Title 2020

Kibanzi na Boriti ni nini kama tunavyosoma kwenye biblia?

Kibanzi Na Boriti, kwenye biblia vinamaanisha nini?


Boriti ni kipande kikubwa sana cha mbao, kinaweza kikawa ni ki-gogo, au nguzo, au mbao yoyote pana..

Lakini kibanzi, ni kichembe kidogo sana cha mbao, kama mchanga, hata wakati mwingine kufikia kuwa kama vumbi  la mbao ambalo ni ngumu sana kuliona. Hicho ndicho  kibanzi.

Sasa Bwana Yesu alitoa mfano huo, wa picha ili kuweka msisitizo kile alichotaka kukisema, yaani katika hali ya kawaida, kama wewe huwezi kuona nguzo iliyosimama mbele ya macho yako inayokuzuia usione kabisa, utaona vipi vumbi la mbao lililo katika jicho la mwenzako?..Umeona moja kwa moja huo ni unafki..

Vivyo hivyo na sisi kabla hatujawahukumu watu, tuyachunguze maisha yetu Je! hayo wanayoyafanya Je, hayapo ndani yetu na sisi? Kabla hujamwambia Fulani acha usengenyaji, Je! na wewe si msengenyaji? Kama  sivyo basi ni heri ukae tu kimya, kwasababu mistari ya juu yake inasema, kipimo kile kile tuhukumucho ndicho tutakachokuhumiwa na sisi.

Mathayo 7:1 “Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.

2 Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.

3 Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?

4 Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?

5 Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.

Bwana atusaidie sote tuyashinde hayo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/

KAMA MMOJA TU NDIO HIVI! SI ZAIDI 153?

UNYAKUO.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Israeli ipo bara gani?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Jiunge na channel yetu ya Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/GWxBOH2GXncIc0pwVIhnch

Mistari ya biblia ya faraja.


Unaweza ukawa unapitia katika wakati mgumu, wakati wa mateso, wakati wa majaribu, wakati wa jangwa, wakati wa shida wewe kama mkristo kwa ajili ya imani yako,. Lakini nachoweza kukwambia ni kuwa biblia peke yake, ndiyo inayoweza kukupa faraja ya kweli.. Haijalishi utaambiwa maneno elfu kumi ya faraja na wanadamu, lakini ni biblia pekee ndiyo inayoweza kukupa faraja ya kweli.

Hivyo itafakari mistari ifuatayo, ni lipo jambo ambalo litakutia nguvu katika safari yako ya Imani..

Unlock the Power of crystals: Elevate Your Space with Feng Shui Essentials! Discover the Magic of Crystals for a Harmonious Home. Our store offers a curated selection of premium feng shui products, including exquisite crystals that bring positive energy and balance to your surroundings. Embrace the beauty and serenity that crystals can bring into your life. Enhance your living space with the timeless allure of crystals today!

Wafilipi 4:13 “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.

Isaya 41:10 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”.

Isaya 40:31 “bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Kumbukumbu 31: 6 “Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana Bwana, Mungu wako, yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha”.

Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo”.

1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili”.

Kutoka 15:2 “Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza”.

Kumbukumbu 20: 4 “kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi”.

2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu”.

Tembelea washirika wetu, https://www.swisswatch.is/product-category/richard-mille/ – viongozi katika viatu vya mtindo!

Isaya 12:2 “Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana Bwana YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu”.

Mathayo 6:34 “Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”.

Zaburi 27:1 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani”?

Zaburi 31: 24 “Iweni hodari, mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja Bwana”.

Zaburi 73:26 “Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele”.

Zaburi 29: 11 “Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani”.

Zaburi 23:4 “Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.

Zaburi 118:14 “Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu”.

Habakuki 3:19 “YEHOVA, aliye Bwana, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka”.

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

2Wathesalonike 3:3 “Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu”.

Luka 1:37 “kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu”.

Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.

Wafilipi 1:6 “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu”;

Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini”.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.

Jiunge na Forum ya Neno la Mungu hapa ya mada zaidi zihusuzo Faraja >> FARAJA FORUMS

Inawezekana  pia hujaokoka, lakini leo hii unataka Yesu asikupite bila kuyaokoa maisha yako. Unasema mimi na dunia sasa basi, mimi na dhambi basi..Hivyo Kama umeamua leo kumgeukia Mungu kwa moyo wako wote, yeye mwenyewe anasema, “kila ajaye kwangu sitamtupa Nje kamwe”..Kwahiyo Leo hii Yesu ataingia ndani ya maisha yako kama umeamua kweli kumfuata…hivyo kama upo tayari fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba..>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu, kwa njia ya email, au whatsapp yako basi tutumie ujumbe kwenye namba hii tukuweke : +255789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Arabuni maana yake ni nini?

Tukiachilia mbali, Eneo linaloitwa Arabuni ambalo limetajwa sana katika biblia,  .

Kama tunavyosoma katika vifungu vifuatavyo..

2Nyakati 9:14 “mbali na ile waliyoileta wachuuzi na wafanya biashara; tena wafalme wote wa Arabuni, na maliwali wa nchi wakamletea Sulemani dhahabu na fedha”.

 

Isaya 21:13 “Ufunuo juu ya Arabuni. Ndani ya msitu wa Arabuni mtalala, Enyi misafara ya Wadedani”.

 

Yeremia 25: 13 “Ufunuo juu ya Arabuni. Ndani ya msitu wa Arabuni mtalala, Enyi misafara ya Wadedani”.

 

Wagalatia 1:17 “wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa hao waliokuwa mitume kabla yangu; bali nalikwenda zangu Arabuni, kisha nikarudi tena Dameski”.

 

Wagalatia 4:25 “Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto”.

Eneo ambalo walikuwa wanaishi jamii ya watu wa kiarabu.. Au kwa jina lingine linaitwa Arabia.Tazama picha juu.


Lakini Neno hili limetajwa kwa namna nyingine, katika biblia kama tunavyosoma katika vifungu vifuatavyo

2Wakorintho 1:22 “naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu”.

 

2Wakorintho 5:5 “Basi yeye aliyetufanya kwa ajili ya neno lilo hilo ni Mungu, aliyetupa arabuni ya Roho”.

 

Waefeso 1:3 “Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu.

14 Ndiye aliye arabuni ya urithi wetu, ili kuleta ukombozi wa milki yake, kuwa sifa ya utukufu wake”.

Sasa Mungu alipotugawia ahadi zake za uzima wa milele na nyinginezo, hakutaka kutupa mikono mitupu tu hivi hivi bila uthibitisho wowote, Hivyo ili kututhibitishia kuwa ahadi zake ni kweli alitupa uhakika huo kwa kutugawia Roho Mtakatifu,  kama garantii au tunaweza kusema, kuponi, ya kuwa ahadi zake tutafikia, au atatutimizia.. Sasa hiyo garantii/kuponi  ndio inayoitwa arabuni.

Ukipokea Roho Mtakatifu basi unayo arabuni ya uzima wa milele, kama alivyowaahidia wale waliomwamini.

Ukipokea Roho Mtakatifu basi una uhakika kuwa wewe ni mbarikiwa wa Mungu, hakuna laana yoyote inayoweza kukaa juu yako.

Ukipokea Roho Mtakatifu basi maombi yako ni hakika kuwa yanasikiwa na kujibiwa mbinguni, sawasawa na ahadi za Yesu kwa wote waliomwamini.

Lakini ukiwa huna Roho Mtakatifu, na unasema umeokoka, bado mbinguni hutaenda..Kama vile maandiko yanavyosema..

Warumi 8:9 “…Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.

Hivyo kama na wewe unataka upate hii arabuni(garantii) ya urithi wa ahadi za Mungu zote za mwilini na rohoni,, basi ni sharti umpokee Roho Mtakatifu. Na mtu anampokea Roho Mtakatifu kwa kuzaliwa mara ya pili.

Mtu anazaliwaje mara ya pili?

Pale unapotubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, , na baada ya kutubu  ukawa tayari kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, sawasawa na Mdo 2:38, hapo utakuwa tayari umeshazaliwa mara ya pili.

