Maadamu tunaishi hapa duniani, kila siku tupo mapambanoni….Unapomwamini Yesu Kristo tu na kuamua kumfuata kwa moyo wote, kwa kitendo hicho tu tayari umeshatangaza vita na ufalme wa giza..Na vita hivyo huna budi kuvikabili mpaka siku unaondoka hapa duniani. Hakuna siku hivi vita vya imani vitaisha..utapitia hiki, utatulia kidogo ghafla kitanyanyuka kingine, lakini Bwana atakuwa upande wako kukupa ushindi. Lakini shetani huwa hakati tamaa kama sisi wanadamu…Kuanzia mwanzo wa safari yako mpaka mwisho utakuwa vitani tu!…kwahiyo jiandae kwa hilo…Kama alikupa shamba wakati ukiwa wake, leo umemsaliti atalidai shamba lake, kama alikupa heshima hiyo heshima atakunyang’anya na atawatumia watumishi wake.
Tunaweza kujifunza kwa ufupi kwa Bwana wetu Yesu, jinsi shetani alivyoanzana naye kwenye huduma yake na alivyomaliza naye. Inadhaniwa na wengi kuwa siku ile shetani alipomjaribu Bwana kule jangwani ndio ilikuwa mwisho wa majaribu.. Lakini nataka nikuambie sivyo!…Ndio ilikuwa ni mwanzo tu wa majaribu…ingekuwa ndio ilikuwa mwisho sidhani kama Bwana angesulubiwa…Hebu tusome.
Luka 4:12 “Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
13 Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha AKAENDA ZAKE KWA MUDA”.
Nataka uone hicho kipengele cha mwisho kinachosema “akaenda zake kwa muda!”…Maana yake ni kwamba atarudi tena baadaye!. Anakwenda kuandaa vita vingine vipya..hivyo kakubali kashindwa lakini hiyo haimpi sababu ya kukata tamaa…Na utaona aliporudi tena alirudi kwa nguvu nyingi akishindana na Bwana kupitia watu na wakuu…Aliwavaa mpaka viongozi wa dini wakubwa, na wakuu wa nchi kupambana na Yesu…Mpaka ilifikia wakati mfalme Herode anatafuta kumuua Bwana Yesu. Hebu jiweke kwenye nafasi kama hiyo,!..viongozi wa dini wanakupinga! Na bado mkuu wa nchi anatafuta kukuua?..Bila shaka hivyo ni vita vikali sana..
Na haikutosha hapo, kuonyesha jinsi gani shetani hakati tamaa…japokuwa alimshindwa, lakini bado hata wakati yupo pale msalabani anamjia tena na kumwambia maneno yale yale kama aliyomwambia kule jangwani… “ikiwa kweli wewe ni mwana wa Mungu jishushe msalabani!”…bado anaamini anaouwezo wa kumwangusha Bwana hata akiwa bado amebakisha dakika moja ya pumzi ya uhai wake…Mpaka sekunde ya mwisho Bwana yupo vitani.. Na ndio maana Bwana aliwaambia hivi wanafunzi..
Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.
Sasa dhiki inayozungumziwa hapo ndio hayo majaribu…Na mfano wa dhiki hizo sio kuvunjiwa bar yako iliyokuwa inakupatia kipato, au kuibiwa fedha zako na mfanyakazi wako wa Bar!…au kupigwa baada ya kufumaniwa, au kuingizwa jela baada ya kushikwa unaiba!… Hapana hizo sio dhiki(sio vita vya imani) bali ni majibu ya dhambi zako!…Dhiki hasa ni zile unazozipitia baada ya wewe kuukataa ubaya!..mfano unafukuzwa kazi kwasababu umekataa kufanya uasherati, unasingiziwa kitu Fulani kwasababu umekataa kwenda katika njia zao, unachukiwa na kutengwa kwasababu umebadilisha njia zako na umeacha kuwa wa kidunia au kuabudu sanamu, au mizimu au kufanya matambiko…Mfano wa dhiki hizo ndio majaribu..
Kwasababu majaribu haya yataendelea mpaka mwisho wa maisha yetu!..biblia inatuonya TUVUMILIE! Na TUSTAHIMILI na pia tusiogope!…kwasababu Bwana atakuwa upande wetu kutusaidia tukijua kuwa lipo taji la uzima linatungojea huko mbeleni.
Yakobo 1:12 “Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea TAJI YA UZIMA, Bwana aliyowaahidia wampendao”.
Ufunuo 2:9 “Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.
10 USIOGOPE MAMBO YATAKAYOKUPATA; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa TAJI YA UZIMA”.
Bwana akubariki.
Kama hujaokoka, mlango wa neema upo wazi..lakini hautakuwa hivi siku zote…nyakati hizi muda unaenda kwa kasi sana…kufumba na kufumba dunia itaisha..na utaanza utawala mpya wa Bwana wetu Yesu Kristo..ambapo Huko atawalipa watakatifu wake kwa kadri ya Uvumilivu wao…Waliostahimili zaidi watapewa thawabu kubwa zaidi..Bwana atusaidie tufike huko.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?
Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.
Tunaweza kujiuliza maswali mengine ni kwanini mara nyingi malaika walipokuwa wakishindana na shetani, hawakutumia uweza wao wote kupambana naye,bali walimwachia Mungu aamue, japokuwa walikuwa na mamlaka na uwezo wa kufanya lolote juu yake..
Tunaweza kuona baadhi ya maeneo katika biblia, kwamfano kama lile tukio la Yoshua kuhani mkuu alipokuwa anahudumiwa na Yule malaika, na shetani naye akiwa pembezoni mwao kulipinga kusudi la Mungu..Utaona pale yule malaika hakutoa maneno ya kulaani , japokuwa ibilisi ni mlaaniwa sikuzote..bali alisema..
Zekaria 3:1 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye.
2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni”?
Unaona? Sehemu nyingine tena ni pale Mikaeli alipopewa jukumu la kuuhifadhi mwili wa Musa, lakini shetani akatokea ghafla ili kushindana naye lakini utaona hakudiriki, kumtamkia hukumu palepale, japokuwa tayari ibilisi ni mlaaniwa, badala yake alimkabidhi Mungu hukumu yote..
Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee’.
Kama hilo halitoshi, malaika watakatifu bado, wanapotuona tunafanya mambo yasiyompendeza Mungu, wanaporudisha ripoti mbinguni juu ya mienendo yetu duniani, wanapofika mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, hawatupelekei yale mashitaka mabaya kwa Mungu, wanajaribu kuyasitiri kwa kadiri wawezavyo, Uone jinsi wanavyoogopa hata kutoa neno la laana kwa kiumbe chochote cha Mungu kiwe ni kizuri au kibaya..
2Petro 2:11 “Wenye ushupavu, wenye kujikinai, hawatetemeki wakiyatukana matukufu; IJAPOKUWA MALAIKA AMBAO NI WAKUU ZAIDI KWA UWEZO NA NGUVU, HAWALETI MASHITAKA MABAYA JUU YAO MBELE ZA BWANA.
12 Lakini hao kama wanyama wasio na akili, ambao walizaliwa kama wanyama tu wa kukamatwa na kupotezwa, wakikufuru katika mambo wasiyoyajua, wataangamizwa katika maangamizo yao”
Hiyo ni kutufundisha na sisi pia tunavyopaswa tuchukuliane na maadui zetu mbele za MUNGU, Pale wanaposhindana na sisi, Je na sisi tushindane nao kwa kuwalaani au kuwalaumu?..Pale unaposikia umesengenywa kidogo je na wewe uende kuwaombea mabaya mbele za Mungu, wapigwe? Je! wewe ni mtu wa kupeleka mashitaka tu kila siku zote mbele za Mungu..Huna lingine..?
Wapigwe, waangushwe, warudishwe nyuma, wafedheheshwe, ni hayo tu ndio tunayoweza kumwambia Mungu kwenye maombi yetu ya kila siku?, Hatuna Muda wa kumuomba Mungu ufalme wake uje juu ya roho zetu kama Bwana alivyotufundisha, sisi ni kushindana na maadui zetu ?
Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.
10 Lakini watu hawa huyatukana mambo wasiyoyajua, na mambo wayatambuayo kwa asili wajiharibu kwayo kama wanyama wasio na akili.
11 Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya Kora”.
Kaka/Dada watu watakaokwenda kinyume na wewe watakuwepo tu daima kutupinga, lakini sisi tumwachie hayo Mungu ayashughulikie kama wafanyavyo malaika, tuendelee na kusudi lililotuleta hapa duniani la kumtafuta Mungu na hiyo ndio ishara nzuri ya unyenyekevu tunayopaswa tuige kwa malaika watakatifu dhidi ya maadui zetu (wanadamu).
Mithali 24:17 “Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;
18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?
SWALI: Nina swali juu ya uchawi, Biblia iliposema kuwa usimwache mwanamke mchawi kuishi ilimaanisha nini?
JIBU: Katika agano la kale Mungu aliwapa wana wa Israeli hukumu…akawaambia wazishike hizo..na hukumu hizo ni kwa wale wote watakaokwenda kinyume na Torati…Kwamfano Torati ilikataza KUZINI..Mojawapo wa zile amri kumi ilikuwa ni USIZINI.
Hivyo mwanamke/mwanamume yeyote atakayeivunja hiyo sheria..adhabu yake ilikuwa ni KIFO!..Na walioitekeleza hiyo hukumu walikuwa ni hao hao wana wa Israeli kufuatia maagizo waliyopewa na Mungu mwenyewe…Kwamfano mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, adhabu yake ilikuwa ni kupigwa mawe mpaka kufa!..aliyekamatwa vilevile analala na mnyama adhabu yake ilikuwa ni kifo,
Hebu tusome baadhi ya hukumu hizo
Walawi 20:10 “Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa.
11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.
12 Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo uchafuko; damu yao itakuwa juu yao.”
Kutoka 22: 19 “Mtu awaye yote alalaye na mnyama sharti atauawa”.
Na sio hizo tu!…kulikuwa na sheria zilizokuwepo za kumuua ndugu yako wa damu endapo atakwenda kuabudu miungu mingine tofauti na Mungu wa Israeli. Na zaidi ya hayo Mungu alikataza shughuli zozote za kishirikina na kichawi katika Taifa takatifu la Israeli..
Kumbukumbu 18: 9 “Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.
10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,
11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, WALA MCHAWI, wala mtu awaombaye wafu.
12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.
13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako”.
Sasa yeyote Yule aliyekiuka amri hiyo Mungu aliyoitoa ya kutojihusisha na ushirikina na uchawi..hukumu yake ilikuwa ni kifo tu!..Ndio hapo Musa akaiandika hiyo hukumu katika..
Kutoka 22:18 “Usimwache mwanamke mchawi kuishi. 19 Mtu awaye yote alalaye na mnyama sharti atauawa”.
Maana yake mwanamke/mwanamume akikamatwa katika ushirikina ni kuuawa kwa aidha kupigwa kwa mawe au kwa vyovyote vile…(ilimradi afe tu)
Kwahiyo sheria ya kuwaua wachawi ilikuwepo kama tu sheria ya kumuua mwanamke aliyekamatwa katika uzinzi..
Lakini sasa katika agano jipya la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo..wanadamu hatujapewa tena mamlaka ya kuhukumu kutoka kwa Mungu, kama wana wa Israeli walivyopewa amri ya kuhukumu na Mungu mwenyewe. Hatuna tena hukumu ya jino kwa jino, jicho kwa jicho, mguu kwa mguu, Wakati huu wa sasa wa agano jipya, Hukumu yote amekabidhiwa Yesu Kristo.
Yohana 5:22 “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, BALI AMEMPA MWANA HUKUMU YOTE”
Umeona hapo? Mwana (yaani Yesu Kristo) Ndio kakabidhiwa hukumu yote sasa…na ndiye atakayewahukumu walio hai na walio kufa (Kasome 2Timotheo 4:1)…hakuna tena mtu yeyote mwenye mamlaka ya kumuua mwanamke aliyeshikwa katika uzinzi, wala kumuua mtu aliyekamatwa analala na mnyama wala kumuua mwanamke/mwanamume aliyekamatwa katika uchawi. Hukumu hizo Yesu Kristo ndio kakabidhiwa na Baba, na sasa ametupa neema….Ambapo tunamkosea Mungu lakini tuna nafasi ya kutubu kabla ya kuhukumiwa…
Maasi tunayoyafanya sasa tunastahili kuhukumiwa na Bwana Yesu papo kwa hapo!!…lakini tumependelewa na kupewa nafasi ya kukimbilia msalabani na kupata msamaha kabla ya hukumu ya mwisho!…Utafika wakati hii neema itaisha na huyu Yesu Kristo tunayemwona sasa anayeturehemu bure watu tusiostahili kurehemiwa, atafunga mlango wa Neema na atasimama kwenye kiti chake cha hukumu na atawahukumu wazinzi wote, wachawi wote na watenda dhambi wote kwa kuwatupa katika ziwa la moto..Lenye adhabu kali kuliko ya kupigwa kwa mawe.
Hivyo haturuhusiwi kwa namna yoyote kuwaua wezi kwa kuwapiga kwa mawe,wala kuwaua tuliowafumania katika uzinzi wala tuliowakamata katika uchawi, wala kulaani mtu yeyote yule..kwa kuutumia huo mstari wa “usimwache mwanamke mchawi kuishi”..Wasiolielewa Neno ndio wanaoutumia huo mstari kwa kukosa maarifa…lakini mimi na wewe tusikose hayo maarifa…Kwasababu hakuna astahiliye kuhukumu sasa isipokuwa Mwana wa Mungu pekee.
Jukumu letu ni sisi kuomba kwa bidii dhidi ya nguvu zote za giza, kwamba zisiwe na nguvu juu yetu, wala juu ya watu wetu na familia yetu, na vitu vyetu…na kumwomba Mungu awaokoe ndugu zetu waliozama katika nguvu za giza, ambao wanatumika na mamlaka ya giza aidha kwa kujua au kwa kutokujua, kwasababu nao pia ni watu kama sisi wanaohitaji wokovu, na sio kutafuta njama za kuwaua,au kuwaombea vifo ni kinyume na maandiko…
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kwanini Bwana aliongea na Abramu baada ya kutengeana na Lutu?
…Japokuwa ameokoka katika bahari,haki haimwachi kuishi…
Ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu, unapaswa ujue kuwa kuna wakati sio mambo yote yataenda vizuri kama unavyofikiri, Hilo ni vizuri ukaliewa kwasababu watu wengi wameishia njiani na kuona kama wokovu ni mgumu wakidhani kuwa ndio utaendaelea kuwa hivyo hivyo wakati wote.
Biblia ni kitabu ambacho kimeturahisishia kuielewa vizuri hii njia ya imani, kiasi kwamba yale ambayo tunaona kama sisi ndio wa kwanza kuyapitia, Kumbe tayari wengine walishayapitia zamani sana huko nyuma, na hivyo Habari zao zikaandikwa ili kututia moyo na kutupa nguvu sisi tuliotokea huku mwishoni.
Sasa tusipokuwa watafakariji wazuri wa maandiko namna hiyo, hapo ndipo shetani anapata njia rahisi ya kutuangusha katika hatua za awali kabisa za wokovu wetu.
Leo tutakiangazia kile kisa cha Mtume Paulo, baada ya kufungwa na kusafirishwa kupelekwa Rumi kutoka Yerusalemu, sasa Ili kuifanya Habari kuwa fupi, ni kwamba safari ile ilikuwa ni ya kufa na kupona, bahari iliwachafukia katikati ya vilindi, dhorubu kali iliwakumba, kaisi kwamba hawakuona jua wala nyota kwa siku nyingi..Yeye akiwa kama mmojawapo wa mfungwa, wakiwa wameishiwa chakula kutokana na kwamba shehena nyingi za hazina zilitupwa baharini ili kuifanya meli iwe nyepesi, sasa wakiwa katikati ya njaa kali ,anasema walifikia hatua wakakata tamaa ya kuokoka.. kwa jinsi hali ilivyokuwa mbaya, mpaka kuvunjikiwa meli yao, na kunusurika kibahati bahati kwa neema za Mungu..(Soma Habari hiyo yote katika Matendo 27&28).
Lakini walipofika kwenye kisiwa kimoja walichotulia, wakiwa wamepewa hifadhi kwa muda na wenyewe wa pale, wakati wa usiku wanaota moto, Paulo akiwa ameshika mzigo wa kuna, ghafla akatokea nyoka (jamii ya kifutu), akajifiringisha na kujikaza kwa nguvu mkononi mwake, Wenyeji kuona vile wakasema huyu ni lazima atakuwa Muuaji tu, japokuwa kanusurika kule baharini, lakini haki haimwachi aishi, ..Tusome..
Matendo 28:3 “Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni, na kuuweka motoni, nyoka akatoka kwa ajili ya ule moto akamzonga-zonga mkononi.
4 Wenyeji walipomwona yule nyoka akilewa-lewa mkononi, wakaambiana, Hakosi mtu huyu ni mwuaji; ambaye ijapokuwa ameokoka katika bahari haki haimwachi kuishi.”
Jaribu kutengeneza picha, jinsi Paulo alivyokuwa anaonekana mbele za watu wakati huo, kwasasa watu wanaweza kusema, Ana Nuksi huyu, ana mikosi, ni laana za wazazi wake zinamwandama, au za ukoo.. haiwezekani apitie shida tu yeye sikuzote..
Kwanini afilisike, kwanini nyumba yake iinguliwe na moto, kwanini aibiwe mali zake, kwanini afiwe na Watoto wake wote watatu kwa mpigo.. Kama Mungu yupo naye, si angemuepusha na mambo hayo yote? Mungu gani huyo.. Kwanini akose mahali pa kulala, n.k.n.k.
Maneno mengi sana yanaweza kuzuka, kwa njia hizo, Lakini Paulo alipoumwa na nyoka yule mwenye sumu kali, kwasababu nyoka wale wanakufanya uvimbe kwa haraka, na baadaye damu inaganda, na kisha kukutwa na kifo cha ghafla kama hutawahishiwa matibabu.. Lakini Paulo hakuhitaji matibabu yao, bali alimtupa motoni akatulia kimya..
Muda ukapita, masaa yakapita, siku ikapita wakaona mbona havimbi, mbona haonyeshi hata dalili ya kuumwa.. Ndipo zile shutma zao zikageuka kuwa kitu kingine.
Matendo 28:5 “Lakini yeye akamtukusia motoni asipate madhara.
6 Wao wakadhani ya kuwa atavimba au kuanguka chini kwa kufa ghafula; na wakiisha kumwangalia sana, na kuona kwamba halimpati dhara lo lote, wakageuka, wakasema kwamba yeye ni mungu”.
Jambo tunalopaswa tujifunze (Sisi kama watakatifu), ni kuwa si kila tatizo ni Mkosi, au laana, au mapigo wala matokeo ya uchawi..…
Hapana, mengine Mungu anayaruhusu tu, kwasababu lipo kusudi anataka kulipitisha nyuma yake.. Kama Paulo asingeumwa na nyoka , wasingemwamini pale alipokuwa anawahubiria Habari za Kristo na uponyaji wa kiungu. Lakini kwa tukio lile baada ya muda Mungu alitukuzwa.
Vivyo hivyo na sisi, tukijijua maadamu hatuna tatizo lolote na Mungu wetu, basi tutulie kimya tuiache mitazamo ya watu ipite, lakini wakati utafika watagundua kuwa haukuwa na nuksi, au mkosi, bali ulikuwa katika njia ya mafanikio yako rohoni.
Lakini ikiwa wewe ni mwenye dhambi, hilo ni jambo lingine. Hapo Mungu hausiki, ni vizuri ukampa Kristo Maisha yako, shetani hana urafiki na wewe, ukifa leo mwisho wako utakuwa ni kuzimu na ndicho anachokitafuta na kukifurahia..Biblia inasema..
1Petro 4:18 “Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?”
Jiulize utaonekania wapi siku ile? Kama leo hii hutampokea Kristo?
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA
Mtu astahiliye hofu ni yupi?
KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.
WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.
KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?
TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.
SWALI: Waebrania 1:7 “Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto”..Je Mungu anawageuza malaika zake kuwa mapepo?
JIBU: Ndio! Wale malaika walioasi mbinguni waligeuka na kuwa mapepo baada ya kutupwa duniani, ndio haya yanayowasumbua wanadamu leo. Lakini mstari huo hapo juu hauzungumzii roho za malaika walioasi(yaani mapepo)… bali unazungumzia juu ya upepo huu wa asili(yaani hewa iliyopo kwenye mwendo). Sasa sio kwamba Mungu anawageuza na kuwafanya upepo hapana bali anafananisha na upepo malaika wake. Ili kuelewa hilo Zaidi tusome mstari ambao umelizungumzia jambo hilo vizuri..ambao ndiko Mtume Paulo aliko linukuu..
Zaburi 104:1 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Umejivika heshima na adhama.
2 Umejivika nuru kama vazi; Umezitandika mbingu kama pazia;
3 Na kuziweka nguzo za orofa zake majini. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, Na kwenda juu ya mabawa ya upepo,
4 HUWAFANYA MALAIKA ZAKE KUWA PEPO, NA WATUMISHI WAKE KUWA MOTO WA MIALI
5 Uliiweka nchi juu ya misingi yake, Isitikisike milele”.
Katika mistari hiyo unaona Mungu anavifananisha vitu vya asili kama hifadhi yake..utaona anasema umejivika nuru kama vazi!..kiuhalisia Nuru haliwezi kuwa vazi…hali kadhalika anasema ameyafanya mawingu kuwa kama gari lake, vilevile mawingu hayawezi kuwa gari…lakini kwake yeye ni kama gari…na mbingu amezifananisha kama pazia, hizo zote ni lugha za picha tu..ni kama isemavyo kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa Taifa…kuonyesha kilimo ni kama vile mfupa uliopo nyuma ya mngongo wa mtu unaoufanya mwili uwe wima. Pasipo huo mwili hauwezi kusimama vivyo hivyo pasipo kilimo nchi haliwezi kuwepo!
Na hapa Mungu anawafananisha Malaika wake na upepo…Upepo ndio unayoyafanya mawingu yatembeee, kama vile ulivyo wa muhimu kwa merikebu baharini, bila upepo mawingu hayawezi kutembea, wala merikebu haziweki kutembea, wanasema Upepo ndio kitu chenye nguvu kuliko vitu vyote vya asili, hata majini hayakuti….na hapo tayari Mungu kashayafananisha mawingu na gari lake ambalo linakwenda juu ya upepo. Ikifunua kuwa malaika wana sehemu kubwa katika kulitimiza kusudi la Mungu na kulisogeza mbele kusudi lake.
Lakini ukisoma hiyo Waebrania utaona, Yesu Kristo ambaye ni Mwana wa Mungu, yeye hajafananishwa na upepo kama Malaika…Yeye amefananishwa na yule aketiye juu ya kiti cha enzi mwenyewe ndio maana anaitwa (chapa ya nafsi ya Mungu)..Alipopaa alikwenda kuketi katika mkono wa kuume wa Mungu Baba, hivyo ni mfano wa Baba, yeye naye mawingu yatakuwa ni Gari lake, na Malaika ni kama upepo wa kulisukuma gari lake..Ndio maana biblia inasema hapo “amefanyika bora kuliko malaika”…Haleluya!..
Na kwakuwa yeye kafanyika bora, na wale waliomwamini na watakaomwamini..watafanyika bora kama yeye..kwasababu yeye alipo ndipo na sisi tutakapokuwepo. Na hapo ndipo malaika wanatuhudumia (Waebrania 1:14)
Atukuzwe Mungu kwa kumtoa mwanawe kwaajili yetu.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UCHAWI WA BALAAMU.
FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.
KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.
MTANGO WA YONA.
NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.
MAJESHI YA PEPO WABAYA.
KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.
SWALI: Mathayo 23:39 “Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, AMEBARIKIWA AJAYE KWA JINA LA BWANA.”
JIBU: Ukisoma kuanzia juu utaona habari hiyo alikuwa anaizungumza Bwana Yesu alipokuwa anaingia Yerusalemu, Na kuona jinsi mji ule ulivyo mkataa, na kukataa wokovu tangu zamani za Manabii wa agano la kale hadi wakati wake, Na jinsi ulivyowaua wale wajumbe wote waliotumwa kwake,..Ndipo hapa sasa Yesu akautabiria kuwa atauacha katika hali ya ukiwa mpaka hapo watakapogeuka..
Embu tusome..
Mathayo 23:37 “Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
38 Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
39 Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana”.
Unaona, Na historia inaonyesha kweli, Wayahudi waliachwa na Mungu, tangu huo wakati hadi sasa ni miaka 2000 imeshapita, bado hajawarudiwa na mji wa Yerusalemu nao ulikuwa ni magofu tangu zamani, ni karne za juzi juzi tu ndio umeanza kujengwa tena na kukaliwa na watu.., lakini Bwana hakuishia tu pale, bali alisema, utaendelea kuwa hivyo hivyo katika hali ya ukiwa mpaka siku hiyo watakaposema tena Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana..Yaani ikiwa na maana watakapotubu na kumtambua Kristo kuwa ni yule masihi kweli..
Lakini ni kwanini aseme “hata mtakaposema, AMEBARIKIWA AJAYE KWA JINA LA BWANA.” Na si mpaka hapo mtakaposema mimi ni Masihi?
Utakumbuka tukio lililotendekea nyuma kidogo kabla hajafika Yerusalemu alikuwa anaimbiwa hayo maneno Hosana, Hosana Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana…
Na ndio maaana utaona Bwana akitumia maneno hayo hayo tena kuashiria kuwa mpaka siku wayahudi watakapompokea yeye kwa namna hiyo hiyo, ndipo wokovu utageuka kwao. Na dalili zote zimeshaanza kuonekana sasa, Israeli imeshakuwa taifa huru, wayahudi wanaanza kuyagundua makosa yao kidogo kidogo..Je! Unadhani ni kitu gani kitatokea muda mfupi baadaye.. Bila shaka watamgeukia na kutubu..Na biblia inasema siku watakapomgeukia uovu wao utaondolewa wote ndani ya siku moja..
Kama unabii inavyosema..
Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.
11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido.
12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;
13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.
14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.
Sasa tukishaona mambo hayo yanatokea, basi ujue kuwa Neema ya wokovu imeshaondoka kwetu, na Unyakuo tayari umeshapita.
Ni nyakati za mwisho tunazoishi, Je, bado na wewe upo vuguvugu? Unataka na wewe uachwe ukiwa kwa mfano wa Wayahudi walivyoachwa zamani kwa kutokutubu kwao? Wakati ambao utamtafuta Bwana hutamwona, utautafuta wokovu hutaupata?. Usitamani kabisa wakati huo ukukute hali bado upo dhambini, tubu, itii injili inapohubiriwa kwako kila siku,..UNYAKUO upo mlangoni.
Maran atha!.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Ujana ni wa thamani..hususani unapotumika vyema…Na kila mahali panaitaji vijana kwaajili ya nguvu kazi, nchi inahitaji vijana kwaajili ya nguvu kazi, shetani naye anawahitaji vijana zaidi kuliko wazee kwa ajili ya nguvu kazi zake…Hali kadhalika Roho Mtakatifu anawahitaji vijana pia.
Na takwimu zinaonyesha kuwa kipindi cha kati ya miaka 13-20 ndio kipindi ambacho watu wengi wanausikia wito wa ki-Mungu, 21-30 mara nyingi ni kipindi cha madarasa ya kiroho na 30-50 ni wakati wa kazi… Sasa ni wachache sana wanapata neema ya kuvutwa kwa Kristo wakiwa na miaka 40 au 50… Utakuwa umepewa neema kubwa sana kama utampokea Kristo katika umri huo Kwasababu ujana pia unathamani mbele za Mungu…
Sasa katika umri wa ujana…Ndio wakati wa kuwa na nguvu nyingi za kiroho..(hiyo ni neema ya kipekee ambayo Mungu anaiachia kwa vijana tu)..haiwahusu wazee.
1Yohana 2:14 “Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna NGUVU, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, NANYI MMEMSHINDA YULE MWOVU”.
Kama vile nguvu kazi ya Taifa ni vijana, vivyo hivyo Taifa la Mungu linajengwa na vijana watakatifu, kwasababu hao ndio wamepewa nguvu!..wazee hawana nguvu hizo..Kwahiyo UJANA ni wa kuuthamini sana.
Mtume Paulo mwishoni mwa huduma yake, alilijua hilo ndipo akatafuta vijana kadha wa kadha kwaajili ya kazi maalumu ya kuujenga ufalme wa Mbinguni…Baadhi yao walikuwa ni Timotheo na Tito. (walikuwepo wengi lakini hebu tuwatazame hawa wawili).
Hawa ni vijana ambao Mtume Paulo aliwaandaa..akawa anawatuma pia…walikuwa ni vijana tu! Labda miaka 20-25 hapo!..Lakini walikuwa wanaifanya kazi kubwa Sana! na kuleta uharibifu mkubwa kwenye ufalme wa giza…Mpaka Paulo ilimbidi kuwaandikia nyaraka zao binafsi, Timotheo alipewa jukumu kubwa sana la kuyasimamia makanisa yaliyopo Asia, na Tito naye hivyo hivyo, Huyu Tito Mtume Paulo alimpa jukumu kwa uwezo wa Roho wa kuteua maaskofu wa kanisa, ambao walikuwa ni wa umri mkubwa kuliko yeye…
Hebu jiulize ni kijana lakini ndiye anayesimamia makanisa yote na ndiye anayepewa jukumu la kuteua wazee na maaskofu wa makanisa…(kasome kitabu cha Tito chote utaona) na Timotheo naye ni hivyo hivyo, alikuwa ni kijana mdogo lakini alipewa majukumu kama hayo kasome 1Timotheo 3, na utaona kwa majukumu hayo Mtume Paulo alikuwa anawaasa pia wakaripie na kukemea na kuwaonya wazee kama wazazi.
Lakini lililo kubwa na muhimu pia Mtume Paulo alilowaasa hawa vijana ni kwamba MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO!..Hebu tusome kidogo
1Timotheo 4:12 “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi”.
Huyu ni Timotheo, hebu tumwangalie na Tito naye..
Tito 2:15 “Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote”.
Maana yake unapofika wakati wa injili, Hubiri injili usitazame uso wa mtu au kichwa cha mtu kina mvi kiasi gani….Sema kwa ujasiri kwamba WAZINZI WOTE WASIPOTUBU WATAKWENDA MOTONI !!!…usijiangalie wewe ni mdogo na wao ni wakubwa!!..kwamba watakudharau..Kile kitu ambacho Roho Mtakatifu amekiweka ndani yako kizungumze kwasababu ni Mungu ndiye aliyekuambia ufanye hivyo na sio wao!!… Na utaona wote unaowahubiria hata kama wana umri wa Baba yako wanakuja kwa Kristo..Kwasababu Injili ni Uweza wa Mungu uletao wokovu. Hivyo usiudharau ujana wako wala mtu yeyote asikudharau.
Ukidharauliwa na kuambiwa wewe hujui kitu..puuzia hayo maneno!..Lihubiri Neno kwasababu kuna nguvu nyingi za Mungu katika ujana kuliko walizonazo wazee.. Na shetani analijua hilo ndio maana hawapendi vijana na ndio anaowatafuta wengi awaangushe.
Lakini pia Mtume Paulo aliwaonya hawa vijana kwamba wazikimbie TAMAA ZA UJANANI! Katika utumishi wao.
1Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.
Maana yake ni kwamba ujanani kuna vishawishi vingi,na kuna tamaa nyingi…(sio kwamba ukishakuwa mtumishi wa Mungu kijana basi ndio hautakutana na vishawishi/tamaa)…Utakutana navyo lakini biblia imesemaje? TUZIKIMBIEEE…na sio TUZIOMBEEE…Hakuna maombi yeyote ya kuziepuka tamaa wala kuzishinda!…Hakuna maombi yoyote ya kuepukana na uasherati na ulevi na uzinzi!!..HAKUNA! wala usidanganywe na mtu yeyote hata anayejiita mtumishi! …suluhisho ni kuzikimbia…maana yake ni kwamba kama ulikuwa unamahusiano au unaona kuna dalili ya kuzama kwenye uasherati na mtu Fulani, unajiepusha naye! Sio unamwomba Mungu akuepushe naye! Ni wewe ndiye unayeanza kujiepusha naye..unakata mazoea naye.…kadhalika kama ni marafiki ndio waliokuwa wanakushawishi kwenda kuzini kwa mazungumzo yao au tabia zao..unajitenga nao…huko ndiko kuzikimbia tamaa….Yusufu alimkimbia mke wa Potifa hakumwombea!.
Picha za uchi na pornografia unazoziangalia kwenye simu ndizo zilizokuwa zinakupeleka kujichua na kufanya uasherati…hakuna maombi yeyote katika maandiko ya kuiondoa hiyo tabia!…Suluhisho ni wewe kuamua kuachana na hiyo tabia…kufuta hizo picha kwenye simu yako na kama bado inakushinda unajikuta unazifungua, badilisha hiyo simu yako ya smart unayoitumia na anza kutumia simu ya tochi!..Hilo tatizo utakuwa umelitatua moja kwa moja/umelikimbia….Biblia inasema kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate, ili usije ukapoteza roho yako yote..
Usisubiri ujana wako uharibiwe na ibilisi, umri ulionao ni wa thamani, kama hutastuka leo, utafika wakati utajuta sana kwanini hukumtumikia Mungu katika ujana wako. Zinduka usingizini.
Bwana akubariki, kijana!..
Kama hujampa Kristo maisha yako, basi tayari yapo mikononi mwa shetani hata kama utakuwa hujui…Kuwa nje ya Kristo tayari upo kinyume cha Kristo kwasababu hukusanyi pamoja na Kristo, Na hivyo unatapanya..(Mathayo 12:30). Hivyo geuka leo mpe maisha yako, ujana wako unathamani sana katika ufalme wake…Wengi watabadilika kupitia wewe endapo utakubali kumtii Kristo, na siku ile utapewa taji ya Uzima.
Maran atha!.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Madhara ya kutoa mimba rohoni.
Licha ya kwamba yapo madhara mengi ya mwilini mtu atakayoyapata kwa kutoa mimba, hata wakati mwingine kukumbwa na mauti au kuharibika kwa kizazi kabisa, lakini yapo madhara mengine ya rohoni ambayo ni makubwa zaidi ya hayo mtu atayapata ikiwa atajaribu kikifanya kitendo hicho ..Haijalishi atafanikiwa kutoa mimba mara nyingi kiasi gani bila kupata tatizo lolote la kiafya, bado lakini yapo madhara makubwa sana ya rohoni atakumbana nayo katika maisha yake yote atakayoishi duniani..
Mungu alimwambia Nabii Yeremia maneno haya;
Yeremia 1:5 “Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa”.
Natamani sana hili Neno lingezama katika moyo wa kila mwanamke ambaye anafikiria kwenda kutoa mimba. Kwamba Kulingana na maneno hayo Mungu huwa unamwandaa mtu kabla hata hajatungishwa mimba na ndio maana anasema ‘Nalikujua’, na pale anapotungishwa, anakuwa tayari ni mtu kamili, na wakati huo huo Mungu ‘Anamtakasa’, kwa ajili ya kutimiza kusudi Fulani maalumu duniani.
Na wengine utaona wanajazwa na Roho Mtakatifu hata wakiwa bado angali wapo katika matumbo ya mama zao. Mfano mmojawapo ni Yohana Mbatizaji..
Luka 1:15 “Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye”.
Hivyo kazi ya Mungu kwa mwanadamu huwa inakamilika tangu akiwa tumboni mwa mwanamke. Sasa pale mtu anapojaribu kulikatisha kusudi hilo la Mungu juu ya kiumbe hicho cha Mungu kwa kutoa mimba, Basi moja kwa moja anakuwa ametiza dhambi kubwa sana ya UUAJI.
Anakuwa hana tofauti na wachunaji ngozi za wanadamu, hana tofuati na watoaji kafara mbele za Mungu, hana tofauti na wauaji watu, hana tofauti na mtu aliyemwekea mwenzake sumu kwenye chakula afe,.. dhambi aliyoifanya ni ile ile isipokuwa tu imechukua umbile tofauti.
Sasa kwa kuwa mtu huyo anakuwa amemwaga damu isiyokuwa na hatia.. Biblia inasema damu yake itakuwa inalia hapo ardhini daima..
Utauliza imeandikwa wapi hiyo? Kasome habari za Kaini pale alipomuua ndugu yake, Mungu alimwambia hivi..
Mwanzo 4:10 “Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. 11 Basi sasa, UMELAANIWA WEWE KATIKA ARDHI, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; 12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani”.
Angalia hilo Neno.. “Umelaaniwa wewe katika ardhi”..Ndugu, Laana ya Mungu ni zaidi kutofanikiwa kimaisha..Ni laana ambayo itakufanya hata ujitahidije, hutakaa uione njia ya wokovu, na mwisho wa siku utaishia katika dhambi na kwenda motoni..
Unapaswa ufahamu ni heri ukapitia dhiki za wanadamu kuliko kutengwa na Mungu daima..
Wapo watu katika biblia walizaliwa kwa njia isiyohalali, wakafikia hatua hata ya kutengwa na ndugu zao wa mama halali, lakini baadaye walikuja kuwa Mashujaa wa Mungu.. Nenda kamsome mwamuzi mmoja anayeitwa YEFTHA katika biblia utalithibitisha hilo (Waamuzi 11).
Hapo ndipo utakapojua kuwa kila kiumbe kina kusudu chini ya jua. Hicho kiumbe ni nani ajuaye ndio Mungu alikikusudia kije kuwa raisi wa nchi, au Mhubiri wa kimataifa.?
Ikiwa wewe ni mmojawapo uliyepata mimba, unapousoma ujumbe huu, usifikirie kabisa kwenda kuitoa kwa namna yoyote ile. Hata kama utashurutishwa na watu kiasi gani usifanye hivyo kamwe. Usijitafuta ziwa la moto.
Vile vile ikiwa wewe ni mtu ambaye umeshawahi kutoa mimba huko nyuma, au ulimshawishi mwenzako akatoe mimba basi ujue kuwa Damu ya hao uliowatoa inamlilia Mungu ardhini.. Lakini habari njema ni kuwa Nafasi ya kutengeneza upya bado unayo..
Na ndio hapo utaona umuhimu wa Damu ya Yesu Kristo iliyomwagika kwa ajili yetu, inayofuta deni la dhambi zote, ambayo inanena mema kuliko ile ya Habili..Ukimkaribisha Yesu katika maisha yako, kuanzia huo wakati ile damu yake inaanza kunena mema kwa ajili yako, mbele za Mungu, kuomba ufutiwe kosa hilo na yale mengine yote uliyoyafanya katika maisha yako.
Utakuwa mpya, kama vile hukuwahi kumkosea Mungu hapo kabla, na wala laani hizo zote hazitakuandama tena kuanzia huo wakati na kuendelea. Lakini kama hutataka kumpokea Yesu maishani mwako, basi ujue hatakulazimisha lakini fahamu kuwa laana ya Mungu itakufuata siku zote za maisha yako,. Na ikitokea umekufa ghafla leo au kesho, au baadaye, ni moja kwa moja katika lile ziwa la moto,milele.
Kwanini usimpokee leo? Haijalishi wewe ni mwislamu, au mpagani, Yesu ndiye pekee njia ya kutufikisha mbinguni..
Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.
Ukimkaribisha atakutengeneza upya na wewe utaona badiliko la ajabu atakalolileta ndani yako. Sasa Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Ubarikiwe sana
Ikiwa utahitaji msaada zaidi wa kiroho basi utatutumia ujumbe au kutupigia kwa namba hizi hapo chini.
+255 789001312
Mada Nyinginezo:
UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI.
WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.
FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.
NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!
RACA
UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?
Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.
2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.
3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako.
4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”.
Kuhukulu maana yake ni “kutengeneza”..Kwahiyo hapo Bwana anamwambia Yakobo aliyemtengeneza na kumuumba kwamba asiogope!. Yakobo anayezungumziwa hapo sio Yule Yakobo mwana wa Isaka…Yule alishakufa kitambo lakini Yakobo anayezungumziwa hapa ni Taifa la Israeli, Taifa zima la wana wa Israeli ndio linalojulikana kama Yakobo..Na ndilo linaambiwa lisiogope!..wapitapo katika maji mengi Mungu atakuwa pamoja nao.. na katika mito, hawatagharikishwa; na waendapo katika moto, hawatateketea; wala mwali wa moto hautawaunguza..Kwasababu alikuwa wa thamani machoni pa Bwana.
Haya ni maneno machache tu lakini ya faraja kubwa sana…Kama Mungu analikumbuka agano lake na Ibrahimu kwa watu wake Israeli..kamwe hawezi kulisahau agano la mwanawe mpendwa Yesu Kristo, ambaye alikuja kufa kwa ajili yetu sisi na kutufanya kuwa Taifa teule na Takatifu, watu wa milki yake. Agano lake hilo la ukombozi, linatufanya tuonekane wa thamani sana kuliko lile la kwanza. Na hivyo maneno hayo pia yanatuhusu sisi tuliomwamini Yesu, na wewe ambaye utamwamini leo…kwamba USIOGOPE!…Usiogope vitisho vya adui!..usiogope magonjwa!..usiogope shida na majaribu!..Bwana Mungu wako ndiye aliyekuhuluku(yaani aliyekutengeneza)…
Majaribu unayoyapitia sasa ni maji mengi…lakini amesema atakuwa pamoja na wewe!…shida unazozipitia sasa baada tu ya kusimama kiimani ni mafuriko, lakini amesema hayatakugharikisha!..misiba na mateso unayoyapitia sasa ni miali ya moto, lakini amesema haitakuunguza! Hivyo jipe moyo, simama endelea mbele..kwasababu wewe ni wa thamani machoni pake.
Na mwisho amesema “kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”…Maana yake ni kwamba maisha yako kwake yanathamani kuliko ya watu wengine wasiomtumainia yeye na Taifa lingine lisilomcha yeye.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Tunajifunza kisa, ambacho kinamuhusu Petro, wakati wakiwa kule baharini yeye na wenzake, walipotokewa na Bwana,.. Swali la kwanza ambalo Petro aliulizwa na Bwana mara tatu ni Je! unanipenda?, Naye akajibu ndio Nakupenda,..Na hapo hapo Bwana akaanza akamweleza jinsi kifo chake kitakavyokuja kuwa siku atakapokuwa mzee, kwamba atafungwa na kuchukuliwa na watu asiowajua na kupelekwa kuuawa..
Lakini Petro aliposikia vile, hakuishia pale, alipeleka macho yake moja kwa moja kwa Yule mwanafunzi ambaye Bwana Yesu alimpenda [Ambaye ni Yohana], na Kumuuliza Bwana kuhusu habari yake naye, je! Na yeye Atakufaje?..Lakini maneno ya Bwana Yesu yalikuwa haya..
Yohana 21:18 “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka.
19 Akasema neno hilo kwa kuonyesha ni kwa mauti gani atakayomtukuza Mungu. Naye akiisha kusema hayo akamwambia, Nifuate.
20 Petro akageuka akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu anafuata; (ndiye huyo aliyeegama kifuani pake wakati wa kula chakula cha jioni, akasema, Bwana, ni nani akusalitiye?)
21 Basi Petro akamwona huyo, akamwambia Yesu, Bwana, na huyu je?
22 YESU AKAMWAMBIA, IKIWA NATAKA HUYU AKAE HATA NIJAPO, IMEKUPASAJE WEWE? Wewe unifuate mimi.
23 Basi neno hilo lilienea katikati ya ndugu ya kwamba mwanafunzi yule hafi. Walakini Yesu hakumwambia ya kwamba hafi; bali, Ikiwa nataka huyu akae hata nijapo, imekupasaje wewe?
Utaona Petro alipomuuliza aliambiwa.., Ikiwa huyu nataka akae hata nijapo..Kwa lugha rahisi ni hii “Hata kama nikitaka huyu asife mpaka nijapo, Wewe inakuhusu nini? Unapaswa Unifuate mimi…
Hilo Neno “Imekupasaje wewe” Kwa Kiswahili fasaha ukiangalia katika tafsiri nyingine, limeandikwa kama ‘’Inakuhusu nini?’…
Hivyo Petro alikuwa anajaribu kijilinganisha njia yake na wengine, Lakini Kristo alikatisha maneno yake na kumwambia, hata nikiwa nataka Yohana aishi mpaka nijapo, wewe inakuhusu nini? , au inakuongezea nini kwenye niliyokupangia? Wewe fuata njia yako uliyowekewa.
Leo hii, tunajaribu kujifananisha na wengine, kisa mtumishi Fulani ahubiri namna hii, na mimi nihubiri hivyo, kisa Yule kafungua kanisa, na mimi nikafungue wakati huo huo, kisa Yule anahubiri kwa staili ile na mimi nikahubiri vile vile tunadhani ndio Mungu anavyotaka, au Yule anaimba namna hii na mimi ngoja nikaimbe kama yeye. Tunashindwa kukaa katika mapito ambayo Mungu ametuwekewa sisi, Ikiwa Yule anahubiri kwa kuandaa semina kubwa na kwaya nyingi, mimi ninayehubiri tu mtaani, Yale ya kwake yananihusu nini? Au yanaathiri vipi huduma yangu?
Kwanini niige kila anachokifanya yeye?.. Na kama ikitokea Mungu kamuandikia kifo kwa njia ile mwisho wa siku apigwe mawe, Je na mimi nitakuwa tayari kufa kama yeye?. Yeye amepangiwa kuishi miaka michache, hivyo kazi yake Mungu kampangia iende haraka haraka, lakini wewe umepangiwa miaka mingi ya kuishi uhubiri injili kwa miaka mingi, lakini pale unapoiga cha mwenzako na kuacha cha kwako, ndivyo unavyokwenda nje ya kusudi la Mungu.
Petro alipoona yeye, atakwenda kufa kwa namna ile, akasema ikiwa mimi nataondoka hivi, vipi kuhusu huyu ambaye aliyependwa na Yesu mpaka kuegema katika kifua chake, si ndo atakufa kifo cha utukufu zaidi yangu mimi?. Akadhani kila mtu ni wa kufa tu, ndio katimiza mapenzi yote ya Mungu.
Kila mmoja wetu kawekewa na Bwana jambo lake la kipekee, na njia yake ya kuifuata (kamwe hatuwezi tukafanana).. Kristo anasema nifuate, anamaanisha hivyo hivyo NIFUATE!..Hatutahukumiwa kwa sababu hutukuishi kama maisha ya mtu Fulani, au hutukufanya huduma kama ya mtume Fulani, bali tutahukumiwa pale ambapo hatukumfuata Yesu alipotuita kila mmoja wetu kwa njia yake.
Ukisimama kama wewe, iwe ni katika udogo, au katika wingi, maadamu upo katika mstari wa Bwana, hiyo inathamani kubwa sana kuliko kutumia kitu cha mtu mwingine kama kipimo cha utendaji wako kazi.
Bwana akubariki sana na atubariki sote.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?
UZAO WA NYOKA.
UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?
Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?