Title May 2021

MILANGO YA KUZIMU.

Milango ni wingi wa neno “mlango”..( Malango na Milango), ni neno moja. Katika biblia tunasoma Neno hilo likitajwa na Bwana Yesu..

Mathayo 16:18 “ Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; WALA MILANGO YA KUZIMU HAITALISHINDA.

19  Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”.

Tunasoma Mamlaka hayo alipewa Mtume Petro,  na Mitume wengine pia walipewa mamlaka kama hayo (soma Yohana 20:23).

Sasa Mlango maana yake ni maingilio ya mahali, Vitu au watu wanaingia ndani ya nyumba au ndani ya mji kupitia milango yake, hakuna namna wanaweza kupitia kwingine.

Kwahiyo Kristo aliposema atalijenga kanisa ambalo milango ya kuzimu haitalishinda, Maana yake ni kwamba kanisa Bwana Yesu atakalolijenga, litakuwa na nguvu dhidi ya Milango yote ya kuzimu.

Sasa Milango ya kuzimu ni ipi?

Milango ya kuzimu ni mambo yote ambayo yanayompa mtu tiketi ya moja kwa moja kuingia kuzimu. Ifuatayo ni baadhi tu!

1Wakorintho 6:9  “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? MSIDANGANYIKE; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”

Kwahiyo Ibada za sanamu: Ni lango la kuzimu…Uasherani: ni lango la kuzimu!. Mtu anayefanya uasherati kajifungulia mlango wa kwenda kuzimu, Uuaji ni lango la kuzimu, Wizi ni lango la kuzimu, Anasa ni lango la kuzimu, Ulevi ni lango la kuzimu. Na mengine mengi yanayofanana na hayo!.. ndio maana Bwana Yesu kaitaja kama “Milango”..maana yake ipo mingi… Maana yake hata ukitenda mojawapo kati ya hayo bado utaingia kuzimu tu! Hata kama hutafanya hayo mengine yaliyosalia.. Ukiwa mzinzi tu, hata kama huibi, au sio mlevi, tayari utaenda kuzimu tu!..Kwasababu uzinzi, ni moja wapo ya lango la kuzimu..utafika kule kule tu, alipo mlevi na muuaji. Kwasababu kuzimu ina milango mingi.

Yakobo 2:10  “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.

11  Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria”.

Kwahiyo Kanisa Bwana atakalolitengeneza Maana yake litakuwa ni Kanisa Takatifu lisilo na kunyanzi wala hila, Kanisa ambalo litaliendea LANGO MOJA TU LA MBINGUNI (Yaani Yesu), na wala halivutwi na Malango ya kuzimu!. Kanisa la namna hiyo ndio Bwana aliahidi kulijenga.

Na alianza kulijenga siku ile ya Pentekoste, Roho Mtakatifu aliposhuka juu  ya watu wake, akawajaza Roho Mtakatifu, na kuwapa nguvu za kushinda milango yote ya kuzimu.

Roho Mtakatifu ndio Muhuri wa Mungu, anaposhuka juu ya mtu, anaondoa ile kiu yote ya kufanya dhambi, kiasi kwamba dunia inamshangaa mtu huyo anawezaje kuishi bila kufanya zinaa katika kizazi hiki, anawezaje kuishi bila kuvuta sigara wala kunywa pombe, na hata hatumii nguvu kujizuia, anawezaje kuishi bila kutukana, bila kuiba, anawezaje kuishi maisha ya ustaarabu kiasi hicho, anawezaje kuwa na amani na huku hana kitu mfukoni, anawezaje kuwa na amani na huku kila mtu yupo kinyume naye, anawezaje kuishi bila kumkana huyo Yesu, anawezaje kuishi bila kuvutwa na anasa na starehe za dunia?..n.k pasipo kujua kuwa ipo nguvu waliyopewa ya kuishinda MILANGO YA KUZIMU.

Je na wewe unayo hiyo nguvu?. Au malango ya kuzimu yana nguvu juu yako?.

Kwa ufunuo Petro aliopewa ndio Bwana aliosema atalijenga kanisa lake juu yake, na  milango ya kuzimu haitalishinda…na ufunuo huo si mwingine zaidi ya YESU NDIYE MWANA WA MUNGU.

Mathayo 16:15  “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16  Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

17  Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18  Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”

Hivyo ukitaka milango ya kuzimu uishinde, njia ni moja tu, nayo ni KUMWAMINI YESU KUWA NDIYE MWANA WA MUNGU, Huo ndio Msingi, ambao kanisa la Mungu linajengwa juu yake. Ukitafuta msingi mwingine kamwe hutaweza kupata nguvu ya kuishinda milango ya kuzimu.

Na kumwamini Yesu, ni kutubu kwa kudhamiria kuacha kabisa dhambi zote, na baada ya hapo ubatizo, na mwisho kupokea Roho Mtakatifu, kama muhuri wa Mungu, ambaye huyo ndio ukamilifu wa kazi ya Mungu juu ya Mtu, ndiye anayetoa nguvu za kuyashinda malango ya kuzimu.

Kumbuka biblia inasema kuzimu haishibi..(Mithali 30:16), wanaoshuka huko ni wengi kila siku.Na ina milango mingi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin


Mada Nyinginezo:

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

LANGO LIMEBADILIKA.

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

Print this post

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe mtumishi wa Mungu, samahani naomba kuuliza swali kwenye 2Wafalme 8:7-15. Kwanini Elisha alimwambia Hazaeli amwambie mfalme kuwa atapona na wakati Bwana alimuonyesha Elisha kuwa mfalme atakufa. Je! Ni kwanini Elisha alisema hivyo?. Je! Ni kweli alidanganya? Na ni kwanini alifanya hivyo?


JIBU: Tusome vifungu vyenyewe kwa faida ya wengine pia..

2Wafalme 8:7 “Kisha, Elisha akaenda Dameski; na Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, alikuwa hawezi; akaambiwa ya kwamba, Yule mtu wa Mungu amefika hapa.

7 Kisha, Elisha akaenda Dameski; na Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, alikuwa hawezi; akaambiwa ya kwamba, Yule mtu wa Mungu amefika hapa.

8 Mfalme akamwambia Hazaeli, Chukua zawadi mkononi mwako, ukaende ili kumlaki yule mtu wa Mungu, ukamwulize Bwana kwa kinywa chake, kusema, Je! Nitapona ugonjwa huu?

9 Basi Hazaeli akaenda kumlaki, akachukua zawadi mkononi mwake, za kila kitu chema kilichopatikana Dameski, kiasi cha mizigo ya ngamia arobaini, akaenda, akasimama mbele yake akasema, Mwana wako Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, amenituma kwako, kusema, Je nitapona ugonjwa huu?

10 Elisha akamwambia, Enenda, ukamwambie, BILA SHAKA UTAPONA; LAKINI BWANA AMENIONYESHA YA KWAMBA BILA SHAKA ATAKUFA.

11 Akamkazia macho hata akatahayari; na yule mtu wa Mungu akalia machozi.

12 Hazaeli akasema, Bwana wangu analilia nini? Akajibu, Kwa sababu nayajua mabaya utakayowatenda wana wa Israeli; utazichoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, utawaseta-seta watoto wao wachanga na wanawake wao wenye mimba utawapasua.

13 Hazaeli akasema, Lakini mimi mtumwa wako ni nani, mimi niliye mbwa tu, hata nifanye jambo hili kubwa? Elisha akajibu, Bwana amenionyesha ya kwamba wewe utakuwa mfalme juu ya Shamu.

14 Ndipo akamwacha Elisha, akarudi kwa bwana wake; naye akamwambia, Elisha alikuambiaje? Akajibu, Aliniambia ya kuwa bila shaka utapona.

15 Ikawa siku ya pili yake, akatwaa tandiko la kitanda, akalichovya katika maji, akalitandaza juu ya uso wake, hata akafa. Na Hazaeli akatawala badala yake”.

Ukingalia hapo, Elisha hakumdanganya Ben-hadadi kuhusiana na ugonjwa wake. Asingeweza kufanya vile kwani Ben-hadadi hakwenda kwa shari wala kwa dharau, bali alikwenda kwa unyenyekevu mwingi mpaka kuchukua uamuzi wa kubeba na sadaka zake kwa mtumishi wa Mungu. Kwahiyo Elisha kama mtumishi wa Mungu asingewezeka kufanya jambo kama hilo

Hivyo Elisha alipomwambia kuwa atapona, lakini bila shaka kuwa atakufa.. alikuwa anazungumza mambo mawili tofauti, jambo la kwanza ni kuwa kuhusiana na ugonjwa wake aliouulizia kuwa utamletea mauti,  Elisha alimwambia kuwa huo hautamletea mauti, bali atapona, lakini mauti yake itakuja kwasababu nyingine kabisa.

