IIGE RATIBA YA MUNGU YA WIKI IKUSAIDIE

IIGE RATIBA YA MUNGU YA WIKI IKUSAIDIE

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.

Tunaposoma kile kitabu cha Mwanzo sura ya kwanza , wengi wetu tunachokiona pale ni tendo la uumbaji tu lakini hatuoni mikakati na ratiba alizojipangia Mungu ili kuukamilisha huo mpango wake mzima wa uumbaji.

Walimwengu wanasema, mtu mwenye akili huwa anajifunza kwa waliofanikiwa.. Sasa sisi wanadamu hatuna aliyefanikiwa Zaidi ya Mungu wetu si ndio?. Tunapoziangalia mbingu na nchi tunachokiona ni kazi stadi iliyobuniwa kwa  umakini  sana isiyokuwa na mapungufu au madhaifu yoyote, hivyo na sisi pia kama tunataka tuwe na mafanikio makubwa hatuna budi kujifunza ratiba ya Mungu jinsi alivyoweza kupangilia mambo yake. Mpaka tukakiona hichi tunachokiona sasa hivi.

Sasa katika zile siku 7 za uumbaji, Mungu alizigawanya shughuli zake katika vipengele vikuu vitatu.

Kipengele cha kwanza: Alijikita katika kufanya kazi ya utenganisho

Kipengele cha pili :Kilikuwa ni uumbaji

Na kipengele cha  tatu: Kupumzika.

Tukianza na kipengele cha Kwanza: Kufanya utenganisho.

Ukisoma Mwanzo 1:2 Utaona utenganisho wa kwanza alioufanya Mungu katika siku ya kwanza ulikuwa ni kati ya Nuru na giza.

Mwanzo 1:3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.

Siku ya pili tena akaendelea na kazi hiyo hiyo.. akayatenga maji ya juu ya nchi, na ya chini ya nchi kwa kuweka kitu kinachoitwa anga katikati..

Mwanzo 1:7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.

8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.

Unaona Kama hiyo haitoshi, bado aliendelea hadi siku ya tatu kufanya matenganisho, kati ya maji na ardhi, ili nchi kavi ionekane

Mwanzo1:9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.

10 Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Na Siku ya Nne pia, akatenganisha, siku na siku, na mwezi na mwezi, na mwaka na mwaka,..kwa kuumba jua na mwezi na nyota..

Soma Mwanzo 1:16-19 utalithibitisha hilo

Sasa mpaka anafikia siku ya nne, alikuwa bado hajaumba mnyama yoyote, ni kazi tu ya utenganisho tukiachilia mbali mimea ambayo iliumbwa siku ya tatu..

Mungu kuanzana na utenganisho ni kutufundisha nini?

Hii ni kutufundisha kuwa, hatupaswi kukimbilia kufanya jambo lolote, kwanza  kama kuna mambo ambayo bado hayajatenganishwa na sisi rohoni. Tutumie nguvu kubwa kutenganisha nuru na giza kwenye wiki yetu, ..Usianze tu wiki yako hivi hivi, bila kuiambia kwanza iwe nuru kwako, kwa kwenda ibadani nyumbani kwa Bwana usianze wiki bila kuomba, hakikisha unayatenga mambo maovu mbali na wewe kwa kadiri uwezavyo. Ndicho Mungu alichokuwa anakifanya katika siku za mwanzo.

Kama kuna mtu umemdhulumu mlipe..kama una madeni ya watu yasawazishe..kama kuna dhambi ulitenda ziungame mbele za Bwana.

Kipengele cha  Pili: Ni uumbaji,

baada ya pale ndipo utaona Mungu anaanza kuumba, samaki , na wanyama wa kila namna wa mwituni na wa kufugwa pamoja na ndege wote angani..na mwisho kabisa akamwuumba na mwanadamu, katika siku ile ya sita.

Hii ni kutufundisha kuwa, mara baada ya kutenganisha mambo yasiyofaa mbali nasi ndipo hapo sasa tuwe na uhakika kuwa kila tunachotia mkono kukifanya, kitakuwa ni chema sana.. Kisichokuwa na mapungufu au kasoro..Kama Mungu alivyoona jinsi uumbaji wake ulivyokuwa vema sana usio na mapungufu yoyote.

Mwanzo 1:31 Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.

Kipengele cha Tatu: Kupumzika.

Sasa alipomaliza kazi yake yote, kwa siku 6, akaona ni vema atenge siku moja apumzike. Akatenga muda wa saa 24 wa kutofanya kazi yoyote.

Hii ni kutufundisha pia, kuwa sisi tusijifanye tupo buzy sana kuliko Mungu, ikiwa yeye alipumzika, wewe ni nani usipumzike? Kama unatenda kazi kama mashine wiki nzima, usiku na mchana huna muda wa kupumzika, wiki nenda wiki rudi, miaka nenda miaka rudi.. Tambua kuwa hata hicho unachokifanya hakiwezi kuwa na ubora wowote. Hivyo na wewe ukienenda kwa ratiba kama hii ya Mungu katika wiki yako, jiandae kukutana na matokeo chanya katika mambo yako yote unayoyasumbukia. Uwe ni mtumishi wa Mungu katika huduma yako, au mwanafunzi, au mfanyakazi, au kiongozi, ijaribu ratiba hii ya Mungu uone. Lakini kama wewe  ibada si kitu cha muhimu kwako, unachowaza siku zote ni kazi tu, hujitenganishi, na kazi haramu, au marafiki wabaya, au mazungumzo mabaya, hujitengi na dhambi, huna muda na kuomba, au kujifunza Neno la Mungu, au kujirekebisha, unachowaza ni pesa tu ujue kuwa wiki yako, na masumbuko yako ni hasara tu. Kwasababu unapanda katika giza..unaumba katika maji..mahangaiko yako uwe na uhakika yatakuwa ni bure tu..

Kumbuka tunapoizungumzia ratiba hii ya Mungu, haimaanishi na wewe uifuate hivyo hivyo kwamba siku ya 1-4 ufanye hivi au vile, hapana, bali, walau katika wiki yako nzima, uhakikishe kila kipengele umekigusia, kwa muda unaolingana na huo Mungu alioutumia. Kama ni kupumzika, unaweza usiwe na saa 24 mfululizo, lakini hakikisha walau kwa wiki hukosi hizo saa 24 za kupumzika, vivyo hivyo na hayo mengine yote.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi nyumbani

Print this post

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

Baada ya Israeli kuondolewa na Waashuru kutoka katika nchi yao, Mfalme wa Ashuru aliwaleta watu wengine, wakakae katika nchi hiyo,waliyoondolewa.. ili kwamba nchi hiyo , isibakie mapori.

