Shalom, mtu wa Mungu.. karibu tujifunze biblia Neno la Mungu, ambalo ni mwanga wa njia yetu na taa iongozayo miguu yetu.
Leo tujikumbushe umuhimu wa kuwa wakaribishaji, na wa kujitoa kuifanya kazi ya Mungu.
Kipindi kirefu kidogo nimekuwa nikiwasiliana na binti mmoja humu facebook, ambaye anaishi kwao na wazazi wake, kiukweli ni binti anayempenda Mungu na kujitoa kwa Mungu ingawa ni mdogo kiumri. Amekuwa akitutumia maswali kadha wa kadha na kumjibu..kama ni mfuatiliaji wa masomo ya humu utakuwa umewahi kusoma swali tulilolijibu linalouliza… “Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?”…na lingine “Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?”.. Maswali haya mawili yaliulizwa na huyu binti..Na yapo mengine aliyouliza ambayo majibu yake tulimtumia pasipo kuyaweka wazi.
Huyu binti ni mtanzania lakini anaishi Zambia, karibu na mpaka wa Tanzania. Japokuwa ni binti mdogo lakini amekuwa akituuliza maswali kuhusu siku za mwisho na pia maswali ya namna ya kwenda kuwahubiria wengine Habari za Yesu mitaani. Katika udogo wake tulimtia moyo asiache kuwashuhudia wengine kwa bidii zote, haijalishi mazingira aliyopo, na mambo mengine mengi tulimshauri. Alienda kuyafanyia kazi hayo tuliyomshauri..na baada ya muda akatuletea mrejesho kwamba ametoka kuwashuhudia baadhi… “Anasema ijapokuwa huku nilipo makanisa yamefungwa kutokana na hofu ya corona, lakini mimi nilitoka hivyo hivyo sikujali.. na niliowashuhudia wengine wametaka namba zangu niwaombee na kuwaongoza sala ya toba” (kama kawaida hizo ni Habari za furaha kwetu sisi kama wakristo)..
Ni binti pia ambaye anayepitia changamoto nyingi, na hata nyumbani alipo sio kwamba ni watu wa Imani sana, hata wale anaowashuhudia na kuokoka anaogopa kuwakaribisha nyumbani kwasababu ya vita vya nyumbani….yaani kwa ufupi ni binti aliyejitoa kweli, na mwenye upendo wa ki-Mungu, yupo tayari kwenda kuwasaidia watu roho pasipo kujali mazingira aliyopo.
Sasa siku kadhaa nyuma, alipata mgeni kama yule Ibrahimu aliyekutana naye wakati anatoka kumpiga Kedorlaoma (Mwanzo 14:8-18)..
Hebu msikilize…
“Jana asubuhi sana niliamka nikawa naosha vyombo asa nikaenda kumwaga maji machafu ya vyombo nje nikachukua funguo nikapitia kufungua geti kubwa la nje , nikasikia sauti ikiita jina langu kwa sauti ya mbaali niliisikia lakini nikajua labda Ni mawazo tu, ikaita Tena ile nataka kuingia ndani nikainua macho getini nikamuona Mtu nisiyemjua anabisha hodi nikafungua nilivyofungua nikamsalimia kwa Adabu na heshima ya Hali ya juu kama kawaida yangu japo alikuwa m-baba mrefu mweusi amevaa nguo mbaya mbaya za (kimasikini) Mimi simjui asa nikajua labda Ni mgeni wa Baba labda alimpigia simu aje , kumbe sio, akaniambia unahitaji nini nikamwambia hamna Baba, huku naendelea kumsikiliza kwa makini kwa karibu , akaniambia chukua pesa hizi usiwe na shida, akanipa na vyakula Kisha akatoa pesa nyingine akanipa Sasa ile nimeshapokea pesa na vitu, nikamwambia YESU anakupenda akasema ndio nawewe (Mimi) anakupenda pia nikamwambia Asante! ,Sasa nikaweka vitu chini nikwambie umeokoka?, unaitwa Nani? Ile nainuka sikumuona Tena yule m-baba” .
Mwisho wa nukuu.
Sasa Baada ya kumuuliza alikupa nini kingine tofauti na hizo pesa?…akaniambia alimpa BIBLIA, TENZI ZA ROHONI, DIARY Pamoja na KALAMU.
Ndipo nikajua ni malaika kamtembelea…Na bahati nzuri huyu binti anayajua maandiko na analijua hili andiko pia…
Waebrania 13:2 “Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua”.
Hivyo baada ya tukio hilo ajijua kabisa ni malaika wa Bwana, na amani ya ajabu iliingia ndani yake..
Ndugu, haya mambo sio hadithi, ni vitu vya kweli kabisa…Kwasababu hata Mimi binafsi vilishawahi kunitokea mara mbili katika mazingira yanayokaribiana kufanana na huyu binti. Malaika wa Mungu mamilioni kwa mamilioni wanazunguka ulimwenguni..na wala usitegemee watakuja wamevaa nguo nyeupe na mabawa…Hapana!. Wale waliomtembelea Lutu hawakuwa na mavazi meupe, waliomfuata Ibrahimu chini ya mialoni ya Mamre hawakuwa na mavazi meupe…wanakuja kama watu tu wa kawaida kabisa..Ndio maana Paulo anasema “wengine mnawakaribisha Malaika pasipo kujua”.
Huyu binti yeye kaletewa zawadi chache za kumtia moyo kwamba azidi kusoma Neno na kujifunza (Ndio maana kapewa biblia na diary) Pamoja na kuwashuhudia wengine, na Bwana amemfanyia vile kumwonesha kuwa anampenda na yupo Pamoja naye kumhudumia katika mahitaji yake hata ya chakula hivyo asiogope! Na zaidi alimpa pesa nyingi sana..ndio maana kamtuma Malaika wake kumfariji. Na ule ni udhihirisho mdogo tu wa mambo yanayoendelea katika roho, katika roho anazungukwa na hilo jeshi la malaika wengi sana. Popote anapokwenda wapo naye, kumlinda na kumtunza.
Jiulize je angekuwa si mtu wa kujali na kujitoa kwa ajili ya roho za wengine malaika wa Bwana angetumwaje kwake?..Biblia inasema malaika ni viumbe wa roho wanaofanya kazi ya kuwahudumia Watoto wa Mungu wale watakaoirithi ahadi..na si kila mtu tu!
Waebrania 1:14 “Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?”
Sasa angetumwaje kumhudumia kama angekuwa si mtu wa kuifanya kazi ya Mungu?..Malaika wa Mungu angetumwa amletee zawadi gani ya kumfariji kama angekuwa ni binti wa kushinda tu kuzurula zurula mtaani au kuzungumza umbea au kutembea tembea na wavulana mitaani?..Unaona?..hakuna chochote angeambulia…
Na kitu kimoja ambacho hakifahamiki na wengi ni kwamba Malaika wana kazi ya kupeleka mambo yetu mema tunayoyafanya mbele za Mungu..Lolote zuri unalolifanya malaika wanalipeleka kama hoja mbele za Mungu..kama utapenda tukutumie somo juu ya hilo..utatutumia ujumbe mfupi inbox.
Naamini ushuhuda wa huyu dada ni darasa tosha kwetu!…Katika nafasi tulizopo, hebu tujitoe kwa Mungu…usijitoe ili utokewe na Malaika hapana!..jitoe kwasababu unaona umuhimu wa wengine kuujua ukweli na kupata wokovu maishani mwao. Nafasi ndogo unayopata kama ni shuleni, nyumbani, kazini, kwenye mitandano, usitengeneze visingizio vingi..kwamba siwezi kwasababu ya hichi au kile..kwasababu nipo bize..Ifanye kazi ya Mungu, wengi bado wanahitaji kuokolewa. Malaika wa mbinguni wanafurahi mtu mmoja tu anapotubu!
Bwana atubariki na Bwana atusaidie.
Kama hujaokoka!..Wokovu unaanzia hapa hapa duniani!..usidanganywe na shetani kwamba hakuna kuokoka duniani, usidanyike mtu wa Mungu…Tubu leo kama bado..na kisha acha yote machafu uliyokuwa unayafanya kama ulevi, uasherati, wizi, utazamaji pornograph, utukanaji, uuaji, usengenyaji na mengine yote..Na baada ya hapo, tafuta kanisa lililo hai, lililopo karibu na mahali ulipo, hakikisha unabatizwa hapo katika ubatizo sahihi wa jina la Yesu na wa kuzamishwa mwili wote(Matendo 2:38). Na baada ya hapo Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia.
Unyakuo upo karibu na hizi ni siku za mwisho..siku yoyote! Mambo yatageuka ghafla, unyakuo utapita, watakatifu watatoweshwa..dhiki kuu ya mpinga-Kristo itaanza, na ghadhabu ya Mungu itamwagwa duniani.. hakuna mtu atategemea, itakuwa ni ghafla tu!..kama vile corona ilivyozuka ghafla tu! pasipo ulimwengu kutegemea.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.
MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.
UFUFUO TUNAOUSUBIRIA UTAHITIMISHA YOTE.
HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.
MAJESHI YA PEPO WABAYA.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
KWANINI HUNA HAJA YA KUANDIKIWA JUU YA NYAKATI NA MAJIRA?
Rudi Nyumbani:
Print this post
Siku ile Bwana Yesu alipokufa biblia inatuambia makaburi yalipasuka na miili ya watakatifu wengi iliinuka, lakini katika ufufuo huo hawakuondoka pale makaburini mpaka siku Yesu alipofufuka, Ndipo wakaanza safari ya kuuelekea mji mtakatifu (Yerusalemu), Na walipofika kule biblia inatuambia wakawatokea watu wengi sana…
Lakini lipo swali tunaweza kujiuliza kulikuwa na umuhimu gani wale wafu watoke makaburini kwa kipindi kama kile, pili na ni kwanini walielekea mji mtakatifu Yerusalemu na sio mahali pengine..
Tusome.
Mathayo 27:50 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. 51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka; 52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; 53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi”.
Mathayo 27:50 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.
51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;
53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi”.
Maswali kama hayo, tukiweza kuyatafakari vizuri naamini yatatupa mwanga wa jinsi siku ile kuu ya ufufuo wa wafu(katika unyakuo) itakavyokuwa.
Sasa ni kwanini, wakati ule makaburi yapasuke na watakatifu wafufuke,..Ni kwasababu Mungu alikuwa anataka kuwathibitishia baadhi ya wale watu wake, kuwa tendo la ufufuo lipo kweli, na mwanawe Yesu Kristo amefufuka kweli kweli.. Na alifanya hivyo ili baada ya hapo wakawe mashahidi wa ufufuo wa wafu kwa watu wengine..Kwasababu wakati huo yalikuwepo makundi mengi ya watu waliokuwa hawaamini suala la ufufuo wa wafu (Masadukayo), Na wengine walikuwa wanapinga na kuwatangazia watu kuwa ameibiwa..Hivyo ili Mungu kuwathibitishia kuwa suala la Ufufuo lipo ndipo akaruhusu makaburi yapasuke, wafu wafufuke waonekane na watu wengi.
Lakini Je! Hilo lilionekana na kila mtu tu?
Jibu ni Hapana, bali lilionekana na wale watu (watakatifu) waliokuwa Yerusalemu wakati ule. Kama tu vile Bwana alivyofufuka hakumtokea tu kila mtu isipokuwa wale waliokuwa wanamwamini. Na hao wafu ni hivyo hivyo hawakuwatokea watu wote isipokuwa tu wale watakatifu..
Kwasababu biblia inatuambia wafu wale walielekea Yerusalemu. Ni kwa vile tu biblia haiwezi kueleza kila kitu, lakini tukio lile liliwaacha katika butwaa kubwa sana wale watu waliokuwa Yerusalemu..Jaribu kufikiria, unatembea kila kona unawaona ndugu zako wa kale waliokufa katika Bwana, wengi sana, unawaona waliokuwa majirani zako kitambo, na wengine wanazungumza na wewe kabisa wanakuambia mimi ni Yusufu, mimi ni Sulemani, mimi ni Yeremia n.k…
Wewe unadhani watu hao walioshuhudia utaanzaje kuwaaninisha kuwa hakuna ufufuo wa wafu? kuwa Kristo hakufufuka bali aliibiwa?
Ufufuo huo uliwapa uthibitisho mkubwa sana, Ili kwamba wakawe mashahidi wa kufufuka kwake ulimwenguni kote, hilo ndio lilikuwa lengo lake..
Lakini upo ufufuo mwingine tunaoungojea sasa, ambapo upo karibu sana kutokea kuliko tunavyofikiria..Wakati huo PARAPARANDA kuu ya Mungu italia kutoka mbinguni..Na tukio kama lile lile la kwanza litatokea kwa mara nyingine, la makaburi kupasuka..Lakini safari hii watanyanyuka watakatifu wengi sana, wa vizazi vyote vilivyotangalia duniani..watu wengi sana..
Wakati huo watakatifu walio hai hawatajua chochote kwanza, wala ulimwengu pia..Ili lile Neno la kwamba hatutawatangulia wafu waliolala litimie..
1Wathesalonike 4:15 “Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika HATUTAWATANGULIA wao waliokwisha kulala mauti. 16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; NAO WALIOKUFA KATIKA KRISTO WATAFUFULIWA KWANZA. 17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. 18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo”
1Wathesalonike 4:15 “Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika HATUTAWATANGULIA wao waliokwisha kulala mauti.
16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; NAO WALIOKUFA KATIKA KRISTO WATAFUFULIWA KWANZA.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo”
Vivyo hivyo na wao hawataonekana na kila mtu tu aliye duniani…
wataonekana na watakatifu watakaonyakuliwa, (Yaani wale watu tu waliozaliwa mara ya pili ndio watakaowaona)..…na wenyewe wataenda katika mji mtakatifu (Yerusalemu ya rohoni, soma Wagalatia 4:24-31)…
Siku hiyo sisi tuliokuwa hai siku tutakapowaona, ndio tutakapojua kuwa Ufufuo wenyewe umefika, na kitendo cha kufumba na kufumbua tutatoweka, hatutaonekana tena ulimwenguni..
1Wakorintho 15:51 “ Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, 52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.
1Wakorintho 15:51 “ Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,
52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.
Wakati huo dunia haitaelewa chochote!. Wengi watasema wameibiwa, kama ilivyokuwa kipindi cha Bwana Yesu, wengine watasema tumepotea tu! Watapatikana n.k. Lakini suala la kwamba kanisa limenyakuliwa hilo halitaaminika na wengi hata kidogo. Kwasababu tutakuwa ni kundi dogo sana kama vile Bwana Yesu alivyosema.
Hivyo ndugu, mimi na wewe tujue kuwa tunaishi katika hayo majira ya Kunyakuliwa kwa kanisa, Dalili zote zinathibitisha hilo, hakuna asiyejua.. Lakini Swali ni Je! tumejiwekaje tayari? Je! Parapanda ikilia leo, unao uhakika wa kunyakuliwa? Kumbuka baada ya wakati huo mlango wa rehema hautakuwa tena wazi kwa ajili yetu, Bali kitakachokuwa kinaendelea duniani ni kumiminwa kwa ghadhabu ya Mungu. Na hukumu.
Muda bado tulio bakiwa nao mfupi sana. Hivyo ikiwa wewe ni mmojawapo ambaye Kristo yupo mbali na wewe, basi chukua uamuzi wa leo hii kumgeukia na atakupokea na kukufanya mwana wake.
Bwana akubariki sana.
Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza
IJUE NGUVU YA IMANI.
KUZIMU ni mahali pa namna gani, Je! huko wanaishi watu wakifa na kwenda kupata mateso au ni vinginevyo?
USIRUHUSU MUNGU AWEKE UADUI KATI YAKO NA WATU WAKO.
MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?
WhatsApp
Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.
Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Karibu tujikumbushe baadhi ya mambo muhimu katika safari ya Imani.
Tukiwa kama wakristo ni wajibu wetu kuifanya kazi ya Mungu, kulingana na karama tulizopewa. Faida ya kuifanya kazi ya Mungu ni kubwa kuliko kutoifanya kabisa. Kwa jinsi tunavyozidi kuukaribia ule mwisho wa dunia, kazi ya Mungu inazidi kurahisishwa Zaidi lakini inazidi kuongezeka kiwango.
Kwamfano mtu anaweza kupewa alime shamba lenye kichaka la hekari mbili, aanze kwa kuondoa nyasi na miti yote na kisha alilime kwa jembe la mkono, na baada ya hapo apande mbegu, na mwingine anaweza kupewa kazi ya kuvuna hekari 10.
Sasa huyo wa kwanza amepewa kazi ngumu lakini kwa hekari chache..lakini huyo wa mwisho amepewa kazi nyepesi tu! Ya kuvuna lakini hekari nyingi. Na ndio hivyo hivyo siku hizi za mwisho, kazi ya Mungu si ngumu kwasababu haihusishi kulima, kupanda wala kumwagilia…bali inahusisha tu kuvuna!…Lakini hiyo haitoshi…mashamba ya mavuno ni mengi sana, hivyo inaifanya kazi iwe kubwa sana..
Bwana Yesu alisema…
Yohana 4:35 “ Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, INUENI MACHO YENU MYATAZAME MASHAMBA, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno. 36 Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja. 37 Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine. 38 Mimi naliwatuma MYAVUNE YALE MSIYOYATAABIKIA; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao”
Yohana 4:35 “ Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, INUENI MACHO YENU MYATAZAME MASHAMBA, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.
36 Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja.
37 Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine.
38 Mimi naliwatuma MYAVUNE YALE MSIYOYATAABIKIA; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao”
Anaendelea kwa kusema…
Mathayo 9:36 “Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji. 37 Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, MAVUNO NI MENGI, LAKINI WATENDA KAZI NI WACHACHE. 38 Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake”.
Mathayo 9:36 “Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.
37 Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, MAVUNO NI MENGI, LAKINI WATENDA KAZI NI WACHACHE.
38 Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake”.
Ndugu katika Kristo, zama hizi sio zama za kanisa la kwanza ambalo utakwenda mahali ambapo utakuta watu ambao hawajawahi kumsikia kabisa Yesu..(hao watu wapo ila ni wachache sana) asilimia kubwa ya watu tayari wameshawahi kumsikia Yesu mahali Fulani, wawe nii wakristo au wasio waKristo, tayari wameshawahi kumsikia Yesu..fanya utafiti mwenyewe, mfuate mtu yeyote muulize Je! Unamfahamu Yesu..utasikia jibu atakalokuambia..Hiyo ni kwasababu tayari wengine walishapanda na kutia maji, tayari yanao msingi Fulani ndani ya Maisha yao…kazi iliyobaki ni mavuno tu!.
Na kazi ya mavuno sio ngumu! Ni nyepesi sana isipokuwa ni kubwa sana!..Kwahiyo tunategemewa kufanya kazi sana kuliko watu wa kanisa la kwanza. Wengi wameshamjua Kristo tayari, lakini bado wapo mashambani (ulimwenguni) kazi inayohitajika ni kuwatoa mashambani na kuwaingiza ghalani mwa Bwana, wakibaki huko mashambani wapo ngedere, wapo wezi kuiba, wapo ndege, wapo wadudu wanaoharibu mazao n.k..
Lakini wakiwekwa ghalani kwa Bwana watakuwa salama..mbali na wadudu na Wanyama, na wezi…watakuwa wamefichwa mbali na kuhifadhiwa na kila aina ya uharibifu.
Ghalani mwa Bwana ni wapi?
Mtu aliyemtii Kristo na kuamua kuacha uovu na kumgeukia Yeye kikamilifu na kubatizwa, katika ulimwengu wa roho anakuwa tayari kashaingia ghalani mwa Mungu, kafichwa na Mungu…ataonekana kwa macho lakini katika roho hataonekana, uhai wake unakuwa umefichwa kama biblia inavyosema katika..
Wakolosai 3:3 “ Kwa maana mlikufa, NA UHAI WENU UMEFICHWA PAMOJA NA KRISTO KATIKA MUNGU. 4 Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu”.
Hivyo Ghala la Mungu linaanzia hapa hapa duniani!..Wokovu unaanzia hapa hapa duniani. Kama upotevu unaanzia hapa hapa duniani, na wokovu ni hivyo hivyo…Huwezi kumwona mtu ambaye anafanya uovu wa kupitiliza na kusema bado hajapotea kwamba atapotea akishakufa hapana!..katika uovu wake tayari kashapotea, labda ageuke tu! Lakini pale alipo tayari kashapotea!…hali kadhalika huwezi kusema mtu mwenye haki bado hajaokoka..na kwamba ataokoka akifika kule…huo ni uongo wa shetani…katika haki yake tayari kashaokoka!!
Wokovu unaanzia hapa hapa duniani…GHALA LA MUNGU LINAANZIA HAPA HAPA ULIMWENGUNI…Mavuno yanaingizwa ghalani hapa hapa ulimwenguni…mbingu ni mwendelezo wa ghala, ambalo tayari limeshaanzia kazi zake duniani.
Kwahiyo ni wajibu wetu kuitenda kazi ya Mungu…Tayari wameshamsikia Yesu akitajwa katika Maisha yao, pengine tangu utoto wao? Wamebakia tu kuwa wakristo-jina, wakristo wa-kidini tu lakini Yesu hayupo ndani ya mioyo yao….hivyo hatua iliyobaki ni kuwaeleza kwa maarifa yote umuhimu wa Yesu katika Maisha tofauti na walivyosikia huko nyuma. Jinsi Yesu anavyoweza kuwabadilisha watu mioyo.
Lakini likumbuke pia hili neno la Bwana “Mavuno ni mengi ila watenda kazi ni wachache”. Maana yake kazi bado ni kubwa sana…na hivyo ni wa kujitoa sisi na pia kumwomba Bwana anyanyue watenda kazi wengi duniani kote. Kipengele hicho cha maombi ni muhimu sana katika Maisha na kinapuuziwa na wengi…lakini ni kipengele cha muhimu sana cha kuomba Bwana apeleke watenda kazi. Na sisi pia kila mmoja wetu akisimama katika nafasi yake.
Bwana atusaidie na kutushika mkono, na Zaidi sana atubariki wote.
KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.
KAMA MHUBIRI NI WOKOVU UPI UNAUPELEKA KWA WATU?
UTAFIKA WAKATI WA WEWE KUACHWA NYIKANI.
MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.
HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Kwanini Mungu aitwe Bwana wa majeshi? Je! Ni kweli anayo majeshi au ni cheo tu amependa kujivika?
Watu wengi hatufahamu kuwa Mungu anayo majeshi yake…Ni kweli hili jina limekaa sana ulimini mwetu, lakini bado hatufahamu vizuri ni kiwango gani Mungu anajiita Bwana wa majeshi..Naamini siku tukilifahamu hilo vema basi tutaishi maisha yasiyo na woga na wasiwasi hata kidogo hapa ulimwenguni.
Kumbuka hajiiti Mungu wa “Jeshi” kana kwamba ni moja hapana bali anajiita Mungu wa “Majeshi” ikiwa na maana ni mengi.
Ni majeshi ambayo yaanzia mbinguni mpaka duniani. Na kama tunavyojua sikuzote majeshi kazi yake, kulinda usalama, kutunza amani, na kuupigania ufalme, kinyume na maadui zao.
Mungu alijitambulisha kama Bwana wa Majeshi, sio kwamba alitaka sisi tumwogope, Hapana, bali alitaka sisi tujue nguvu aliyonayo katika kutupigania watu wake dhiki maadui zao (Shetani na mapepo yake). Embu Jaribu kutengeneza picha Mungu angejiita tu majina haya, ingekuwaje?
Unadhani hiyo ingetosha tu?..Kwamfano tungekuwa tunapitia katika vita vikali tumezungukwa na maadui wa mwilini na rohoni, kilichobaki ni kufa na kupona, unadhani Bwana mpaji wetu(Yehova yire), tungemuhitaji wakati huo? Wakati unaona unakaribia kuchinjwa Je, utamwambia Mungu nipatie mali?..Jibu la, kinyume chake atamuita Bwana kwa nguvu zote asimame mwenyewe akupiganie na kuwasambaratisha maadui zako ili upone.
Hapo ndipo jina la BWANA WA MAJESHI linapoitwa (Yehova-Saboati)…
Ilifika wakati Daudi alikuwa anakwenda kupigana na adui yake mkubwa Goliathi, moyoni alijua kabisa mtu kama huyu wa vita, haiwezekani kumshinda, Lakini alipogundua kuwa yupo Bwana wa Majeshi Mungu wa vita,karibu naye ndipo aliposimama kwa ujasiri na kwenda kupigana naye..tusome..
1Samweli 17:43 “Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake. 44 Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni. 45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe KWA JINA LA BWANA WA MAJESHI, MUNGU WA MAJESHI ya Israeli uliowatukana. 46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli. 47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu”.
1Samweli 17:43 “Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.
44 Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni.
45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe KWA JINA LA BWANA WA MAJESHI, MUNGU WA MAJESHI ya Israeli uliowatukana.
46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.
47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu”.
Unaona hapo Daudi alimuita Bwana wa Majeshi, aje kumsaidia..
Ndugu fahamu kuwa, Unapokuwa mkristo, hupaswi kuwa woga wa kitu chochote, Inasikitisha kuona ni mkristo wa muda mrefu halafu bado anaogopa wachawi na washirikina, pamoja na mapepo na majini.
Shetani mwenyewe anawashaangaa, anapoona watu wa Bwana wa majeshi kama sisi, nasi tunamwogopa yeye..
Kuna wakati Elisha alikuwa anatembea na mtumishi wake Gehazi, wakafika mahali wakajikuta wamezungukwa na majeshi mengi ya maadui zao, yule mtumishi akawa anatetemeka na kuogopa sana..Lakini Elisha hakuogopa kwasababu alijua majeshi ya Mungu wa Israeli aliyo nayo ni mengi kuliko ya wale wengine..Bwana wa majeshi ndio nguvu yake.. Ndipo Elisha akamwomba Mungu amfungue macho alione hilo.
2Wafalme 6:17 “Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote. 18 Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha. 19 Elisha akawaambia, Njia hii siyo, na mji huu sio, nifuateni mimi, nami nitawapeleka kwa mtu yule mnayemtafuta. Akawapeleka Samaria”.
2Wafalme 6:17 “Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.
18 Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha.
19 Elisha akawaambia, Njia hii siyo, na mji huu sio, nifuateni mimi, nami nitawapeleka kwa mtu yule mnayemtafuta. Akawapeleka Samaria”.
Hivyo hata wewe ukiwa unapitia mahali ambapo, unaona vita vikali vipo mbele ya basi mwite Bwana wa Majeshi atakusaidia,..
Lakini ikiwa wewe bado upo nje ya wokovu, nataka nikuambie hata umwite vipi Mungu katika vita vyako hawezi kukusikia wala kukusaidia, kwasababu wewe sio wa ufalme wake. Wachawi watakutesa, mapepo yatakutesa, ibilisi atakutesa,.. Lakini ukitaka leo awe upande wako, basi ni sharti kwanza umpokee YESU KRISTO katika moyo wako. Akusemehe dhambi zako, ndipo pale utakapoliita jina la Bwana wa majeshi atakusikia na kukusaidia.
Ikiwa upo tayari Kumpa YESU leo maisha yako basi bofya hapa, kwa Sala ya toba >>> SALA YA TOBA.
Pia yapo mafundisho mengi unahitaji kujua juu ya majeshi ya mbinguni(malaika) wanavyofanya kazi na sisi(tuliookoka), hivyo nakusihi fungua na masomo mengine hapa chini, ufahamu zaidi juu ya ulimwengu wa roho wa malaika wa Bwana na utendaji kazi wao.
Zaburi 24: 10 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Bwana wa majeshi, Yeye ndiye Mfalme wa utukufu.
Mungu akubariki.
ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.
WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.
JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.
Yapo makundi tofauti tofauti ya Malaika wa Mbinguni. Wapo Maserafi ambao ndio tutakaowazungumzia leo, wapo Makerubi (ambao ndani yake ndio alikuwa shetani), wapo wenye uhai wanne, wapo wazee ishirini na nne.. na wapo Malaika wa vita ambao ndani yake ndio wakina Mikaeli na wenzake.
Na katikati ya hayo makundi, yamegawanyika vipengele vingi!..wapo malaika wenye mbawa na wasio na mbawa, wapo wenye maumbo kama ya wanadamu lakini pia wapo wenye maumbo kama ya wanyama na ndege.
Kwa ufafanuzi kuhusu makundi hayo ya Malaika, mwisho kabisa wa somo hili utaona LINK za masomo hayo, zifungue ili uweze kuzisoma.
Sasa Maserafi ni kundi la Malaika ambao kazi yao ni kumsifu na kumtukuza Mungu mbinguni, Wamekizunguka kiti cha enzi kwa maelfu yao, wakimsifu Mungu usiku na mchana. Maserafi wana mabawa sita kila mmoja. Mawili yanakifunika kichwa kufunua kuwa KUFUNUA MAMLAKA YA MUNGU, NA UTAWALA WA KIMUNGU. Kwamba Mungu ndiye kichwa cha mambo yote. Na pia wanafunika kichwa kwasababu wanaona hata hawastahili kumtazama Mungu, wala Mungu kuwatazama wao kwajinsi yeye Mungu alivyo mtakatifu sana.
Na pia hawaishii tu! Kufunika kichwa..bali wanafunika pia Miguu, kufunua jambo kufunua kuwa hawastahili hata Mungu aliye mtakatifu kuona miguu yao.
Na mabawa mawili yaliyosalia ni kwaajili ya kuruka (yaani kupaa).
Kundi hili la malaika tunaona limetajwa katika Kitabu cha Isaya.
Isaya 1: 1 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu. 2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka. 3 Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi, dunia yote imejaa utukufu wake”.
Isaya 1: 1 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.
2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.
3 Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi, dunia yote imejaa utukufu wake”.
Bwana aliwaumba malaika hawa kwa lengo hilo la kumsifu yeye na kuufunua utakatifu wake kwa viumbe vyake vyote…ndio maana katika sifa zao wanaanza na neno.. “Mtakatifu mtakatifu”.
Na malaika hawa (maserafi) wanatufundisha na sisi jinsi ya kumsifu Mungu..Kwamba tuwapo mbele zake tujisitiri!..
Hebu tujifunze kitu hapa!..sio malaika wote wanaofunika vichwa mbele za Mungu…lakini kundi hili linafanya hivyo? kwanini?…Huoni pia katika kanisa kuna kundi la watu ambao ni lazima lifunike vichwa liwapo ibadani?..na sio tu kufunika kichwa bali hata kujisitiri mwili mzima ikiwemo na miguu.
