Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maandiko..
Mathayo 13:51 “Yesu aliwauliza, Mmeyafahamu hayo yote? Wakamwambia, Naam.
52 Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.
53 Ikawa Yesu alipoimaliza mifano hiyo, alitoka akaenda zake”.
Swali: unaweza kujiuliza kwanini Bwana Yesu aliufananisha ufalme wa mbinguni na mtu mwenye nyumba ambaye anatoa katika hazina yake vitu vipya na vya kale..
Siku zote mtu mwenye busara, katika nyumba yake (hususani katika store yake)..ni lazima utakuta vitu vipya na vile visivyo vipya. Na lengo la kuwepo vitu visivyo vipya ni ili kukarabati vile ambavyo si vipya wakati unaofaa.
Kwamfano utaona mtu aliyejenga nyumba..na hatimaye ikabaki misumari kadhaa, au rangi, au vikabaki vipande vya mabati, wengi huwa hawaendi kuvitupa badala yake wanaviweka stoo, kwaajili ya matumizi ya baadaye ambayo yanaweza kujitokeza. Pengine baadaye atakuja kufikiria kutengeneza banda la mifugo yake kama kuku, na vile vipande vya mabati au mbao vilivyosalia vinaweza kumsaidia..au pengine kukatokea hitilafu kwenye nyumba yake, na hivyo itambidi afanye ukarabati, ile hazina ya rangi na misumari na mabati vinaweza kuja kumsaidia…au yeye anaweza asivihitaji lakini pengine ndugu yake mwingine atakuja kuvihitaji huko mbeleni, hivyo ni lazima vihifadhiwe…
Ndio hapo utakuta kitu kinaweza kukaa stoo hata miaka 5 au zaidi.. kadhalika mtu mwenye busara aliyevaa viatu mpaka vikachakaa huwa haendi kuvitupa, ataviweka stoo, kwasababu anajua utakuja kufika wakati hivyo viatu vitapata matumizi aidha atapewa mtu mwingine pengine mwenye haja navyo…au vitatumika kwa shughuli zisizohitaji umaridadi, kama kazi za mashambani au ujenzi.
Na nguo ni hivyo hivyo, zikichakaa huwa watu hawazitupi badala yake wanazihifadhi kwenye makabati ya stoo kwa matumizi ya baadaye kwasababu anaweza kutokea mtu anazihitaji, au maskini, au zinaweza kutumika kama matambara ya kudekia au kusafishia vitu, hivyo hata kama vitakaa stoo miaka 5, au 10 lakini havitatupwa..Sasa mtu huyo huyo huyo wakati huo huo anazo nguo mpya katika makabati yake ndani anazozitumia kwa kutokea nje, vile vile katika stoo yake anazo nguo zilizochakaa na zisizofaa kwa kusudi maalumu. (Hiyo ni hekima).
Na katika elimu ya ufalme wa Mbinguni, na yenyewe ni hivyo hivyo, inafananishwa na mtu mwenye nyumba…
Ipo elimu ya ulimwengu huu na ipo Elimu ya Ufalme wa Ulimwengu. Elimu ya ulimwengu huu inalenga l katika kumfundisha mtu kuishi jinsi ulimwengu unavyotaka ili afanikiwe. Na kadhalika Elimu ya Ufalme wa mbinguni inalenga kumfundisha mtu, mambo ya kimbinguni ili afanikiwe.
Lakini Bwana Yesu alisema hapo juu Mtu mwenye elimu ya ufalme wa Mbinguni amefanana na na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale..
Maana yake ni kwamba, Mtu mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni (yaani muhubiri yeyote yule, awe Mchungaji, Muinjilisti, nabii, Mwalimu, au yoyote yule), anapaswa awe anajua na kuelewa jinsi ya kulichambua na kulitumia Neno la Mungu kama lilivyogawanyika katika pande zote mbili, (yaani Agano la Kale na Agano jipya).
Huwezi kusema tunalitumia tu agano jipya na wala hatulihitaji agano la kale, Kadhalika huwezi kulifanya agano la kale, lifae kwa sehemu ya agano jipya, na wala huwezi kufanya agano jipya lifae sehemu ya agano la kale….Ni sawa utumie nguo zisizofaa ulizoziweka stoo uanze kuzifanya nguo rasmi za kutokea. Lakini unaweza kuzifanya zile zilizopo store ziwe za kuzikarabati hizi mpya,..unaweza kutumia kipande cha nguo za kale kufutia vumbi katika kiatu chako..Lakini huwezi kutumia suti yako kabatini kufutia vumbi kiatu kilichopo stoo, unachokitumia kuendea shamba.
Marko 2:21 “Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu; ikiwa ashona, kile kipya kilichotiwa huliharibu lile vazi kuukuu, na pale palipotatuka huzidi”
Vivyo hivyo agano la kale ni kwaajili ya kulipamba agano jipya na kulifanya lieleweke zaidi..
Kwamfano huwezi kuichukua sabato ya agano la kale, na kuilazimisha iwe ni agizo la agano jipya…Lakini unaweza kuitumia sabato ya Agano la kale, kuizungumzia sabato halisi ya Agano jipya ambayo ndio hilo pumziko tunalolipata baada ya kumpokea Kristo (Mathayo 11:28). Na hilo pumziko tunalipata baada ya kumpokea Kristo ambaye ndiye Bwana wa Sabato.
Kwahiyo maagano yote mawili yana umuhimu, na ni wajibu wetu kila siku kutafuta kujua hekima ya kuyatumia maneno ya Mungu ipasavyo. Ndege hawezi kupaa kwa bawa moja tu, atayahitaji yote mawili. Vivyo hivyo na sisi.
2Timotheo 2:15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kwel”
Maran atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Biblia inatuambia kuwa viumbe vya Mungu navyo vinaugua, na vinapitia shida kama sisi tu tunavyopitia..
Warumi 8:22 “Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa”.
Hivyo kama vinaugua kama sisi, vinaumia kama sisi, ni kosa kuvipiga au kuviua bila sababu yoyote.
Biblia imetoa sababu kuu mbili ya kuviua au kuviadhibu.
Ya kwanza ni pale tunapovitumia kwa chakula, au kwa matumizi ya msingi: (Kumbukumbu 12:15). Utachinja kuku, au ng’ombe, au mnyama yoyote ikiwa ni kwa lengo la kula, au biashara,..Hiyo sio dhambi wala sio kosa.
Na sababu ya pili ni pale, vinapofanya makosa, au vitatusababishia madhara au hasara: Utalisoma hilo katika (Kutoka 21:28-29). Vilevile kuna viumbe kama nyoka, mende, nzi, mbu, kunguni, n.k. hivyo vikiuliwa hakuna shida, kwasababu havina kazi nyingine yoyote zaidi ya kutuletea magonjwa au kutudhuru.
Lakini kwasababu nyingine yoyote nje ya hizo ni dhambi.
Utalithibitisha hilo kwa Balaamu, siku ile alipokuwa anamfuata Balaki mfalme wa Moabu, Ili awalaani Israeli, utaona Mungu alipomfumbua macho punda yule na kumwona yule malaika, Balaamu alianza kumpiga, na yule punda akafumbuliwa kinywa na Mungu, akamwambia unanipigia nini? (Hesabu 22:21-39)
Na kama hiyo haitoshi yule malaika naye alikuja kumuuliza tena Balaamu kwanini alimpiga punda bila kosa lolote? Unaona, Mungu hapendi tuvitese viumbe vyake, bila sababu yoyote. Sio lazima ukimkuta mbwa barabarani ambaye kakaa tu bila kosa lolote, wala dhara lolote, uanze kumpiga kwa mawe.
Si vizuri ukamkuta kinyonga katulia zake pale mtini, uanze kumlenga kwa manati, Si vizuri ukamwona punda wako amechoka katulia, ukaanza kumpiga piga ovyo tu bila sababu..Hiyo ni dhambi.
Biblia sehemu nyingine inatoa thawabu nono sana kwa wanaowatenda fadhili wanyama..Soma hapa.
Kumbukumbu 22:6 “Kiota cha ndege kikitukia kuwa mbele yako njiani, katika mti wo wote, au chini, chenye makinda au mayai, naye koo ameatamia juu ya makinda, au juu ya mayai, usimtwae yule koo pamoja na makinda;
7 sharti umwache yule koo aende zake, lakini makinda waweza kuyatwaa uwe nayo; ili upate kufanikiwa, ufanye siku zako kuwa nyingi”.
Unaona, kwa mambo madogo tu, mtu unajiongezea siku za kuishi.
Hivyo, ikiwa hatuna sababu zozote za msingi, tusivipige au kuviua viumbe vya Mungu.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Katika Warumi 8:18-25. Je! Viumbe vinatazamiaje kwa shauku kufunuliwa kwa Mwana wa MUNGU?
Je! ni kweli kuna viumbe vinavyoishi sayari nyingine (ALIENS)?
Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?
Fadhili ni nini? Nini maana ya “fadhili zake ni za milele” kibiblia?
Ayala ni mnyama jamii ya swala, ambaye anapatikana sana maeneo ya nchi za barini, wana pembe ndefu zilizotawanyika kama mashina ya miti (Tazama picha juu).
Paa ni jamii ya swala wenye mistari meupe, (Maarufu kama Gazelle kwa lugha ya kiingereza). Paa wanapatikana zaidi maeneo ya ukanda wa joto, kama Afrika. (Tazama picha chini). Na pia kwenye biblia kuna watu waliitwa Paa.
Matendo 9:36 “Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa”.
Na Kulungu pia ni jamii ya swala, ambao nao pia wanapatikana nchi za ukanda wa baridi kama Ulaya. (Tazama picha chini).
Wanyama hawa kwa pamoja tunawasoma wametajwa katika biblia katika kitabu cha Isaya..
1Wafalme 4: 22 “Na vyakula vya Sulemani vya siku moja vilikuwa kori therathini za unga wa mzuri, na kori sitini za ngano.
23 na ng’ombe kumi walionona, na ng’ombe ishirini za malisho, na kondoo mia, pamoja na ayala, na paa, na kulungu, na kuku walionona”.
Sasa kwanini biblia iwataje wanyama hawa?
Kwanza ni wanyama ambao kimwonekano ni wazuri, na wepesi, na pia wana-mbio sana, (soma Habakuki 3:19, Isaya 35:6, Zaburi 18:33, 2Samweli 22:34, na 2Samweli 2:18). simba ni rahisi kumkamata punda milia lakini si swala… Sasa katika roho vijana wanafananishwa jamii ya hawa wanyama wa swala. Vijana wana nguvu na pia kimwonekano ni wazuri kuliko wazee, na pia ni wepesi wa kufanya mambo..
Na ndio maana biblia inatoa maonyo haya..
Wimbo 2: 7 “Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.
Maana yake usiwe mwepesi kuruka huko na huko kama kulungu kuzichochea tamaa za mwili, waasherati wote biblia imesema hawataurithi uzima wa milele.
2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.
Maran atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?
Tusome..
Wimbo 2:1 “Mimi ni ua la uwandani, Ni nyinyoro ya mabondeni. ”
Hapo kuna vitu viwili, 1) Ua la uwandani, na 2) Nyinyoro ya mabondeni.
Sasa kwa urefu juu ya Ua hili la uwandani unaweza kufungua hapa ili tuende pamoja >> Ua la Uwandani
Lakini tutaiangalia sehemu ya pili inayozungumiza Nyinyoro ya mabondeni...
Sasa Nyinyoro ni jamii ya maua ijulikanayo kama “Lil” kwa lugha ya kiingereza.. (Tazama picha juu). Ua la uwandani au kwa lugha nyingine “Ua la Sharon, lenyewe linaota sehemu tambarare”. Lakini jamii ya haya maua ya Nyinyoro (au Lily) yanasitawi sehemu za mabonde na miteremko. Ni maua mazuri sana kwa mwonekano kama hayo ya maua mengine ya Sharon.
Sasa hilo ua ni nani?
Si mwingine zaidi ya Mwokozi wa Ulimwengu, yeye ndiye Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho…Yeye ndiye Ua la Sharon linalostawi sehemu tambarare na ndiye Ua la Nyinyoro linalostawi mabondeni, ndio Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho..
Kama vile maua yavutiavyo na yatoavyo harufu nzuri, ndivyo Yesu alivyo mzuri naye, hakuna aliyemtumainia akajuta, wala kumkinai, amejaa Mema, na raha. Wana raha na heri wote wanaomkimbilia. Je wewe ni mmoja wao?
Kama bado hujampokea basi umekosa kitu cha muhimu sana katika maisha yako, hivyo fanya hima leo, mpokee na utapata raha nafsini mwako..
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Jibu: Pambaja ni neno linalo maanisha “upendo” (ule wa mwanaume na mwanamke). Upo upendo wa ndugu kwa ndugu, mfano upendo wa Mzazi na mtoto, dada na kaka wa familia moja na pia upo upendo wa mwanamke na mwanamke. Sasa upendo huu wa mwanaume na mwanamke kwa lugha nyingine ndio unaoitwa PAMBAJA. Neno hili linaweza kutumika kama wingi, lakini linamaanisha vile vile upendo.
Wimbo ulio Bora 1: 2 “Kubusu na anibusu kwa kinywa chake. Maana pambaja zako zapita divai”
Wimbo ulio Bora 4: 10 “Jinsi zilivyo nzuri pambaja zako, umbu langu, Bibi arusi, ni nzuri kupita divai; Na harufu ya marhamu yako Yapita manukato ya kila namna”
Pia unaweza kulipata neno hilo kwenye mistari hii; Wimbo 1:4, Wimbo 7:12.
Sasa ni kwanini upendo huu umetajwa hapo?, je una umuhimu wowote kwetu sisi wakristo?. Ndio una umuhimu mkubwa, kwanza kwa wana-ndoa na Pili kwa Kristo na Kanisa lake.
Kumbuka Sisi wakristo katika roho tunafananisha na bibi-arusi na Kristo ndiye Bwana Arusi. Hivyo jinsi Kristo anavyolipenda kanisa upendo wake ni kama wa mke na mume (yaani Pambaja). Na kama unavyojua wivu ni mbaya kuliko ghadhabu..Na ndivyo Kristo anavyotuonea wivu, tunapoiacha njia ya haki na kuufuata ulimwengu.. Tunamtia wivu.
Wimbo 8: 6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu”
Hivyo sisi tuliookoka ni watu wa thamani mbele ya Kristo, ni bibi-arusi wake, anayetupenda na kutujali na katuandalia mambo mengi mazuri mbinguni katika karamu yake aliyotuandalia..
Ufunuo 21: 9 “Akaja mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na vile vitasa saba vilivyojaa yale mapigo saba ya mwisho, naye akanena nami, akisema, Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo.
10 Akanichukua katika Roho mpaka mlima mkubwa, mrefu, akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mwenyezi Mungu”
Je utaikosa hiyo Yerusalemu mpya iliyoandaliwa mahususi kwa bibi-arusi?. Kama hujampokea Kristo hutaurithi uzima huo wa milele. Hivyo mpokee leo, kwa kutubu na kwenda kubatizwa na yeye atakupokea.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.
Kwamfano tukisoma katika injili ya Mathayo, tunaona, mwandishi anaanza kueleza ukoo wa Yesu tangu Ibrahimu Mpaka Yusufu, lakini alipofika kwa Daudi, aliendelea na kusema Daudi akamzaa Sulemani, (Mathayo 1:6)..Lakini tukirudi tena kwenye Luka hapo hapo tunaona Daudi alimzaa Nadhani (Luka 3:31), Hiyo ni kuonyesha kuwa Yesu alipitia uzao wa Nathani na sio wa Sulemani, kulingana na Luka. Lakini Mathayo anasema alipitia kwenye uzao wa Sulemani, kwanini iwe hivyo?
Pia ukisoma tena mwishoni utaona kulingana na Injili ya Mathayo, baba yake Yusufu alikuwa ni Yakobo, lakini Luka anatuambia baba yake Yusufu alikuwa ni Eli (Luka 3:23).. Naomba ufafanuzi juu ya hili.
JIBU: Ni wazi kuwa ukisoma kitabu cha Mathayo na kile cha Luka utaona kuna tofauti kubwa kwenye vizazi vya ukoo wa Yesu. Luka anatuambia baba wa Yusufu alikuwa ni Eli, na Mathayo inasema babaye alikuwa ni Yakobo. Lakini je! Hilo linamaanisha biblia inajipinga?
Jibu ni la! Ikumbukwe kuwa zamani katika taifa la Israeli walikuwa na desturi ya mtu kumnyanyulia ndugu yake uzao, na mtoto huyo kuitwa kwa jina la marehemu ikiwa mtu huyo atakufa kabla hajapata mtoto.. Soma. Kumbukumbu 25:5-6,
Kwamfano, kama wewe ni mwanaume umezaliwa katika familia, na ukaoa, lakini kwa bahati mbaya ukafa bila kupata mtoto, basi anatafutwa ndugu yako wa karibu aidha katika familia au katika ukoo, Yule aliye karibu zaidi na wewe, kisha anakwenda kumuoa huyo mke wako uliyemwacha, kisha anamzalia mtoto, lakini huyo mtoto hataitwa kwa jina lake, bali ataitwa kwa jina lako wewe marehemu, haijalishi kuwa watoto huyo watakuwa wametoka katika viungo vya mtu mwingine. Na Wanafanya hivyo ili kulitunza jina lako lisipotee.
Na ndicho walichokifanya Israeli wakati ule, ndicho alichokifanya Boazi kwa Ruthu, (ukisoma Ruthu 4:6-9)
Sasa tukirudi katika Injili. Mathayo aliandika Uzao wa Yusufu (Babaye Yesu), akifuata ubaba wa kibaolojia, na Luka aliandika uzao wa Yusufu akifuata ubaba wa kijina.
Ikiwa na maana kuwa Eli pengine alikufa kabla ya kupata mtoto, hivyo Yakobo akamchukua mke wake, na kuzaa naye ili kumtunzia jina, ndipo akamzaa Yusufu. Hivyo kibaolojia Yusufu alikuwa ni mtoto wa Yakobo lakini kisheria alikuwa ni mtoto wa Eli.
Na ndio maana Yakobo hatajwi katika injili ya Luka, bali ni Eli.. Lakini Mathayo anamtaja Yakobo Kama baba wa Yusufu lakini kibaolojia. Hivyo maandiko yapo sawa.
Kwafaida ya asiyekuwa na biblia anaweza kuvipitia, vifungu hivyo vya biblia hapa chini:
Mathayo 1:1-16
1 Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
2 Ibrahimu alimzaa Isaka; Isaka akamzaa Yakobo; Yakobo akamzaa Yuda na ndugu zake;
3 Yuda akamzaa Peresi na Zera kwa Tamari; Peresi akamzaa Esromu; Esromu akamzaa Aramu;
4 Aramu akamzaa Aminadabu; Aminadabu akamzaa Nashoni; Nashoni akamzaa Salmoni;
5 Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu; Boazi akamzaa Obedi kwa Ruthu; Obedi akamzaa Yese;
6 Yese akamzaa mfalme Daudi.
7 Sulemani akamzaa Rehoboamu; Rehoboamu akamzaa Abiya; Abiya akamzaa Asa;
8 Asa akamzaa Yehoshafati; Yehoshafati akamzaa Yoramu; Yoramu akamzaa Uzia;
9 Uzia akamzaa Yothamu; Yothamu akamzaa Ahazi; Ahazi akamzaa Hezekia;
10 Hezekia akamzaa Manase; Manase akamzaa Amoni; Amoni akamzaa Yosia;
11 Yosia akamzaa Yekonia na ndugu zake, wakati wa ule uhamisho wa Babeli.
12 Na baada ya ule uhamisho wa Babeli, Yekonia akamzaa Shealtieli; Shealtieli akamzaa Zerubabeli;
13 Zerubabeli akamzaa Abihudi; Abihudi akamzaa Eliakimu; Eliakimu akamzaa Azori;
14 Azori akamzaa Sadoki; Sadoki akamzaa Akimu; Akimu akamzaa Eliudi;
15 Eliudi akamzaa Eleazari; Eleazari akamzaa Matani; Matani akamzaa Yakobo;
16 Yakobo akamzaa Yusufu mumewe Mariamu aliyemzaa YESU aitwaye Kristo.
Na..
Luka 3:23-38
23 Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,
24 wa Mathati, wa Lawi, wa Melki, wa Yana, wa Yusufu,
25 wa Matathia, wa Amosi, wa Nahumu, wa Esli, wa Nagai,
26 wa Maathi, wa Matathia, wa Semei, wa Yusufu, wa Yuda,
27 wa Yoana, wa Resa, wa Zerubabeli, wa Shealtieli, wa Neri,
28 wa Melki, wa Adi, wa Kosamu, wa Elmadamu, wa Eri,
29 wa Yoshua, wa Eliezeri, wa Yorimu, wa Mathati, wa Lawi,
30 wa Simeoni, wa Yuda, wa Yusufu, wa Yonamu, wa Eliakimu,
31 wa Melea, wa Mena, wa Matatha, wa Nathani, wa Daudi,
32 wa Yese, wa Obedi, wa Boazi, wa Salmoni, wa Nashoni,
33 wa Aminadabu, wa Aramu, wa Hesroni, wa Peresi, wa Yuda,
34 wa Yakobo, wa Isaka, wa Ibrahimu, wa Tera, wa Nahori,
35 wa Serugi, wa Ragau, wa Pelegi, wa Eberi, wa Sala,
36 wa Kenani, wa Arfaksadi, wa Shemu, wa Nuhu, wa Lameki,
37 wa Methusela, wa Henoko, wa Yaredi, wa Mahalaleli, wa Kenani,
38 wa Enoshi, wa Sethi, wa Adamu, wa Mungu.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Biblia haijatoa idadi kamili ya malaika Mungu aliowaumba, inatumia neno “MAJESHI” ambayo majeshi yenyewe hayo yapo maelfu kwa maelfu.
Waebrania 12:22 “Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na MAJESHI ya malaika ELFU NYINGI”,
Umeona ni wengi sana kiasi kwamba hata mwandishi ameshindwa kutoa idadi kamili ya majeshi hayo, anaishia kusema tu elfu NYINGI..maana yake hayahesabiki.
Sehemu nyingine, inasema idadi yake ni elfu mara elfu na elfu kumi mara elfu kumi..utaona hapo mwandishi bado anapata shida kuelezea idadi hiyo kamili ya malaika hao, jinsi walivyo wengi, Ni malfu mengi yanayojizidisha, na kujizidisha na kujizidisha..
Ufunuo 5:11 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,”
Katika biblia Malaika wapo wa aina tofauti tofauti,
Wapo malaika wa Sifa: Hawa wapo mbele za Mungu usiku na mchana kuilinda enzi yake, ndio wale Maserafi na makerubi; ambao tunawasoma kwenye biblia. Ezekieli 1:4-28, Isaya 6:2-6
Wapo malaika wa vita: Mfano wa hawa ni Mikaeli na malaika zake: 2Wafalme 6:17, Ufunuo 12:7, Yeremia 5:14, 38:17, Hosea 12:5
Wapo malaika wajumbe: Mfano wake ni Gabrieli. Danieli 8:16, 9:21, Luka 1:19,26.
Wapo malaika wa vitu vya asili tu: kama vile moto, maji n.k. Ufunuo 16:5, 14:18
Wapo malaika wa ulinzi, (Mji, na mataifa): Danieli 4:13
Wapo malaika wa ulinzi (wanadamu): Mathayo 18:10, Zaburi 34:7
Wapo malaika wa Huduma (watumishi): Matendo 5:19, 7:30, 8:26, 12:15, 27:23,Waebrania 1:14,
Wapo malaika wa mapigo: Zaburi 78:49, Ufunuo 16
Wapo malaika wa uponyaji: Yohana 5:4, Isaya 6:7
Pamoja na hayo wapo pia malaika walioasi. Ambao biblia inatuambia walikuwa ni theluthi tu ya malaika wote waliokuwa mbinguni. Na hao idadi yao haihesabiki, katikati yao kuna ambao wapo vifungoni saa hii wanasubiria hukumu ya mwisho, (Yuda 1:6)
Wengine wapo vifungoni lakini watakuja kuachiliwa kwa muda kidogo wafanye kazi duniani kwa muda mfupi kisha wataondolewa(Ufunuo 9:1-11),
na wengine wapo bado hapa hapa duniani wakizurura zurura tu kuwaharibu watu, na kusababisha maovu duniani..
Jaribu tu kutengeneza picha tu yale mapepo yaliyomwingia Yule kichaa, kule makaburini, Yesu alipowauliza jina lako nani, yakasema LEGIONI, yaani jeshi, yakimaanisha hatuhesabiki..Sasa Kama ndani ya mtu mmoja yanaweza kukaa mapepo yasiyohesabika, jiulize mapepo yaliyopo ndani ya watu wote ambao hawajampa Kristo maisha yao leo hii yapo mangapi?
Hivyo hiyo inafanya idadi ya malaika ambao Mungu aliwaumba kuwa nyingi sana isiyoweza kuhesabika, hata zaidi ya idadi ya wanadamu wote walioishi na wanaoishi duniani tangu dunia iumbwe.
Hiyo ni kutuonyesha jinsi Mungu alivyojawa na uweza na nguvu na utukufu.
Zaburi 139:17 “Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake!
18 KAMA NINGEZIHESABU NI NYINGI KULIKO MCHANGA; NIAMKAPO NIKALI PAMOJA NAWE”.
JINA LA BWANA LIHIMIDIWE DAIMA.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?
Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?
MALAIKA WAPELELEZI WA HUKUMU WANAPITA SASA.
KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.
UTAWALA WA MIAKA 1000.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tulitafakari Neno la Mungu pamoja, kwani ndicho chakula pekee kinachoweza kuziponya roho zetu kabisa kabisa.
Lipo swali tunaweza kujiuliza ni kwanini kuna wasaa ilimgharimu Bwana wetu kulia sana na kutoa machozi ? Tunajua alikuwa ni mkamilifu , alikuwa hana hofu na chochote, na lolote alilomwomba Mungu, dakika hiyo hiyo alipewa, lakini ni kwanini wakati mwingine ilimpasa atoe machozi mengi, na kulia ili apoke?
Kitabu cha Waebrania kinatuambia hivyo;
Waebrania 5:7 “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja NA KULIA SANA NA MACHOZI, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu”;
Wakati mwingine Bwana wetu Yesu alilia sana kama katoto kadogo, mbele za Mungu wake, alitoa machozi mengi, Yesu huyo ambaye leo hii tunamwita Bwana wa Mabwana na Mfalme wa Wafalme, na kama hilo halitoshi tunamwita mwanaume wa wanaume.
Lakini mwanaume huyu alilia, alitoa machozi katika kumwomba Mungu wake, na kwasababu hiyo Mungu akamsikia, japokuwa hata asingefanya hivyo angesikiwa tu, lakini hisia zake zilizidi uwezo wake, na mamlaka yake, na nguvu zake..alipokuwa mbele za Baba yake machozi yalimtoka mwenyewe tu, pale alipoutafakari uwezo wake jinsi ulivyo mkuu, yalimtoka mwenyewe alipoona Upendo wa Baba yake unavyozidi upeo, yalimtoka mwenyewe pale alipowahurumia watu aliopewa na Baba yake.
Jambo hilo halikuishia tu kwake, tunaona pia aliwaambukiza mpaka na mitume wake waliomtumikia baadaye..Kwa mfano utamwona Paulo wakati mwingi sio tu alilia katika kuomba bali hata alipokuwa anawahubiria watu alitoa machozi, kwa vile alivyokuwa anawahurumia roho zao.
Matendo 20:31 “Kwa hiyo kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi”.
Soma tena..
2Wakoritho 2:4 “Maana katika dhiki nyingi na taabu ya moyo niliwaandikia na machozi mengi; si kwamba mhuzunishwe, bali mpate kujua upendo wangu nilio nao kwenu jinsi ulivyo mwingi”.
Na…
Wafilipi 3:18 “Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo”;
Unaona hisia hizo nyingi za Paulo ndizo zilizochangia pia hata huduma yake duniani kuwa na mafanikio makubwa. Kwasababu aliyachukulia mambo ya Mungu kwa uzito mkubwa, aliithamini neema katika hisia za hali ya juu sana, ambazo zilimpelekea hata kutoa machozi wakati mwingi alipokuwa anafanya kazi ya Mungu.
Na sisi pia, tuziamshe hisia zetu kwake. Mwingine anaweza kusema mimi siwezi! Ndio huwezi kulia kwasababu hujakaa chini na kuutafakari kwa makini uweza wake wote kwako, aliokufanyia tangu umekuja hapa duniani.
Ungetafakari kwa undani ni kwanini Mungu amekupa uhai mpaka leo hii, na hujampa chochote, ni kwanini unavuta hewa yake bure, na hajawahi kukuchaji hata senti, ni kwanini umekuchagua wewe na kukupa wokovu na muda huo huo kuna wengine hawataki hata kusikia habari za mUNGU, ukidhani kwamba wewe kichwa chako ni chepesi sana kuelewa kuliko wale?, Hilo ondoa akilini, ni kwamba Mungu kachagua tu kukuvuta wewe kwake, hilo tu, huna cha ziada ulichomfanyia. Ukikumbuka siku ile ulikuwa katika jaribu fulani akakuvusha, kama sio yeye ungekuwa ni marehemu sana.. Ukikumbuka hayo yote, hutabaki kama ulivyo,
Ukikumbuka ni kwanini mwaka huu unakwisha, wewe hujafa na KORONA, wakati mamilioni ya watu wamekufa na bado wanaendelea kufa duniani leo hii.. nakwambia utabaki kama ulivyo.. utalia tu, na kutoa machozi kwa kumpa Mungu shukrani, kwa kulibariki jina lake.
Unapoumaliza huu mwaka, usizizuie hisia zako kwa Mungu. Huu ni mwaka ambao sote tunahitaji kumshukuru Mungu, kwa nguvu zaidi kuliko hata miaka mingine yote iliyowahi kututangulia.
“Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele”. (1Nyakati 16:34)
Mungu atujalie kulijua hilo, ayagange macho yetu.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Biblia inapozungumza juu ya fadhili za Mungu, ni zaidi ya zile fadhili ambazo tunazojua ambazo mtu anaweza kuzifanya kwa mtu mwingine, yaani kumuonyesha ukarimu na wema..
Kibiblia Fadhili za Mungu ni Neno pana sana, kwa kiebrania linatamkwa “Hesed”, ambalo tafsiri yake huwezi kuelezea kwa neno moja, au kwa maneno machache.
Fadhili za Mungu sio tu wema na ukarimu Mungu anaotufanyia sisi, bali linamaanisha pia Upendo wa Mungu usioelezeka, upendo wa kusaidia, upendo wa kuvumilia, Upendo wa kuokoa upendo wa kutoa,..
Ni wema usio na masharti, kwamba hatutendei fadhili zake kisa sisi tumemfanyia kitu kwanza, au tumekuwa marafiki zake, Hapana. Anatenda kama vile ni wajibu wake kufanya, Wema huo hauwezi kuelezeka, kwasababu unagusa kila Nyanja, ambazo haziwezi kufikiwa na mwanadamu yoyote Yule, au kiumbe chochote kile mbinguni au duniani., umeingia ndani kabisa.
Na ndio maana Neno hili utalisoma sehemu nyingi sana katika biblia, Na pia utaona Daudi kila alichokiona au alichokitaja alihitimisha na neno “kwa maana fadhili zake ni za milele”..
ZABURI 136
1 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 Mshukuruni Mungu wa miungu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
4 Yeye peke yake afanya maajabu makuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
5 Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
6 Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7 Yeye aliyefanya mianga mikubwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8 Jua litawale mchana; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9 Mwezi na nyota zitawale usiku; Kwa maana fadhili zake ni za milele. 10 Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11 Akawatoa Waisraeli katikati yao; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12 Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
13 Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
14 Akawavusha Israeli katikati yake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
15 Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
16 Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Vipo vifungu vingi sana Soma pia.. 1Nyakati 16:34, Zaburi 106:1 n.k.
Utaona pia Musa alipofumbuliwa macho yake na kumwona Mungu kwa sehemu, alipokuwa kule mlima alitangaza na kusema;
Kutoka 34:6 “Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, MWENYE FADHILI, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;
Vivyo hivyo kilichomchea Mungu kumtuma mwanawe duniani kuja kutuokoa, hakikuwa kingine zaidi ya Fadhili zake za milele zinazodumu kwetu daima..
Alikuwa tayari kumtoa mwanawe wa pekee kafara ili sisi tupate wokovu, Jiulize wewe unaweza kumtoa mwanao, tena yule unayempenda kuliko wote awe sadaka ili jirani yako ambaye hakusaidii chochote apone au afaidike? Unaweza kufanya hilo? Huwezi kwasababu hujafikia kiwango hicho cha fadhili za Yehova.
Hivyo kama tukiyajua hayo ni wajibu wetu kumwimbia usiku na mchana, kumshukuru juu ya wema wake aliotuonyesha na anaotufanyia kila siku. Na Tunampa Mungu sifa za vinywa vyetu, pamoja na kwa MATOLEO YETU.
Jina la Yesu Kristo libarikiwe daima.
Haleluya.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Vikuku ni vitu mfano wa bangili ambavyo vinavaliwa aidha mikononi au miguuni, kwa lengo la urembo. Tazama picha juu. Katika enzi za zamani vikuku vilivaliwa na jinsia zote, yaani wanaume na wanawake.
Katika biblia tunaona neno hilo likitokea mara kadhaa..
2 Samweli 1:10 “Basi, nikasimama karibu naye, nikamwua, kwa sababu nalijua hakika ya kuwa hawezi kupona baada ya kuanguka; kisha nikaitwaa ile taji iliyokuwa kichwani mwake, na kikuku kilichokuwa mkononi mwake, nami nimevileta hapa kwa bwana wangu”.
Na pia unaweza kusoma mistari ifuatayo binafsi iliyozungumzia juu ya vikuku Mwanzo 24:47, Isaya 3:19, Ezekieli 16:11 na Ezekieli 23:42.
Lakini sio hilo tu, vikuku pia vilitumika katika kutengenezea mishikio ya masanduku. Kwa mfano utaona sanduku la Agano lilitengenezwa kwa vikuku katika pande zake za chini ili kuwezesha upitishaji wa zile fimbo zake, na kufanya ubebaji wake uwe mrahisi… Tazama picha chini.
Kutoka 25: 14 “Nawe tia hiyo miti katika vile vikuku vilivyo katika pande mbili za sanduku ili kulichukua hilo sanduku.
15 Hiyo miti itakaa katika vile vikuku vya sanduku; haitaondolewa.
16 Kisha tia ndani ya sanduku huo ushuhuda nitakaokupa”.
Lakini je! Katika agano tunaruhusiwa kuvaa vikuku?
Jibu ni la!. Mwanaume au mwanamke wa kikristo hapaswi kutoboa pua na kuweka hazama, hapaswi kujiharibu ngozi kwa kujichubua, hapaswi kuvaa vikuku katika mikono yake au miguu yake..Kwasababu miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu.
1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.
5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao”
Mwanamke anayevaa kikuku mguuni, anakuwa hana tofauti na kahaba. Matumizi ya vikuku yabaki katika kutengenezea masanduku na bidhaa nyingine lakini si kuivalisha miili yetu.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Hazama ni nini katika biblia?(Ezekieli 16:12, Kutoka 24:47)
KUJIPAMBA NI DHAMBI?
UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.
UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?
UFUNUO: Mlango wa 3 part 3