Watu hao walioletwa kukaa katika nchi ya Israeli, hawakuwa Wayahudi bali walikuwa ni wapagani, wanaoabudu miungu yao.
Na walipoletwa walienda kukaa mahali pajulikanapo kama Samaria, huku wakiwa bado na miungu yao.

Lakini maandiko yanasema walipofika katika nchi takatifu, walisumbuliwa sana na simba (simba walikuwa wanaua watu sana).

Mpaka Mfalme wa Ashuru alipotuma kuhani mmoja wa kiyahudi kwenda kuwafundisha desturi za hiyo nchi..kwamba ni nchi takatifu hivyo hawana budi kuishi kulingana na kanuni za Mungu wa Israeli na si kulingana na kanuni za miungu yao.
Hivyo walupopelekewa Kuhani walivipokea vitabu vitano tu vya Musa, pamoja na kitabu cha Yoshua, lakini vitabu vingine vilivyosalia vya manabii hawakuviamini wala kuvipokea.

Hivyo wakawa ni jamii ya watu wanaozishika sheria za Mungu wa Israeli nusu..na nusu wanaitumikia miungu yao.

2 Wafalme 17:24
“Naye mfalme wa Ashuru akaleta watu kutoka Babeli, na Kutha, na Ava, na Hamathi, na Sefarvaimu, akawaweka katika miji ya Samaria badala ya wana wa Israeli; wakaumiliki Samaria, wakakaa katika miji yake.

25 Basi ikawa, wakati ule walipoanza kukaa huko, hawakumcha BWANA; kwa hiyo BWANA akapeleka simba kati yao, nao wakawaua baadhi yao.

26 Kwa hiyo wakamwambia mfalme wa Ashuru, wakasema, Wale wa mataifa uliowahamisha, na kuwaweka katika MIJI YA SAMARIA, hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi; kwa hiyo amepeleka simba kati yao, na tazama, wanawaua, kwa sababu hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi.

27 Ndipo mfalme wa Ashuru akatoa amri, akasema, Mpelekeni mmojawapo wa makuhani, mliowachukua kutoka huko; aende akakae huko, akawafundishe kawaida ya Mungu wa nchi.

28 Basi mmoja wa makuhani waliochukuliwa kutoka Samaria akaenda akakaa katika Betheli, akawafundisha jinsi ilivyowapasa kumcha BWANA.

29 Lakini pamoja na hayo watu wa kila taifa wakajifanyia miungu yao wenyewe, wakaiweka katika nyumba za mahali pa juu, walipopafanya Wasamaria, kila taifa katika miji yao walimokaa.

30 Watu wa Babeli wakafanya Sukoth-benothi kuwa mungu wao, watu wa Kutha wakafanya Nergali, watu wa Hamathi wakafanya Ashima,

31 Waavi wakafanya Nibhazi na Tartaki; nao Wasefarvi wakawaunguza wana wao katika moto kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.

32 Basi hivyo wakamcha BWANA, nao wakijifanyia wengine wao kuwa makuhani wa mahali pa juu, ambao waliwafanyia dhabihu katika nyumba za mahali pa juu.

33 WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA miungu YAO WENYEWE, sawasawa na kawaida za mataifa ambao wao walihamishwa kutoka kwao.

34 Hata siku hii ya leo hufanya sawasawa na kawaida za kwanza; wala hawamwogopi BWANA, wala hawazifuati sheria zao, wala hukumu zao, wala ile torati, wala ile amri BWANA aliyowaamuru wana wa Yakobo, ambaye alimpa jina la Israeli”

Umeona hapo, mstari wa 33..maandiko yanasema wakamca Bwana na kuitumikia miungu yao wenyewe..

Yaani walifanya mambo mawili kwa wakati mmoja..

Kwa tabia hiyo basi wayahudi ambao walikuwa wanaishika sheria ya Mungu wa Israeli kwa ukamilifu wote,..wakawa hawachangamani na hawa Wasamaria.

Mpaka wakati wa kuja kwa Bwana, Wayahudi walikuwa bado hawachangamani na Wasamaria (Yohana 4:9).

Lakini Bwana Yesu alipokuja, alikiondoa hicho kiambaza cha kati,

Hata mahali pa kuabudia pakawa si tena Yerusalemu katika mlima Moria (katika hekalu la Sulemani) wala si Samaria katika mlima Gerizimu, ambao Wasamaria ndio waliamini mahali oanapowapasa wao kuabudia..bali pakawa ni KATIKA ROHO NA KWELI.. Hapo ndipo mlimani pa Bwana alipopachagua.

Yohana 4:21 “Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, AMBAYO WAABUDUO HALISI WATAMWABUDU BABA KATIKA ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.

Je na wewe leo unamwabudu Baba katika Roho na Kweli? Yaani katika Roho Mtakatifu na katika Neno lake?

Kama bado mpokee leo Kristo, na ukabatizwe ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu, upate ondoleo la dhambi na upokee kipawa cha Roho Mtakatifu.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MSAMARIA MWEMA.

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA(Luka 6:36)

OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

Mount Gerizim and Mount Ebal: Their Meaning and Spiritual Significance

Rudi nyumbani

Print this post

JIPE MOYO MKUU.

Ukimtafakari yule mwanamke ambaye alitokwa na damu kwa muda wa miaka 12, na kwenda kushika pindo la vazi lake, unaweza kudhani aligundua jambo la maana sana machoni pake, au machoni pa watu waliomfuata Yesu, Jibu ni la!,

Kwa namna ya kawaida kuacha kutafuta Uso wa Yesu, unakimbilia nguo, tena sehemu ya mwisho kabisa ya nguo (pindo), ni uendawazimu na ndio maana ikambidi afanye  hilo jambo kwa siri sana, kutomshirikisha mtu yeyote, hadi Yesu mwenyewe alipouliza ni nani kanigusa bado aliogopa kusema… kwasababu hata yeye mwenyewe machoni pake lilikuwa ni kama jambo la kijinga..akijua kinachofuata kama sio kugombezwa, au kuzomewa, basi ni kufukuzwa.

Lakini tunaona, Bwana Yesu alipogeuka..majibu yake yalikuwa ni tofauti, badala ya kumgombeza na kumfukiza alimwambia, “Jipe moyo mkuu”, binti yangu..kuonyesha kuwa Kristo anayathamini sana mawazo manyonge, maadamu yamekusudiwa tu kwake kwa moyo wote.

