JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

Mwanzo 47:9 “Yakobo akamjibu Farao, Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni mia na thelathini; siku za miaka ya maisha yangu zimekuwa chache, TENA ZA TAABU, wala hazikufikilia siku za miaka ya maisha ya baba zangu katika siku za kusafiri kwao.”

Hakuna dhambi isiyokuwa na gharama. Unaweza ukajiuliza ni kwanini Yakobo alimwambia Farao siku zake za kusafiri duniani zimekuwa ni za taabu, zisizoweza kufananishwa na za baba zake..?..

Ni kwasababu ya ujanja alioufanya wa kumdanganya baba yake na kuchukua mbaraka wa ndugu yake, Japo ni kweli ndani yake kulikuwa na mpango wa Mungu uliobeba ujumbe uliomhusu Mesia, lakini kitendo alichokifanya bado kilikuwa ni uovu..Na hiyo haikuzuia kutumikia adhabu ya uovu wake.

Na ndio maana utaona Yakobo baada ya kufanya kitendo kile alikimbilia kwa mjomba wake, hata yule mama yake aliyependana naye na kupatana kutenda uovu, ndio ikawa mwisho wa kuonana kwao tena mpaka mwisho wa miaka 20 mbeleni, kuonyesha kuwa upendo wowote wenye makubaliano yasiyo makamilifu huwa haudumu..

Na alipofika kwa mjomba yake Labani, na kukaa huko, akimtumikia kwa ajili ya Raheli mke wake, kwa miaka saba, akidhani sasa ndio anakwenda kumpata Raheli, kumbe mjomba yake Labani akamfanyia hila kama ile ile aliyomfanyia ndugu yake Esau, matokeo yake akapewa dada yake Lea ndio awe mke wake badala ya Raheli, hivyo Labani akamwambia akimtaka na Raheli pia ni lazima amtumikie miaka saba mingine..

Akaendelea kuwa mtumishi kwa muda mrefu, mpaka wakati anaondoka, Na kwenda kule Kaanani nchi ya baba yake. Huko nako Watoto wake wawili Simeoni na Lawi, wakamfanyia hila kwa kudanganya, mpaka wakaenda kuwauwa watu wasiokuwa na hatia (Mwanzo 34),

Kama hiyo haitoshi, mwanawe wa kwanza Reubeni, akamzunguka baba yake, naye pia akamfanyia hila akaenda kulala na mke wake.

Tena Zaidi ya hayo, Watoto wake wakamfanyia hila kubwa Zaidi, kumdanganya kuwa mtoto wake Yusufu ampendaye ameliwa na mnyama mkali porini..Ikamfanya alie sana na kuomboleza kwa uchungu mwingi..

Kwahiyo unaweza kuona Maisha ya Yakobo, yalikuwa ni ya kudanganywa danganywa tu, na kufanyiwa hila kila kukicha, tofauti na ilivyokuwa kwa Ibrahimu na Isaka..

Kwasababu biblia inasema…

Mathayo 7:2 “Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa”.

Na ndio maana utaona anakiri kabisa Maisha yake yalikuwa ni ya taabu,..Lakini mwishoni kabisa Mungu alikuja kumpa faraja, kupitia mwanawe Yusufu.

Sasa huyo alikuwa ni Yakobo, mtu aliyebarikiwa na Mungu, lakini hakuachwa bila adhabu ya muda mrefu hapa duniani. Tujiulize sisi ambao tunaoendelea kuishi katika Maisha ya dhambi, Maisha yetu sikuzote ni ya dhuluma, tutawezaje kupona tusipouthamini wokovu mkuu namna hii?

Mithali 11:31 “Tazama, mwenye haki atalipwa duniani; Basi mwovu na mkosaji si mara nyingi Zaidi”

Adhabu hizi za mwilini zinafunua zile za rohoni..Wapo wanaodhani ukifa tu, ndio umekufa hakuna adhabu baada ya hapa…Adhabu ipo kwa wakosaji wote. Lakini Neema ya Mungu pia ipo kutukinga na adhabu hizo.

Na neema yenyewe ni kupitia YESU KRISTO. Tukimkabidhi Maisha yetu atatusamehe na kutugeuza na kutufanya kuwa wapya tena. Atafuta hata deni la dhambi na adhabu tulizostahili kuzipokea katika utoaji mimba wetu, katika uuaji wetu, katika rushwa zetu, katika uongo wetu, katika wizi wetu, katika uzinzi wetu, katika utapeli wetu n.k. Na hiyo ndio faida ya agano hili jipya la neema lililo katika damu ya YESU.

Hivyo kimbilia leo msalabani ikiwa bado hujaokoka, tubu dhambi zako, ukabatizwe, usamehewe dhambi zako kisha upokee Roho Mtakatifu, atakaye kuwa na wewe hadi siku ile ya mwisho ya Unyakuo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

USIJITAFUTIE KULAMBWA NA MBWA KWA DHAMBI YA KUTAMANI.

MAONO YA NABII AMOSI.

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

MPINGA-KRISTO

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

JIBU: Yapo makundi mawili kanisani..kundi la kwanza ni lile ambalo linahusisha washirika, ambalo ndani yake kuna wachungaji, waalimu, wainjilisti, mashemasi na waumini na wengineo…Kundi lote hili linahusisha washirika ambao tayari wameshamwamini Yesu Kristo, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu…hali kadhalika wameshajifunza Neno vya kutosha na kukolea katika maarifa ya ki-Mungu…hata kufikia kiasi cha kuweza kuwaelekeza na kuwaelekeza wengine katika njia ya wokovu.

Na kundi la pili ni lile la watu waliookoka karibuni, au walioingia katika Imani kipindi cha hivi karibuni..Wengi wa hawa unakuta ni wachanga kiimani, na mara nyingi wanakuwa ni wageni…Hivyo wanakuwa bado wanahitaji msaada katika kujifunza Imani na uweza wa Mungu..Na kwasababu wametoka katika ulimwengu bado kuna tabia baadhi baadhi wanakuwa hawajaziacha kutokana na kwamba pengine hawajajua Neno la Mungu linasemaje kuhusu mambo hayo wanayoyafanya.

Sasa katika lile kundi la kwanza ambalo linahusisha washirika ambao tayari wameshaijua kweli ya Mungu kwa utimilifu mkubwa…wameshajua na kufundishwa uasherati ni dhambi, wizi ni dhambi, ulevi ni dhambi n.k…Wakakengeuka na kurudia matapishi na kufanya mojawapo ya dhambi hizo ambazo tayari walishajifunza kuwa ni machukizo kwa Mungu…Mtu wa Namna hiyo kimaandiko ANAPASWA ATENGWE!!…Na endapo asipotengwa wale ambao wanapaswa wamtenge watakuwa WANAFANYA DHAMBI MBELE ZA MUNGU!!…Hivyo ni agizo la Mungu kwamba ni lazima atengwe…

Na kutengwa huko kunahusisha, yeye kutoonekana maeneo au mazingira ya kanisa kwa kipindi kirefu…Na washirika wengine hawatakiwi hata kumsalimia wala kushirikiana naye kwa lolote lile, hata hata kama atatubu…atakaa mwenyewe kwa kipindi chote hicho…mpaka wakati ambao Kanisa litasikia amani ya Roho kumrudisha…na wakati huo wa kutengwa huku akiwa katika hali ya toba na maombolezo, Mungu atakuwa anamrudi kwa aliyoyafanya. Hivyo hakuna raha yoyote katika kutengwa, kama kweli ni mtoto wa Mungu. Kwasababu asipotolewa katika kanisa, watu wote wataiga na hawatamwogopa Mungu..Hivyo ili kuzuia hilo, biblia imeruhusu kumwondoa mtu huyo ili kanisa zima lisiharibike…

Utauliza ni wapi maandiko yanasema hivyo?

