Moyo ni neno ambalo linaweza kuwakilisha aidha nafsi ya mtu au roho ya mtu, inategemea na linapotumika.
Kwa kawaida hakuna lugha ya kuielezea nafsi ya mtu jinsi ilivyo, au roho ya Mtu jinsi ilivyo, kwamba inafananaje, au iko namna gani, hivyo lugha nyepesi ambayo inaweza kuwakilisha vitu hivyo viwili (yaani Roho na Nafsi) ni Moyo.
Kama vile tunavyokosa lugha ya kuzielezea nguvu za Mungu zikoje zikoje, au uweza wake ukoje ukoje, una rangi gani, una mwonekano gani, au unafanyaje kazi, hivyo tunaishia tu kusema “mkono wa Mungu umefanya hichi au kile”… tukimaanisha kwamba Nguvu za Mungu zimetenda hayo au uweza wa Mungu umefanya hayo. Hapo tumetumia kiungo cha mwili kuwakilisha kitu Fulani cha rohoni kisichoonekana. Na lengo la kufanya hivyo ni ile kitu kile kiweze kueleweka zaidi na kuleta maana.
Ingawa si wakati wote tutaziwakilisha nguvu za Mungu kwa “mkono wake” lakini pia tukitumia “mkono wa Mungu ” kuwakilisha “nguvu za Mungu” tutakuwa hatujakosea.
Na ni kwanini tunatumia kiungo mkono na si mguu??… Kwasababu mkono ndio unaofanya mambo yote, mkono ndio unaotumika kutia sahihi ya jambo Fulani liwe baya au zuri.. Hivyo mkono siku zote unawakilisha mamlaka ya Mtu au nguvu zake.
Kadhalika ili ipatikane lugha rahisi ya kuwakilisha roho ya mwanadamu au nafsi yake, ambayo haionekani kwa macho, ndipo lilipotumika neno “moyo” kama mbadala, Kwamfano badala ya kusema “Nina huzuni nyingi rohoni” unaweza kusema “nina huzuni nyingi moyoni”. Au badala ya kusema “nafsi yangu ina huzuni” unaweza kusema “moyo wangu una huzuni” ni kitu kile kile.
Sasa kwanini kitumike kiungo moyo na si kiungo kingine kama figo:
Kama tunavyojua kiungo pekee kinachoendesha na kuzungusha damu katika miili yetu ni moyo. Na ndio kiungo pekee ambacho ni chepesi kuitikia mabadiliko yoyote ya hisia za mwili. Utaona likitokea jambo la kushtusha ghafla, mapigo ya moyo yataanza kwenda kasi!..pakitokea hali ya utulivu sana, mapigo ya moyo yanashuka.. Ni ngumu mtu ashtushwe halafu asikie maini, au figo zinabadilika tabia.. Moyo ni kama vile mtu mwingine wa pili, anaishi ndani ya mwili.
Hivyo tabia hiyo ya kipekee ya kiungo hicho ambacho kipo ndani ya mwili lakini kina uwezo wa kuitikia na kuelewa mambo yanayoendelea nje ya mwili, na zaidi ya yote ndicho kinachozungusha uhai ndani ya mwili, imekifanya kifananishwe na roho au nafsi ya mtu.
Kwahiyo popote pale katika maandiko neno hilo “moyo” linapotumika.. basi fahamu kuwa linawakilisha aidha “nafsi ” au “roho”. Kujua tofauti iliyopo kati ya nafsi na roho unaweza kufungua hapa >> Tofauti ya Nafsi, mwili na roho
Je umempokea Yesu?. Je umempenda Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nguvu zako zote? Au unautumikia ulimwengu na fahari zake?..Kumbuka biblia inasema..
Mathayo 6:21 “kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako”.
Moyo wako upo wapi leo? Kama upo kwa Bwana ni vyema..lakini kama upo katika ulimwengu na fahari zake, kumbuka maandiko yanasema…
Yakobo 4:4 “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu”
Ndugu kitendo cha kuipenda dunia tu tayari wewe ni adui wa Mungu, haihitaji useme kwamba wewe ni adui wa Mungu, hapana! Kitendo cha wewe kupenda fasheni tu, kitendo cha wewe kupenda kuvaa nusu uchi, kitendo cha wewe kuwa mshabiki wa mipira, kitendo cha wewe kupenda kutazama tamthilia na filamu za kidunia, tayari umejifanya kuwa adui wa Mungu. Na maadui wa Mungu wote! Sehemu yao itakuwa ni lile ziwa la Moto..(Luka 19:27).
Kama utapenda kumpokea leo Yesu, mlango wa neema upo wazi, ila hautakuwa hivyo siku zote..ipo siku utafungwa, tukiwa hapa hapa duniani, utafungwa kwa tendo linalojulikana kama unyakuo. Baada ya unyakuo kupita, kitakachokuwa kimebakia duniani ni dhiki kuu tu!, na baada ya hapo ni mapigo ya vitasa saba kama tunavyosoma katika Ufunuo 16. Duniani patakuwa si mahali salama kabisa. Hivyo kama upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako leo, hapo ulipo jitenge kwa dakika chache tafuta sehemu ya utulivu kisha Ungama dhambi zako kwa kumaanisha kukiri makosa yako na kuyaacha. Baada ya hapo, acha vyote kwa vitendo ulivyokuwa unavifanya… Acha udunia wote!! Na hatua ya mwisho tafuta ubatizo sahihi kukamilisha wokovu wako, Ubatizo sahihi ni wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu, kulingana na maandiko (Matendo 2:38)
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Shalom, karibu tujifunze maneno ya uzima.
Wengi wetu tunadhani Bwana Yesu alizaliwa akiwa na ufahamu kamili wa kila kitu, au ujuzi wa mambo yote, Hapana alizaliwa akiwa kama sisi kabisa, hajui kitu chochote, japo alikuwa ni Mungu kweli katika mwili.
Ilipasa iwe hivyo, ili kutimiza kusudi la Mungu, la kumfananisha na sisi katika mambo yote ili awe kielelezo cha sisi kuifuata njia yake. Hivyo kwa kuyatazama tu Maisha ya Bwana Yesu tunaweza kujifunza mambo ambayo hata sisi wenyewe tunaweza kuyafanya.
Mpaka Bwana kufikia hatua ya kufahamu siri nyingi sana za Mungu, halikuwa ni jambo alilozaliwa nalo, hapana, biblia inasema..
“Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu”.
Kuendelea katika hekima na Kimo, maana yake ni kukua kila siku katika hekima ya kumjua Mungu, yaani kutoka kiwango kimoja hadi kingine, hatua moja hadi nyingi.. Na hilo halikuja tu hivi hivi, Bali alikuwa na bidii tangu akiwa mtoto, ya kujifunza maneno ya Mungu, kwa kuwatafuta waalimu ili wamsaidie, Na alipokutana nao alikuwa akiwauliza maswali pale ambapo alikuwa haelewi na kutoa maoni yake pale ambapo alikuwa anapaelewa zaidi,..Jambo hilo unaweza kulisoma katika…
Luka 3:46 “Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.
48 Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
50 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.
51 Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
52 Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu”.
Jaribu kutafakari, kijana wa miaka 12 anatumia siku tatu usiku na mchana, kakaa tu kanisani, akijifunza Biblia, na hiyo ni desturi yake ya mara kwa mara.. Unategemea vipi kijana kama huyo akiwa mtu mzima, atakuwa sawa na watu wengine?
Ni lazima tu, atakuwa katika maarifa ya kumjua Mungu kwa kasi, na ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana, mambo yote hayakumjia tu ghafla ndani yake, labda kazaliwa nacho, hivyo hakuwa na haja ya kuongeza maarifa au kujifunza hapana.
Leo hii, utaona mkristo, hana habari ya kujifunza Biblia, hata akienda kujifunza haulizi maswali, wachungaji wake, au manabii wake, au waalimu wake, yeye ni kusikiliza tu na kuondoka, akiambiwa jambo Fulani hata kama ni gheni kwake, atalipokea tu na kusema AMEN! Baba..Basi..
Kwa mtu ambaye ni msomaji wa biblia, ni lazima tu atakutana na mambo mengi sana yasiyoeleweka, Na Mungu ameyaficha hivyo makusudi, ili atujengee tabia ya kupenda kutafuta, na mwisho wa siku ampe majibu.. Lakini kama utasoma tu biblia kwa kujiburudisha, au kutimiza ratiba, ufahamu kuwa huo sio mpango wa Mungu.
Mungu anataka tujifunze biblia sio, tuisome kama gazeti, Biblia ni kitabu cha mafumbo, hakuna namna mkristo akose maswali ya kumuuliza Mungu..hilo haliwezekani..Embu kaa chini usome kitabu chochote kwa kumaanisha halafu uniambie kama ni mambo yote yaliyopo kule umeyaelewa..Hilo halipo..
Lakini Yesu hakuona aibu ya kutaka kujifunza pale ambapo alikuwa haelewi, na alitumia fursa hiyo vizuri kuwafuata waalimu wake wa torati…Vivyo hivyo na wewe kama unataka kukua katika hekima na Kimo katika kumjua Mungu, wafuate wale waliokutangulia katika Imani, yaani wachungaji wako, manabii wako, mitume wako, waalimu wako, waulize maswali kwa yale uliyojifunza katika biblia..ukiona majibu yao hayajakuridhisha..tafuta tena wachungaji wengine, kawaulize, maswali, hivyo hivyo mpaka Roho Mtakatifu atakufunulia jibu sahihi..
Japo Bwana Yesu alikaa chini ya waalimu, lakini mwisho wa siku yeye ndiye aliyekuwa MWALIMU WA WAALIMU… Alikuwa ni RABI, Alijua siri nyingi za ufalme wa mbinguni, kuliko watu wote waliokuwa duniani, sio tu wale walioishi naye, mpaka pia wale waliomtangulia.
Hata wewe ukiwa ni mtu wa kutoridhika na hali ya ufahamu wako kuhusu Mungu, ukaanza kujifunza, uwe na uhakika kuwa upo wakati, utakuwa ni mtu wa viwango vya mbali sana, na Mungu atajifunua kwako kwa namna ambazo wewe mwenyewe utashangaa.
Anza sasa, kumtafuta Mungu wako, kwa bidii kama za Bwana wetu YESU KRISTO.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?
Shalom, karibu tujifunze Neno la Mungu, lakini kabla hatujaendelea, ningependa kwanza uzitafakari hizi habari mbili, kwasababu ndio kiini cha somo letu kilipo, zingatia sana sana hiyo mistari iliyowekwa katika herufi kubwa.
Luka 5:4 “Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, TWEKA MPAKA KILINDINI, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.
5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.
6 Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika;
7 wakawapungia mikono washirika wao waliokuwa katika chombo cha pili, waje kuwasaidia; wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili, hata vikataka kuzama”.
Pia, soma..
Yohana 21:3 “Simoni Petro aliwaambia, Naenda kuvua samaki. Nao wakamwambia, Sisi nasi tutakwenda nawe. Basi wakaondoka, wakapanda chomboni; ila usiku ule hawakupata kitu.
4 Hata asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufuoni; walakini wanafunzi hawakujua ya kuwa ni Yesu.
5 Basi Yesu akawaambia, Wanangu, mna kitoweo? Wakamjibu, La.
6 Akawaambia, LITUPENI JARIFE UPANDE WA KUUME WA CHOMBO, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki”.
Nataka ufananishe hizo habari mbili, utaona mara ya kwanza Kristo anakutana na akina Petro baada ya kuwahubiria aliwapa maagizo ya kwenda kuvua samaki, akamwambia atweke mpaka vilindini, akiwa na maana waanze safari ya kutoka pale walipo, waende mbali sana kwenye bahari kuu (Ndipo vilindini) ili wakavue samaki zao. Hatujui walisafiri umbali wa kilometa ngapi, lakini mpaka mtu ufike vilindini, ni sharti uende mbali sana na fukwe..Na walipofika wakazishusha nyavu zao kwa Neno la Bwana, kisha wakapata samaki wengi sana, mpaka nyavu zikawa zinakaribia kukatika kama tunavyosoma hiyo habari.
Lakini tunaona pia katika tukio lingine ambalo ni baada ya Kristo kufufuka, aliwaona tena wakihangaika usiku kuchwa kama pale mwanzo wakitafuta samaki wasipate.. Pengine safari hii Petro alitazamia ataambiwa “atweke mpaka vilindini” kama alivyoambiwa hapo kwanza, wakavue, lakini maagizo yalikuwa ni tofauti kabisa, bali palepale UFUKWENI walipokuwepo wametegesha vyombo vyao, Kristo aliwapa maagizo, wazitupe nyavu zao upande wa pili tu wa chombo. Ndipo walipofanya vile walipata samaki wengi sana tena wakubwa, kiasi cha kuwafanya hata wao washindwe kulivuta lile jarife pale pwani walipokuwepo.
Ni nini Kristo alitaka wanafunzi wake na sisi sote tujue?
Kuna majira Kristo atakupa maagizo ya kukihangaikia kidogo kile unachokihitaji, na mwisho wa siku atakufanyia muujiza mkubwa sana katika jambo hilo.. Lakini pia kuna wakati hatokuagiza ukihangaikie hata kidogo, bali hapo hapo ulipo, atakupatia, kuhangaika kwako wewe kutakuwa ni kukusanya tu.
Mambo haya mawili ni vizuri ukayafahamu, wewe uliyeokoka, kwasababu wapo watu wanadhani, Mungu wa “Mana” amekufa, hawezi kutenda kazi tena leo hii, wanadhani njia pekee aliyobakiwa nayo ya Mungu kukubariki, au kukutendea miujiza ni lazima ukajitaabishe huko vilindini! Basi. Nataka nikuambie hilo kweli linawezekana, na likaja kama agizo la Mungu, lakini pia lile lingine nalo linawezekana, tena sana.
Bwana Yesu alisema maneno haya..
Mathayo 6:25 “Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?
27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?
28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti
29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.
30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?
31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?
32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.
33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.
34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”.
Hivyo usilipindue Neno la Kristo, kwa kuegemea upande mmoja tu, Yote yawezekana kwa Mungu (Mathayo 19:26), na vilevile Bwana Yesu alisema yote yawezekana kwake yeye aaminiye, sio Mungu tu peke yake, hata kwa mtu yeyote atakayemwamini Mungu, yatawezekana kwake (Marko 9:23). Hivyo ukimwamini Mungu katika njia ile atajifunua kwako katika hiyo, halikadhali ukimwamini katika njia ile nyingine atajifunua kwako katika hiyo. Hakuna formula kwa Mungu. Yeye sio mwanadamu. Ni Mungu wa milimani, pia ni Mungu wa mabondeni,.Njia zake hazitafutikani,
Warumi 11:33 “Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani!”
Hivyo huna haja, ya kuogopa lolote, unachopaswa kufanya ni kuhakikisha unatembea naye katika njia zako zote, popote pale ulipo, uwe ni katika vilindi au katika fukwe, matokeo yatakuwa ni yale yale. Mwamini tu, huku ukimtumikia kwa moyo wako wote.
Mtafute Mungu ndugu yangu, hizi ni siku za mwisho, Usitoe kisingizio cha kusema nipo busy, siwezi kuomba, siwezi kwenda ibadani, siwezi kusoma Neno, nina majukumu ya kifamilia, hicho kisingizio hakitakuwa na mashiko siku ile ya mwisho utakaposimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu. Kwasababu wataletwa wenzako kama wewe ambao walikuwa buzy kuliko wewe mmojawapo ni Danieli, lakini watakuambia hatukuacha kumtafuta muumba wetu.
Je! Na wewe unatembeaje na Mungu wako, ukiwa hapa duniani?. Je umemkabidhi Maisha yako? Kama sivyo ni heri ukampokea leo kwasababu hakuna anayejua kesho kutatokea nini. Ondoa hofu ya Maisha, anza kumwamini Mungu, na atakuonekania katika mambo yako yote.
Zaburi 27:1 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani”?
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
TUNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.
Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)
NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?
Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?
SWALI: Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi?
Kwanini kuna mahali Bwana Yesu anawaita wale aliowaita mitume, na sehemu nyingine anawaita wanafunzi, tofauti yao ni ipi? Au ni kitu kimoja?
JIBU: Si kila mwanafunzi ni mtume, lakini kila mtume ni lazima awe mwanafunzi wa Yesu.
Mwanafunzi ni mtu ambaye anaketi chini kufundishwa, kupewa ujuzi au utashi au maarifa ya kumsaidia kuishi au kufanya jambo Fulani, Na Bwana Yesu naye alikuwa na watu wa namna hiyo hiyo,
Lakini kumbuka si wote waliomfuata waliitwa wanafunzi wake, isipokuwa wale tu waliokidhi vigezo vyake alivyoviweka, na vigezo vyenyewe ndio hivi;
Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,
26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?
29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,
30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.”.
Lakini Mtume maana yake ni “aliyetumwa”, Wale walioitwa na Bwana Yesu na kuandaliwa kwa jukumu Fulani maalumu waliitwa mitume, ambao walikuwa kumi na mbili tu kwa wakati ule. Na kusudi lenyewe waliloitiwa lilikuwa hili;
Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa Dahari”.
Mitume pia waliendelea kuitwa na Kristo hata baada ya yeye kuondoka duniani.. Mfano utawaona mitume kama Paulo, Barnaba, na Epafrodito (Wafilipi 2:25)
Hata kwa wakati huu wa sasa, watumishi wote wa Mungu wanaofanya kazi kama waliyoifanya mitume, Yesu anawatambua kama mitume wake, hawa ni Zaidi ya wanafunzi, kwasababu hawawi wakristo tu peke yake, bali Zaidi wanajitaabisha kwa ajili ya ufalme wa mbinguni.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.
Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?
Jibu: Tusome kuanzia juu kidogo,
Mathayo 6:1“ Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.
2 Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu
3 Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;
4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Kwa namna ya kawaida haiwezekani kufanya jambo mkono wako mmoja usiwe na mawasiliano ufanyalo mkono wako wa pili, Kwasababu mwili wako wote umeungamanishwa na kuwa kitu kimoja. Kwahiyo Bwana Yesu alipotoa huo mfano hakumaanisha kuwa tutafute namna ambayo wakati tunatoa sadaka mkono wa kushoto usijue ufanyalo mkono wa kulia. Bali alitumia huo mfano kama kionjo tu!. Ambacho kingetusaidia kuelewa kwa kina anachotaka kumaanisha.
Kwamba sadaka zetu ziwe za siri za hali ya juu, zisiwe za kutangaza tangaza, kiasi kwamba hata wewe mwenyewe kwenye nafsi yako (mwili wako) huitangazi tangazi…Unakuwa unaitoa na kuisahau..
Luka 18:10 “ Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.
Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.
12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; HUTOA ZAKA KATIKA MAPATO YANGU YOTE.
13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.
14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa”.
Sasa sio kwamba huyo mtoza ushuru hapo juu, hakuwa anatoa zaka, au sadaka.. Alikuwa anazitoa, pengine zaidi hata ya huyo Farisayo, lakini kila alipotoa katika nafsi yake anakuwa anazisahau, hajinyanyui mbele za Mungu, wala hazitaji taji mbele za Mungu, kila siku anajiona kama hajamtolea, anakuwa hazihesabu, anajiona kama bado ana deni kubwa la kumtolea Mungu…. Hivyo hiyo ikamfanya awe wa haki zaidi kuliko ya yule Farisayo, ambaye alikuwa anajiinua inua katika nafsi yake.
Lakini zama hizi ni kinyume chake, hebu mtu amtolee Mungu sadaka Fulani, labda kiwango Fulani cha fedha, utaona jinsi atakavyotangaza kwa watu, atawejiwekea mazingira kila mtu ajue, na hata wakati mwingine kunung’unika nung’unika, anapoona jambo Fulani halipo sawa (kila mara utasikia anataja..sadaka zetu zinafanyiwa hichi au kile!!).. na hata akifaulu hilo (akawa hanung’uniki), utaona anavyojinyanyua kila siku mbele za Mungu katika sala zake.. Akisali utasikia, mwezi uliopita nilikutolea sadaka hii!..wiki iliyopita nikakutolea tena.. jambo hilo atalirudia rudia mara nyingi…kila sadaka anayotoa anaihesabu na anaona ni kama anamnufaisha Mungu kwa sadaka zake na wala si kama ni wajibu wake.
Lakini wakati huo huo yupo mwingine ambaye hawezi kupitisha wiki, hajamtolea Mungu sadaka nono, na kila anapopiga magoti mbele za Mungu anajiona kama hajawahi kumtolea chochote. Sadaka aliyoitoa wiki iliyopita hata haikumbuki! (Huyo ndio mfano wa mtu yule anayetoa sadaka ambayo hata mkono wake mmoja haujui ifanyacho mkono wake wa pili).
Hivyo Neno hilo ni kutufundisha tu, jinsi ya kuenenda mbele za Mungu, ili tupate thawabu, tufahamu kuwa tunapomtolea Mungu, au tunapowapa vitu watu, tusijionyeshe mbele za watu wala mbele za Mungu, Ukishatoa sahau kama umetoa, zaidi ya yote tutafute kumtolea tena na tena.. Ndivyo tutakavyopata thawabu kutoka kwa Mungu, lakini kinyume cha hapo, Bwana Yesu alisema, tumekwisha kupata thawabu zetu.
Bwana atubariki na kutusaidia.
Kumbuka, kama unaisikia injili leo na kuipinga, kama unahubiriwa uache uzinzi, na hutaki kuamua kuacha makusudi, kama unahubiriwa uache ulevi, na wizi na mambo yote machafu hutaki na unatafuta kumtolea Mungu sadaka, biblia inasema “kutii ni bora kuliko dhabihu (1Samweli 15:22)”.. na pia inasema…
Mhubiri 5:1 “Jitunze mguu wako uendapo nyumbani kwa Mungu; Maana ni heri kukaribia ili usikie, Kuliko kutoa kafara ya wapumbavu; Ambao hawajui kuwa wafanya mabaya”.
Na pia inasema “Sadaka ya wasio haki ni chukizo;..(Mithali 15:8)” Na tena…
Kumbukumbu 23: 8 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.
Usichukue mshahara wako wa kazi ya Bar na kumpelekea Mungu, ukidhani inamfurahisha sana hiyo sadaka.. Yeye anaihitaji roho yako ipate wokovu na si fedha yako. Sadaka ni matokeo ya shukrani, sasa utamshukuru vipi mtu ambaye umemkataa moyoni mwako?..si utakuwa ni mnafiki na kumfanya ahuzunike juu yako?.
Hivyo kama hujampokea Yesu, leo unayo nafasi, kabla ya kufikiria kwenda kumtolea Mungu, fikiria kwanza kuondoa roho ya uasherati, ulevi, kujichua, wizi na nyinginezo ndani yako. Baada ya hapo ndipo fikiria kwenda kumtolea Mungu, na unapomtolea hakikisha hujinyanyui mbele zake.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana wetu, Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, neno la Mungu lililo hai, lenye nguvu na uwezo.
Tunapomwamini Bwana Yesu na kubatizwa, na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, biblia inasema tunatiwa muhuri mpaka siku ya ukombozi wetu.
Waefeso 4:30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi”.
Hapo biblia inasema tumetiwa muhuri hata siku ya ukombozi.. Ukombozi unaozungumziwa hapo ni ukombozi wa miili yetu, yaani siku ile tutakapovikwa miili mingine ya utukufu isiyoharibika.. Na tendo hilo litatokea siku ile ya unyakuo. Ambapo kama biblia inavyosema, kufumba na kufumbua parapanda ya mwisho italia, na wafu waliokufa katika Kristo watafufuka, na kwa pamoja miili yetu itabadilishwa na kuvaa kutokuharibika (1Wakorintho 15:52-54).
Upo ukombozi wa Roho zetu, ambao huo tunaupata pale tu tunapompokea Yesu na Roho Mtakatifu na kubatizwa. Hapo roho zetu zimekombolewa kwa damu ya Yesu.. Lakini ipo siku nyingine aliyoiandaa Mungu, kwaajili ya ukombozi wa miili yetu (ambayo ndio siku ile ya parapanda).
Ndio maana ijapokuwa tumempokea Yesu bado miili yetu hii wakati mwingine inapitia magonjwa, maumivu, mateso n.k..Ni kwasababu gani??..
Ni kwasababu bado ukombozi wake haujakamilika, siku ya ukombozi wa miili yetu itakapofika hatutaugua tena, hatutakuwa na maumivu, hatutasikia njaa, hatutashindana na mwili tena kama tunavyoshindana nao sasa.
Warumi 8:23 “Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, UKOMBOZI WA MWILI WETU”.
Kwahiyo kwasasa tunapookoka, (yaani tunapomwamini Yesu, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu) tunapata ukombozi wa Roho zetu. Roho zetu zinakuwa zipo salama, haziteseki tena, haziteswi tena na adui, ndio maana mtu aliyeokoka japokuwa anaweza kulala njaa, lakini utaona bado ana furaha, ijapokuwa anapitia magonjwa lakini amani na furaha ndani yake bado vinatawala, ijapokuwa anapitia mambo yote ya kutesa katika mwili lakini roho yake bado haijakata tama, ipo salama (hata anafikia kusema na kuimba “Ni salama rohoni mwako”).. roho yake inakuwa ni ya ushindi siku zote.
Ni kwanini?..Jibu ni rahisi ni kwasababu kashapata ukombozi wa roho yake siku ile alipookoka na kupokea Roho Mtakatifu. Mtu wa namna hiyo biblia inazidi kusema kwamba uhai wake unakuwa umefichwa pamoja na Mungu (Wakolosai 3:3). Roho yake, adui hawezi kuipata tena.
Sasa kipindi hicho ambacho tumepata ukombozi wa roho zetu, huku tukisubiri ule wa miili yetu.. Kipindi hicho hapo katikati, biblia inasema tunakuwa tunalindwa na NGUVU ZA MUNGU.
1Petro 1:5 “Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho”.
Hivyo pindi tu tunapopata wokovu wa roho zetu, hapo hapo nguvu za Mungu zinashuka juu yetu, kutufunika na kutulinda, mpaka siku ya ukombozi wa miili yetu. Maana yake ni kwamba, Majaribu yote kuanzia huo wakati yatakayokuja mbele yako yatakuwa ni kwa lengo la kukufundisha (yaani madarasa), na si kukuangusha au kukupoteza, na ni Mungu anakuwa ameyaruhusu.
Yakobo 1:2 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;
3 mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”.
Lakini kama hujapata ukombozi wa roho yako (yaani hujamwamini Yesu na kubatizwa ubatizo sahihi, na kupokea Roho Mtakatifu).. Usijihesabie kwamba kuangukia kwenye majaribu ni furaha, bali huzuni!!… Kwasababu hayajatoka kwa Mungu hayo bali kwa adui shetani, na lengo la hayo majaribu ni kukupoteza.
Majaribu yote unayopitia kabla ya kumpokea Yesu, ni shetani ndiye aliyekuwa anakutesa nayo, na lengo lake lilikuwa ni ufe!! Na upotee kabisa…kwasababu ulikuwa umetoka nje ya nguvu za Mungu. Lakini Majaribu yanayokuja ukiwa ndani ya Kristo, lengo lake ni kukuimarisha na kukufanya imara na si kukuangusha au kukupoteza na mwisho wake yanakuwa na mlango wa kutokea. Lakini hayo mengine yanakuwa hayana mlango wa kutokea, Mlango wake wa kutokea ni aidha kumpokea Yesu au kufa!!.. Lakini hayatatuliki kwa njia nyingine yeyote.
Hivyo uchaguzi ni wetu!. Kumpokea Yesu, na kukaa CHINI YA NGUVU ZA MUNGU, tukilindwa mpaka siku ya ukombozi wa miili yetu, au kukaa nje ya nguvu za Mungu, tukiteswa na adui shetani bila kuwa na suluhu yoyote, mpaka tunakufa.
Kama leo hii unataka kukaa chini ya ulinzi wa Nguvu za Mungu, ni rahisi sana. Nguvu za Mungu hutazipata kwa kuombewa, wala kuwekewa mikono, bali utazipata kwa kulielewa na kulipokea Neno la Mungu, hilo tulilojifunza. Kwamba zitakuja juu yako kwa kumwamini Yesu kwanza kwamba ni Bwana na mwokozi, na kwamba anazo NGUVU NYINGI SANA, zisizo na ukomo!..na kwamba alizaliwa na bikira miaka zaidi ya elfu 2 iliyopita, na akazikwa na siku ya tatu akafufuka, na sasa hivi yupo Mbinguni, hafi tena!!!. Na atarudi tena kwaajili ya kulinyakuwa kanisa lake (yaani wale wote waliompokea), na kuhukumu ulimwengu, na kwamba hakuna njia nyingine yeyote ya kumfikia Mungu zaidi yake yeye.
Ukishaamini hivyo hatua inayofuata ni ubatizo. Alisema katika Marko 16:16, kwamba aaminiye na kubatizwa ataokoka!!..maana yake ukombozi bila ubatizo haijakamilika. Hivyo unapaswa ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO, ambalo ndio jina la Baba,Mwana na Roho Mtakatifu, hilo jina moja la Yesu ndio tunalopaswa kubatiziwa kwalo. Na Baada ya hapo Yule Roho ambaye ataingia ndani yako wakati unabatizwa au ambaye alishaingia kipindi kifupi kabla ya kubatizwa, atakuongoza na kukutia katika kweli yote ya kuyaelewa maandiko.
Na kuanzia hapo na kuendelea, NGUVU ZA MUNGU, zitashuka juu yako, zitakazokulinda kuanzia hapo na kuendelea, hivyo utakapoanza kuona unapitia majaribu Fulani madogo madogo, usiogope, yachukulie tu kama darasa, kwasababu ni Mungu kayaruhusu na zipo nguvu zake zinakulinda na kukushikilia, huwezi kuanguka wala kupotea.
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
SWALI: Je! Mke wa ujana ni yupi.. Je! siruhusiwi kumwacha Rafiki yangu wa kike (Girlfriend) au wa kiume (Boyfriend) na kwenda kuwa na mahusiano na mwenzi mwingine, kwasababu yule wa kwanza ndio mwenzi wa ujana wangu?
JIBU: Mke wa ujana kama inavyozungumziwa katika biblia sio Rafiki wa kike (GF) Bali ni mke ambaye ulishafunga naye ndoa tangu ukiwa kijana, hadi sasa umeshakuwa mtu mzima au umeshazeeka. Huyo mke uliyenaye sasa ndio anaitwa mke wa ujana wako.Ulikuwa naye tangu enzi na enzi.
Neno hilo utakutana nalo katika vifungu hivi,
Malaki 2:14 “Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako”.
Mithali 5:18 “Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako”.
Hivyo kulingana na swali lako ni kwamba, hupaswi kumwacha mke wako ambaye ulikuwa naye tangu ujanani, ukaenda kuoa mwingine, hiyo ni dhambi kubwa sana, vilevile hupaswi kumwacha mume wako, uliyeolewa naye tangu ujanani mwako, ukaenda kuolewa na mume mwingine hiyo ni dhambi. Utakuwa unafanya dhambi ya uzinzi, haijalishi hakuvutii tena kwako kiasi gani.
Lakini hapo haizungumzii, Boyfriend au Girlfriend. Katika Imani ni kosa mtu kuishi na msichana au mvulana, au kuwa na mahusiano yoyote ya kimapenzi na mtu ambaye bado hajawa mke/ mume wake.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.
35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.
36 Kwa kuwa ITAMFAIDIA MTU NINI KUUPATA ULIMWENGU WOTE, AKIPATA HASARA YA NAFSI YAKE?
37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake”
Kufaidia maana yake “mtu atapata faida gani, aupate ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake”.
Umepata majumba yote, fedha zote duniani ni zako, magari yote ni ya kwako, madini yote (fedha, dhahabu, almasi) ni yako, ardhi yote dunia ni yako, na kila kitu ni chako, yaani hakuna kisicho chako..Halafu umekufa umejikuta jehanamu!!…Swali tunaulizwa na aliyeacha Mbingu za mbingu akaja duniani, aliyeacha Milki, aliyeacha utajiri, na kushuka duniani kwenye mavumbi…anatuuliza swali… ITATUFAIDIA NINI KUPATA HAYO YOTE HALAFU TUMEPATA HASARA ZA NAFSI ZETU???.
Huyo huyo aliyeacha mbingu na utajiri mbinguni anasema mahali Fulani..
Marko 10:22 “Walakini yeye akakunja uso kwa neno hilo, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Yesu akatazama kotekote, akawaambia wanafunzi wake, JINSI ITAKAVYOKUWA SHIDA WENYE MALI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU!
24 Wanafunzi wakashangaa kwa maneno yake. Yesu akajibu tena, akawaambia, WATOTO, JINSI ILIVYO SHIDA WENYE KUTEGEMEA MALI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU!
25 Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu ya sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”.
Anasema.. “jinsi ilivyo shida”…sio kwamba “haiwezekani kabisa”..inawezekana lakini… “JINSI ILIVYO SHIDA !!!”.
Mpaka Bwana mwenyewe anasema “Ni shida!”.. tena anakwambia ni rahisi ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia kwenye ufalme wa mbinguni!!!…. Sentensi hiyo moja kwa moja, inaonyesha jambo ambalo uwezekano wake ni mdogo sana… Kwasababu mpaka leo hii bado huo muujiza haujatendeka wa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano!!!…. (ngamia huyo awe ngamia mnyama, au kamba..lakini bado hatujaona!!)..
Sasa basi kama uwezekano wake ni mdogo hivyo!!!….Kwanini tunajisumbua sana kutafuta hayo mambo????.
Mithali 23:4 “USIJITAABISHE ILI KUPATA UTAJIRI; Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe”.
Ni kweli, Ukimuomba sana Mungu akupe utajiri, na ukiutafuta utaupata..na atakupa nguvu za kuupata kulingana na Neno lake, lakini kumbuka pia…
UNAZIDI KUIFANYA NJIA YAKO YA KUINGIA MBINGUNI KUWA NYEMBAMBA ZAIDI. Kwasababu wewe unakuwa Ngamia, na Mlango wa Mbinguni unakuwa tundu la sindano..
Ushauri huo ametupa!!…yeye aliyetoka mbinguni, ambaye anaujua kila kitu!.. ameona si vyema atuambie tu! Ni ngumu?..bali aonyeshe na mfano wake!..Ni sisi kuchagua kujitanua kuzidi kuwa ngamia, au kujitajirisha katika mambo ya ufalme wa Mbinguni.
Na kwanini katika ule mfano alimwambia Yule kijana akauze kila kitu awape maskini kisha amfuate??…Si kwasababu Bwana Yesu alikuwa anataka kumfukarisha, bali alitaka kumtoa mungu-mali katika moyo wake na kumpa moyo wa unyenyekevu ambao utamtegemea Mungu..ambao huo pekee ndio Mungu anaweza kutembea nao..na si ule moyo wa kiburi cha mali aliokuwa nao. Na kamwe asingeweza kukosa chakula, baada ya pale, kwasababu angekuwa tu kama mmoja wa mitume wake (wakina Petro), labda angekuwa ni mtume wa 13, kwasababu wakina Petro nao, waliambiwa waache nyavu zao wamfuate Bwana. Lakini katika kumfuata kwao kote Bwana hawajawahi kufa njaa, wala kupungukiwa.
Dada/Kaka inawezekana umehubiriwa sana na kuombewa upate mali na utajiri!! … Leo mimi nakushauri ushauri , ushauri ule ule Bwana aliotupa!… “Kwa kuwa ITAMFAIDIA MTU NINI KUUPATA ULIMWENGU WOTE, AKIPATA HASARA YA NAFSI YAKE?”.
Wengi wa wanaokuhubiria kwamba “Njoo uwe tajiri” ni kwasababu wanatafuta kitu kutoka kwako!!..wanataka wapate kitu kutoka kwako, lakini hawataki Roho yako iende mbinguni, ndio maana hawatakuambia kamwe hili neno >> “JINSI ITAKAVYOKUWA SHIDA WENYE MALI KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU!”..
Itakuwa ni shida!.. Itakuwa shida!..
Bwana anasema tujikane nafsi, tunapoanza kumfuata Yesu, ni wakati wa kupunguza mizigo yetu, hata ikiwezekana mali, na si kuiongeza.. ili zisitusonge kuingia mbinguni… si wakati wa kutia jitihana kutafuta utajiri!!!.. Ni wakati wa kuupunguza..Kama kazi yako ya Bar ndio iliyokuwa inakupa utajiri na mali! Unaiacha…Ni rushwa ndio zilikuwa zinakutajirisha unaacha…
Ulikuwa una maduka matau yaliyokuwa yanakufanya ufanye kazi masaa 24, hebu punguza bakiwa na moja tu! Litakalokufanya ufanye kazi masaa 8 au chini ya hapo, ili upate muda wa kuutafuta uso wa Mungu.. Muda wa kuishi hapa duniani haikusubirii. Itakufaidia nini upate kila kitu halafu upate hasara ya nafsi yako???..Au utatoa nini kuifidia hiyo nafsi siku ile??.
Luka 21:33 “Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
34 Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo”.
Kama nitakula chakula cha aina moja kila siku, halafu nitapata muda wa kusali na kusoma neno kwa utulivu kila siku, si ni heri kuliko nile mboga saba, nikae chini ya dari zuri, halafu nakosa hata muda wa kusoma Neno na kuomba!!.. Ni heri niwe mtu wa daraja la chini kabisa lakini ni Tajiri wa Roho kuliko niwe mtu wa daraja la kwanza halafu ni ngamia katika roho, ambaye sitaweza kupenya kuingia katika ufalme wa Mungu!!.. Ni heri niwe na rafiki maskini ambaye atanifundisha na kunishurutisha kumcha Bwana, kuliko niwe na rafiki tajiri ambaye atanipeleka mbali na Mungu.
Bwana mkuu wa hekima zote atusaidie tuweze kuyatafakari mashauri yake na kuchukua uamuzi sahihi.
Kama hujampokea Yesu, kumbuka tupo mwisho wa nyakati, na Hukumu ya ulimwengu huu ni juu ya wale wote waliomkataa Yesu na maneno yake. Hivyo mgeukie leo, tubu dhambi zako kwake, na yeye atakusamehe na kukupokea na kukufundisha.
Maran atha!!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.
Wakati ule Bwana Yesu anafufuka, utaona, lipo kundi la watu alilitokea akiwa kule kule Yerusalemu, lakini lipo kundi lingine alilipa masharti ni wapi atakapokutana nalo.
Kwa mfano Yesu wale watu wawili waliokuwa wanakwenda kwenye Kijiji kimoja kilichoitwa Emau, karibu na Yerusalemu, Kristo aliwatokea huko huko (Luka 24:13-33). utaona pia aliwatokea wale wanawake waliokwenda Kaburini siku ile ya kwanza ya juma alipofufuka, akazungumza nao, kisha akaondoka.
Lakini hakuwatokea mitume wake 11 hata mmoja akiwa huko Yerusalemu, badala yake, aliwaagiza wale wanawake, kuwa wakawaambie, Bwana amesema atawatangulia kwenda Galilaya ndipo watakapomuona.
Mathayo 28:9 “Na tazama, Yesu akakutana nao, akisema, Salamu! Wakakaribia wakamshika miguu, wakamsujudia.
10 Kisha Yesu akawaambia, Msiogope; enendeni, mkawaambie NDUGU ZANGU waende Galilaya, ndiko watakakoniona”.
Unaweza kujiuliza ni kwanini awape masharti ya mahali pa kukutana nao, Kumbuka pia hata kabla ya Yesu kufa, aliwaambia pia wanafunzi wake maneno hayo hayo, utasoma hilo katika
Marko 14:27 “Yesu akawaambia, Mtakunguwazwa ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika.
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya”.
Kwahiyo hilo halikuwa agizo la kila mtu bali lilikuwa mahususi kwa baadhi ya watu wale ambao aliwaita “NDUGU ZAKE”,tofauti na wale wengine, Na ukisoma pale vizuri utagundua kuwa haikuwa mahali popote tu kule Galilaya, hapana bali Bwana Yesu aliwapa na eneo husika kabisa watakalomwonea, nalo lilikuwa katika ule mlima aliowaelekeza.
Ndipo ukisoma pale utaona baada ya Bwana Yesu kufufuka wakafunga safari kweli, kutoka Yerusalemu, mpaka Galilaya, umbali wa kama KM 120, hivi, , wakaenda moja kwa moja mpaka kwenye huo mlima aliowaagiza, ndipo wakakutana naye uso kwa uso na kuwapa maagizo;
Mathayo 28:16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu.
17 Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka.
18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”.
Sasa unaweza ukajiuliza ni kwanini, ajidhihirishe kwao akiwa Galilaya na sio kule Yerusalemu ,kama alivyofanya kwa wale wengine? Kulikuwa na sababu gani ya yeye kuwachosha wasafiri umbali wote ule mrefu mpaka Galilaya wakati angeweza tu kuwatokea palepale Yerusalemu na kuwapa maagizo?
Jibu ni kuwa Bwana alikuwa anataka mawazo yao kwa wakati ule yaelekee kule.
Utakumbuka kuwa Galilaya ndio mji Yesu alikolelewa, mpaka anaanza huduma, yaani kwa ufupi ni kuwa sehemu kubwa ya Huduma yake aliifanya akiwa Galilaya, hata mitume wake wote aliwaitia huko, ishara nyingi na miujiza yake mingi aliifanya Galilaya, ni sehemu ndogo sana ya huduma yake aliifanya akiwa Yerusalemu.
Hivyo Kristo kuwaambia mitume wake ninawatangulia Galilaya ni kuwaonyesha kuwa Moyo wake, baada ya kufufuka kwake haukuwa tena Yerusalemu kwa mitume wake.. Hakutaka wamwone kwa jicho ya Yerusalemu, kama wale wengine bali kwa jicho la Galilaya, kule alipotumikia muda wake wote akiifanya kazi ya Mungu.
Huko ndipo alipowaambia enendeni ulimwenguni kote mkawafanya mataifa kuwa wanafunzi, kama mimi nilivyokuwa ninawafanya huku Galilaya, nami nitakuwa pamoja nanyi mpaka ukamilifu wa dahari.
Nini Kristo alitaka tufahamu katika habari hiyo.?
Ni kuwa hata sasa, ikiwa wewe ni mwanafunzi wa Yesu, au unataka uwe mwanafunzi wa Yesu kweli, basi fahamu kuwa hutamwona Kristo Yerusalemu, aliposulibiwa, hutamwona Kristo katika mafundisho ya msalaba tu kila siku, mafundisho ya kuamini, au ya vitubio, yaani kama wewe miaka nenda rudi, hujui kingine Yesu anachokitaka kwetu zaidi ya kutubu na kuokoka, basi, wewe bado upo Yerusalemu.
Kristo anataka uitazame na kazi yake pia, anataka uone alivyofanya yeye akiwa duniani na wewe ukafanye vivyo hivyo, anataka uone kuwa kuna watu wanahitaji kuhubiriwa Injili, kuna watu wanahitaji kupata wokovu, kufunguliwa, kuwekwa huru kutoka katika dhambi na vifungo mbalimbali, hicho ndicho Kristo anataka uone kwa wakati wa sasa. Hiyo ndio Galilaya yako unapopaswa uende ukakutane na Yesu.
Lakini kama wewe ni wa kusikia tu injili, na kusema AMEN, au kusema mimi nimeokoka, basi, huna cha Ziada, ujue kuwa wewe si “NDUGU” yake Kristo, Wewe si “MWANAFUNZI WAKE”. Huwezi kumfurahisisha kwa lolote.
Nyakati hizi tunazoishi ni nyakati ambazo, zilitabiriwa kuwa kutakuwa na njaa mbaya sana, sio ile njaa ya kukosa chakula, bali ni ile ya kukosa kuyasikia maneno ya Mungu, Nabii Amosi alionyeshwa hilo
Amosi 8:11 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana”.
Jiulize kwa upande wako, tangu Kristo amefufuka ndani yako, ni kazi gani ya ziada umeifanya kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Bado upo Yerusalemu tu, Galilaya hutaki kwenda..Upo buzy na kazi zako, upo buzy na shughuli za kidunia, upo buzy na familia yako, Galilaya kwako ni mbali sana, kule hakuna pesa, hakuna kujulikana, utaonekana mshamba, utadharauliwa, utachekwa,
Ndugu jitathmini ukristo wako ikiwa hata unaona ugumu kuichangia kazi ya injili, unategemea vipi utaweza kuwahubiria wengine habari za ufalme wa mbinguni, hata hicho kitakushinda tu, Na taji lako litakuwa hafifu, au usipokee kabisa taji huko unapokwenda!
Tuamke sote, tuanze kuwagawia na wengine kile Bwana alichotugawia sisi, katika kipindi hiki cha njaa cha siku za mwisho.
Maran atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
RABI, UNAKAA WAPI?
NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.
KURUDI ISRAELI KWASASA NI KUGUMU, SIO KAMA KULE MWANZONI.
Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.
OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.
Neno “hiana” maana yake ni “usaliti” ule wa mapenzi. Endapo mtu mmoja akimwacha mke wake/mume wake na kwenda kufanya uzinzi , mtu huyo amefanya mambo ya hiana kwa mwenzake. Na Bwana anauchukia usaliti.
Malaki 2:14 “Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, ULIYEMTENDA MAMBO YA HIANA, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako.
15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake MAMBO YA HIANA.
16 Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; BASI JIHADHARINI ROHO ZENU, MSIJE MKATENDA KWA HIANA”.
Lakini mbali na hilo, Watu wote waliokoka mbele za Kristo tunahesabika katika roho kama BIBI ARUSI.. na Kristo ndiye Bwana wetu (2Wakorintho 11:2).
Maana yake tunapoacha kufanya maagizo yake, kama utakatifu, kuwa na upendo, kuwa watu wa msamaha, wasiolipiza visasi, wasio wazinzi, wezi, walevi, watukanaji, waabudu sanamu n.k katika roho ni tumemsaliti (Yaani tumefanya mambo ya HIANA). Maana yake tunamtia wivu. Na siku zote kumbuka, Mungu aliposema yeye ni mwenye wivu, hakumaanisha wivu huu wa kawaida, labda mtu anapoona mwenzake kapata kitu Fulani ambacho yeye hanapa! Hakumaanisha huo..kwasababu ni heri ungekuwa huo!… bali wivu alioumaanisha ni a ule wivu wa mtu anapochukuliwa mke wake kipenzi!..Wivu ambao ni mbaya sana, ambao kwetu sisi wanadamu wengi unaishia aidha upande mmoja ufe, au pande zote zife!!..Ndio hapo utasikia aidha mtu kajinyonga..au kaua na yeye mwenyewe kajimaliza!..
Mithali 27:4 “Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu”
Hiyo ndio maana Bwana Mungu alisema katika…
Kutoka 20: 4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; KWA KUWA MIMI, BWANA, MUNGU WAKO, NI MUNGU MWENYE WIVU; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Wakati Fulani Yuda, na Israeli walimwacha Bwana, na kufanya mambo maovu yasiyofaa ikiwemo kwenda kuabudu miungu mingine, na Bwana akasema maneno haya juu yao…
Yeremia 3:6 “Tena, Bwana akaniambia siku za mfalme Yosia, Je! Umeyaona aliyotenda Israeli mwenye kuasi? Amepanda juu ya kila mlima mrefu, akafanya huko mambo ya ukahaba, tena, chini ya kila mti wenye majani mabichi.
7 Nami nalisema baada ya yeye kuyatenda hayo yote, Atanirudia mimi, lakini hakurudi; na dada yake, Yuda MWENYE HIANA, akayaona hayo.
8 Nami nikaona, wakati nilipokuwa nimemwacha Israeli mwenye kuasi, nikampa hati ya talaka kwa sababu hiyo ya kuzini, dada yake, Yuda mwenye hiana, hakufanya hofu; bali yeye naye akaenda akafanya MAMBO YA UKAHABA.
9 Hata ikawa, kwa sababu alikuwa mwepesi wa kufanya ukahaba, nchi ikatiwa unajisi, naye akazini na mawe na miti.
10 Na pamoja na hayo yote dada yake, Yuda mwenye hiana, hajanirudia mimi kwa moyo wake wote, bali kwa unafiki, asema Bwana.
11 Bwana, akaniambia, Israeli mwenye kuasi amejionyesha kuwa mwenye haki kuliko Yuda mwenye hiana.
12 Enenda, ukatangaze maneno haya kuelekea upande wa kaskazini, ukaseme, Rudi, Ee Israeli mwenye kuasi, asema Bwana; sitakutazama kwa hasira; maana mimi ni mwenye rehema, asema Bwana, sitashika hasira hata milele.
13 Ungama uovu wako tu; ya kwamba umemwasi Bwana, Mungu wako, na njia zako zimekuwa nyingi kuwaendea wageni chini ya kila mti wenye majani mabichi, wala hamkuitii sauti yangu, asema Bwana.
14 Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; MAANA MIMI NI MUME WENU; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni”.
Je na wewe leo unafanya mambo ya Hiana kwa kuvaa mavazi yasiyofaa??, unavaa suruali, unapaka wanja, unapaka lipstick, unavaa hereni na kuweka wigi kichwani?..je unafanya mambo hayo ya hiana mbele za Mungu wako kwa kulewa na kufanya uasherati na anasa, je unafanya mambo ya hiana kwa kutazama picha za ngono mitandaoni, na kujichua?.. je umefanya mpira kuwa ndio Mungu wako na kuwa mshabiki wa mambo hayo?…Fahamu kuwa kwa matendo yako unamtia Mungu wivu. Na kuzivuta hasira za Mungu karibu nawe. Kumbuka mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu. Hivyo huwezi kuufanya kama unavyotaka wewe, na pia kumbuka tulinunuliwa kwa thamani kubwa, hivyo hatuwezi kuishi tu kama tunavyotaka sisi.
Soma mistari hii uone ni jinsi gani, mambo ya Hiana yanavyomchukiza Mungu wetu >>Yeremia 9:2, Yeremia 5:11, Hosea 6:7, 1Samweli 14:33.
Rudi leo! Kwa Bwana na kutubu!..choma hizo nguo zisizo za kiMungu unazozivaa, wala usimpe mtu!. Na mwombe Bwana akupe badiliko la kweli maishani mwako. Vunja hizo chupa za bia, na vikao vya ulevi na anasa, achana na huyo mvulana/au msichana mnayefanya uasherati sasa, achana na huyo mke/mume wa mtu unayeishi naye, au kutembea naye. Futa hiyo miziki yote ya kidunia katika simu yako. Ukifanya hivyo hiyo ndio TOBA!.. Kisha Bwana mwenyewe atakuongezea nguvu ya kuweza kushinda dhambi!..Lakini usipofanya hayo kwa vitendo, hakuna nguvu yoyote itakayoshuka juu yako.
Na pia kumbuka tunaishi katika siku za mwisho na Bwana Yesu alisema itatufaidia nini tukiupata ulimwengu mzima halafu tupate hasara za nafsi zetu. Hivyo tafakari hilo siku zote, na ujue kuwa vitu vya ulimwengu huu havina umuhimu sana kama vinavyotukuzwa na watu.. Bwana Yesu anarudi.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo: