Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

SWALI: Tunajua kuwa Nabii Eliya alipaa mbinguni katika upepo wa kisulisuli, lakini tunakuja kuona miaka mingi baadaye akituma waraka kwa mfalme mfalme Yehoramu juu ya ugonjwa wake (2Nyakati 21:12). Jambo hilo linawezekanikaje?


Jibu: Labda tusome,

2Nyakati 21:11 “Tena ndiye aliyefanya mahali pa juu milimani pa Yuda, na kuwaendesha katika uasherati wenyeji wa Yerusalemu, na kuwakosesha Yuda.

12 LIKAMJIA ANDIKO KUTOKA KWA ELIYA NABII, kusema, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asema hivi, Kwa sababu hukuziendea njia za Yehoshafati baba yako, wala njia za Asa mfalme wa Yuda;

13 lakini umeiendea njia ya wafalme wa Israeli, ukawaendesha katika uasherati Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu; tena umewaua ndugu zako wa nyumba ya baba yako, waliokuwa wema kuliko wewe;

14 tazama, Bwana atawapiga pigo kubwa watu wako, na watoto wako, na wake zako, na mali yako yote;

15 nawe utakuwa na ugonjwa mkuu kwa maradhi ya matumbo, yatakapotokea matumbo yako kwa sababu ya ugonjwa huo siku kwa siku”

Ni kweli kabisa unabii huo ni wa kipindi cha mbele kabisa, wakati ambao Nabii Eliya ameshachukuliwa juu… Lakini swali la msingi hapo ni kwanini Eliya aonekane tena hapa akimtolea unabii huyu mfalme, je alituma huo waraka kutoka mbinguni huko alikokuweko au?

Jibu ni la! Hakutuma waraka kutoka mbinguni, bali ulikuwa ni waraka ambao aliuandika kabla ya kunyakuliwa juu. Alipewa unabii wa mbeleni, kwamba atatokea mfalme anaitwa Yehoramu ambaye atafanya mambo yasiyompendeza Mungu, na Bwana Mungu akampa maagizo aandike habari ya mambo yake pamoja na adhabu atakayoipata, hivyo Nabii Eliya akaandika katika waraka, na baada ya hapo pengine alimpa Eliya au mtumishi mwingine chini yake ili baada ya yeye kuondoka na huyo mfalme atakapotokea basi apewe ujumbe wake.

Na kweli baada ya hapo waraka ule ulihifadhiwa mpaka Mfalme Yohoramu alipotokea, na kufanya mabaya sawasawa na unabii huo wa Eliya, na mwisho akapatwa na mabaya kama Eliya alivyoandika..Kwani maandiko yanasema Yehoramu alipata ugonjwa wa matumbo, utumbo ukawa unatoka nje, huku unaoza!, na alikufa kifo cha kutokutamanika.

2Nyakati 21:18 “Na baada ya hayo yote Bwana akampiga matumbo kwa ugonjwa usioponyeka.

 19 Ikawa baada ya siku, ikiisha miaka miwili, matumbo yake yakatokea kwa sababu ya ugonjwa wake, akafa akiugua vibaya. Wala watu wake hawakumfukizia mafukizo kama ya baba zake”.

Hivyo sio kwamba Nabii Eliya alirudi kumtabiria wala kutuma wakara kutoka mbinguni, hapana bali aliuandika kabla ya kuondoka kwake.

Jambo kama hilo hilo pia tunaliona kwa Nabii mmoja ambaye alipewa unabii wa kuzaliwa mfalme atakayeitwa Yosia, ambaye atazibomoa bomoa madhabahu zote za baali katika Israeli..

1Wafalme 13:1 “Na tazama, akatoka mtu wa Mungu katika Yuda kwa neno la Bwana, akafika Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa akisimama penye madhabahu, afukize uvumba.

 2 Basi mtu huyo akapiga kelele juu ya madhabahu, kwa neno la Bwana akasema, Ee madhabahu, madhabahu, Bwana asema hivi, Angalia, mtoto atazaliwa katika nyumba ya Daudi, jina lake Yosia; na juu yako atawachinja makuhani wa mahali pa juu, wanaofukiza uvumba juu yako, na mifupa ya watu itateketezwa juu yako”

Baada ya unabii huu kutoka kwamba atazaliwa mtoto anayeitwa Yosia, uliandikwa chini, na kisha kuhifadhiwa, ilipita miaka zaidi ya 100 ndipo mtoto huyo alipokuja kuzaliwa.. na akafanya yote sawasawa na yaliyotabiriwa kuhusu yeye.. Unaweza kusoma habari hiyo katika kitabu cha 2Wafalme 23:16-20.

Sio hao tu!, hata Nabii Isaya alishatabiri habari za kutokea Mfalme anayeitwa Koreshi ambaye atamjengea Mungu nyumba katika Israeli, na akamwandikia waraka huo, na ukahifadhiwa na wakati ulipofika miaka mingi baadaye, mfalme huyo alitokea kweli na akapewa ujumbe wake huo. Unaweza kusoma unabii huo katika Isaya 44:28, Isaya 45:1 na kutimia kwa unabii huo unaweza kusoma Ezra 1:2

Hivyo tunachoweza kujifunza ni kuwa Mungu anayajua yote yanayokuja, na kwamba Neno la Mungu halipiti, kama aliweza kuandika habari za Yehoramu miaka mingi kabla hajaja, na habari zake zikatimia kama zilivyo, vile vile kama aliweza kuziandika habari za Koreshi mfalme wa Uajemi na zikatimia kama zilivyo…  Basi tujue kuwa maneno yake aliyosema kuwa walevi, waasherati, waabuduo sanamu, wezi, n.k hawataurithi uzima wa milele  sawasawa na Wagalatia 5:21, basi tutambue kuwa Neno lake sio uongo, ni lazima litimie tu!, kwasababu Mungu ni yeye Yule jana, leo na hata milele habadiliki.

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20  ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21  husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”

Hivyo kama bado hatujamkabidhi Bwana maisha yetu, huu ni wakati wa kufanya hivyo.. Kama bado hujaokoka, ni  vizuri kufanya sasa kama mambo hayajaharibika, na ikashindikana kuyafanya upya tena. Hivyo hapo ulipo usipoteze muda, jigenge dakika chache na kisha tubu dhambi zako zote ukimaanisha kuziacha, na kisha tafuta ubatizo sahihi ambao ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu ili ubatizwe upate ondoleo la dhambi zako, na hatimaye utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu, ambaye atakuongoza na kukutia katika kweli yote ya maandiko.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

Rudi nyumbani

Print this post

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

Ikiwa Bwana Yesu atarudi leo, atakutana na makundi matatu ya watu wanaomsubiria yeye.

  • Kundi la kwanza ni kundi la HENOKO,
  • kundi la pili ni kundi la NUHU,
  • Na kundi la tatu ni kundi la LUTU.

Sasa ni vizuri ukafahamu wewe upo katika kundi lipi, kuanzia sasa, kabla ya wakati huo kufika. Kwasababu wakristo wengi wanadhani ukishamkiri tu YESU basi, inatosha wewe ni tiketi ya moja kwa moja, kwenda katika unyakuo.

Ndugu yangu, hizi ni siku za mwisho, hatuna muda mrefu wa kuishi hapa duniani, kama hulijui hilo ndio ulifahamu sasa, ni wajibu wetu sisi, tunaosema tumeokoka, kuyatathimini maisha yetu ya wokovu, ili tujue tupo upande upi.

1) Tukianzana na kundi la kwanza la HENOKO.

Kama sote tunavyojua Henoko alikuwa ni mtu wa saba tangu Adamu, na mtu pekee aliyenyakuliwa kutoka ulimwenguni pasipo kuonja mauti kwenye dunia ya wakati ule. Na biblia inatueleza sababu ya kuhamishwa kwake ni kwasababu alishuhudiwa kuwa alimpendeza Mungu,

Waebrania 11:5 “Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu”.

Biblia inasema alitembea na Mungu kwa muda wa miaka 300. Hivyo Mungu hakuona vema awepo katika uharibifu  wa gharika uliokuwa unakuja ulimwenguni kote.

Vivyo hivyo wakati tunaoishi sasa ni wakati wa nyakati ya SABA ya kanisa kwa mujibu wa kalenda ya Mungu kama tunavyosoma katika kitabu cha Ufunuo sura ya 2&3. Hivyo hadi sasa lipo kundi dogo sana la watakatifu linalofananishwa na Henoko, litakalotembea na Kristo hadi wakati wa kuja kwake, Watu hawa katika biblia wanajulikana kama Wanawali werevu na Bibi-arusi wa Kristo (Ufu 21). Ndio watakatifu watakaokwenda katika unyakuo ikiwa parapanda ya mwisho italia leo.

Hawa Mungu atawaepusha na dhiki kuu, na adha zitakazokuja huko mbeleni, kwa tukio linaloitwa UNYAKUO, kwasababu ni vipenzi wa Mungu.

Ufunuo 3:10 “Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi”.

Ni watu ambao thawabu yao mbinguni ni kubwa sana.. ndio wale ambao watatawala na Kristo kama Wafalme, mabwana na makuhani. Na makao yao itakuwa ni katika ile Yerusalemu mpya ishukayo kutoka mbinguni kwa Baba.

Kundi la Pili, ni NUHU.

Hili kundi halituhusu sisi watu wa mataifa, Bali linawahusu Wayahudi. wayahudi tu peke yao ndio watakaokuwa katika kundi hili na Nuhu, Kristo atakaporudi. Ikiwa na maana kuwa, Unyakuo utakapopita hawatakwenda popote, kwasababu hawakuwa ndani ya Kristo. Na Mungu alifanya hivyo kwa makusudi, kuwapiga upofu ili sisi tuipokee hii neema. Lakini wakati utafika, hii neema Kristo atairudisha kwao, (Soma Warumi 11)  na baadhi yao wataiamini. Sasa hao, ndio wataingizwa katika Safina(mafichoni) ambayo Mungu ataindaa wakati huo, ili kuwalinda na hiyo dhiki kuu ya mpinga-Kristo, pamoja na ghadhabu ya Mungu itakayokuja ulimwenguni wakati huo. Soma (Ufu 7:1-8, 14:1)

Ufunuo 12:14 “Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo”.

Na hawa vilevile hawatakuwa wengi, idadi yao itakuwa ni 144,000 tu Basi, hawa watahifadhiwa mbali na mpinga-Kristo, hivyo mpaka dunia inateketezwa kwa moto, hawa watakuwa mafichoni mahali ambapo Mungu amewaandalia wao tu. Hawakufa, mpaka utawala wa miaka 1000 utakapoanza, kama vile Nuhu alivyoishi hadi gharika ilipoisha.

Kundi la tatu ni LUTU.

Kundi hili ndio gumu zaidi, kwasababu halinyakuliwi, wala halitunzwi, bali linajiokoa lenyewe. Kama vile Lutu, wakati wa maangamizi ulipofika, hakunyakuliwa kama Henoko, wala hakuhifadhiwa kwenye safina, au handaki Fulani, kama Nuhu, bali aliambiwa na wale malaika, jiponye nafsi yako. (Mwanzo 19:17). Ikiwa na maana akiendelea kubaki pale, ni kifo.

Na utaona Lutu, alikuwa ni tajiri sana, lakini siku alipolazimika kuondoka, hakuondoka na kitu chochote pamoja naye hata kijiko, isipokuwa familia yake.

Ndivyo itakavyokuwa kwa kundi hili la wakristo vuguvugu watakaokosa unyakuo, ambao wanaojulikana kama wanawali wapumbavu. Siku hiyo watalazimika, kuingia katika dhiki kuu, ambayo kujiponya kwao ni lazima kuambatane na vifo na dhiki, na mateso mengi sana.

Na kwa bahati mbaya wengi sana hawataweza kustahili, wategeuka nyuma. Na matokeo yake ni kuwa jiwe la chumvi kama mke wa Lutu. Wengi wanadhani, kipindi cha dhiki kuu, kitakuwa ni chepesi, usidanganyike, mke wa Lutu, alidhani hivyo alipokuwa anatoka, lakini mbeleni aliona alipotoka ni heri kuliko alipokuwa anaelekea na ndio maana akagueka nyuma akawa jiwe la chumvi. Nataka nikuambia Siku hiyo ya dhiki kuu, na ya mapigo Mungu, mateso utakayokuwa unayapitia,  utaona ni heri upokee tu chapa,  kama sio  kumkufuru Mungu kabisa, kuliko kuvumilia dhiki hizo.

Kulithibitisha hilo soma.

Ufunuo 16:8 “Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto.

9 Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu”.

Na kibaya zaidi, ni kuwa kundi hili hata kama litafanikiwa kustahimili dhiki(yaani kufa bila kuikana imani), kule litakapokwenda litakuwa la chini kabisa, halitakuwa na thawabu yoyote. Kwasababu halina chochote mkononi mwao, kama vile Lutu alivyopoteza vyote.

Ndugu, haya mambo yapo karibuni sana. Swali la kujiuliza Je! Wewe upo katika kundi lipi, Je! Ni la HENOKO au la LUTU. Jibu unalo moyoni mwako, ikiwa leo hii maisha yako yote ni kufikiria tu mambo ya ulimwenguni, hutaki kuishi maisha ya utakatifu yanayompendeza Mungu, Usitazamie kuwa Utakuwa katika kundi la Henoko. Ikiwa habari za siku za mwisho hazikuvutii, lakini habari za kutabiriwa biashara yako ni zenye kipaumbele, basi ujue hapa duniani utabaki tu kama paraparanda italia leo.

