Category Archive Home

Yesu aitwaye Yusto alikuwa ni nani? (Wakolosai 4:11).

Swali: Je huyu Yesu anayetwaja katika Wakolosia 4:11 alikuwa ni nani, na je ni kwanini aitwe hilo jina tukufu?


Jibu: Turejee..

Wakolosai 4:11 “Na YESU AITWAYE YUSTO; hao ni watu wa tohara. Tena hao peke yao ni watendaji wa kazi pamoja nami kwa ajili ya ufalme wa Mungu; nao walikuwa faraja kwangu”.

Katika Biblia Kristo mwokozi wetu hakuwa wa kwanza kuitwa jina YESU, bali walikuwepo watu wengine kadhaa kabla yake walioitwa kwa hilo jina, kwani lilikuwa ni jina linalojulikana Israeli yote,

Na tafsiri ya jina YESU ni  (YEHOVA-MWOKOZI), kama vile ilivyokuwepo YEHOVA-YIRE ambayo tafsiri yake ni YEHOVA mpaji n.k

Kwahiyo YESU ni jina lililokuwepo hapo kabla, kama tu Simeoni aliyeitwa Petro, hakuwa wa kwanza kuitwa Simeoni, au Yuda aliyemsaliti Bwana YESU hakuwa wa kwanza kuitwa Yuda, kwani hata mtoto wa Yakobo,  aliitwa Yuda, na ndio ukoo Bwana YESU aliotokea.

Sasa ni kitu gani kilichomtofuatisha YESU mwokozi wetu na maYesu wengine?.. si kitu kingine bali ni kiunganishi cha mwisho cha jina hilo,.. Aliyetufia anajulikana kama YESU KRISTO,  maana yake YESU MTIWA MAFUTA na MUNGU…

Wengine wanaitwa “Yesu wa Yusto”, wengine “Bar-YESU” (soma Matendo 13:6) lakini ni mmoja tu anaitwa “YESU KRISTO”.. Huyu kwa jina lake hili ndio tunapata ondoleo la dhambi na wokovu (Matendo 4:12).

Na kwa jina la YESU KRISTO, Tunafunguliwa na kuponywa magonjwa yetu, na ziadi sana ndio kwa jina hili tunapaswa tuhubiri na kuhubiriwa ili tupate ukombozi.

Lakini katika hizi siku za mwisho shetani amewanyanyua maYesu wengi wa uongo, ambao na si Yule wa uzima.

2Wakorintho 11:3 “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.

4 MAANA YEYE AJAYE AKIHUBIRI YESU MWINGINE AMBAYE SISI HATUKUMHUBIRI, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!”

Yesu mwingine, (asiye KRISTO) anahubiriwa sasa na manabii na watumishi wa uongo, ambaye yeye hahitaji utakatifu.. ukiona unahubiriwa kwa jina la YESU lakini injili hiyo haikupeleki kuwa msafi mwilini na rohoni, badala yake unazidi kuwa wa kidunia, fikiri mara mbili ni Yesu gani uliyempokea, kwahiyo hatuna budi kujipima.

Lakini tukirudi kwenye swali!, Je huyu Yesu aitwaye Yusto alikuwa ni nani?..

Huyu Yesu aitwaye Yusto, alikuwa ni mmoja wa wafuasi wa Bwana wetu YESU KRISTO, ambaye alishirikiana na akina Paulo (watumishi wa MUNGU) kuhubiri injili, na alikuwa ni Myahudi (ndio maana Biblia inasema hapo alikuwa ni mtu wa tohara, maana yake aliyetahiriwa).

Maana ya jina Yusto ni “mwenye haki”.. na aliitwa “Yesu aitwaye Yusto”, kumtofautisha na YESU KRISTO. Huyu hakusimama kutaka aabudiwe, bali kinyume chake alikuwa anamhubiri YESU KRISTO.

Je umempokea Bwana YESU KRISTO?. Kama bado unasubiri nini?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE BWANA YESU ALIMTOKEA YUDA BAADA YA KUFUFUKA KWAKE?.

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Print this post

Je YESU KRISTO alikuwa na wadogo zake?

Swali: Je YESU alikuwa na dada na kaka (ndugu wa kike na kiume), kama watu wengine?


Jibu: Ndio! Bwana wetu YESU KRISTO alikuwa na ndugu wengine wa kike na kiume, waliozaliwa na Mariamu mamaye!, maandiko yanathibitisha hilo katika Mathayo 13:55-56 na Marko 6:3.

Mathayo 13:54 “Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?

55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? NA NDUGUZE SI YAKOBO, NA YUSUFU, NA SIMONI, NA YUDA?

56 NA MAUMBU YAKE WOTE HAWAPO HAPA PETU? Basi huyu amepata wapi haya yote?”

Kulikuwa na sababu ya kuanza na “Mwana wa seremala (Yusufu) na  kisha Mariamu mamaye na kumaliza na akina Yakobo, Yusufu, Simeoni na Yuda na maumbu (yaani wadada)”.. Ikimaanisha kuwa iliyokuwa inatajwa hapo ni familia, na si ukoo.

Ikimaanisha kuwa Marimu baada ya kumzaa Bwana YESU hakuendelea kuwa Bikira, bali alizaa watoto wengine pamoja na Yusufu mumewe, na watoto hao walikuwa wakike na kiume kama walivyotajwa hapo juu.

Ipo imani kuwa Mariamu hakuendelea kuzaa watoto wengine baada ya kumzaa Bwana YESU na kwamba watoto hao waliotajwa hawakuwa watoto waliozaliwa na Mariamu bali walikuwa ni ndugu wengine kama watoto wa mjomba, au baba mdogo ambao walikuwa karibu sana na Mariamu na Yusufu..

Hoja hii ni dhaifu na haina ukweli, kwani kusingekuwa na sababu ya MUNGU kuruhusu Mariamu achumbiwe na YUSUFU kama hawakuwa na mpango wowote wa kukutana na kuzaa watoto huko mbeleni,.. Malaika angeweza kumtokea Mariamu hata kabla hajachumbiwa, na hilo lingeweza labda kutufanya tuamini kuwa Mariamu aliendelea kuwa bikira mpaka anakufa!.

Lakini kitendo cha mpango wa MUNGU kuingilia kati wakati ambao tayari Mariamu kashachumbiwa, na kuonyesha kuwa hao tayari wamekusudiwa kuwa mume na mke na kuzaa watoto, na hata hivyo kipindi ambacho Yusufu amekusudia kumwacha Mariamu kwasababu ya ujauzito wake, bado kulikuwa na nafasi ya Malaika kumruhusu Yusufu amwache Mariamu, na kumruhusu akaoe mwanamke mwingine, ili Marimu abaki bikira maisha yake yote.

Lakini tunaona Yule Malaika hakumruhusu Yusufu amwache mkewe, ikifunua kuwa Yule ataendelea kuwa mke na ataendelea kutumika kama mwanamke mara baada ya kumzaa Bwana YESU.

Kwahiyo Bwana YESU alikuwa na ndugu wengine na Mariamu hakupaa, wala hakufa bikira, bali alikuwa na watoto wengine, na kati ya hao (yaani Yuda na Yakobo) ndio walioandika vitabu vya Yuda na Yakobo vya agano jipya katika Biblia.

Lakini pamoja na kuwa Bwana YESU alikuwa na ndugu wengine katika mwili, bado alisema kuwa ndugu zake hasa ni wale wayafanyayo mapenzi ya Baba yake.

Luka 8:19 “Wakamwendea mama yake na ndugu zake, wasiweze kumkaribia kwa sababu ya mkutano.

20 Akaletewa habari akiambiwa, Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kuonana nawe. 21 Akawajibu akasema, Mama yangu na ndugu zangu ndio hao walisikiao neno la Mungu na kulifanya”.

Je umempokea YESU?, Je Umefanyika kuwa ndugu yake Bwana kwa kulishika Neno lake na kulifanya?

YESU ANARUDI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni halali kubatiza watoto wadogo?

HUYU SI YULE SEREMALA, MWANA WA MARIAMU?

Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

Ipi tofauti kati ya Sheria na kanuni kibiblia.

Print this post

Je hakukuwa na njia nyingine ya ukombozi zaidi ya kifo cha BWANA YESU?

Kwanini Mungu alichagua njia ya kifo cha msalaba kuwa njia ya ukombozi na si njia nyingine?, kwamba hakukuwa na njia nyingine ya ushindi? Amen.

Jibu: Ni kweli, MUNGU hakushindwa kutumia njia nyingine ya ukombozi wetu tofauti na hiyo ya kifo cha mwanawe wa pekee, kwani yeye ni MUNGU anayeweza mambo yote.

Lakini siri ya kwanini KIFO kitumike kama NJIA ya ukombozi wa dhambi ya mwanadamu ni matokeo ya dhambi za mwanadamu.

Bwana MUNGU alimwambia Adamu kabla ya kuasi kuwa pindi tu atakapokula matunda ya mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya basi atakufa! (Mwanzo 2:17).. Hilo neno ATAKUFA!… Ndilo linalojibu swali letu, kwanini KRISTO afe ili kutukomboa sisi!.

Maandiko yanasema mshahara wa dhambi ni MAUTI! (Warumi 6:23).. Maana yake ili dhambi iweze kulipwa ni lazima MAUTI ihusike.. Kwahiyo KRISTO alipokuja ili aiondoe dhambi ya mwanadamu ilikuwa ni lazima alipe hilo deni!.

Hata mtu aliyepewa mkataba wa kazi, akiukatisha ule mkataba ni sharti alipe gharama za mkataba ule, na vivyo hivyo Kristo ili akatishe mkataba tuliongia sisi na dhambi, ni sharti alipe gharama za dhambi ambayo ni MAUTI.

Kwahiyo alikikubali kifo ili dhambi iondoke kwetu, na hakukuwa na njia nyingine ya mbadala ya kuondoa dhambi!.

Je umempokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha yako?

Kama bado hufajanya hivyo, ni heri ukafanya hivyo sasa, kwa maana hizi ni siku na ule mlango wa rehema unakaribia kufungwa.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

JE UTAKATIFU NI MATENDO YA SHERIA?

Print this post

Nini maana ya Selahamalekothi?

Ilikuwa ni desturi ya wayahudi kuyapa majina, maeneo yote ambayo walikutana na Mungu kipekee.

Kwamfano Yakobo alipokutana na Mungu mahali fulani palipoitwa Luzu, kwa kuona maono yale ya ngazi kushuka kutoka mbinguni, na malaika wanashuka na kukwea, hakuondoka hivi hivi bali alipaita mahali pale Betheli yaani ‘ nyumba ya Mungu’ (Mwanzo 28:10-22).

Sehemu nyingine Mungu alipowasaidia Israeli kuwapiga wafilisti kwa kishindo kikubwa, Samweli alilisimamisha jiwe na kuliita Eneb-ezeri akimaanisha ‘hata sasa Bwana ametusaidia’ na 1Samweli 7:12.

Hivyo pia tukisoma kisa cha Mfalme Sauli na Daudi, tunaona mara nyingi Daudi alipowindwa ili auawe alifanikiwa kumtoroka Sauli, lakini upo wakati ambao alihusuriwa pande zote, Daudi akawa hana namna isipokuwa kungojea tu kuuliwa palepale pangoni, sasa wakati ambapo Sauli amemkaribia sana Daudi. Taarifa za ghafla zilimfikia na kuambiwa kwamba wafilisti wamevamia Israeli, hivyo ikambidi aache kumfuatilia Daudi arudi Israeli kupambana na adui zake.

Sasa tendo hilo la wokovu halikumwacha Daudi awe vilevile kinyume chake, alipaita mahali pale Selahamalekothi

1 Samweli 23:26-28

[26]Sauli akaenda upande huu wa mlima, na Daudi na watu wake wakaenda upande huu wa mlima; naye Daudi akafanya haraka sana kwenda zake kwa hofu ya Sauli; kwa sababu Sauli na watu wake wakamzunguka Daudi na watu wake ili kuwakamata.

[27]Lakini akaja mjumbe kwa Sauli, kusema, Njoo upesi, kwa kuwa Wafilisti wameishambulia nchi.

[28]Basi Sauli akarudi kutoka kumwinda Daudi, akaenda kinyume cha Wafilisti; kwa hiyo wakapaita mahali pale, Selahamalekothi.

Selahamalekothi ni neno la kiebrania lenye maana ya MWAMBA WA KUTOROKEA.

Daudi na watu wake walipaita mahali pale hivyo kufuatana ba jinsi Mungu alivyowaepusha na mkono wa Sauli, kwa njia isiyodhaniwa/ kutegemewa hata kidogo.

Ni kwanini wayaite majina maeneo hayo?

Ni Ili kuendelea kukumbuka matendo makuu Mungu aliyowatendea wasizisahau wafidhili zake kabisa.

Je na sisi ni alama gani tunaacha mahali ambapo tunamwona Mungu ametutendea makuu. PENDA kuandika shuhuda zako, ili wakati ujao zikusaidie kukumbuka fadhili za Mungu umshukuru.

Kikawaida Mungu huwa anatufanyia maajabu mengi Sana kila siku, lakini tunakuwa wepesi kuyasahu, ni vema tujifunze kwa namna yoyote kutunza kumbukumbu, hata kama si kwa kuandika lakini kwa njia zozote zile, mfano wa mababa zetu hawa.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

SIKU YA HOFU YANGU NITAKUTUMAINI WEWE.

Print this post

“Hakuna aniulizaye unakwenda wapi”, maana yake nini? (Yohana 16:5).

Swali: Bwana YESU aliposema kuwa “wala hakuna mmoja wenu aniulizaye unakwenda wapi” alimaanisha nini? (Yohana 16:5)?


Jibu: Turejee..

Yohana 16:5 “Lakini sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, WALA HAKUNA MMOJA WENU ANIULIZAYE, UNAKWENDAPI?

6 Ila kwa sababu nimewaambia hayo HUZUNI IMEJAA MIOYONI MWENU”.

Maneno haya Bwana YESU aliwaambia wanafunzi wake usiku ule mmoja kabla ya kusulibiwa kwake kwamba umefika wakati wa yeye kuondoka na kuwaacha….Na kwasababu ni maneno ya kuhuzunisha, wanafunzi wake waliingiwa na hisia kiasi cha kushindwa hata kumwuliza anakokwenda.

Si kwamba walikuwa hawataki kujua Bwana anakokwenda, La! Walikuwa wanatamani sana…lakini ile hali tu ya kufikiri kumwuliza hivyo haikuwa katika vichwa vyao kwa wakati ule, kwani walikuwa wanatafakari zaidi ni nini kitaendelea kwao baada ya Bwana kuondoka!.. Hivyo hiyo ikazuia hata kufikiri kumwuliza anakokwenda!.

Naam hata taarifa  za mtu kufariki zinapowafikia wafiwa, ni wafiwa wachache sana wanaweza kufikiri Yule mtu ameenda wapi, wengi wanaishia kuhuzunika na kufikiri maisha ya upweke watakayokumbana nayo baada ya hapo kwa kumkosa Yule mtu katika kipindi chote cha maisha yao!.

Ndivyo ilivyokuwa kwa wanafunzi wa YESU, hisia zilifunika tafakari ndani yao, na Kristo aliliona hilo, ndipo akawaambia yale maneno kwamba yafaa yeye aondoke ili msaidizi aje (yaani Roho Mtakatifu), nao watapokea nguvu mpya.

Yohana 16:6 “Ila kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu.

7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.

Na wakati ulipofika wa Roho Mtakatifu kushuka juu yao, wote walipokea nguvu kana kwamba BWANA YESU mwenyewe katika mwili anatembea nao, huzuni na unyonge wote ulipotea na badala yake ujasiri na nguvu viliingia ndani yao.

Je na wewe umempokea Roho Mtakatifu?.. kama bado basi mwamini Bwana YESU, na tubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha kisha tafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, na Bwana atakupa kipawa hiko.

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

KUWA NA  MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.

ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

Print this post

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

Kabla ya Bwana wetu YESU KRISTO, Mkuu wa Uzima, Mfalme mwenye Nguvu, Mwamba Mgumu, na Mkombozi, na Mfalme wa wafalme, kuutoa uhai wake, ili baadaye aurudishe tena (Yohana 10:17), yapo maneno saba (7) aliyasema pale msalabani, ambayo tunayapata katika zote nne (yaani Mathayo, Marko, Luka na Yohana), na maneno hayo ni kama yafuatayo.

  1. BABA UWASAMEHE, KWA KUWA HAWAJUI WATENDALO.

Luka 13:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura”.

Hili ndilo Neno la Kwanza Bwana YESU kulisema akiwa pale msalabani, kuonyesha upendo wa hali ya juu na huruma kwetu, ijapokuwa yeye tayari alishawasamehe, lakini alijua pia umuhimu wa kuwaombea msamaha kwa Baba, kwani si kila msamaha unaoweza kutoa wewe ukawa pia umetolewa na MUNGU, waweza kumsamehe mtu lakini Baba wa mbinguni akawa hajamsamehe huyo mtu bado, hivyo tunajifunza hata sisi kuwaombea wengine msamaha kwa Baba yetu wa mbinguni, kama alivyofanya Bwana wetu YESU KRISTO.

  2. AMIN, NAKUAMBIA LEO UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI.

Luka 13:42 “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.

Hili ni neno la Pili Bwana kuzungumza msalabani, kuonyesha huruma za Bwana YESU hata katika hatua za mwisho kabisa za maisha ya mtu.

    3. MAMA TAZAMA MWANAO, NA KISHA AKAMWAMBIA YULE MWANAFUNZI TAZAMA MAMA YAKO.

Yohana 19:26 “Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao.

27 Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake”.

Hili ni neno la tatu, lenye ujumbe wa kuangaliana sisi kwa sisi, kwani kwa kufanya hivyo tunaitimiza amri ya Kristo la upendo.

    4. MUNGU WANGU, MUNGU WANGU MBONA UMENIACHA?

Mathayo 27:46 “Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”

Hili ni neno la nne, lenye kuonyesha Uzito wa dhambi Bwana wetu alizozibeba kwaajili yetu, zilikuwa ni nyingi kiasi cha kuuzima uwepo wa MUNGU mbele zake pale msalabani.

   5. NAONA KIU.

Yohana 19:28 “Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu”.

Hili ni neno la tano, lenye kuonyesha uzito wa mateso ya Bwana YESU kuwa yalikuwa ni makuu.

   6. IMEKWISHA

Yohana 19:30 “Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake”.

Hili ni neno la sita, lenye kutangaza mwisho wa utumwa wa dhambi.. na kuanza kwa majira mapya, hakuna tena mateso, wala kilio wala uchungu kwake YESU, na kwa wote watakaokuwa ndani yake.

  7. BABA MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU.

Luka 23:46 “Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu”.

Hili ni neno la mwisho, kabla ya kukata roho.

Maneno haya yalifunga kauli ya Bwana duniani na baada ya siku tatu, alitoka kaburini, Mauti ilimwachia, na akaja na ushindi MKUU, Wokovu kwetu, Haleluyaa!…

Je bado upo dhambini?.. bado huoni ni gharama gani aliyoiingia YESU kwaajili yako?.. Tubu leo na kumkaribisha maishani mwako kabla ya nyakati mbaya na hatari zinazoikaribia dunia kufika.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka?

PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA?

Nini tofauti kati ya kileo na divai?

Je kibiblia ni sahihi kuadhimisha jumapili ya mitende?

Ipi tofauti kati ya Sheria na kanuni kibiblia.

 

Print this post

Ni kwanini manabii wa uongo, wanaweza kutoa pepo kwa jina la YESU?

Swali: Inakuwaje manabii wa uongo wanakuwa na uwezo wa kutoa pepo kwa jina la YESU?, na ilihali hawana mahusiano na Mungu wa kweli? je ni nguvu gani wanazitumia? Za Mungu au shetani?.


Jibu: Zipo aina mbili za manabii wa uongo. Aina ya kwanza ni ile inayotumia nguvu za giza asilimia mia moja (100%), kundi hili halihusishi kabisa jina la YESU katika huduma zake, wala halimhubiri YESU wa kweli bali shetani.

Hawa wanakuwa ni wachawi waliovaa suti na kushika biblia, na Neno la MUNGU linasema tutawatambua kwa matunda yao, na si mwonekano wao wa nje.

Kundi la Pili: la manabii wa Uongo, ni wale ambao sio wachawi lakini halina mahusiano na MUNGU, maana yake aidha wanamtumikia MUNGU kwa faida za matumbo yao, au walishamwacha MUNGU na kufuata akili zao, kundi hili ndio hatari zaidi kwasababu bado linaweza kutumia jina la YESU na miujiza ikatendeka.

Mtu anakuwa kashapoteza mahusiano na MUNGU lakini bado upako anao!.. utauliza hilo linawezekanaje?.. Mkumbuke MUSA!.. Bwana MUNGU alimwambia auambie mwamba utoe maji, lakini yeye pamoja na ndugu yake Haruni, hawakumsikiliza MUNGU wakaenda kufanya kinyume na walivyoagizwa, na jambo la ajabu ni kwamba ijapokuwa walikuwa wameenda kinyume na agizo la MUNGU (wapo nje na mpango wa Mungu) lakini walipouchapa mwamba ulitoa maji, binafsi ningetegemea maji yasitoke mwambani kwasababu walikuwa nje na agizo la MUNGU, lakini haikuwa hivyo.

Hesabu 20:6 “Musa na Haruni wakatoka pale palipokuwa mkutano, wakaenda hata mlangoni pa hema ya kukutania, wakaanguka kifudifudi; utukufu wa Bwana ukawatokea.

7 Bwana akasema na Musa, akinena,

8 Twaa ile fimbo, ukawakusanye mkutano, wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba, na hivyo utawanywesha maji mkutano na wanyama wao.

9 Musa akaitwaa hiyo fimbo kutoka mbele za Bwana kama alivyomwamuru.

10 Musa na Haruni wakawakusanya kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, Sikieni sasa, enyi waasi; je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu?

11 Musa akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na wanyama wao pia.

12 Bwana akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa”.

Umeona hapo?.. ijapokuwa Musa alikuwa anatembea nje ya agizo la MUNGU, lakini bado upako alikuwa nao, na manabii wa uongo ni hivyo hivyo, wanaweza kuwa wanatembea na upako wa MUNGU wa kweli lakini hawana MUNGU maishani mwao, na mwisho wao ni mbaya…na hawa tumeambiwa tutawatambua kwa matunda yao na si upako wao, wala mwonekano wao.

Mfano mwingine ni Yule nabii mzee tunayemsoma katika biblia, aliyemwambia uongo nabii mwenzake, na badala nguvu za MUNGU zimwondoke baada ya kusema kwake uongo, kinyume chake ndio kwanza anapokea unabii mwingine kumhusu mwenzie. Soma habari hiyo katika 1Wafalme 12:11-30.

Ikifunua kuwa unabii, au muujiza au upako mtu/mtumishi alionao sio kipimo cha kwanza cha kumtambua nabii/mtumishi wa Mungu wa kweli, bali ni mtu kuwa na mahusiano mazuri na MUNGU, kwani maandiko yanasema Yohana Mbatizaji hakufanya ishara wala muujiza hata mmoja lakini mbinguni alihesabika kuwa  mkuu kuliko manabii wote na watu wote wa agano la kale (Yohana 10:41 na Mathayo 11:11).

Na tena Bwana YESU alisema wengi watakuja siku ile wakisema,  hatukutoa pepo na kufanya unabii kwa jina lako?.. na yeye atasema siwajui mtokako! (Mathayo 7:21-22).

Ili kumtambua kuwa huyu ni Nabii wa kweli na si wa uongo, ni matunda anayoyatoa.. Maana yake Matunda ya maisha yake, na matunda ya kazi yake.

Matunda ya maisha yake ni jinsi anavyoishi, je anazaa matunda ya Roho mtakatifu tunayoyasoma katika Wagalatia 5:22?.. au ni mtu wa namna gani?..kama maisha yake si kulingana na Neno la MUNGU bali ni mtenda dhambi, basi huyo hata kama anauwezo wa kusimamisha jua, bado hatupaswi kudanganyika kwake.

Vile vile kama matunda anayoyazaa kutokana na kazi yake (maana yake watu anao wahubiria) hawawi wasafi mwilini na rohoni, hiyo ni ishara nyingine ya kumtambua nabii huyo kuwa si wa MUNGU. Kwani kama watu anaowatengeneza hawana tofauti na wa ulimwengu, maana yake matunda yake si matunda ya kiMungu bali ya adui.

Hiyo ndio namna pekee ya kuwapima manabii au wachungaji au waalimu au mitume wa kweli na wale wa uongo, na tunapowafahamu biblia imetuonya tujihadhari nao.

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.

20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.

21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)

SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.

SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

MTAWATUPIA MBWA NYAMA HIYO.

Print this post

Tunathibitisha vipi kuwa Yule Malaika wa (Yohana 5:4) ni wa MUNGU?

Swali: Je! tunaweza kuthibitisha vipi kuwa Yule malaika aliyekuwa anashuka na kuyatibua maji alikuwa ni malaika wa MUNGU na si wa shetani, kwasababu maandiko yanasema  kuwa shetani naye anaweza kujigeuza na kuwa mfano wa malaika wa nuru (2Wakorintho 11:14).

JIbu: Turejee..

Yohana 5:1 “Baada ya hayo palikuwa na sikukuu ya Wayahudi; naye Yesu akakwea kwenda Yerusalemu. 2 Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano.

3 Ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala, vipofu, viwete, nao waliopooza, [wakingoja maji yachemke.

4 Kwa maana kuna wakati ambapo MALAIKA HUSHUKA, AKAINGIA KATIKA ILE BIRIKA, AKAYATIBUA MAJI. Basi yeye aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, AKAPONA UGONJWA WOTE ULIOKUWA UMEMPATA.]”

Ni kweli Biblia inasema shetani anaweza kujigeuza na kuwa mfano wa Malaika wa Nuru, lakini haisemi kuwa anaweza kujigeuza na kuwa Malaika wa Nuru, bali mfano wa..

Kwahiyo huyu tunayemsoma hapa katika Yohana 5:4 hakuwa malaika wa giza, kwasababu matunda yake si ya giza kwani Maandiko yanasema “shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake”.

Mathayo 12:25 “Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.

26 Na SHETANI AKIMTOA SHETANI, AMEFITINIKA JUU YA NAFSI YAKE; basi ufalme wake utasimamaje?”

Sasa wote waliokuwa wamelala pale walikuwa wanasumbuliwa na magonjwa yaliyoletwa na mapepo, kwasababu asilimia kubwa ya magonjwa yanasababishwa na mapepo (soma Mathayo 9:32 na Mathayo 12:22).

Sasa kwa mantiki hiyo haiwezekani malaika wa giza kushuka na kuwatoa malaika wenzake wa giza (yaani mapepo) wenzao ndani ya watu, ni jambo ambalo haliwezekani!, vinginevyo ufalme wa giza usingesimama, kwahiyo Yule malaika alikuwa anashuka kuyatibua maji ni malaika wa Nuru na si wa giza.

Jambo la ziada la kujifunza ni kwamba watu wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji kwaajili ya kutatuliwa shida zao au magonjwa yao na baada ya kupiga ramli wanaona kama wamepona..

 Kiuhalisia ni kwamba hawajatatuliwa matatizo yao bali ndio yameongezwa, kwamfano mtu ataenda kwa mganga akiwa na tatizo la homa, na anaaguliwa na kujiona amepona kabisa, na kuambiwa kuwa majini yamefukuzwa ndani yake.

Sasa kiuhalisia kulingana na biblia yale mapepo hayajaondoka!, bali yamehamishwa kutoka sehemu moja ya mwili kwenda nyingine, au kutoka sehemu moja ya maisha kwenda nyingine, lakini si kwamba yamefukuzwa/kuondolewa kabisa kutoka katika maisha yake,

 Maana yake sasa huyu mtu atapata unafuu kwenye kifua kilichokuwa kinamshumbua, au kwenye mguu, lakini lile pepo limehamia kwenye tumbo, au miguu, au limepelekwa kusababisha matatizo mengine katika maisha ya Yule mtu, na tena mtu anayeenda kwa mganga anakuwa anaongezewa mapepo mengine kwa ajili ya matatizo mengine yatakayotokea wakati huo huo au wakati mwingine huko mbeleni, kwasababu shetani kamwe hawezi kumtoa shetani mwenzake.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

BIRIKA LA SILOAMU.

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

JE BADO UNASUBIRIA MAJI YACHEMKE?

AKAWAPONYA WALE WENYE HAJA YA KUPONYWA

WAKO WATATU WASHUHUDIAO MBINGUNI NA DUNIANI.

Print this post

Theofania ni nini?

Theofania ni neno la kiyunani lenye muunganiko wa maneno ya mawili “theos (Mungu)” na “faino (kuonekana)”. Hivyo ukiunganisha linazalika neno “kuonekana kwa Mungu”

Theofania sio kuonekana kwa Mungu katika ule utimilifu wake wote, hapana, kwasababu maandiko yanasema hakuna mtu awezayo kumwona Mungu akaishi (Kutoka 33:20). Hivyo Theofania ni njia mbadala (isiyo ya moja kwa moja) ambayo Mungu  aliitumia kujitokeza na kuongea na watu, kuthibitisha agano lake, au kuwapa maagizo.

Mfano wa njia hizo,

> Ni kijiti cha moto, alichotumia kuzungumza na Musa kule jangwani. (Kutoka 3)

> Mtu Yule aliyeshindana na Yakobo mweleka (Mwanzo 32:24-30)

> Melkizedeki (Mwanzo 14: 18-20)

> Yule mtu wanne aliyewatokea Shedraka, Meshaki na Abednego ndani ya moto (Danieli 3)

> Nguzo ya moto na wingu jangwani (Kutoka 13:21-22)

> Mungu kumtokea Samweli  (1Samweli 3:10)

> Maono ya Ezekieli (Ezekieli 1)

Je! theofania ipo hadi sasa?

Yesu Kristo alipozaliwa katika mwili, sio tena theofania, Bali ni utimilifu wote wa Mungu katika mwili.

Wakolosai 2:9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.

Hapo mwanzo watu hawakumwona Mungu katika utimilifu huo, kwasababu kama wangemwona Mungu wangekufa kwasababu ya dhambi. Lakini Kristo alipokuja kuondoa dhambi kwa damu yake, wanadamu wote tunamwona Mungu katika utilimilifu wote, kwa Roho Mtakatifu aliyemweka ndani yetu.

Tunakikaribia kiti cha rehema, na neema kwa ujasiri bila kufa kama kule mwanzo, kwasababu damu ya Yesu inanguvu ya kuzificha dhambi zetu zote. Ukimwona Kristo(moyoni) umemwona Mungu (Yohana 14:6-11)

Ndio maana ni kwanini leo hii mtu huwezi kumfikia Mungu bila Yesu Kristo.

Okoka leo upokee neema hii, ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Theolojia ni nini?. Na je ni sahihi kuisoma?

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

NINI TUNAJIFUNZA KWA THEOFILO MTUKUFU?

Print this post

Wanethini ni watu gani kwenye biblia?

Wanethini ni kundi la watu ambao walitumika katika hekalu, ambao sio asili ya wayahudi. Wanatajwa sana kwenye kitabu cha Nehemia na Ezra. Maana ya neno ‘Nethini’  kwa kiyahudi linamaanisha “waliotolewa”. Wakimaanisha watu waliotelewa kuwasaidia walawi katika shughuli za hekaluni.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowataja;

Ezra 8:20 na katika Wanethini, ambao Daudi, na wakuu, walikuwa wamewaweka kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini mia mbili na ishirini; wote wametajwa kwa majina yao.

Nehemia 7:73 Hivyo makuhani, na Walawi, na mabawabu, na waimbaji, na baadhi ya watu, na Wanethini, na Israeli wote, wakakaa mijini mwao. Hata ulipowadia mwezi wa saba, wana wa Israeli walikuwa wakikaa katika miji yao.

Soma pia, (Ezra  2:43, 2:58, 7:24)

Asili yao:

Biblia haituonyeshi moja kwa moja asili yao ni wapi, lakini wanazuoni wengi huamini walitokea katika chimbuko la wale wagibeoni waliowadanganya Israeli wakati ule mpaka wakafanya nao maagano, Ambao Yoshua aliwapa kazi ya kupasua kuni, na kuteka maji.

Yoshua 9:27 Siku iyo hiyo Yoshua akawafanya kuwa ni wenye kupasua kuni, na wenye kuteka maji, kwa ajili ya mkutano, na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana, hata siku hii ya leo, katika mahali hapo atakapopachagua

Mbali na hawa wagibeoni wengine wanaweza wakawa ni wageni au mateka., ambao baadaye wakaja kuwekwa kwenye utumishi wa hekaluni.

Kazi yao:

Wanethini hawakufanya kazi zozote za kikuhani, ikumbukwe kuwa ilikuwa ni kosa, mtu ambaye sio myahudi tena wa kabila la Lawi kufanya shughuli zozote za kihekalu, Hawa walikuwa wanafanya kazi za usaidizi ule wa nje, kama vile kutweka maji, kukusanya kuni, usafi, na kazi nyingine zilizohitaji msaada wa pembeni.,Ili kuwaruhusu walawi wasilemewe  wajikite zaidi katika kazi za hekaluni.

Maandiko yanaonyesha walikuwa na makao yao maalumu palipoitwa Ofeli kule Yerusalemu karibu na hekalu (Nehemia 3:26)

Hata Baadaya ya uhamisho wa Babeli, tunaona mabaki yaliyorudi Israeli kufanya shughuli za kihekalu, hawa wanethini pia walirejea

Kwa ufupi wanethini walikuwa ni la watu (wasio-wayahudi) waliowekwa kwa ajili ya kusaidia shughuli za hekaluni.

Kwanini Bwana aruhusu jambo hili?

Licha ya kwamba Mungu ameliita kanisa lake na amelitenga, limtumikie lenyewe katika shughuli zote za kimadhabahu. Lakini Bado Bwana anaweza kunyanyua watu wengine nje ya kanisa, kusaidia kanisa kusonga mbele. Mfano wa hawa ni Yule akida wa kirumi ambaye alilipenda taifa la Israeli na  kulijengea sinagogi (Luka 7:1-5). Hakuwa myahudi lakini aliwasaidia wayahudi.

Hata sasa wanethini wapo wengi, hawapaswi kuzuiliwa, endapo wanasaidia kanisa au kazi ya Mungu, kwasababu ni Bwana ndiye aliyewavuta.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post