Na ndio maana utaona hapo baada ya siku mbili, biblia inasema alitwaa tandiko la kitanda, (blanketi). Kisha akalichovya kwenye maji, akalitandaza juu ya uso wake akafa. Kwa kawaida ukichukua hata shuka tu jepesi, akafunikwa uso, kisha maji yakamwagwa juu yake, huwezi pata pumzi, utakufa tu. Ndivyo ilivyokuwa kwa Ben-hadadi. Aliuawa kwa kifo kingine kabisa lakini sio cha ugonjwa wake.

Hatujui ni nini kilimpelekea mpaka akafanya vile, pengine labda alipokea taarifa mbaya kutoka kwa maadui zake za kuvamiwa, au alifanyiwa hila na watumishi wake, ikiwemo huyu Hazaeli, hatajui, lakini utaona kifo kilikuja kwa njia nyingine kabisa ya kujinyonga kwa kukosa pumzi na sio kwa ugonjwa.

Hivyo, jambo ambalo tunaweza kujifunza ni kuwa, Mungu anaweza kusema na wewe, juu ya habari ya uzima wako, au mafanikio yako, au amani yako. Lakini wakati huo huo anaweza kuzungumza juu ya kifo chako.

Kwamfano unaweza muuliza Mungu, Je! Nikifanya biashara fulani, nitafanikiwa na kupata faida? Akakujibu ndio utafanikiwa na kuwa tajiri sana mpaka kumiliki mashirika 20 . Lakini kwasababu ulimuuliza juu ya biashara yako tu, hukumuuliza juu ya hatma ya maisha yako ya milele. Unashangaa, baada ya mwezi mmoja unakufa.

Tunapaswa tuwe na hekima ya kutaka kujua pande zote, kama Daudi ambaye alimwomba Mungu, amjalie pia kujua hesabu ya miaka yake hapa duniani. Ili aishi maisha ya kumcha Mungu…

Zaburi 39:4 “Bwana, unijulishe mwisho wangu, Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani; Nijue jinsi nilivyo dhaifu”.

Inasikitisha kuona kuwa watu wanathamini sana mambo ya mwilini, lakini ya rohoni wanayatupalia nyuma. Kana kwamba huko watakapokwenda yatafuatana nao.  Ukiwaeleza habari za mbinguni na kuzimu, wanakupuuzia, wao wanapoona Mungu anapozungumza nao juu ya mafanikio yao, ndio wanadhani wamefika. Kumbe hawajui, hapa duniani ni tuna pita tu.

Mtafute Mungu ndugu yangu.. Vya duniani vinapita!

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?

JIBU: Watu wengi wanajaribu kutoa  tofauti katika  maneno hayo mawili, lakini ukweli ni kwamba yanamaanisha jambo lile lile moja, ufalme wa mbinguni ndio ufalme wa Mungu.

Na ndio maana kuna mahali Bwana Yesu  alisema maneno haya kwa wanafunzi wake;

Mathayo 19:23 “Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika UFALME WA MBINGUNI.

24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika UFALME WA MUNGU”.

Ukichunguza hapo utaona Bwana Yesu alikuwa anamaanisha kitu kimoja katika hayo maneno mawili, ufalme wa Mungu na ule wa mbinguni..Hivyo unapokutana na mwandishi mmoja anatumia sana neno ufalme wa mbinguni, na mwingine ufalme wa Mungu, usichanganyikiwe ujue wanamaanisha kitu kilekile kimoja.

Ni sawa na ule mfano wa “kuapa” ambao Bwana Yesu aliwaambia mafarisayo, wao walidhani kama ukiapa kwa mbingu sio kosa, bali ukiapa kwa yeye akatiye juu ya kiti cha enzi mbinguni ndio kosa…Wakijaribu kutofautisha kati ya Makao ya Mungu na Mungu mwenyewe.. Lakini Yesu aliwaita viongozi vipofu kwasababu  hawakujua kuwa ukishaitaja mbingu, tayari moja kwa moja umeshamtaja na Yule akaaye ndani yake .  Soma..

Mathayo 23:16 “Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga.

17 Wapumbavu ninyi na vipofu; maana ni ipi iliyo kubwa, ile dhahabu, au lile hekalu liitakasalo dhahabu?

18 Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga.

19 Vipofu ninyi; maana ni ipi iliyo kubwa, ile sadaka, au ile madhabahu iitakasayo sadaka?

20 Basi yeye aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hiyo, na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.

21 Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo, na kwa yeye akaaye ndani yake.

22 Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa yeye aketiye juu yake”.

Vivyo hivyo unaposema Ufalme wa Mbinguni, unapaswa ufahamu kuwa unautaja Ufalme wa Mungu mwenyewe anayeishi huko. Jambo ni lile lile hakuna tofauti yoyote.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

DANIELI: Mlango wa 11

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

ITAKUFAIDIA NINI?

UFUNUO: Mlango wa 11

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kwanini tunambariki Mungu? Je! Mungu huwa anabarikiwa?

SWALI: Tafadhali naomba ufafanuzi wa jambo hili, kibiblia tunaambiwa kwamba mkubwa atambariki mdogo. Sasa kuna baadhi ya wakristo waliookoka wanapokuwa katika maombi, wamezoea kusema “Nakubariki Mungu wa mbingu kwa wema wako.”. Je ni sahihi kumwambia Mungu wetu hivyo?


JIBU: Neno kubariki linamaana Zaidi ya ile ya kumuombea mtu mafanikio, ambayo tumeizoea,  kwamba mkubwa anambariki mdogo, lengo  likiwa ni ili aje kupokea mema kutoka kwa Mungu baadaye.

Bali Neno kubariki kibiblia linamaanisha pia ya kutukuza, au kuheshimisha jambo,kitu au jina. kwamba limestahili kupokea sifa zote njema..

Hivyo mkristo anaposema nalibariki jina la Bwana. Hana maana kuwa analiombea mafanikio kana kwamba linategemea baraka kutoka kwake ili lifanikiwe pasipo hizo haliwezi kufanikiwa, hapana.

Bali linamaana  ya juu Zaidi, yaani “analipa heshima zake zote kwamba limestahili heri”

Katika biblia utaona Ayubu alilibariki jina la Mungu wakati ule alipokuwa anapitia matatizo, alisema maneno hayo…

Ayubu 1:21 “akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; JINA LA BWANA NA LIBARIKIWE”.

Unaona? vilevile malaika mbinguni, usiku na mchana wanalibariki jina lake.

Ufunuo 5:11 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,

12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu NA BARAKA”.

13 Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, BARAKA NA HESHIMA na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele.

Soma pia.. Ufunuo 7:12.

Hivyo, na sisi tunapolibariki jina la Bwana, ni kwamba tunaonyesha kuwa tunathamini haki  yote na uzima, na amani, na furaha,  na upendo, unaotoka katika jina hilo. Ni lugha nzuri Zaidi tuliyonayo  ya kumtukuza Bwana , na hakuna shida yoyote kusema hivyo.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Mafundisho

UFUNUO: Mlango wa 7 & 11

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

SWALI: Mstari huu unamaanisha nini?

Waefeso 3:14 “Kwa hiyo nampigia Baba magoti,

15 ambaye kwa jina lake UBABA WOTE WA MBINGUNI NA WA DUNIANI UNAITWA”,


JIBU: Mungu ni Baba wa kila kitu, Baba wa vilivyo mbinguni, na vilevile  Baba wa vilivyo duniani. Na kama tunavyojua jukumu la Baba ni kuhakikisha anaihudumia familia yake vizuri, anaitunza, anailisha, anaivisha, anaiburudisha, vivyo hivyo Mungu wetu ni Baba wa viumbe vyake vyote, vilivyo juu mbinguni (yaani malaika zake wote), na vilivyo chini duniani (Wanadamu wote). Anavihudumia na kuvitosheleza vyote kulingana na mahitaji yao. Kwasababu yeye ndiye aliyeumba kila kitu, Na ndiye mpaji wa wote.

Wakolosai 1:16 “Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake”.

Na ndio maana mtume Paulo anasema Anampigia magoti yeye, kwasababu uweza wake wa ubaba haupo tu, hapa duniani, bali pia upo kule mbinguni. Na utaendelea kuwa hivyo milele na milele. Hivyo Baba kama huyo ndiye anayestahili kupigiwa magoti.

Wafilipi 2:9 “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

Na sisi pia tuliookoka tunapaswa tukumbuke kuwa tunaye BABA MKUU juu mbinguni. Na kwamba anaowezo wa kututimizia mahitaji yetu yote ya mwilini na rohoni. Lakini ni sharti kwanza tujue kuenenda katika kanuni zake, ili afanyike kwetu Baba kweli kweli. Na kanuni yenyewe ni ile ile, ya kuutafuta kwanza ufalme wake na haki yake, ndipo hayo mengine atatuzidishia kirahisi.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 6:26 “Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao? 27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Mbari ni nini kibiblia?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Ufunuo 12 inaelezea vita vya wakati upi?

Rudi nyumbani

Print this post

KUWA RAFIKI WA DUNIA NI KUWA ADUI WA MUNGU.

Yakobo 4:4  “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu”.

Shalom.

Kitendo tu cha kuipenda dunia, na mambo yake, tayari umefanyika kuwa adui wa Mungu. Mtu akipenda anasa, akipenda uzinzi, akipenda fashion, akipenda starehe za ulimwengu huu, kama miziki, ushabiki wa mipira, ulevi, ukahaba, wizi, utapeli, tamaa za fedha, tamaa mbaya ya vitu vya kiulimwengu vinavyopita kama magari, nyumba, kiasi kwamba unaweza kufanya chochote ili uvipate n.k Mtu huyo tayari kashafanyika kuwa Adui wa Mungu.

1Yohana 2:15  “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16  Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na KIBURI CHA UZIMA, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17  Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”

Kiburi cha Uzima, kinachozungumziwa hapo ni ile hali ya mtu kujiona hawezi kuambiwa lolote kutokana na aidha Elimu aliyonayo au mali alizonazo. Mtu yeyote ambaye anaidharau injili na Mungu, kutokana na kitu Fulani cha kidunia alichokipata, ambacho kinaheshimika katika dunia, mtu huyo ana kiburi cha uzima. Na mtu yeyote mwenye kiburi cha uzima tayari ni adui wa Mungu.

Biblia inatuambia dunia inapita, na tamaa zake zote.. Na tena Bwana Yesu alituambia katika Marko..

Marko 8:36  “Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?

37  Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?”

Hebu jiulize umepata kila kitu leo hii, halafu unakufa unakwenda motoni?, Umejifurahisha na kila starehe halafu unakufa ghafla, na kule Bwana anakuweka katika kundi la maadui zake?. Ni heri tukakosa kila kitu leo, lakini kule tukapate kila kitu..

Jihadhari na kiburi cha Uzima, BelshazaMfalme wa Babeli alikuwa nacho, hata ikafikia hatua ya kumdharau Mungu wa mbingu na nchi, kwa kwenda kuvitumia vyombo vitakatifu kushiriki anasa zake pamoja na wake zake, lakini siku ile kilitokea kiganja kikamwandikia MENE, MENE, TEKELI na PERESI. Na ufalme wake wote haukumsaidia, kwasababu usiku ule ule alioona kile kiganja alikufa.

Yule Tajiri aliyekuwa na Lazaro katika Luka 16, Alikuwa na kiburi cha Uzima, kiasi kwamba aliweza kumlisha mtumishi wa Mungu kwa makombo yaliyoanguka katika meza yake, lakini alipokufa alitamani aburudishe ulimi wake kwa tone moja la maji, alipokuwa katika yale mateso kuzimu. Na kiburi chake chote alichokuwa nacho duniani, hakikumsaidia kitu.

Malkia Yezebeli alikuwa na kiburi cha uzima, mpaka kufikia kuua manabii wa Mungu, na zaidi ya yote alikuwa mchawi, na ndiye mwanamke pekee katika Israeli,  aliyekuwa anajipaka uwanja na kujipaka rangi uso. Kwa kiburi chake chote hicho, lakini fahari yake iliondoka katika siku moja, Mbwa walipomla nyama yake.

Hayo yote yaliwatokea hao na kuandikwa ili sisi tusirudie makosa yaliyofanyika na tumwogope Mungu, kama Neno la Mungu linavyosema…

1Wakorintho  10:11  “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani”.

Swali: Je! Wewe ni Rafiki wa Mungu?.. au Adui wa Mungu?… Kama bado unaupenda ulevi, uasherati, fashion, anasa, wizi, matusi, ni mshabiki wa mipira na mambo mengine yote ya uliwemwengu huu, ni Adui wa Mungu bila hata kutamka kwa kinywa chako.  Kama hujampokea Kristo leo hii ni siku yako, hapo ulipo tubu! Kwa kumaanisha kuacha dhambi zako, na pia tafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa Jina la Yesu, kulingana na Matendo 2:38, na Roho Mtakatifu atakufanya rafiki wake wa kweli na wa kudumu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi


Mada Nyinginezo:

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

SWALI: Je! kuna mchango wowote sisi tunaweza kuuweka ili tupate wokovu wetu? Na  kama sio kwanini basi maandiko yanasema, ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu nao wenye nguvu ndio wanaouteka (Mathayo 11:12)?


JIBU: Kuhusu mchango wetu katika Neema ya wokovu, maandiko yapo wazi ni kuwa HAUPO.

Waefeso 2:8 “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;

9 wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu”.

Lakini swali linakuja kama ni hivyo basi kwanini, maandiko yanasema..

Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”.

Jibu ni kuwa adui yetu tupo naye ni shetani, huyo ndiye anayeifanya njia ya wokovu ionekane ni ya jitahada kidogo. Hivyo inahitaji nguvu ya ziada kuiona na vilevile kuiendea kwasababu ni nyembamba sana na imesonga.

Mathayo 7:13 “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

14 Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache”.

Kwamfano leo hii, shetani anaweza kukuzuia usimfanyie Kristo ibada, kisa tu wazazi wako wamekataa, au kazi yako imekusonga, au mazingira si rafiki hakuna mtu atakayekuelewa, unadhani ukiiruhusu hiyo hali, ataurithi uzima wa milele?. Haiwezekani, inahitaji kulazimisha mambo, kutumia nguvu, kukubali kuchukiwa, au wakati mwingine kupoteza hata kile ulichonacho, ili mradi tu usiopoteze wokovu wako.

Hapo ndipo neno ufalme wa mbinguni unapatikana  kwa nguvu, nao wenye nguvu ndio wanauteka.

Kwamfano, Kristo alituambia tukeshe tuombe, lengo la kusema vile lilikuwa ni kusudi tusiingie majaribuni(Mathayo 26:41), kwasababu adui yetu shetani anaishi kutuwinda. Sasa kama wewe husali, ili kuulinda wokovu wako uliopewa bure na Kristo bila kuusumbukia, unaona uvivu, ufahamu kuwa shetani atakesha kwa ajili yako, na siku ya siku ikifika atakuletea majaribu mazito, kama alivyowaletea wakina Petro usiku ule mpaka kufikia hatua ya kumkana Bwana na wengine kumtoroka uchi, unadhani walipenda? Hapana hiyo yote ni kutokana na kupuuzia kwao maagizo ambayo Yesu aliwapa muda mchache kabla kwamba wakeshe waombe, wao wakalala.

Vivyo hivyo, na wewe usipokuwa mwombaji, usipojitesa kufunga wakati mwingine, hata kutumika kwa ajili ya Kristo, ni ngumu  sana kuutunza wokovu wako kama sio kuupoteza kabisa.

Hivyo, hatumwamini Yesu na kubakia hivyo hivyo tu, hapana hiyo ni hatua moja, hatua ya pili ni lazima tushindane na tupambane, tupigane vita, na tuumie ili kuulinda wokovu wetu kwasababu adui yetu shetani yupo kuuwinda wokovu wetu usiku na mchana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

Neema ni nini?

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

SWALI: Je! Mungu anashindwa na mwanadamu? Kama sio Kwanini siku ile aliposhindana na Yakobo alikiri kushindwa?

Mwanzo 32:25 “Naye alipoona ya kuwa hamshindi, alimgusa panapo uvungu wa paja lake; ukateguka uvungu wa paja la Yakobo alipokuwa akishindana naye.

26 Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.

27 Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo.

28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda”.

JIBU: Jibu ni ndio Mungu anakubali kushindwa, Pengine utauliza unakubalije kushindwa wakati yeye ni Mungu asiyeshindwa na chochote.

Tabia za Mungu sio kama  zetu, Mungu huwa anathamini sana, NIA, BIDII na MATAMANIO ya mtu, kiasi kwamba hata kama matamanio hayo yatakuwa  kinyume na mpango wake, au mapenzi yake, ikiwa tu mtu huyo ataendelea kuking’ang’ania basi mwisho wa siku atamwachia, akipate anachokitafuta haijalishi kitakuwa ni kibaya au chema. Huko ndiko kushindwa kwa Mungu.

Na ndicho kilichotokea kwa Yakobo, aliposhindana na Mungu usiku kucha, akiomba apewe jambo ambalo halikuwa mpango wa Mungu kumpa wakati ule, lakini alipong’ang’ania bila kukata tamaa, kwa kupigana mieleka, ikambidi Mungu ampe tu kulingana na haja yake.

Jambo hili hili utaliona pia wakati ule Bwana Yesu akiwa duniani, utakumbuka kuwa mwanzoni kabisa alitumwa kwa Wayahudi na sio kwetu sisi mataifa, lakini siku moja alikutana na mwanamke mmoja king’ang’anizi wa kimataifa aliyeishi nchi moja iliyoitwa Tiro. Mwanamke huyo alikuwa na binti yake aliyesumbuliwa na mapepo. Na alipokutana na Yesu alitaka aponywe, lakini Yesu hakuongea naye chochote, kwasababu sio hakutumwa kwao, lakini mama huyo hakukata tamaa, baada ya kumlilia sana,  ndipo Yesu akafungua kinywa chake akamwambia, maneno haya;

Mathayo 15:24 “Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli

25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Unaona, hapo, neema ya wokovu ilikuwa haijatufikia bado watu wa mataifa, kwasababu Kristo alikuwa hajasulibiwa bado, lakini mwanamke huyu, aliiwahi kabla hata ya wakati wenyewe kujika, jambo ambalo lilikuwa kinyume kabisa na mpango wa Mungu. Na ndio maana Kristo alitumia maneno magumu kama yale ili mradi tu adhoofishe mataminio yake, akawa hajibiwi, akawa anaitwa mbwa. Lakini mwisho wa siku Yesu kuona bado ni king’ang’anizi basi akakubali kushindwa. Akampa haja ya moyo wake, kama alivyofanya kwa Yakobo.

Hata wewe leo hii, unaweza shindana na Mungu nawe ukamshinda, hilo linawezekana kabisa, pengine hukustahili kupokea  uponyaji wa ugonjwa wako sasa, kutokana na mambo uliyomkosea Mungu, pengine,hustahili kupewa hilo hitaji lako kwa sasa hivi, labda pengine  limekusudiwa ulipokee baadaye sana, baada ya miaka 15, pengine hustahili kuwa na hiyo karama sasa hivi, lakini uking’ang’ana na Mungu, anaweza kukusogezea karibu hilo hitaji lako haijalishi alitaka litimie baada ya miaka 20.

Na ndio maana Bwana Yesu alituambia mfano huu, naomba nawe pia uutafakari vizuri;

Luka 18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”.

Usichoke kung’ang’ana na Mungu wako..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

BWANA HUWAJUA HAO WAMKIMBILIAO.

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

1Wakorintho 12:3 “Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.”

Katika hali ya kawaida kila mtu anaweza kusema “Yesu ni Bwana”, hata watu wa kidunia, wanaweza kulitamka hilo neno, lakini wasiwe wamemaanisha, au wamejua uzito wake, wakawa wamelitaja tu.. Lakini kwa mtu ambaye amempokea Roho Mtakatifu, na kufunuliwa kwa Roho kuwa Yesu ni nani, kwanini amekuja duniani, kwanini  amwage damu yake, afe na kufufuka, na yupo wapi sasahivi?..Mtu wa namna hiyo kama akitamka “Yesu ni Bwana”,… kutamka kwake kunakuwa na maana sana na nguvu kubwa. Kwasababu amekutamka katika Roho.

Hivyo Mtu anayetaja “Yesu ni Bwana” katika Roho Mtakatifu ni lazima atakuwa ni mtakatifu, kwasababu amemjua Mungu, kadhalika atakuwa anamheshimu Mungu na kumwogopa, kutokana na ufunuo mzito alioupata kumhusu Yeye (Yesu).

Lakini Yule anayesema  tu “Yesu ni Bwana” bila Roho, maana yake hamjui Yesu, hana mpango na maneno yake, hana  ufunuo wowote alioupata unaomfanya  yeye aseme hivyo, mtu wa namna hiyo kutamka kwake hakuna manufaa yoyote, ndio maana hapo biblia inasema.. “mtu hawezi kusema Yesu ni Bwana isipokuwa katika Roho Mtakatifu”..maana yake atakuwa anasema tu kimdomo, na si kwa kuelewa na kumaanisha.

Bwana Yesu alisema maneno haya…

Mathayo 7:21 “SI KILA MTU ANIAMBIAYE, BWANA, BWANA, ATAKAYEINGIA KATIKA UFALME WA MBINGUNI; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22  Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23  Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Umeona?.. Kusema tu “Yesu ni Bwana” bila ya kuwa na badiliko halisi la ndani, ambalo hilo linaletwa na Roho Mtakatifu mwenyewe, ni kazi bure!.. Vile vile huwezi kuwa na Roho Mtakatifu halafu useme Bwana Yesu kalaaniwa.. hilo haliwezekani.

Hivyo ili tuyafanye mapenzi ya Mungu, na maneno ya midomo yetu pamoja na sala zetu zikubalike mbele za Mungu, hatuna budi kuzaliwa mara ya pili, na kuzaliwa mara ya pili kunakuja kwa kutubu dhambi, kwa kumaanisha kuziacha, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi pamoja na kupokea Roho Mtakatifu.

Baada ya hapo, lolote tunalolitamka la kumwadhimisha Mungu, kumsifu, kumwomba, na kumkiri linakuwa katika Roho, na hivyo linaleta matokeo makubwa sana. Lakini kama hatutatubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, hata sala zetu zinakuwa ni bure, hata sifa zetu kwake zinakuwa ni bure…

2Timotheo 2: 19  “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

Rudi nyumbani

Print this post

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Bwana Yesu alitupa dalili za kurudi kwake, akatuambia mkiona dalili Fulani Fulani kama vile matetemeko, mlipuko wa magonjwa, manabii wa uongo, vita n.k. Basi tujue yupo mlangoni kurudi. Lakini kamwe hakutupa dalili ya SIKU yenyewe atakayorudi itakuwaje.. Na hiyo ndio hatari Zaidi kwasababu watu wengi leo hii japokuwa wanajua Yesu atarudi siku yoyote kutokana na kuwa dalili hizo zimeshatimia zote, Lakini bado wanachunguza chunguza siku yenyewe, wakidhani  labda watashtukia lolote.

Bwana Yesu alisema siku ya kuja kwake, inafanana na siku zile za Nuhu, Siku zile mpaka Nuhu anaingia kwenye Safina hakuna mtu yeyote alitambua kuwa tayari Mungu ameshaihukumu dunia.. mpaka zikapita siku saba, nyingine ndipo mvua ya gharika ikashuka kwenye dunia.

Mathayo 24:38 “Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina,

39 WASITAMBUE, HATA GHARIKA IKAJA, IKAWACHUKUA WOTE, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

40 Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;

41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.

42 Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu”.

Unaona? Leo hii, kama wewe sio “bibi-arusi” wa kweli wa Kristo, nikimaanisha, kama sio mkisto aliyesimama katika wokovu kweli kweli, usitazamie utatambua lolote siku  Kristo anarudi kuwanyakua watakatifu wake. Kwasababu hata Bibi-arusi wake mwenyewe hatojua siku hiyo itakavyokuwa sembuse wewe?..

Na ndio maana aliwaambia mpaka na wateule wake, kwamba wajiweke tayari, waifanye kazi yake, watimize wajibu wao walioitwa hapa duniani wa kuitangaza injili yake, kwasababu saa wasiodhani ndio atakayokuja..

Mathayo 24:43 “Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.

44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika SAA MSIYODHANI MWANA WA ADAMU YUAJA.

45 Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47 Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.”

Hakuna mtu atakayeitambua siku hiyo, itakuja ghafla tu bila hodi, hakuna dalili yoyote itakayotutambulisha, itakuwa kama tu ilivyo leo, au jana,  wakati ambapo watu wanapanga mipango yao ya kimaisha, wanalijenga taifa lao, wanauza pombe, na kufanya biashara hapo hapo, Unyakuo unapita , mmoja anatwaliwa mmoja anaachwa..

Watu wengi sana wataingiwa na butwaa, wakisema mbona Bwana hakutupa taarifa au kiashirio fulani, mbona, angani hakukuonekana chochote, mbona tulitazamia jambo Fulani kwanza tulione, ndio unyakuo upite, imekuwaje, amesharudi, wakati watu wengine hawajahubiriwa bado injili. Lakini ndio hivyo tayari watakatifu wameshaondolewa.

Wakati huo upo karibu sana ndugu yangu, ridhika na dalili tunazoziona, kwasababu hakutakuwa na nyingine Zaidi ya hizo zilizoandikwa kwenye biblia.  Usidhani malaika atatokea hapo mawinguni kutuhubiria injili kwamba kesho Yesu ndio anarudi.

Kama utakosa unyakuo, basi ujue, utakuwa katika majuto na vilio na kusaga meno kusikokuwa kwa kawaida. Majuto hayo, unaweza ukayaona sio kitu leo kwasababu bado hayajakukuta, lakini  subiri siku hiyo ikufikie, hutatamani uishi. Hicho kiburi cha uzima ulichonacho leo, siku hiyo kitayeyuka chote, utamtafuta Mungu hutamwona. Utalia hakuna atakayekusikia, makanisa yatakuwa hayana faida yoyote kwako. Hakuna chochote kitakuwa na maana kwao, kwasababu hata pesa hazitafanya kazi wakati huo.

Ndugu, ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho bado unayo nafasi ndogo sana ya kutubu, Tubu leo kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako, na Kristo atakupokea.

Shalom.

Kumbuka katika saa usiyodhani Kristo anakuja!

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

MATESO YA KUZIMU.

Rudi nyumbani

Print this post