NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, Ni siku nyingine tena tumepewa neema ya kuiona, hivyo nasi hatuna budi kutumia nafasi hiyo kujifunza maneno yake maadamu tumepewa nafasi hiyo.

Tukiwa hapa duniani ni lazima tujue kuwa upo ufalme ambao Bwana Yesu alienda kutuandalia huko mbinguni. Lakini kwa bahati mbaya ufalme huo hautakuwa wa watu wote, watakaopewa neema ya kuingia huko. Wengine watakuwa waalikwa tu, lakini hawatakuwa wafalme na makuhani, bali ni Bibi-arusi tu wa Kristo peke yake, na ndugu za mfalme ndio watakaokuwa na ufalme huko mbeleni. Soma (Mathayo 22:1-13)

Na hao Yesu alisema watakuwa ni watu   “waliodumu naye katika Majaribu yake”

Luka 22:28 “Nanyi ndinyi mliodumu pamoja nami katika majaribu yangu.

29 Nami nawawekea ninyi ufalme, kama vile Baba yangu alivyoniwekea mimi”.

Umeona, wale waliodumu naye katika majaribu yake tangu, kuzaliwa kwake, mpaka anaanza hudumu, na hadi kufa kwake. Na hao si wengine zaidi ya akina Mariamu, ma mitume na wengine baadhi waliomfuata Yesu kila mahali alipokwenda kama vile Mathiya. Na sisi tuliotokea kipindi hichi ambao tutashiriki kama wao hapa duniani kwasasa.

Sasa leo tutamwangalia mtu  mwingine mmoja, ambaye naye alishikiriki, kwa sehemu katika majaribu ya Yesu, na kwa kupitia yeye, tutajifunza na sisi tufanye nini ili, tuwe na nafasi katika ufalme huo mkuu sana. Na mtu mwenyewe si mwingine zaidi ya Simoni Mkirene.

Utakumbuka wakati ambao Bwana Yesu anakaribia kwenda kusulibiwa, baada ya kupigwa sana, kutemewa mate, kupigwa makofi, kuvikwa taji la miiba n.k., hali yake haikuwa nzuri kabisa. Biblia inasema aliharibiwa kuliko mtu yeyote duniani, hakuwa tena kama mwanadamu ukimtazama, kwa mapigo aliyoyapata (Isaya 52:14).

Lakini wale askari bado waliona hiyo haitoshi, wakamtwika msalaba wake, ili aubebe mpaka Goligotha, lakini alipojitahidi kuubeba mwendo kadhaa, hakuweza kutembea kabisa, mwendo wake ulikuwa ni mdogo sana, hakuwa na nguvu ya kuunyanyua msalaba kwasababu aliumizwa sana, Pengine wakawa wanampiga kwa mijeledi  kama punda, walau waone kama ataongeza mwendo, lakini hakukuwa na mwitikio wowote katika hilo, ni jinsi gani Bwana alivyochoka..

Hatimaye wakaona, atawacheleweshea tu muda, hivyo ikawabidi watafute njia mbadala. Hapo ndipo wakaangalia kulia na kushoto miongoni mwa watu waliokuwa pale, lakini hawakuona hata mmoja aliyeweza kuunyanyua msalaba ule. Tengeneza picha biblia inasema, kulikuwa na mkutano mkubwa sana wa watu waliokuwa wanamfuata Yesu kwa nyuma hiyo siku, lakini askari hawakuona hata mmoja miongoni mwao mwenye uwezo wa kuubeba msalaba wa Yesu. Wengi wao walikuwa ni watakazamaji tu, wengine walalamikaji, wengine wahurumiaji tu, hakuna hata mmoja aliyeweza kusogeza hata shingo yake, kuimsaidia Yesu.

Lakini kwa bahati nzuri kulikuwa na mtu mmoja aliyekuwa anatokea SHAMBA, ambaye hakuwa hata na habari za kusulibiwa kwa Yesu, lakini askari wakamwona huyo ndiye anayefaa, wakamkamata kwa lazima, wakamshurutisha aunyanyue ule msalaba mzito mabegani mwake mpaka Goligotha.

Luka 23:26 “Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.

27 Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea”.

Sasa jiulize ni kwanini awe ni huyu mtu aliyetoka SHAMBA na si wale wengine? Ni kwasababu askari walimwona ni mtu wa KAZI, aliyezoelea utumishi, mtu wa kupiga majembe, mtu wa kukata mashoka huko misituni, hivyo wakimkatama huyo amsaidie ili  safari ile ndefu ya msalaba mzito isiishe katikati bali itawafikisha Goligotha walipokusudia. Na kweli ikawa hivyo.

Jiulize tena kwa upande wa pili, Bwana Yesu alijisikiaje moyoni mwake kwa mtu kama huyu. Akiona katwikwa mzigo ule uzito asiostahili kuubeba, ni wazi kuwa moyo wake ulimhurumia, kwa kila jasho alilokuwa analitoa nyuma yake, wakipandisha kilima kile kirefu hadi Kalvari. Unategemea vipi mtu kama huyu asiwe sehemu ya Ufalme aliokwenda kuwaandalia watakatifu wake mbinguni. Ikiwa tu Yule mwizi pale msalabani hakufanya chochote chema, wala hakumsaidia Yesu kwa lolote lakini alipoomba tu aliambiwa usiku ya leo utakuwa pamoja nami peponi, Si zaidi kwa mtu kama huyu ambaye alikuwa sehemu ya majaribu ya Yesu Kristo duniani?

Marko 15:21 “Wakamshurutisha mtu aliyekuwa akipita, akitoka mashamba, Simoni Mkirene, baba yao Iskanda na Rufo, ili auchukue msalaba wake.

22 Wakamleta mpaka mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa”.

Ni nini tunajifunza?

Bwana hawezi kutupa sehemu ya msalaba wake, ikiwa sisi si watu wa SHAMBA. Si watu wa kuzoelea  kazi ya Mungu, Kwasababu ataona kama tutaishia njiani, tukautupa msalaba wake tukakimbia, tusilitimize kusudi lake, kwasababu ni watu laini laini.

Kuwa mtu wa shamba ni pamoja na kuwa mtu wa kulitendea kazi Neno la Mungu, na sio kuwa msikiaji tu au msomaji tu. Kama wale makutano ambao walikuwa wanafuata tu kwa nyuma, lakini wasifanye chochote kwa ajili ya Kristo.

Kuwa mtu wa shamba ni pamoja na kujitoa kwa ajili ya Kazi ya Kristo, kwa vile vidogo ulivyojaliwa, kwa karama Mungu aliyoiweka ndani yako.

Kuwa mtu wa shamba ni pamoja na kujizoesha kuishi maisha ya Utauwa(1Timotheo 4:7-8). Yaani kuwa mwombaji, mfungaji, na mshuhudiaji wa habari njema.

Hapo ndipo Bwana ataona sababu ya kukupa wewe neema ya kuubeba msalaba wake. Na faida yake ni kuwa utakuwa sehemu ya ufalme huko mbinguni alipokwenda kutuandalia. Kwasababu ufalme huo ni kwa wale tu walioshiriki taabu yake wakiwa hapa duniani.

Hivyo sisi sote kuanzia sasa, tuwe wakakamavu rohoni, tuwe hodari kama Simoni, sio walegevu walegevu, wasikiaji tu lakini sio watekelezaji wa kile tunachokisikia, vitu vidogo vidogo tu vinatutoa katika mstari wa wokovu,  bali kila siku tutafute ni nini mapenzi ya Mungu.

Bwana akubariki sana, na nikutakie mafanikio mengi katika safari yako ya wokovu hapa duniani.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

TUFANANE NA WATAKATIFU WA MAKEDONIA.

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

TEGEMEA MUNGU KUZUNGUMZA NAWE KATIKA MAMBO MADOGO

Shalom, karibu tujifunze maandiko.

Kama kuna njia tunaiendea ambayo itakuja kuleta majuto mbele yetu, basi Mungu wetu huwa anatangulia kututahadharisha kabla ya hatari yenyewe kutufikia!..Lengo ni tuiache hiyo njia ili madhara yasitukute!

Lakini jambo la kuogopesha ni kwamba mara nyingi Mungu hatumii tu mambo makubwa kututahadharisha,  au kuzungumza na sisi, bali pia  anatumia vitu vidogo, na vilivyo dharaulika, na visivyo na heshima kuzungumza na sisi au kututahadharisha..

Wakati Fulani Mungu alitumia Punda kumtahadharisha Balaamu, hatari iliyopo mbele yake.. Ghafla akiwa njiani kuelekea kufanya jambo ambalo ni kinyume na mapenzi ya Mungu, punda wake aliyempanda alifunga breki ghafla wakiwa katikati ya safari!.. Na kwasababu alimdharau mnyama Yule pasipo kujua kuwa kusimama kule kwa punda wake kusikokuwa kwa kawaida,  inawezekana kuna jambo, lakini yeye hakulitafakari hilo..badala yake aliona ni punda tu!, na kuanza kumpiga!.. Kumbe Mungu alimtumia punda kuyanusuru maisha yake asiende kufa!! (habari hiyo kwa urefu unaweza kuisoma katika kitabu cha Hesabu 22).

Sio huyo tu!, tunaweza kujifunza kwa mtu mwingine ambaye alitahadharishwa na mnyama lakini hakusikia.. Na huyo si mwingine zaidi ya Petro.

Wakati Fulani Petro alifikia hatua ya kufanya jambo la hatari la kumkana Bwana, na wakati anaanza tu! Kumkana kwa mara ya kwanza.. Maandiko yanasema Jogoo aliwika!, sasa sauti ile ya jogoo!, haikuwa ya kawaida.. Petro aliona ni sauti ya kawaida tu!, kumbe ni Roho Mtakatifu aliingia ndani ya jogoo na kumfanya awike muda ule, ili kumtahadharisha Petro kuwa anakoelekea sio kuzuri, lakini  Petro hakuelewa chochote, akaendelea kumkana Bwana kwa mara nyingine ya pili na ya tatu!, lakini Mungu jinsi alivyo wa huruma akazungumza naye tena kupitia Yule Yule jogoo ili kwamba aache hiyo njia, atubu lakini tunaona  jogoo alipowika tena mara ya pili bado Petro hakuelewa wala kukumbuka.. Mpaka Bwana alipomgeukia na kumtazama, ndipo Petro akafahamu na kukumbuka, na kwenda kutubu…Kama tu Balaamu baada ya kufumbuliwa macho na kumwona Yule malaika, ndio akatambua!.

Marko 14: 66 “Na Petro alikuwa chini behewani; akaja mmoja wa vijakazi wa Kuhani Mkuu,

67  akamwona Petro akikota moto; akamkazia macho, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na yule Mnazareti, Yesu.

68  Akakana, akasema, Sijui wala sisikii unayoyasema wewe. Akatoka nje hata ukumbini; JOGOO AKAWIKA.

69  Na yule kijakazi akamwona tena, akaanza tena kuwaambia waliosimama pale, Huyu ni mmoja wao.

70  Akakana tena. Kitambo kidogo tena wale waliosimama pale wakamwambia Petro, Hakika u mmoja wao, kwa sababu u Mgalilaya wewe.

71  Akaanza kulaani na kuapiza, Simjui mtu huyu mnayemnena.

72  NA MARA  JOGOO AKAWIKA MARA YA PILI. Petro akalikumbuka lile neno aliloambiwa na Yesu, Kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu. Na alipolifikiri, akalia”

Sasa ili tuzidi kuelewa vizuri baada ya jogoo kuwika mara ya pili ni nini kilitokea… hebu tusome tena habari hiyo katika kitabu cha Luka..

Luka 22:59  “Halafu, yapata saa moja, mtu mwingine alikaza kusema, Hakika na huyu alikuwa pamoja naye, kwa kuwa yeye pia ni Mgalilaya.

60  Petro akasema, Ee mtu, sijui usemalo. Na papo hapo alipokuwa katika kusema, jogoo aliwika.

61  BWANA AKAGEUKA AKAMTAZAMA PETRO. Petro akalikumbuka lile neno la Bwana jinsi alivyomwambia, Leo kabla hajawika jogoo utanikana mara tatu.

62  Akatoka nje akalia kwa majonzi”

Umeona hapo?.. Bwana alipomtazama Petro, ndipo Petro akakumbuka kuwa Bwana alimwambia na vile vile akafahamu  kuwa sauti ile ya jogoo ilikuwa ni ya kumtahadharisha aache kumkana Bwana, Njia aliyokuwa anaieleka sio salama, maneno aliyokuwa anayatamka ni hatari, mwisho wake ni uharibifu!…

Laiti kama Bwana asingemgeukia Petro, au asingemwambia unabii ule, pengine Petro angeendelea kumkana Bwana hata kwa mara ya nne na tano.. na usalama wa Petro ungeendelea kuwa chini, kwasababu wale watu tayari walikuwa wameshamjua na labda wangemkamata!..na kumdhuru katika hali yake ile ile ya kumkana Bwana, lakini baada ya Bwana kumtazama, akajua kosa lake na akatoka kule behewani..Akatoka nje!, kutubu, hakuendelea kukaa kule ndani!

Ndugu, jambo hilo hilo linaendelea sasa, Ipo sauti ya Mungu inayotuonya katika mambo mengi tunayoyafanya!..Yule mhubiri unayemdharau na kumwona si kitu, ni huyo huyo Mungu anamtumia kuzungumza na wewe, hata mara tatu au nne, tofauti na Yule unayemdhania sana.. Wakati wewe unategemea kwenda kusikia sauti ya Mungu kwa mtu Fulani ambaye umemkuza sana katika kichwa chako, kumbe Mungu hatumii hiyo njia sana.

