Category Archive Home

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

Shalom karibu tujifunze Biblia, kwasababu Neno la Mungu ndio mwanga wa njia zetu na taa iongozayo miguu yetu.

Ni wapi mahali sahihi pa kulipa zaka je ni kanisani, au kwa mayatima au kwa wajane?..Hili ni swali linaloulizwa na wengi..Leo kwa neema za Bwana tutajifunza..

Andiko linalofahamika na wengi wetu lihusulo mahali sahihi pa kulipa zaka ni hili..

Kumbukumbu 26:12 “Utakapokwisha kutoa zaka, katika zaka zote za maongeo yako mwaka wa tatu, ambao ndio mwaka wa kutolea zaka, umpe zile zaka Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane, wapate kula ndani ya malango yako na kushiba;”  

Sasa kabla ya kuingia kwa undani kulielezea andiko hili..ni muhimu kwanza kufahamu mambo machache yafuatayo..

Kwa mtu aliyeokoka na kuitambua Neema ya Yesu kikweli kweli, Zaka ni jambo la lazima ingawa sio la sheria.(Mathayo 23:23)

Ipo michango mingine tofauti na Zaka..ambayo ni ya muhimu pia kwa kila aliyebadilishwa na kuwa mkristo kuitoa…na michango hiyo ni CHANGIZO, na SADAKA…Hii miwili ni tofauti na Zaka…Zaka ni sehemu ya Kumi ya Mapato…Changizo ni chochote ambacho mtu anaweza kumtolea Mungu kama mchango, (hakina sheria, wala kiwango maalumu)..na sadaka ni dhabihu mtu anayomtolea Mungu wake, inaweza kuwa sadaka ya shukrani, ya malimbuko, au ya ombi ya kutimiziwa hitaji fulani.(Warumi 15:26, 1Wakorintho 16:1 )

Jambo la tatu la kufahamu ni kwamba..Zaka/fungu la 10…Ndiyo sadaka inayopaswa ichukuliwe kuwa ya kiwango cha chini kuliko hizo nyingine zote… haipaswi kuchukuliwa kama ni adhabu wala kitu kikubwa kuliko vingine…(maana yake changizo na sadaka zinaweza kuzidi mara nyingi sana Zaidi ya zaka).

Sasa tukirudi kwenye swali letu..Je! zaka inapaswa itolewe wapi..JIBU NI RAHISI INAPASWA ITOLEWE KANISANI TU!!…Na si penginepo!..Michango mingine inaweza kwenda kwa masikini, kwa wasio jiweza ambayo hiyo inaweza ikawa hata ni nyingi sana kuliko zaka..Kwa mfano mtu aliyepata mapato ya laki moja, maana yake hapo zaka ni elfu 10..kilichosalia ana uhuru nacho kusaidia kiwango chochote kwa wasiojiweza na masikini wa mitaani, kama atawapa elfu 50 au Zaidi ya hapo ni mapenzi yake mwenyewe..na tena ni vizuri Zaidi…Kwasababu ndivyo atakavyojiwekea daraja zuri Zaidi la kubarikiwa kama maandiko yanavyosema heri kutoa kuliko kupokea, lakini ZAKA ni kanisani tu!.

Sasa swali linakuja..kwanini hapo juu kwenye Kumbukumbu la Torati, maandiko yanasema zaka iliwe na maskini, mjane, yatima na Mlawi?.

Jibu rahisi ni kwamba katika Agano la kale…Kanisa la Mungu lilikuwa ni jamii nzima ya wana wa Israeli…Wote waliovuka bahari ya shamu hilo ndilo lililokuwa kanisa la kwanza yaani uzao wa Ibrahimu…Hivyo Zaka zililihusu kanisa hilo lote kwa ujumla…ambapo ilikuwa inawekwa kwa utaratibu maalumu kwamba walio wajane kweli kweli ambao hawana watu wa kuwasaidia, Pamoja na walawi(yaani makuhani na uzao wao) ambao hawa hawakuwa na shughuli yoyote Zaidi ya kuhudumu katika nyumba ya Mungu…pamoja na mayatima wasio na ndugu wala wazazi na wageni walio wayahudi..Kwa utaratibu maalumu Zaka waligawanyiwa wao.

Hivyo kwa ujumla hilo ndilo lililokuwa kanisa la Mungu la kwanza…Utauliza ni wapi wana wa Israeli walijulikana kama ni kanisa…Soma, Matendo 7:37-38. Hivyo zaka ziliwahusu wana wa Israeli tu.. yaani maskini, walawi, wajane, na mayatima na wa Israeli tu..hazikuwahusu maskini waliokuwepo Babeli, wala wajane wa Ashuru.

Na katika Agano jipya…Zaka zinalihusu kanisa la Kristo peke yake…na si penginepo…Yaani maana yake ni kwamba (wajane,yatima, maskini, na walawi ambao kwasasa wanawakilisha wachungaji, waalimu,manabii, mitume na wote wanaohudumu madhahabuni, au wanaoifanya kazi ya Mungu kwa ujumla wake)..Hao ndio wanaopaswa kunufaika na zaka zitolewazo…na si wajane wa mitaani, au maskini tunaopishana nao barabarani…hao wanaweza kupewa michango ambayo mtu anaweza kutoa kama apendavyo..na pia inaweza ikazidi hata kiwango cha zaka..sio dhambi….lakini zaka ni kwa KANISA TU!. Maana yake kwa wajane ambao ni wakristo waliopo pale kanisani ambao ni wajane kweli kweli, wamedumu katika utakatifu na kuosha watakatifu miguu kama maandiko yanavyosema katika…1Timotheo 5:9-16,..Na mayatima ni hivyo hivyo…wale ambao ni wakristo au wazazi wao walikuwa ni wakristo walioshuhudiwa na kanisa.

Sasa swali linakuja..je nikipata zaka nimtafute Yatima fulani au mjane fulani pale kanisani nimpe, au nimtafute mchungaji pale kanisani au nabii nimpe kwa siri, nitakuwa tayari nimeshalipa Zaka??…Jibu ni hapana!..hupaswi kwenda kumpa mchungaji binafsi zaka yako, wala yatima binafsi, wala mjane..Kama unataka kufanya hivyo basi unaweza kufanya kama mchango tu kwao, yaani ukawatafuta wao binafsi kwa fedha yako ukawapa lakini zaka usifanye hivyo…

Tayari tumeshapewa utaratibu katika biblia wa namna ya kulipa zaka..

Tusome…

Matendo 4: 32 “ Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika. 

33  Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote. 

34  Wala hapakuwa na mtu mmoja miongoni mwao mwenye mahitaji; kwa sababu watu wote waliokuwa na viwanja au nyumba waliviuza, wakaileta thamani ya vitu vile vilivyouzwa, 

35  wakaiweka miguuni pa mitume; kila mtu akagawiwa kwa kadiri ya alivyohitaji”.

Umeona hapo?..wote walipeleka sadaka zao na zaka zao miguuni mwa mitume…Na ndipo Mitume wakawa wanawagawia kila mtu kama alivyohitaji (maana yake kila mkristo mwenye mahitaji, na sio maskini wa barabarani), Hivyo wenye mahitaji walikuwa wanachunguzwa kwanza wenye vigezo vya kimaandiko vya kupewa ndipo wanapewa sio tu kila mtu ambaye anashida anapewa tu hapana!..palikuwa na utaratibu…Na kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utakuja kuona kuwa hata bado huo mfumo ulikuwa ni ngumu kuusimamia mitume..mpaka wakaweka watu wengine 7 wenye hekima Zaidi, ambao wataweza kujua na kusimamia ni nani anastahili Zaidi na nani hastahili, na ni nani anapaswa apate Zaidi na nani asipate, Ndio wakapatikana wakina Stefano huko huko ambao ndio walikuwa mashemasi…Sasa Mashemasi kazi yao ndio hiyo kusimamia bajeti ya kanisa na kuigawanya kwa watu kulingana na katiba ya kimaandiko.

