Tofauti na makabila mengine 11 ambayo Yakobo aliyabariki kama tunavyosoma katika kitabu cha Mwanzo ile sura ya 49. Kabila la Isakari ndio kabila, lililokubali utumishi, tena sio utumishi tu ilimradi utumishi bali utumishi kama wa Punda kwa watu wa Mungu. Unaweza kusema wana wa Isakari walikuwa wajinga, kuongozwa na roho ya punda kama wasemavyo watu sasa hivi. Lakini maandiko yanatuambia, walifanya hivyo kwasababu waliona ni nini kipo mbele yao. Waliona nchi nzuri ya utukufu ikiwangojea, waliona mahali pa mapumziko ya milele pako mbele yao panawasubiri, na hivyo ili kufikia nchi hiyo ni sharti leo hii watumike sana. Soma..
Mwanzo 49:14 “Isakari ni punda hodari, Ajilazaye kati ya mazizi ya kondoo;
15 Akaona mahali pa raha, kuwa pema, Na nchi, ya kuwa ni nzuri, Akainama bega lake lichukue mizigo, Akawa mtumishi kwa kazi ngumu”.
Unaona, alikubali kujishusha, ili awe mtumishi wa kazi ngumu. Kama vile Punda moja anayebeba chakula cha kondoo wengi zizini. Ndivyo alivyojiona kwa wengine. Na matokeo yake biblia inatuambia, wana wa Isakari walikuja kuwa wenye akili nyingi za kujua majira ya nyakati Zaidi ya wote. Ndio waliokuwa wanategemewa na Israeli nzima, kutoa taarifa juu ya nyakati za neema na hukumu zilizoamriwa na Mungu. Akili hizo na hekima hizo walipewa na Mungu mwenyewe.
1Nyakati 12:32 “Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao”.
Je! Na sisi tunaweza kufananishwa na wana wa Isakari? Unajua ni kwanini leo watu hatutaki kumtumikia Mungu, ni kwasababu hatuoni yaliyo mbele yetu, tunaona ya hapa hapa tu, hatuona majira ya neema yanayokuja huko mbeleni, hatuioni Yerusalemu mpya na nchi mpya tuliyoahidiwa na Mungu. Hatuoni Karamu ya mwanakondoo ambayo Yesu alikwenda kutuandalia kwa miaka 2000 sasa ipo karibuni kuanza. Na ndio maana hatutaki leo hii kujitia katika utumishi wa Mungu. Tunachojua ni kujitia katika utumishi wa kusumbukia maisha, tupate magari, tupate majumba, mashamba, tuwe mabilionea., hayo tu, Mambo ambayo fahari yake inaishia hapa hapa duniani.
Hata kuhudhuria ibada tunaona ni mzigo mzito, lakini tupo radhi kufanya kazi siku 365 bila kuchoka, usiku na mchana, tupo radhi kutazama Tv kila siku, lakini kusoma aya moja ya biblia na kuitafakari ni mtihani kwetu..Kama hayo yakitushinda tutawezaje, kuwa watumishi wa Mungu?
Wana wa Isakari waliitambua ile kauli ya Bwana Yesu kabla hata ya yeye mwenyewe kuja..kwamba ukubwa katika ufalme wa mbinguni, sio kuwa na sifa, na ujuzi, na vyeo, na kutumikiwa, hapa duniani, bali ni katika utumishi kwa wengine.. ndio maana wao wakaamua kuwa vile.
Mathayo 20:25 “Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.
26 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu;
27 na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu;”
Je! Na sisi tunaiona sawasawa hiyo nchi nzuri na ya kumeta meta kule ng’ambo? Kama ndivyo basi tuwe radhi kuwa Punda kwa kondoo wa Mungu, kama ilivyokuwa kwa wana wa Isakari. Tukubali kumtumikia Mungu,bila kutafuta faida zetu wenyewe. Tukubali kuwatanguliza wengine, na sio sisi tu wenyewe na matumbo yetu, kila siku. Ili siku ile Kristo akaketi pamoja na sisi katika kiti chake cha enzi mbinguni.
Kumbuka hizi ni siku za kumalizia, wakati tuliobakiwa nao ni mfupi sana,Injili tuliyonayo sio ya kuliliwa liliwa tena uokoke. Kwasababu muda wake umeshaisha, tumebakiwa na injili ya Ushuhuda tu. Ili siku ile watu wasije wakasema hawakuhubiriwa injili. Embu jiulize wewe ambaye upo kwenye mawazo mawili mawili, ni ujasiri gani unapata kuishi maisha ya namna hiyo?
Unyakuo ukipita leo hii usiku na ukaachwa utamweleza nini Kristo? Au kifo kikikuta ghafla, huko unapokwenda utakuwa mgeni wa nani? Kuzimu ipo na haishi watu kama maandiko yanavyosema. Na ibilisi anataka uendelee katika hali hiyo hiyo, ili mabaya yakukute kwa ghafla, kama yalivyowakuta wenye dhambi wote waliotangulia kuzimu.
Tubu dhambi zako, na Zaidi sana ukawe mtumishi wa Mungu, ufanye kusudi lake hapa duniani. Kwasababu hilo ndilo uliloitiwa.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
WAENDEE WANA WA ISAKARI, UWE SALAMA.
UFUNUO: Mlango wa 17
NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.
Wibari ni nani?(Mithali 30:26)
SWALI: Shalom naomba kujua nini maana ya huu mstari “Roho za manabii huwatii manabii? (1Wakorintho 14:34)
JIBU: Labda tusome kuanzia juu kidogo ili tupate picha kamili mstari huo ulikuwa unamaana gani..
1Wakorintho 14:26 “Basi, ndugu, imekuwaje? Mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi, ana fundisho, ana ufunuo, ana lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kwa kusudi la kujenga.
27 Kama mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri.
28 Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu.
29 Na manabii wanene wawili, au watatu, na wengine wapambanue.
30 Lakini mwingine aliyeketi akifunuliwa neno, yule wa kwanza na anyamaze.
31 Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.
32 NA ROHO ZA MANABII HUWATII MANABII.
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu”.
Ukisoma hapo utaona kuna ustaarabu ulizuka miongoni mwa wakristo wa kanisa la Korintho. Walipokuwa kutanika kanisani, kila mtu alikuwa na neno la kusema, kila mtu alikuwa na wimbo wake spesheli wa kumwabudu Mungu, kila mtu alikuwa na ufunuo wake, kila mtu alikuwa na fundisho lake jipya la kuliwasilisha kanisani, kila mtu alikuwa na lugha na tafsiri yake mwenyewe..
Embu tengeneza picha, kila mtu kanisani anazo karama zote, wote wanataka kufundisha kwasababu wamepokea mafunuo, wote wanataka kutabiri kwasababu ni manabii, wote wanataka kufasiri lugha, wote wanataka kuwa waongozaji kwaya n.k…
Utagundua jambo kama hilo likiwepo kanisani, ni wazi kuwa hakutakuwa na kujengana tena, bali mavurugano tu, kwasababu hakuna utaratibu, hivyo hata kuielewa sauti ya Mungu itakuwa ni shida.
Kwamfano tengeneza picha umeenda kwenye shule yenye waalimu wengi, halafu kila mwalimu anataka afundishe masomo yote, hesabati, yeye, kemia yeye, baolojia yeye, na mwingine hivyo hivyo, jiulize wanafunzi wataelewaje? Hawawezi kuelewa bali watachanyikiwa, ni wapi wajifunze, au mwalimu yupi wamsikilize…
Halikadhalika na katika kanisa la wakorintho, Paulo aliwaagiza, wasiwe na utaratibu huo, hata kama imetokea watu 10 au 20 au 50 katika kanisa wamepewa ufunuo kwa wakati mmoja, hawapaswi wanene wote, bali wawape ruhusa walau wawili au watatu tu, na hao wengine wabakie kupambanua..
Na kama ikitokea hao ambao hawajapewa nafasi ya kunena na bado wanang’ang’ania tu wanene na wao, wanapaswa wakumbuke huo msemo wa Paulo kwamba “ROHO ZA MANABII HUWATII MANABII”
Maana yake ni kuwa kama wao ni manabii, wanapaswa watii utaratibu wa manabii wenzao uliowekwa. Hata kama wao hawajapewa nafasi. Kwasababu Mungu sio Mungu wa machafuko,. Na vilevile kama ikatokea mwingine aliyeketi amefunuliwa jambo kubwa zaidi, basi yule wa kwanza, anapaswa awe radhi kumpisha mwenzake, na yeye atulie, kwasababu mambo yote yanafanywa kwa lengo la kulijenga kanisa, na sio kwa lengo la mashindano, au kwa lengo la kutoa mafunuo mengi, ambayo yatafanya kanisa likose shabaha ya kujua kusudi la Mungu ni nini.
Hata sasa, utaratibu huu unapaswa uwe mwendelevu katika makanisa, sio maono yote au mafunuo yote watu waanaoonyeshwa na Mungu yanapaswa yafundishwe ndani ya kanisa kwa wakati huo huo, hapana, vinginevyo tutazama kwenye machafuko na mikanganyiko mingi, bali vichaguliwe viungo viwili au vitatu katika vyenye karama hiyo, kisha sisi wengine tubakie kupambua, na hao wengine wapewe nafasi wakati mwingine..Ili tuweze kumwelewa Mungu.
Lakini kama ikitokea mmojawetu anataka kujiona na yeye ni lazima ya kwake isemwe, akumbuke usemi ule..”Roho za Manabii, huwatii manabii”. Awe tayari kuwatanguliza wenzake kwanza, Kwasababu Mungu si Mungu wa machafuko bali wa utaratibu.
Bwana akubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Ampokeaye nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; Mstari huu unamaana gani?.
SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.
Nabii Eliya alikuwa na Imani ya kutosha hata kushusha moto kutoka mbinguni, kuwaangamiza maadui zake, lakini masaa machache tu! baada ya kushusha moto juu ya dhabihu ile, alimkimbia mwanamke mmoja mchawi aliyeitwa Yezebeli (alimkimbia kwa hofu kabisa), ili kujiokoa nafsi yake (1Wafalme 19). Ni sawa na fahali la ng’ombe na nguvu zake zote, halimwogopi fahali mwenzake, linapigana naye, lakini linamwogopa mbwa na kumkimbia kabisa..ndicho kilichomtokea Nabii Eliya. Alikuwa na Imani ya kuangushwa maadui zake walio magwiji, lakini aliizimisha kwa kumwogopa mwanamke mmoja tu!.
Pia tunaweza kujifunza kwa Petro, mtume wa Bwana Yesu..
Mathayo 14:24 “Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho.
25 Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.
26 Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu.
27 Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope.
28 Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.
29 Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu.
30 Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.
31 Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, EWE MWENYE IMANI HABA, MBONA ULIONA SHAKA?”
Hapo Mtume Petro, alikuwa na imani ya kuanzia lakini ya kumalizia hakuwa nayo, hatimaye akaanza kuzama kabla ya lengo lake kutimia.
Nasi pia tukumbuke Moto tuliokuwa nao wakati tunamwamini Yesu, ni lazima tuwe nao huo huo, tena na zaidi wakati wa mwisho wa maisha yetu..Hatupaswi hata kidogo kubaki na historia kichwani tu kwamba, miaka Fulani nilikuwa moto sana, miaka Fulani nilikuwa naweza kukesha kusali, miaka Fulani nilikuwa nashuhudia sana, miaka Fulani nilikuwa nasoma Neno sana.
Ukijiona juzi, au mwaka jana ulikuwa moto kuliko mwaka huu, tambua kuwa tayari umeshaanza kuzama…Imani yako imeshaanza kuwa haba!.. Unahitaji kumpigia yowe Bwana Yesu leo! Akusaidie.. Ukiona zile dhambi ambazo ulikuwa unaweza kuzishinda kirahisi mwaka jana lakini mwaka huu huwezi, leo ni wakati wa kupiga yowe, kabla ya hujamalizikia kuzama kabisa..Ukiona ulikuwa unaweza kusali masaa kadhaa lakini leo nusu saa tu ni shida!, unasinzia!, nguvu ya kulisoma Neno huna tena…hapo huna budi kupiga yowe kuomba msaada..kwasababu imani yako imeanza kupungua.
Ukiona ule ujasiri dhidi ya dhoruba zote za shetani, unaanza kupotea ndani yako, unahitaji kumlilia Bwana, ukiona hofu ya wachawi na madhara ya adui yamekuzingira, tofauti na hapo kwanza, ambapo ulikuwa na ujasiri wa kutohofu chochote, basi jua imani yako imeanza kutindika!.. huna budi kumpigia Bwana yowe! Kama ishara ya kutaka msaada..
Poteza kila kitu lakini usipoteze imani yako…kwasababu Imani ni ulinzi. Kamwe huwezi kumshinda adui shetani, na dhoruba zake kama imani yako ipo chini.
Hivyo chunguza maisha yako leo!.. Je! Bado unayo imani ya kumalizia? Kama huna..leo hii kumbuka uliko toka, kumbuka uweza wa Mungu, mwanzo ulipomwamini, na mlilie Bwana, umwambie unahitaji Imani ya kwanza, na fanya hivyo kwa kumaanisha huku, ukirekebisha makosa yako yote ambayo yalikufanya urudi nyuma..Na Bwana atakusaidia kama alivyomsaidia Petro.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?
Katika kitabu cha Kutoka 3:2, tunasoma ni Malaika wa Mungu ndiye aliyemtokea Musa, lakini tukiendelea mbele katika Mstari wa 4, tunaona ni Mungu ndiye anayezungumza na Musa, na si Yule malaika tena, hapo imekaaje?
Jibu: Tuisome habari hiyo…
Kutoka 3: 2 “Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea
3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.
4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.
5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.
6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu”.
Aliyemtokea Musa ni Malaika wa Mungu, na si Mungu mwenyewe… na malaika huyo alimtokea katika mwonekano wa Moto.. (kumbuka malaika wanaweza kuchukua mfano wa umbile lolote, wanaweza kuchukua umbile la mtu, au moto, au mwanga), wanapochukua umbile la kibinadamu wanaonekana kama wanadamu, mfano wa yule aliyemtokea Yoshua katika kitabu cha Yoshua 5:14, wanapokuja katika maumbile haya wanakuwa kama watu kabisa, wanaweza kuonekana na kuzungumza. Kadhalika wanaweza kuja katika maumbile kama ya mwanga au moto..katika maumbile haya, unaweza kusikia sauti tu na usione mtu..ukaona tu huo mwanga au moto!. N.k
Sasa Malaika huyu alitumwa na Mungu kwa Musa akiwa amebeba ujumbe wa Mungu, na alimtokea Musa katika umbile la Moto, maana yake Musa aliona moto tu kwenye kile kijiti na kusikia sauti lakini hakuwa anaona mtu.
Sasa jambo moja la kujifunza ni kwamba, Malaika wanapobeba ujumbe wa Mungu, na Mungu anapoweka jina lake ndani yako,na kuwatuma, wanaweza kutoa ujumbe kana kwamba ni Mungu mwenyewe ndiye anasema ndani yao..Sasa katika huyu Malaika aliyezungumza na Musa, Mungu alikuwa ameweka neno lake ndani yake, kiasi kwamba lolote atakalozungumza ni Mungu ndio kazungumza…(Sasa sio kwamba ni lolote atakalojiamulia tu yeye kusema!..hapana..bali ni lile ambalo Mungu atakalomwambia alifanye na kulisema ndilo atakalolisema).. Tunaweza kusoma hilo vizuri…
Kutoka 23:20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.
21 Jitunzeni mbele yake, MWISIKIZE SAUTI YAKE; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa JINA LANGU LIMO NDANI YAKE.
22 LAKINI UKIISIKIZA SAUTI YAKE KWELI, NA KUYATENDA YOTE NINENAYO MIMI; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao”.
Hapo mstari wa 22, anasema “lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi”..Maana yake “Bwana atanena kupitia yule malaika, chochote Yule malaika atakachokisema ni Bwana kakisema”. Jambo hilo liliwezekana kwa malaika tu! ila kwa sehemu ndogo! (si wakati wote Mungu alizungumza na watu kupitia malaika wake kama alivyofanya kwa Musa hapo)..…
Lakini zamani hizi limewezekana kwa asilimia zote kupitia mmoja tu YESU KRISTO!! MKUU WA UZIMA.. Huyo amefanyika bora kupita malaika, akisema ni Mungu kasema asilimia 100!, Maneno yake ni Maneno ya Mungu,..kwasababu amefanyika Bora kupita malaika haleluya!!! (Tutakuja kuliona hilo vizuri mbeleni kidogo!!).
Lakini tukirudi katika upande wa Malaika aliyezungumza na Musa, tunaona baadaye, mbeleni kabisa wana wa Israeli walipoanza kuzembea kuwafukuza wale wenyeji wa miji ile, tunaona Yule malaika aliyepewa maneno ya Bwana kinywani mwake, akitokea na kuanza kuzungumza, kana kwamba ni Bwana mwenyewe ndiye anayezungumza…
Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi;
2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?
3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.
4 Ikawa, hapo huyo malaika wa Bwana alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia
5 Nao wakaliita jina la mahali pale Bokimu; nao wakamchinjia Bwana sadaka huko”.
Umeona hapo?..aliyewatoa wana wa Israeli Misri kuwapeleka Kaanani ni Bwana, na si malaika, lakini Bwana alimpa Malaika wake jukumu zima, na vile vile, aliweka maneno yake ndani ya Yule malaika, kiasi kwamba atakachokinena Malaika yule, ni Bwana kakinena, na atakachokifanya malaika Yule ni Bwana kakifanya, vile vile Agano lake aliliweka ndani ya Yule malaika, kiasi kwamba atakayevunja agano lile la Yule malaika, ni sawa kalivunja agano la Mungu..kwasababu Neno lake limejaa ndani ya Malaika yule, anakuwa si yeye tena, bali ni Mungu anazungumza ndani yake.
Sasa katika agano hilo la kwanza, Mungu alizungumza ndani ya Malaika, lakini si wakati wote,(wakati mwingine Bwana alisema pasipo kuwatumia hao malaika).. lakini katika agano jipya, Mungu amejitwalia chombo chake, ambacho ametia maneno yake yote ndani yake, na agano lake lote ndani yake, zaidi ya alivyofanya kwa malaika…Chombo hicho hakina pumziko, wakati wote kikinena ni Mungu kanena..na chombo hicho si kingine zaidi ya Bwana Yesu…Huyu kafanyika bora kuliko malaika!!..
Waebrania 1:1 “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,
2 mwisho wa siku hizi AMESEMA NA SISI KATIKA MWANA, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.
3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;
4 AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA, KWA KADIRI JINA ALILOLIRITHI LILIVYO TUKUFU KULIKO LAO”
Umeona sauti ya Mungu leo ipo wapi?..umeona agano la Mungu leo lipo wapi?..si kwa mwingine zaidi ya kwa YESU!.. Huyo ni zaidi ya Yule malaika aliyezungumza na Musa pale kwenye ule mwali wa Moto.. Na kama agano la kwanza ambalo Bwana alinena kupitia malaika lilikuwa na utukufu mkubwa vile, kiasi kwamba yeyote atakayelivunja neno la malaika Yule alikufa,. hili la pili ni mara nyingi zaidi..biblia inasema hivyo..
Waebrania 2:1 “Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.
2 Kwa maana, IKIWA LILE NENO LILILONENWA NA MALAIKA LILIKUWA IMARA, na kila kosa na uasi ULIPATA UJIRA WA HAKI,
3 sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? AMBAO KWANZA ULINENWA NA BWANA, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”.
Je umempokea Yesu?.. Je! Umeyakabidhi maisha yako yote kwake?..fahamu kuwa Mamlaka yote ya mbinguni na duniani kapewa yeye..na yeye ndiye sauti ya Mungu kwetu!, ukimkataa yeye umemkataa Mungu, ukimkubali yeye umemkubali Mungu..
Kama bado hujamwamini, nafasi yako ya kumpokea ndio sasa, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kujitenga kwa muda, kisha kupiga magoti binafsi na kumkiri Yesu kwa kinywa chako kuwa ndiye Bwana na mwokozi wa ulimwengu, na kisha kukiri makosa yako kwa kutubu, huku umedhamiria kutofanya tena dhambi hizo, na baada ya hapo haraka sana bila kuchelewa tafuta ubatizo sahihi kama bado hujabatizwa ubatizo sahihi, kumbuka ubatizo ulioagizwa na Bwana Yesu ni ule wa maji mengi na kwa jina la YESU (Matendo 2:38), na baada ya hapo, Roho Mtakatifu atakuongoza katika yote yaliyosalia, ikiwemo kukupa uwezo wa kushinda dhambi.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.
Jibu: Tusome,
Marko 12:26 “Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, SURA YA KIJITI, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?”
Neno “sura” kama lilivyotumika hapo sio “uso”..kama huu wenye pua, na macho na masikio.. bali limetumika kuwakilisha “mlango fulani” katika maandiko.. Kama tunavyojua tukitaka kupata habari Fulani katika maandiko, huwa tunafungua biblia na kusema fungua kitabu Fulani, mlango Fulani utapata habari hiyo.
Kwamfano tukitaka kupata habari ya kufufuka kwa Bwana tunazipata katika kitabu cha Luka Mlango wa 24..Sasa badala ya kutumia neno mlango, wakati mwingine tunatumia neno “Sura”..hivyo ni sawasawa na kusema “habari za kufufuka kwa Bwana Yesu tunazipata katika kitabu cha Luka sura ya 24”.
Kadhalika hapo Mtume Paulo alikuwa anamaanisha “Sura ile katika maandiko ambayo Mungu alizungumza na Musa kupitia kile kijiti kilichokuwa kinawaka moto lakini hakiteketei”.. Na hiyo si nyingine zaidi ya ile sura ya 3 katika kitabu cha “Kutoka”…tusome.
Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.
2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea.
3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu KIJITI HIKI HAKITEKETEI.
4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka KATIKATI YA KILE KIJITI, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.
5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.
6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.
7 Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri”
Kwahiyo “Sura” ni “Mlango”..Na kijiti kilichozungumziwa hapo sio kipande kidogo cha mti, bali ni “kichaka”.
Hivyo kikubwa tunachoweza kujifunza hapo ni kwamba Mungu ni Mungu wa walio hai… Alijitambulisha kwa Musa kama Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.. Kwasababu Watu hao ingawa wamekufa sasa, lakini huko waliko wanaishi…kama Bwana Yesu mwenyewe alivyosema katika kitabu cha Yohana..
Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi”
Hivyo Ibrahimu, Isaka na Yakobo wanaishi sasa, na hivyo Mungu ni Mungu wao hata sasa… kadhalika na sisi tukiishi kwa kumwamini Yesu, na kuishi kulingana na mapenzi yake hapa duniani, tutakapokufa bado tutakuwa tunaishi katika paradiso ya raha, na baadaye tutafufuliwa kutoka huko paradiso na kuvikwa miili ya utukufu na kwenda na Bwana mbinguni, katika siku ile ya unyakuo..
Waebrania 11:16 “Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. KWA HIYO MUNGU HAONI HAYA KUITWA MUNGU WAO; maana amewatengenezea mji”.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?
Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?
Bwana Yesu sio tu mzaliwa wa kwanza wa waliokufa bali pia ni mzaliwa wa kwanza wa wanadamu wote walio hai.
Kwanini ni mzaliwa wa kwanza wa walio hai pia?.
Ni Kwasababu wote walio hai, hawana budi kuzaliwa tena mara ya pili ili wahesabike kuwa wana wa Mungu (Yohana 3:6). Ndio maana Bwana Yesu anabaki kuwa mzaliwa wa kwanza wa wanadamu wote..kwasababu ni yeye pekee tu ndiye aliyezaliwa mkamilifu, hana haja ya kuzaliwa mara ya pili, lakini sisi wengine wote hatuna budi kuzaliwa mara ya pili…
Warumi 8:29 “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ILI YEYE AWE MZALIWA WA KWANZA MIONGONI MWA NDUGU WENGI”.
Na ni kwanini yeye pia ni Mzaliwa wa kwanza wa waliokufa!.
Kabla ya kujua ni kwanini yeye ni mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, ni vyema tukajua kwa kina maana ya kuzaliwa.. Kuzaliwa ni kitendo cha kutoka katika upeo mmoja kuingia katika upeo mwingine..Tunapozaliwa hapa ulimwenguni, ni kwamba tumetoka katika upeo mwingine tusioujua sana ulio juu, na kuja katika huu ulimwengu.. hapo tunasema tumezaliwa.. Kadhalika mtu anayetoka katika upeo mwingine ulio chini na kuja katika huu ulimwenguni, naye pia huyu kazaliwa!, kwasababu hakuwepo katika ulimwengu lakini sasa yupo!..kuzaliwa huko ndio tunakuita kufufuka!
Hivyo baada ya Kristo kufa, yeye pekee ndiye mtu wa kwanza kufufuka!. (kuzaliwa kutoka katika wafu)
Sasa utauliza kama yeye ni wa kwanza vipi wale watu waliofufuliwa na nabii Elisha kabla yake, na Eliya, au vipi kuhusu Lazaro ambaye Bwana mwenyewe alimfufua!..
Kumbuka hao wote ni kweli walifufuliwa lakini baadaye walikuja kufa tena!.. Lazaro ni kweli alifufuliwa lakini alikuja kufa tena!..na wengine wote ni hivyo hivyo.. Lakini Bwana Yesu alipofufuka hakufa tena, yupo hai milele na milele..Na baada yake yeye ndio wafu wote wanafuata kufufuliwa, ili wasife tena.. ambapo yeye anabaki kuwa mzaliwa wa kwanza kutoka katika mauti..
Ndio maana biblia inasema..
Wakolosai 1:17 “Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.
18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, NI MZALIWA WA KWANZA KATIKA WAFU, ili kwamba awe mtangulizi katika yote.
19 Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;
20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni”.
Na tena inasema..
Yohana 1:5 “tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, MZALIWA WA KWANZA WA WALIOKUFA, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake”
Pia unaweza kusoma Waebrania 1:5, 1Wakorintho 15:20, na Wakolosai 1:15.. Inaelezea zaidi juu ya Kristo kama mzaliwa wa kwanza waliokufa.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Kristo ndiye Mzaliwa wa kwanza wa kila kitu.(Ni mwanzo na Mwisho) Na mzaliwa wa kwanza siku zote ndiye mrithi!..sisi wengine tuliozaliwa mara ya pili katika roho ni kama wadogo zake. (Yeye ndio wa kwanza, sisi tunafuata) .Hivyo na sisi tunapozaliwa mara ya pili, tunazirithi ahadi za Mungu pamoja na Kristo..
Lakini kama hatutazaliwa mara ya pili, hatutaweza kuwa warithi..
Sasa tunazaliwaje mara ya pili?
Tunazaliwa mara ya pili, kwa kumwamini Yesu kama mzaliwa wa kwanza wa vitu vyote, na kwamba yeye ndiye aliyakabidhiwa urithi wote wa ahadi za Mungu, kwasababu ndiye mzaliwa wa kwanza..
Na baada ya kujua hilo na kuamini hilo, basi hatua inayofuata ni kutubu dhambi zetu zote tunazozifanya kwa wazi au kwa siri, na kujinyenyekeza chini yake na kisha tunatafuta ubatizo sahihi, ambao ni ule wa maji mengi na kwa Jina la Yesu Kristo kulinga na (Matendo 2:38) na kwa ubatizo wa Roho Mtakatifu ambao tutakuwa tumeupokea, huo unatufanya kuwa wakamilifu..Kwasababu Bwana Yesu mwenyewe alisema katika Marko 16:16, kwamba aaminiye na kubatizwa ataokoka, na pia alifafanua vizuri kwa Farisayo Nikodemo maana ya kuzaliwa mara ya pili, kwamba ni kwa Maji na kwa Roho.. Maana yake kwa ubatizo wa maji na wa Roho Mtakatifu!.
Yohana 3:4 “Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”
Na kumbuka kuzaliwa ni hatua ya kwanza tu!..huna budi kuukulia wokovu kwa kumtafuta Mungu kwa bidii, unapozidi kumtafuta Mungu, ndivyo unavyozidi kukua kiroho, na hatimaye unafikia utimilifu ule Mungu anaotaka wewe uufikie.
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Habari za Esau na Yakobo zina mafunzo makubwa sana kwetu,. Unajua biblia inaposema mambo yote yaliyoandikwa katika agano la kale yalikuwa ni kwa ajili ya kutuonya sisi, ilimaanisha kweli (Soma 1Wakor 10:11). Hivyo tunapaswa tusome kwa umakini mkubwa sana kwasababu hakuna jambo ambalo linaendelea sasa hivi duniani halijaandikwa kwenye biblia.
Ulishawahi kujiuliza ni kipindi cha siku ngapi, au wiki ngapi, au miaka mingapi kilipita, tangu ule wakati Esau anauza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa mdogo wake, mpaka ule wakati Baba yao anawabariki. Unaweza kudhani ni kipindi kifupi sana wakiwa bado ni watoto, lakini sio.
Ni kweli wakati Esau anauza haki yake, walikuwa bado ni vijana wadogo, kulingana na hadithi za wayahudi, siku ile Esau alipomfuata ndugu yake ni kumuuzia haki yake kwa chakula cha dengu alipokuwa ana njaa inasadikika walikuwa na umri wa miaka 15.
Lakini wakati ambao Baba yao sasa anakaribia kufa, walikuwa si watoto tena, bali watu wazima sana, Kulingana na hadithi hizo hizo za kiyahudi walikuwa ni wazee wa miaka 63, kwasababu wakati tu Esau anaoa wake wahiti alikuwa na umri 40, (Mwanzo 26:34) na hapo bado sana baba yao kuwabariki kwahiyo zaidi ya miaka 48, Yakobo alikuwa anaipigania tu ile haki ya mzaliwa wa kwanza.
Lakini nataka leo tuone kwa undani ni kwanini, Mungu alimchukia Esau, kwa ile tabia yake kama tunavyoma katika maandiko.
Warumi 9:13 “Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia”.
Wengi tunadhani ni kwa kosa la kule tu kile chakula alichopewa na ndugu yake baada ya kutegewa mtego wakati alipokuwa na njaa.. Ukweli ni kwamba Mungu asingeweza kuchukizwa na Esau kirahisi hivyo, kwa kosa la njaa, bali alichukizwa na Esau kwa ile kauli yake aliyoitoa ambayo aliendelea kuisimamia katika maisha yake yote..
Na kauli yenyewe ndio ile tunayoisoma katika biblia..(Zingatia vifungu vilivyo katika herufi kubwa)
Mwanzo 25:29 “Yakobo akapika chakula cha dengu. Esau akaja kutoka nyikani, naye alikuwa amechoka sana.
30 Esau akamwambia Yakobo, Tafadhali, unipe hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo walimwita jina lake Edomu.
31 Yakobo akamwambia, Kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza.
32 Esau akasema, TAZAMA, MIMI NI KARIBU KUFA, ITANIFAA NINI HAKI HII YA UZAZI?
33 Yakobo akamwambia, Uniapie kwanza. Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza.
34 Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. HIVYO ESAU AKAIDHARAU HAKI YAKE YA MZALIWA WA KWANZA”.
Sasa zingatia hiyo kauli ya Esau..”mimi ni karibu na kufa, itanifaa nini hii haki ya uzazi”.. Ni heri angesema, “Haya nitakupa” Lakini yeye alisema ninakaribia kufa, itanifaidia nini hiyo haki za uzazi, akiwa na maana hiyo haki kama haiwezi kumtatulia matatizo yake aliyokuwa anapitia kwa wakati ule, haina maana yoyote, ni ya kudharauliwa tu,
Na ndio maana ukindelea kusoma utaona biblia inasema.. tangu huo wakati Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza,..Unaona bado aliendelea kushikilia msimamo wake huo huo, kwa miaka zaidi ya 40, mpaka siku ile ya kubarikiwa na baba yao ilipofika, alipogundua umuhimu wa Baraka hizo alikuwa ameshachelewa, japo alitafuta kila namna ya kumpendeza baba yake lakini jambo hilo halikufanikiwa hata kidogo, biblia inatuambia, alilia kwa machozi mengi yasiyoelezeka. Soma
Waebrania 12:16 “Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja.
17 Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), ijapokuwa aliitafuta sana kwa machozi”.
Ndugu, hii roho ya Esau mpaka leo inafanya kazi sana, tena sana , nimekutana na watu wengi, unapowahubiria injili, ambayo ni kwa faida yao wenyewe, jambo la kwanza watakalokuuliza, nikiokoka, Yesu atanipa pesa za kumudu maisha yangu leo?, ukimwambia zitakuja kwa wakati wake, atasema, Basi simtaki hana faida kwangu, mwingine utampa kipeperushi chenye habari za wokovu,atatazama kidogo, halafu saa hiyo hiyo atakuambia nilidhani unanipa pesa, wewe unanipa makaratasi, anakitupa hapo hapo mbele yako,.. Sasa watu kama hawa hawana tofuati na Esau, ambaye alikuwa anaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwasababu haikuweza kumtatulia matatizo yake ya wakati ule.
Ndugu usiutafute wokovu wa kutatuliwa shida zako za sasa, kamwe usifanya hivyo, Mungu atakuona wewe ni kama Esau tu. Vilevile kama na wewe ni mmojawapo, wa wanaoidharau injili, ipo siku utautafuta wokovu kwa machozi mengi na kulia na kusaga meno na hautaupata.. Siku hiyo utakapoona, wenzako hawapo tena duniani wameshanyakuliwa wameenda mbinguni kwenye karamu ya mwana-kondoo, wanashangalia, kwa furaha isiyo na kifani, na wewe upo hapa duniani, huna lolote nakuambia siku hiyo utalia sana..Leo unacheka lakini hiyo siku utalia sana,.
Mathayo 8:11 “Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;
12 bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.
Mpaka sasa hakuna asiyejua kuwa unyakuo upo karibuni kutokea, tumebakiwa na siku chache sana pengine wiki, au miezi, lakini tujue kizazi chetu kimekidhi vigezo vyote vya kushuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa Yesu duniani. Swali ni je! Wewe umejiwekaje tayari leo? Je! Ni kama Yakobo ambaye usiku na mchana alikuwa anautafuta urithi usioharibika kwa hali na mali, au kama Esau aliyedharau Baraka za mbali kwa mafanikio, na pesa za muda tu.
Jibu unalo.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?
Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?
Jina la Bwana wetu Yesu, libarikiwe, karibu tujifunze biblia..
Mwanzo 22: 6 “ Basi Ibrahimu akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja.
7 Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinena, Babangu! Naye akasema, Mimi hapa, mwanangu. Akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?
8 Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. Basi wakaendelea wote wawili pamoja.
9 Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko, akaziweka tayari kuni, kisha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.
10 Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.
11 Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.
13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire, kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana”.
Kabla ya kufika mlimani Isaka alimwuliza Baba yake “Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?”.. Lakini Ibrahimu hakuwa na jibu la uhakika!.. Akaishia tu kusema.. “Bwana atajipatia mwanakondoo”..lengo la Ibrahimu kusema vile ni kumfumba tu macho!, mwanae Isaka asijue kuwa yeye ndiye anayekwenda kuchinjwa..
Na walipofika katika mlima wa Bwana, Ibrahimu tayari akiwa ameshamfunga mwanawe kwaajili ya kumchinja, tunasoma… Malaika wa Bwana alimzuilia na kumfumbua macho amwone mwanakondoo aliyekuwa amenaswa pembe zake kwenye kichaka kilichopo nyuma yake.
Kondoo yule haijulikani alitoka wapi, pengine alipotea wakati wachungaji walipokuwa wanachunga huko milimani, na kunaswa kwenye kichaka kimoja wapo katika huo mlima, mahali pale pale Ibrahimu alipofika..Hivyo kwa vyovyote vile ilivyokuwa, lakini mwisho wa siku tunaona, tayari Mungu alikuwa amemwandaa mwanakondoo yule kwaajili ya sadaka ya kuteketezwa..
Nanichotaka uone ni kuwa sadaka inayompendeza Bwana haipatikani chini, bali inapatikana juu katika Mlima wa Bwana… Ndio maana hapo katika mstari wa mwisho tunasoma…
“Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire, kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana”…
Kumbuka sio katika mlima mwingine wowote itapatikana, la! Bali katika MLIMA WA BWANA TU!..Ndio maana hapo anasema “kama watu wasemavyo”..maana yake watu walishafanya utafiti na kugundua kuwa Baraka za Mungu hazipatikani mahali pengine popote, au katika mlima mwingine wowote isipokuwa katika Mlima wa Bwana. Sasa tangu huo wakati wayahudi wakapaheshimu mahali hapo Ibrahimu alipomchinja huyo mwana kondoo, na mahali hapo ndipo pakajulikana kama Mlima wa Bwana tangu wakati huo, na ndipo hekalu la Mfalme Sulemani lilipojengewa.. Hivyo baraka zote walikuwa wanazipata kutoka katika nyumba ile ya Mungu, ambayo ilijengwa juu ya mlima huo wa Bwana, uliojulikana kama Mlima Moria..(ndipo mahali pa juu Bwana alipopachagua)
Lakini baada ya Bwana Yesu kuja, Mlima wa Bwana ulibadilika kutoka “kuonekana kwa macho” mpaka “kutokuonekana kwa macho”
Tusome,
Yohana 4:20 “Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.
21 Yesu akamwambia, Mama, UNISADIKI, SAA INAKUJA AMBAYO HAMTAMWABUDU BABA KATIKA MLIMA HUU, WALA KULE YERUSALEMU.
22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.
23 LAKINI SAA INAKUJA, NAYO SASA IPO, ambayo waabuduo halisi WATAMWABUDU BABA KATIKA ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.
Umepaona mlimani kwa Bwana leo?.. Si kule Yerusalemu, wala si katika mojawapo ya milima tunayopanda kwenda kuomba kila siku… bali ni katika Roho, na si katika Roho tu..bali katika Roho na kweli.
Unapompokea Yesu katika maisha yako, na kubatizwa na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu na kuishi katika Neno la Mungu.. Hapo tayari upo mlimani kwa Bwana. Kwasababu umebatizwa katika Roho Mtakatifu na vile vile unaishi katika Kweli ya Neno la Mungu.
Je leo upo mlimani kwa Bwana au bado upo chini?.. Kumbuka Baraka za kweli za Mungu zipo mlimani..huna budi kumchukua mwanao mpendwa na kuanza safari ya kwenda naye mlimani…Njia ya mlimani ni msalaba wa Bwana Yesu.
Mwanao mpendwa ni nini leo hii?..je! ni kazi yako?, elimu yako?, fedha zako?, hazina yako? Ndugu zako?.. Zichukue leo na kwenda naye kwa Bwana mlimani..kuwa radhi kuvipoteza vyote kwaajili ya Bwana kama Ibrahimu, na nakuambia badala ya kufikiri utavipoteza hivyo, kinyume chake utavipata kama Ibrahimu…
Lakini unapomfuata kuwa tayari kupoteza kila kitu!..ili upate kila kitu..
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”
Na pia alisema…
Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.
25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake ?”
Hiyo ndio gharama ya kwenda mlimani kwa Bwana, ndio gharama ya kumwabudu Mungu katika Roho na Kweli.
Kama hujampokea Yesu na unataka kufanya hivyo leo, basi hapo ulipo jitenge dakika chache kisha piga magoti na zungumza na Bwana, kiri wewe ni mwenye makosa, na mwombe Bwana akurehemu, na baada ya hapo, dhamiria kuacha mambo yote maovu uliyokuwa unayafanya kwa wazi na kwa siri, kama ulevi, wizi, chuki, utukanaji, tamaa mbaya, kujichua, uasherati, usengenyaji n.k. Na baada ya hapo..Na baada ya hapo tafuta ubatizo sahihi, ambao ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kuijua kweli yote. Hapo utakuwa umefika mlimani kwa Bwana, na yale yote ambayo ulikuwa unadhani umeyapoteza..Bwana atayarejesha upya katika usahihi Zaidi.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?
SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.
Kwanini vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.
Kama leo hii Mungu akikutoa katika utumwa wa dhambi (Yaani kuokoka), basi weka akilini kuwa unapopelekwa kutakuwa ni nje ya matarajio yako, na pengine pasiwe ni pa kuvutia kabisa katika macho yako. Ni vizuri tukafahamu njia za Mungu, ili pale tunapokutana nazo tusiwe ni watu wa kulaumu laumu, au kuuliza uliza ni kwanini hivi, kwanini vile?
Kipindi kile Mungu alipowatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri, walitazamia kupitishwa katika NJIA kuu ya mataifa yote, iliyojulikana kama njia ya wafilisti. Njia hiyo ilikuwa ni ya haraka na ya chap chap, kiasi kwamba kama wangeipitia hiyo, ingewachukua wiki kadhaa tu wangeshafika Kaanani. Lakini Mungu alikuwa na sababu ya wao kutowapitisha njia ile..Tusome..
Kutoka 13:17 “Ilikuwa hapo Farao alipokwisha kuwaacha watu hao waende zao, Mungu hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri;
18 lakini Mungu akawazungusha hao watu kwa njia ya bara kando ya Bahari ya Shamu; wana wa Israeli wakakwea kutoka nchi ya Misri hali wamevaa silaha”.
Unaona wana wa Israeli walipitishwa katika njia ngeni kabisa machoni pao, njia yenye ukingo wa mbeleni ya bahari, njia ya vichakani, isiyopitwa na watu, njia ya upweke..Mpaka biblia inatuambia hicho ndicho kilichomvutia Farao, kuwafuatilia tena ili wawateke nyara wawarudishe Misri. Lakini hawakujua kuwa Mungu yupo kule kuwatetea.
Kutoka 14:1 “Bwana akasema na Musa, akamwambia,
2 Waambie wana wa Israeli, kwamba warudi na kupiga kambi yao mbele ya Pi-hahirothi, kati ya Migdoli na bahari, kukabili Baal-sefoni; mtapanga mbele yake karibu na bahari.
3 Naye Farao atasema katika habari za wana wa Israeli, Wametatanishwa katika nchi, ile jangwa imewazuia wasitoke.
4 Nami nitaufanya uwe mgumu moyo wa Farao, naye atafuata nyuma yao; nami nitajipatia utukufu kwa Farao, na kwa jeshi lake lote; na Wamisri watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. Basi wakafanya hivyo.
5 Mfalme wa Misri aliambiwa ya kuwa wale watu wamekwisha kimbia; na moyo wa Farao, na mioyo ya watumishi wake, iligeuzwa iwe kinyume cha hao watu, nao wakasema, Ni nini jambo hili tulilotenda, kwa kuwaacha Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?
6 Akaandalia gari lake, akawachukua watu wake pamoja naye;”
Hata sasa, wapo watu wanapookoka, na ghafla kuona mambo yanakwenda kinyume na matazamio yao, wanapolazimika kuishi staili nyingine ya maisha, wanageuka na kurudi nyuma na kuuacha wokovu. Na tena pale wanapoona, kuna ukigo mzito mbele yao na kwamba wakiendelea na njia hiyo ya wokovu watakwama ndio kabisa wanakimbia kwa miguu yote miwili, na kusema huyu si Mungu.
Pengine mwingine atapitia shida kidogo, au dhiki kutoka kwa ndugu, au kupungukiwa, jambo ambalo ni kinyume na matarajio yake, wakati hapo mwanzo yeye alidhani akimpokea Kristo siku hiyo hiyo mambo yataanza kuwa safi, sasa anapoona kumetokea mitikisiko Fulani katika maisha, anamwacha Mungu anasema huyu sio Mungu.
Ndugu ikiwa kweli umetubu dhambi zako, na umejitwika msalaba wako kumfuata Kristo, umesema mimi na ulimwengu ndio kwaheri, kamwe usitazame nyuma, pale unapoona mambo yanakuja kinyume na matarajio yako, wewe songa mbele. Ni Mungu ndiye kakusudia kukupitisha hapo, usianze kulaumu laumu au kunung’unika, na kusema kwanini mimi, maadamu Kristo yupo ndani ya moyo wako, songa mbele. Unapoona njia hiyo imekuwa ndefu sana, kama vile huielewi itaisha lini? Bado usiwe mwepesi wa kutazama nyuma. Wewe endelea mbele maadamu unamwona Kristo kila siku katika maisha yako. Kumbuka iliwachukua miaka 40 wana wa Israeli kuifikia Kaanani yao.
Nawe pia upo wakati Bwana aliouweka atakufikisha katika Kaanani yako ya hapa duniani na mbinguni. Ni wewe tu, kutambua kuwa njia za Mungu sio njia zetu. Jambo ambalo wengi wetu hatulijua pale tunaposema tumemfuata Kristo, na huku tunamtaka Mungu atatupitisha kwa njia ya wengi.
Kamwe tuondoe hayo mawazo. Yeye ana njia zake, na wanadamu wana njia zao. Hilo tulifahamu. Na pia tukumbuke mtoto yoyote wa Mungu, atapitishwa tu kwenye njia hizo, haijalishi ni mjanja, au hodari, au tajiri au maskini kiasi gani, ni lazima atakutana tu na njia hizi zisizoeleweka za Mungu, kwasababu madarasa ya Mungu hayarukwi. Na tabia ya hizi njia ni kuwa zinaambatana ni miujiza mingi ya Mungu, ikiwa na maana mtu anaweza kufikia mahali anaona amekwama, ghafla anashangaa amepitaje pitaje mazingira hayo, huo ndio uthitibisho kuwa yupo katika njia hiyo ya Mungu.
Lakini kama akistahimili, basi ajue, licha tu ya kuupokea uzima lakini mwisho wako atakuwa ni wa mafanikio na wa Baraka sana hapa duniani.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Zamani nilipokuwa mdogo nilijaribu kufanya zoezi ambalo lilikuwa ni hatarishi kwangu. Nilidhani, kila “balbu” ilihitaji kitu kinachoitwa “Umeme”tu bila kujua ni umeme kiasi gani unahitajika ili uwake. Hivyo, siku hiyo nikachukua nyaya mbili, nikazichomeka moja kwa moja kwenye soketi, lengo langu ni zile nyaya nitakapozigusanisha sasa na balbu nione ikiwaka, nifurahie.
Lakini nilipozigusanisha tu zile waya na balbu, matokeo yalikuwa ni tofauti na nilivyotarajia. Balbu ile ilipasuka. Na kwa neema za Mungu tu vile vipande vilivyorukwa havikuniingia machoni, vinginevyo leo hii ningekuwa kipofu.
Shida ni nini? Nilidhani kilichohitajika ni umeme tu, ilimradi umeme. Na hiyo yote nikwasababu nilikurupukia kitu ambacho sijafahamu kanuni zake kwanza, Ni kwanini watu wanaitanguliza ile holder kwanza kabla ya kuiunganisha na umeme..! sikuwa na muda wa kufuatilia.
Mambo kama hayo yanaendelea leo hii rohoni, Watu wanajaribu kumfanyia Mungu ibada bila kufahamu kanuni sahihi ambazo Mungu anataka zifuatwe. Na matokeo yake ndio hapo tunaishia kuona matokeo hasi kama sio kuadhibiwa na Mungu kabisa..
Katika biblia tunaona kulikuwa na watoto wawili wa Haruni, ambao walijaribu kufanya zoezi kama hili. Wenyewe waliingia hemani pa Mungu, na kuvukiza uvumba kinyume na utaratibu wa Mungu, na Mungu akawaua saa ile ile kwa kuwashushia moto na kuwateketeza kabisa,. Biblia inatuambia kosa walilolifanya lilikuwa ni KUTUMIA MOTO WA KIGENI, kuvukiza uvumba.
Walawi 10:1 “Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mtu chetezo chake, wakatia moto ndani yake, wakatia na uvumba, nao wakatoa moto wa kigeni mbele ya Bwana, ambao yeye hakuwaagiza.
2 Kisha moto ukatoka hapo mbele za Bwana, nao ukawala, nao wakafa mbele za Bwana.
3 Ndipo Musa akamwambia Haruni, Jambo hili ni hilo Bwana alilolinena, akisema, Nitatakaswa mimi”
Moto wa kigeni ulikuwa ni upi? Ni moto wowote ambao ulitoka nje ya madhabahu ya Mungu. Utakumbuka wakati ule makuhani walipotaka kufanya upatanisho wa makosa na dhambi za watu, walikuwa wanaagizwa wachinje wanyama, Sasa moto uliokuwa unawateketezea hao wanyama ndio ulikuwa unaitwa moto wa madhabahuni, moto huo wa makaa haukuzimwa mchana wala usiku, uliwaka daima.
Sasa huo ndio waliokuwa wanauchukua makuhani, na kwenda nao ndani ya hema, kisha wanaweka uvumba uliosagwa vizuri, juu yake na kuvukiza. Pale moshi na harufu ya uvumba ule unapopanda juu, basi Mungu alikuwa anawasemehe makosa yao, waliomkosea.
Sasa hawa wana wawili wa Haruni, wao walidharau kanuni hii ya Mungu, wakadhani kinachohitajika ni Moto ilimradi moto tu,.. Wakauacha moto wa madhabahuni,ambapo upo pale hemani daima, wakaenda chukua moto wanaoujua wao kutoka huko nje, hatujui pengine waliutolea kwenye majiko yao ya nyumbani, hatujui, wakauleta nyumbani mwa Mungu, kisha wakaweka uvumba juu yake, ili wamvukizie Mungu kwa kupitia huo. Kilichotokea ni kuuliwa badala ya kupewa rehema.
Tunapaswa tujue kuwa wakati wowote tunapomfanyia Mungu ibada ya aina yoyote ile, tujiulize je tumefuata taratibu zake? Tunapowasilisha maombi yetu kwake je, tupo ndani ya wokovu? Je na sisi ni watakatifu? Kama sio ni heri tuache tu, kwasababu maombi yanayowekwa juu ya moto wa madhabahuni ya Mungu ni yale watakatifu tu, na si ya wengine, biblia inasema hivyo katika.
Ufunuo 8:3 “Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na MAOMBI YA WATAKATIFU wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi.
4 Na moshi wa ule uvumba ukapanda mbele za Mungu pamoja na maombi ya watakatifu, kutoka mkononi mwa malaika”.
Unaona? Hivyo kama wewe si mtakatifu, na unasema mimi ninasali, ninashiriki meza ya Bwana, ninaimba kwaya,, ninatawadha watakatifu miguu, ninamtolea Mungu.. ujue kuwa unaweka moto mgeni madhabahuni pa Mungu. Na upo hatarini sana kupigwa kama sio kuuliwa kabisa.
Huu ni ule wakati ambao Mungu anataka waabuduo halisi, wa kumwabudu yeye katika Roho na kweli. Na sio katika uongo, kama waliofanya akina Anania na Safira wakafa.
Yohana 4:23 “Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli”.
Mungu hataki ukristo feki, ndugu yangu, anasema ukitaka kuwa moto kuwa moto, au uwe baridi kabisa, kuliko kuwa vuguvugu, unasema umeokoka na bado unaendelea kuvaa vimini, na suruali, unavaa milegezo, unajichubua ngozi yako, unakunywa pombe, unazini. Hayo mambo si ya wakati wake huu, ambao Mungu anataka aabudiwe katika Roho na Kweli. Na wala usiyajaribu kwa Mungu, kwasababu unaweza ukadhani unampendeza Mungu, kumbe ndio unajitafutia mapigo kama ilivyokuwa kwa Nadabu na Abihu.
Kama hujaokoka kwa kumaanisha, basi okoka leo, Yesu aingie maishani mwako, dhamiria kabisa kuacha matendo yako maovu unayoyafanya, kisha ukabatizwe kama hukubatizwa na yeye mwenyewe atakupokea na kukusamehe, na ibada yako itaipokea na kukubariki.
Bwana atupe macho ya kuona..
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengin
Mada Nyinginezo:
Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?
Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?
Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?