Mungu alimtumia Punda kumtahadharisha Balaamu, kadhalika alimtumia  jogoo kumtahadharisha Petro, ambaye alikuwa ni mtume wake aliyemchagua yeye, ambaye leo hii ni nguzo katika Imani.. Atashindwaje kukutahadharisha wewe na mimi kupitia mjusi au bata?.  Anaweza kufanya hivyo!. Ni kuzidi kuwa wanyenyekevu tu na kuongoza umakini tu!. Na sio tu kututahadharisha, bali pia kuzungumza na sisi.

Unapopita mahali na kusikia mahubiri yanayomtaja Yesu Kristo wa kwenye biblia, usidharau chochote kile!, hata kama wewe una maarifa mengi kuzidi hapo unaposikia,  tega sikio lako kwa makini sana, kwasababu kuna uwezekano Mungu anasema na wewe hapo!, haijalishi Yule anayehubiri ni mdhaifu na wewe ni Mchungaji au mtumishi!.. ni wajibu wako kujinyenyekeza kwasababu, Mungu anatumia chochote kuzungumza na  sisi, hivyo hatujui ni kwa njia gani atatumia kusema na sisi, ni kuwa tayari tu muda wote na kwa chochote.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Akawaambia Enendeni ulimwenguni mwote,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE.(Marko16:15.) Yesu Anamaanisha nini kusema MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE?

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Nakusalimu katika jina la Mkuu ya uzima, Mfalme wa wafalme, Bwana wetu Yesu Kristo. Sifa heshima na utukufu vina yeye milele na milele Amina.

Karibu tujifunze biblia. Leo tutatazama viashiria vikuu vitakavyomtambulisha huyo mpinga—kristo ambaye anatarajiwa kuja duniani. Kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na mikanganyiko mwingi, kuhusiana na ujio wake, na chapa yake ya 666, na hiyo imepelekea wengine kudhania kuwa mpinga-Kristo ni mkuu wa freemason atatokea kuzimu au ni ugonjwa wa Corona, kwamba mtu akichanjwa tayari ameshaipokea hiyo chapa ya 666. Lakini je! Biblia inatufundisha hivyo?

Ni kweli Bwana Yesu alisema wapinga-kristo wengi watatokea duniani, ambao kimsingi hadi sasa wapo wengi, lakini yupo mmoja ambaye atakuja. Ili kuleta uharibifu huku ulimwenguni (Soma 1Yohana 2:18). Ambaye ndio huyo tutakayekwenda kusoma tabia zake, na kwamba tukiona hizo zote zipo ndani yake, basi tujue ule mwisho umefika, tayari ameshafunuliwa, dunia imebadikiwa na kipindi kifupi sana zisichozidi miaka 7 (2Wathesalonike 2:1-6).

Zifuatazo ni tabia zitakazomtambulisha.

1) ATATOKEA KATIKA DINI KONGWE.

Mpinga-kristo tofauti na watu wanavyodhani kwamba atazuka tu ghafla kama mwanaharakati Fulani, pasipokuwa na chanzo, hapana, biblia inatuonyesha atatokea katika utawala utakaokuwa unaongoza ulimwengu wakati huo, ambao ulishawahi kuongoza pia hapo kabla, Na  utawala wenyewe ni Rumi-ya-rohoni, na utakuja kupata nguvu tena kipindi cha kukaribia mwisho wa dunia, na utafanya kazi kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu tu, yaani kwa maelezo mafupi ni kuwa mpinga-Kristo hatotokea mahali pengine isipokuwa katika ofisi ya UPAPA.

Ufunuo 17:11  “Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu”

2) DUNIA NZIMA ITAMSTAAJABIA:

Tabia nyingine ni kuwa dunia nzima itamstaajabia, kustaajabia maana yake ni kushangazwa na matendo yake, na ukuu wake, ikiwa na maana atakubalika sana na makundi yote, biblia inasema mataifa yatakubaliana naye, na watu wa itikadi zote, na kabila zote, na jamii zote za watu ulimwenguni. Hakuna hata mmoja atakayemwona kuwa ni mtu mwovu, isipokuwa tu wale masalia machache yatakayokuwa yamebaki duniani wakati huo.

Ufunuo 13:3  “Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstaajabia mnyama yule….

8  Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia”.

Lakini sio Corona, au mtu Fulani mbaya, mwenye mapembe ambaye, leo hii anaogopeka, hapana mpinga-Kristo ataonekana ni mkombozi wa ulimwengu wakati huo.

3) ATAITWA MTU WA AMANI:

Sio mtu wa vurugu, au mchinjaji, kwani mikakati atakayokuwa ameipanga na ulmwengu, italenga katika kuleta amani ya dunia, na hivyo jambo lolote atakalolianzisha, au mfumo wowote atakaouleta duniani utapokewa na mataifa yote kwa moyo  mmoja, na huko huko atapatia nguvu ya kuileta chapa yake yenye 666 ndani yake, na kwamba hakuna mtu yeyote atakayeruhusiwa kuuza au kununua asipokuwa nayo.

Danieli 11: 21 “Kisha badala yake atasimama mmoja, mtu astahiliye kudharauliwa, ambaye hawakumpa heshima ya ufalme; naye atakuja wakati wa amani, naye ataupata ufalme kwa kujipendekeza.

22 Na wale wenye silaha mfano wa gharika watagharikishwa mbele yake, na kuvunjika, naam, mkuu wa maagano pia”.

4) ATAKUJA NA ISHARA NA MIUJIZA YA UONGO:

Mpinga-Kristo atakuwa na uwezo pia wa kufanya miujiza, Kwasababu roho ya shetani itakuwa nyuma yake, mfano wa Yane na Yambre kipindi kile walipokuwa wakishindana na Musa, ambao tunaona nao pia shetani aliwapa uwezo wa kufanya miujiza,. Ili tu kushindana na kuwapinga watakatifu wa Mungu. Hivyo mpinga-Kristo naye atakuwa na uwezo huo wa shetani,lengo likiwa ni kuwachukua wale ambao watadhani ni yeye ni mpinga Kristo.

2Wathesalonike 2:8 “ Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;

9  yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;

10  na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

11  Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;

12  ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”

5) ATATAKA KUABUDIWA KAMA MUNGU.

Kwasababu atakuwa ni mtu wa rohoni, na vilevile mtu wa mwilini, lengo lake litakuwa ni kufikia kilele cha kiti cha enzi cha Mungu duniani. Atataka watu wamwone yeye kama Mungu,.Hivyo atajiinua juu ya dini zote, na madhehebu na imani zote duniani,  ili apewe sifa na utukufu kana kwamba ni yeye ni Kristo.

2Wathesalonike 2:3  “Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;

4  yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu”.

6) ATATOA MANENO YA MAKUFURU.

Kutaka kuwa kama  Mungu tu peke yake haitoshi, bado atakuwa anaitukana njia ya  wokovu, Ataukandamiza ukristo wa kweli pia, atadiriki kumtakana Mungu anayeabudiwa na watakatifu. Ili tu aonekane yeye ndio kila kitu.

Ufunuo 13:5  “Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.

6  Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni.

7  Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa”

7) HESABU YA JINA LAKE ITAKUWA NI 666.

Vilevile jina lake litakuwa ni hesabu ya 666. Yaani ukizihesabu tarakimu za jina lake, ni lazima ziishie na jumla ya 666

Ufunuo 13:16  “Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao;

17  tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.

18  Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.

Sasa haya yote kwa jumla ukiyaona kwa wakati mmoja ndani ya huyo mtu mmoja, basi ujue huyo ndiye mpinga-Kristo mwenyewe, ambaye ataipelekea duniani ifikie kiama chake. Wakati huo ukifika dunia haitakuwa na zaidi ya miaka 7 tu mpaka itakapoisha, Na kulingana na maandiko watakaokumbana na kazi zake ni wale wote ambao hawatakwenda katika unyakuo, ambao hivi karibuni unakwenda kutokea.

Huyu mpinga-Kristo ataleta dhiki kubwa sana kwa wale watakaoachwa katika unyakuo. Kwasababu hutaruhusiwa kuuza wala kununua kama huna chapa yake. Ni dhiki ambayo watu watatamani vifo lakini vifo vitawakimbia.

Dalili zote zimeshatimia, Na huyu mtu wakati huu pengine anaishi duniani, ndio, anaishi duniani, kwasababu atatokea katika dini kongwe duniani, ya kirumi, katika kiti cha UPAPA,.kinachongojewa tu ni unyakuo wa kanisa, na baada ya hapo, aanze kutenda kazi yake ya kuuharibu ulimwengu. Huyu ndio lile Chukizo lenyewe la uharibifu linalozungumziwa katika maandiko.

Ndugu Je! Hadi sasa upo upande gani, Yesu akirudi leo utakuwa mgeni wa nani huko uendako?. Jibu unalo.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

UFUNUO: Mlango wa 18

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

UFUNUO: Mlango wa 14

Rudi nyumbani

Print this post

TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tuyatafakari pamoja maneno ya uzima ya Mungu wetu.

Kuna wakati mtume Petro alialikwa kama mgeni, nyumbani kwa mtu mmoja aliyeitwa Simoni, Lakini siku moja alisikia njaa sana, Na njaa ile inaonekana haikuwa ya kawaida, pengine Petro hakula kitu chochote tangu jana yake, hivyo ulipofika muda wa chakula ikambidi akatafute kitu cha kula, lakini biblia inatuambia muda huo ndio walikuwa katika maandalizi kwamaana ilikuwa ni saa sita mchana..

Lakini tunaona Petro hakusubiri mpaka chakula kiive, ale kwanza ndio aendelee na shughuli zake za ibada, bali alitumia muda huo kuingia uweponi mwa Mungu ili aombe katika njaa yake, aliendelea hivyo mpaka alipozimia katika maono, ndipo Mungu akatumia Ono linalofanana na njaa yake kumfunulia Siri kubwa sana ya ukombozi, ambayo haikuwahi kufunuliwa kwa vizazi vyovyote vilivyomtangulia. Na siri yenyewe ilikuwa ni kuhusu “Ukombozi wetu sisi watu wa mataifa”

Matendo 10:9 “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana;

10 akaumwa na njaa sana, akataka kula; lakini walipokuwa wakiandaa, roho yake ikazimia,

11 akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi;

12 ambayo ndani yake walikuwamo aina zote za wanyama wenye miguu minne, na hao watambaao, na ndege wa angani.

13 Kisha sauti ikamjia, kusema, Ondoka, Petro, uchinje ule”.

Sasa nachotaka tuone ni kuwa, wakati wa kusubiria huduma, Petro hakuona vyema muda huo upite hivi hivi tu, ni heri autimie kwa Bwana, hata kama atakuwa katika njaa.

Hata sasa, sisi kama watumishi wa Mungu, sisi kama wakristo, tunavurugiwa muda wetu kwa Mungu, kwasababu tu ya huduma tunazozisubiria za kimwili,. Na hiyo imetufanya tukose kuzijua siri nyingi za Mungu katika maisha yetu, na kanisa.

Wakati tunasubiri kwenda masomoni, kwanini  tusitumie muda huo hapo katikati kuutafuta uso wa Mungu, au kuifanya kazi yake, kwanini tusitumie kuhudhuria mikesha, au kumfanyia Mungu ibada, nani ajuaye atatuonyesha njia iliyo bora zaidi, kuliko hiyo tuliyokuwa tunaiendea?.

Wakati tumemaliza chuo tunasubiria kupata kazi, ni sawa na kusema njaa ya kazi imekushika, kwanini usiende kuhubiri injili na wengine mitaani, kuliko muda wote, kuwaza ufanye hiki au kile ili utoke, hujui kuwa unapoteza muda wako mwingi kusubiria na wakati mwingine inapita hata miezi au miaka, ukisumbukia tu hicho hicho kitu kimoja ambacho bado hujakipata, kwanini usitumie muda huo ukiwa nyumbani, kuhudumu nyumbani kwa Mungu.

Wakati unasubiria kuolewa, njaa ya kuolewa imekukamata, pengine umri umeenda sana, ujana unakukimbia, Embu fanya kama Petro, wakati Mungu anakuandalia mume wako, au mke wako, tumia muda huo kujishughulisha na masuala ya Mungu, usipoteze muda wako mrefu kutanga tanga huku na huko, au kujiweka hivi au vile, vitakupotezea tu muda, wakati muda huo Mungu angekuwa anakufunulia mambo makubwa na ya ajabu.

Wakati njaa ya mafanikio imekushika, unasubiria siku ya kupewa mkopo ifike, au kupandishwa cheo, au kupata promosheni, kwanini usijishughulishe na mambo ya ufalme wa mbinguni?, kuliko kutwa kuchwa, unapambana umpendeze huyu au Yule, ili upate upendeleo, unakosa hata muda na Mungu wako, upo buzy kusubiria kitu ambacho bado kipo kwenye maandalizi.

Hivyo, tujifunze kuutumia muda wetu vizuri kama mitume, kwasababu hapa duniani, mambo ya kusubirisha yapo mengi. Na huwa yanavuruga akili kweli, na kupotezesha muda sana, kwa mfano unapoona wengine wamepata kazi wewe huna, fikra zako zote ni rahisi kuelekea kwenye njia mbalimbali, ili tu na wewe ukipate kwa haraka kama wao walivyopata, na hapo ndipo kumsahau Mungu kunapokuja, au kupunguza muda wako na Mungu kunapokuja. Kwasababu unapigana ili na wewe usipitwe nyuma Hivyo, hali kama hiyo ikikukuta wakumbuke mitume, Kwasababu hata wao walikuwa na sababu zote za kusubiri, lakini walitumia muda wao wa hapo katikati vizuri na ndio maana mpaka leo hii tunafaidi matunda ya kujitoa kwao.

