Jibu: Shalom.
Neno “Amali” maana yake ni “kazi ngumu” hususani ile inayohusisha mwili, kama vile kazi ya kibarua cha kulima au kukata mti.
Katika biblia neno hilo limeonekana mara nne..
Mhubiri 4: 4 “Tena nikafikiri AMALI ZOTE, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.
Mistari mingine inayoainisha neno hilo ni pamoja na Mhubiri 4:8, Mhubiri 5:19, na Mhubiri 8:15.
Neno “Ijara” maana yake ni “mshahara anaolipwa mtu kwa siku”. kumbuka mshahara anaolipwa mtu kwa mwezi hauitwi Ijara, Ijara ni mshahara wa siku tu, mara nyingi unawahusu vibarua.
Walawi 19:13 “Usimdhulumu jirani yako, wala kumnyang’anya mali yake; IJARA YAKE aliyeajiriwa isikae kwako usiku kucha hata asubuhi”.
Isaya 3:11 “Ole wake mtu mbaya; shari itakuwa kwake, kwa maana atapewa IJARA ya mikono yake”
Isaya 40: 10 “Tazameni, Bwana Mungu atakuja kama shujaa, Na mkono wake ndio utakaomtawalia; Tazameni, thawabu yake i pamoja naye, Na ijara yake i mbele zake”.
Mistari mingine inayoanisha neno hilo ni 2Nyakati 15:7, Mhubiri 4:9, Mhubiri 9:5, Isaya 5:23, Mika 1:7, Zekaria 8:10, na 2Wakorintho 5:10.
Hivyo hakuna Amali isiyo na Ijara. Vile vile kazi ya Mungu ina ujira wake, kama Bwana alivyosema katika kitabu cha Ufunuo..
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Mbu ni mdudu ambaye endapo akitua juu ya mwili wa mtu, kama hatasumbuliwa kwa namna yoyote ile, basi atanyonya damu na mwisho wa siku tumbo lake litajaa sana mpaka kupasuka akiwa pale pale ananyonya!..na hapo ndio unakuwa mwisho wa maisha yake!.
Utafiti unaonyesha, kuwa wakati mbu ananyonya damu, mfumo wa taarifa wa tumbo lake na ufahamu wake unakatika, hivyo hajijui kuwa kama hapa kashiba au bado, yeye ile njaa ya kwanza ipo pale pale, anaendeleo kunyonya tu, mpaka anafia pale pale..
Biblia inasema pia katika Mhubiri 5:10 kuwa..
Mhubiri 5:10 “APENDAYE FEDHA HATASHIBA FEDHA, Wala apendaye wingi hatashiba nyongeza. Hayo pia ni ubatili.
11 Mali yakiongezeka, hao walao nao waongezeka na mwenyewe hufaidiwa nini, ila kuyatazama kwa macho yake tu?”
Sio vibaya kutafuta fedha, ni jambo la muhimu, lakini lisiwe jambo linalotawala maisha kiasi kwamba, unapoangalia kushoto, au kulia unaona fedha, au unawaza fedha!. Ukiwa katika hali kama hiyo, nataka nikuambie “kupenda fedha kupo ndani yako hata kama hutakiri kwa kinywa”.
Hekima ya ulimwengu huu inatuambia na kutufundisha, kuwa muda wote tuwaze fedha, tufikiri fedha, tuziishi fedha, tuzitafute lakini hekima ya Mungu haisemi hivyo.. hekima ya kiMungu inasema hivi…
Waebrania 13:5 “MSIWE NA TABIA YA KUPENDA FEDHA; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”.
Hekima hii kwa ulimwengu inaonekana ni upumbavu!, lakini kwa watu wa Mungu ni nguvu ya Mungu.
Hekima ya kiMungu pia inasema, shina moja la mabaya yote ni kupenda fedha!
1Timotheo 6:10 “Maana SHINA MOJA LA MABAYA YA KILA NAMNA NI KUPENDA FEDHA; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.
Mtu anayependa fedha anakuwa hashibi fedha siku zote, akipata elfu hashukuru wala haridhiki, atatamani tena laki, akipata laki hali yake ni ile ile, atataka milioni, akipata milioni atataka milioni 100, wala hutaona badiliko lolote kwake, hashukuru wala hatosheki..ni kama mbu anayenyonya damu, pasipo kujijua kuwa tayari tumbo lake limeshajaa na linakaribia kupasuka, yeye anaendelea tu!, mwisho wa siku anapasuka matumbo!.
Ndicho kilichomtokea Yuda, alianza kupenda fedha kidogo kidogo, na kwasababu kupenda fedha ni roho!, ikampelekea asitosheke kuiba fedha iliyokuwa inapatikana katika mfuko wa Bwana!, akapiga hatua nyingine ya kutamani hata apate fedha nyingi zaidi, kwa kumsaliti Bwana Yesu! Pasipo kujua kuwa tayari tumbo lake limejaa na linakaribia kupasuka!, yeye aliendelea kuzisaka fedha kwa nguvu, na ulipofika wakati matumbo yake yalipasuka kama maandiko yanavyosema…
Matendo 1:18 “(Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka.
19 Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.)”
Biblia inatuonya tusiwe na tabia ya kupenda fedha.., haijatukataza kufanya kazi!, bali tusiwe watu wa kupenda fedha!…unaweza kuipenda kazi unayoifanya lakini usiwe na tamaa ya kupenda fedha katika hiyo!, kiasi kwamba upate kingi au kidogo!, moyo wako hauutaabiki!!, maadamu umetoa huduma iliyo bora, furaha yako inakuwa ni ule uaminifu katika kazi yako, yaani siku ukiona hujafanya kazi kwa uaminifu ndio moyo wako unauma, na sio siku umeona hujapata faida nyingi!… Na wengi wanaoipenda kazi zao kuliko faida na fedha, ndio wanaofanikiwa kuliko wale ambao kipaumbele chao ni fedha tu!.. Hao wapo tayari mwingine alie ili wao wapate faida, au mwingine adhurike wao wapate fedha, kama Yuda!, wapo radhi wakuuzie hata sumu, au wafanye biashara haramu ilimdari tu matumbo yao yajae…
Ndio maana wanafananishwa na mbu anayenyonya damu!.. mbu ananyonya uhai wa mtu, ambayo ni damu yake..ndio maana mwisho wake unakuwa ni kupasuka matumbo!..
Bwana atusaidie, tuwe watu wa kumpenda yeye zaidi ya kupenda fedha!.
Mathayo 6:33 “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Leo hii dunia imekuwa na sikukuu nyingi sana za maonyesho. Na sikukuu hizo Mungu ameruhusu makusudi kabisa ziwepo ili kutupa picha halisi ya jinsi sikukuu yake kubwa ya maonyesho itakavyokuwa mbinguni.
Kwamfano kipindi hiki, kwa taifa kama la Tanzania, lipo katika sikukukuu ya maonyesho ya wafanyabiashara maarufu kama saba saba (7’7). Na mwezi ujao kutakuwa na maonyesho mengine makubwa ya wakulima yajulikanayo kama nane nane (8’8). Kama ulishawahi kutembelea maonyesho haya, au yanayofanana na haya nadhani utakuwa unaelewa ni nini hasaa kinaendelea kule.
Kwa ufupi ni kwamba utakutana na mabanda mengi sana, na kila banda lina onyesho lake la kipekee, kiasi kwamba mpaka utakapomaliza mabanda yote, hutatoka kama ulivyo. Utakutana na mambo mengi sana usiyoyajua, ni jinsi gani vitu vinatengezwa, ni technolijia gani inafanya kitu kiwe hivi au vile n.k.
Sasa, mambo hayo na kwa Bwana Yesu pia yapo. Ipo siku kubwa sana ya maonyesho, ambayo itafanyika huko mbinguni, Sikukuu hiyo biblia inatuonyesha tumeandaliwa sisi, mahususi ili kuuona utukufu wa Yesu aliopewa na Baba yake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kwa ajili yetu sisi.
Yohana 17:24 “Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, WAPATE NA KUUTAZAMA UTUKUFU WANGU ULIONIPA; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu”.
Umeona hapo? Anasema, lengo la yeye kutaka tuwepo na yeye popote alipo ni kusudi kwamba tuutazame utukufu wake aliopewa… Ndugu hadi sasa Bwana Yesu ameshajiandaa kutuonyesha ukuu wake, huko mbinguni.. Tengeneza picha jinsi siku hiyo itakavyokuwa, tutakapotembezwa katika mabanda ya mbinguni(tukitumia lugha ya kibinadamu).. Tunatoka sehemu moja anatuonyesha nchi nzuri ya dhahabu, tukidhani ndio basi, tunatoka hapo anatupeleka kwingine anatuonyesha makasri mazuri ya kifalme, halafu anasema hayo yote ni ya kwenu, niliyokuja kuwaandalia huku kwa miaka 2000, kama nilivyowaambia katika Yohana 14
Yohana 14:1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”.
Anatoka hapo anatupeleka tena katika banda lingine, anatuonyesha viumbe wa kimbinguni, ambao hutujawahi hata kuwaona huku duniani, anakuambia hawa watawatumikia nyinyi.. Tunatoka hapo anawapeleka na kwa malaika zake wote, anatutambulisha kwa mmoja baada ya mwingine, kisha Bwana anasema hawa nao watawahudumia siku zote.. Tunatoka hapo tunakwenda kuonyeshwa vyombo vizuri za muziki, ambavyo kwa hivyo tutakuwa tunamwimbia Mungu daima. Mnaenda sehemu nyingine mahali pa mafunzo mnaambia hapa mtafundishwa jinsi ya kuwa na uwezo wa kiroho kama wa malaika, mnatoka hapo mnapelekwa tena kwingine kuonyeshwa mambo ya ajabu, ambayo kimsingi hatuwezi kuyaeleza hapa, kwasababu ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala, sikio kusikia, wala halijawahi kuingia katika moyo wa mwanadamu yoyote.
1Wakorintho 2:9 “lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao”.
Siku hiyo ndiyo tutakapojua Bwana Yesu ni mkuu namna gani. Leo hii huwezi kujua lolote, kwasababu wakati wa yeye kudhihirisha utukufu wake haujafika, lakini siku si nyingi, atatunyakua na kutupeleka huko aliko. Tukauone utukufu wake aliopewa na Baba yake.
Tutaona mambo mengi sana, kila mahali tutakapokuwa tunapelekwa tutabakia kutoa macho tu, kwasababu tutasema hiki nacho tumepewa sisi? Hata hiki? Hata kile? Na Yesu atasema NDIO niliwaandalia nyinyi haya yote..Kama hatujaelewa Tutauliza maswali, na yote yatajibiwa, tutatembea katika maonyesho hayo makuu kwa muda wa miaka saba mfululizo.
Kwakweli tukose vyote sasa lakini sio hilo. Tukose mali sasa, tukose umaarufu, tukose vya kidunia, tusikose karamu kuu ya mwanakondoo, mbinguni. Lakini kwa bahati mbaya ni kuwa watu wengi watayakosa maonyesho hayo makuu, kwasababu kama mpaka leo hii, mtu akiambiwa aokoke kwa kumaanisha kabisa kumfuata Yesu, anaona kama analetewa habari za kilokole, unategemea vipi mtu huyo, ataingia kwenye karamu hiyo na maonyesho hayo?
Hatakwenda popote,atabaki tu hapa duniani, hata akifa leo, hiyo siku yenyewe ikifika, hatoweza kufufuliwa aende katika UNYAKUO. Ndugu huo ndio wakati ambao kutakuwa na kilio na kusaga meno kama Bwana Yesu alivyosema.. Hutalia kwasababu inaingia kwenye dhiki kuu tu, bali utalia sana kwasababu umekosa tendo hilo kuu la karamu ya Bwana Yesu, ambayo itaambatana na MAONYESHO hayo MAKUBWA SANA.
Yohana 17:24 “Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, WAPATE NA KUUTAZAMA UTUKUFU WANGU ULIONIPA; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu”.
Maneno hayo ni lazima yatimie. Haleluya.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Jibu: Ni vizuri kufahamu kuwa kuna vitu vimeumbwa na Mungu na kuna vitu vimeumbwa na viumbe wa Mungu.
Kwa mfano Mungu hajaumba gari, wala treni, wala pikipiki. Gari tunaloendesha limeumbwa na wanadamu, vile vile hajaumba ndege, wala kiti, mambo hayo yote ni sisi wanadamu ndiyo tuliyoyatengeneza… tumeichukua malighafi hii iliyoumbwa na Mungu, tukaichanganya na malighafi ile, tukatengeneza gari. N.k
Vile vile Mungu hajaumba chapati tunazokula wala maandazi, wala pilau.. alichokiumba ni malighafi hizo, yaani unga, mafuta, chumvi na maji.. Kwa utashi wetu sisi wanadamu, ndio tukachukua malighafi hizo na kuzichanganya pamoja na kuzichoma ndipo vikatokea vyakula hivyo tunavyokula kama maandazi au chapati au chakula kingine chochote.
Kadhalika Mungu hajaumba dhambi, wala matatizo wala shida.. Mambo hayo ni sisi tumeyatengeneza wenyewe, kupitia malighafi au vitu ambavyo Mungu kaviumba. Tunapochukua ukweli na kuuchanganya na vitu vingine na kuugeuza hapo ndipo unapozaliwa uongo!.. Ndio DHAMBI YENYEWE!!
Kitendo cha kukutana kimwili si kibaya lakini kinapofanyika wakati usio sahihi, au na mtu asiyesahihi kinageuka kuwa uzinzi au uasherati, Hivyo uasherati ni kitu sahihi kilichochanganywa na muda usio sahihi na mtu asiyesahihi. Kwahiyo Mungu hajaumba uasherati, bali ni watu ndio walioumba uasherati.
Hivyo dhambi zote zimeumbwa na wanadamu pamoja na shetani na malaika zake. Na si Mungu aliyeziumba kwasababu yeye ni mtakatifu, na wala hachangamani na uchafu. Ndio maana anaichukia dhambi.. Kwasababu ingekuwa ni yeye kaiumba asingeichukia.. Mtu hawezi kuchukia kitu alichokitengeneza yeye mwenyewe..
Na kila siku dhambi zinaendelea kuumbwa na wanadamu.. Ndio maana biblia inasema siku za mwisho maasi yataongezeka, maana yake kila siku maovu mapya yanazaliwa..Ndio maana katika kilele cha maovu haya Bwana lazima aiangamize hii dunia.
Hivyo hatuna budi kukaa mbali na dhambi, kwasababu Mungu wetu ni mtakatifu na wala hachangamani na dhambi.
Mathayo 5:48 “Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Na hatuwezi kuishinda dhambi tukiwa nje ya agano la mwanae mpendwa Yesu. Tunaishinda dhambi na kuacha kuiumba kwa kuungama dhambi zetu zote, kwa kumaanisha kutozitenda tena, na kisha kwenda kubatizwa ubatizo sahihi na kupokea Roho Mtakatifu.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Bwana Yesu ni mzaliwa wa kwanza wa waliokufa?”(Ufunuo 1:5)
Ipo faida ya kufuata mambo yako na kutojishughulisha na mambo ya wengine!.. Lakini pia ipo hasara kubwa ya kutojishughulisha na mambo ya wengine na kufuata mambo yako tu!. Faida ya kufuata mambo yako ni kwamba utakuwa huru katika mambo yako, na hautaishi kwa wasiwasi wala hofu!…kwasababu utakuwa hufuatilii mambo ya wengine, na wala hushirikiani nao, hivyo hutakuwa na mtu wa kushindana naye wala kujilinganisha naye..Kwahiyo utaishi maisha ya uhuru sana..
Lakini pamoja na hayo kuna hatari kubwa sana ya kuishi maisha ya namna hiyo, Maana yake yanapozidi sana, kiasi kwamba unakuwa umefunga milango yote, umejitenga na hutaki kufuatilia chochote cha nje! Ipo hatari!!
Leo tutajifunza kupitia biblia, mojawapo ya hatari ya maisha ya namna hiyo..
Katika maandiko tunausoma mji mmoja ulioitwa Laisha, mji huu ulikuwepo kaskazini mwa Taifa la Israeli, kabla haujatwaliwa na Israeli, ulikuwa unaitwa hivyo Laisha, lakini mji huu ulikuwa ni wa kipekee sana, kwanza ulikuwa ni mji ambao umejitenga, upo mbali sana na miji mingine, na pili ulikuwa ni mji ambao haukushirikiana na miji mingine, hivyo watu wake walikuwa wanafuata mambo yao tu!, wanafanya kazi kwaajili ya kuuendeleza mji wao, na wala hawakuwa na shughuli na mataifa mengine.. Hiyo ikawafanya wafanikiwe sana, kwasababu mambo yao yote hawakuyaendesha kwa hofu wala kwa mashindano.. Na zaidi ya yote, wakajiwekea utaratibu kuwa watu wote ni sawa katika ile jamii, hakuna wa kumtawala mwenzake wala kunyanyasana..
Lakini biblia inatuambia uharibifu wake ulikuja ghafla bila wao kutegemea..na mji mzima uliangamizwa pasipo msaada, kwasababu walikuwa mbali na miji mingine ambayo pengine ingewasaidia, na vile vile haikuwa na mahusiano na mji wowote ule.. ni wao kama wao..
Tusome habari hiyo kidogo katika maandiko.. (Zingatia vipengele vilivyoainishwa kwa herufi kubwa)
Waamuzi 18:7 “Ndipo hao watu watano wakaenda zao, WAKAFIKA LAISHA, wakawaona wale watu waliokuwamo ndani yake, jinsi walivyokaa salama salimini kwa mfano wa walivyokaa hao Wasidoni, WENYE STAREHE NA HIFADHI, kwa maana hapakuwa na mtu katika nchi hiyo aliyekuwa na amri, aliyeweza kuwatweza katika neno lo lote, nao walikuwa wa mbali na hao Wasidoni, WALA HAWAKUWA NA SHUGHULI NA MTU YE YOTE.
8 Kisha wakawarudia ndugu zao huko Sora na Eshtaoli; ndugu zao wakawauliza; Haya, mna habari gani?
9 Wakasema, Haya, inukeni, twende tukapigane nao; KWA MAANA TUMEIONA HIYO NCHI NAYO NI NCHI NZURI sana; nanyi, je! Mwanyamaa tu? Msiwe wavivu kwenda, na kuingia, ili mpate kuimiliki nchi hiyo.
10 Hapo mtakapokwenda mtawafikilia WATU WAKAAO SALAMA SALIMINI, na hiyo nchi nayo ni kubwa; kwa kuwa Mungu ameitia mikononi mwenu; ni mahali ambapo hapana kupungukiwa na kitu cho chote kilicho duniani.
11 Basi wakatoka hapo watu mia sita waliovaa silaha za vita, wa jamaa ya Wadani, kutoka Sora, na kutoka Eshtaoli……………………………………
27 Nao wakakitwaa hicho alichokuwa amekifanya Mika, na kuhani aliyekuwa naye nao wakafikilia Laisha, KWENYE WATU WALIOKUWA WENYE STAREHE NA HIFADHI, wakawapiga kwa makali ya upanga; wakaupiga moto mji wao.
28 WALA HAKUWAKO MWOKOZI, KWA SABABU HUO MJI ULIKUWA NI MBALI SANA NA SIDONI, NAO HAWAKUWA NA SHUGHULI NA MTU AWAYE YOTE; na mji huo ulikuwa katika hilo bonde lililo karibu na Bethrehobu. Nao wakaujenga huo mji na kukaa humo.
29 Wakauita mji jina lake Dani, kwa kuliandama jina la baba yao Dani, aliyezaliwa kwake Israeli; lakini jina la mji huo HAPO KWANZA ULIKUWA UKIITWA LAISHA”.
Umeona?.. Laiti mji huo ungekuwa na mahusiano na miji mingine, labda wangepata mwokozi, na wangeokoka na maangamizi hayo, kwani ingekuwa ni rahisi wao kusaidiwa na majirani zao, lakini maadui zao walipowasoma udhaifu wao kuwa ni watu wanaojiona kuwa hawawezi kuhitaji msaada kutoka kwa mwingine yeyote, ni watu ambao wapo wenyewe wenyewe, ndipo wakapata nguvu!, kwani walitambua hata watakapowavamia hakuna atakayekuja kuwasaidia. Na siku ya maangamizi yao ilipofika, wakaangamia wote!, pamoja na utajiri wao, na fedha zao, na mali zao na kila kitu chao, waliopotea wote.
Hiyo inatufundisha nini?
Umoja ni ulinzi, biblia inasema katika Mhubiri….
Mhubiri 4:12 “ Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi.”
Wakati mwingine unaweza kufikiri kuwa peke yako ndio afya, lakini kinyume chake ndivyo unavyodhoofisha ulinzi wako! Na usalama wako!.. Ni vizuri kutojishughulisha na mambo ya wengine na kufuata mambo yako!.. lakini isizidi sana, kiasi kwamba hata hutaki kuwa na mahusiano na wengine!, hutaki kujifunza kutoka kwao, hutaki kusaidiwa na wao, hutaki kuwasaidia, hutaki kujinyenyekeza kwao, ni wewe kama wewe tu! n.k
Kwasababu huo ubinafsi wako ambao unadhani ni ulinzi kumbe ndio nguvu ya adui yako shetani. Yeye anatamani uendelee kukaa hivyo hivyo bila kuwa na shughuli na mtu mwingine yeyote ili siku atakapokuletea madhara!, ukose msaada. Ni kweli ubinafsi wako utakupa uhuru!, hata unaweza kukupa utajiri, lakini siku ya hautakusaidia siku ya maangamizi..
Hata katika kanisa kitu cha kwanza shetani anachokiua ni Umoja!.. kwasababu anajua ni ngumu kulishambulia kundi kubwa kuliko mtu mmoja mmoja!.. hivyo anachokifanya kwanza ni kuhakikisha analitenganisha kundi, na kutenga mtu mmoja mmoja, hivyo anahakikisha anaweza roho ya kila mtu kufuata mambo yako, na kutojishughulisha na mambo ya wengine.. Na akishafanikiwa hilo, ndipo anaanza kuwamaliza mmoja mmoja.
Ndugu! Usikimbie vikundi vya maombi, na kutafuta kuomba mwenyewe mwenyewe kila mara, ukidhani ndio salama!… Tenga muda wako mwingi wa kusali mwenyewe lakini usiache kukusanyika na wengine katika maombi.
Vile vile usijione kuwa una hekima kwa wewe kutokwenda kanisani kukusanyika na wengine!, kwasababu tu ya vikasoro vidogo vidogo unavyoviona pale!..na huku ukijitumainisha katika kusali mwenyewe ! Bali kinyume chake uogope!… kwasababu upo katika rada ya shetani!!.. Hutadumu muda mrefu, utapotea kabisa..
Yohana 17: 21 “WOTE WAWE NA UMOJA; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ILI WAWE NA UMOJA KAMA SISI TULIVYO UMOJA.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ILI WAWE WAMEKAMILIKA KATIKA UMOJA; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Bwana atubariki.
Kama hujampokea Yesu, mlango wa neema bado upo wazi!.. ila hautakuwa hivyo siku zote, hivyo mpokee Yesu leo akuoshe dhambi zako na kukupa uzima wa milele.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
UNYAKUO.
Unyakuo ni kitendo ambacho Bwana Yesu atawahamisha watakatifu wake, kutoka katika huu ulimwengu na kuwapeleka mbinguni yeye alipo. Kwa mujibu wa biblia Tendo hilo litakuwa ni la ghafla sana, kama vile mtu anafumba macho na kufungua.
Siku hiyo paraparanda ya Mungu italia, ulimwenguni kote, lakini haitasikiwa na watu wote, bali wale watu waliomwamini Yesu hapa duniani, na wale watakatifu waliokufa katika yeye.
1Wakorintho 15:51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,
52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.
Unaona? Siku hiyo, itakuwa ya kipekee sana, Bwana Yesu aliendelea kusema..
Mathayo 24:40 “Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;
41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.
42 Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu”.
Sasa kulingana na majira tuliyopo sasa, dalili zote zinaonyesha Yesu yupo karibu sana kurudi, hatujui pengine ni leo usiku, au kesho au mwezi ujao, lakini kulingana na tabiri zote za kimaandiko, inatuonyesha kuwa siku yoyote Kristo anarudi. Haleluya.
Na kama ikitokea amerudi leo, wewe uliyempokea Yesu, Utaisikia paraparanda hiyo ya Mungu, ikilia. Na ghafla utayaona makaburi ya watakatifu yanafunguka, na wao wakitoka makaburini (Mathayo 27:51-53), kisha baada ya hapo mtakuwa kitu kimoja, na kwa pamoja, mtanyakuliwa mawinguni kumlaki Bwana Yesu ,.
Tendo hilo litakuwa ni la kufumba na kufumbua, na moja kwa moja mtaelekea mbinguni, kule ambapo Yesu alisema amekwenda kutuandalia makao (Yohana 14:1-3). Huko tutakutana na mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, kutakuwa na furaha isiyo na kifani, tutakapoingia katika hiyo karamu ya mwanakondoo. Ni mahali ambapo hata mmoja wetu hapaswi kukosa.
Ufu 19:9 “Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.
Lakini ikiwa wewe hujaokoka, parapanda hiyo ikilia, siku hiyo hutafahamu au kusikia chochote, kinyume chake, utashangaa tu, fulani ambaye aliyempokea Yesu ulikuwa naye sekunde chache tu nyuma, ametoweka, uliyekuwa unalima naye shambani humuoni, mume/mke uliyekuwa umelala naye ameondoka na milango imefungwa. Hapo ndipo utakapojua Kristo amesharudi na kulinyakua kanisa lake.
Vilevile ikiwa utakufa leo katika hali ya dhambi na bado Bwana hajarudi. Siku ya unyakuo ikifika, hautafufuliwa badala yake utaendelea kubaki hapo makaburini mpaka siku ya hukumu ya mwisho ambayo utafufuliwa na kuhukumiwa kisha kutupwa katika lile ziwa la moto (Ufu 20:11-15).
Ndugu yangu, Ipo sababu kwanini leo umekutana na ujumbe huu, wakati tunaoishi ni wakati wa nyongeza tu, Yesu hajarudi bado ni kusudi kwamba wewe ambaye hujampokea, umpokee sasa, vinginevyo angekuwa amesharudi siku nyingi sana. Anakusubiria wewe ambaye pengine ni mmoja wa wale kondoo wa mwisho mwisho, utubu dhambi zako uokoke.
Hataki hata mmoja wetu aikose hiyo karamu aliyokwenda kutuandalia mbinguni kwa miaka 2000 sasa. Haijalishi wewe ni dini gani au dhehebu gani, Yesu anawapokea watu wote, anawapa tumaini jipya, kisha anawaandaa kwa ajili ya kuwakaribisha nyumbani kwake mbinguni.
Hivyo tubu leo, kisha uwe tayari kubatizwa kwa ajili ya kuukamilisha wokovu wako, Na baada ya hapo yeye mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu. Hivyo kama utahitaji msaada wa kuokoka/kubatizwa, basi wasiliana nasi kwa namba hizo mwishoni mwa kipeperushi hichi, au tafuta kanisa la kiroho lililo hai, wakusaidie.
Bwana akubariki.
Neno Ahera limeonekana mara tatu tu katika biblia, limeonekana katika kitabu cha 1Wafalme 2:6 na 9 na katika kitabu cha Wimbo ulio bora 8:6, mara zote hizi Neno hilo limetumika likimaanisha “kaburi”. Hivyo Ahera maana yake ni kaburi.
1Wafalme 2:5 “Na zaidi ya hayo, umejua alivyonitenda Yoabu, mwana wa Seruya, yaani, alivyowatenda majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri, mwana wa Neri, na Amasa, mwana wa Yetheri, ambao aliwaua, na kuimwaga damu ya vita wakati wa amani, akautia damu ya vita mshipi uliokuwa viunoni mwake, na viatu vilivyokuwa miguuni mwake.
6 Kwa hiyo ufanye kama ilivyo hekima yako, wala usimwachie mvi zake kushukia AHERA KWA AMANI”.
Ahera inatukumbusha kuwa kuna mwisho wa maisha haya… hivyo hatuna budi kutengeneza maisha yetu, kabla hatujaingia kaburini… Kwasababu baada ya kifo kitakachokuwa kimebakia kwetu ni hukumu..
Waebrania 9:27 “Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu”.
Bwana atujalie tuishi maisha yanayompendeza yeye, angali bado tunaishi.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu katika kuyatafakari maandiko.
Je! Umewahi kujiuliza kwanini biblia inasema upendo una nguvu kama mauti?.
Wimbo ulio bora 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana UPENDO UNA NGUVU KAMA MAUTI, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu”
Upendo wa Mungu kwetu! Unafananishwa na upendo wa Mtu kwa mpenzi wake. Jinsi mwanaume anavyompenda mke wake ndivyo Kristo anavyotupenda sisi. Na mtu anapozama sana katika upendo huwa anakitu kingine kinachofuatana na huo mpendo, na hicho si kingine zaidi ya Wivu!.. hivi vitu viwili ni Pacha!.. vinakwenda pamoja..
Kadhalika Kristo naye analipenda kanisa na sio tu analipenda bali pia analionea wivu. Endapo watu wake aliowapenda wakikengueka na kujitenga naye, basi wivu wake unawaka!, na kuweza kufanya lolote, kama vile mtu aliyesalitiwa na mke wake.
Lakini leo tutajifunza ni kwa namna gani upendo wa Kristo ulivyo na nguvu!.
Hapo biblia inasema “Upendo una nguvu kama mauti”. Maana yake tukiielewa nguvu ya mauti, basi tutaielewa nguvu ya upendo wa Kristo kwetu.
Kama tunavyojua Mtu anayekumbwa na Mauti, anakuwa haishi tena, anakuwa amepotea moja kwa moja, kumbukumbu lake linapotea duniani, hawezi kutenda jambo lolote wala shughuli yoyote ya huu ulimwengu.
Kadhalika mtu anayeingia na kuzama katika pendo la Kristo, ule upendo wa Kristo unamuua na mambo yote ya kidunia.. unamfanya anakufa kwa habari ya dhambi, anapotea kabisa kwenye dira ya mambo ya ulimwengu huu, anakuwa katika umoja na Kristo, ambao hakuna mtu anayeweza kuukaribia.. na hakuna kitu chochote kinachoweza kumtenga yeye na Kristo..
Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?”
Je na wewe leo umeingia katika pendo la Mwana wa Mungu??..
Kumbuka huwezi kuushinda ulimwengu kama hutakufa kwa habari za uliwengu.
Yohana 15:9 “Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu.
10 Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
11 Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe”.
Ni kwanini leo hii huwezi kushinda ulevi?, ni kwasababu pendo la Kristo halijaingia ndani yako, ambalo lingeweza kuua nguvu yote ya ulevi, vile vile kwanini leo huwezi kuacha uzinzi, ukahaba, wizi, uuaji n.k?.. ni kwasababu bado Pendo la Kristo halijamiminwa ndani yako, ambalo lingekufanya ufe kwa habari ya dhambi ndio maana bado ulimwengu una nguvu juu yako.
Lakini habari njema ni kwamba, Kristo mpaka sasa yupo hai na anaokoa!.. utakapompokea kwa kumaanisha kutubu na kuacha dhambi, basi ataingia moyoni mwako, na lile pendo lake litaua kazi zote za ibilisi ndani yako, na kukuacha huru, na hutaona uzito wala ugumu katika kuishi maisha yanayompendeza Mungu. Kumbuka “UPENDO UNA NGUVU KAMA MAUTI”.
Hivyo ukitaka mauti katika kazi zote za ibilisi juu ya maisha yako, zama katika pendo la Kristo. Kwasababu Kristo mwenyewe hawezi kuruhusu wewe usumbuliwe na mambo ya ulimwengu huu!, hivyo lazima aue kazi zote za ibilisi ndani yako..
Kama hujaingia katika pendo hili, basi tubu leo kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako zote, na kisha tafuta ubatizo sahihi, ambao ni ule wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo. Na kwasababu Kristo ni mwenye upendo, atakuingiza katika pendo lake na kukupa uzima wa milele.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibu tena tuyatafakari maneno ya uzima.
Kuna wakati Mtume Paulo alifunuliwa siri nyingi sana zimuhusuzo Bwana wetu Yesu Kristo, hususani zile zinazomlinganisha yeye na Melkizedeki. Na hamu yake ilikuwa ni kanisa zima lifahamu siri hizo, lakini alikumbana na kipingamizi kikubwa, ambacho kilimfanya asiweze kuzieleza zote, na kipingamizi chenyewe ni ule UVIVU WA WATU KUSIKIA.
Waebrania 5:10 “kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.
11 Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia”.
Embu tengeneza picha kama Paulo angeendelea, kumwelezea Melkizedeki kama alivyokuwa anamwelezea katika sura hizo chache za kitabu cha waebrania, ungefahamu mangapi ya ziada yamuhusuyo Bwana Yesu, kuliko hayo unayoyajua sasa hivi, Lakini asingeweza kuwaeleza kwasababu hata yale ya mwanzo machache tu, bado watu walikuwa ni wavivu wa kufuatilia..Hivyo kama mwalimu asingeweza kufundisha hesabu za maumbo wakati hesabu kujumlisha na kutoa bado watu hawazijui.
Hata sasa tabia hii, ipo miongoni mwa watakatifu. Ni rahisi kusikia mkristo fulani akisema tena kwa ujasiri, “Aah huu ujumbe ni mrefu siwezi kusoma” lakini wakati huo huo anaweza kumaliza vitabu vitatu vya hadithi, na asione shida. Anaweza kusikiliza mahubiri dakika 10, lakini muvi za kidunia, akakesha nazo usiku kucha.. Anaweza akatumia dakika 2 kutazama video ya ki-Mungu, lakini akatumia saa 6 kuchat Instagramu, na Facebook. Huyo ni mkristo, hatuzungumzii mpagani. Na bado atagemea Mungu atajidhihirisha kwake zaidi ya hicho kiwango anachomjua.
Ndugu, kila siku Bwana anataka tujae maarifa, ili tuweze kuishi kulingana na viwango anavyovitaka yeye kwetu. Mtume Paulo japokuwa alipewa mafunuo makubwa sana yamuhusuyo Mungu, na kule mbinguni, mpaka Mungu akamwekea mwiba maishani mwake ili asijisifu kupita kiasi kwa wingi wa mafunuo hayo (2Wakorintho 12:7).. Lakini bado hakuwa mvivu wa kusoma Neno la Mungu, na kutaka kujua habari za Mungu, Na ndio maana utaona mpaka dakika yake ya mwisho anamwagiza Timotheo ambebee vile vitabu vya ngozi (torati na manabii) ampelekee.
2Timotheo 4:12 “Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.
13 Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi”.
Sisi tumekuwa kikwazo cha Mungu kujifunua kwetu katika utimilifu wote, Kwasababu ya uvivu wetu wa kusikia/kusoma. Leo hii Bwana atusaidie tuzidishe bidii, kumtafuta Mungu. Ili Bwana ajifunue kwetu zaidi. Bwana Yesu alisema..
Yohana 3:12 “Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni”?
Kumbe alitamani pia kuwaeleza watakatifu wa kipindi kile mambo ya mbinguni, lakini kwa ajili ya uvivu wao wa kutamani kujifunza, hawakuambiwa. Ndugu yangu Leo hii ua TV unazoangalia muda wote, ua huo muda unaokesha Instagramu, na facebook, kutazama video ambazo hazikujengi. Usipokuwa na instagramu, hupungukiwi chochote, si lazima uwe nayo, Muda utakuwa nao mwingi sana na wa kutosha,wa kusikiliza habari za Mungu, na kusoma, kama utaacha mitandao ya kijamii ikupite.
Kumbuka, Mungu anatazamia kile mkristo akue siku baada ya siku.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.
Jibu: Tusome kuanzia juu kidogo.
Mwanzo 19:4 “ Hata kabla hawajalala, watu wa mji, wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote.
5 Wakamwita Lutu, wakamwambia, Wa wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Uwatoe kwetu, tupate kuwajua.
6 Lutu akawatokea mlangoni, akafunga mlango nyuma yake.
7 Akasema, Basi, nawasihi, ndugu zangu, msitende vibaya hivi.
8 Tazama, ninao binti wawili ambao hawajajua mtu mume, nawasihi nitawatolea kwenu mkawafanyie vilivyo vyema machoni penu, ila watu hawa msiwatende neno, kwa kuwa wamekuja chini ya dari yangu”
9 Wakasema Ondoka hapa! Kisha wakanena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, ANATAKA KUHUKUMU! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, wakakaribia wauvunje mlango.”
Kuhukumu kunakozungumziwa hapo sio kutoa hukumu ya adhabu.. hapana! Bali kunamaanisha “kutoa maamuzi” au “kuamua”.. Mtu anayetoa maamuzi kwa lugha ya kibiblia ni mhukumu. Watu wawili wanapopigana na akatokea mtu akawasuluhisha huyo mtu aliyewasuluhisha ni mhukumu wao, kadhalika mtawala wowote wa nchi mhukumu wa hiyo nchi.
Mfano mzuri wa kujifunza katika biblia ni Sulemani… Mfalme Sulemani aliomba kutoka kwa Mungu moyo wa kuweza kuwahukumu/kuwaamua watu kwa adili.
1 Wafalme 3:7 “Na sasa, Ee Bwana, Mungu wangu, umenitawaza niwe mfalme mimi mtumwa wako badala ya Daudi baba yangu; nami ni mtoto mdogo tu; sijui jinsi inipasavyo kutoka wala kuingia.
8 Na mtumwa wako yu katikati ya watu wako uliowachagua, watu wengi wasioweza kuhesabiwa, wala kufahamiwa idadi yao, kwa kuwa ni wengi.
9 Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili NIWAHUKUMU WATU WAKO, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?
10 Neno hili likawa jema machoni pa Bwana, ya kuwa Sulemani ameomba neno hili.
11 Mungu akamwambia, Kwa kuwa umeomba neno hili, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; wala hukutaka utajiri kwa nafsi yako; wala hukutaka roho za adui zako; BALI UMEJITAKIA AKILI ZA KUJUA KUHUKUMU;
12 basi, tazama, nimefanya kama ulivyosema. Tazama, nimekupa moyo wa hekima na wa akili; hata kabla yako hapakuwa na mtu kama wewe, wala baada yako hatainuka mtu kama wewe”.
Tukiendelea mbele kidogo.. tunaona uwezo wa kuhukumu wa Sulemani, ukidhihirika..
“22 Ndipo yule mwanamke wa pili akasema, Sivyo hivyo; bali mtoto wangu ndiye aliye hai, na mtoto wako ndiye aliyekufa. Na mwenzake akasema, Sivyo hivyo; bali mtoto wako ndiye aliyekufa, na mtoto wangu ndiye aliye hai. Ndivyo walivyosema mbele ya mfalme.
23 Ndipo mfalme akasema, Huyu anasema, Mtoto wangu yu hai, na mtoto wako amekufa. Na huyu anasema, Sivyo hivyo; bali mtoto aliyekufa ni wako, na mtoto aliye hai ni wangu.
24 Mfalme akasema, Nileteeni upanga. Wakaleta upanga mbele ya mfalme.
25 Mfalme akasema, Mkate mtoto aliye hai vipande viwili, kampe huyu nusu, na huyu nusu.
26 Ndipo mwanamke yule, ambaye mtoto aliye hai ni wake, akamwambia mfalme kwa maana moyoni mwake alimwonea mtoto wake huruma, akasema, Ee bwana wangu, mpe huyu mtoto aliye hai, wala usimwue kamwe. Lakini yule mwingine akasema, Asiwe wangu wala wako; na akatwe.
27 Ndipo mfalme akajibu, akasema, Mpe huyu wa kwanza mtoto aliye hai, maana yeye ndiye mama yake.
28 Na Israeli wote wakapata HABARI ZA HUKUMU ILE ALIYOIHUKUMU mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ILI AFANYE HUKUMU”
Umeona?…maana ya hukumu ni pana, sio tu kutoa adhabu, au kauli ya kuadhibu…kama inavyoaminika sasa…
Kwahiyo hapo, hao watu wa Sodoma walitaka Luthu asitoe maamuzi yoyote juu ya shauri lao hilo, walilokusudia kulitenda.. Kwani walitaka watolewe wale malaika waliofika kwa Luthu ili walale nao. Na hawakutaka shauri lolote juu ya hilo, walichokisema wamekisema, na walichokiamua wamekiamua…
Sasa anatokea huyu Luthu ambaye kwanza ni mgeni tu katika hiyo nchi wa Sodoma, halafu anataka kuwapangia cha kufanya, “kwamba awape binti zake wawili walale nao badala ya wale malaika”…Jambo ambalo wao hawakulitaka.. Ndio maana wakasema maneno hayo.. “Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, ANATAKA KUHUKUMU! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa”
Na sisi katika maisha yetu tuna mambo mengi ya kuhukumu, katika imani yapo mengi ya kuhukumu, katika familia zetu, katika shughuli zetu n.k kuna mambo mengi ya kuhukumu.. Na hivyo inahitajika siku zote hekima ya kiMungu ili kuhukumu kwa adili. Si lazima wakati wote tuombe tu mali na mafanikio ya kidunia kutoka kwa Mungu. Ni vizuri tukamwomba hekima ya kuhukumu kwa Adili kama Sulemani alivyoomba, na kwasababu Mungu anajua pia hayo mengine tuna haja nayo, hivyo atatuzidishia sawasawa na Neno lake, kama alivyomzidishia Sulemani.
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?