinguni kunaweza kumaanisha “sehemu iliyo inuka sana”.

Mtu aliyejiinua sana moyo wake katika roho anaonekana amepanda mpaka mbinguni.

Hali kadhalika sio kila mahali panalipoandikwa neno “kuzimu” katika biblia hususani agano la kale, kuna maanisha kule kuzimu, roho za viumbe walioasi zilipo!..hapana! sehemu nyingine panapotajwa neno kuzimu panamaanisha mahali pa chini sana. Kwamfano mtu aliye katika vifungo vingi vilivyomfanya awe chini sana, katika roho ni kama yupo kuzimu. (Yona na Mariamu na Hana).

Kwamfano tunaweza kusoma mistari ifuatayo ili tupate kuelewa vizuri.

Yona 2:1 “Ndipo Yona akamwomba Bwana, Mungu wake, katika tumbo la yule samaki,

  2 Akasema, Nalimlilia Bwana kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; KATİKA TUMBO LA KUZİMU NALİOMBA, Nawe ukasikia sauti yangu.

3 Maana ulinitupa vilindini, Ndani ya moyo wa bahari; Gharika ya maji ikanizunguka pande zote; Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu”

Sasa hapo Yona sio kwamba alishuka kuzimu, mahali pa wafu, hapana, bali katika mazingira ya lile tumbo la samaki alilokuwemo ndio akakufananisha na KUZIMU. Mahali pabaja mfano wa kuzimu. Na mtu anapokuwa katika mazingira hayo yanayofananishwa na kuzimu, anaweza kupandishwa juu na kutoka huko, kama Yona na Hana mama yake Samweli.

1Samweli 2:6 “Bwana huua, naye hufanya kuwa hai; Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu.

7 Bwana hufukarisha mtu, naye hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu”

Na andiko lingine ndio hilo la kwenye Amosi 9:2 “Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko”

Lakini mtu anayeshuka katika ile kuzimu halisi ya sehemu ya wafu walioasi, biblia inasema hawezi kurudi tena wala hawezi kutoka huko.

Ayubu 7:9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, Ni vivyo huyo ashukaye kuzimuni hatazuka tena kabisa.  Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena”.

Kwahiyo unaweza ukawa unapitia hali fulani katika hii dunia, ambapo mahali ulipo ni kama kuzimu, kila kona unaona giza limekuzunguka na mashaka, huoni unafuu popote, nataka nikuambie lipo tumaini kwa Kristo, maadamu bado unaishi, Bwana anaweza kukunyanyua tena na kukutoa huko Kuzimu, ulipo na kukupandisha juu, Hivyo Mwamini, omba kwa bidii na mshukuru, siku isiyokuwa na jina utaona miujiza.

Vivyo hivyo unaweza kuwa katika mahali fulani, au ukawa katika nafasi fulani na moyo wako  ukainuka sana, pengine ukajiona ni mungu-mtu, kila mtu anakuogopa, kila mtu anakuhofu au wewe ukajiona ni bora sana kuliko wengine wote wanaokuzunguka, nataka nikuambia mbele za Mungu, umejiinua na kufika mbinguni, na biblia inasema wote wajikwezao watashushwa (Luka 14:11).

Kwa maelezo marefu kuhusu  mbungini fungua hapa  >> mbinguni  ni wapi?

Hivyo mstari huo katika Amosi hauzungumzii Mbingu halisi, Malaika watakatifu waliopo, bali wala hauzungumzii Kuzimu halisi, wafu waliokufa katika dhambi walipo… Bali inazungumzia hali fulani ya maisha ambayo mtu yupo chini sana mfano wa kuzimu, na hali fulani ya maisha ambayo mtu kajiinua sana juu mfano wa mbingu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

ALIKUWAKO NAYE HAYUKO, NAYE YU TAYARI KUPANDA KUTOKA KUZIMU.

CHAPA YA MNYAMA

UJIO WA BWANA YESU.

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAJIFUNGUA.

Kuota unajifungua kuna maanisha nini?


Ndoto hii inaweza ikawa na maana mbili, maana ya kwanza ambayo ninaweza  kusema inawapata wengi, ni ile inayotokana na shughuli nyingi au mambo tuliyowahi kuyapitia, au kuyawaza, au kuyatenda mara kwa mara huko nyuma.

Biblia inasema.

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;…….”.

Hivyo sishangai kama ndoto hii atakuwa anaotwa na mwanamke, kwasababu yeye kwa sehemu kubwa katika maisha yake, amekuwa akiwaza pengine siku moja atajifungua, au hivi karibuni anakwenda kujifungua au mwengine tayari huko nyuma alishawahi kujifungua,..

Hivyo matukio kama hayo kujirudia rudia katika ndoto zake litakuwa ni jambo la kawaida sana. Kwahiyo kama wewe ni mmojawapo wa wanaoyapitia hayo, basi ipuuzie tu ndoto ya namna hiyo, kwasababu haina maana yoyote rohoni.

Lakini maana ya pili, ambayo ni ya rohoni, ni kwamba ikiwa ndoto hii umekujia kwa namna ambayo sio ya kawaida, yaani kwa uzito mkubwa sana, na unahisi kuna uzito Fulani ndani ya moyo wako, basi ujue ndoto hiyo imebeba ujumbe. Na tafsiri yake ni kuwa lipo jambo zuri au baya linakwenda kukujia, kulingana na ulichokuwa unakifanya katika maisha yako.

Tunajua sikuzote mpaka mtu anafikia hatua ya kuzaa ni wazi kuwa tayari huko nyuma alishabeba mimba kwa muda mrefu, hivyo angalia katika maisha yako ni nini umekuwa ukikibeba, na ukikisubiria, basi ujue hivi karibuni utakwenda kukiona kikijidhihirisha (kukuletea matokeo fulani). Kama umekuwa ukifanya jambo jema basi tazamia kuona matunda ya wema wako hivi karibuni.

Luka 1:30 “Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

Lakini kama wewe ni mwenye dhambi (yaani haupo ndani ya Kristo) basi jiandae hivi karibuni kukutana na matunda ya mambo maovu uliyokuwa unayafanya katika maisha yako,

biblia inasema..

Ayubu 15:35 “Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Nalo tumbo lao hutengeza udanganyifu”.

Zaburi 8:14 “Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo”

Yakobo 114 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti”.

Unaona wanachozaa sikuzote watu waovu ? Na ndio maana sehemu nyingine inasema..

Mathayo 3:10 “Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.

Hivyo jiangalie wewe katika maisha yako yote, na mambo yako yote unayoyatenda Je, ni jambo gani unakwenda kulizaa hivi karibuni? Je! ni uzima, au mauti?

Lakini habari njema ni kuwa Yesu leo anaweza kukuokoa, na kukufanya umzalie matunda mazuri, na akabatilisha mabaya yote ambayo yamepangwa mbele yako, ikiwa tu utakubali kumruhusu ayageuze maisha yako, Yeye yupo tayari kukusamehe ikiwa utakuwa tayari kutubu kwa moyo wako wote, Hivyo ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, basi uamuzi huo ni wa busara sana. Unachotakiwa kufanya ni kufungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Na Mungu peke yake atakigeuza unachokizaa kiwe chema.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Au jiunge kwa kubofya link hii>> 

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

HERODE NA PILATO, MAADUI WAWILI WAPATANA.

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Arabuni maana yake ni nini?

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA;

Mtu akikufanyia fadhila ya hali ya juu, ni wazi kuwa nafsi yako haitatulia mpaka na wewe utakapohakikisha umemrudishia naye pia fadhila..hiyo ni hali ya kawaida ya kibinadamu kabisa, hata kama hakitafikia kile alichokufanyia walau utaonyesha shukrani kwa kumwombea dua kwa Mungu.

Hata sisi tunapookoka, tunapogundua kuwa kumbe kuna mtu alitupenda upeo, kumbe kuna mtu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu na kama asingekufa leo hii sisi tungekuwa ni wa kuzimu.

Ni dhahiri kuwa kama tumeithamini fadhila hiyo ya kipekee basi na sisi ni lazima tutaonyesha kurudisha kitu Fulani kwake, ni kweli hatuwezi kumrudishia fadhila za matendo yetu mema kama yeye aliyotufanyia, kwasababu mpaka hapa tulipo tulishamkosea Mungu mara nyingi sana. Lakini fadhili tunayoweza kumrudishia ni kuupeleka Upendo wake, uwafikie na wengine, ambao bado haujawafikia, ili nao pia waokolewe kama sisi. Na hiyo ndio inayotufanya tuwahubirie injili na wengine, na kuwaombea.

Mtume Paulo alisema maneno haya;

2Wakorintho 5:14 “MAANA, UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote”;

Unaona? Vivyo hivyo na sisi, huu upendo wa ajabu wa Yesu kutoa maisha yake kwa ajili yetu sisi bure, ugeuke na kuwa deni kwetu,..Huu ndio utupe sababu ya kuwapelekea watu wengine habari njema, tusiuchukulie bure tu..

2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.
2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”.

Kama wewe umeokolewa mshukuru Mungu sana kwa neema hiyo , lakini kumbuka wapo watu wengi wanaohitaji kuokolewa kama wewe, swali tujiulize tangu tumeokoka Je viungo vyetu vimeleta faida yoyote kwa Kristo? Je kilishamleta mmoja katika neema ya wokovu au la? Kama karama yako haijawahi kufanya hivyo, badala yake imetumika kuwaburudisha tu watu, basi ujue karama hiyo ni feki, haijatoka kwa Mungu.

Hivyo kwa pamoja sote, tuufanye upendo wa Kristo kama deni kwetu. Huo utubidiishe kumtumikia Mungu, kwa karama zetu na kwa tulivyonavyo, ili neema ya Mungu iwafikie na wengine kama sisi nao pia waufurahie wokovu wa Bwana wetu Yesu Kristo.

Kilichoawafanya mitume waupindue ulimwengu kwa wakati wao, ni kwasababu kwa pamoja waliutambua Upendo wa Kristo, hivyo ukageuka kuwa deni kwao, wakamtumikia Mungu kwa vyote walivyokuwanavyo, na ndio maana na hapo wanasema Upendo wa Kristo watubidiisha, vivyo hivyo na sisi, tuugeuze Upendo huu kuwa deni.

Na Bwana atatuonekania katika maisha yetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

Rudi Nyumbani:

Print this post