Beliari ni nini? (2Wakorintho 6:15).

Beliari ni nini? (2Wakorintho 6:15).

Jibu: Turejee…

2Wakorintho 6:15 “Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na BELIARI? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?”

Neno Beliari ni muunganiko wa maneno mawili ya kiebrania, ambayo ni “Beliy-ya’al” lenye maana ya “Asiyefaa kitu” na Neno lingine la “Baradhuli”

Sasa hapo kwenye 2Wakorintho 6:15 inaweza kusoma hivi kwa Kiswahili kirahisi… “Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na mtu asiye na maana? ”

Kibiblia mtu asiyefaa kitu ni mtu asije mcha Mungu, asiye na hofu ya Mungu, mwenye roho ya ibilisi ndani yake, kwaufupi ni Baradhuli, mfano wa Beliari/baradhuli ni wale tunaowasoma katika 2Nyakati 13:7..

2Nyakati 13:7 “Wakamkusanyikia watu mabaradhuli, WASIOFAA KITU, waliojitia nguvu juu ya Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana na wa moyo mwororo, asiweze kuwazuia”.

Waamuzi 19:22 “Hapo walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, tazama, watu wa mji huo, watu mabaradhuli wakaizingira hiyo nyumba pande zote, wakagonga mlango; wakasema na huyo mwenye nyumba, huyo mzee, na kumwambia, Mlete nje mtu yule aliyefika nyumbani kwako, ili tupate kumjua”.

Soma pia Kumbukumbu 13:13, Waamuzi 11:3,  Waamuzi 20:13, 2Samweli 6:20 na Ayubu 11:11.

Na kama maandiko yanavyosema hakuna mapatano au ulinganifu kati ya Kristo na Beliari, maana yake Kristo hawezi kuchanganywa na uchafu, wala hawazi kutembea na Mabeliari au Mabaradhuli, hivyo hatuna budi kujitakasa na uchafu wote wa mwilini na rohoni, ili tutembee na Kristo.

2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

WATU WASIOJIZUIA.

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

Watu wenye kuvunja maagano ndio watu wa namna gani? (Warumi 1:31)

Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)

Print this post

About the author

Nuru ya Upendo administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments