Category Archive Home

USINIPITE MWOKOZI Lyrics

Usinipite mwokozi Lyrics| Swahili, – “Pass me not, O Gentle Savior”


Historia ya nyimbo Usinipite mwokozi.


Wimbo huu uliandikwa mwaka 1868, na mwanamke wa kimarekani aliyeitwa Fanny Crosby. Mwanamke huyu mkristo alizaliwa akiwa mzima lakini wiki 8 baada ya kuzaliwa kwake alipatwa na opofu, ambao ulidumu mpaka kufa kwake, lakini katika maisha yake yote aliyoishi hapa duniani  (yaani miaka 94), haikuwa bure kwa Mungu wake, alifanikiwa kuandika  nyimbo zaidi ya 8,000..Hivyo hiyo ikamfanya apate umaarufu na kumfanya ajulikane kwa jina la “mtunzi-kipofu-wa-nyimbo-za-tenzi”, na  “Malkia wa nyimbo za Injili”.

Lakini siku moja alipokuwa amealikwa kwenda kuzungumza na wafungwa wa mji,  na alipokuwa akitembea kule gerezani alimsikia mfungwa mmoja akisema “Bwana mwema usinipite, usinigeuzie mgongo wako,unikumbuke”,

Fanny anasema aliguswa sana na maneno yale, jambo ambalo halikuondoka kwenye kichwa chake mpaka alipofika nyumbani. Na huko ndipo alipoandika beti zote nne za wimbo ujulikanao kama USINIPITE MWOKOZI.

Alipomaliza kuuandika akampa muhusika wa kuweka midundo, na mwaka, 1870 wimbo huo, ulizinduliwa rasmi katika machapisho..

Na kwa kipindi kifupi` sana ukapata umaarufu mkubwa  duniani kote.

*****

Usinipite wokozi,
Unisikie;
Unapozuru wengine,
Unisikie.
 
Yesu, Yesu, Unisikie;
Unapozuru wengine,
Usinipite,
 
Kiti chako cha rehema,
Nakitazama;
Magoti napiga pale,
Nisamehewe.
 
Yesu, Yesu, Unisikie;
Unapozuru wengine,
Usinipite.
 
Sina ya kutegemea,
Ila wewe tu;
Uso wako, uwe kwangu,
Nakuabudu.
 
Yesu, Yesu, Unisikie;
Unapozuru wengine,
Ila wewe tu,
Usinipite.
 
U Mfariji Peke yako;
Sina mbinguni,
Wala Duniani pote,
Bwana mwingine.
 
Yesu, Yesu, Unisikie;
Unapozuru wengine,
Usinipite.

*****

Jambo hili tunaliona kwa wale kipofu wawili waliomsikia Yesu anapita..

Mathayo 9:27 “Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, UTUREHEMU, MWANA WA DAUDI.

28 Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana. 29 Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate”.

Na itakuwa hivyo na kwako:

Ikiwa wewe umeokoka, na unaona unapita katika hali ngumu, ambayo unaona kwa namna ya kawaida huwezi kutoka, basi wakumbuke watu kama hawa, wakutie nguvu,..Zidi kumwita Yesu, atakuonekania kwa wakati wake. Kwasababu yeye anatupenda na kutujali, na yote yanawezekana kwake.

Lakini kama hujaokoka, basi ni vizuri leo ukamwita kwanza mwokozi akuokoe maisha yako, usiruhusu akupite, anapokwenda kuwapa wengine uzima wa milele, sema na mimi leo nauhitaji huo uzima, hivyo kama upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa, kwa ajili ya Sala ya Toba..>>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki..

Tazama historia ya nyimbo nyingine za Tenzi chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAMBA WENYE IMARA

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

TENZI ZA ROHONI

Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?

MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

Ni salama rohoni mwangu lyrics- It is well with my soul.


Nyimbo hii ilitungwa na mwanasheria mmoja mkristo aliyeitwa Horatio Spafford, alitunga wimbo huu kutokana na mambo mazito aliyoyapitia katika maisha yake, Matatizo yake yalianza kwa kufiwa na mtoto wake wa pekee wa kiume aliyekuwa na miaka minne, hiyo ilikuwa ni mwaka 1870

Muda mfupi baadaye (mwaka 1871) moto mkubwa uliozuka huko Chicago Marekani mjini kwake, ukaharibu mali zake nyingi ukizingatia alikuwa ni mwanasheria aliyekuwa amefanikiwa sana. Hilo likafuatana na biashara zake pia kuporomoka kutokana na anguko la uchumi lililotokea mwaka 1873, Hivyo ikambidi apange safari ya kwenda Ulaya pamoja na familia yake, Lakini aliahirisha safari kwa ajili ya kuweka mambo yake ya vibiashara vizuri yaliyokuwa yameathiriwa na moto, hivyo ikambidi msafirishe kwanz mkewe na mabinti zake wanne,akiahidi kuwa atawafuta baadaye.

Lakini Meli ilipokuwa inakatisha bahari ya atlantiki, ilizama ghafla kwa kugongana na meli nyingine na mabinti zake wote wanne wakafariki kwenye ajali hiyo akasalimika mke wake tu, akiwa kule Marekani alipokea ujumbe wa telegrafu kutoka kwa mke wake unaosema “Nimepona peke yangu” ndipo Spafford akaondoka kumfuata mkewe, na huko huko akauandika wimbo huu..

https://www.high-endrolex.com/15

Baadaye vina vingine vya mashairi viliongezwa ndipo ukazaliwa wimbo huu, Ni salama Rohoni Mwangu.

****

Nionapo amani kama shwari,

Ama nionapo shida;

Kwa mambo yote umenijulisha,

Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,

Rohoni, Rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

Ingawa Shetani atanitesa,

Nitajipa moyo kwani;

Kristo ameona unyonge wangu,

Amekufa kwa roho yangu.

Salama, Salama,

Rohoni, Rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

Dhambi zangu zote, wala si nusu,

Zimewekwa Msalabani;

Wala sichukui laana yake,

Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,

Rohoni, Rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

Ee Bwana himiza siku ya kuja,

Panda itakapolia;

Utakaposhuka sitaogopa,

Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,

Rohoni, Rohoni,

Ni salama rohoni mwangu.

****

Hata sisi Je! Tunapopitia shida na magumu tunazo nguvu za kusema ni salama rohoni mwangu?, Tunapopitia njaa, tunapopitia misiba, tunapopitia matatizo mazito Je! Bado Tunaweza kumwambia shetani ni Salama rohoni mwangu? Kama ilivyokuwa kwa Ayubu?

Siku zote kumbuka hili Neno..

Mithali 24: 10 Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache.

Hivyo jipe moyo songa mbele ikiwa wewe ni mkristo, Kwasababu mwisho wa Mungu sikuzote ni mzuri, kama ilivyokuwa kwa Yusufu, kama ilivyokuwa kwa Ayubu, na ndivyo itakavyokuwa na kwako.

Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma”.

Shalom.

Tazama chini historia ya nyimbo nyingine za Tenzi:

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Kwa maombezi/ubatizo/ Kumpokea Yesu. Wasiliana nasi kwa namba hizi; +255789001312/+255693036618

Mada Nyinginezo:

MWAMBA WENYE IMARA

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

TENZI ZA ROHONI

YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.

YESU AKALIA KWA SAUTI KUU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?

SWALI: Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, Je! Ina maana hakuwa na wana wengine au hana wana wengine zaidi yake?


JIBU: Tusome..

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Hivyo ndivyo inavyotafsiriwa na watu wengi na madhehebu mengi ya dini..Lakini sivyo inavyomaanisha hapo, Mungu kumwita Yesu mwanawe pekee, haimaanishi, hajawahi kuwa na wana wengine,(ambao ndio sisi), bali alimaanisha Yesu ni mwana-wake-wa-kipekee tofauti na sisi wengine aliyebakiwa naye, mwenye mahusiano ya kitofauti na wengine, mwana wa maagano ndio maana akimwita Kristo  mwanawe pekee.

Ili kulithibitisha jambo hilo embu tutazame baadhi ya vifungu vya maandiko vinavyoelezea habari inayofanana na hiyo, Na hiyo si nyingine zaidi ya ile ya Ibrahimu na mwanawe Isaka..tusome.

Mwanzo 22:2 “Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia”.

Soma tena..

Mwanzo 22:12 “Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee”.

Soma tena…

Waebrania 11:17 “Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee”;

Unaona ukisoma mistari hiyo yote, unaweza kudhani Isaka ndio aliyekuwa mwana  tu wa Ibrahimu hakuwa na wengine, lakini tunajua kuwa kabla ya Isaka alikuwepo Ishmaeli. Na baada ya Isaka walikuja wengine wengi (Mwanzo 25:1-4).

Lakini ni kwanini Mungu amwite Isaka kama mwana pekee wa Ibrahimu, ni kwasababu alikuwa mwana wa maagano, mwana wa ahadi, tofauti na wale wengine,…Isaka alifananishwa na Kristo

Hivyo Kristo Bwana wetu ndio mwana pekee wa Mungu, ambaye ameshikilia maagano yetu yote, kwa kupitia yeye, Mungu ametupenda tena, kwa kupitia yeye sisi tumebarikiwa, na kwa kupitia yeye, tunapata uzima wa milele, na tumaini la ufufuo baada ya kifo.  Hivyo tukimwamini na kumpokea tunaingia katika huo mnyororo wa Pendo la Mungu.

“Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye”. Kama hujampokea huu ni wakati wako sasa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

  Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABİSA lyrics ~Swahili  (How Great Thou Art).


Toleo la kwanza kabisa la Wimbo huu liliandikwa na mtu mmoja raia wa Sweden, aliyeitwa Carl Boberg wimbo huu aliuandika mnamo mwaka 1885 baada ya kuvutiwa na mazingira aliyopishana nayo alipokuwa akitoka Kanisani yeye na marafiki zake. Anasema muda wa mchana walipokuwa njia hali ya hewa iliwabadilikia ghafla, wakaona wingu la tufani likitokea kwa mbali, na mara hiyo hiyo kukaanza kumulika mianga mingi kama ya radi angani, upepo mzuri ukaanza kuvuma juu ya mashamba yaliyokuwa pembeni, Na kisha manyunyu ya mvua matulivu  yakaanza kudondoka juu yao, na baada ya muda kidogo, wingu lile la tufani likapotea, muda huo huo ukatokea upinde mzuri wa mvua angani..

Na alipofika nyumbani na kufungua madirisha atazame nje, aliona ufukwe ya mji wake kama vile kioo, akatazama upande wa pili akasikia ndege wazuri wakitoa milio yao na kwa mbali kegele za kanisa zikilia, Hapo ndipo wimbo huu ulipomjia kichwani kuutunga na kuuandika.

****

Bwana Mungu nashangaa kabisa,

Nikifikiri jinsi ulivyo,

Nyota, ngurumo, vitu vyote pia,

Viumbavyo kwa uwezo wako.

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu,

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu.

Nikitembea pote duniani,

Ndege huimba nawasikia,

Milima hupendeza macho sana,

Upepo nao nafurahia.

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu,

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu.

Nikikumbuka vile wewe Mungu,

Ulivyompeleka mwanao,

Afe azichukue dhambi zetu,

Kuyatambua ni vigumu mno.

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu,

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu.

Yesu Mwokozi atakaporudi,

Kunichukua kwenda mbinguni,

Nitaimba sifa zako milele,

Wote wajue jinsi ulivyo.

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu,

Roho yangu na ikuimbie,

Jinsi wewe ulivyo mkuu.

*****

Tujiulize na sisi tunao utaratibu kwa kukaa chini na kuushangaa utukufu wa Mungu na kumtukuza?..Au kila kitu tunaona ni kawaida tu..Kumbuka Sifa kamili kama hizi mbele za Mungu ni bora kuliko dua na sala tunazompelekea kila siku.

Mungu anataka kuona, na sisi tukiufurahia uumbaji wake, kwa kumwimbia.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia kwa  email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

MWAMBA WENYE IMARA

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

CHA KUTUMAINI SINA, Swahili Lyrics. (My hope is built on nothing less)


Tenzi hii iliandikwa na mchungaji wa kanisa la kipatisti, aliyeitwa Edward Mote, raia wa nchi ya uingereza, mnamo mwaka 1834, Edward Mote alifanikiwa pia kuandika tenzi nyingine nyingi Zaidi ya 100, lakini iliyopata umaarufu mkubwa ni hii ijulikanayo kama “Cha Kutumaini sina”.

Tenzi hii aliibuni akirejea ule mfano alioutoa Bwana Yesu wa mjenzi mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba imara, Na yule mpumbavu ambaye aliijenga nyumba yake https://www.high-endrolex.com/2juu ya mchanga (Mathayo 7:24-27), Na kuonyesha ni jinsi gani mtu anapaswa aishi kwa kwa kumtegemea Kristo aliye mwamba salama, na ulio imara.

1Wakorintho 10:4  “wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo”

Na ndio hapo akaundika wimbo huu;

Cha kutumaini sina
Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha
Dhambi zangu kuziosha;

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba; ni salama
Ndiye mwamba ni salama

 

Njia yangu iwe ndefu
Yeye hunipa wokovu;
Mawimbi yakinipiga
Nguvu zake ndiyo nanga.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba; ni salama
Ndiye mwamba ni salama

Damu yake na sadaka
Nategemea daima,
Yote chini yakiisha,
Mwokozi atanitosha.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba; ni salama
Ndiye mwamba ni salama

Nikiitwa hukumuni,
Rohoni nina amani;
Nikivikwa haki yake
Sina hofu mbele zake.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba; ni salama
Ndiye mwamba ni salama

*****

Amen hata mimi na wewe, tukiwa ndani ya Kristo, tupo salama wakati wote, lakini tukimkosa yeye ndani yetu, basi hata kuimba kwetu ni bure, tutakuwa tu sawa na yule mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga..

Hivyo ukiwa unahitaji kuokoka ili Yesu leo awe kweli Mwamba ulio salama, basi fungua hapa kwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAMBA WENYE IMARA

MWAMBA WETU.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/2-swali-kwanini-mtu-atoe-pepo-aombee-wagonjwa-wapone-asikie-sauti-ya-mungu-ikimwambia-hiki-na-kile-kuhusu-watu-na-yeye-mwenyewe-kufunua-siri-za-mioyo-yao-aone-maono-na-kutembea-na-malaika-katika/

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?

Shalom karibu tujifunze biblia.

Mojawapo wa uhuru Mungu aliompa mwanadamu ni kuoa/kuolewa…Mtu yeyote anayeoa/kuolewa sawasawa na maagizo ya Mungu (yaani ndoa ya mume mmoja na mke mmoja) basi anabarikiwa.

Mathayo 19:4 “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?”.

Lakini Pamoja na hayo sio lazima pia kuoa au kuolewa kwa sababu maalumu.

Kwamfano biblia inasema katika..

1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. YEYE ASIYEOA hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.

34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. YEYE ASIYEOLEWA HUJISHUGHULISHA NA MAMBO YA BWANA, APATE KUWA MTAKATIFU MWILI NA ROHO. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe”.

Hivyo sababu kuu ya mtu kujizuia kuoa au kuolewa ni ili apate nafasi kubwa ya kujishughulisha na kazi ya Mungu.. Ni kweli Mume au Mke ni msaidizi mzuri pia katika kazi ya Mungu lakini…kuwa kumtumikia Mungu binafsi pia ni vizuri Zaidi.. Kwasababu ukiwa na mke/mume kuna mambo ya kidunia ambayo hautayakwepa…kwamfano vitakuwepo vipindi vya kutunza Watoto, vitakuwepo vipindi vya kutafuta sana vya kidunia ili kuitunza familia na mke au mume. Vitakuwepo vipindi vya kukaa pamoja faragha!..

Huwezi kusema unasafiri miezi 5 mbali na mke/mume wako umeenda kufanya huduma…ni lazima kwa sehemu Fulani utamkwaza tu mwenzako! au utakuwa hujamtendea haki. Na biblia inasema ukishaoa/ukishaolewa..mwili wako ni mali ya mwenzako, huna amri juu ya mwili wako(kasome 1Wakorintho 7:3-5)..Sasa hayo ndio baadhi ya mapungufu katika kuoa/kuolewa.

Lakini usipooa au usipoolewa…utakuwa huru Zaidi..unaweza kufunga safari muda wowote unaotaka kuifanya kazi ya Mungu, unaweza kufunga siku nyingi bila usumbufu, unaweza kwenda kusali mlimani kipindi kirefu au kuhubiri bila kukumbuka una jukumu Fulani umeliacha nyumbani …kadhalika, hutapata usumbufu wa Watoto wanahitaji hiki, wanahitaji kile.. kadhalika hutaishi kwa matakwa ya mtu Fulani, bali kwa kile Mungu anachokuongoza kila mara. Jambo ambalo lina faida katika ufalme wa mbinguni mara dufu kuliko hilo lingine.

Wa kwanza kabisa ambaye tunaona hakuoa na huduma yake iliikuwa na matokeo makubwa sana ni Bwana wetu Yesu. Mwingine ni Paulo ambaye ndiye aliyeandika mistari hiyo hapo juu kwa uwezo wa roho..Paulo hakuwa miongoni mwa Mitume 12 wa Bwana Yesu, lakini alifanya kazi kubwa kuliko hata mitume wa Yesu (kasome1Wakorintho 15:10), na wengine ni Yohana Mbatizaji na Eliya Mtishbi.

Lakini hilo sio lazima na wala sio amri, kwamba kila mtu ni lazima asiolewe/asioe. Ni jinsi mtu aonavyo yeye kwamba anaweza kujizuia au la!…Wapo wanaoweza kujizuia na wapo wasioweza!…Biblia inasema kama huwezi kujizuia ni afadhali uoe/uolewe kuliko kuwakwa na tamaa.

1Wakorintho 7:8 “Lakini nawaambia wale WASIOOA BADO, na wajane, Ni heri wakae kama mimi nilivyo. LAKINI IKIWA HAWAWEZI KUJIZUIA, NA WAOE; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa”……

 

1Wakorintho 7:1 “Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke. 2 Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe”.

Bwana akubariki.

Kumbuka kama unaishi na mwanamke/mwanaume ambaye hamjafunga ndoa..basi mnaishi katika uzinzi!..haijalishi mmeishi miaka mingapi Pamoja, au mmezaa Watoto wangapi..Mnapaswa mkatubu na kufunga ndoa takatifu, mbele ya kanisa la Kristo, ndipo mbarikiwe (na ndoa sio sherehe na matarumbeta)..mmeshaishi miaka yote hiyo, sherehe ya nini tena?..hatua mliyopo ni ya kutubu tu, na kwenda mbele ya kanisa kufungishwa ndoa mbele ya mashahidi na kurudi nyumbani kuendelea na maisha basi haihitaji maandalizi kana kwamba ndio mmketana kwa mara ya kwanza!. Lakini msipofanya hivyo mkifa leo mtahukumiwa, hiyo ni kulingana na maandiko.

Na mwisho kama hujaolewa na unatafuta wa kukuoa..Ni vizuri ukamtafuta kwanza Mwokozi. Kwasababu ukifa leo bila mwokozi utapotea milele, na Zaidi ya yote mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa, hayo mambo yataishia humu humu duniani..miili tutakayopewa tukifika kule haina hisia za kimwili. Huko tutaishi na Kristo milele. Hivyo Wokovu ni muhimu na wa kwanza katika Maisha, hayo mengine ndio yafuate.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana alimaanisha nini kusema JIKANE mwenyewe?(Mathayo 6:24)

 MAVUNO NI MENGI

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

KUOTA UNASAFIRI.

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIAMA KINATISHA.

Ikiwa leo hii Unyakuo utapita, na wewe ukabaki, basi fahamu dunia itakuwa na miaka 7 tu mbele yako kabla haijaisha, yaani kama leo ni mwaka 2020, basi haitapita mwaka 2027, kabla ya kila kitu unachokiona leo hii kuwa jivu.. Miaka hiyo saba imepatikana kutoka katika ule Unabii wa Danieli wa yale majuma 70, (Danieli 9:24) ambapo mpaka sasa limebakia juma moja tu, lenye miaka 7 kuanza.

Sasa katika hicho kipindi cha miaka 7 dunia haitakuwa tu umestarehe ikisubiria mwisho ufike hapana.. Kutaanza kuwa na mabadiliko ya haraka na ya ghafla sana duniani, jambo ambalo litawashitusha wengi, hapo ndipo ule unabii wa Bwana Yesu unaosema siku hiyo itawajilia kwa ghafla utakapotimia (Luka 21:34-35), kama tu unavyoona huu ugonjwa wa Corona ulivyoijilia hii duniani kwa ghafla bila taarifa, ndivyo itakavyokuwa hicho kipindi.

Miaka hii 7 inajulikana kama miaka ya dhiki, na imegawanyika katika vipengele vikuu viwili, Kipengele cha kwanza, ni cha miaka 3 na nusu, ya kwanza, na cha pili ni miaka 3 na nusu ya mwisho.

Sasa katika hiyo miaka mitatu na nusu ya kwanza, kitakuwa ni kipindi cha mpinga-kristo, kujiimarisha, na kuingia agano na watu(mataifa mengi),Danieli 9:27, ikiwemo taifa la Israeli,.na wakati wa watu kupokea chapa. Lakini wakati huo huo Wale manabii wawili (Mashahidi 2), tunaowasoma katika ufunuo 11, watasimama kuihubiria Israeli, kwa muda huo wa miaka mitatu na nusu ya kwanza,.Injili yao haitakuwa ya maneno matupu tu, bali itafuatana na mapigo kadha wa kadha mwishoni mwishoni karibia na kumaliza ushuhuda wao, soma Ufunuo 11, mapigo hayo yatakuwa ni makali na ya kutesa kiasi kwamba siku mpinga-Kristo atakapowaua, dunia nzima itafurahia tukio hilo na kuepelekeana zawadi wao kwa wao.

Sasa hiyo miaka 3 na nusu ya mwanzo itakapokwisha, Mpinga-Kristo atakuwa ameshapata nguvu za kutosha, wakati huo, ndio atanyanyuka sasa, kuleta dhiki kuu juu ya wale wote ambao hawatakuwa na chapa/Utambulisho wake (666).. Hapa hatanusurika mwanadamu yeyote ulimwenguni aliyeikwepa chapa hiyo, kutakuwa na mawili aidha upokee chapa, au ufe.. Na kifo sio cha kupigwa risasi au kunyongwa…Ni heri ingekuwa hivyo!…lakini kifo watakachokufa wale walioikataa chapa kitakuwa ni cha kuteswa mda mrefu sana…Watu watateswa hata kwa mwaka mmoja au miwili bila kuruhusiwa wafe…Ni mateso ya kuwekwa kwenye kambi maalumu za mateso..yale ya kale ambayo unatolewa macho, unavuliwa nguo, wakati wa baridi..halafu unafanyishwa kazi ngumu, huku unapewa mlo mmoja kwa wiki,(na mlo wenyewe ni supu tu) na huku unachapwa na viboko, yatakuwa ni mateso madogo sana…Watu watatamani wafe huko lakini hawatakufa..watateseka katika hiyo hali hata kwa miaka miwili ndio uje wafe!…

Bwana Yesu alisema dhiki hiyo ambayo itakuja kutokea haijawahi kutokea tangu dunia iumbwe na wala haitakaa itokee tena baada ya hapo.. Kiasi kwamba watakaowezi kuyastahimili hayo watakuwa ni watu wachache sana, wengine wote wataipokea chapa ya mnyama. Na jambo hilo litaendelea kwa muda wote wa miaka mitatu na nusu ya mwisho.

Hapo katika kutakuwa ni mapigo mengine mengi sana, mapigo ya baragumu saba yataendelea..na mapigo ya vitasa saba vya Mungu nayo pia yatafuata, mwishoni mwa miaka mitatu na nusu, kwa urefu wa somo hili fungua hapa >> SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!..hatuwezi kueleza yote hapa sehemu moja.

Sasa mwisho kabisa ya dhiki hizo kupita, unaweza kudhani, mambo ndio yamekwisha?, Wale waliopokea chapa, basi wamepona,? Hapana, ndugu kinyume chake huo ndio mwanzo wa ukurusa mwingine ujulikanao kama SIKU YA BWANA.

Hii siku ya Bwana, itakuwa ni kipindi cha siku 30 nyingine juu ya ile miaka saba kupita…Watu watadhani kuipokea chapa ndio kupona, lakini ni sawa na mtu aliyemkimbia Simba akakutana na dubu biblia inasema hivyo..ni heri wangekufa kwenye dhiki kuu ya mpinga-Kristo.

Amosi 5:18 “Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru.

19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma”.

Hichi kipindi watakaokuwepo duniani hawataamini macho yao, watashikwa na butwaa la ajabu, kwasababu, watashuhudia hii dunia ikigeuzwa na kuwa kama mojawapo ya sayari Fulani huko angani isiyokaliwa na watu, Kwasababu hili jua tunaloliona litazimwa lote, (kutakuwa na giza kubwa) mwezi utakuwa mwekundu kama damu, nyota zote zitaondoka huko mbinguni kutakuwa na giza tororo ambalo halijawahi kutokea duniani…

Amosi 5:20” Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga”.

Lengo la siku hiyo ya Bwana, ni kuifanya dunia kuwa ukiwa kama tulivyoikuta siku ile ya uumbaji..Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. NAYO NCHI ILIKUWA UKIWA, TENA UTUPU, NA GIZA lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji”

Hivyo dunia itafanywa ukiwa tena..

Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ILI IIFANYE NCHI KUWA UKIWA, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.

11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;

12 nitafanya wanadamu kuadimika kuliko dhahabu safi, na watu kuliko dhahabu ya Ofiri”.

Siku hii itaambatana na tetemeko kubwa la Ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu dunia iumbwe, visiwa vitahama,..

Ufunuo 16:18 “Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo.

19 Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake.

20 Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.

21 Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno”.

Unaona, tutakayokuwa yanaendelea kwenye hii dunia wakati huo?? Ndugu kuna vifungu vingi sana vya kuandika hapa,vinavyoilezea hii siku ya kuogofya ya Bwana, lakini hatuwezi kuviorodhesha vyote, kwa muda wako pitia vifungu hivi (Yoeli 1:15, Yoeli 2:1, 2:11, Yoeli 3:14),

Sasa baada ya hayo kupita, Ndipo Kristo atatokea mawinguni, Na kila jicho litamwona, naye atawaua waliosalia na majeshi yao, na kumaliza kila kitu, wale waovu waliosalia (Mathayo 24:29-30, Ufunuo 19:11-21)..

Na baada ya hapo kutakuwa ni siku nyingine 45, juu ya zile siku 30, ambapo ndani ya siku hizo, wafu watafufuliwa watawale pamoja na yeye, pamoja na ile hukumu ya mataifa ya kuwatenga kondoo na mbuzi, na katika kipindi hicho hicho Kristo ataitengeneza tena hii dunia upya, Nayo itakuwa nzuri zaidi ya Edeni, nasi tutawala naye kwa kipindi kingine cha amani cha miaka 1000, wakati huo hakuna mwovu yoyote, ayatakayenusuruka..

Sasa hapa tumefupisha tu, unaweza kudhani kama hizi ni hadithi tu, au mambo hayo bado sana, yatachukua mamia ya miaka huko mbeleni, Lakini fahamu kuwa hivyo ndivyo shetani anavyotaka ujue ili siku ile ikujie kwa ghafla..Lakini maandiko yanakuambia hivi..

Sefania 1:14 “Hiyo siku ya Bwana iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya Bwana; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko!

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,

16 Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.

17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.

18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha”.

Tusiwe na mengi ya kusema, ila ombi langu ni kuwa kama hujampa Kristo maisha yako, basi fanya uamuzi huu haraka, Kumbuka anakupenda sana, anakujali sana, anakuthamini, na anatamani sana uyarithi aliyokwenda kukuandalia miaka 2000 iliyopita kule juu mbinguni..Kwa muda wote huo! Ni lazima ni mambo mengi na mazuri aliyotuandalia….Wokovu wake ni bure, tena unapatikana sehemu yoyote, bila malipo. Fanya hivyo naye atajifunua kwako. (kiama kinatisha!)

Bwana akubariki, Bwana atubariki sote.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

Kabla ya kufahamu ubatizo ni nini…Hebu jiulize mtu katokea na akakuuliza “kuzamisha maana yake ni nini?”..utamjibuje?…Bila shaka utamwelezea kwa kina kwamba ni kitendo cha kukitosa kitu chote kwenye kimiminika Fulani au kitu Fulani, pasipo kubakisha sehemu ambayo ipo wazi. Meli iliyopata ajali na kushuka chini ya bahari, tunasema meli hiyo imezama baharini. Mtu anayechimba shimo la taka akachimba chini sana na kuzitupa humo na kuzifukia, hapo ni sawa na kusema kazizamisha/kazizika.

Sasa mpaka hapo tutakuwa tumeshajua maana ya neno “KUZAMA au KUZAMISHA”..Sasa ukilichukua neno hilo “kuzamamisha”  ukalitafsiriwa kwa lugha ya kigiriki linakuwa ni BAPTIZO…Ni sawa uchukue Neno la kiswahili “kanisa” na kulitafsiri kwa kiingereza na kuwa “CHURCH”…Vivyo hivyo Neno “kuzamishwa” likitafsiriwa kwa kigiriki linakuwa ni Baptizo..neno hilo hilo likipelekwa kwa lugha ya kiingereza linakuwa ni “IMMERSION”..na linaweza kutafsiriwa kwa lugha mbali mbali..

Kwahiyo mtu anayesema “leo naenda chachi”..ni sawasawa na mtu aliyesema “leo naenda kanisani”…neno “chachi” sio Kiswahili, na wala sio kiingereza fasaha lakini utakuwa umemwelewa amemaanisha nini kusema hivyo.

Vivyo hivyo mtu akikuambia “leo nime batizwa kwenye maji” utakuwa umemwelewa kwamba amemaanisha leo kazamishwa kwenye maji…kwa lengo Fulani.. (katumia tu msemo wa kigiriki lakini utakuwa umeshamwelewa).

Kwahiyo mpaka hapo utajua kuwa hakuna mtu atakayekuambia kwamba kabatizwa kwenye maji halafu awe “amenyunyuziwa”…Mtu aliyenyunyuziwa hajabatizwa!…kwasababu kubatizwa sio kunyunyuziwa bali kuzamishwa kabisa. (mpaka hapo tutakuwa tumeshaelewa ubatizo ni nini)

TUKIRUDI KATIKA IMANI YA KIKRISTO.

Katika imani ya kikristo, yapo mambo ambayo yanafanyika kama ishara lakini yanafunua kitu kikubwa sana katika roho. Kwamfano utaona Bwana Yesu alitoa maagizo ya kushiriki meza ya Bwana, ambapo wakristo wakutanikapo wanakula mkate pamoja na divai. Hivyo ni vyakula vya kimwili lakini vinapolika kwa maagizo hayo ya Bwana Yesu vinakuwa vinafunua vitu vingine katika roho. Kwamba ni sawa na tunainywa damu ya Yesu na Mwili wake katika ulimwengu wa roho. Na alisema mtu asiyefanya hivyo basi hana uzima ndani yake. (maana yake hana ushirika na Yesu).

Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu”.

Umeona ni agizo dogo tu, la kula chakula cha kimwili, lakini lina maana kubwa sana katika roho, sio la kulipuuza wala la kulifanya isivyopaswa…Na hapo hajasema tuonje!..bali tuule..

Kadhalika Bwana Yesu alitoa maagizo mengine yanayofanana na hayo ya watu kuzamishwa katika maji kwa jina lake(au kirahisi kubatizwa), ambapo alisema kwa kufanya hivyo katika mwili..kunafunua jambo kubwa sana katika roho, ambalo jambo lenyewe ni “kufa na kufufuka pamoja naye”

Wakolosai 2:12 “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu”.

Umeona na hapo?..maana yake usipobatizwa (yaani kuzamishwa katika maji)..basi katika roho bado hujafa wala kufufuka pamoja naye…wewe bado si wake!. Vile vile kama hujazamishwa na badala yake umenyunyuziwa hapo bado hujabatizwa, unapaswa ukabatizwe tena katika maji mengi.. kwasababu ndio tafsiri ya neno ubatizo.

Sasa yapo maswali machache machache ya kujiuliza?

Je ina maana kama mtu hajabatizwa katika maji mengi na badala yake katika kunyunyiziwa hawezi kwenda mbinguni?..Na kama hawezi vipi Yule mwizi aliyesulibiwa na Bwana pale msalabani..mbona yeye aliokolewa na wala hakubatizwa?..mbona wakina Musa hawakubatizwa?…mbona wakina Eliya hawakubatizwa?…Majibu ya maswali haya yote utayapata hapa >> Mtu akifa bila kubatizwa atakwenda mbinguni?

Hivyo ndugu mpendwa kamwe usiudharau “ubatizo”..kama bado hujaelewa kwa undani ubatizo ni nini, na umuhimu wa ubatizo tafadhali rudia kusoma tena taratibu na nakuomba chukua muda mwingi…katafute kuuliza huko na huko na pia piga magoti peke yako mwulize Roho Mtakatifu, halafu kasome biblia yako atakupa majibu.

Na ubatizo sahihi ni wa Jina la Yesu kulingana na mistari hii; Matendo 2:38, 8:16,10:48 na 19:5. Jina la Yesu ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kufahamu haya zaidi fungua masomo mwisho kabisa mwa somo hili (sehemu ya chini)..yanaelezea kwa kina masuala ya ubatizo.

Bwana akubariki.

Kama hujampokea Yesu saa ya wokovu ni sasa. Kristo yupo mlangoni kurudi kuwachukua wateule wake..hivyo ingia leo ndani ya neema hii, kabla mlango wa neema haujafungwa. Yesu anakupanda na anataka kukupa raha nafsini mwako leo kama utamkubali…sawasawa na neno lake hili..

Mathayo 11: 28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:

BIBLIA TAKATIFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.

Hivi unajua kuwa Wayahudi walikuwa wanamtazamia Kristo?..

Kila siku walikuwa wanamwomba Mungu wa mbingu na nchi… amtume Kristo wake duniani, aje awakomboe kutoka katika utumwa wa kirumi na wa dhambi. Na walidhamiria kabisa pindi atakapokuja wamheshimu na wamfurahie. Na hiyo ilimfanya kila mtu alitengeneza picha yake kichwani jinsi atakavyokuwa.

Lakini kama tunavyosoma biblia kipindi alipokuja hawakumjua kama ndio yeye…Na kosa kubwa walilolifanya ni KUTOKUJUA MAJIRA, hilo tu!. Siku zote ukishapoteza kujua majira, basi vitu vitakuja kwa kushtukiza mbele yako.

Umewahi kumwona mtu aliyepata tatizo Fulani na akapoteza kumbukumbu kabisa!..anakuwa katika hali ngumu sana, kwasababu anaweza kuja hata ndugu yake aliyeishi naye miaka yote na asimkumbuke hata kidogo!..kwake kila kitu ni kipya, lakini kumbukumbu zinapomrejea ndipo anashtuka huyu si ni Fulani?.

Umewahi kukaa na saa iliyopoteza majira?..Unaweza kujikuta kunapambazuka ukiwa bado kitandani ukidhani bado ni usiku, kwa kuitazama saa iliyopoteza majira! Hivyo na wewe ukapoteza majira.

Ndicho kilichowatokea wayahudi. Hawakujua wakati wa BWANA KUWAJILIA, walidhani Masihi hawezi kuja wakati kama huo, walijua ni kweli anakaribia kuja, lakini si katika kile kipindi walichopo..walizipeleka tarehe mbele kidogo..na wakajua Masihi atakapokuja atakuwa katika jumbe la kifalme, na atatawala kwa fimbo ya chuma, na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake.

Luka 19:43 “Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote;

44  watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO”.

Ndugu upo WAKATI WA KUJILIWA KWA KILA MTU!. Sizungumzii wakati wa kujiliwa kupata Maisha mazuri au nyumba nzuri au fedha nyingi, au mali bali wakati wa kujiliwa na NEEMA YA MUNGU. Kama Wayahudi walivyojiliwa na Bwana lakini hawakuyatambua majira hayo, wakaikataa na mpaka sasa wameachwa katika hali ya ukiwa. Na siku sio nyingi watajua makosa yao na kutubu na kugeuka kumwamini Mwokozi wao waliyemkataa miaka Zaidi ya eflu 2 iliyopita.

Luka 12:54 “ Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya?”

Nguvu unayoisikia inakuvuta kwake jua ni majira ya kujiliwa kwako hayo…usiipuuzie hata kidogo! Na wala usikawie kawie…Na sasa tunaishi katika majira ya kurudi kwa Yesu mara ya pili. Wakati dunia inasema hawezi kuja leo..bado sana aje!…lakini alisema atakuja kama Mwivi…hawatajua chochote!…

Ukimwambia mtu kwamba Yesu amekaribia kurudi…kitu cha kwanza atatengeneza picha ya kipindi kirefu sana mbele, siku ambayo atatokea mpinga-kristo mwenye mapembe..pasipo kujua kuwa tayari Ofisi ya Mpinga-kristo ipo sasa duniani. na cheo chake kinajulikana…na tayari maandalizi ya ile chapa yapo tayari..Ni parapanda tu inasubiriwa mambo yote yaanze.

Huu ni wakati wa kuyasoma  na kuyatambua haya Majira tuliyopo!..tupoteze kujua kila kitu lakini tusipoteze kujua majira yetu ili mambo yasije yakatutokea ghafla..

1Wathesalonike 5:1  “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2  Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3  Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

UFUFUO TUNAOUSUBIRIA UTAHITIMISHA YOTE.

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI UKATE TAMAA?

Kwanini ukate tamaa ya  kumtafuta Mungu? Nataka nikuambie hata Mungu mwenyewe akikuambia sikutaki haunifai, bado hupaswi kukata tamaa…

Kuna mbegu Fulani ya uharibifu ambayo shetani ameipanda ndani ya mioyo ya wakristo wengi, ambayo kuna hatua wanafikia ya kujiona kuwa hawafai tena mbele za Mungu, ya kujiona kuwa Mungu hawezi kuwa nao tena, ya kujiona kama hawastahili kwenda mbele za Mungu tena,….Hivyo wanaishia kukata tamaa ya kuendelea mbele pale wanapoona hata majibu ya maombi yao yanachelewa, nimekutana na watu wa namna hiyo wengi.

Lakini nataka nikuambie hupaswi kukata tamaa, wapo ambao Mungu alikuwa hana mpango nao,wengine hawakuwa  hata wakristo, na wengine walikuwa wamesha muudhi Mungu kupindukia kwa kiwango cha juu sana mpaka Mungu kuwatamkia vifo, lakini katika uovu wao hawakukata tamaa ya kumkimbilia Mungu awarehemu, si Zaidi wewe ambaye ulishaokoka? Kwanini ukate tamaa?

Zaburi 107:10 “Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma,

11 Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, Wakalidharau shauri lake Aliye juu.

 12 Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa wala hakuna msaidizi.

13 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.

14 Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akayavunja mafungo yao.

15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu”.

Kumbuka Biblia ni kitabu kilichoandikwa ili kutuonya sisi, na kwa sehemu nyingine ili kututia nguvu, na kutufariji..

Kwa mfano embu mwangalie huyu mama ambaye hata wakati wake neema ya wokovu ilikuwa haijamfikia, alikuwa na miungu yake huko Tiro, pengine alipata hilo tatizo kutokana na dhambi zake kwa Mungu, lakini ilipofika wakati wa kutaka msaada kutoka kwa Mungu, hakujali “kutokujali kwa Mungu“, hakujali majibu makali kutoka kwa Mungu, bali aling’ang’ania mpaka akapata alichokuwa anakitafuta, haijalishi kuwa angeendelea kwenda kuiabudu miungu yake.

Mathayo 15:22  “Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23  Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24  Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25  Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26  Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27  Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28  Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Unaona tabia ya huyo mwanamke?, Mfano mwingine ni Mfalme Ahabu..Ambaye tunajua alikuwa ni mume wa yule mwanamke mchawi Yezebeli, biblia inasema huyu Ahabu alikuwa mfalme mwovu, kuliko wafalme wote waliomtangulia na alishiriki kuwakosesha sana Israeli mbele za Mungu (1Wafalme 21:25), mpaka ikafikia wakati Mungu akamwambia inatosha sasa..kufa utakufa, na nyumba yako itakuwa jaa..

Lakini Habari hizo mbaya kutoka kwa Mungu zilipomfikia, haikumfanya akate tamaa, na kusema sasa ndio basi!, Mungu hawezi tena kunitazama, badala yake alikwenda kujinyenyekeza..

1Wafalme 21: 27 “Ikawa, Ahabu alipoyasikia maneno hayo, akayararua mavazi yake, akavaa magunia mwilini mwake, akafunga, akajilaza juu ya magunia, akaenda kwa upole.

 28 Neno la Bwana likaja kwa Eliya Mtishbi, kusema,

29 Huoni jinsi Ahabu alivyojidhili mbele yangu? Basi kwa sababu amejidhili mbele yangu, sitayaleta yale mabaya katika siku zake; ila katika siku za mwanawe nitayaleta mabaya hayo juu ya nyumba yake”..

Yupo na mwingine aliyetokea baada ya Ahabu, aliyeitwa Manase, Huyu ndiye alifanya mabaya Zaidi kuliko hata Ahabu na ndio aliyesababisha hata Mungu asiwasemehe Israeli tena, huyu alikuwa anawatoa mpaka Watoto wake kafara kwa kuwapitisha kwenye moto, alikuwa anakwenda kufanya uganga na mambo maovu kweli kweli..Mungu akachukizwa naye sana Ikiafikia hatua ya kuchukuliwa mateka kwa minyororo na pingu, na waashuru mpaka Babeli.

Lakini akiwa huko akijijua kuwa yeye ni adui wa kwanza wa Mungu,  alijinyenyekeza kwa Mungu akamlilia sana mpaka akasikiwa..

2Nyakati 33:12 “Hata alipokuwa katika taabu, akamsihi Bwana, Mungu wake, akajinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.

13 Akamwomba; naye akamtakabali, akayasikia maombi yake; akamrudisha tena Yerusalemu katika ufalme wake. Ndipo Manase akajua ya kwamba Bwana ndiye Mungu”.

Sasa hiyo ni mifano michache ya watu ambao walikuwa ni waovu na wenye dhambi, ambao tayari walikuwa wameshahukumiwa tayari na Mungu kutokana na makosa yao..Lakini hawakukata tamaa, kujinyenyekeza kwake (sasa wewe kwanini ukate tamaa?)..Lakini sikuambii hivi ili na wewe ukafanye dhambi umwombe Mungu halafu akusikie hapana, hilo ni kosa.

Naandika hivi kwa ajili yako, wewe ambaye umeokoka, halafu unaona kama Mungu hawezi kukusikia, au hakujali.. Jiulize! tu kama Mungu Yehova alivisikia vilio vya wenye dhambi kama wakina Ahahu na Manase ambao walimkasirisha kwa kiwango kile, ataachaje kukusikia wewe ambaye, tayari ulishampa Maisha yako?..Anakusikia sana. Na anakuhurumia kuliko wewe unavyodhani, na anakujali, na anayasikia maombi yako…Hivyo huna sababu ya kukata tamaa?..Endelea mbele kumwamini na kumwomba kwa bidii.

Hebu soma tena hapa..

Zaburi 107: 4 “Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa.

5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.

6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.

7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa”.

Zaburi 105:8 “Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema”

Nataka nikuambie ukiwa umeokoka, Bwana anakupenda na yupo karibu sana na wewe kuliko hata wenye dhambi, ukiwa umeokoka kilio chako mbele zake kinasikika Zaidi kuliko kilio cha akina Ahabu na Manase.., Hivyo endelea tu kumtafuata Mungu kwa bidii zote kwasababu wewe ni wa thamani nyingi kwake, wenye dhambi wasikushinde, ng’ang’ana na Bwana, popote pale, atakuwa na wewe wakati wote..

Wanaomtegemea Mungu, mwisho wao huwa unakuwa mzuri kama wa Ayubu.

Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Kuungama ni nini?

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

NGUVU YA SADAKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post