Siku moja nikiwa njiani nilikutana na mama mmoja mwenye mtoto, akaniomba shilingi elfu moja apande gari aelekee nyumbani kwake chanika, basi kwa kuwa hiyo pesa nilikuwa nayo nikampa, lakini baadaye kidogo, nilipanda gari, nikasahau kuwa sikuwa na hela nyingine yoyote ya cash mfukoni, tukiwa safarini kondakta, akaniomba nauli, nikajisachi sina pesa, ila ninayo kwenye simu, nikamwambia kondakta sina pesa hapa, naomba tukifika kituoni, nikatoe nikupe, lakini kondakta akaonekana kama sio mwelewa akadhani kama natumia ujanja tu ili nisimpe nauli yake..
Wakati naendelea kufikiria, na huku nikiangalia safari yangu haiishii mwisho wa kituo, nitashukia njiani hata nikienda kutoa atakuwa radhi kunisubiri?,.kulikuwa ni kijana mmoja anaonekana kama maskini, akatoa shilingi elfu moja akanipa, akaniambia chukua hii kondakta atakusumbua, nikamwambia ninayo nauli wacha tu tufike kituoni nitampa, lakini alinishurutisha kuichukua ile hela.
Nikakaa nayo kwa muda, nikitafakari, nikawa sina jinsi baadaye kidogo nikampa yule konda na yule kijana akashuka kwenye gari. Nikapata somo, wakati nadhani wenye shida ndio wanahitaji msaada, kumbe hata wewe usiye na shida utahitaji msaada ule ule kama wa yule mwenye shida.
Mama yule alikuwa na haja ya sh. Elfu moja, muda mchache baadaye uhitaji huo huo ulinigeukia mimi, japokuwa nilikuwa nayo. Ndugu yangu, utatembea, na gari lako, utatembea na mabilioni yako benki, utatembea na afya yako nzuri, lakini kamwe usiache kuwasaidia wenye uhitaji, kwasababu uhitahitaji ule ule wakati Fulani utaupitia hata wewe isipokuwa tu katika maumbile mengine.
Katika utajiri wako huo huo, unaweza ukafa njaa, kama tu vile yule mtu asiye na chakula kabisa, katika afya yako hiyo hiyo unaweza ukasumbuliwa na magonjwa kama tu mtu yule aliyelazwa pale muhimbili, katika nyumba yako nzuri, unaweza kulala nje kama tu yule mtu alalaye mabarazani, Vilevile katika elimu yako kubwa, hiyo hiyo unaweza kuwa mjinga sawa tu na yule ambaye hajasoma kabisa. Kamwe usifikirie kwasababu umeshapata kitu Fulani, ndio tayari umeepukana na tatizo hilo, ambalo watu wengine wanalipitia kwa kukikosa hicho. Lipindue hilo wazo kuanzia sasa.
Bwana atusaidie tujifunze unyenyekevu kwa watu wote, na kusaidiana sisi kwa sisi, kwasababu biblia inasema.
Mhubiri 1:6 “Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake.
7 Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; huko iendako mito, ndiko irudiko tena”.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Mhubiri mmoja maarufu huko India, siku moja alionyeshwa maono, anasema alipokuwa anakwenda katika ziara zake za kuhubiri katika kijiji kimoja, ilikuwa ni desturi yake kukutana na baadhi ya wenyewe wa maeneo hayo nyumbani kwao na kuzungumza nao, Sasa anasema alipokuwa anakaribia nyumbani kwa mwanamke mmoja aliyemfahamu, yule mwanamke alipomwona anaingia uwani mwake, akatoka jikoni moja kwa moja kwenda kukutana naye, na kabla hata hajamuamkia vizuri, muda huo huo alimwangukia magotini kwake, akaanza kulia. Wakati muhubiri huyu anafanya jitahada za kumwinua, amuulize shida yake, muda huo huo anasema alimwona Bwana Yesu amesimama pembeni yake, akimwangalia, kisha kitambo kidogo akamwona anamkaribia huyu mwanamke aliyekuwa Analia, akaenda kwenye shavu lake la kushoto, na kuweka mikono yake, na kukinga machozi yake, mpaka yalipojitengeneza kama kibwawa.
Na ghafla akamwona Bwana Yesu akipaa mbinguni, na yeye yupo naye, akafika sehemu nzuri sana, ambapo kwa mbele aliona kitu kama sanduku la agano limewekwa, kisha akamwona Bwana Yesu akiyamimina machozi ya yule mama juu ya sanduku lile la agano. Kisha akaanza kumwombea kwa Baba, kwa kuuugua sana na kwa machozi mengi.. Aliomba pale kwa kitambo, mpaka ikasikika sauti kama ya radi ikisema, AMESIKIWA. Anasema Hapo ndipo Bwana Yesu alipoacha kuomba. Akageuka akamwangalia huyu mhubiri, akamwambia mwambie binti yangu, maombi yake manne aliyokuwa anamwomba Mungu yamesikiwa.
Na dakika hiyo hiyo alijikuta amesimama karibu na yule mwanamke, kisha akamwinua na kumweleza alichoonyeshwa, yule mwanamke akaruka ruka kwa kuraha na kicheko kwa kujibiwa kule.
Kwanini, nimeandika ushuhuda huo, nikwasababu, biblia inasema machozi ya watakatifu yanathaminiwa sana na Mungu, jambo ambalo watakatifu wengi, pengine hawalijui, wanadhani kulia kwao ni bure, Si kweli, Mungu anayakusanya machozi yetu na kuyahifadhi katika chupa, biblia inasema hivyo;
Zaburi 56:8 “Umehesabu kutanga-tanga kwangu; Uyatie machozi yangu katika chupa yako; (Je! Hayamo katika kitabu chako?)
Umeona Machozi yetu kwa Bwana, yanatiwa katika chupa, kama vile divai nzuri inavyotunzwa katika viriba vipya. Na wakati huo huo bado yanaandikwa katika kitabu cha Mungu cha ukumbusho. Kaka/Dada Umekuwa ukilia kwasababu ya dhiki unazopitia kutokana na Imani yako, kumbuka kuwa Mungu anasikia, umekuwa ukilia kwasababu ya misiba iliyokukuta hivi karibuni Mungu anasikia, kwasababu ya magonjwa yasiyotibika, Mungu anasikia, Kwasababu ya injili Mungu anasikia na kuyatunza hayo machozi kama vile alivyoyatunza ya akina Paulo.
Matendo 20:19 “nikimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, na kwa machozi, na majaribu yaliyonipata kwa hila za Wayahudi;
20 ya kuwa sikujiepusha katika kuwatangazia neno lo lote liwezalo kuwafaa bali naliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba”,
Unapaswa ukumbuke kuwa huduma ya Bwana wetu Yesu Kristo ya kutuombea haikuishia tu alipokuwa duniani, hapana, bali bado inaendelea hadi leo hii mbinguni, biblia inasema hivyo;
Waebrania 7:25 “Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee”.
Hivyo usiogope ni nini unapitia leo, wala usikate tamaa, kumbuka Yesu, faraja yetu yupo. zidi kumtumaini yeye na kumtegemea yeye, kwasababu daima yupo na wewe, kukusaidia, mkono wake hautakuacha kamwe.
Hakika sifa na heshima, na utukufu, ni kwa Bwana wetu YESU KRISTO milele na milele,
Amen.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
SWALI: Naomba kujua tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni ipi ?, kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 7:1
2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na UCHAFU WOTE WA MWILI NA ROHO, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.
JIBU: Ili tuwe wakamilifu kwa kiwango cha kuweza kuzikaribia ahadi za Mungu, Tujue kuwa Mungu anataka tuwe watakatifu kote kote yaani Mwilini na rohoni.
Sasa hapo anaposema tujitakase na Uchafu wote wa mwilini. Anamaanisha kuwa tujiweke mbali na dhambi zote zinazozalika katika miili yetu. Mfano wa dhambi hizi ni kama vile, uzinzi, ulevi, wizi, uvutaji sigara, utukanaji, uvaaji mbovu, kama vile vimini na suruali kwa wanawake, kujichubua, kujipaka make-up, kutoa mimba, kuvaa milegezo, kujichoraji tattoo, na ushoga, utumiaji wa madawa ya kulevya na mambo mengine yote yanayofanana na hayo, ambayo asili yake ni mwilini.
Na pale aliposema tuweke kando Uchafu wa rohoni, Anamaanisha dhambi zote zinazotoka ndani ya mtu, ambazo hazihusiani na mwili moja kwa moja, mfano wa dhambi hizi ni kama vile, wivu, hasira, tamaa, mawazo mabaya, unafki, uchoyo, husuda, fitna, majigambo, kiburi, ibada za sanamu, uongo. Hizi ni dhambi ambazo zinazalika ndani, na Mungu anazichukia sana, kama vile tu anavyozichukia zile zinazozalika katika mwili.
Hivyo tujue kuwa Mungu anaangalia kote kote, Kuna watu wanadhani kuwa Mungu anaangalia roho tu, hatazami mwili. Ndugu, mwili wako unathamani sawa na roho yako mbele za Mungu, kwasababu siku ile ya mwisho si roho yako tu itaokolewa, bali hata na mwili wako pia (kasome biblia utalithibitisha hilo). Hivyo mtukuze Mungu katika mwili wako, usidanganywe na mafundisho ya manabii wa Uongo, wanaokuambia Mungu anatazama roho haangalii mwili. Hizi ni nyakati za mwisho, Tii Neno la Mungu Zaidi ya maneno ya mwanadamu. Kwasababu hilo ndilo litakalokutetea siku ile, na hilo ndilo litakalokuhumu siku ile. Neno la Mungu ni upanga. Liogope sana.
Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?
Jibu: Kuna hatari kubwa sana ya kulihubiri Neno isivyopaswa, Ni vizuri kulielewa Neno vizuri kabla ya kulifundisha.. Leo nitakuambia ni kwanini.
Miaka ya nyuma nikiwa bado ni mchanga katika Imani, nilikuwa natamani sana kuhubiri, kwasababu tu nilikuwa naona watu wanahubiri.. Hivyo na mimi, nilikuwa na shauku ya kuhubiri, hata ikiwezekana kuielezea biblia yote,. Hivyo hiyo ikanifanya, nisiwe na muda mwingi wa kulitafakari Neno, wala kulielewa sana wala kulichimba kwa undani, badala yake nilishika tu biblia na kuhubiri kwa jinsi nilivyolielewa Neno, nikiamini kuwa kila nitakachokisema kitakuwa ni cha Roho Mtakatifu!.. kumbe sikujua nilikuwa nafanya jambo la hatari sana kwangu.
Siku moja niliota ndoto nimekaa kwenye kiti, kama sehemu ya dining hivi, halafu chini ya miguu yangu kuna kama sufuria inatokota maji, na miguu yangu ilikuwa ndani ya hayo maji ila nilikuwa sijui kama miguu yangu ipo kwenye hayo maji ya moto tena yanayotokota kabisa, kwasababu nilikuwa sisikii maumivu yoyote. Baada ya muda kukaja kama sahani mbele yangu ambayo ilikuwa na mchemsho wa nyama, ilipokuja ile sahani nikawa naanza kuzila zile nyama, zilipopungua nikawa kama nazivuta nyingine kwa chini, zinakuja juu ya hiyo sahani kubwa iliyopo mbele yangu..
Halafu baada ya muda wakaja watu Fulani mbele yangu ambao huwa nawahubiria..nikawa nawapa na wenyewe zile nyama wale…wakawa wanakula huku wanashukuru, wote tukawa tunafurahia mlo.. wakati hilo jambo linaendelea, nikajikuta naitazama miguu yangu, kumbe zile nyama nilizokuwa nakula na kuwalisha wengine zilikuwa ni nyama kutoka kwenye miguu yangu, hivyo zilivyokuwa zinazidi kwenye ile sahani ndivyo nilivyokuwa naimaliza miguu yangu. Baada ya hapo nikashtuka kutoka usingizini!, nikiwa na hofu!
Nikiwa kitandani natafakari maana ya hiyo ndoto!, Roho Mtakatifu akazungumza na mimi, na kuniambia… Ndivyo ninavyojimaliza mwenyewe kwa kuwalisha watu wake chakula kinachotoka katika akili zangu badala ya kutoka kwake!.
Tangu siku hiyo nikaacha! Kukimbilia kuhubiri kabla ya kuhakikisha kuwa jambo hilo halitoki katika akili zangu bali linatoka kwa Bwana. Nikajifunza kama jambo sijalielewa vizuri katika maandiko nitangoja mpaka nilielewe ndipo niwafundishe wengine!.. Nisije nikawalisha watu nyama kutoka katika mwili wangu mwenyewe.. Mwisho wa siku mimi ndiye nitakayepata madhara wa kwanza kabla ya wao!..
Hivyo Bwana alinionyesha hatari hiyo na tahadhari yake, na nikamshukuru sana mpaka leo, nazidi kuwa makini..
Hivyo ndugu!.. kamwe usihubiri, wala kufundisha wengine, jambo ambalo wewe mwenyewe hulielewi vizuri… ukifanya hivyo katika roho unajimaliza mwenyewe kabla ya kuwamaliza wale unaowafundisha.. Usiwe na haraka na utumishi!, bali keti chini kwanza kumtafuta Mungu, na kujifunza mambo kwa kina!
Jambo moja lisilojulikana na wengi ni kufikiri kuwa jambo la kwanza linalompendeza Mungu ni sisi kuhubiri!.. la! Nataka nikuambie jambo la kwanza linalompendeza Mungu ni sisi kukaa kujifunza(kuwa wanafunzi wake). Ndio maana ilibidi awaweke mitume wake chini ya madarasa kwa miaka mitatu kabla ya kuwatuma..
Jambo hili linawafanya wengi wairuke hatua ya kuwa wanafunzi wa Yesu.. vile vile inawafanya waruke kanuni ya vigezo vya kuwa mwanafunzi ambavyo Bwana Yesu alivisema katika…
Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.
Wengi tunairuka hii hatua, na kutaka kuwa waalimu, kabla hatujawa wanafunzi!..kumbuka huwezi kuwa mwanafunzi kama hujajikana nafsi, wala kuuchukua msalaba wako. Siku zote kumbuka hilo! Huwezi kuwa mwalimu kwa wengine kama wewe hujapitia uanafunzi..na huwezi kuwa mwanafunzi kama hukujikana nafsi na kubeba msalaba wako kumfuata Yesu.
Bwana atubariki na kutusaidia.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe.
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Jibu: Tusome,
Yeremia 23:18 “Maana, ni nani aliyesimama katika baraza la Bwana, hata akalifahamu neno lake na kulisikia? Ni nani aliyelitia moyoni neno langu, na kulisikia”
Ili tuweze kuelewa vizuri, hebu tuendelee kidogo kusoma hadi mstari wa 22
“19 Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea; ni dhoruba ya kisulisuli; itapasuka, na kuwaangukia waovu vichwani.
20 Hasira ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtalifahamu neno hili kabisa.
21 MIMI SIKUWATUMA MANABII HAO, lakini walikwenda mbio; sikusema nao, lakini walitabiri.
22 Lakini kama wangalisimama katika BARAZA YANGU, ndipo wangaliwasikizisha watu wangu maneno yangu, na kuwageuza waziache njia zao mbaya, na uovu wa matendo yao.”
Katika mistari hiyo, Bwana alikuwa anazungumza juu ya manabii wa uongo, ambao hawakuketi kusikia kutoka kwa Mungu bali walijitungia nabii zao na kuwapa watu…na nabii hizo walizowapa watu hazikuwa zinawafanya watu waache dhambi zao, bali zilikuwa zinawafanya watu wazidi kustarehe katika dhambi, manabii hao wa uongo walikuwa wanawatabiria watu kuwa kuna amani na shwari na Bwana hajawakasirikia ilihali hakuna amani yoyote, na Bwana amewakunjia uso, kutokana na maasi yao.
Sasa ndio Bwana anawaambia wana wa Israeli kupitia kinywa cha Yeremia kuwa.. manabii hao wanaowatabiria uongo, hawakuketi barazani pa Mungu na kusikia Mungu anasema nini, bali wamejituma wenyewe…
Hivyo Barazani pa Mungu panapozungumziwa hapo ni “mahali ambapo Mungu anakutana na watu wake katika roho na kuwapa ujumbe”.
Mfano wa watu walioketi barazani pa Bwana, na kupokea ujumbe ni nabii Isaya..
Isaya 6:1 “ Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.
2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka…………….
6 Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu;
7 akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa”.
8 Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.
