Title December 2021

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 4)

Nakusalimu katika jina kuu sana  la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu katika kujifunza Neno la Bwana. Bado tupo katika mwendelezo wa thawabu mbalimbali za Mungu, na vigezo anavyovitumia kuzitoa. Hii sehemu ya 4.

4) Zipo thawabu kwa wanaowasadia  maskini na wasiojiweza.

Bwana Yesu alimwambia yule Farisayo Tajiri aliyemwalika katika karamu yake maneno haya;

Luka 14:12 “Akamwambia na yule aliyemwalika, Ufanyapo chakula cha mchana au cha jioni, usiwaite rafiki zako, wala ndugu zako, wala jamaa zako, wala jirani zako wenye mali; wao wasije wakakualika wewe ukapata malipo.

13 Bali ufanyapo karamu waite maskini, vilema, viwete, vipofu,

14 nawe utakuwa heri, kwa kuwa hao hawana cha kukulipa; kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki.

15 Basi aliposikia hayo mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye alimwambia, Heri yule atakayekula mkate katika ufalme wa Mungu”.

Ikiwa wewe ni mtakatifu Umeokoka, usisahau, kuwakumbuka watu wenye mahitaji, na wasiojiweza kwa kile Mungu alichokujalia, kwasababu kina thawabu yake kubwa mbinguni siku ile Bwana atakapowafufua wateule wake ili kuwapa thawabu.

Unapotoa msaada, au unapofanya sherehe, usiwaalike tu, watu wenye uwezo, bali tafuta na wengine wasio na kitu cha kukurudishia, tusiwaalike watu tu waliotuchangia, bali tuwaalike pia, na wasioweza kuchangia, kwasababu, tutakuwa tumejiwekea hazina nzuri mbinguni.. Mtume Paulo alikuwa na bidii kulifanya hilo, pale alipousiwa na mitume waliomtangalia. Alisema..

Wagalatia 2:9 “tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; Yakobo, na Kefa, na Yohana, wenye sifa kuwa ni nguzo, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;

10 ila neno moja tu walitutakia, tuwakumbuke maskini; nami neno lilo hilo nalikuwa na bidii kulifanya”.

Unaona? Hivyo na sisi tuwaonapo maskini, na mayatima, na wenye mahitaji, basi tujue hapo ni mahali petu pa kujichumia thawabu zetu nyingi, tufanye bidi kuwasaidia. Kwasababu tukifika mbinguni, utajiri wetu, utapimwa kwa matendo kama haya, lakini kama kila tulichokuwa tunakipata, tunakula wenyewe, au na watu wenye uwezo kama sisi, tujue kuwa tunapunguza kiwango cha utajiri wetu mbinguni. Kutoa si mpaka tuwe na vingi, ukipata sh.100, inatosha, kuwaga 50, kwa maskini na nyingine ukatumia wewe.

Bwana atusaidie tulione hilo, tuanze sasa kuwakumbuka na watu wengine wenye uhitaji.

Bwana akubariki.

Usikose mwendelezo..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini hatuirithi neema kama tunavyoirithi dhambi?

Kristo atukuzwe! Kama dhambi ilikuja kupitia mtu mmoja (Adamu), na kila aliyezaliwa ameirithi, kwanini Neema iliyoletwa na Bwana Yesu hatujairithi, yaani wote wanaozaliwa wasiwe na dhambi?


Jibu: Ni kweli maandiko yanasema katika Warumi 5:12-21, Kwamba kwa kupitia mtu mmoja Adamu dhambi iliingia, na hivyo na sisi uzao wake wote tukaingia katika hali ya kukosa (yaani tukazaliwa huku tumerithi dhambi)..

Lakini swali ni je kwanini haipo hivyo kwa Bwana, kama yeye anafananishwa na Adamu wa pili, kwanini na sisi tusizaliwe hali tumeirithi hiyo neema bila kupitia hatua nyingine hizo za wokovu?.

Jibu ni kwamba, hatujairithi Neema kwa namna ya kimwili kwasababu Bwana Yesu hajatuzaa katika mwili kama Adamu alivyotuzaa sisi katika mwili.

Endapo Bwana angetuzaa upya watu wote katika mwili, kama vile Adamu alivyotuzaa kupitia Hawa, basi na sisi tungeirithi hiyo neema kwa njia ya mwili na kungekuwa hakuna haja ya kupitia hizo hatua za wokovu.

