LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.

LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.

Livunjeni hekalu hili nami katika siku tatu nitalisimamisha..

Mara nyingine Bwana Yesu alipotaka kufikisha ujumbe Fulani, alikuwa anatumia mfano wa mahali husika ili kuchanganya mada mbili kwa wakati mmoja …Kwamfano utaona wakati ule mitume wa Bwana Yesu waliposahau kuchukua ile mkate ambayo ilibaki wakaanza kugombana wao kwa wao kwa kulaumiana kwanini hawakuibeba, …lakini Bwana Yesu alipowasikia, mabishanao yao alitumia mfano mwingine kuzungumza nao kana kwamba alikuwa hamaanisha hicho walichokuwa wanakibishania kwa wakati huo..

Marko 8:13 “Akawaacha, akapanda tena chomboni, akaenda zake hata ng’ambo.

14 Wakasahau kuchukua mikate, wala chomboni hawana ila mkate mmoja tu.

15 Akawaagiza, akasema, Angalieni, jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.

16 Wakabishana wao kwa wao, kwa kuwa hawana mikate.

17 Naye Yesu akatambua, akawaambia, Mbona mnabishana kwa sababu hamna mikate? Hamfahamu bado, wala hamjaelewa? Je! Mioyo yenu ni mizito?

18 Mna macho, hamwoni; mna masikio, hamsikii? Wala hamkumbuki?

19 Nilipoivunja ile mikate mitano na kuwapa wale elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vimejaa vipande? Wakamwambia, Kumi na viwili.

20 Na ile saba kuwapa wale elfu nne, mlichukua makanda mangapi yamejaa vipande? Wakamwambia, Saba.

21 Akawaambia, Hamjafahamu bado?”

Unaona hapo? Bwana Yesu alitumia mfano wa chachu, na kusema, jilindeni na chachu ya mafarisayo…Lakini mitume wakadhani anazungumzia chachu ya mikate ya mafarisayo, hiyo ikiwafanya wazidi kugombana zaidi ili apate kuwanasa vizuri,..Hapo ndipo Bwana akapata nafasi ya kuwakemea kwa kukosa kwao ufahamu, akawaambia hamjafahamu bado?, mimi sizungumzii habari za mikate, mmesahau ni mikate mingapi mlikusanya kama masalia wakati ule?, hamjafahamu bado, hamjaelewa, mioyo yenu ni mizito, hamna imani kwa Mungu bado kuwa hata sasa anaweza kuwafanyia muujiza kama ule ule wa mikate mengine mkala mkashiba, pasipo kuwa na chochote?…lakini bado mnamtilia shaka Mungu?…Mimi sizungumzii habari za mikate ninaachomaanisha ni jilindeni na mafundisho ya mafarisayo..

Sasa utaona hapo mitume walipata mafundisho mawili, la kwanza ni kutokana na kile walichokuwa wanakifiria juu ya tumbo, kuwa Mungu bado anaweza kuwahudumia hata kama kunaonekana hakuna mlango wa kupata chakula, na cha pili ni kuhusu mafundisho ya mafarisayo (ambayo yanafananishwa na chachu/hamira) ambayo kazi yake ni kuumua na kupindua uhalisia wa Neno la Mungu…Lakini waliupata ule ujumbe uliokuwa unawahusu kwa wakati wao.

Ndivyo hivyo hata wakati ule Bwana Yesu alipokwenda hekaluni, akaona jinsi watu walivyoweka tumaini lao lote katika lile hekalu, jinsi lilivyokuwa limepambwa kwa namna ya ajabu, jinsi lilivyokuwa kubwa, na kukarabatiwa kwa muda mrefu wa miaka 46 na Herode..jinsi watu wengi walivyokuwa wanatoa sadaka zao kwa ajili ya hekalu lile.. Lakini jicho la Bwana Yesu lilikuwa linaona mbali zaidi yao, lilikuwa linaona muda si mrefu hekalu lile halitakuwepo, litakuwa limebomolewa, mahali pale patakuwa pamechomwa moto, watu watauawa na kuchinjwa kama kuku..lakini wale watu hawakuliona hilo, walikuwa wanajisifia tu majengo yake, hawaoni wakati umekaribia mji huo waliokuwepo ambao wanaupenda utateketezwa kwa moto…

Ndipo sasa wakati Bwana akiwa pale hekaluni anavuruga vuruga bishara zao.. wayahudi wakamfuata na kumuuliza, Ni ishara gani utuonyeshayo, kwamba unafanya haya?

Yesu akawajibu…

Yohana 2:19 “…..Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha.

20 Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?

21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake.

22 Basi alipofufuka katika wafu, wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa alisema hivi, wakaliamini lile andiko na lile neno alilolinena Yesu”.

Unaona, Bwana Yesu alimaanisha kweli juu ya hekalu la mwili wake kuwa atakufa na siku ya tatu atafufuka, lakini pia alitaka wafikirie vile vile juu ya habari za kubomolewa kwa hekalu, ili awafundishe jambo..lakini wengi wao hawakuwa tayari kutaka kujua zaidi, wakamwona kama karukwa na akili..anazungumza ujinga.

Lakini baadaye wanafunzi wake wanyenyekevu waliliweka hilo akilini…wakaanza tena kumwonyesha majengo ya hekalu lile ambalo yeye alisema watu walibomoe,..jinsi lilivyojengwa vizuri kwa mawe ya thamani…

Mathayo 24:1 “Yesu akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya hekalu

2.Hamyaoni haya yote? Amin, nawaambieni, Halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa”.

Lakini wanafunzi walivyosikia vile, hawakuishia pale, walizidi kuendelea kutaka kujua hatma ya hayo mambo itakuwaje, wakamfuata sasa faraghani, wakiwa peke yao tu Bwana, ndipo wakamuuliza..mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja kwako? Na ya Mwisho wa dunia? Maswali matatu.

Hapo sasa ndipo Bwana Yesu akaanza kuwafunulia hatua kwa hatua, mambo yatakayotendeka kuanzia ule wakati, mpaka siku mji ule utakapozingirwa na majeshi, na hekalu kubomolewa, mpaka siku za mwisho..ambayo maneno haya hata sisi wa kizazi hiki tunayatumia kama dira ya kutambua majira ya kuja kwa Bwana Yesu..Soma Mathayo 24, Marko 13, na Luka 21. Utaona habari zote za siku za mwisho zitakavyokuwa.

Lakini mafunuo hayo yote yalitoka katika Neno moja tu la Kubomolewa kwa hekalu..Kama mtume wasingetaka kujua zaidi, basi habari za kuteketezwa kwa Yerusalemu na warumi mwaka 70W.K, ambapo watu waliuawa kikatili, wasingekaa wajue pia habari za manabii wa uongo, na kusimama kwa chukizo la uharibifu wasingekaa wajue..

Vivyo hivyo hata sasa, tukiwa tayari kutaka kujua zaidi juu ya maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo katika Neno lake, kwa kumaanisha kujifunza Neno lake na sio kusoma tu kama gazeti, ndipo tunapojijengea nafasi nzuri ya kupokea mafunuo zaidi yamuhusuyo yeye.

Lakini kama tutasoma biblia juu juu tu, na kusema aa hii haiwezekani, au tunasema kile Bwana alimaanisha vile sio hivi..Tutabakia, kuujua upande mmoja tu wa maandiko..Na kufanana na wale watu waliomsulubisha pale msalabani na kumdhihaki…walisikia tu upande mmoja (livunjeni hekalu hili)

Zaburi 25:14 “Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake”.

Hivyo Bwana atusaidie tuzidi kumjua Zaidi yeye, mpaka tutakapofikia ukamilifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! UMEFANYIKA KUWA MWANAFUNZI WA BWANA?

Kuna mambo machache ya muhimu sana ya kufahamu pindi tu unapoamua kumfuata Yesu(kuwa mwanafunzi wa Bwana)..Mambo haya ni ya muhimu sana, ingawa wengi hawayajui na hata wakiyasikia wanaziba masikio yao wasitake kuyasikia wala kuyapokea. Na mojawapo ya hayo ni “kujikana nafsi”. Kama unasema umemwamini Yesu na bado hujajikana nafsi bado unakuwa hujaokoka.

Tafsiri ya kumfuata Yesu ni kujikataa wewe mwenyewe, kuyakataa mapenzi yako…kwamba hapo kwanza ulikuwa unapenda hichi na sasa unalazimika kukiacha, hapo kwanza ulikuwa unapenda kunywa hichi au kile na sasa unaamua kukiacha…hapo kwanza ulikuwa unapenda kufanya hivi au vile na sasa unakatisha, unaacha kufanya hayo mambo.

Hatua hiyo ukiikimbia kamwe huwezi kuzalisha chochote katika Imani.

Hali kadhalika, sio tu kuyakana mapenzi yako binafsi, bali pia na mapenzi ya Baba yako, au mama yako, au mwana wako… Baba yako hataki uokoke hapo huna budi kuyakataa Mashauri yake na kufuata ushauri wa biblia, mama yako anataka muende kwa mganga hapo huna budi kuyakataa mawazo yake hayo na kufuata ya kibiblia. Mtoto wako anakufanya usimtafute tena Mungu kama hapo zamani, unampenda kiasi kwamba upo tayari kula rushwa ili tu umpatie fedha za kwendea kwenye michezo…upo tayari kuiba na kutapeli au kufanya chochote kinachomchukiza Mungu ili tu umpatie mwanao kitu Fulani kitakachompendeza.

Bwana Yesu alisema maneno haya…

Mathayo 10:37  “Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38  Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.

39  Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.

Usipojikana namna hiyo bado hujawa mkristo kabisa…Bwana amekukana, na wala huna ushirika wowote na wewe, haijalishi mchungaji wako atakufariji kiasi gani, haijalishi utafarijiwa na wapendwa kiasi gani, haijalishi utasoma mistari mingine ya biblia na kuona inakufariji kiasi gani, haijalishi utakuwa unahudhuria kanisani namna gani.…Lakini mbele za Kristo umekataliwa!.. Anasema mwenyewe hapo juu… “ukimpenda baba au mama au mwana kuliko yeye humstahili”..yaani maana yake haumfai. Anakwenda kumtafuta mwingine wewe haumfai.

Hutaki kuamua kuacha pombe, kuacha kuishi na mwanamke/ mwanamume ambaye hamjaona…yeye kakukataa, huna ushirika naye…unasema umeokoka lakini uasherati kwako ni kama chakula, haijalishi unalipa zaka, au unahudhuria ibada kiasi gani, au unaimba kwaya, au ni kiongozi wa maombi kiasi gani…Neno lake lipo pale pale… MTU ASIYECHUKUA MSALABA WAKE AKANIFUATA, HANISTAHILI.

Unasema umeokoka lakini unachati kwenye magroup ya ngono, magroup ya mizaha na matusi, unasema umeokoka bado unafanya mustarbation kwa siri, bado unavaa kama wanawake wanaojiuza. Hapo hujajikana nafsi..Hivyo HUMFAI!..kulingana na maneno yake mwenyewe. Hata sala zako hazisikilizi kwasababu wewe sio wake.. una mambo yako na yeye ana mambo yake…una mapenzi yako na yeye ana mapenzi yake…hamhusiani kwa lolote.. Yeye anatembea na kujidhihirisha kwa wale waliojikataa nafsi zao,.waliyoyakataa mapenzi yao na kuamua kuyafuata mapenzi yake yeye. Wengine wote walio nje na Neno lake hilo, kasema hawajui. Haijalishi ni mchungaji au muumini wa kawaida..kama hajajikana nafsi HAMFAHAMU.

Kama unaona aibu kuacha pombe, kama unaona aibu kumwambia ukweli huyo mwanamume/mwanamke unayeishi naye sasa kwamba umeokoka na hivyo Maisha ya dhambi huwezi kuishi tena…fahamu wewe na Bwana Yesu ni vitu viwili tofauti, kama unaona aibu kuacha kuvaa suruali na nguo zinazobana na na vimini kupaka make-up kwamba unaogopa/unaona aibu utaonekanaje mbele za wale waliozoea kukuona hivyo, au utaonekanaje mbele ya mume wako.. Kama unaogopa kufanya hivyo…tayari Kristo hayupo na wewe.

Luka 9:23 “Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

24  Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.

25  Kwa kuwa yamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, kama akijiangamiza, au kujipoteza mwenyewe?

26  KWA SABABU KILA ATAKAYENIONEA HAYA MIMI NA MANENO YANGU, MWANA WA ADAMU ATAMWONEA HAYA MTU HUYO, ATAKAPOKUJA KATIKA UTUKUFU WAKE NA WA BABA NA WA MALAIKA WATAKATIFU”

Kama ulikuwa hujajikana nafsi na ulikuwa unadhani unaye Yesu moyoni mwako..Tubu tena leo!..Na baada ya kutubu, GEUKA! Acha yale maovu uliyokuwa unayafanya pasipo kutazama kwamba utamkwaza mtu au utachukiwa na mtu, au utagombana na mtu…acha ulevi, acha rushwa, acha uasherati, acha kujichua, acha kampani za marafiki wabaya..Wengi wanasema wamejaribu kuacha kufanya uasherati na kujichua wameshindwa hivyo wanahitaji maombi…nataka nikuambie bado hujajikana nafsi! hakuna maombi yoyote ya kuondoa hiyo tabia ndani yako..ni wewe kuamua kuiacha!…mbona hulali na kuku anayekatiza hapo pembeni yako, au mbuzi au ndugu yako wa damu, au mzazi wako? Hata ile hamu tu haipo!..hapo umeombewa na nani mpaka ukaishinda hiyo hali?..Umeona? hivyo hata hayo mengine usitafute kuombewa..Ni kutoyaendekeza tu na kuyaacha kabisa.

Na baada ya kutubu, usifanye tena hayo, ndipo Roho Mtakatifu atakuongezea uwezo wa kuyashinda hayo. Bwana anakupenda sana.

Bwana akubariki sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.

NI KWANINI MUNGU HAONEKANI?

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini tofauti kati ya Husuda, faraka na uchafu?

SWALI: Husuda ni nini?, faraka ni nini? na uchafu ni nini katika biblia?


JIBU: Husuda limeonekana sehemu kadhaa katika biblia na maana yake ni “WIVU”  na mtu kuwa na HUSUDA/WIVU ni Dhambi…..Ifuatayo ni baadhi ya mistari iliyozungumzia husuda.

Wagalatia 5:21 “HUSUDA, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”

Na mwingine ni huu…

1Petro 2:1 “Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na HUSUDA na masingizio yote”

Na mingine ambayo unaweza kusoma kwa muda wako ni hii; Tito 3:3,Mathayo 27:18, Marko 15:10, Warumi 1:29, 1Wakorintho 3:3 n.k

Faraka ni nini?

Neno Faraka inatokana na neno mafarakano…Tafsiri yake inakaribiana na tafsiri ya neno matengano, na kuwa na faraka ni dhambi, Biblia imekataza wakristo kufarakana..na baadhi ya mistari kwenye biblia inayozungumzia “faraka” ni kama ifuatayo.

1Wakorintho 1:10 “Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu FARAKA, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja”

Na mwingine ni..

1Wakorintho 12:25 “ili kusiwe na FARAKA katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe”

Na mingine ambayo unaweza kuisoma kwa muda wako ni kama ifuatayo; 1Wakorintho 11:17 na Wagalatia 5:20.

Uchafu ni nini?

Uchafu kila kitu kinachomtia mtu unajisi…mfano uasherati, ulawiti, ufiraji, ulevi na mambo yanayofanana na hayo, vile vile wachafu wote hawataurithi ufalme wa mbinguni biblia inasema hivyo….Baadhi ya mistari katika biblia inayozungumzia uchafu ni kama ifuatayo.

2Wakorintho 7:1″Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”

Na mwingine ni huu..

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, UCHAFU, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Na mingine inayozungumzia uchafu ni Waefeso 4:19,Wakolosai 3:5, 1Wathesalonike 4:7 n.k

Je umeokoka?..Je una husuda? au una faraka au ni mchafu?..Biblia imesema watu wa namna hiyo hawawezi kuurithi uzimwa wa milele…Mpe Kristo leo maisha yako ayaokoe kama hujaokoka.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAJISAIDIA SEHEMU ZA WAZI.

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

WAKAMWACHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SALA YA TOBA

Sala ya Toba ni nini?..Je ni lazima kuongozwa sala ya Toba pale mtu unapoamini?

Jibu: Sala ya Toba ni sala, ambapo mtu mmoja aliyeamini anamwongoza mwingine ambaye ndio anaingia katika Imani..Mtu anayeingia katika Imani anakuwa anafuatiliza maneno yale kwa Imani na kumkiri Yesu kwa kinywa chake, kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yake na alikufa kwa ajili ya dhambi zake.

Sasa hakuna maagizo yoyote katika biblia yanayosema mtu baada ya kumwamini Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake..basi anahitaji kuongozwa sala ya toba. Hakuna andiko kama hilo,  Lakini lipo andiko moja tu linalosema..

Wagalatia 6:2 “Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo”

Maana yake ni kwamba..aliye dhaifu wa Imani hana budi kushikwa mkono na kusaidiwa kusimama na hatimaye kutembea mwenyewe…Kama vile mtoto mchanga anayejitahidi kusimama ili atembee…Mzazi huna budi kumshika mkono na kumnyanyua na kumsaidia atembee..

Vivyo hivyo katika safari ya Imani. Mtu anayetoka katika dhambi moja kwa moja na kumpokea Kristo ni sawa na kitoto kichanga kilichozaliwa…wengi wa hawa hata kusali tu hawajui, zaidi ya yote hata wakiomba wanahisi Mungu hawasikii…wanakuwa hawajamjua Mungu, wala hawaujui uweza wa Mungu vizuri. Hivyo unapowashika mkono na kuwasaidia kusali pamoja nao kwa mara ya kwanza…Imani zao ni rahisi kukua na kunyanyuka na kusonga mbele.

Lakini ukiwaachia kwamba waombe wenyewe katika siku za kwanza kwanza…ni rahisi shetani kuwaletea mawazo kwamba bado hawajaokoka wala kumpokea Yesu..Hivyo wataendelea siku chache na baada ya hapo ni rahisi  kurudi nyuma. Wapo wachache ambao wanaweza kujishika wenyewe hata kusimama na kukua kiroho bila hata kuongozwa sala hiyo.. lakini wengi wa wanaomwamini Bwana Yesu katika hatua za awali wanahitaji msaada mkubwa sana..Kwasababu ni watoto wadogo kabisa kiroho waliozaliwa.

Lakini baada ya kipindi fulani, wakishakuwa basi hawana haja ya kushikwa tena mkono bali wanapaswa wakawasaidie wengine walio dhaifu kama wao walivyokuwa.

Hivyo sala ya Toba inatokana na upendo wa mkristo kwa mtoto mpya aliyezaliwa kiimani, na sio dhambi kuwaongoza watu wala kuongozwa. Hivyo upendo hauna masharti..Bwana wetu Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kusali..si zaidi sisi kuwafundisha na kuwaongoza sala wale walio wachanga kiroho katika hatua za awali?

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA?.Mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAJISAIDIA SEHEMU ZA WAZI.

Kuota Unajisaidia sehemu za wazi. Maana yake ni nini?


Ndoto hii, imekuwa ikiotwa mara kadhaa wa kadha na watu wengi. Kwa mfano mtu mmoja alinisimulia ndoto yake, anasema katika ndoto alijikuta yupo stendi ya basi, na pale palikuwa na watu wengi sana, ghafla akaanza kujisaidia lakini yeye alikuwa anajitahidi kufanya vile asionekana..Na alipomaliza akidhani hajaonekana wakati akiwa anarudi nyumbani mtu mmoja ambaye alikuwa anamjua akamfuata akamwambia mbona nilikuona unajisaidia pale stendi?..Anasema kwa kweli aliposikia hivyo   alijisikia aibu sana.

Na ndivyo ilivyo ndoto za namna hii, ni lazima mwisho wa siku utajisikia aibu tu, wengine wanaota wamejinyea, mavi, wengine wakiwa shuleni, kazini, uwanjani n.k. ..kwasababu kitendo cha kujisaidia huwa sikuzote ni cha aibu na ndio maana kinafanyika kwa siri chooni.. Lakini ikiwa unajisaidia kwa wazi ni Mungu anakuonyesha ni jinsi gani, mambo yako machafu yatakavyokuja kuwa dhairi siku moja mbele za watu wengi..kama hutatubu dhambi zako au hutasimama imara leo hii kwa Mungu wako.

Inaweza isiwe sasa, lakini kumbuka siku ile ya hukumu inafika..ambapo mambo yote yaliyokuwa yanafanyika kwa siri yatawekwa wazi.

2Wakorintho 5:10  “Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya”

1Wakorintho 4:5  “Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye ATAYAMULIKISHA YALIYOSITIRIKA YA GIZA, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu”.

Unaona? Hivyo ikiwa hujatubu dhambi zako, maisha yako bado ni machafu, YESU KRISTO bado hajaingia ndani yako kukusafisha uwe hai..Ni heri ukaamua kufanya hivyo kabla nyakati hizo mbaya hazijafika..Huu ndio wakati wa wewe, kusema basi..Nahitaji kuanza upya na Kristo..Usiseme mimi ni muislamu, hata wewe Unapaswa umgeukie YESU Kristo kwasababu yeye ndio njia na kweli na Uzima ya kukufikisha wewe mbinguni.

Ukimkaribisha leo maishani mwako, atakupokea na kukufanya upya. Unaona ni hali gani ulijisikia ulipojiona unafanya kitendo cha aibu katikatika ya umati wa watu..Sasa embu fikiria siku ile ya hukumu, Maisha yako yataanza kutazamwa  na Mungu mbinguni, pamoja na majeshi ya malaika zake, pamoja na watakatifu wa Mungu mamilioni kwa mamilioni..wote wanakutazama siku ile ulivyokuwa unazini na mume au mke ambaye si wako, watakutazama ulivyokuwa unajisaga kisirisiri mwenyewe nyumbani mwako..watakutazama ulivyokuwa unafanya mustarbation kwa siri chumbani, watakutazama ulivyokuwa unaangalia picha za uchafu, lakini kwa nje unaonekana wewe ni mwema, watakutazama mimba ulizotoa japo ulikuwa unajulikana kama ni mwanamke mstaarabu, machoni pa watu watu..watakutazama ufiraji uliokuwa unaufanya kwa mkeo, japo kwa nje unaonekana mtu unayejiheshimu….Siku hiyo watakutazama..Ni itakuwa ni AIBU KUU, ambayo utatamani hata usingezaliwa.

Lakini hayo yote ya nini mpaka yakukute wakati Kristo bado anakupenda?..Njoo kwa YESU ayabadilishe maisha yako leo hii..biblia inasema..saa ya wokovu ni sasa..Umeshindwa kuacha pombe, lakini Ukimruhusu Yesu aingie maishani mwako, ataikata hiyo kiu ya pombe, itakwisha kabisa..Umeshindwa kuacha uzinzi lakini ukimfuata Yesu leo hii, atakusaidia na hiyo hali utaishinda..na mambo mengine yote maovu unayoyatenda saa hii, ukimkabisha Yesu maishani mwako atakugeuza..anachohitaji kwako ni moyo wa toba tu basi..Na kumaanisha kweli kweli wala sio kujaribu..

Hivyo ikiwa umemaanisha kufanya hivyo..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

KUOTA UPO UCHI.

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MTETEZI WAKO NI NANI?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.

Muonekano mpya wa yesu baada ya kufufuka, unabeba somo gani?


Bwana Yesu alipokuwa bado anaishi duniani, ilikuwa ni rahisi kumtambua, kwani kwa sura yake tu watu waliweza kumtambua kuwa huyu ndiye. Lakini mara baada ya kufufuka kwake, mambo yalikuwa tofauti kabisa, haikuwezekana kumtambua tena Bwana Yesu kwa sura yake..Ilihitaji kipimo kingine tofauti..

Hilo tunalithibitisha sehemu kadha wa kadha, wengine walipomwona walidhani ni mtunza bustani makaburini, wengine walidhani ni mpita njia tu, na wengine walidhani ni mzee Fulani tu anapunga upepo beach..Na kama wangekikosa hicho kipimo kingine ndani yao cha kumtambua Yesu basi wasingekaa wamjue daima haijalishi huko nyuma waliishi naye na kutembea naye na kulala naye muda mrefu kiasi gani..kamwe wasingemjua.

Kwamfano embu tumwangalie Mariamu Magdalene, yeye ile siku ya kwanza ya juma, siku Yesu aliyofufuka, ndio aliyekuwa wa kwanza kufika pale makaburini, lakini alipomkosa Bwana, akidhania kuwa ameibiwa, alikwenda kuwaambia mitume, nao walipokwenda hawakukuta mtu kaburini.. wakaamua kuondoka zao, Sasa wakati Mariamu akiwa pale kaburini analia, kulikuwa na mtu yupo pale muda mrefu tu, anazunguka zunguka, pengine wakina Petro walimwona wakadhani ni watu wale wasio na shughuli wanaozunguka makaburini, lakini Mariamu alipokaa pale muda kidogo akiwa analia, ndipo Huyu mtu ambaye alimwona kama mtunza bustani akamfuata na kumuuliza unatafuta nini?.

Mariam akasema: ikiwa ni wewe ndio umemuiba Bwana wangu niambie..Kumbe hakujua anayezungumza naye ni YESU mwenyewe..Ndipo Yesu akalitaja jina lake Mariamu!..Na alipolitaja tu, Hapo hapo Mariamu akaitambua sauti ile, ni ile sauti yake yenye uweza, sauti ile ile iliyomwita Lazaro atoke makaburini kipindi kile kule nyuma, sasa imemwingia na yeye mpaka kwenye vilindi vya moyo wake ikampa uhakika kuwa huyu ndiye BWANA….Haikujalisha sauti ilikuwa ni ya mtu mwingine,inayofanana na mtu wa taifa lingine, lakini uweza tu wa ile sauti ulimpa uhakika kwamba huyu ndiye Bwana..(Soma..Yohana 20:1-18).

Lakini kama Mariamu asingekuwa na ushuhuda huo huko nyuma, basi ingekuwa ni rahisi kumpoteza Yesu..

Vivyo hivyo wale watu wawili ambao walikuwa wanakwenda katika kile Kijiji cha Emau, nao pia walipokuwa wanatembea njiani, Yesu alikutana nao isipokuwa katika sura nyingine..Na akaanza kuzungumza nao habari za kutabiriwa kwake, kuja kwake, na kufufuka kwake..Wale watu waliposikia tu yale maneno, jinsi yalivyokuwa yenye nguvu kwa namna ile ile waliyokuwa wanamsikia Bwana akifundisha makutano akiwa bado hai, hawakumuacha aondoke hivi hivi, wakamkaribisha nyumbani kwao, ndipo baada tu ya kuumega mkate na kuwapa, wakafumbuliwa macho wakatambua kuwa alikuwa ni YESU. Na saa hiyo hiyo akatoweka mbele ya macho yao.(Luka 24:13-33)..Lakini kama wasingetilia maanani uweza uliokuwa unatoka ndani ya maneno yale..wasingekaa wamtambue Kristo.

Mwisho kabisa Petro na wenzake, walipokuwa wanakwenda kuvua samaki, baada ya kuhangaika usiku kucha hawajapata kitu..Asubuhi yake kwa mbali walimwona mtu kama mzee akiwa pwani, mwenye sura wasioijua, mtu yule akawauliza wanangu mmepata kitoweo, wakasema hapana Bwana, akawaambia, tupeni jarife upande wa pili, wakidhani ni mzee tu wa kawaida anawashauri, wajaribu bahati yako, ..Na walipotupa tu jarife, wakapata samaki wengine..Mwanafunzi mmoja alipoiona ile ishara, akatambua kuwa hii ni ishara ile ile aliyotufanyia Bwana kipindi kile akiwa hapa duniani..Ndipo Yule mwanafunzi akamwambia Petro aliyetupa maagizo haya ni Bwana Yesu..Petro kusikia hivyo muda huo huo akapiga makasia kumfuata Pwani..

Biblia inatuambia walipomwona Bwana japo aliwatokea katika sura nyingine tofuati kabisa..Lakini hakuna hata mmojawao aliyetaka uthibitisho kama yeye ni Bwana kweli au la, Wote walipata uhakika ule, kwa ule uweza wake mkuu , na yale maneno aliyokuwa anazungumza nao akiwa pale ufukweni..(Yohana 21:1-25)..Lakini kama wasingeyaona matendo makuu kama yale Bwana aliyowahi kuwafanyia huko nyuma, kamwe wasingejua hata kama yule ni YESU. Wangedhani ni mzee Fulani tu amewapa dili la kazi.

Hivyo ndivyo Kristo alivyochagua kujidhihirisha kwa watu baada ya kufufuka kwake..Mpaka ikawafanya hata wengine wamtilie shaka..Hao ndio wale ambao walioukosa ushuhuda wake ndani yao..ndio wale waliokuwa wanalitazama umbo la Yesu, lakini hawayatafakari matendo yake, na ishara zake.

Mathayo 28:16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu. 17 Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka”.

Sasa kwa mabadiliko hayo, mitume kuanzia huo wakati wakatoa akili zao kabisa katika kuitegemea sura ya YESU, kama kipimo cha kumtambua Kristo mpaka kuutegemea ushuhuda wa YESU Maishani mwao.

Hivyo sura ya Yesu ikawa haina umuhimu tena kwao..Na ndio maana utaona Mitume mahali popote hawakuwahi kujisifia umbile la Yesu au Sura yake, au sauti yake..Bali ule Ushuhuda wa YESU uliokuwa ndani yao, ndio uliowafanya wamjue na kumtambua Yesu.

Vivyo hivyo leo hii KRISTO yupo kila mahali, lakini kama umeukosa ule ushuhuda wake ndani yako, utamwona tu kama mtunza bustani, utamwona tu kama mpita njia, utamwona tu kama mzee Fulani..

Ndio maana kuna umuhimu sisi tunaojiita wakristo, kujifunza biblia sana..kwasababu wakati utafika Kristo atajidhihirisha kwako, lakini hutamtambua kwasababu huujui ule ushuhuda wake alipokuwa hapa duniani ulivyokuwa.

Kwamfano Injili ya Kristo inapohubiriwa kwako, na unaona kabisa imekuja kwa ukali, na uzito, na kwa nguvu, labda inakutaka wewe ufanye jambo Fulani.. Sasa kwa kuwa wewe huna ushuhuda wa Yesu ndani yako, unaokushuhudia hata katika maandiko kuwa kulikuwa na watu wawili wa Emau, ambao neno la Kristo liliwajia kwa uzito kama huo, wakachukua hatua ya kusikiliza mpaka mwisho..Wewe unapuuzia, Unadhani ni mlokole Fulani anahubiri, au mchungaji tu Fulani, au kijana tu Fulani anauhibiri..kumbe hujui unampuuzia Kristo mwenyewe.

Na wakati huo huo unakesha kuomba kwamba Bwana akutokee, unataka akutokee vipi? Unataka umwone kavaa mavazi meupe, mwenye nywele ndefu, ndio umtambue?. Hilo wazo na ufute. YESU ameshafufuka, haji kwetu kwa muonekano ule tena.

Huu ni wakati wa kumjua yeye kwa ushuhuda wake.Hapo ndipo tutakapomwona akitembea katika Maisha yetu kila siku. Na hiyo inakuja pale tu Neno la Kristo linapokaa kwa wingi ndani yetu.

Vingenevyo tutamtilia shaka tu sikuzote, hata akitokea kwa sura ipi, kama wale wengine walivyomtilia shaka kule Galilaya, na wewe utamtilia shaka hivyo hivyo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye boksi la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

TULICHUNGUZE UMBO LA YESU NA MWENENDO WAKE.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ni dhambi kuchukua riba?

Biblia inasema tusikopeshe kwa riba, je! Wanaowakopesha watu kwa riba wanafanya dhambi?


JIBU: Biblia imezuia kutozana riba ndugu kwa ndugu tu..lakini kwa wengine nje ya ndugu sio dhambi kuwatoza riba.

