Title November 2020

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

Kuna pepo moja lililowasumbua sana mitume wa Yesu, hilo halikuwa sawa na pepo mengine waliyokutana nayo, walihangaika nalo mchana kutwa lakini hawakufua dafu mpaka alipokuja Bwana Yesu mwenyewe kulikemea na kulitoa.

Lakini leo hatutazungumzia juu ya pepo hilo kwasababu habari yenyewe tunaijua, ila katika habari hiyo lipo jambo ambalo ni vizuri sisi tukajifunza, husasani kwa wazazi au walezi, wanaoishi na watoto wadogo. embu tusome tena alichokifanya Yesu kisha, tuende kwenye ujumbe wenyewe..

Marko 9:20 “Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa, akitokwa na povu.

21 Akamwuliza babaye, AMEPATWA NA HAYA TANGU LINI? Akasema, TANGU UTOTO.

22 Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia”.

Sasa katika habari hiyo, usidhani Yesu alikuwa hajui matatizo ya huyo mtoto ndio maana akamwuliza vile, Kumbuka Yesu alikuwa anajua kila kitu wala alikuwa hana haja ya mtu kumuadhithia chochote, biblia inatuambia hivyo katika  Yohana 16:30, Lakini  aliuliza vile kwa lengo la kutaka watu wote wajue matatizo ya Yule mtoto yalianzia wapi, na ndio maana akamuuliza vile yule mzazi “Amepatwa na haya tangu lini?”.

Ndipo yule mzee akamjibu na kusema,  “amepatwa na haya tangu utotoni”. Ulishawahi  kuutafakari vizuri huu mstari, tangu utotoni? ..Hiyo ni kutuonyesha kuwa kuna mapepo ambayo, agenda yao kuu, ni watoto. Kwasababu yanajua yakianzia katika msingi, baadaye yatakuwa ni magumu kutoka.

Inashangaza leo hii kuona wazazi hawajali maisha ya kiroho ya watoto wao, wanaona kama wao ni watoto tu, shetani hawezi kuwashambulia, hawajui kuwa wanapaswa kulindwa kwasababu shetani huwa hatambui cha mtoto au cha mzee, lengo lake ni kuharibu. Kama alimuingia Nyoka ambaye ni mnyama tu, ataachaje kumwingine mtoto ambaye ni mwanadamu? ndio target yake kubwa?

Mzazi, anamruhusu mtoto wako mdogo atezame tv masaa 24 wakati wote hata zile programu ambazo haziendani na umri wake anamwacha azitazame, anamwacha asikilize miziki ya kidunia, tena Zaidi ya yote unafurahi anapocheza,  lakini nyimbo za tenzi hata moja haujui, Mzazi mwingine hata hampeleki mtoto wake Sunday school ili afundishwe njia ya kikristo angali akiwa mdogo, yeye anachojua ni kumnunulia mtoto wake nguo nzuri tu, kumtafutia nursery nzuri ya kusoma, anajali vya mwilini vya mwanawe anapuuzia na vile vya rohoni. Hata kumwombea mtoto wake anashindwa.

Nachotaka nikuambie ni kuwa tusipowawekea msingi mzuri watoto wetu, shetani atatusaidia kuwawekea wake, kama alivyofanya kwa mtoto wa huyu mzee tunayesoma habari zake.  Lile pepo lina haki ya kuwa gumu kutoka kwasababu tayari lilikuwa na msingi tangu utotoni. Na ukiangalia lengo la hilo pepo si lingine zaidi ya kumwangamiza tu, mara litake kumtupa kwenye maji, kwa bahati nzuri pengine watu wanamuona wanamuokoa, mara litake kumtupa kwenye moto, lakini Mungu anafungua rehema zake anaepukika.

Leo hii utaona kumenyanyuka kundi kubwa la watoto ambao wanaonyesha tabia ambazo hazieleweki chanzo chake ni nini, na wewe unaweza ukadhani ni yeye anafanya kumbe ni pepo ambalo tayari lilishamvaa tangu utotoni ndio linaonyesha tabia hizo ndani yake.

Wazazi ndio wanapaswa waanze kubadilika, ndio watoto wabadilike.  Wewe kama mzazi, kama hutaonyesha kujali maisha ya kiroho ya mtoto wako, usidhani mtoto atabadilika mwenyewe au atakuwa na tabia njema huko mbeleni.

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”

SASA UTAYAZUIAJE MAPEPO YA UHARIBIFU KAMA HAYO YASIMWINGIE MWANAO?

Kwanza ni kwa kutumia kiboko: Biblia inasema hivyo, …Pale unapoona kuna tabia Fulani ambayo sio nzuri, mfano kiburi, anatukana, hana nidhamu, hapo hapo hupaswi kuiacha hiyo tabia imee, mpaka hilo pepo liumbike ndani yake.. Utalitoa hilo kwa kiboko.

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

Pili Ni  kwa kumfundisha kanuni za imani: Unamfundisha biblia, unamfundisha nyimbo za kikristo, unamfundisha kusali, unamfundisha hata kukariri  vifungu vya biblia, hata kama hataelewa sasahivi lakini vitabaki moyoni mwake kama hazina itakayokuja kumsaidia baadaye. Na  hakikisha pia unampelekea kwenye mafundisho ya watoto kanisani.

Tatu  Unamwombea; Mara kwa mara unahakikisha unamfunika mwanao, kwa damu ya Yesu Kristo, unatenga muda mrefu wa kumuombea.

Na Nne unamzuia kufanya/kutazama mambo ambayo hayapasi: Si lazima kila unachokitazama wewe, mtoto naye akitazame, magemu anayoyacheza mtoto si yote yanamaudhui mazuri, vilevile nguo unazomvisha mtoto si zote ni njema. Hivyo jifunze kumchagulia mtoto vinavyomfaa.

Ukizingatia hayo, basi mapepo kama hayo ambayo ni hatari na sugu, hayatamkuta mwanao. Kumbuka biblia inasema shetani ni kama simba angurumaye, akitafuta mtu ammeze, hivyo usipuuzie haya maagizo, mjenge mwanao, mjenge mdogo wako, mjenge mtoto yoyote auishiye naye.

Na Bwana atakubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI LAZIMA KUBADILISHA JINA BAADA YA KUOKOKA?

Jina la Bwana wetu Yesu, libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Katika biblia Mungu hakuwabadilisha watu majina kutokana na tafsiri za hayo majina. Ni muhimu kufahamu sana hili, vinginevyo shetani anaweza kukutesa na tafsiri ya jina lako. Kwasababu usipomwelewa Mungu jinsi anavyotenda kazi, utachukuliwa na kila aina ya upepo wa elimu, na mafundisho ya mashetani, ambayo kazi ya hizo elimu ni kuwafunga watu wala sio kuwafungua, Kuwatwisha watu mizigo mizito na wala si kuwatua.

Yohana 8:36 “Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”

Sasa hebu tuangalie watu wachache waliobadilishwa majina katika biblia, na tafsiri za majina yao kabla na baada ya kubadilishwa, ndipo tutajua tabia ya Mungu.

  1. Ibrahimu

Huyu mara ya kwanza alikuwa anaitwa “Abramu”. Tafsiri ya jina Abramu ni “Baba aliyeinuliwa” na Ibrahimu tafsiri yake ni “Baba wa mataifa mengi”.

Sasa kulingana na tafsiri hizo, sio kwamba Mungu aliona tafsiri ya jina lake la kwanza ilikuwa ni mbaya, na hivyo akataka kumpa jina jipya lenye tafsiri zuri, hapana!..ilikuwa ni nzuri tu… kuitwa “Baba aliyeinuliwa” sio jina baya, lakini ilipofika wakati wa Mungu kumpa agano kwamba atakuwa Baba wa mataifa mengi, ndipo jina lake likabadilishwa na kuwa Ibrahimu. (Hivyo lilibadilishwa kwasababu ya huduma iliyopo mbele yake).

  1. Sara

Huyu alikuwa ni mke wa Ibrahimu, ambaye hapo kwanza alikuwa anaitwa “Sarai” maana yake ni “binti wa mfalme” lakini jina lake lilibadilishwa na kuwa “Sara” ambalo maana yake ni “mama wa wana wa wafalme”. Hivyo halikubadilishwa kwasababu lilikuwa na maana mbaya, bali kwasababu ya Ahadi ya Mungu, ya mumewe Ibrahimu kuwa Baba wa mataifa mengi, hivyo hana budi na yeye kuwa mama wa mataifa na wafalme wengi,  Ni sawa wewe ubadilike sasa kutoka kuitwa mtoto, na kuitwa Baba wa watoto wengi…au kutoka kuitwa binti mpaka kuitwa mama wa mabinti wengi..(Ni kutokana na kubadilika majukumu, umetoka kwenye utoto sasa umeingia kuwa mama/baba)

  1. Yakobo

Mtu wa tatu ni Yakobo, mwana wa Isaka, jina lake lilibadilishwa kutoka kuitwa Yakobo hadi kuitwa Israeli.. Tafisiri ya jina “Yakobo” ni “mshika kisigino”..Jina hilo aliitwa kutokana na jinsi alivyozaliwa, kwani alipozaliwa alizaliwa huku kamshika ndugu yake kisigino.(Mwanzo 25:26)..na Tafsiri ya jina Israeli ni “Kushindana na Mungu”. Sasa Yakobo jina hilo halikubadilishwa kutokana na tafsiri yake ni mbaya..Hapana bali ni kutoka na ahadi mpya Mungu aliyokwenda kumpa baada ya kushindana na yule malaika na kumshinda..Kwasababu kama tafisiri ya Jina Yakobo lingekuwa ndio sababu ya Mungu kumbadilisha jina, basi Mtume wa Yesu aliyeitwa Yakobo, angepaswa naye pia abadilishwe jina. Na aliyeandika kitabu cha Yakobo, naye pia angepaswa abadilishwe.. Lakini tunaona hawajabadilishwa, lakini bado waliendelea kuwa Mitume wa Yesu, waaminifu mpaka mwisho.

  1. Petro

Petro hapo kwanza alikuwa anaitwa Simoni.. Yohana 1:42  “Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe)”.  Sasa tafsiri ya jina Simoni ni “Amesikia”.. Na tafisiri ya Kefa/Pertro ni “jiwe dogo la kurusha” na sio “mwamba”. Hivyo kwa hali ya kawaida, Simoni ndio lenye tafsiri bora kuliko Petro..

Sasa utaona Bwana Yesu hakumbadilisha jina Simoni kwasababu lina maana mbaya, hapana bali ni kwasababu ya huduma yake inayokwenda kuanza, kwamba Bwana atamtumia kama jiwe lake, kwa kazi yake. Sasa jina “Simoni” lingekuwa na tafsiri mbaya inayomchukiza Mungu au yenye madhara kiroho kwa Petro, basi angembadilisha pia mtume wake mwingine miongoni mwa wale 12, ambaye naye pia alikuwa anaitwa Simoni mkananayo (Mathayo 10:4). Kwasababu Bwana asingeweza kumbadilisha mtume mmoja na kumwacha mwingine mwenye jina kama hilo hilo. (Kwahiyo Petro naye alibadilishwa kutokana na huduma iliyopo mbele yake)

  1. Sauli

Na wa mwisho tunayeweza kumwona ni Mtume Paulo ambaye hapo kwanza alikuwa anaitwa “Sauli” ambapo tafsiri ya jina hilo ni “Ombea” (mf. Kuombea kitu fulani kwa Mungu), hiyo ndiyo tafisiri ya jina Sauli, lakini jina hilo lilikuja kubadilishwa na kuwa “Paulo” ambalo maana yake ni “Mdogo”.

Hivyo unaona hapo, jina lake halikubadilishwa kwasababu lilikuwa na tafsiri mbaya, hata wewe katika hali ya kawaida ungeambiwa uchague uitwe jina lenye tafsiri ya “mdogo” au uitwe jina lenye tafsiri ya “Ombea”..Bila shaka ungechagua lenye tafsiri ya “ombea”. Lakini Mungu alimbadilisha Sauli na kumpa hilo lenye tafisiri ya mdogo.

Na kwanini Mungu alimpa jina hilo Paulo?. Ni kwasababu ya huduma yake, ambayo anakwenda kuifanya hapo mbeleni (ambayo itampasa awe mdogo sana na mnyenyekevu).

Waefeso 3:7  “Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake.

8  MIMI, NILIYE MDOGO KULIKO YEYE ALIYE MDOGO WA WATAKATİFU WOTE, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa utajiri wake Kristo usiopimika;

9  na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote”.

 Kwahiyo jambo kubwa la kujifunza ni kwamba… tafsiri za majina yetu, hazina maana sana mbele za Mungu wetu. Ndio ni vizuri kuwa na jina lenye tafsiri nzuri, lakini hilo halikusogezi mbele za Mungu. Kwasababu majina yaliyoandikwa kwenye kitabu cha uzima, hayajaandikwa kulingana na maana za majina hayo, bali kulingana na matendo ya mtu.

Watakuwepo wengi mbinguni ambao majina yao hayana tafsiri nzuri, na vile vile watakuwepo wengi kuzimu wenye majina mazuri, watakuwepo wakina Ibrahimu wengi kuzimu, watakuwepo wakina Paulo wengi kuzimu, watakuwepo wakina Petro wengi kuzimu, na watakuwepo wakina Yohana wengi kuzimu. Vile vile watakuwepo wakina Sauli wengi mbinguni, watakuwepo wakina Yakobo wengi mbinguni, watakuwepo wakina matatizo wengi mbinguni, watakuwepo wakina Majuto wengi mbinguni, watakuwepo wakina masumbuko wengi n.k

Kwahiyo baada ya kuokoka, Tafsiri ya jina lako isikusumbue sana. Kama umependa kulibadilisha kwa mapenzi yako mwenyewe (kwamba hupendwi kuitwa hilo jina katikati ya jamii yako)ni sawa hutendi dhambi, na Kama Bwana amekuongoza kubadilisha jina lako pia ni sawa fanya hivyo!!, lakini kama Bwana hajakuongoza wala usiwe na hofu,  wala usitishwe na elimu zilizozagaa kwamba utapata mikosi kwa jina hilo, au jina hilo ni kikwazo kwako na mafanikio yako.

Kuwa tu kama Simoni Mkananayo mwanafunzi wa Yesu, ambaye jina lake lilibakia kuwa lile lile, lakini bado aliendelea kuwa mwanafunzi wa Yesu..ijapokuwa mwenzake alibadilishwa na kuwa Petro, yeye aliendelea kuwa vile vile Simoni. Kwasababu Mungu hatembei na wewe kwasababu ya tafsiri bora ya jina lako, bali kwasababu ya uaminifu wako kwake katika kuyafanya mapenzi yake. Kama vile asivyobagua rangi, vivyo hivyo habagui watu kutokana na tafsiri za majina yao.

Katika Biblia kuna mtu anaitwa Tabitha au Dorkasi, tafisiri ya jina hilo ni “Paa” kasome Matendo 9:36, sasa “paa” kwa lugha inayoeleweka ni “mnyama Swala”..Lakini pamoja na jina lake hilo lenye tafisiri isiyo na maana, tunasoma Tabitha alimpendeza Mungu sana..

Matendo 9:36 “ Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa”.

Kadhalika katika biblia kuna mtu aliyeitwa Yabesi (1Nyakati 4:9-10), huyu alipewa jina lenye tafsiri mbaya ya HUZUNI, lakini alimpendeza Mungu sana.(Kwa habari zake ndefu unaweza kututumia ujumbe inbox). Na ipo mifano mingine mingi kwenye biblia ambayo hatuwezi kuitaja hapa yote. Lakini kwa hiyo michache itoshe tu kusema kwamba, Kama ulikuwa na hofu na tafsiri ya jina lako, badilisha mtazamo sasa..Anza kuwa na hofu na mwenendo wa maisha yako katika hatima ya maisha yako, zaidi ya tafisir ya jina lako.

Ufunuo 20:12  “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, SAWASAWA NA MATENDO YAO”.

Hivyo utazame mwenendo wako, je umesimama katika Imani sawasawa?..Je matendo yako yanampendeza Mungu?..kama bado basi rekebisha leo kabla hujafikia mwisho wa siku zako za kuishi hapa duniani.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

CHAKULA CHA ROHONI.

CHAKULA CHA ROHONI.

TUMEPEWA MAMLAKA YA KUKANYAGA NG’E NA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

SWALI: Bwana Yesu apewe sifa Ukisomo kitabu cha 2 WAFALME 2:24 napenda kuelewa mbona pale wanatokea dubu wawili wa kike mwituni na sio wa kiume?

2Wafalme 2:24 “Akatazama nyuma akawaona, akawalaani kwa jina la Bwana. Wakatoka dubu wawili wa kike mwituni, wakawararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao”.


JIBU: Tofauti na sisi wanadamu, kwa upande wa wanyama, asilimia kubwa ya wanyama wenye asili ya kike (majike) huwa  wanakuwa ndio wakali zaidi, na washapu kuliko wa jinsia ya kiume. Utaona kwa simba, Dubu na kadhalika. Majike ndio wawindaji n.k.

Ukisoma Mithali 17:12 inasema;

“Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake, Kuliko na mpumbavu katika upumbavu wake”.

Hapo imetumia mfano wa dubu mke, na sio dume, hii ni kuonyesha kuwa hao ndio wakali zaidi hususani pale wanapokuwa na watoto.

Utasoma tena sehemu nyingine Mungu alijifananisha na dubu mke, kwa hasira yake atayaoichia juu ya Israeli kwasababu ya makosa yaliyofanya kinyume chake. Akaifananisha hasira yake na hasira ya dubu jike.

Hosea 13:7 “Basi nimekuwa kama simba kwao; kama chui nitavizia njiani;

8 nitakutana nao kama dubu aliyenyang’anywa watoto wake; nami nitararua nyama ya mioyo yao; na huko nitawala kama simba; huyo mnyama mkali atawararua.

9 Haya ndiyo maangamizo yako, Ee Israeli, ya kuwa wewe u kinyume changu mimi, kinyume cha msaada wako”.

Ni nini tunajifunza? Kwanini walitumiwa dubu wa kike na sio wa kiume?

Hiyo ni kuonyesha uwezo wa jamii ya kike , kuwa wanawake, wanaweza kuwa vyombo viteule vya kumponda ibilisi kwa Bwana, ikiwa tu watasimama katika nafasi zao katika wokovu. Wanawake waliosimama ibilisi anawaogopa sana, kwasababu anajua  madhara yatakayoyasababisha katika ufalme wake.

Hivyo ikiwa wewe ni mwanamke unapaswa usimama sasa, uwe na ushujaa kama wa dubu jike, rarua, angamiza, teketeza  kazi zote za shetani bila kuona huruma yoyote, kwasababu uwezo huo unao ndani yako.

Zaburi 68:11 “Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;”

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

KIAMA KINATISHA.

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

TUMEPEWA MAMLAKA YA KUKANYAGA NG’E NA NYOKA.

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

GOGU NA MAGOGU, Katika biblia ni nani?

Neno Gogu na Magogu limeonekana sehemu mbili katika biblia, Sehemu ya kwanza ni katika kitabu cha Ezekieli 38:2, na katika Ufunuo 20:8.

Sasa ni vizuri kujua kwanza Magogu ni nini, ndipo tuje kwa Gogu.

Magogu sio wingi wa Gogu.. hapana!.. bali ni jina la mtu mmoja, ambalo tunalipata katika kitabu cha Mwanzo 10:2.

Mwanzo 10: 1 “Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuhu, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika.

2 Wana wa Yafethi ni Gomeri, na MAGOGU, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi.

Hivyo “Magogu” alikuwa ni Mjukuu wa Nuhu, alikuwa ni Mtu. Sasa mtu huyu biblia haijaeleza alikuwa ni mtu mwenye sifa gani, lakini kutokana na uwepo wake katika sehemu nyingine za biblia, inaonekana wazao wake walikuja kuwa watu Hodari kipindi hicho, na mwenye uwezo mkubwa sana wa kijeshi, na kiuchumi, mfano wa Nimrodi aliyeujenga Babeli.

Na Magogu naye ni hivyo hivyo, uzao wake ulikuja kuwa Hodari..na kuwa Taifa lenye nguvu kijeshi, na watu hao wote kwa ujumla wakaitwa Magogu kufuatia jina la baba yao huyo.

Kama vile mji wa Moabu ulivyoitwa kufuatia jina la baba yao aliyeitwa Moabu. (Mwanzo 19:37 “Yule mkubwa akazaa mwana, akamwita jina lake Moabu; huyo ndiye baba wa Wamoabi, hata leo”)

Na Magogu ni hivyo hivyo, Uzao wake ulikuja kuitwa kwa jina hilo la Magogu, na nchi yao ikaitwa nchi ya Magogu, kufuatia jina la baba yao huyo aliyeitwa Magogu.

Tunalisoma hilo vizuri katika Ezekieli..

Ezekieli 38:1 “Neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, kaza uso wako, umwelekee GOGU, wa NCHI YA MAGOGU, mkuu wa Roshi, Mesheki, na Tubali, ukatabiri juu yake”,

Na nchi hiyo lilikuwa upande wa kaskazini mwa Asia na Ulaya, ambayo sasahivi ni Maeneo ya nchi ya Urusi.  Hatima ya hilo Taifa la Magogu, biblia haijaieleza, lakini ni wazi kuwa lilikuja kupotea kama yalivyopotea mataifa mengine yaliyokuwa hodari kama Babeli.

Sasa baada  ya kujua hilo, twende kipengele cha pili, cha GOGU. Kama tulivyotangulia kusema Magogu sio wingi wa Gogu. Bali Gogu ni kiongozi wa Taifa la Magogu. Yaani mfalme wa taifa la Magogu. Kwahiyo tunaposoma, neno Gogu na Magogu, Ni sawa na kusema Farao na Misri, au Sulemani na Israeli.

Ndio maana tunasoma hapo katika Ezekieli 38:3… “useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe GOGU, mkuu wa Roshi, na Mesheki, na Tubali;”

Umeona hapo mstari wa 2, unasema Gogu mkuu wa…. Neno “mkuu wa” linaashiria ni kiongozi, hivyo Gogu ni jina la kiuongozi kama vile Farao, au Sultani. Na Magogu ni Taifa hilo lenye nguvu ambalo linatawala mataifa mengine madogo madogo (Tubali, Mesheki na Roshi)

Sasa kama tulivyotangulia kusema huo mji wa Magogu haupo tena wala mkuu wake Gogu hayupo…Lilikuwepo enzi hizo, lakini sasa halipo tena, lakini huo unabii wa Ezekieli 38 bado haujatimia.. Ambapo ukisoma hiyo Ezekieli 38 yote, utaona inazungumzia Habari za vita vitakavyopiganwa Israeli, ambapo Mataifa mengi katika nchi ya mashariki ya kati (kwasasa ni mataifa ya kiarabu), yataungana pamoja na Gogu na Magogu, atakayekuwepo kipindi hicho kuja kuivamia Israeli, lakini biblia inasema Gogu atashindwa vibaya sana Pamoja na mataifa hayo aliyoshirikiana naye.

Sasa huyo Gogu na Magogu, atakuwa ni nani, kama mji huo ulishapotea kitambo?..

Gogu atakayeasisi vita hivyo vya Ezekieli 38, Uthibitisho wote unaonyesha kuwa atakuwa si mwingine Zaidi ya Mkuu wa Taifa la URUSI .

Kwanini ni Taifa la Urusi, ndio linalofananishwa na Magogu na si Taifa lingine?.

Kwasababu ndio taifa lililopo kaskazini mwa Asia na ulaya, eneo lile lile Magogu walipokuwepo, pili ndio taifa lenye nguvu kijeshi kaskazini mwa Ulaya, mfano wa magogu wa mwanzo.

Hivyo Urusi ndiyo itakayotimiza unabii huo wa Gogu na Magogu, wakati wa vita hivyo.

Mbali na hilo tunakuja kuona tena Gogu na Magogu, wakitokea mwishoni mwa Utawala wa miaka elfu moja. Sasa ni muhimu kufahamu kuwa sio wale wale, wamezaliwa tena upya..hapana…bali ni roho ile ile iliyokuwa inaiendesha Gogu na Magogi kipindi cha zamani, sasa imerudi tena kutenda kazi katika zama hizo, ni kama tu vile Babeli ilivyokuwepo wakati wa zamani na kupata nguvu na kujulikana duniani kote, na kutiisha mataifa yote chini,  lakini ikaja kuanguka, ikapotea kabisa…Lakini bado tena tunakuja kuiona ipo, imerudi tena katika kitabu cha Ufunuo. Sasa haimaanishi kwamba ni Babeli ile ile imerudi,  bali ni ile roho iliyokuwa inaiendesha Taifa hilo nyakati za zamani, imerudi na kuivaa na kuliendesha Taifa Fulani lingine siku za mwisho..

Hivyo Gogu na Magogu, wa kwenye Mwanzo wa kwenye Ezekieli 38 (yaani Taifa la Urusi), sio wa kwenye Ufunuo 20:8 (mwishoni mwa utawala wa miaka elfu), ingawa roho ni ile ile moja, inayofanya kazi ya kukusanya mataifa na kupambana na Taifa la Mungu.

Je umempokea Kristo? Kama bado, kumbuka tunaishi ukingoni mwa nyakati kabisa na Kristo yupo karibuni kurudi, na mpinga kristo kuanza kufanya kazi yake, ya kuwatia watu chapa. Kama unafikiri ni utani kwamba Kristo hatarudi, siku moja utayahikiki haya maneno unayoyasikia. Wakati huo waliokudanganya na wao watagundua kuwa walidanganywa, itakuwa ni huzuni sana.. Je utakuwa wapi siku hiyo?. Kama hujampokea Kristo na leo hii unasema upo tayari kumpokea Kristo na kudhamiria kutubu basi fungua hapa kwa msaada >> SALA YA TOBA

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)

JE WEWE NI LAZARO YUPI, WA KWANZA AU WA PILI?

WAFALME WATOKAO MAWIO YA JUA.

Watakaodanganywa baada ya miaka 1000,watatoka wapi?

ULIMWENGU WA ROHO UPO NA UNA MADHARA KATIKA MAISHA YETU! 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wevi na wanyanga’anyi waliomtangulia Yesu walikuwa ni wapi?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe mtumishi habari ya uzima, samahani nini swali;  Yohana 10:7-8 inasema;

“7 Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.

8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi; lakini kondoo hawakuwasikia”.

Hapo sijaelewa Bwana alichokimaanisha aliposema wote waliomtangulia walikuwa ni wevi na wanyang’anyi?


JIBU: Mstari huo hauzungumzii, wale waliomtangulia Bwana yaani Manabii na makuhani  wa agano la kale hapana, kwani wao ndio waliokuwa wanamwandalia njia yeye, aliye mlango wa kondoo wenyewe.

Bali mstari huo ulikuwa unawazungumzia watu waliokuwa wanajifanya kuwa wao ndio masihi ( yaani Mwokozi) kama yeye. Hao ndio alikuwa anawasemea hapo, kwamba ni wevi na wanyang’anyi na kwamba kondoo wa kweli wa Mungu hawakuwafuata.

Kumbuka wana wa Israeli kwa muda mrefu walikuwa wanangojea masihi ambaye atawaokoa katika shida zao, na dhambi zao kama ilivyotabiriwa katika torati. Hivyo ilikuwa ni jambo la kawaida kutangulia ma-kristo wa uongo wengi kabla yake wakijifanya wao ndio. Utalithibitisha hilo katika maneno ya Yule Gamalieli, mwalimu wa torati, pale alipokuwa anahojiana na wakuu wa makuhani juu ya mitume walichokuwa wanakifanya kwa habari ya Yesu..Alisema;

Matendo 5:35 “akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa.

36 Kwa sababu kabla ya siku hizi aliondoka Theuda, akijidai ya kuwa yeye ni mtu mkuu, watu wapata mia nne wakashikamana naye; naye aliuawa na wote waliomsadiki wakatawanyika wakawa si kitu.

37 Baada ya mtu huyo aliondoka Yuda Mgalilaya, siku zile za kuandikiwa orodha, akawavuta watu kadha wa kadha nyuma yake, naye pia akapotea na wote waliomsadiki wakatawanyika.

38 Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa,

39 lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu”.

Unaona, hapo anasema alitangulia, Theuda, na Yuda Mgalilaya, na walikuwepo na wengine wengi  pia biblia haijawazungumzia tu. Kwahiyo  wezi na wanyang’anyi Yesu aliokuwa anawazungumzia hapo ndio hawa.

Hata sasa wevi  na wanyang’anyi Bwana Yesu aliwatabiri watakuwepo katika siku za mwisho. Ndio wale aliowaita Makristo wa uongo na manabii wa uongo.

Mathayo 24:24 “Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule”.

Hivyo Kristo ameshatuonya, ni wajibu wetu kuwa macho, na hiyo inakuja kwa kuwa wakristo kweli kweli na kumruhusu Roho Mtakatifu kutenda kazi ndani yetu.

Swali ni Je! Umeokoka? Na Kama umeokoka Je! Umesimama? Kumbuka, makristo hawa watajaribu kuwadanganya yamkini hata wateule, hiyo ni kuonyesha kuwa ni jinsi gani ilivyo ngumu kuwatambua kama wewe utakuwa ni mkristo jina tu, au mkristo vuguvugu. Hizi si nyakati tena za kukaa gizani.

Ni heri ukaanza maisha yako upya na Kristo leo. Ikiwa bado hujaokoka, na unataka leo kumpa Yesu maisha yako, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako. Kama jibu ni ndio .Fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba na kupokea maagizo mengine ya rohoni>>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USIIGEUZE NYUMBA YA MUNGU KUWA PANGO LA WANYANG’ANYI.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

WALIOITWA NI WENGI, ILA WATEULE NI WACHACHE.

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MTETEZI WAKO NI NANI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Masuke ni nini? (Luka 6:1, Marko 4:28)

Masuke ni nini  katika biblia?

Masuke ni ile sehemu ya nafaka inayotoa ua na mbegu ndani yake, Kwamfano Ngano suke lake linachipuka kwa pale juu, tazama picha, na nafaka kama mahindi suke lake ndio lile linalochipukia hindi lenyewe. Lakini nafaka yote sio suke, wala hindi lote sio suke, bali ile sehemu inayotoa mbegu au ua au tunda ndio inaitwa suke.

suke la ngano

suke la hindi

Hivyo  zamani, kama mtu akitaka kula ngano iliyo mbichi, ambayo kiafya ilikuwa haina shida, kwani jamii za watu wa mashariki ya kati kama vile wapalestina na waarab,  zamani na hata sasa, wanaoutarabu huo wa kula, nafaka mbichi, hususani ngano ambayo haijapikwa..

Na katika kula kule, ni sharti, uipukuse pukuse au uipure pure kwanza ili kuondoa yale makapi yake, ibakie tu ngano, kisha ndio uile.

Sasa zamani Mungu alishatoa maagizo, kuwa kama mtu ukisikia njaa, na akakutana na shamba la jirani pembeni yake, unayoruhusu ya kwenda na kula kile kilicho katika shamba lile, lakini sio kuvuna na kuondoka navyo.

Kumbukumbu 23:25 “Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako”.

Sasa utaona tukio lingine kuna wakati Bwana Yesu alikuwa anapita na wanafunzi wake, na wanafunzi wake walikuwa na njaa, na kwa bahati nzuri wakakutana na shamba la nafaka njiani, kama tunavyoijua habari wakaingia na kuanza kupura yale masuke ili wale ngano, na siku hiyo ilikuwa ni siku ya sabato.

Luka 6:1 “Ikawa siku ya sabato moja alikuwa akipita katika mashamba, wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke na kuyala, wakiyapukusa-pukusa mikononi mwao”.

Na  mafarisayo walipoona  wakaanza kuwashutumu kuwa wanaihalifu sabato kwa wanachokifanya, ndipo Bwana Yesu akawaeleza habari ya alichofanya Daudi alipokuwa na njaa jinsi alivyokula ile mikate ya wonyesho ambayo sio sahihi yeye kuila bali makuhani tu peke yao.

Na mwisho kabisa  akawaambia mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.

Nasi pia Je ni sahihi kuingia katika shamba la mtu yeyote na kula matunda  ya mashamba yake, kwa mfano miwa yake, au machungwa yake bila ya kupewa ruhusu kwa kigezo cha mstari huo?

Tunapaswa tujue Israeli walipewa agizo hilo kama taifa, kwahiyo sheria hiyo ilijulikana kwa watu wote. Lakini sisi tuliokatika mataifa, tunaishi katikati ya makundi ya watu wengi, na asilimia kubwa sio wacha Mungu. Hivyo tunapaswa tutumie hekima, ya kwenda kuomba kwanza, vinginevyo ukikutana na mtu asiyekuwa na huruma ya kibinadamu anaweza kukuletea matatizo.

Bwana akubariki.

Hivi ni baadhi ya vifungu vingine vinavyolizungumzia Neno hilo  “Masuke”

Marko 4:28 “Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.

29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika”.

 

Mwanzo 41:5 “Akalala, akaota ndoto mara ya pili. Tazama, masuke saba yalimea katika bua moja, makubwa, mema.

6 Na tazama, masuke saba membamba, yamekaushwa na upepo wa mashariki, yakatokeza baada yao.

7 Kisha hayo masuke membamba saba yakayala yale masuke saba makubwa yaliyojaa. Basi Farao akaamka, kumbe! Ni ndoto tu.”

Walawi 23:14 “Nanyi msile mkate, wala bisi, wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu; hii ni amri ya milele katika vizazi vyenu katika makao yenu yote”.

Soma pia Mathayo 12:1  na Marko 2:23

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

HERODE NA PILATO, MAADUI WAWILI WAPATANA.

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya “heri mtu asiyekaa barazani pa wenye mizaha?”

 SWALI: Zaburi 1:1 inasema ..“heri mtu asiyekaa barazani pa wenye mizaha”. Je, ni mizaha gani inaongelewa hapo na kuna tofauti gani kati ya Utani na mizaha, na Kama hamna tofauti je hata kutaniana na mtu ni dhambi pia?


JIBU: Kuna mambo ya msingi tunatakiwa tujifunze katika vifungu hivyo, Embu tuvisome tena vizuri..Anasema;

Zaburi 1:1 “Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha”.

Ukitazama hapo utaona vitu vitatu; KWENDA, KUSIMAMA, na KUKETI.

Vyote hivyo tumezuiwa tusivifanya. Hapo inaposema ‘kwenda’ maana yake ni ‘kutembea’. Hivyo kwa namna ya kawaida, tukizungumzia katika Nyanja ya dhambi, Kutembea kuna heri kidogo kuliko kusimama kwenye dhambi, na kusimama kuna heri pia kidogo kuliko kuketi chini. Kwasababu mpaka unaketi ni wazi kuwa unaonyesha ndio umefika, yaani umetia nanga, hapo ndio panakuvutia. Lakini vyote hivyo biblia imetukataza tusivifanye kwa makundi hayo matatu ya watu.

Kundi la kwanza ni la watu wasio haki

Watu wasio haki ni watu ambao hawana habari na Mungu, watu ambao hawana hofu ya Mungu hata kidogo, wapo tayari kutenda mambo maovu bila kujali kuwa ni machukizo mbele za Mungu au la. Hawa tumeonywa tusitembee katika mashauri yao.

Kundi la pili ni wakosaji.

Hawa ni watu wanaovunja amri za Mungu kwa makusudi, wanaweza wakasema wao ni wakristo, au wana hofu ya Mungu, lakini matendo yao, yanawathibitisha wao ni wakosaji utakuta (ni wazinzi, wafiraji, washirikina, wezi, warushi, n.k.) hao nao tumeambiwa tusisimame karibu nao.

Kundi la tatu ni Watu wenye MIZAHA.

Hawa ndio wabaya zaidi kwani sio tu ni waovu, na wakosaji, bali wamevuka hiyo mipaka hadi kufikia hatua ya kuleta mizaha mpaka kwenye mambo matukufu ya Mungu, kudhihaki, kukejeli, kukashfu Neno la Mungu, na wokovu kwa ujumla kwao ni jambo la kawaida.. Biblia inasema..

2Petro 3:3 “Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe,

4 na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa”.

Hawa tumeonywa tusiketi nao kabisa, kwasababu wapo mabarazani (maana yake kwenye majukwaa, au sehemu yenye mkusanyiko wa watu).

Ni mara ngapi utaona  watu wanaifanyia biblia comedy kwenye majukwaa na watu wamelipa kiingilio, wameketi pale chini wanacheka na kufurahia, huku wakimtaja Bwana Yesu, au mmojawapo wa manabii wa kwenye biblia, na kuwatolea mifano kana kwamba Yule biblia ni kitabu cha story za vichekesho? Ni mara ngapi umewaona kwenye tv au umewatazama youtube?. Hao tumeambiwa tujitenge nao. Hata tusisikilize vichekesho vyao, kwasababu ni machukizo makubwa mbele za Mungu.

Hivyo tukirudi kwenye swali? Je kuna tofauti gani kati ya utani na mzaha,?

Mzaha ndio unaopelekea utani, hivyo ni vitu vinavyoshadidiana. Na pia sisi kama wakristo, hatupaswi kuwa na mizaha kwenye mambo yanayohusiana na imani zetu, au yanayovuka mipaka ya maadili yetu. Vinginevyo tutakuwa tunatenda dhambi. Biblia inasema hivi;

1Wakorintho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.”

Kitu kimoja kinachoharibu tabia ya Mkristo, ni mizaha… Mtu anayejizoeza mizaha, ndivyo anavyopalilia tabia nyingine mbaya ndani yake kama uzinzi, na uongo..Siku zote uzinzi unaanzia kwenye mizaha na utani uliopitiliza, vile vile tabia ya uongo inafunikwa na kivuli cha utani..

Mithali 26:19 “Ndivyo alivyo amdanganyaye mwenzake, Na kusema, JE! SIKUFANYA MZAHA TU?”

Hivyo tunapaswa tuwe na kiasi kama Mtume Paulo alivyomwonya  Timotheo

2Timotheo 4:5 “Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote,….”

Bali tufurahishwe na sheria za Bwana.

Mithali 19:29 “Hukumu zimewekwa tayari KWA WENYE MZAHA; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu”

Tukifanya hivyo. Shetani hatatuweza.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.

CHEMBE YA NGANO ISIPOANGUKA KATIKA NCHI, IKAFA,

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

Tusome..

Matendo 3:1  “Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali, saa tisa.

2  Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu, ambaye walimweka kila siku katika MLANGO WA HEKALU UİTWAO MZURİ, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu”.

Biblia inasema Hekalu lilijengwa vizuri sana, na kwa vitu vya thamani. (1Wafalme 6, imeelezea mwonekano wa hekalu la Mungu). Hivyo Hekalu lilikuwa limejengwa kwa vitu vya thamani, na lilikuwa linamwonekano mzuri..

Tunalithibitisha hilo tena katika kitabu cha Luka..

Luka 21:5  “Na watu kadha wa kadha walipokuwa wakiongea habari za hekalu, JİNSİ LİLİVYOPAMBWA KWA MAWE MAZURİ na sadaka za watu, alisema,

6  Haya mnayoyatazama, siku zitakuja ambapo halitasalia jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa”.

Umeona?. Kwahiyo Hekalu lilikuwa zuri, na kama tunavyojua..Mlango wa kuingilia mahali popote siku zote unatengenezwa kuwa mzuri kuliko, milango mingine ya ndani midogo midogo, Mlango wa mapokezi unakuwa unapambwa sana. Mageti ya kuingilia mijini yalikuwa yanapambwa sana kuliko mageti madogo madogo ya ndani ya hiyo miji, hali kadhalika hata leo mageti ya kuingilia kwenye maonyesho fulani huwa yanapambwa sana ili kuvutia wanaokuja, na kuyapandisha hadhi maonyesho hayo.

Na ndio hivyo hivyo, Mlango wa kuingilia hekaluni ulikuwa umepambwa sana na wenye mwonekano mzuri, hivyo Wayahudi wakauita Mlango MZURI kwasababu kwanza, ndio ulikuwa mzuri kwa mwonekano kuliko milango yote, na ndio mlango wa kuingilia Nyumbani kwa Mungu wa mbingu na nchi. Hivyo wakauita MLANGO MZURI.

Matendo 3:9 “Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu.

10  Wakamtambua, ya kuwa yeye ndiye aliyekuwa akiketi na kuomba sadaka penye MLANGO MZURİ WA HEKALU; wakajaa ushangao wakastaajabia mambo yale yaliyompata”.

Lakini pamoja na uzuri wake wote, Bwana Yesu alisema hapo kwenye (Luka 21:6)..halitasalia jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa, na kweli miaka michache tu baadaye hekalu hilo lilipotea, na hakukuwa tena na kitu kinachoitwa MLANGO MZURI, Israeli. Hata waliokimbilia kuingia katika huo mlango walikufa kwa upanga.

Lakini biblia imetaja mlango mwingine MZURI ambao huo unadumu milele..

Tuusome..

Yohana 10: 9 “ MİMİ NDİMİ MLANGO; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.

10  Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; MİMİ NALİKUJA İLİ WAWE NA UZİMA, KİSHA WAWE NAO TELE.

11  Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo”.

Yesu ndiye MLANGO MZURI unaodumu milele. Na alikuja ili tuwe na Uzima, kisha tuwe nao tele, je umempokea?. Kama bado basi maisha yako yapo hatarini, hivyo mpokee leo akupe uzima wa milele.

Kama hujampokea na unatamani kufanya hivyo sasa, basi uamuzi unaofanya ni wa thamani, kwa msaada wa namna wa kuongozwa sala ya Toba, basi fungua hapa >> KUONGOZWA SALA YA TOBA.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

YAKINI NA BOAZI.

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Kwanini Samweli aliruhusuiwa kuhudumu hekaluni kama vile Walawi wakati yeye ni mu-Efraimu?

MAANDALIZI YA UJENZI WA HEKALU LA TATU YAPO TAYARI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USINIE MAKUU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, Karibu tujifunze biblia.

Neno la Mungu linasema katika..

Warumi 12:3 “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu ASINIE MAKUU KUPITA ILIVYOMPASA KUNIA; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha Imani”.

Sasa kunia makuu kunakozungumziwa hapo ni kupi?

Tukiendelea mbele kidogo katika mistari hiyo inayofuata tutapata jibu kamili…

“4 Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;

5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.

6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;

7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;

8 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.”

Umeona?. Maana yake ni kwamba…Usiwaze moyoni mwako, na kujiona kuwa… “unaweza kuwa na karama zote au nyingi”.

Kwamfano mtu mmoja, atataka yeye ndio awe mchungaji, yeye ndio awe Nabii, yeye ndio mwalimu, yeye ndio Mtume, yeye ndio Muinjilisti n.k… Kwaufupi karama zote za rohoni yeye ni zake. Anajiona yeye hawezi kuwa na karama moja tu”..yeye hawezi kuwa mwinjilisti tu peke yake ni lazima atakuwa ni Nabii pia..hawezi kuwa Mwalimu peke yake ni lazima atakuwa Mwalimu na Nabii mkuu, hawezi kuwa Mtume tu peke yake, ni lazima atakuwa ni Mtume na Nabii mkuu.. N.k Sasa hiyo ni mifano tu, ambayo ndio biblia inatuonya kwamba Tusinie Makuu kuliko tunavyopaswa kunia.

Roho ya kunia Makuu, inaua roho ya unyenyekevu ndani ya mtu, na hatimaye kuundoa kabisa uwepo wa Mungu ndani ya mtu.

1Petro 5: 5 “…Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema”

Na karama tulizopewa sio za mashindano wala za kujionyesha yupi bora Zaidi, au yupi mwenye neema kubwa zaidi. Karama yeyote inayotumika kwa matumizi hayo, tayari imeshavamiwa na shetani. Karama tulizopewa ni za kuhudumiana ili kuwakamilisha watakatifu na kazi ya huduma itendeke ili mwili wa Kristo ujengwe. na sio kuringishiana wala kuzitumia hizo kujinyanyua juu ya wengine.

Waefeso 4:11 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;

12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe”;

Bwana atusaidie.

Kama bado hujampokea Kristo, mlango wa Neema upo wazi sasa, ila hautakuwa hivyo siku zote. Hivyo geuka leo, na kumkabidhi Maisha yako, kwasababu muda tuliobakiwa nao hapa duniani sio mwingi, wakati wowote parapanda ya mwisho inalia na Kristo atalinyakua kanisa lake, kitakachosalia huku duniani ni hukumu. Hivyo mimi na wewe tusiwe miongoni mwa watakaoangukia kwenye hukumu ya Mungu.

Kumbuka kuzimu ipo na mbingu vile vile ipo. Na Uzima au Mauti, tunachagua tukiwa hapa hapa duniani, baada ya kifo hakuna nafasi ya kufanya uchaguzi. Hivyo fanya uamuzi uliobora sasa kabla siku zako za kuishi hapa duniani hazijaisha.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

KARAMA YA MUNGU NI UZIMA WA MILELE.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

BONDE LA KUKATA MANENO.

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

Rudi Nyumbani:

Print this post

Neema ni nini?

Neema ni nini kibiblia?


Neema ni “upendeleo usio na sababu”. Upo upendeleo wenye sababu na usio na sababu. Mfano wa upendeleo wenye sababu ni huu tulionao sisi wanadamu, sisi tunapendelea walio wetu, yaani watu tunaowajua au wenye manufaa katika Maisha yetu kama vile ndugu zetu, marafiki zetu n.k.

Hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kumpendelea adui yake..Hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kumpendelea yule mtu anayemuudhi. Hakuna mwanadamu yeyote mwenye uwezo wa kutoa huo upendeleo, isipokuwa Mungu peke yake. Ni Mungu tu ndio mwenye uwezo wa kufanya hivyo, Mungu ana uwezo wa kumpendelea yule mtu ambaye hastahili kabisa mbele zake.

Sasa ili tuielewe neema vizuri hebu soma hichi kisa..

Mathayo 20:9  “Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari.

10  Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.

11  Basi wakiisha kuipokea, wakamnung’unikia mwenye nyumba,

12  wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa.

13  Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari?

14  Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.

15  Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema?

16  Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho”.

Umeona hapo, hao waliofanya kazi lisaa limoja tu wamelipwa sawa na wale waliotaabika mchana kutwa. Ni kama vile wamependelewa, lakini hakukuwa na  sababu yeyote iliyowafanya wao walipwe sawa na wale wengine waliotaabika mchana kutwa, basi tu ni kama wamependelewa, wangepaswa walipwe kiwango kidogo Zaidi ya wenzao, na Zaidi ya yote hao ndio wangepaswa walipwe wamwisho, lakini chaajabu ndio wametangulia kulipwa…Sasa huo ndio mfano wa NEEMA.

Lakini ipo NEEMA moja kubwa sana ambayo sisi wanadamu tumepewa na Mungu. Nayo hiyo si nyingine Zaidi ya UZIMA WA MILELE. Baada ya anguko pale Edeni, hatukustahili tena tupate nafasi ya kuishi milele, Habari yetu ndio ilikuwa imeishia pale. Hatujui labda angeamua kuumba viumbe wengine, hilo hatulijui..lakini shughuli yetu ndio ilikuwa imeishia pale..

Lakini Mungu akatazama, na pasipo sababu yoyote (kama bahati tu!) ikatokea akapenda tu kutupa UZIMA WA MILELE, Wala usidhani ni kwasababu tulikuwa tunatilisha huruma sana mbele zake, ndio sababu akatuhurumia akatupa uzima wa milele..la!, wala sio sababu tulimwomba. Ni neema tu!..Ni neema tu…

Hakukuwa na sababu yoyote ya sisi kuupata tena uzima wa milele. Wala Mungu kutupoteza daima isingekuwa ni kitu kikubwa sana kwake, kwasababu kabla ya kutuumba sisi alikuwepo milele huko mamilioni na mamilioni ya miaka, alikuwepo huko peke yake pasipo sisi..Kwahiyo kamwe tusifikiri kwamba tulikuwa ni lulu sana mbele zake, ndio maana akatupa tena nafasi ya kuupata uzima wa milele.. Ni Neema tu!..Ni neema tu!..tumependelewa pasipo sababu yeyote. Angeweza kufuta na kuumba wengine na angetusahau sisi moja kwa moja…

Na alianza mpango huo wa wokovu kwa kumtuma Mwanawe mpendwa Yesu Kristo, ambaye kila amwamini huyo ATAPATA UZIMA HUO WA MILELE.

Yohana 1:14  “Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; AMEJAA NEEMA NA KWELI”.

Kwahiyo hebu tutafakari kama tumeokolewa kwa neema, (maana yake tumepata upendeleo ambao hatukustahili)..tunawezaje leo kuudharau Msalaba wa Yesu?.

Biblia inasema katika…

Waebrania 2:3  “sisi je! Tutapataje kupona, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”.

Neema ya Msalaba sio kitu cha kuchezea hata kidogo. Kwasababu ndio kitu pekee kilichoificha ghadhabu ya Mungu juu yetu sasa, ikiondoka Neema hapo ndio tutajua kuwa hatukuwa watu maalumu (special) sana mbele za Mungu. Hapo ndipo tutakapojua kuwa kumbe Mungu anaweza kuishi bila sisi.

Waebrania 10:28  “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29  Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?”.

Ndugu tuko ukingoni kabisa mwa hii Neema kuisha, Hii nafasi tuliyopewa ya kuokoka haitakuwepo milele. Siku parapanda ya mwisho itakapolia ndio utakuwa ukomo wa hii neema. Na kwa wale watakaoukosa unyakuo ndio watahakiki nini maana ya neema maana, watakapoona kilio cha maumivu yao hayasikiwi na Mungu, wakiwa katika ziwa la moto, watakapokuwa wanaungua na kulia kwa machozi, ndipo wakiwa huko watajua kuwa hisia zao si kitu mbele za Mungu, wataona kumbe hatukuwa watu maalumu sana, mbele za Mungu kama tulivyokuwa tulikuwa tunadhani au tunahubiriwa, ndipo watajua kuwa waliichezea neema..

Ndugu mimi na wewe tusiwe miongoni mwa watakaotengwa na Mungu milele. Leo hii mpokee Kristo kama hujampokea kwa kutubu dhambi zako zote ulizokuwa unazifanya na kuziacha kabisa, Kristo yupo mlangoni mwa moyo wako sasa, anatamani aingie ili ayaokoe Maisha yako..Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa na wala si kesho basi fungua hapa >> SALA YA TOBA

Neema ya Kristo ikae nasi sote.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

KUZIMU NI WAPI

ITAFAKARI SIKU YA HUKUMU.

KITABU CHA UZIMA

Ni kweli mtu anaweza akafa lakini roho yake ikawa inatumika kama msukule (kumilikiwa na mtu fulani kwa wakati) mahali pengine?

Rudi Nyumbani:

Print this post