1Wakorintho 5:1 “Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.

2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.

3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo.

4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu;

5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu.

6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima

9 Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.

10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.

11 Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.

12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?

13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.”

Soma pia..

2Wathesalonike 3:14 “Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari; 15 lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu”.

Hivyo kuna hatari sana ya kufanya dhambi za makusudi baada ya kuujua ukweli..Tunakuwa tunakabidhiwa shetani ashughulike na sisi, Hivyo tujihakiki na Bwana atuepushe na hayo yote.

Maran atha!

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Je! mtu aliyeokoka anaruhusiwa kumiliki Lodge ambayo ina Bar ndani yake?

Mahuru ndio nini?

Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/maana-ya-huu-mstari-ni-ipi-mithali-144-zizi-ni-safi-ambapo-hapana-ngombebali-nguvu-za-ngombe-zaleta-faida-nyingi/

Rudi Nyumbani:

Print this post

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Ufunuo 1: 17 “…Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu”.

Hayo ni Maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo, akiliambia kanisa.. Sasa ukiona mpaka Bwana Yesu anasema anazo funguo za mauti, na kuzimu, ni dhahiri kuwa hapo mwanzo hakuwa nazo, zilikuwa kwa mwingine..Na huyo si mwingine zaidi ya Ibilisi.

Kumbuka Tahadhari ya kwanza Mungu aliyowapa Adamu na Hawa pale Edeni, kuhusu kula Tunda, haikuwa kwamba matokeo yake watakuwa uchi, au watajua mema na mabaya au watakula kwa jasho, au watazaa kuwa uchungu . Hapana, bali tahadhari aliyowapa ya kwanza na ya mwisho ilikuwa ni kuwa WATAKUFA(‘KIFO’)..Siku watakapokula matunda ya mti ule watakufa..akimaanisha watakufa kweli kweli..sio kwamba watakufa halafu siku moja watafufuka hapana, bali watakufa moja kwa moja..

Kwasababu Mungu alimwona muhasisi wa kifo hicho pale Edeni, Lakini wazazi wetu hawakuzingatia hilo badala yake wakala, Na matokeo yake ndio yale tuliyoyaona yalifuata baada ya pale..watu wakawa na makao mengine, baada ya pale yaliyoitwa KUZIMU. Chini ya mungu wao mpya aliyeitwa Ibilisi.

Na ndio maana katika agano la kale, hakukuwa na mtu aliyekuwa na uhakika wa maisha baada ya kifo, ni waisraeli tu ndio walifahamu hilo, nao si wote, isipokuwa wale tu waliokuwa wanafuatailia masuala ya Mesiya, ambaye alitabiriwa kuwa huko mbele atakuja kuwafufua wafu, lakini wengine waliosalia hawakujua hilo…

Na ndio maana tena utaona kulikuwa na mapambano makali kati ya mafarisayo na masadukayo, wengine waliamini kuna ufufuo wa wafu, na wengine hawakuamini hicho kitu (Soma, Matendo 4;1-2,23:7-8, Marko 12:18)..Ni kwasababu gani? Ni kwasababu suala la wafu kufufuliwa lilikuwa si jambo lililoandikwa kwa uwazi sana katika maandiko kama wengi wanavyodhani.. isipokuwa tu waliotambua jambo hilo ni wale waliokuwa wanafuatilia habari za Mesiya kuwa atakuja kufanya jambo hilo.

Kwahiyo wakati wote huo watu walikuwa wametawaliwa na roho ya mauti ya ibilisi.

Warumi 5:14 “walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata wao wasiofanya dhambi ifananayo na kosa la Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja”.

Unaona wakati huo wote shetani alikuwa na funguo hizo, alikuwa wakati mwingine anao uwezo hata wa kuwaendea wafu walio watakatifu na kuzungumza nao, soma habari za samweli(1Samweli 28)..

Lakini sasa Kristo alipokuja alipindua kila kitu,(majira yakageuka), kwanza aliiondoa hofu ya mauti ambayo ilikuwa imewatawala wanadamu kwa muda mrefu tangu zamani..

Waebrania 2:14 “Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,

15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa”.

Na pili akaiteka ile Kuzimu iliyokuwa chini ya shetani, ambayo ndio ilikuwa makao ya wafu wote…

Na ndio maana siku ile alipokufa tu, utasoma makaburi yalipasuka na watakatifu wengi wakatoka makaburini

Mathayo 27:51 “Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;

52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;

53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi”.

Tangu huo wakati hadi leo ibilisi hajui wafu wapo wapi na wanafanya nini saa hii, anachojua tu, ni kuwa wale watakatifu wapo upande wa PEPO(Paradiso) na wale waovu wapo sehemu ya mateso (Jehanum)..Hana uwezo wa kuleta mzimu wa mtu yeyote aliyekufa kwasababu sasahivi Kristo ndiye anayewamiliki walio hai na waliokufa soma Warumi 14:9. Kwahiyo hivyo vinavyoonekana na watu vyenye sura kama za wapendwa waliokufa..kiuhalisia sio wale watu wenyewe, bali ni roho tu za mapepo zilizovaa sura za watu waliokufa…

Kristo sasa ameshashikilia mamlaka yote, ya mbinguni, ya duniani na ya kuzimu..Haleluya.

Hivyo ikiwa wewe ni mtakatifu, kama utakufa leo basi ujue roho yako na nafsi yako itakwenda sehemu salama, yenye raha na pumziko la kweli, mahali pasipoelezeka panapoitwa Pepo, lakini wewe ambaye ni mwenye dhambi, ukifa leo, shetani hakuchukui bali utakayekuchuwa na Mungu mwenyewe na kwenda kukutupa katika jehanamu ya moto ukingoja hukumu ya siku ile ya mwisho..

Unatanga tanga nini kwa waganga wa kienyeji? Hao hawatakusaidia chochote, unawatafuta wanadamu, hao nao hawawezi kukuondolea hofu ya mauti na mashaka uliyonayo sasa, kwamba ukifa utakwenda wapi..Anayeweza kufanya hivyo ni Kristo tu peke yake, mwenye funguo za mauti na kuzimu.Yeye ndiye atakayeweza kukufanya uwe huru na hofu ya kifo, kiasi kwamba hata ikitokea unakufa leo, utakuwa na uhakika kuwa roho yako imekwenda sehemu salama. Ukingojea siku ile kuu ya kwenda mbinguni kwa Baba.

Hivyo leo mpe Kristo maisha yako kama bado hujampa, vivyo hivyo kama ni vuguvugu huu ni wakati wa kuwa moto!.. Tubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha, hizi ni nyakati za mwisho, parapanda italia wakati wowote, na Yesu atawafufua kwanza wale waliokufa katika haki nao kwa pamoja na sisi tulio hai tutakwenda kumlaki mawinguni,..lakini jiulize wewe mwenye dhambi utakuwa wapi siku hiyo?..Au ukifa leo hii ni nani atayekusaidia huko uendako? Shetani anaivizia roho yako kwasababu anajua ukifa katika dhambi ni umepotea kwelikweli hata yeye mwenyewe hata kuona milele…Hivyo acha leo ulevi, wizi, rushwa, anasa, uasherati, vipodozi unavyopaka, vimini unavyovaa, matusi unayotukana na mambo yote yanayofanana na hayo..Na upokee Roho Mtakatifu ambaye ni ahadi kwetu tutakaomwamini Yesu.

Uamuzi ni wako, tafakari tena kisha chagua uzima. Wokovu ni bure kwa wote wanaouhitaji..Kristo anaokoa kweli.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/nini-maana-ya-maneno-haya-ya-bwana-nami-nikiinuliwa-juu-ya-nchinitawavuta-wote-kwanguyohana1232/

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAOMBI YA VITA

Maombi ya vita yakoje?..Je! ni lazima kuomba maombi ya vita?

Maombi yamegawanyika katika sehemu kuu 3

  1. Maombi ya shukrani
  2. Maombi ya kuwasilisha haja mbele za Mungu.
  3. Na Maombi ya KUTANGAZA.

Katika aina aina ya kwanza ya maombi ni ile ya KUSHUKURU, Ambapo mwamini atapiga magoti au atasimama na kumshukuru Mungu kwa mema yote anayomtendea yeye binafsi, na familia yake, na jamaa zake, na Taifa lake…hali kadhalika na kwa kila kitu ambacho anastahili kukishukuru mbele za Mungu. Na maombi haya ndio maombi ya muhimu kuliko yote, na yanayopaswa kuchukua muda mrefu kuliko maombi mengine yoyote.

Aina ya pili ya maombi ni ya kuwasilisha haja mbele za Mungu…Haya ni yale ambayo mtu atapiga magoti na kumwomba Mungu hitaji fulani amtimizie, hilo linaweza kuwa hitaji lake binafsi au la mtu mwingine au la kanisa au la Taifa.

Na Aina ya tatu na ya mwisho ya maombi ni maombi ya KUTANGAZA…Katika aina hii ya mwisho ya maombi ndipo panapopatikana maombi ya vita kama yanavyotajwa na wengi, yanaangukia katika kundi hili.

Katika maombi ya kutangaza..hapa ndipo mtu atatumia kinywa chake na mamlaka aliyopewa kuamuru na kuamrisha kila nguvu zote za giza, zilizo kinyume na nguvu za Mungu zipate kuanguka chini kwa jina la Yesu..

Mfano wa maombi ya kutangaza ni maombi ya kutoa pepo. Tunapoamuru pepo amtoke Mtu au kitu kwa jina la Yesu hapo tumetangaza kile kitu kifunguliwe kwa mamlaka ya kimbinguni, na hivyo ni lazima kitii.

Hali kadhalika kama kuna maneno maovu, au mitego ya adui, au kuna mipango na mikakati iliyopangwa na wanadamu au watumishi wa shetani dhidi yako au ndugu,au jamaa au kanisa au Taifa, kwa kutumia vinywa vyetu na kwa jina la YESU, tunaweza kuifuta mipango hiyo, na ratiba hizo na mikakati hiyo, na ikafutika sawasawa na tulivyotamka/kutangaza.

Sasa maombi haya ndio yanayojulikana na wengi kama MAOMBI YA VITA..Mwamini anaweza kutumia muda wa kutosha kutamka baraka juu yake na kwa ndugu zake na kwa kanisa la Kristo kwa jina la Yesu, hali kadhalika anaweza kutangaza kufuta kila mipango ya ibilisi iliyopangwa juu yake, juu ya familia yake, ndugu zake, kazi zake, afya yake, kanisa lake, nchi yake na kila kitu kinachohusiana na yeye. Maombi haya yanaweza kuchukua masaa kadhaa kwa kadiri mtu alivyojaliwa kuomba, na yanaweza kufanyika kila siku. Na pia ni maombi ya muhimu sana. Na maombi haya yanahusisha kutoa au kupaza sauti kwa nguvu…Huwezi kukemea pepo lililopo ndani ya mtu kimoyomoyo…Katika biblia Bwana wetu Yesu, pamoja na Mitume walitamka kwa nguvu na pepo wakawatoka watu…Bwana alipoulaani ule mtini, alitoa sauti kutoka katika kinywa chake..Hali kadhalika tunapozilaani kazi za Adui shetani, ni lazima sauti zitoke katika vinywa vyetu. Sio lazima itoke sauti kama kilio, lakini angalau sauti isikike..Na ndivyo shetani na mapepo yake tutakavyoyaangusha chini..

Maombi haya hayana muda maalumu wa kuomba…Ni vizuri zaidi kuomba kwa pamoja kama kikundi, au peke yako binafsi wakati wa utulivu.

Kwa kina kuhusu Aina tatu hizi za maombi Mwishoni kabisa mwa somo hili chini kuna somo lenye kichwa cha FAIDA ZA MAOMBI. Lifungue hilo ulisome kwa msaada wa Roho Mtakatifu naamini utapata kuongeza kitu juu ya vile unavyovijua.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

JE MOYO WAKO NI MNYOFU MBELE ZA MUNGU

Je kuzalishwa na mkunga wa kiume ni dhambi?

KIJITO CHA UTAKASO.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu?

Bwana alimaanisha nini kusema “Hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu”


Tusome;

Mathayo 10:23 “Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia HAMTAIMALIZA MIJI YA ISRAELI HATA AJAPO MWANA WA ADAMU”

JIBU: Ukiusoma mstari huo kuanzia juu kabisa, yaani kuanzia mstari wa kwanza…Utaona ni Habari inayohusu tendo la Bwana Yesu kuwatuma wanafunzi wake kwenda kuhubiri injili katika miji ya Israeli…Na utaona alipowaagiza wakahubiri aliwapa na baadhi ya maagizo au masharti, kwamba wasichukue chochote na pia wawe wavumilivu kwa watakayoyapitia huko..Lakini mwishoni kabisa mwa maagizo tunaona Bwana anawaambia…“hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu”..

Sasa swali linalojitengeneza kwenye vichwa vyetu hapo ni kwamba…mbona Bwana Mitume walikuwa wameshaimaliza hiyo miji na Yesu bado alikuwa hajarudi?..ina maana mpaka leo injili haijasambaa kwenye miji yote ya Israeli ndio maana Bwana hajarudi mpaka leo?.

Jibu rahisi la swali hili tunaweza kulipata kwenye Habari kama hii hii katika kitabu cha Luka…Tusome,

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.

2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.

3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.

4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njia”

Tuvichunguze baadhi ya vipengele katika mstari huo wa kwanza ambavyo ndivyo vitakavyotupa dira ya kuelewa Habari nzima….katika mstari wa kwanza biblia inasema… “Bwana aliweka na wengine, sabini, AKAWATUMA WAWILI WAWILI WAMTANGULIE kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe”…Zingatia hilo neno “WAMTANGULIE”..Kama wewe ni mswahili mzuri utaelewa maana ya neno “kutangulia” ni nini…kutangulia maana yake ni mtu anakwenda mahali kisha wewe unafuata baadaye…yaani anawahi kufika kule kabla wewe kufika…hiyo ndiyo maana ya kutangulia…

Hivyo mstari huo una maana kuwa “hao wanafunzi sabini na wale 12 Bwana aliokuwa anawatuma kwenda huko katika miji ya Israeli hakuwatuma tu…huko wenyewe…bali Bwana aliwaahidi kwamba atawafuata, hivyo aliwatuma tu kama wamtangulie.”

Ili kuelewa vizuri tafakari tena kamfano haka… “Umemwagiza mfanyakazi wako atangulie asubuhi na mapema sehemu ya kazi kuendelea na kazi, na ukamwambia hatamaliza kazi zote kabla ya wewe kufika hapo ofisini, maana yake utafika kabla hata hajamaliza kazi zote”.. Ndicho Bwana alichowaambia wanafunzi wake, kwamba huko wanakwenda naye pia atakuja kabla hawajaimaliza miji yote ya Israeli (Hilo ni neno la Faraja)…Na kweli aliiungana nao baadaye hakuwaacha yatima…

Sasa kuna jambo moja la kujifunza hapo…Kwamba Desturi ya Bwana ilikuwa hafiki mahali kabla ya kutuma kwanza wajumbe wake wakamtengenezee njia…Maana yake kabla ya yeye kuja mahali anatuma kwanza watumishi wake wakahubiri injili..Ndivyo alivyofanya kwa Yohana Mbatizaji…yeye alitumwa kumtengenezea Bwana njia na kuiandaa mioyo ya watu kabla Bwana mwenyewe hajaanza kuhubiri..ili atakapoanza kuhubiri vile Bwana atakavyohubiri visiwe ni vitu vigeni sana kwa watu wake.(kasome Yohana 10:41-42, na Luka 1:17).

Utaona sehemu zote kabla Bwana hajaenda mahali huwa anatuma wanafunzi wake kwanza na baadaye anaungana nao.. (kasome Luka 9:52-54, Marko 14:12-18, Marko 11:1-4)..

Ndugu Mpendwa hata sasa, Bwana bado anatuma watu wake kuitengeneza njia yake…Umesikia injili mara ngapi?, kila mahali upitapo, mtaani, kwenye magari, mashuleni, unapofanyia kazi?..lakini unadharau kwasababu labda anayekuhubiria umemzidi kipato, au umemzidi elimu, au umri?..Lakini lisikie hili neno ambalo Bwana Yesu alilisema..

Marko 9:37 “Mtu akimpokea mtoto mmoja wa namna hii kwa jina langu, anipokea mimi; na mtu akinipokea mimi, humpokea, si mimi, bali yeye aliyenituma”

Hako katoto unakokadharau sasa, huyo uliyemzidi elimu, pengine na kipato…huyo ambaye hata maandiko hawezi kuyatamka vizuri na anakuhubiria utubu umgeukie Mungu lakini unamchukulia unavyojua wewe…Bwana Yesu ambaye sasa hivi yupo mbingu za mbingu anamheshimu, siku ile tutaonyeshwa tumemkataa yeye Dhahiri.

Bwana atusaidie.

Kama bado hujampa Yesu Kristo Maisha yako, tupo ukingoni sana mwa siku za mwisho, ambapo ghafla tu unyakuo utapita na watakatifu watatoweka….waliobaki hawatasikia tena usumbufu wa mahubiri wanayohubiriwa sasa..watakuwa wamefungua jalada lingine la maisha..na watakatifu vivyo hivyo..Kwahiyo sio wakati wa kukaa nje..Mlango wa Safina unakaribia kufungwa, waasherati,walevi, wezi, watukanaji, watazamaji picha chafu mitandaoni, wanaokula rushwa, na wanaofanya kila aina ya machafuko biblia inasema sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la moto. Ingia leo ndani ya Safina ya Yesu, wokovu unapatikana bure.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?

JE! WEWE NI MWAKILISHI MWEMA?

Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?

Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?

Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?

SWALI: Ukisoma Yohana 1:19-26 inaelezea habari za Yohana mbatizaji akijitambulisha yeye ni nani! Napata shida katika mstari wa 21, alipoulizwa ” wewe u nabii yule” akajibu la!.

Huyu nabii yule, ambaye wayahudi walimtegemea kuja, ni nani?

Maana Yohana alishaulizwa kama yeye ni KRISTO, au ELIYA mwanzoni na akakanusha kuwa yeye si hao…Sasa huyu nabii yule ni nani?


JIBU: Tusome..

Yohana 1:19 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?

20  Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.

21  Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La.

22  Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako”?

Mstari huu umetafsiriwa vibaya hususani kwa watu wasio wakristo wanaosema huo ni unabii unaomzungumzia mtume Mohamedi, kuwa atakuja baada ya Kristo kuwarejeza watu kwa Mungu

Lakini biblia haitabiri jambo lolote kuhusu kuja kwa mtu mwingine baada ya Kristo, yeye ndiye Alpha na Omega, hakuna nabii au mtume mwingine yoyote ambaye atatumwa baada ya Kristo, kuwaongoza watu katika njia ya kweli..Kama mtu atajiita mtume au Nabii basi ajue huduma yake italenga katika kuwaelekeza watu kwa  huyu nabii mkuu Yesu Kristo,..Lakini sio kupokea maagizo yake tofauti yanayodai kuwa yanawaongoza watu kwa Mungu.

Sasa swali ni nani aliyekuwa anazungumziwa pale?

Kabla ya kufahamu ni nani aliyekuwa anazungumziwa pale, ni vizuri kufahamu Unabii Musa aliutoa huko nyuma kuhusu nabii mwingine ambaye Mungu atamnyanyua kama yeye, (Kumbukumbu 18:15-22)..Sasa biblia inaweka wazi kabisa nabii huyo aliyezungumziwa ni Yesu Kristo na hilo tunalithibitisha katika (Matendo 3:22-23) ukipata nafasi unaweza kuvisoma kwa muda wako vifungu hivyo…

Sasa Je hawa wayahudi walimaanisha nabii gani tena huyu? Ambaye walimuulizia Yohana..?

Jibu ni kwamba enzi zile wayahudi walikuwa na mitazamo mingi ambayo mengine haikuwa sahihi, na hiyo ni kutokana na kuwa na ukimya wa miaka mingi bila kuzukiwa na nabii yoyote Israeli, tangu nabii wa mwisho ambaye aliyejulikana kama Malaki..Hiyo ikawafanya wengi wao waamini kuwa wapo manabii wa kale kama Yeremia watafufuka au watashushwa kwa ajili ya kuwatolea unabii na maneno ya Mungu..

Na ndio maana utaona pale Bwana Yesu alipowauliza mitume wake, kuwa yeye ni nani walimjibu hivi..

Mathayo 16:13 “ Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? 14  Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.

Soma tena..

Luka 9:7 “Na Herode mfalme akasikia habari za yote yaliyotendeka, akafadhaika kwa sababu watu wengine walisema ya kwamba Yohana amefufuka katika wafu,

8  na wengine ya kwamba Eliya ametokea, na wengine ya kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amefufuka”.

Soma pia Luka 9:19..utaona jambo hilo hilo…

Mistari hii yote inathibitisha kuwa, wayahudi walikuwa wanatazamia kuwa mmojawapo wa manabii wa kale atanyanyuka kabla ya kuwasili masihi (Kristo) duniani, ambaye labda ni Yeremia, au Danieli, au Isaya… mtazamo ambao haukuwa sahihi.

Na ndio maana hata pale utaona sasa kwanini Yohana aliulizwa je “wewe u nabii yule” wakirejea mmojawapo wa manabii wa kale amekuja kuwahubiria maneno ya Mungu…Lakini yeye akajibu  La!.

Hivyo kwa hitimisho hakuna Nabii mwingine aliyetokea wala tunayemngojea sasa, atakayekuwa mkuu Zaidi ya Masihi YESU KRISTO. Huyo ndiye chapa na nafsi ya Mungu, na mkuu wa wa wafalme wa Dunia, na Bwana wa Mabwana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Shetani ni nani?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?

SWALI: 1Timotheo 4:14 “Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee.”.. Je ni kweli huwezi kuijua au kuitumia karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?


JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu wazee wanaozungumziwa hapo ni wakina nani?..wazee wanaozungumziwa hapo sio wazee wa ukoo, wala wazee wa vijiji, bali wazee wa Imani ambao ni viongozi wakongwe kiimani katika Kanisa…Na hawa wanaweza kuwa Wachungaji, Maaskofu au Mashemasi..ambao wamekaa muda mrefu wakitumika katika kazi ya Mungu. Wengi wa hawa Bwana anakuwa amewafundisha kipekee na kuwapitisha katika mambo mengi, hivyo wanakuwa wamekirimiwa hekima zaidi ya wengi katika ufahamu wa Neno..Kama vile Sulemani, alivyoandika hekima zile na kuwaita wale aliowaandikia “wanangu”

Mithali 3: 11 “Mwanangu, usidharau kuadhibiwa na Bwana, Wala usione ni taabu kurudiwa naye.

12 Kwa kuwa Bwana ampendaye humrudi, Kama vile baba mwanawe ampendezaye”.

Ni kama vile Mtume Paulo alivyowaita wanawe, wale aliowageuza na kumgeukia Kristo.

2Timotheo 2:1 “Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu; kwa ajili ya ahadi ya uzima ulio katika Kristo Yesu; kwa Timotheo, mwanangu mpendwa. Neema na iwe kwako, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sasa hili kundi katika kanisa ndio linaloitwa wazee wa kanisa. Lakini pamoja na hayo, sio wote ni watumishi wa kweli wa Mungu, wapo pia wazee ambao ni mapando ya shetani..biblia imesema tutawatambua kwa matunda yao.

Sasa tukirudi kwenye swali, Je ni lazima kuwekewa mikono na wazee hawa ili karama au huduma ijidhihirishe?, na kwamba pasipo kuwekewa mikono na wazee hawa huwezi kuifahamu karama yako au huwezi kuifanya kazi ya Mungu?

Jibu rahisi la swali hili ni HAPANA!..Mikono ya wazee haiumbi karama ndani ya mtu, wala haidhihirishi karama ndani ya mtu…bali ina bariki karama ambayo tayari ipo ndani ya mtu.

Wengi wasiouelewa mstari huu, wanafikiri mpaka wazifahamu karama zao ni lazima kwanza wawekewe mikono na wazee…jambo ambalo sio sahihi kibiblia.

Katika biblia Agano jipya, tunamsoma mtu anayeitwa Paulo na Barnaba…hawa baada ya watu wote kuijua karama ambayo Mungu kaiweka ndani yao, yaani karama ya kitume…Ndipo wazee wa kanisa wakawawekewa mikono kwa uongozo wa Roho Mtakatifu, kama kuibariki huduma/ karama ambayo tayari ipo ndani yao..na hawakuwawekea kwanza mikono ndipo wakawa mitume..Hapana…Paulo alikuwa mtume tayari na alikuwa ameshapokea maagizo ya utume wake kutoka kwa Bwana Yesu mwenyewe, tangu alipokuwa anaeleke Dameski…hivyo kilichokuwa kimesalia ni watu tu kuibariki huduma hiyo, na hata kama watu wasingeibariki bado Mungu angeendelea kuibariki tu, isipokuwa kuombeana kule kunazidi kuongeza neema ya Mungu juu ya huduma ya mtu, hivyo kuna umuhimu pia mkubwa sana…Tusome,

Matendo 13:2 “Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.

3 Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao”.

Umeona hapo?..Neno linasema “Nitengeeni Paulo na Barnaba kwa kazi ile niliyowaitia” maana yake..tayari walikuwa wameshapewa huduma/kazi na Mungu..na sio kwamba walipokea huduma au karama ile siku ile ya kuwekewa mikono au baada ya kuwekewa mikono.

Hali kadhalika hata sasa, mtu aliyeokoka anapewa huduma na Mungu mwenyewe na si mwanadamu…hakuna mantiki yoyote kwenda kutafuta kupokea karama yako kutoka kwa mtumishi au mchungaji au mwanadamu yoyote Yule..Mungu aliyekuita atakufunulia wewe mwenyewe wito aliokuitia….na baada ya kukufunulia, wewe mwenyewe utaujua na watu wote wa kanisa watauona wito wako…na wakishaona kwamba Fulani anawito kweli katika eneo Fulani, labda anahubiri Neno kwa bidii na kwa moyo, anaombea watu kwa bidii, anaimba kimaandiko kwa bidii, anafariji watu kwa bidii, anahudumia watu hivi au vile kwa bidii n.k..Hapo sasa ndipo wazee wanakusanyika pamoja kwa uongozo wa Roho Mtakatifu na kuweka mikono juu ya mtu huyo…Na lengo la kufanya vile ni kuibariki ile kazi Mungu aliyoianzisha ndani yake, kumbariki kwamba Bwana azidi kuichochea karama ile iliyomo ndani yake kwa bidii sana hilo tu na si kumpa ile karama..Na tendo hilo lina nguvu sana katika Roho.

Lakini sio tu, mtu hajaokoka, au hajui lolote, wala hatumiki popote na anakwenda kutafuta kuwekewa mikono ili aipate karama..kama leo hii utaona manabii wa uongo wanawaita watu na kuwashika na kuwaambia nimekupa karama ya kinabii, kuanzia leo utaona maono, au nimekupa karama ya kiualimu kuanzia leo utafundisha, au nimekupa karama ya kiutume, au ya uimbaji…hapo hutaambulia chochote zaidi ya maroho ya Yule adui. Vipawa na karama anayetoa ni mmoja tu! naye ni BWANA YESU! MKUU WA UZIMA. Huyo pekee ndio biblia inasema alipopaa mbinguni aliteka mateka akawapa wanadamu vipawa (Waefeso 4:8)…hivyo hakuna mwadamu wala mwinjilisti, wala mwalimu wala Padre, wala nabii wala papa mwenye uwezo wa kumpa mtu karama au kipawa.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KUMBUKA, VIVUKO VYA YORDANI VINAKUNGOJA MBELENI.

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

https://wingulamashahidi.org/2018/07/10/279/

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KAMA TUNATAKA KUWA ASKARI WA BWANA, NI LAZIMA TUJUE VIGEZO.

Shalom mpendwa, Karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima..

Tunaijua Habari ya Gideoni na wanajeshi wake 300, lakini ni vizuri tukajikumbusha tena, naamini lipo jambo jipya tutajifunza leo ndani yake..Tusome..

Waamuzi 7:4 “Bwana akamwambia Gideoni; Hata sasa watu hawa ni wengi mno; uwalete chini majini, nami nitawajaribu huko kwa ajili yako; kisha itakuwa ya kwamba yule nitakayekuambia, Huyu atakwenda pamoja nawe, ndiye atakayekwenda pamoja nawe; na mtu yule nitakayekuambia, Huyu hatakwenda pamoja nawe, basi mtu huyo hatakwenda.

5 Basi akawaleta watu chini majini. Bwana akamwambia Gideoni, Kila mtu atakayeyaramba maji kwa ulimi wake, kama vile arambavyo mbwa, huyo utamweka kando; kadhalika kila mtu apigaye magoti kunywa.

6 Na hesabu ya hao waliokunywa kwa kuramba-ramba, wakipeleka mkono kinywani, ilikuwa watu mia tatu; bali watu wengine wote walipiga magoti kunywa maji.

7 Bwana akamwambia Gideoni, Kwa watu hawa mia tatu walioyaramba maji nitawaokoa, nami nitawatia Wamidiani katika mikono yako; lakini watu hawa wote wengine na waende zao, kila mtu mahali pake”.

Amen.

Ukitazama hapo, utaona lile kundi la kwanza walipofika tu majini jambo la kwanza walipiga magoti, jambo ambalo wale wengine hawakulifanya…

Pili walikutanisha midomo yao na yale maji ya mto moja kwa moja.Kwasababu walikuwa na kiu sana, hivyo njia pekee walioina kuwa itaondoa kiu yao kwa haraka ni kwa kupelekea midomo moja kwa moja majini, ili wanywe kwa haraka haraka bila bugdha yoyote.

Tofauti na wale wenzao, ambao walikuwa kwanza wanayakusanya maji kwenye mikono yao, kisha wanayalamba kidogo kidogo, kisha tena wanachota na kulamba hivyo hivyo, kidogo kidogo hadi walipokata kiu yao..

Walikuwa wanahakikisha kwanza kile wanachokinywa kabla ya kukinywa, bila kujali kuwa yatakuwa yanakaa kidogo tu kwenye mikono yao, na kuvuja vuja..Bila kujali kujitesa kuchota chota kila mara.

Pia walikataa kupiga magoti kuelekea maji, bali waliinama tu, au walichuchumaa, na hiyo ikawapa wigo mzuri wa kuona hatari iliyo mbele yao, kiasi kwamba hata adui angetokea mbele yao wangeweza kuacha wanachokifanya na kupigana nao, tofauti na wale wengine..

Vivyo hivyo, hata sisi, ni kweli tupo ulimwenguni, na wakati mwingine itatupasa tuchume vya ulimwenguni kidogo, lakini tukijisahau kuwa tupo mapambanoni na adui yetu shetani yupo mbele yetu, tukayapigia magoti mambo ya ulimwengu huu.. yaani kufanya mambo ya ulimwengu huu kuwa ndio kila kitu kwetu.Tujue kuwa hatufai kwa ufalme wa mbinguni.

Sio kila kinachokuja mbele yetu, ni cha kukipaparikia kwa moyo wote, sio kila fursa ni kutoka kwa Mungu vingine ni mitego ya adui,..Unapaswa uchague kazi, unapaswa uchague marafiki, unapaswa uchague mazingira ya kuishi..Sio kila kazi ilimradi tu inakupa pesa ni ya kuifanya..Unapaswa uipitishe kwanza kwenye mikono yako ya rohoni, uangalie je! Hii kazi ni salama, haitaniletea athari yoyote katika wokovu wangu huko mbeleni? Je hii kazi ni kulingana na Neno?..

Sasa ukishaiona haiikinzani na Neno la Mungu na haina madhara kiimani, ndipo unairamba tena kidogo kidogo, na sio kuikurupukia.. Kila tenda inayokuja inaipitisha kwenye maandiko kwanza, je ina sumu ya adui?..kama askari hawa walivyoipitisha maji mikononi kwanza kabla ya kuyanywa…Unaitazama je! Ina rushwa ndani yake?, je ina utapeli ndani yake n.k

Lakini kama hutajiuliza chochote wewe, kila fursa inayokuja mbele yetu, tunaipaparikia hutufai kuwa askari wa Mungu..haijalishi ni nzuri vipi, kwasababu huwezi jua baadaye itakufanya hata ule wakati wako uliokuwa unautumia kuomba unamezwa na shughuli hizo, au jumapili yako ulikuwa unakwenda ibadani sasa, inaingiliwa na kazi hizo, au mavazi yako uliyokuwa unavaa ya staha yanageuzwa na kuwa ya kikahaba.

Vile vile na marafiki pia, sio kila mtu unayekutana naye ni lazima awe Rafiki yako tu, unapaswa umpitishe kwanza kwenye mikono yako ya rohoni, kisha ukimwona anaendana na Imani yako, ndipo uanze kuunga naye urafiki, tena kidogo kidogo, mpaka utakapomthitisha kamili baada ya muda mrefu..Wengi leo wanawachunguza marafiki kama ni washirikina tu!..hicho ndicho wanachoweza kuchuguza..lakini hawawez kuchunguza huyu rafiki kama ni mlevi, au kama ni mtu wa rushwa, au mtu wa kutomjali Mungu..wengi hayo macho hawana, wana macho tu ya kuchunguza ushirikina.

Vilevile na mazingira, sio kila mazingira yanayokujia mbele yako ni ya kuishi au kukubaliana nayo..chunguza kwanza..Chunguza chochote kile kabla hujakifanya ukikilinganisha na wokovu wako, Je, ni salama?..kwasababu wokovu ni kitu cha kulinda na kukipigania kuliko kitu kingine chochote. Biblia inasema Imani tumekabidhiwa mara moja tu!

Kwasababu mitego ya adui ipo kila kona. Mungu aliona mbele ndio maana hakuwaruhusu wale wengine waende vitani, kwasababu alijua huko mbeleni, askari wataishiwa nguvu sana, watakuwa na kiu na njaa, lakini bado mapambano hayajaisha, Je watakuwa tayari kutotazama mambo ya mwilini wakaendelea na mapambano? (Soma Waamuzi 8:4). Ndio maana akawatenga wale 300 tu..waliovumilia kunywa maji kwa uangalifu na taratibu taratibu.

Na sisi pia tukitaka tuwe askari kamili wa Kristo, Bwana atusaidie tuyazingatie hayo….

Mungu akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

KILA MTU ATATOA HABARI ZAKE MWENYEWE.

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?

JE! KUBET NI DHAMBI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIMWOGOPE YEZEBELI.

Mungu anapompa mtu kazi ya kufanya, na mtu yule akawa na hofu na maadui wa Imani yake au akawa anakawia kawia basi nafasi yake anapewa mtu mwingine…Moja ya sababu kati ya nyingi inayompelekea mtu kupoteza nafasi yake ya utumishi ni HOFU.

Hofu ya kuwaogopa maadui wa Imani yako, hofu ya kuogopa endapo ukihubiri kinyume na mifumo ya adui shetani itakuwaje?..endapo ukiziharibu na kuzidhihirisha kazi za shetani itakuwaje?..Endapo nikizitukana kazi za adui, kama Daudi alivyozitukana itakuwaje?..Nikizidhalilisha kazi za kichawi itakuwaje?..hofu ya kwenda kuhubiri vijijini kuhofia wachawi wa kule, hofu ya kutamke jina la Yesu palipo na nguvu za giza n.k…Hofu ya namna hii ina madhara makubwa sana kiroho..

Katika biblia tunajifunza mtu mmoja aliyeitwa Eliya, ambaye alipewa jukumu la kuisafisha Israeli na kumwondoa mungu baali katikati ya Taifa la Mungu, lakini mwisho wa siku akaingiwa na hofu..na kulikimbia kusudi..

Kama ni mwanafunzi wa biblia, utakuwa unaielewa vyema Habari ya Nabii Eliya jinsi alivyowaua wale makuhani 450 wa Baali na 400 wa Ashera jumla yao 850 (1Wafalme 18:16-40)..Idadi hii ilikuwa ni kubwa sana Eliya aliyoiua ambayo ikasababisha upungufu mkubwa wa makuhani wa Baali katika nchi ya Israeli, hivyo kupelekea kiwango kikubwa cha Uovu kupunguzwa Israeli…Kwani makuhani hao waliajiriwa na mwanamke Yezebeli kutoka huko Lebanoni kuja kuingiza miungu migeni katika Taifa Takatifu la Mungu..

Kwani makuhani hao wa Baali walikuwa wanafanya uchawi na kuipotosha Israeli nzima…Hata wakati wanashindana na Nabii Eliya kushusha moto juu ya ile sadaka, sio kwamba hawakuwa na huo uwezo..huo uwezo wa kutengeneza moto wa kimiujiza ulikuwa ni uchawi mdogo sana kwao, ndio maana walikuwa na ujasiri wa kukubali changamoto ile na Eliya….lakini kwasababu hakuna uchawi wowote ambao unaweza kuwa na nguvu mbele ya Nguvu za Mungu aliye hai, ndio maana ghafla walijikuta wameshindwa kutengeneza moto wao wa kichawi juu ya ile sadaka siku ile…

jambo ambalo hapo kabla halikuwa jambo gumu kwao kulifanya.

Hivyo walikuwa ni wachawi ambao waliajiriwa na mwanamke Yezebeli ambaye ndiye aliyekuwa malkia wa Israeli wakati huo..(2Wafalme 9:22)… Lakini Eliya pamoja na kuipunguza idadi hiyo yote ya wachawi juu ya Israeli, bado hawakuisha wote…wapo wengine ambao walikuwa wapo mbali…na wengine walibaki Samaria …na Zaidi ya yote hata Yezebeli mwenyewe ambaye alikuwa amewaajiri, alikuwa bado yupo hai…

Hivyo Eliya japokuwa alipunguza machukizo juu ya Israeli kwa sehemu kubwa..lakini bado alikuwa hajautoa ule mzizi wote. Na Mungu alimkusudia yeye ndiye autoe mzizi wote na aisafishe Israeli yote lakini kwasababu ya vitisho vya Yezebeli kuutoa uhai wake alimwogopa na kumkimbia kunusuru uhai wake.…Eliya akakimbia mpaka Herobu kwa hofu ya Yezebeli na kumwomba Mungu autoe uhai wake….Hivyo kwa hofu alimwomba Mungu aikatishe hudama yake…Na Mungu aliitoa Huduma hiyo na kuwapa watu wengine watatu waimalizie ambao ni HAZAELI, ELISHA na YEHU.

1Wafalme 19:15 “Bwana akamwambia, Enenda, urudi njia ya jangwa la Dameski; ukifika, mtie mafuta Hazaeli awe mfalme wa Shamu.

16 Na Yehu mwana wa Nimshi mtie mafuta awe mfalme wa Israeli; na Elisha mwana wa Shafati wa AbelMehola mtie mafuta awe nabii mahali pako.

17 Na itakuwa atakayeokoka na upanga wa Hazaeli, Yehu atamwua; na atakayeokoka na upanga wa Yehu, Elisha atamwua”.

Sasa Neno la Mungu ni lazima litimie kwa mkono wa Hazaeli na Elisha na Yehu..kwamba uovu wa baali na makuhani wake na waanzilishi wake waondolewe Israeli kwa mikono ya hawa watatu…Sasa Habari za mambo aliyoyafanya Elisha na Hazaeli zipo katika maandiko…Lakini leo nataka tumtazame huyu mtu wa mwisho anayeitwa YEHU, jinsi gani alilimaliza kusudi la Mungu vizuri.

Yehu, alitiwa Mafuta na Eliya mwenyewe awe mfalme juu ya Israeli…ingawa hakuwa mkamilifu sana, lakini Mungu alimpa ujasiri mkuu kuliko wa Eliya…pale ambapo Eliya alimwogopa Yezebeli na kumkimbia huyu Yehu alimfuata Yezebeli kwenye jumba lake la kifalme na kumtoa kwenye umalkia ili auawe…na sio hilo tu!…bali aliwaua manabii wote wa Baali ambao walikuwa wamesalia kwa siku moja Zaidi hata ya ile idadi ya Eliya aliyoiua kule Karmeli. Na akamtoa mungu anayeitwa baali katika Taifa la Israeli, na baada ya hapo, wana wa Israeli hawakuabudu tena baali..

2Wafalme 10:18 “Yehu akawakusanya watu wote, akawaambia, Ahabu alimtumikia Baali kidogo; bali Yehu atamtumikia sana.

19 Basi niitieni manabii wote wa Baali, wote wamwabuduo, na makuhani wake wote; mtu asikose kuwapo hata mmoja. Maana ninayo dhabihu kubwa ya kumtolea Baali; ye yote atakayekosa kuwapo hataishi. Lakini Yehu alifanya hayo kwa hila, ili awaharibu waliomwabudu Baali.

20 Yehu akasema, Takaseni kusanyiko la dini kwa Baali. Wakalitangaza.

21 Yehu akatuma wajumbe katika Israeli yote, nao wote waliomwabudu Baali wakaja, wala hakusalia mtu ye yote asiyekuja. Wakaingia nyumbani mwa Baali; ikajaa nyumba ya Baali tangu mlango hata mlango.

22 Akamwambia yule aliyekuwa juu ya hazina ya mavazi, Uwatolee mavazi wote wanaomwabudu Baali. Akawatolea mavazi.

23 Akaingia Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu nyumbani mwa Baali, akawaambia waliomwabudu Baali, Tafuteni mkaangalie, asiwepo hapa pamoja nanyi mtu amtumikiaye Bwana, ila wamwabuduo Baali peke yao.

24 Wakaingia ili watoe dhabihu na sadaka za kuteketezwa. Basi Yehu alikuwa amejiwekea nje watu themanini, akasema, Mtu mmoja akiokoka wa watu niliowatia mikononi mwenu, amwachaye huyo, roho yake itakuwa badala ya roho yake.

25 Ikawa mara alipokwisha kutoa sadaka ya kuteketezwa, Yehu akawaambia walinzi na maakida, Ingieni mwapige; mtu awaye yote asitoke. Basi wakawapiga kwa makali ya upanga; walinzi na maakida wakawatupa nje, wakaenda mpaka mji wa nyumba ya Baali.

26 Wakazitoa nguzo zilizokuwamo nyumbani mwa Baali, wakaziteketeza.

27 Wakaibomoa nguzo ya Baali, na kuiangusha nyumba ya Baali, wakaifanya choo hata leo.

28 NDIVYO YEHU ALIVYOMHARIBU BAALI KATIKA ISRAELI”

Sasa katika Habari hiyo tunajifunza ni kwamba..kama sio Nabii Eliya kumwogopa Yezebeli, Mungu angelimaliza kusudi lote mkononi mwake,…kwasababu huyo Yezebeli ambaye alikuwa anamwogopa Yehu alikuja kumuua kirahisi sana, wala hata hakutumia upanga wala silaha kumuua…aliwaambia tu watu wamkamate wamtupe dirishani..hivyo tu!..(2wafalme 9:30-35).

Na sisi hatupaswi kumwogopa Adui shetani na vitisho vyake, katika kulitimiza kusudi la Mungu..Maadui wa Imani yetu ni wengi, na wana vitisho vikali…lakini hatupaswi kusikiliza vitisho vyao…

Haihitaji mapanga na marungu kumwangusha Yezebeli…ni amri tu! Kama Yehu alivyofanya…Na sisi haihitaji majeshi wala michanganyiko mingi kumwondoa Adui shetani mbele yetu..bali inahitajika amri tu!..Unatamka na Yezebeli anakwenda chini..

Hivyo usiogope mganga mtaani kwako, usiogope wachawi vijijini kwako, usiogope mwanasiasa mbele yako, usiogope chochote kijiitacho kikuu mbele yako ambacho kinakutishia Imani yako au huduma yako..wewe litazame kusudi la Mungu tu kulitimiza na kulimaliza.

Zekaria 4:6 “Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi”..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

Wakatoliki wanaabudu sanamu?

NITAFUNGUAJE MILANGO ILIYOFUNGWA MBELE YANGU?

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

UCHAWI WA BALAAMU.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”;

Mwishoni mwa mstari huo wa 18 biblia inatuambia ‘”bali mjazwe Roho”.. Hili Ni neno endelevu, Sasa kumbuka Mtume Paulo alipokuwa anazungumza na kanisa hili la Efeso Alijua kabisa walishapokea Roho Mtakatifu tangu zamani walipoamini, na ndio maana likawa kanisa kubwa lilolitwa Efeso, Lakini hiyo haikumfanya mtume Paulo aone wamefika, bali aliwaasa siku baada ya siku wajazwe Roho, kwasababu alijua kuwa Roho anaweza kuzimishwa ndani ya mtu, hali kadhalika pia anaweza kujaa na kupungua kwa jinsi mtu atakavyokuwa makini au mzembe katika wokovu wake.

Hata sisi wakristo wa zama hizi ambazo uovu wetu ni mkubwa kuliko ule wa kanisa la Efeso, kusema tu, tumeokoka, au tumepokea Roho Mtakatifu, na huku bado uhusiano wetu na Mungu haueleweki haitoshi kutufikisha mbinguni, bali tunapaswa tujazwe Roho Mtakatifu siku baada ya siku mpaka siku ile ya Unyakuo itakapotukuta..

Kwasababu tukipuuzia jambo hilo, tutafananishwa na wale wanawali wapumbavu tunaowasoma katika Mathayo 25 ambao walikuwa wanamngojea Bwana wao lakini hawakuwa na mafuta ya kutosha ya kuwafikisha hadi ule wakati wa kumlaki Bwana wao.. matokeo yake saa ile ilipofika ya Bwana wao kutokea, ndio wakajishtukia kuwa taa zao zinakwenda kuzima…Sasa wakati wanakwenda kununua huku nyuma tayari Bwana arusi ameshawasili na kuwachukua wale aliowakuta wapo tayari na kuingia nao karamuni..Na wale wengine waliokwenda kuchukua mafuta waliporudi wakajikuta wameshachelewa.. Hasara ikawa ni kwao na taabu yao yote ya kumngojea Bwana ikiwa ni bure.. Japokuwa nao pia walikuwa ni wanawali (mabikira) yaani wameokoka, ambao wanamngojea tu Bwana wao kwa saburi kama wale wengine.. Lakini kwasababu ya kupuuzia jambo la msingi la mafuta katika chupa zao ikawafanya wakose karamu..

Siku zote mafuta yanafananishwa na Roho Mtakatifu..Tunapompokea Roho Mtakatifu siku zile za kwanza tulipookoka, tulipokea mafuta ya kuwasha tu vyombo vyetu vya usafari..Lakini tukiridhika na yale tu, hatutafika mbali. Ndugu ili kukivuka hichi kipindi cha Uovu uliokirithiri duniani sasa..Tunapaswa tuendelee kujazwa Roho..

Pengine utauliza nifanye nini ili nijazwe Roho Mtakatifu?

Roho Mtakatifu anaweza kuendelea kujaa ndani yetu, kwa walau mambo makuu manne.

  1. Kwa kuomba;

Biblia inasema, Luka 13:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”

Ukiwa mtu wa kuomba, na kukataa uvivu kwa kutokusali walau saa moja kwa siku, ndivyo utavyojiongezea mafuta yako ya rohoni na hivyo Roho Mtakatifu atapata wigo mpana wa kuyatawala maisha yako siku baada ya siku.

    2.  Kwa kujifunza kwa bidii Neno la Mungu..; Neno ndio chakula cha uzima wa mtu. Usipojibidiisha kujifunza Neno la Mungu, kutafuta habari za uzima, usidhani kuwa Roho Mtakatifu atapata nafasi ya kukufundisha kitu chochote ndani yako. Kwasababu Mungu yupo katika Neno lake(Sauti ya Mungu ni Neno lake). Ukiwa umeokoka, halafu unaona uvivu kujifunza Biblia basi ujue Roho wa Mungu ameshazimika ndani yako kitambo..Na hivyo hata wakati wa unyakuo utakapofika utafananishwa na wale wanawali wapumbavu.

     3.  Kaa mbali na uovu; Siku zote dhambi inavutia, lakini mwisho wake ni mbaya..Tunapoivumilia dhambi katika maisha yetu ndivyo Mungu anavyouficha uso wake. Na matokeo yake Roho Mtakatifu anazimika, au anaondoka kabisa ndani yetu.(Isaya 59:2)

    4.  Tangaza habari njema: Ukiwafundisha wengine, na wewe hapo hapo Roho wa Mungu anakufundisha, ukiwafungulia wengine hazina ya maneno ya uzima, Roho Mtakatifu anapata nafasi ya kukufunulia wewe Zaidi na kukutumia, ili kuwaokoa watu wake..Na hivyo ni sharti atakaujaza tu Roho wake, kwasababu siku zote unafanya kazi yake..Na hapo utakuwa na nafasi nyingine ya kuwa karibu na yeye.

Hivyo tusiridhike tu, na hali za kiroho tulizopo, tukajificha nyuma ya kivuli cha Neno nimeokoka..Tunapaswa tujiulize Je! Mafuta tuliyonayo yanatutosha mpaka wakati wa kuja kwa Bwana? Kama sivyo basi huu ndio wakati wa kuzitengeneza upya taa zetu..kwa kuhakikisha kuwa kila siku Roho Mtakatifu anapata nafasi maishani mwetu..Ili ile siku ambayo hatujui ni lini itakapotujilia kwa ghafla basi tuwe na uhakika kuwa UNYAKUO hautatupita.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

RABI, UNAKAA WAPI?

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post