Mathayo 9:20 “Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.

21 Kwa maana ALISEMA MOYONI MWAKE, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.

22 Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile”.

Leo hii watu wengi wamekuwa na mawazo mengi ya kufanyia Mungu, Lakini wamevunjwa moyo pengine na dhamiri zao wenyewe, au na wanadamu, mpaka mawazo yale mazuri yamekufa ndani yao, wakidhani kuwa kumtumikia Mungu ni mpaka uwe askofu au shemasi. Kumbe katika mawazo hayo yanayoonekana ni ya kijinga sana, mbele za Mungu yanathamani kubwa mno, maadamu tu yameelekezwa kwake.

Hujawa mchungaji, hujawa mtume, hujawa shemasi, hujawa mwinjilisti, hujawa mwalimu, hilo lisikufanye kuona kuwa kitu kingine chochote unachoweza kumfanyia Mungu, kitakuwa hakuna umuhimu kwake..

Bwana anachokuambia leo ni kuwa JIPE MOYO MKUU. Hilo wazo ulilonalo kwake si, dogo.. pengine unaujuzi wa kuchora picha zenye jumbe tofauti tofauti za ki-Mungu, na kuzisambaza sehemu mbalimbali wazo hilo ni rahisi kudharaulika miongoni mwa watakatifu, lakini kwa Yesu, sivyo anakuambia Jipe moyo mkuu..mtumikie yeye katika hilo.

Pengine Umekuwa na wazo la kuchapisha jumbe fupi fupi, na kuzisakafia kwa karatasi gumu la plastiki, na kwenda kuzigongelea kwenye nguzo za mabarabarani..Usivunjike moyo fanya hivyo… Kama waganga wa kienyeji hawaoni shida, kwanini wewe uone haya? Jipe moyo mkuu.

Umekuwa na wazo la utengenezaji bustani kwenye nyumba za Mungu bure..fanya tu, hata kama litadharauliwa na watu. Unataka kutengeneza studio ya kurekodi kipindi vya shuhuda, bila shida fanya hivyo.. Au Unajisikia, kutoa, kitu Fulani, au mali au eneo, au uanzishe mradi Fulani ambao lengo lake kuu ni kwa ajili ya kuifikisha injili ya Bwana mbele na si kitu kingine, zidi kuitenda. N.k.

Kwasababu, huko pia kuna umuhimu mkubwa sana ambao Bwana Yesu anapafikiria pia japokuwa watu wengi hawapaoni, ni mahali ambapo panaweza kumfanya Kristo ageuke aache kuwahudumia makutano akutazame wewe na kukubariki.

Hivyo usipuuzie mawazo manyonge yaliyowahi kuingia kichwani pako kwa ajili ya Kristo. Bali yatekeleze na Bwana atakufurahia. Uwe na nia njema tu!

Kumbuka, “mwishoni mwa vazi la YESU kuna huduma na pia upo uponyaji”. Hivyo Usikae bila kufikiria ni nini utamfanyia Mungu wako angali ukiwa hapa duniani. Yeye mwenyewe alisema,

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

NUNUA MAJI YA UZIMA.

UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Rudi nyumbani

Print this post

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

Katika Yohana 5:31, tunasoma Bwana Yesu anasema “Mimi nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu si kweli.” Na ukiendelea mbele kidogo katika Yohana 8:14 anasema tena “mimi ningawa ninajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ndio kweli”.. Sasa hapo, tuamini lipi na tuache lipi?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa kauli zote hizo mbili zimeoka ndani ya kitabu kimoja, cha Yohana, tena ni katika utofauti wa sura 3 tu, na mwandishi ni huyo huyo mmoja Yohana, hivyo kwa vyovyote vile asingeweza kuandika kauli mbili zinazokinzana, tena ndani ya  waraka mmoja, kwasababu ni lazima alihakiki waraka huo mara nyingi kabla ya kuutoa..

Kwa muhtasari huo basi tutakuwa tumeshajua kuwa Kauli mbili hizo hazikinzani, bali ni fahamu zetu ndio zimeshindwa kuzipambanua.

Hivyo leo tutakwenda hatua kwa hatua  kuzichambua kauli hizo, na mwisho tutaona kabisa kuwa hazikinzani hata kidogo.

Hebu tuanze na kauli ya kwanza tunayoisoma katika Yohana 8:14, lakini tuanzie juu kidogo kuanzia mstari wa 12 halafu tuendelee hadi wa 18..

Yohana. 8:12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.

13 Basi Mafarisayo wakamwambia, Wewe unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako si kweli.

14 YESU AKAJIBU, AKAWAAMBIA, MIMI NINGAWA NINAJISHUHUDIA MWENYEWE, USHUHUDA WANGU NDIO KWELI; kwa sababu najua nilikotoka na niendako; lakini ninyi hamjui nilikotoka wala niendako………..

17 TENA KATIKA TORATI YENU IMEANDIKWA KWAMBA, USHUHUDA WA WATU WAWILI NI KWELI.

18 MIMI NDIMI NINAYEJISHUHUDIA MWENYEWE, NAYE BABA ALIYENIPELEKA ANANISHUHUDIA.”

Hapo katika mstari wa 17, anasema “Ushuhuda wa watu wawili ni kweli”. Maana yake wakitokea wawili wanaoshuhudia kitu kimoja basi ule ushuda ni wa kweli..

Sasa kulingana na Maneno hayo ya torati..maana yake ni kwamba Ushuhuda wa Yesu kwamba yeye ndiye Nuru ya ulimwengu, Mwana wa Mungu NI KWELI!!

Kwasababu Yeye mwenyewe (Yesu) kwanza anajishuhudia, HUYO NI WA KWANZA!! na kisha Baba yake mwenyewe amemshuhudia HUYO NI WA PILI…(Na alimshuhudia pale sauti ilipotoka  mbinguni na kusema huyu ni mwanangu mpendwa wangu niliyependezwa naye)…

Hivyo mpaka kufikia hapo, tayari wameshapatikana wawili wanaoshuhudia kitu kimoja, ambao ni YESU MWENYEWE na BABA MBINGUNI.. Kwahiyo ushuhuda anajishuhudia Yesu ni kweli.. kwasababu torati imesema “ushuhuda wa watu wawili ni kweli”..na hapo idadi imeshatimia wawili..

Maana yake angekuwa ni Yesu peke yake anajishuhudia na hakuna mwingine, huo ushuhuda ungekuwa ni uongo.

Ndio maana tukirudi sasa kwenye Mlango wa 5 katika kitabu hicho hicho cha Yohana, tunaona Bwana Yesu ndio analifafanua jambo hilo kwamba, angekuwa ni yeye mwenyewe anajishuhudia (yaani yupo yeye peke yake na hakuna mwingine wa kumshuhudia, basi ushuhuda wake ungekuwa ni wa UONGO),

Yohana 5:31 “MIMI NIKIJISHUHUDIA MWENYEWE, USHUHUDA WANGU SI KWELI.

32 YUKO MWINGINE ANAYENISHUHUDIA; NAMI NAJUA YA KUWA USHUHUDA WAKE ANAONISHUHUDIA NI KWELI. …………….

37 Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.”

Umeona hapo? hakuna ukinzani wowote katika kauli hizo mbili. Ni fahamu zetu tu ndizo zinazojichanganya, na kushindwa kuelewa.. Yesu kamwe hajawahi kujichanganya katika maneno yake wala hajawahi kusema uongo.. Sisi ndio tunaojichangaya katika maneno yetu na ndio tunaosema uongo!, na kuwa vigeugue.

Hivyo kupitia habari hiyo  tunachoweza kujifunza kikubwa ni kwamba YESU kashuhudiwa na Baba, kuwa ni Mwana wa Mungu.. “Sauti ilisikika kutoka mbinguni kuwa yeye ni Mwana wa Mungu”, na zaidi ya yote ni NURU ya Ulimwengu. Na mtu yeyote atakayemfuata hatakwenda gizani.

Je wewe tayari umemfuata mwokozi Yesu, ambaye ndiye Nuru ya Ulimwengu?.. au bado upo gizani?.

Na utajitambuaje kama upo gizani, ni kwa matendo ya giza unayoyafanya..na mfano wa matendo ya giza ndio hayo; uzinzi, usengenyaji, wizi, utukanaji, uasherati, kutazama picha chafu mitandaoni, kujichua, kuvaa nguo za kubana, na zisizo na heshima, kujipodoa, kuupenda ulimwengu zaidi ya Mungu (kama kuwa mshabiki wa mipira na mambo ya kidunia, ambayo yanaziba hata nafasi ya kuwa karibu na Mungu) n.k Hakuna mtu yeyote aliyemfuata Yesu kweli kweli akawa anafanya hayo matendo au yanayofanana na hayo…

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”.

Kama bado hujampokea Yesu, saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubalika ndio huu..Hakuna wakati fulani utasema “nitampokea Yesu, au nitaokoka!”. Huo wakati HAUPO!.. Kama utakuwepo basi biblia itakuwa ni Uongo!, iliposema “saa ya wokovu ni sasa!!”.

Hivyo usingoje kesho, fanya uamuzi sasa hivi, pale ulipo piga magoti, kisha kiri na tubu dhambi zako zote kwa Bwana Yesu, naye ni mwaminifu, atakusamehe.. Na baada ya kutubu, fanya hima kutafuta ubatizo, kwa maana ubatizo ni nguzo muhimu sana katika kuukamilisha wokovu wako, ni huyo huyo uliyemwomba Toba, ndiye aliyeagiza kuwa baada ya kuamini ukabatizwe, na ubatizo sahihi sio wa kunyunyiziwa wala wa vichanga, bali ni wa kuzama mwili wote na kwa JINA LA YESU KRISTO (Matendo 2:38) na si vyeo vya utatu.

Kama utahitaji msaada katika kuongozwa sala ya toba basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizo hapo chini.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

MAMA, TAZAMA, MWANAO.

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi nyumbani

Print this post

NUNUA MAJI YA UZIMA.

Maji ya uzima, tunayoyasoma katika biblia sio maji ya chemchemi, wala ya bombani,  wala kisimani, wala ya mto Yordani ulioko kule Israeli na wala sio maji ya upako, yanayouzwa leo huku na huko.

Maji ya uzima ni jambo lingine la kiroho ambalo leo ningependa tuliangalie kidogo.

Katika kitabu cha Yohana, Bwana Yesu alijaribu kugusia kidogo kuwa maji ya uzima yaliyo hai…sio maji ya kisimani..

Yohana 4:5“ Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.

6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

 7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.

8 Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.

9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)

10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, UNGALIMWOMBA YEYE, NAYE ANGALIKUPA MAJI YALIYO HAI.

11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo MAJI YALIYO HAI?

12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?

13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; BALI YALE MAJI NITAKAYOMPA YATAKUWA NDANI YAKE CHEMCHEMI YA MAJI, YAKIBUBUJIKIA UZIMA WA MILELE.

15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka”.

Umeona hapo? jinsi Bwana alivyomfafanulia huyo mwanamke kuwa Yale maji anayoyadhania ya kisimani, sio maji ya uzima..Bali maji ya uzima ni kitu kingine kabisa lakini chenye tabia zinazofanana na hayo maji ya asili.

Sasa swali hayo maji ni nini?

Bwana Yesu, yeye mwenyewe alitupa majibu ya swali hili katika kile kitabu cha Yohana.

Yohana 7:37 “ Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.

38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, MITO YA MAJI YALIYO HAI ITATOKA NDANI YAKE.

39 Na NENO HILO ALILISEMA KATIKA HABARI YA ROHO, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; KWA MAANA ROHO ALIKUWA HAJAJA, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa”.

Umeona hapo?..Maji ya uzima ni ROHO MTAKATIFU.

Maana yake mtu anayepokea Roho Mtakatifu, anakuwa amekata kiu yote ya dhambi.

Kiu ya kunywa pombe na kuvuta sigara inakufa..kiu ya kufanya zinaa na uasherati inakufa, kiu ya kufanya mabaya inakufa, na mambo mengine yote mabaya..

Kwasababu yeye anatoa raha ambayo inazidi raha zote zinazopatikana katika mambo hayo ya  ulimwengu yasiyompendeza yeye..

Ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kumpokea Roho Mtakatifu.

Lakini pia jambo la muhimu kufahamu ni kuwa MAJI HAYA YA UZIMA maandiko yanasema TUNAYANUNUA. Lakini si kwa fedha, wala kwa mali..BALI KWA MAISHA YETU!. Yaani tunapompa Yesu maisha yetu, hiyo ni gharama tosha ya kununua maji hayo.

Fedha haiwezi kununua hayo maji..kwasababu si maji ya kimwilini bali ya kiroho.

Isaya 55:1 “Haya, kila aonaye kiu, njoni majini, Naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; Naam, njoni, nunueni divai na maziwa, Bila fedha na bila thamani.

2 Kwani kutoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula? Na mapato yenu kwa kitu kisichoshibisha? Nisikilizeni kwa bidii, mle kilicho chema, Na kujifurahisha nafsi zenu kwa unono”.

Umeona tena hapo??..anasema Njooni MNUNUE bila fedha na si NJOONI MCHUKUE BILA FEDHA. Maana yake hayo maji yananunuliwa lakini si kwa fedha bali kwa kitu kingine..Na hicho si kingine zaidi ya MAISHA YETU. Yaani kumpa yeye na kubatizwa.

Swali ni je??. Umempokea huyu Yesu? Na kubatizwa ubatizo sahihi wa maji tele na kwa Jina la Yesu?..Kumbuka hiyo ndiyo tiketi pekee ya kuyapata hayo maji, hakuna njia nyingine.

Bwana Yesu anasema..

Ufunuo wa Yohana 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.

Je unayataka maji ya uzima leo?

Mwamini Yesu na tubu dhambi zako leo kwa kumaanisha kuziacha, na ukabatizwe kama bado hujafanya hivyo.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Tusome,

Warumi 3:22 “ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti;

23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;”

Hapo maandiko yanasema “Wote wamefanya dhambi” na sio “Wote wanafanya dhambi”. Ikiwa na maana kuwa kuna dhambi ambayo imeshafanyika huko nyuma ambayo imewafanya wote wawe katika dhambi.

Na dhambi hiyo si nyingine Zaidi ya ile ya Adamu na Hawa. Maandiko yanasema kwa kukosa kwake mtu mmoja Adamu, sisi wote tumeingia katika hali ya kukosa.

Warumi 5:19 “Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki”.

Umeona?..Kwa dhambi ya Adamu na sisi tunaonekana tumefanya dhambi, kwasababu tulikuwa katika viuno vya Adamu, wakati Adamu anafanya makosa hayo..Hivyo kwa dhambi yake ikafanya vizazi vyake vyote kuwa katika dhambi. Ndio maana wanadamu wote tunazaliwa na dhambi ya asili bila hata ya sisi kutaka, tunazaliwa tayari tukiwa tumepungukiwa na utukufu wa Mungu.

Ndio maana utaona mtoto anazaliwa na hasira, uchoyo, kiburi n.k.. Hiyo ni kutoka na dhambi ya asili aliyoirithi kutoka kwa Adamu. Na ndio maana maandiko yanasema “wote tumetenda dhambi” na sio tunatenda dhambi.

1 Yohana 1:8 “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.

9 tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.

10 Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu”.

Na hiyo ndio sababu pia tunamhitaji Bwana Yesu, atuondolee hiyo dhambi ya asili.

Kwasababu Kristo anafananishwa na Adamu wa pili. Maana yake kama Adamu wa Kwanza alivyotuingiza matatizoni sisi wanawe katika vizazi vyote, kadhalika Adamu wa pili (yaani Yesu Kristo), atatuingiza katika hali ya kuwa watakatifu, endapo tukimwamini na kumpokea..

Warumi 5:18 “Basi tena, kama kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima.

19 Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki”.

Pale tunapompokea na tunapotubu dhambi zetu na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, tunakuwa tumezaliwa mara ya pili, na hivyo ile dhambi ya asili tuliyozaliwa nayo inaondoka. Tunakuwa watakatifu, kwasababu Kristo anashusha nguvu ya kipekee juu yetu ya kutusaidia kushinda dhambi…Hivyo tunajikuta tunaishi maisha ya utakatifu na usafi bila sheria.

1Yohana 3:9 “Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu”

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba, wote walio ndani ya Kristo, dhambi haiwatawali, kwasababu wameuvua utu wa kale na kuvaa utu upya.

2Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Na ndio maana maandiko pia yanatuonyesha kuwa watakatifu waliopo duniani ndio wanaompendeza Mungu..ikimaanisha kuwa duniani kuna watakatifu.

Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.

Je! Na wewe ni Mtakatifu?.. Umempokea Yesu na kutubu na kubatizwa ubatizo sahihi?. Kama bado kumbuka Kristo yupo mlangoni, na atakaporudi atawachukua tu wale wateule wake na kwenda nao mbinguni, yaani wale wote waliozaliwa mara ya pili, na kuishi maisha ya utakatifu. Lakini wengine waliosalia ambao hawamtaki yeye watatupwa katika lile ziwa la moto.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

https://wingulamashahidi.org/2018/07/04/5-swali-je-kuna-dhambi-kubwa-na-ndogo-na-kama-hakuna-je-mtu-aliyeua-na-aliyetukana-je-watapata-adhabu-sawa/

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post

WAKO WATATU WASHUHUDIAO MBINGUNI NA DUNIANI.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu.

Maandiko yanasema kuwa wapo watatu washuhudiao mbinguni, na vile vile wapo watatu washuhudiao duniani.

1Yohana 5:7 “Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.

8 Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, BABA, NA NENO, NA ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja.

9 Kisha wako watatu washuhudiao duniani], ROHO, NA MAJI, NA DAMU; na watatu hawa hupatana kwa habari moja. Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe”.

Lakini swali la kujiuliza ni je!, hao watatu NI WAKINA NANI na WANASHUHUDIA NINI na WANASHUHUDIAJE?

Kama ukianzia juu kidogo katika habari hiyo utaona Mtume Yohana alikuwa anajaribu kuelezea habari za ushuhuda wa Yesu kuwa ndiye “Mwana wa Mungu”. Alikuwa anajaribu kuelezea kuwa habari ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, sio jambo la kutunga tu!, bali mbingu na nchi zimelishuhudia hilo. Na akawa anajaribu kueleze vitu vikuu vilivyoshuhudia au kulithibitisha hilo, vilivyopo duniani na vilivyopo mbinguni..

Na vitu hivyo ndio Mtume Yohana kwa ufunuo wa Roho anaviorodhesha. Kwamba kwa duniani ni ROHO, MAJI na DAMU.. Na kwa mbinguni ni BABA, NENO na ROHO. Sasa ni kwa namna gani vitu hivi vinashuhudia

1Yohana 5:5 “Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba YESU NI MWANA WA MUNGU?

6 Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu.

7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli”.

Hebu tuanze kuutazama Ushuhuda kutoka mbinguni.

Tusome.

Mathayo 3:16 “Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona ROHO WA MUNGU akishuka kama hua, akija juu yake;

17 na tazama, SAUTI KUTOKA MBINGUNI IKISEMA, HUYU NI MWANANGU, MPENDWA WANGU, ninayependezwa naye”.

Hapo tunaona vitu vitatu vimeshirikiana kumshuhudia Kristo kama ni Mwana wa Mungu. Cha kwanza ni SAUTI ambayo ndio NENO. (Huyu ni Mwanangu mpendwa wangu). Cha pili ni BABA ambaye ndiye kazungumza maneno hayo, na cha tatu ni ROHO ambaye ndiye kashuka juu yake kama Hua (yaani njiwa)..kuyathibitisha maneno ya Baba.

Kwahiyo unaweza kuona hapo BABA, kazungumza NENO kutoka mbinguni, kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu kweli,  na Kamshusha ROHO wake kulithibitisha neno lake hilo.

Hivyo kutimiza hilo Neno linalosema wapo watatu washuhudiao mbinguni BABA, NENO na ROHO.

Lakini Sehemu ya pili inasemaje?.. Wapo watatu pia washuhudiao duniani, nao ni ROHO, DAMU NA MAJI..Sasa ni kwa namna gani hawa wanashuhudia kuwa ni kweli Yesu ni Mwana wa Mungu, kama vile Baba alivyoshuhudia kwa Neno na Roho?.

Tusome,

Yohana 19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu;

34 lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara IKATOKA DAMU NA MAJI.

35 NAYE ALIYEONA AMESHUHUDIA, NA USHUHUDA WAKE NI KWELI; naye anajua ya kuwa anasema kweli ili ninyi nanyi mpate kusadiki”.

Umeona hapo?. Huyu Askari alipofika kwa Bwana Yesu na kumchoma ubavuni kwa mkuki, akashangaa kuona MAJI mengi yanatoka,  jambo ambalo sio la kawaida, na baadaye inatoka DAMU. Kwa ishara ile Askari yule akakiri ya kwamba YESU NI MWANA WA MUNGU, na hapo Mtume Yohana anatia msisitizo kuwa “huyo Askari aliyeona ameshuhudia na ushuhuda wake ni kweli”.

Sasa utauliza mbona hapo maandiko hayajaonyesha kama Askari huyo kashuhudia kwamba YESU NI MWANA WA MUNGU kwa tukio hilo?.

Jibu ni kwamba alishuhudia hilo, na kukiri kwamba YESU NI MWANA WA MUNGU Baada ya kulishuhudia tukio hilo la kifo cha Yesu.Tunaweza kusoma habari hiyo vizuri tena katika kitabu cha Marko..

Marko 15:39 “Basi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu”.

Kwahiyo MAJI na DAMU vilivyotoka katika mwili wa Bwana Yesu, Na SAUTI (yaani NENO) la BABA, lililoshuka juu yake wakati anabatizwa. VINASHUHUDIA KUWA YESU NI MWANA WA MUNGU. Kadhalika Maji yaliyotoka ubavuni mwa Yesu, na Damu yake iliyomwagika Kalvari, vinatushuhudia kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu.

Ndio maana na sisi ili Baba atushuhudie kuwa ni WANA WA MUNGU, kama alivyomshuhudia mwanaye ni lazima na sisi tuwe na ushuhuda wa MAJI, na ROHO na DAMU tukiwa hapa duniani.

Maana yake ni kwamba lazima tubatizwe kwa MAJI na kwa ROHO MTAKATIFU na kutakaswa kwa DAMU. Tusipofanya hivyo sisi sio wana wa Mungu mbele za Baba mbinguni na wala hatatushuhudia. Bwana Yesu aliposhuka pale Yordani kubatizwa kwa MAJI na ROHO aliposhuka juu yake ndipo sauti ikasikika kuwa yeye ni mwana wa Mungu. Na sisi ni hivyo hivyo, ni lazima tuwe na ushuhuda huo wa kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu, ili Damu ya Yesu iweze kutusafisha.. kutushuhudia kuwa sisi ni wana wa Mungu.

Yohana 3:5 “Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu”.

Leo hii ubatizo unapuuziwa sana na wengi ni kwasababu bado hawajaelewa ufunuo uliopo katika ubatizo.

Ukielewa ufunuo uliopo katika ubatizo, ndipo utajua hicho kitu ni cha umuhimu kiasi gani.. Ilimpasa Kristo abatizwe ili sauti ije juu yake kuwa yeye ni Mwana wa Mungu, inatupasaje sisi?.. Ubatizo ni tendo dogo lakini lina madhara makubwa sana katika Roho.

Na kumbuka ubatizo halisi na wa kweli, si ule wa vichanga bali ni lazima mtu ajitambue na kuamua kukiri kwa kinywa chake, Bwana hakushindwa kubatizwa wakati akiwa na siku nane, kipindi anakwenda kutahiriwa.. vyote hivyo viwili vingeweza kwenda pamoja.. Lakini ilimpasa awe mtu mzima kwanza.

Vile vile ubatizo sahihi ni kwa jina la BWANA YESU KRISTO, kulingana na Matendo 2:38, Matendo 8:16, Matendo 10:48, na Matendo 19:5.

Bwana atufumbue macho tuzidi kumwelewa.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

Neno “Via” linamaanisha nini katika biblia?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

BIRIKA LA SILOAMU.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18

Jibu: Tusome,

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Neno “Mbwa” kama linavyotumika hapo, linamaanisha “Mwanaume anayejiuza mwili wake”, kwa lengo la kupata fedha, kama vile mwanamke anayejiuza anavyojulikana kama Kahaba, vivyo hivyo mwanaume anayejiuza alijulikana kama “mbwa”.

Na kujiuza huko kuko kwa namna mbili. Namna ya kwanza ni mwanaume anayejiuza kwa wanawake, na namna ya pili, ni mwanaume anayejiuza kwa wanaume wenzake (yaani Hanithi). Makundi haya yote mawili yanajulikana kama “mbwa” kibiblia.

Hivyo Mungu alikataza kwa mtu yeyote awe mwanamke au mwanaume anayejiuza mwili wake na kupata fedha, asizilete hizo fedha katika nyumba ya Mungu kama sadaka, kwaajili ya nadhiri, na si tu nadhiri bali pia kama sadaka!..kwani ni machukizo mbele zake.

Mithali 15: 8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Kwahivyo biblia inatufundisha kuwa Utakatifu ndio sadaka ya kwanza kwa Mungu wetu..Maana yake tusipokuwa watakatifu wa mwili na roho, na tukaenda kumtolea sadaka, huku hatutaki wala hatuna mpango wa kubadilika, bado ni wazinzi, bado ni waasherati, bado ni makahaba, bado ni wachawi, bado ni watu tuliojaa vinyongo na chuki..basi tujue kuwa sadaka ile tunayokwenda kuitoa ni machukizo makubwa sana kwa Bwana. Kwasababu kitu cha kwanza Bwana anachotafuta kwetu si PESA, wala SADAKA, bali anataka tuwe wakamilifu, anataka tupate Rehema..

Mathayo 9:13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.

Bwana Yesu mwenyewe alitupa ushauri mzuri, wa namna ya kumtolea Mungu..kwamba tujitakase kwanza kabla ya kwenda kumtolea yeye, ili sadaka yetu ikubalike na iwe na matokeo. Na kujitakasa huko sio kujitakasa leo, na kesho kurudia yale yale..bali ni kule kwa badiliko la kudumu ndani yetu..

Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,

24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”.

Kinyume chake tukimtolea sadaka na huku hatuna mpango wa kuacha maisha yetu mabaya ya dhambi, tufahamu kuwa sadaka zetu hazitakubaliwa na zaidi ya yote hatutaurithi uzima wa milele..Na maandiko yanasema wazi kuwa waasherati na MBWA hawataurithi uzima wa milele.

Ufunuo 22:14 “Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya”

Bwana atubariki na kutujalia neema zake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

MTAWATUPIA MBWA NYAMA HIYO.

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

Noeli ni nini, na je! Neno hili linapatikana katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

Ulishawahi kujiuliza hoja ya msingi shetani aliyotumia kumshitakia Yesu mpaka kufanikiwa kumpeleka msalabani ilikuwa ni ipi?

Tukilifahamu hilo tutaelewa ni wapi ibilisi anapandaa ili kuwaletea dhiki wakristo katika siku za mwisho.

Ukisoma biblia utaona Wakati ule wayahudi wanatafuta sababu nyingi sana za kumshitaki Bwana Yesu lakini hawakuziona, mpaka dakika za mwisho mwisho wakatokea na hoja nyingine moja, ambayo ilikuwa na mashiko sana kwao..

Na hoja yenyewe ilikuwa ni katika lile HEKALU.

Mathayo 26:59 “Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;

60 wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi.

61 Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu.

Nataka ujifunze jambo moja, kulikuwa na kauli nyingi sana zenye makwazo ambazo wayahudi wangeweza kuzisimamia kumuulia Yesu, kwamfano alipowaita wao ni wa baba yao Ibilisi na sio Ibrahimu(Yohana 8:44). Kwa kauli kama hiyo kwamfano ingetosha tu kumfanya wamuue. Lakini sio hiyo ya  kusema “Bomoeni hili Hekalu nami nitalijenga ndani ya siku tatu…”

Ulishawahi kujiuliza, kwanini kauli hiyo ilipata nguvu?

Hilo ni jambo ambalo shetani alijaribu kulijenga tangu zamani za akina Zerubabeli katika ujenzi wa Hekalu, kama wewe ni msomaji wa biblia, utakumbuka kuwa kipindi wanalijenga Hekalu la pili, maadui zao (ambao hawakuwa wayahudi) waliomba waungane nao ili kulijenga hekalu la Mungu, lakini Zerubabeli na wenzake kwa ufunuo wa Roho, wakawakatalia, kwasababu walijua madhara yake yatakayokuja huko baadaye (Ezra 4:3)..

Lakini muda mrefu ulipopita mamia ya miaka, hekalu hilo lilichakaa, likawa kama limepitwa na wakati, kwa ujenzi wake. Hapo ndipo akatokea mtawala mmoja wa ki-Rumi aliyeitwa HERODE, Akaomba alikarabati hekalu lile,. Sasa wayahudi bila ya Kutaka kumuuliza Mungu, wakakurupuka wakamruhusu, hivyo Herode akaanza kulikarabati tena, akalijenga kwa fedha nyingi sana na kwa muundo wa kisasa.

Muda alioutumia kukarabati ulizidi hata muda uliotumika kujenga Hekalu lile, kwani Herode alitumia miaka 46 kulikarabati, (Soma Yohana 2:20 utaona), wakati wakina Zerubabeli walitumia miaka  isiyozidi 7. Na alifanikiwa kulipamba kweli kweli, mpaka wakati Fulani mitume wakaenda kumuonyesh Bwana uzuri wa jengo hilo jinsi lilivyopambwa vizuri.

Sasa kitendo kile kilikuwa na agenda ya ibilisi nyuma yake. Kwasababu alijua upo wakati Masihi atakuja, na ataingia katika hekalu lile na kuwafundisha watu sheria za Mungu, Hivyo akatumia nguvu zake nyingi sana kutafuta namna ya  kupalimiliki. Ndipo hapo akamwingia Herode, ambaye roho ya mpinga-Kristo ilikuwa nyuma yake, mtu ambaye alikuwa hana hata upendo na Mungu, na ndio maana wakati tu Kristo anazaliwa badala afurahie mwokozi kaja ulimwenguni, kinyume chake akatuma watu kwenda kumuangamiza, lakini cha ajabu ndio mtu huyo huyo aliyelikarabati Hekalu la Mungu.

Sasa kwasababu yeye ndiye aliyelitengeneza upya. Mamlaka yote ikahamia mikononi mwake kutoka kwa wayahudi, wayahudi wakawa hawana la kusema, hapo ndipo akaanzisha biashara kubwa kubwa sana , ndani ya hekalu, akalifanya pia kuwa kama eneo la kitalii, la watu kuja kushangaa uzuri wake.

Vilevile kukawekwa sheria kali, mtu yeyote akitaka kufanya jambo, au kuleta mfumo mpya ni lazima kwanza apokee kibali kutoka kwa HERODE, vinginevyo utaonekana kama ni muhalifu, na msaliti, ambaye anastahili adhabu ya kifo.

Kwahiyo, hakukuwa na mtu aliyeweza kufumbua kinywa chake, kukemea jambo lolote baya lililofanyika katika hekalu la Mungu takatifu, kwa hofu ya Herode na wayahudi. Hivyo hiyo ikaifanya  hali ikaendelea kuwa mbaya kupindukia hadi wakati Kristo anatokea dunia,

Ibilisi alijua kabisa, mwisho wa Siku Bwana Yesu, ni lazima aje aingie katika hekalu lake takatifu. Na kweli wakati ulifika akaingia, ndipo akasambaratisha  biashara zote, na shughuli zote zilizokuwa zinaendelea ndani ya Hekalu.

Wayahudi kuona vile, wakadhani maagizo hayo kapewa na Herode ndipo walipomuuliza…..

Luka 20:2 “wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii?”

Na baada ya kugundua kuwa hakuyapokea Kwa Herode, hapo ndipo wakajua mtu huyu ni msaliti, na gaidi, anataka kutuletea harufu mbaya duniani, ili sisi tuonekane kama waasi, ni lazima tumuue.

Ndipo wakamshitakia kwa kitendo chake kile, na kauli ile.

Nachotaka tuone ni kwamba. Shetani anafahamu kuwa Kristo yupo mlangoni kurudi tena mara pili kulinyakua kanisa lake takatifu. Hivyo alichokifanya tangu kile kipindi cha mitume hadi sasa ni kujiingiza kwa siri , ili kujifanya kama analisaidia kanisa la Mungu..

Lakini lengo lake sio Kristo, na ndio maana utaona sasa, madhehebu mengi ya uongo, yamefanikiwa sana, lakini ukijaribu kuchunguza mifumo yao utaona ipo mbali sana na biblia.

Ukiuliza ibada za sanamu za kumwomba bikira Maria zipo wapi kwenye biblia, au kwenda toharani tunakupata wapi, utaishia kuonekana ni msaliti, na gaidi, msambaza, chuki. Shetani sikuzote hataki mfumo wake mbovu kuhojiwa.. Hataki kwasababu anajua pale sio mahali pake.

Leo hii, bado hajapokea nguvu kamili,za kuleta uharibifu kwa watu, wakati unafika atapokea nguvu ya kuleta mauaji kwa wale wakristo ambao UNYAKUO utakuwa umewapita. Atataka kuwaondosha wote asibakie mtu.

Je! Umeokoka ndugu yangu? Au bado unajisifia dini na madhehebu? Hautanyakuliwa kwa dhehebu lako zuri, utanyakuliwa kwa kukamilishwa katika wokovu, yaani kutubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, na kuishi katika utakatifu. Tubu leo kama hujatubu, Kumbuka wakati wowote Kristo anarudi.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kikoto ni nini?(Yohana 2:15)

UFUNUO: Mlango wa 11

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

Je! Wokovu umekufikia?

Wengi wanasema wamepata wokovu lakini kiuhalisia wokovu bado haujawafikia.
Leo napenda tujifunze juu ya viashiria vinavyorhibitisha kuwa wokovu umetufikia, au umefika nyumbani kwetu.

Tusome habari za mtu mmoja aliyeitwa Zakayo, ambaye kupitia yeye tutajua kama wokovu na sisi umefika nyumbani kwetu au la!

Luka 19:1-10
“1 Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.

2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.

3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.

4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.

5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako.

6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.

7 Hata watu walipoona, walinung’unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.

8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.

9 Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.

10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea”.

Nataka tuuone huo mstari wa 8, ni kitu gani Zakayo alichokifanya kikamsababisha mpaka Mwokozi Yesu aseme.. “Leo Wokovu umefika nyumbani humu”

Na kitu chenyewe ndicho hicho tunachokisoma..huo mstari wa 8.

“8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.”

Umeona?..Zakayo alijiona yeye ni mwenye dhambi, na kutubu…lakini aliona toba ya midomo peke yake haitoshi, na ilihali mali nyingi alizonazo ni kutokana na kuwadhulumu watu..akaona aib mbele za Bwana na vile vile moyo wake ukamchoma.
Alichofanya alitoa nusu ya mali yake yote iliyo ya halali na kuwapa masikini, na zaidi ya yote, wale wote aliowadhulumu aliwarudishia mara 4,.

Maana yake ni kwamba kama kuna kiwanja alimdhulumu mtu, alimrudishia mara 4, maana yake viwanja 4..

Kama kuna fedha alimdhulumu mtu, alimrudishia mara 4..

Na huo moyo wa toba yenye matendo ndio Bwana aliokuwa anauhitaji.. Na Bwana ndio akamwambia maneno yale “Leo wokovu umefika nyumbani humu”

Hebu jiulize leo ndugu, tangu umempokea Yesu, vile vitu vya wizi ulivyoiba, umemrudishia mwenyewe?..au umetubu tu kwa mdomo na kuishia hapo, na kuendelea kuwa navyo?

Zile mali za dhuluma ulizozipata bado unafurahia kukaa nazo baada ya kuokoka?..Zakayo hakuona vyema kukaa nazo, aliona aibu mbele za Bwana na alipoziondoa na ndipo Wokovu ulipoingia nyumbani mwake.

Sisi tunaonaje raha kubakiwa na simu za wizi?, Kubakiwa na fedha za dhuluma, kubakiwa na heshima wa hila n.k
Bwana wetu hafurahiwi na toba za midomo tu!..bali na za matendo,

Tunapotubu ni lazima na maisha yetu yabadilike, hata watu wa nje waone kweli pale pana mtu aliyebadilika, watu wa nje hawashawishiki kwa maneno ya midomo tu, ndipo waamini kuwa tumebadilika..wanashawishika wanapoona umewarudishia vile ulivyowadhulumu.

Kadhalika hawatashawishika kusikia kuwa umetubu kwa mdomo huku mavazi yako na mwonekano wako ni bado ule ule wa kikahaba au kihuni.

Wakikuona bado unavaa nguo za kubana, bado unavaa vimini, bado unajipamba uso kama Yezebeli, haijalishi unahudhuria kanisani kila siku kiasi gani..bado watakuona wewe ni kahaba na muhuni tu.

Wakisikia umetubu lakini bado huyo mke uliye naye si wako ni wa mtu mwingine, huyo mume uliye naye si wako ni wa mtu mwingine, hawashawishiki hata kidogo..na zaidi ya yote Kristo hakujui.

Tunapotubu hatuna budi kuzaa matunda yanayotokana na toba zetu hizo..

Mathayo 3:8-10
“ 8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;

9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.

10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.

Je! Toba yako ina matunda?

Kama bado basi ni wakati wa kuanza upya, kama ni mwanamke baada ya kutubu weka mbali vipodozi vyote, kaa mbali na dhuluma na biashara haramu..na kama ni mwanamume ni hivyo hivyo, kuviondoa vyote ulivyovipata kwa dhuluma na kujitenga na udunia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.

Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

KUONGOZWA SALA YA TOBA

MAOMBI YA TOBA.

Sala ya Toba na Rehema.

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

NGUVU YA MSAMAHA

Rudi nyumbani

Print this post