YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.

YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.

Hivi unajua kuwa Wayahudi walikuwa wanamtazamia Kristo?..

Kila siku walikuwa wanamwomba Mungu wa mbingu na nchi… amtume Kristo wake duniani, aje awakomboe kutoka katika utumwa wa kirumi na wa dhambi. Na walidhamiria kabisa pindi atakapokuja wamheshimu na wamfurahie. Na hiyo ilimfanya kila mtu alitengeneza picha yake kichwani jinsi atakavyokuwa.

Lakini kama tunavyosoma biblia kipindi alipokuja hawakumjua kama ndio yeye…Na kosa kubwa walilolifanya ni KUTOKUJUA MAJIRA, hilo tu!. Siku zote ukishapoteza kujua majira, basi vitu vitakuja kwa kushtukiza mbele yako.

Umewahi kumwona mtu aliyepata tatizo Fulani na akapoteza kumbukumbu kabisa!..anakuwa katika hali ngumu sana, kwasababu anaweza kuja hata ndugu yake aliyeishi naye miaka yote na asimkumbuke hata kidogo!..kwake kila kitu ni kipya, lakini kumbukumbu zinapomrejea ndipo anashtuka huyu si ni Fulani?.

Umewahi kukaa na saa iliyopoteza majira?..Unaweza kujikuta kunapambazuka ukiwa bado kitandani ukidhani bado ni usiku, kwa kuitazama saa iliyopoteza majira! Hivyo na wewe ukapoteza majira.

Ndicho kilichowatokea wayahudi. Hawakujua wakati wa BWANA KUWAJILIA, walidhani Masihi hawezi kuja wakati kama huo, walijua ni kweli anakaribia kuja, lakini si katika kile kipindi walichopo..walizipeleka tarehe mbele kidogo..na wakajua Masihi atakapokuja atakuwa katika jumbe la kifalme, na atatawala kwa fimbo ya chuma, na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake.

Luka 19:43 “Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote;

44  watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO”.

Ndugu upo WAKATI WA KUJILIWA KWA KILA MTU!. Sizungumzii wakati wa kujiliwa kupata Maisha mazuri au nyumba nzuri au fedha nyingi, au mali bali wakati wa kujiliwa na NEEMA YA MUNGU. Kama Wayahudi walivyojiliwa na Bwana lakini hawakuyatambua majira hayo, wakaikataa na mpaka sasa wameachwa katika hali ya ukiwa. Na siku sio nyingi watajua makosa yao na kutubu na kugeuka kumwamini Mwokozi wao waliyemkataa miaka Zaidi ya eflu 2 iliyopita.

Luka 12:54 “ Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya?”

Nguvu unayoisikia inakuvuta kwake jua ni majira ya kujiliwa kwako hayo…usiipuuzie hata kidogo! Na wala usikawie kawie…Na sasa tunaishi katika majira ya kurudi kwa Yesu mara ya pili. Wakati dunia inasema hawezi kuja leo..bado sana aje!…lakini alisema atakuja kama Mwivi…hawatajua chochote!…

Ukimwambia mtu kwamba Yesu amekaribia kurudi…kitu cha kwanza atatengeneza picha ya kipindi kirefu sana mbele, siku ambayo atatokea mpinga-kristo mwenye mapembe..pasipo kujua kuwa tayari Ofisi ya Mpinga-kristo ipo sasa duniani. na cheo chake kinajulikana…na tayari maandalizi ya ile chapa yapo tayari..Ni parapanda tu inasubiriwa mambo yote yaanze.

Huu ni wakati wa kuyasoma  na kuyatambua haya Majira tuliyopo!..tupoteze kujua kila kitu lakini tusipoteze kujua majira yetu ili mambo yasije yakatutokea ghafla..

1Wathesalonike 5:1  “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2  Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3  Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

UFUFUO TUNAOUSUBIRIA UTAHITIMISHA YOTE.

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI UKATE TAMAA?

Kwanini ukate tamaa ya  kumtafuta Mungu? Nataka nikuambie hata Mungu mwenyewe akikuambia sikutaki haunifai, bado hupaswi kukata tamaa…

Kuna mbegu Fulani ya uharibifu ambayo shetani ameipanda ndani ya mioyo ya wakristo wengi, ambayo kuna hatua wanafikia ya kujiona kuwa hawafai tena mbele za Mungu, ya kujiona kuwa Mungu hawezi kuwa nao tena, ya kujiona kama hawastahili kwenda mbele za Mungu tena,….Hivyo wanaishia kukata tamaa ya kuendelea mbele pale wanapoona hata majibu ya maombi yao yanachelewa, nimekutana na watu wa namna hiyo wengi.

Lakini nataka nikuambie hupaswi kukata tamaa, wapo ambao Mungu alikuwa hana mpango nao,wengine hawakuwa  hata wakristo, na wengine walikuwa wamesha muudhi Mungu kupindukia kwa kiwango cha juu sana mpaka Mungu kuwatamkia vifo, lakini katika uovu wao hawakukata tamaa ya kumkimbilia Mungu awarehemu, si Zaidi wewe ambaye ulishaokoka? Kwanini ukate tamaa?

Zaburi 107:10 “Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma,

11 Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, Wakalidharau shauri lake Aliye juu.

 12 Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa wala hakuna msaidizi.

13 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.

14 Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akayavunja mafungo yao.

15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu”.

Kumbuka Biblia ni kitabu kilichoandikwa ili kutuonya sisi, na kwa sehemu nyingine ili kututia nguvu, na kutufariji..

Kwa mfano embu mwangalie huyu mama ambaye hata wakati wake neema ya wokovu ilikuwa haijamfikia, alikuwa na miungu yake huko Tiro, pengine alipata hilo tatizo kutokana na dhambi zake kwa Mungu, lakini ilipofika wakati wa kutaka msaada kutoka kwa Mungu, hakujali “kutokujali kwa Mungu“, hakujali majibu makali kutoka kwa Mungu, bali aling’ang’ania mpaka akapata alichokuwa anakitafuta, haijalishi kuwa angeendelea kwenda kuiabudu miungu yake.

Mathayo 15:22  “Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23  Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24  Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25  Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26  Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27  Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28  Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Unaona tabia ya huyo mwanamke?, Mfano mwingine ni Mfalme Ahabu..Ambaye tunajua alikuwa ni mume wa yule mwanamke mchawi Yezebeli, biblia inasema huyu Ahabu alikuwa mfalme mwovu, kuliko wafalme wote waliomtangulia na alishiriki kuwakosesha sana Israeli mbele za Mungu (1Wafalme 21:25), mpaka ikafikia wakati Mungu akamwambia inatosha sasa..kufa utakufa, na nyumba yako itakuwa jaa..

Lakini Habari hizo mbaya kutoka kwa Mungu zilipomfikia, haikumfanya akate tamaa, na kusema sasa ndio basi!, Mungu hawezi tena kunitazama, badala yake alikwenda kujinyenyekeza..

1Wafalme 21: 27 “Ikawa, Ahabu alipoyasikia maneno hayo, akayararua mavazi yake, akavaa magunia mwilini mwake, akafunga, akajilaza juu ya magunia, akaenda kwa upole.

 28 Neno la Bwana likaja kwa Eliya Mtishbi, kusema,

29 Huoni jinsi Ahabu alivyojidhili mbele yangu? Basi kwa sababu amejidhili mbele yangu, sitayaleta yale mabaya katika siku zake; ila katika siku za mwanawe nitayaleta mabaya hayo juu ya nyumba yake”..

Yupo na mwingine aliyetokea baada ya Ahabu, aliyeitwa Manase, Huyu ndiye alifanya mabaya Zaidi kuliko hata Ahabu na ndio aliyesababisha hata Mungu asiwasemehe Israeli tena, huyu alikuwa anawatoa mpaka Watoto wake kafara kwa kuwapitisha kwenye moto, alikuwa anakwenda kufanya uganga na mambo maovu kweli kweli..Mungu akachukizwa naye sana Ikiafikia hatua ya kuchukuliwa mateka kwa minyororo na pingu, na waashuru mpaka Babeli.

Lakini akiwa huko akijijua kuwa yeye ni adui wa kwanza wa Mungu,  alijinyenyekeza kwa Mungu akamlilia sana mpaka akasikiwa..

2Nyakati 33:12 “Hata alipokuwa katika taabu, akamsihi Bwana, Mungu wake, akajinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.

13 Akamwomba; naye akamtakabali, akayasikia maombi yake; akamrudisha tena Yerusalemu katika ufalme wake. Ndipo Manase akajua ya kwamba Bwana ndiye Mungu”.

Sasa hiyo ni mifano michache ya watu ambao walikuwa ni waovu na wenye dhambi, ambao tayari walikuwa wameshahukumiwa tayari na Mungu kutokana na makosa yao..Lakini hawakukata tamaa, kujinyenyekeza kwake (sasa wewe kwanini ukate tamaa?)..Lakini sikuambii hivi ili na wewe ukafanye dhambi umwombe Mungu halafu akusikie hapana, hilo ni kosa.

Naandika hivi kwa ajili yako, wewe ambaye umeokoka, halafu unaona kama Mungu hawezi kukusikia, au hakujali.. Jiulize! tu kama Mungu Yehova alivisikia vilio vya wenye dhambi kama wakina Ahahu na Manase ambao walimkasirisha kwa kiwango kile, ataachaje kukusikia wewe ambaye, tayari ulishampa Maisha yako?..Anakusikia sana. Na anakuhurumia kuliko wewe unavyodhani, na anakujali, na anayasikia maombi yako…Hivyo huna sababu ya kukata tamaa?..Endelea mbele kumwamini na kumwomba kwa bidii.

Hebu soma tena hapa..

Zaburi 107: 4 “Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa.

5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.

6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.

7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa”.

Zaburi 105:8 “Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema”

Nataka nikuambie ukiwa umeokoka, Bwana anakupenda na yupo karibu sana na wewe kuliko hata wenye dhambi, ukiwa umeokoka kilio chako mbele zake kinasikika Zaidi kuliko kilio cha akina Ahabu na Manase.., Hivyo endelea tu kumtafuata Mungu kwa bidii zote kwasababu wewe ni wa thamani nyingi kwake, wenye dhambi wasikushinde, ng’ang’ana na Bwana, popote pale, atakuwa na wewe wakati wote..

Wanaomtegemea Mungu, mwisho wao huwa unakuwa mzuri kama wa Ayubu.

Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Kuungama ni nini?

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

NGUVU YA SADAKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIFUNZE KUJITOA KWA MUNGU NA KUWA MKARIBISHAJI.

Shalom, mtu wa Mungu.. karibu tujifunze biblia Neno la Mungu, ambalo ni mwanga wa njia yetu na taa iongozayo miguu yetu.

Leo tujikumbushe umuhimu wa kuwa wakaribishaji, na wa kujitoa kuifanya kazi ya Mungu.

Kipindi kirefu kidogo nimekuwa nikiwasiliana na binti mmoja humu facebook, ambaye anaishi kwao na wazazi wake, kiukweli ni binti anayempenda Mungu na kujitoa kwa Mungu ingawa ni mdogo kiumri. Amekuwa akitutumia maswali kadha wa kadha na kumjibu..kama ni mfuatiliaji wa masomo ya humu utakuwa umewahi kusoma swali tulilolijibu linalouliza… “Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?”…na lingine “Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?”.. Maswali haya mawili yaliulizwa na huyu binti..Na yapo mengine aliyouliza ambayo majibu yake tulimtumia pasipo kuyaweka wazi.

Huyu binti ni mtanzania lakini anaishi Zambia, karibu na mpaka wa Tanzania. Japokuwa ni binti mdogo lakini amekuwa akituuliza maswali kuhusu siku za mwisho na pia maswali ya namna ya kwenda kuwahubiria wengine Habari za Yesu mitaani. Katika udogo wake tulimtia moyo asiache kuwashuhudia wengine kwa bidii zote, haijalishi mazingira aliyopo, na mambo mengine mengi tulimshauri. Alienda kuyafanyia kazi hayo tuliyomshauri..na baada ya muda akatuletea mrejesho kwamba ametoka kuwashuhudia baadhi… “Anasema ijapokuwa huku nilipo makanisa yamefungwa kutokana na hofu ya corona, lakini mimi nilitoka hivyo hivyo sikujali.. na niliowashuhudia wengine wametaka namba zangu niwaombee na kuwaongoza sala ya toba” (kama kawaida hizo ni Habari za furaha kwetu sisi kama wakristo).. 

Ni binti pia ambaye anayepitia changamoto nyingi, na hata nyumbani alipo sio kwamba ni watu wa Imani sana, hata wale anaowashuhudia na kuokoka anaogopa kuwakaribisha nyumbani kwasababu ya vita vya nyumbani….yaani kwa ufupi ni binti aliyejitoa kweli, na mwenye upendo wa ki-Mungu, yupo tayari kwenda kuwasaidia watu roho pasipo kujali mazingira aliyopo.

Sasa siku kadhaa nyuma, alipata mgeni kama yule Ibrahimu aliyekutana naye wakati anatoka kumpiga Kedorlaoma (Mwanzo 14:8-18).. 

Hebu msikilize…

“Jana asubuhi sana niliamka nikawa naosha vyombo asa nikaenda kumwaga maji machafu ya vyombo nje nikachukua funguo nikapitia kufungua geti kubwa la nje , nikasikia sauti ikiita jina langu kwa sauti ya mbaali niliisikia lakini nikajua labda Ni mawazo tu, ikaita Tena ile nataka kuingia ndani nikainua macho getini nikamuona Mtu nisiyemjua anabisha hodi nikafungua nilivyofungua nikamsalimia kwa Adabu na heshima ya Hali ya juu kama kawaida yangu japo alikuwa m-baba mrefu mweusi amevaa nguo mbaya mbaya za (kimasikini) Mimi simjui asa nikajua labda Ni mgeni wa Baba labda alimpigia simu aje , kumbe sio, akaniambia unahitaji nini nikamwambia hamna Baba, huku naendelea kumsikiliza kwa makini kwa karibu , akaniambia chukua pesa hizi usiwe na shida, akanipa na vyakula Kisha akatoa pesa nyingine akanipa Sasa ile nimeshapokea pesa na vitu, nikamwambia YESU anakupenda akasema ndio nawewe (Mimi) anakupenda pia nikamwambia Asante! ,Sasa nikaweka vitu chini nikwambie umeokoka?, unaitwa Nani? Ile nainuka sikumuona Tena yule m-baba” .

Mwisho wa nukuu.

Sasa Baada ya kumuuliza alikupa nini kingine tofauti na hizo pesa?…akaniambia alimpa BIBLIA, TENZI ZA ROHONI, DIARY Pamoja na KALAMU.

Ndipo nikajua ni malaika kamtembelea…Na bahati nzuri huyu binti anayajua maandiko na analijua hili andiko pia…

Waebrania 13:2  “Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua”.

Hivyo baada ya tukio hilo ajijua kabisa ni malaika wa Bwana, na amani ya ajabu iliingia ndani yake..

Ndugu, haya mambo sio hadithi, ni vitu vya kweli kabisa…Kwasababu hata Mimi binafsi vilishawahi kunitokea mara mbili katika mazingira yanayokaribiana kufanana na huyu binti. Malaika wa Mungu mamilioni kwa mamilioni wanazunguka ulimwenguni..na wala usitegemee watakuja wamevaa nguo nyeupe na mabawa…Hapana!. Wale waliomtembelea Lutu hawakuwa na mavazi meupe, waliomfuata Ibrahimu chini ya mialoni ya Mamre hawakuwa na mavazi meupe…wanakuja kama watu tu wa kawaida kabisa..Ndio maana Paulo anasema “wengine mnawakaribisha Malaika pasipo kujua”.

Huyu binti yeye kaletewa zawadi chache za kumtia moyo kwamba azidi kusoma Neno na kujifunza (Ndio maana kapewa biblia na diary) Pamoja na kuwashuhudia wengine, na Bwana amemfanyia vile kumwonesha kuwa anampenda na yupo Pamoja naye kumhudumia katika mahitaji yake hata ya chakula hivyo asiogope! Na zaidi alimpa pesa nyingi sana..ndio maana kamtuma Malaika wake kumfariji.  Na ule ni udhihirisho mdogo tu wa mambo yanayoendelea katika roho, katika roho anazungukwa na hilo jeshi la malaika wengi sana. Popote anapokwenda wapo naye, kumlinda na kumtunza.

Jiulize je angekuwa si mtu wa kujali  na kujitoa kwa ajili ya roho za wengine malaika wa Bwana angetumwaje kwake?..Biblia inasema malaika ni viumbe wa roho wanaofanya kazi ya kuwahudumia Watoto wa Mungu wale watakaoirithi ahadi..na si kila mtu tu!

Waebrania 1:14  “Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?”

Sasa angetumwaje kumhudumia kama angekuwa si mtu wa kuifanya kazi ya Mungu?..Malaika wa Mungu angetumwa amletee zawadi gani ya kumfariji kama angekuwa ni binti wa kushinda tu kuzurula zurula mtaani au kuzungumza umbea au kutembea tembea na wavulana mitaani?..Unaona?..hakuna chochote angeambulia…

Na kitu kimoja ambacho hakifahamiki na wengi ni kwamba Malaika wana kazi ya kupeleka mambo yetu mema tunayoyafanya mbele za Mungu..Lolote zuri unalolifanya malaika wanalipeleka kama hoja mbele za Mungu..kama utapenda tukutumie somo juu ya hilo..utatutumia ujumbe mfupi inbox.

Naamini ushuhuda wa huyu dada ni darasa tosha kwetu!…Katika nafasi tulizopo, hebu tujitoe kwa Mungu…usijitoe ili utokewe na Malaika hapana!..jitoe kwasababu unaona umuhimu wa wengine kuujua ukweli na kupata wokovu maishani mwao. Nafasi ndogo unayopata kama ni shuleni, nyumbani, kazini, kwenye mitandano, usitengeneze visingizio vingi..kwamba siwezi kwasababu ya hichi au kile..kwasababu nipo bize..Ifanye kazi ya Mungu, wengi bado wanahitaji kuokolewa. Malaika wa mbinguni wanafurahi mtu mmoja tu anapotubu! 

Bwana atubariki na Bwana atusaidie.

Kama hujaokoka!..Wokovu unaanzia hapa hapa duniani!..usidanganywe na shetani kwamba hakuna kuokoka duniani, usidanyike mtu wa Mungu…Tubu leo kama bado..na kisha acha yote machafu uliyokuwa unayafanya kama ulevi, uasherati, wizi, utazamaji pornograph, utukanaji, uuaji, usengenyaji na mengine yote..Na baada ya hapo, tafuta kanisa lililo hai, lililopo karibu na mahali ulipo, hakikisha unabatizwa hapo katika ubatizo sahihi wa jina la Yesu na wa kuzamishwa mwili wote(Matendo 2:38). Na baada ya hapo Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia.

Unyakuo upo karibu na hizi ni siku za mwisho..siku yoyote! Mambo yatageuka ghafla, unyakuo utapita, watakatifu watatoweshwa..dhiki kuu ya mpinga-Kristo itaanza, na ghadhabu ya Mungu itamwagwa duniani.. hakuna mtu atategemea, itakuwa ni ghafla tu!..kama vile corona ilivyozuka ghafla tu! pasipo ulimwengu kutegemea.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.

UFUFUO TUNAOUSUBIRIA UTAHITIMISHA YOTE.

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

KWANINI HUNA HAJA YA KUANDIKIWA JUU YA NYAKATI NA MAJIRA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Neno la Mungu ni upanga.

Ni kwa namna gani Neno la Mungu ni upanga?


Biblia haisemi Neno la Mungu ni upanga tu, hapana bali inasema  ni zaidi ya upanga wowote mkali ukatao kuwili..

Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.”.

Unaona? Ni zaidi ya upanga. Na kama tunavyojua upanga unaokata kuwili ni upanga ambao unatumika sana sana katika vita, yaani ukiupeleka upande wa kulia unakata na vilevile ukiurudisha upande wa kushoto bado unakata(Ufunuo 1:16, 2:12, 19:12).. Ni mfano wa msimeno unakata mbele na nyuma.

Sasa Mungu anakuambia Neno lake ni zaidi ya huo upanga. Akiwa na maana kuwa linakata pande zote, kwa wale wote watakaokwenda kinyume nalo, linakata matajiri, linakata maskini, linakata wenye vyeo linakata wasio na vyeo, linakata weupe, linakata weusi, linakata wenye dhambi vilevile linakata na waliookoka ikiwa hawatadumu katika maagizo yake.

Na kukata kwake sio butu, bali kwa ukali sana, likipita linatenganisha kabisa kabisa, yaani mfano Mungu akipitisha upanga katika taifa basi ujue taifa hilo ndio mwisho wake umefika, akipitisha upanga katika familia basi ujue ni upanga kweli kweli unaotenganisha, haijalishi  ndugu hao watakuwa wanapendana au wameshikamana kiasi gani.Soma.

Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.

35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;

36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake”.

Vilevile alisema, katika wakati wa Mwisho atayaangamiza mataifa kwa Neno lake, ambao ndio huo upanga utokao katika kinywa chake..

Ufunuo 19:14 “Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana”.

Hivyo, Mungu anatuasa tutubu, tumgeukie yeye, ili kusudi kwamba Neno lake, liwe chakula na uzima kweli badala ya upanga, Kwasababu kwa kupitia hilo hilo Mungu alifanya mbingu na nchi, kwa kupitia hilo hilo, alituumba sisi, kwa kupitia hilo hilo alinatuponya na kutuokoa, na kutubariki. Lakini kwa kupita hilo hilo atatuhukumu kama tusipotaka kuitii injili. Na ndio anatuhimiza mpaka sasa tutubu kwa kurudi kwake kumekaribia.

Ufunuo 2.16 Basi tubu; na usipotubu, naja kwako upesi, nami nitafanya vita juu yao kwa huo upanga wa kinywa changu.

Neno la Mungu ni upanga.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

ROHO ZILIZO CHINI YA MADHABAHU:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Neno la Mungu la leo.

Neno la Mungu la leo ni lipi?


Kwanza nakupongeza kwa kupenda kutafuta kujua Neno la Mungu la leo..

Bwana Yesu alisema kila atafutaye huona (Mathayo 7:8), Hivyo kwa kuwa na wewe umetafuta kujua Neno la Mungu la leo kwako, basi ni hakika kuwa lipo jambo jipya Mungu atakufundisha.

Sio kwa bahati mbaya umefika mahali hapa.,

Paulo alimwambia Timotheo.

1Timotheo 4:13 “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma…..”

Unaona ni jukumu la kila mmoja wetu kuonyesha bidii katika kusoma(kujifunza) Neno la Mungu.

Wewe unaonyesha bidii hiyo  hivyo, usiache kupitia somo hili mpaka mwisho, lipo ambalo Mungu amekuandalia leo..

Lakini kabla hatujaendelea unaweza kufungua hapa  uingie katika horodha ya masomo ya kujifunza yaliyotangulia zaidi ya 1000, pamoja na maswali na majibu ..

>>> MAFUNDISHO MAPYA.


Leo tutajifunza nini maana ya Upendo na je! kuna aina ngapi za upendo?

Upendo ni kitendo cha kuonyesha hisia za tofauti za ndani kwa mtu mwingine, Ni hisia zinazoonyesha matokeo chanya, aidha umeridhishwa na mtu huyo, au umemkubali, au umemuhurumia, au unataka kumkaribia uwe karibu naye.

Kuna aina kuu tatu za upendo.

  1. Upendo unaotokana na Hisia, (Eros), Mfano wa upendo huu ni mke na mume. Sulemani aliutaja upendo huu sana katika kitabu cha Wimbo ulio bora (Wimbo 1:13-17)
  2. Upendo unatokana na  mahusiano mtu mmoja aliyo nayo kwa mwingine.(Phileo). Kwamfano unaweza ukawa unampenda mtu kutokana na kwamba ni mchezaji mwezako, au mfanyakazi mwenzako, au mkristo mwenzako, au mwanafunzi mwenzako n.k. mazingira yakishawatawanyisha, au itikidi zikitofautiana basi Upendo huu unakufa.
  3. Upendo wa ki-Mungu (Agape). Upendo huu ndio Upendo mkuu kuliko yote, Ni upendo usiokuwa na Masharti, Ni upendo ambao mtu anakupenda sio kwasababu ulimfanyia hiki au kile, au kwasababu unaendana naye kitu Fulani, hapana..Ni upendo usiohesabu mazuri wala mabaya kama kigezo cha kukupenda, ..

Upendo huu ndio ule ambao Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe wa pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele (Yohana 3:16).

 Na Upendo aliokuwa nao Yesu, ukamfanya mpaka auote uhai wake kwa ajili yetu sisi wenye dhambi. Upendo wa namna hii ukiwa nao basi ujue kuwa Upo karibu na Mungu sana kuliko mwanadamu mwingine yeyote duniani.

Na unamjua Mungu, zaidi mwanadamu mwingine yoyote duniani haijalishi atasema anaona maono, au ana mafunuo mengi kiasi gani..

1Yohana 4:7 “Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.

8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo”.

Tabia za upendo huu unaweza kuzisoma katika kitabu cha 1Wakorintho 13:4-8

Kwa urefu wa maelezo haya juu ya aina hizi za upendo fungua hapa usome..>> UPENDO

Hivyo hiyo yote ni kuonyesha jinsi gani Mungu anatupenda na kutujali, Hivyo kama wewe ni mwenye dhambi ujue kuwa Mungu anakupenda bado na hivyo hataki upotee, uende kuzimu, mgeukie leo akuoshe dhambi zako. Ili ukaurithi uzima wa milele aliotuandalia. Hilo ndilo Neno la Mungu la leo.

Shalom.

Tazama vichwa vingine vya masomo chini, kwa maarifa zaidi ya kiroho.

Mada Nyinginezo:

RABI, UNAKAA WAPI?

KWANINI YESU ALIMUITA BABA YAKE “ABA”?

MANENO ALIYOWEZA KUTAMKA YESU TU PEKE YAKE.

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

WAFALME WATOKAO MAWIO YA JUA.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NENO LA MUNGU NI NINI?.

Neno la Mungu ni nini?


Neno la Mungu ni ujumbe kutoka kwa Mungu, au mkusanyiko wa jumbe kutoka kwake. Ukisoma katika maandiko utaona mara nyingi manabii walikuwa wanasema maneno haya “Neno la Bwana linakanijia kusema”..Soma (Yeremia 1:11, Yeremia 13:3, 1Nyakati 22:8)

Wakiwa na maana ujumbe wa Mungu umenifikia kuwaambia. Hivyo biblia kwa ujumla inajulikana kama  Neno la Mungu.

Lakini pia Neno la Mungu ni jina la YESU KRISTO.

Ukisoma..

Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu….

14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.

Neno la Mungu ni nini?

Kwanini YESU aitwe Neno?

Anaitwa Neno Kwasababu yeye ndiye kinywa chote cha Mungu,(Yohana 8:38), Yeye ndio wazo lote la Mungu, yeye ndiye utimilifu wote wa Mungu kwa jinsi ya mwili (Wakolosai 2:9)..Yeye ndiye aliyepewa hukumu yote na Mungu, na yeye ndiye aliyepewa milki ya vitu vyote..

Hivyo chochote afanyacho, chochote asemacho, ni sauti ya Mungu kweli, na ujumbe wa Mungu kweli kweli kwetu..

Na ndio maana utamsoma katika Ufunuo akijitambulisha kwa jina hilo.

Ufunuo 19:12 “Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi”.

Hivyo ukiyashika maneno ya Yesu, basi umelishika Neno la Mungu, ukiyashika maagizo ya Yesu basi umeyashika maagizo yake…Naamini umeshafahamu sasa Neno la Mungu ni nini!

Bwana akubariki.

Je! Unatambua kuwa tunaishi katika siku za mwisho? Je! Una habari kuwa hili ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, na kwamba hatutakuwa na kanisa lingine zaidi ya hili,.Pengine kizazi chetu zitashuhudia tukio la ujio wa pili wa Kristo? Dalili zote zinaonyesha, Kama ni hivyo Je! Umejiwekaje tayari?..Bado upo kwenye dhambi?

Ikiwa utahitaji kumpa Yesu maisha yako leo basi uamuzi utakaoufanya ni wa busara sana, hivyo fungua hapa kwa ajili ya sala ya toba..>>>

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

NITAFUNGUAJE MILANGO ILIYOFUNGWA MBELE YANGU?

USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.

HUYU SI YULE SEREMALA, MWANA WA MARIAMU?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UFUFUO TUNAOUSUBIRIA UTAHITIMISHA YOTE.

Siku ile Bwana Yesu alipokufa biblia inatuambia makaburi yalipasuka na miili ya watakatifu wengi iliinuka, lakini katika ufufuo huo hawakuondoka pale makaburini mpaka siku Yesu alipofufuka, Ndipo wakaanza safari ya kuuelekea mji mtakatifu (Yerusalemu), Na walipofika kule biblia inatuambia wakawatokea watu wengi sana…

Lakini lipo swali tunaweza kujiuliza kulikuwa na umuhimu gani wale wafu watoke makaburini kwa kipindi kama kile, pili na ni kwanini walielekea mji mtakatifu Yerusalemu na sio mahali pengine..

Tusome.

Mathayo 27:50 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.

51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;

52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;

53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi”.

Maswali kama hayo, tukiweza kuyatafakari vizuri naamini yatatupa mwanga wa jinsi siku ile kuu ya ufufuo wa wafu(katika unyakuo) itakavyokuwa.

Sasa ni kwanini, wakati ule makaburi yapasuke na watakatifu wafufuke,..Ni kwasababu Mungu alikuwa anataka kuwathibitishia baadhi ya wale watu wake, kuwa tendo la ufufuo lipo kweli, na mwanawe Yesu Kristo amefufuka kweli kweli.. Na alifanya hivyo ili baada ya hapo wakawe mashahidi wa ufufuo wa wafu kwa watu wengine..Kwasababu wakati huo yalikuwepo makundi mengi ya watu waliokuwa hawaamini suala la ufufuo wa wafu (Masadukayo), Na wengine walikuwa wanapinga na kuwatangazia watu kuwa ameibiwa..Hivyo ili Mungu kuwathibitishia kuwa suala la Ufufuo lipo ndipo akaruhusu makaburi yapasuke, wafu wafufuke waonekane na watu wengi.

Lakini Je! Hilo lilionekana na kila mtu tu?

Jibu ni Hapana, bali lilionekana na wale watu (watakatifu) waliokuwa Yerusalemu wakati ule. Kama tu vile Bwana alivyofufuka hakumtokea tu kila mtu isipokuwa wale waliokuwa wanamwamini. Na hao wafu ni hivyo hivyo hawakuwatokea watu wote isipokuwa tu wale watakatifu..

Kwasababu biblia inatuambia wafu wale walielekea Yerusalemu. Ni kwa vile tu biblia haiwezi kueleza kila kitu, lakini tukio lile liliwaacha katika butwaa kubwa sana wale watu waliokuwa Yerusalemu..Jaribu kufikiria, unatembea kila kona unawaona ndugu zako wa kale waliokufa katika Bwana, wengi sana, unawaona waliokuwa majirani zako kitambo, na wengine wanazungumza na wewe kabisa wanakuambia mimi ni Yusufu, mimi ni Sulemani, mimi ni Yeremia n.k…

Wewe unadhani watu hao walioshuhudia utaanzaje kuwaaninisha kuwa hakuna ufufuo wa wafu? kuwa Kristo hakufufuka bali aliibiwa?

Ufufuo huo uliwapa uthibitisho mkubwa sana, Ili kwamba wakawe mashahidi wa kufufuka kwake ulimwenguni kote, hilo ndio lilikuwa lengo lake..

Lakini upo ufufuo mwingine tunaoungojea sasa, ambapo upo karibu sana kutokea kuliko tunavyofikiria..Wakati huo PARAPARANDA kuu ya Mungu italia kutoka mbinguni..Na tukio kama lile lile la kwanza litatokea kwa mara nyingine, la makaburi kupasuka..Lakini safari hii watanyanyuka watakatifu wengi sana, wa vizazi vyote vilivyotangalia duniani..watu wengi sana..

Wakati huo watakatifu walio hai hawatajua chochote kwanza, wala ulimwengu pia..Ili lile Neno la kwamba hatutawatangulia wafu waliolala litimie..

1Wathesalonike 4:15 “Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika HATUTAWATANGULIA wao waliokwisha kulala mauti.

16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; NAO WALIOKUFA KATIKA KRISTO WATAFUFULIWA KWANZA.

17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.

18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo”

Vivyo hivyo na wao hawataonekana na kila mtu tu aliye duniani…

wataonekana na watakatifu watakaonyakuliwa, (Yaani wale watu tu waliozaliwa mara ya pili ndio watakaowaona)..…na wenyewe wataenda katika mji mtakatifu (Yerusalemu ya rohoni, soma Wagalatia 4:24-31)…

Siku hiyo sisi tuliokuwa hai siku tutakapowaona, ndio tutakapojua kuwa Ufufuo wenyewe umefika, na kitendo cha kufumba na kufumbua tutatoweka, hatutaonekana tena ulimwenguni..

1Wakorintho 15:51 “ Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.

Wakati huo dunia haitaelewa chochote!. Wengi watasema wameibiwa, kama ilivyokuwa kipindi cha Bwana Yesu, wengine watasema tumepotea tu! Watapatikana n.k. Lakini suala la kwamba kanisa limenyakuliwa hilo halitaaminika na wengi hata kidogo. Kwasababu tutakuwa ni kundi dogo sana kama vile Bwana Yesu alivyosema.

Hivyo ndugu, mimi na wewe tujue kuwa tunaishi katika hayo majira ya Kunyakuliwa kwa kanisa, Dalili zote zinathibitisha hilo, hakuna asiyejua.. Lakini Swali ni Je! tumejiwekaje tayari? Je! Parapanda ikilia leo, unao uhakika wa kunyakuliwa? Kumbuka baada ya wakati huo mlango wa rehema hautakuwa tena wazi kwa ajili yetu, Bali kitakachokuwa kinaendelea duniani ni kumiminwa kwa ghadhabu ya Mungu. Na hukumu.

Muda bado tulio bakiwa nao mfupi sana. Hivyo ikiwa wewe ni mmojawapo ambaye Kristo yupo mbali na wewe, basi chukua uamuzi wa leo hii kumgeukia na atakupokea na kukufanya mwana wake.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

IJUE NGUVU YA IMANI.

KUZIMU ni mahali pa namna gani, Je! huko wanaishi watu wakifa na kwenda kupata mateso au ni vinginevyo?

USIRUHUSU MUNGU AWEKE UADUI KATI YAKO NA WATU WAKO.

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

YESU AKALIA KWA SAUTI KUU.

Yesu akalia kwa sauti kuu..


Wengi tunajiuliza ni maneno gani aliyatoa Bwana Yesu pale msalabani alipolia kwa sauti ya juu namna hiyo?

Embu tusome vifungu vyenyewe;

Marko 15:34 “Na saa tisa Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Maana yake, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

35 Na baadhi yao waliosimama pale, walisema, Tazama, anamwita Eliya.

36 Na mmoja akaenda mbio, akajaza sifongo siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha, akisema, Acheni, na tuone kwamba Eliya anakuja kumtelemsha.

37 NAYE YESU AKATOA SAUTI KUU, AKAKATA ROHO.

38 Pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini.

39 Basi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu”.

Ili kujua ni  maneno gani aliyasema, ni vizuri tukaangalia katika vitabu vingine vya injili vinasema katika wakati huo huo alipokuwa anakaribia kukata roho Tusome..

Yohana 19:28 “Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu.

29 Kulikuwako huko chombo kimejaa siki; basi wakatia sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakampelekea kinywani.

30 Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, IMEKWISHA. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.”.

Unaona hapo mstari wa 30 unaonyesha dakika ile ya mwisho kabla ya kuikata roho yake alisema haya maneno “IMEKWISHA”..

Maneno haya hakuyasema kwa unyonge, au kwa utaratibu, au kwa sauti ya kawaida kama yale mengine..Hapana, bali alipofika hapo biblia inasema AKATOA SAUTI KUU.. IMEKWISHA.

Sauti ambayo kila mmoja aliyekuwa maeneo yale aliyasikia maneno haya..kiasi kwamba Yule akida wa askari alipoona jinsi alivyokata roho kwa Tamko zito kama lile..Akakiri kuwa Yule alikuwa kweli ni mwana wa Mungu.

Yesu akalia kwa sauti kuu,

Lakini kwanini Bwana Yesu aamue kufanya vile?,

Ilikuwa ni kutuambia mimi na wewe kuwa Ile hati ya mashitaka imekwisha. Na ndio maana saa ile ile pazia la hekalu likapasuka, na kiti cha rehema kikaonekana, ikiwa na maana kuwa tangu wakati wa Kristo kufa,  rehema inapatikana bure, na kwa uwazi, sio tena nyuma ya pazia ambapo ilihitaji kuwepo na mtu wa kuwapatanisha na Mungu(Kuhani mkuu)..Lakini sasa hilo halipo tena, kwasababu hati ya mashitaka imeondolewa.

Mtu yeyote anaweza kumkaribia Mungu na kusamehewa kupitia YESU KRISTO.

Hivyo hata na wewe leo, kama ni mwenye dhambi unaweza kuupokea msamaha kutoka kwake hapo hapo ulipo. Yesu anaweza kuja ndani ya moyo wako siku hii hii ya leo, bila hata ya kuhani kuwepo karibu yako, au mchungaji, au mtu yeyote..Ni wewe tu kufungua moyo wako, na kukubali kumpokea Yesu.

Ikidhamiria kufanya hivyo alisema mwenyewe..

Yohana 6:37 “Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.”

Hivyo leo hii ukimpa maisha yako utaanza kuona badiliko la ajabu sana ndani yako. Kama upo tayari sasa kutubu dhambi zako..Basi fungua hapa kwa ajili ya sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana Yesu alisema pale msalabani naona kiu?

USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE.

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuzimu kuna nini?

Kuzimu kuna nini?


Kuzimu sio mahali pa kupatamani hata kidogo, wala sio mahali ambapo utatamani hata adui yako aingie..

Na ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya..

Marko 9:43  “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;

44  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]

45  Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum;

[ 46  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]

47  Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;

48  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki”.

Unaona, akiwa na maana kuwa kama itabidi kiungo chako kimoja tu cha thamani, kiondoke ni heri ukafanya hivyo kuliko uende kuishia huko milele.

Ikiwa unataka kujua kwa Urefu Jehanum ni nini? Unataka kujua hao funza wanamaanisha nini?, kuzimu kuna nini ,fungua hapa usome Habari yao.. >>>> Jehanamu ni nini?

Haya Maisha tuliyopewa ni ya kitambo kifupi sana, tunapaswa tujitathimini tukifa leo tutakwenda wapi ikiwa tupo nje ya Kristo? Biblia inatuambia Kuzimu haishibi watu, wala uharibifu hauna kifuniko, ikiwa na maana kuwa kila dakika, kila sekunde watu wanashuka huko wengi sana..

Lakini kwanini hayo yote yatukute angali bado tunao muda wa kutubu? Tutubu dhambi zetu, na kuyasalimisha Maisha yetu kwake, tuseme ulimwengu sasa basi, leo hii tunamgeukia Kristo.

Hivyo Ikiwa wewe ni mmojawapo ambaye unasema leo nipo tayari kumpa Yesu Maisha yangu, basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana.

Basi, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuwa na uhalali kwa kuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwabudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Hongera kwa kuokoka.

Pia nakualika kutembelea tovuti hii mara kwa mara, yapo mafundisho mengi zaidi ya 1000, na maswali mengi sana yaliyojibiwa ya kwenye biblia..

Au kama utakuwa unapenda utumiwe kwa njia ya whatsapp basi utatumia ujumbe katika namba hii +255789001312 .. Bwana akubariki sana.

Mada Nyinginezo:

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuota upo na mtu maarufu/kuota unaongea na mtu maarufu.

Kuota upo mtu na maarufu/kuota unaongea na mtu maarufu kuna maana gani?

Ndoto zipo katika makundi makuu matatu, zipo ndoto zinazotokana na Mungu, pia zipo ndoto zinazotokana na shetani, halikadhalika zipo ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe.

Ili kufahamu vizuri juu ya makundi haya. Bofya hapa usome. >>> Nitajuaje kama ndoto ni ya Mungu au ya Shetani?

Wengi wetu tunakosa shabaha pale tunapotaka kila ndoto ipatiwe tayari yake ya rohoni, lakini ukweli ni kwamba si kila ndoto inayotafsiri ya maana, husususani hizo zinazotokana na sisi wenyewe.

Sasa tukirudi kwenye swali Kuota upo na mtu maarufu/kuota unaongea na mtu maarufu kuna maana gani?

Jibu ni kwamba, ndoto nyingi za namna hii zinatokana na shughuli zetu za kila siku

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno”

Unaona Shughuli za kila siku ni Pamoja na yale mambo ambayo tunayoana mara kwa mara kila siku, au tunayasikia, kwamfano mtu kama raisi wa nchi, huyu ni mtu ambaye karibu kila siku tunamwona katika vyombo vya Habari, au tunamsikia katika radio, au tunamsoma katika magazeti, au tunamsikia akizungumziwa na watu wengine..

Ni mtu ambaye kila mmoja wetu amemkaa kichwani, kama vile tu ndugu zetu wa nyumbani. Hivyo mtu kuota raisi wa nchi, au kuota unaongea na raisi,au kuota uko na raisi si jambo la kushangaza.

Naamini ni maelfu ya watu kila siku yanamuota raisi wa nchi yao.

Na sio raisi tu, unaweza kumwota mtu mwingine yoyote maarufu, ambaye tayari anajulikana sana katika jamii, inaweza ikawa ni msanii, au mbunge, au mchungaji, au mchezaji n.k.

Hivyo ndoto ya namna hii, ikikujia usiitilie maanani sana.

Lakini ikija katika uzito wa hali ya juu, na ndoto yenyewe umeiota imeonekana kama ilikuwa ni kweli. Na ukaona kama ni bahati umekutana na mtu huyo,

Basi ujue ni Mungu anataka kukupa hisia  Fulani ya kipekee uionje pale unapokutana na mtu Fulani maarufu. Anataka uone, jinsi inavyokuwa,  ikiwa watu maarufu wa dunia hii ukikutana nao unajihisi wewe ni mtu Fulani spesheli uliyepata bahati, vipi kuhusu kukutana na yeye ambaye ni Maarufu na Mkuu kuliko watu wote na vitu vyote duniani siku ile? Utakuwa katika hali gani?

Anataka uone siku ile maelfu kwa maelfu wa watu watakapo kusanyika mbele zake , kupokea heshima zao kutoka kwake wewe utakuwa wapi?

Je! atakuita, uwe karibu naye, au atakukataa na kukufukuza?

Bwana Yesu mwenyewe alisema..

Luka 9:26  “Kwa sababu kila atakayenionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu”.

Hivyo usimwonee haya Kristo mpe leo Maisha yako. Ili siku ile, atakapopokea heshima kutoka kwa watu wote na malaika zake, basi na wewe pia akuite.

Hiyo ndio maana ya Kuota upo na mtu maarufu/kuota unaongea na mtu maarufu.

Hivyo Kama upo tayari kumpa Yesu Maisha yako leo, utataka kuongozwa sala ya toba basi fungua hapa >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ubarikiwe sana..

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

BASI MUNGU ALIMWADHIMISHA MNO.

MFALME ANAKUJA.

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

MTINI, WENYE MAJANI.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post