Kama wewe ni Raisi fahamu tu kuna WALINZI mbinguni wanakutazama kama vile wale waliokuwa wanamtazama Mfalme Nebukadreza, kama wewe ni waziri,mbunge, mkuu wa mkoa, balozi, diwani, m/kijiji, mjumbe, n.k. fahamu tu wapo walinzi juu wanakutazama mienendo yako kama je unaenenda katika haki au la!..Kama wewe ni mchungaji, mwinjilisti, Nabii, mwalimu, shemasi, mwimba kwaya, mfanya usafi kanisani, mwandishi, n.k. fahamu tu wapo walinzi mbinguni wanakutazama kama je! unasimama katika njia ya haki au la!, Kama wewe ni baba, au mama, au mlezi au boss, jua tu kuna walinzi watakatifu mbinguni wakifuatilia nyendo zako kama kweli hao unaowalea unawatendea haki au la!….n.k.