9 Naye akaniambia, Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione”
Mfano mwingine ni Nabii Ezekieli, Nabii Danieli na Nabii Musa. Sehemu nyingi, Bwana amemketisha Musa barazani kwake na kumpa ujumbe kwa wana wa Israeli.
Pamoja na hayo, Mungu pia anaketi katika baraza na malaika wake mbinguni, na kuzungumza nao na kuwatuma.. na pia shetani na mapepo wake wanaweza kuhudhuria barazani mwa Mungu kuwashitaki wateule..
Nyakati 2:18 “Mikaya akasema, Sikieni basi neno la Bwana; Nalimwona Bwana ameketi katika kiti chake cha enzi na jeshi lote la mbinguni wamesimama mkono wake wa kuume na wa kushoto.
19 Bwana akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu mfalme wa Israeli, ili akwee Ramoth-gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi.
20 Akatoka pepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, Mimi nitamdanganya. Bwana akamwambia, Jinsi gani?
21 Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo vinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka, ukafanye hivyo”
Hivyo katika agano la kale, barazani pa Mungu palifikiwa na wanadamu wachache tu!… yaani manabii wa Bwana!, hao ndio Bwana aliowaita barazani pake na kuwapa ujumbe kwa wana wa Israeli. Lakini katika zamani hizi za agano jipya, Wote waliompokea Roho Mtakatifu wanapakaribia barazani pa Bwana, na kuisikia sauti yake anataka nini pamoja na mashauri yake. Hatuhitaji tena Nabii Fulani anyakuliwe mbinguni akasikie ni nini Bwana anasema juu yetu, kisha aje kutuambia… Kwasababu tayari Roho Mtakatifu aliye ndani yetu, anatwaa yale yaliyo ya Kristo, katika baraza lake lililo mbinguni na kutupasha habari..
Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari”.
Hivyo Baraza la Mungu leo ni Roho Mtakatifu!.. Tukimpata huyo basi, tutajua yote Mungu anayotaka tuyajue, hatutahitaji kunyakuliwa mbinguni tukayasikie..la!, wala hatuhitaji kumshusha Kristo chini aje atuambie! tukiwa hapa hapa duniani tutayajua na kuyasikia..kwasababu Roho Mtakatifu aliye ndani yetu, atatupasha habari..
Warumi 10:6 “Bali ile haki ipatikanayo kwa imani yanena hivi, Usiseme moyoni mwako, Ni nani atakayepanda kwenda mbinguni? (Yaani, ni kumleta Kristo chini), …….
8 Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo”
Ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kumpokea Roho Mtakatifu, kwasababu yeye ndio baraza la Mungu. Kwake yeye tunapokea mashauri na maonyo na mafunzo. Na biblia inasema katika Warumi 8:9 kuwa wote wasio na Roho Mtakatifu hao si wake.. ikimaanisha kuwa pasipo Roho Mtakatifu haiwezekani kumwona Mungu.
Na Roho Mtakatifu anafanya kazi kamili kwa aliyemwamini Bwana Yesu, na kuoshwa dhambi zake kwa damu yake. Na aliyebatizwa katika ubatizo sahihi, wa maji mengi na kwa jina la Yesu kulingana na Matendo 2:38.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
Jina la Bwana wetu Yesu, libarikiwe karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu, ambalo ndio mwanga wa njia zetu na taa iongozayo miguu yetu. Leo tutajifunza vipindi VINNE ambavyo ni vigumu mtu kumkumbuka muumba wake.
Biblia inasema..
Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, KABLA HAZIJAJA SIKU ZILIZO MBAYA, WALA HAIJAKARIBIA MIAKA UTAKAPOSEMA, MIMI SINA FURAHA KATIKA HIYO.
2 KABLA JUA, NA NURU, NA MWEZI, NA NYOTA, HAVIJATIWA GIZA; KABLA YA KURUDI MAWINGU BAADA YA MVUA; ……
6 KABLA HAIJAKATIKA KAMBA YA FEDHA; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani”
7 NAYO MAVUMBI KUIRUDIA NCHI KAMA YALIVYOKUWA, NAYO ROHO KUMRUDIA MUNGU ALIYEITOA”
Biblia inaposema mkumbuke muumba wako “KABLA”. Maana yake ni kwamba kama hutamkumbuka katika hicho kipindi, basi utafika wakati itakuwa ni ngumu wewe kumkumbuka Muumba wako. Ikimaanisha kuwa kitendo cha mtu kumkumbuka Mungu, ni neema, na huwa hakidumu muda wote!, ni cha kitambo tu!..tofauti na wengi wanavyofikiri kuwa watakapofikia miaka fulani watamkumbuka Mungu, pasipo kujua kuwa nguvu ya mtu kuvutwa kwa Mungu inatoka kwa Mungu, na si kama mtu apendavyo yeye..
Yohana 6: 44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka;..”.
Ndio maana leo hii kuna idadi kubwa ya vijana na watoto wanaompokea Yesu, kuliko wazee!.
Sasa kufuatia hiyo mistari katika kitabu hicho cha Mhubiri, biblia imetupa vipindi 6 ambavyo tunapaswa tufanye maamuzi, maana yake ndani ya hivyo vipindi, tunatakiwa tuwe tumeshafanya maamuzi thabiti ya kumkumbuka muumba wetu na kumtumikia.
Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.
Nyakati za utoto na ujana, ni nyakati ambazo mtu anapokosa furaha, ni rahisi kumrudia Mungu, mtu anapopitia matatizo Fulani ndipo anapomkumbuka Mungu, kwasababu bado yupo katika miaka ya ujana, lakini sivyo atakavyokuwa mzee. Miaka ya uzee ni miaka ambayo mtu anapopitia matatizo au shida ndivyo anavyozidi kukaa mbali na Mungu. Ndio maana ni ngumu sana kumbadilisha mzee ampokee Yesu, hata akiwa katikati ya mateso na tabu!.. kwanini?..Ni kwasababu ile nguvu ya kumfanya amrudie muumba wako inakuwa haipo!.. Na mara nyingi ni kwasababu muda wa ujana, hakuutumia kumkumbuka muumba wake.
Lakini pia hapa biblia inatuonya kwamba tumkumbuke muumba kabla haijakaribia hiyo miaka!..sio haijafika!.. bali haijakaribia!!..maana yake hata kabla ya kuifikia hiyo miaka, bado kuna shughuli kumkumbuka Mungu..ikiwa na maana kuwa hii neema ya sisi kuvutwa kwa Mungu, haidumu juu yetu milele, inawahi kuondoka kabla hata ya sisi kufikia uzee. Ni wazee wachache sana, wanaopata neema ya kumpokea Yesu katika miaka ya uzee.. Na wengi wa hao ni kwasababu labda katika ujana, waliishi katika mazingira ambayo hawakufikiwa na injili sana.. Lakini wengi ambao wapo tangu ujana wao wanaisikia injili, lakini wanaipuuzia, katika uzee ni ngumu pia kumrudia Mungu.
Mhubiri 12:2 “Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua”
Kipindi ambacho Jua litatiwa giza kwa mtu, ni kipindi cha uzee.. Ni kipindi ambacho Mwili wako umeisha nguvu, macho yako hayana nguvu, miguu yako haina nguvu, mikono yako haina nguvu..
Bwana Yesu alimwambia Petro maneno haya..
Yohana 21:18 “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka”
Kipindi hichi ni kipindi ambacho ni ngumu kumkumbuka muumba wako!.. ile kiu, hamu, au motisha ya kumtafuta Mungu inakuwa haipo, kadhalika uwezo wa kutafakari mambo ya Mungu unakuwa ni hafifu!.. kwahiyo Mungu anatupa tahadhari kuwa tumkumbuke yeye kabla hiyo miaka haijakaribia!..kwasababu itakapofika tofauti na tunavyofikiri kwamba tutakuwa na nguvu za kumkumbuka Mungu, kumbe la! Kinyume chake ndio tutakwenda mbali naye..
Na kipindi ambacho mawingu yatarudi baada ya mvua, ni kipindi hicho hicho ambacho, mvua ya neema imeisha juu ya mtu..hivyo mawingu yanarudi kama kawaida na kiangazi kinaanza.
Mhubiri 12:6 “kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani”
Kikawaida umri wa kukatika kamba ya fedha ni miaka 60, huo ndio umri wa kustaafu!…wengine wanastaafu kabla ya huo umri miaka 55, na wengine baada ya huo kidogo, miaka 65 na hapo anasema kukatika kamba ya fedha, na si kukatika fedha!..kamba ya fedha ni shughuli unayoifanya inayokuingizia kipato Fulani cha kila mwezi.. wengi!, kamba hiyo inakatika miaka 60.
Hivyo kabla ya hiyo miaka haijafika, Bwana Mungu anatupa tahadhari, tumkumbuke yeye kabla ya kuifikia hiyo miaka..kwasababu tusipomkumbuka na katika hiyo, na huku maisha yetu yote tumeisikia injili, baada ya miaka hiyo, hakutakuwa tena na nafasi ya sisi kumgeukia yeye.. kwasababu nguvu ya kuvutwa kwake haitokani na sisi, bali inatoka kwake.. hivyo hatupaswi kuipuuzia kipindi hichi cha ujana..
Hili ni neno la kuhitimisha. Kuwa tumkumbuke muumba kabla hatujamaliza maisha yetu hapa duniani. Baada ya kifo hakuna wokovu tena, biblia inasema “mti uangukiapo huko huko utalala Mhubiri 11:3”.
Hakuna nafasi ya pili baada ya kifo!. Bwana anasema tumkumbuke yeye kabla “roho zetu hazijamrudia yeye”. Kwasababu hakutakuwa na nafasi ya pili, kwamba tufufuliwe tutubu, ndipo tufe.. biblia inasema “tumewekewa kufa mara moja na baada ya kifo hukumu (Waebrania 9:27)”
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana Mungu anatuonya kwamba tuutumie muda wetu vizuri tukiwa hapa duniani!.. Na yale mawazo adui aliyoyaweka katika vichwa vyetu kwamba tutakapokuwa wazee ndipo tutamrudia Mungu, hayo mawazo tuyakatae!, kwasababu ni ya adui.. kiufupi!, kwajinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo ile njia ya wokovu inasonga!, na kuzidi kuwa nyembamba.. Ndio maana Bwana akatuambia..
2Wakorintho 6:2 “(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa”
Tubu na kumpokea Kristo leo, usiseme ngoja nimalizie kuiba kidogo, au ngoja niendele kufanya ukahaba, au ngoja nimalizie kunywa pombe, baada ya kipindi Fulani nitaokoka!.. Ndugu hayo ni mahubiri ya shetani anayokuhubiria kichwani pako. Pia usiseme ngoja nitakapostaafu, nitapata muda mwingi wa kumtafuta Mungu..jambo hilo lifute kwenye akili yako kuanzia sasa, “mkumbuke muumba wako kabla kamba ya fedha haijakatika”.
Kwa kadiri muda unavyozidi kwenda ndivyo ile njia inavyozidi kusonga na kuwa nyembamba, wakati uliokubalika ndio huu!, saa ya wokovu ndio sasa. Kumbuka pia hujui siku yako ya kuondoka duniani ni lini!, na yeye anasema mkumbuke kabla roho yako haijamrudia yeye!.
Je upo tayari kumkumbuka leo!, na kusema siutaki tena ulimwengu na tamaa zake zote?.. Pengine umri wako ni mkubwa lakini bado unaisikia hii sauti ikikuambia tubu tubu!.. hiyo ni neema fahamu kuwa ndio upo kipindi cha kumalizia!… muda si mrefu hutaisikia tena! Kwasababu hatuamui sisi kipindi cha kumfuata Yesu, bali neema ya Mungu ndiyo inayoamua juu ya maisha yetu. Ikiisha hiyo, hata tufanyaje hatutaweza kumtafuta Mungu.
Kama upo tayari kumpokea Yesu leo, hapo ulipo jitenge kwa muda mchache, kisha tubu dhambi zako zote kwa Bwana Yesu, na dhamiria kuziacha, kama ni ulevi, uzinzi, wizi, uuaji, uvaaji mbaya, utukuanaji, kamari, na mambo mengine yote yasiyompendeza Mungu, unadhamiria kuacha yote, na baada ya kutubu kwa dhati kabisa, hatua inayofuata ni kwenda kubatizwa, kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo kulingana na matendo 2:38, na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako kukupa uwezo wa kushinda dhambi, na kukuongoza katika kweli yote.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Biblia ituambia tusalimiane kwa busu takatifu. Hili busu ndio lipi?
Dhambi inafananishwa na mnyama mkali sana wa porini, kama vile simba au chui, au chatu. Utagundua tabia moja waliyonayo hawa wanyama pale wanapowinda ni kuwa hawana papara, Wanakuwa wavumilivu sana mbele ya kitoweo chao, hawakurupuki ovyo kwa kuanza kukikimbiza kutokea mbali, hapana, bali utaona wanajisogoza karibu navyo, taratibu na kwa upole sana, na kwa kuvizia,kana kwamba hawana habari navyo, kiasi kwamba yule anayewindwa, hawezi kugundua chochote.. Hadi pale anapokaribiwa sana, na kurukiwa, au kikimbizwa kwa ghafla ndipo anapogundua haa, kumbe adui yangu alikuwa karibu sana na mimi. Akiwa anajiandaa kukimbia tayari ameshakamatwa..
Na ndivyo ilivyo dhambi tabia yake, haina papara.. Wakati ule kabla Kaini hajamuua ndugu yake Habili, kuna maneno ambayo Mungu alimwambia, embu tusome..
Mwanzo 4:3 “Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana.
4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;
5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.
6 Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? USIPOTENDA VYEMA DHAMBI IKO, INAKUOTEA MLANGONI, NAYO INAKUTAMANI WEWE, WALAKINI YAPASA UISHINDE,
8 Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani,Kaini akamwinukia Habili nduguye,akamwua.”.
Unaona? Kumbe dhambi ilikuwa imeshamsogelea sana Kaini mlangoni kama chui, lakini yeye hakuiona, ilikuwa inasubiria tu afungue mlango Fulani katika maisha yake, kisha yenyewe imrukie kwa ghafla, na habari yake iwe imekwisha. Hivyo Mungu akamtahadharisha mapema lakini yeye hakusikia, Na kama tunavyosoma biblia, Kaini hakutubu na kugeuka kuachana na mahasira zake na wivu, badala yake, siku moja akamwambia ndugu yake twenda huko maporini, walipofika kule, alishangaa nguvu ya ajabu ya kuua imemwingia ndani yake kwa ghafla, na moja kwa moja, akachukua kisu akamchinja ndugu yake bila hata huruma.
Jiulize swali ni nani alimfundisha Kaini kuua?, hakuna aliyemfundisha bali ni ile dhambi iliyomnasa ndio ilitekeleza hayo yote. Unapoona mauaji ya kikatili yanatekelezwa na watu usidhani kuwa ni akili zao ziliwatuma hivyo,.Unapoona Yuda anakwenda kumsaliti Bwana wake, tena kwa kumbusu macho makavu, usidhani mwanadamu wa kawaida anaweza kufanya kitendo kama kile hapana, bali dhambi ikishakaba koo, huwezi kunasuka tena, ni sharti utimize mapenzi yake.
Ndugu yangu, leo hii, tabia ya dhambi bado ni ile ile.. Unapohubiriwa utubu dhambi, sio kwa faida ya mchungaji wako, au mwalimu wako, ni kwa faida yako mwenyewe. Kwasababu mimi na wewe sasa hivi tunawindwa vikali sana,..Na kama tutafungua milango yetu kuruhusu kila aina ya dhambi ituchezee tu, tufahamu kuwa mwisho wetu upo mlangoni.
Dhambi ina shinikizo kubwa sana, ikishafanikiwa kukuvaa kama Kaini, au Yuda, ujue hutoki tena, hutajali kifo, hutajali chochote. Kama unaendelea kutoka nje ya ndoa yako, kumbuka upo hatarini kufa, kama unazini zini ovyo, ujue dhambi imeshakuandalia mauti yako. Hatujui itakuwa ni kwa njia ya ukimwi, au kifo, au mapepo, lakini safari yako ipo ukingoni.
Hatupaswi kumwogopa shetani hata kidogo, lakini tunapaswa tuiogope dhambi kweli kweli. Kwasababu yeye ndio yule mnyama atuwindaye. Shetani kazi yake ni kututengenezea mazingira ya sisi kunaswa na dhambi, lakini yeye hana nguvu yoyote ya kukushinda.
Hivyo, tuwe makini, kama hujatubu, ni heri ukatubu sasa, na sio kesho. Hakuna wokovu wa kesho au ule wa “siku moja nitaokoka”. Wokovu wa namna hiyo haupo, wala hautakaa uje milele. Tubu mpendwa ukabatizwe, ukaoshwe dhambi zako, upokee na Roho Mtakatifu, hizi si zama za kutanga tanga na huu ulimwengu wa dhambi, mitandao inawaharibu watu wengi sana. Yesu alituambia, tumkumbuke mke wa Lutu. Tukitaka kuziponya nafsi zetu tutaziangamiza, na tukiziangamiza kwa ajili yake tutaziponya.
Acha mambo ya dunia yakupite, acha fashion zikupitie, acha anasa zikupite, ipoteze nafsi yako kwa Mungu, lakini mwisho wa siku utapona, kuliko kuupata ulimwengu mzima halafu baadaye unakwenda kuzimu milele itakusaidia nini?. Dhambi ni mnyama katili sana.
Bwana atusaidie sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.
NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.
Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?
Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?
UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI.
HUDUMA YA UPATANISHO.
Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu, ambalo ndio taa iongozayo miguu yetu, na mwanga wa njia yetu. Tumekwisha kuvipitia vitabu 20 vya mwanzo, hivyo kama hujavipitia basi ni vyema ukavipitia kwanza, ili tuweze kwenda pamoja katika vitabu hivi vinavyofuata.
Leo tutavitazama vitabu vitatu vya mbele, ambavyo ni Mithali, Mhubiri na Wimbo ulio bora. Vitabu hivi vitatu vimeandikwa na mtu mmoja anayeitwa Sulemani, katika majira tofauti tofauti. Kitabu cha Mithali na Wimbo ulio bora viliandikwa na Sulemani katika kipindi cha ujana wake, lakini kitabu cha Mhubiri alikiandika karibia na mwisho wa maisha yake. Hivyo leo tutakitazama kimoja baada ya kingine. (Lakini pia kabla ya kwenda kuvitazama ni vyema ukaavipitia wewe mwenyewe binafsi, ndipo uufuatilie ufupisho huu)
Kitabu cha Mithali kama tulivyosema ni kitabu kilichoandikwa kwa sehemu kubwa na Mfalme Sulemani na alikiandika katika ujana wake.. Zipo sehemu chache za kitabu hicho zilizoandikwa na Mtu aliyeitwa Aguri, na mfalme Lemueli (Mithali 30 na Mithali 31), lakini Kwingine kote kuliandikwa na Mfalme Sulemani.
Ikumbukwe kuwa Sulemani, alimwomba Mungu hekima badala ya mali, na hivyo Mungu akampa vyote viwili, hekima pamoja na Mali ambazo hakuziomba (1Wafalme 3:11). Na hekima ni neno la kiujumla lenye maana ya “akili, na uwezo wa kupambanua mambo”. Na kuna hekima ya kiMungu na hekima ya kiulimwengu!. Sulemani alipewa hekima zote mbili! (Za kiMungu na za kiulimwengu).
Hekima za Kiulimwengu, zinamwezesha mtu aweze kuishi maisha ya mafanikio katika huu ulimwengu! Jinsi ya kutumia malighafi za ulimwengu huu, kufanikisha mambo yake. Kwamfano watu waliogundua gari, au ndege, au simu wametumia hekima ya kiulimwengu kugundua vitu hivyo, ili viwasaidie katika changamoto za usafiri, na mawasiliano, kadhalika walioweka Methali kama “Asiyefunza na mamaye hufunzwa na ulimwengu” au “asiyesikia la mkuu, huvunjika guu” au “mtoto akililia wembe,mpe umkate”.. wametumia hekima za kibinadamu kujiwekea tahadhari wao na watoto wao, kiasi kwamba mtu yeyote akiisikia hiyo hekima na kuitii basi hatafunzwa na ulimwengu!. Sasa hekima kama hiyo sio hekima ya kiMungu, bali ya kiulimwengu lakini ina ukweli ndani yake.
Kwahiyo Mfalme Sulemani alipewa hekima za aina zote mbili (za KiMungu na za kiulimwengu). Ni muhimu kuufahamu huu msingi kwasababu, utatusaidia huko mbele kuelewa kwanini Sulemani alisema hekima zilimpoteza…(kwamba hazikuwa za kiMungu zilizompoteza bali za kiulimwengu).
Hivyo kwa akili nyingi Sulemani alizopewa na Mungu aliweza kutazama watoto, akatunga mithali za kidunia na kiMungu kuwahusu wao, vile vile aliweza kutazama watu wazima na wazee akatunga mithali kuhusu wao, kadhalika aliweza kutazama wafanya biashara akaweza kutunga mithali na kutunga mashauri kuwahusu wao na vile vile aliweza kutazama maisha ya watu waovu na wema, wapumbavu na werevu, pamoja na viumbe kama wanyama na miti, akatunga mithali juu ya hivyo vyote na akawapa wana wa Israeli wazitumie katika kuendesha maisha yao..
1Wafalme 4:29 “Mungu akampa Sulemani hekima, na akili nyingi sana, na moyo mkuu, kama mchanga ulioko pwani.
30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.
31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.
32 Naye akanena mifano elfu tatu, na nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano.
33 Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata hisopo umeao ukutani; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki.
34 Wakaja wa mataifa yote ili waisikie hekima ya Sulemani, toka wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamepata habari za hekima yake”
Sasa kwa uwezo huo Mungu aliompa Sulemani na akili hizo, alijikuta anaweza kufanya biashara na kufanikiwa sana kwasababu alipewa akili za jinsi ya kuendesha biashara na zikafanikiwa, (Hicho ndio kilikuwa chanzo cha utajiri wa Sulemani), biblia inasema Sulemani alifanya biashara sana… Alifahamu siri nyingi za jinsi ya kufanya biashara na kufanikiwa!, mpaka wafalme wa dunia wakawa wanamfuata kutaka kujua anafanyaje fanyaje mpaka anafanikiwa…(hakuwa amekaa tu! Na kujikuta mali zinamjia, hapana bali alikuwa ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa akili wa jinsi ya kutafuta mali).
1Wafalme 10:22 “Kwa kuwa mfalme alikuwa na merikebu za Tarshishi baharini pamoja na merikebu za Hiramu; mara moja katika miaka mitatu huja merikebu za Tarshishi, zikileta dhahabu, na fedha, na pembe, na nyani, na tausi.
23 Basi mfalme Sulemani akawapita wafalme wote wa duniani kwa mali, na kwa hekima.
24 Ulimwengu wote ukamtafuta Sulemani uso wake, ili waisikie hekima yake, Mungu aliyomtia moyoni. 25 Wakaleta kila mtu zawadi yake, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na mavazi, na silaha, na manukato, na farasi, na nyumbu, hesabu yake ya mwaka kwa mwaka.
26 Sulemani akakusanya magari na wapandao farasi; naye alikuwa na magari elfu na mia nne, na wapandao farasi kumi na mbili elfu, aliowaweka katika miji ya magari, na pamoja na mfalme huko Yerusalemu.
27 Mfalme akafanya fedha humo Yerusalemu kuwa kama mawe, na mierezi akaifinya kuwa kama mikuyu iliyomo Shefela, kwa kuwa mingi.
28 Nao farasi aliokuwa nao Sulemani wakaletwa toka Misri; wakapewa wafanya biashara wake mfalme kwa makundi, kila kundi na thamani yake.
29 Tena gari huja kutoka katika Misri kwa shekeli mia sita za fedha, na farasi mmoja kwa mia hamsini; vivyo watu wakawaletea wafalme wote wa Wahiti, na wafalme wa Shamu, mikononi mwao”.
Vile vile Sulemani alikuwa na akili nyingi za “Jinsi ya kushinda vita”. Tofauti na wafalme wengine ambao jambo kidogo tu likizuka suluhisho ni kwenda vitani!.. Sulemani hakuwa hivyo, aliweza kutatua mambo kwa hekima tu!..Hivyo ikamfanya kuwa Mfalme katika Israeli ambaye hakuwahi kwenda vitani kupigana pigana hovyo!, hivyo uchumi wake ukastawi na watu wake!. Baba yake Daudi hakuwa na hiyo hekima!, yeye lolote likitokea kwamba maadui zake wamepanga vita, basi na yeye alipanga vita!, pasipo kufikiri sana njia mbadala ya kuvimaliza hivyo vita. Lakini Sulemani Mungu alimpa hiyo hekima..hakupigana vita katika ufalme wake wote na aliishi kwa amani.
Vile vile hakupungukiwa chakula wala mifugo, kwasababu alikuwa na akili za jinsi ya kuiongeza hiyo mifugo. Na aliyatimiza malengo yake hayo kwa kuwalazimisha watu wake kufanya kazi kwa nguvu (Israeli hawakupumzika), walifanyishwa kazi sana. (1Wafalme 12:4),
Kwa muhtasari huo basi, tutakuwa tumeshaanza kujua ni nini kimeandikwa katika kitabu cha MITHALI. Kwamba ni kitabu kilichojaa hekima za kiMungu na hekima za kidunia.
Hivyo tunaweza kukigawanya kitabu cha Mithali katika makundi hayo mawili.
Mithali 1:7“Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu”.. Mithali kama hii haiwezi kukubaliwa na wenye hekima ya ulimwengu huu…
Mithali 18:10 “Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama”.
Soma pia Mithali 19:23, Mithali 16:5, Mithali 3:11 n.k
Mithali 5:6 “Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima.
7 Kwa maana yeye hana akida, Wala msimamizi, wala mkuu,
8 Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua; Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?
Mithali12: 27 “Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani”
Mithali 18:18 “Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu”
Mithali 19: 7 “Ndugu zote wa maskini humchukia; Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye! Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka”
Mithali 27: 7 “Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali; Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu”.
Soma pia Mithali 26:13, Mithali 26:20 n.k
Ni jambo gani tunajifunza katika kitabu cha Mithali?
Jambo kuu na la kwanza tunalojifunza ni hekima za KiMungu, ambazo zinatupeleka moja kwa moja kumpenda Mungu, kumtafuta, na kumtumikia. Kadhalika pia tunajifunza hekima za kidunia, ambazo zitatusaidia katika maisha yetu ya hapa duniani, hayo ndiyo mambo mawili makuu, tunayoweza kujifunza katika kitabu hichi.
Kama jina lake lilivyo “wimbo ulio bora”.. maana yake kuna nyimbo nyingi..lakini upo ulio bora!.. Zamani na hata sasa, nyimbo zilitungwa kwa lengo pia la kufikisha ujumbe!.. Na mara nyingi nyimbo zinakuwa ni jambo fulani la kama igizo lakini limebeba ujumbe Fulani ndani yake.. Sasa Sulemani alitunga nyimbo nyingi, biblia inasema alitunga nyimbo elfu moja na tano (1005), zinazohusu miti, mimea, maisha ya watu (soma 1Wafalme 4:30) lakini katika hizo zote, alikuwa na wimbo mmoja ambao aliuona ni bora kuliko mwingine wote.. Na huo ndio tunaousoma katika kitabu hicho cha Wimbo ulio bora.. (Ni wimbo unaomhusu Mtu na Mpenzi wake).
Hata sasa nyimbo zinazoonekana ni bora na watu wa kidunia ni nyimbo zinazohusu mahusiano zinazidi sana nyimbo za kawaida za kuelimisha au za Taifa. Kwanini?…kwasababu shetani naye anajua “wimbo ulio bora”
Hivyo kitabu cha Wimbo ulio bora ni kitabu chenye mashairi na Mwanaume mmoja, anayemsifia mke wake (yaani bibi arusi wake), na vile vile bibiarusi anamsifia mume wake.. kwa ufupi ni kitabu chenye mpangilio wa mashairi na majibizano, baina watu wawili, mume na mke. Na kimegawanyika katika sehemu kuu tatu. (Uchumba, ndoa changa na Ndoa iliyokomaa).
Kuanzia Mlango wa 1-3, inazungumzia mazungumzo ya wapenzi hao wakiwa bado katika hatua ya uchumba, Kuanzia Mlango wa 3 hadi wa 5, ni mazungumzo ya wapenzi hao wawili wakiwa tayari ndani ya ndoa, na kuanzia Mlango wa 5-8 ni Mazungumzo ya wapenzi hao wakiwa katika kilele cha ndoa yao.
Kitabu hichi kwa namna ya kimwili kinahubiri sana sana upendo kwa wana-ndoa, Maana yake watu waliofunga ndoa, kitabu hichi kimejaa maonyo na mafundisho kuwahusu wao(Jinsi inavyowapasa kupendana na kutunzana). Vile vile kimejaa maonyo na mashauri kwa watu ambao bado hawajaingia kwenye ndoa..kwamba wasiyaamshe mapenzi wala kuyachochoe mpaka wakati wake utakapofika.
Wimbo 2:7 “Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.
Mbali na mafunzo tunayoyapata kuhusu wana ndoa na wale ambao hawayaingia bado kwenye ndoa, Mungu aliruhusu pia kitabu hiki kiwepo miongoni mwa vitabu vya biblia, na kiitwe wimbo uliobora kwasababu katika roho pia Kuna wimbo ulio bora ambao Mungu analiimbia kanisa lake!!, na kanisa vile vile kanisa linamwimbia yeye.
Ikumbukwe kuwa katika roho kanisa la Yesu linafananishwa na bibiarusi, na Kristo ndiye Bwana arusi mwenyewe..(soma 2Wakorintho 11:2, Ufunuo 21:9, Yohana 3:29), Kwahiyo upo wimbo unaoimbwa katika roho sasa, wimbo wa Bwana arusi kumrejesha mkewe, Bwana anawaita watu wake sasa, kwa sauti ya upole, na ya upendo kwa mashairi mazuri, anawaita watu katika hatua zote tatu…(hatua kabla ya kumpokea yeye, hapo ndio pale Bwana anamtumia mtu wahubiri wa kumvuta kwake, na mtu Yule anapotii, basi Bwana anakwenda naye katika hatua ya pili ya ndoa, hapo ndio pale mtu anapoamua kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, na baada ya hatua hiyo, Mungu anamwongoza katika hatua nyingine ya mwisho ya kukua kiroho..
Ni nini tunajifunza katika kitabu cha Wimbo ulio bora?
Cha kwanza ni kwamba sisi (kanisa) tuliompokea tunafananishwa na bibi-arusi wa Yesu, na kama ni bibiarusi maana yake hatupaswi kuudharau wito wake, unapotuita…ambao umekuwa kama wimbo kwetu!..vile vile tunapaswa tuushikilie wokovu na kudumu katika huo, kwasababu uhusiano wetu na Mungu wetu hauishii tu katika kumwamini, bali pia katika kudumu katika imani(ndio kudumu katika ndoa)….na hatupaswi kufanya uasherati, ukifanya uasherati wa kiroho kwa kumwacha Mungu na kwenda kuabudu miungu mingine, tukifanya hivyo basi tunamtia Bwana wivu..na wivu wa kimahusiano ni mbaya kuliko mwingine wowote ule.. kama yeye mwenyewe alivyosema
Wimbo 8: 6 “…Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu”.
Pia tunajifunza kuwa na upendo na kuwa waaminifu kwa wapenzi wetu, tuliofunga nao ndoa!..
Na mwisho kitabu hichi kinawafunza wale ambao bado hawajaingia kwenye ndoa!, kwamba wasiyachochee mapenzi, kuyachochea mapenzi ni pamoja na kutazama picha chafu (pornography), kutazama filamu za kidunia ambazo nyingi sehemu kubwa zina maudhui ya mapenzi, vile vile kuzungumza mazungumzo machafu na kuwa na kampani ya watu ambao muda wote mada zao ni uasherati, hivyo ndio baadhi ya vichocheo vya mapenzi, ambavyo mwisho wake ni kuanguka katika uasherati na uzinzi.
Hichi ndio kitabu cha mwisho kilichoandikwa na Sulemani. Sulemani alikiandika kitabu hichi katika uzee wake..na ni kitabu cha hitimisho na kutoa jumla ya mambo yote!.. baada ya yeye kujaribu mambo yote, kuzipima hekima zote za kidunia, kufanya biashara nyingi na kufanikiwa, kujiongezea mali nyingi kuliko watu wote waliotangulia…mwisho wa siku anakuja na hitimisho!..na hitimisho hilo analiandika kama mahubiri!.. Anawahubiri wana wa Israeli.. anasema..
Mhubiri 1:1 “Maneno ya Mhubiri mwana wa Daudi, mfalme katika Yerusalemu.
2 Mhubiri asema, Ubatili mtupu, ubatili mtupu, mambo yote ni ubatili.
3 Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua”
Anaendelea kwa kusema..
Mhubiri 1:12 “Mimi, Mhubiri, nalikuwa Mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.
13 Nikatia moyo wangu ili kuyatafuta yote yanayotendeka chini ya mbingu, na kuyavumbua kwa hekima; ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.
14 Nimeziona kazi zote zifanywazo chini ya jua; na, tazama, MAMBO YOTE NI UBATILI NA KUJILISHA UPEPO.
15 Yaliyopotoka hayawezi kunyoshwa, Wala yasiyokuwapo hayahesabiki.
16 Nikatafakari nikisema, Nimejipatia hekima nyingi kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; naam, moyo wangu umeona kwa wingi hekima na maarifa.
17 Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.
18 YAANI, KATIKA WINGI WA HEKIMA MNA WINGI WA HUZUNI, Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko”.
Ukikitafakari kwa makini maneno hayo, utaona ni maneno ya kama mtu ambaye alikuwa anatamani jambo Fulani sana, kisha akalipata hilo jambo, halafu mwisho wa siku akaja kuliona kuwa si la maana sana kama alivyolitazamia!..
Kama tulivyojifunza mwanzo Sulemani alipewa hekima ya kiMungu na pia ya kidunia, hivyo kwa akili zake nyingi aliweza kuvumbua njia nyingi za kufanya biashara, na kufanikiwa.. akawa mwanauchumi mkubwa mpaka watu wa mataifa mengine wakaja kutaka kujua siri ya mafanikio yake, hata akapendwa na wanawake wengi wa kiulimwengu, na yeye pia akawapenda, na mwisho wa siku wakaja kumgeuza moyo,.. hivyo hekima za kidunia zikampotosha Sulemani, hata akamsahau Mungu na kusahau kufanya mema.. akazitumainia hekima zake za kidunia.
Lakini alipokuwa mzee akagundua kuwa siku moja atakufa!, na mwingine atakuja kuvirithi hivyo vyote!.. na kama akifa na huku moyoni mwake hana utajiri kwa Mungu!.. ni sawa na kazi bure!..ni kujilisha upepo tu!!..hakuna faida yoyote ya yeye kuwa na kila kitu halafu anakuwa hajajaa mema??
Mhubiri 2:1 “Nikauambia moyo wangu, Haya, nitakujaribu kwa njia ya furaha basi ujifurahishe kwa anasa. Na tazama, hayo nayo yakawa ubatili.
2 Nikasema juu ya kicheko, Ni wazimu; na juu ya furaha, Yafaa nini?
3 Moyoni mwangu nikapeleleza jinsi ya kuuburudisha mwili kwa mvinyo, na (moyo wangu ukali ukiniongoza kwa hekima) jinsi ya kushikana na upumbavu, hata niyaone yaliyo mema ya kuwafaa wanadamu, ili wayafanye hayo chini ya mbingu siku zote za maisha yao.
4 Nikajifanyizia kazi zilizo kubwa; nikajijengea nyumba; nikajipandia mashamba ya mizabibu;
5 nikajifanyizia bustani na viunga, na kuipanda humo miti yenye matunda ya kila namna;
6 nikajifanyizia birika za maji, ya kuunyweshea mwitu mlimopandwa miti michanga.
7 Nami nikanunua watumwa na wajakazi, nikawa na wazalia nyumbani mwangu; tena nikawa na mali nyingi za ng’ombe na kondoo, kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu;
8 tena nikajikusanyia fedha na dhahabu, na tunu za kifalme na za kutoka katika majimbo. Nikajipatia waimbaji, waume kwa wake, nao wale ambao wanadamu wanawatunuka, masuria wengi sana.
9 Basi nikawa mkuu, nikaongezeka kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; pia hekima yangu nikakaa nayo.
10 Wala sikuyanyima macho yangu cho chote yalichokitamani; wala sikuuzuia moyo wangu katika furaha yo yote; maana moyo wangu ulifurahi kwa sababu ya kazi yangu yote, na hii ilikuwa sehemu yangu katika kazi yangu yote.
11 Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kujilisha upepo, wala faida hakuna chini ya jua”.
Ukiendelea kusoma kitabu hicho utaona Sulemani, anauchukia mpaka uhai.. anaona hakuna faida yoyote kujitumainisha katika hekima ya kidunia, ambayo hapo kwanza alikuwa anaiona ya maana!.. Magari, na majumba aliyokuwa anayatafuta!, mwisho wa siku anakuja kusema ni upumbavu yote!.. wanawake wengi aliokuwa anawatafuta mwisho wa siku anakuja kujuta anasema ni upumbavu!..biashara anazozifanya anakuja kusema ni kujilisha upepo!… Maana yake ni kwamba laiti kama angerudishwa nyuma, angefanya marekebisho makubwa sana!.. lakini tayari kashakuwa mzee, hivyo anatoa mahubiri wa Israeli.. anawashauri jambo jema la kutafuta!.. kwamba si hekima ya kidunia bali wamtafute Bwana..
Mhubiri 12:8 “Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!
9 Walakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa, naam, akatafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi.
10 Huyo Mhubiri akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli.
11 Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.
12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.
13 HII NDIYO JUMLA YA MANENO; YOTE YAMEKWISHA SIKIWA; MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE, MAANA KWA JUMLA NDIYO IMPASAYO MTU.
14 KWA MAANA MUNGU ATALETA HUKUMUNI KILA KAZI, PAMOJA NA KILA NENO LA SIRI, LIKIWA JEMA AU LIKIWA BAYA”.
Umeona hapo jumla ya mambo yote Sulemani anayoitoa??….Anasema Mche Bwana na uepukane na uovu!.. hasemi tafuta mali, hasemi tena wala hashauri watu kutafuta utajiri, wala hagusii hekima yoyote ya kiulimwengu, bali anahitimisha kwa kusema maneno hayo mawili tu!!!..” MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE, MAANA KWA JUMLA NDIYO IMPASAYO MTU”
Je! Unamcha Mungu na kuzishika amri zake?.. Huyu ni Sulemani ambaye alikuwa ni tajiri kupita sisi, ambaye ameonja kila kitu, ndio anahitimisha hivi, kashatusaidia kufanya utafiti, hatuhitaji tena sisi kufanya utafiti, yeye kafanya utafiti wa kupata mali nyingi na mwisho wa siku kaona ni ubatili!, na kujilisha upepo!.. basi na sisi hatuna haja ya kurudia hayo hayo, kwamaana tukirudia hayo hayo mwisho wa siku tutafika kwenye jibu hilo hilo la Sulemani, na wakati huo tutakuwa tumeshapoteza muda wa kutosha.
Bwana Yesu ambaye alikuwa na hekima kuliko Sulemani alisema maneno haya..
Marko 10: 24 “Wanafunzi wakashangaa kwa maneno yake. Yesu akajibu tena, akawaambia, Watoto, jinsi ilivyo shida wenye kutegemea mali kuingia katika ufalme wa Mungu!
25 Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu ya sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”
Na tena akasema..
Marko 8:36 “ Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?
37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?
38 Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.
Imemfaidia nini Sulemani kuwa na hekima za kufanya biashara kuliko watu wote duniani, halafu hekima hizo zimekuja kumfanya akengeuke na kuabudu miungu mingine mwishoni?.. Ndio maana mwisho anasema na kutushauri kuwa ni ubatili hayo yote..tusiyatafute hayo!..kwasababu tutakufa na kuyaacha..bali tuutafute kwanza kutenda mapenzi ya Mungu hapa duniani.
Ndugu kama hujampokea Yesu, huu ndio wakati wako sasa wa kufanya hivyo, Yesu yupo mlangoni, Utafutaji wa mali usikusonge hata ukajikuta unaikosa mbingu!, kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate!.. Ni heri ukose mali nyingi lakini uingie mbinguni kuliko upate dunia nzima halafu ukose uzima wa milele.
Hivyo kama hujaokoka!, hapo ulipo tubu, na kisha tafuta ubatizo sahihi ambao ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu, na baada ya hapo Roho Mtakatifu atakuongoza katika kweli yote.
Maran atha!
Usikose mwendelezo wa vitabu vinavyofuata!!!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?
Ukweli ni kwamba hatuishi tena wakati wa mavuno, kama ilivyokuwa kipindi cha mitume. Bali tunaishi wakati wa makusanyo ya masazo. Utauliza ni kwa namna gani?