Na moja kuwa moja, kuanzia huo wakati na kuendelea Roho anashuka ndani yako..Na unakuwa tayari umeshapokea garantii hiyo(arabuni) ya kuwa wewe ni mwana wa ahadi… Hivyo kama hutarudi nyuma utaendelea tu kuishi katika maisha matakatifu ya wokovu ya kumpendeza Mungu na kudumu katika ushirika wa Mungu..Ni uhakika kuwa hata ukifa usiku huo huo, wewe ni wa mbinguni tu mrithi wa ahadi zote za Mungu..

Hivyo kama hujaokoka, basi anza sasa kufuata hatua hizo kwa moyo wako wote..Kama unahitaji leo kumpa Yesu maisha yako basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Na ikiwa utahitaji kubatizwa usisite kuwasiliana nasi kwa namba hizi +255789001312: Ubatizo ni bure, na unafanyika pindi tu mtu anapotubu dhambi zake..Hakuna madarasa ya kupitia, wala hakuna kutoa fedha, kwasababu biblia haitufundishi kanuni hizo..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

USIFIKIRI FIKIRI.

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya “Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake?”

SWALI: Biblia inamaanisha nini inaposema “Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”


JIBU: Huu ni msemo ambao umeonekana ukipachikwa katikati ya vifungu kadha wa kadha kwenye biblia..

Kwa mfano utaona.. pale kwenye Kutoka 23:18-19 inasema..

18 Usisongeze damu ya dhabihu zangu pamoja na mkate uliotiwa chachu, wala mafuta ya sikukuu yangu usiyaache kusalia hata asubuhi.

19 Ya kwanza ya malimbuko ya nchi yako utayaleta na kuyatia ndani ya nyumba ya Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.

Ukisoma tena..Kutoka 34:25-26, utaona inasema hivi..

“25 Usisongeze damu ya sadaka yangu pamoja na mkate uliotiwa chachu; wala hiyo sadaka ya sikukuu ya pasaka haitasazwa hata asubuhi.

26 Vitu vya kwanza vya malimbuko ya nchi yako utavileta na kuvitia ndani ya nyumba ya Bwana Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake”.

Ukirudi tena kwenye Kumbukumbu 14:21 nayo pia utaona ikisema.

“Msile nyamafu yo yote; waweza kumpa mgeni aliye ndani ya malango yako, ili apate kula; au kumliza mtu wa mataifa; kwa kuwa wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mamaye”.

Sasa pale anaposema, usimtokose mwana-mbuzi, katika maziwa ya mama yake, anamaanisha kumchemsha mtoto wa mbuzi, kwa maziwa ya mama yake, yaani badala ya kumchemsha kwenye maji, wewe unachukua yale maziwa anayoyanyonya kutoka kwa mama yake na kumchemshia nayo..

Kwa namna ya kawaida ni kitendo kisicho cha kiungwana chenye ukakasi kidogo, hata kwako wewe unayesikia eti?..Utajiuliza ni kwanini ufanye hivyo? Kwani hakuna maji ya kumchemshia, au kitu kingine mpaka utumie maziwa, tena yale yale ya mama yake? Ni sawa na nguruwe aliyezaa mtoto, halafu unampa mtoto wake mwenyewe amle kama chakula chake..sasa hiyo ndio picha iliyopo hapo.

Ni kitendo kinachoonyesha unyama si unyama, ukosefu wa nidhamu..?

Ni utaratibu na mfumo wa kipagani ambao ulikuwa unafanyika na watu wa mataifa wasiomjua Mungu, walikuwa wanafanya hivyo kwa sababu za kishirikina, ni kama mila zinazoendelea siku hizi, hivyo Mungu aliwaonya wana wa Israeli wasifanye mambo kama hayo, kwasababu ni machukizo mbele zake, ni Utaratibu ambao hauna tofauti na ule wa kuwapitisha watoto kwenye moto, (soma 2Wafalme 21:6, 2Wafalme 16:3).

Hata sasa, wengi wetu tunafanya kafara kama hizo rohoni?.

Tunamtolea Mungu dhabihu zilizochanganyikana na mambo ambayo Mungu ameyakataza, tunafanya mambo kama watu wa mataifa. Tunamsifu Mungu na huku vinywa vyetu vimejaa matusi, na masengenyo, chuki na visasi, tunamtolea Mungu na huku biashara zetu ni haramu, tunahudhuria kanisani lakini tunaendelea kudumisha mila zetu za kishirikina, hali kadhalika tumeokoka lakini heshima kwa mzazi haipo, na heshima kwa Watoto wetu haipo (hiyo yote katika roho ni sawa na kumtokosa mwanambuzi katika maziwa yake) N.k.

Bwana atusaidie, tuzishike amri zake na tumpendeze yeye.

Bwana atuokoe na kutubariki..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

USITUMAINISHWE NA MANENO YA UONGO.

YESU KWETU NI RAFIKI

Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao.

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

CHOCHOTE UMFANYIACHO KRISTO KINA THAMANI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Imani ya mitume ipo katika maandiko?

Imani ya mitume (Apostle’s creed), inapatikana wapi kwenye biblia?


Imani ya mitume ambayo unaisikia mara kwa mara ikikiriwa katika baadhi ya madhehebu hususani Katoliki, Lutherani, na Anglikana, haipo mahali popote katika maandiko, na wala haikuwahi kukikiriwa na mitume wa Kristo sehemu yoyote.

Imani hii, ilikuja kuaandikwa miaka mingi mbeleni(zaidi ya miaka 300),baada ya mitume kuondoka, waliiandika wakizingatia kiini cha wazo kuu la mitume walichokuwa wanaamini  katika maandiko.

Na kimsingi imani hii ipo kimaandiko. Hivyo mtu kuikiri hakuna shida, kwasababu haimpotezi katika misingi ya imani ya biblia.

Inasema hivi.

Namwamini Mungu Baba mwenyezi, muumba wa mbingu na nchi, na Yesu Kristo, mwana wake wa pekee, Bwana wetu.

Aliyechukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Akazaliwa na bikira Mariamu. Akateswa zamani za Pontio Pilato. Akasulubiwa. Akafa. Akazikwa.

Akashuka mahali pa wafu. Siku ya tatu akafufuka. Akapaa mbinguni. Ameketi mkono wa kuume wa Mungu Baba mwenyezi. Kutoka huko atakuja kuwahukumu walio hai na wafu.

Namwamini Roho Mtakatifu, kanisa takatifu lililo moja, ushirika wa watakatifu, ondoleo la dhambi, ufufuo wa wafu na uzima wa milele.

Amina.

Jambo la kuzingatia ni kuwa, ukiikiri/usipoikiri sio tiketi ya wewe ni mkristo, au utakwenda mbinguni, huu ni utaratibu tu au mapokeo tu ya baadhi ya wakristo. kitachokufa wewe uwe mkristo, ni kuamini, kutubu na kuoshwa dhambi zako kwa damu ya YESU Kristo, kwa njia ya ubatizo( sawasawa na Matendo 2:38).

Na ubatizo sahihi wa kimaandiko ni ule wa kuzamwishwa katika maji mengi,(Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo.

Hivyo kama utahitaji upate ubatizo huu sahihi.  Na Kama utapenda tuwe tunakutumia masomo  ya biblia  kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

Je mtu akifa anakuwa hana dhambi tena?

KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Adamu alikuwa na mwanamke mwingine anayeitwa Lilith?

Je! Adamu alikuwa na mwanamke mwingine anayeitwa Lilith?


JIBU: Biblia imetupa majibu kama ifuatavyo..

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa MUNGU ALIMWUMBA, MWANAMUME NA MWANAMKE ALIWAUMBA.  

28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”.

Huo ni mstari wa kwanza kabisa unaozungumzia uumbaji wa mwanadamu katika biblia, hakuna mstari mwingine kabla ya huu.. Na unasema Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke. (maneno hayo mawili yapo katika umoja.). Na haijasema Mungu alimwumba Mwanaume na wanawake.. wala haijasema Mungu alimuumba mwanamke na wanaume. 

Kwahiyo hakukuwa na mwanaume Zaidi ya Adamu, na wala hakukuwa na mwanamke mwingine Zaidi ya Hawa katika uumbaji.

Jambo linalowachanganya wengi ambalo ndilo limezua swali hili, ni kuhusu mke wa Kaini, kwamba Kaini alitolea wapi mke?

