Category Archive Home

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)

Jina la Bwana YESU Kristo libarikiwe, karibu katika mwendelezo wa uchambuzi wa vitabu vya biblia, Tumekwisha kuvitazama vitabu kadhaa nyuma, na leo kwa neema za Bwana tutapiga hatua moja mbele, kukitazama kitabu cha Isaya.

Kabla ya kuendelea mbele,  ni muhimu kufahamu kuwa huu ni ufupisho tu!, na sio utimilifu wenyewe! hivyo kila mtu analo jukumu la kukisoma kitabu hichi cha Isaya kabla na baada ya kusoma ufupisho huu. Na vile vile, kama hujapitia uchambuzi wa vitabu vilivyotangulia, ni vizuri uupitie kwanza ili tuweze kwenda pamoja katika vitabu hivi vya mbeleni.

Kama hujapata uchambuzi huo basi unaweza kufungua hapa >>> Vitabu vya Biblia: Sehemu ya kwanza (www.wingulamashahidi.org) au unaweza ukatujuza kupitia inbox kwa namba zilizopo mwisho wa somo ili tuweze kukutumia.

Mwandishi wa kitabu cha Isaya ni Nabii Isaya mwenyewe, kitabu cha Isaya kina sura 66 sawasawa kabisa na jumla ya vitabu vyote vya biblia, ambavyo ni 66.

Tofauti na vitabu vingine vya kinabii kama Hosea, Zekaria, Hagai, Obadia, Yona, Habakuki, Malaki na vingine baadhi, ambavyo vimebeba Nabii za kipindi fulani tu au za jamii ya watu fulani tu!, labda kuhusu Mwisho wa dunia, au kuchukuliwa kwa Israeli kwenda Babeli, au hukumu ya Taifa fulani litubu!, vinakuwa havijabeba, au vinabeba kwa sehemu ndogo sana..

Lakini kitabu cha Isaya  ni kitabu ambacho kimebeba UNABII wa mambo karibia yote kwa mapana na marefu.

Kitabu cha Isaya, kina unabii kuanzia Israeli kuchukuliwa Mateka na kupelekwa Babeli, vile vile kina unabii wa kurejeshwa kwao, kina unabii wa kuanguka kwa Babeli, na hukumu ya Babeli, kina unabii wa kujengwa tena hekalu lililobomolewa, kadhalika kina unabii kuanguka na kunyanyuka kwa Mataifa mengine nje ya Israeli, vile vile kina unabii wa UJIO WA MASIHI, (Hakuna kitabu kingine chochote kilichotabiri kwa kina jinsi Masihi atakavyokuwa na tabia zake kama kitabu hiki, tutakuja kuliona hilo vizuri mbele kidogo)..

Kitabu cha Isaya pia kimetabiri Siku ya Ghadhabu ya Mungu, ambayo itakuja  baada ya Unyakuo wa kanisa kupita!, kimetabiri mpaka kipindi cha utawala wa miaka 1000,wakati ambao Kristo atatawala na watakatifu wake kwa miaka elfu akiwa hapa duniani, na mambo mengine mengi.

Leo tutazitazama nabii hizi chache, Lakini kabla ya kwenda kuzitazama.. Ni vyema pia kufahamu jambo lingine la muhimu, kwamba Kitabu cha Isaya hakijaandikwa kwa muda wa siku moja, au mwezi, au mwaka mmoja. Hapana!.

Kitabu cha Isaya kimeandikwa kwa kipindi cha Miaka 58 kuanzia mwaka (739KK-681KK)

Kwa kadiri Isaya alivyokuwa anapewa maono ndivyo alivyokuwa anaandika, na sio kila siku alikuwa anapewa maono, wakati mwingine ilipita kipindi kirefu hata zaidi ya mwaka, pasipo kupokea unabii wowote wa kuandika.. Hivyo Sura zote 66 za kitabu hicho, ni mfululizo wa Maono aliyoyaona Isaya, katika kipindi chote cha Maisha yake, tangu alipoanza kuona maono mpaka alipokufa (yaani miaka 58).

Ndio maana utaona maono ya kitabu hicho ni kama yamechanganyikana..Ni kwasababu hakupewa kipindi kimoja.. Leo anaweza kupewa Ono linalomhusu Masia, akaliandika katika Sura moja, mwezi ujao au mwaka ujao akapewa linalohusu kuanguka kwa Babeli akaliandika chini katika sura ya pili, baada ya miaka miwili tena anapewa ono linalomhusu Masia tena (Yesu Kristo), tofauti na lile la kwanza, akaliandika katika sura ya 3, baada ya miezi kadhaa anapewa unabii tena kuhusu Utawala wa miaka elfu n.k Kwahiyo ni unabii juu ya unabii, kwa vipindi tofauti tofauti.

MAISHA YA ISAYA.

Isaya alikuwa ni Mwana wa mtu aliyeitwa Amozi, biblia haijaleza huyu Amozi, baba yake Isaya alikuwa ni mtu wa namna gani, lakini ni wazi kuwa alikuwa ni mtu maarufu, aliyekuwa anajulikana). maana ya jina Isaya ni “Bwana ni Wokovu”..(Isaya alianza kuona maono ya Mungu baada ya kifo cha mfalme Uzia (Isaya 6:1), Na ni nabii aliyetokea mapema kabla ya wakina Yeremia, Danieli, Ezekieli, Yona na wengine wengi..

Biblia haijaeleza kwa undani sana maisha ya Isaya, lakini maandiko yanasema alioa Nabii Mke na kuzaa nae watoto (Isaya 8:3), Na mwanamke huyo aliyemwoa, alimwoa kwa agizo la Bwana, kwasababu Mungu aliyafanya maisha yake kuwa ishara kwa Israeli, kama vile alivyoyafanya ya Hosea na Ezekieli.

Ni kawaida ya Mungu kuyafanya maisha ya watumishi wake kuwa Ishara kwa dunia, Kwamfano utaona Nabii Ezekieli kuna mahali aliagizwa na Mungu ale kinyesi, lengo ni kufikisha ujumbe fulani kwa watu fulani, kadhalika kuna mahali Nabii Hosea aliambiwa na Mungu akaoe mwanamke wa uzinzi, na kuzaa naye watoto ili kufikisha ujumbe fulani kwa watu fulani. Vile vile Nabii huyu  Isaya Mungu aliyachagua maisha yake kuyafanya ishara kama hawa wengine, ili kufikisha ujumbe fulani. Kwamfano utaona kuna mahali Nabii Isaya, aliambiwa na Mungu, atembee uchi..

Isaya 20:2 “wakati huo Bwana alinena kwa kinywa cha Isaya, mwana wa Amozi, akisema, Haya, uvue nguo ya magunia viunoni mwako, na viatu vyako miguuni mwako.

3 Naye akafanya hivyo akaenda uchi, miguu yake haina viatu. Bwana akasema, Kama vile mtumishi wangu Isaya anavyokwenda uchi, hana viatu, awe ishara na ajabu kwa muda wa miaka mitatu juu ya Misri na juu ya Kushi;

4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawachukua uchi, wafungwa wa Misri, na watu wa Kushi waliohamishwa, watoto kwa wazee, hawana viatu, matako yao wazi, Misri iaibishwe.

5 Nao watafadhaika, na kuona haya kwa ajili ya Kushi, matumaini yao, na Misri, utukufu wao”.

Kwa maelezo marefu kwanini Isaya aliagizwa atembee uchi unaweza kufungua hapa >>Kwanini Isaya aliagizwa atembee uchi?, (www.wingulamashahidi.org) Au ukatujuza kwa njia ya inbox, tukutumie somo kamili .

Kwahiyo Maisha ya Isaya, mbali na kutoa Unabii, Mungu aliyatumia maisha yake pia kama Ishara, kulingana na historia, Nabii Isaya alikufa kifo cha kukatwa na Msumeno sawasawa na Waebrania 11:37.

NABII ZA ISAYA.

Nabii za Isaya zimegawanyika katika vipengele vitano, 1) Unabii juu ya Yuda na Israeli kabla ya Uamisho wa Babeli, 2) Unabii juu ya Israeli baada ya Uamisho 3) Unabii wa kuja kwa Masihi, mara ya kwanza na mara ya pili  4) Unabii wa kuanguka kwa mataifa  5) Unabii wa hukumu ya Mungu na Utawala wa miaka Elfu .

Tutaziangalia Nabii hizi kwa uchache moja baada ya nyingine.

 1. Unabii wa Yuda na Israeli kabla ya Uamisho wa Babeli.

Nabii Isaya alitokea miaka miaka karibia 155 kabla ya Uamisho wa Babeli, Na Israeli pamoja na Yuda ilikuwa tayari imeshafanya machukizo makubwa mbele za Bwana, hivyo Nabii Isaya alianza kutabiri kuanguka kwa Yerusalemu miaka 155 kabla ya maangamizi hayo kutokea. (kuonyesha ni jinsi gani Mungu alivyo na huruma, jinsi anavyotoa kipindi kirefu cha watu kutubu, na kugeuka), lakini tunaona hawakutubu na siku ilipofikia uharibifu uliwajia ghafla na wote wakapelekwa utumwani.

Ufunuo 22: 4 “Kwa sababu hiyo nasema, Geuza uso wako usinitazame, nipate kulia kwa uchungu; usijishughulishe kunifariji, kwa ajili ya kuharibika kwake binti ya watu wangu.

5 Kwa maana siku ya kutaabika, siku ya kukanyagwa, siku ya fujo inakuja, itokayo kwa Bwana, Bwana wa majeshi, katika bonde la Maono; inabomoa kuta; na kuililia milima”.

Huo ni unabii wa kuharibiwa kwa Yuda, na Mfalme Nebukadreza.

 2. Unabii wa Israeli baada ya kuhamishwa.

Pamoja na Isaya kutabiri kuanguka kwa Yerusalemu, lakini pia alitabiri wayahudi kurejeshwa tena Yerusalemu kutoka Babeli, aliabiri atatokea mfalme anayeitwa Koreshi, atakayewaweka huru wayahudi, na kuwapa ruhusa warejee nchini mwao wakiwa huru..

Isaya 44:26 “nilithibitishaye neno la mtumishi wangu, na kuyafikiliza mashauri ya wajumbe wangu; niuambiaye Yerusalemu, Utakaliwa na watu, nayo miji ya Yuda, Itajengwa, nami nitapainua mahali pake palipobomoka;

27 niviambiaye vilindi, Kauka, nami nitaikausha mito yako;

28 nimwambiaye Koreshi, Mchungaji wangu, naye atayatenda mapenzi yangu; hata ataunena Yerusalemu, Utajengwa; na hilo hekalu, Msingi wako utawekwa”.

Unaweza kusoma tena juu ya Unabii huo wa Koreshi katika Isaya 45:1-2

 3. Unabii wa kuja kwa Masihi.

Baada ya Nabii Isaya kuonyeshwa kurejeshwa kwa Wayahudi kutoka utumwani, na kustarehe katika nchi yao, Mungu aliendelea kumwonyesha maono ya kuja kwa Masihi yaani Yesu, alimwonyesha tangu kuzaliwa kwake jinsi kutakavyokuwa kwamba, atazaliwa na Bikira(Isaya 7:14), Na jinsi atakavyopitia mateso na kufa, kwaajili ya dhambi zetu, kama vile mwanakondoo apelekwaye machinjoni.

Isaya 53:1 “Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?

2 Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.

3 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.

4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

6 Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.

7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.

8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu”.

Hakuna mahali pengine popote katika biblia palipotabiri Bwana kuzaliwa na Bikira isipokuwa hapa katika Isaya tu,  wala hakuna kitabu kingine chochote kilichoelezea mateso ya Bwana Yesu kwa mapana namna hii kama hichi kitabu cha Isaya.

Nabii Isaya hakuishia tu kufunuliwa hayo juu ya Masihi, bali alifunuliwa mpaka utawala wake wa kifalme ambao utakuja baada ya hasira ya Bwana kupita, yaani utawala wa miaka elfu moja. (tutakuja kuuona  vizuri mbele kidogo), Lakini kwa habari za unabii wa ujio wa Masihi na tabia zake, unaweza pia kuzisoma katika mistari hii>>Isaya 11:1-2, Isaya 61, na Isaya 9:6.

 4. Unabii wa kuanguka kwa Mataifa.

Sehemu hii ya unabii ndio iliyochukua nafasi kubwa katika kitabu cha Isaya. Bwana Mungu alimwonyesha Isaya, Nabii juu ya Mataifa yote ambayo kwa namna moja au nyingine yalihusiana na taifa la Israeli, kuanzia Misri, Babeli, Ashuru, Moabu, Filisti, Tiro, Kushi, Edomu na mengine machache.

Mataifa hayo Bwana Mungu alitabiri kuanguka kwao, kwasababu na yenyewe yalifanya mabaya kama Israeli tu!, Kwamfano Taifa la Babeli liliwatesa Israeli watu wa Mungu, ijapokuwa aliliruhusu hilo kwa lengo la kuwaadhibu Israeli, lakini bado Babeli ilikuwa na hatia juu ya hilo, kadhalika Babeli ndio ilikuwa kitovu cha machukizo yote ya ulimwengu kipindi hicho. (Kumbuka katika siku hizi za mwisho pia kuna Babeli nyingine ya kiroho, ambayo inawachukua watu utumwani na vile vile Mungu kaitabiria hukumu, kama alivyoitabiria Babeli hii, kama utapenda kujua Babeli hiyo unaweza kufungua hapa  >>> Babeli ya rohoni au ukatutumia ujumbe inbox, tukutumie somo kamili). Hivyo Mungu aliyaadhibu na kutabiri kuanguka kwao.

Tutapitia mataifa machache, na mengine tutayasoma kwa nafasi zetu..

Taifa la Babeli.

Isaya 14: 4 “utatunga mithali hii juu ya mfalme wa Babeli, na kusema, Jinsi alivyokoma mwenye kuonea; Jinsi ulivyokoma mji ule wenye jeuri!

5 Bwana amelivunja gongo la wabaya, Fimbo ya enzi yao wenye kutawala.

6 Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu”.

Soma tena..

Isaya 47:1 “Haya, shuka, keti mavumbini, Ewe bikira, binti Babeli; Keti chini pasipo kiti cha enzi, Ewe binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.

2 Twaa mawe ya kusagia, usage unga; Vua utaji wako, ondoa mavazi yako, Funua mguu wako, pita katika mito ya maji.

3 Uchi wako utafunuliwa, Naam, aibu yako itaonekana. Nitalipa kisasi; simkubali mtu ye yote.

4 Mkombozi wetu, Bwana wa majeshi ndilo jina lake, Mtakatifu wa Israeli.

5 Kaa kimya, ingia gizani, Ee binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena Malkia wa falme.

6 Nalikuwa nimekasirika na watu wangu, naliutia unajisi urithi wangu, nikawatia mkononi mwako; wewe hukuwatendea rehema; uliwatia wazee nira yako, nayo nzito sana.

7 Ukasema, Mimi nitakuwa bibi milele; hata hukuyatia hayo moyoni mwako, wala hukukumbuka mwisho wa mambo hayo.

8 Sasa, basi, sikia haya, wewe upendaye anasa, ukaaye na kujiona salama, wewe usemaye moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi; sitaketi mfano wa mjane, wala sitajua kufiwa na watoto”

Pia unaweza kusoma Isaya 13, inazungumzia unabii huo huo wa kuanguka kwa Babeli.

Misri.

Misri ni taifa lililowatesa Israeli, kipindi kabla hawajaingia nchi ya Ahadi, Taifa hili limekuwa adui kwa Israeli mara kadhaa, na pia limekuwa kitovu cha maasi mengi duniani, hata baada ya Israeli kuingia nchi ya kaanani. Bwana alilitabiria pia kuanguka kwake katika mistari hii >> Isaya 19:1-5

Ashuru.

Taifa Ashuru ni taifa lililowachukua pia Israeli utumwani, nalo pia Bwana alilitabiria kuanguka.. Hukumu ya taifa hilo unaweza kuisoma kupitia mistari hii >> Isaya 10:5, Isaya 14:25-27.

Ufilisti

Filisti ni mji uliokuwa unawatesa Israeli mara nyingi, na uliokuwa unaabudu miungu kwa kiwango kikubwa, Unabii kwa kuanguka kwake unaweza kuusoma kupitia mistari hii >> Isaya 142:8-38.

Moabu

Moabu ni Taifa lililokuwa adui wa Israeli kwa kipindi chote, ndilo taifa lililomwajiri Balaamu awalaani Israeli walipokuwa wanaiendea nchi yao ya Ahadi..Bwana alilitabiria kuanguka kwake kupitia nabii Isaya, katika mistari hii >> Isaya 15:1-5

Tiro

Tiro ni mji uliokuwa karibu na Sidoni, katika nchi ya Lebanoni, huku ndiko Yezebeli alipotokea na ndipo kulipokuwa kitovu cha ibada za mungu baali. Ulikuwa ni mji wa kibiashara, na wafanya biashara na ulikuwa umejaa udhalimu. Bwana aliutabiria kuanguka kwake katika mistari hii >> Isaya 23:1-6

Mataifa mengine madogo madogo kama Edomu, Kushi, Dameski na mengine yanayohusiana na miji hiyo, Bwana aliitabiria kuanguka kwao kupitia mistari hii>>(Isaya 63:1-6, Isaya 34:1-10, Isaya 17:1-6, na Isaya 18:1-3).

 5. Unabii wa hukumu ya Mungu na Utawala wa miaka Elfu .

Pamoja na Isaya kupewa unabii wa Kuanguka kwa Mataifa, alionyeshwa pia mwisho wa dunia, yaani hukumu ya ulimwengu mzima, wakati Ghadhabu ya Mungu itakapomwagwa duniani kutokana na maasi na maovu ya ulimwengu, na vile vile akaonyeshwa utawala wa amani wa Bwana Yesu wa miaka elfu moja duniani na mbingu mpya na nchi mpya.

Siku ya Ghadhabu ya Bwana na hasira yake.

Isaya 24:1 “Tazama, Bwana ameifanya dunia kuwa tupu, aifanya ukiwa, aipindua, na kuwatawanya wakaao ndani yake.

2 Na itakuwa kama ilivyo hali ya watu, ndivyo itakavyokuwa hali ya kuhani; kama ilivyo hali ya mtumwa, ndivyo itakavyokuwa hali ya bwana wake; kama ilivyo hali ya mjakazi, ndivyo itakavyokuwa hali ya bibi yake; kama ilivyo hali yake anunuaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake auzaye; kama ilivyo hali yake akopeshaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake akopaye; kama ilivyo hali yake atwaaye faida, ndivyo itakavyokuwa hali yake ampaye faida.

3 Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo.

4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.

5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele.

6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.

Utawala wa amani wa miaka elfu na wa mbingu mpya na nchi mpya.

Isaya 65:17 “Maana, tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.

18 Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.

19 Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.

20 Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.

21 Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake.

22 Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.

23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na Bwana, na watoto wao pamoja nao.

24 Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.

25 Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng’ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema Bwana”.

Ni nini tunajifunza katika kitabu hichi cha Isaya?

Tunajifunza kuwa maneno ya Mungu hayapiti kamwe!. Alitabiri habari za kuanguka kwa Yerusalemu, zikatimia kama zilivyo, alitabiri habari za kuzaliwa Masihi kupitia bikira, na zikatimia kama zilivyo, na ametabiri kuanguka kwa mataifa pamoja na siku ya kisasi cha Bwana, vile vile zitatimia kama zilivyo.

Hizi ni siku za mwisho, siku ya hasira ya Bwana imekaribia, unyakuo wa kanisa utakapopita tu!, kitakachokuwa kimebaki ni dhiki kuu na hiyo siku ya hasira ya Bwana!, Jua litatiwa giza, maji yote yatakuwa damu, milima na visiwa vitahama, na Bwana atawahukumu wanadamu wote wanaotenda maasi, na mwisho wao utakuwa katika lile ziwa la moto. Lakini watakatifu, yaani wote waliooshwa kwa damu ya mwanakondoo, watairithi hiyo mbingu mpya na nchi mpya.

Je mimi na wewe tutakuwa wapi siku hiyo?

Bwana akubariki.

Usikose mwendelezo wa vitabu vinavyofuata.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

MNARA WA BABELI

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NANI ATAKAYEWAPA ILIYO YENU WENYEWE?

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.

Ulishawahi kuutafakari kwa ukaribu huu mstari ambao Bwana Yesu aliusema katika..

Luka 16:12 “Na kama hamkuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?

Kauli hii ni kinyume na sisi tunavyoweza kuitafsiri. Kwa kawaida, ni sharti kwanza mtu atazame uaminifu wa kile cha kwako kwanza, ndipo ashawishike kukuongezea kilicho cha kwake. Ukienda kukopa Benki ni sharti waangalie mipango/ mikakati yako na matumizi yako kwa kile ambacho tayari umeshaanza kukifanya, ndipo wakupe mkopo wa kuongezea biashara yako.

Vinginevyo ukienda hoe hae, huna malengo au mipango, ni wazi kuwa hutaambulia chochote, kwasababu wanahofia kama tu hicho cha kwako kidogo kimekushinda kukitazama, ukiongezewa kikubwa utawezaje?

Kama cha kwako mwenyewe haukijali, utajali vipi vya wengine?. Kama unajiibia mwenyewe ofisini kwako, utayahurumiaje mashirika ya wengine uliyopewa uyasimamie..

Lakini kwa Mungu ni tofauti, ili akupe kitu chako mwenyewe, ni sharti kwanza ukijali cha mtu mwingine. Ni sharti kwanza uonyeshe uaminifu kile cha mwingine ulichowekewa dhamana.

Unataka Mungu akupe uchungaji wako, Atakuangalia Je ulishawahi kuwajali kondoo wa Mungu, katika hilo kanisa ulilowekwa chini yake sasa? Ulishawahi kuwahudumia kwa upendo kabisa na kuwajali kama Mungu anavyotaka, Kama hukuweza basi ni ngumu sana Mungu kukupa cha kwako.

Mtu anamwomba Mungu ampe watoto wa kulea, lakini watoto wa familia nyingine hawajali, wala hata hana mpango nao kisa tu hajawazaa yeye.. Mungu akishaona hivyo, anasema, hata akikupa wa kwako hutaweza kuwalea, ni heri tu ubaki hivyo hivyo ..

Leo watu wengi wanamwomba Mungu awape ofisi zao wenyewe, Je, pale ulipowekwa kama muajiriwa unatumika kwa uaminifu?.

Unataka Mungu akupe nyumba yako mwenyewe, Je! Umekuwa mwaminifu katika hiyo nyumba ya mwingine Mungu aliyokuweka chini yake? Unaijali, unaitunza, unaipa thamani kama vile ni ya kwako?

Chochote tunachokitaka kwa Mungu, tujue kuwa atatujaribu kwanza kwa kutuletea hicho hicho kutoka kwa wengine,aupime uaminifu wetu. Mungu alimpima Yusufu katika nyumba ya Potifa kama je! Atakuwa mwaminifu? Na alipouona uaminifu wake, ndipo akampa cha kwake, akawa waziri mkuu kule Misri.

Hata katika ufalme wa Mungu, hatutapewa miji yetu wenyewe tuimiliki kule kwenye mbingu mpya na nchi mpya kama hatutakuwa waaminifu hapa duniani, kwa utumishi Mungu aliotuwekea chini yake katika kanisa lake.

Ikiwa tunalegea legea, au tunavipuuzia vya Mungu, au tunafanya mambo ya aibu, tusahau kule kupewa chochote na Mungu wetu ili tumiliki.

Tafakari tena habari hii..

Luka 19:12 “Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.

13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.

14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.

15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.

16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.

17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.

18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.

19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.

20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.

21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.

22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;

23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?

24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.

25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.

26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho”.

Hivyo tuwe waaminifu, mahali popote Mungu alipotuweka. Kwasababu hiyo ndio itakayofungua milango ya kuwepa vya kwetu wenyewe.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KUWA MWAMINIFU KWA MANENO YAKO MWENYEWE,

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

Rudi nyumbani

Print this post

LITURJIA NI NINI? NA JE IPO KIMAANDIKO?.

Liturjia/Litrujia ni mwongozo wa jinsi ya kufanya ibada unaotumiwa na makanisa mengi.

Ibada inaundwa na vitu vikuu vitano, ambavyo ni Maombi, Neno, Matoleo, Sifa, na Meza ya Bwana. Vitu hivi vitano ndivyo vinavyoiunda ibada.

Kwahiyo ukiwapo mwongozo wowote wa jinsi ya kuviendesha vitu hivi, na mwongozo huo ukawekwa kwenye kitabu maalumu..Mwongozo huo ndio unaojulikana na wengi kama Liturjia.

Kikawaida hakuna kanisa lisilo na mwongozo, na ni jambo la kimaandiko makanisa yawe na mwongizo fulani, ili mambo yote yafanyike kwa uzuri na utaratibu..

1 Wakorintho 14:40 “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu”.

Kanisa lisilo na utaratibu, ni rahisi kushambuliwa na shetani na kuvurugwa.

Lakini sasa mwongozo huu unatakiwa ufanyika kwa kipimo fulani, sio uzidi mipaka hata kuchukua nafasi ya Roho Mtakatifu.

Mwongozo wa kanisa unapovuka mipaka, hata kuchukua nafasi ya Roho Mtakatifu ndani ya kanisa, mwongozo huo unageuka na kuwa sumu ya kuliharibu kanisa kiroho.

Kwamfano, kanisa linapoweka ratiba ya masomo na mahubiri ya mwaka mzima, na kuyaweka kwenye kitabu maalumu..kwamba jumapili hii, litasomwa Neno kutoka kitabu fulani, jumatano ni kutoka kitabu fulani, sura namba fulani, na mstari namba fulani..Hivyo kunakuwa hakuna ruhusa ya kufundisha jambo lingine lolote nje na utararibu huo (Liturjia hiyo).

Mfumo kama huo (Liturjia/Litrujia) unamzuia Roho Mtakatifu, na kumzimisha asifanye kazi ndani ya kanisa, na hivyo kudhoofisha nguvu ya kanisa..

Kwasababu hata Roho Mtakatifu akitaka kusema jambo lingine jipya kupitia mhubiri huyo, tayari kuna mfumo unaolizuia hilo unaosema, fundisha tu kilichopo kwenye liturjia.

Roho mtakatifu akitaka kuwafungua watu kwa njia ya maombezi, kunakuwa tayari kuna mfumo uliowekwa unaolizuia hilo, mtu akitaka kutoa unabii upo mfumo tayari unaomzuia, ambao unasema ni kusoma Neno tu, Roho akishuka na kuwaongoza watu kunena kwa lugha na kufasiri, kunakuwa na mfumo unaozuia hilo n.k.

Na maandiko yanasema..tusimzimishe Roho..

1 Wathesalonike 5:19 “Msimzimishe Roho”.

Sasa mfumo kama huo (au Litrujia hiyo), ni mpango wa adui.

Makanisa mengi sasa, hususani yale yanayojulikana sana ndio yamemzimisha Roho Mtakatifu kwa sehemu kubwa sana kupitia hizo Liturjia. Unakuta Kanisa kwa nje linapendeza, lina vutia, linawashirika wengi, lakini ndani halina Roho Mtakatifu..bali miomgozo ya wanadamu, na kanuni za kibinadamu.

Roho Mtakatifu ndio uhai wa kanisa, mtu yeyote au kanisa lolote likikosa Roho Mtakatifu hilo sio kanisa la Mungu tena, bali la wanadamu (Warumi 8:9).

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba, Liturjia ni nini?.. ni mifumo ya wanadamu ya jinsi ya kufanya ibada, na katika zama hizi, Litrujia zote zimezidi kimo cha Kristo na hata kuchukua nafasi za Roho Mtakatifu.

Hivyo hatuna budi kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu na si Liturjia zetu zilizomzimisha Roho Mtakatifu.

Utaratibu bora ni ule wa kupanga muda wa ibada, siku za kukusanyika, utaratibu wa matoleo, ratiba za wakati wa maombi, na kujifunza biblia..(Na hata huo pia unaweza kugeuzwa kulingana na wakati na wakati, jinsi Roho atakavyo liongoza kanisa).

Na usiofaa ndio huo wa kupanga nini cha kufundisha cha mwaka mzima, na kukiweka kwenye kitabu… kamwe hatuwezi kumpangia Roho Mtakatifu nini cha kusema cha mwaka mzima, yeye anatoa ufunuo siku kwa siku, kwa jinsi atakavyo yeye..na sio sisi tumpangie cha kusema kupitia liturjia zetu, huo ni mpango wa adui wa kuliharibu kanisa.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

Nini maana ya kuabudu?

Rudi nyumbani

Print this post

Furaha ni nini?

Furaha kwa tafsiri ya kawaida, ni muhemko chanya wa kihisia unaotakana na aidha kuridhishwa na jambo fulani au kupata kitu fulani.

Kwa mfano katika biblia Wale mamajusi walipoina tena ile nyota  ya Bwana kule Bethelehemu, walifurahi.

Mathayo 2:10 “Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno”.

Utaona pia wale waliokwenda kaburini kwa Yesu,Na kukuta ameshafufuka, Biblia inasema walifurahi sana.

Mathayo 28:8 “Wakaondoka upesi kutoka kaburini, kwa hofu na furaha nyingi, wakaenda mbio kuwapasha wanafunzi wake habari”.

Hata mbinguni malaika wanapoona mtu mmoja ametubu dhambi, huwa wanafurahi pia.

Luka 15:10 “Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye”.

Kwahiyo utaona hapo furaha tunayoijua,  huwa inazaliwa kutokana  na kupatikana kwa kitu fulani kilichokuwa kinatarajiwa au jambo fulani.

Lakini furaha halisi ya ki-Mungu.  Ni furaha inayozidi mipaka, , hata katika shida furaha hii ipo. Ni furaha ambayo huwezi kuielezea kwa upatikanaji tu, kama furaha nyingine, inazidi mipaka hiyo.. Kwa kifupi ni kuwa haiathiriwi na hali au mazingira.

Na furaha yenyewe inaletwa na KRISTO YESU mwenyewe.

Ikiwa na maana mtu anayempokea Kristo, kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. Mungu anakuwa na jukumu la kumininia furaha hii kwa Roho Mtakatifu atakayempokea kipindi hicho.

Warumi 15:13 “Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu”.

1Nyakati 16:27 “Heshima na adhama ziko mbele zake; Nguvu na furaha zipo mahali pake”.

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.

Luka 2:10 “Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;

11 maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana”.

Yokobo 1:2 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;

3 mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”

1Petro 4:13 “Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe”.

Kwa muda wako pitia vifungu hivi

1Petro 1:8, Yohana 17:13

Na wewe ikiwa ni mmojawapo wa wale wanaotaka kuonja FURAHA hii ya Ki-Mungu ambayo si watu wote wanaweza kuonjeshwa utakuwa umefanya uamuzi wa busara sana. Kwasababu ni kwake tu peke yake ndipo Furaha inapopatikana, hakuna mwingine, Bwana anasema hivi;

Zaburi 5: 11 “Nao wote wanaokukimbilia watafurahi; Watapiga daima kelele za furaha. Kwa kuwa Wewe unawahifadhi, Walipendao jina lako watakufurahia”.

Zaburi 51:12 “Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi.

Unaona? Basi fungua leo moyo wako, Kristo aingie ndani yako, kukusamehe, na kukuwekea furaha idumuyo. Ikiwa Upo tayari leo kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.

Bwana akubariki.

Wafilipi 4:4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

Unyenyekevu ni nini?

Gombo ni nini?

Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

SWALI: Naomba kufahamu maana ya mstari  huu”

Mithali 29:25 “Kuwaogopa wanadamu huleta mtego, ..”
Ni mitego gani hiyo hukupata iwapo utamwogopa mwanadamu?..


JIBU: Ukiendelea kusoma inasema..
Mithali 29:25
[25]Kuwaogopa wanadamu huleta mtego;
Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.
Hofu ya kwamba mwanadamu atakuonaje, ukitenda jambo fulani la haki..hofu ya mwanadamu atakuchukuliaje siku ukivaa mavazi ya kujisitiri ,hofu ya wazazi,  watakupokeaje pale unapoamua kuokoka..n.k kwa kawaida hofu kama hizi za kuwapendeza wanadamu mwisho wa siku huwa zinakupeleka katika mtego wa kupotea..
Kwamfano..
Sauli aliupoteza ufalme wake kwa kuwaogopa watu na kumwacha Agagi hai. 1Samweli 15:25
Haruni alikuwa katika hatihati ya kuuliwa na Mungu kwa kosa la kuwapendeza wana wa Israeli pale walipomwomba awatengenezee ndama wa dhahabu wamwabudu.
Kutoka 32:22-24
Herode alimwua Yohana mbatizaji kwa kumpendeza mke wake na binti wake Marko 6:21-27..
Herode mwingine naye alimuua Yakobo mtume wa Bwana..pamoja na kumfunga Petro kwa lengo tu la kuwapendeza wayahudi.Matendo 12:1-4
Umeona wote hawa waliishia katika mitego mibaya kwa hofu za wanadamu…
Lakini kinyume chake ni kuwa wanaomtumaini Mungu watakuwa salama.
Shedraka, Meshaki na Abednego walikaidi amri ya mfalme na kumtii Mungu japokuwa walitupwa katika tanuru la moto lakini walitoka salama..
Danieli kwa hofu ya Mungu alikuwa tayari kutupwa katika tundu simba lakini Mungu alitomtoa salama huko nako..
Bwana Yesu alisema  …
Yohana 5:44
[44]Mwawezaje kuamini ninyi mnaopokeana utukufu ninyi kwa ninyi, na utukufu ule utokao kwa Mungu aliye wa pekee hamwutafuti?
Na sisi ili tuwe salama tuutafute utukufu unaotoka kwa Mungu..tukubali njia Kristo aliyoichagua  hata kama dunia nzima itatutenga..na njia yenyewe ni ile ya wokovu na kujikana nafsi.
HivyoTubu dhambi zako ikiwa wewe ni mwenye dhambi. Yesu yupo mlangoni kurudi. Unyakuo ni wakati wowote, kwasababu tunaishi katika kizazi kilichoshuhudia kutimia kwa dalili zote za kurudi kwake mara ya pili.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.

Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)

SIKU YA HOFU YANGU NITAKUTUMAINI WEWE.

AOGOPACHO MTU ASIYE HAKI NDICHO KITAKACHOMJILIA.

Waoga ambao hawataurithi uzima wa milele ni watu wa namna gani?(Ufunuo 21:8).

Rudi nyumbani

Print this post

Gombo ni nini?

Gombo ni aina ya vitabu vilivyo katika mfumo wa kuviringishwa, kwa lugha ya kiingereza “Scrolls” (tazama picha juu).

Aina ya vitabu hivi vilitumika sana katika enzi za zamani na vilikuwa mara nyingi ni vya ngozi.

Lakini katika zama zetu hizi za sasa, hatuvitumii tena kutokana na kuongezeka kwa maarifa.

Vitabu tunavyotumia sasa, vinatengenezwa kwa karatasi, na vinakuwa na kurasa..Lakini Gombo hazikuwa na kurasa, bali ni ngozi uliyokuwa na maandishi na kuviringishwa.

Mfano wa Gombo ni lile tunalolisoma katika kitabu cha Ezekieli na Ufunuo.

Katika kitabu cha Ufunuo, tunasoma Bwana Yesu akikipokea kile kitabu chenye mihuri saba. Sasa kitabu hicho hakikuwa kama vitabu vyetu hivi vyenye kurasa la!..bali kilikuwa ni gombo, yaani kitabu kilichoviringishwa, na vitabu hivi vya kuviringishwa ndivyo vilivyokuwa vinafungwa kwa mihuri.. vilikuwa vinafungwa kama vile shati linavyofungwa kwa vifungo vyake, (tazama picha chini).

Mfumo wa kuviringishwa

Kwahivyo popote katika biblia panapotajwa neno kitabu, palimaanisha aina hiyo ya vitabu (yaani Gombo)..na haikumaanisha aina ya vitabu tulivyo navyo sisi.

Unaweza kulipata neno hilo Gombo katika biblia, kupitia mistari ifuatayo. Zaburi 40:7, Yeremia 36:2-6, Ezekieli 2:9, Ezekieli 3:3, Zekaria 5:1-2, na Waebrania 10:7.

Kwa msingi huo wa kuelewa nini maana ya Gombo, utatusaidia kuelewa vizuri juu ya juu ya MIHURI SABA ya kitabu cha ufunuo.
Kama utapenda kujua juu ya ufunuo wa Mihuri saba unaweza kufungua hapa >> Mihuri saba

Je umempokea Yesu?, je Umebatizwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu?, Je umepokea Roho Mtakatifu a unaishi maisha matakatifu ya kumpendeza Mungu?.

Kumbuka Bwana yupo mlangoni, na unyakuo wa kanisa ni siku yoyote.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Biblia ina vitabu vingapi?

Tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu ni ipi?

Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?

USIPUNGUZE MAOMBI.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Rudi nyumbani

Print this post

Je ushabiki wa mpira ni dhambi?

Je! Kucheza mpira au kushabikia mpira ni dhambi kulingana na maandiko?.


Bwana kutuumba miili yetu hii ili kuishughulisha, hajatuumbia ikae tu bila kujishughulisha..Na njia mojawapo ya kuishughulisha ni kwa kufanya mazoezi.

Na mazoezi hayo yanaweza kufanyika kwa njia ya kawaida au ya kucheza..Kwamfano watu wawili marafiki wanaweza kusimama na kushindana mbio, na mwisho wa mbio wakafurahi na kucheka, hatimaye wakawa wamecheza na hapo hapo kufanya mazoezi.
Sasa kucheza kwa namna hiyo sio dhambi lakini tatizo linakuja mfumo unaochanganyikana na mchezo huo.

Kwamfano mchezo unapohusisha kuvaa kuilimwengu, au matusi, au miziki ya kiulimwengu, au mambo yoyote yasiyo na adabu mchezo huo ni dhambi, na sisi wakristo hatupaswi kuushiriko.

Kwamfano riadha za siku hizi ili wanawake au wanaume washiriki, hawana budi kubaki na nguo za ndani tu!..na sehemu nyingine yote ya mwili kubaki wazi.

Utakuta wanawake wanakimbia riadha wakiwa na chupi tu, na wanaume hivyo hivyo. Sasa michezo ya namna hiyo ni dhambi kushiriki kwa mkristo.

Na kama ni dhambi, basi na hata kuishabikia vile vile ni dhambi.

Kadhalika watu wawili wanaweza kitengeneza mpira wao na kisha kuipiga piga kwa miguu yao kujifurahisha..jambo hilo sio dhambi.

Lakini inapotokea mchezo huo unachanganyikana na mfumo fulani wa kishetani, tayari mchezo huo unakuwa ni najisi kwakristo, kwamfano utakuta mchezo fulani unadhaminiwa na shirika la pombe au la sigara, au la kubeti kiasi kwamba hata sare za mchezo huo ni nembo la mashirika hayo najisi.

Au utakuta michezo mingine ni lazima ihusishe miziki ya kidunia ambayo ni najisi kwa mkristo.

Hapo hatupaswi sisi kama wakristo kushiriki michezo hiyo, wala kuwa wafuasi wa hiyo michezo.

Hivyo kwaasili michezo sio mibaya,
Hata Yakobo alicheza Mieleka na yule Malaika..

Lakini mieleka ya leo ni lazima ubakiwe na nguo za ndani tu!..Na tena siku hizi ni jinsia mbili tofauti zinapigana mieleka, kiasi kwamba huwezi kutazama mara mbili michezo hiyo imejaa matusi na ushetani.

Imefungamana na ushetani kiasi kwamba kitendo cha kuangalia tu tayari umenajisika..

Na siku zinavyozidi kwenda hiyo mifumo inazidi kuongezwa juu ya hiyo michezo na kuharibu kabisa maana ya michezo.

Huko mbeleni, riadha zitakuwa zinafanyika uchi wa mnyama kabisa, tofauti na leo ambapo ni nguo za ndani tu ndio zina sitiri.
Kama tunataka kucheza (sisi kama wakristo), tunaweza kucheza sisi kwasisi bila kutumia mifumo hiyo ya kishetani.

Lakini pia biblia imetuonya kuwa na kiasi, maana yake sio kucheza mpaka unakuwa unafanana na watu wa kidunia.

Vile vile mambo yote tunapaswa kuyafanya kwa utukufu wa Mungu. Ukicheza na mtoto wako inaweza ikatosha, ukicheza na kaka yako inatosha, ukicheza na rafiki zako wawili au watatu inatosha, sio lazima tujichangange na harambee za watu wengi wa kiulimwengu, kushiriki nao michezo iliyojaa unajisi na mizaha.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; KWA MALAIKA NA WANADAMU.

Kucheza karata ni sahihi kwa Mtu aliye MKRITO?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

JE! KUBET NI DHAMBI?

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Rudi nyumbani

Print this post

MAOMBI YA KUFUNGULIWA KIUCHUMI.

Kabla ya kwenda katika maombi Awali ya yote ni vizuri ukafahamu kuwa mafanikio ya kiuchumi yanaweza kuletwa na vitu vikuu vitatu

  1. Mwanadamu mwenyewe.
  2. Shetani.
  3. Mungu.

Na kila mmoja anayo kanuni yake ya kuyafikia hayo mafanikio.

Kwamfano kwa mwanadamu, ili aweze kujikomboa kiuchumi, kanuni ni moja nayo ni “kuwa na bidii katika kufanya kazi”..haijalishi kazi hiyo itakuwa ni ya kuuza pipi, maadamu unatia bidii ndani yake, utafanikiwa kwasababu  katika bidii hiyo, huko huko ndio unazalika ubunifu  na mikakati, ya kupiga hatua, na kuwekeza,n.k. na mwisho wa siku utafanikiwa, Hata kama hatofikia utajiri ule, lakini mwisho wa siku utajikomboa kiuchumi, haijalishi atafanya hivyo kwa muda gani. Na hapo atakuwa tayari kashajikomboa kiuchumi.

Lakini kanuni za ibilisi ni tofauti na zile za kibinadamu. Pengine kwake si lazima ujishughulishe sana, lakini akakupa mafanikio tu, Kwasababu ndicho alichojaribu kufanya kwa Bwana Yesu, kwa kumwambia  tu amsujudie ndipo atakapompa mali zote.

Mathayo 4:9 “akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.”

Unapokwenda kwa waganga watakupa mafanikio, lakini wakiwa na masharti yao kwamba ni lazima ufanye kitu fulani kwa shetani n.k..

Lakini tunaporudi kwa Mungu, napo pia kuna kanuni zake, za kufanikiwa. Ukienda nje ya hizo, na huku unahitaji mafanikio, au kukombolewa kiuchumi usijidanganye, unapoteza muda. Nenda tu kajibidiishe huko kama wanadamu wengine, utafanikiwa pia kwa njia hizo.

Lakini Kanuni za Mungu za kumkomboa mtu kiuchumi  ni zipi?;

Kabla ya kuombewa ni lazima uwe mwana wake. Na mtu anakuwa mwana wake kwa kutubu dhambi zake zote, na kubatizwa, kisha kupokea Roho Mtakatifu. Na baada ya hapo kuanzia huo wakati na kuendelea kuishi maisha yampendezayo Mungu.

Biblia inasema..

Mathayo 6:31 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”.

Unaona? Ukishautafuta kwanza ufalme wake na haki yake, kuanzia huo wakati unakuwa tayari sasa, kushiriki Baraka zote kutoka kwa Mungu, kiwepesi  pale unapomwomba.

Neno la Mungu linasema hivi..

2Wakorintho 8:9 “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”.

Na pia Yesu mwenyewe alisema..

Mathayo 19:28 “Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele.

30 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza”.

Hivyo kabla ya kwenda kukuombea Baraka zako kutoka kwa Mungu.. ni sharti kwanza uwe  tayari leo kumkabidhi Bwana Yesu maisha yako, kwa kumaanisha kabisa. Kama upo tayari basi hapo ulipo tafuta sehemu yenye utulivu, kisha piga magoti, kisha sema sala hii kwa imani, kwa kumaanisha kabisa, na Mungu atakuokoa siku ya leo.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa kwa sala hiyo fupi, amini kuwa Bwana Yesu ameshakusamehe, Na kuanzia sasa unakuwa tayari kushiriki, Baraka zote kutoka kwa Mungu.

Yeye mwenyewe alisema maneno haya;

Kumbukumbu: MLANGO 28

1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.

3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.

5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.

6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.

7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

8 Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako.

9 Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya Bwana, Mungu wako, na kutembea katika njia zake.

10 Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako.

11 Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako, katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako kwamba atakupa.

12 Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.

13 Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;

14 msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lo lote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia.

Baraka hizo zote, zitakufuata endapo utadumu tu katika WOKOVU.

Basi sasa, nitakuombea, ili milango hii ifunguke, katika maisha yako. Hapo ulipo Piga tena magoti, niombe kwa ajili yako. Fuatisha kwa sauti sala hii;

Baba Mwenyezi, Mungu wa milele, ahsante kwa kutupa zawadi ya kutuletea mkombozi duniani, Bwana wetu Yesu Kristo. Asante kwa kuwa alikuja kutukomboa kutoka katika dhambi zetu na laana zetu. Lakini hakuishia hapo tu, bali alitukomboa, mpaka na UCHUMI wetu.

Nami leo hii nimempokea na kumkiri kwa kumaanisha kabisa kumfuata tangu sasa hadi milele. Naomba Mungu wako zile Baraka zote ulizoziahidi katika Kumbukumbu la Torati 28:1-14, zinijilie juu yangu. Nami nikawe Baraka kwa jamii na kwa kanisa lako. Kuanzia sasa ikiwa kuna kazi zozote za ibilisi zilizotangulia nyuma yangu kunizuilia Baraka zangu, ninazikataa kwa jina la Yesu Kristo. Naiita Damu ya Yesu ikasafishe kapu langu, na mfuko wangu.

Asante Mungu wangu kwa kunikomboa.

Amen.

Basi, ikiwa umeyafuatilisha maombi hayo, ujue kuanzia sasa, Mungu atatembea na wewe katika uchumi wako, kwa kile unachokifanya, tenda mapenzi ya Mungu, utaona akikupigania. Lakini kumbuka Kama tulivyotangulia kusema, inahitaji Kutembea na Mungu ili akukamilishie ahadi hizo, sio tu kukiri kwa mdogo, unakwenda kuendelea na mambo yako..nikuambie ukweli tu, inahitaji maisha.

Mungu akubariki sana.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi wa kumjua Mungu, au ubatizo, au unaswali lolote kuhusu biblia,  basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi Simu/Whatsapp: +255693036618 /  +255789001312

Mada Nyinginezo:

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

TWEKA MPAKA VILINDINI.

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

  1. MISTARI YA WAZAZI/WALEZI KUHUSU WATOTO.

Haya Mafungu ya biblia ambayo wazazi/walezi wanapaswa wayajue kuhusu watoto wao.

Zaburi 8:2a “Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu;..”

Mungu anaonyesha kuwa kupitia watoto wachanga, ambao unaweza kuwadharau hawajui kitu, hapo ndipo Mungu ameweka nguvu zake. Hivyo anza kumlea mtoto katika misingi ya kumcha Mungu tangu akiwa mdogo, kwasababu hapo ndipo Mungu anapoketi.

 Na ndio maana biblia inasema..

Mithali 22:6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

Tabia ya kudharau watoto, au kuona kama umri wao wa kumjua Mungu bado, Yesu aliukemea sana, tunalithibitisha hilo katika..

Marko 10:13 “Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.

14 Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.

15 Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.

16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.

Biblia inasema pia..

Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu”.

Biblia bado inasisitiza wazazi, wasiwaudhi watoto wao, kwasababu zisizo na msingi, kisa tu wao ni watoto,

Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.

Kwasababu malaika wao mbinguni wanawatazama uwatendeapo mabaya..

Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”.

Zaidi pia Bwana Yesu anataka wazazi/walezi wajifunze kupitia watoto walionao, hivyo kwa kupitia wao tutapata kujua siri kubwa za ufalme wa mbinguni.

Mathayo 18 : 1-5

“1 Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,

2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,

3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.

5 Na ye yote atakayempokea mtoto mmoja mfano wa huyu kwa jina langu, anipokea mimi;”

Lakini bado Mungu anasisitiza juu ya kuwarekebisha watoto, kwamba ni jukumu la kila mzazi/mlezi kumwadhibu mtoto wake, pale anapokosea . Hilo ni agizo la Mungu. Usipomwajibisha mtoto wako, Mungu atakuwajibisha wewe siku ile, kwa kutomtengeneza mwanao.

Mithali 22:15 “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali”.

Mithali 23: 13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

2) WAJIBU WA MTOTO.

Vilevile mzazi, unapaswa umfundishe mwanao wajibu wake kama mtoto, Sawasawa na Neno la Mungu linavyosema,

Na mojawapo ni kuwafundisha kukutii wewe.

Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,

3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.

Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.

Pia umfundishe kujua wajibu wake wa kumtafuta Mungu tangu akiwa mdogo..kwasababu kwa Mungu hakuna utoto.

Yeremia 1:6 “Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.

7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru”.

Na mwisho Mkumbushe pia hata watoto watahukumiwa, na  kuzimu wapo watoto ambao hawakuwajibika katika kuwatii wazazi wao, na kumcha Mungu.

Ufunuo 20:12 “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao”.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Unyenyekevu ni nini?

Biblia inasema nini kuhusu unyenyekevu?

Unyenyekevu ni ile hali ya “kujishusha” na kuwa tayari “kutumika kwa utumishi ule usiostahili kutumika” bila kiburi wala majivuno.

Biblia inasema Mungu huwapinga wote wenye kiburi na wajikuzao lakini “wanyenyekevu” anawapa Neema.

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, MUNGU HUWAPINGA WAJIKUZAO, bali huwapa neema wanyenyekevu”.

1Petro 5:5 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI, LAKINI HUWAPA WANYENYEKEVU NEEMA”.

Na tena kitabu cha Mithali kinasema…

Mithali 3:33 “Laana ya Bwana i katika nyumba ya waovu, Bali huibariki maskani ya mwenye haki.

34 Hakika yake huwadharau wenye dharau, Bali huwapa wanyenyekevu neema.”

Na zaidi ya yote, Injili ya Bwana Yesu ni kwa wote walio wanyenyekevu..

Isaya 61:1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta NIWAHUBIRI WANYENYEKEVU HABARI NJEMA; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao”.

Maana yake ni kwamba “watu wajikwezao” na “wenye kiburi”.. Hawawezi kuipokea Habari njema ya Yesu, Neema ya Wokovu inakuwa haipo juu yao.

Na pia Bwana Yesu alitufundisha ni kwa namna gani tutakuwa wa kwanza, katika ufalme wa Mbinguni.. alisema tukitaka kuwa wa kwanza, basi hatuna budi kujinyenyekeza na kuwa wadogo kuliko wote, maana yake tuwe watumwa na watumishi kwa wengine.. tofauti na hekima ya dunia inavyosema au kufundisha kuwa mtu mkubwa ni Yule anayetumikiwa na mwenye kiburi.

Marko 10.42 “Yesu akawaita, akawaambia, Mwajua ya kuwa wale wanaohesabiwa kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.

43 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu,

44 na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote.

45 Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.

Hivyo biblia inatufundisha kuwa wanyenyekevu siku zote, yaani kuwa “wadogo”, sehemu nyingine Bwana Yesu anasema tunapaswa tujinyenyekeze na kuwa kama vitoto.

Mathayo 18:3 “akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

4 Basi, YE YOTE AJINYENYEKESHAYE mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni”.

Unaweza kusoma pia, Mathayo 11:11, Waefeso 5:21, Zaburi 138:6, Mithali 11:2, na Mithali 18:12.

Hivyo na sisi hatuna budi kuwa wanyenyekevu siku zote, ili tukwezwe na tupate NEEMA zaidi, na sio tu kuwa wanyenyekevu kwa Mungu, bali pia kwa watu wengine wote, ikiwemo wazazi, wafanyakazi wenzetu na maboss zetu na kwa wenye mamlaka pia (Tito3:1).

Lakini tukiwa ni watu wa kiburi, au tukijiinua basi tutashushwa chini kama maandiko yanavyosema..

Luka 14:11 “Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Neema ni nini?

SALA YA ASUBUHI

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post