Category Archive Home

Kwanini Yeremia ailaani siku yake ya kuzaliwa? (Yeremia 20:14)

Swali: Kwanini Nabii Yeremia ailaani siku aliyozaliwa?, na je ni sahihi kulaani siku tulizozaliwa?


Jibu: Turejee maandiko hayo kuanzia ule mstari wa 14 hadi wa 17..

Yeremia 20:14 “Na ilaaniwe siku niliyozaliwa, isibarikiwe siku ile aliyonizaa mama yangu.

15 Na alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, akisema, Umezaliwa mtoto mwanamume; akimfurahisha.

16 Mtu huyo na awe kama miji ile, ambayo Bwana aliiangamiza, asijute; na asikie kilio asubuhi, na kelele za fujo adhuhuri;

17 kwa sababu hakuniua nilipotoka tumboni, na hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, na mimba yake sikuzote nzito”.

Utaona sababu kuu ya Nabii Yeremia kuzungumza maneno yale ni “mateso aliyokuwa anayapitia katika huduma yake”.. kwani alipitia mapigo na  vifungo vingi na aliwindwa kila mahali kwasababu ya maneno ya Mungu (Soma Yeremia 20:1-2, Yeremia 37:15-16, Yeremia 38:6, Yeremia 15:5)…kama mstari wa 18 unavyoelezea.

“..18 Nalitoka tumboni kwa sababu gani, kuona taabu na huzuni, hata siku zangu ziharibike katika aibu?”

Na si tu Nabii Yeremia aliyeilaani siku yake aliyozaliwa, bali tunaona pia Ayubu naye alisema hayo hayo..

Ayubu 3:1 “Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.

2 Ayubu akajibu, na kusema;

3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.

4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.

5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.

6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi”.

Sasa swali ni je! Walifanya sahihi kuzilaani siku zao?, na sisi je tunapopitia dhiki zilizozidi ni sahihi kuzilaani siku tulizozaliwa na watu waliotuzaa, na matumbo yaliyotuzaa?.

Jibu ni La! Si sahihi kabisa kuzilaani siku tulizozaliwa, wala kulaani matumbo yaliyotuzaa, hata tupitie dhiki kiasi gani?..

Nabii Yeremia na Ayubu walisema maneno yale kwakuwa yalionekana kama ni mambo mapya kwao, kwamba inawezekanaje uwe Nabii uliyetumwa na Mungu, unayesema maneno ya kweli, au inakuwaje uwe mtu wa Mungu, mwelekevu na mkamilifu halafu unakubwa na mambo mazito kama yale?.

Kwahiyo yale yaliyowapata yalikuwa ni mambo mapya kwao, hawakuwa na mifano ya waliowatangulia waliopitia kama hayo katika kiwango hiko, hivyo walisema yale kwa udhaifu wa kibinadamu, lakini hawakuwa sahihi, ndio maana baadaye utaona Ayubu anakuja kutubu, kwa kusema “amesema maneno yazidiyo”

Ayubu 42:3 “Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua.

4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie.

5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona.

6 Kwasababu hiyo NAJICHUKIA NAFSI YANGU, NA KUTUBU Katika mavumbi na majivu”.

Umeona? Hapa Ayubu anakuja kutubia maneno yake, baada ya kumjua Mungu zaidi, na ni hivyo ivyo Yeremia alikuja kuona makosa yake, soma Yeremia 15:18-19.

Na hatuoni tena Ayubu baada ya kuponywa msiba wake wala Yeremia baada ya kustahereshwa wakirudia kusema hayo maneno, hivyo wao walipitishwa katika mapito hayo ili iwe darasa kwetu sisi, kwamba ukiwa mtumishi wa Mungu, au mtu mkamilifu mbele za MUNGU, sio tiketi ya kutopitia majaribu!, LA! Majaribu yanawapata watu wote (wakamilifu na wasio wakamilifu), hivyo hatupaswi kulalamika wala kulaani yanapokuja bali kuomba na kumngoja BWANA.

Na hiyo ndio sababu ya Bwana wetu YESU kuwatahadharisha wanafunzi wake, na hivyo anatutahadharisha hata sasa kwamba tutakapopitia dhiki kwaajili ya Imani tunapaswa tuwe wapole kama hua na wenye busara kama nyoka.

Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.

17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;

18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba si sahihi kuzilaani siku za kuzaliwa au siku nyingine yoyote, wakati wote tunapaswa tuwe watu wenye busara, na watulivu..hakuna faida yoyote katika kunung’unika wala kulalamika.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Laana ya torati maana yake ni nini?

JE NI LAANA KULELEWA NA BABA AU MAMA WA KAMBO?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

NAKUJUA JINA LAKO!

Print this post

Uchimbueni udongo wa mashamba yenu.

Hosea 10:12

[12]Jipandieni katika haki, vuneni kwa fadhili; uchimbueni udongo wa mashamba yenu, kwa maana wakati umewadia wa kumtafuta BWANA, hata atakapokuja na kuwanyeshea haki.

Tunaishi katika majira ambayo kumtafuta Mungu hakupaswi kuwe kwa juu juu tu… kumbuka Neno la Mungu linatufananisha sisi na wakulima wapandao na wenye malengo ya kuvuna kwa vile tuvipandavyo…

Na sikuzote mkulima yoyote labda tuseme yule wa nafaka hatupi mbegu zake tu juu ya ardhi akitarajia ziote, bali utamkuta Na jembe, tena lile imara analikita chini ardhini kwa nguvu, huku jasho likimtoka.

Kimsingi kupiga jembe chini ndio kazi aliyonayo mkulima, haijalishi ardhi itakuwa ngumu kiasi gani hana budi kuichimba kwa nguvu, ili mbegu izame aone matokeo… vinginevyo hatavuna chochote.

Bwana anasema…

Uchimbueni udongo wa mashamba yenu, kwa maana wakati umewadia wa kumtafuta BWANA,

Kumtafuta BWANA…ni kuchimba chini…

Yaani kama ni maombi basi ni Maombi ya masafa marefu sio yale mfano wa kuombea chai ya asubuhi, kama ni kusoma na kujifunza Neno, basi ni kufanya hivyo vya kutosha kila siku sio kuamka na mstari mmoja, au kusubiri Tu kuhubiriwa YouTube halafu basi..

Kama ni ibada, kujifunza Kudumu uweponi mwa Mungu kwa nyakati ndefu…huko ndiko kuchimba chini ambako Bwana anakutaka…

Tusipende mambo ya juu juu, yatatugharimu vibaya sana, na tutajikuta tunapata hasara ya mbegu zetu kuliwa na ndege..

Fahamu kuwa Yesu amekaribia kurudi.. Je umezama Kweli ndani yake? Je unamtafuta kwa bidii, je umejiweka tayari kumpokea? Kama ni hapana basi anza sasa..

Kwasababu mbinguni hakitaingia kinyonge.

Chimba ardhi yako.

Neema ya Bwana akufunike.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.


Print this post

SAUTI YA BWANA I JUU YA MAJI MENGI.

Zaburi 29:3

[3]Sauti ya BWANA i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; BWANA yu juu ya maji mengi.

Ulishawahi kujiuliza kwanini ulimwengu ufunikwe kwanza na maji kote, ndipo Mungu atue juu yake lakini pia aseme Neno?(Mwanzo 1:1-2)

Vipi kama maji yasingekuwepo je Mungu asingesema lolote?….ndio ni kweli Neno la Bwana linasimama mahali popote lakini amejiwekea utaratibu wake wa kuzungumza..si kila eneo sauti yake yenye mamlaka ataiachia..

Palipo na maji sauti yake hutokea…

Ndio maana baadaye mwandishi wa zaburi Kwa uvivio wa Roho anasema…

Zaburi 29:3

[3]Sauti ya BWANA i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; BWANA yu juu ya maji mengi.

Sasa ni lazima tufahamu kwamba Mungu hakai kwenye maziwa, au bahari au mito…hapana bali Mungu hukaa katika moyo wa Mtu..

Lakini moyo wenye maji mengi… na hapo ndipo Sauti yake yenye nguvu kama radi inaposikika…

Hata mawingi ili yatoe radi huhitaji yajawe kwanza na maji, bila hivyo kamwe huwezi sikia sauti yoyote nyuma yake

Biblia inasema…

Yohana 4:13-14

[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Na mahali pengine anasema maji hayo ni Roho Mtakatifu. (Yohana 7:39)

Mtu yeyote anayempa nafasi Roho Mtakatifu, ndani yake, kwa kutii, kwa kuwa mwombaji, mwenye ibada nyingi kumtafuta Mungu, kujitenga na dhambi …Huyo Anaongeza wingi wa maji ndani yake na matokeo yake ni kuwa sauti ya Mungu inasikika, na sio tu kisikika lakini pia inakuwa na nguvu kama ngurumo.

Tukiwa wakame, au tuna maji machache, kinyume chake, ni kuwa hatuwezi kumwona Mungu, wala kuisikia sauti yake. Penda kumtii Roho Mtakatifu. Tafuta kwa bidii kumjua Mungu, ongeza maji yako, Bwana aseme.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kwanini Bwana alipowatuma wanafunzi wake kuhubiri aliwaambia wasihame- hame nyumba watakazo Karibishwa?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu alipowatuma wanafunzi wake kuhubiri aliwaambia wasihame- hame nyumba watakazo Karibishwa?

Luka 10:7

[7]Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.


JIBU: Luka 10, Mathayo 10, Na Marko 6, Kristo inawafundisha mitume wakee nidhamu ya kimisheni. Pale ambapo watu wa Mungu watatoka na kwenda kuhubiri injili kwenye miji, mataifa au nyumba za Watu.

Ukisoma pale utaona Kristo anawapa maagizo kadha wa kadha mfano amri ya kutoa huduma zao bure, anawaagiza wawe wapole kama Hua, na wenye busara kama nyoka, vilevile nyumba watakazokaribishwa kisha chakula kikawekwa mbele yao wale bila kuuliza- uliza…

Lakini agizo lingine lilikuwa ni kutohama-hama nyumba moja kwenda nyingine. Kwamfano wameingia mji fulani halafu ikatokea familia moja ikawaalika kukaa kwao kwa kipindi chote cha huduma, hawapaswi kuhama- hama bali wakae pale mpaka watakapotoka na kwenda mji mwingine ikiwa yule mfadhili hana neno nao. Hata kama wakialikwa nyumba nyingine hawapaswi kuhama- hama..

Swali linakuja kwanini iwe hivyo?

Bwana Yesu alijua kuwa katika ziara mialiko kwa watumishi wa Mungu, huwa ni mingi. Na hivyo ili kuzuia dhamiri mbaya na wengine kuvunjika mioyo, akatoa agizo hilo Kwasababu mfano imetokea mtumishi amealikwa kisha kesho yake akahamia nyumba nyumba nyingine, Yule wa kwanza atajisikiaje? Pengine picha itakayoonekana hapo ni kuwa wanatafuta maisha mazuri, au matajiri wenye hadhi ya kuwatunza..

Lakini wakitulia sehemu moja huleta adabu na kuonyesha tabia ya kuridhika.

Lakini pia Kristo alitaka akili zao zijikite zaidi kwenye huduma.. Kwani kitendo cha kila siku kuhama hapa kwenda kule, hupoteza umakini kihuduma, ni sawasawa na mtu ambaye kila siku anahama nyumba moja ya kupanga kwenda nyingine…unaelewa ni usumbufu gani anaokutana nao.. kuanza tena kuyazoelewa mazingira mapya ni gharama.

Hasa sasa kama watumishi wa Mungu…tunafundishwa utulivu tuwapo ziarani…Mara nyingi ule mlango wa fadhili ambao unafunguliwa wa kwanza, huwa ni wa Mungu…tulia katika huo huo…nyumba ile ya wageni unayoingia ya kwanza…ikiwa amani ya Kristo imekaa ndani yako…tulia hiyo hiyo mpaka utakapomaliza ziara zako…usiwe mtu wa kutafuta makao mazuri, Kwasababu kumbuka upo ziarani… mahali pa muda tu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Anaposema Nisiaibike milele” Ni aibu ipi? (Zab 31:1)

SWALI: Maandiko yanasema “Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele”, Je! ni aibu gani anaomba aepushwe nayo?. Mbona tunapitia kuabishwa, ijapokuwa tumemkimbilia Mungu?


JIBU: Vifungu kadha wa kadha kwenye zaburi vinaeleza, habari hiyo,

Zaburi 31:1 Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye

Zaburi 25:20 Unilinde nafsi yangu na kuniponya, Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe

Soma pia Zaburi 22:5, 71:1

Daudi ni mtu ambaye alizungukwa na maadui pande zote, na hivyo alijua nguvu zake zipo kwa Mungu tu, hivyo akishindwa nao basi itakuwa ni fedheha na aibu kwake, Vilevile ni mtu ambaye aliahidiwa mambo makubwa na Mungu, ikiwemo kudumishiwa kiti chake cha enzi milele, lakini kutokana na mapito na masumbufu mengi aliyokuwa anapitia na kukawia katika ufalme, ilionekana kama jambo hilo haliwezekani..Lakini hakuacha kumwomba Mungu, azitazame ahadi zake asiabike, kwa kumtumaini yeye.

Zaburi 89:49 Bwana, zi wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako?
50 Ee Bwana, ukumbuke, Wanavyosimangwa watumishi wako; Jinsi ninavyostahimili kifuani mwangu Masimango ya watu wengi.
51 Ambayo adui zako wamesimanga, Ee Bwana, Naam, wamezisimanga hatua za masihi wako.
52 Na ahimidiwe Bwana milele. Amina na Amina.

Hapo ndio utaona sasa kwanini sehemu nyingi, kwenye Zaburi Daudi anamwambia Bwana, akumbuke asiabike milele, kwa kuzitumainia fadhili zake..

AGANO JIPYA.

Lakini katika agano jipya pia,

Nasi pia tunamtumaini Mungu ili tusiabike milele.Na Aibu kuu ni ile ya kutengwa na uso wa Mungu milele, ambayo watakutana nayo wenye dhambi, ile aibu ya kufukuzwa mbele ya uso wa Mungu.

2 Petro 3:13 Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.
14 Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa WALA AIBU mbele yake.

Hiyo ndiyo Bwana atatuepusha nayo sisi tuliomtumainia.

Ni vema kufahamu kuwa tukiwa kama watoto wa Mungu, haimaanishi kuwa hatutaaibishwa au kudhalilishwa kwa ajili ya jina lake, vipindi hivyo tutapitia, lakini mwisho wetu utakuwa ni kutukuzwa katika utukufu mkuu milele..

Ni heri leo ukubali aibu ya kidunia, kuliko kukutana na ile ya Kristo wakati ule..

Mathayo 7:23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Mathayo 25:31-34, 41

31 Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;
32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;
33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.
34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu…
41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yuaabisha kichwa chake! Je ni aibu ya namna gani? (1Wakorintho 11:5)

Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

Print this post

Na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii.

Isaya 30:21

[21]na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.

Sisi kama watoto wa Mungu tunaweza kufanya Maamuzi Sahihi katika maisha yetu lakini pia tunaweza kufanya maamuzi yasiyo sahihi katika maisha…tunaweza pita mkono wa kulia lakini pia tukakosea na kupita mkono wa kushoto..

Lakini wengi wetu tunadhani yale maamuzi sahihi tuliyoyafanya ndio kwamba njia tumeiona na yale yasiyo sahihi tumepotea…lakini ukweli ni kuwa kwa Mungu bado tunahitaji maongozo yake sahihi sio tu katika yale mabaya tuliyokosea, lakini pia katika maamuzi mazuri yote tuliyoyachukua bado tunamwita Yeye sana atuonyeshe njia.

Kwasababu kwa Mungu maamuzi sahihi sio kuona mafanikio ya kweli, unaweza kufikia yaliyo sahihi lakini mwisho wake ukapotea.

Mstari huo unasema…

mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto. 

Mtaisikia sauti yangu ikisema njia ni hii..”

Ni ajabu kuona watu wanamlilia Mungu awaonyeshe njia kwenye nyakati za mambo mabaya tu zile za shida, nyakati za majuto, Nyakati za kupata hasara, nyakati za magonjwa, nyakati za kutafuta mwezi wa maisha, nyakati za kunyauka…nyakati za mkono wa kushoto.

Lakini hawana muda wa kumlilia Mungu awaonyeshe njia yake nyakati za mkono wa kuume..yaani za kufanikiwa, za kustawi, za kuinuka, za afya, za amani, za kupandishwa cheo, za kutajirika, nyakati ambazo chakula kipo, makazi yako, elimu ipo, Fedha ipo,

Wakiona mambo yote yapo sawa, wanadhani njia ndio wameshaiona..ndugu yangu humu duniani wapo watu wamefanikiwa sana, wapo watu imara na makini, wana bidii na ufanisi mzuri, ndoa zao zipo thabiti, watu wema, na kwasababu wamechagua njia hiyo basi juhudi zao zimewapa mafanikio sahihi ya ki- Mungu, wanatenda sawasawa wala hawana shida..si watu wajinga..pande zote wapo imara, hata wao wenyewe wanajiona hawakufanya maamuzi mabaya, lakini baadaye wanaishia katika majuto aidha ya kunaswa na mitego mibaya ya ibilisi au majuto baada ya kufa kukosa uzima wa milele..

Kwasababu maamuzi sahihi sio kuona njia sahihi…

Biblia inasema..

Mithali 16:25

[25]Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

Tunamwitaji Mungu ndugu..

Bwana Yesu alitoa mfano huu..

Luka 12:16-21

[16]Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;

[17]akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.

[18]Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.

[19]Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.

[20]Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?

[21]Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.

Ndugu kila siku uamkapo asubuhi anza na siku ya na Bwana, ibilisi ni kama simba angurumaye kutafuta mtu kama wewe akumeze…acha kiburi cha uzima..katika nyendo zako zote mwombe Mungu akuonyeshe njia, na hiyo huja kwa kuwa mwombaji, na kujinyenyekeza sana mbele za Mungu..haijalishi wewe ni mchungaji, nabii, raisi, bilionea au nani…jinyenyekeze Kwa Bwana…kuwa mwombaji uisikie sauti ya Bwana..

Na hakika atakujibu..na kukupa mwongozo wake mwema..

Mungu atakujibu daima aidha Kwa Sauti ya Roho wake Mtakatifu ndani yako, au kupitia Neno lake, au kupitia amani moyoni mwako, katika kila hatua. Kwasababu yupo sikuzote kutusaidia tusipotee.

Isaya 30:21

[21]na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nzi wa Misri, na Nyuki wa Ashuru vilimaanisha nini? (Isaya 7:18-20).

Isaya 40:12 ‘maji kwa konzi ya mkono, na mbingu kwa shubiri’

Huyu Imanueli tunayemsoma katika Isaya ni nani?.

Print this post

KISIMA BADO KINA MAJI, KIFUKUE TENA.

Isaka, alipofika mahali panaitwa Gerari alivikumbuka visima vilivyochimbwa na baba yake Ibrahimu zamani, lakini alipotazama na kuvikuta vimeharibiwa, alianza kazi ya kuvichimba tena, Alipokifukua cha kwanza na kutoa maji maandiko yanatuambia wachungaji wa mahali pale wakakigombania..

Akakiita Eseki, akasogea mbele kodogo akakichimbika Kingine tena nacho kikagombaniwa akikiita Sitna, akasogea tena Mbele akachimba kingine cha tatu..

Hicho hawakukigombania akakiita..Rehobothi

Kisha akasema..Kwa kuwa sasa BWANA ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.

Mwanzo 26:18-22

[18]Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.

[19]Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika.

[20]Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, Maji haya ni yetu. Ndipo akakiita jina la kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.

[21]Wakachimba kisima kingine, wakagombania na hicho tena. Akakiita jina lake Sitna.

[22]Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa BWANA ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.

Sauti ya Mungu nyuma ya habari hii ni nini?

Fahamu ukishaokoka, kuna kisima cha maji ya uzima kinapandwa ndani yako na Yesu Kristo mwenyewe. Kisima hiki licha ya kukupa uzima wa milele..lakini kina kazi ya kukupa raha, kukustawisha na kukufanikisha, maisha yako hapa duniani na mbinguni.

Yohana 7:38

[38]Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

Anasema tena..

Yohana 4:14

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Lakini ni kazi ya adui kukifukia kisima hicho, na hatimaye uwe mkavu kabisa usione raha ya wokovu au matunda yoyote ya imani yako ndani ya Kristo.

Hapo mwanzo ulikuwa ni moto rohoni, ulikuwa unaweza kuomba, kusoma Neno, Bwana alijifunua kwako kwa viwango vya juu..Ukitembea uliuhisi uwepo wa Roho Mtakatifu karibu na wewe…lakini sasa huhisi chochote,huwezi tena kuomba, kushuhudia n.k ukiona hivyo fahamu kuwa kisima kimefukiwa…lakini tumaini ni kuwa maji yapo chini waweza kuanza tena kuchimba na kurudia viwango vyako vya juu hata na zaidi..

Ulirudi nyuma, mpaka ukafikia hatua ya kuyatenda yale machafu ya dunia uliyoyaacha, Ukahisi kama Mungu hawezi kukusamehe tena…ukweli ni kwamba tumaini lipo, anza tu kukichimba kisima chako, maji utayaona.

Ulikuwa na maono mazuri, Na shauku ya kufikia hatma yako, ulikuwa unaona mwendelezo mzuri wa kile ulichokuwa unakifanya hata katika magumu hukutukisika lakini yale maono yamekufa, huelewi ni nini kimetokea, ujue kisima kimefukiwa…anza Upya tena.

Ila ni lazima ukubali kuchukua hatua bila kukata tamaa..Ilimgharimu Isaka visima vitatu lakini hakukata tamaa, hata alipofukua cha kwanza alisumbuliwa, akaendelea tena na tena…alipofikia cha tatu..ambacho ni Rehobothi..basi ikawa ni pumziko lake la daima.

Sisi kama watoto wa Mungu ni Lazima tujue adui ana wivu na hapendi kuona chemchemi za uzima na mafanikio zinabubujika ndani yetu…atafanya juu chini kuhakikisha vinafukiwa na hatimaye kutoona matokeo yoyote ya wokovu kwenye maisha yetu, na wakati huo sio mpango wa Mungu ..ataleta majaribu, misuko-suko, tufani n.k. Lakini ukistahimili Mpaka mwisho utashinda..na hatimaye utakaa mahali pa kudumu pa raha yako kama Isaka..

Ufanye nini?

Anza sasa kujizoesha kwa nguvu kusoma Neno, hata kama mwili hautaki, omba, hudhuria Mikesha acha uvivu, jitenge na dhambi zote. Na hatimaye utaona mwanzo mpya tena wenye nguvu rohoni mpaka mwilini.

Chimba kisima chako

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Uzao wa Ibrahimu unamilikije mlango wa adui? (Mwanzo 22:17)

Je yale Makabila kumi na mawili ya Israeli, kila kabla lilikuwa na kazi gani maalumu?

Huyu “Yeye ashindaye”  Ni mtu mmoja maalumu au wengi?

Print this post

Mwandishi wa kitabu cha wimbo uliobora.

Aliyekiandika kitabu hiki ni Sulemani, mwana wa Daudi. Kufuatana na utambulisho wake mwanzoni kabisa mwa kitabu hichi.

Wimbo 1:1 Wimbo ulio bora, wa Sulemani

Mfalme Sulemani alijaliwa hekima na Mungu kuandika nyimbo nyingi sana Pamoja na Mifano mingi. Kama 1Wafalme 4:32 inavyosema aliandika Nyimbo elfu moja, na tano.

Sasa miongoni mwa hizo nyimbo, basi huu ulikuwa mmojawapo. Na ndio uliokuwa bora kuliko zote. Ndio maana umeitwa wimbo ulio bora.

Ni sawa na kusema Mfalme wa Wafalme, au Patakatifu pa Patakatifu. Ikiwa na maana kuna pazuri  kweli, lakini papo pazuri Zaidi ya kote, au kuna wafalme kweli lakini yupo aliyezidi wote. Ndivyo ilivyo katika vitabu vya Sulemani.

Hichi ndio kitabu ambacho, kimebeba hekima ya juu kuliko zote Sulemani alizojaliwa na Mungu kuziandika. Ni kitabu chenye maudhui ya kimahusiano kati ya mtu na mpenzi wake, ikifunua mahusiano yaliyopo kati yetu sisi na Kristo rohoni.

Kwa Maelezo mapana juu ya uchambuzi wa kitabu hichi bofya hapa >>> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Lakini pia kwa mafunzo mbalimbali yaliyomo ndani ya kitabu hichi, bofya masomo yafuatayo.>>

 Nini maana ya Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, (Wimbo 2:7)

USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO

NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

 

 

Print this post

Kitabu cha Esta kiliandikwa na nani?

Kitabu hicho hakijafunua jina la mwandishi wake moja kwa moja kama baadhi ya vitabu vingine vinavyofunua..Hivyo kwa kuwa hakina uthibitisho wowote wa jina la mwandishi,  miongoni mwa wayahudi na wakristo wengi, kumekuwa Na mitazamo tofauti tofauti juu ya muhusika wa uandishi ule.

Baadhi husema ni mordakai, wengine husema ni Ezra, wengine Nehemia na wengine myahudi fulani ambaye alikuwa na uelewa mzuri wa kihistoria katika dola uajemi wakati ule.

Lakini uzito mkubwa umewekwa kwa Mordekai, kutokana na habari zake kuchukua sehemu kubwa katika kitabu hichi.

Lakini pia maneno Yake mwenyewe kunukuliwa katika kitabu hichi; kuonyesha kuwa yamkini ni yeye ndiye mwandishi wa kitabu hichi.

Esta 9:20-21

[20]Basi Mordekai aliyaandika mambo hayo; naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote waliokaa katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero, waliokuwa karibu na waliokuwa mbali,

[21]kuwaonya wazishike siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, na siku ya kumi na tano yake, mwaka kwa mwaka,

Lakini pia upatikanaji wa taarifa za ndani ya kwenye jumba la kifalme, mfano karamu za kifalme, hukumu zao, sasa taarifa kama hizi ni wazi kuwa hujulikana na watu walio karibu na ikulu za kifalme, mfano wa Mordakai ambaye alikuwa mfungua malango (Esta 2:19,21)

Lakini pia Kuhifadhiwa Kwa kumbukumbu ya sikukuu ya Purimu (Esta 9: 29-32).

Kwani kitabu kinaonyesha kuwa yeye ndiye aliyesambaza habari…hivyo ni sawa kufikiri  pia habari hizo angetaka zihifadhiwe Hata katika vizazi vijavyo vya mbeleni, ambazo ndio hizi mpaka sasa tunazisoma.

Esta 9:29-31

[29]Ndipo malkia Esta, binti Abihaili, pamoja na Mordekai Myahudi, alipoandika kwa mamlaka yote kuithibitisha barua hii ya pili ya Purimu.

[30]Akapeleka barua kwa Wayahudi wote katika majimbo yote mia na ishirini na saba ya ufalme wake Ahasuero, maneno ya amani na kweli,

[31]ili kuzithibitisha siku hizo za Purimu kwa majira yake, kama Mordekai Myahudi na malkia Esta walivyoamuru, na kama walivyojiagizia juu yao wenyewe, na juu ya wazao wao, kwa habari ya kufunga na kilio.

Kwa hitimishi ni kubwa…awe ni Mordekai au mwingine yoyote, Lililo la msingi ni kufahamu agizo la Kristo lililo nyuma ya kitabu hichi.

Hivyo kwa msaada wa uchambuzi wa mafundisho kadha wa kadha yaliyo katika kitabu hichi..basi fungua hapa uweze kujifunza.. >>>

ESTA: Mlango wa 1 & 2

Mabibi wastahiki walikuwa ni watu gani? (Esta 1:18).

Sikukuu ya kutabaruku ni ipi?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?.

Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote” (1Petro 5:10)

Print this post

Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya?

SWALI: Ayubu alipopata yale majaribu, alimwambia mkewe;

Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Swali ni je! Mambo mabaya yanatoka pia kwa Mungu?


JIBU:

Ayubu 2:10

[10]Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.

Ukweli ni kwamba Mungu hatoi mabaya, bali sikuzote hutoa mema…mabaya huwa yanatoka kwa adui..

Isipokuwa katika kuyapokea mema ya Mungu, yapo mapito ambayo (mbele ya macho yetu), tunayaona kuwa ni mabaya lakini kiuhalisia ni njia tu ya kufikia Mema yetu Mungu aliyotuandalia..wala hakuna lolote linaloharibika..

Angalia mwisho wa Ayubu…kumbe Mungu alitaka kumpatia mara dufu, ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzo, na ndio maana ilinpasa vile vya mwanzo viondoke…

Tengeneza picha miaka mingi baadaye labda tuseme miaka 30 baada ya lile pito, akiwa na watoto wake wapya ambao ni mashuhuri wenye hadhi na nguvu za Mungu..Tena Akiwa Mwenye utajiri mwingi na heshima kuliko mwanzoni..bila shaka huwenda alipokumbuka zile nyakati ambazo alikuwa analia na kusema “ilaaniwe siku ile niliyozaliwa” alikuwa anacheka na kusema Mungu Nisamehe nilikuwa sijui nitendalo!

Yakobo 5:11

[11]Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.

Mungu hutujenga katika nyakati zote nyakati za furaha lakini pia nyakati za mateso.Ukishalitambua hili kama mwana wa Mungu hutasumbuliwa na tufani..Bali utamtukuza Mungu katika mazingira yote,, ukijua kuwa kusudi la Mungu linatimia katika mazingira yote…Wala hakuna lolote linalo haribika..

Nyakati tuzionazo mbaya huleta baraka..majeshi ya washami yalipowazunguka Israeli, mwisho wake ulikuwa ni kuziachilia nafaka na mali kwao, Samsoni alipokutana na Simba, kumbe ni asali aliletewa..mwanamke apatapo na utungu hawezi kusema ni mabaya anapitia, kwasababu anajua kuwa hiyo ni njia tu ya kupata kiumbe kipya duniani.

Vitu kama Saburi, unyenyekevu, upole Mungu anavijenga ndani ya watoto wake katika nyakati kama hizi (ambazo sisi tunaziita ni mbaya)…

Hivyo jifunze kuliona kusudi la Mungu katika nyakati zako zote.

Kwa hitimishi ni kuwa Ayubu aliposema ‘Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya?’

Alimaanisha nyakati za huzuni..ambazo zinatimiza kusudi la Mungu….lakini sio mabaya mfano wa mabalaa na vifo, ambayo mwisho wake ni uharibifu. Mungu kamwe haleti uharibifu kwa mtoto wake, hawezi kutupatia samaki  na wakati huo huo kutupatia nyoka.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post