Kwahiyo kwa hitimisho katika Agano la kale na agano jipya…hakuna mahali popote zaka walipelekewa watu wa nje ya kanisa…na kulikuwa na utaratibu maalumu. Hivyo kama kuna mtu umemwona ana uhitaji labda umekutana naye barabarani, au mtaani au popote pale nje ya kanisa mpe kwa kadiri uwezavyo lakini si zaka..zaka yako peleka katika kanisa lako unaloshiriki(hiyo inawahusu watakatifu)…Huko kama ni kanisa la kweli la Kristo wanaujua utaratibu wa kimaandiko wa namna ya kuigawanya.

Bwana akubariki..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UFANYE NINI KAMA MKRISTO WAKATI HUU WA JANGA LA CORONA?

UFUNUO:Mlango wa 6-( Maelezo ya Muhuri saba)

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Kutubu sio kuomba rehema kwa Mungu!.


Jina la Bwana libarikiwe.

Ipo tofauti kati ya kutubu na kuomba rehema…Wengi tunaomba rehema lakini hatutubu…Ndugu, Rehema bila Toba ni bure!.

Kuomba rehema hakuna tofauti na kuomba msamaha…Unapomwomba Mtu msamaha hapo ni umemwomba rehema…(akurehemu), Lakini Toba haiombwi, toba ni inafanywa na wewe.

Sasa Toba/kutubu ni nini?

Toba maana yake ni KUGEUKA NA KUCHA KILE ULICHOKUWA UNAKIFANYA. Ulikuwa unakwenda mbele ghafla ukaghairi ile njia uliyokuwa unaiendea na kugeuka nyuma na kurudi ulikotoka au kuiendea njia nyingine kutokana labda na sababu fulani ambazo unazijua wewe….sasa hicho kitendo cha kugeuka na kughairi ndicho kinachoitwa Toba. Lakini kuomba msamaha sio kutubu.

Ili kuelewa tofauti Zaidi tofauti ya vitu hivi viwili..tafakari mfano ufuatao.

Mzazi kamwita mwanawe ili amtume mahali, lakini yule mtoto akamfanyie jeuri mzazi wake yule na kumtusi na akaenda kuendelea na michezo…Wakati yupo njiani anaelekea kwenye michezo njiani, dhamiri ikamchoma akagundua amefanya kosa…Hivyo akaghairi safari yake ya kwenda kwenye michezo, akarudi kwa mzazi wake..akampigia magoti akamwambia nisamehe Mama kwa jeuri yangu nimekosa, nipo tayari kwenda kule ulikonituma.

Sasa mtoto huyo pale alipokuwa njiani na kughairi njia yake na kugeuka na kurudi kwa Mama, Hapo ndipo alipotubu…Na hatua ya pili kwenda kumwomba mama yake msamaha kwa jeuri yake ile pale ndipo alipoomba Rehema. Hivyo umeona tofauti ya mambo hayo mawili?…Hauwezi ukasema umeomba rehema na huku hujatubu…Toba inaanza ndipo ndipo kuomba rehema kunafuata.

Ndio mfano ambao Bwana Yesu aliutoa juu ya wale wana wawili..Tusome

Mathayo 21:28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.

29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.

30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.

31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili…”

Wakati huu wa matatizo haya yaliyoikumba dunia..sio wakati wa kuomba rehema…ni wakati wa kutubu, maana yake ni wakati wa kuacha dhambi…kughairi mabaya tunayoyafanya…kughairi rushwa tulizokuwa tunakula na tunazoendelea kuzila sasa, ni wakati wa kuacha uasherati kabla ya kumkaribia Mungu wetu kumwomba rehema…ni wakati wa kutupa na kuchoma vimini…niwakati wa kutupa mahereni, mabangili, na kuondoa make-up na kutuacha kuwa asili kama Mungu alivyotuumba, na baada ya hapo ndipo tunamwambia Baba tumeacha sanamu zote hizi tunaomba uturehemu..Ni wakati wa kuwarudishia watu vitu tulivyowarusha au kuwatapeli, ni wakati wa kuwasamehe waliotukosea, ni wakati wa kupatana na ndugu zetu ambao tulikuwa tumewachukia mpaka tukawawekea  vinyongo, Ni wakati wa kuacha kutukana kabisa, ni wakati wa kuacha kuwaseng’enya jirani zetu na kuwatakia shari, Ni wakati wa kuacha ULEVI, na kwenda Disko, ni wakati wa kuacha starehe za kidunia na kumgeukia Mungu..

Tukiyafanya hayo, mbele za Mungu wetu ndio tutakuwa tumetubu..kwasababu tutakuwa tumegeuka na kuziacha njia zetu mbaya..na hivyo akiona Toba yetu hiyo ndipo hata pasipo kutumia nguvu nyingi kuomba rehema..yeye mwenyewe ataturehemu kwasababu ni mwingi wa rehema…Lakini tukienda na lipstick zetu midomoni, mbele zake kumwomba rehema, tukienda na zinaa zetu mbele yake kumwomba aturehemu, tukienda na nguo zetu za nusu uchi mbele zake na kumwomba msamaha…Ni sawa na kijana anayekwenda huku amelewa pombe na huku ana sigara mdomoni mbele za Baba yake na kumwambia Baba naomba unisamehe kwa ulevi wangu. Hapo atakuwa anamdhihaki mzazi wake. Na ndivyo tunavyoonekana mbele za Mungu wetu tunapokwenda kumwomba rehema huku bado hatujadhamiria kuacha dhambi zetu tunazozifanya kwa siri au kwa wazi.

Wakati huu tunayo nafasi ya kuomba rehema kwaajili ya nchi Pamoja na nafsi zetu na ndugu zetu…Ni wakati wa kutanguliza TOBA kwanza kabla ya REHEMA. Na hilo linatosha kabisa kupata rehema bila hata ya sisi kutumia nguvu nyingi…Kama Habari ile ya mwanampotevu..alipoghairi Maisha yake yale na kugeuka kuamua kurudi kwa Baba..hata alipokuwa mbali Baba yake alimwona na kumpokea..hakutumia nguvu nyingi sana Kupata rehema kutoka kwa Baba yake.

Bwana akubariki, kama hujampa Yesu Kristo Maisha yako..unangoja nini?..Wewe ni shahidi wa nyakati hizi tunazoishi na majira haya..bado makubwa zaidi ya haya unayoyaona yanakuja huko mbeleni kwa wote ambao wapo nje ya Kristo. Hivyo tubu leo na Bwana atakurehemu na kukupa Roho wake Mtakatifu kwasababu anatupenda sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

MTINI, WENYE MAJANI.

JE MOYO WAKO NI MNYOFU MBELE ZA MUNGU

JE UNAMTHAMINI BWANA?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini kabila la Dani limeondolewa kwenye Ufunuo 7?

SWALI: Hujambo ndugu.Nina ulizo kuhusu kabila 12 ya Yakobo (Israeli) katika mwanzo 49 tunaona kabila la DANI lipo, lakini katika ufunuo 7 kabila la Dani halipo badala yake lipo manase. Kwanini?


JIBU: Katika kitabu cha Ufunuo sura ya 7, kabila la Dani halionekani miongoni wa watu wale watakaoitiwa muhuri siku ya mwisho ili kuiamini Injili itakayokuja kuhubiriwa pale Israeli..Sasa Mungu hakulisahau kabila hilo, hapana bali aliliondoa kwa makusudi kabisa pale na kuliweka hilo la manasae.

Lakini ni kwanini Mungu afanye vile?.. Tukijua jambo hilo jinsi laana za Mungu zilizo kali basi na sisi hatutauchezea wokovu wetu tuliopewa sasa na Mungu wetu.. Kwasababu neema ikishaondoka imeondoka kweli kweli.

Sasa tukisoma kwenye biblia Mungu alishatoa angalizo hili tangu zamani…

Kutoka 20:2 “Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.

3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.

4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”

Unaona Mungu alisema kabisa katika amri zake, kuwa yeye ni Mungu mwenye wivu, na pia anapatiliza maovu yao hata kizazi cha tatu na cha nne..ikiwa na maana kuwa ukifanya dhambi ya makusudi baada ya kuujua ukweli mapatilizo yake yanaweza kuendelea hata kwa vizazi vya wanao huko mbele.

Na tena alisema katika kitabu cha Mambo ya walawi..

Walawi 18:27 “(kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;)

28 ili kwamba hiyo nchi isiwatapike na ninyi pia, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu.

29 Kwani mtu awaye yote atakayefanya machukizo hayo mojawapo, NAFSI HIZO ZITAKAZOYAFANYA ZITAKATILIWA MBALI NA WATU WAO”.

Sasa kabila la DANI lilikuwa ni kabila mojawapo la makabila ya Israeli, na kwamba kabila hili lingetakiwa lionyeshe kielelezo kwa watu wa Mataifa kuwa Mungu wa Israeli ndio Mungu na ndiye pekee anayepaswa kuabudiwa,..Lakini lilifika wakati hilo kabila lenyewe likaamua kumuacha Mungu na kwenda kusimamisha SANAMU katika mji wake, na kuiabudu na kuitolea kafara..Ni kabila pekee katika biblia nzima liliokuwa na ujasiri wa kufanya jambo kama hilo..Habari yote hiyo unaweza kuisoma mwenyewe katika kitabu cha Waamuzi sura ya 17 na 18

Sasa jambo hilo lilimfanya Mungu, alifute katika mpango wake wa wokovu..(sawasawa na Neno lake alilolisema) na ndio maana hapo tunaona katika kitabu cha ufunuo ambacho kinazungumzia habari za siku za mwisho, wakati ambapo wana wa Israeli watarejeshewa tena neema hii ya wokovu tuliyonayo sisi, kabila hilo la Dani halitakuwepo katika hesabu hiyo.

Hiyo inatukumbusha na sisi, tusipoizingatia neema hii ya wokovu, tukawa tunaifanyia mzaha, tunajiweka hatarini kwa Mungu kutuacha na kwenda kwa wengine.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Kwanini kabila la Dani na Efraimu hayaonekani yakiorodheshwa miongoni mwa yale makabila 12 ya Israeli katika Ufunuo 7?

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

KITABU CHA UZIMA

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

MIHURI SABA

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mahuru ndio nini?

SWALI: Mahuru ndio nini? Kama Bwana alivyosema katika Mathayo 17:26, Na ni jambo gani tunajifunza pale?


JIBU: Tusome;

Mathayo 17:25 “Naye alipoingia nyumbani, Yesu alitangulia kumwuliza, akisema, Waonaje, Simoni? Wafalme wa dunia hutwaa kodi ama ushuru kwa watu gani? Kwa wana wao au kwa wageni?

26 Naye aliposema, Kwa wageni, Yesu alimwambia, Basi, kama ni hivyo, WANA NI MAHURU.

27 Lakini tusije tukawakwaza, enenda baharini ukatupe ndoana, ukatwae samaki yule azukaye kwanza; na ukifumbua mdomo wake utaona shekeli ichukue hiyo ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako”.

Ukisoma mstari huo..Bwana alikuwa anazungumzia juu ya wale wanaostahili kulipishwa kodi kulingana na tamaduni za wakati huo…Kwamba kwa wakati huo watu wanaotoka mji mmoja kuingia mwingine ambao si wa kwao walikuwa wanatozwa ushuru…lakini wale wenyeji walipokuwa wanarudi kuingia kwao hawatozwi ushuru kwasababu wao ni wenyeji au wana wa huo mji…

Hivyo hapa Bwana alikuwa ametoka na wanafunzi wake kutoka mji mmoja kwenda mwingine ndani ya Mkoa wake mwenyewe ulioitwa Galilaya…lakini wakataka kumtoza nusu shekeli na ilihali yeye ni mwenyeji wa Mkoa ule na wala si mgeni (Galilaya ilikuwa inajumuisha majimbo ya Nazareti, Korazini, Kapernaumu, Tiberia, Naini, Magdala na mengine machache madogo madogo), na Galilaya yote ilikuwa chini ya Mfalme Herode wa kirumi. Hivyo yoyote aliyekuwa mzawa wa majimbo hayo alikuwa huru kwenda popote katikati ya hayo majimbo pasipo kutozwa ushuru wowote…

Ni sawa na sisi tulivyo na uhuru wa kusafiri mkoa wowote bila vizuizi.

Lakini hawa walipomwona Yesu waliingiwa na tamaa ingawa walijua kabisa ni mzawa, lakini waliingiwa na tamaa labda pengine walimwona anafuatwa na watu wengi wakadhani atakuwa na pesa nyingi hivyo wakawa wanatafuta sababu za kupata fedha kutoka kwake..

Sasa Bwana ndio anamwuliza Petro je wanaotozwa ushuru ni wageni au WANA ?(neno wana ni sawa na wenyeji)…Ndio Petro anamjibu kwamba ni Wageni ndio wanaopaswa kutozwa ushuru na si wenyeji…Ndipo Bwana akamwambia basi kama ni hivyo Wana au kwa lugha nyingine wenyeji ni MAHURU..yaani maana yake wazawa WAPO HURU…Hawapaswi kutozwa chochote kulingana na sheria ya nchi.

Lakini kwasababu Bwana ana hekima nyingi na siku zote anampendeza Mungu na wanadamu hakutaka kuwakwaza kwa vyovyote vile..ndio akamwambia Petro akavue na samaki atakayezuka wa kwanza mdomoni atakuta fedha aje kuilipa kwaajili yake na ya Petro.

Tunajifunza hapo na sisi…sio kila vita vya kupambana nayo…vingine mwachie Bwana akupiganie..Hebu jiulize hapa Petro angeanza kugoma..oo hapana hiyo sio haki, mnatuonea, mnatunyanyasa..sisi ni wenyeji n.k Bila shaka asingeuona ule muujiza Bwana alioufanya…Na kama ukichunguza pale hawakuwa hata na senti..ndio maana Bwana akamwambia Petro akavue…Sasa kwa utulivu wa Petro faida aliyoipata ya kuwa mtulivu na kumtii Bwana na kumwamini alipoenda kuvua ili aje kulipa ushuru ambao si halali yake kuulipa.. alipata faida mara mbili..

Faida ya kwanza aliyoipata ni kwenda kulilipa lile deni alilokuwa anadaiwa ambalo halikuwa halili kwake kulilipa…na faida ya pili na ya muhimu ni Yule samaki…pengine alikwenda kumuuza au kumtumia kwa kitoweo baada ya kumtoa ile sarafu mdomoni…

Vivyo hivyo wakati mwingine tunaweza kusingiziwa kesi au madeni ambayo si halali kwetu kuyalipa…usining’unike katika hali kama hiyo..umejaribu kuonyesha kwamba sio halali lakini hueleweki usianze kunung’unika na kulalamika mpaka kuonekana sasa huna imani na maana..mpaka watu wakaanza kushangaa kama kweli wewe ni mkristo au la!..kwa matusi hayo na manung’uniko hayo..

Wewe unachopaswa kukifanya nenda katafute namna ya kulipa deni lile au kuikabili kesi ile, hata kulipa kile chote wanachokushitaki..na huko huko njiani Mungu atakufanyia muujiza wa kuilipa ile na utapata cha ziada.

Hizo zilikuwa ni kanuni za Bwana wakati wote, nasi tupate kitu kidogo cha kujifunza hapo..

Luka 6: 29 “Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang’anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.

30 Mpe kila akuombaye, na akunyang’anyaye vitu vyako, usitake akurudishie”.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

MOJA YA HIZI SIKU TUTAONA MABADILIKO MAKUBWA SANA.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUMBUKA, VIVUKO VYA YORDANI VINAKUNGOJA MBELENI.

Ni jambo la kawaida, kuona tabia za watu zinabadilika hususani pale wanapoona wanakaribia kwenda kuangamizwa wote,..Utaona wengi wao wanajigeuza na kujifanya kama vile wao ni kama wale wengine, ili wafanikiwe kijipenyeza kisirisiri katikati yao wasalimishe roho zao..

Hiyo ilitokea wakati wa kipindi cha Esta, pale ambapo maadui wa Wayahudi walipokusudia kuwaua wayahudi wote kwa kibali cha mfalme Ahasuero, lakini kibao kilipowageukia na kuona mfalme ndio amewapa heshima mara dufu,na ziadi ya yote amewapa mamlaka ya kuwatafuta wale maadui zao wawaue, biblia inatuambia jamii kubwa ya watu wakajigeuza na wenyewe kujifanya ni wayahudi ..

Esta 8:16 “Ikawa nuru na furaha na shangwe na heshima kwa Wayahudi.

17 Na katika kila jimbo, na kila mji, po pote palipowasili amri ya mfalme na mbiu yake, Wayahudi wakapata furaha na shangwe, karamu na sikukuu. Hata wengi wa watu wa nchi wakajifanya Wayahudi, kwa kuwa hofu ya Wayahudi imewaangukia”.

Unaona hapo?..

Tunasoma tena habari nyingine, kuna wakati jamii mbili za wana wa Israeli zilipigana, ambazo ni Ni jamii ya watu wa Efraimu, na watu wa Gileadi… Sababu ya vita yenyewe ilikuwa ni wale watu wa Gileadi walikwenda kupigana na maadui zao, bila kuwashirikisha watu wa Efraimu kwenda kuwasaidia, hivyo watu wa Efraimu wakakasirika kuona uamuzi ule waliouchukua ndugu zao hivyo wakapanga vita wawapige na Wagileadi, Lakini mambo yalikuwa ni tofuati, kinyume chake wao ndio waliopigwa..

Sasa baada ya kuona wanazidiwa na hali ndio inakuwa mbaya, ikawabidi, watoroke watu wengi, wajaribu kuvuka kujichanganya na jamii ya wagileadi. Sasa ilikuwa ili kufika ng’ambo ni sharti uvuke mto wa Yordani..Lakini wao walidhani ni rahisi rahisi tu kama siku zote, unavuka tu na kuingia bila kuulizwa chochote..wengine wakadhani hata wakiulizwa wewe ni nani, je ni mwenyeji wa huku watasema tu ndio, halafu basi wataruhusiwa kuvuka..

Hawakujua kuwa wale wagileadi walipata taarifa juu ya njama zao, Hivyo walichokifanya ni kwenda kusimama pale kwenye vivuko vya Yordani, pale mpakani, na watu wote, waliochanganyikana nao walipofika wavuke wasijue kuwa huyu ni nani na huyu ni nani, walitumia njama moja ya kuwakamata waefraimu katikati ya wagileadi, waliwaambia watamke Neno “shibolethi” tusome..

Waamuzi 12:5 “Nao Wagileadi wakavishika vivuko vya Yordani kinyume cha hao Waefraimu; kisha ilikuwa, hapo watoro waliotoroka Efraimu mmojawapo aliposema Niache nivuke, hao watu wa Gileadi wakamwambia, Je! Wewe u Mwefraimu? Kwamba alisema, La;

6 ndipo wakamwambia, Haya, tamka sasa neno hili, Shibolethi; naye akasema, Sibolethi; kwa maana hakuweza kufanya midomo yake kutamka neno hilo sawasawa; ndipo wakamshika, na kumwua hapo penye vivuko vya Yordani; basi wakaanguka wakati huo watu arobaini na mbili elfu wa Efraimu”.

Unaona, walitumia kigezo cha Lugha, kuwashika, vinginevyo wasingewatambua kwa namna yoyote, kwasababu walijua lugha ya asili ni kitu kinachoshikamana na mtu kuliko kitu kingine chochote, walijua lugha ya asili inaweza kweli kuigwa lakini haiwezi kuigwa kwa ufasaha wake wote, haijalishi mgeni atajifunza kwa miaka mingapi, ile lugha ambayo hajazaliwa nayo hawezi kuiiga kwa ufasaha wote..Hata leo hii mzungu aishi uswahilini hata miaka 50 na akakijua Kiswahili chote, bado kuna vimelea vya lugha hatoweza kuvitamka ipasavyo kama Yule mzawa..

Sasa Biblia inatuambia agano la kale ni kivule cha mambo yatakayotokea katika kipindi cha agano jipya..Na habari hizo hazijaandikwa ili kutusisimua tu, hapana bali zina ujumbe mkubwa sana kwetu katika roho.

Inamaana kuwa utafika wakati mambo ya wokovu hayatakuwa kama yalivyo leo hii, kuna wakati wale waovu watatamani sana kwa nguvu kujiingiza katika ufalme, watajigueza kwa kila namna ili tu wapate nafasi, lakini safari hii, haitakuwa ni kwa njia rahisi kwa wanavyodhani, bali watakuwa na mtihani mkubwa wa kufanya..

Luka 16:16 “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.

Utapimwa wokovu wako, sio kwa kusema tu mimi nimeokoka, mimi nilibatizwa, mimi ninakwenda kanisani bali vitazingatiwa vigezo vya ndani zaidi, utaulizwa je! Huo wokovu unauzoefu nao kiasi gani, Je, ni wa kujifunza tu, au ulikuwa ni sehemu ya maisha yako tangu zamani..

Hili ndio lile kundi ambalo Bwana alilitolea mfano wake, wa mtu Yule aliyekutwa ndani ya harusi lakini hana vazi la harusi mpaka watu wakawa wanashangaa ameingiaje ingiaje mule ndani na wakati hana vazi la harusi..Kumbuka wakati huu kule nje kulikuwa kunaendelea machinjo.. Akatoroka akaingia ndani, lakini alionekana kwasababu hakuwa na vazi (hakuwa na kadi ya mwaliko tangu zamani) Kilichofuata ni kwamba alikamatwa na kufungwa na kwenda kutupwa nje..

Ndipo Bwana akamalizia kwa kusema maneno haya.. “Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache”. Soma (Mathayo 22:1-14)

Hivyo ndugu anza kuujenga uhusiano wako na Mungu kuanzia sasa, usisubiri wakati Fulani, kubali kuzaliwa mara ya pili leo uikulie wokovu ujifunze lugha ya kimbinguni, kama bado hujaokoka.. kwasababu unafika wakati hapo mbele hakutakuwa tena na mlango wa neema ya yule atakayetaka kuingia.. kwa maana hizi ni nyakati za mwisho jambo ambalo hakuna mtu asiyelijua hilo.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

 

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UFANYE NINI KAMA MKRISTO WAKATI HUU WA JANGA LA CORONA?

Watu baadhi kutoka nchi mbalimbali wamenitumia ujumbe wanasema, mtumishi huku kwetu hali sio nzuri hatuwezi kwenda kanisani kama tulivyozoea, hatuwezi kufanya chochote isipokuwa tu ni kukaa nyumbani, na wala hakuna dalali ya jambo hilo kuisha hivi karibuni…Tufanye nini?

Shalom, ndugu,

Ipo Habari moja katika biblia tunapaswa tujue na  tujifunze kama wakristo katika wakati huu ambao dunia ipo katika taharuki kubwa, Tukisoma kitabu cha matendo ya Mitume, kuna wakati ambapo mitume wa Bwana walipitia kipindi fulani cha ukimya mkubwa sana, jambo ambalo liliwapasa wasifanye kitu kingine Zaidi ya kwenda kujifungia gorofani. Kwanini walilazimika kuwa vile, ni kwasababu ni kipindi ambacho, Sio  YESU tu peke yake ambaye walizoea kumwona na kutembea naye kila siku hakuwa nao, bali pia Roho Mtakatifu ambaye walisikia habari zake alikuwa bado hajashuka juu yao.. walikuwa katikati ya pengo, kama vile mayatima fulani..

Kitu pekee kilichowafanya wawezi kukivuka hicho kipindi kifupi cha ukimya, ilikuwa ni ile AHADI TU, waliopewa na Bwana Yesu siku ile aliyokuwa anapaa..

Hiyo ndio iliyokuwa salama yao kwa wakati huo waliokuwa wanapitia..Kumbuka hawakujua ahadi hiyo itatimia lini, lakini maaadamu wana Neno la Ahadi, basi hiyo iliwafanya wapate nguvu siku baada ya siku, wavumilie hicho kipindi cha mpito mbele yao wakitumai kuwa siku si nyingi itatimia, na AHADI yenyewe ilikuwa ni kungojea YERUSALEMU, mpaka wakatakapopokea kipawa cha Roho Mtakatifu..Basi.

Matendo 1:3 “wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.

4  Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu;

5  ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache”.

Hivyo baada ya ile siku ya 40, hawakumwona, wala hawakusikia chochote, wala hawakuoona uwepo wowote, wala hawakuwa na shughuli nyingine yoyote ya kuhubiri, au kushuhudia kama pale mwanzo, au kuzunguka huku na huko kuhubiri..Bali iliwagharimu kwenda kukaa tu sehemu moja..na zaidi ya yote biblia inasema nje kulikuwa na hofu ya wayahudi.

Lakini biblia inatuonyesha ahadi hiyo haikuchelewa, bali ndani ya siku 10 mbeleni ilitimia, ambayo ndio iliyokuwa siku ya Pentekoste, Roho Mtakatifu aliwashukia mitume wake kwa nguvu ya ajabu, na hapo ndipo Mungu akaleta uamsho mwingine tena ambao uliitikisa dunia nzima katika historia..

Sasa swali ni Je ndani ya kipindi kile cha mpito ambacho hakukuwa na sapoti yoyote ya kimbinguni mitume walikuwa wanafanya nini ndani, Je! walikuwa wamelala tu au wameacha wakovu wao sasa wafikirie mambo yao ya kale, au walikuwa wamekaa wanapiga tu story na kuzungumzia Maisha ya wengine, au wanaangalia movie, au wanachat whatasapp kila wakati au wanacheza magemu, au wanafanya nini??

Embu Tusome..

Matendo 1:10  “Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,

11  wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.

12  Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.

13  Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.

14  Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja KATIKA KUSALI, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake”.

Unaona, biblia inasema hapo walikuwa WAKIDUMU KWA MOYO MMOJA KATIKA KUSALI,..

Ndugu, wakati huu wa LOCKDOWN, na kuwa karantini kutokana na janga la Corona, nchi yoyote uliyopo. Wakati huu Wa kuzuiwa kufanya ibada, au kuzunguka huku na huko, wa kuzuiwa kwenda mtaani kuhubiri kama ulivyokuwa unafanya  hapo mwanzoni, wa kuzuiwa kuitishi mikutano ya injili, wa kuzuiwa kwenda kumwabudu Mungu kanisani, kwenda kwenye masomo ya biblia, kila baada ya siku mbili, sio wakati wako wa wewe kuwa na kisingizio cha kuacha kumtafuta Mungu, na kurudi nyuma kwenye ulimwengu ulipokuwepo, wa kurudi kuanza sasa kutokusoma biblia yako,..bali huu ndio unapaswa uufanye muda wakati wako wa kudumu katika KUSALI kwa bidii ukiingalia ahadi ya Mungu iliyo mbele yako, kwamba hivi karibuni atakwenda tena kutuachilia, lakini hatatuachilia hivi hivi, bali atatuachilia na UAMSHO MKUBWA WA ROHO ambao haujawahi kutokea..kama ilivyokuwa katika kipindi cha Pentekoste.

Hivyo huu sio wakati wa kuzimia mioyo,  wala sio wakati wa kuogopa maadamu tupo ndani ya Kristo, badala yake ndio tuongeze kutazama juu, tukiziangalia Ahadi za Bwana ndani ya kipindi hichi cha mpito, tukiongeza viwango vyetu vya kujisomea biblia nyumbani, na kusali sana tena Zaidi ya pale tulipokuwa mwanzoni, ikiwezekana kufunga, na kila wakati kumtafakari Mungu kweli kweli..

Sisi hatujapitia kipindi cha kuachwa na mbinguni kwa Muda kwa ilivyokuwa kwa mitume, lakini wao hawakuiacha Imani, badala yake walidumu katika kusali tena walipanda OROFANI, juu kabisa mahali ambapo hapana  usumbufu wa watu kuingia na kutoka, ili wamtuafakari Mungu vizuri na kusali..

Vivyo hivyo huu ni wakati wa wewe, kupanda OROFANI (mahali penye utulivu), Umtafute Mungu peke yako, kwasababu UAMSHO MKUU SANA, Unakwenda kuzuka duniani kote hivi karibuni. Kipindi cha nyuma pengine ulikuwa na visingizio vya kutokusali, kwamba upo bize kutafuta riziki na shughuli leo hii mazingira yanakulazimisha kukaa nyumbani, na tena kuna agizo limetolewa la kuomba, hivyo isiwe sababu ya wewe kuhukumiwa siku ile kwa kutokuomba sasahivi…Unayo sababu inayoeleweka kidunia ya wewe kutozurura zurura mtaani, basi kaa nyumbani kuomba…utajitetea vipi siku ile??..Utasema ulikosa muda? Utasema serikali ilikuzuia kuomba? Leo hii imekutangazia wewe kuomba?.. Utasema sikuomba kwasababu mazingira yalikuwa hayaruhusu?..jibu unalo.

Hivyo nakutia moyo wewe mkristo ambaye umeathiriwa na hali hii ya sasa duniani, Fahamu kuwa ni kipindi kifupi tu cha Siku 10 rohoni kinapita ambacho ni Mungu mwenyewe kakiruhusu..hivyo kuwa na akili, kujua nyakati na majira, ongeza viwango vyako vya utakatifu kama vile hukuwahi kuishi hivyo hapo kabla, ni wakati wa kutubu (kutubu maana yake ni kuacha yale uliyokuwa unayafanya yasiyo mpendeza Mungu) ili hiyo  PENTEKOSTE itakapokuja kwa watu wa Mungu duniani, uwe na wewe ni mmojawapo..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia na kujikumbusha mambo yale yale ambayo tumekwisha kujifunza huko nyuma kupitia sehemu mbalimbali..

Wengi wanajiuliza je ubatizo ni wa muhimu?..Jibu ni NDIO ni wa muhimu sana na si kidogo. Shetani hapendi wengi wajue siri iliyopo katika ubatizo sahihi kwasababu anajua madhara yake.

Wakati wana wa Israeli wanatoka Misri, Farao bado alikuwa anawafuatilia fuatilia..lakini walipovuka tu bahari ya shamu na majeshi ya Farao yote kuzama kwenye ile bahari ya shamu ndio ikawa mwisho wa Farao na majeshi yake kuwafuatilia wana wa Israeli.

Kutoka 14:26 “Bwana akamwambia Musa, Nyosha mkono wako juu ya bahari, ili maji yarudi tena juu ya Wamisri, juu ya magari yao, na juu ya farasi zao.

27 Musa akaunyosha mkono wake juu ya bahari, na kulipopambazuka, bahari ikarudi kwa nguvu zake; Wamisri wakakimbia mbele yake; na Bwana akawakukutia mbali hao Wamisri kati ya bahari.

28 Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja.

29 Lakini wana wa Israeli wakaenda katika nchi kavu katikati ya bahari; na hayo maji yalikuwa ni kuta upande wao wa kuume, na upande wao wa kushoto.

30 Ndivyo Bwana alivyowaokoa Israeli siku ile mikononi mwa Wamisri; Waisraeli wakawaona Wamisri ufuoni kwa bahari, wamekufa”.

Sasa siri ilikuwa ni nini mpaka Mwisho wa Farao ukawa kwenye hiyo bahari ya Shamu?..Jibu ni rahisi: Ni huo ubatizo wana wa Israeli waliobatizwa kwa kupita katikati ya bahari hiyo.

Utauliza je!..ina maana wana wa Israeli walibatizwa katika bahari ya Shamu?..Jibu ni ndio!..

1Wakorintho 10:1 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;

2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;”

Unaona hapo?..kitendo cha Wana wa Israeli kupitishwa katika yale maji ya Shamu, pasipo kupatikana na madhara ndiko kunakofananishwa na ubatizo. Hivyo ule ubatizo ndio uliohitimisha kazi ya shetani na majeshi yake kuwafuatilia, haijalishi kuwa tayari walishapewa ruhusu huko nyuma ya kuondoka.

Hali kadhalika, ubatizo sahihi wa maji mengi sasa unafanya kazi hiyo hiyo. Unapoingia katika yale maji na kubatizwa katika jina la Yesu na kutoka katika yale maji…wewe utatoka salama ukiwa na furaha, na amani lakini nyuma yako yale majeshi ya mapepo wabaya yaliyokuwa yanakufuatia yanakufa na maji huko nyuma.

Hivyo maji ni ishara ya wokovu kwako na maangamizi kwa shetani na majeshi yake. Ndio maana Bwana Yesu alisema katika Roho kwamba pepo amtokapo mtu hupitia mahali pasipo maji(maana yake mahali ambapo hapana maji) ili apumzike na akirudi na kukuta nyumba yake imefagiliwa anakwenda kuwachukua pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye, na hali ya mwisho ya Yule mtu inakuwa mbaya kuliko ya kwanza.

Maana yake ni kwamba pepo likimtoka mtu na Yule mtu kama hatachukua uamuzi wa kuukamilisha wokovu wake ikiwemo kubatizwa ubatizo sahihi wa kuzama mwili mzima kulingana na maandiko na kudumu katika usafi..Mtu huyo yupo hatarini kurudiwa na zile zile nguvu za giza zilizomwacha hapo kwanza. Hivyo ubatizo sahihi ni wa muhimu sana…Na ubatizo sio dini mpya bali ni maagizo ya  Bwana wetu Yesu…na kwa faida yetu kama ilivyokuwa kwa faida kwa wana wa Israeli wakati wanatoka Misri, kama sio yale maji Farao angeendelea kuwafuatilia daima.

Shetani na mapepo yake yataendelea kumfuata Yule mtu ambaye hajakamilisha wokovu wake…Na Bwana alishatuambia katika Neno lake, kwamba “aaminiye na kubatizwa ataokoka”..maana yake mambo hayo mawili yanakwenda pamoja, hayaachani, vinginevyo ni ngumu sana kuokoka na mkono wa Adui.

Kama unakumbuka kile kisa cha Yule mtu aliyekuwa na mapepo yaliyojitambulisha kama JESHI. Mtu Yule aliingiwa na mapepo, na mapepo yale yalipomtoka yaliwaingia nguruwe…Jinsi wale Nguruwe walivyokwenda kuangamia majini ni mfano wa Farao na majeshi yake yalivyozama majini…Kwahiyo unaweza kuona kuna uhusiano mkubwa sana wa maji na majeshi ya Adui. Hivyo ubatizo ni wa muhimu sana. Pale tu mtu anapoamini na kutubu anapaswa akabatizwe bila kuchelewa…

Itakuwa ni jambo la kushangaza, mtu utasema umeokoka, halafu miezi inapita, miaka inapita, bado hujabatizwa, unaishi kwa kanuni ipi ya wokovu?

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM

Rudi Nyumbani:

Print this post

MALAIKA WAPELELEZI WA HUKUMU WANAPITA SASA.

Kabla Mungu hajaleta maangamizi katika dunia, huwa anawatuma kwanza malaika zake wapelelezi kwenda kuhakiki hicho kilichomfikia kuwa ni kweli au La, na ikithibitika kuwa ni kweli basi hatua inayofuata saa hiyo hiyo  ni wale malaika kutekeleza hukumu ya Mungu juu ya watu hao au Mji huo. Kwananini anawaagiza malaika hawa kwanza kupeleleza, je ni kwasababu yeye mwenyewe hajui kiwango cha maasi na haki yaliyomo ulimwenguni?..jibu ni hapana!..anajua kila kitu pasipo hata kutegemea malaika zake, wala mwanadamu..lakini anafanya hivyo ili pawepo na mashahidi ya kile kinachoendelea…Kama biblia inavyosema “Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa.(2Wakorintho 13:1)”

Ndicho kilichotokea kipindi kifupi kabla ya miji ya Sodoma na Gomora kuangamizwa. Mungu aliwatuma malaika zake wawili, kwenda kuipeleleza miji ile, na kama tunavyoifahamu habari, malaika wale walipofika jioni ile, wakakutana na Lutu, Lutu naye akawalazimisha kuingia nyumbani kwake, mwanzoni walikataa, lakini baadaye wakafika, na walipofika tu kumbe huku nyuma, walikuwepo pia wapelelezi wengine wanawafuatilia malaika wale, na hao si wengine zaidi ya watu wa miji ile..

Hivyo sio malaika tu waliokuwa wanapeleleza, na wao pia walikuwa wanapelelezwa, jambo ambalo linaendelea sasa katika roho..

Sasa walipoona hatma yao ni wapi, kuwa ni ile nyumba ya Lutu, hawakufanya chochote, bali walisubiri mpaka usiku ulipoingia  ndipo wakakusanyika wote wakaizingira ile nyumba ya Lutu na kumwambia Lutu, awatoe hao watu  ili wapate kulala nao..Embu fikiria hali yao ilivyokuwa mbaya..Sasa kama ukichunguza pale utaona, wale malaika hawakuchukua hatua yoyote kwanza, ni kama walikuwa wanawasikiliza walichokuwa wanamueleza Lutu pale nje, na mashindano yao pale mlangoni..Na baadaye ilipoonekana Lutu anashindwa, wakawa wanakaribia kuuvunja mlango, ndipo wakanyanyuka wakamvuta Lutu ndani, kisha wakawapiga upofu wale watu waliokuwepo pale mlangoni..

Hiyo ilisababisha ripoti yao ya upelelezi iwe imekamilika, kwamba Sodoma kumeoza na wao ni mashahidi, kilichobakia kwao ni kumuhimiza Lutu kwa haraka aondoke Sodoma kwa sababu miji ile wanakwenda kuiteketeza. (Soma Mwanzo 19 yote)

Ndugu yangu, dalili kubwa inayotutambulisha kuwa tunaishi katika wakati wa upelelezi wa malaika hawa, Sio kuzuka kwa vitendo vya Ushoga na usagaji tu peke yake, hapana, kwani hivyo vilikuwepo tangu zamani..lakini ni kuzuka kwa vitendo vya Ushoga na Usagaji katika nyumba ya Mungu…Tunavyoona leo hii ushoga unafungishwa katika nyumba ya Mungu, basi tujue hiyo ni dalili mbaya, ni sawa na kutaka kuzini na malaika wa Mungu walio katika kanisa lake..

Malaika hao wameshapita na wameshaona kile ambacho kilitokea wakati wa sodoma na Gomora ndicho kinachotokea na sasa hivi, hivyo wanachokifanya sasa ni kuwapiga watu upofu kwa kasi sana, ili wasione mlango wa neema tena ambao wenyewe wanauvunjia heshima, na kinachobakia kwa watu hao  ni maangamizi tu..

Unapojiona wewe ni mtazamaji wa Pornography, ujue kuwa wewe ni kundi moja na hawa wanaoufanya  ushoga nyumbani mwa Mungu, isipokuwa wewe tu ni mfuasi wa nyuma, lakini adhabu yenu ni moja,,..na hivi sasa unapigwa upofu, ambao hutakaa uuone mlango wa neema kamwe kama hutatubu. Ukiona unazini, na kwako wewe zinaa ni kama kitu cha kawaida na huku unajiita ni mkristo bado, ujue upofu unaendelea sasahivi duniani, ukiona unajihusisha na mambo yote ya kizinzi (iwe ni kujichua, au ulawiti) ujue upo katika kundi hilo la kupigwa upofu na malaika hawa wapelelezi wa Bwana.

Wanapopita na kuangalia makundi mengi ya watu, leo hii yapo kwenye simu zao mikononi, kutwa kuchwa ku-download video za pornography na kutazama video hizo, na miziki ya kidunia..ujue kuwa hao watu wanapigwa upofu, na malaika hao waliotumwa na Mungu kuipepeleza dunia, kabla ya kwenda kuangamizwa dunia hii kwa moto siku hizi za mwisho.

Wakati huu ni wakati wa hatari nyingi, ikimbie dhambi, unaweza kuona inavutia leo machoni pako, na ndivyo ilivyo dhambi siku zote ni ya kuvutia lakini mwisho wake ni majuto ya milele. Mungu tayari ameshakikasirikia kizazi hiki, kinachoichezea madhabahu yake mpaka kufikia hatua ya kufanya mambo ya ajabu kama hayo madhabahuni pake..Utasema ni hao sio mimi, kumbuka kile kikundi kichache kilichokuwa kinacheza mlangoni mwa Lutu ndicho kilichouwashia moto mji mzima wa Sodoma na Gomora..ikasababisha hata wengine walio mbali wasiojua chochote ambao wanafanya mambo kama hayo mwisho wao kufika. Kwahiyo uovu unapoendelea katika nyumba ya Mungu ni jambo la kuomboleza kwa wote.

Hivyo na sisi Bwana atusaidie tusiwe wamoja wapo, bali tuchukue hatua ya kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kabisa kumgeukia yeye, katika huu wakati mfupi wa kumalizia kabla ya unyakuo kupita. Kwasababu tusidhani kuwa yaliyowakuta wale, hawayawezi kutukuta na sisi.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

USINIPITE MWOKOZI

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

JIRANI YANGU NI NANI?

Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA?.Mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?

DANIELI: Mlango wa 8

Rudi Nyumbani:

Print this post

BASI, JIANGALIENI MIOYO YENU ISIJE IKALEMEWA NA ULAFI, NA ULEVI.

Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;

35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima”

Shalom, Jina kuu la mwokozi wetu Yesu libarikiwe daima.

Wengi tunayafahamu maneno hayo ya Bwana, lakini hatujui ni ulevi na ulafi wa namna gani unaozungumziwa katika Habari hiyo mpaka siku hiyo iwajilie ghafla, kama mtego unasavyo..

Ili kupata picha embu tutazame mfano mmoja halisi kabisa wa kwenye biblia na jinsi walivyolemewa na ulafi na ulevi wa kipekee mpaka, mwisho wao ulipowakuta kwa ghafla..

Sasa kama tukisoma kile kitabu cha Danieli sura ya 5, tunamwona mfalme mmoja aliyejulikana kwa jina la Belshaza, huyu alikuwa ni mtoto wa Nebukadreza, kama wengi tunavyoifahamu Habari, ni mtu ambaye alibahatika kuona mambo yote ambayo Baba yake aliyoyapita na jinsi alivyoadhibiwa kutokana kiburi chake na ukatili wa kutesa watu wasiokuwa na hatia na wengine kuwatupa katika matanuru ya moto, kama sio kuwachinja, lakini baadaye Mungu alikikomesha kiburi chake, kwa kumng’oa katika ufalme wake, akawa anaishi misituni kama sokwe Fulani tu, mpaka miaka 7 ilipoisha, na pale alipogundua kuwa Mungu ndiye anayetawala dunia nzima, na kwamba yeye ndio anatakiwa aogopwe ndipo akatubu na kumgeukia Mungu na Mungu akamrehemu na akamrejeshea enzi yake kupita kiasi hata kuliko pale alipokuwepo mwanzo.

Sasa huyu mtoto wake aliyeitwa Belshaza, alikuwa anayaona hayo yote, na alikuwa ameshapata somo kamili ambalo haikumpasa yeye tena alipitie kwasababu babayake tayari ameshafanyika mfano..Kama tu vile sisi, watu wa kizazi hiki, tayari mifano mingi ilishatangulia mbele yetu huko nyuma, mfano ile ya watu wa Nuhu, na Watu wa sodoma na Gomora, jinsi walivyoangamizwa kwa maovu yao, lakini sasa tunaona na kuzipuuzia, na kuzichukulia tu kama Habari zilizopitwa na wakati kama tu huyu mtoto wa Nebukadreza.

Yeye alipuuzia yale yote ambayo Baba yake aliyotendewa na Mungu.. Na kibaya Zaidi akaamua kuchukua hatua nyingine mbaya kuliko zote, ambayo ndiyo iliyompelekea hata Mungu kumwangamiza kwa ghafla na kwa haraka sana..Na hicho ndicho wote tunachopaswa tujifunze leo hii.

Alichofanya ni kuchukua vile vyombo vya hekaluni, ambavyo baba yake alivichukua kutoka Yerusalemu, alipouteketeza mji na hekalu, na kuvihifadhi asivitumie kwa kitu chochote kwasababu vilikuwa ni vitakatifu, lakini yeye (huyu Belshaza), akawa mlevi, na mlafi wa kupindukia, akawa anafanya karamu, akaona kuwa haitoshi kunywea vyombo vyake mwenyewe, chupa zake za vilabu vyake, na kutumia visu vyake vya kifalme kuchinjia nyama zake, na hata sahani zake akaona hazitoshi kuzitumia kuwekea vyakula vyake haramu…

hivyo akaenda kwenye hazina ya baba yake, na kupekua pekua na kuvikuta vile vyombo vya hekaluni ambavyo vilikuwa vimefunga na kuhifadhiwa visitumike, yeye akavichukua vile vyombo vitakatifu vya Mungu, akaanza kuvinywea na kuvilia yeye Pamoja na wakuu wake, na makahaba wake..Unaweza kuona Ni uvunjifu wa heshima kiasi gani.?? Hayo ndio mambo yanayoendelea katika roho sasa hivi..

Na alipomaliza kufanya vile tu, saa hiyo hiyo kiganja cha mkono kikatokea, kikasogea mpaka ukutani mahali ambapo mwanga ulikuwa unapiga, akaona kikiandika maneno yale, MENE, MENE, TEKELI NA PERESI.. Kama tunavyoijua habari maneno yale yalikuwa ni Hukumu, kwamba mwisho wake umeshafika, ufalme wake ndio umeishia pale..

Sasa huyu Belshaza, utaona tena aliposikia vile badala atubu, ndio kwanza anafikiria kumpandisha Danieli cheo, na kumfanya awe mkuu, unajua ni kwanini?.. Ni kwasababu alidhani, jambo hilo haliwezekani kutokea kwake, na hata kama likiwezekana basi litakuwa ni jambo la baadaye sana, kwasababu mji wake wote ameshauzungushiwa kuta kubwa sana pande zote, ambazo juu yake wapo walinzi wamekaa wakiangalia malango yake usiku na mchana yenye askari waliobebea wenye sifa dunia nzima, (kwasababu kipindi hicho Babeli ndio iliyokuwa inatawala dunia nzima)..

Hivyo Habari hizo za Danieli hazikumwogopesha hata kidogo, akiangalia kuwa hayo mataifa ambayo ameambiwa yatakuja kuuchukua ufalme wake, yaani umedi na uajemi ni vitaifa vidogo, visivyokuwa na nguvu, hivyo akawa hana hofu tena..

Lakini ndivyo alivyojidanganya..Biblia inasema usiku ule ule, alivamiwa na kuuliwa, na ufalme wake kuchukuliwa kirahisi na Wamedi na Waajemi, ni jambo la ghafla sana..utajiuliza wale watu walitokea wapi asipate Habari siku zote..

Ili kufahamu ukirudi katika historia inasema, ule mji wa Babeli ulikuwa na mto mkubwa ambao ulikuwa unaingiza maji katika mji, sasa kwa namna ya kawaida, maji yanayoingia katika mji hayawezi kuwekewa kuta, hivyo pale pale kwenye maingilio ya mto ule ndipo hapo hapo Wamedi walipokuja kuingilia usiku ule, walichokifanya ni kuupindisha ule mto mbali sana hivyo maji yakapungua ndipo walipopatia nafasi ya kuuingia mji, na kuwaua watu wale kwa ghafla sana na haraka usiku ule..wakati walinzi wa mji wanaendelea kulinda mageti makubwa kule..kumbe huku kwa njia ya chini ya watu wameshaingia mjini na kuanza kuangamiza watu.

Hata leo, Kanisa la sasa limeshalemewa na ulafi na ULEVI WA ROHONI, ni heri ungekuwa ni ulevi wa kawaida, lakini ni ulevi unaotumia vyombo vya hekaluni mwa Bwana na hiyo ndiyo inayoleta ghadhabu.. Yaani watu wanapomchanganya MUNGU NA DUNIA..leo wapo kanisani, kesho disko, leo wanamwimbia Mungu, kesho shetani, leo wanashiriki meza ya Bwana, kesho wanakwenda kuzini, yaani hayo yamekuwa mambo ya kawaida kabisa, mtu kusema ameokoka, na huku, anakunywa pombe kisirisiri, anazini nje ya ndoa, anajichua, anatazama picha za ngono ni mambo ya kawaida, anakula rushwa, ana honga..

Huo ndio ulevi na ulafi Bwana Yesu aliokuwa anauzungumzia pale..

Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;

35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima”

Moja ya hizi siku, dunia nzima itaingia katika mtego huo, wakati watu wakiwa katika vilele vya amani, katika furaha, ndipo mambo yatakapobadilika kwa ghafla. Hivyo ndugu, huu ni wakati wa kutengeneza uhusiano binafsi na Mungu..Dunia hii imeshaandikiwa MENE, MENE, TEKELI na PERESI..Ukizidi kung’ang’ania kwenda nao, mwisho wa siku itakuchukua kama ilivyomchukua Belshaza, Leo hii tubu itii injili, uokolewa, Usafishwa Maisha yako, Na Bwana atakusaidia kwa yale yaliyobakia.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

RABI, UNAKAA WAPI?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

ANGALIA USIJE UKANG’OA NGANO KATIKATI YA MAGUGU.

MUNGU AKIKUPITA LEO, HAIMAANISHI KUWA HAJAKUCHAGUA.

HATA NA BARNABA PIA AKACHUKULIWA NA UNAFIKI WAO!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

Chukua tahadhari juu ya neema ya Mungu.


Hakuna ulinzi mkubwa ambao mwanadamu anaweza kuupata kama ulinzi wa kuwa ndani ya Yesu..Kama wengi wetu tunavyojua au tulivyosikia kwamba watu wote waliompokea Yesu Kristo uhai wao unakuwa umefichwa pamoja na Kristo.(Wakolosai 3:3). Kiasi kwamba tunalindwa dhidi ya nguvu za giza na mipango yote ya Ibilisi.

Wengi wetu tunaifurahia neema hii na kutamani kuingia ndani yake lakini hatujui kuwa ikichukiliwa isivyopaswa ina madhara makubwa kuliko kitu kingine chochote tunachoweza kukijua.

Neema ya Mungu inafananishwa na nyumba ya karamu, yenye mlango…Mathayo 7:13. Sasa kama tujuavyo nyumba yoyote ile ya muhimu kama Ikulu au ukumbi wa sherehe ya muhimu sana ina mlango na vile vile ina uzio…na mara nyingi kuta zake zinakuwa zimezungushiwa uzio mwingine ambao ni wa umeme..Na kama ni nyumba yenye umuhimu mkubwa zaidi ya hayo inakuwa na walinzi wanaotembea tembea wenye silaha kuizunguka, lengo ni kuzuia watu wa wasiruke ukuta na kuingia ndani…Na ikitokea mtu akijaribu kukiuka na kuusogelea ukuta kutaka kuruka aingie ndani ndipo anaweza akajikuta kapigwa risasi au kapigwa shoti ya umeme, na hivyo hata kuweza kujisababishia kifo…Lakini ulinzi huo haujawekwa kwaajili ya kuangamiza watu, bali kulinda usalama.

Na Neema ya Mungu ni hivyo hivyo…Ipo nguvu ya ziada iwalindao wale watu walioingia ndani ya Neema ya Kristo..Nguvu hiyo ndiyo inayotulinda dhidi ya nguvu zote za giza, dhidi ya shetani na majeshi yake (mapepo na wachawi) na kila mpango mwovu wa Ibilisi..Hivyo yoyote anayejaribu kuingia kutaka kuwaharibu watu wa Mungu walio chini ya neema ya Mungu basi atakuwa anajitafutia matatizo yeye mwenyewe..

Lakini jambo lingine la kuogopesha ni kwamba ikitokea mtu aliyeko ndani ambaye tayari kashaingia ndani ya jengo hilo, akatoka na kwenda kupanda ukuta na kurukia zile nyaya za umeme zilizouzunguka ukuta, yeye naye atajeruhiwa vile vile kama sio kufa kabisa. Maumivu yale yale atakayoyasikia Yule anayetaka kuruka ukuta na kuingia ndani ndio hayo hayo atayapata Yule anayetaka kuruka na kutoka nje.

Madhara atakayoyapata mchawi anayetaka kuwadhuru watu wa Mungu, ndio hayo hayo atakayoyapata mkristo anayeuacha wokovu na kuurudia ulimwengu. Mkristo ambaye ameshaonja kipawa cha Mungu na kuburudika na neema ya Mungu, na ghafla anarudia uasherati wake, anarudia wizi wake, anarudia matusi yake, anarudia mauaji yake, usagaji wake, utoaji mimba wake, mambo ambayo alikuwa ameshayaacha machafu anayarudia tena…akidhani kwamba mkono wa Mungu ni kinyume cha wale waliopo nje pasipo kujua hata waliopo ndani ambao wanataka kutoka vile vile mkono wa Mungu upo kinyume chao.

Wengi wetu hatupendi kusikia mambo kama haya kwasababu hatupendi kuumizwa mioyo, hatupendi kusikia habari mbaya, lakini fahamu kuwa tahadhari siku zote sio habari njema, lakini zina umuhimu sana katika maisha hususani katika siku za baadaye…hata vidonge tupewacho na wataalamu wa afya ambavyo vinatumika kwa tiba, bado vina tahadhari zake…lengo la tahadhari zile sio kuwatisha watumiaji wala kuwakatisha tamaa bali kuwanufaisha zaidi.

Vivyo hivyo Neema ya Kristo inayo tahadhari…Na ni lazima kila mtu aijue tahadhari hiyo, wahubiri wengi hawaifundishi kwasababu watakosa waumini, na wao bado wanatafuta waumini…Lakini sikia leo hii mtu wa Mungu tahadhari, ili baadaye tusije kujuta, na tahadhari hii haikuhusu wewe unayesoma tu, hapana hata mimi ninayeandika inanihusu. Biblia inasema..

Waebrania 10:26 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;

27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.

28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Kama umeamua kumfuata Yesu basi umfuate kweli kweli..usiusogelee kabisa ukuta wa Neema..uwe ndani au nje ni upanga ukatao kuwili..Neno la Mungu linasema usizini…hizo ni kuta!..neno linasema usiibe, usiue hizo ni kuta..ukipanda na kuzivuka nguvu ya Mungu utakumaliza..ambayo hiyo Mungu hakuiweka kwaajili ya kuua watu, bali kwaajili ya kuwalinda watu wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

Rudi Nyumbani:

Print this post