Je! ni kweli dunia iliumbwa takribani miaka 6000 iliyopita? na je! shetani alikuwepo duniani wakati dunia inaumbwa?

Je! ni kweli dunia iliumbwa takribani miaka 6000 iliyopita? na je! shetani alikuwepo duniani wakati dunia inaumbwa?

JIBU: Kulingana na hesabu ya vizazi na miaka yao waliyoishi katika biblia, inakadiriwa tangu Edeni mpaka wakati wa Gharika, ni miaka elfu 2, na tangu wakati wa gharika mpaka kuzaliwa kwa Bwana Yesu ilipita miaka elfu 2 hivi, na tangu kipindi cha Bwana wetu Yesu hata leo nacho pia ni kipindi cha miaka elfu 2 kimepita. Kwahiyo jumla yake tangu Edeni mpaka sasa ni miaka kama elfu 6 hivi, au imezidi kidogo au imepungua kidogo..Sasa kumbuka huo ulikuwa ni mwanzo wa Edeni, lakini haukuwa mwanzo wa Dunia..dunia ilikuwepo kabla ya Edeni..Tunasoma.
 
Mwanzo 1:1 “hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”
 
…hapa hajasema huo mwanzo ulikuwa ni wa miaka mingapi iliyopita inaweza ikawa ni miaka elfu kumi,milioni kumi au vinginevyo…
 
lakini mstari wa pili unasema nayo nchi ilikuwa ukiwa na utupu inamaanisha kuwa kuna jambo lilitokea likaifanya hiyo nchi kuwa ukiwa baada ya Mungu kuziumba mbingu na nchi na hapa si mwingine zaidi ya shetani ndiye aliyeiharibu na kuifanya ukiwa (kama anavyoendelea kuiharibu sasa hivi) maana Mungu hakuiumba ukiwa yaani dunia iwe ukiwa bali ikaliwe na watu,
 
Isaya 48:18 inasema
 
18 Maana Bwana, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine. “.
 
Lakini baada ya dunia kuharibiwa kwa viwango vya hali ya juu, ikapoteza umbo lake ikawa kama moja ya sayari nyingine, na ndio tunaona Mungu akaanza kufanya uumbaji upya baada ya nchi kukaa muda mrefu katika hali ya ukiwa, hapo mbingu na nchi zilikuwa tayari zimeshaumbwa muda mrefu nyuma.
 
Kwahiyo mwanadamu na viumbe vyote inakadiriwa viliumbwa takribani miaka  6000 iliyopita lakini dunia iliumbwa kabla ya hapo na shetani alikuwepo duniani kabla ya mwanadamu kuumbwa, kwasababu tunamuona alionekana katika bustani ya Edeni na biblia inamwita shetani kama yule nyoka wa zamani
 
Ufunuo 20:2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;,
 
kwahiyo inamaanisha alikuwepo toka zamani kabla hata ya mwanadamu kuumbwa, ambapo tunaona alitupwa huku duniani baada ya kuasi mbinguni pamoja na malaika zake.
 
Ubarikiwe sana.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada zinazoendana:

JUMA LA 70 LA DANIELI

Kati ya Unyakuo wa kanisa, Dhiki kuu, Vita vya har-magedoni, Utawala wa miaka 1000, Vita ya Gogu na Magogu, hukumu ya kiti cha enzi cheupe. Je, ni kipi kinaanza na kingine kufuata?

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA!


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments