Title December 2021

THREE TYPES OF CHRISTIANS

I greet you in the name of our Lord Jesus Christ. Welcome to learn the glorious words of life, as we have seen them today.

Christians are divided into three main groups, which are likened to fruit trees.

And the fruit trees are of three kinds;

1) Trees that bear real fruits

2) Trees that bear no fruits

3) Trees that bear wild fruits.

Starting with Trees that produce real
Fruits.

These are the trees that the Lord Jesus spoke of in the parable of the sower, saying that the seed sown in fine soil, some yielded 30 and some 60 and some 100 (Matthew 13: 8).

He said that they were Christians who, withstanding all the temptations of the devil, persevered and were able to bear fruit for God.

Luke 8:15 “But that on the good ground are they, which in an honest and good heart, having heard the word, keep it, and bring forth fruit with patience”.

What did they endure?

They endured the hardships and tribulations the devil brought upon them from their Christianity, they were able to keep the Word of God in their hearts, by not allowing the distractions of this life to interfere with them, to the point of disregarding the Word, and this group is very small. And Christ has promised to weed it, and cleanse it so that it will continue to bear more fruit. (John 15:2)

2) Trees that do not bear any fruits.

The parable of these trees, is the one that the Lord Jesus gave example of this parable;

Luke 13:6 “He spake also this parable; A certain man had a fig tree planted in his vineyard; and he came and sought fruit thereon, and found none.

7 Then said he unto the dresser of his vineyard, Behold, these three years I come seeking fruit on this fig tree, and find none: cut it down; why cumbereth it the ground?

8 And he answering said unto him, Lord, let it alone this year also, till I shall dig about it, and dung it:

9 And if it bear fruit, well: and if not, then after that thou shalt cut it down.

These are Christians, who, once saved, are relaxed, thinking that salvation is only a verbal confession and believing, then, and after that you go on with your own affairs.

They do not want to engage in spiritual pursuits after believing and being baptized, although God daily feeds them by teaching them and preaching His ways, but they do not show any change, They are neither evil nor good. But all the while, listening to God’s Word and receiving it, the group is very large.

Christ has promised not to deal with it for too long, it will come a time when it will be cut off, and when you are cut off, your story ends there, you are spiritually dead, no matter what you say I was saved long time ago.

The Lord Jesus expects, when we are saved, to show us the works that work for our salvation, from that time on, to be beggars, fasting, to share with others the good news of salvation, to contribute to our income the work of God to move forward, etc. But we are only God’s receivers, but we do not give up with him, let us know that our journey will not be long.

3) Wild fruit-bearing trees;

An example of these trees, is this one that God spoke of in Isaiah chapter 5.

Isaiah 5: 1 “Now will I sing to my wellbeloved a song of my beloved touching his vineyard. My wellbeloved hath a vineyard in a very fruitful hill.

2 And he fenced it, and gathered out the stones thereof, and planted it with the choicest vine, and built a tower in the midst of it, and also made a winepress therein: and he looked that it should bring forth grapes, and it brought forth wild grapes.

3 And now, O inhabitants of Jerusalem, and men of Judah, judge, I pray you, betwixt me and my vineyard.

4 What could have been done more to my vineyard, that I have not done in it? wherefore, when I looked that it should bring forth grapes, brought it forth wild grapes?

5 And now go to; I will tell you what I will do to my vineyard: I will take away the hedge thereof, and it shall be eaten up; and break down the wall thereof, and it shall be trodden down:

6 And I will lay it waste: it shall not be pruned, nor digged; but there shall come up briers and thorns: I will also command the clouds that they rain no rain upon it.

7 For the vineyard of the LORD of hosts is the house of Israel, and the men of Judah his pleasant plant: and he looked for judgment, but behold oppression; for righteousness, but behold a cry.

This group is the worst, because, it is the group that bears the fruit of the other side,. These are Christians who, once saved, once they have been in the church for a long time, the things they show by their actions are the exact opposite of what Christianity should be. cheater etc and yet he says I am saved, I have been baptized, I have received the Holy Spirit, that is, in short what the worldly people do and he does, likewise, there is no difference.

This group is also very large and God has promised to remove it from its nursery (Killing).

Knowing that it is your responsibility as a Christian to examine yourself as to which group you are falling into, and what the consequences will be in the future.

Remember your in the period he has set you on earth he will come to spy. If you have been in salvation for many years and do not see anything your doing that is pleasing to God , or helping his gospel to move forward, ask yourself what are you doing? Is it cut or weeded. The answer you have, the answer I have.

So repent and turn around, receive Christ literally, and show diligence in reading his word, praying and worshipping him, then you will find the strength to bear fruits for him.

God bless you.


Related Topics:

WHATEVER YOU DO FOR CHRIST , COUNTS.

THE WILL OF THE LORD JESUS ​​TO HIS DISCIPLES.

What is the meaning of ” For the letter killeth but the spirit giveth life” (2 Corinthians 3:6)

ENTER THROUGH THE NARROW DOOR.

Home:

Print this post

Wanafunzi wa Yesu, walimaanisha nini kusema kama “Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa”?

SWALI: Wanafunzi wa Yesu, walimaanisha nini kusema kama “Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa”?


JIBU: Walisema hivyo, baada ya kusikia majibu ya swali lililoulizwa na Mafarisayo kwa Bwana Yesu. Ambapo swali lenyewe lilikuwa linahusiana na  talaka katika ndoa, Hivyo wakataka kujua je! Ni sawa mtu kumpa talaka mwanamke kwa sababu yoyote ile mtu anayoiona mbele yake?.

Waliuliza hivyo wakitazamia, majibu ya “Ndio” kutoka kwa Yesu, Lakini kinyume chake, Bwana aliwaambia, Mtu hapaswi kumwacha mke wake, kwa kila sababu anayoiona tu, labda ni mchafu, au mchoyo, au msengenyaji, au hawapendi ndugu zako, au anakudharau,  n.k. Hapana, bali sababu tu ambayo aruhusiwa kumwacha mke wake ni ile ya usherati tu, lakini nyingine hakuna..

Mitume waliposikia hayo majibu, ndipo hapo wakamwambia sasa, kama Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.. Ikiwa na maana kuwa kama sababu ni moja tu ya uzinzi? Mbona itahitaji uvumilivu mwingi sana kuiishi hiyo ndoa?.

Embu tusome…

Mathayo 19 :1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng’ambo ya Yordani.

2 Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko.

3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe KWA KILA SABABU?

4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.

7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?

8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.

9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.

10 Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.

11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.

Maana yake ni kwamba, Mwanamke anaweza akawa sio mzinzi, lakini hana heshima katika nyumba, na tayari kashakuwa mke wako, hapo hauruhusiwi kumwacha, utaendelea naye tu hivyo hivyo mpaka kifo kitakapowatenganisha, Ikiwa mke wako ni mshirikina, na haachi kufanya hivyo vitendo, hupaswi kumwacha na kwenda kuoa mwingine, utaendelea naye hivyo hivyo bila amani mpaka kufa kwako..

Ikiwa mke wako, ni mgumba, hawezi kuzaa, na mmeshaingia katika ndoa, hata kama hatazaa milele utaendelea naye hivyo hivyo bila watoto mpaka kufa kwako..hakuna kutoka nje ya ndoa.

Kanuni hii inatumika pande zote mbili pia hata kwa mwanamke, ikiwa mume wako ulipooana naye alikuwa hanywi pombe, lakini sasa hivi ni mlevi wa kupindukia na ameshindwa kurekebikika, hauruhusiwi kumwacha, utaendelea kuishi naye hivyo hivyo, mpaka kufa kwake,

Kama, alikuwa ni tajiri lakini sasa amefilisika, au kafukuzwa kazi,  utaishi naye katika hiyo hali, Kama amepata ajali ni mlemavu, au anamadhaifu Fulani ya kindoa, utaishi naye hivyo hivyo..hakuna talaka

Ndio maana Mitume wakamwambia Bwana, ikiwa mambo ya mtu na mke wake yako hivi ni heri basi mtu aishi bila kuoa, kuepuka hayo yote.

Hivyo Habari hiyo inatufundisha kuwa, kabla ya kuingia katika ndoa tutambue kuwa zipo  na changamoto zake nyingi sana,hivyo  tuwe tayari kuzibeba, Lakini kama tutaona ni nzito kwetu basi ni heri tubakie kama tulivyo, tusioe wala tusiolewe. Kwani ni vizuri Zaidi, kwa Mungu.

Mithali 21:9 “Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi…

9 Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi”.

Fikiri mara mbili,

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi nyumbani

Print this post

TWAENENDA KWA IMANI NA SI KWA KUONA.

Jina la Bwana YESU KRISTO, aliye Mkuu wa mbingu na nchi libarikiwe.

Maandiko yanasema..

2 Wakorintho 5:6 “Basi siku zote tuna moyo mkuu; tena twajua ya kuwa, wakati tuwapo hapa katika mwili, tunakaa mbali na Bwana.

7 (Maana twaenenda kwa imani, si kwa kuona.)

Leo tujifunze nini maana ya “tunaenenda kwa Imani na si kwa kuona”.

Wengi wetu tunadhani kuona kwa macho ndio njia pekee ya kulithibitisha jambo, lakini kiuhalisia kuona sio njia pekee ya kuthibitisha jambo, hata hivyo ni moja ya njia hafifu sana.

Kwa mfano macho hayawezi kupambanua ubwabwa wenye chumvi na ule usio na chumvi, maana yake huwezi kutazama ubwabwa na kujua ule umewekwa chumvi au la!. Macho yatapambanua tu aina ya chakula kilichopo mbele yako, kwamba ule ni ubwabwa na si ugali lakini hayawezi kufanya kitu kingine zaidi ya hicho.

Lakini ulimi unaweza kupambanua vyote, ubwabwa ukiwekwa kinywani ulimi unaweza kupambanua kuwa ule ni ubwabwa na si ugali, vile vile unaweza kupambanua kuwa ubwabwa ule umewekwa chumvi au la!.

Kwahiyo kuona si njia kamilifu ya kuthibitisha jambo.

Na katika mambo ya rohoni ni hivyo hivyo, maandiko yanasema “hatwenendi kwa kuona bali kwa Imani”.

Macho yetu hayana uwezo kamilifu wa kupambanua mambo ya rohoni. Ndio maana leo hii Bwana hajaruhusu tuujue uso wake, au tuwe tunamwona, ndipo tumthibitishe kwamba yupo, au tuweze kumsikia na kumwelewa.

Ni kwasababu hata tukimwona bado hatutamjua, kama vile macho yalivyo na uwezo wa kuona jambo lakini si kuonja jambo. Vivyo hivyo hata leo hii katika maisha haya tukimwona Bwana kwa macho, haitatusaidia sana, zaidi ya kumwona kwa Imani.

Leo hii watu wengi sana wanatafuta kumwona Bwana katika mwili, wengi wanafunga na kuomba Bwana Yesu awatokee kwa namna ya kimwili, wamwone na kuzungumza naye.

(Hata mimi nilishawahi kufanya hivyo, nilifunga na kuomba Bwana anitokee na kusema nami, niliendelea hivyo kwa muda mrefu mpaka Bwana aliponipa ufahamu, na kujua kuwa maombi niombayo sio ya kishujaa bali ni ya kitoto.

Kwamba sio ushujaa kutokewa na Bwana na kuzungumza naye bali ni utoto na uchanga..na wlaa.hakitaniongezea chochote kiroho. Tomaso alitafuta kumwona Bwana kwa namna ya mwili baada ya kufufuka kwake, lakini baada ya kutokewa alidhani atasifiwa na Bwana, lakini hakusifiwa.

Yohana 20:29 “Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona,wakasadiki”

Nataka nikuambie na wewe usijaribu kufanya hivyo (Ndio unaweza kufanya hivyo, na Bwana akakusikia na kujidhihirisha kwako kwa namna ya kimwili,na ukamwona na mkazungumza), lakini nataka nikuambie Tukio kama hilo kukutokea ni nadra sana kwasababu sio njia kamilifu ya Bwana alitoichagua kwa nyakati hizi.

Ni sawa sawa na mtu aje akuombe wewe mzungumze kwa njia ya barua za posta na si SIMU, kwamba yupo Morogoro halafu akitaka kukujulia hali au kukupa ujumbe fulani basi atumie aandike barua aipeleke posta na kuituma, kisha wewe uipokee na kumjibu kwa njia hiyo hiyo ya posta!.

Umeona? Ni jambo ambalo ni gumu kwako wewe kulifanya kwasababu ni teknolojia ya zamani na inayogharimu fedha na muda.

Kadhalika na njia ya Mungu kuzungumza nasi kimwili kwake ni teknolojia ya Zamani.

Ndio maana ni ngumu leo hii kututokea na kuzungumza nasi.

Bwana Yesu kukaa katika hali hiyo ya kutotutokea tokea kimwili ni yeye ndio kaichagua hiyo njia kwa faida yetu sisi, na si kwasababu sisi ni wenye dhambi ndio maana hatutokei tokei, wala si kwasababu hatuna maombi ya kutosha ndio maana hatutokei..hapana ni kwasababu teknolojia hiyo ni ya zamani kwake na haitufai sana sisi.

Bwana alisema..

Yohana 16:7 “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.

Umeona?.. hapo anasema mimi yanipasa niondoke ili msaidizi aje, na Si yeye aondoke kwasababu hatuombi au kwasababu sisi ni wenye dhambi.

Hakuna maombi yoyote ambayo yangeweza kumbakisha Bwana Yesu katika mwili hapa duniani.

Sasa swali “Tunaenendaje kwa Imani”?

Tunaenenda kwa Imani kwa kumpokea huyo Roho Mtakatifu, ambaye amemwagwa kwetu.

Tukimpata huyu hata Bwana Yesu asipotutokea kwa namna ya mwili katika maisha yetu yote, bado tutakuwa tumeyajua Yesu sana, tutakuwa tumemwelewa kwa undani wote kana kwamba yupo nasi katika mwili.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.

15 Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari”.

Leo hii wengi hawamtaki Roho Mtakatifu lakini wanamtaka Bwana Yesu katika mwili. Pasipo kujua kuwa Roho Mtakatifu ndio ukamilifu wote wa Bwana Yesu.

Na hawamtaki kwa matendo yao na si kwa midomo, ndio maana hawamwoni Yesu katika maisha yao, ndio maana hawamwelewi na ndio maana shetani anawasumbua sana.

Je na wewe umempata Roho Mtakatifu?
Kama bado na unamtamani uwe naye basi usihofu! Kwasababu haihitaji utoe fedha ili umpate, wala haihitaji ufunge kwa maombi, wala haihitaji uende kwenye shule au chuo cha biblia, wala huhitaji mhubiri au mchungaji ndipo akupatie..

Unachokihitaji sasa ni kanuni ya jinsi ya kumpata, na kanuni hiyo ni rahisi, na ipo katika biblia tu! Na hakuna sehemu nyingine unaweza kuipata.

Na kanuni hiyo ni KUTUBU DHAMBI ZAKO KWA KUMAANISHA KUTOZIFANYA TENA, NA KUBATIZWA!!…Basi!!!

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Hapo mstari wa 39 hbiblia inasema… “Ahadi hiyo ni kwaajili YENU na watoto wenu”..
Maana yake ni kwaajili yako na wewe ndugu yangu!.

Sasa kama kanuni ni rahisi hivyo kwanini leo hii usitubu, na kwanini leo hii usibatizwe kwa jina la Yesu?

Bwana akupe kuchagua njia bora!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Dini ni nini, na Imani ya kweli ni ipi?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

KUOTA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BE NOT RIGHTEOUS OVER MUCH

Shalom People of God let us study the Bible… God’s Word tells us in the book of …

Ecclesiastes 7:16 “Be not righteous over much; neither make thyself over wise: why shouldest thou destroy thyself?

What does it mean?

There are a few questions we can ask ourselves… .Why does it say that? .. Why is it wrong to be overly righteous… Why is it better to be overly righteous than to be wicked or to be a little righteous ?

It is true that if we read that verse in that sense we may be confused and see if the Bible confuses us to see that one part exhorts us to be righteous and here it tells us not to be overly righteous…. And this is none other than God, who created the heavens and the earth, who are revealed in JESUS CHRIST (Hebrews 1: 1-2, 2 Corinthians 5:19).

He cannot deceive us, Try to imagine since the creation of the sun. After all, we are the ones who always look to the sun to fix our seasons, and it is not the sun that relies on us… other gods made of sand and wheat, and limestone and pieces of wood that can be wrong but not our God Jehovah we worship through Jesus Christ to him There are no shortcomings.

When the Bible said we should not be overly it means..

“We should not be too self-righteous!”

Aperson that count for himself righteous he became proud and ignore others and see himself as a perfect than others.

Jesus saw Pharisees and Sadducees that are very self-righteous.

Luke 18:9 “And he spake this parable unto certain which trusted in themselves that they were righteous, and despised others:

10 Two men went up into the temple to pray; the one a Pharisee, and the other a publican.

11 The Pharisee stood and prayed thus with himself, God, I thank thee, that I am not as other men are, extortioners, unjust, adulterers, or even as this publican.

12 I fast twice in the week, I give tithes of all that I possess.

13 And the publican, standing afar off, would not lift up so much as his eyes unto heaven, but smote upon his breast, saying, God be merciful to me a sinner.

14 I tell you, this man went down to his house justified rather than the other: for every one that exalteth himself shall be abased; and he that humbleth himself shall be exalted.

 Do you see? … Even the purity and holiness we have should not exceed the limits of self-righteousness!

Likewise if we have godly wisdom then we should not consider ourselves so wise of the Word of God that no one like us, and no one can add anything to us… if we do so we will be overly wise! .. and so we will destroy ourselves.

Ecclesiastes 7:16 “Be not righteous over much; neither make thyself over wise: why shouldest thou destroy thyself”

The Pharisees and Sadducees destroyed themselves with their own excess of righteousness and thought they knew the Scriptures better than anyone else. At the end they found themselves not believing in Jesus and they end up resist and later they killed him.

Likewise you are a Pastor, or a Prophet or a Preacher or a Teacher or You have the Word of Wisdom and Knowledge, or you have the gift of healing, or the Faith or the miracles or you are a Believer who has a special Grace that God has bestowed upon you that may distinguish you from others in some way or wherever you are… Do not forget this word… “DO NOT BE RIGHTEOUS OVER MUCH”. Every day see yourself as nothing in the sight of God..it is only by the Grace of God you are as you are and not power .

Your right should not exceed the limits and see yourself you deserve to be as you are now, no one deserves it , we have been chosen by Grace …so no need of boasting ourselves because it’s by God’s grace.

Ephesians 2:8 “For by grace are ye saved through faith; and that not of yourselves: it is the gift of God:

9 Not of works, lest any man should boast.

If you are not saved yet! So the rapture is about to happen the wrath of the Lord will be poured out on the earth and those who resist the son of God Jesus Christ they will be destroyed as it is written in Revelation 16.

The rapture is near when the saints (that is, all those who have accepted Jesus Christ and lived holy lives) will be caught up and go to heaven for the Lord to turn the wrath away. Where will you be? .. if today you are still rejecting Christ? If you still drink alcohol ,applying lipstick, wig wearer, adulterer, looking phonographic, charting unnecessary things (dirty), wearing half naked clothes, wearing trousers? .. Where will you be that day?

Today does not pass you by before you turn around, the bible says the hour of salvation is now. For that Repentance begin today to carry your cross and follow Christ.

Delete today all the secular music on your phone and all the dirty pictures as well as the numbers of the men / women you were chatting unnecessary things with. Also burn half naked clothes and cosmetics..stay as you are in your reality. And all the other ungodly things you were doing.

If you have done that … then you will have shown Christ that you have truly decided to follow Him in your actions. As it is written in

John 6:37 “All that the Father giveth me shall come to me; and him that cometh to me I will in no wise cast out”.

So He will be with you and you will feel a wonderful Peace that you have never heard before.

And after you have turned to Jesus in such a practical way. it is that of the baptism with many waters (John 3:23) and of the Name of Jesus Christ (Acts 2:38). And the Holy Spirit in you will help you to discern good and evil afterwards and so on. He will guide you until you reach perfection and above all he will enable you to overcome all the sins and temptations of this world, He will take care of it all.

If you do so sincerely you will be born again..and be among the chosen ones whom the Lord loves. And if the rapture pass today you will be among the chosen one to witness the feast of the Lamb which Christ had gone to prepare for us for two thousand years now.

Maran atha.


Related Topics:

Bible questions answered

THERE’S POWER WHICH DRAWS US TO CHRIST, VALUE IT!

THERE’S POWER WHICH DRAWS US TO CHRIST, VALUE IT!

UNDERSTAND HOW CHRIST HEALS PEOPLE’S SOULS.

Home

Print this post

TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.

Shalom.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia..

Maandiko yanasema.

Waefeso 6:10 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake”.

Biblia inatufundisha kuwa mahodari katika Bwana na vile vile katika Uweza wa Nguvu zake.

Hapo kuna vitu viwili, 1). Kuwa Hodari katika Bwana. 2) Kuwa hodari katika uweza wa nguvu zake.

1) Kuwa hodari katika Bwana ni kupi?.

Kuwa Hodari katika Bwana ni katika kumtafuta yeye; yaani, kujituma katika kuutafuta uso wake.

Marko 12:30 “nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.

2) Kuwa hodari katika uweza wa nguvu zake.

Kuwa hodari katika uweza wa nguvu zake ni kuwa na uwezo wa kuzitumia zile silaha za roho ambazo tunazisoma katika mistari inayofuata.

Tusome,

Waefeso 6:10 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

11 Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu”.

Biblia inatuasa tuwe hodari, tusiwe walegevu, kwasababu uweza wa Mungu unadhihirika katika uhodari wetu katika kuzitumia silaha hizo za roho.

Na silaha hizo ndio hizo zilizotajwa hapo ambazo ni Chepeo ya wokovu, Dirii ya Haki, Upanga wa Roho, Utayari miguuni, Kweli kiunoni na ngao ya Imani.

Askari ambaye si hodari ni yule ambaye anazo silaha lakini hana ujuzi au utaalamu wa kutosha wa kuzitumia.

Askari aliyeshika upanga halafu hana ujuzi wa kutosha namna ya kuutumia, adui akija atamdhuru pamoja na silaha yake.

Kadhalika na sisi tunapoushikilia upanga wa Roho, ambao ni Neno la Mungu, na tukawa hatujui namna ya kulitumia inavyopaswa, adui yetu shetani anaweza kutudhuru kirahisi au kutupokonya upanga huo na kutudhuru nao.

Ndio maana utaona Bwana alipokuwa kule jangwani, shetani alipomjia kumjaribu kupitia Neno la Mungu, Bwana alikuwa ni hodari katika kulitumia Neno, hivyo alimjibu shetani kwa kumwambia “tena imeandikwa”.

Au kama Apolo alivyokuwa hodari katika maandiko.

Matendo 18:24 “Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderia, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alikuwa hodari katika maandiko”.

Hivyo biblia inatuasa tuwe na ujuzi wa kulitumia kihalali Neno la Mungu.

2 Timotheo 2:15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli”.

Je wewe ni hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake?.

Je umejivika silaha za wokovu, na kuweza kusimama, na kuzipinga hila za shetani.

1 Wakorintho 16:13 “Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari”.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi nyumbani

Print this post

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

Ipo haki na ipo Haki yote.

Mathayo 3:13 “Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.

14 Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?

15 Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali”

Kuna maneno mawili hapo ambayo ningependa tuyatazame. 1) ITUPASAVYO 2) HAKI YOTE.

1) ITUPASAVYO.

Hapo Bwana hajasema, Ndivyo inipasavyo kuitimiza haki yote” bali amesema “Ndivyo Itupasavyo”.. Maana yake hiyo haki haipaswi kutimizwa yeye peke yake tu, bali watu wote, na hao watu ni wale wote walio upande wake, ndio maana Bwana Yesu akasema Imet ujeupasa, maana yake yeye pamoja na wote watakaomfuata..ni lazima waitimize haki yote.

Sasa hiyo haki yote ni ipi?

2) HAKI YOTE.

Kama tulivyosema ipo haki na ipo haki Yote.
Unapomwamini Bwana Yesu, hapo umeitimiza haki, unaposhiriki meza ya Bwana hapo umeitimiza haki, unapohubiri hapo umetimiza haki, unapoishi maisha ya utakatifu hapo umetimiza haki, lakini bado si haki yote. Haki yote inakamilika na wewe kukamilisha UBATIZO WA MAJI.

Bwana Yesu alikuwa mkamilifu, alikuwa tayari mtakatifu kiasi kwamba asingekuwa na haja ya kubatizwa. Lakini aliona asipobatizwa atakuwa hajaitimiza haki yote.

Sasa kama Bwana Yesu alibatizwa ili kuitimiza haki yote, mimi na wewe leo ni nani tusibatizwe! Au tuone ubatizo hauna maana?.

Kumbuka tena Bwana anasema Imetupasa!!..maana yake sio yeye peke yake tu! Bali yeye na sisi, wote imetupasa kuitimiza Haki ya Mungu.

Katika siku hizi za mwisho shetani anawazuia watu kwa nguvu wasiitimize haki yote, anataka waitimize Nusu haki tu!..kwasababu anajua mtu akiitimiza haki yote atakuwa amempoteza, na yeye bado anataka watu wengi zaidi, wapotee naye kwenye ziwa la moto.

Na kumbuka sio kila ubatizo ni ubatizo sahihi, shetani kashafika mpaka hatua ya kuupindisha ubatizo.

Ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38), na si kwa kunyunyiziwa, Bwana Yesu hakwenda kwa Yohana mbatizaji na kunyunyiziwa, maandiko yanasema “alipanda kutoka majini” na si “kutoka kwenye kikombe chenye maji”.

Marko 1:9 “Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka Nazareti ya Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani.

10 Mara alipopanda kutoka majini, akaona mbingu zinapasuka, na Roho, kama hua, akishuka juu yake”

Yohana alibatiza katika maji mengi sehemu zote (Yohana 3:23).

Sasa swali ni hili: Kama nisipobatizwa kabisa au nikibatizwa kwa ubatizo usio sahihi, baada ya kuujua ukweli sitaokolewa!

Jibu rahisi ni NDIO! Hutakolewa siku ya mwisho, kwasababu umeijua Njia ya Haki na hujaifuata, watakaopata neema ni wale ambao hawakuwahi kusikia kabisa, ambao pengine wangesikia ukweli unaoupata au tunaoupata, wangebadilika haraka sana.

Swali ni je! UMEITIMIZA HAKI YOTE?.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi nyumbani

Print this post

Neno “Uchungu wa mauti” lina maana gani kibiblia?

Uchungu wa mauti ni nini, kibiblia?


Matendo 2:23 “mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

24 ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

JIBU: Uchungu wa mauti, ni kufa bila kuwa na matumaini ya kufufuka, yaani kuoza na kupotea kabisa, ndicho kilichowakuta wanadamu wote, waliokufa, kabla ya Kristo walioza wakapotea kabisa, roho zao zikawa zipo ardhini tu, (makao ya wafu),  Lakini Bwana wetu Yesu Kristo, yeye alipokufa, hakupotelea mavumbini, wala hakuoza, bali alifufuka siku ya tatu. Akawa mtu wa kwanza, aliyekufa akafufuka, kisha akapaa mbinguni, akiishi milele.

Na ndio maana hapo biblia inasema..

“ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao”.

Walipodhani, Kristo hawezi kufufuka, mpaka wakamwekea na muhuri na walinzi kwenye kaburi lake, hilo bado halikuwezekana, alifufuka tu. Kwasababu haiwezekani, uchungu wa mauti umshike Bwana.

Hata sasa sisi, sote, tuliomwamini, tunapokufa, uchungu wa mauti hautukamati, na ndio maana siku ile Bwana alipofufuka alifufuka na watakatifu wake akawapeleka peponi, (Mathayo 27:51-53), sisi kama watakatifu tunapokufa hatulali makaburini tena, wala hatuendi jehanamu, bali tunahamishwa na kupelekwa peponi,(sehemu nzuri sana ya raha) tukingojea siku ile kuu ya ukombozi wa miili yetu, ndipo tutakapoichukua miili yetu ardhini, na moja kwa moja tutakwenda mbinguni, Bwana wetu Yesu Kristo alipo.

Lakini kama bado upo nje ya Kristo, uchungu wa mauti, ni lazima ukupate tu, kwasababu ukifa utakwenda jehanamu huko chini, kuteswa, huku ukisubiria siku ile ya ufufuo uhukumiwe, kisha utupwe katika lile ziwa la moto. Ndugu Usichukulie rahisi rahisi kifo kama wewe ni mwenye dhambi, uchungu wa mauti hauelezeki, soma ile Habari ya Tajiri na Lazaro,(Luka 16:19-31) ndipo utapata picha halisi ni nini kinawakuta watu wote, wanaokufa sasa nje ya Kristo.

Je bado unaishi katika dhambi? Bado unaishi Maisha ya uvuguvugu, kumbuka, hakuna anayejua siku yake ya kuondoka hapa duniani, Ikiwa leo ndio siku yako, Jiulize Huko utakapokwenda utakuwa mgeni wa nani?

Majibu tunayo sote mioyoni mwetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

DHAMBI YA MAUTI

Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?

KU WAPI, EWE MAUTI, KUSHINDA KWAKO?

Nini maana ya “Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea;?

Rudi nyumbani

Print this post

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

Je! Ule Unabii wa mifupa mikavu una maana gani kwetu?


Ezekieli alionyeshwa maono,ambayo yalimshangaza sana, maono yenyewe yalihusu mifupa ya watu ambao walionekana kama walishakufa  kipindi kirefu sana nyuma, na inavyoelekea yalikuwa ni mauaji ya halaiki, (watu wengi waliouawa kwa wakati mmoja).Kwasababu mifupa hiyo ilikuwa mingi sana katika bonde kavu.

Hivyo alipopitishwa kwenye bonde hilo, alisikia sauti ya Mungu ikimuuliza Ezekieli Je! Mifupa hii inaweza kuwa hai tena?, Ezekieli akajibu wewe Bwana wajua, yaani wewe ndiye unayejua kama yaweza kuwa hai tena au la.

Lakini kama tunavyosoma Habari muda huo huo aliambiwa aitabirie uhai, na alipofanya vile  alishuhudia uumbaji wa Mungu kwa mara nyingine tena. Jinsi mifupa ilivyopata mishipa,  mara nyama, mara uhai na kutembea na kuongea tena..

Tusome.

EZEKIELI: MLANGO 37

1 Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanichukua nje katika roho ya Bwana, akaniweka chini, katikati ya bonde; nalo limejaa mifupa;

2 akanipitisha karibu nayo pande zote; na tazama, palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo, tazama, ilikuwa mikavu sana.

3 Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe.

4 Akaniambia tena, Toa unabii juu ya mifupa hii, uiambie, Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Bwana.

5 Bwana MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama, nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi.

6 Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.

7 Basi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, tetemeko la nchi, na ile mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe.

8 Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake; lakini haikuwamo pumzi ndani yake.

9 Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi.

10 Basi nikatabiri kama alivyoniamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.

11 Kisha akaniambia, Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli; tazama, wao husema, Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yametupotea; tumekatiliwa mbali kabisa.

12 Basi tabiri, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli.

13 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, enyi watu wangu.

14 Nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimesema hayo, na kuyatimiza, asema Bwana.

Hii ni mistari ya Faraja, kwasababu inaeleza ukuu wa Mungu, kwenye matumaini ambayo yalishakwisha potea. wana wa Israeli walipopelekewa unabii huu walipata nguvu mpya,kwasababu wakiwa Babeli walikuwa wameshapoteza matumaini ya kurudi katika taifa lao tena, kuishi na kumwabudu Mungu. Lakini Mungu akawaambia japokuwa mmekuwa kama mifupa mikavu iliyokauka, mimi nitawafufua tena na kuwarudisha katika nchi yenu, na kupanda na kujenga na kunitumikia tena.

Na kweli jambo hilo lilikuja kutokea vilevile, Bwana aliwarejesha tena katika taifa lao.

Hata sasa, unaweza ukawa umekufa, kwa namna nyingi, mpaka umekata tamaa ya kuishi au ya kuendelea mbele katika Imani, pengine afya yako imepoteza matumaini kabisa, labda unaugonjwa wa kiharusi huwezi kutembea umelala tu kitandani miaka mingi au una kansa hatua ya nne, umeambiwa na daktari una wiki chache tu za kuishi, au umeishi na virusi vya ukimwi kwa muda mrefu sasa, na kinga yako imeshuka sana, siku yoyote umeambiwa unaondoka, usiogope, Bwana anaweza kukurejesha ukawa mzima tena, kama zamani.

Ibrahimu alikuwa na matumaini hayo, na ndio maana hakuona shida kumtoa mwanaye kafara kwa ajili ya Bwana, mpaka Mungu akamuita baba wa Imani,

Waebrania 11:17 “Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee;

18 naam, yeye aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa,

19 akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka kuzimu; akampata tena toka huko kwa mfano”.

hivyo na wewe kuwa na Imani na Mungu wako, hakuna linalomshinda yeye.

Mwingine, unaweza ukawa hata chakula ni shida, hujui kesho utaamkaje, familia inakutegemea, kazi huna, umekuwa mifupa mikavu kwelikweli, kumbuka uwezo wa Mungu ni mkubwa sana. Anaweza kukufufua kutoka huko tena, na kukutajirisha.

Unachopaswa kufanya ni kutulia katika mapenzi yake. Yaani, kama hujaokoka basi OKOKA leo, na kama umeshaokoka, basi zidi kumwamini yeye, na hakika atakutengenezea njia pasipo na njia.

Ikiwa wewe ni mmojawapo wa mifupa hii mikavu, ningependa tusali Pamoja sala hii;

Basi magoti mahali ulipo  kisha nyanyua mkono wako mmoja juu kisha sema sala hii kwa Imani na Bwana atakusaidi.

Baba yangu, Nimejua hakika wewe ni Mungu, wala hapana mwingine mwenye ishara kuu na za ajabu kama wewe. Nimesoma maneno yako, nami nimeamini, kuwa wewe MUNGU unaweza kurejesha uhai tena kwa watu waliokwisha kufa na kuoza na kubakia mifupa tu. Naomba Bwana wangu, unisamehe makosa yangu yote, niliyokukosea kwa kujua na kutokujua. Naomba Damu ya mwanao Yesu Kristo initakase kuanzia sasa, nami nakiri kuwa nitatembea katika maisha ya utakatifu, sikuzote za Maisha yangu.

Naomba unisaidie tatizo langu hili (Taja tatizo lako, kama ni ugonjwa, shida, n.k. mwambie ), Unifufue upya, nisimame, nikutukuze, nikutumikie, nikuabudu Mungu wangu. Asante kwa kunisamehe, Asante kwa kunisaidia, asante kwa kuniweka huru.

Amen.

Irudie sala hiyo kwa mara nyingine tena, hadi usikie amani ndani ya moyo yako.

Na amini kuwa Bwana ameshaanza kutenda jambo katika Maisha yako,.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali./Ubatizo
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

Bwana Yesu asifiwe, nakukaribisha katika Makala zinazoeleza juu ya thawabu mbalimbali za Mungu, na vigezo ambavyo Mungu atavitumia kuzitoa thawabu hizo. Tumeshatazama vigezo vya thawabu kadha wa kadha huko nyuma, na sasa, tutaendelea na sehemu yetu ya tano (5)

5) Zipo thawabu za kumiliki miji mingi Zaidi katika ule ufalme wa Mungu.

Mungu ameahidi,kuwapa utawala mkubwa, wale watu ambao watatumika kwa uaminifu wakiwa hapa duniani.

Tuupitie mfano huu tutaelewa zaidi;

Luka 19:12 “Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.

13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.

14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.

15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.

16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.

17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.

18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.

19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.

20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.

21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.

22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;

23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?

24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.

25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.

26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho”.

Mfano huo unajieleza wenyewe.. Ikiwa Bwana amekupa kiwango Fulani cha neema umtumikie hapa duniani, anatarajia kuona umekizalisha kwa wingi kwa jinsi uwezavyo. Mfano amekupa neema ya kufagia uwanja wa kanisa, anatarajia, kuona na vyoo pia, ni visafi, na madirisha na viti vinakaa katika hali ya usafi siku zote.

Kwasababu siku atakayokuja, atatazama, kama kile alichokupa mwanzo, na utawajibikaji wako je! vinaendana, lakini ikiwa utaona kazi ya kufagia kanisa, haina maana yoyote, ukaendelea na shughuli zako, atakuja kukuambia kama uliona uvivu kufagia basi si ungemwajiri mtu akusaidie kuifanya hiyo kazi umlipe, kuliko kuuacha uwanja wangu ukiwa na vichaka na matakataka namna ile? Unaona Kama tu alivyomwambia yule aliyepewa fungu moja, si ungeweka kwa watoa riba, ili nijapo nikute na faida yangu?. Ndivyo atakavyotuambia na sisi!

Lakini kama tutakuwa waaminifu wa kile alichotupa, tukazalisha na Zaidi ya  pale, tujue kuwa, uaminifu wetu, utaamua umiliki wetu katika ufalme ule…Kama ni miji basi tutamiliki hiyo miji kulingana na uaminifu wetu sasa.

Hivyo hiyo inatupa hamasa, tuitende kazi ya Bwana bila kutoa visingizio, bila kudharau, tena tutende Zaidi ya pale kwa kadiri tuwezavyo, kwasababu hivyo hivyo vidogo ndivyo vitakavyopima utajiri wetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Jibu: Hii ni moja ya hoja ambayo ni muhimu sana mkristo yeyote kuijua.

Ukweli ni kwamba shetani hawezi kuingia kwenye ufahamu wa mtu na kujua anachokifikiri au kukiwaza au kukipanga.

Huo uwezo hana, na hajawahi kuwa nao. Na sio yeye peke yake bali hata malaika hawana huo uwezo, wala wanadamu hawana huo uwezo.

Ni Mungu peke yake na mtu mwenyewe ndio wenye Nywila (password) ya kuingia ndani ya mawazo yako.

Maana yake ni kwamba kile unachokiwaza sasahivi ni wewe peke yako ndiye unayekijua na Mungu, shetani hakijui, wala malaika wala mwanadamu mwenzako.

Labda wewe ndio uamue kuwafunulia yaliyopo ndani yako.

Sasa swali hili; kama ni hivyo inakuwaje shetani anaonekana kama anajua mambo yetu hata yale ya siri?.

Jibu ni kwamba, anajua mambo yetu kwa kuzisoma fahamu zetu.

Hata wewe unaweza kumsoma mtu na kujua anachowaza kwa wakati huo, kama una utashi wa kutosha, lakini hiyo haijamaanisha kwamba umeingia katika ubongo wake na kuyaona mawazo yake kama Tv. Hapana!

Vivyo hivyo na shetani, ana uwezo mkubwa wa kumsoma mwanadamu na hata kujua anachowaza.. kwasababu amekabiliana na mwanadamu kwa miaka mingi, tangu Edeni anazijua tabia za wanadamu, hivyo ni rahisi pia kuyasoma mawazo yao lakini si kuingia ndani ya mawazo yao.

Kama vile wewe mtu mzima unavyoweza kuyasoma mawazo ya mtoto mdogo na kujua kila kitu anachokifikiri kwa wakati huo na shetani ni hivyo hivyo.

Lakini pamoja na kwamba shetani ana uwezo wa kuyasoma mawazo ya mtu, lakini bado anapata shida sana kuyasoma na kuwaelewa mawazo ya watu waliozaliwa mara ya pili kwa Roho.

Maandiko yanasema kuwa hali ya mtu aliyezaliwa mara ya pili ni kama upepo, haujulikani unapoanzia wala unapoishia.

Yohana 3:8 “Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho”.

shetani anapata wakati mgumu sana kuyasoma mawazo ya mtu aliyezaliwa mara ya pili.

Kwasababu atadhani yale majaribu aliyomjaribu nayo jana, yatamfanya leo asiendelee na wokovu, kinyume chake anashangaa ndio kwanza anasonga mbele.

Au anategemea vile vitisho alivyomtisha navyo jana usiku, vitamfanya leo sidhubutuu kuendelea kuhubiri, au kuendelea na shughuli zake za kawaida, kinyume chake anaona yule mtu anaendelea kuhubiri kwa raha au anaendelea na shughuli zake.

Anategemea ule uchumi alioutikisa jana, utamfanya huyu mtu leo awe katika dimbwi kubwa la mawazo na hata kukufuru kinyume chake anamwona hata hawazi.

Kila anachojaribu kukifanya ili kumtikisa mtu aliyezaliwa mara ya pili, anakutana na matokeo tofauti na anayoyategemea.

Mtu aliyezaliwa mara ya pili anakuwa hatabiriki katika upeo wa shetani na mapepo yake. Tofauti na mtu ambaye hajazaliwa mara ya pili ambapo akitishiwa na wachawi kidogo tu ndani ya nyumba yake, tayari kashatishika kiasi kwamba shetani na mapepo yake wanajua kesho huyo mtu hatalala tena kwenye hiyo nyumba..Na kweli kesho yake halali tena huko ndani.

Mtu na namna hiyo shetani anakuwa anaweza kumsoma kirahisi na vile vile anakuwa anampangia maisha.

Swali ni je! Mimi na wewe tumezaliwa mara ya pili kwa Roho?. Kama bado basi tufahamu kuwa maneno haya yafuatayo yanatuhusu.

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.

YESU ANA KIU NA WEWE.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 4)

Rudi nyumbani

Print this post