Kumbukumbu 23:19 “Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;

20 mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki”.

Kwa mfano ndugu yako unamwona anayoshida, anaomba umkopeshe fedha kidogo, halafu wewe unatumia ile fursa kumwambia aongeze na kiwango kingine cha fedha juu yake(riba), kama faida yako, Hiyo ni dhambi, akikopa, basi arudishe kile kile alichokopa..Usigeuze shida za ndugu yako kuwa mtaji..

Katika hali ya kawaida hata bila kuambiwa na mtu au kufundishwa, ukiwa na nyumba ya biashara, halafu ndugu yako wa karibu amekuja kukaa hapo kwa kipindi fulani tu.. Huwezi kumwambia alipie kodi kamili kama watu wengine, anaweza kulipia tu zile gharama za kawaida ndogo ndogo lakini sio kulipia kila kitu..hakuna mtu mwenye utu anaweza kumfanyia hivyo ndugu yake.

Hali kadhalika katika Ukristo, wote tuliomwamini Yesu Kristo tunafanyika kuwa ndugu..Upendo wa Kristo unatuunganisha pamoja.tunakuwa tunapendana bila masharti..Upendo huo unatufanya kusiwepo hata na hamu ya kutaka faida kutoka kwa ndugu zetu katika Imani kama vile ilivyo katika ndugu zetu wa mwili. Ndio hapo biblia inatuasa kwamba tusitozane riba sisi kwa sisi. Lakini kwa mtu mwingine nje na ndugu zetu wa kimwili na kiimani, tunaweza kuwatoza ili tupate faida katika tunavyovifanya..kwasababu riba ndio inayokifanya kile kitu au ile shughuli ile iendelee mbele zaidi.

Lakini tukiwatoza ndugu zetu kwa lengo la kupata faida hapo upendo wa Kristo haupo ndani yetu, na hivyo tunafanya dhambi na kumkosea Mungu.

Ezekieli 22:12 “Ndani yako wamepokea rushwa ili kumwaga damu; umepokea riba na faida; nawe kwa choyo umepata mapato kwa kuwadhulumu jirani zako, nawe umenisahau mimi, asema Bwana MUNGU.

 Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEACHWA NA GARI.

Kuota umeachwa na gari, Maana yake ni nini?


Hii ni ndoto inayowapata watu wengi sana.Hususani wale ambao walishaokoka, lakini mambo mengine ya kidunia yanawasonga sasa hivi..Au walisharudi nyuma kabisa na kuacha wokovu

Ndogo hii inakuja katika maumbile tofuati tofauti wengine wanaota wameachwa na ndege, wengine wanaota wameachwa na wenzao ambao walikuwa wanakwenda pamoja,  lakini wengi wao wanaota wameachwa na gari walilokuwa wanasafiria.

Kwa mfano mtu mmoja alinihadhithia ndoto hii, ambayo rafiki yake aliiota ikawa inamsumbua sana..

Aliota alikuwa kwenye basi anasafiri, sasa lile basi likafika mahali kwenye foleni, na yeye baada ya kuona vile limesimama pale,  akaamua kushuka kidogo, na aliposhuka tu lile gari likaanza safari, anasema akaanza kulikimbilia, kumbe wakati analikimbilia kulikuwa na watu wengi nao wanalikimbilia lile gari, mchanganyiko wamama, watoto, na watu wengine n.k. Lakini baadaye yeye akajitahidi kwa nguvu sana kuliwahi akafanikiwa kuingia lakini kwa shida sana, na alipofika ndani akakuta siti yake imeshakaliwa na mtu mwingine..Ikimbidi ajikalie tu mwenyewe pale pembeni, lakini baada ya muda mfupi mzee mmoja akatokea akamsukuma atoke hata pale alipokuwa amekaa, akiwa hana sehemu ya kukaa kwa bahati nzuri akaona siti moja ipo wazi pembeni yake akaenda kuikalia na muda huo huo akashtuka..

Nilipo hoji nikagundua kuwa mtu huyo alikuwa ameokoka lakini baadaye alirudi nyuma, amesongwa na mambo ya ulimwengu huu..Na pale Mungu alikuwa anamwonyesha mwenendo wake jinsi ulivyo alipoona anakawia kukipata kile alichokuwa anakitafuta katika njia yake ya wokovu akaamua kwenda kukitafuta katika mambo ya ulimwenguni..Na hiyo itamgharimu kwasababu upo wakati atatamani kurudi lakini itakuwa ngumu sana kwake kwasababu wokovu sio safari ya kujaribu jaribu kama yule mke wa Lutu alivyofanya, aligeuka mara moja tu, na saa hiyo hiyo akageuka kuwa jiwe la chumvi.

Ikiwa na wewe ni mfano wa mtu kama huyu umeota ndoto ya namna hii umeachwa na basi ujue huo ni ujumbe kamili kutoka kwa Mungu, kuwa unaupoteza wokovu wako, na kuwa ukiendelea katika hali hiyo inayoendelea sasahivi ya kujitenga na wokovu, au kusongwa na mambo ya ulimwengu basi hautaupata tena daima na nafasi yako atapewa mwingine..

Lakini kama wewe hujaokoka kabisa yaani Bwana YESU hajayabadilisha maisha yako, wala huna habari na Mungu.. wewe umekuwa mkristo jina tu, au Muislamu, au huna dini kabisa..Hapo ni Mungu anakuonyesha jinsi gani inavyoogopesha na inavyosikitisha mtu unapoachwa safarini..Sasa jiulize, kwa mtu ambaye haujaanza kabisa safari, yeye atakuwa katika hofu nyingi kiasi gani?..Ndivyo ilivyo hali yako wee Upo katika dhambi, upo mautini, mbingu ipo mbali na wewe.

Sikia sauti ya Kristo, inayokuambia njoo kwangu leo.. Uanze naye safari njema ya kuelekea ufalme wa mbinguni. Kukutana na ujumbe kama huu si bure, Ni Mungu anazungumza na wewe.

Yesu anasema..

Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.(Yohana 14:6)..

Ikiwa unataka na wewe kwenda mbinguni basi YESU ndiye njia..wala hakuna mwingine.

Vile vile biblia inasema..

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo”.

Dunia hii inapita na mambo yake..Utauhangaikia huu ulimwengu mpaka lini, Ukifa leo, ni nani atakuwa mgeni wako huko uendako?. Ni nani atakayekupokea, utaulizwa safari yako ilikuwa ya kuelekea wapi, utajibu nini..Kwanini leo usichukue tiketi yako mkononi, uanze maisha mapya na Bwana Yesu..Kwasababu ni kweli atayabadilisha maisha yako na wewe mwenyewe utaona ni jinsi gani umeianza safari njema, ya uhakika na yenye matumaini..Ulevi, uzinzi, starehe, sema leo ni mwisho ninaamua kumgeukia Kristo.

 Ikiwa unataka kufanya hivyo leo.

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

Maswali na Majibu

KUOTA UPO UCHI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

USHUHUDA WA RICKY:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya huu mstari “sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”

Swali: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema.. “sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”? Ni kwa namna gani atatupwa nje? Na ni kwanini atupwe nje na sio chini?


JIBU: Tusome huo mstari…

Yohana 12:31 “Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo; sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.

32 Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu. ”

Kama ukichunguza vizuri hapo utaona anatumia neno “ATA” na si “ALI”.. yaani atatupwa na sio alitupwa au anatupwa..Ikionyesha kuwa ni kitendo kijacho ambacho bado hakijatokea..

Kumbuka tena hapo anasema atatupwa NJE, na sio atatupwa CHINI.. Shetani alishatupwa chini zamani sana, Kile kitendo cha yeye kuasi kule mbinguni biblia inasema kilimsababishia atupwe chini yeye pamoja na malaika zake (soma Ufunuo 12:7-10), Hivyo akawa ameganda tu hapa duniani kwenye giza nene, bila shughuli yoyote, wala tumaini lolote, akisubiria siku yake ya maangamizo ifike,apotee.. Mpaka sisi tunakuja kuumbwa, yeye alikuwa bado yupo hapa hapa anatazama tu, mwanadamu akimilikishwa kila kitu..

Lakini Adamu alipoasi, ndipo shetani akapata nafasi ya kuingia ndani ya ufalme ambao ulikuwa ni milki ya mwanadamu tu, Adamu akaiuza ile hati yake ya umiliki kwa shetani..Na tangu huo wakati shetani akapata nguvu akawa na mamlaka juu ya mambo mengi sana katika huu ulimwengu, akawa na uwezo hata wa kuwaendea wafu waliokufa(ikiwemo watakatifu) na kuzungumza nao kama alivyofanya kwa Samweli, akawa na uwezo hata wa kuzuia maombi ya watakatifu, yasimfikie Mungu …Yaani kwa ufupi japo watakatifu walikuwa wanalindwa na Mungu..lakini bado shetani alikuwa na uwezo fulani juu yao..

Sasa wakati ulipofika wa Mungu kuirudisha ile hati ya umiliki kwake, Ndipo akamletea mwanadamu aliyefanana na Adamu, ndiye Bwana wetu YESU KRISTO.. yeye alikuja kufanya kazi moja, na kazi yenyewe ilikuwa ni KUMFUKUZA SHETANI atoke ndani ya milki ya wanadamu..

Lakini si kwa wanadamu wote, bali wale tu watakaomwamini na kumpokea..

Na ndio maana sasa utaona Bwana Yesu anasema hapo.. sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”? Ikiwa na maana bado kitambo kifupi tu atakwenda kutupwa nje ya milki ya utawala wa watakatifu..Na tukio hilo lilikuja kutimia siku ile, pale KALVARI Bwana Yesu alipokufa na kuchukua funguo zote za uzima, pia na za kuzimu na mauti (Ufunuo 1:18).

Sasa tangu huo wakati hali yake shetani ikarudia kama mwanzoni alipokuwa pale Edeni kabla ya Adamu kuasi, akawa hana nguvu yoyote kwa wale watu waliomwamini Yesu na kuoshwa kwa damu yake, akawa hawezi kujiamulia tena kitu chochote juu yao, hawezi kuwaendea wafu na kuzungumza nao tena, hawezi kumdhuru mtu yoyote wa Mungu, ikiwa Mungu hajaruhusu.

Hivyo leo hii mtu aliyeokoka, hahitaji kuogopa wachawi, hahitaji kuogopa mapepo au majini, hahitaji kuwa na wasiwasi labda shetani atamuua, hahitaji kuwa na hofu labda maombi yake yamezuiliwa sehemu fulani hapo juu ya wakuu wa anga kama Danieli.. Sasa hivi shetani hawezi kufanya hivyo kwa mtu aliyeokoka kweli kweli.

Lakini kama upo nje ya Kristo..basi Maisha yako yapo hatarini..Wewe unapaswa uwe na hofu ya kila kitu, hukosei kuwaogopa wachawi, au majini, au wanadamu..kwasababu huna ulinzi wowote wa Mungu na shetani bado yupo ndani ya maisha yako, kila siku akikupangia njama za kukuangamiza..hivyo upo sahihi kabisa kuwaogopa kikweli kweli.

Ni neema za Mungu tu zinakushikilia ili utubu ndio maana upo hai.. Mpe Kristo Maisha yako kama hujampa, Uwe salama.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001312.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Mapambano dhidi ya shetani.

Katika vita siku zote wanaopambana ni wanajeshi dhidi ya wanajeshi..na si raia dhidi ya wanajeshi…Na ndio maana vita huwa vinakuwa ni vigumu sana na vikali…hiyo yote ni kwasababu mwanajeshi anafundishwa kwenda kupambana na mwanajeshi mwenzake ambaye anautaalamu kama yeye, ambaye ni mjuzi wa silaha kama yeye, ambaye anavaa dirii ya kuzuia risasi kifuani kama yeye anavyovaa..ambaye anavaa chepeo kichwani ambayo ni ngumu isiyoweza kuingia risasi kama yeye anavyovaa…ambaye anasilaha na vifaa vya kijeshi kama vya kwake…

Ndio maana unaweza kuona Taifa moja linajiongezea uwezo wa silaha za kijeshi kila kukicha ni kwanini?….Ni kwasababu wanajeshi wanapokwenda vitani wanakwenda kupambana na watu wanaotumia vifaru kama wao…wanakwenda kupambana na watu wenye ujuzi kama wao…Kwa ufupi wanakwenda kupambana na watu wanaofanana na wao karibia kila kitu..na hawaendi kupambana na raia.