Tujifunze kwa Henoko, yeye alitembea na Mungu mpaka Mungu mwenyewe akamwonyesha Siku ya Kiama itakavyokuwa, unategemea vipi Mungu asimwepushe na ile gharika iliyokuwa mbele yake?

Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,

15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake”.

Bwana atusaidie.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Torati na manabii”?

SWALI: Tukisoma katika maandiko tunaona sehemu kadha wa kadha likitajwa neno “Torati na manabii”. Sasa hii torati na manabii maana yake ni nini? Kwamfano  Mathayo 7:12  inasema

“Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii”.

JIBU: Bwana Yesu aliposema Torati na manabii, alimaanisha Agano la kale, ambalo ndio limeundwa na vitabu vya Musa (Torati), ambavyo ni vitano (5), Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati.  Pamoja na vitabu vyote vya manabii, kama vile, Yeremia, Isaya, Danieli, Ezekieli, Hababuki, Amosi, n.k. hapa ikijumuisha pia, vile vingine kama  Waamuzi, Zaburi, Ayubu, Wafalme,  Mithali, Ruthu n.k. Ambavyo sio moja kwa moja vya manabii, lakini vimebeba nabii za Mungu ndani yake.

Kwahiyo torati na manabii kwa ufupi ni lile agano lote la kale. Hivyo Pale Bwana Yesu alipokuwa anawafundisha juu ya kanuni za kufuata, alirejea biblia yao, akiwaambia kuwa kiini cha biblia hiyo ni UPENDO. Wala hakuna siri nyingine nyuma yake, Torati yote, pamoja manabii wote, walichokuwa wanahubiri ni Upendo, (Ambao umegawanyika, wa Mungu na wanadamu)

Hata sisi wa leo tulio katika agano jipya, tunaposoma biblia yote tujue Ujumbe mkuu tunaoupata katika agano letu ni ule ule UPENDO. Na ndio maana Mtume Paulo alisema.

1Wakorintho 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu”.

Hivyo na sisi, tunapaswa tuutafute huu, kwa bidii zote, ili tuonekane kuwa wakamilifu mbele za Mungu.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Yesu aliwaambia wale wakoma wakajionyeshe kwa makuhani?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wale watu wenye ukoma waende kujionyesha kwa makuhani?, kwanini asiwaponye tu hivyo hivyo na kuwaacha mpaka awaambie waende kwa makuhani.

Luka 17:12 “Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika”.


JIBU: Kama vile Injili ya Kristo inavyowafikia watu katika namna mbili, wengine kuwaokoa na wengine kama ushuhuda kwao (Mathayo 24:14)

Vivyo hivyo na uponyaji wake alivyouachia, alikusudia uwafikie watu kwa namna mbili. Kuokoa na wakati huo huo kuwa Ushuhuda.Si kila uponyaji au muujiza Yesu aliokuwa anaufanya ulikuwa ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Hapana, bali ponyaji nyingine aliziruhusu mahususi kwa lengo la kuwa ushuhuda kwa wengine, ili siku ile ya hukumu wasije wakasema hatukuona, au hatukusikia.

Tunasoma jambo kama  hilo katika..

Mathayo 8:1 “Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.

2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.

3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika.

4 Yesu akamwambia, Angalia, usimwambie mtu; ila enenda zako, ukajionyeshe kwa kuhani, ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa, IWE USHUHUDA KWAO”.

Ndicho kilichowakuta Makuhani, pamoja na mafarisayo na waandishi. Ni watu ambao walikuwa hawataki kusikia wala kuamini, Hivyo Bwana Yesu, alipowaponya baadhi ya watu hakuwaacha tu hivi hivi waende,kama alivyofanya sehemu nyingine, bali aliwaagiza waende kuwaeleza makuhani miujiza iliyowakuta,. Hivyo walikuwa wanapokea shuhuda nyingi sana kutoka kwa watu  mbalimbali walioponywa.. Pengine kwa siku  hata watu 100. Na kila walipoulizwa ni nani kawaponya wanasema YESU.

Hivyo hata sasa na sisi, tusifurahie tu miujiza ya Mungu anatuletea miujiza mingi, watu wanaponywa, wanafunguliwa, na huku maisha yetu yapo nje ya Kristo. tusifurahie kwasababu tujue ni hukumu tu tunajiandikia. Na ndio maana Bwana alisema maneno haya sehemu fulani;

Mathayo 11:21 “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.

22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.

23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Hivyo hiyo ndio iliyokuwa sababu kwanini aliwaambia wakajionyeshe kwa makuhani, kwasababu wao ndio waliokuwa hawamwamini wala kuziamini kazi zake.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

MIUJIZA YA KRISTO, HAITEGEMEI KANUNI ZA KIBINADAMU.

Rudi nyumbani

Print this post

JE CHANJO YA KORONA NI ALAMA YA MNYAMA?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu, libarikiwe, karibu katika kujifunza maandiko.

Leo tutajifunza swali la msingi na la muhimu, linalozunguka katika vichwa vya watu wengi, walio wakristo na wasio wa kristo, na swali lenyewe ndio hili> Je chanjo ya Korona/corona ndio chapa ya mnyama yenyewe au ni kitu kingine?

Ili kupata jibu la swali hili vizuri, ni vyema kwanza kujua maana ya chapa na lengo la chapa!. Chapa maana yake ni lebo, au utambulisho. Kitu kilichotiwa chapa maana yake kimewekwa utambulisho wa hicho kitu, kwamfano bidhaa Fulani inayouzwa katika duka, ni lazima iwe na chapa au lebo, lengo la hiyo lebo/chapa ni kuitambulisha ile bidhaa Mmiliki wake pamoja na asili yake na vile vile ni nembo ya hati miliki ya wenye bidhaa.

Na kawaida chapa, au nembo ya bidhaa inawekwa mwishoni kabisa mwa bidhaa ile inapokamilika kutengenezwa, na huwa haiwekwagi mwanzoni mwa bidhaa ile inapotengenezwa.

Kadhalika, biblia imetabiri, kipindi kifupi sana kabla ya dunia kuisha, Shetani atawatia alama/nembo watu wake. Ili kwamba ithibitike kuwa wao ni milki yake ya halali, na hatua ya kutiwa chapa ni hatua ya mwisho kabisa ya uthibitisho wa mtu kwa shetani. Maana yake ni kwamba mpaka mtu aipokee chapa, tayari alikuwa katika kuandaliwa na shetani muda mrefu, hivyo sio jambo la kufumba na kufumbua tu.

Maana yake ni kwamba wote watakaoipokea chapa, ni sawa na mtu aliyemaliza kuiandika barua, anamalizia na sahihi tu pale chini!, ile sahihi ndio chapa!, lakini habari yenyewe sio ile sahihi bali ni ule ujumbe!.. kadhalika chapa!, ni sahihi tu ya uhalali wa mtu kwa shetani. Msingi huu utatusaidia kujua kuwa chapa ya mnyama sio jambo la kwanza kumtambulisha mtu kuwa ni milki ya shetani, bali ni jambo la mwisho!. Kwasababu kama ingekuwa ni jambo la kwanza, wapo watu waliokufa na hali hawana hiyo chapa ya mnyama na bado walikuwa ni milki ya shetani, na siku ya mwisho wataingia katika ziwa la moto!.  Hivyo jambo la kuogopa sasa sio hiyo chapa inayokuja ambayo ni 666, bali ni kujiupusha na shetani muda huu na kazi zake zote, kwa kumpokea Bwana Yesu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi na kuishi maisha matakatifu.

Kwa kufanya hivyo utakuwa umejitoa kabisa kwenye mkondo wa watu wa Yule mwovu, na wanaotengenezwa kuwa wake, na mwisho kutiwa chapa yake.

Sasa tukirudi kwenye swali letu, linalouliza, Je! Chanjo ya Corona ni alama ya mnyama au ni kitu kingine?. Jibu ni kwamba chanjo ya corona sio chapa ya mnyama!.. Isipokuwa inatangaza ujio wa chapa ya mnyama.

Katika maandiko tunasoma kulikuwepo na matukio ambayo yalikuwa yanatangulia kutokea, ambayo yalikuwa yanatangaza ujio wa tukio Fulani kubwa mbeleni. Kwamfano utaona janga mafuriko ya gharika ya Nuhu, ambayo yalitokea duniani kutokana na maasi ya wanadamu, na janga lile likafuta idadi kubwa karibia yote ya watu duniani… Kwa janga lile kubwa ijapokuwa liliangamiza na kubakisha watu nane tu!.. Lakini bado mwisho wa dunia ulikuwa haujafika!.

Lakini tukio lile lilikuwa linatangaza au kuhubiri jinsi mwisho wa dunia utakavyokuwa… Kwamba siku moja kabla mwisho wa dunia kufika, siku hizo zitafanana sana na siku za Nuhu,.. maasi yataongezeka, na vile vile dunia itaharibiwa yote kwa moto (2Petro 3:6), kama ilivyoharibiwa kwa maji kipindi cha Nuhu.

Mathayo 24:37  “Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

38  Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina,

39  wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu”

Vile vile hii chanjo ya korona sio chapa ya mnyama, bali inatangaza habari za chapa ya mnyama ambayo ipo mbioni kuja.. Kama vile gharika ya Nuhu inavyotangaza au kuhubiri gharika ya moto inatakayokuja mwisho wa dunia.

Kwahiyo tunaweza kuisema hii mithali na sisi “kama ilivyokuwa siku za chanjo ya Korona”.. “ndivyo itakavyokuwa siku za chapa ya mnyama”.. Kama ilivyokuwa siku za chanjo ya Korona, watu walikuwa hawawezi kusafiri sehemu baadhi, au kufanya shughuli Fulani bila kuwa na hiyo chanjo, ndivyo itakavyokuwa siku za ile chapa ya mnyama zitakapotimia.. katika siku hizo watu hawataweza kununua wala kuuza, wala kufanya biashara yoyote bila kuwa na chapa hiyo ya mnyama katika vipaji vya nyuso zao na katika mikono yao ya kuume.

Kwahiyo Chanjo ya Korona, wala ugonjwa wa korona sio chapa ya mnyama.

Sasa unaweza kuuliza ni kwanini isiwe chapa ya mnyama?. Maandiko yametupa majibu yote jinsi chapa ya mnyama itakavyokuwa na itakavyotenda kazi. Hivyo tukitumia maandiko tunaweza kupata majibu yote na kutusaidia kutoyumbishwa na upepo wowote wa elimu unaokuja mbele yetu sawa sawa na Waefeso 4: 14…

Waefeso 4: 14 “ ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu” (www wingulamashahidi org)

Sasa mambo  yafuatayo ndiyo yatakayoitambulisha Chapa ya Mnyama.

  1. Chapa ya mnyama itaanza kufanya kazi baada ya kanisa kunyakuliwa na si kabla:

Hili ni jambo la kwanza ambalo kila mkristo anapaswa alifahamu. Chapa ya mnyama haiwezi kufanya kazi kabla ya kanisa la Kristo kunyakuliwa. Baada ya watakatifu kuondolewa duniani kwa tendo maarufu lijulikanalo kama unyako, ndipo chapa ya mnyama itakapoanza kutenda kazi..

Na sasa (wakati huu tunaoishi) kanisa bado halijanyakuliwa, watakatifu bado wapo duniani. Na maandiko yanasema kanisa la Kristo ndilo linaloizuia ile siku isifike, kwasababu ndilo lenye Roho Mtakatifu.. Hivyo siku litakapoondolewa ndipo yule mpinga-kristo atanyanyuka na kuihimiza chapa yake..

2Wathesalonike 2:5  “Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?

6  Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7  Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa. 8  Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake”

  1. Chapa ya mnyama itaanza kutenda kazi baada ya Mpinga-Kristo kunyanyuka:

Hili ni jambo la  pili ambalo kila mkristo anapaswa alifahamu….

Huyu mpinga-Kristo biblia inamtaja kama ASI, au MWANA WA UHARIBIFU.

Maandiko yanasema hivyo katika kitabu cha…

2Wathesalonike 2:3  “Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; AKAFUNULIWA YULE MTU WA KUASI, MWANA WA UHARIBIFU;

4  yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.

5  Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?

6  Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake”.

Na mpaka sasa ofisi atakayotokea Mpinga-kristo imeshajulikana (ni ofisi ya kipapa, kulingana na maandiko), lakini kwamba ni papa yupi, bado haijajulikana.. Na wakati chapa ya mnyama inazinduliwa duniani kote, biblia inasema mpinga kristo atakuwa ameshapata nguvu duniani kote, na kupewa nguvu na mataifa yote, na ndiye atakayeiratibu na kuihimiza, na vile vile atakuwa ameshajiweka tayari kutaka kuabudiwa kama Mungu. Jambo ambalo mpaka sasa halijatimia…ingawa lipo mbioni sana kutimia baada ya unyakuo wa kanisa kupita.

  1. Dhiki kuu itakuwa ni miaka mitatu na nusu.

Hili ni jambo la tatu na la muhimu pia kila mkristo kufahamu. Dhiki kuu ya mpinga Kristo itadumu kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu, yaani miezi 42 (Ufunuo 13:5). Na tendo la watu kulazimishwa kuipokea chapa, litakuwa ni tendo la haraka sana na lenye kuchukua muda mfupi, ili kuiruhusu ile dhiki kwa miaka mitatu na nusu. Maana yake ni kwamba wakati chapa inazinduliwa, kitakuwa ni kitendo cha muda mfupi na cha shinikizo kubwa sana..haitachukua miaka au mwezi, kukamilisha zoezi hilo.. kama sasa inavyofanyika katika chanjo.

Sasa hebu jiulize, tangu huu ugonjwa wa Korona umetokea ni miaka mingapi imepita?.. Na tangu chanjo ziache kutolewa ni muda gani umepita?, na mpaka zoezi hili limalizike kwa watu wote, maana yake kila mtu awe amechagua kupokea au kutokupokea itachukua muda gani?, huoni  ni jambo ambalo litachukua muda mrefu sana, pengine hata linaweza kuchukua miaka zaidi ya miaka miwili au mitatu mbeleni au hata zaidi ya hapo?..Sasa endapo likichukua miaka miwili mbeleni muda wa dhiki kuu utapatikana wapi?, muda wa vile vitasa saba vya ufunuo 16 utapatikana wapi?.

Umeona?.. kwahiyo hii chanjo sio chapa ya mnyama?.. chapa ya mnyama itakapoanza kufanya kazi itakuwa ni kipindi kifupi sana, kila mtu duniani ambaye hakwenda kwenye unyakuo atakuwa ameshachagua aidha kuipokea au kutoipokea, pengine zoezi hilo litaendeshwa chini ya mwezi mmoja tu!.. ili kuruhusu muda wa dhiki kuu ya miaka mitatu na nusu kwa wale ambao wataikataa. (tembelea www wingulamashahidi org)

  1. Chapa itasimamia sana Masuala ya kiimani:

Hili ni jambo la Nne na la mwisho ambalo kila mkristo anapaswa alifahamu. Chapa haitaletwa duniani kutokana na matatizo ya kiafya wala kiuchumi. Hapana!… Sababu kubwa ya chapa ya mnyama italetwa kutokana na masuala ya kiimani.. Yaani kile watu wanachokiamini na kukiabudu!… (Hicho ndicho kiini cha ile chapa).

Maana yake ni kwamba kipindi kifupi sana kabla ya chapa hiyo kuzinduliwa, shetani atanyanyua majanga na matatizo mengi ambayo yatakuwa yanasababishwa na imani za watu, vikundi kama vya kigaidi kama ISIS, BOKOHARAM, ANTI-BALAKA, ALQAEDA, ALSHABAAB n.k vitanyanyuka kwa kasi na kuleta shida kubwa sana duniani kote..vile vile manabii wengi wa uongo wataleta shida kubwa sana duniani kwa kufanya vitu vya ajabu na vyenye kutishia amani ya dunia.

Kutokana na hilo basi, dunia itatafuta mtu mmoja na taasisi moja maarufu ambayo inaweza kutoa mashauri na hata kutatua hayo matatizo, ndipo hapo atatafutwa mtu wa kidini mwenye ushawishi mkubwa kuliko wote, na mwenye nguvu kiusemi. Na huyo dunia nzima itamwamini na kumpa nguvu. Kiongozi huyo wa juu sana wa kidini, ndipo atakuja na wazo la namna ya kushughulikia kutatua matatizo hayo ya kiimani, ndipo atatoa wazo la kila mtu kusajiliwa katika Kanisa, au msikiti, au taasisi yoyote ambayo ipo chini ya mfumo wake huo. (www wingulamashahidi org)

 Na yeyote ambaye atakosa au kuukataa huo utambulisho basi hataweza kuuza wala kununua wala kufanya shughuli yoyote, na zaidi ya yote ndiye atakayeonekana anachafua amani ya dunia. Na hivyo atakamatwa kwa kipindi kifupi sana na kupelekwa katika magereza maalumu, ambapo huko atapitia dhiki ambayo biblia inasema haijawahi kuwepo wala haitakuwepo baada ya hapo, kwa muda  wa miaka mitatu na nusu na ndipo atakufa… Wakati wengine waliosalia ambao wameipokea chapa ya mnyama, wakingoja kuingia katika mapigo ya vitasa saba (tunayoyasoma katika Ufunuo 16). Kumbuka haya yote yatatokea baada ya kanisa kunyakuliwa juu mbinguni.

Huu ni mhutasari tu wa Chapa ya Mnyama jinsi utakavyokuwa, kwa maelezo marefu juu ya chapa hii ya mnyama, unaweza kuwasiliana nasi inbox kwa namba hizi 0693036618/0789001312. (www wingulamashahidi org)

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba chanjo ya korona si chapa ya mnyama, lakini inatangaza ujio wa chapa ya mnyama. Na ugonjwa wa Korona haujatengenezwa na wanadamu, bali ni Tauni kutoka kwa Mungu (sawasawa na Luka 21:11), ambapo ugonjwa huu ni dalili mojawapo kubwa sana ya kurudi kwa Kristo.

Dalili zote za kurudi kwa Yesu zimeshatimia… unyakuo upo karibu sana, je! Umempokea Yesu?..kwa kutubu dhambi zako zote na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu?, kama bado kumbuka kuwa unyakuo utakapopita, utaachwa, na hutaachwa kwasababu unachapa ya mnyama, hapana utaachwa kwasababu tayari wewe ni wa Yule mwovu hata bila chapa!,.. Chapa itakuwa ni muhuri tu wa kuhitimisha kwamba wewe ni milki ya shetani.. Hivyo si wakati wa kuifikiri chapa na kuiogopa!, kitu cha kuogopa sasa ni dhambi..Hicho ndio cha kuogopa na kukikimbia, na kwa nguvu zetu hatuwezi kuikwepa wala kuishinda dhambi bali kwa kumpokea na kumwamini Yesu.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

CHAPA YA MNYAMA

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?

UFUNUO: Mlango wa 18

YONA: Mlango 1

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

Rudi nyumbani

Print this post

Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?

SWALI: Biblia inasema mshahara wa dhambi ni Mauti, (Warumi 6:23) je wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?

Jibu: Ni vizuri kufahamu kuwa katika maandiko kuna Mauti za aina mbili. Mauti ya kwanza ni mwili uliokufa na kutupwa katika kaburi!, na mauti ya pili ni roho kutupwa katika ziwa la moto.

Bwana Yesu alisema maneno haya..

Mathayo 10:28  “Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum”

Umeona?, mwili unaangamizwa katika dunia hii, ndio hapo mtu anakufa na mwili wake kuzikwa,  lakini roho ni katika jehanamu ya moto…  Hii mauti ya pili ya kuiangamiza roho katika ziwa la moto, ndio mshahara wa dhambi biblia inayoizungumzia katika Warumi 6:23

Warumi 6:23 “KWA MAANA MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”

Hivyo mshahara wa dhambi ni Mauti ya Pili, na si ya kwanza, Katika mauti ya kwanza watakatifu wengi wamekufa, wataendelea kufa wengi.. lakini watafufuliwa na kuurithi uzima wa milele, hivyo biblia haikumaanisha kabisa mauti ya mwili huu kuwa ndio mshahara wa dhambi, vinginevyo mpaka sasa kungekuwa hakuna mwenye haki. Maana watakatifu wote waliotangulia tayari wamekufa!. Kwahiyo mauti iliyomaanishwa hapo katika Warumi 6:23 ni MAUTI YA PILI, yaani lile ziwa la moto, mahali roho ya wanadamu waovu zitakapoangamizwa..

Sasa labda unaweza kuuliza ni wapi tena katika maandiko, pametajwa mauti hii ya pili kuwa ni katika ziwa la moto..

Tusome..

Ufunuo 20:14 “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.

15  Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”

Hivyo hatuna budi kujitenga na dhambi!, kwa kadri tuwezavyo ili tusije tukakubwa na mauti ya pili kwa kutupwa katika lile ziwa la moto, kama maandiko  yanavyosema..

Ufunuo 2:11 “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya MAUTI YA PILI”.

Lakini kama hatutaishinda dhambi, kwa kumwamini Yesu, na kutubu na kubatizwa katika ubatizo sahihi na wa kimaandiko, basi tufahamu kuwa, mshahara wake utakuwa ni Mauti ya piil, ambayo ndio ziwa la moto..kama Bwana alivyosema..

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, SEHEMU YAO NI KATIKA LILE ZIWA LIWAKALO MOTO NA KIBERITI. HII NDIYO MAUTI YA PILI”.

Je umempokea Yesu?, kama bado unangoja nini?, je unatamani kukumbwa na mauti ya pili?.. je unatamani kuingia jehanamu ya moto..mahali ambapo utateswa usiku na mchana, kwa maangamizi ya milele?

Fahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho na Bwana Yesu yupo mlangoni sana kurudi!.. siku yoyote parapanda inalia na ngano zitakusanywa ghalani, na magugu yote yatakusanywa na kwenda kuchomwa moto.

Bwana azidi kutubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai?

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.

Noeli ni nini, na je! Neno hili linapatikana katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda na sio kwenye koo nyingine kama vile  Yusufu?


JIBU: Hatma ya yale makabila 12, na tabia zao tunaona kwa mara ya kwanza zikifunuliwa na Yakobo Baba yao siku ile alipokuwa anakaribia kufa, alipowaita na kuwabariki. ukisoma pale utaona kila mtoto alinenewa habari zake. Kwasasa hatuwezi kuziandika zote hapa lakini kwa muda wako soma Mwanzo 49:1-28. Utaona.

Sasa,  kulingana na tabiri zile ni kabila moja  la Yuda, ndio lilibeba, vimelea vikuu sana, vimstahili Kristo.

Kwamfano pale makabila hayo yalipofananishwa na Wanyama, utaona Ni Yuda peke yake ndiye aliyefananishwa na SIMBA. Wakati wengine kama vile Naflati lilifananishwa na Ayala, Isakari  kama na Punda, Dani kama na nyoka aumaye, Benyamini kama mbwa-mwitu mkali. Yusufu kama mti mchanga uzaao. Lakini Yuda ni kama SIMBA .

Na sikuzote simba anajulikana kama ni mfalme wa pori, tena jasiri.

Mwanzo 49:8 “Yuda, ndugu zako watakusifu, Mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako. Wana wa baba yako watakuinamia.

9 Yuda ni mwana-simba, Kutoka katika mawindo, mwanangu, umepanda; Aliinama akajilaza kama simba, Na kama simba mke; ni nani atakaye mwamsha?

10 Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake, Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki, Ambaye mataifa watamtii.

11 Atafunga punda wake katika mzabibu, Na mwana-punda wake katika mzabibu mzuri. Amefua nguo zake kwa mvinyo, Na mavazi yake kwa damu ya zabibu.

12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa mvinyo, Na meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa”.

Vilevile kama tunavyosoma utabiri wake, utaona anaambiwa, FIMBO YA ENZI, haitaondoka kwake, ikimaanisha  kuwa fimbo ya kifalme, itakuwa katika uzao wake daima. Yaani kabila hili la Yuda litakuwa ni kabila la kifalme.

Mambo ambayo yanabeba kabisa tabia zote za masihi atakayekuja. Kwamba ni lazima AWE simba, jasiri, mwenye nguvu, na hodari.. Na ndio maana hatushangai kwanini  Bwana Yesu alijiita Simba wa Yuda (Ufunuo 5:5).

Vilevile ni lazima awe Mfalme mkuu sana mwenye nguvu sawasawa na unabii wa (Isaya 9:6). Hivyo kabila lenye enzi za kifalme lilikuwa ni hili na tunathibitisha hilo tangu enzi wa Daudi.

Hivyo hiyo ndio sababu kwanini Bwana Yesu hakutokea kabila lingine lolote Zaidi ya kabila la Yuda, Kwasababu, ilimpasa awe juu ya yote..Lakini kama angetokea kabila ya Yusufu ambalo limetajwa kama kabila lenye mafanikio makubwa, ni wazi kuwa kusingekuwa na vimelea vyovyote vya kifalme kwake.. Jambo ambalo haliwezekani kwa Kristo. Yeye ni lazima awe juu, atawale kama Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana. Hivyo ni lazima tabia hizo zianze kuonekana tokea mbali sana, kwenye vizazi vya vya nyuma, hadi kumfikia yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi nyumbani

Print this post

MIMI SIOMBI KWAMBA UWATOE KATIKA ULIMWENGU.

Shalom, ulishawahi kuutafakari vizuri huu mstari?

Yohana 17:14 “Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.

15 MIMI SIOMBI KWAMBA UWATOE KATIKA ULIMWENGU; bali uwalinde na yule mwovu”.

Embu takafakari, Bwana Yesu anasema sisi(watakatifu), sio wa ulimwengu huu, akiwa na maana kuwa hapa dunia hapatustahili kwa namna yoyote ile, kwasababu sio mahali petu, tunapaswa tukishamwamini tu yeye, tuondolewe, twende zetu mbinguni nyumbani kwetu, lakini wakati huo huo bado anasema, “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwenguni”..

Yaani kwa lugha nyepesi tunaweza kusema, unapelekwa kwenye nyumba ya mtu mwingine, ambaye itikadi zake na za kwako haziendani kabisa, Na pale unapojaribu kutoka na kurudi nyumbani kwako, unazuiwa,unaambiwa uendelee kubaki pale pale, hakuna kuondoka. Si kazi rahisi kama unavyodhani.

Ndicho anachokifanya Mungu sasa kwa watoto wake, na anafanya hivyo kwa makusudi maalumu. Na makusudi yenyewe ni ili sisi tuiangaze NURU yake kwa walimwengu. ukiokoka, jiandae kuendelea kuishi katika mazingira haya haya ya walimwengu kwa kipindi Fulani kirefu tu.. tukisema ulimwenguni tunamaanisha miongoni mwa waovu, Hilo huwezi kuliepuka. Ni mara chache sana itatokea Mungu kukuweka katika mazingira ambayo utaishi na wapendwa wenzako, mnaoendana.

Utawekwa katikati ya watu wasioendana na wewe kabisa, ukaishi nao, Na pengine umemwomba Mungu mara nyingi akuondoe hapo, lakini unashangaa, ombi hilo halijibiwi,lakini mengine yanajibiwa. Ukiona hivyo likumbuke tu hilo Neno la Bwana Yesu.. “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwenguni, bali uwalinde na yule mwovu”..

Pengine umeokoka, lakini mazingira ya kazini kwako, hayana utukufu kabisa, umezungukwa na watu waovu na wenye mizaha kila namna, na umemwomba Mungu sana, akufungulie mlango wa kazi nyingine nzuri zaidi yenye wapendwa wenzako. Ndugu kama umeomba sana na bado hujaona jibu lolote, ufahamu kuwa  umewekwa ulimwenguni  Huwezi kuondolewa, unachopaswa kufanya ni kuyatenda mapenzi ya Mungu hapo hapo ulipo, kwasababu huwezi jua kuwa ni Mungu kakuweka hapo ili awaokoe wengine kwa ile nuru yako unayoangaza.

Mtazame Danieli, alipopelekwa kwenye ufalme wa Nebukadreza, alikutana na mambo mengi sana ya kipagani, yanayokinzana na dini ya kiyahudi kwa kila kitu, lakini katika upagani wote ule, alimcha Mungu, na kumdhihirisha, na mwisho wa siku Mungu wake akatukuzwa katikati ya mataifa yote ulimwenguni kupitia yeye.

Hivyo na wewe uliyeokoka, inawezakana kabisa mazingira uliyopo, yasiwe mazuri, unatamani hata unyakuo upite leo uende zako mbinguni, au umetamani Mungu akuchukue uende ukaishi naye milele mbinguni, au unatamani walau akuweke katika mazingira mazuri yenye utulivu Fulani wa kiroho. Jambo unaloliomba ni kweli kabisa ni la ki-Mungu, na ni kweli ingepaswa iwe hivyo. Lakini usivunje moyo pia unapoona ombi hilo halijajibiwa kama ulivyotamani, badala yake, endelea kuyatenda mapenzi ya Mungu hapo mahali ulipo, wahubirie wengine habari njema, wakumbushe juu ya tumaini la uzima wa milele, na mwisho wa siku utakuwa umelitimiza kusudi la Mungu alilolikusudia katika maisha yako. Kwasababu Bwana Yesu hakuomba tuondolewe ulimwengu kwenye maudhi na makwazo, japokuwa alijua kabisa kuwa sisi sio wa ulimwengu huu. Bali alitaka tuendee kuishi nao kwa makusudi hayo waione nuru yake kwa kupitia sisi.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

KWANINI MIMI?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

Wazimu ni “ugonjwa wa akili”.. Mtu mwenye wazimu ni mtu mwenye matatizo ya akili. Kwahiyo katika maandiko popote palipoandikwa neno wazimu, pamemaanisha mtu mwenye shida ya akili. Na wazimu huu upo katika mwili na vile vile upo katika roho.

Katika mwili ni ile hali mtu anakuwa hajitambui, yaani kwaufupi anakuwa kama kichaa. Mfano wa wazimu wa mwilini katika biblia… ni wakati ule  Daudi alipojigeuza na kujifanya mwenye wazimu..

1Samweli 21:12 “Naye Daudi akayatia maneno hayo moyoni mwake, akamwogopa sana Akishi, mfalme wa Gathi.

 13 Akaubadilisha mwenendo wake mbele yao, akajifanya mwenye WAZIMU mikononi mwao, akakuna-kuna katika mbao za mlango, na kuyaacha mate yake kuanguka juu ya ndevu zake.

14 Ndipo huyo Akishi akawaambia watumishi wake, Angalieni, mwaona ya kuwa mtu huyu ANA WAZIMU; basi, maana yake nini kumleta kwangu?

15 Je! Mimi nina haja ya watu wenye wazimu, hata mmemleta kiumbe hiki ili aonyeshe WAZIMU WAKE machoni pangu? Je! Huyu ataingia nyumbani mwangu?”

Lakini wazimu katika roho ni ile hali ambayo mtu anakuwa hajitambui katika roho, anakuwa anaonyesha tabia za utahira katika mambo ya rohoni, hawezi kuyaelewa wala kuyapambanua, anakuwa anafanya mambo ya ajabu ajabu tu katika roho, sawa na mtu mwenye wazimu katika mwili, mifano wa watu  kwenye maandiko waliokuwa na wazimu wa rohoni ni Balaamu na Kaini.

Balaamu alifikia hatua ya kuongea na punda, halafu hata hashangai!, wala kujiuliza!…Inakuwaje kuwaje punda anaongea…na yeye bila kufikiri akawa anajibizana na punda!, jambo ambalo ni la kiwazimu.. mtu mwenye akili zake timamu za kiroho, hawezi kuonyesha hizo tabia…

Hesabu 22:27 “Yule punda akamwona malaika wa Bwana, akajilaza chini ya Balaamu; hasira yake Balaamu ikawaka, akampiga punda kwa fimbo yake.

28 Bwana akakifunua kinywa cha yule punda, naye akamwambia Balaamu, Nimekutenda nini, hata ukanipiga mara tatu hizi?

  29 Balaamu akamwambia punda; Kwa sababu umenidhihaki; laiti ningekuwa na upanga mkononi mwangu ningekuua sasa hivi”.

Hivyo Balaamu alikuwa ni mfano wa watu wenye wazimu wa rohoni, na hata biblia inasema hivyo katika…

2Petro 2:15 “wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu”.

lakini alikaripiwa kwa uhalifu wake mwenyewe; punda, asiyeweza kusema, akinena kwa sauti ya kibinadamu, aliuzuia WAZIMU WA NABII YULE”.

Vile vile, Kaini alikuwa na wazimu, kwasababu mtu mwenye akili timamu za rohoni, hawezi kujibizana na muumba wake, lakini Kaini aliweza kufanya hivyo..

Mistari mingine inayozungumzia wazimu wa rohoni ni pamoja na 1Timotheo 6:4, kumbukumbu 28:28, Zekaria 12:4, na Yeremia 25:16.

Bwana atusaidie na kutuepusha na wazimu, hususani wa kiroho ambao ndio mbaya zaidi..kwasababu huo unatufanya tusiweze kupambanua wala kuelewa mambo ya rohoni. Ambayo madhara yake ni kifo kiroho. Tusiwe kama Kaini au Balaamu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je mtu anayeua anabeba dhambi zote za yule aliyemuua?

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

JE! UNAIONA ILE NCHI NZURI YA KUMETA-META MBELE YAKO?

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

CHAPA YA MNYAMA

Rudi nyumbani

Print this post

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

Jina la Mwokozi Yesu, libarikiwe.

Karibu tujifunze maandiko, Neno la Mungu wetu ambalo ndio taa iongozayo miguu yetu, na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Safari ya wana wa Israeli ni funzo tosha, kwetu sisi tunaosafiri kutoka katika ulimwengu kwenda Kaanani yetu (yaani mbinguni). Hivyo tukijifunza kwa undani, jinsi safari ile ilivyokuwa tutaweza kujua tahadhari na sisi tunazopaswa kuzichukua katika safari yetu ya kwenda mbinguni.

Maandiko yanasema wana wa Israeli, walitolewa Misri kwa mkono hodari, lakini walipokuwa jangwani katika safari yao ya kwenda Kaanani, walikutana na changamoto chache, ambazo hizo ziliwafanya wamnung’unikie Mungu, na hata kufikia hatua ya kutamani tena kurudi Misri, walikotoka.

Hesabu 14:3 “Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; JE! SI AFADHALI TURUDI MISRI?

4 Wakaambiana, NA TUMWEKE MTU MMOJA AWE AKIDA, TUKARUDI MISRI”.

Hesabu 11:4 “Kisha mkutano wa wafuasi waliokuwa kati yao, wakashikwa na tamaa; wana wa Israeli nao wakalia tena, wakasema, N’nani atakayetupa nyama tule?

5 Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu;

6 lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu cho chote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hii mana tu. ”.

Na maandiko yanasema kwa kunung’unika huko, na kwa kutamani huko kurudi Misri, tayari walisharejea Misri katika mioyo yao, ijapokuwa katika mwili bado wapo jangwani.

Matendo 7:39 “Mtu huyo baba zetu hawakutaka kumtii, bali wakamsukumia mbali, NA KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI,

40 wakamwambia Haruni, Tufanyie miungu, watakaotutangulia; maana huyo Musa, ALIYETUTOA KATIKA NCHI YA MISRI, hatujui lililompata”.

Ndio maana katika wote walionung’unika na kutamani kurudi Misri, hakuna hata mmoja aliyeingia nchi ya Kaanani, wote walikufa jangwani. Kwanini?, kwasababu katika mwili walikuwa wametoka Misri lakini katika roho/moyo walikuwa  wapo Misri. Na kwasababu nia ya ndani inazungumza Zaidi kuliko mwonekano wa nje, wakaangamia wote jangwani bila kufika kule wanakokwenda.

Kadhalika mtu mwingine tunayeweza kujifunza kwake ni Mke wa Lutu, ambaye Bwana alisema “mkumbukeni huyo”(Luka 17:32).

Mke wa Lutu ni kweli alikuwa ameshaanza safari ya kutoka Sodoma, na Zaidi ya yote ameshaokoka kabisa(na inavyoelekea wakati anatoka alitoka kwa Amani na furaha kabisa kama wana wa Israeli walivyotoka Misri).. lakini biblia inasema alipofika mbele katika safari ile ALIGEUKA NYUMA!!..

Maana yake ni kwamba, mawazo yake, fikra zake, tamaa zake, zikatamani tena ya  Sodoma alikotoka… Labda alifika mahali akaanza kumlalamikia sana Lutu, na Mungu, kwanini katoka kule, sehemu nzuri na wanakwenda sehemu mbaya.. na kwa kosa hilo tu (la kurejea Sodoma kwa moyo wake).. mbele za Mungu alionekana tayari kastahili adhabu sawa na watu wa Sodoma na Gomora, haijalishi mwili wake haupo Sodoma. Na hivyo akageuka kuwa nguzo ya chumvi.

Ni kweli alikuwa ametoka, ameokoka, mwili wake haupo tena Sodoma, lakini Moyo wake upo Sodoma.. Na pasipo kujua kuwa moyo wa mwanadamu unanena zaidi kuliko kitu kingine chochote cha nje..akapumbazika na hivyo akajikuta anaangamia tu sawa na watu wa Sodoma.

Sasa mambo haya yaliyoandikwa katika biblia yanayowahusu wana wa Israeli na Mke wa Luthu, maandiko yanasema hayajaandikwa tu kutufurahisha! Au kutuhuzunisha, bali yaliandikwa kwaajili yetu ili sisi tusijifunze tusirudie makosa kama yao.

1Wakorintho 10:6 “Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani.

7 Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.

8 Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.

9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

10 Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.

11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Ndugu Dada/kaka.. kumbuka unapookoka, ni sawa na umeanza safari yako ya kutoka Misri, au Sodoma… Ulimwengu huu umefananishwa na Sodoma na Misri (Ufunuo 11:8). Hivyo hatuna budi kutoka Misri kweli kweli kwa miili yetu na mioyo yetu!.. sio tu kwa miili bali pia kwa mioyo yetu!.

Maana yake ni kwamba tunapomkiri Yesu, hatuna budi tuukatae ulimwengu kimwili na kiroho, tunapaswa tuache ulevi, mwilini na rohoni, tunapaswa tuache uasherati wa mwilini na wa rohoni, kama Bwana alivyosema katika…

Mathayo 5:27 “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;

28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake”.

Hivyo tukisema hatuzini tu, na huku mioyoni tunaziwasha tamaa, hapo bado mioyo yetu ipo Misri, ijapokuwa kimwili tumetoka Misri, Tunapookoka na kusema si wauaji, si watoaji mimba, lakini mioyoni mwetu tunavinyongo na chuki kwa ndugu zetu na adui zetu, sisi bado ni wauaji tu (Mathayo 5:21-22) na bado tupo Misri kiroho, ingawa kimwili tunaelekea kaanani ambayo hatutaifikia..

Kadhalika ukiwa Misri na moyo wako upo kaanani, hapo bado upo Misri, haikusaidii chochote! Unapaswa utoke Misri, maana yake ni kwamba upo katika ulimwengu lakini una hamu ya kufika mbinguni, kila siku unasema siku moja nitaokoka, siku moja nitabadilika, siku moja nitaacha kuvaa vimini, siku moja nitaacha kujiuza, siku moja nitaacha ulevi.. Fahamu kuwa hiyo siku haitafika, na utakufa ukiwa bado Sodoma. Huu ni wakati wa kujiokoa roho zetu. Kwa kuamua kuokoka kweli kweli na si kuwa vuguvugu. Kwasbabu Bwana alisema watu wote walio vuguvugu atawatapika watoke katika kinywa chake.. (Ufunuo 3:15)

Bwana atusaidie tuokoke kweli kweli, tutoke Misri na Sodoma kiroho na kimwili..

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Sodoma ipo nchi gani?

JE YESU AMEJIAMINISHA KWAKO?

NJIA YA MSALABA

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Rudi nyumbani

Print this post