Lakini kwasababu Bwana hakuwa na mke, na wala hajazaa kwa namna ya mwili, kwasababu kama angekuja kwa njia hiyo ya kuzaa katika mwili basi wangezaliwa wanadamu wengine ambao ni uzao wa Bwana ulio mkamilifu kama Bwana, na hivyo sisi wengine ambao ni uzao wa Adamu ambao tumekwishazaliwa tayari tungekuwa bado tupo kwenye dhambi..na hapo kungekuwa hakuna wokovu.

Lakini ashukuriwe Mungu, Kristo hakuja kuleta uzao mwingine duniani bali kuukomboa ule ambao tayari upo, (yaani sisi tulio uzao wa Adamu).

Hivyo ni lazima Bwana aje na mpango mwingine wa kutuzaa katika roho na si katika mwili, ili tuwe uzao wake katika roho, na tuzirithi ahadi zake hizo katika roho..Ndio maana Bwana Yesu alisema hatuna budi kuzaliwa mara ya pili katika Roho.

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.

Umeona hapo?

Na tunazaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho, yaani kwa Ubatizo wa maji na Kwa Ubatizo wa Roho Mtakatifu.

Maana yake ni kwamba mtu aliyebatizwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu (Matendo 2:38, Yohana 3:23), na akapokea Roho Mtakatifu anakuwa tayari amezaliwa mara ya pili, na hivyo ni mzao wa Bwana Yesu katika Roho. (Na tayari kapata ukombozi wa roho yake).

Ukombozi wa miili yetu utakuja siku ile ya unyakuo itakapofika (Waefeso 4:30), wakati parapanda itakapolia tutakapovikwa miili mipya ya utukufu isiyo na kasoro.

Swali ni je!. Mimi na wewe tumezaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho, kumbuka Bwana anasema mtu asiyezaliwa mara ya pili hawezi kuurithi uzima wa milele.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Noeli ni nini, na je! Neno hili linapatikana katika biblia?

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

JE! USIPOTIMIZA NADHIRI ZAKO ZOTE KWA BWANA. HAWEZI KUKUSAMEHE?

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 3)

Shalom, huu ni mfululizo, wa Makala ambazo zinaeleza vigezo ambavyo Mungu, atavitumia kuwapa watu wake thawabu mbalimbali, au atakavyovitumia kuwakaribisha katika ufalme wake, hii ni sehemu ya tatu, ikiwa hukupitia sehemu zilizotangulia utatumia ujumbe inbox tukutumie chambuzi zake.

3) Biblia inatuonyesha kuna watu watu wataingizwa katika ufalme wa Mungu, bila kutambua sababu.

Inashangaza lipo kundi la watu ambalo litapewa neema ya kuungia ufalme wa Bwana wetu Yesu Kristo, bila lenyewe kutambua sababu mpaka litakapofunuliwa na Kristo mwenyewe siku ile.

Tunalisoma kundi hilo katika vifungu hivi.

Mathayo 25:31 “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;

32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;

33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.

34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;

35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele”.

Kundi hili, ni lile, lilowahifadhi, watumishi wa Kristo, wakiwa hapa duniani, wasijue kuwa walikuwa wanamtendea Kristo mwenyewe, hapa hazungumzii maskini, na omba omba, au  mayatima hapana, wanaowahudumia hao wanayothawabu yao, ambayo tutaiona katika Makala inayofuata, bali wanaozungumziwa hapa ni watakatifu wa Bwana, ambao kutokana na maisha yao ya  utumishi, walipitia kupungukiwa, kuumwa, kukosa chakula, nguo, makazi n.k. Sasa wapo ambao waliwaona na kuwahifadhi, wasijue kuwa wanamtendea Kristo mwenyewe.

Sasa siku ile itakapofika, hawa watumishi wa Bwana watasimama na kuwataja mbele ya Kristo, na kwasababu hiyo Kristo atawapa neema ya kuuingia ufalme wake. Sawasawa na ule mfano wakili dhalimu tunaousoma katika Luka 16:1-12.

Mtume Paulo aliwaombea rehema ndugu wa mtu mmoja aliyeitwa Onesiforo, kwa jinsi walivyomtunza na kumuhudumia kwa mahitaji mbalimbali alipokuwa anahubiri.

2Timotheo 1:16 “Bwana awape rehema wale walio wa mlango wake Onesiforo; maana mara nyingi aliniburudisha, wala hakuuonea haya mnyororo wangu;

17 bali, alipokuwapo hapa Rumi, alinitafuta kwa bidii akanipata.

18 Bwana na ampe kuona rehema machoni pa Bwana siku ile. Na jinsi alivyonihudumia kwa mengi huko Efeso, wewe unajua sana”.

Vivyo hivyo, na wale ambao, wanawaona watu wanaomtafuta Mungu, ni kama mizigo kwao, wanawadhihaki, wanawatukana, wanawafukuza, hata wakiomba maji wanawaona ni wavivu. Watu ambao wanaposikia watumishi wa kweli wa Mungu ni kama kero kwa kwao, Watu kama hawa upo wakati Kristo naye atawakana.

Inatufundisha nini?, tukisema tunampenda Kristo, tunamaanisha kuwa tunawapenda na wale wampendao, kama unawachukia watakatifu, utampendaje Kristo?. Hivyo, wapo watu ambao Kristo atawakaribisha kwa namna hii,. Vilevile wapo watu ambao Kristo atawafukuza kwa namna hii. Kwasababu hawakumkaribisha Kristo kwao.

Shalom.

Usikose mwendelezo..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)

Tumetazama, wapo watu ambapo siku ile ya hukumu, watalipwa thawabu sawa na wale ambao wameteseke Maisha yao yote katika kumtumikia Mungu. Na kigezo chenyewe kwanini Mungu afanye hivyo, tumeshakiona katika maandiko, ikiwa hujapata uchambuzi wake, tutumie ujumbe, inbox tukutumie..

Tutaendelea, na vigezo cha pili cha thawabu, za Mungu. Hichi tunakisoma katika Mathayo 24:44-51

2) Kwamba wapo watu watawekwa juu ya kazi yote ya Mungu, mbinguni.

Unaweza kujiuliza, Je! Inamaana kuna watu ambao hawatawekwa, juu ya kazi za Mungu siku ile? Jibu ni ndio, twende moja kwa moja katika Habari hii, tuone ni kigezo gani, Kristo anakitumia, katika kutoa thawabu kama hiyo.

Mathayo 24:44 “Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

45 Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47 Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

48 Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

49 akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;

50 bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51 atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

Katika Habari hiyo, tunaona, mtu mmoja Tajiri aliondoka bila kutoa taarifa ya lini atarudi, lakini akamwacha mtumwa wake mmoja awe mwangalizi wa watu wake, ahakikishe anawahudumia, pasipo kusimamiwa. Lakini anasema kama mtumwa huyo atadhani kuwa Bwana wake atachelewa. akaanza kuwa mzembe, mara hawapi watu chakula, mara anawapiga, mara anaamrisha vibaya. Siku asiyodhani atakuja, na kumkata vipande vipande.

Lakini akimkuta yupo katika majukumu yake, basi ameahidi, kuwa atamweka juu vitu vyake vyote.

Leo hii kama wewe ni mtumishi wa Mungu, aidha mchungaji, nabii, mwalimu, mtume, mwimbaji, au unafanya kazi yoyote ile ya kuujenga ufalme wa Mungu..Fahamu kuwa Bwana anataka kukuona, wakati wote, muda wote, ukitumika kwa uaminifu katika hiyo kazi, ili siku atakapokujia ghafla (aidha kwa kifo au unyakuo ) akukute katika utumishi wako.

Lakini ukianza kuidharau kazi ya Mungu na kuigeuza kama vile biashara, hutaki kutumika mpaka ulipwe, hutaki kusimamia kundi lako kama mchungaji, unazini na washirika,  hutaki kuwafundisha watu kama mwalimu, unaona uvivu wa kuwahubiria wengine Habari njema, kama mwinjilisti, unamgeuza Mungu kama mtu baki, unamtumikia tu pale unapojisikia, ukiwa huna mudi, unaendelea na mambo yako.

Ndugu, thawabu kama hii itakupita, Kazi ya Mungu inapasa iwe ni sehemu ya Maisha yako, ikiwa umeitwa kweli na Bwana, usiruhusu mapengo pengo yasiyokuwa na lazima yakusonge, mpaka kusudi lote liyeyuke ndani yako.

Lakini ukisimama katika nafasi yako, kama vile, huyu ambaye Bwana Yesu alimzungumzia hapo kwamba alimkuta anawapa watu wake chakula kwa wakati, aliahidi kumweka juu ya kazi yake yote.

Katika huo ufalme wa milele unaokuja huko, zitakuwepo kazi na majukumu, na hivyo, tangu sasa Bwana anatafuta watakaozisimamia kama viongozi kazi hizo za kimbinguni tukufu sana. Na watakaopewa nafasi hizo za kipekee ni wewe na mimi endapo tutakuwa tunagawa posho la Bwana kwa wakati.

Hivyo tuamke, kama tulikuwa tunalegea mahali, tuanze kuitenda kazi ya Bwana kwa bidii mpya.

Bwana akubariki.

Usikose mwendelezo..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

Bwana Yesu asifiwe, katika Makala hizi, tutazama vigezo ambavyo Mungu atavitumia kutoa thawabu zake, tutakapofika kule ng’ambo, Hii itatusaidia kuzidisha hamasa zetu katika kumtumikia Mungu, kama vile mtume Paulo, alivyoliona hilo, mpaka akasema..

Wafilipi 3:14 “nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu”.

 Tutapitia baada ya vifungu, ambavyo vitatupa picha jinsi thawabu hizo Mungu atakavyozigawa; Kigezo cha thawabu ya kwanza tunakisoma katika Mathayo 20:1-16

  1. Wapo watu watafanya kazi kidogo, lakini watalipwa sawasawa na wale waliofanya kazi nyingi.

Unaweza ukasema ni kwanini Mungu afanye hivyo? Embu tupitie Habari hii, tutapata majibu yote.

Mathayo 20 : 1-16

“1 Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.

2 Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.

3 Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;

4 na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.

5 Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.

6 Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?

7 Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.

8 Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia msimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza.

9 Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari.

10 Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.

11 Basi wakiisha kuipokea, wakamnung’unikia mwenye nyumba,

12 wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa.

13 Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari?

14 Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.

15 Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema?

16 Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho”.

Lakini ni wakina nani hawa, ambao, watakuja kulipwa sawasawa na wale waliotaabika katika kazi ya Mungu kwa muda mrefu.

Ukitazama, utaona, wale wa mwisho, hawakuwa wanashughulika mahali popote hapo kabla.. Bali mwenye shamba alipowafuata na kuwauliza kwanini mmesimama hapa mchana kutwa wakasema “Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri”.. Hii ikiwa na maana kama wangebahatika kufuatwa na mwenye shamba tangu asubuhi nao pia wangefanya kazi kubwa tu kama wale wengine, lakini hakutokea mtu wa kuwaajiri mpaka jioni.

Ikifunua kuwa, kuna watu mpaka sasa bado hawajafikiwa na neema ya wokovu, na pengine umri umeenda, labda tuseme mpagani Fulani mwabudu ng’ombe, lakini akiwa na miaka 80, ndio anahubiriwa injili na kuokoka kwa kumaanisha, na baada ya hapo anakuwa tayari kumtumikia Mungu kwa moyo wake wote, pengine akamtumikia Mungu kwa uaminifu kwa mwaka 1 tu akafa.

Au mwingine, neema imemkuta katika ujana wake, labda miaka 20 tu, lakini akatumika miaka 2 tu, alipofikisha miaka 22 akafariki.

Sasa watu kama hawa, kama walitumika kwa uaminifu kwa muda huo mfupi tu. Usishangae kuwakuta kule ng’ambo wamepewa thawabu sawa mitume. Ni kwanini? Ni kwasababu wakati neema inawafikia, na muda wao wa kutumika ulipokuja, waliandikiwa muda mchache sana. Hivyo kama wangekutwa tangu zamani ni wazi kuwa wangemtumikia Mungu kwa uaminifu.

Lakini,ikiwa wewe leo hii unaisikia neema, unaichezea, leo upo na Kristo, kesho upo na shetani, yaani hueleweki, usitazamie, Kristo atakupa thawabu yoyote, ikiwa utakufa leo katika hali kama hiyo, yaani umezaliwa katika familia ya kikristo, unajua kabisa misingi ya kiimani kwamba, pasipo wokovu huwezi kwenda popote, usitazamie, utalingana na yule mpagani au mtu wa dini nyingine ambaye kaokoa hivi karibuni, halafu akafa.

Bwana alisema wamwisho watakuwa wa kwanza, na kwanza watakuwa wamwisho. Ithamini neema uliyopewa , hizi ni siku za mwisho.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu alie machozi, na ilihali yeye ni Mungu?

Jibu: Tusome,

Yohana 11:32 “ Basi Mariamu alipofika pale alipokuwapo Yesu, na kumwona, alianguka miguuni pake, akamwambia, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa.

33 Basi Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliofuatana naye wanalia, aliugua rohoni, akafadhaika roho yake,

34 akasema, Mmemweka wapi? Wakamwambia, Bwana, njoo utazame.

35 Yesu akalia machozi.

36 Basi Wayahudi wakasema, Angalieni jinsi alivyompenda.

37 Bali wengine wao wakasema, Je! Huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”

Ukisoma kwa makini habari hiyo utaona Bwana Yesu hakulia machozi kwa sabababu ya uchungu wa msiba, bali alilia kwasababu ya ugumu wa mioyo yao katika kumwamini Mungu.

Bwana hakuwa na uchungu na msiba kwasababu yeye ndiye ufufuo na uzima, alijua dakika chache mbeleni Lazaro atakuwa hai.

Lakini kitendo cha wale wafiwa walivyokuwa wanahuzunika, na kutokuamini kama Lazaro anaweza kuwa hai tena, na walivyokuwa wanalia kwa uchungu kama watu waliopoteza tumaini, kitendo hicho kilimuhuzunisha sana Bwana mpaka akalia machozi.

Amekaa nao mara nyingi, wamesikia akifufua wafu mara nyingi lakini bado walikuwa hawaaamini kama Mungu anaweza kumfanya akawa hai tena, ni jambo la kuhuzunisha sana..

Yohana 11:38 “Basi Yesu, hali akiugua tena nafsini mwake, akafika kwenye kaburi. Nalo lilikuwa ni pango, na jiwe limewekwa juu yake.

39 Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.

40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?

41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia.

42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.

43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje”.

Utaona pia mara kadhaa, Bwana alihuzunishwa na Mafarisayo..

Marko 3:1 “Akaingia tena katika sinagogi; na palikuwako huko mtu mwenye mkono uliopooza;

2 wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato; wapate kumshitaki.

3 Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, Simama katikati.

4 Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza.

5 Akawakazia macho pande zote kwa hasira, AKIONA HUZUNI KWA AJILI YA UGUMU WA MIOYO YAO, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.

6 Mara wakatoka wale Mafarisayo, wakawa wakifanya shauri juu yake pamoja na Maherodi, jinsi ya kumwangamiza”.

Na hata sasa Bwana analia machozi, kwasababu ya ugumu wa mioyo yetu, Hata sasa tunamhuzunisha Mungu kwa kutomwamini kwetu, na hata wakati mwingine tunapomjaribu.

Hivyo hatuna budi kuishi maisha ya Imani, ili tumpendeze Mungu.

Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza…”

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

UYATIE MACHOZI YANGU KATIKA CHUPA YAKO EE! BWANA.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

Rudi nyumbani

Print this post

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Unaweza ukajiuliza Je shetani anaweza kuwazuia watu wasihubiri injili?

Jibu ni ndio Tusome,

1 Wathesalonike 2:17 “Lakini ndugu, tukiwa tumefarakana nanyi kwa kitambo, kwa uso si kwa moyo, tulizidi kutamani kwa shauku nyingi kuwaona nyuso zenu.

18 Kwa hiyo tulitaka kuja kwenu, naam, mimi Paulo, mara ya kwanza, na mara ya pili, na Shetani akatuzuia”.

Kulingana na maneno hayo ya Mtume Paulo, ni wazi kuwa shetani anahusika pakubwa sana katika kuizuia injili.

Siku zote shetani ni adui wa injili hakuna mahali alishawahi kukubaliana na watu kuipeleka injili. Hataki injili ihubiriwe kwasababa anajua ni uweza wa Mungu uletao wokovu. (Warumi 1:16).

Na yeye hataki kamwe watu wapate wokovu, anataka wasiisikie injili ili wafe katika dhambi zao na wajikute katika hukumu kama yeye siku ile ya mwisho.
Kwahivyo atafanya juu chini aizuie injili.
Sasa swali anaizuiaje?.

Anaizuia kwa kunyanyua matukio ambayo yataikwamisha safari ya kwenda kuhubiri.
Kwamfano akina Paulo labda walipanga kwenda huko Thesalonike lakini tarehe walizopanga kwenda hakukuwa na mashua za kuelekea huko au tufani zilianza kiasi kwamba haiwezekani kuanza safari kwa kipindi hicho.

Au wakati wameanza tu safari kufika maili kadhaa mbelen baharini ikachafuka, jahazi likavunjika, hivyo safari kuishia pale.

Au unakuta wamepanga safari vizuri tu inatokea wanapoteza nauli au wanaibiwa, hivyo safari inakuwa imeisha hapo.
Au wamepanga safari, ghafla mmojawao anaugua n.k.

Hayo ndio mambo shetani anayoyafanya kuizuia injili, na zaidi ya yote Mtume Paulo mwenyewe aliyashuhudia hayo mambo wanayokutana nayo katika safari zao za kwenda kuhubiri.

2 Wakorintho 11:25 “Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;

26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;

27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi”.

Mambo hayo pia yaliwatokea wanafunzi wa Bwana Yesu walipokuwa wanavuka kwenda nchi ya Wagerasi, wakiwa katikati ya safari baharini, shetani alijaribu kuwazuia kwa kuwaletea tufani kubwa, shetani alitaka kuwazuia kwasababu aliona kuna watu wawili kule nga’ambo wenye pepo wanaishi makaburini, wanakwenda kufunguliwa, hivyo hilo jambo hawezi kuliruhusu, ndipo akawaletea tufani njiani, mpaka Bwana alipoamka na kuinyamazisha.(Mathayo 8:23-34).

Hivyo kilichomtokea Paulo na Wanafunzi wa Bwana Yesu kinaweza kumtokea mhubiri yeyote yule, haijalishi umeitwa kwa wito gani kamwe shetani hawezi kuruhusu wewe uhubiri injili kirahisi, ni lazima atakupinga tu.

Sasa swali kama hivyo ndivyo tunapaswa tufanyeje kila tunapotaka kwenda kuhibiri injili?.

Bwana Yesu alitupa dawa ya kuepukana na majaribu ya namna hiyo, na hiyo si nyingine zaidi ya kuomba kwa bidii.
Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake mara kadhaa waombe ili wasije wakaingia majaribuni, kwasababu alijua silaha moja kubwa ya kudhoofisha vizuizi vya shetani ni kuomba, ndio maana ijapokuwa yeye mwenyewe alikuwa ni Mungu lakini alikuwa anakesha kuomba, ili kutufundisha sisi.

Na jukumu la kuomba sio tu la Mhubiri, au mchungaji, au Muinjilisti, au Mtume.

Jukumu la kuomba ni la kila mtu aliye mkristo, kila mtu anapaswa kuiombea ili injili iweze kupelekwa bila kizuizi chochote, unapotenga muda na kuiombea injili ya Bwana Yesu, hujui ni mchango gani mkubwa uliouchangia.. Kwa kuomba kwako huko unaharibu mipango ya shetani ya kumvunjia jahazi mhubiri fulani mahali fulani.

Kwa kufunga kwako kuiombea injili ya Bwana Yesu, umeharibu mipango ya wizi na magonjwa shetani aliyoipanga juu ya wahubiri fulani waliopanga kwenda kupeleka injili mahali fulani. Hivyo na wewe unakuwa ni mojawapo ya jeshi la Bwana katika kuipeleka injili mbele.

Lakini ukiacha tu na kusema.. Aaah mimi sio mhubiri, sio muinjilisti hiyo sio karama yangu, huombi, hufungi, huchangii, hufanyi chochote, basi fahamu kuwa unaupa nguvu ufalme wa giza.

Ndio maana Mtume Paulo baada ya kuwaandikia waraka hawa Wathesalonike kwamba ameshindwa kuja kwao shetani kamzuia, alimalizia na kuwaambia hao Wathesalonike kwamba WAMWOMBEE.

Wasikae tu wakasubiri, kwani vita ni vikali.

1 Wathesalonike 5:24 “Ndugu, tuombeeni”

Na zaidi ya yote katika waraka wake wa pili aliwakumbusha tena jambo hilo hilo..