Kwanza kabisa Ni muhimu kufahamu kuwa Adamu na Hawa, walizaa Watoto wengine wengi wakike na wa kiume baada ya Habili na Kaini. Watoto wa Adamu hawakuwa wawili tu, bali wengi.

Mwanzo 5:4 “Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa”.

Kwahiyo miongoni mwa hao Watoto wa kike aliowazaa Adamu, mmojawao ndio alikuwa mke wa Kaini, na Kaini na mkewe walizaa Watoto, na watoto wao walizaa Watoto, na wajukuu zao pia walizaa..Na wakati huo watu walikuwa na uwezo wa kuishi mamia ya miaka.

Kwahiyo ni uongo kusema kuwa Adamu alikuwa na mke mwingine tofauti na Hawa.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

BUSTANI YA NEEMA.

 

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

SALA YA BABA YETU/SALA YA BWANA.

Sala ya Baba yetu/ Sala ya Bwana.


Sala hii inapatikana katika sehemu kuu mbili kwenye biblia..

  1. Ya kwanza ni Mathayo 6:9-13 Inasema.

“9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.

11 Utupe leo riziki yetu.

12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.

13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]

 

       2.   Na ya pili ni  Luka 11:1-4

“1 Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.

2 Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]

3 Utupe siku kwa siku riziki yetu.

4 Utusamehe dhambi zetu, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu]”.

Sala hii inachukuliwa kirahisi rahisi na watu wengi, kama ni sala kutamka tu, sekunde nne,,tano umemaliza..

Lakini sivyo ambavyo Bwana Yesu alimaanisha pale.. Kumbuka wanafunzi wake walipomuuliza Bwana tufundishe jinsi ya kusali, walikuwa wanamaanisha kweli kufahamu kwa undani jinsi ya kusali, Walikuwa wanataka kujua siri ya Bwana Yesu kujibiwa maombi yake na Mungu ni nini?, walikuwa wanatamani kujua siri za kufanya maombi yao yawe na nguvu mbele za Mungu..  Walikuwa wanahitaji muongozo sahihi.

Hivyo usifiri waliambiwa watamke maneno yale tu machache ni tayari wameshasali, na sala zako zimeshasikiwa, hapana kama na wewe ulikuwa na mtazamo huo kama mimi..Basi leo ujue jinsi ya kusali mbele za Mungu kama Bwana Yesu alivyotuelekeza/

Ni kwa namna gani tusali sala ya Baba yetu/sala ya Bwana ipasavyo?

Kwa ufupi ni kuwa, maneno yale yalikuwa kama mwongozo tu, kama Ilani, kama ramani ya mtu anaposalia apite wapi na wapi,..Ili maombi ya Mtu yawe yana hoja za nguvu na mashiko, yafuate vigezo vipi na vipi.

Unapoomba sio tu, kuzungumza maneno ilimradi maneno tu, muda uende, fahamu, kanuni za uombaji, na kanuni zenyewe ndio hizo Bwana Yesu alizozihorodhesha hapo. Kipengele kimoja hadi kingine ni eneo la kuomba, kwa mfano anapoanza kwa kusema, Baba yetu uliye mbinguni..Hicho ni kipengele kimojawapo kama utangulizi wa maombi yako yafikije kwa Baba..

Sasa kwasababu somo hili tulishaliandika kwa urefu..Fungua hapa, ili uanze sasa kupitia kipengele kimoja hadi kingine, na mwisho wa somo hilo utakuwa tayari sasa umefudhu kuwa mwombaji mwenye nguvu katika ulimwengu war oho sawasawa na maagizo ya Yesu.

Fungua sasa hapa usome..>>>>>> ZIFAHAMU HOJA SABA ZENYE NGUVU MBELE ZA MUNGU.

Bwana akubariki.

Masomo Mengineyo:

RABI, UNAKAA WAPI?

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

https://wingulamashahidi.org/2019/05/13/zifahamu-huduma-kuu-10-za-shetani-duniani/

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

HUDUMA YA WALE MASHAHIDI WAWILI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, libarikiwe. Nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko.

Tunajua kuja kwa Yesu mara ya kwanza, kulibeba siri nyingi za kuja kwake mara ya pili, kwa mfano wakati ule kabla ya Herode, kutaka kumuua Yesu pindi alipozaliwa, kulitangulia kwanza sensa kubwa kwa watu wote wa ulimwengu, ambayo ilimlazimu kila mmoja aende kwenye mji wake aliozaliwa ili ahesabiwe huko..Na ndivyo itakavyokuja kuwa kipindi kifupi kabla ya Yesu kurudi mara ya pili duniani, mpinga-Kristo ataleta utaratibu mpya wa watu wote kuhakikiwa, mfumo huu mpya ndio ile  inayojulikana kama chapa ya Mnyama ambao utamlazimu kila mmoja awe nayo, kama mtu hana basi hataweza kuuza au kununua au kufanya biashara, au kuajiriwa mahali popote..kwa urefu wa somo hilo tutumie ujumbe inbox tukutumie ..

Lakini pia kulikuwa na jambo lingine, ambalo lilichochea kwa haraka sana dhiki kutokea pale Yerusalemu pindi tu Yesu alipozaliwa. Na jambo lenyewe, lilikuwa kwa wale Mamajusi kutoka Mashariki.

Sasa ukiangalia pale, utagundua habari ya kuzaliwa kwa Yesu ilikuwa imeshajulikana hata kabla ya baadha ya watu pale Israeli kujua, utaona kulikuwa na wale wachungaji kule makondeni waliotokewa na malaika na kuambiwa wamfuate mtoto..Ni kweli walienda na kushuhudia waliyoambiwa, na pengine baaada ya pale walisambaza taarifa za kuzaliwa kwa watu wengi vijijini na mijini, lakini habari zao hazikuwa na nguvu sana, wala hazikuleta mabadiliko yoyote kwa Israeli au kwa Herode, Vivyo hivyo, walikuwepo wakina Simoni na Hana, ambao Mungu aliwashuhudia kuwa huyu ndiye mwokozi na mfalme, pengine nao walitangaza, lakini taarifa zao pia hazikufika mbali  sana.

Walikuwepo wakina Zekaria kuhani na mke wake Elisabeti, ambao walitangaza habari za Yesu na Yohana, ambazo kwa habari ya Yohana biblia inasema zilijulikana katika mji wote ule lakini bado hazikuwa na mashiko sana..Lakini tunaona kulikuwa na kundi lingine la watu, toka mbali sana, lililoleta habari,..Hilo halikuwa la watu  wa pale Israeli, bali lilitoka mbali sana, ndio wale mamajusi wa Mashariki, walioina nyota yake na kufunga safari mpaka Israeli, na walipofika moja kwa moja wakamuuliza  mfalme Herode, yupo wapi mfalme wa Wayahudi aliyezaliwa..Sasa kwa taarifa hizo Biblia inatuambia sio tu Herode zilimfadhaisha, bali na Israeli nzima. Hapo ndipo pakawa mwanzo wa sura nyingine kwa taifa la Israeli.

Mathayo 2:1 “Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,

2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.

3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.

4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi”?

Sasa kama tunavyoijua habari kilichofuata pale ni Herode kwenda kuwaua watoto wote waliokuwa Bethlehemu wakati ule (kukawa na kilio kikuu Bethlehemu).

Mathayo 2:18 “Sauti ilisikiwa Rama, Kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, Asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako”.

 Lakini kabla ya kuwaua, Mama na mtoto walihamishwa, na kupelekwa Misri kuikwepa dhiki.

Sasa, katika siku za mwisho, mambo kama hayo hayo yataenda kujirudia,. Baada ya Unyakuo kupita, dunia itakuwa imebakiwa na miaka 7 tu mpaka iishe kabisa, katika kipindi hicho, Mungu atawanyanyua watu watu wawili ambao watawatenga kwa lengo moja tu, la kwenda kuwatolea Unabii Israeli, juu ya kurudi kwa Kristo ulimwenguni kutawala kama mfalme wa wafalme…ndio mfano wa wale mamajusi wa Mashariki. (Na Huo ndio utakuwa wakati wa neema kuhamia Israeli)

Watu hawa ndio wale mashahidi wawili tunaowasoma katika Ufunuo 11, Watahubiri pale Israeli, kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu kama biblia inavyotuambia,..Na wakati huo mpinga-Kristo, atawasikia, na hiyo ndio itakuwa kama alert yake, kuwa mwisho umefika.Atakachofanya ni kufanya vita na hawa watu, na kuleta dhiki Israeli, na duniani kote, hiyo ndio ile dhiki kuu,

Ufunuo 11:3 “Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia.