Vivyo hivyo na sisi tusiruhusu hata kidogo mambo ya kusubirisha yatuvurugie muda wetu na Bwana. Tusiruhusu njaa zetu, zimweke Mungu nyuma.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NJAA ILIYOPO SASA.

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Nini maana ya “Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai?

Rudi nyumbani

Print this post

TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.

Wagalatia 5:22 “Lakini TUNDA LA ROHO ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.

Hapo biblia inasema  “Tunda la Roho” na si “Tunda la roho”.. Roho hapo imeanza kwa herufi kubwa, vile vile inasema “Tunda” na si  “Matunda”.. maana yake lipo moja tu!.. Hivi ni vitu viwili vya msingi kuvijua, katika andiko hili kabla ya kuzidi kuendelea kusoma..

Leo kwa neema za Bwana tutajifunza kwa ufupi, tofauti ya vitu hivi viwili, ili itusaidie kujua ni nini tunachopaswa kuwa nacho sasa!.

  1. Tunda la Roho.

Ikumbukwe kuwa popote pale neno “Roho” linapoandikwa likianza kwa herufi kubwa “R” linamaanisha Roho Mtakatifu, lakini mahali linapoanza kuandikwa kwa herufi ndogo “r” linamaanisha aidha roho ya mwanadamu au roho ya mwovu. Hivyo katika mstari huo Roho imeanza kwa herufi kubwa ikimaanisha ni Roho Mtakatifu na si roho ya mwanadamu.

Mahali pengine ambapo unaweza kusoma kuhusu hilo ni (Yohana 16:13,Yohana 15:26, Matendo 2:18, Matendo 6:10).

Kwahiyo Roho Mtakatifu anapoingia ndani yetu ndipo Tunda hili linapozaliwa, hatuwezi kuwa na Tunda lolote ndani yetu linalompendeza Mungu bila kupokea Roho Mtakatifu… Sasa hebu tusogee mbele kidogo kujifunza ni kwanini sio Matunda bali ni Tunda.

  1. Tunda la Roho

Labda katika mstari huo, tungeweza kuusahihisha na kusema.. “Lakini MATUNDA ya Roho ni Upendo, furaha, uvumilivu, fadhili n.k”.. lakini biblia haijasema hivyo!, bali imesema “TUNDA la Roho ni upendo, furaha, uvumilivu n.k”.. Ikimaanisha kuwa tunda ni moja tu na si mengi!.

Jambo ambalo ni sahihi kabisa, hata katika uhalisia wa maisha, hakuna mti ambao unaweza kuzaa matunda aina mbili.. mti mmoja unazaa tunda la aina moja tu!, haiwezekani katika Mchungwa, ukakuta maembe katika shina moja, na katika shina lingine ukakuta, papai au pera, hapana!, bali utakuta kama ni mchungwa, unazaa machungwa tu!, kama ni mpera utakuta ni mapera tu mti mzima!..

Luka 6:44 “kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu”.

Sasa na katika maandiko tunda la Roho Mtakatifu ni moja tu!, kama tulivyojifunza..Sasa kama ni hivyo basi hayo yaliyotajwa mbele yake ni nini?

Jibu ni kwamba, hayo yaliyotajwa ni LADHA ZA HILO TUNDA!. Maana yake ni kwamba Tunda ni moja lakini ndani yake lina ladha hizo nyingi..(ambazo ndio Upendo, furaha, amani, fadhili, kiasi, utu wema n.k).

Ni sawa niseme leo, Tunda la muembe ni tamu, zuri, laini, chachu kidogo, lenye harufu nzuri n.k. Hapo nimetaja tabia za tunda moja tu na si mengi!.

Sasa na Tunda la Roho ni hivyo hivyo, Mtu mwenye Roho Mtakatifu anazaa tunda lenye mchanganyiko wa ladha hizo: yaani upendo,  amani, furaha, fadhili, utu wema, kiasi, KWA UFUPI UTAKATIFU!. Hivyo tabia zote hizo zipo ndani ya tunda moja.

Haiwezekani mtu awe na upendo halafu akose fadhili, kama hana fadhili maana yake hana upendo, haijalishi atauigiza upendo kiasi gani, vile vile haiwezekani mtu awe na amani akose utu wema au kiasi..Mambo hayo yote yanakwenda pamoja kwasababu yote yanapatikana katika tunda moja la Roho Mtakatifu.

Hivyo siku zote kumbuka mtu wa Mungu, kwamba kama huna Roho Mtakatifu ndani yako huwezi kuwa na amani, upendo, uvumilivu, ambayo yote hayo kwa ujumla ni utakatifu. Na vile vile unapopokea Roho Mtakatifu ni lazima tabia zote hizo zionekane, haitakiwi kupunguka hata mojawapo!!.

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”

Umeona umuhimu wa Roho Mtakatifu???…Je umepokea Roho Mtakatifu?.. kwa kutubu na kumwamini Yesu, na kubatizwa??.. kama bado kumbuka huwezi kamwe kuzaa tunda lolote katika Roho, vile vile biblia inasema wote wasio na Roho Mtakatifu hao sio wake (soma Warumi 8:9). Je na wewe ni miongoni mwa ambao sio wake?.. Habari njema ni kwamba, Mungu anatupenda wote, na ahadi hiyo ya Roho Mtakatifu sio ya watu Fulani baadhi tu!, hapana! Bali ni ya watu wote watakaomkimbilia yeye, haijalishi ni warefu, wafupi, wanene, wembamba, wazima, wagonjwa, maskini, matajiri, waliosoma au ambao hawajasoma.. Hiyo ni ahadi ya Baba kwa kila mtu anayepumua!..

Matendo 2:38  “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39  KWA KUWA AHADI HII NI KWA AJILI YENU, NA KWA WATOTO WENU, NA KWA WATU WOTE WALIO MBALI, NA KWA WOTE WATAKAOITWA NA BWANA MUNGU WETU WAMJIE”.

Lakini huna budi kwanza kumkubali Yesu moyoni mwako, na kwenda kubatizwa ubatizo sahihi ili ahadi hii ya Roho Mtakatifu ije juu yako. Na kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kulingana na mstari huo hapo juu!.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi nyumbani

Print this post

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Madhabahuni ni mahali ambapo Mungu amepachagua kukutana na mwanadamu. Hivyo palipo na madhabahu ya Mungu mtu anaweza kuwasilisha dua zake, ibada yake, na shukrani zake, na Mungu akazipokea. Mahali pasipo na madhabahu haiwezekani kukutana na Mungu, na kama ikitokea hivyo basi ujue ni kwa neema zake tu, kakujibu pengine kwasababu hukuujua ukweli. Lakini hakuna njia mtu anaweza kuwasiliana na Mungu pasipo madhabahu.

Sasa tunapozungumzia madhabahu hatumaanishi lile eneo la mbele kanisani linalopambwa, hapana, hicho ni kivuli tu cha madhabahu, madhabahu halisi kwasasa ipo rohoni kule mbinguni, kiti cha enzi cha Mungu kilipo. Na Yesu mwenyewe ndio nyenzo ya kutufikisha hapo, Ikiwa na maana ili uweze kumfikia Mungu ni sharti DAMU ya Yesu ikutangulie kwanza kuzifunika dhambi zako. Hapo ndipo utajua ni kwanini alisema yeye ndio njia kweli na uzima, mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye.(Yohana 14:6) .Watu wengi wanadhani wanaweza kumkaribia Mungu kwa matendo yao wenyewe au dini zao. Hilo halipo kabisaa.

Sasa turudi kwenye kiini cha somo. Ni nini kinaendelea sasahivi  katika madhabahu ya Mungu rohoni. Kama tulivyotangulia kusema madhabahuni ni mahali ambapo watakatifu wanafikisha Maombi yao au  haja zao kwa Bwana.

Na ni vizuri kufahamu watakatifu wamegawanyika katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni watakatifu walio hai duniani, na kundi la pili ni watakatifu waliokufa. Na wote hawa wanawasilisha mahitaji yao mbele ya madhabahu ya Mungu mbinguni. Na leo kwa ufupi tutajifunza ni mahitaji gani wanayawasilisha mbele za Mungu.

Utakumbuka Bwana Yesu alitufundisha kuomba, na katika kuomba kule alisema tutamke neno hili..

Mathayo 6:9 “Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, UFALME WAKO UJE,…

Hii ikiwa na maana kuwa kila mtakatifu aliyepo duniani, kumwomba Mungu ufalme wake uje, ni sehemu ya maisha yake ya kila siku. Hivyo mbele ya madhabahu ya Mungu iliyopo mbinguni, maombi haya yanafikishwa na malaika na kuwekwa mbele ya madhabahu ya Mungu,..Na hivyo Mungu anachofanya ni kuiharakisha ile siku ya kurudi kwake, ifike upesi.

Ufunuo 8:3 “Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi”.

Unaona? Lakini si hilo tu, bado upande wa pili wa watakatifu nao waliokufa katika dhiki, wanayo maombi yao wanayoyapeleka..embu tusome..

Ufunuo 6:9 “Na alipoifungua muhuri ya tano, NIKAONA CHINI YA MADHABAHU ROHO ZAO WALIOCHINJWA KWA AJILI YA NENO LA MUNGU, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.

10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?

11 Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao”.

Unaona, hawa nao wanaonekana wapo chini ya madhabahu, wakiomba.. Hivyo wakati watakatifu wa duniani wanaomba ufalme wake uje..Watakatifu walio ardhini wanaomba mwisho wa waovu ufike.

Walio mbele ya madhabahu wanalia Unyakuo ufike upesi, utawala wa amani wa miaka 1000 uje haraka, karamu ya mwanakondoo ianze upesi.. wakati huo huo waliochini ya madhabahu wanaomba, waovu walipizwe kisasi, wauaji, wafikishwe katika kiama chao, mbingu zikunjwe kunjwe kama ukurusa, mapigo ya vitasa saba yamiminwe juu ya nchi, ili isafishwe, waje wastarehe na Bwana ulimwenguni milele.

Haya ni maombi mazito sana, na yanausumbua moyo wa Mungu, usiku na mchana, vilio vyao na vyetu vinamfikia kila dakika kila sekunde, kutoka huku duniani na kule peponi walipo watakatifu waliokufa.

Na tunasoma majibu Bwana aliyowapa wale waliolala yalikuwa ni haya..”WASTAREHE KIPINDI KIFUPI SANA”.. Kumbe kimebaki kipindi kifupi, majibu ya maombi yote yajibiwe, ndugu yangu, siku isiyokuwa na jina Yesu atarudi, Kama tunavyoona dalili zote, jinsi zinavyotimia kwa kasi sasa, mfano wa gonjwa hili la Corona (Luka 21:11). Hii ni kuonyesha kuwa siku yoyote tutashuhudia tukio la UNYAKUO.

Siku hiyo pengine ni leo usiku, tutashangaa ghafla kundi fulani dogo sana la watu halipo. Ukiona hivyo basi ujue umebaki, na utakachokuwa unasubiria ni kisasi cha Mungu mwenyewe duniani.  Ambacho kitatanguliwa kwanza na ile dhiki kuu ya mpinga-kristo (666), ile ambayo Bwana Yesu alisema haijawahi kutokea wala haitakaa itokee . Na baada ya hapo ndipo mapigo ya vitasa saba yafuate (Ufunuo 16), Kisha, ulimwengu wote kumalizwa. Watu watatamani mauti lakini itawakimbia, ni kilio na kusaga meno.

Usifikiri tuna muda mrefu tena kama zamani, injili ya sasa sio ya kubembelezewa wokovu. Ni wewe mwenyewe ushtuke utoke usingizini, utengeneze mambo yako na Mungu wako. Ukipumbazwa na injili za manabii wa uongo, wanaokufundisha, ustarehe hapa duniani, kana kwamba hii dunia ni urithi wako utaishi hapa milele. Jihadhari sana, kwasababu Yesu alishatuonya juu yao kwamba watawadaganya hata yamkini walio wateule(Marko 13:22).

Hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kugeuka, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi, wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo. Na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu. Hapo ndipo utakuwa umezaliwa mara pili. Na ukiendelea kudumu katika wokovu na utakatifu basi hata Kristo akirudi usiku wa leo, unakwenda naye mbinguni.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

TUFANANE NA WATAKATIFU WA MAKEDONIA.

Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio?

Ni nani aliyesema “Nitume mimi”? katika (Isaya 6:8)

Rudi nyumbani

Print this post

KU WAPI, EWE MAUTI, KUSHINDA KWAKO?

Ipo siku moja mauti itashindwa kabisa kabisa…

Siku moja tutavikwa miili mipya ya utukufu!, katika siku hiyo, parapanda ya Mungu italia, na wote tuliomwamini Yesu, tulio hai..kama hatutakufa mpaka siku ile ya kurudi kwake, basi tutamwona Bwana akitokea mawinguni, na kisha wafu waliopo makaburini nao pia wataisikia sauti ya parapanda, na wao pia watafufuka.

Katika siku hiyo, kama mtu alikufa katika udhaifu fulani labda alikufa akiwa kiwete, au kiziwi au kipofu, au alikufa na ugonjwa wa kansa, lakini alikuwa ndani ya Imani, basi atafufuliwa na kurudi katika mwili wake, akiwa mzima kabisa, akiwa si kipofu tena, wala si kiziwi tena, wala si kiwete tena, wala si mgonjwa tena, kama mtu alikufa na Kisukari, basi atafufuliwa bila huo ugonjwa..