1Wakorintho 11:5 “Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa”
Na ukiendelea kusoma mistari hiyo utaona suala la wanawake kufunika vichwa ibadani limehusishwa na “Malaika”..kasome 1Wakorintho 11:10.
Kwahiyo pia si vyema mwanamke kuingia kanisani bila kufunika kichwa wala kujisitiri mwili..Utakuta mwanamke anaingia ibadani kichwani kaweka wigi, chini kavaa kimini au suruali. Jiulize hapo unakwenda kumwabudu Mungu gani?..Maserafi wasio na dhambi wanajisitiri wewe uliye na dhambi inakupasaje?
Mwisho, Kumbuka Malaika yoyote yule sio wa kuabudiwa!..wala hatupaswi kuweka picha au sanamu ya malaika yoyote yule na kuisujudia, ni Mungu pekee ndiye anayestahili kuabudiwa na kusujudiwa.
Bwana atubariki.
MAKERUBI NI NINI?
WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?
Kuna Malaika wangapi?
Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?
Malaika wa maji ni yupi na Je kuna aina ngapi za malaika?
Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?
Mjumbe asiyekuwa na ujumbe:
Ukisoma katika biblia utakumbuka habari ile ya Daudi na mwanawe Absalomu, jinsi walivyoingia katika mapambano makali,.mpaka kuepelekea vita vizito kupiganwa kule msituni..Kama wengi wetu tunavyofahamu, katika vita vile Daudi hakuwepo bali alimtuma amiri jeshi wake mkuu aliyeitwa Yoabu, kupigana nao. Lakini kabla ya kuanza vita Daudi alimwagiza Yoabu, kuwa ahakikishe kijana hawamuui bali wanamleta mikononi mwake akiwa mzima.
Lakini Yoabu alipomkamata Absalomu, alimuua, na kisha akamtupa kwenye shimo refu sana. Na Israeli walipoona kiongozi wao Absalomu amekufa, vita vikaishia pale pale, watu wote wakatawanyika na kwenda makwao.
Sasa kilichokuwa kimebakia, ni kumpelekea Daudi taarifa za vita, Lakini ni nani wa kumpelekea Daudi Habari ya kifo cha mwanawe. Hapo ndipo wakatokea wajumbe wawili mmoja aliitwa, Ahimaasi, mwana wa Sadoki na mwingine, alikuwa ni mkushi.
Sasa huyu Ahimaasi, akamwomba Yoabu, akimbie ampelekee ujumbe Mfalme Daudi kuhusu vita, lakini Yoabu alimwambia, kwasasa wewe huwezi kupeleka ujumbe, na sababu ya kutopeleka ujumbe ni kwasababu zile sio Habari njema apelekazo..
Ndipo Yoabu akamwita kijana mwingine mkushi akamtuma badala yake akamwambia nenda ukamwambie mfalme uliyoyaona..
2Samweli 18:21 “Ndipo Yoabu akamwambia Mkushi mmoja, Nenda ukamwambie mfalme hayo uliyoyaona. Na huyo Mkushi akajiinamisha mbele ya Yoabu, akaenda zake mbio.”
Ndipo huyu mkushi akatii akaondoka mbio mara moja..Lakini yule Ahimaasi, alipoona mwenzake katumwa halafu yeye bado kabaki, akaendelea kumsisitiza Yoabu na yeye aende..Tusome.
2Samweli 18:22 “Ndipo Ahimaasi, mwana wa Sadoki, akamwambia Yoabu mara ya pili, Haidhuru, tafadhali nipe ruhusa, nipige mbio na mimi nyuma ya huyo Mkushi. Naye Yoabu akasema, Mbona wewe unataka kupiga mbio, mwanangu, kwa maana hutapata kitu kwa habari hizo unazopeleka? 23 Akasema, Haidhuru, nitapiga mbio. Akamwambia, Haya, piga mbio. Ndipo Ahimaasi akapiga mbio, akishika njia ya uwandani, akampita yule Mkushi”.
2Samweli 18:22 “Ndipo Ahimaasi, mwana wa Sadoki, akamwambia Yoabu mara ya pili, Haidhuru, tafadhali nipe ruhusa, nipige mbio na mimi nyuma ya huyo Mkushi. Naye Yoabu akasema, Mbona wewe unataka kupiga mbio, mwanangu, kwa maana hutapata kitu kwa habari hizo unazopeleka?
23 Akasema, Haidhuru, nitapiga mbio. Akamwambia, Haya, piga mbio. Ndipo Ahimaasi akapiga mbio, akishika njia ya uwandani, akampita yule Mkushi”.
Hivyo wote wawili wakaanza safari, lakini tofauti ya mjumbe wa kwanza na yule wa pili ni kuwa yule mkushi, alikuwa na ujumbe wa kupeleka kwa yale aliyoyaona vitani jinsi Absalomu alivyouliwa, lakini yule mwingine hakuona chochote, alisikia tu..
Sasa biblia inatuambia yule wa pili alipiga mbio Zaidi ya yule wa kwanza na kufika kwa mfalme, (hatujui alipiga short-cut au vipi), lakini alifikia wa kwanza kuliko yule mwingine.
Akafika mpaka malangoni mwa mfalme, akaulizwa, umeleta ujumbe gani? Akasema, Mungu ashukuruwe kwa kuwa maadui zako wametawanyishwa.
Lakini Daudi alipomuuliza Habari za kijana? … sikiliza majibu yake.
2Samweli 18:29 “Mfalme akauliza, Je! Yule kijana, Absalomu, yu salama? Ahimaasi akajibu, Yoabu aliponituma mimi mtumishi wa mfalme, mimi mtumishi wako, NALIONA KISHINDO KIKUBWA, LAKINI SIKUJUA SABABU YAKE”.
Daudi aliposikia hivyo akamwambia simama pembeni, akamngojea yule mwingine afike.. Ndipo alipofika yule mwingine na kuulizwa..naye akajibu, “wote wainukao ili kukudhuru, na wawe kama alivyo yule kijana”(akimaanisha kuwa Absalomu Amekufa).
Ndipo Daudi aliposikia vile alienda kulia sana, akimwombolezea mwanawe..
NI NINI BWANA ANATAKA TUJIFUNZE?.
Kama haujafikiria, kuwa mhubiri, au mchungaji, au nabii au mwinjilisti au mtume, au mjumbe yoyote wa Mungu, kwa njia yoyote ile,iwe katika uimbaji, au uandishi n.k. ni vizuri kwanza ukafahamu na kuuelewa vizuri ni ujumbe gani unakabidhiwa kuupeleka..
Ujumbe/ Agizo kuu tulilopewa na Bwana Yesu kwa mtu yeyote anayetaka kuifanya kazi ya Mungu ni hili..
Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; 20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi;..”
Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi;..”
Sasa jiulize, Je, katika kujibidiisha kwako kuwahubiria watu, Je! Lengo lako ni kuwafanya watu kuwa wanafunzi wa Kristo?, Je! Ni kuwafundisha kuyashika yale yote Yesu aliyotuamuru au mambo ya kidunia tu?..
Wengine wakiulizwa kwanini auhubiri injili kama ile ya mitume injjili kamilifu na ya utakatifu, watakwambia, mimi sikuitwa kuhubiri injili hiyo! Mimi nimeitwa kuwa mfariji tu!! ..Nataka nikuambie ndugu hapo ni sawa na unakimbia bure bila ujumbe wowote kama yule Ahimaasi. Kumbuka hapo kwenye Mathayo 28, agizo hilo lilipewa kwa watu wote kiujumla, hapo Bwana alikuwa hazungumzi na Petro peke yake, au Mathayo peke yake, au Filipo…alikuwa anazungumza na wote waliokuwepo pale Pamoja na sisi wote tunaosoma.
Ikiwa mafundisho yako, hayalengi kuwavuta watu wa Kristo, kinyume chake, ni kuwahubiria tu jinsi ya kufanikiwa hapa duniani..Basi ujue wewe ni mjumbe usiyekuwa na ujumbe.. Na kazi yako haina faida yoyote, haijalishi utakuwa unawakusanya maelfu ya watu kiasi gani kukusikiliza, au wanakusifia kiasi gani.
Ujumbe tuliopewa ni mmoja tu, nao ni kuwafanya “mataifa yote kuwa wanafunzi wake”. Na unamfanyaje mtu kuwa mwanafunzi, Bwana Yesu alishasema katika Luka 14:27
Hivyo chochote tukihubiricho hakipaswi kwenda mbali na kiini hicho cha agizo..Hata kama tutahubiri hayo mengine lakini kiini hicho kionekane, na hiyo ni kwa faida yetu wenyewe ili kazi yetu isiwe bure mbele za Mungu.
Bwana akabariki.
Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?
SADAKA YA MALIMBUKO.
KUOTA UNACHEZA MPIRA.
MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.
WAKATI WA KRISTO KUSIMAMA,UMEKARIBIA SANA.
Ijue nguvu ya sadaka.
Kuna nguvu ya kipekee iliyo ndani ya sadaka ambayo watu wengi hawaifahamu.
Mungu anaweza kweli akawa ni Rafiki yako mkubwa sana, anaweza kweli akawa anazungumza na wewe, na ukaisikia sauti yake, ikikwambia nimekusikia mwanangu na nitakupa kitu Fulani..Lakini ukashangaa kitu hicho hujakipata japokuwa alikuahidia kabisa atakuwa na wewe..
Hiyo ni kutokana na kuwa ulichomwomba Mungu, hukukiambatanisha na sadaka..Leo hii nitakuonyesha mfano wa watu wa namna hiyo katika biblia ambao walimwomba Mungu sana Na Mungu akawasikia na kuwaahidia kuwa anatakuwa nao, lakini majibu yalikuja tofauti na walivyokitarajia mpaka walipogundua kuwa tatizo ni nini?….
Bwana atusaidie tuifahamu Nguvu ya Sadaka.
Hiyo ni Habari ya wana wa Israeli siku ile walipotaka kwenda kupigana na ndugu zao Benyamini kutokana na wao kuwa na tabia ya kuutamia uovu wa wazinifu, bila kuwashaadhibu. Hivyo vita vikapangwa dhiki yao na waisraeli wengine wote waliosalia, Sasa Israeli wote walimwomba Mungu aende nao ili wakawapige Benyamini, mara ya kwanza, Mungu akawajibu akawaambia nitakuwa Pamoja nanyi, nanyi mtashinda, Lakini walipokwenda walipigwa mapigo makubwa sana..
Wakamrudia Mungu wakamuuliza tena, Je utakwenda Pamoja nasi mara hii nyingine?, Mungu akawaambia ndio nitakuwa Pamoja nanyi, lakini walipoenda kapigwa, tena wakafa watu wengi kweli.
Wakamrudia tena Mungu kwa mara ya tatu, lakini safari hii hawakumrudia mikono mitupu, walimrudia kwa kufunga, na kwa sadaka nyingi sana, jambo ambalo hapo Mwanzo hawakulifanya..Kisha wakamuuliza Mungu tena Je! Utakwenda Pamoja na sisi, ndipo Mungu akawaambia, Hakika nitakwenda Pamoja na nyie..
Na kweli walipokwenda waliwapiga Wabenyamini wengi sana, wakatoka na ushindi mnono (Waamuzi 20:22-29)..Hapo ndipo walipojua nguvu ya sadaka ipo wapi!
Kwa marefu ya Habari hiyo na fundisho lake fungua hapa usome. >>> UMUHIMU WA SADAKA.
Hata wewe, inawezekana unamtii Mungu sana, unajibidiisha sana katika kumwomba kwa bidii, lakini kwenye suala la kumtolea Mungu, hulizingatii sana, unaona kama halina umuhimu kwa mkristo, ni pengine kwasababu hukujua nguvu ya sadaka…
Ndugu Ijue nguvu ya sadaka..
Umekuwa ukimwomba Mungu akupe kitu Fulani, na muda mrefu umepita..Leo hii fahamu kanuni za kupokea kutoka kwa Mungu. Kumbuka Mungu hana shida na fedha zako..Kwasababu vyote ni mali yake, alishasema hivyo (Hagai 2:8) , lakini anataka kuona mtu anayemwomba anao moyo wa kujali..Hicho tu..
Pale unapomtolea kinono, ndipo unapougusa moyo wake Zaidi na kuona sababu ya kwanini wewe akujibu haraka kuliko yule mwingine asiyemjali?. Fedha unazomtolea Mungu, zinakwenda katika kuwabariki wengine pia rohoni,
Hivyo unapomwomba Mungu akupe, au akutendee jambo lolote, hakikisha kwa uwezo ulio nao, ambatanisha sadaka yako tena iliyo NONO ya hicho unachomwombea… Usiombe tu Mungu nipe, gari, nipe nyumba, nipe hiki, nipe kile halafu huna mpango wa wewe pia kumtolea Mungu, nataka nikuambie, ukiwa na tabia hiyo majibu yako yatakuwa ni ya kuchelewa sana.
Hivyo anza leo, kujifunza kuambatanisha sadaka ya kila unachomwomba Mungu, kwa jinsi Mungu alivyokujalia…
Ijue nguvu ya sadaka..
Na kumbuka pia sadaka hiyo haipaswi kupelekwa sehemu nyingine yoyote Zaidi ya madhabahuni pa Mungu.. Haipaswi kupelekwa kwa watoto yatima, au watu wasiojiweza, au kwa mtu mwingine yoyote hapana..Inapaswa ifikishwe madhabahuni pa Mung utu! yaani Kanisani kwako.
Hivyo zingatia vigezo hivyo, Na hakika utaona matokeo chanya, katika maombi yako.
Hiyo ndiyo nguvu ya sadaka.
Bwana akubariki.
Soma masomo mengine chini…
TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.
HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.
HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.
FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.
KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?
NGUVU YA MSAMAHA
UNYAKUO.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia leo tena.
Vipo vipindi tofauti tofauti ambavyo kila mkristo atavipitia…maana biblia inasema katika..
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; …. 4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”.
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; ….
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”.
Hata uwe unampendeza Mungu kiasi gani/ hata uwe mkamilifu mbele za Mungu kiasi gani..ni lazima utapitia vipindi vya kulia tu katika Maisha yako!..ni kweli asilimia kubwa ya Maisha yako itatawaliwa na furaha na amani..lakini ni lazima utapitia tu vipindi tofauti tofauti vya kulia na vya huzuni.
Sasa katika Imani pia vipo vipindi ambavyo utamwona Mungu sanaaa..na vipindi ambavyo hutamwona (utaona kuna ukimya Fulani maishani mwako)!…Sio kwamba atakuwa amekuacha kabisa! Au hakufuatilii wala kukusaidia…Hapana atakuwa yupo anakuona na kukujua lakini atakuwa kama amejiepusha na wewe”. Bwana Yesu kuna kipindi alisema “Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha”…hivyo huo wakati wa kuachwa upo!…Wengi hawalijui hili, ndio maana wanapopitia kipindi Fulani cha Maisha wanarudi nyuma na kuuacha wokovu…
Sasa leo tutajifunza hicho kipindi ni kipi lakini kabla ya kuendelea mbele zaidi hebu usome mfano huu taratibu sana, kisha tutaendelea…
Luka 15:3 “Akawaambia mfano huu, akisema, 4 Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda NYIKANI, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone? 5 Naye akiisha kumwona, HUMWEKA MABEGANI PAKE AKIFURAHI. 6 Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea. 7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu”.
Luka 15:3 “Akawaambia mfano huu, akisema,
4 Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda NYIKANI, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone?
5 Naye akiisha kumwona, HUMWEKA MABEGANI PAKE AKIFURAHI.
6 Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea.
7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu”.
Mfano huo unaonyesha ni jinsi gani..Bwana anaweza akawaacha kondoo 99 nyikani na kwenda kumtafuta kondoo mmoja aliyepotea. Umewahi kujiuliza kwanini awaache wale kondoo 99, na kwanini asiende nao?..na kwanini awaache NYIKANI na si kwenye zizi, mahali palipo salama?…
Maana yake ni kwamba anawaacha peke yao sehemu ya wazi isiyo na uzio, ambayo inaonekana ni sehemu hatari, lakini ni salama….Sehemu ambayo Wanyama wakali wanapita, sehemu ambayo inaogopesha!…na mbaya zaidi wanaachwa peke yao…Na lengo la Bwana kuwaacha ni ili akatafute kondoo wengine..
Sasa hao kondoo walioachwa nyikani pengine ni wewe unayepitia ukame sasa, humwoni Bwana kama ulivyomwona wakati umeokoka. Sasa ufanye nini katika hiyo nyika yenye utata?
Kumbuka hapo ni nyikani, mahali pasipo na uzio.. hivyo sio wakati wa kuzunguka zunguka huko na kule…kaa hapo hapo ulipo ndio mahali salama!…hapo hapo mahali Bwana alipokuacha!..(maana yake ni kwamba anaelewa kabisa mahali alipokuacha utakuwa salama mpaka atakaporudi) tulia hapo hapo hata kama ukitazama kushoto humwoni Bwana, ukitazama kulia umwoni Bwana kama ilivyokuwa hapo kwanza…wewe tambua kuwa hapo ulipo upo sehemu salama..lishike Neno lake lile lile na Imani!…
Haupo ndani ya uzio, ikiwa na maana kuwa vishawishi vya kukuvuta utoke kwenye mstari wa wokovu, utaviona, usianze kuzurula…wala kuhama hama…tulia hapo hapo….Hali kadhalika pembeni unaweza kuona dalili ya kudhurika na wanyama wanaopita kule, na unaweza kuona kama vile hakuna ulinzi, usiogope! Kaa hapo hapo ndio sehemu salama (aliyekuacha hapo sio mjinga)….Hivyo tumia muda wako kujifunza Neno na kuwaimarisha wengine na kuwalinda wasitoke kwenye hifadhi ya Mungu..kwa kuwafundisha wokovu na kuwafariji mpaka wakati wa Bwana kurudi.
Kumbuka tena kuna wakati Fulani Kristo alikuweka mabegani alipokupata…lakini si wakati wote utakuwa mabegani mwake…wakati ukiwa mabegani mwake ulikuwa unamwona kwenye ndoto kila siku, ulikuwa unauhisi uwepo wake kila mahali, ulipomwomba kitu ulikipata papo kwa hapo…(wakati huo ulikuwa mabegani mwake, mbingu ilifurahia kukupata) lakini hautakuwa hivyo siku zote…utafika wakati utashushwa mabegani na wewe utakwenda kuungana na wenzako nyikani na Bwana atakwenda kutafuta kondoo wengine waliopotea.
Kama ni leo umempa Kristo Maisha yako, basi uwe tayari kwa hicho kipindi kuja mbele yako. Jifunze kumwelewa sana Bwana wakati huu wa sasa, ambao unamwona sana… kwasababu wakati wa ukame utafika!..kama hutamwelewa sana wakati huu, wakati wa kuachwa nyikani utaikimbia na kuiacha nyika.
Na hapo ndipo watu wengi walipopotelea. Imani ni ya kuilinda sana.
Bwana atubariki
MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO
MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.
IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
JUMA LA 70 LA DANIELI
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Ukisoma kitabu cha Warumi sura ya 9, ya 10, na ya 11..utaona mambo mazito sana mtume Paulo aliyokuwa akiyazungumza juu ya ndugu zake wayahudi. Akieleza jinsi neema ya Mungu ilivyoondolewa kwao, kiasi kwamba hata wangehubiriwa vipi injili wasingeweza kuipokea.
Chukua muda kwa wakati wako, pitia sura hizo kwa utulivu sana, ukisoma juu juu hutaona chochote, lakini ukisoma kwa utulivu huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, nakuambia hutaichezea hata kidogo hii neema tuliyopewa sisi watu wa mataifa.
Mtume Paulo alipewa kulijua hilo mpaka akawa anasema, anayo huzuni nyingi, na maumivu yasiyokoma moyoni mwake kwa ajili ya ndugu zake (yaani wayahudi), maumivu ya kila siku, akijua kuwa wokovu umeondolewa kwao..
Kiasi kwamba alitamani hata kama ingewezekana yeye mwenyewe aupoteze wokovu wake, atengwe na Kristo ili kusudi kwamba ndugu zake wote wapone, basi angefanya hivyo..soma..
Warumi 9:1 “Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu, 2 ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu. 3 Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe NIHARIMISHWE NA KUTENGWA NA KRISTO kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili”;
Warumi 9:1 “Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,
2 ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.
3 Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe NIHARIMISHWE NA KUTENGWA NA KRISTO kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili”;
Kauli hiyo si rahisi kuizungumza, lakini kwa huruma ya watu wengine, na huzuni unayoisikia moyoni mwako inakulazimu uitamke, si kwamba unatamani iwe hivyo, lakini kama ingewezekana.. Ni sawa leo umuone mtoto wako mchanga, kapata ajali halafu kakatika mikono, halafu anatapata tapa pale chini kwa maumivu,akilia, ni wazi kuwa utatamani ungeyapitia wewe yale maumivu yake..Kuliko kumuona anaendelea kuteseka katika ile hali.
Ndivyo ilivyokuwa kwa mtume Paulo, alitamani kama ingekuwa inawezekana yeye kuharamishwa, (kufanywa kuwa mwana-haramu,atengwe na Kristo) kusudi kwamba ndugu zake wayahudi waiamini Injili waokolewe.. Lakini ilikuwa haiwezekani.
Ndugu kama hufahamu wakati ule wa kanisa la kwanza ni wayahudi wachache sana, waliiamini Injili, japokuwa ilikuwa ni mamilioni waliokuwa wanaisikia, na ndio maana ukisoma mbele kidogo mtume Paulo anasema.
Warumi 9.27 “..Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa”
Waliokolewa wachache sana, mpaka akasema, kama Mungu asingewaachia mabaki basi wangefananishwa na Sodoma na Gomora,(yaani akiwa na maana asingeokoka myahudi hata mmoja wakati wao)..
Na hiyo yote ilikuwa ni kwasababu waliikataa neema ya wokovu iliyoletwa na Yesu Kristo, alipokuwa duniani, na kuendelea na njia zao za kumtafuta Mungu, huku wamemweka Kristo pembeni. Ikapelekea mlango wa neema kufungwa juu yao. Na ndio maana utaona haijalishi walikuwa na bidii kiasi gani kwa Mungu lakini hawakuweza kuuona mlango wa neema hata kidogo kwasababu tu walimkataa Kristo (kasome Luka 13:34-35). Mtume Paulo alisema hivyo katika ile sura ya 10
Warumi 10:1 “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe. 2 Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa”.
Warumi 10:1 “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.
2 Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa”.
Hilo jambo linaendelea mpaka sasa, takribani miaka 2000 imepita, lakini bado mlango wa neema haujafunuliwa kwao. Na hiyo yote ni ili mimi na wewe (watu wa mataifa), tuipokee neema.
Lakini mwisho kabisa mtume Paulo alipewa siri na Mungu, na siri hiyo aliiweka wazi akataka sisi nasi tuijue (yaani mimi na wewe), kwamba utafika wakati ambao Mungu atawarehemu tena..Na kikisha fika hicho kipindi basi sisi tufahamu Habari yote ndio imeishia hapo, kama mtu yeyote wa mataifa atakuwa hajaingia ndani ya Kristo, ndio basi tena..Soma
Warumi 11:25 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili. 26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.
Warumi 11:25 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.
Jiulize wayahudi kwa miaka 2000 wanautafuta uso wa Mungu lakini hawaupati, unadhani siku hiyo neema ikiondolewa kwetu, sisi tutaipatia wapi? Na dalili zote zinaonyesha wakati wao upo karibuni sana…Tayari taifa hili lilishachipuka tangu mwaka 1948, unadhani ni nini kinachosubiriwa hawa watu Mungu asiwageukie? Usiku na mchana wapo pale kwenye “ukuta wa maombolezo wa Nehemia” wanamlilia Mungu awaokoe (hayo yalikuwa ni majonzi ya mtume Paulo)..Lakini Bwana anakawia kidogo kwa ajili yangu mimi na wewe.
Moja ya hizi siku, Mungu atakisikia kilio chao,.mlango wa neema utafunguliwa kwao, na kwetu utafungwa,. Huo ndio ule wakati wa mwenye nyumba kusimama na kuufunga mlango, na watu watakuwa wakisimama nje na kugonga wafunguliwe lakini Bwana atawaambia siwajui mtokako.(Luka 13:25-28)…Duniani kutakuwa na kilio na kusaga meno.
Hivyo tunaposikia maneno haya, tujitathimini Je! Ni kweli bado tupo ndani ya Kristo? Au tupo vuguvugu. Kama wewe unaisikia injili na bado unasua sua basi uingie sasa kwa nia yote acha kusitasita kwenye mawazo mawili muda unazidi kwenda, kwasababu siku hizi ni za mwisho. Lango hili likishafungwa, halitafunguliwa kamwe.
Maran Atha.
MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.
MADHARA YA KUTOA MIMBA.
TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?
MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.
Ulokole/ Walokole wametoka wapi?
JIBU: Kabla ya kwenda kujua maana ya ulokole, ni muhimu kujua kwanza maana ya neno ‘kanisa’..Tafsiri ya kwanza ya kanisa sio “jengo” bali ni “mkusanyiko wa watu waliomwamini Yesu”..Kwahiyo popote palipo na mkusanyiko wa watu waliomwamini Yesu, tayari hilo ni kanisa hata kama hakuna jengo. Soma mistari ifuatayo itakusaidia Matendo 2:47,1Wakorintho 1:2,14:5,14:23,15:9,16:19 n.k
Na kanisa la Kristo ni moja tu duniani kote ambalo linajulikana kama Bibi-arusi wa Kristo…Hilo ndio linajumuisha wakristo wote waliomwamini Yesu na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake (kumbuka hapa hatuzungumzii madhehebu), bali kanisa la Kristo moja ambalo pia sio jengo, bali watu wote duniani waliomwamini Yesu. Na watu hawa ambao ndio kanisa la Kristo, ndio watakaokuja kunyakuliwa siku ya parapanda katika tukio lijulikanalo kama UNYAKUO WA KANISA. Unaitwa unyakuo wa kanisa na si makanisa…kwasababu kanisa la Kristo ni moja tu.
Lakini sasa Kanisa la Kristo ni kweli ni moja lakini lina washirika wengi, na haliwezi lote kukusanyika pamoja na kwa wakati mmoja kufanya ibada, au kumwabudu Mungu, kama ni hivyo basi halina budi kuwepo na makusanyiko tofauti madogo madogo katika kila eneo ili kukamilisha kusudi lile lile la kukusanyika pamoja…Ndio hapo wakristo waliopo Mkoa wa kilimanjaro watakusanyika kivyao, na waliopo Morogoro watakusanyika kivyao huko waliko, n.k..
Lakini kumbuka Imani ni moja, na Kristo ni yule yule anayeabudiwa kote, utendaji kazi unaweza ukawa unatofautiana kulingana na kanisa na kanisa, lakini Imani ni sharti iwe ile ile moja, Bwana mmoja, Roho Mmoja, Ubatizo mmoja sawasawa na (Waefeso 4:3-7), tofauti na hapo hilo ni jambo lingine.
Sasa katika mkoa huo huo wa Morogoro pia sio wakristo wote wapo Morogoro mjini, kuna wengine wapo vijiji vya ndani huko…hao nao hawana budi wakusanyike huko walipo, hakuna sababu ya kusafiri mpaka mjini….na huko vijijini pia kuna uwezekano wa watu wasiwe karibu karibu…hivyo tena yatazaliwa makundi mengine madogo madogo mengi kulingana na mahali, hata inaweza kufikia kanisa likawa na watu watano..lakini yote yenye imani moja. Umbali ndio unaosababisha yajigawanye hivyo.
Sasa haya makanisa mengi madogo madogo ambayo yanakuwa katika eneo husika kwa kiingereza yanajulikana kama LOCAL CHURCHES, (Yaani kanisa la eneo husika aidha mtaa, au kijiji).
Na makanisa haya zamani, kutokana na uchache wa watu yaliyonayo na maeneo yalipo mengi yaliishia kudharaulika… na asilimia kubwa ya washirika wake ni maskini…kwasababu wengi wanaoishi vijijini au katika miji midogo midogo si matajiri kulinganishwa na wale wanaoishi mijini. Hivyo walidharaulika lakini kama biblia inavyosema kuwa..
Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao”
Hivyo hao waliodharaulika na kujulikana kama “Local churches”… ndio waliokuwa wa kiroho zaidi..Ishara nyingi na miujiza mingi ilifuatana na haya makanisa madogo madogo, kuliko hayo makubwa, …ndio watu waliokuwa na bidii zaidi ya kumtafuta Mungu, na ndio waliokuwa wanamheshimu zaidi Mungu.
Sasa kutokana na makanisa hayo madogo madogo kufahamika kama local churches…na washirika wao ndio wakajulikana kama “local people”..na kwa lugha yetu hii wakatafsiriwa kama (wa-locally) au WALOKOLE.
Hivyo kama mtu utaitwa mshamba kwa sababu unamwamini Yesu na kuzishika amri zake basi hiyo ni THAWABU. Kuliko kama utaitwa mwenye Elimu na wa-kisasa na huku umemwacha Kristo.
Ufunuo 3:17 “Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. 18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona”
Ufunuo 3:17 “Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona”
Usijisifie ukubwa wa kanisa unaloabudu, wala wingi wa watu wa kanisani kwenu…Jisifie Yesu uliye naye maishani mwako hata kama upo kanisa la watu watano..jitathmini je! unazishika amri zake hapo ulipo?, je! unaishi kulingana na neno lake? Kiasi kwamba hata parapanda ikilia utakwenda naye!..Je hapa nilipo nanufaika roho yangu kiasi gani?..kama sinufaiki rohoni ni heri nikatafute wenzangu wenye Imani ya kweli hata kama ni wachache, ninusuru roho yangu..kuliko kuendelea kwenye umati wa watu wengi na kuipoteza nafsi yangu…
Ni heri nijulikane mlokole lakini naenda mbinguni kuliko kukubalika na kila mtu, mwisho wa siku naishia kwenda jehanamu. Na kama pia hapo ulipo penye watu wachache huoni dalili ya kuurithi uzima wa milele ni heri ukaenda kutafuta penye watu wengi ambao wanakwenda mbinguni..Lakini siku zote kumbuka mlango ni mwembamba na njia ile imesonga na ni wachache wanayoiona…na mlango ni mpana wa njia iendayo upotevuni na wengi wanauendea.
Bwana akubariki na Bwana atusaidie.
Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?
MIHURI SABA
Wafilisti ni watu gani.
YEREMIA
MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.