Title 2020

Kama ulimwengu ujao utakuwa na watakatifu tu, sasa hao watakaotawaliwa watatoka wapi?

JIBU: Kuna mambo mawili ya kufahamu jambo la kwanza ni kuwa mara baada ya huu ulimwengu wa sasa kuisha, kutakuwa na utawala mwingine mpya ujulikanao kama utawala wa amani wa Yesu Kristo wa miaka 1000 (Ukisoma Ufunuo 20:6 utaona jambo hilo). Na mara baada ya huo utawala wa miaka 1000 kuisha kutakuwa na umilele ambapo wakati huo ndio ile mbingu mpya na nchi mpya vitafunuliwa..Na maskani ya Mungu itakuwa ni pamoja na wanadamu. Ambapo Mungu atafanya makao yake na wanadamu milele na milele isiyokuwa na mwisho (Ufunuo 21:3)

Sasa katika ule utawala wa miaka 1000, ambapo Kristo atarudi na watakatifu wake aliowanyakua zamani, (Yuda 1:14) utakuwa ni utawala wa amani lakini bado biblia inarekodi waovu watakuwepo pia (Isaya 65:20)…Lakini katika mbingu mpya na nchi mpya ambayo itaanza mara baada tu ya utawala huu wa miaka elfu moja kuisha, waovu hawatakuwepo kabisa.

Sasa hawa waovu watakaokuwepo ndani ya utawala huo (waliozaliwa humo) ndio watakaotawaliwa na watakatifu wakati ule utakapofika.. Na ndio maana Bwana Yesu anatuhimiza sasa na kutuambia..

Ufunuo 2:26 “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu.

28 Nami nitampa ile nyota ya asubuhi.

29 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”.

Vilevile katika huo utawala wa miaka elfu moja, na pia baada ya utawala huo kupita kutakuwa na shughuli maalumu (au tuseme sekta maalumu) ambazo Mungu ameziandaa zifanywe na zisimamiwe na watakatifu wake tu. Lakini sasa hizo hazifanywi na kila mtakatifu tu, hapana, bali zitafanywa kulingana na auminifu wa mtakatifu husika alipokuwa hapa duniani..Tunasoma hilo katika.

Mathayo 24:45 “Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47 Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

48 Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

49 akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;

50 bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51 atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Unaona? Sasa hapa ndipo yatakapotokea matabaka hata katikati ya watakatifu. Wale ambao walikuwa waaminifu katika kazi ya Mungu na katika utakatifu wakiwa hapa duniani watapewa vyeo vya juu zaidi katika enzi ya Mungu, na wale waliokuwa waaminifu kidogo watapewa kidogo..kama Bwana Yesu alivyosema katika kitabu cha Luka…

Luka 19:16 “Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.

17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.

18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.

19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.

20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.

21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.

22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;

23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?

24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi”

Hivyo kwa kuhitimisha ni kwamba, vyeo vitakuwepo na kutawala pia kutakuwepo..Isipokuwa kutawala kutaishia katika ule utawala wa miaka 1000, lakini vyeo na ngazi zitaendelea mpaka umilele kwenye mbingu mpya na nchi mpya.. kwasababu huko hakutakuwa na waovu tena, Isipokuwa sote tutamilika na yeye. Lakini sote hatutakuwa ngazi moja…

2Timotheo 2:12 “Kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi”;

Hivyo tufanye bidii ili tuwepo na Bwana katika utawala wake na mpaka mwisho hadi tutakapoifikia ile nchi mpya na mbingu mpya..

2Petro 3:13 “Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.

14 Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake”.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255693036618/ +255789001312

  Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada nyinginezo

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

UTAWALA WA MIAKA 1000.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.

Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

Milima ya Ararati ipo wapi kwasasa? (Mwanzo 8:4)

Rudi Nyumbani

Print this post

TAZAMA KRISTO YUPO HAPA,AU YUKO KULE MSISADIKI.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Bwana Yesu alisema maneno yafuatayo…

Mathayo 24:23 “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.

24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule”.

Bwana Yesu anapomwita mtu, au anapomvuta mtu kwake kitu cha kwanza kumwonesha sio kanisa la kujiunga…bali Neno lake. Ni muhimu kulijua hilo ili tusidanganyike na roho zituambiazo..”tazama Kristo yupo hapa ama kule”

Zamani kidogo kuna mtu alitutumia ujumbe akatuambia… “Ameota ndoto, alikuwa ndani ya kanisa lake ambalo ndilo analokwenda siku zote…katika hiyo ndogo alijiona alikuwa anaimba na kuabudu kwa furaha pamoja na washirika wenzake…wakati anaabudu kwa nje ya kanisa akamwona mdada mwingine ambaye anamfahamu anamwangalia kama kwa kumhuzunikia hivi…Na alipoona anamwangalia sana na tena kwa huzuni…yeye kitu Fulani kikamjia kwenye kichwa chake, kwamba pengine hayupo sehemu salama…hivyo akaamua kutoka kule ndani alipokuwa anaimba na wenzake na akamfuata Yule dada aliyekuwepo kule nje!..Na huyo dada alipomfuata aligundua kuwa anasali kanisa Fulani analolijua kisha akashtuka usingizini” .

Baada ya ndoto hiyo akatutumia meseji kwamba anahisi Mungu anamwambia aondoke hilo kanisa alilopo sasa aende kwenye kanisa lingine…ambalo ni la Yule dada aliyemwona kwenye ndoto. Akatuhadithia na hiyo ndoto aliyoiota. Ikabidi tuanze kumhoji kanisa alilopo sasa hivi ni kanisa gani! Akatutajia..na hilo analotaka kwenda pia akatutajia.. Tulichokuja kugundua kuwa mahali anaposali sasa pana uafadhali mkubwa sana kuliko kule alikokuwa anataka kwenda…

Kwanza mahali anaposali panahubiriwa maonyo ya siku za mwisho kwa nguvu, na pia wanafundishwa utakatifu, pamoja na wanawake kujiheshimu kwa kujisitiri, ni mahali ambapo wanawake hawavai suruali, hawavai mawigi, hawaruhusiwi kuvaa vimini, hawapaki wanja na mambo yote ya kidunia hayaruhusiwi kanisani…Na huko anakotaka kwenda ni mahali ambapo mambo hayo yote ni ruksa…kuvaa suruali na kuingia nazo kanisani ni ruksa, kujipodoa na kuingia kanisani ni ruksa, na wala hakuna msisitizo wowote wa ujio wa pili wa Kristo.

Tukamwuliza huyu dada ni kitu gani ambacho unahisi hakiendi sawa katika kanisa ulilopo sasa?..akasema hakuna..kila kitu kipo sawa, kanisani hakuna tatizo lolote kuna amani na kuna upendo tu. Lakini naogopa hiyo ndoto niliyoiota isije kuwa Mungu ananionya niondoke halafu simtii?.

Tukamwambia hiyo ndoto sio ya Ki-Mungu…Mungu kamwe hawezi kumtoa mtu kwenye kanisa na kumwonyesha kanisa…kamwe hafanyi hivyo!..Atamtoa mtu kwenye kanisa na kumwonyesha Neno lake kwanza…hicho ndicho kitu cha kwanza kumwonyesha…Kwamfano mtu anaweza kuwa katika kanisa ambalo kunafanyika ibada za sanamu….Sasa Roho Mtakatifu akitaka kumwondoa mtu hapo..hatamwonyesha kanisa Fulani lingine labda la kiroho akajiunge…kamwe hatafanya hicho kitu…atakachofanya ni kumwonyesha kwanza yule mtu maandiko yanavyosema…Atamwonyesha kwanza Neno linasema “usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, wala duniani, wala chini kuzimu usivisujudie wala kuvitumikia (Kutoka 20:4)”.

Hilo ndilo Neno la kwanza atakalomwonyesha…na kwa kupitia hilo neno sasa ndipo mtu atapata ufahamu kuwa hayupo sehemu salama…na kuondoka pale alipo kwenda kutafuta mahali pengine ambapo hataabudu sanamu kulingana na Neno lile….Lakini Mungu hawezi kuliruka Neno lake na moja kwa moja kukupeleka kwenye kanisa Fulani…kama ilivyokuwa kwa huyu dada..Lazima akuonyeshe kwanza kuna kitu hakipo sawa kulingana na Neno mahali ulipo ndipo uondoke…lakini kama huoni chochote halafu unasikia kitu kinakuambia uondoke hizo ni roho zidanganyazo zisemazo “Kristo yupo huku au kule..”

Sasa hiyo roho inamtoa huyu dada mahali ambapo wanawake wanajisitiri na kumpeleka mahali ambapo ataruhusiwa kuvaa vimini na kuingia navyo kanisani, ataruhusiwa kujipodoa, mahali ambapo hatakemewa dhambi wala kukumbushwa habari za ujio wa pili wa Bwana Yesu.

Ndugu usikimbilie kutafuta kanisa..tafuta kulijua Neno la Mungu…ukilifahamu hilo ndipo utakapoweza kujua mahali ulipo kama ni salama au sio salama..kadhalika sio kila ndoto unayoota inatoka kwa Mungu…Nyingine zinatoka kwa Ibilisi, hivyo hupaswi kuamini kila roho, bali unapaswa uijaribu…na huwezi kuijua kama hiyo ndoto inatoka kwa Ibilisi au kwa Mungu kama hulijui Neno (Hivyo Neno la Mungu litabaki kuwa msingi wa kila kitu)….Usipolijua Neno Siku zote utatii kila ndoto na kumbe zinakupeleka upotevuni..Na jambo la mwisho la kufahamu ni kwamba…Sio kila ndoto ina maana!..nyingine zinatokana na shughuli zetu za kibinadamu tu(Mhubiri 5:3)… Usitafute kujua tafsiri ya kila ndoto unayoota nyingine ziache zipite.

Kama ni Mungu anazungumza na wewe katika ndoto usiwe na papara!… yeye mwenyewe atakutengenezea njia rahisi tu ya kuielewa tafsiri ya hiyo ndoto kama imetoka kwake..inaweza isiwe siku hiyo hiyo au wiki hiyo hiyo, lakini itafika saa na siku itaijua tafsiri yake…Unachopaswa kufanya ni kudumu katika utakatifu na maombi na kusoma Neno lake.

Hivyo kwa kuhitimisha…Lijue sana Neno hiyo ndiyo silaha yetu..Na pia usihangaike huku na huko kutafuta ni kanisa gani lipo sahihi…hangaika usiku na mchana kujifunza Neno la Mungu, hangaika usiku na mchana kutafuta kuijua biblia inasema nini?…hangaika kumjua Yesu Kristo ni nani katika Maisha yako?,..kujua biblia inasema nini kuhusu uumbaji, kuhusu siku tunazoishi, kuhusu ubatizo kwanini uwepo?, kwanini tumeumbwa, kwanini tuanguke dhambini, na kwanini tuokolewe…isome sana kwasababu majibu yote yamo kwenye biblia…soma kitabu cha Matendo angalia kanisa la kwanza lilianzaje!..soma kitabu cha wakoritho angalia upendo unapaswa uweje, Soma kitabu cha Waebrania angalia tunaokolewaje kwa agano la damu.. tenga muda mrefu kusoma vitabu vyote taratibu na kwa umakini…na ufahamu utakaoupata huko kwa msaada wa Roho Mtakatifu ndipo utakaoamua ni wapi utulie,…Bwana atautumia huo kukuweka sehemu sahihi ya kumwabudu yeye.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

MPINGA-KRISTO

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

MADHABAHU NI NINI?

MAANA YA RANGI KIBIBLIA.

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Leo tutaona kimaandiko ni jinsi gani Roho wa Mungu anavyowasaidia watu kuyaelewa maandiko. Watu wengi, wanaposoma biblia na kuona kama ni ngumu haieleweki hususani vile vitabu vya manabii, kama vile Danieli, Isaya, Ezekieli, Yeremia, Zekaria, Ufunuo na vinginevyo, basi wanakata tamaa kabisa ya kuvimaliza, wanaona ni afadhali tu waache, au wanaona pengine hawastahili kufahamu habari zile kwasasa ni za watumishi Fulani tu, au viongozi Fulani wa dini waliokomaa ndio wanaouwezo wa kuelewa.

Lakini nataka nikuambie kutolielewa Neno la Mungu, sio ujinga, bali Mungu mwenyewe ndio karuhusu sehemu nyingine kulifunga kwa makusudi maalumu ili awafunulie wale waliotayari kujifunza (Danieli 12:4, Mathayo 13:11-14). Hivyo leo tutaangazia mfano mmoja wa kwenye biblia ili na wewe kwa kupitia habari hii, upate motisha ya kupenda kujifunza Neno la Mungu peke yako ukiongozwa na Roho Mtakatifu mwenyewe.

Sasa tukisoma kile kitabu cha Matendo ya Mitume tunaona habari ya mtu mmoja aliyetoka Kushi kwenda kuhiji Yerusalemu, Mtu huyu hakuwa myahudi, wala hakuwa chini ya viongozi wa kidini wa kiyahudi kama Gamalieli na wenzake, bali alikuwa ni kiongozi tu mkuu wa nchi hiyo ya Kushi (ambayo kwasasa ni nchi ya Ethiopia), lakini mtu huyu alimpenda Mungu wa Israeli, na hiyo ikawa inamfanya kila wakati wa sikukuu za kiyahudi na yeye awe anapanda Yerusalemu kuungana na wayahudi wengine kumwabudu Yehova.

Lakini pia alikuwa ni mtu aliyependa kujifunza maandiko. Tunasoma alipokuwa anarudi kutoka Yerusalemu akiwa kwenye gari lake, safarini kurejea nyumbani, biblia inatuambia mule ndani ya gari lake alikuwa akisoma vitabu vya manabii vya agano la kale..Kitabu cha Isaya sura ile ya 53, Mtu huyu alikuwa hayaelewi haya maandiko hata kidogo, pengine alikuwa anayasoma kwa kuyarudia tena na tena,labda pengine atapata tafsiri yake, au ufunuo..akifikiria habari ile ilikuwa inamzungumzia nani, anawaza moyoni mwake, mistari ile inamaanisha nini,..

Sasa kwa kitendo tu kama kile cha kutia nia kutaka kujua maana ya maneno yale..Hapo hapo Roho Mtakatifu akaanza kufanya kazi, akaanza kumwandalia mwalimu wa kumfundisha tokea mbali sana na yeye alipokuwepo.. Roho Mtakatifu akamtafutia mtu, akampata Filipo.. Filipo akiwa huko Samaria akihubiri na kubatiza watu, Roho Mtakatifu akamkatisha kazi yake, na kumwambia anza safari kuelekea mahali pasipo kuwa na watu, Kusini Njia ya jangwa la Gaza, Wakati anaondoka pengine Filipo anawaza kichwani kwake mbona Mungu anafanya niache maelfu ya watu huku Samaria na kuniambia niende huku mahali pasipokuwa na watu..Lakini yeye alitii kwasababu alijua Mungu anamakusudio yake, pengine alidhani huko anapokwenda atakutana na watu wengi zaidi ya wale aliowaacha Samaria,..Akasafiri kupita jangwa lile mpaka akafika mahali akaliona gari Fulani kwa mbali njiani, Roho Mtakatifu akamwambia lisogelee karibu kabisa..Na yeye akalisogelea, alipolisogelea akamwona mtu ndani yake yupo bize akisoma kwa sauti kitabu cha Isaya sura ile ya 53…

Ndipo kuanzia hapo Filipo akaanza kuzungumza naye tusome..

Matendo 8:26 “Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.

27 Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu,

28 akawa akirejea, ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.

29 Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.

30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?

31 Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.

32 Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.

33 Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.

34 Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?

35 Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?

37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Unaweza kuona hapo, Mkushi Yule sio tu aliishia kuyaelewa maandiko yale bali maandiko yale bali pia yalimpelekea kupata mpaka na ubatizo. Lakini hiyo yote ni kwasababu alitia nia moyoni mwake ya kutaka kuyatafakari maandiko kufahamu maana ya yale yaliyoandikwa. Na ndipo akafunuliwa mambo ambayo, hata kuhani mkuu kule Yerusalemu alikuwa hayajui, viongozi wote wa dini na waandishi wanayasoma kila siku lakini hawayaelewi..anakuja kufunuliwa mkushi ambaye hana ujuzi wowote na torati.

Vivyo hivyo na wewe na mimi, Kama umeokoka na unaye Roho Mtakatifu ndani yako, sio wakati wa wewe kukaa kungojea fundisho Fulani uletewe na mhubiri Fulani, au mchungaji Fulani tu peke yake,..Anza kwa kujijengea utaratibu wa wewe mwenyewe kuyatafakari maandiko binafsi kwa bidii na kumwomba Mungu akufunulie, ndipo hapo Mungu atakapotumia njia zake yeye mwenyewe alizozipanga kukufunulia, aidha kwa ufunuo au kwa muhubiri, hapo ndipo utakapopata uhakika kuwa Roho Mtakatifu amesema na wewe.. Wapo wengine wanasema nilikuwa ninautafakari sana mstari Fulani jana usiku, lakini sikuelewa, ghafla kesho yake nikasikia mhubiri Fulani anauhubiri mstari ule ule au nikakutana na mafundisho yale yale,.Hiyo ni ishara kuwa Mungu amemfunulia maana ya mstari ule. Sasa zipo njia nyingine nyingi ambazo Mungu anaweza kumfunulia mtu ikiwa tu atataka yeye mwenyewe kufahamu.

Lakini usikae tu bila kujishughulisha, kusubiria tu kufundishwa wakati wote, ujue kuwa yapo mambo ambayo Roho Mtakatifu anataka kukufundisha wewe kama wewe, vile vile anataka kukujengea uwezo wa wewe kuisikia sauti yake. Hivyo kama wewe umeshaokoka anza kuchukua hatua ya kuyatafakari maandiko bila kuogopa hichi ni kitabu cha manabii kisichoeleweka, au sio, suala la kutafsiri sio lako bali ni la Mungu, yeye mwenyewe ndiye atakayekufungulia njia zake za kuliewa.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

SEHEMU YA MAANDIKO ILIYOFICHWA.

KITABU CHA UZIMA

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

 

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

Pamoja na mengi tunayoweza kujifunza kwa Mariamu mama yake Yesu..lakini pia yapo mengi ya kujifunza kwa Yusufu Babaye Yesu. Leo kwa Neema za Bwana tutajifunza tabia moja ya Yusufu ambayo katika hiyo itatusaidia nasi kujifunza kumpendeza Mungu.

Mathayo 1:19 “Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.

20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao”.

Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa Yusufu hakuwa baba wa damu wa Bwana wetu Yesu Kristo. Kama tunavyofahamu Mimba ya Bwana Yesu ilitungwa kimiujiza (kwa uweza wa Roho Mtakatifu)..hakukuhusisha Baba wa kimwili. Hivyo Bwana wetu Yesu Kristo hakuwa na baba wa kimwili.

Lakini pamoja na hayo tunajifunza tabia moja ya Yusufu ambaye alimkubali kama mwanawe wa kimwili. Na tabia hiyo sio nyingine Zaidi ya kuwa na HAKI..Mtu mwenye haki anakuwa anaonekana kuwa na haki mbele za Mungu, kadhalika anakuwa na haki mbele za Watu na pia anakuwa mwenye kutenda haki.

Hivyo kipindi fulani alimposa huyu mwanamke Mariamu..na akiwa katika hatua za kumwoa ghafla akamwona anaujauzito…Ni wazi kuwa Mariamu hakumwambia siku ile ya kwanza Malaika Gabrieli alipomtokea…aliificha siri ile, akiwaza pengine itakuwaje siku Yusufu akifahamu jambo hilo…Na mimba ikaendelea kukua mpaka ikafika kipindi ikaanza kuonekana kwa macho..na Yusufu akaiona.

Ilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa Mariamu…akiwaza endapo Yusufu akimkataa itakuwaje!..jamii itamwelewaje?..Ni nani atakayeamini eti kwamba kapata mimba bila kukutana na mwanamume?..Ni wazi kuwa hakuna ambaye angemwelewa…Hivyo ni mawazo juu ya mawazo. (Ndugu kubeba kusudi la Mungu si jambo ambalo ni la kueleweka, wala si jambo la kupata heshima..lina gharama zake kubwa). Mariamu akiwa katika hali hiyo pengine alisema litakalo kuwa na liwe…Mimi nitamtegemea Bwana. (Hivyo ilihitaji Imani kubwa sana, kuitunza ile mimba isiyokuwa na Baba..haikuwa jambo jepesi). Leo tu hebu mwanamke apate mimba katika mazingira yasiyoeleweka eleweka ya uzinzi uone kama hatakwenda kuitoa…lakini haikuwa hivyo kwa Mariamu.

Baada ya Yusufu kugundua ile mimba…hata hakumuuliza Mariamu akaazimu kumwacha kwa siri…kwasababu alijua tayari kashakutana na mwanamume…Lakini katika ndoto Malaika akamwambia asimwache mkewe kwasababu mimba ile haikupatikana kwa uasherati bali kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Malaika yule katika ndoto akamtajia na jina la mtoto…Na alipokwenda kumuuliza pengine Mariamu na yeye akamuhadithia vile vile na jina la mtoto ni lile lile, hivyo hiyo ikawa ni uthibitisho wa kwamba mtoto yule ni wa kipekee katoka kwa Mungu..

Sasa hawa wawili Mariamu na Yusufu, mumewe wameshalitatua tatizo (wote wamekubali kuwa mimba ile ni ya kimiujiza)…Sasa Vipi kuhusu watu wa nje watawaelewaje?…Je! Yusufu atoke tu na kwenda kutangaza nje huko kuwa mke wangu kapata mimba kimiujiza?..si ataonekana mwendawazimu kwa watu wa kizazi alichopo?..nani atamuamini?….zaidi sana atamsababishia mke wake matatizo hata ya kupigwa kwa mawe kwa kosa la uzinzi…kwasababu watamhoji katolea wapi ile mimba?..Hivyo hapo inahitajika hekima nyingine ya ziada.

Na hekima hiyo si nyingine Zaidi ya kukubali tu kuchukua mashutumu…Yusufu ikambidi akubali kwamba yule ni mtoto wake kabisa….kwa namna nyingine tunaweza kusema “akakubali aonekane na watu kuwa alikutana na Mariamu kipindi kabla hawajaoana, na kwamba ile mimba ni ya kwake”..Alifanya hivyo kuzuia kumwaga lulu zake mbele za nguruwe…kama Bwana Yesu alivyokuja kusema huko mbeleni.

Mathayo 7: 6 “Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua”.

Hivyo pengine kama Yusufu kutukanwa basi alitukanwa…kama kudharauliwa alidharauliwa, kama kuonekana ni mtu mwenye tamaa alionekana hivyo…Watu wote wakaona ni mtu tu mwenye tamaa kwanini asingesubiri wafunge ndoa ndipo amkaribie mkewe?..walionekana yeye na mkewe Mariamu wote ni waasherati, na huyo mtoto atakayezaliwa atakuwa kazaliwa katika zinaa… Na mambo mengine mengi…

Leo hii wengi wanapenda Bwana Yesu aje katika Maisha yao…lakini wanazikimbia gharama za kumpokea Yesu…(Yusufu na Mariamu hawakuzikimbia) badala yake walizikabili walisema liwalo na liwe…itakuja kujulikana baadaye ukweli ni upi…Acha leo tuonekane ni watu waovu na tusiofaa lakini siku moja tutang’aa na kutukuzwa.

Luka 6:22 “Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.

23 Furahiwani siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni, maana, baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo”

Ndugu kumpokea Yesu maana yake ni kukubali mashutumu, kukubali kuonekana mjinga..kukubali kudharauliwa, kukubali kuchukiwa, kukubali dhiki na wakati mwingine kudhihakiwa. Ukiona umempokea Yesu Kristo na unapendwa na watu wote katika hatua za awali basi bado hujampata.

Unapoona aibu leo kuacha kuvaa vimini, na suruali kwasababu unaogopa kuonekana mshamba..Usitegemee kamwe Mungu kutembea na wewe..Bado kusudi la Mungu halipo ndani yako..Unapokataa leo kuacha kuvaa mawigi na hereni na kupaka lipstick, wanja na kujipamba na mavipodozi…ukweli ni kwamba bado Kristo hajaingia ndani yako..upo katika njia ielekeayo upotevuni…pengine kanisani huambiwi haya, kwasababu wanahisi hivi au vile, labda utawakimbia lakini leo umeyasikia na umeyasoma…Utakwenda jehanamu ya moto usipoyaacha!!.

Usipotaka kuacha ulevi kisa tu unaogopa utaonekanaje na jamii ya walevi wenzako..fahamu kuwa Mungu hayupo na wewe kabisa, unapokataa kuacha wizi, uasherati, ufanyaji masturbation, utoaji mimba, ulaji rushwa, ulawiti, ufiraji, utukanaji, uuaji, n.k Mungu yupo mbali na wewe sana..kama ulisikia mahali wanakuambia kuwa ukiambiwa mambo hayo unahukumiwa…Leo hii isikie tena hukumu hiyo!..huko uendako unapotea!.

Mariamu na Yusufu walibaki wenyewe…wanarudi mjini kwao Bethlehemu pengine hata ndugu zao kule hawakuwa na habari nao, hata kuwatengea chumba na kuishia kwenda kupanga, na huko walikopanga hata pia hawakupata nafasi..Mfalme mkuu Yesu Kristo akazaliwa katika zizi la ng’ombe..na Huyo aliyezaliwa katika zizi la ng’ombe leo hii ndio sababu ya wokovu wetu sisi…Leo hii hata kuzaliwa kwake kwenye zizi la ng’ombe ni fahari kwetu. Haleluya!.

Je ungependa kumgeukia leo Kristo kwa moyo wako wote? Na kuacha dhambi na kukubali kubeba msalaba wako na kumfuata yeye na kuwa mwenye haki kama Yusufu?..Kumbuka tunaishi katika siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni sana kurudi..Dakika hii tunapozungumza hayupo tena zizini..yupo mbingu za Mbingu, katika Nuru isiyoweza kukaribiwa biblia inasema hivyo katika..1Timotheo 6:14-16.

Kama upo tayari kufanya hivyo sasahivi.. basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .

NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Fanya hayo na Bwana azidi kukubariki.

Tafadhali share na wengine, kadhalika kama utapenda kupata masomo haya kwa njia ya whatsapp,au inbox inaweza kututumia ujumbe mfupi inbox, pamoja na namba yako ya whatasapp..Vile vile tunakukaribisha kutembelea website yetu hii kwa mpangilio mzuri wa masomo haya na yaliyotangulia..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

MARIAMU AKUTANA NA ELISABETI.

MARIAMU

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

Tabia pekee inayoufautisha uzao wa Mungu na ule wa ibilisi, ni kwamba ule wa Mungu unapohubiriwa kuhusu habari ya dhambi na madhara ya dhambi baada ya kufa huwa unatabia ya kuitikia mara moja na kwenda kutubu kwa kuugua na kumaanisha kweli kuacha dhambi zake, kama vile watu wa Ninawi. Au pale unapoadhibiwa kutokana na makosa yake, basi ni rahisi kutambua makosa yao na kugeuka, kama vile ilivyokuwa kwa Daudi..

Lakini uzao wa ibilisi ni tofauti sana. Unapoelezwa habari za hukumu, badala utubu, wenyewe huwa unakwenda kinyume unaokuwa wa kwanza kupinga, kwa nguvu zote..badala ushukuru kwa kuelezwa habari za uzima wa milele, utaona unaanza kutoa maneno ya kejeli..Na pale inapotokea Mungu anaudhibu kwa makosa yake, hapo ndipo maneno ya kufuru yataanza kutoka katika vinywa vyao. Labda mtu ni mzinzi halafu Mungu kampiga kwa magonjwa ya zinaa yasiyoponyeka, badala atubu kwa makosa yake aliyoyafanya, utamwona anamtukana Mungu na kusema Mungu gani huyu anaruhusu watu wake wateseke, n.k anasahau kuwa ni kwa makosa yake ndio yamemkuta hayo yote..

Halikadhalika siku ile Mungu atakapoiadhibu hii dunia kwa mapigo yake 7 ya mwisho, kwa wale waovu wote ambao watakuwa wamebakia duniani, biblia inatuambia badala watubu, waombe rehema Mungu awasamehe kwa maovu yao, Lakini kwao itakuwa ni kinyume chake..Watamtukana Mungu na kulikufuru jina lake.

Ufunuo 16:8 “Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto.

9 Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu.

10 Na huyo wa tano akakimimina kitasa chake juu ya kiti cha enzi cha yule mnyama; ufalme wake ukatiwa giza; wakatafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu,

11 wakamtukana Mungu wa mbingu kwa sababu ya maumivu yao, na kwa sababu ya majipu yao; wala hawakuyatubia matendo yao”.

Unaona? Uzao wa Nyoka unavyojidhirisha wazi wazi. Hao ndio wale tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu walikuwa wameshaandikiwa hukumu (Ufunuo 13:8 na 17:8). kama tu vile shetani na mapepo yake walivyo leo hii, japo wanajua kuwa wamekosa, wanajua kuwa ziwa la moto linawangoja huko mbeleni lakini mioyo wa toba hata chembe haupo ndani yao, wala hauwezi kuwepo ndani yao kinyume chake ndivyo anavyozidi kuiharibu kazi ya Mungu,Na kumkufuru Mungu.

Leo hii ukishajiona, habari za hukumu hazikuogopeshi tena hata kidogo, Nataka nikuambie hali yako ya rohoni ni mbaya, sana, una dalili ya kuangukia katika hili kundi la watoto wa ibilisi kamili.. Kama leo hii habari za toba ni kama hadithi tu, ukihubiriwa YESU yupo mlangoni kurudi unasema hilo jambo halipo, unaishia kudhihaki tu na kukejeli na kutukana..moyoni mwako.. Nataka nikuambie upo hatarini sana.

Yuda 1:17 “Bali ninyi, wapenzi, yakumbukeni maneno yaliyonenwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo,

18 ya kwamba waliwaambia ya kuwa, Wakati wa mwisho watakuwako watu wenye kudhihaki, wakizifuata tamaa zao wenyewe za upotevu.

19 Watu hao ndio waletao matengano, watu wa dunia hii tu, wasio na Roho.

Tukizidi kuwaona Watu wa namna hii basi ni dalili madhubuti inayothibitisha kuwa tunaishi nyakati za mwisho. Na hivi karibuni Bwana atatokea mawinguni na watakatifu wake, kukomesha kauli kama hizo na kufuru zake zote wanadamu wanazozitoa.

Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,

15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake”.

Siku ya hukumu inakuja ndugu, Dunia hii imeshaharibika sana, haina muda mrefu, haya mambo yote unayoyaona yanaelekea kufikia mwisho, usidanganyike na amani unayoiona kama ni amani iliyopo duniani biblia inasema pale wasemapo kuna amani ndipo uharibifu unapokuja kwa ghafla, na hawataokoka (1Wathesalonike 5:1-3)…Kama vile unavyopenda kujionyesha mbele za watu wewe ni mtanashati, unavaa vizuri utokapo kwenda mjini, lakini pengine unamatatizo mengi ya siri..kadhalika watu wote unaopishana nao huko barabarani wamependeza wengine wanamatatizo kuliko yako..kadhalika vyote unavyoviona huko nje na duniani kote vinavyovitua nyuma yake vina matatizo makubwa sana…Uzuri wa dunia usikupumbaze na kudhani dunia haina matatizo…Mwisho wa mambo yote umekaribia..na dakika zinavyozidi kwenda ndivyo tunavyozidi kuukaribia ule mwisho..

Na hata kama dunia itakuwa bado miaka 200 mbele je wewe binafsi utakuwa na muda huo wa kuishi?..Muda wako ni mfupi sana hapa duniani..Kama bado unazunguka zunguka kutafuta njia ya uzima mbali na Kristo, acha kupoteza muda, kama bado unaishi maisha ya dhambi na uovu, hutaki kutega sikio lako kusikia habari za hukumu inayokuja, na umilele unaokuja…wakati utafika utakapoungana na kundi hili kufungua kinywa chako kumtukana Mungu wako aliyekuumba wewe..Lakini itasaidia nini, kwasababu biblia inasema Mungu hadhiakiwi..Utakufa na kuelekea katika lile ziwa la Moto, na nafsi yako itakuwa imesahaulika milele.

Lakini kwanini hayo yote yakukute angali unao uwezo wa kuyakwepa sasa?. Katika Muda huu mfupi uliobakiwa nao Mungu anataka kuyabadilisha maisha yako, akuburudishe akupe na uzima wa milele, akulinde wakati wote ukiwa hapa duniani, akupe na tumaini la uzima wa milele baada ya kufa..Kama upo tayari kufanya hivyo leo, basi ujue atakusamehe makosa yako yote na dhambi zako zote ulizowahi kuzifanya huko nyuma, na kufuru zako zote ulizowahi kumtolea huko nyuma..Pengine ulizitoa kwa ujinga tu, na pasipo kujua madhara yake.. leo hii Yupo tayari kukusamehe..Ni wewe tu kuufungua moyo wako.

Hivyo kama umeamua kufanya hivyo Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 16.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Neno Hofu linatokana na  kuogopa. mfano ukishaogopa kitu Fulani tu basi hapo hapo hofu inaingia na mashaka pia.. tuchukulie mfano umekutana na nyoka njiani, usipomuogopa ni wazi kuwa hofu haiwezi kukuingia bali utaweza aidha kumpisha apite, au kukabiliana naye. Lakini ukishaogopa tu, basi hapo hapo hofu nayo inapata nafasi, na vilevile wasiwasi au  mashaka yatakujia ambayo yatakufanya udumu katika hofu ya muda mrefu kiasi kwamba hata siku ukipita karibu na majani na ukahisi  kitu kidogo tu kinakugusa mguuni bado utadhani ni nyoka anakutembelea kwasababu mashaka tayari yalishakuingia..

Hivyo chanzo cha Hofu ni kuogopa. Lakini tukirudi katika biblia zipo hofu za aina mbili, ya kwanza ni hofu ya Mungu..Ambayo hii Mungu amekusudia tuwe nayo lakini si kwa lengo la kututisha sisi , hapana bali kwa kutufanya tumche yeye na kuzithamini amri zake.

1Petro 1:17 Na ikiwa mnamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni.

Luka 12:4 “Nami nawaambia ninyi rafiki zangu, msiwaogope hao wauuao mwili, kisha baada ya hayo hawana wawezalo kutenda zaidi.

5 Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana uweza wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo”.

Unaona? Mtu mwenye hofu ya Mungu, ni wazi kuwa atamuheshimu Mungu, na vilevile ataziogopa hukumu zake, Hivyo itamfanya aishi katika maisha ya uangalifu zaidi na ya kumpendeza yeye.

Lakini zipo hofu nyingine zinazoasisiwa na shetani mwenyewe, mfano wa hizi ni kama.

Hofu ya magonjwa, hofu ya kuhisi hutosamehewa na Mungu (umemkufuru Roho Mtakatifu), hofu ya maadui, hofu za kukataliwa, hofu ya uzee, hofu ya kutokufanikiwa, hofu ya kushindwa, hofu ya kesho itakuwaje, hofu iliyopitiliza ya kifo,  hofu ya wachawi na mapepo kama ile waliyokuwa nayo mitume walipokuwa baharini usiku na kuona kivuli tu cha Bwana kinakuja na kuhisi kama ni mzimu umewafuata kuwaua..Hizi zote ni hofu ambazo zina asisiwa na shetani mwenyewe.  N.k

Na lengo la shetani kumletea mtu  hofu hizi zote ni kwa lengo la kumfanya akate tamaa, au arudi nyuma au akufuru au hata ikiwezekana afikie hatua ya kuutoa uhai wake au asione thamani kabisa ya maisha yake hapa duniani..

Nataka nikuambie…

Hakuna njia au suluhisho lolote la kuimaliza hofu ndani ya maisha yako, mbali na Mungu, hata uwe umefanikiwa kiasi gani, hata uwe na fedha nyingi kiasi gani, hata uwe na afya njema na elimu nzuri kiasi gani, kama Mungu hayupo ndani yako basi kipengele kimojawapo cha hofu hizi kitakuvaa tu.. Na bado utakuwa unaishi katika mateso na nafsi..

Biblia inatuambia..

1Yohana 4:16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

17 Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.

18 KATIKA PENDO HAMNA HOFU; LAKINI PENDO LILILO KAMILI HUITUPA NJE HOFU, KWA MAANA HOFU INA ADHABU; NA MWENYE HOFU HAKUKAMILISHWA KATIKA PENDO.

Unaona hapo? Ukilipata hili pendo la Mungu..Basi uhakika wa kuishinda hofu ya namna yoyote ile upo ndani yako, kwasababu hilo Pendo ndilo litakaloitupa nje hofu ya namna yoyote ile. Kwasababu pale unapoamua tu kumpa Kristo maisha yako, wakati huo huo   Amani yake anaanza kuachilia juu yako ili kuiua hofu yote iliyokuwa imeufunika moyo wako kwa muda mrefu.

Sikiliza maneno ya YESU..

Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga”.

Yesu anatoa amani ambayo huwezi kuipata kwa mtu yeyote, wala kutoka katika dini yeyote wala katika chuo chochote  kile, yeye hakufariji katika hofu yako kwa wanadamu wafanyavyo bali anakupa Amani inayoondoa hofu yote.

Anasema tena..

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Mimi kabla sijaokoka nilikuwa ni mtu mwenyewe hofu ya hukumu, na ya maisha isiyokuwa ya kawaida, mpaka ilifikia wakati ikanifanya nijione kama maisha yangu hayana thamani yoyote na kujisemea moyoni kwanini Mungu aliniumba mimi si ni heri angeniumba mjusi au ndege ningekuwa sina hatia yoyote ile..lakini ashukuruwe Mungu ulipofika wakati wa YESU kunifungua kutoka katika minyororo hiyo ya shetani..Na kunipa wokovu..Tangu huo wakati hadi sasa nimekuwa nikiisha maisha ya amani nyingi sana..Sina hofu yoyote haijalishi nipo katika hali gani ile amani yake ya tumaini la uzima wa milele linabubujika ndani yangu kila siku.

Sina hofu ya wachawi, wala hukumu, wala ya kushindwa, wala ya chochote kwasababu, Pendo lake kalimwaga ndani yangu..

Vivyo hivyo na wewe leo hii, ukiwa tayari kumruhusu Bwana Yesu ayabadilishe maisha yako, atakupa AMANI hii ambayo anaitoa bure..Unachopaswa kufanya ni kufungua tu moyo wako leo..

Kama upo tayari kufanya hivyo leo basi nataka nikuambie uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao utaufurahia maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwangu mimi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Na ile amani ya Mungu utaanza kuiona inaumbwa upya ndani yako.

Vile vile baada ya kutubu kwako bila kukawia kawia, unahitaji kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Luka 12:32 “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme”

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

KWANINI NAYAWEZA MAMBO YOTE KATIKA YEYE ANITIAYE NGUVU?

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

Utii ni nini kibiblia?


Utii ni kitendo cha kukubali kufanya maelekezo au maagizo unayopewa na aliye na mamlaka ya juu Zaidi yako wewe bila kujali  linakubaliana na maamuzi yako au la!.

Lakini pamoja na hayo watu wengi hawajui kuwa utii unaweza pia kutanguliwa na isihesabiwe kuwa ni dhambi ya kutokutii mbele za Mungu, Lakini hiyo ni katika mazingira maalumu ambayo tutajifunza mbele kidogo katika somo letu hili.

Ili kujua ni wakati gani tunapaswa tusitii Ni vizuri kwanza tukawajua watu ambao biblia imetuagiza tuwatii wakati wote:

1 Utii kwa wazazi wetu:

Wakolosai 3:20  “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana”

Hili ni agizo la Mungu kwa kila mwenye baba, au mama au mlezi, Mungu ametuagiza tuwatii wazazi wetu, kwa kila wanachotuelekeza kufanya. Na zipo baraka nyingi  katika kufanya hivyo  ikiwemo kupewa upendeleo wa kuishi umri mrefu hapa duniani

Kutoka 20:12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.

https://www.high-endrolex.com/12

Hata Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa na utii huu ukisoma Luka 2:51 inasema .. “Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.

Vivyo hivyo na sisi tunapaswa tuwe na huu utii kwa faida zetu wenyewe. Na pia kuyatimiza maagizo ya Mungu.

2 Utii kwa Mume:

Wake wamepewa maagizo ya kuwatii waume zao kwa kila namna.

1Petro 3:1 ” Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; ……5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao. 6  Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”

Soma pia Wakolosai 3:18 utaliona jambo hilo hilo.. Ikiwa wewe ni mke, halafu huisikii sauti ya mume wako labda kwasababu anakipato cha chini au anamapungufu fulani, au ni mwenye dhambi usidhani kuwa Mungu yupo upande wako. Unapaswa umtii na ujishushe kwasababu hayo ndiyo maagizo ya Mungu.

#3 Utii kwa wazee:

1Petro 5:5  “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu,..”

Mungu ametupa maagizo kama vijana, kuwathamini wazee, katika kanisa na vilevile katika jamii. Wanapotoa Mashauri hatupaswi kuwapinga au kujibishana nao,..Tukifanya hivyo tusidhani kuwa Mungu yupo upande wetu. Tunapaswa tuwape heshima kama vile wazazi wetu wenyewe ndivyo Mungu atakavyotufanikisha.

1Timotheo 5:17  Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha

1Timotheo 5.1  Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;

#4 Utii kwa viongozi wetu wa Imani:

Bwana anatuagiza, tuwatii wale wanaotungoza katika njia ya wokovu. Na ndio maana Paulo alimwandikia Filemoni maneno haya:

Filemoni 1:21  “Kwa kuwa nakuamini kutii kwako ndiyo maana nimekuandikia, nikijua ya kuwa utafanya zaidi ya hayo nisemayo”

Lakini tukipashana nao kauli au kuwavunjia heshima, au kutowasikiliza, basi tujue kuwa tunampinga Mungu, na Hivyo Mungu hawezi kuwa upande wetu hata katika huduma zetu.

#5 Utii kwa mabwana zetu (ma-boss):

Waefeso 6:5  “Enyi watumwa, watiini wao walio bwana zenu kwa jinsi ya mwili, kwa hofu na kutetemeka, kwa unyofu wa moyo, kana kwamba ni kumtii Kristo;

6  wala si kwa utumwa wa macho tu kama wajipendekazao kwa wanadamu bali kama watumwa wa Kristo, mkitenda yampendezayo Mungu kwa moyo;

7  kwa nia njema kama kumtumikia Bwana wala si mwanadamu;

8  mkijua ya kuwa kila neno jema alitendalo mtu atapewa lilo hilo na Bwana kwamba ni mtumwa au kwamba ni huru.”

Ikiwa utamvunjia heshima boss wako, ukafukuzwa kazi, usidhani kuwa Mungu atakuwa na wewe hata katika hiyo kazi nyingine mpya utakayokwenda kuitafuta. Haijalishi wewe ni mkristo au la..Maadamu umewekwa chini ya boss wako, basi huna budi kutii yale yote anayokuagiza kufanya bila unafiki..

#6 Utii kwa wenye mamlaka (Serikali):

Tito 3:1  “Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; 2  wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote.

Serikali na mamlaka zote zinafanya kazi ya Mungu, hivyo pale inapotuagiza tulipe kodi tunapaswa kufanya hivyo, inavyotuagiza tusifanye hiki au kile tunapaswa tutii..Lakini kama tutakwenda kinyume na serikali, kwa kiburi chetu wenyewe basi tujue kuwa Mungu hapo nasi hawezi kuwa na sisi.

#7 Utii kwa Mungu:

Huu ndio utii ulio wa juu Zaidi kuliko wote.. Biblia inatuambia katika Yakobo 4:7  “Basi mtiini Mungu…”.. Utii huu tunaweza kuuona  ukijidhihirishwa katika ukamilifu wote kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Wafilipi 2:7  “bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8  tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa MTII hata mauti, naam, mauti ya msalaba. 9  Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; 10  ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; 11  na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

Inatuambia tena…

Waebrania 5:7  Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;

8  na, INGAWA NI MWANA, ALIJIFUNZA KUTII kwa mateso hayo yaliyompata;

9  naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;

Vivyo hivyo na sisi kila mmoja Maisha yetu yanapaswa yawe ya utii, tukilitii Neno la Mungu, kila tunapoagizwa tulifanye.

Lakini sasa Je! ninapaswa kuwatii wote hawa hata kama mmojawao anachoniambia kinakinzana na maagizo ya Mungu?

Biblia imeweka wazi kabisa katika hali kama hiyo tunapaswa tusitii maagizo ya mtu yeyote bali ya Mungu kwanza..Ukisoma katika biblia utaona kuna wakati mitume walizuiliwa kuhubiri injili na wenye mamlaka na viongozi wa Dini lakini mitume walewale waliosema watiini wenye mamlaka ndio wakawa wa kwanza kusema..Imetupasa kumtii Mungu kuliko mwanadamu,

Matendo 5:27  “Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza,

28  akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu.

29  Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu”

Leo hii mama au baba yako anaweza kukwambia ufanye mila za matambiko, Na huku wewe unajua kabisa jambo hilo linakinzana na maandiko, hapo hupaswi kumtii mzazi wako hata kama itaonekana amewavunjia heshima kiasi gani…

Wazazi

Au wazazi wanakushurutisha unywe pombe, au ufanye dhambi, hapo unaruhusiwa kutowatii kwasababu utii huo hautokani na Mungu na hivyo mbele za Mungu hutahesabika kuwa hajawatii wazazi wako.. Maandiko yanathibitisha hilo (Mathayo 10:37)

Serikali

Vilevile, Serikali imekupiga marufuku usiabudu. Au usihubiri injili, Hapo unapaswa usiitii serikali hata kama ni Mungu ndiye aliyeruhusu tutii mamlaka hizo. Ilimtokea Danieli, lakini yeye alihesabu mamlaka na Mungu ni kubwa kuliko mamlaka zote, hivyo alichofanya ni kufungua madirisha kabisa watu wote wamwone akiabudu, bila woga wowote, Na sisi vivyo hivyo hatupaswai kuogopa kuyashika maagizo ya Mungu Zaidi ya wanadamu.

Mume.

Au Mume, anakushurutisha mfanye tendo la ndoa kinyume cha maumbile, hapo hupaswi kumtii, mume wako, kwasababu maagizo hayo yanakinzana na Neno la Mungu..Hata kama akikutisha kukuacha, mwache aende, utiifu wa Mungu ni Zaidi ya utiifu mwingine wowote.

Au boss wako anakulazimisha uingie katika mikataba ya rushwa, Na huku unajijua kabisa kuwa unachofanya kinakinzana na Imani yako, hapo hupaswa kumkubalia, au anakulazimisha ufanya naye uzinzi, hapo pia hupaswa kumkubalia haijalishi ni boss wako anayeheshimika kiasi gani. Au maandiko yamekuagiza uwatii hao kiasi gani.

Hivyo UTIIFU wowote ni lazima upatane na maagizo ya Mungu, kama haukinzani na Neno la Mungu hapo unapaswa utii yote unayoelekezwa kwa moyo wote bila kiburi..Na ndivyo Mungu atakavyokufanikisha..

Kwasababu kinyume na hapo, ukosefu wa utiifu wowote, ni kazi ya shetani ambayo siku hizi za mwisho ndio umekita mizizi..

2 Timotheo 3:1  Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.2  Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, WASIOTII WAZAZI WAO, wasio na shukrani, wasio safi.

Je! Umeokoka?

Je ndani yako kiburi kimekaa? Je unajua kuwa watu wa namna hiyo hawataurithi uzima wa milele? Je Unafahamu kuwa tunaishi katika kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, na hatutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili, Na unyakuo ni wakati wowote kwasababu dalili zote zimeshatimia?.. Kwanini usimpe leo Kristo Maisha yako.? Kwanini usiwe na uhakika wa kwenda mbinguni hata ukifa leo?

Kama upo tayari kufanya hivyo sasahivi.. basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .
NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu, unatii sasa kwa kunayaacha na kujitenga nayo, Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako piga namba hii 0789001312

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

MAAGIZO AMBAYO HAYAJAAGIZWA!

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Rudi Nyumbani:

Print this post

NGUVU YA MSAMAHA

Karibu tujifunze mambo yafuatayo; Nguvu ya msamaha ipo wapi? Biblia inaposema achilieni nanyi mtaachiliwa ina maana gani?Je kumpeleka mtu polisi au mahakamani ni kutokusamehe?

Neno Msamaha, halina tofauti sana na Neno ‘kuachilia’ au ‘kufungulia’. Unapomsamehe mtu aliyekukosea ni sawa na umemwachilia huru katika moyo wako. Huna naye deni tena, anakuwa anatoka katika kifungo cha moyo wako. Na kila mwanadamu anapaswa awe na huo uwezo wa kusamehe..Kwasababu msamaha ni ufunguo wa kitu kikubwa sana katika maisha.

Ingawa kwa akili za kawaida za kibinadamu ni ngumu kusamehe. Lakini ukiwa Mkristo(uliyeoshwa kwa damu ya Yesu Kristo na kufanyika kiumbe kipya) ni rahisi kusamehe. Na msamaha ule unaohusisha vitu ambavyo ni vigumu kusamehe huwa ndio unamaana kubwa sana na unafaida kubwa zaidi kuliko ule wa vitu vidogo.

Nguvu ya Msamaha upo katika Mistari ifuatayo.

Luka 6:36 ‘Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.

37 Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.

38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa’

Hapo anasema ‘achilieni’….Faida za kuachilia ni nini?..mbele kidogo anasema ‘nanyi mtaachiliwa’. Ikiwa na maana kuwa unapomsamehe mtu na wewe umeweka deni mahali fulani la kusamehewa…kwa kipimo kile kile na uzito ule ule uliomsaheme mtu…Na wewe unalo deni la kusamehewa kwa kiwango hicho hicho mahali fulani..wakati fulani.

Wengi wetu hatujui au hatuna taarifa kuwa kuna Mungu juu anayeyatazama maisha..Ukishaikosa au kupungukiwa na hiyo Imani basi ni ngumu sana kuyaishi maneno ya Mungu. Siku zote kumbuka Mungu yupo juu anatutazama, kila tendo, kila neno na kila tukio tulifanyalo..na yeye hasahau, wala hasinzii, wala hapumziki..Kwahiyo kila kitu tukifanyacho kiwe kibaya kiwe kizuri anakirekodi na kila kitu kina mshahara wake..Vingine mishahara yao ni hapa hapa duniani na vingine ni kule katika ulimwengu ujao.

Ufunuo 22:12 ‘Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo’.

Kwahiyo kama ulitukanwa na hujasamehe…Na wewe pia hujasamehewa matusi ya siri uliyoyatoa moyoni mwako dhidi ya mwingine. Haijalishi unayakumbuka au huyakumbuki…mbele za Mungu hayajasahaulika hata moja.

Tusome tena mfano ufuatao wa mwisho.

Mathayo 18:21 ‘Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho

29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.

32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake’.

Umeona…Nguvu ya msamaha ipo kwenye vile unavyovisamehe…Unapomsamehe mtu 100 basi na wewe unastahili kusamehewa 100..Kadhalika unaposamehewa vitu 100 na wewe una deni la kusamehe vitu 100.

Hakunaga short-cut ya kupokea msamaha…bila kusamehe, hakikisha unasamehe kwanza ili na wewe pia usamehewe…Bwana Yesu alisema hivyo katika…

Mathayo 6:14 “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.

15 Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu”.

Sasa utauliza hata mtu akinidhulumu vitu vyangu vyote nimsamehe?…Ndio msamehe..hiyo ni kwa faida yako binafsi…Utakuwa umemwachia Mungu wako deni kubwa la yeye kukurehemu wewe sawasawa na jinsi ulivyomsamehe mwingine…Ukumbuke huo mfano hapo juu.

Sasa swali lingine linakuja…Je kumpeleka mtu polisi au mahakamani ni kutomsamehe?

Yapo mazingira ya mtu kupelekwa polisi au mahakamani…ambapo sio dhambi.

Kwamfano imetokea mwizi kakuibia na umemfahamu, na ulipojaribu kumwendea ukakuta kakificha kile kitu au kashakitumia na hataki kukiri kwamba yeye ni mwizi wala kutubu…Mtu kama huyo moyoni unamsamehe kabisa kwa moyo wote…lakni pia anapaswa akashtakiwe kwa watu wa karibu au polisi ili asiendeleze wizi huo kwako na kwa wengine. (Kwa kufanya hivyo Sio dhambi) na hautahesabika kama hujamsamehe mbele za Mungu.

Kadhalika kama umedhulumiwa mali yako isivyo halali na kuna nafasi ya kuirudisha, pambana kuirudisha kwa hekima…Mfuate aliyeichukua mwambie akurudishie akikataa na kuna nafasi ya kumshtaki..mshataki ili aogope akurudishie na ili siku nyingine asirudie kufanya hivyo kwako au kwa wengine…Lakini akija kwako na kutubu na kukiri kwamba ni kweli kakudhulumu lakini mali ile kashaitumia na hana tena..na anatubu mbele zako…hapo huna budi kumsamehe asilimia zote na kumkumbatia. Hupaswi kwenda kumshtaki, kwasababu kashakiri kosa lake. Unapaswa umsamehe kabisa. (Ukikumbuka siku zote kwamba nguvu ya msamaha ipo katika kusamehe).

Ukiwasamehe waliokuudhi, Bwana atakusamehe uliyomuudhi…Ukiwasamehe waliokudhulumu…Bwana atakusamehe dhuluma ulizozifanya ndogo ndogo hata kama huzikumbuki…Ukimsamehe mtu aliyekuudhi siku moja na wewe utamuudhi mwingine na Bwana atampa moyo wa kukusamehe wewe.

Ukimsaheme mtu anayetamani kusamehewa na wewe, siku moja na wewe utasamehewa na mtu ambaye ungetamani akusamehe.

Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.

Bwana akubariki.

Usisahau tena “nguvu ya msamaha ipo katika kusamehe”

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312


Mada Nyinginezo:

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

UMUHIMU WA KUOMBA MSAMAHA.

DHAMBI ISIYO NA MSAMAHA.

Kwanini pale Bwana Yesu alichukua hatua ya kumsamehe dhambi kwanza kabla ya kumponya yule mtu mwenye kupooza?(Marko 2).

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

DUNIANI MNAYO DHIKI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Biblia..

Jambo mojawapo ambalo shetani anapenda kulitumia ili kuikatisha kazi ya Mungu ni kutumia vitisho?..Kwamfano utaona katika agano la kale wakati fulani ambapo Mungu aliwarudisha tena wana wa Israeli katika nchi yao baada ya kukaa utumwani Babeli kwa muda wa miaka 70 aliwaagiza watakaporudi wamjengee nyumba….Na kweli waliporudi walianza harakati za kuijenga nyumba ya Bwana huo Yerusalemu.Lakini kilichotokea ni kwamba..kazi ile haikudumu kwa muda mrefu..kwani maadui zao baada ya kuona wanaijenga nyumba ile waliwainulia visa…ikiwemo kwenda kupeleka taarifa kwa Mfalme kwamba watu baadhi fulani wanaijenga nyumba ambayo ilibomolewa kwa makusudi fulani…Hujuma zile zilipomfikia Mfalme akatoa amri kazi ile isimamishwe mara moja…Na wale watu wakamwogopa mfalme wakaacha kuifanya ile kazi..

Ezra 4:11 “Hii ndiyo nakili ya waraka waliyompelekea mfalme Artashasta; watumishi wako,watu walio ng`ambo ya mto wakadhalika.

12 Ijulikane kwa mfalme ya kuwa Wayahudi, waliokwea kutoka kwako, wamefika kwetu Yerusalemu; nao wanaujenga ule mji mwasi, mbaya; wamemaliza kuta zake, na kuitengeneza misingi yake.

13 Basi, ijulikane kwa mfalme, ya kuwa mji huu ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hawatatoa kodi, wala ada, wala ushuru, na mwisho wake wafalme watapata hasara.

14 Na sisi, kwa kuwa tunakula chumvi ya nyumba ya mfalme, wala si wajibu wetu kumwona mfalme akivunjiwa heshima, basi tumetuma watu na kumwarifu mfalme.

15 Ili habari zitafutwe katika kitabu cha tarehe za baba zako; ndivyo utakavyopata kujua kwa kitabu cha tarehe ya kuwa mji huo ni mji mwasi, wenye kuwadhuru wafalme, na maliwali, na ya kuwa wenyeji wake wamefanya fitina katika mji huo zamani; ndiyo sababu mji huo ukaangamizwa.

16 Twamwarifu mfalme ya kuwa mji huo ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hutakuwa na sehemu ya nchi ng’ambo ya Mto.

17 Ndipo mfalme akapeleka majibu;Kwa Rehumu,Bwana shauri, na Shimshai,mwandishi na wenzao wengine waliokaa katika Samaria,na penginepo ng`ambo ya mto, Salamu; wakadharika.

18 Ule waraka mlionipelekea umesomwa mbele yangu, nami nikaelewa na maana yake.

19 Nikatoa amri, na watu wametafuta habari; ikaonekana ya kuwa mji huu zamani umefanya fitina juu ya wafalme, na ya kuwa uasi na fitina zimefanyika ndani yake.

20 Tena walikuwako wafalme wakuu juu ya Yerusalemu, waliotawala nchi yote iliyo ng’ambo ya Mto; wakapewa kodi, na ada, na ushuru.

21 Sasa toeni amri kuwakomesha watu hawa kazi yao, mji huu usijengwe, hata mimi nitakapotoa amri. 22 Tena jihadharini, msilegee katika jambo hili; kwa nini madhara yazidi, na wafalme wapate hasara?

23 Hata nakala ya waraka huo wa mfalme Artashasta uliposomwa mbele ya Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na wenzao, wakaenda Yerusalemu upesi, kwa Wayahudi, wakawakomesha kwa nguvu na kwa kuwashurutisha.

24 Hivyo kazi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu ikakoma; nayo ikakoma hata mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi”.

Kama tunavyoona tendo hilo likawafanya wayahudi waiogope amri ya mfalme Zaidi ya maagizo ya Mungu ambayo waliambiwa waijenge nyumba ile bila woga!..Wakaendelea kukaa katika hali hiyo kwa muda mrefu mpaka Mungu alipozifunga mbingu mvua ziwe chache na chakula cha shida, Mpaka Mungu alipowatuma tena manabii wake Zekaria na Hagai kuwaambia watu watoke wakaijenge nyumba ya Mungu pasipo kuogopa chochote na Bwana atakuwa nao. Na walipowatii manabii wale walitoka na kwenda kukusanya vifaa vyote na vitu vyote vya ujenzi tayari kuanza kazi bila kujali tamko la mfalme..wakati wanaanza wale maadui zao tena wakapata taarifa na kumpelekea mfalme…

Lakini Mungu aliugeuza moyo wa mfalme kwa namna isiyoelezeka badala ya kuwapinga wayahudi kinyume chake alikubaliana nao..na zaidi ya yote akawafadhili kwa mali katika ujenzi wao..hivyo nyumba ya Mungu ikajengwa na kusitawi pasipo shida yoyote..Na Mungu akawabariki Israeli.

Ezra 5:1 “Basi manabii, Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido, wakawafanyia unabii Wayahudi waliokuwako Yerusalemu na Yuda; waliwafanyia unabii kwa jina la Mungu wa Israeli.

2 Ndipo akaondoka Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, wakaanza kuijenga nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na pamoja nao walikuwa manabii wa Mungu, wakiwasaidia.

3 Wakati ule ule Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakawajia, wakawaambia, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?

4 Ndipo wakawauliza hivi, Majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani na nani?

5 Lakini jicho la Mungu lilikuwa likiwaelekea wazee wa Wayahudi, hao wasiwazuie, hata habari ile imfikilie Dario, ndipo jawabu litakapopatikana kwa waraka.

6 Hii ndiyo nakala ya waraka waliyompelekea mfalme Dario; na Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzake wa Kiajemi, waliokuwako huko ng’ambo ya Mto,

7 walimpelekea waraka nao; na maneno haya yakaandikwa ndani yake; Kwa Dario, mfalme; Salamu sana.

8 Na ajue mfalme ya kuwa sisi tuliingia nchi ya Yuda, tukafika kunako nyumba ya Mungu mkuu, iliyojengwa kwa mawe makubwa, na miti imetiwa katika kuta zake, na kazi hii inaendelea kwa bidii, na kusitawi katika mikono yao.

9 Ndipo tukawauliza wale wazee, tukawaambia hivi, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?

10 Tukawauliza pia majina yao, ili kukuarifu wewe, tupate kuandika majina ya watu waliokuwa wakubwa wao.

11 Wakatujibu hivi, wakasema, Sisi tu watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunaijenga nyumba iliyojengwa zamani sana, yapata miaka mingi, ambayo mfalme mkuu wa Israeli aliijenga na kuimaliza.

12 Lakini hapo baba zetu walipomkasirisha Mungu wa mbingu na nchi, hata akaghadhibika, akawatia katika mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Mkaldayo, naye ndiye aliyeiharibu nyumba hii, akawachukua watu mateka mpaka Babeli.

13 Lakini katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Babeli, Koreshi, mfalme, alitoa amri ijengwe tena nyumba ya Mungu.

14 Na vyombo vya dhahabu na fedha, vya nyumba ya Mungu, alivyovitoa Nebukadreza katika hekalu lililokuwako Yerusalemu, na kuviingiza katika hekalu la Babeli, vyombo hivyo mfalme Koreshi alivitoa katika hekalu la Babeli, akakabidhiwa mtu, jina lake Sheshbaza, ambaye alikuwa amemfanya liwali;

15 naye akamwambia, Chukua vyombo hivi, uende, ukavitie katika hekalu lililoko Yerusalemu, na nyumba ya Mungu na ijengwe mahali pake.

16 Ndipo ye yule Sheshbaza alipokuja, akaupiga msingi wa nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na tangu wakati ule hata leo imekuwa ikijengwa, wala bado haijamalizika.

17 Basi, sasa, mfalme akiona vema, watu na watafute katika nyumba ya hazina ya mfalme, iliyoko huko Babeli, kama ni kweli ya kuwa mfalme Koreshi alitoa amri kuijenga nyumba hiyo ya Mungu katika Yerusalemu, na mfalme akatuletee habari ya mapenzi yake katika jambo hili”.

EZRA 6:1 Ndipo mfalme Dario akatoa amri, na watu wakatafuta katika nyumba ya vyuo vya tarehe, hapo akiba zilipowekwa katika Babeli.

2 Na chuo kimoja kilipatikana huko Akmetha, katika nyumba ya mfalme iliyo katika wilaya ya Umedi, na ndani yake maneno haya yameandikwa ili yakumbukwe.

3 Katika mwaka wa kwanza wa mfalme Koreshi, mfalme Koreshi alitoa amri, Kwa habari ya nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, nyumba hiyo na ijengwe, mahali watoapo dhabihu, na misingi yake ipigwe na kufanywa imara sana; kuinuka kwake kuwe mikono sitini, na upana wake mikono sitini;

4 ziwepo safu tatu za mawe makubwa, na safu moja ya miti mipya; gharama zake zitolewe katika nyumba ya mfalme.

5 Na vyombo vya dhahabu na fedha, vya nyumba ya Mungu, ambavyo mfalme Nebukadreza alivitoa katika nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu, akavileta mpaka Babeli, na virudishwe, vikaingizwe tena katika hekalu lililoko Yerusalemu, kila kimoja mahali pake, na wewe uvitie katika nyumba ya Mungu.

6 Basi sasa ninyi, Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na hao wenzi wenu wa Kiajemi, mlio ng’ambo ya Mto, jitengeni na mahali pale;

7 iacheni kazi hii ya nyumba ya Mungu, msiizuie; waacheni liwali wa Wayahudi, na wazee wa Wayahudi, waijenge nyumba hii ya Mungu mahali pake.

8 Tena, natoa amri kuwaagiza ninyi mtakayowatendea wazee hao wa Wayahudi, kwa kazi hii ya kuijenga nyumba ya Mungu; katika mali ya mfalme, yaani, katika kodi za nchi iliyo ng’ambo ya Mto, watu hao wapewe gharama zote kwa bidii, ili wasizuiliwe.

9 Na kila kitu wanachokihitaji, katika ng’ombe wachanga, na kondoo waume, na wana-kondoo, kwa sadaka za kuteketezwa watakazomtolea Mungu wa mbinguni, na ngano, na chumvi, na divai, na mafuta, kama makuhani walioko Yerusalemu watakavyosema, na wapewe vitu hivyo vyote siku kwa siku, msikose kuwapa;

10 wapate kumtolea Mungu wa mbinguni sadaka zenye harufu nzuri, na kumwombea mfalme, na wanawe, wapate uzima.

11 Pia nimetoa amri kwamba, mtu awaye yote atakayelibadili neno hili, boriti na itolewe katika nyumba yake, akainuliwe na kutungikwa juu yake; tena nyumba yake ikafanywe jaa kwa ajili ya neno hili.

12 Na Mungu huyu, aliyelifanya jina lake likae pale, na aangamize wafalme wote, na watu wote, watakaonyosha mikono yao kulibadili neno hili, na kuiharibu nyumba hii ya Mungu, iliyoko Yerusalemu. Mimi, Dario, nimetoa amri; na ifanyike kwa bidii nyingi.

13 Ndipo Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakafanya hayo kwa bidii, kwa sababu mfalme Dario alikuwa ametuma watu kwao.

14 Nao wazee wa Wayahudi wakajenga, wakafanikiwa, kwa msaada wa kuhubiri kwao Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido. Wakajenga, wakaimaliza kazi yao, kwa maagizo ya Mungu wa Israeli, na kwa amri ya Koreshi, na Dario, na Artashasta mfalme wa Uajemi.

15 Nyumba hiyo ikamalizika siku ya tatu ya mwezi Adari, katika mwaka wa sita wa kutawala kwake mfalme Dario”

Unaona, Lakini endapo wangekaa na kuendelea kusubiri..huku wanaiogopa amri ya mfalme..wangeendelea kukaa katika hali ile ile na hakuna chochote kingetokea…

Hivyo inatufundisha kuwa…tusiogope Kuifanya kazi ya Mungu maadamu ni yeye ndiye aliyetuagiza…Bwana Yesu alisema…

Mathayo 28:19 “ Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE, HATA UKAMILIFU WA DAHARI”.

Yupo pamoja nasi…haijalishi sheria ya nchi imesema tusihubiri…Hilo haliwezi kutuzuia sisi kuhubiri, haijalishi watu wanasema tusihubiri hiyo haipaswi kutufanya sisi tusihubiri..Haijalishi tayari kuna mswada ulipitishwa wa injili isihubiriwe…Injili itahubiriwa tu..Katika kuhubiri huko Bwana amesema atakuwa pamoja na sisi..Kama alivyokuwa na wayahudi hao hhapo juu.

Tujifunze tena katika habari hii ya mwisho..katika tutapata moyo zaidi katika kwenda kuhubiri habari njema…

Tusome…

Matendo 5:17 “Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu,

18 wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;

19 lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema,

20 Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu.

21 Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha. Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete.

22 Hata watumishi walipofika hawakuwaona gerezani, wakarudi wakatoa habari,

23 wakisema, Gereza tumeikuta imefungwa salama, nao walinzi wamesimama mbele ya mlango; lakini tulipoufungua hatukukuta mtu ndani.

24 Basi jemadari wa hekalu na wakuu wa makuhani waliposikia haya, wakaingiwa na shaka kwa ajili yao, litakuwaje jambo hilo.

25 Mtu mmoja akaja akawapasha habari ya kwamba, Watu wale mliowaweka gerezani wako ndani ya hekalu, wamesimama wakiwafundisha watu.

26 Ndipo yule jemadari akaenda pamoja na watumishi, wakawaleta, lakini si kwa nguvu, kwa maana waliogopa watu wasije wakawapiga kwa mawe.

27 Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza,

28 akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu.

29 Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.

30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti.

31 Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

32 Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wamtiio”.

Katika habari hiyo unaweza kuuliza… “kwanini malaika wamevunja sheria ya nchi?”…Kwasababu wamewatoa watu gerezani kinyume na utaratibu na bado wanawarudisha wahalifu wakafanye yale yale waliyozuiliwa kuyafanya tena kule kule hekaluni wanapopingwa.

Hebu jiulize umekamatwa na jeshi la polisi kwa kosa fulani…na usiku malaika anakuja kukutoa mahabusu pasipo ripoti yoyote na kukuambia ukaendelee kufanya kile kile kitu ambacho umezuiliwa kukifanya…Unaona hilo linaingia akilini?..kwasababu biblia inasema pia “tutii mamlaka iliyokuu”..Sasa kwanini hapa mamlaka hiyo inavunjwa?.

Jibu ni kwasababu ipo mamlaka nyingine iliyo kuu Zaidi ya hiyo ambayo ilishasema “Tukahubiri Injili kwa kila kiumbe, na yeye atakuwa na sisi hata ukamilifu wa Dahari”. Hakuna mamlaka nyingine duniani, wala kuzimu ambayo inaweza kuzidi hiyo Amri. Hakuna kikundi chochote, wala chama cha siasa, wala dini,wala wenye mamlaka, wala serikali yoyote ambayo ipo juu ya hiyo AMRI.. Na wala hakuna chochote kinachoweza kuizuia isitekelezeke.. Injili itahubiriwa tu mamlaka ya nchi ipende au isipende..Amri iwe imetolewa au haijatolewa…iwe imehalalishwa au haijahalalishwa…Yesu Kristo yupo upande wa wanaoihubiri injili haijalishi ni vikwazo vingapi vinaonekana mbele..haijalishi kuna hatari kiasi gani endapo itahubiriwa…lakini Injili(yaani Neno la Mungu)…Litahubiriwa tu..Bwana Yesu Kristo atahakikisha inafika kwa kila kiumbe…na hiyo ni AMRI sio OMBI. Kwasababu mamlaka yote ya mbinguni na duniani kapewa yeye..na hakuna aliye juu yake.

Hivyo simama hubiri injili leo..usiangalie mazingira yanayokuzunguka..usiangalie hatari zinazokuzunguka..yeye amesema “atakuwa pamoja nasi hata ukamilifu wa dahari”…

Warumi 8:31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?”.

Ubarikiwe sana.

Kama hujaokoka..simama leo uokoke…Tubu kwa dhati na kusudia kuacha yote uliyokuwa unayafanya yaliyo kinyume na Neno la Mungu. Na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?

 

 

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

 

MADHARA YA KUPUUZIA MAAGIZO YA MSINGI MUNGU ANAYOKUPA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.

Pale unapookoka au unapoamua kumtumikia Mungu ni vizuri kufahamu, aina za maadui ambao utakutana nao kuiharibu imani yako kwa namna moja au nyingine. Hiyo itakusaidia ili siku utakapokutana nao usiyumbishwe kiasi cha kukata tamaa ya kuendelea mbele.

#1 Adui wa kwanza ni Shetani na mapepo yake:

Luka 22:31 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;

32 lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako”.

Shetani akishaona umeokoka kweli kweli, hawezi kutulia tu kukuangalia unafanikiwa rohoni kiwepesi wepesi tu ni lazima atanyanyuka ili kukuandalia baadhi ya visa, hapo ndipo wengine atawaletea misiba, wengine atawasababishia kufukuzwa kazi, wengine magonjwa Fulani ya ajabu ajabu tu, wengine atawaletea majanga n.k. hiyo yote ni kwa lengo tu la kumfanya utetereke na ukate tamaa uiche imani yako, umkufuru Mungu..Kama alivyojaribu kufanya kwa Ayubu, kumletea majanga yote yale.

#2 Watu ya nyumbani kwako mwenyewe:

Mathayo 10:36 “na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.

37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili”.

Hapa ndipo shetani anapopenda kupatumia hasaa kwa mtu ambaye ndio kwanza mchanga kiroho, aliyekusudia kujitwika misalaba wake na kumfuata Yesu. Dada/Kaka unapoamua kumfuata Yesu kwa kujikana..jiweke tayari kupishana na baba yako au mama yako, au ndugu zako, au watoto wako, au jamii yako na marafiki zako, jiandae kuonekana umerukwa na akili, au umelogwa. Na Wakati mwingine kutengwa, kudharauliwa, na wengine wanafikia hatua hata ya kufukuzwa nyumbani, au kuzuiwa kula chakula au kunyimwa ada ya shule n.k. Ikiwa Yesu ni Bwana wetu ambaye hakuwa na dhambi hata moja hakuaminiwa na ndugu zake, (soma Yohana 7:5), Zaidi walipomwona anaanza kuhubiri walitaka kwenda kumkamata na kusema amerukwa na akili (Soma Marko 3:21). Si zaidi mimi na wewe ambao tunakasoro nyingi?.

Hata wewe ukimfuata yeye, utakutana na hayo hayo. Huwezi ukaelewana na ndugu zako wote moja kwa moja kwa uamuzi uliouchukua. Ipo sehemu utapishana nao tu. Lakini hilo lisikuvunje moyo. Songa mbele katika Imani…Ni shetani anawatumia tu lakini hao ni ndugu zako …Na hatawatumia hivyo milele kwa hivyo wapende tu.

#3 Ndugu yako wa karibu sana katika Imani:

Tofauti na ndugu wa mwilini. Adui mwingine ambaye unapaswa uweke akili kuwa unaweza kukutana naye mahali Fulani katika safari yako ya wokovu au huduma, ni ndugu mwenzako wa karibu sana katika imani.

Huyu ni Mtu ambaye huwezi kumtegemea, ni miongoni mwa wale ambao pengine unasali nao kila siku, unashirikishana nao kila siku habari njema za wokovu, unaokwenda kushuhudia nao, mnafanya kazi ya Mungu pamoja. Ghfla tu akakugeuka bila sababu yoyote yenye mashiko…anaweza kuingiliwa na kitu tu Fulani kidogo sana pengine tamaa Fulani, Na hiyo ikamfanya awe tayari kukusaliti au kuwa adui yako bila kujali mmekuwa katika safari pamoja kwa muda gani , bila kujali kwa kukusaliti huko kunakuachia madhara makubwa nyuma kiasi gani…

Hichi Ni chanzo ambacho huwezi kukitegemea, Hivyo jiweke tayari kiakili ili kusudi kwamba ikikutokea usivunje moyo kiasi cha kushindwa kuendelea mbele..

Mfano wa mtu wa namna hii ni Yuda. Alikuwa tayari kumuuza Bwana wake kwa tamaa ndogo tu ya fedha.

Zaburi 41: 9 “Msiri wangu tena niliyemtumaini, Aliyekula chakula changu, Ameniinulia kisigino chake”.

#4 Manabii wa uongo:

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti”?

Hawa licha tu ya kuwa na lengo la kukupotosha kwa mafundisho yao ya uongo., lakini pia kama wewe ni mtu wa Mungu uliyesimama wapo tayari hata kutoa ushuhuda wa uongo kinyume na wewe kwa lengo la aidha kujisafisha wao au kukuangusha wewe kwa makusudi ili wapate faida Fulani kutoka kwako.(3Yohana 1:10).

Hawa nao jiandae kukutana nao katika utumishi wako, au ukristo wako.

#5 Watumishi wenzako:

Hawa sio lazima wawe wa uongo, wanaweza wakawa wa ukweli, lakini kama hawajasimama vizuri, na kukosa ufahamu wa kuyapambanua maandiko vizuri, wanaweza kwa sehemu Fulani shetani akawatumia kuwafanya kuwa maadui wa Imani yako kwa muda.. Lakini bado wataendelea kubakia kuwa watumishi wa Mungu.

Mfano wa hawa ni Elfazi, Sofari, na Bildadi, Marafiki wa Ayubu. Ni wazee waliokuwa na hekima, washauri wa karibu sana wa Ayubu. Lakini walipoona Ayubu amekumbwa na matatizo kama yale, wao pasipo kukaa chini na kumwuliza Mungu ni nini maana yake..Wao wakakimbilia moja kwa moja kumlaumu Ayubu kuwa ametenda dhambi ndio maana yale yote yakampata..Na wakatumia vipengele kabisa vya maandiko ili kuthibitisha wanachokisema.. Na hiyo ndiyo iliyomfanya Ayubu akafadhaike zaidi hata ya kufiwa na watoto wake.

Kwasababu wale aliowategemea kuwa watakuwa na hekima ya kupambanua kilicho sahihi na kisicho sahihi, ndio wamekuwa wa kwanza kuwa mwiba kwake.

Vivyo hivyo, wapo watumishi ambao ni kweli wameitwa na Mungu, lakini watakapokuona unapitia katika hali Fulani kwenye imani tofauti na matazamio yao pengine ulitegemea na wao wawe wa kwanza kukuelewa..Ndio wanakuwa wa kwanza kukupinga tena wanatumia maandiko ..pengine ili tu kumridhisha mtu Fulani.

Hivyo hawa nao utakutana nao sehemu Fulani katika safari yako ya wokovu. Usiwachukie bali waombee kama Ayubua alivyowaombea marafiki zake, na baada ya muda mambo yote yatakuwa sawa.

#6 Viongozi wa dini za Uongo:

Nikisema viongozi wa dini za uongo simaanishi tu wale wa dini za mbali hapana, namaanisha wale ambao wanaonekana wapo katika Imani yako. Hawa ndio maadui wa ngazi ya juu sana, akitoka shetani na mapepo yake, hawa ndio wanaofuata .. wanaitumia serikali na wakati mwingine hata dola kupingana na kushindana na watu wa Mungu wa kweli.

Na hii itakupata ikiwa unaihubiri kweli kinyume na mafundisho yao. Wapo tayari kukupeleka mabarazani kukuhoji, na kukupiga na wakati mwingine hata kukuua..Vifo vingi vya mashahidi wa Yesu na mitume vilisababishwa na hawa.

Hawa ndio mfano wa Mafarisayo na Masadukayo. Walimpinga Bwana Yesu wakati wote, na kumpeleka kwa Herode na Pilato ili auawe.

Hata sasa, wapo wameshikamana na dola sana, na katikati ya hawa ndipo Yule mpinga-Kristo atakapotokea. Ibada za sanamu na mafundisho ya kipagani yasiyoambatana na maandiko ndiyo wanayoyahubiri.

Mathayo 10:17 “Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;

18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”.

Bwana anasema tazama nimekwisha kuwaonya mbele..(Mathayo 24:25).

Lakini pamoja na majaribu yote hayo, Mungu aliahidi kuwa hatamwacha mtu yeyote atakayemwendea,.Anamwachilia nguvu ya ziada ya kuweza kukabiliana na hivyo vizuizi,..Hapo ndipo mtu aliyeokoka anapojua kweli Mungu yupo pamoja na yeye. Lakini pia kwa kupitia hayo yote mwisho wake hauwi bure..

Ukiyastahimili hayo yote basi ufahamu kuwa thawabu yako ni kubwa sana mbinguni. Na Mungu atakufanya chombo chake kiteule kwa kazi yake.

Hivyo zidi kusonga mbele katika Imani ikiwa wewe upo tayari safarini katika wokovu. Ukifahamu kuwa taji lako limeshawekwa tayari mbinguni…

Luka 6:22 “Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.

23 Furahiwani siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni, maana, baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo”.

Hivyo furahi, kwasababu mbinguni unaheshimika. Kadhalika kumbuka pia kuwaombea wote wanaokuudhi, wote wanaotumika na shetani pasipo wao kujijua..waombee heri wala usiwaombee shari kama Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha..(katika Mathayo 5:43-46 na warumi 14:12).

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

ZIFAHAMU HOJA SABA ZENYE NGUVU MBELE ZA MUNGU.

NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

JE WAJUA?

NI NINI KINAKUPATA UNAPOIPUUZIA INJILI?

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

BONDE LA KUKATA MANENO.

Rudi Nyumbani:

Print this post