2 Wathesalonike 3:1 “Hatimaye, ndugu, tuombeeni, neno la Bwana liendelee, na kutukuzwa vile vile kama ilivyo kwenu ”.

Je na wewe unaiombea Injili ya Bwana Yesu?.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni madhara gani yatampata mtu yule anayetafsiri Neno isivyopaswa!

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Rudi nyumbani

Print this post

AKIKI NA YASPI NI MADINI GANI?

Akiki ni aina ya madini inayokaribia kufanana kimwonekano na madini ya Marijani (Rubi). Kwa lugha ya kiingereza madini ya Akiki yanajulikana kama “Sardius”. (Tazama picha juu).

Na madini ya Yaspa ni aina nyingine ya madini, ambayo rangi yange ni ya kahawia (Tazama picha chini), mawe haya kwa kiingereza ndio yanayojulikana kama “JASPER”. Kimwonekano ni mawe mazuri kama yalivyo Akiki na Marijani.

Mawe haya (Akiki na Yaspi) yametajwa katika biblia kuwakilisha Utukufu wa Mungu.

Ufunuo 4:2 “Na mara nalikuwa katika Roho; na tazama, kiti cha enzi kimewekwa mbinguni na mmoja ameketi juu ya kile kiti;

3 na yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la YASPI NA AKIKI, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi.

4 Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti naliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wamevikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji za dhahabu”.

Mwonekano wa Mungu ulikuwa ni Mithili ya Madini haya ya Yaspi na Akiki, kumbuka hapo biblia inasema ni “Mithili” na sio Mwonekano halisi. Biblia imetumia madini yetu ya kidunia yaliyo mazuri kuuelezea utukufu wa Mungu, lakini kiuhalisia Utukufu wa Mungu ni mkuu na mzuri kuliko mawe hayo, mwonekano wake hauwezi kulinganishwa na chochote. Lakini biblia imetumia mfano wa mawe hayo kuuwakilisha utukufu wa Mungu, ili tuweze kujua kuwa kwa Mungu kuna uzuri.

Vile vile tunasoma mji ule mpya ushukao mbinguni (Yerusalemu Mpya), umepambwa kwa mawe hayo mazuri (Akiki na Yaspi).

Ufunuo 21:17 “Akaupima ukuta wake, ukapata dhiraa mia na arobaini na nne, kwa kipimo cha kibinadamu, maana yake, cha malaika.

18 Na majenzi ya ule ukuta wake YALIKUWA YA YASPI, na mji ule ulikuwa wa dhahabu safi, mfano wa kioo safi.

19 Na misingi ya ukuta wa mji ilikuwa imepambwa kwa vito vya thamani vya kila namna. Msingi wa kwanza ulikuwa YASPI; wa pili yakuti samawi; wa tatu kalkedoni; wa nne zumaridi;

20 wa tano sardoniki; WA SITA AKIKI; wa saba krisolitho; wa nane zabarajadi; wa kenda yakuti ya manjano; wa kumi krisopraso; wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili amethisto”.

Maandiko yanasema pia shetani kabla ya kuasi, alikuwa amepambwa na kufunikwa na haya mawe ya thamani.

Ezekieli 28:13 “Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, AKIKI, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, NA YASPI, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari.”

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Mbinguni ni kuzuri na si pa kukosa, tukose kila kitu katika haya maisha lakini tusiikose mbingu, kwasababu maandiko yanasema mambo tuliyoandaliwa huko jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

ZUMARIDI NI MADINI GANI?

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Ufisadi una maanisha nini katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

ZUMARIDI NI MADINI GANI?

Zumaridi ni aina ya madini yenye rangi ya kijani,

Madini haya kimwonekano ni mazuri sana,
Matumizi ya madini haya ni kama yale ya Marijani (Rubi) pamoja na Yakuti (Sapphire). Yote haya kazi yao ni moja ambayo ni kutengenezea vito vya thamani kama vile saa, pete na vitu vingine vya urembo.

Kimwonekani madini ya Zumaridi ni mazuri mno, na ni ya gharama kubwa, kama ilivyo Rubi na Yakuti.

Katika biblia madini haya ya Zumaridi yametajwa mara kadhaa.

Sehemu mojawapo na ya muhimu yalipotajwa ni katika kile kiti cha Enzi, ambapo ule upinde uliokizunguka Kile kiti cha Enzi, ulikuwa na mwonekano mithili ya madini hayo ya Zumaridi.

Ufunuo 4:3 “na yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la yaspi na akiki, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi”.

Mistari mingine inayozungumzia mawe hayo ni pamoja na Kutoka 28:18, Kutoka 39:11, Ezekieli 27:16, Ezekieli 28:13 na Ufunuo 21:19.

Biblia imetumia mawe haya kufunua uzuri uliopo katika Enzi yake, Enzi ya Mungu ni nzuri sana, mbinguni kuna makao mazuri sana tumeandaliwa, ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia. Hapo maandiko yanasema “upinde ulikizunguka mithili ya Zumaridi”..kumbe sio Zumaridi, bali mithili ya Zumaridi, maana yake ni kwamba uzuri wa mambo yaliyopo mbinguni, hauelezeki.

Biblia imetumia tu lulu na madini ya kidunia, kutusaidia angalau tulate picha, ya ni nini kilichopo kule.

Je unao uhakika wa kwenda mbinguni?.Kama hauna basi huna budi kuutafuta, kwasababu mbinguni si pa kukosa.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

YAKUTI NI MADINI GANI?

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Rudi nyumbani

Print this post

YAKUTI NI MADINI GANI?

Yakuti ni aina ya madini inayokaribiana kufanana sana na madini ya Rubi (yaani Marijani).

Madini ya Yakuti kwa lugha ya kiingereza ndio yanajulikana kama SAPPHIRE. Kazi yake ni kutengenezea vito bya thamani kama pete, saa za mkononi n.k, na thamani yake inakaribiana kufanana na ile ya madini ya Rubi, na yana muonekano mzuri sana.

Madini ya Yakuti yapo ya aina mbili, yapo Yakuti ya manjano na Yakuti ya Samawi (yaani blue).

Katika biblia Yakuti ya manjano imetajwa katika mistari kadhaa..

Ayubu 28:19 “Yakuti ya rangi ya manjano ya Kushi haitasawazishwa nayo, Wala haitatiwa kima kwa dhahabu safi”.

Unaweza pia kusoma juu ya Yakuti hiyo ya manjano katika Kutoka 28:17, na Ezekieli 28:13.

Kadhalika unaweza kusoma juu ya Yakuti-Samawi katika mistari ifuatayo.. Kutoka 28:18, Kutoka 39:11 na Isaya 54:11.

Hivyo Kwaufupi madini haya kwenye biblia yametumika kuwakilisha vitu visafi na vitukufu, na vyenye heshima, kwamfano utaona kile kiti cha enzi cha Mungu, Nabii Ezekieli alichooneshwa kilikuwa ni mfano wa Yakuti-Samawi.

Ezekieli 10:1 “Ndipo nikaangalia, na tazama, katika anga lililokuwa juu ya vichwa vya makerubi, kulionekana juu yao kana kwamba ni yakuti samawi, kuonekana kama mfano wa kiti cha enzi”.

Halikadhalika katika ule mji Yerusalemu mpya, utakaoshuka kutoka mbinguni, maandiko yanasema utakuwa umepambwa kwa vito vya thamani, vya mfano Yakuti.

Ufunuo 21:19 “Na misingi ya ukuta wa mji ilikuwa imepambwa kwa vito vya thamani vya kila namna. Msingi wa kwanza ulikuwa yaspi; wa pili yakuti samawi; wa tatu kalkedoni; wa nne zumaridi;

20 wa tano sardoniki; wa sita akiki; wa saba krisolitho; wa nane zabarajadi; wa kenda yakuti ya manjano; wa kumi krisopraso; wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili amethisto”.

Kama vile tunavyoona madini ya Yakuti yalivyo mazuri, basi mbinguni kuna mazuri zaidi ya hayo tuliyoandaliwa, biblia imetaja tu Yakuti ili tuweze kuelewa na kutengeneza picha uzuri wa kule, lakini kiuhalisia vito vilivopo kule sio vya kidunia.

Mji ule Yerusalemu mpya ni mzuri sana, tujitahidi tuuingia,na tunauingia kwa kuishi maisha ya wokovu kwa uaminifu wote.

Ufunuo wa Yohana 22:14 “Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Risasi inayotajwa kwenye Ezekieli 27:12 ni ya namna gani?

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post