ITAKUFAIDIA NINI?

ITAKUFAIDIA NINI?

Marko 8:34  “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.

35  Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.

36  Kwa kuwa ITAMFAIDIA MTU NINI KUUPATA ULIMWENGU WOTE, AKIPATA HASARA YA NAFSI YAKE?

37  Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake”

Kufaidia maana yake “mtu atapata faida gani, aupate ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake”.

Umepata majumba yote, fedha zote duniani ni zako, magari yote ni ya kwako, madini yote (fedha, dhahabu, almasi) ni yako, ardhi yote dunia ni yako, na kila kitu ni chako, yaani hakuna kisicho chako..Halafu umekufa umejikuta jehanamu!!…Swali tunaulizwa na aliyeacha Mbingu za mbingu akaja duniani, aliyeacha Milki, aliyeacha utajiri, na kushuka duniani kwenye mavumbi…anatuuliza swali… ITATUFAIDIA NINI KUPATA HAYO YOTE HALAFU TUMEPATA HASARA ZA NAFSI ZETU???.

Huyo huyo aliyeacha mbingu na utajiri mbinguni anasema mahali Fulani..

Marko 10:22  “Walakini yeye akakunja uso kwa neno hilo, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

23  Yesu akatazama kotekote, akawaambia wanafunzi wake, JINSI ITAKAVYOKUWA SHIDA WENYE MALI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU!

24  Wanafunzi wakashangaa kwa maneno yake. Yesu akajibu tena, akawaambia, WATOTO, JINSI ILIVYO SHIDA WENYE KUTEGEMEA MALI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU!

25  Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu ya sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”.

Anasema.. “jinsi ilivyo shida”…sio kwamba “haiwezekani kabisa”..inawezekana lakini… “JINSI ILIVYO SHIDA !!!”.

Mpaka Bwana mwenyewe anasema “Ni shida!”.. tena anakwambia ni rahisi ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia kwenye ufalme wa mbinguni!!!…. Sentensi hiyo moja kwa moja, inaonyesha jambo ambalo uwezekano wake ni mdogo sana… Kwasababu mpaka leo hii bado huo muujiza haujatendeka wa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano!!!…. (ngamia huyo awe ngamia mnyama, au kamba..lakini bado hatujaona!!)..

Sasa basi kama uwezekano wake ni mdogo hivyo!!!….Kwanini tunajisumbua sana kutafuta hayo mambo????.

Mithali 23:4 “USIJITAABISHE ILI KUPATA UTAJIRI; Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe”.

Ni kweli, Ukimuomba sana Mungu akupe utajiri, na ukiutafuta utaupata..na atakupa nguvu za kuupata kulingana na Neno lake, lakini kumbuka pia…

UNAZIDI KUIFANYA NJIA YAKO YA KUINGIA MBINGUNI KUWA NYEMBAMBA ZAIDI. Kwasababu wewe unakuwa Ngamia, na Mlango wa Mbinguni unakuwa tundu la sindano..

Ushauri huo ametupa!!…yeye aliyetoka mbinguni, ambaye anaujua kila kitu!.. ameona si vyema atuambie tu! Ni ngumu?..bali aonyeshe na mfano wake!..Ni sisi kuchagua kujitanua kuzidi kuwa ngamia, au kujitajirisha katika mambo ya ufalme wa Mbinguni.

Na kwanini katika ule mfano alimwambia Yule kijana akauze kila kitu awape maskini kisha amfuate??…Si kwasababu Bwana Yesu alikuwa anataka kumfukarisha, bali alitaka kumtoa mungu-mali katika moyo wake na kumpa moyo wa unyenyekevu ambao utamtegemea Mungu..ambao huo pekee ndio Mungu anaweza kutembea nao..na si ule moyo wa kiburi cha mali aliokuwa nao. Na kamwe asingeweza kukosa chakula, baada ya pale, kwasababu angekuwa tu kama mmoja wa mitume wake (wakina Petro), labda angekuwa ni mtume wa 13, kwasababu wakina Petro nao, waliambiwa waache nyavu zao wamfuate Bwana. Lakini katika kumfuata kwao kote Bwana hawajawahi kufa njaa, wala kupungukiwa.

Dada/Kaka inawezekana umehubiriwa sana na kuombewa upate mali na utajiri!! … Leo mimi nakushauri ushauri , ushauri ule ule Bwana aliotupa!… “Kwa kuwa ITAMFAIDIA MTU NINI KUUPATA ULIMWENGU WOTE, AKIPATA HASARA YA NAFSI YAKE?”.

Wengi wa wanaokuhubiria kwamba “Njoo uwe tajiri” ni kwasababu wanatafuta kitu kutoka kwako!!..wanataka wapate kitu kutoka kwako, lakini hawataki Roho yako iende mbinguni, ndio maana hawatakuambia kamwe hili neno >> “JINSI ITAKAVYOKUWA SHIDA WENYE MALI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU!”..

Itakuwa ni shida!.. Itakuwa shida!..

Bwana anasema tujikane nafsi, tunapoanza kumfuata Yesu, ni wakati wa kupunguza mizigo yetu, hata ikiwezekana mali, na si kuiongeza.. ili zisitusonge kuingia mbinguni… si wakati wa kutia jitihana kutafuta utajiri!!!.. Ni wakati wa kuupunguza..Kama  kazi yako ya Bar ndio iliyokuwa inakupa utajiri na mali! Unaiacha…Ni rushwa ndio zilikuwa zinakutajirisha unaacha…

Ulikuwa una maduka matau yaliyokuwa yanakufanya ufanye kazi masaa 24, hebu punguza bakiwa na moja tu! Litakalokufanya ufanye kazi masaa 8 au chini ya hapo, ili upate muda wa kuutafuta uso wa Mungu.. Muda wa kuishi hapa duniani haikusubirii. Itakufaidia nini upate kila kitu halafu upate hasara ya nafsi yako???..Au utatoa nini kuifidia hiyo nafsi siku ile??.

Luka 21:33  “Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

34  Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo”.

Kama nitakula chakula cha aina moja kila siku, halafu nitapata muda wa kusali na kusoma neno kwa utulivu kila siku, si ni heri kuliko nile mboga saba, nikae chini ya dari zuri, halafu nakosa hata muda wa kusoma Neno na kuomba!!.. Ni heri niwe mtu wa daraja la chini kabisa lakini ni Tajiri wa Roho kuliko niwe mtu wa daraja la kwanza halafu ni ngamia katika roho, ambaye sitaweza kupenya kuingia katika ufalme wa Mungu!!.. Ni heri niwe na rafiki maskini ambaye atanifundisha na kunishurutisha kumcha Bwana, kuliko niwe na rafiki tajiri ambaye atanipeleka mbali na Mungu.

Bwana mkuu wa hekima zote atusaidie tuweze kuyatafakari mashauri yake na kuchukua uamuzi sahihi.

Kama hujampokea Yesu, kumbuka tupo mwisho wa nyakati, na Hukumu ya ulimwengu huu ni juu ya wale wote waliomkataa Yesu na maneno yake. Hivyo mgeukie leo, tubu dhambi zako kwake, na yeye atakusamehe na kukupokea na kukufundisha.

Maran atha!!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Zainab Shakiru.
Zainab Shakiru.
2 years ago

Mungu awabariki kwa kujitoa kwa moto mmoja kpeleka injiri yake.