Siku hiyo kama vile Bwana alivyomfufua Lazaro ambaye alikufa pengine katika ugonjwa Fulani uliomsababishia mauti, lakini alipofufuliwa alifufuka katika uzima! Hakuwa na huo ugonjwa tena, vinginevyo angerudia kufa tena wakati ule ule!, kadhalika kabla ya kufufuliwa alikuwa kaburini ananuka, lakini baada ya kufufuka ile harufu ilipotea!, vinginevyo asingeweza kuishi na watu tena..

Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile.. Wote waliokufa katika dhiki zao watafufuliwa katika uzima, wote waliokufa katika huzuni watafufuliwa katika ushindi na amani.. na baada ya kuvikwa miili mipya ya utukufu wataimba maneno haya… KU WAPI! EWE MAUTI KUSHINDA KWAKO?, KU WAPI EWE MAUTI KUSHINDA KWAKO??… MAUTI IMEMEZWA KWA KUSHINDA.

Ni kweli walikufa katika udhaifu wao, lakini tumaini la ufufuo walikuwa nalo!. Kwamba siku moja wataishinda mauti, watarudi tena kuwa hai na hawatakufa tena!

1Wakorintho 15:51 “ Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52  kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

53  Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.

54  Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, MAUTI IMEMEZWA KWA KUSHINDA.

55  Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako? ”

Swali la kujiuliza kwa wewe uliye nje ya wokovu, au uliye vuguvugu, siku hiyo utakuwa wapi wakati watakatifu wanafufuliwa na kuvikwa kutokuharibika??. Kwasababu watakaoshinda mauti si wote!, bali ni wale waliokufa katika Kristo tu!, walioyatakasa maisha yao walivyokuwa duniani.

Je umempokea Yesu? Je unauhakika siku ile, utaishinda mauti? kwa kufufuliwa na kuingia katika uzima??..au Kama ukikutwa ukiwa hai, utanyakuliwa na kwenda na Bwana mawinguni?.. Kama huna uhakika sana, basi tayari huo ni uthibitisho kuwa hutaishinda mauti?, hutafufuliwa siku ile Bwana atakapokuja, na hata kama akija na kukukuta hai katika hali uliyopo hutanyakuliwa, badala yake utabaki na kukutana na dhiki kuu ya mpinga kristo na kufa katika ile siku ya Bwana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

MUNGU ATAKUUA UKIWA MBAYA MACHONI PAKE.

Nini maana ya “Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai?

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni sahihi kusikiliza miziki ya kidunia?.

Jibu: Mpaka imeitwa miziki ya kidunia maana yake imebeba maudhui ya kidunia: Na biblia inasema yeye aliye rafiki wa dunia ni adui wa Mungu.

1Yohana 2:15  “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16  Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17  Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”

Miziki yote ya kidunia inahubiri au kutangaza mojawapo ya vitu vifuatavyo: uasherati, vurugu, kiburi, kutukuza vitu vya ulimwengu huu kama mali na fahari zake, na kilicho kikuu Miziki hii inachokihubiri ni UVUGUVUGU.

Sasa kwanini uvuguvugu?

Utakuta wimbo una beti moja au mbili zinazotangaza kupendana, au zinazotaja uweza wa Mungu, na kumsifia Mungu, lakini ina beti sita za matusi, au beti 4 zinazotangaza uasherati na anasa za ulimwengu huu, Hivyo zinatangaza uvuguvugu asilimia mia moja!..na Mtu anapoisikiliza, na yeye ile roho ya uvuguvugu, ni lazima imwingie…na  Bwana Yesu aliukataa na kuulani uvuguvugu!.

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16  Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu”

Mungu anauchukia uvuguvugu kuliko hata kuwa baridi!..yaani kwa Mungu ni heri mtu awe baridi kabisa lakini si vuguvugu.

Hivyo si sahihi kabisa kwa Mkristo kusikiliza miziki ya kidunia. Kwasababu inatangaza mambo ya kidunia.

Na mtu anayeokoka ni lazima aifute miziki hiyo na kuacha kuisikiliza kabisa.. na kuanza kuujaza moyo wake mambo ya kiMungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Je watu ambao hawajasikia kabisa injili watahukumiwa?

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Ukweli dhidi ya uongo.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini iwe ni nchi ibubujikayo maziwa na asali?

SWALI: Kwanini Mungu aliufananisha uzuri wa Kaanani na kama nchi ibubujikayo maziwa na asali? Kwanini isiwe kitu kingine chochote, labda dhahabu na nafaka?

Kutoka 3:8 “nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi”.


JIBU: Mungu aliposema Kaanani ni nchi ibubujikayo maziwa na asali, hakumaanisha kuwa kuna mito ya maziwa, au mabomba ya asali, kila mahali hapana. Bali alitumia lugha hiyo ya picha kuonyesha uzuri wa nchi ile jinsi ulivyo.

Kama tunavyojua maziwa yanatolewa na mifugo, kama ng’ombe,. Na ng’ombe ili atoe maziwa mengi na ya kutosha, anategemea sana mazingira yenye malisho mazuri ya kijani na chemchemi nzuri za  maji. Hivyo Hapo ni Mungu alikuwa anawaonyesha wana wa Israeli kuwa nchi waiendeayo si nchi kame, bali ni nchi yenye rutuba nyingi sana, ambayo mboga mboga na malisho mazuri vinastawi, kiasi kwamba tukisema  ni maziwa basi mifugo yao itamwaga maziwa mengi sana, hadi yasiwatoshe kwa wingi wa malisho yaliyopo huko.

Vilevile aliposema asali, aliwalenga nyuki. Na nyuki ni wadudu wanaotegemea sana, aina mbalimbali za mimea na maua ili kutengeneza asali yao, Kama tunavyojua mahali ambapo pana jamii chache za miti na mimea, inawachukua muda mrefu sana kuunda asali kidogo, kwani inawagharimu kutembea umbali mrefu sana, kutafuta virutubisho hivyo.

Lakini kama wapo eneo lenye misitu, na jamii tofauti tofauti za miti na mimea, huwa inawachukua muda mfupi sana. Hivyo Mungu aliposema hiyo nchi ibubujikayo asali, alimaanisha kuwa ni nchi yenye aina mbalimbali ya miti ya vyakula na matunda, Kama tukisema ni nyuki watengeneze asali, basi asali itakuwa ni ya kumwagika sana.tofauti na hiyo nchi ya ukame waliyotoka.

Na ndio maana wale wapepelezi waliotumwa na Musa kwenda kuipeleleza Kaanani, aliporudi na  kichala kikubwa cha mzabibu na tini na mkomamanga,  waliwaambia wana wa Israeli maneno haya;

Hesabu 13:27 “Wakamwambia wakasema, Tulifika nchi ile uliyotutuma, na hakika yake, ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali, na haya ndiyo matunda yake”

Unaona, kwa yale waliyoyakutana nayo huko walithibitisha maneno ya Mungu kuwa ni kweli, kuwa nchi hiyo ni ya maziwa na asali.

Hata sasa, Mungu ana mpango huo kwa watoto wake , kuwafikisha katika nchi hii, lakini ni lazima kwanza, awafundishe kanuni zake, na jinsi ya kuishi ndani yake. Vinginevyo wakiifikia na huku maisha yao bado hajabadilishwa, nchi hiyo itawatapika kama ilivyowatapika wenyeji wa Kaanani. Na kanuni zenyewe ni kuishi sawasawa na amri za Mungu (Neno lake).

Walawi 18:26 “Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu;

27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;)

28 ILI KWAMBA HIYO NCHI ISIWATAPIKE NA NINYI PIA, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu”.

Lakini tukiishi sawasawa na Neno lake, wakati huo utafika na Bwana atatuingiza katika nchi hiyo kama alivyofanya kwa wana wa Israeli walipozitii amri zake.

Hesabu 14:8 “Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?

UFUNUO: Mlango wa 18

Kuota upo nchi nyingine.

ESTA: Mlango wa 4

Rudi nyumbani

Print this post

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

Daudi ni mfalme ambaye alikuwa amezungukwa na mashujaa hodari sana, na mashujaa hao aliowachagua walikuwa wamegawanyika katika makundi makuu matatu, Kundi la kwanza kabisa ambalo lilikuwa ndio la juu kabisa zaidi ya yote liliundwa na maaskari watatu, na lile pili yake liliunda na wawili, na lile la tatu liliundwa na mashujaa 37.

Sasa ukitaka kujua kwa urefu ushujaa wao, na mashujaa wenyewe walikuwa ni wakina nani fungua link hii usome zaidi…

Lakini leo tutaona kwa ufupi, ni nini kilimtokea  mmojawapo kati ya wale mashujaa watatu wa kwanza, Na ni ujumbe gani Kristo anataka tuupate kupitia ushujaa wake.

shujaa huyu aliitwa Eleazari, yeye kuna wakati walikutana na jeshi kubwa la wafilisti, wakati huo alikuwa peke yake tu, Israeli yote ilikuwa imeondoka, hata wale mashujaa wenzake hawakuwepo.. Lakini hakuogopa vita bali alinyanyuka na kuushikilia upanga wake mmoja.. akaanza kupigana na wafilisti yeye peke yake kama vile Samsoni, aliushikilia upanga wake kwa nguvu sana kiasi kwamba haikuwa rahisi kuuondoa mkononi mwake.

Lakini kwasababu maadui walikuwa wengi,kuna muda ulifika alilemewa sana, na ile nguvu ya kuendelea kuushikilia upanga ikamwishia, akataka kuuachilia ule upanga kwasababu alichoka sana, lakini biblia inatuambia upanga ule hakuwezi kutoka katika mkono wake, ikiwa na maana ulijiganda kama gundi katika mkono wake. Pale alipojaribu kurusha mkono, upanga haukuchomoka mkononi mwake, bali ulikwenda naye Hivyo akaendelea kupigana na wafilisti mpaka akawamaliza wote. Baadaye Israeli walipokuja kazi yao ikawa ni kuteka nyara tu huko nyuma, kwa kipigo cha jeshi la mtu mmoja.

2Samweli 23:9 “Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao;

10 huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye Bwana akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu”.

Hiyo ni kuonyesha jinsi gani, mtu anapotaka kung’ang’ana na kusudi la Mungu, kusudi nalo litang’ang’ana naye, ili kutimiza lile lengo.

Leo hii ukiling’ang’ania kusudi la Bwana kwa moyo wako wote na kwa bidii, lile kusudi nalo litang’ang’ana na wewe tu, hamna namna, kwasababu hiyo ni kanuni ya ki-Mungu, hata kama utafikia wakati umechoka, bado litaendelea kukung’ang’ania tu. Na ndio maana unaona ni kwanini watumishi wa Mungu wa kweli, hawachoki kumtumikia Mungu, japokuwa hawafanyi kazi ya mshahara, sio kwamba hawachoki, au hawapitii magumu, au hawapungukiwi nguvu..wanachoka, lakini wakati wanakaribia kuanguka, lile kusudi la Mungu linang’ang’ana nao, hivyo wanajikuta bado wanaendelea mbele na safari.

Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;

31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Hata sisi sote, tunapodhamiria kweli kwa mioyo yetu yote, kutembea na Mungu, kamwe Mungu hawezi kutuachia katikati tuaibishwe na shetani, tunakuwa mfano wa Eleazari, nguvu za Mungu zitaambatana na sisi kuhakikisha kuwa lile kusudi la Mungu linatimia kwa gharama zozote zile.

Lakini tukiwa watu vuguvugu, leo tupo na Mungu kesho shetani, hatujajikana nafsi zetu na kusema kuanzia leo mambo ya ulimwengu basi, tunakwenda na Kristo. Kamwe nguvu ya Mungu haiwezi kushikamana na sisi kama alivyokusudia, pale tunapoishiwa nguvu au tunapokumbana na majaribu. Na ndio hapo utaona mkristo anakuwa moto na Mungu siku za mwanzoni mwanzoni, tu ikifika baadaye, anapoa, mpaka anauacha wokovu kabisa..ukimuuliza ni kwanini atasema, hali ya maisha ilikuwa ngumu, mwingine nilipitiwa na ujana, mwingine nilikuwa katika mazingira yasiyo rafiki,..Sasa tatizo halipo kwa Mungu bali kwa huyu mtu.

Kwasababu Mungu akishaianzisha safari ndani ya maisha ya mtu  huwa haikatishi katikati, Kwasababu Mungu huwa hashindwi , anaelewa kabisa kuwa yapo majira mbalimbali tutapitia hapa duniani kama wakristo, hivyo anatuhakikishia nguvu ya ziada kutoka kwake,  lakini hiyo inakuja  endapo tu tutakuwa na nia ile ile ya kutembea naye.

Paulo alisema

Wafilipi 1:6 “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;”

Hivyo ishi maisha ya kumaanisha mbele zake, ishi ndani ya kusudi la Mungu, ili Mungu awe nawe nyakati za taabu. Swali ni Je umemaanisha kweli kumfuata Kristo? Kama bado basi leo ndio wakati wako wa kudhamiria kutoka katika moyo wako kutubu na kuacha dhambi zako zote, Fanya hivyo kisha baada ya hapo nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO ikiwa hukubatizwa hapo kabla, Na Mungu mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu, akutie nguvu hadi siku ukombozi wako.

Zingatia: Waliokombolewa na Mungu hawashindwi na ulimwengu.

Ikiwa utapenda upate huduma ya ubatizo sahihi, basi utawasiliana na sisi kwa namba hizi 0693036618, tukusaidie.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post