Category Archive Home

JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.

Jiepusha na dhambi ya wivu/husuda ambayo mwisho wake ni mauaji.

Silaha moja kubwa shetani anayoitumia kuwadhuru watu ni wivu…mtu mwenye wivu ni rahisi kutumiwa na shetani kwa viwango vikubwa sana… Mauaji mengi yanasababishwa na wivu, uchawi mwingi unatokana na wivu, hila nyingi zinatokana na wivu..na mambo yote mabaya yanatokana na wivu.

Hivyo ni muhimu kujifunza kutokuwa na wivu ili tusiwe kifaa cha kutumiwa na shetani kuwadhuru wengine.

 Roho ya wivu ndiyo iliyowafanya  Mafarisayo na Masadukayo wamchukie Bwana, pale walipoona Bwana anatenda miujiza ambayo wao hawawezi kuitenda, pale walipoona Bwana anawarejeza watu wengi kwa Mungu kuliko wao…Na mioyoni Roho Mtakatifu alikuwa akiwashuhudia kabisa kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu…na walikuwa wanajua kabisa katumwa na Mungu lakini kwasababu ya wivu..wakawa wanajitoa ufahamu na kumkufuru.. Soma..

Mathayo 22:15 “Ndipo Mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri, jinsi ya kumtega kwa maneno.

16 Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu”.

Unaona, walijua kabisa Kristo alikuwa mtu wa kweli aliyetumwa na Mungu..

Soma tena.. Yohana  3:1-3 utalithibitisha hilo…

Yohana 3:1 “Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.

2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye”.

Lakini pamoja na hayo yote nguvu ya wivu ilikuwa kubwa ndani yao ikazidi nguvu ya kumpenda..na hatimaye wakafanya hila mpaka za kutaka kwenda kumsulubisha mfalme wao..Walimsulubisha moyoni wakijua kabisa huyu ni mwana wa Mungu aliyetumwa kutoka mbinguni…Hilo halikuwa na shaka mioyoni mwao. Walijua kabisa ndiye mfalme aliyetabiriwa kuja ulimwenguni.

Na hata walipompeleka kwa Pilato..Haraka sana Pilato ambaye hakuwa Myahudi akajua kuwa hakukuwa na kosa lolote alilolifanya Bwana Yesu ambalo linastahili yeye kusulubiwa lakini ni kwasababu tu ya wivu…Hawa wayahudi wamesikia tu wivu alivyojiita yeye ni mwana wa Mungu..Hilo tu! Wala hakuna lingine…walimwonea wivu kwa miujiza aliyokuwa anaitenda ambayo wao walishindwa kuitenda na wala hakuna lingine, na jinsi anavyowajalia watu wengi kupata wokovu…Kwahiyo hata Pilato aliliona hilo kama biblia inavyosema katika..

Marko 15:9 “Pilato akawajibu, akisema, Je! Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?

10 Kwa maana alitambua ya kuwa wakuu wa makuhani wamemtoa kwa HUSUDA.

11 Lakini wakuu wa makuhani wakawataharakisha makutano, kwamba afadhali awafungulie Baraba”.

Sasa neno ‘HUSUDA’ maana yake ni ‘WIVU’ soma tena (Mathayo 27:17-18)..Kwahiyo unaona Pilato alishawajua kabisa hawa watu ni wivu ndio uliowafanya watake kumwua Yesu na wala hakuna lingine..alijua kabisa mioyoni mwako wanamwamini Yesu na kwamba “Yesu katoka kwa Mungu, na ni mfalme wao” lakini kwa kuwa wamemwonea wivu ndio maana wanataka afe…Ndio maana Pilato alikuwa akiwauliza kwa kurudia rudia.. “kama kweli wamemaanisha kumuua mfalme wao”

Yohana 19:13 “Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha.

14 Nayo ilikuwa Maandalio ya pasaka, yapata saa sita. Akawaambia Wayahudi, TAZAMA, MFALME WENU!

15 Basi wale wakapiga kelele, Mwondoshe! Mwondoshe! Msulibishe! Pilato akawaambia, JE! NIMSULIBISHE MFALME WENU! Wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari”.

Wivu ni mbaya sana unakufanya umkane Mtu, hata kama unamwamini na kumpenda…

Na ndio maana mwishoni kabisa baada ya kusulubishwa Bwana Yesu, Pilato aliandika anwani juu ya msalaba wa Bwana Yesu kwa lazima.. “Yesu Mnazareti, Mfalme wa Wayahudi”

Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.

20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani.

21 Basi wakuu wa makuhani na Wayahudi wakamwambia Pilato, Usiandike, Mfalme wa Wayahudi; bali ya kwamba yule alisema, Mimi ni mfalme wa Wayahudi.

22 PILATO AKAJIBU, NILIYOANDIKA NIMEYAANDIKA”.

Unaona hapo?..Pilato aling’ang’ania kuandika anwani ile kwa lazima?…kwanini?..ni kwasababu anaujua unafiki wa mafarisayo..mioyoni mwao walimwamini lakini mdomoni walimkana na kumtukana na kumsulubisha na hiyo yote ni kwasababu ya wivu tu!. Na ndio maana Pilato akaandika anwani ile.

Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi”.

Sasa sio wote kabisa waliomwamini, Bwana Yesu…wapo ambao ni kweli hawakumwamini kabisa pamoja na ishara zote zile alizozifanya…lakini asilimia kubwa ya mafarisayo na wakuu wa makuhani walimwamini Bwana mioyoni mwao lakini WIVU ukawasababisha kumsulubisha Bwana, na sio Bwana tu bali hata mitume wake walisumbuliwa na mafarisayo hao hao..na yote hiyo ni kutokana na wivu tu.

Matendo 5:16 “Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa.

17 Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), WAMEJAA WIVU,

18 wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;”

Hiyo ndiyo silaha shetani aliyotumia kumpeleka Bwana msalabani…Na silaha hiyo hiyo anaitumia leo kuangamiza watu..Je! na wewe una wivu?…kama unaingiwa na wivu ndugu yako akipata jambo Fulani ambalo wewe huna ujue unakaribia kufanyika chombo cha shetani kumwangamiza, kama unasikia wivu jambo Fulani zuri ndugu yako, au jamii yako, au rafiki yako analolifanya, kama unasikia wivu, mwingine anapooa, au anapoolewa au anapofanya hiki au kile..au anapotoka hatua moja mpaka  nyingine…kuna hatari kubwa ya kufanyika chombo cha shetani. Na wivu ukizidi sana unakuwa huna tena huruma..unakuwa unatamani kifo kwa huyo ndugu yako kama vile Kaini, alivyomwonea wivu ndugu yake mpaka akaenda kumwua.

Hivyo ni kwa namna gani utashinda Wivu?

Kwanza ni kwa kumpa Yesu Kristo maisha yako?..Unapookoka Bwana anakufanya kuwa kiumbe kipya, na ya kale yote yanakuwa yamepita, unakuwa umefanyika kiumbe kipya…Ule utu wa zamani, Bwana anauzika, Nia yako Bwana anaigueza kutoka kutazama vitu vya ulimwengu huu vinavyopita na kutazama mambo ya ulimwengu ujao ya milele yasiyoharibika..Hivyo kunakuwa hakuna shughuli yoyote ya kidunia ambayo itaweza kukupa wivu ndani ya moyo wako kwasababu nia yako imeshageuzwa na kuutazama ulimwengu ujao ambao utajiri wake na hazina yako hauna mwisho.