4 Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi.

5 Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa.

6 Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo.

7 Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua”.

Lakini kabla hajafanikiwa, lipo kundi dogo ambalo litasikia injili ya wale mashahidi wawili, na kuondoshwa na kwenda kufichwa, ndio wale wayahudi 144,000, hao watafichwa na dhiki kuu haitawapata (Ufunuo 7&11).

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.

Unaona, Lakini wayahudi wengine wote, waliosalia duniani, pamoja na wale watu ambao hawakuipokea chapa ya mnyama, Watapitia dhiki kubwa isiyokuwa na mfano tangu dunia kuumbwa.

Injili inayohubiriwa sasa hivi haiwezi kutikisa au kuleta matatizo duniani, ila kipindi cha injili za hawa manabii wawili watakaposimama, na kutoa unabii pale Israeli, na kwa yale mapigo yaliyoorodheshwa pale ndipo ulimwengu utakapojua rangi halisi ya mpinga-Kristo.

Hawa watu pengine tayari wapo duniani, kwasababu dalili zote zinaonyesha.. Lakini mpaka hayo yote yatokee sisi tuliookoka ambao tumejiweka tayari, tutakuwa siku nyingi tumeshakwenda utukufuni (kanisa halitashuhudia mambo hayo ya manabii wawili). Jiulize na wewe ndugu ikiwa unyakuo utapita leo, wewe utakuwa wapi? Utajisikiaje kuona wenzako wapo mbinguni, wanaona vitu ambavyo jicho halijawahi kuona, na wewe bado upo hapa duniani, kwenye dhiki za mpinga-Kristo, ukizingatia ulihubiriwa injili mara nyingi na hukutaka kusikia?..

Je! bado unadanganywa na manabii wa uongo? Je bado, unapumbazwa na ulimwengu huu unaopita, Je! bado unasita sita kwenye mawazo mawili. Tubu kama bado hujafanya hivyo, ukabatizwe, dunia hii ipo ukingoni. Hatuna muda mrefu sana.?.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

USHIRIKINA NA MADHARA YAKE.

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)

Mhubiri 7:17 “Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwani ufe kabla ya wakati wako?

Mstari huo haumaanishi kuwa uwe mwovu kiasi, hapana, uovu ni uovu tu, na una hukumu, Uwe unatenda dhambi nyingi au chache, ukifa utahukumiwa na jehanum utaenda..

Lakini kinachomaanishwa, hapo ni kuwa upo uovu unaozidi ambao, unaweza kukusababishia uondoke hapa duniani kabla ya siku zako,..Na aina nyingine ya uovu huu ni ule unaendekezwa kwa muda mrefu, pale unapojua madhara yake lakini hutaki kuacha.

Tengeneza picha unafanya kazi ya ujambazi, wa kuua watu kisa mali, unategemea vipi usipigwe risasi siku moja na polisi?

Wale wahalifu waliosulibiwa na Yesu pale msalabani, walijua kabisa yale yamewapata kwasababu ya makosa yao ya uuaji na wizi, na ndio maana mmojawao akasema.

Luka 23:41 “Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa”.

Au unasafirisha madawa ya kulevya, kimataifa, unategemea vipi usikamatwe na kunyongwa? Au unaiba mali za watu na umeonywa mara nyingi auche lakini husikii unategemea vipi usichomwe moto?

Au unamtukana Mungu unategemea vipi uhai wako usifupishwe? n.k n.k.

Au unauchukua utukufu wa Mungu kupita kiasi unategemea vipi Mungu asikuondoe, kwasababu yeye mwenyewe anasema, mimi ni Mungu mwenye wivu. Mtazame Herode alifanya jambo kama hilo, na Mungu anampiga saa ile ile na chango.

Matendo 12:21 “Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao.

22 Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu.

23 Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho”.

Huo ni mifano michache ya maovu yanavuka mipaka, au yanayoendekezwa kwa muda mrefu. Umekuwa mzinzi au uasherati, na unajua kabisa tabia hiyo haimpendezi Mungu lakini bado unaendelea kufanya hivyo, siku baada ya siku, hapo unajitafutia mwenyewe Mungu kukupiga na janga la Ukimwi, na kufa kabla ya siku zako.

Mhubiri 7:17 “Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwani ufe kabla ya wakati wako”?

Hivyo lililo la msingi, ni kujiepusha na uovu kabisa, kwasababu ouvu wowote uwe hata kama huna adhabu hapa, lakini kule utakutana nayo. ambayo ni ziwa la moto.

Warumi 2:5 “Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu”,

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

Yuko mwenye haki apoteaye katika haki yake.

Huyu Azazeli ni nani tunayemsoma katika(Walawi 16:8)

Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.’

Kama unaishi, basi unayo kila sababu ya kumshukuru Mungu, hata kama huna shilingi 10 mfukoni mwako, unazo kila sababu za kumshukuru Mungu.

Kwasababu dakika hii tunayozungumza, wakati wewe unaumwa kichwa tu!..yupo mtu ICU, kapoteza fahamu, yupo mwingine kalazwa unaugua sana. Na wakati pengine wewe upo kitandani umelazwa, ukitafakari matatizo unayoyapitia, kuna mwingine sehemu nyingine ndio yupo katika hatua ya kukata roho.

Wakati wewe hujala tangu asubuhi, yupo mwingine tangu jana hajala kabisa. Wakati wewe unao wazazi na ndugu, yupo mwingine hana hao, yupo peke yake..

Wakati wewe macho yanakusumbua (unavaa miwani), yupo mwingine hana macho kabisa. Wakati unatembea kwa kuchechemea, yupo mwingine hata hiyo miguu hajawahi kuwa nayo. 

Wakati wewe huna fedha wala mali, lakini unao uhuru wa kuamka asubuhi na kwenda unapotaka, wapo wengine sasahivi wamefungwa magerezani na tena kwa miaka mingi, hawana uhuru kama ulionao wewe, wanatamani wangeupata hata walau kwa siku moja tu, lakini hawana… 

Wakati wewe leo siku yako imeenda vizuri, wapo wengine dakika hii hii wapo misibani, wameamka na taarifa za misiba, wanazika wapendwa wao, watu wao wa thamani na wa muhimu. Na sio kwamba wamemchukiza Mungu ndio maana yamewapata hayo hapana! wengine ni watumishi wa Mungu wa thamani kabisa mbele zake, lakini ni wagonjwa, wengine wamefungwa, wengine wametengwa, na wengine hata hawana chakula n.k Lakini wewe hupitii hayo mazito kama ya kwao..Tafakari mara mbili!!..Mshukuru Mungu wala usiwe mtu wa kulalamika kabisa!.

Kitendo cha wewe kuimaliza siku unaishi, huo tayari ni muujiza mkubwa sana. Hivyo katika hali yoyote ile uliyopo, maadamu unao uzima mshukuru Mungu. Siku zote usijilinganishe na yule aliyenacho, bali jilinganishe na yule asiyenacho, ndipo utakapokuwa na kila sababu za kumshukuru Mungu. 

Tena mshukuru Mungu kwa kumwimbia, kumshangilia na kumtolea. Unapofanya hivyo, unaonyesha kumheshimu Mungu na kutambua uwepo wake katika maisha yako. Na pia ni mapenzi ya Mungu sisi tumshukuru yeye.

1Wathesalonike 5:17  “ombeni bila kukoma;  shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.

 

Wakolosai 3:15 “…tena iweni watu wa shukrani”.

Siku hizi za kumalizia, shikilia imani kwa nguvu zaidi, kamwe usiruhusu, taabu za dunia kukukatisha tamaa, Mwisho upo karibu sana.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JIOKOE WEWE NA NYUMBA YAKO.

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

YAKINI NA BOAZI.

BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Rudi Nyumbani:

Print this post