Category Archive Uncategorized @sw-tz

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Maana inayojulikana ya Unafiki ni ile hali ya kutoa maneno, au kuonyesha hisia au vitendo kwa nje tu, ambavyo kiuhalisia ndani ya mtu huyo havipo.

Kwamfano mtu anaweza kuwa anakuchukia, lakini kwa nje akawa anaonyesha kama kukujali na kukuchekea. Huo ndio unafiki.

Pengine unaweza ukawa unafahamu aina hiyo moja ya unafiki, lakini Leo tutaona aina mbalimbali za unafiki ambazo zinazungumziwa kwenye biblia, na namna gani ya kuzikwepa, kwasababu moja ya dhambi ambazo zinamchukiza Mungu sana ni unafiki, na inawapeleka watu wengi kuzimu pasipo wao kujua.

  1. Aina ya kwanza ni pale unapoijua elimu ya dunia hii kuliko elimu ya Mungu.

Hilo Bwana Yesu aliliweka wazi kabisa akasema..

Luka 12:54 Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya?

Ikiwa Geografia ipo kichwani, kanuni za fizikia umezitunza mpaka unafahamu ni kwanini jani linaanguka chini na haliendi juu, unajua ukiumwa unaweza kwenda kutumia mwarobaini ukapona..Lakini unashindwa kujua kwa Mungu yupo, au hizi ni siku za mwisho. Ukweli ni kwamba Mungu anakuona kama ni mnafiki, na mwisho ukifika hatahangaika kukupa neema ya kumtambua bali utaishia kupotea kwasababu anajua wewe unajiweza, lakini hutaki tu.

  2. Ni pale unapoona matatizo ya wengine sana, kuliko matatizo yako mwenyewe;

Bwana alisema;

Mathayo 7:3 “Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?

4 Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?

5 Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako”.

Hali hii inakufanya, uwaone wengine wote ni wakosaji, au hawastahili, na matokeo yake Mungu anakuona na kukuhukumu vilevile kama unavyowahukumu wao, Soma habari ya Yule farisayo aliyejihesabia haki zaidi ya mtoza ushuri( Luka 18:9-14) utalithibitisha hilo. Hivyo, hatuna budi, kujiuhubiria kwanza sisi, ndio tuende na kwa wengine.

3. Pale unaposali au unapotoa sadaka, lengo lako likiwa ni utazamwe na watu, kuwa wewe ni mtoaji au mwombaji mzuri, huo Bwana anauona pia ni unafiki.

Alisema:

Mathayo 6:1 “Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.

2 Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu”.

4. Pale unapoufahamu ukweli lakini unawazuia wengine wasiujue ukweli huo kwa makusudi.

Mathayo 23:13 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.”

Hii inawahusu sana sana viongozi wa dini, kwamfano pengine wanajua ubatizo sahihi ni wa kuzamishwa katika maji mengi, lakini hawawafundishi kondoo wao hilo, wanajua, hizi ni siku za mwisho na Yesu yupo mlangoni kurudi, kwamba watu waache dhambi wamgeukie Mungu, kinyume chake wanawahubiria mafanikio tu miaka yote, ili tu wapate fedha. Huo Bwana anauona kama ni unafiki, mbaya sana, na adhabu yake ni ziwa la moto.

5. Unafiki ni pamoja, na kujifanya msafi lakini, ndani ni mchafu:

 Mathayo 23:27 “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote.

28 Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi”.

Hili bado lipo kwa viongozi wa imani, unakuwa askofu au mchungaji, unavaa kanzu nyeupe, unaitwa baba, lakini unafumaniwa na skendo za uzinzi,  unakunywa pombe kichini chini, unapenda mambo ya ulimwenguni. Kwa Bwana ni heri tujionyeshe kuwa sisi ni wakosaji, kuliko kujificha nyuma ya kivuli cha utakatifu ni hatari sana.

6. Unafiki ni pale unapojua unapaswa umtumikie Mungu, lakini hufanyi hivyo kwa kutoa udhuru:

Soma Mathayo 24:45-51, utaona anazungumzia habari ya Yule mtumwa mwaminifu, ambaye alifanya vyote alivyoagizwa na Bwana wake bila udhuru, lakini mwingine, akajisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia akaanza kuwapiga wafanyakazi wake. Bwana Yesu anasema atakaporudi, atamweka fungu lake pamoja na wanafiki. Epuka udhuru na uvivu katika kumtumikia Mungu.

Mathayo 24:50 “bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51 atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

7. Na mwisho, unafiki ni pale unaposisitizia watu wayatimize yale maagizo, madogo, lakini yale ya msingi, na yenye kuokoa, huna habari nayo.

Kwamfano kuhimiza sana utoaji wa sadaka, ambao kimsingi Bwana mwenyewe alisema tufanye hivyo, lakini pale inapokuwa imezidi kila ibada ni sadaka tu, sadaka tu, mpaka ya mchicha, na tunasahau mambo makuu kama Utakatifu, kumcha Mungu na upendo. Huo ni unafiki mkubwa kwa Bwana..

Mathayo 23:23 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.

24 Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia”.

Bwana atusaidie tujiepusha na hizo aina saba (7) za unafiki, kwasababu zitatupelekea jehanamu ikiwa zipo ndani yetu.

Lakini swali ni Je! Tunazikwepaje? Jibu ni kwa kumaanisha kumfuata Yesu kwa mioyo yetu yetu.  Kwa jinsi tunavyomkaribia yeye ndivyo anavyotukaribia na sisi, kutusaidia kuwa kama yeye. Hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kutoka katika moyo wako, kisha nenda kabatizwe ikiwa hukufanya hivyo, kumbuka ubatizo sahihi ni kwa jina la YESU KRISTO sawasawa (Matendo 2:38). Kisha Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu, ikiwa utapenda upate msaada huo wa wokovu, basi wasiliana nasi kwa namba zinazoonekana chini;

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

MAMA UNALILIA NINI?

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

YESU ANA KIU NA WEWE.

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Upole ni nini?

Upole ni kitendo cha kutokuonyesha madhara, kwa mtu au kiumbe kingine, huwa unaambatana na utulivu . Upole unakuwa na maana Zaidi pale ambapo unaouwezo wa kuleta madhara kwa kiumbe kingine lakini hutumii uwezo huo, kumdhuru, Kwamfano ni kitu gani kinachomtofautisha nyoka na ng’ombe.

Nyoka ni kiumbe kidogo, dhaifu, hakina miguu, wala mikono, tofauti na ng’ombe, ambaye ni mkubwa, mzito, na mwenye pembe kiasi kwamba ukiwekwa naye katika mapambano ni rahisi kuuliwa naye. Lakini kwanini wewe itakuwa ni rahisi kumkimbilia ng’ombe na sio nyoka?.

Ni kwasababu ng’ombe ni mpole, si rahisi kutumia uweza wake wa pembe, na nguvu zake kukudhuru . Lakini ukimkaribia tu nyoka muda huo huo, atakuuma na utakufa.

Vivyo hivyo na katika wanadamu. Wapo ambao ni wapole lakini wapo ambao si wapole.

Katika biblia ipo mifano ya watu wawili ambao walishuhudiwa kuwa ni wapole. Wa kwanza ni Bwana wetu Yesu Kristo. Na wa pili ni Musa.

YESU KRISTO:

Bwana Yesu mwenyewe alisema.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Alikuwa ni mpole mfano wa mwanakondoo. Na kwasababu ya upole huo, ilimpelekea mpaka Roho Mtakatifu kushuka juu yake kipekee sana kama HUWA (Njiwa). Kumbuka sikuzote njiwa hatui sehemu isiyo na utulivu, wala hawezi kutua juu ya mnyama mkali kama vile mbwa mwitu, Bali anatua juu ya mnyama mpole kama vile kondoo, na ndio maana Bwana Yesu alitambulika kama mwanakondoo wa Mungu.

Hatushangai ni kwanini Mungu alimtukuza namna ile, kwanini leo hii watu wote wanamkimbilia Kristo, ni kwasababu alikuwa mpole sana rohoni. Sio kwamba alikuwa mnyonge, hawezi kuangamiza, au kuharibu watu, kumbuka Anaitwa pia “Simba wa Yuda”, Tunajua tabia za simba sio upole. Lakini yeye alikuja katika upole.. Hiyo ndio sifa kuu ya mtu mpole.

MUSA:

Mtu mwingine tunamsoma katika biblia aliitwa Musa. Utajiuliza ni kitu gani cha kipekee alichokuwa nacho Musa, mpaka kikamfanya awe karibu sana na Mungu kwa namna ile?

Ni kwasababu ya Upole wake, Tunasoma;

Hesabu 12:3 “Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi”.

Musa aliwazidi watu wote waliokuwa duniani kwa upole. Na hiyo ikamfanya awe karibu sana na Mungu, kuliko wanadamu wote walioishi duniani wakati huo.

Hata sasa, kanuni ya Mungu ni hiyo hiyo, Tukitaka tumkaribie Bwana sana, hatuna budi kuwa Wapole.

Tunakuwaje wapole?

Kwanza ni Kwa kujishusha: Unapokubali kuonekana wewe ni dhaifu, ni hatua nzuri sana ya kuelekea upole, Lakini unapotaka kujiona wewe ni Hodari wa mambo yote, ni ngumu kuwa  mpole. Usipokubali kuchungwa, , ujue kuwa utabikia kuwa mbuzi sikuzote na si mwanakondoo

Pili Kwa kuzizuia hasira zetu: Hatuna budi, kuwa watu wa kuvizuia sana vinywa vyetu. Hasira huwa ndio chimbuko la ugomvi na vita. Hivyo ukiweza kudhibiti hasira zako hata kama utaudhiwa kiasi gani, hujibu, basi upole taratibu utaanza kujengeka ndani yako.

Tatu Kwa kusoma Neno na kuomba: Hii ni tiba kubwa sana, ukitaka ujue hesabu soma kitabu cha hisabati, halikadhalika ukitaka uwe na upole, usikwepe biblia. Kwasababu hiyo ndio itakukumbusha, misingi ya kuwa mpole kama Kristo alivyokuwa. Vilevile kusali, kunaukaribisha uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yako, na hatimaye utafikia kiwango hicho.

Bwana atusaidie sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Furaha ni nini?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

TUMAINI NI NINI?

Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?

Rudi nyumbani

Print this post

DORKASI AITWAYE PAA.

Matendo 9:36 “Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.

37 Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani.

Bwana Yesu asifiwe..

Ulishawahi kujiuliza kulikuwa na umuhimu gani, biblia kueleza tafsiri ya jina la mwanafunzi huyu aliyeitwa Tabitha?. Ukishaona mahali Fulani tafsiri ya jina la mtu inatolewa basi ujue kuna jambo Mungu anataka tujifunze, kwa huyo.

Mfano wa mtu mwingine kama Tabitha alikuwa ni Petro, Ukisoma Yohana 1:42, Bwana Yesu anafunua tafsiri ya jina lake.

Yohana 1:42 “Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).”

Unaona, kulikuwa na sababu ya Bwana kueleza tafsiri ya lile jina kwamba ni Jiwe/mwamba , ikiwa na maana kuwa zipo tabia, ambazo alikuwa  nazo, au atakuja kuzionyesha zinazomwakilisha JIWE KUU mwenyewe ambaye ni Yesu Kristo..

Jambo hilo utalithibitisha mbeleni kidogo, katika Ufunuo alioupata kutoka kwa Mungu, kuhusiana na Bwana wetu Yesu Kristo, tusome;

Mathayo 16:15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”.

Umeona akiwa anamaanisha kuwa juu ya mwamba(yaani Ufunuo alioupata kuhusiana na Yesu ni nani), ndio Bwana Yesu atalijengea kanisa lake hapo. Kwahiyo utaona kutolewa tafsiri ya jina lake tangu kule mwanzoni ni kwasababu ya matendo au funuo alizokuwa anazipata kuhusiana na Yesu Kristo, kama msingi wa Kanisa.

Sasa tukirudi kwa Tabitha naye, tafsiri ya jina lake linatolewa, kwamba ni PAA.

Paa, ni aina ya swala. Mwanzoni nilitafakari sana kwanini aitwe swala, asiitwe labda simba, au au kifaru, au dubu, majina yenye sifa, lakini badala yake anaitwa swala.

Je swala anatabia gani nzuri?

Swala ni mnyama ambaye ni mwepesi sana, miguu yake ipo haraka mno, na ni mwepesi wa kurudia juu, kiasi kwamba akikimbia, katika nyasi ndefu au uwanda tambarare, hata simba hawezi kumkamata, mnyama pekee pirini ambaye anaweza kumkimbiza swala (Paa). Ni duma tu peke yake, tena kumpata kwake ni kwa shida sana.

Hivyo hiyo inamfanya, awe salama muda mwingi, akiwa porini.

Katika biblia mashujaa wa Bwana vitani walifananishwa na Paa, Kwamfano mmoja wa mashujaa wakuu wa Daudi aliyeitwa Asaheli alisifika kuwa mwepesi wa miguu kama swala hawa..

2Samweli 2:18 “Na wana watatu wa Seruya walikuwako huko, Yoabu, na Abishai, na Asaheli; na Asaheli alikuwa mwepesi wa miguu kama kulungu”.

“Kulungu, Paa, na Ayala” ni jamii hiyo hiyo moja ya Swala.

Soma pia,

1Nyakati 12:8 “Na wa Wagadi wakajitenga kumfuata Daudi ngomeni huko nyikani, waume mashujaa, watu waliozoea vita, walioweza kutumia ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kama nyuso za simba, nao walikuwa wepesi kama kulungu juu ya milima;

Soma tena;

2Samweli 22:34 “Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu; Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

35 Ananifundisha mikono yangu vita; Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba”.

Wimbo 8:14 “Ukimbie, mpendwa wangu, Nawe uwe kama paa, au ayala, Juu ya milima ya manukato”.

Sasa mpaka hapo utapata picha ni kwanini Tabitha, aliitwa Paa, ni kwasababu miguu yake ilikuwa ni mepesi katika kutenda matendo mema. Mpaka akasifika katika mji mzima wa Lida, jinsi gani alikuwa tayari kwenda kuwashonea mitume nguo, na kanzu, Pamoja na watakatifu wengine,bila kuombwa wala kuulizwa, Jinsi gani alivyokuwa mwepesi wa kumtolea Mungu. Bila kusukumwa sukumwa, au kukumbushwa kumbushwa, yeye mwenyewe kama swala, alikimbia kutekeleza majukumu yake ya kiutumishi, Zaidi ya watu wote waliokuwa katika ule mji wa Lida.

Hatimaye akafa, lakini watu walimwona kama hastahili kuondoka mapema, watu waliliona pengo  lake lilivyo kubwa, hadi wakati ule Petro, alipokwenda katika mji huo, kulikuwa na maiti nyingi lakini hakuitwa kwa mojawapo ya maiti hizo bali ya Dorkasi tu;

Matendo 9:36 “Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.

37 Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani.

38 Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu.

39 Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao.

40 Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi”.

Hii ni kutufundisha kuwa, ili Mungu awe naye mwepesi kama Swala kutuhudumia, basi na sisi tuonyeshe wepesi wetu kwake. Je sisi nasi ni wepesi wa kutenda matendo mema kama Tabitha? Je tu wepesi kutoa mali zetu na vitu vyetu kwa ajili ya utumishi wa Bwana? Au tu wabinafsi, au mpaka tukumbushwe, au mpaka tulazimishwe, au mpaka tuvutwe vutwe?

Wakati mwingine kwanini, majibu ya maombi yetu yanachelewa?, Ni kwasababu sisi wenyewe sio wepesi kwa Bwana, tunamfanya yeye naye awe mzito.

Tuifanya miguu yetu mepesi, ili wakati wa haja zetu Bwana naye awe mwepesi kutusaidia, kama alivyofanya kwa Dorkasi.

Habakuki 3:19 “YEHOVA, aliye Bwana, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

hMada Nyinginezo:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?

Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?

MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.

USIPUNGUZE KUTUMBUIZA!

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI UPIGE MISHALE CHINI?

Ahimidiwe Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele.Amen

Wakati fulani mfalme wa Israeli aliyeitwa Yehoashi alimfuata Elisha ili kumjulia hali kabla hajafa.

Kama tunavyosoma habari ile  Elisha alimwambia achukue mshale kisha aurushe upande wa mashariki kupitia dirishani. Na alipofanya vile Elisha alimwambia huo ni mshale wa ushindi dhidi ya maadui zake washami..

Hivyo mfalme alipoona vile jinsi alivyopewa maagizo mepesi na yenye uhalisia wa ushindi  kwa tendo la kutupa mishale, hakuwa na shaka yoyote kusikia pengine Elisha atampa maagizo mengine kama hayo, ya kurusha mishale mingine mingi Zaidi ili kuwapiga maadui zake walio karibu naye.

Lakini mambo yalikuwa ni kinyume na mtazamo wake kwani Elisha alimwagiza apige mishale yake ardhini badala ya kuirusha juu, kama alivyofanya hapo kwanza, tendo hilo  likaweka ukakasi kwake “kutupa mishale ardhini”!? pengine alidhani ni mishale inayomrudia yeye.

Tusome..

2 Wafalme 13:14-19

[14]Basi Elisha alikuwa ameshikwa na ugonjwa wake uliomwua; naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatelemka amtazame, akamlilia mbele yake, akasema, Baba yangu! Baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake!

[15]Elisha akamwambia, Twaa uta na mishale; naye akatwaa uta na mishale.

[16]Akamwambia mfalme wa Israeli, Weka mkono wako katika uta; naye akaweka mkono wake juu yake. Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.

[17]Akasema, Lifungue dirisha linaloelekea mashariki; akalifungua. Basi Elisha akasema, Piga; akapiga. Akasema, Mshale wa BWANA wa kushinda, naam, mshale wa kushinda Shamu, kwa maana utawapiga Washami katika Afeki hata utakapowaangamiza.

[18]Akasema, Itwae mishale; akaitwaa. Akamwambia mfalme wa Israeli, Piga chini; akaipiga nchi mara tatu, akaacha.

[19]Yule mtu wa Mungu akamkasirikia, akasema, Ingalikupasa kupiga mara tano au mara sita; ndipo ungaliipiga Shamu hata kuiangamiza; bali sasa utaipiga Shamu mara tatu tu.

Umeona, hakujua kuwa ile ya kupiga chini ndio mishale ya ushindi, kinyume chake akawa na hofu matokeo yake akapiga michache tu (yaani mitatu)..

Ni jambo la kawaida hata leo, Mungu anawaagiza watakatifu wake warushe mishale mingi mahali ambapo ni  kinyume na matarajio yao..lakini mashaka yanawaingia, wanaona kama wanafanyakazi bure, na kupoteza nguvu.

Ndugu yangu vita vya kiroho  ukivitazama kwa jicho la mwilini ni rahisi sana kukata tamaa, kwasababu unaweza ukajiona kama unapoteza tu nguvu zako na muda..kama vile kupiga mishale chini..

Unapokuwa katika maombi, usitazamie kuona badiliko lolote la nje labda  mbingu imekuwa  ya blue, au usikie mapanga yakipigwa na malaika katika anga la kwanza hapana..zaidi sana utaona  ni kama siku nyingine tu ya kawaida, umeomba bure, umeuchosha mwili bure. Lakini katika roho umeangusha ngome nyingi sana za ibilisi, tena na kwa jinsi unavyozidi kudumu zaidi na zaidi katika kuomba ndivyo unavyomfukuza shetani mbali nawe kabisa kabisa .

Hivyo hupaswi kukata tamaa au kuacha kuomba kwasababu hiyo mishale ya ardhini ndio yenye mapigo ya Mungu kuliko ile ya juu.

Unaposhea Neno la Mungu na wengine mtandaoni unaweza usione Matokeo yoyote ya kile unachokifanya, lakini wewe endelea Shea sana kwasababu hiyo ndio mishale ya ushindi unayoidharau wewe.

Unapohubiri mitaani au masokoni, unaweza ukaona kama unawapigia tu watu makelele, au watu hawakusikilizi, lakini hiyo ndio mishale ya ushindi katika vita vyako.

Njia za Mungu sio njia zetu. Wewe utarusha juu, yeye atataka urushe chini..huwezi kumpangia kanuni ya vita.

Hivyo tufanyapo jambo lolote la ki-Mungu tusipime-pime sana au kuchunguza-chunguza sana kwa jicho la nje, kwasababu ukifanya hivyo itakuwa ni rahisi kukata tamaa…bali tufanye kile alichotuagiza kwa bidii kana kwamba tunapoteza nguvu zetu bure, na matokeo yake tutakuja kuyaona baadaye katika ulimwengu wa roho.

Ongeza michale yako ya chini.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

Rudi nyumbani

Print this post

Kigao ni nini? Na Je kinafunua nini kwa agano jipya?

Kigao ni aina ya silaha inayofanana na ngao,

Inachokitofautisha kigao na ngao ni kwamba kigao ni kidogo na chepesi, rahisi kubebeka, na huwa kinafungwa mkononi, lakini ngao huwa ni kubwa na nzito kidogo.

Mara nyingi katika vita vikubwa vya zamani, askari walikuwa wanakwenda vitani na ngao kubwa kwasababu vita vile, vilikuwa ni vya wengi, na mishale, mingi ilirushwa kutoka kila mahali, hivyo  palihitajika kifaa kikubwa kidogo cha kujilinda, hapo ndipo ngao ilibebwa.

Lakini katika hali ya kawaida si kila mahali askari walitembea na ngao kubwa, hivyo walibeba vigao vyepesi na umuhimu wake ulikuwa ni pale, walipojikuta katika vita vya mtu na mtu, vya kurushiana mapanga, hapo kigao kilikutumika, kupangua mapanga na sio ngao, kwasababu  ngao ni nzito, mahususi kwa kuzuia mishale ya mbali, lakini kwa vita vya mtu na mtu ni ngumu, kidogo ilihitaji kifaa chepesi..Ndio hicho kilichojulikana kama kigao.

Tazama picha juu..

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia;

Zaburi 35:1 “Ee Bwana, utete nao wanaoteta nami, Upigane nao wanaopigana nami.

2 Uishike ngao na kigao, Usimame unisaidie”.  

Zaburi 91:3 “Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo.

4 Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao.

5 Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana”,

Soma pia,

1Wafalme 10:17, 2Nyakati 9:16

Je! Kigao kinafunua nini kwa agano jipya?

Sisi kama watakatifu Bwana anatushauri, tuvae silaha zote za haki ili tuweze kuzipinga hila za shetani (Waefeso 6:11). Na moja ya silaha hizo zilizozungumziwa hapo ni Ngao., Ikimaanisha na kigao.

ngao na kigao

Ambayo biblia inasema, ndio IMANI. Hivyo Imani yetu inapaswa isimame katika vita vikubwa, na katika vita vidogo, katika mapambano makubwa na katika mapambano madogo, tushike NGAO NA KIGAO.

Yeremia 46:3 “Tengenezeni kigao na ngao, mkakaribie ili kupigana”.

Mara nyingi tunadhani shetani atatuangusha kwa mamilioni ya majeshi ya mapepo atakayotutumia.. Lakini, anaweza kutumia askari wake mmoja wa giza akatuondolea Imani yetu kwa Bwana kabisa, akaturudisha nyuma.

Hivyo ni kuwa makini, tuwe na Ngao Pamoja na vigao vyetu rohoni. Imani yetu ithibitike kotekote. Kwasababu Imani ni kitu cha msingi sana kukilinda. Na hiyo tumeambiwa tuishindanie kwasababu tumekabidhiwa tu MARA MOJA tukiipoteza basi kuipata tena ni ngumu..

Yuda 1:3 “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu”.

Ndugu kama umeokoka, shikilia wokovu kwa nguvu zote, usirudishwe nyuma na mwanadamu mmoja au majeshi ya maadui. Simama imara na Bwana atakusaidia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

hMada Nyinginezo:

Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi

Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

Tofauti kati ya lijamu na hatamu ni ipi kibiblia?

MJUMBE WA AGANO.

Ufunuo 12 inaelezea vita vya wakati upi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)

​​SWALI: Kulingana na Hesabu 9:11 Je! kuna sikukuu za pasaka mbili kwa mwaka?

Hesabu 9:11 “mwezi wa pili, siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, wataishika; watamla pamoja na mikate isiyotiwa chachu na mboga za uchungu;”


JIBU: Mungu aliwaagiza wana wa Israeli kila tarehe kumi na nne (4) ya mwezi wao wa kwanza, itakuwa ni sikukuu ya pasaka kwao, ambayo wataila kama kumbukumbu la siku ambayo Mungu aliwatoa katika nchi ya Misri katika nyumba ya utumwa.

Hivyo kila inapokaribia tarehe hiyo ya mwezi wa kwanza wayahudi wote walijitakasa na kukusanyika pamoja ili kuila pasaka hiyo..Na ilikuwa ni sheria na lazima.

Lakini tunaona hapo katika kitabu cha Hesabu kuna mwezi mwingine ambao ni wa pili, tarehe kama hiyo hiyo ya 14, wayahudi walikuwa wanakusanyika tena waile pasaka..

Swali ni Je kulikuwa na pasaka nyingine ya pili?

Jibu ni ndio Mungu aliruhusu iwepo pasaka nyingine ndogo.. Na ni kwanini aliruhusu, ni kwasababu kulikuwa na watu ambao kipindi cha sikukuu ya kwanza hawakuweza kufika kwa wakati kutokana na umbali wa safari…na wengine walikuwa wamenajisika kwa kushika maiti, ambayo iliwagharimu muda wa siku saba mpaka wawe safi(Hesabu 19:11)..Na sheria ilikuwa hauruhusiwi kwa namna yoyote kuingia katika kusanyiko lolote la watakatifu mpaka utakapokuwa safi kabisa. 

Kwahiyo kulikuwa na kundi kubwa la watu ambao walishindwa kuila sikukuu hiyo ya pasaka kwa kwasababu hizo zilizoorodheshwa.

Hivyo kwa makundi kama haya ya watu, walipewa nafasi yao ya kipekee na Mungu ili kusudi kwamba sikukuu hii isiwapite kabisa katika mwaka huo.

Tusome..

Hesabu 9:10-12

[10]Nena na wana wa Israeli, kuwaambia, Mtu wa kwenu, au wa vizazi vyenu, ye yote atakayekuwa na unajisi kwa ajili ya maiti, au akiwako mbali katika safari, na haya yote, ataishika Pasaka kwa BWANA;

[11]mwezi wa pili, siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, wataishika; watamla pamoja na mikate isiyotiwa chachu na mboga za uchungu;

[12]wasisaze kitu chake cho chote hata asubuhi, wala wasimvunje mfupa wake; kama hiyo sheria yote ya Pasaka ilivyo ndivyo watakavyoishika.

Hiyo ndio sababu ya kuwepo kwa sikukuu nyingine ndogo ya pasaka..iliyofanyika mwezi mmoja baadaye.

Lakini Je hadi sasa tunayo maagizo kama haya ya kuzishika sikukuu za pasaka?

Katika agano jipya hatusheherekei tena sikukuu za pasaka kwa jinsi ya mwili, bali kwa jinsi ya Roho tukikumbuka kuwa pasaka wetu Yesu Kristo tayari alishachinjwa zamani..

Hivyo wakati wote tupo katika pasaka yake.

Lakini leo hii wengine wanaifananisha siku hii na siku ya Valentino (Valentine’s day)..yaana siku ya wapendanao duniani kama wanavyosema ambayo huwa inaadhimishwa kila tarehe 14 mwezi wa 2 duniani kote..Jambo ambalo halihusiani kabisa na Sikukuu hii ya Bwana. 

Kwanza mwezi wa pili wa kiyahudi sio sawa na mwezi wetu wa pili wa kalenda ya Gregory..

Pili Upendo uliotangazwa na Valentino.Hauhusiani kabisa na Upendo uliotangazwa na Yehova Mungu wetu katika maandiko yake matakatifu.

Hivyo hatupaswi kuyalinganisha mambo ya kimbinguni na sherehe za kidunia. Sisi kama wakristo hatusheherekei Valentine’s day. Ni sikukuu ya kipagani. Tunaisheherekea pasaka ya Bwana kila siku katika Roho.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?

Sikukuu ya kutabaruku ni ipi?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

UNYAKUO.

Rudi nyumbani

Print this post

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu, utukufu na ukuu vina yeye milele na milele amina.

Huu ni mwendelezo wa mafundisho ya wana-ndoa.

Ustawi  bora wa ndoa, hautegemei tu, mume au mke kutimiza wajibu wao wa mwilini,. Hiyo ni sehemu moja wapo, lakini pia ipo nyingine ambayo ni ya muhimu sana, na shetani pia anaifahamu, na kuipiga vita sana, na wewe kama mwanandoa, ukikosa jicho hilo la rohoni kulitambua, yapo mambo mengi sana mazuri utayakosa katika maisha yako ya ndoa.

Kama vile mafanikio ya mtoto  yanavyochangiwa na kuwaheshimu na kuwasikiliza wazazi wake. Vivyo hivyo mafanikio bora ya ndoa yanategemea sana, utii na heshima, na kuwasikiliza wakwe zako. Leo tutaona kibiblia ni kwa namna gani hili jambo lilivyo na nguvu nyingi sana katika ustawi mzuri wa ndoa.

MAMA-MKWE.

Ikiwa wewe ni binti uliyeolewa, fahamu kuwa baraka zako za kimaisha, hazipo tena kwa mama yako mzazi, bali zipo kwa mama-mkwe wako.

Vilevile ikiwa wewe ni kijana uliyeoa, fahamu pia, ubora na ustawi mzuri wa boma lako, hautegemei tena, wazazi wako, bali Baba-mkwe wako.

Ni ngumu kupokea, na ndio hapa, vita vinapokuwepo, lakini ndivyo Mungu alivyopenda iwe.

Ukisoma kitabu cha Ruthu kinaeleza kwa marefu, jinsi mama-mkwe alivyokuwa msingi wa Ruthu kufanikiwa na kupendwa na Mungu, kiasi kwamba hadi leo hii, tunakisoma kitabu hiki, ni kwasababu ya siri aliyoitambua kwa mkwe wake Naomi, utasoma, wakati Ruthu amefiwa na mume wake, hakutaka kuachana na mkwe wake, na kwenda kuolewa tena kwao, lakini alienda naye mpaka nchi ya ugenini, akakubali kuwa kama kijakazi wake, akakubali kuwa kama bibi mjane, japokuwa alikuwa kijana, lakini hakuachana naye hata kwa nukta moja, wakati mke-mwenza Orpa karudi kwao kuolewa, tena yeye hakumwacha mkwe wake Naomi kama tunavyosoma Habari, Lakini mwisho wa siku tunajua ni nini alikutana nacho Ruthu..Badala ya unyonge, ikiwa furaha. Hadi kupewa neema ya uzao wa Bwana Yesu kupitia kwake, angali hakuwa hata mwanamke wa kiyahudi bali wa kimataifa.

Kwa maelezo  marefu juu ya Habari hiyo  fungua link hii, >> https://wingulamashahidi.org/2020/02/19/ewe-mke-heshima-yako-ipo-kwa-wakwe-zako/

Au nitumie msg inbox nikutumie somo lake kwa urefu..

Hiyo ni kuonyesha kuwa mwanamke yeyote uliyeolewa, hatua kubwa za mafanikio yako, ipo kwa mkwe-wako. Shusha kiburi chako, jinyenyekeze, utamwona Bwana, hata kama ni mbaya bado, lipo zuri utalipata tu kwake ambalo ndio litakuwa chanzo cha kupanda juu kwako.

BABA-MKWE

Lakini leo nataka tuone pia baraka zilizo kwa Baba-Mkwe. Na hii hasaa inamuhusu mwanamume. Kamwe usimdharau baba wa mke wako, hata kama atakuwa ni mnyomge kiasi gani, lipo zuri moja tu atakuwa nalo, ambalo huwezi kulipata mahali pengine popote isipokuwa kwake, ambalo litakufaa sana.

Embu mtafakari Musa, alikuwa ni mtu aliyezungumza na Mungu uso kwa uso, akitaka jambo lolote kutoka kwa Mungu alikwenda moja kwa moja kuzungumza naye, Mungu alimpa Musa idadi kubwa ya watu, ili awachunge, lakini katika kuwachunga kule, kulikuwa hakuna utaratibu maalumu, watu walikuwa wanaenda tu, hivyo hivyo,kwa foleni kama vile hospitalini, na wakati wote huo, Mungu hakuwahi kuzungumza na Musa juu ya jambo hilo.

Sio kwamba alikuwa halioni, alikuwa analiona, lakini ni utaratibu wa Mungu, si kila jambo atakuagiza ufanye au atazungumza na wewe moja kwa moja, haijalishi wewe ni nani.. Hata wakati wote Mungu alipokuwa anazungumza na wana wa Israeli, hata siku moja hakuwahi kuwaambia mbona mnaniweka katika mahema yenye giza aliwaacha tu hivyo hivyo,.Lakini utaona miaka mingi sana baadaye Daudi aliligundua hilo, akasema nitamjengea Mungu nyumba. Na Mungu alipoona Daudi kawaza vile akapendezwa naye sana akambariki.(2Samweli 7)

Ndivyo ilivyokuwa kwa Musa, Kusanyiko lote, hakuweza kulimudu, hakuweza kulichunga ipasavyo, lakini Mungu alikuwa anazungumza naye kila siku, lakini  sio kwa Habari hizo. Ndipo siku moja Baba-mkwe wake (yaani baba wa mke wake), alipomtembelea kule jangwani, akaona jambo ambalo, Musa wala Israeli hawakuliona. Tusome;

Kutoka 18:14 “Mkwewe Musa alipoyaona yote aliyowafanyia watu, akasema, Ni jambo gani hili uwatendealo hao watu? Kwani wewe kuketi hapo peke yako, na watu wote kusimama kwako tangu asubuhi hata jioni?

15 Musa akamwambia mkwewe, Ni kwa sababu watu hunijilia mimi wapate kumwuliza Mungu;

16 wakiwa na neno, hunijilia; nami naamua kati ya mtu na mwenziwe, nami nawajuvisha amri za Mungu, na sheria zake.

17 Mkwewe Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema.

18 Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni zito mno kwako; huwezi wewe kulitenda peke yako.

19 Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao;

20 nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya.

21 Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi;

22 nao wawaamue watu hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe; basi kwako wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe.

23 Kwamba utafanya jambo hili, na Mungu akikuagiza hivyo, basi utaweza kusimama wewe, na watu hawa wote nao watakwenda mahali pao kwa amani.

24 Basi Musa akasikiza neno la mkwewe, akayafanya yote aliyokuwa amemwambia.

25 Musa akawachagua watu wenye uwezo katika Israeli yote, akawaweka wawe vichwa juu ya watu, wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi.

26 Nao wakawaamua watu sikuzote; mashauri magumu wakamletea Musa, lakini kila neno dogo wakaliamua wenyewe.

27 Kisha Musa akaagana na mkwewe; naye akaenda zake, mpaka nchi yake mwenyewe”.

Umeona? Alichokifanya Musa, kilileta matokeo makubwa sana kwake na kwa wale aliowachunga. Hata sasa, wewe ni Baba, una familia ndogo au kubwa, usimdharau mkwe wako, kama yupo hai, kaa naye, msikilize kwa makini, hata kama atakuwa mjinga, usione shida kumwomba ushari wa kindoa, lipo moja litakusaidia kwa ustawi bora wa familia yako. Halikadhalika na mwanamke pia, shikamana na mama-mkwe wako.

Hizo ni kanuni za kiroho, zizingatie kwa afya ya maisha yako ya kindoa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

MAFUNDISHO YA NDOA.

NDOA NI NINI?

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kitanga/Vitanga ni nini?

Kibiblia Kitanga ni sehemu ya mwisho wa mkono wa Mtu, au mnyama..kwa jina lingine ni kiganja.

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi.

Danieli 5:24-25
[24]Ndipo kile kitanga cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa.
[25]Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI.

Huu ni ule wakati mfalme Belshaza wa Babeli alipokuwa ameketi nankufanyia anasa vyombo vitakatifu vya Mungu pamoja na makahaba wake..ndipo hapo hapo kiganja cha mkono kikatokea na kuanza kuandika ukutani maneno hayo, mene mene tekeli na peresi.

Utalisoma Neno hilo pia katika vifungu hivi.

Mambo ya Walawi 14:26-27
[26]kisha kuhani atamimina sehemu ya hayo mafuta katika kitanga cha mkono wake mwenyewe wa kushoto;
[27]kisha kuhani atanyunyiza baadhi ya hayo mafuta yaliyo katika mkono wake wa kushoto, kwa kidole chake cha mkono wa kuume mara saba mbele za BWANA;

Mambo ya Walawi 11:27
[27]Tena kila mnyama aendaye kwa vitanga vyake, katika hao wanyama wote waendao kwa miguu minne, hao ni najisi kwenu; awaye yote atakayegusa mizoga yao, atakuwa ni najisi hata jioni.

Isaya 49:16
[16]Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima.

Soma pia; ( 2Wafalme 9:35, Danieli 10:10,

Lakini Je nini tunaweza kujifunza kila tutazamapo kitanga/ vitanga vyetu.?

Ukiwa mwovu..kumbuka kuwa siku moja kitanga cha Mungu kitakuandikia hukumu kama kilivyomwandikia Belshaza mfalme wa Babeli..kama wewe ni mfanyaji wa anasa, ni mzinzi, ni mlevi, ni mchawi, unaabudu sanamu..Bwana atakuadhibu kwa hukumu mbaya sana. Ya mene, mene, tekeli na Peresi.

Ukifikia hii hatua basi habari yako inakuwa imeishia hapo hapo.

Lakini ikiwa wewe unampenda Mungu na kumcha yeye, na kuyafanya maagizo yake..Vilevile ameahidi atakuandika katika vitanga vyake…ikiwa na maana mtu akiandika jambo katika kiganja chake lengo lake ni ili asikusahau, si ndio?..Ndivyo ilivyo kwa Mungu, kwa watu wake wampendao..amewaandika katika viganja vyake kamwe hawezi kuwasahau.

Isaya 49:14-16
[14]Bali Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau.
[15]Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.
[16]Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Walakini ataokolewa kwa uzazi wake.

SWALI: Biblia inaposema mwanamke ataokolewa kwa uzazi wake, inamaanisha nini?

1Timotheo 2:14 “Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.

15 Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi”.


JIBU: Tofauti na inavyotafsiriwa na watu wengi, kwamba andiko hilo linamaanisha kuwa mwanamke yeyote ambaye atakuwa na watoto wa kulea, basi mwisho wa siku ataokolewa kwa kutimiza tu kusudi hilo.  Mtazamo ambao sio sahihi na unakinzana na maandiko, Kwasababu kama kila mwanamke angekuwa anaokolewa kwa namna hiyo, hata wanawake wachawi nao wangeokolewa kwasababu na wao pia wanao watoto wa kulea.

Lakini biblia ilimaanisha nini kuandika hivyo? 

Mtume Paulo aliandika maneno hayo, kuonyesha jinsi gani huduma ya mwanamke ambaye ana watoto jinsi ilivyo na nguvu hata kusababishia wokovu kwake mwenyewe IKIWA atawalea watoto wake katika misingi ya imani, upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi kama ilivyoainishwa hapo..Na sio kwa kuzaa tu basi.

Kwasababu atakuwa ameifanya huduma ya kuokoa kizazi kingine.. Tengeneza picha kama wanawake wote ulimwenguni wangekuwa wanatimiza wajibu wao huu wa kuwalea watoto wao katika misingi ya imani, leo hii, kusingekuwa na haja ya kuhubiri injili kwasababu watoto wote wangekuwa tayari wanamjua Mungu. Lakini injili imekuwa ngumu kwa kizazi cha sasa kwasababu jambo la kwanza mzazi analolithamini kwa mtoto wake ni elimu tu, Mungu ni ziada, mtoto akifaulu darasani ndio furaha yake kubwa, wakati hajui hata mstari mmoja wa biblia. Hajui hata pambio moja la kumsifu Mungu. Mzazi haoni aibu hata mtoto wake anakuwa hadi mtu mzima hajui biblia ina vitabu vingapi.

Kwahiyo hapo mtume Paulo alikuwa anaonyesha nguvu iliyopo katika mwanamke kulea watoto wake vema, ambayo mwisho wa siku itampelekea hata na wokovu wake mwenyewe. Kwamfano Mungu akiona mtoto Yule ambaye alilelewa katika misingi kama Samweli, amekuwa sababu ya wokovu kwa Israeli, unategemea vipi Mungu amwache mama aliyemlea?. Ni sawa tu na yule anayewavuta watu kwa Kristo, ambao biblia inasema kitendo hicho kina nguvu ya kuokoa roho ya mhubiri na kufunika wingi wa dhambi zake.

Yakobo 5:20 “jueni ya kuwa yeye amrejezaye mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na kufunika wingi wa dhambi”.

Kwahiyo ikiwa wewe ni mwanamke na Mungu kakujalia watoto ujue jukumu lako la kwanza, la injili ni kwa watoto wako, hakikisha hao wanakuwa katika misingi ya kumcha Mungu, wafundishe, na pale wanapokosea Mungu kakupa ruhusu ya kuwaadhibu, lengo ni kuwaweka katika mstari wa kumcha Bwana, na sio kuwatesa. Ukifanya hivyo matokeo yake utakuja kuyaona baada ya haya maisha hapa duniani.

Tito 2:4 “ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI UNAJISI UNAVYOMGHARIMU MTU.

Bwana wetu Yesu Kristo atukuzwa. Ni siku nyingine tena tumepewa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha tujifunze Neno la Mungu, maadamu siku yenyewe inakaribia.

Kama vile “Utakatifu na utakaso” vinavyokwenda Pamoja, vivyo hivyo, “Dhambi na Unajisi” ni vitu vinavyokwenda bega kwa bega.

Tofauti na Dhambi na unajisi ni ipi?

Dhambi ni kitendo mtu anachofanya kinyume na Mungu, na huwa inaambatana na kuvunja sheria, au maagizo yake. Kama vile kuzini, kuua, kuabudu sanamu n.k.

Lakini unajisi ni kitendo mtu anachokifanya kinyume na yeye mwenyewe, ambacho mwisho wa siku kinampelekea, Mungu kujitenga naye au kumuacha kwa muda Fulani.

Mtu mwenye dhambi unajisi hauna nguvu kwake bali dhambi tu, ..Lakini mtu aliyeokoka vyote vina madhara kwake, yaani dhambi na unajisi.

Ni sawa na doa jeusi lililopo katika shati, jeupe, doa hilo lingekuwa katika shati jeusi, shati hilo lingeendelea kuvalika kwasababu doa halionekani, lakini likiwa katika shati jeupe hata kama litakuwa safi vipi, doa lile tayari limeshaharibu kila kitu. Sasa huo ndio unajisi. Ambao mtu mchafu, hauna madhara yoyote kwake, lakini kwa msafi ni pigo kubwa.

Sasa kabla kufahamu Zaidi, embu tuangalie kwa agano la kale baadhi ya unajisi ulikuwa katika mambo gani.

Zamani, ilikuwa ukila au ukishika mzoga wa wadudu, au Wanyama ambao ni najisi, adhabu yake ilikuwa na wewe unakuwa najisi, kwa muda wa siku nzima..

Walawi 11:23 “Lakini vyote vitambaavyo vyenye mabawa, vilivyo na miguu minne, ni machukizo kwenu.

24 Nanyi mtakuwa najisi kwa wanyama hao; kila atakayegusa mzoga wao atakuwa ni najisi hata jioni;

Soma pia Walawi 11:29-32

Halikadhalika, kulikuwa na unajisi, wa kujifungua, ikiwa mwanamke atajifungua tu, kile kitendo cha kutokwa damu, tayari ni unajisi ambao  unakugharimu siku saba, Pamoja na hayo, unajisi huo ulimgharimu siku nyingine tena 33, au 66 ikiwa ni mtoto wa kiume.. Kufanya jumla ya siku 40 kwa wa kiume, na siku 80 kwa wakike.

Unajisi huu ulikuwa pia katika kugusa maiti, au kutokwa na uchafu mwilini Soma(Walawi 15:16-20). Ulikuwa unakuwa najisi kwa muda wa siku 7, baada ya kujitakasa.

Sasa nachotaka uone ni kuwa, makosa kama haya aliyafanya mtu juu yake mwenyewe, ambayo hata huwezi kuyaona katika zile amri 10, lakini Mungu aliyatazama sana.

Katika agano la kale, wapo ambao walikuwa wanajitahidi kutotenda dhambi, yaani hawazini, hawaabudu sanamu, hawaibi, wanazitunza sabato n.k.

Lakini walikuwa wanakoseshwa na vitu vidogo tu kama hivyo vya unajisi, Na hivyo vikawa vinatia doa ukamilifu wao. Na matokeo yake, wakawa hawaruhusiwi kuingia hemani kwa Mungu, au katika mkusanyiko wowote wa watakatifu kwa kipindi Fulani, kulingana na aina ya unajisi wenyewe.. kama ni siku moja, au wiki, au miezi..

JE! Katika agano jipya unajisi upoje?

Unajisi wa sasa sio kama ule wa zamani, wa kushika, au kuionja, au kutokwa na vitu mwilini hapana.. Unajisi wa sasa wa mtu upo moyoni, Bwana Yesu alisema hivi;

Mathayo 15:17 “Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?

18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;

20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi”.

Kama tunavyosoma, hapo, yale mambo ambayo yanakutoka moyoni, kama vile tamaa, uzinzi, uasherati, n.k. Sasa kumbuka hasemi kufanya uzinzi, au uasherati, bali kukutoka..yaani mawazo ya uzinzi au ya uasherati, hayo ndiyo yanayokutia wewe unajisi, kama mtakatifu.

Unaweza kweli ukawa huzini na wanawake, lakini kuruhusu tu tamaa ndani yako, tayari umeshajitia unajisi, unaonekana kama vile tayari umezini sawasawa na maneno ya Bwana Yesu (Mathayo 5:28).

Na matokeo yake, inaweza kukuchukua kipindi Fulani kirefu, usiuone uwepo wa Mungu maishani mwako, kwasababu ya unajisi tu kama huo.

Pengine, unawasengenya wengine, unatukana, una chuki na wengine, kiburi, kijicho n.k.(Soma Marko 7:17-23) mambo kama hayo yanaweza kukufanya uikose furaha ya wokovu kwa kipindi kirefu sana, hata baada ya kutubu kwako.

Hivyo unajisi ni wakujiepusha nao sana wewe kama mtakatifu wa Mungu, unaweza ukawa hauuji lakini kitendo tu cha kumchukia ndugu yako, tayari ni sawa na muuji. Umeshajitia unajisi.

Ili uendelee kubaki katika uwepo wa Mungu wakati wowote, uulinde sana moyo wako.

Bwana atusaidie sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

JIEPUSHE NA UNAJISI.

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

SHINA LA UCHUNGU, LISICHIPUKE NDANI YETU.

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Rudi nyumbani

Print this post