Pili baada ya kuokoka unapaswa uanze kujiwekea hazina yako mbinguni, Biblia inasema hazina yako ilipo ndipo na moyo wako utakapokuwepo…Hazina yako ikiwa kubwa katika mambo ya ulimwengu huu na moyo wako lazima utakuwa huko huko, hilo haliepukiki, kama ndoto zako kubwa kuliko zote ni wewe kupata mali nyingi sana ili hatimaye watu wote waje kukuona na kukuangukia na kukuheshimu, hapo roho ya wivu hauwezi kuiepuka, kwasababu atakapotokea mtu kakuzidi kidogo tu au unamwona ananyanyuka utamwonea wivu. Ndicho kilichowakuta mafarisayo na masadukayo, walikuwa na ndoto kubwa za wao waonekane wapo juu ya watu wote, na alipotokea mwingine mwenye nguvu kuliko wao wakaishia kumwonea wivu.

Lakini kama hazina yako ipo mbinguni, kwamba ndoto yako kubwa ni siku ile uirithi mbingu kwa daraja la kwanza, na kuwa na thawabu kubwa kule, kamwe hutakaa umwonee mtu wivu kwa vitu vya kidunia vinavyopita…Hazina yako inapoongezeka mbinguni, mawazo yako, akili yako, na moyo wako wote unakuwa kule, unakuwa kila siku unatafakari utukufu na thawabu zinazokungoja kule, na hivyo habari ya kuanza kuona wivu kwa vitu vya kidunia unakuwa huna..

Na hazina ya mbinguni unaitengeneza kwa kumpendeza Mungu na kwa kuifanya kazi yake…Na kazi yake sio kuhubiri tu, bali hata ile ya kuosha choo cha nyumba ya Mungu ni kazi yake yenye thawabu kubwa kule, hata ile ya kuwaombea watakatifu ni kazi yake yenye thawabu kubwa sana…n.k Unapofanya hayo bila ulegevu Roho Mtakatifu kila siku atakuwa anakushuhudia ndani yako kwamba thawabu yako ni kubwa mbinguni, na inazidi kuongezeka siku baada ya siku, hivyo kamwe huwezi kumwonea wivu mtu aliyeoa/ kuolewa na wewe hujaolewa, au jirani yako ambaye ni bilionea..

Ufunuo 2:17 “Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea………

26 Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu”……

Ufunuo 3:5 “Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake”………..

12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya…….

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.N.k

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NI NANI ALIYEWALOGA?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

MSIJISUMBUE KWA NENO LOLOTE.

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

Je ni kweli kuna samaki nguva?..Je kwenye  biblia nguva katajwa?

Jibu: Ukweli ni kwamba hakuna mahali popote katika biblia palipotajwa uwepo wa samaki aina ya nguva. Maana yake ni kwamba hakuna kiumbe cha namna hiyo kilichoumbwa na Mwenyezi Mungu.

Lakini utauliza je! hicho wanachokiona watu ni nini? ambacho kimaumbile kinaonekana nusu mtu nusu samaki?

Jibu ni kwamba vinavyoonekana na watu vyenye umbo kama hilo ni roho za mapepo. Kumbuka biblia inasema shetani anao uwezo wa kujigeuza na kuwa hata Malaika wa Nuru (Kasome 2Wakorintho 11:14), sasa si zaidi kujigeuza na kuwa kiumbe kiumbe kingine chochote chenye umbo la ajabu?. Anao huo uwezo, anaweza kujiguza na kuwa kama nusu mtu nusu mbuzi, anaweza kujigeuza na kuwa nusu mtu nusu nyoka, vivyo hivyo anao uwezo wa kujigeuza na kuwa nusu mtu nusu samaki (ambao ndio hao wanaojulikana kama nguva).

Sasa shetani na mapepo yake wote wanao huo uwezo wa kujigueza na kuwa hivyo viumbe vya ajabu..Na lengo lao ni lile lile moja..Kuwapoteza wanadamu na kuwaweka mbali na kweli ya Mungu, na hatimaye wafe katika dhambi zao na kuingia Jehanamu ya moto, wala hana lingine. Hivyo shetani kila siku anabuni njia mpya za kuwafanya watu wawe wabaya zaidi na kuzidi kuuamini uongo wake.

Sasa haya mapepo ambayo yanajigeuza maumbile..huwa hayawatokei wala hayawaingii watu waliookoka (Yaani waliomwamini Yesu Kristo na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake). Huwa yanawatokea na kuwaingia watu ambao katika roho wapo dhaifu sana, na hao ni wale wote ambao wapo nje ya Neema ya Yesu Kristo. Huwa yanawajia katika ndoto, kuwahimiza kufanya jambo fulani lililo kinyume na neno la Mungu au kuwapa hisia ambayo ni kinyume na Neno la Mungu..

Na hisi kubwa na ya kwanza yanayopeleka kwa mtu ni hisia ya ZINAA na UASHERATI. Kwasababu hiyo ndio dhambi ya kwanza ambayo shetani anatumia kumwangusha nayo mwanadamu na ndio Dhambi ya asili.

Hisia ya pili ni.. kutenda mabaya, aidha kuabudu sanamu, au miungu, kuwa mshirikina, au wakati mwingine yanamletea mtu hisia za kuwa na chuki na jamii ya watu fulani, au mtu fulani na kumpeleka hata kutamani kuua, au kuiba au kudhuru. Hiyo ndio kazi ya mapepo hayo yanapomwingia mtu ndani yake…na haya yana majina mengi (wengine wanayaita majini, wengine vibwengo n.k)..lakini ndio hayo hayo mapepo…

Mapepo haya yakiwemo hayo yanayojigeza na kuwa huo mfano wa nguvu, huwa hayamtokea mtu kwa macho, yanakuwa ni roho ambazo zinamwingia mtu au zinatembea na mtu, na mtu anaweza kuziona tu katika ndoto..lakini si katika macho ya asili..Lakini pia kama mtu huyo hali yake ya roho ipo chini sana yanaweza kumtokea kabisa na akayaona dhahiri, wengi wa wanaoyaona hayo ni wale ambao ni wachawi au waganga, au washirikina…ambao wameshajiuza kwa shetani kikabisa.

Kwahiyo nguva si kiumbe kilichoumbwa ambacho kinaishi baharini, bali ni roho za mapepo, kama umewahi kuota upo na nguva au umewahi kumwona..Basi tambua kuwa hali yako katika roho ipo chini sana na ni hatari.

Hivyo suluhisho ni kumpa Yesu maisha yako, unapoamua kugeuka na kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi na maisha ya machafu uliyokuwa unaishi huko nyuma, na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, roho hizo zitakuacha hata pasipo kwenda kuwekewa mikono na mtu yoyote na utakuwa huru mbali na utumwa wa roho za mapepo.

Bwana akubariki sana.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuna haja gani ya kumwamini Yesu aliyezaliwa kama sisi?

SWALI: Mimi Nina MUNGU Wangu ambae Ni ALLAH subhanallah…sasa kwanini nimkabidhi maisha Yesu wakati naye alizaliwa Kama mimi?


JIBU: Mama yako alizaliwa kama wewe…lakini ilifika wakati Mwenyezi Mungu aliyakabidhisha maisha yako kwake. Ili uwe salama, ulindwe, uhifadhiwe, ulishwe na upendwe..na pamoja na hayo ufundishwe kanuni za maisha ambazo peke yako bila wazazi au mlezi usingeweza kujifunza.

Vivyo hivyo ulipaswa ukae chini ya sheria za wazazi wako ndipo uweze kufanikiwa, endapo ungekuika sheria hizo basi maishani usingefanikiwa….Na kama sio Mwenyezi Mungu kuyakabidhisha maisha yako kwa wazazi wako ambao wamezaliwa kama wewe, maisha yako yangukuwa magumu sana hapa duniani au hata pengine usingezaliwa kabisa au kama ungezaliwa ungekufa.

Vivyo hivyo Yesu alizaliwa kama sisi tulivyozaliwa, (Ingawa hakuzaliwa na dhambi ya asili kama sisi, kwasababu mimba yake ilitungishwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu), na katika nyakati hizi za uovu na mateso na dhiki za ulimwengu.

Mungu kwa huruma zake na kwa jinsi anavyotupenda akamtuma huyu Yesu Kristo, ili awe kama mzazi kwetu kwasababu sisi wenyewe hatutaweza kwa nguvu zetu na kwa akili zetu kujiongoza..Ndio maana hatuna budi wote tuyakabidhi maisha yetu kwake ili tuwe salama sasa na ahera.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

17 Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.

18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”

Yesu anapoingia maishani mwetu, anatupa furaha, faraja, amani, upendo na tunapata ulinzi dhidi ya Adui shetani na mapepo yake yote, siku zote za maisha yetu na tumaini la uzima wa milele.

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

Ubatizo wa moto ni upi?

YULE JOKA WA ZAMANI.

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

https://wingulamashahidi.org/2018/07/04/5-swali-je-kuna-dhambi-kubwa-na-ndogo-na-kama-hakuna-je-mtu-aliyeua-na-aliyetukana-je-watapata-adhabu-sawa/

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

Ni mistari ipi shetani anapenda kuitumia kuwaangusha watu waliosimama?


Shetani akitaka kumwangamiza mtu aliye mwamini Mungu, anachofanya ni anamchukua na kumpeleka juu sana,.. hamwachi pale alipo, kwasababu anajua mtu aliye chini hata akinguka, ataumia kidogo tu, lakini bado akawa na uwezo wa kusimama na kuendelea mbele tena..Badala yake anachokifanya yeye ni anamchukua na kumpelekea juu sana kwenye kilele cha mnara, mahali ambapo anajua akifanya kosa kidogo tu, na kuteleza basi habari yake ndio inakuwa imeishia pale pale…

Ndivyo alivyofanya kwa Bwana wetu Yesu, alimnyanyua na kumpeleka juu sana kwenye kilele cha hekalu,..Na wakati anampandisha, akaanza kumuhubiria Zaburi ya 91 moyoni mwake (Hii ndio zaburi shetani anayoitumia sana kama silaha yake)…

Inayozungumzia jinsi Mtu yule aliyekubaliwa na Mungu anavyopokea ulinzi wa kipekee kutoka kwa Mungu, haijalishi itakuwa ni wakati wa mchana au wa usiku, haijalisha atakuwa anazungukwa na magonjwa ya hatari kiasi gani ambayo ni tuishio katika dunia yaliyowaangamiza watu makumi elfu, lakini kwake yeye hayatamgusa hata moja..Jinsi mtu huyo anavyofunikwa chini ya mbawa zake ili mabaya yasimpate.. jinsi atakavyowekwa mahali pa juu..jinsi atakavyowakanyaga simba na majoka, na jinsi Mungu atakavyomtumia malaika zake wamlindie njia zake zote, asiteleze….

Kwa muda wako pitia zaburi yote ya 91, uone jinsi inavyouzungumzia ulinzi wa kipekee anaoupokea Mtu yule aliyekubalika na Mungu..lakini hapa tutatazama tu vifungu vichache..

Zaburi 91:10 “Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.

11 KWA KUWA ATAKUAGIZIA MALAIKA ZAKE WAKULINDE KATIKA NJIA ZAKO ZOTE.

12 MIKONONI MWAO WATAKUCHUKUA, USIJE UKAJIKWAA MGUU WAKO KATIKA JIWE.

13 Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.

14 Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;

16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu”.

Unaona? sasa Wakati anampandisha juu sana, alikuwa anamthibitishia mistari hiyo kichwani pake..Na kweli shetani alichokuwa anamwambia Bwana ni sahihi kabisa, lakini sio katika mazingira yale..Na alipomfikisha pale juu sasa, ndipo akamwambia huu ni wakati wa wewe kujitupa chini kwasababu Bwana Mungu wako amekupenda na kukuthibitisha, hakuna baya lolote litakaloweza kukupata …. Hivyo usiogope kujitupa chini kwasababu malaika zake wapo kila mahali ili Wakulinde katika njia zako zote. Na Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe

Unaweza kudhani alimaanisha jitupe tu chini kikawaida peke yake, La, sio hivyo tu.. shetani alimaanisha pia dondoka, kutoka katika msimamo wako wa Imani kidogo tu. Ukifanya hivyo Mungu wa mbinguni hatakuacha uangamie kabisa kwani atakutumia malaika zake ili kukurudisha pale ulipokuwa.

Lakini shetani alijua kitakachofuata baada ya pale ni nini..kwasababu alishawahi kuwaangusha watu wengi kwa njia hiyo hiyo akadhani itakuwa hivyo pia na kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Lakini Bwana alimwambia Neno fupi tu..Imeandikwa “Usimjaribu Bwana Mungu wako”.

Kama wewe ni umesimama katika wokovu, nataka nikuambie, katika mahali ambapo unapaswa uwe napo makini basi ni hapa..

Kwenye mahubiri yanayokuaminisha kwamba wewe umekubaliwa na Mungu wakati wote.., na hivyo unaoulinzi wa kipekee kutoka kwake.. kama hujui hiyo ndio mistari shetani anayoipenda kuitumia kuliko mistari mingine yeyote ili kukuangusha wewe uliyesimama..

Ni kweli Mungu ameahidi kufanya hivyo lakini ni kwanini aje kukuhubiria hivyo hivyo kila siku , hakuhubirii habari nyingine za kumcha Mungu? …Jiulize kwanini shetani hakumwambia Bwana, kwa maana imeandikwa mpende Bwana Mungu wako, kwa moyo wako wote, kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote…Badala yake anamwambia kwa kuwa imeandikwa atakuagiza malaika zake wakulinde, usiteleze….Utaona Ni mistari ya kusifiwa tu, na kufarijiwa tu na ya kutoa sifa tu ili ujione wewe ni kitu Fulani mbele za Mungu…hata kama utakuwa katika mahusiano mabaya na Mungu, atakuletea tu hiyo mistari..

Na kibaya Zaidi siku hizi za mwisho mafundisho ya namna hii ndio yanapewa kipaumbele, pale tunapohubiriwa kwamba Mungu ametukubali, Mungu ametuweka juu, hatutakwenda chini, maadui zetu watashindana wala hawatashinda, watakuja kwa njia moja lakini watatoweka kwa njia saba….mahubiri kama haya tunayapenda, ni kweli ni maneno ya Mungu lakini kumbuka hayo ndiyo yanayokupeleka katika kilele cha hekalu ili kukuangamiza kama hutakuwa makini..

Sasa ukiwa katika kilele cha mahubiri kama hayo, hutaki kusikia kingine chochote, hapo ndipo ibilisi anakuletea mambo maovu, kwasababu shetani alishakujaza ujasiri wote kuwa wewe ni mteule wa Mungu, huwezi kupotea?, Inakuwa ni rahisi kwako wewe kwenda kufanya uzinzi, kwasababu shetani ndani anakuhubiria na kukwambia Mungu anaelewa, bado anakupenda, ulishaokoka,atakulinda..Mungu haangalii mavazi yako, haangalii vimini vyako, anaangalia moyo wako, wewe ni mshindi tayari usikubali kushindwa…hata ukiendelea tu kuvaa uchi uchi na kutembea barabarani, haina shida wewe ni mtoto wa Mungu.

Kumbe hujui ndio ndio unaukaribia mwisho wako..Ukiingia huko ndio moja kwa moja, utakuwa umeshateleza na kuanguka kama yeye alivyoanguka alivyoasi zamani, Na mpaka utakapofika chini tayari umeshakuwa mfu rohoni..hufai tena.

Hizi ni siku za mwisho. Utakatifu hauhubiriwi, bali maneno ya kututia faraja tu, ya kutufanya tujione kuwa sisi tumekubaliwa na Mungu, ili kwamba tuendelee kustarehe katika dhambi zetu..

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”

Bwana atusaidie.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

JE! UMEFANYIKA KUWA MWANAFUNZI WA BWANA?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6

MJUMBE WA AGANO.

NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

YULE JOKA WA ZAMANI.

Kwanini Shetani ni joka wa zamani?


Shalom, ni kwa neema za Mungu wetu tumeliona tena jua leo..wapo ambao hawakupata nafasi hiyo, hivyo hatuna budi kumshukuru sana Mungu wetu. Karibu tujifunze Neno la Mungu chakula cha kweli cha roho zetu.

Biblia inasema katika..

Ufunuo 20:1 “Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.

2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;”

Shetani anajulikana kama joka wa zamani..ikiwa na maana kuwa ameishi muda mrefu, na ameishi katika hali hiyo hiyo ya ujoka tangu zamani…Na kama unavyojua kitu chochote ambacho kimeishi muda mrefu, kwa mfano mtu aliyeishi muda mrefu ni lazima atakuwa anajua mambo mengi…wazee wenye umri mkubwa wanakuwa wanajua mambo mengi zaidi kuliko vijana..

Kwasababu wamekumbana na mambo mengi katika maisha yao na wamejifunza mambo mengi, wamejifunza kutokana na makosa yao na kutokana na makosa ya watu wengine…hivyo hawawezi kufananishwa hata kidogo na watoto waliozaliwa hivi karibuni.

Vivyo hivyo shetani naye anajulikana kama joka wa zamani…

maana yake ni kwamba anajua mambo mengi sana yamhusuyo mwanadamu…alikuwepo tangu Edeni, anamjua Adamu kwa sura na tabia hajamsahau,..anamjua Hawa…anamjua Nuhu, na alikuwa anashuhudia jinsi dunia ilivyokuwa inaangamizwa kwa gharika…alikuwepo anatazama…Bado anaikumbuka sura ya Ibrahimu na ya Sara…anakumbuka ni wapi walipomsumbua katika maisha yao..Anamkumbuka Musa..na bado anazijua tabia zake zote na anaujua udhaifu wake..Anayo sura ya Danieli na ya Nebukadneza, na ya Eliya kichwani mwake na anazikumbuka tabia zao…Na zaidi ya yote anamfahamu sana Mkuu wa Uzima Yesu Kristo, anakumbuka matukio yote tangu anazaliwa mpaka alipokuwepo kule jangwani akimjaribu, na alipokufa na kufufuka, anajua nguvu zake na mamlaka yake aliyonayo sasa…

Vivyo hivyo anawajua watu, anawajua watu na tabia zao, anajua wanapenda nini, na hawapendi nini…Ameviona vizazi vyote tangu Adamu mpaka sasa…Hebu jiulize wewe tu mpaka umri ulioufikia sasa ambao pengine haujazidi hata miaka 60 lakini tayari umeshajua tabia za baadhi ya watu na baadhi ya makabila kiasi kwamba pengine hata ukimwona tu mtu Fulani tayari umeshajua kundi la kumweka hata kabla ya kuendelea mbele sana…Sasa kama wewe na miaka yako hiyo 50 tu tayari unajua jamii za watu na tabia zao…Unafikiri shetani atakuwa anawajua wanadamu kwa kiwango gani?..maana yeye tangu Edeni mpaka leo yupo.

Nataka nikuambia anawajua wanadamu vizuri..anajua ni wapi pa kuwashikia watoto, watu wazima na wazee…kwasababu mwanadamu ni Yule Yule…na biblia inasema hakuna jipya chini ya jua…anajua namna ya kummaliza mtu mchanga kiroho pindi tu anapotaka kujaribu kumtafuta Mungu…kwasababu alishajaribu kwa watu kadhaa huko nyuma wa vizazi vilivyopita na akafanikiwa…Anajua ni jinsi gani anaweza kuwaangusha watumishi wa Mungu..kwasababu alishajaribu huko nyuma na akafanikiwa kwa baadhi hivyo anatumia huo huo uzoefu kwa watu wa vizazi vyote. Anajua jinsi ya kuwazuia watu wasisali, wasimtafute Mungu n.k kwasababu alishaijaribu hiyo njia huko nyuma na ikafanya kazi.

Ndugu mpendwa usipoingia ndani ya Yesu kisawasawa hutamweza shetani kwa vyovyote vile anazo akili nyingi za kukuzidi wewe na mimi, ukisema humtaki Bwana Yesu na kwamba unaweza kujizuia usizini bila hata ya kuwa ndani ya Kristo, unapoteza muda wako! Siku moja utazini tu..alishawajaribu watu kama nyie huko nyuma na akawanasa hivyo wewe sio wa kwanza kuwaza hivyo au kujaribu hivyo..Ukisema naweza kufanya hichi chema au kile bila kuwa ndani ya Yesu..nataka nikuambie ni muda tu unaupoteza..watu kama nyie shetani alishawatafutia suluhisho lake pengine hata zaidi ya miaka 2000 iliyopita huko nyuma…wewe unaweza kukiri ni wa kwanza lakini kumbe hata ni wa milioni 10 kwenye kalenda zake na orodha zake za watu waliojaribu kufanya kama wewe huku wakiwa nje ya Kristo na akawashinda..

Hivyo wewe uliyezaliwa juzi huwezi kumzidi hekima Yule aliyekuwepo miaka mingi iliyopita huko nyuma…(Hujui ni kwanini shetani anaitwa mungu wa ulimwengu huu? Ni kwasababu anajua mambo ya wanadamu sana kuliko mwanadamu yoyote yule).

Ndio maana Bwana Yesu alimwambia kwamba siku zote anayawaza yaliyo ya wanadamu na si ya Mungu.. Kwanini? kwasababu anakesha kumsoma mwanadamu na namna ya kumtawala. Kasome (Mathayo 16:23)..

Hivyo utauliza kama shetani anayajua mambo ya wanadamu kiasi hicho, kiasi kwamba hakuna upenyo wa kuweza kumzidi ni nani basi atasalimika?

Jibu ni kwamba pamoja na ukongwe wake wote wa kuwafahamu wanadamu, yupo mmoja ambaye ni mkongwe zaidi yake..Na huyo si mwingine zaidi ya Mungu mwenyezi aliye Baba yetu ambaye tunamwabudu sisi kupitia Yesu Kristo(Danieli 7:9). Huyo anajulikana kama MZEE WA SIKU.

Danieli 7:13 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia HUYO MZEE WA SIKU, wakamleta karibu naye.

14 Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa”.

Baba yetu anatujua kuliko shetani anavyotujua..shetani anauzoefu wa kutuangusha lakini Hekima iliyo kwa Mungu inauwezo hata wa kuyajua mawazo yake na nia yake na mipango yake, na kuyaangusha chini mawazo yake..chochote anachotaka kukifikiria kwa uzoefu wake, sisi tulio ndani ya Kristo tayari tunauwezo wa kuitegua mitego yake..hekima ile ya Kiungu inaingia ndani yetu ambayo inatupa uwezo wa kuzitambua na kuziangusha fikra zote za shetani. Lakini hekima hiyo wanapewa wale tu wanaomwamini mwanae mpendwa Yesu Kristo.

Wengine wote walio nje ya Kristo kamwe hawataweza kumshinda Yule joka wa zamani ambaye ni Ibilisi..watapelekwa kule shetani anakotaka waende..hata kama hawataki, ndio maana mtu ambaye hajaokoka kisawasawa kamwe hawezi kuwa na Amani, na hawezi kuishinda dhambi, na mapenzi ya ulimwengu huu ndio anayoyatenda…wakati mwingine anapanga hiki lakini mwishoni kinaishia kuwa kingine…kwanini? Ni kwasababu anataka kujiongoza mwenyewe na kudhani anaweza kufanikiwa kwa nguvu zake na akili zake.

Hivyo kama hujaokoka, bado tumaini la kumshinda Yule joka lipo, Hekima ya kiMungu inataka kuingia leo ndani yako…usimsikilize shetani anayekuwambia akilini mwako sasahivi kwamba huwezi kuokoka kwamba unadhambi nyingi na Mungu hawezi kukusamehe…ndivyo alivyowaambia watu wengi wa vizazi vya nyuma na kuwaangusha..anatumia ukongwe wake tu…lakini wewe leo mkatae na mkane kwa vitendo…Amua leo kuacha dhambi, na kutubu, amua kuacha kwenda disko, amua kuacha kusengenya, amua kuacha ulevi na uasherati na Bwana atakupenda sana…Na hekima ya ajabu itokayo kwa yule MZEE WA SIKU, (YEHOVA) Mungu wetu,itaingia ndani yako itakayoweza kutambua mitego yake na hila zake…

Mithali 2:6 “Kwa kuwa Bwana huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;

7 Huwawekea wanyofu akiba ya hekima kamili; Yeye ni ngao kwao waendao kwa ukamilifu;

8 Apate kuyalinda mapito ya hukumu, Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake.

9 Ndipo utakapofahamu haki na hukumu, Na adili, na kila njia njema.

10 Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 78900131

Mada Nyinginezo:

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

NI NANI ALIYEWALOGA?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Mahusiano ya uchumba, ni tofuati na mahusiano ya kimapenzi. Yapo mahusiano ya uchumba ambayo mtu anakuwa nayo kwa mtu aliyemchumbia, hilo halina tatizo maadamu halihusanishwi na vitendo vyovyote vya zinaa. Watu hao wawili wanaweza wakakutana wakala pamoja, wakazungumza pamoja, wakafurahi pamoja, wakatembeleana nyumbani kwao, wakaweka mpingano pamoja..lakini si kulala, pamoja, au kukaribiana kimapenzi au kuonyesha dalili zozote za kukaribiana kihisia, ..

Lakini wapo watu wanaosema, huyu tayari kashakuwa mke wangu, hivyo hakuna shida, sasa nikifanya naye tendo la ndoa si tayari kashakuwa wangu nitamuoa tu?..

Lakini kabla hujafikiria kuwaza hivyo, embu jaribu kuwaza kwanza ni kwa nini lile tendo linaitwa Tendo la Ndoa?..Ulishawahi kujiuliza hivyo?.Linaitwa hivyo kwasababu ni tendo linalofanywa na wanandoa tu peke yao..Nje ya hapo haijalishi unampenda sana huyo mwenzako au unamalengo naye makubwa kiasi gani au kwamba atakuja kuwa mke wako baadaye au mume wako, haijalishi huo  tayari ni uasherati..Na waasherati wote Mungu atawahukumu.

Kama ingekuwa ni rahisi hivyo tu, hata mtu anayekutana na kahaba barabarani na kwenda kufanya naye uasherati basi na yeye angejitetea na kusema siku moja nitakuja kumuoa wacha nifanye nae kwanza..Unaona? Hilo jambo halimfanyi yeye kutokuwa muasherati…Tendo la ndoa linalofanywa kwa watu ambao sio wanandoa ni dhambi.

Waebrania 13.:4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.

Hivyo ikiwa wewe umempenda binti, na umeshamchumbia, ili ndoa yako ikubaliwe na Mungu..Subiri mpaka wakati Mungu atakapokuunganisha naye rasmi mbele ya Kanisa la Kristo. Na ni kwanini iwe ni katika kanisa la Kristo na si penginepo. Ni kwasababu Mungu unayetaka awaunganishe ndipo alipo. Wapo wengine wanafungishwa ndoa za kimila, au za kiserikali n.k…Unaweza kuziita ni ndoa lakini hizo zote Sio ndoa za kikristo..Ambazo zinaweza kupokea Baraka za Kristo mwenyewe.

Kwasababu kabla ndoa haijaitwa ndoa ni lazima kuwe na makubaliano na mapatano na maagano fulani, sasa kama ukifungishwa nje ya Kristo, hapo ndipo utakutana na nyingine zinaruhusu kuolewa au kuoa mke zaidi ya mmoja, nyingine zinaruhusu kuachana wakati wowote mnapochokana, nyingine ni lazima mtambike, n.k. mambo ambayo yanakinzana kabisa na mpango wa Kristo.

Hivyo ndugu/Dada,..Ndoa yako ikipitia hatua sahihi Kristo anazozihitaji. Basi ujue zipo Baraka tele za kindoa ambazo Mungu ataziachilia kwako na kwa uzao wako baadaye ikiwemo ndoa yenu kupokea ulinzi wa kiMungu tangu huo wakati. Lakini ukiwa na haraka na kuvuruga mipango, na kukimbilia kufanya jambo ambalo wakati wake haujafika, ujue kwa hakika kabisa Mungu hayupo na wewe, na hata ndoa yako hataibarikiwa…Na jaribu kuangalia utaona wengi wa wanaofanya hivyo, mwisho wa siku hawaoani, au wanazaa, na baadaye wanaachana, na watoto wanabakia kuwa na mazazi mmoja,.Hiyo yote ni matokeo ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa.

Hivyo ikiwa leo hii upo katika mahusiano ya kimapenzi(ngono) na mwenza wako, mpaka mmeshafikia hatua ya kuzaa, acha mara moja, mkatubu dhambi zenu wote wawili, kwa kumaanisha kabisa kisha muanze utaratibu wa kwenda kufungishwa ndoa yetu kanisani..Na hapo ndipo Bwana atakapowatazama na kuwaangazia rehema zake…Lakini vinginevyo ukiendelea kufanya hivyo ujue kuwa wewe ni mwasherati mbele za Mungu.

1Wakorintho 6:9  “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Fanya hivyo Na Bwana atakubariki.

Mada Nyinginezo:

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

CHAPA YA MNYAMA

 

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Kifo cha mtakatifu perpetua na felista kimebeba ujumbe gani kwetu?

Perpetua alizaliwa huko Tunis (Mji mkuu wa Tunisia) Afrika ya Kaskazini mwaka unaokadiriwa kuwa wa 182, alizaliwa katika familia ya kitajiri, yenye kuheshimika sana, baba yake alikuwa ni mpagani, lakini Perpetua aliupokea Ukristo na kuwa mfuasi kamili wa Kristo, japo historia haionyeshi ni kipindi gani aligeuzwa kuwa mkristo..Lakini ilifika wakati mfalme wa Kirumi aliyeitwa Septimius Severus…Alipiga marufuku ukristo katika majimbo ya Afrika kaskazini, kwamba mtu yoyote asijihusishe na imani yoyote ya kikristo au ya kiyahudi..Wakati huo Perpetua alikuwa anaishi na mume wake, pamoja na kijakazi wake aliyeitwa Felista, na katoto chake kachanga alichokuwa bado anakinyonyesha wakati huo ..

Sasa wakati agizo hilo linatolewa Perpetua alikuwa katika mafundisho ya kuelekea kubatizwa, lakini alibatizwa kabla ya kupelekwa gerezani..Ndipo baadaye yeye pamoja na wenzake wanne, wote walikamatwa na kupelekwa gerezani.

Baba yake kusikia vile, alikwenda moja kwa moja mpaka gerezani kumtazama binti yake ili kutafuta njia ya kumtoa, ndipo akamshauri Perpetua aukane ukristo, atoke gerezani aendelee na maisha yake ya kawaida..

Lakini Perpetua alimwambia Baba yake maneno haya.. “Baba unakiona hichi chungu hapa?”

Akasema ndio,

Je kinaweza kuitwa jina lingine tofauti na vile kilivyo?

Akasema, hapana!

Basi hata mimi siwezi kuitwa jina lingine tofuati na mimi nilivyo..Mkristo.

Ilipofika Siku ya pili Perpetua, alihamishwa gereza alilokuwepo na kupelekwa gereza lingine zuri zaidi ili aweze kumnyonyesha mtoto wake…Lakini baba yake hakukata tamaa alimfuata tena siku nyingine, lakini safari hii alikuja kwa kumbembeleza sana.

Akimwambia…Nihurumie mwanangu!, nihurumie mwanangu!, ikiwa ninastahili kweli kuitwa baba yako, ikiwa nimekupenda zaidi hata ya kaka zako, ikiwa nimekulea mpaka umefikia hatua hii ya heshima..basi nihurumie mimi baba yako..kubali kukataa tu wewe sio mkristo.

Akamdondokea, mpaka magotini akambusu mikono yake..akamwambia, mwanangu usiniache nikapata aibu kama hii katikati ya watu. Fikiri juu ya kaka zako, fikiri juu ya mama yako, fikiri juu ya shangazi zako, fikiri hata juu ya huyu mtoto wako mchanga ambaye hataweza kuishi pindi utakapokufa..Ghairi hayo maamuzi yako magumu!, uendelee na maisha yako ya kawaida.

Perpetua alizidi kuwa imara na msimamo yake akamtia moyo baba yake..Akaendelea kukaa kule kule gerezani.

Na Siku ya kuhojiwa ilipofika Perpetua na wenzake walipandishwa kizimbani mbele ya gavana, Na wenzake walipoulizwa kwanza juu ya msimamo wao walikiri kuwa wao ni wakristo, na wote wakakataa ibada za mfalme. Swali likageuzwa kwa Perpetua, naye akaulizwa na Gavana kuhusu msimamo wake.

Wakati huo baba yake alikuwa hapo karibu, amembeba mtoto wake yule, akamwambia, kubali ibada za mfalme, achana na hiyo imani yako, mwonee huruma mtoto wako.

Lakini Perpetua akasema mbele ya wote..Siwezi kufanya hivyo!!

Gavana akamuuliza, kwahiyo wewe ni mkristo.

Ndio! Perpetua alijibu..

Baba yake akaingilia kati akimlazimisha Pepertua aikane imani, lakini Hawakuwa na muda tena, wakamchukua yeye na wenzake wakawapeleka katika viwanja vya michezo (Arena) ili wauawe. Kufika kule kuliwa na wanyama wakali ambao tayari wameshaandaliwa, ambapo wanyama kama chui, dubu walikuwa wanaachiliwa kwa wanaume, na nyati kwa wanawake..wakamtupa Perpetua na yeye pamoja na wenzake, na kijakazi wake Felista ambaye kwa wakati huo alikuwa ni mjamzito naye..

Akaachiliwa nyati, akamchota Perpetua juu, wakati akiwa chini akaende kumsaidia kijakazi wake Felista, huku wote wamelowa damu..Wakaona haitaoshi wakawaleta kwa wauaji wa kirumi katika ma-arena hayo ili wauliwe kwa upanga..

Perpetua alikufa mwaka wa 203 akiwa bado mama mdogo mwenye umri wa miaka 22, hakuona ujana wake kuwa ni kitu kuliko Kristo, hakuona heshima yake ya kitajiri kuwa ni kitu kuliko Kristo, wala hakuhesabu kuikana imani kisa baba, au mama au mtoto wake.. Bali aliisimamia imani hadi dakika ya mwisho..

Biblia inatuambia..

Waebrania 11:35 “…..Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;

36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;

37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga;

Swali la kujiuliza kwetu sisi hususani kwako wewe mwanamke kutokana na mada hii:

Je unauthamini wokovu wako vipi?..Unasema umeokoka lakini kuacha kuvaa vimini na masuruali na manguo ya utupu, unaona ni vigumu, unajiona wewe ni kijana, Perpetua pengine alikuwa ni kijana Zaidi yako, tena aliyezaliwa katika nyumba ya kitukufu ya kitajiri pengine kuliko wewe, lakini hakuudosha utakatifu wake.

Kila tusomapo habari kama hizi tusiishie tu kuzisoma kama hadithi bali tufahamu kuwa..tunahimizwa na sisi pia tupige mbio kama hao, na kutupa kila mzigo wa dhambi unaotulemea na kutuzungika kwa upesi, kwasababu hawa ndio watakaotuhuku siku ile mbele za Bwana..kuwa walikuwa wazuri kushinda sisi lakini hawakuikana imani, walikuwa katika hatari kubwa kuliko sisi lakini hawakuupuuzia wokovu, walikuwa ni matajiri kuliko sisi lakini hawakusema utajiri wangu ni kizuizi nisikane nafsi..Walikuwa ni wajawazito, na wenye watoto wachanga, lakini hawakuthamini hicho zaidi ya wokovu wao..wewe na mimi tutajibu nini mbele za Bwana siku ile? Au tunafikiri watu hao walikuwa hawasikii maumivu, au walikuwa wana roho sana..hapana, ni walikana tu!..Biblia inasema hata Eliya hakuwa mtu wa ajabu sana, alikuwa ni mtu mwenye tabia sawa na sisi, lakini walijikana kwa gharama zote.

Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?

BONDE LA KUKATA MANENO.

Yeremia 33:3 (NIITE NAMI NITAKUITIKIA)

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUPATA MAONO YA MBINGUNI SIO KUFIKA MBINGUNI.

Kupata maono ya mbinguni sio kufika mbinguni…ndio mwanzo wa safari.

Bwana anatupenda, na wakati mwingine anawachukua baadhi ya watu (sio wote) ili kuwaonyesha mambo yaliyopo kule nyumbani, juu kwa baba yetu.

Anawapeleka kuwaonyesha mambo mazuri aliyowaandalia wanawe, anawaonyesha makazi yao ya kuduma yasiyoharibika na hazina zinazowangoja kule nga’mbo ikiwa watashinda..Anawaonyesha utajiri aliowaandalia na heshima na utukufu..anawaonyesha ni kwa jinsi gani mbingu inavyowatamani na ilivyojiandaa vya kutosha kuwalaki…na mambo mengine mengi ambayo hata hayaelezeki.

Ni mfano tu wa Wana wa Israeli baada ya kutolewa nchi ya Misri na kufikishwa kule jangwani..ambapo maili chache kabla kufika nchi ya Ahadi…Mungu aliwatuma wakaipeleleze nchi ya ile waliyoahidiwa, na aliruhusu waende watu wachache sana(yaani watu 12 tu) ndio walioteuliwa kwenda kuipeleleza…Na walifika kweli Kaanani na kuipeleleza walirudi kila mtu na jibu lake…lakini wote walikubaliana na jambo moja  kuwa nchi ile ilikuwa ni njema sana na imejaa unono na maziwa na asali, na baraka tele na kweli ni nchi yenye urithi mzuri usioelezeka.

Hesabu 13:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,

 2 Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.

3 Basi Musa akawatuma kutoka nyika ya Parani kama alivyoagizwa na Bwana; wote walikuwa ni watu walio vichwa vya wana wa Israeli……..

17 Musa akawapeleka ili waipeleleze nchi ya Kanaani, akawaambia, Pandeni sasa katika Negebu mkapande milimani,

18 mkaitazame nchi ni ya namna gani; na watu wanaokaa ndani yake, kwamba ni hodari au dhaifu, kwamba ni wachache au wengi;

 19 na nchi wanayoikaa kwamba ni njema au mbaya; kwamba wanakaa katika matuo au katika ngome;

 20 nayo nchi ni ya namna gani, kwamba ni nchi ya unono au ya njaa, kwamba ina msitu au sivyo. Iweni na moyo mkuu, mkayalete matunda ya nchi. Basi wakati ule ulikuwa wakati wa kuiva zabibu za kwanza.

21 Basi wakapanda wakaipeleleza nchi toka jangwa la Sini hata Rehobu, mpaka kuingia Hamathi.

22 Wakapanda katika Negebu, wakafika Hebroni; na Ahimani, na Sheshai, na Talmai, wana wa Anaki, walikuwako huko. Nao Hebroni ulijengwa miaka saba kabla ya Soani wa Misri.

 23 Wakafika bonde la Eshkoli, na huko wakakata tawi lenye kishada kimoja cha zabibu, wakalichukua kwa mti kati ya watu wawili; wakaleta makomamanga pia, na tini.

24 Bonde lile liliitwa bonde la Eshkoli kwa sababu ya hicho kishada walichokata huko wana wa Israeli.

25 Wakarejea baada ya kuipeleleza nchi, mwisho wa siku arobaini.

 26 Wakaenda wakafika kwa Musa, na kwa Haruni, na kwa mkutano wote wa wana wa Israeli, katika jangwa la Parani, huko Kadeshi; wakawaletea habari, wao na mkutano wote, wakawaonyesha matunda ya nchi.

27 Wakamwambia wakasema, TULIFIKA NCHI ILE ULIYOTUTUMA, NA HAKIKA YAKE, NI NCHI YENYE WINGI WA MAZIWA NA ASALI, NA HAYA NDIYO MATUNDA YAKE”.

Watu hawa ni kweli walifika katika ile nchi…lakini sio kwamba kwasababu wamefika basi ndio hawana haja ya kurudi tena kwa wenzao…Muda wa wao kufika kule ulikuwa bado…walikwenda tu kuonyeshwa nafasi zao kule…Lakini bado walikuwa hawajaiteka ile nchi, walipaswa warudi kwanza wakapange vita wapambane wayaondoshe yale majitu yaliyoshikilia urithi wao katika nchi ya Ahadi ambayo wameahidiwa, wakishawaangusha ndipo waimiliki…

Ndio maana Bwana Yesu alisema katika..

 Mathayo 11:12 “ Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”

Shetani sasa kashikilia nafasi zetu katika ulimwengu wa roho, tunapaswa tumwangushe chini kabla ya kufika nga’mbo, na vita tunapambana hapa hapa duniani…tutakapomwangusha chini ndipo tutazirithi baraka zetu….(na tunamwangusha chini kwa kuishi Maisha matakatifu na makamilifu ya Neno la Mungu, yanayompendeza yeye),….hatuna budi kupambana vita hapa…kusikia tu mbinguni ni kuzuri tumeandaliwa hiki na kile haimaanishi kwamba ndio tayari tumekwishafika…bado kuna vita vya kupambana kumwangusha shetani katika Maisha yetu..

Shetani hataki tuende mbinguni kabisa, hataki hata kidogo kwasababu anajua uzuri tutakaoukuta kule, … anapambana sana kuhakikisha hatufiki kule, kama alivyopambana na wana wa Israeli kuhakikisha hawafiki nchi ya Ahadi, au hata wakifika basi watafika wachache sana na kwa shida sana..Hebu tafakari katika ule umati wote waliotoka Misri Zaidi ya watu milioni 2 waliofanikiwa kuingia nchi ya Ahadi walikuwa ni watu wawili tu (2)! Na iliwachukua miaka 40 kuingia tu ile nchi ambayo ni maili chache tu, safari ya mwezi mmoja tu. Alikuwa ananyanyua kila aina ya vikwazo walipokuwa njiani..aliwatumia mpaka manabii wa uongo kuwaangusha wana wa Israeli walipokuwa njiani.

Na sisi ni hivyo hivyo…mbinguni hatuendi kwa miguu kama wana wa Israeli walivyokwenda Kaanani, kama tutaishi Maisha ya kutoujali wokovu kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokuwa, tutaangamizwa na hatutaurithi ufalme wa mbinguni, kama tukikubali maneno ya manabii wa uongo kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokubali kuyasikiliza maneno ya akina Kora na Balaamu basi na sisi hatutairithi nchi.

Kama hatutamheshimu Mungu kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokosa kumheshimu Mungu wakiwa safarini basi haijaishi tumeikaribia mbinguni  kiasi gani hatutairithi.. Kama tutakata tamaa na kutoamini kwamba tunaweza kufika mbinguni basi hatutafika kweli kama wale watu ambao baada ya kwenda kanaani kuipeleleza walileta ripoti za kuwaogopesha watu, na wote walikufa..

1Wakorintho 10:5  Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.

6 BASI MAMBO HAYO YALIKUWA MIFANO KWETU, KUSUDI SISI TUSIWE WATU WA KUTAMANI MABAYA, KAMA WALE NAO WALIVYOTAMANI.

7  Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.

8  Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.

9  Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

10  Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.

11  Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

12  Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Biblia inasema..

Ufunuo 21:7  “Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

8  Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”

Ufunuo 21:27  “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”

Mpe leo Yesu Maisha yako kama hujampa. Na pia jikane nafsi yako, jitwike na msalaba wako mfuate Yesu kama ulikuwa hujafanya hivyo..Safari yetu karibia inafika ukingoni, na shetani ndivyo anavyozidi kuongeza jitihada kuwapunguzia watu kasi ya kuingia uzimani..

Kumbuka mtume Paulo alichokisema, aliponyakuliwa kule juu na kuonyeshwa mambo ambayo hayatamkiki, Hiyo ni kuonyesha ni kwa jinsi yalivyo ya ajabu na ya kushangaza kiasi kwamba hata lugha haziwezi kuelezea, (2Wakorintho 12:4)..sasa unasubiri nini..Kimbilia kwa YESU ayaokoe maisha yako.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

RABI, UNAKAA WAPI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

TUNA WAJIBU WA KUOMBEA MAHALI TULIPO.

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.

HISTORIA YA ISRAELI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.

Livunjeni hekalu hili nami katika siku tatu nitalisimamisha..

Mara nyingine Bwana Yesu alipotaka kufikisha ujumbe Fulani, alikuwa anatumia mfano wa mahali husika ili kuchanganya mada mbili kwa wakati mmoja …Kwamfano utaona wakati ule mitume wa Bwana Yesu waliposahau kuchukua ile mkate ambayo ilibaki wakaanza kugombana wao kwa wao kwa kulaumiana kwanini hawakuibeba, …lakini Bwana Yesu alipowasikia, mabishanao yao alitumia mfano mwingine kuzungumza nao kana kwamba alikuwa hamaanisha hicho walichokuwa wanakibishania kwa wakati huo..

Marko 8:13 “Akawaacha, akapanda tena chomboni, akaenda zake hata ng’ambo.

14 Wakasahau kuchukua mikate, wala chomboni hawana ila mkate mmoja tu.

15 Akawaagiza, akasema, Angalieni, jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.

16 Wakabishana wao kwa wao, kwa kuwa hawana mikate.

17 Naye Yesu akatambua, akawaambia, Mbona mnabishana kwa sababu hamna mikate? Hamfahamu bado, wala hamjaelewa? Je! Mioyo yenu ni mizito?

18 Mna macho, hamwoni; mna masikio, hamsikii? Wala hamkumbuki?

19 Nilipoivunja ile mikate mitano na kuwapa wale elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vimejaa vipande? Wakamwambia, Kumi na viwili.

20 Na ile saba kuwapa wale elfu nne, mlichukua makanda mangapi yamejaa vipande? Wakamwambia, Saba.

21 Akawaambia, Hamjafahamu bado?”

Unaona hapo? Bwana Yesu alitumia mfano wa chachu, na kusema, jilindeni na chachu ya mafarisayo…Lakini mitume wakadhani anazungumzia chachu ya mikate ya mafarisayo, hiyo ikiwafanya wazidi kugombana zaidi ili apate kuwanasa vizuri,..Hapo ndipo Bwana akapata nafasi ya kuwakemea kwa kukosa kwao ufahamu, akawaambia hamjafahamu bado?, mimi sizungumzii habari za mikate, mmesahau ni mikate mingapi mlikusanya kama masalia wakati ule?, hamjafahamu bado, hamjaelewa, mioyo yenu ni mizito, hamna imani kwa Mungu bado kuwa hata sasa anaweza kuwafanyia muujiza kama ule ule wa mikate mengine mkala mkashiba, pasipo kuwa na chochote?…lakini bado mnamtilia shaka Mungu?…Mimi sizungumzii habari za mikate ninaachomaanisha ni jilindeni na mafundisho ya mafarisayo..

Sasa utaona hapo mitume walipata mafundisho mawili, la kwanza ni kutokana na kile walichokuwa wanakifiria juu ya tumbo, kuwa Mungu bado anaweza kuwahudumia hata kama kunaonekana hakuna mlango wa kupata chakula, na cha pili ni kuhusu mafundisho ya mafarisayo (ambayo yanafananishwa na chachu/hamira) ambayo kazi yake ni kuumua na kupindua uhalisia wa Neno la Mungu…Lakini waliupata ule ujumbe uliokuwa unawahusu kwa wakati wao.

Ndivyo hivyo hata wakati ule Bwana Yesu alipokwenda hekaluni, akaona jinsi watu walivyoweka tumaini lao lote katika lile hekalu, jinsi lilivyokuwa limepambwa kwa namna ya ajabu, jinsi lilivyokuwa kubwa, na kukarabatiwa kwa muda mrefu wa miaka 46 na Herode..jinsi watu wengi walivyokuwa wanatoa sadaka zao kwa ajili ya hekalu lile.. Lakini jicho la Bwana Yesu lilikuwa linaona mbali zaidi yao, lilikuwa linaona muda si mrefu hekalu lile halitakuwepo, litakuwa limebomolewa, mahali pale patakuwa pamechomwa moto, watu watauawa na kuchinjwa kama kuku..lakini wale watu hawakuliona hilo, walikuwa wanajisifia tu majengo yake, hawaoni wakati umekaribia mji huo waliokuwepo ambao wanaupenda utateketezwa kwa moto…

Ndipo sasa wakati Bwana akiwa pale hekaluni anavuruga vuruga bishara zao.. wayahudi wakamfuata na kumuuliza, Ni ishara gani utuonyeshayo, kwamba unafanya haya?

Yesu akawajibu…

Yohana 2:19 “…..Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha.

20 Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?

21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake.

22 Basi alipofufuka katika wafu, wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa alisema hivi, wakaliamini lile andiko na lile neno alilolinena Yesu”.

Unaona, Bwana Yesu alimaanisha kweli juu ya hekalu la mwili wake kuwa atakufa na siku ya tatu atafufuka, lakini pia alitaka wafikirie vile vile juu ya habari za kubomolewa kwa hekalu, ili awafundishe jambo..lakini wengi wao hawakuwa tayari kutaka kujua zaidi, wakamwona kama karukwa na akili..anazungumza ujinga.

Lakini baadaye wanafunzi wake wanyenyekevu waliliweka hilo akilini…wakaanza tena kumwonyesha majengo ya hekalu lile ambalo yeye alisema watu walibomoe,..jinsi lilivyojengwa vizuri kwa mawe ya thamani…

Mathayo 24:1 “Yesu akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya hekalu

2.Hamyaoni haya yote? Amin, nawaambieni, Halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa”.

Lakini wanafunzi walivyosikia vile, hawakuishia pale, walizidi kuendelea kutaka kujua hatma ya hayo mambo itakuwaje, wakamfuata sasa faraghani, wakiwa peke yao tu Bwana, ndipo wakamuuliza..mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja kwako? Na ya Mwisho wa dunia? Maswali matatu.

Hapo sasa ndipo Bwana Yesu akaanza kuwafunulia hatua kwa hatua, mambo yatakayotendeka kuanzia ule wakati, mpaka siku mji ule utakapozingirwa na majeshi, na hekalu kubomolewa, mpaka siku za mwisho..ambayo maneno haya hata sisi wa kizazi hiki tunayatumia kama dira ya kutambua majira ya kuja kwa Bwana Yesu..Soma Mathayo 24, Marko 13, na Luka 21. Utaona habari zote za siku za mwisho zitakavyokuwa.

Lakini mafunuo hayo yote yalitoka katika Neno moja tu la Kubomolewa kwa hekalu..Kama mtume wasingetaka kujua zaidi, basi habari za kuteketezwa kwa Yerusalemu na warumi mwaka 70W.K, ambapo watu waliuawa kikatili, wasingekaa wajue pia habari za manabii wa uongo, na kusimama kwa chukizo la uharibifu wasingekaa wajue..

Vivyo hivyo hata sasa, tukiwa tayari kutaka kujua zaidi juu ya maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo katika Neno lake, kwa kumaanisha kujifunza Neno lake na sio kusoma tu kama gazeti, ndipo tunapojijengea nafasi nzuri ya kupokea mafunuo zaidi yamuhusuyo yeye.

Lakini kama tutasoma biblia juu juu tu, na kusema aa hii haiwezekani, au tunasema kile Bwana alimaanisha vile sio hivi..Tutabakia, kuujua upande mmoja tu wa maandiko..Na kufanana na wale watu waliomsulubisha pale msalabani na kumdhihaki…walisikia tu upande mmoja (livunjeni hekalu hili)

Zaburi 25:14 “Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake”.

Hivyo Bwana atusaidie tuzidi kumjua Zaidi yeye, mpaka tutakapofikia ukamilifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ni dhambi kuchukua riba?

Biblia inasema tusikopeshe kwa riba, je! Wanaowakopesha watu kwa riba wanafanya dhambi?


JIBU: Biblia imezuia kutozana riba ndugu kwa ndugu tu..lakini kwa wengine nje ya ndugu sio dhambi kuwatoza riba.

Kumbukumbu 23:19 “Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;

20 mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki”.

Kwa mfano ndugu yako unamwona anayoshida, anaomba umkopeshe fedha kidogo, halafu wewe unatumia ile fursa kumwambia aongeze na kiwango kingine cha fedha juu yake(riba), kama faida yako, Hiyo ni dhambi, akikopa, basi arudishe kile kile alichokopa..Usigeuze shida za ndugu yako kuwa mtaji..

Katika hali ya kawaida hata bila kuambiwa na mtu au kufundishwa, ukiwa na nyumba ya biashara, halafu ndugu yako wa karibu amekuja kukaa hapo kwa kipindi fulani tu.. Huwezi kumwambia alipie kodi kamili kama watu wengine, anaweza kulipia tu zile gharama za kawaida ndogo ndogo lakini sio kulipia kila kitu..hakuna mtu mwenye utu anaweza kumfanyia hivyo ndugu yake.

Hali kadhalika katika Ukristo, wote tuliomwamini Yesu Kristo tunafanyika kuwa ndugu..Upendo wa Kristo unatuunganisha pamoja.tunakuwa tunapendana bila masharti..Upendo huo unatufanya kusiwepo hata na hamu ya kutaka faida kutoka kwa ndugu zetu katika Imani kama vile ilivyo katika ndugu zetu wa mwili. Ndio hapo biblia inatuasa kwamba tusitozane riba sisi kwa sisi. Lakini kwa mtu mwingine nje na ndugu zetu wa kimwili na kiimani, tunaweza kuwatoza ili tupate faida katika tunavyovifanya..kwasababu riba ndio inayokifanya kile kitu au ile shughuli ile iendelee mbele zaidi.

Lakini tukiwatoza ndugu zetu kwa lengo la kupata faida hapo upendo wa Kristo haupo ndani yetu, na hivyo tunafanya dhambi na kumkosea Mungu.

Ezekieli 22:12 “Ndani yako wamepokea rushwa ili kumwaga damu; umepokea riba na faida; nawe kwa choyo umepata mapato kwa kuwadhulumu jirani zako, nawe umenisahau mimi, asema Bwana MUNGU.

 Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post