Zamani kulingana na desturi za wayahudi kulikuwa na makundi mawili ya watendaji kazi shambani, kundi la kwanza ni lile lililoajiriwa rasmi kwa kazi ya uvunaji, hilo lilikuwa linatangulia mwanzoni kabisa mwa uvunaji, na lilikuwa linavuna kila kitu kilichoonekana mbele yao.. Hivyo mpaka wafike mwisho wa shamba, walikuwa na magunia kwa magunia ya mavuno. Lakini pamoja na kuwa wanafanikiwa kuvuna mavuno mengi, bado hawakuweza kumaliza kila kitu shambani.
Hapo ndipo linaporuhusiwa kundi la pili la wavunaji, sasa tabia ya hili kundi la pili ni kuwa lenyewe linatembea likizunguka zunguka kwenye shamba lote, kuangalia walau kama kuna kitu kimebakishwa na wavunaji nyuma, wakichukue wakatumie kwa ajili ya matumizi yao na chakula. Watu hawa waliokuwa ni wale maskini waliokuwa wanaishi katika nchi na wageni (Walawi 19:9)..Kazi yao ilikuwa ni ngumu kwasababu walikuwa wanaweza kuzunguka shamba nzima lenye ekari hata 100 wakaumbulia tu kadebe kamoja cha mahindi, kwasababu mavuno mengi yalishavunwa na wanavunaji wa kwanza.
Ruthu alikuwa ni mmojawapo wa hili kundi la pili la wavunaji. Wakati ule utaona alikwenda kukusanya masazo hayo katika shamba la tajiri mmoja aliyeitwa Boazi.
Ruthu 2:2 “Naye Ruthu Mmoabi akamwambia Naomi, Sasa niende kondeni, niokote masazo ya masuke nyuma yake yule ambaye nitaona kibali machoni pake. Akamwambia, Haya, mwanangu, nenda.
3 Basi akaenda, akaja akaokota masazo kondeni nyuma ya wavunaji; na bahati yake ikamtukia kwamba akaifika sehemu ya shamba iliyokuwa mali yake huyo Boazi, ambaye alikuwa wa jamaa yake Elimeleki.
4 Na tazama, Boazi akaja kutoka Bethlehemu kawaamkia wavunaji, akasema, Bwana akae nanyi. Nao wakamwitikia, Bwana na akubariki”.
Sasa kibiblia Wavunaji wa kwanza waliwawakilisha mitume wa Bwana. Na ndio maana utakumbuka wakati ule, wakihubiri injili kidogo tu, idadi ya maelfu ya watu ilikuwa inakuja kwa Kristo ndani ya siku moja.. Hiyo ni kuonyesha kuwa hao ndio waliokuwa wavunaji, Mungu aliowachagua.
Lakini leo hii hujiulizi licha ya kuwa kila mtu ameshasikia habari za Kristo, ameshasoma mafundisho ya mitume kwenye biblia takatifu, ameshaona miujiza mingi Kristo aliyotenda, lakini bado hawageuki, wala hawana mpango wa kutubu..hata ikitokea wamegeuka basi ni mmoja kati elfu.. Hiyo ni kuonyesha kuwa hakuna mavuno tena shambani.
Wanaopita leo hii ni akina Ruthu,(ambao ndio watumishi wa Mungu wa wakati huu) kukusanya masalio machache sana..Vinginevyo kama yasingekuwepo hadi wakati huu, Mungu angeshakuwa ameshauangamiza ulimwengu wote kwa moto. Soma
Isaya 1:9 “Kama Bwana wa majeshi ASINGALITUACHIA MABAKI MACHACHE SANA, tungalikuwa kama Sodoma, tungalifanana na Gomora”.
Ndugu kama wakati wa mavuno ya kwanza ulikupita, basi usifanye mchezo na huu wakati wa mwisho wa masalia tuliobakiwa nao, Ni neema kubwa sana tumepewa sisi, vinginevyo habari yetu ilikuwa tayari imeshakwisha..Si unakumbuka hili andiko linavyosema..
Yeremia 8:20 “Mavuno yamepita, wakati wa hari umekwisha, wala sisi hatukuokoka”.
Umeona? Lakini Mungu ameahidi yatakuwepo masalia machache sana…
Lakini hivi karibuni huduma ya Ruthu, inakwenda kuisha. Boazi wetu ambaye anamwakilisha YESU KRISTO, anakaribia kurudi shambani mwake, kukagua kazi yake.
Kristo atakaporudi, katika awamu hii, halafu akakuta bado hujaingia ghalani mwake, Ujue, adhabu yako itakuwa ni kubwa sana kwenye lile ziwa la moto siku ile. Kwasababu umejua likupasalo kutenda na hujatenda kwa wakati..
Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.
48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.
Unangoja nini? Unasubiri nini usimgeukie Kristo. Huu ulimwengu hauna muda mrefu sana, Kristo yupo mlangoni kurudi, dalili zote zinaonyesha, mwisho umefika, Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa, kubali kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kwa jina la Yesu Kristo upate ondoleo la dhambi zako. Na Bwana akutie muhuri kwa Roho wake Mtakatifu, ili uwe salama katika nyakati hizi za hatari.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Zeri ni dawa ambayo ilikuwa inakamuliwa kutoka katika aina Fulani ya mmea uliokuwa unapatikana sana sana huko Gileadi. Kwasasa haujulikani mmea huo ulikuwa hasaa ni wa aina gani, kama ni mti au jani, lakini biblia inachoeleza ni thamani yake na sifa zake katika kuponya.
Ukisoma katika biblia kipindi kile wale watoto wa Yakobo walipomuuza ndugu yao kwa wale waarabu waishmaeli, biblia inatuambia, katika safari yao ya biashara ya kwenda Misri walikuwa wamebeba na Zeri pia.
Mwanzo 37:25 “Nao wakakaa kitako kula chakula; wakainua macho yao, wakaona, msafara wa Waishmaeli wanakuja wakitoka Gileadi na ngamia zao, wakichukua ubani na zeri na manemane, wakisafiri kuvichukua mpaka Misri”.
Lakini ukisoma pia kitabu cha Yeremia sura ya 8 inaeleza jinsi Yeremia alipokuwa akiwalilia ndugu zake wayahudi kwa jinsi watakavyochukuliwa na wababiloni mateka, Na ndio katika kulia kwake akisema Je! Kuna zeri ya Gileadi awapake watu wake ili waponywe na majeraha hayo makubwa yatakayowapata.. Akimaanisha kama kuna tiba yoyote nzuri ya rohoni, itakayowaponya watu wake na msiba huo mkubwa utakaowakuta mbeleni.
Yeremia 8:21 “Kwa sababu ya maumivu ya binti ya watu wangu nimeumia mimi; nimevaa kaniki; ushangao umenishika.
22 Je! Hapana zeri katika Gileadi? Huko hakuna tabibu? Mbona, basi, haijarejea afya ya binti ya watu wangu”?
Ukisoma, tena ile sura ya 46 Utaona Mungu anawaambia waisraeli kwa kinywa hicho hicho cha Yeremia kwamba wakachukue Zeri ya Gileadi ili wajipake, kwasababu wamejiharibu kupitiliza, kwa makosa yao mengi.
Yeremia 46:11 “Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe”.
Soma pia Yeremia 51:8, Ezekieli 27:17 utakutana na Neno hilo.
Lakini tunajua, Mungu hakumaanisha, Zeri kama dawa ya mitishamba, ndio ingewaponya watu wake, kwa dhiki zao, na dhambi zao, hapana. Bali alikuwa anamaanisha Zeri ya Rohoni.
Na huyo si mwingine Zaidi ya BWANA wetu YESU KRISTO. Yeye ndiye tiba ya kweli. Akimganga mtu amemganga kweli kweli roho yake, na vilevile hata mwili wake, anaponyeka kweli kweli.
1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.
Upendo wa kweli upo kwa Kristo, tumaini la kweli lipo kwake, furaha ya kudumu inatoka kwake.
Je! Umempokea Kristo maishani mwako? Au unategemea Zeri nyingine zikuponye? Kumbuka fedha haiwezi kuiponya roho yako, mke hawezi kuyaponya hayo majeraha yaliyoko ndani yako,, Ndugu, au rafiki hawezi kuzifuta hizo hatia zilizouchafua moyo wako. Ni Yesu Kristo tu peke ndiye anayeweza kufanya hivyo?
Mpokee Leo ayageuze maisha yako.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo: