Kuota umechomwa kisu au Kuota umepigwa risasi kuna maanisha nini?
Awali, ni vyema kujua kuwa si kila ndoto aotayo mtu, ina maana katika maisha yake, Hilo ni vizuri ukalifahamu, Ndoto nyingi tunazoziota kila siku zinatokana na shughuli zetu za kila siku (Mhubiri 5:3), au mazingira yanayotuzunguka, au mambo ambayo tunayawaza mara kwa mara, au tulishawahi kuyaona, au kuyapitia sehemu Fulani katika maisha yetu (Isaya 29:8)..
Naweza kusema asilimia 90 ya ndoto tunazoziota kila siku zinaangukia katika kundi hili,.Hapo ndipo watu wengi wanaposhindwa kuelewa, wanataka kila ndoto wapate tafsiri ya rohoni, au maishani, hilo jambo halipo, utaishia kudanganywa, au kujidanganya mwenyewe, Kumbuka kinachoweza kueleza hatma ya maisha yetu kwa ufasaha wote, sio ndoto tunazoziota usingizini, bali Neno la Mungu tunaloliishi kila siku.
Mungu anaziita ndoto kama makapi ukifananisha na Neno lake(Yeremia 23:28-29). Akiwa na maana kuwa mtu Yule anayeishi kwa kulishika Neno lake, Ni bora kama ngano, kuliko yule anayetafuta maana za ndoto zilizofananishwa na makapi.
Ni mara chache, ndoto zinabeba ujumbe, ili kutambua ndoto yako inatoka kwa Mungu au kwa shetani, au kwako mwenyewe, basi fungua hapa usome kwanza>>> Nitajuaje kama ndoto ni ya Mungu au ya Shetani?
KUOTA UMECHOMWA KISU/KUOTA UMEPIGWA RISASI.
Hivyo ukiwa umeshasoma, na unao uhakika kabisa kuwa ndoto uliyoota, si ya kawaida, imekujia kwa uzito mwingine wa kitofauti, imekushtua sana, imeonekana kama ni jambo la halisi kabisa, basi upo ujumbe wa rohoni.
Sasa kwa namna ya kawaida, ukishaona mpaka mtu amefikia hatua ya kukuchoma kisu, au amekupiga risasi ni wazi kuwa kuna jambo ulilifanya, au unalifanya sasa hivi, ambalo limemchukiza sana, kiasi cha kufikia uamuzi wa kuona kufa kwako ni bora kuliko kuishi.
Vivyo hivyo katika ndoto ukiona umepigwa risasi, au umechomwa kisu, au upanga, au mkuki,au kitu chenye ncha kali, hiyo ni ishara kuwa maishani mwako, lipo jambo ambalo unalifanya, halifurahiwi na wengine, aidha ni zuri au baya,
Katika biblia tunasoma habari ya mtu mmoja, aliyeitwa Egloni mfalme wa Boabu, huyu, aliwatumikisha Israeli kwa muda wa miaka 18, na hiyo yote ilikuwa ni kutokana na makosa yao wenyewe(Israeli)..Lakini walipomlilia Mungu, awaokoe kutoka katika utumwa na mateso ya mfalme huyu, Mungu akawasikia ndipo akawapelekea mwokozi aliyeitwa Elihu.
Huyu Elihu alijifanya kama mjumbe, aliyeituwa na Israeli, kumbe hila zake zilikuwa ni kwenda naye katika chumba cha siri, ili wakiwa wao wawili peke yao achomoe upanga wake na kumchoma tumboni, Tusome kidogo..
Waamuzi 3:20 “Basi Ehudi akamwendea; naye alikuwa anaketi peke yake katika chumba chake cha baridi. Ehudi akasema, Mimi nina ujumbe utokao kwa Mungu kwako wewe. Basi akainuka katika kiti chake.
21 Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake;
22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma.
23 Ndipo Ehudi akatoka nje barazani, akamfungia milango ya hicho chumba na kuifunga kwa ufunguo.
24 Basi alipokuwa amekwisha toka nje, hao watumishi wake wakaenda; wakaona, na tazama, hiyo milango ya chumba ilikuwa imefungwa kwa ufunguo; nao wakasema, Hapana budi amejifunika miguu yake ndani ya chumba cha baridi.
25 Wakangoja hata wakatahayari; na tazama, hakuifungua milango ya chumba; basi wakatwaa ufunguo, na kuifungua; na tazama, bwana wao alikuwa ameanguka nchi, naye amekufa”.
Umeona? Sasa huyu Elgoni alichomwa kutokana na makosa yake, lakini, pia wapo wengine waliochomwa kutokana na haki zao, mfano mmojawapo ni Bwana wetu YESU KRISTO..Yeye alichomwa mkuki pale msalabani, sio kwasababu alikuwa mwovu hapana.
Hivyo na wewe jiangalie ni wapi katika maisha yako, pana vita kwa wengine, wewe umesimama, Ikiwa upo ndani ya Kristo basi, ujue maadui wa imani wapo, lakini huna haja ya kuogopa, Kwasababu Mungu atakupigania, kikubwa unachopaswa ufanye ni kuzidi kuwa mwombaji.
Lakini kama upo nje ya Kristo, ukweli ni kwamba, licha tu kuzungukwa na hatari za maadui, lakini, maisha yako ya rohoni yapo hatarini.. Mungu anaweza kweli kukuepusha na hatari za mwilini, lakini zile za rohoni za ibilisi hawezi kukuzuia kutokana na kwamba wewe ni milki ya ibilisi.
Jiulize ukifa leo ghafla katika dhambi utakuwa mgeni wa namna huko uendako?
Hivyo ndugu ikiwa unahitaji kumpa leo YESU maisha yako..Basi uamuzi huo utakuwa ni busara sana kwako, Kama upo tayari kufanya hivyo, moja kwa moja fungua hapa, kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Na hayo mengine yaliyosalia Mungu atakujalia rehema zake.
Bwana akubariki.
Kwa mafundisho zaidi ya Neno la Mungu.
Whatsapp: +255 789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kuota unafanya Mtihani.
KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.
HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?
NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.
ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.
Zaburi 91, Ni Zaburi iliyo ya kipekee sana yenye nguvu, Na shetani analijua hilo, ukitaka kuamini jiulize, ni kwanini Shetani aliitumia Zaburi hii kumjaribu Bwana,? Kiasi kwamba mtego wake ungekubali basi Zaburi hii ndio ingekuwa silaha ya kumwangushia Bwana.
Ni kwanini ainukuu Zaburi 91? Shetani aliijua nguvu na ulinzi Mungu aliouweka juu ya wampendao..Lakini wengi wetu hatuifahamu…Alimwambia hivi Bwana..
Mathayo 4:6 “akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako”.
Unaona, alijua kuwa mtu yeyote aliyempendeza Mungu, huwa anaachiliwa ulinzi wa kipekee, Mungu anamuagizia mpaka malaika zake, wamlinde, asijikwae,..
Hivyo kama wewe umeokoka na umesimama vizuri basi fahamu Zaburi 91, Ni salaha yako madhubuti ya kummaliza shetani na vitisho vyake, na majeshi yake..Isipokuwa tu usiitumie hiyo kwa lengo la kumjaribu Mungu, vinginevyo utampa shetani nafasi ya kukuangusha kama alivyojaribu kufanya kwa Bwana Yesu.
Embu tuisome,
ZABURI 91
1 Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
2 Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.
3 Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo.
Bwana anasema, atakuepusha na mitego ya mwindaji(Shetani), na tauni iharibuyo..akiwa na maana atakulinda na magonjwa hatari mfano wa Tauni kama Corona..Unaona ikiwa wewe ni mtakatifu, huna haja ya kuwa na hofu.
Anaendelea kusema…
Zaburi 91:4 Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao.
5 Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,
6 Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri,
Ndugu uliyeokoka, Bwana atakulinda tu, huna haja ya kuogopa, iwe ni mchana au usiku atakuwa na wewe kukulinda na mikono ya magonjwa na maadui.
Zaburi 91:7 Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata hivyo hautakukaribia wewe.
8 Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki.
9 Kwa kuwa Wewe Bwana ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.
10 Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.
Haijalishi utaona ni wangapi, wanadondoka, au wanashindwa pembeni yako, wameanguka, lakini wewe Bwana atakuwa na wewe wakati wote kuhakikisha hushindwi wala hupatwi na mabaya hayo yote, hata kama utaonekana kama unashindwa,lakini mwisho wa siku ushindi utakuwa ni wako tu,
Zaburi 91:11 Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.
12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
13 Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.
Unaona zaidi ya hiyo, Malaika wa Bwana watakuwa na wewe kukulinda kila wakati, usijikwae, na mabaya..Na hiyo yote ni kwasababu gani? Ni kwasababu, umempenda Mungu na umemtafuta kwa bidii, umemfanya yeye kuwa tegemeo lako, na ndio maaana anasema..
Chapisho hili limefadhiliwa na https://www.swisswatch.is/ washirika wetu.
Zaburi 91:14 Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.
15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu.
Maneno ya faraja sana na yanayotia nguvu, lakini mpaka Mungu kukutamkia hivyo ujue ni lazima kwanza uwe ni mwana wake mpendwa, vinginevyo, hakuna ulinzi wowote, utaokao kwake utakufikia..
Ili Mungu akulinde na tauni (Corona) isikuue, au magonjwa mengine ya kutisha yaliyozuka duniani leo hii, ni lazima uwe mwana wake mpendwa, ili Mungu akulinde na maadui (mapepo na wachawi), Ili Mungu akuagizie malaika zake watembee na wewe kila wakati kama alivyofanya kwa Elisha..basi ni lazima kwanza ufanyike mwana wake.
Ndipo hapo nawe utakapoitamka Zaburi 91 kwa ujasiri wote, na iwe kweli na maana kwako. Kumbuka Zaburi hii ilimwingia sana shetani kichwani, na ndio maandiko pekee aliyoyatamka kwa kinywa katika biblia nzima, hiyo ni kuonyesha kuwa ni jinsi gani anaona wivu, kuona watoto wa Mungu wanapokea ulinzi wa kipekee kutoka kwa Mungu.
Maana yake ni kuwa ukimkosa leo Kristo, basi huwezi mshinda shetani, kwasababu ulinzi wa Mungu haupo juu yako.. Hivyo kama upo tayari leo kumpa Yesu maisha yako, basi uamuzi utakaofanya ni mzuri na wa busara sana..Kama ni hivyo fungua hapa kwa ajili ya maelekezo juu ya sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali Share na wengine,
Whatsapp: +255789001312
Mada Nyinginezo:
TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.
AGANO LAKO LINABEBWA NA NANI?.
WEWE NI BWANA UNIPONYAYE.
KIAMA KINATISHA.
JIFUNZE KUJITOA KWA MUNGU NA KUWA MKARIBISHAJI.
UNYAKUO.
Shalom, jina la Bwana wetu libarikiwe daima.
Neno linatuambia..
“Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
Ni mpya kila siku asubuhi..” (Maombolezo 3:22-23).
Na wewe usomaye ujumbe huu rehema za Bwana zisikome juu yako daima.
Leo tutajifunza kwa ufupi, mambo machache ya kuzingatia tunapokwenda nyumbani kwa Bwana aidha kuzungumza naye, au kumwabudu, inaweza ikawa ni kanisani, au kwenye semina, au popote pale unapoweza kumfanyia Mungu ibada.
Kama tunavyosoma katika agano la kale tunaona kuna wakati ulifika wa Sulemani kumjengea Mungu Nyumba (Hekalu) ambalo lingekuwa ni kitovu cha waisraeli wote, na mataifa yote ulimwenguni kumwabudia Mungu , na kufanyiwa upatanisho wa makosa yao kwa wakati ule.. Kama tunavyojua hekalu lile lilijengwa kwa kipindi cha Miaka 7, na katika ujenzi ule, kulikuwa na vigezo vingi sana vya kuzingatia, pamoja na vipimo. Na kila kitu kilichotengenezwa kule kilikuwa kilikuwa kinafunua jambo kubwa sana rohoni kwa kanisa la Sasa, wale makerudi waliowekwa kule walikuwa wanafunua jambo Fulani rohoni, vile vinara 7 vya taa, vilivyokuwa na maana yake pia, halikadhalika zile madhabahu za dhahabu na za shaba , zote zilikuwa na maana, na lile sanduku la agano, mpaka yale mapambo yaliyokuwa kule ndani.
Sasa, karibu na mwisho kabisa wa ujenzi ule, Sulemani aliongozwa kujenga vitu vingine viwili muhimu katika hekalu, navyo si vingine Zaidi ya nguzo kubwa mbili zilizosimama katika maingilio ya Hekalu. Nguzo hizo zilikuwa ni ndefu na pana..
Nguzo ya kwanza iliwekwa upande wa kulia mwa kuingilia hekaluni, Na nguzo pili iliwekwa upande wa kushoto.
Ile iliyokuwa upande wa Kulia iliitwa YAKINI.. Na ile iliyowekwa upande wa kushoto iliitwa BOAZI.
2Nyakati 3:17 “Akazisimamisha nguzo hizo mbele ya hekalu, moja upande wa kuume, na ya pili upande wa kushoto; akaliita jina la ile ya kuume Yakini, na jina la ile ya kushoto Boazi”
Sasa maana ya maneno hayo ni hii:
Yakini ni: IMEDHANIWA KUWA ATATHIBITISHA.
Na Boazi: IMEDHANIWA KUWA IMO NGUVU.
Kulikuwa hakuna namna yoyote kuhani aingie hekaluni, apitilize mpaka patakatifu pa patakatifu, kwenda kufanya mambo ya ibada asipite katikati ya hizo nguzo mbili. Zilikuwa kama mihimili ya hekalu.
Ikifunua kuwa yeyote atakayeingia kule avukapo nguzo hizo ni lazima jambo hilo liwe kichwani mwake, kuwa Mungu atathibitisha(Yakini), Na humo humo ndani pia ipo nguvu ya Mungu (Boazi).
Hivyo kuhani akiingia mule, kwa shughuli yoyote ile aidha ya upatanisho au ya kuwasilisha maombi ya watakatifu, kichwani mwake anauhakika kuwa ni lazima Mungu ajibu maombi yao yaani alithibitishe agano lake alioingia nao kwa kupitia Ibrahimu, Na vilevile anajua kuwa nguvu ya Mungu ipo mule, kwahiyo ni lazima awe makini kwa atayayafanya vinginevyo atakuwa anajitafutia kifo mwenyewe au hata matatizo kwa wana wa Israeli wote.
Nguzo hizo zilisimama kwa wakati wote hekalu lilipokuwepo.
Lakini Ni ujumbe gani tunapewa kwa agano jipya?
Biblia inafananisha kanisa la Kristo kama hekalu la Mungu, tunapotoka na kwenda nyumbani mwake au uweponi mwake, Sisi wote tunaenda kuwa kama makuhani wa Mungu, hivyo Bwana anataka kila mmoja wetu, ajue kuwa nguzo hizo mbili (yaani Yakini na Boazi) zimesimama mbele ya hekalu lake takatifu.
Anataka tujue kuwa tunapokwenda nyumbani mwake tufahamu kuwa Mungu yupo pale, ili kulithibitisha agano lake aliloingia na watakatifu kupitia Yesu Kristo.. Na kwamba unapokwenda kusali, au kumwabudu au kumwomba chochote, yupo pale kukusikia na kukujibu maombi yako, sawasawa na maneno ya Kristo (Yohana 14:13) Huo ni uhakika, Hivyo uingie ukijua jambo hilo kichwani kuwa Mungu ni Mungu mshika maagano.
Vilevile anataka ujue kuwa ipo nguvu yake kule ndani, Hivyo uwe makini pia usiende kidunia/kimazoea.. Wapo watu wanajiamulia tu kuingia kanisani wanavyotaka na mavazi yao kizinzi, wanaingia kanisani na vimini, na suruali, wakidhani kule wanaenda kukutana na miungu isivyoweza kufanya jambo lolote. Hawajua jengo likishaitwa kanisa, Au nyumba ya Mungu, tayari nguzo mojawapo itwayo Boazi imesimama pale nje!, yaani ndani imo nguvu kubwa sana ya Mungu, inayoua na kuhuisha.
Kwahiyo pale mtu anapoingia bila heshima, anakuwa anajitafutia mwenyewe laana..Hilo unapaswa ulijue hili binti wa Mungu, hilo unapaswa ujue kijana,.Unapokwenda kanisani, halafu unajua jana umetoka kuzini, na wakati huo huo unakwenda kushiriki meza ya Bwana,..Unajitafutia matatizo yako mwenyewe..(Soma hapa uone laana iliyowapata watu wa dizaini hiyo katika kanisa la Kristo IWakorintho 11:27-34)
Nyumba ya Mungu, si ya kuifanyia mzaha hata kidogo..
Marko 11:17 “Akafundisha, akasema, Je! Haikuandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi”.
Hivyo ndugu kama wewe ni mkristo, zingatia hayo mambo mawili, yaweke kichwani mwako daima Nyumbani mwake Mungu anathibitisha, na nyumbani mwake imo nguvu. (Yakini na Boazi)
Bwana akubariki.
Ikiwa hujaokoka, kumbuka leo tena tumepiga hatua nyingine ya kuukaribia ule mwisho, pengine itakuwa leo, au kesho asubuhi, au wiki hii au vyovyote vile, hatuhitaji kuishi maisha ya kubahatisha, hivyo tukiyajua hayo, ni wakati wa kuamka usingizini, na kuzisafisha taa zetu.. Mpe leo Kristo maisha yako ayaokoe. Ufanyike kuwa mwana wake.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je Kifo ni nini? Na kuna aina ngapi za vifo?
Kifo ni pale uhai unapoondoka ndani ya kiumbe hai chenyewe. Kwa ufupi kifo ni Mwisho wa Maisha ya mwilini.
Lakini katika Biblia vipo vifo vikuu vya aina tatu.
Kifo cha Mwilini:
Hichi ni pale mwili na roho vinapotengana. Kifo hichi kinamkuta kila mmoja wetu, pale anapomaliza safari yake ya Maisha ya duniani ikiwa unyakuo utakuwa haujakukuta basi utakufa na kuzikwa.
Mwanzo 3:19 “…. kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi”.
Kifo cha namna hii haikuhusishi roho ya mtu..Roho inakuwa bado inaendelea kuishi sehemu nyingine..Bwana Yesu alisema..
Mathayo 10:28 “Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.”
Kifo cha Rohoni:
Hichi ni kifo ambacho kinamkumba mtu kwa ndani, lakini kwa nje bado anakuwa anaendelea kuishi kana kwamba hakuna chochote kinachoendelea.. Na kifo cha namna hii, kila mmoja wetu anacho aidha kwa kujua au kwa kutokujua..Leo hii ikiwa Maisha yako yapo mbali na dhambi (yaani umeokoka), tayari wewe rohoni unaonekana kuna mauti imetokea ndani yako, yaani unaonekana tayari umeshakufa kwa Habari ya dhambi, biblia inasema hivyo..
Warumi 6:1 “Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? 2 Hasha! SISI TULIOIFIA DHAMBI tutaishije tena katika dhambi..
6:11 “Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu”.
Vilevile ikiwa injili inahubiriwa kwako halafu hubadiliki, fahamu kuwa katika ulimwengu wa roho umekufa kwa Habari ya haki hata kama utakuwa unaishii..
1Timotheo 5:6 “Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai”.
Kifo cha Roho:
Kifo hichi ndio kibaya Zaidi, Na ndio kifo cha mwisho kinachojulikana kama Mauti ya pili. Kifo hichi ni pale, unapotenganishwa moja kwa moja na uso wa Mungu milele, katika lile ziwa la moto.. Ambapo utatetezwa huko na roho yako itaangamia milele.
Ufunuo 20:13 “Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.
15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.
Lakini Pamoja na hayo sisi tulio ndani ya Kristo tunalo tumaini la uzima wa milele ikiwa tutakufa leo. Kwasababu Yesu Kristo ambaye alishinda mauti, atakuja kutufufua tena, katika hii hii miili yetu, kisha atatuvika miili mingine mipya ya utukufu ya kimbinguni isiyo kufa wala kuugua, wala isiyo na madhaifu, na hiyo ndiyo tutakayoishi nayo milele.
Lakini ikiwa wewe ni mwenye dhambi bado hujamkabidhi Kristo Maisha yako ayaokoe, ukifa leo hii, huna tumaini lingine lolote Zaidi ya kungojea ile mauti ya pili ambalo ni ziwa la moto..
Lakini kwanini hayo yote yatukute angali tunayo nafasi bado?..Ikiwa wewe ni mmojawapo ambaye yupo bado katika dhambi, Na leo hii unataka Bwana Yesu akuokoe, hutaki neema ya wokovu ikupitie, basi popote pale ulipo anaweza kukusamehe dhambi zako ikiwa tu utamaanisha kufanya hivyo.
Kama upo tayari kutubu sasa dhambi zako, basi fungua hapa kwa ajili ya maelekezo ya sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki sana.
Ikiwa umemfuata maelekezo hayo ya kuokoka, sasa, upo tayari kujifunza na masomo mengine ya rohoni.Tafadhali tazama chini vichwa vya masomo kisha bofya lolote upendalo uzidi kujifunza zaidi.
Mada Nyinginezo:
MAUTI YA PILI NI NINI?
NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.
JIFUNZE KUJITOA KWA MUNGU NA KUWA MKARIBISHAJI.
RABI, UNAKAA WAPI?
KAMA MMOJA TU NDIO HIVI! SI ZAIDI 153?
Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?
KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?
PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.
Kuabudu Sanamu ni nini? Na ibada za sanamu ni zipi?
Kuabudu sanamu: Katika agano la kale ni kitendo chochote cha kwenda kuabudu au kusujudia, au kutumika kitu kingine chochote, tofauti na Mungu mkuu mmoja aliye hai (YEHOVA).
Moja ya amri 10 Mungu alizowapa wana wa Israeli, ilikuwa ni pamoja na kujiepusha na ibada za sanamu za aina yoyote..
Amri ya pili inasema hivi..
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.
Hivyo mtu akikigeuza kitu chochote, kuwa mbadala wa Mungu, huko ni sawa na kuabudu sanamu, ukiweka mdoli nyumbani kwako na kwenda kumpigia magoti na kumwomba kana kwamba ni Mungu, ujue hapo unafanya ibada za sanamu..
Ukitengeneza kinyago chenye sura ya mtakatifu Fulani labda Mariamu, au Bwana Yesu akiwa pale msalabani, kisha ukakihusianisha na mambo ya ibada kwa mfano kukisujudia, au kukiabudu, au kuombea dua zako kwa kupitia hicho, tayari hiyo ni ibada za sanamu,
Ukining’iniza picha ukutani ya mtu Fulani maarufu, au mnyama , au kitu Fulani kwa lengo la kukifanya kama kipatanishi chako na Mungu, au kitu chako kinachoweza kukupa bahati Fulani, hiyo tayari ni ibada za sanamu.
Hata ukipanda mti, au Ua fulani, ukiamini kuwa linaweza kukulinda, au kueleza hatma ya maisha yako, tayari hiyo nayo ni ibada za sanamu.
Kumbukumbu 16:21 “Usipande mti uwao wote kuwa Ashera kwako kando ya madhabahu utakayofanya ya Bwana, Mungu wako.”
Na ni machukizo makubwa sana mbele za Mungu, yanayomtia wivu kiasi cha Mungu kukupatilizia maovu hata ya baba zako, uone ni jinsi gani kitendo hicho kinavyomuudhi Mungu..
Ipo mifano mingi sana katika biblia, ya watu walioadhibiwa kwa makosa kama haya..Kumbuka hili ndilo lililowafanya wana wa Israeli wengi wasiione Kaanani, kadhalika hili ndilo lililochangia wana wa Israeli tena baadaye kuchukuliwa utumwani Babeli.
Hivyo kuhusianisha kitu chochote na Ibada ni hatari sana, Ibada zako zote zinapaswa zimwelekee Mungu peke yake.
JE! KUABUDU SANAMU/IBADA ZA SANAMU KATIKA AGANO JIPYA KUKOJE?.
Tukirudi katika agano jipya, kuabudu sanamu sio tu kwenda kusujudia vinyago tu peke yake n.k., hapana ni Zaidi ya hapo, biblia inasema..
Waefeso 5:5 “Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu”.
Unaona, mtu yeyote ambaye ni mchafu, mbele za Mungu ni mwabudu sanamu, Mtu yeyote aliye na tamaa mbele za Mungu huyu naye ni mwabudu sanamu.
Hawa wote biblia inasema hawana urithi katika ufalme wa Mungu.
Hivyo mimi na wewe tunapaswa tujiepushe na Ibada zote mbili, yaani sanamu za nje, Pamoja na zile Sanamu za ndani. Ili Mungu atupokee tukaurithi uzima wa milele aliyotuandalia tumpendao.
Bwana akubariki.
Ikiwa hujaokoka na unataka kufanya hivyo leo, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara kwako. Fungua hapa kwa ajili ya sala ya toba.>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ubarikiwe.
Mada Nyinginezo:
Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?
USIABUDU SANAMU.
CHAPA YA MNYAMA
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
NEEMA YA MZALIWA WA PILI.
HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.
Ni watu gani hao ambao mahali pao hapakuonekana? (Ufunuo 20:11)
JIBU: Tusome..
Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana”.
Hao wanaozungumziwa hapo kwamba “mahali pao hapakuonekana” sio binadamu!..bali ni “MBINGU NA NCHI”. Tafsiri za lugha nyingine zinaelezea vizuri.
Na kwanini zikimbie uso wake?..ni kwasababu ya utukufu wake…kwasababu hakuna kitu chochote kinachoweza kusimama mbele ya uso wa Mungu kwa kuwa yeye mkuu sana na mtakatifu!. Maserafi tu waliopo mbinguni ambao ni watakatifu, bado wanafunika nyuso zao na miguu yao mbele yake..si Zaidi viumbe vilivyopo katika mbingu na nchi tulizopo sisi?.
Ayubu 41:10 “….BALI NI NANI AWEZAYE KUSIMAMA MBELE YANGU MIMI?
Hivyo hakuna kiumbe chochote ambacho kinaweza kumkaribia Mungu kwa ukamilifu wake. Lakini ashukuriwe Mungu kwa sababu yupo mmoja ALIYESTAHILI KUMKARIBIA YEYE, na huyo si mwingine Zaidi ya mwanawe wa pekee aliyemtoa ambaye yeye alishinda na kustahili kumkaribia Mungu, na kuketi Pamoja naye katika kiti chake..Huyo pekee ndiye aliyestahili kumkaribia Mungu…na kwa kupitia yeye sisi tuliompokea tumepata nafasi ya kumkaribia Mungu..
Ufunuo 3:21 “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.
Ufunuo 5:11 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,
12 wakisema kwa sauti kuu, ASTAHILI MWANA-KONDOO ALIYECHINJWA, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.
13 Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele”.
Hivyo tukimwamini na kuingia ndani yake tunapata ujasiri wa kumkaribia Mungu sana, jambo ambalo katika hali ya kawaida lisingekaa liwezekane kabisa, lakini limewezekana kwa kupitia Yesu, lakini tukimkataa huyu Yesu, basi hatuna ujasiri wowote na hatuwezi kumkaribia Mungu kamwe…Tutaukimbia uso wake na kutengwa naye milele katika ziwa la moto.
Waebrania 10:19 “Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu,
20 njia ile aliyotuanzia iliyo mpya, iliyo hai, ipitayo katika pazia, yaani, mwili wake;
21 na kuwa na kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu;
22 na tukaribie wenye moyo wa kweli, kwa utimilifu wa imani, hali tumenyunyiziwa mioyo tuache dhamiri mbaya, tumeoshwa miili kwa maji safi”.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UFUNUO: Mlango wa 20
DANIELI: Mlango wa 1
HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?
URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?
ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.
ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.
Usinipite mwokozi Lyrics| Swahili, – “Pass me not, O Gentle Savior”
Historia ya nyimbo Usinipite mwokozi.
Wimbo huu uliandikwa mwaka 1868, na mwanamke wa kimarekani aliyeitwa Fanny Crosby. Mwanamke huyu mkristo alizaliwa akiwa mzima lakini wiki 8 baada ya kuzaliwa kwake alipatwa na opofu, ambao ulidumu mpaka kufa kwake, lakini katika maisha yake yote aliyoishi hapa duniani (yaani miaka 94), haikuwa bure kwa Mungu wake, alifanikiwa kuandika nyimbo zaidi ya 8,000..Hivyo hiyo ikamfanya apate umaarufu na kumfanya ajulikane kwa jina la “mtunzi-kipofu-wa-nyimbo-za-tenzi”, na “Malkia wa nyimbo za Injili”.
Lakini siku moja alipokuwa amealikwa kwenda kuzungumza na wafungwa wa mji, na alipokuwa akitembea kule gerezani alimsikia mfungwa mmoja akisema “Bwana mwema usinipite, usinigeuzie mgongo wako,unikumbuke”,
Fanny anasema aliguswa sana na maneno yale, jambo ambalo halikuondoka kwenye kichwa chake mpaka alipofika nyumbani. Na huko ndipo alipoandika beti zote nne za wimbo ujulikanao kama USINIPITE MWOKOZI.
Alipomaliza kuuandika akampa muhusika wa kuweka midundo, na mwaka, 1870 wimbo huo, ulizinduliwa rasmi katika machapisho..
Na kwa kipindi kifupi` sana ukapata umaarufu mkubwa duniani kote.
*****
Usinipite wokozi, |
Unisikie; |
Unapozuru wengine, |
Unisikie. |
Yesu, Yesu, Unisikie; |
Unapozuru wengine, |
Usinipite, |
Kiti chako cha rehema, |
Nakitazama; |
Magoti napiga pale, |
Nisamehewe. |
Yesu, Yesu, Unisikie; |
Unapozuru wengine, |
Usinipite. |
Sina ya kutegemea, |
Ila wewe tu; |
Uso wako, uwe kwangu, |
Nakuabudu. |
Yesu, Yesu, Unisikie; |
Unapozuru wengine, |
Ila wewe tu, |
Usinipite. |
U Mfariji Peke yako; |
Sina mbinguni, |
Wala Duniani pote, |
Bwana mwingine. |
Yesu, Yesu, Unisikie; |
Unapozuru wengine, |
Usinipite. |
*****
Jambo hili tunaliona kwa wale kipofu wawili waliomsikia Yesu anapita..
Mathayo 9:27 “Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, UTUREHEMU, MWANA WA DAUDI.
28 Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana. 29 Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate”.
Na itakuwa hivyo na kwako:
Ikiwa wewe umeokoka, na unaona unapita katika hali ngumu, ambayo unaona kwa namna ya kawaida huwezi kutoka, basi wakumbuke watu kama hawa, wakutie nguvu,..Zidi kumwita Yesu, atakuonekania kwa wakati wake. Kwasababu yeye anatupenda na kutujali, na yote yanawezekana kwake.
Lakini kama hujaokoka, basi ni vizuri leo ukamwita kwanza mwokozi akuokoe maisha yako, usiruhusu akupite, anapokwenda kuwapa wengine uzima wa milele, sema na mimi leo nauhitaji huo uzima, hivyo kama upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa, kwa ajili ya Sala ya Toba..>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki..
Tazama historia ya nyimbo nyingine za Tenzi chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
MWAMBA WENYE IMARA
CHA KUTUMAINI SINA lyrics
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics
TENZI ZA ROHONI
Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?
MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.
UNYAKUO.
Ni salama rohoni mwangu lyrics- It is well with my soul.
Nyimbo hii ilitungwa na mwanasheria mmoja mkristo aliyeitwa Horatio Spafford, alitunga wimbo huu kutokana na mambo mazito aliyoyapitia katika maisha yake, Matatizo yake yalianza kwa kufiwa na mtoto wake wa pekee wa kiume aliyekuwa na miaka minne, hiyo ilikuwa ni mwaka 1870
Muda mfupi baadaye (mwaka 1871) moto mkubwa uliozuka huko Chicago Marekani mjini kwake, ukaharibu mali zake nyingi ukizingatia alikuwa ni mwanasheria aliyekuwa amefanikiwa sana. Hilo likafuatana na biashara zake pia kuporomoka kutokana na anguko la uchumi lililotokea mwaka 1873, Hivyo ikambidi apange safari ya kwenda Ulaya pamoja na familia yake, Lakini aliahirisha safari kwa ajili ya kuweka mambo yake ya vibiashara vizuri yaliyokuwa yameathiriwa na moto, hivyo ikambidi msafirishe kwanz mkewe na mabinti zake wanne,akiahidi kuwa atawafuta baadaye.
Lakini Meli ilipokuwa inakatisha bahari ya atlantiki, ilizama ghafla kwa kugongana na meli nyingine na mabinti zake wote wanne wakafariki kwenye ajali hiyo akasalimika mke wake tu, akiwa kule Marekani alipokea ujumbe wa telegrafu kutoka kwa mke wake unaosema “Nimepona peke yangu” ndipo Spafford akaondoka kumfuata mkewe, na huko huko akauandika wimbo huu..
https://www.high-endrolex.com/15
Baadaye vina vingine vya mashairi viliongezwa ndipo ukazaliwa wimbo huu, Ni salama Rohoni Mwangu.
****
Nionapo amani kama shwari,
Ama nionapo shida;
Kwa mambo yote umenijulisha,
Ni salama rohoni mwangu.
Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.
Ingawa Shetani atanitesa,
Nitajipa moyo kwani;
Kristo ameona unyonge wangu,
Amekufa kwa roho yangu.
Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.
Dhambi zangu zote, wala si nusu,
Zimewekwa Msalabani;
Wala sichukui laana yake,
Ni salama rohoni mwangu.
Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.
Ee Bwana himiza siku ya kuja,
Panda itakapolia;
Utakaposhuka sitaogopa,
Ni salama rohoni mwangu.
Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.
****
Hata sisi Je! Tunapopitia shida na magumu tunazo nguvu za kusema ni salama rohoni mwangu?, Tunapopitia njaa, tunapopitia misiba, tunapopitia matatizo mazito Je! Bado Tunaweza kumwambia shetani ni Salama rohoni mwangu? Kama ilivyokuwa kwa Ayubu?
Siku zote kumbuka hili Neno..
Mithali 24: 10 Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache.
Hivyo jipe moyo songa mbele ikiwa wewe ni mkristo, Kwasababu mwisho wa Mungu sikuzote ni mzuri, kama ilivyokuwa kwa Yusufu, kama ilivyokuwa kwa Ayubu, na ndivyo itakavyokuwa na kwako.
Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma”.
Shalom.
Tazama chini historia ya nyimbo nyingine za Tenzi:
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Kwa maombezi/ubatizo/ Kumpokea Yesu. Wasiliana nasi kwa namba hizi; +255789001312/+255693036618
Mada Nyinginezo:
MWAMBA WENYE IMARA
CHA KUTUMAINI SINA lyrics
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
TENZI ZA ROHONI
YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.
YESU AKALIA KWA SAUTI KUU.
SWALI: Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, Je! Ina maana hakuwa na wana wengine au hana wana wengine zaidi yake?
JIBU: Tusome..
Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.
Hivyo ndivyo inavyotafsiriwa na watu wengi na madhehebu mengi ya dini..Lakini sivyo inavyomaanisha hapo, Mungu kumwita Yesu mwanawe pekee, haimaanishi, hajawahi kuwa na wana wengine,(ambao ndio sisi), bali alimaanisha Yesu ni mwana-wake-wa-kipekee tofauti na sisi wengine aliyebakiwa naye, mwenye mahusiano ya kitofauti na wengine, mwana wa maagano ndio maana akimwita Kristo mwanawe pekee.
Ili kulithibitisha jambo hilo embu tutazame baadhi ya vifungu vya maandiko vinavyoelezea habari inayofanana na hiyo, Na hiyo si nyingine zaidi ya ile ya Ibrahimu na mwanawe Isaka..tusome.
Mwanzo 22:2 “Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia”.
Soma tena..
Mwanzo 22:12 “Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee”.
Soma tena…
Waebrania 11:17 “Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee”;
Unaona ukisoma mistari hiyo yote, unaweza kudhani Isaka ndio aliyekuwa mwana tu wa Ibrahimu hakuwa na wengine, lakini tunajua kuwa kabla ya Isaka alikuwepo Ishmaeli. Na baada ya Isaka walikuja wengine wengi (Mwanzo 25:1-4).
Lakini ni kwanini Mungu amwite Isaka kama mwana pekee wa Ibrahimu, ni kwasababu alikuwa mwana wa maagano, mwana wa ahadi, tofauti na wale wengine,…Isaka alifananishwa na Kristo
Hivyo Kristo Bwana wetu ndio mwana pekee wa Mungu, ambaye ameshikilia maagano yetu yote, kwa kupitia yeye, Mungu ametupenda tena, kwa kupitia yeye sisi tumebarikiwa, na kwa kupitia yeye, tunapata uzima wa milele, na tumaini la ufufuo baada ya kifo. Hivyo tukimwamini na kumpokea tunaingia katika huo mnyororo wa Pendo la Mungu.
“Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye”. Kama hujampokea huu ni wakati wako sasa.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
BWANA MUNGU NASHANGAA KABİSA lyrics ~Swahili (How Great Thou Art).
Toleo la kwanza kabisa la Wimbo huu liliandikwa na mtu mmoja raia wa Sweden, aliyeitwa Carl Boberg wimbo huu aliuandika mnamo mwaka 1885 baada ya kuvutiwa na mazingira aliyopishana nayo alipokuwa akitoka Kanisani yeye na marafiki zake. Anasema muda wa mchana walipokuwa njia hali ya hewa iliwabadilikia ghafla, wakaona wingu la tufani likitokea kwa mbali, na mara hiyo hiyo kukaanza kumulika mianga mingi kama ya radi angani, upepo mzuri ukaanza kuvuma juu ya mashamba yaliyokuwa pembeni, Na kisha manyunyu ya mvua matulivu yakaanza kudondoka juu yao, na baada ya muda kidogo, wingu lile la tufani likapotea, muda huo huo ukatokea upinde mzuri wa mvua angani..
Na alipofika nyumbani na kufungua madirisha atazame nje, aliona ufukwe ya mji wake kama vile kioo, akatazama upande wa pili akasikia ndege wazuri wakitoa milio yao na kwa mbali kegele za kanisa zikilia, Hapo ndipo wimbo huu ulipomjia kichwani kuutunga na kuuandika.
****
Bwana Mungu nashangaa kabisa,
Nikifikiri jinsi ulivyo,
Nyota, ngurumo, vitu vyote pia,
Viumbavyo kwa uwezo wako.
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.
Nikitembea pote duniani,
Ndege huimba nawasikia,
Milima hupendeza macho sana,
Upepo nao nafurahia.
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.
Nikikumbuka vile wewe Mungu,
Ulivyompeleka mwanao,
Afe azichukue dhambi zetu,
Kuyatambua ni vigumu mno.
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.
Yesu Mwokozi atakaporudi,
Kunichukua kwenda mbinguni,
Nitaimba sifa zako milele,
Wote wajue jinsi ulivyo.
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.
*****
Tujiulize na sisi tunao utaratibu kwa kukaa chini na kuushangaa utukufu wa Mungu na kumtukuza?..Au kila kitu tunaona ni kawaida tu..Kumbuka Sifa kamili kama hizi mbele za Mungu ni bora kuliko dua na sala tunazompelekea kila siku.
Mungu anataka kuona, na sisi tukiufurahia uumbaji wake, kwa kumwimbia.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia kwa email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.
MWAMBA WENYE IMARA
CHA KUTUMAINI SINA lyrics
USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.
KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?