Na wakishafanikiwa kumaliza jeshi la maadui basi huwa hawana muda ya kuwaua raia,.. wanachokifanya ni kuchukua tu rasilimali zao, na kuwachukua raia mateka au kuwafanya watumwa wao basii…hawana muda wa kuwaua…kwasababu vile vifaru walivyokuwa wanavitumia vitani havikuwa kwaajili yao bali kwaajili ya wanajeshi wao…

Sasa na sisi wakristo tunafananishwa na wanajeshi waendao vitani…na Biblia inatuambia “Tutwae silaha zote za Mungu”

Waefeso 6:11  “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani

12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15  na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16  zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17  Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

18  kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;”

Kumbuka na sisi hatuendi kupigana na watu wa shetani…bali tunakwenda kupambana na Adui yetu Shetani mwenyewe na mapepo yake. Na kama sisi tulivyo ndivyo na yeye alivyo…kama na sisi tulivyo na upanga mkononi na yeye anao upanga mkononi..kama sisi tulivyo na ngao na yeye pia anayo ngao ya kuzuia mishale kutoka kwetu..kama sisi tulivyo na chepeo kichwani mwetu na yeye ni hivyo hivyo anayo ya kwake…Kwahiyo hapo vita ni lazima viwe vikali tu..kinachohitajika ni kuwa na uwezo wa kuutumia upanga kuliko yeye, kuwa na uwezo wa kuitumia ngao kuliko anavyoitumia yeye, kuwa na uwezo wa kutumia chepeo kuliko anavyoitumia yeye..hiyo ndio njia tu ya kumshinda Adui shetani. Lakini kama yeye anauwezo mkubwa wa kutumia silaha zake kuliko wewe basi atakushinda tu, haijalishi una upanga mkononi, au ngao au chepeo….

Sasa Kwanini tunashika upanga wa Roho mkononi ambao ni Neno la Mungu?..Ni kwasababu Adui yetu na yeye ameshika upanga mkononi…kutupinga sisi…Ndugu usifikiri shetani halijui Neno?…. Analifahamu vizuri sana..na kama biblia inavyosema Neno la Mungu ni upanga ukatao kuwili…maana yake adui akiupata anaweza kuutumia kukuua hata wewe…Hivyo shetani naye ameshikilia upanga wa Neno la Mungu akipambana dhidi yetu…

Kama alivyopambana na Bwana Yesu akiwa kule jangwani…alimwambia Bwana Yesu “imeandikwa hivi katika maandiko”…Na Bwana akawa anamjibu “tena imeandikwa hivi”..Katika ulimwengu wa roho hapo ni pambano kati ya Bwana Yesu na shetani…shetani anaurusha upanga dhidi ya Bwana na Bwana anauzuia na kwa ushapu anamkata na upanga wake ulio mkononi..

Lakini endapo Bwana angekuwa halijui Neno..shetani angemkata kwa Neno hilo hilo..Lakini kwasababu alikuwa analijua kulitumia Neno vizuri aliweza kumshinda shetani..

Kwahiyo ukienda kupambana na Adui shetani na mapepo yake..kama hulijui neno na namna ya kulitumia ipasavyo hakika atakumaliza, kwasababu na yeye kaushikilia upanga unaofanana na wako….(Mapambano dhidi ya shetani  yatakuwa makali sana kwako)

Katika siku hizi za mwisho biblia imetabiri kuwa upendo wa wengi utapoa…Upendo unaozungumziwa hapo ni upendo wa kumpenda Mungu…na si wa kumpenda mwanamke/mwanamume. Watu wengi watakuwa hawana habari ya Neno la Mungu. Leo utamwuliza mtu mara ya mwisho kujifunza mwenyewe binafsi biblia ni lini? Bila kusubiri kutafsiriwa na mtumishi Fulani?..atakuambia ni muda mrefu sana..na hata akisoma, anasoma sura moja mbili kamaliza…Nyakati hizi mbaya tulizopo sio nyakati za kusoma sura moja ya biblia na kutulia baada ya wiki ndio unasoma nyingine…hapo shetani hashindani na wewe anakuona tu kama raia ambaye huna madhara kwake hivyo anakuchukua mateka tu, kama wanajeshi wanavyowachukua raia mateka..

Sasa siku hizi za mwisho, shetani kashawachukua wengi mateka…inawezekana hata wewe umeshachukuliwa lakini hujijui tu, (kwasababu huna silaha yoyote mkononi mwako ya kumwogopesha)…sasa choropoka leo anza kuzifaa silaha chini chini kwa kuanza kujifunza Neno, na baadaye utoke upambane naye ili ukiisha mshinda uwafungue mateka wale wote aliokuwa amewateka kwa uongo wake na kuwafanya kuwa mateka yake kwa uongo wake… wewe wageuze wawe mateko wa Kristo wote aliowateka yeye, kwa elimu yako ya uongo na tabu zake… Kama biblia inavyotuambia..

2 Wakorintho 10:3  “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4  (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII KRISTO;

6  tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”

Na silaha hiyo ni NENO LA MUNGU..Ukilifahamu Neno la Mungu, Bwana atakutumia kumnyang’anya shetani mateka…na yeye atabaki hana kitu..na jeshi la Bwana litakuwa kubwa zaidi kuliko lake.

Sasa utawezaje kuanza kujivika silaha hizo.?

Kwanza tubu, mpe Yesu Kristo maisha yako kama hujaokoka..kisha jikane nafsi na beba msalaba wako..Halafu anza kupunguza mizigo katika maisha yako ya kila siku, ondoka kwenye magroup yote ya kidunia katika mitandao, Kanunue biblia leo kama huna… “Biblia ya maandishi sio ya kwenye simu”,..kila siku tenga muda mrefu wa kusoma Neno, na unaposoma zima simu na pia kaa sehemu ya utulivu..kisha yasome maandiko na utaona mambo Bwana atakayokufunulia ambayo ulikuwa huyajui…usisome kimstari kimoja au sura moja…Soma angalau kitabu kizima…kwasababu ufunuo wa Roho unaachiliwa pale unapolielewa Neno katika msingi wake, lakini ukisoma kijimstari kimoja hutaelewa chochote na hutapata ufunuo wowote. Soma kitabu cha Injili ya Mathayo uone ni vitu vingapi ulikuwa huvijui na jinsi gani likuwa vinakupita tu na shetani alivyokuwa anakudanganya.

Wakolosai 3: 16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote..”

Na siku zote kumbuka, mapambano dhidi ya shetani hayajaisha.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine, na pia kama utapenda kuyapata masomo haya kwa njia ya whatsapp au email au inbox yako ya facebook basi utatutumia ujumbe mfupi, hali kadhalika unaweza kuyapata bure kwa njia ya internet, tembelea website yetu hii kwa masomo Zaidi /www wingulamashahidi org/.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JILINDE NA UNAJISI, UNA MADHARA MAKUBWA.

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

RABI, UNAKAA WAPI?

Shetani ni nani?

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

Rudi Nyumbani:

Print this post